Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Zitambue Kazi za Nywele Katika Sehemu za Siri

0
0

Hivi umewahi kujiuliza kazi ya baadhi ya vitu vilivyopo katika mwili wako?

Kuna baadhi ya vitu viko katika mwili vinaweza kuonekana kama havina kazi (useless) lakini kumbe havikuwapo hapo kwa bahati mbaya.

Nywele za maeneo ya siri imekuwa na baadhi vitu ambavyo umuhimu wake haujatiliwa maanani na watu wengi. Imefikia hatua mpaka wengine wanaziona kama ni uchafu mwilini.

Watu wengi hutumia gharama kubwa na vifaa vya gharama kuhakikisha kuwa wananyoa nywele hizo. Watu hutumia viwembe, wengine hutumia mpaka nta ili kuhakikisha kuwa eneo linalonyolewa nywele hizo linakuwa kama walivyokuwa wakiwa watoto.

Baadhi ya wataalamu wa maswala ya kijamii wanasema kuwa watu hutumia jitihada kubwa kupambana na nywele hizi ikiwa ni sehemu ya utamaduni wao, hasa kwa wale wanaodhani kuwa wameendelea na wanaovaa nguo za ndani zinazojulikana kama ‘bikini’.

Wataalamu wa upasuaji wamegundua kuwa kuondoa nywele kwenye eneo la mwili kabla ya kufanya upasuaji, kunaongeza hatari ya athari na maambukizi katika ngozi.

Imeelezwa kuwa unaponyoa nywele zote ktika maeneo ya sehemu za siri, unaongeza hatari ya maambukizi na huchoche bakteria kuingia ndani ya mwili kupitia vitundu vidogo vinayoachwa baada ya nywele hizo kuwa zimenyolewa.

Vile vile, kunyoa nywele zote za maeneo ya siri huongeza hatari ya maambukizi ya magonjwa ya ngono kutokana na majimaji yanayokuwepo wakati wa ufanyaji wa mapenzi kupenya katika vitundu vidogo vilivyobakia baada ya nwele hizo kunyolewa.

Kunyoa nywele za sehemu za siri kunaweza kukusababishia muwasho na kukuletea kero hata unapokuwa mbele za watu. Hebu fikiria umenyoa nywele za sehemu za siri halafu uko mbele ya mkutano kazini, mara ghafla unapatwa muwasho katika maeneo ya siri na makwapa. Unadhani unapatwa na hali gani? mfadhaiko unaoupata unaweza kukuletea fedheha kubwa.

Nywele za sehemu za siri huwa na kazi ya kuizuia ngozi dhidi ya michubuko, pamoja na bakteria mbalimbali ambao wanaweza kushambulia maeneo nyeti. Vile vile nywele kama za makwapa hudanya kazi ya kufyonza jasho linalotoka ili lisitiririke katika maeneo mengie ya mwili wako.

Uamuzi ni wako. Ikiwa utaamua kunyoa nywele za sehemu za siri ama la, hiyo ni juu yako. Lakini kumbuka kujiweka safi musa wote na kuhakikisha kuwa mwili wako unakuwa nadhivu na wenye afya.


Jerry Muro:Utoto Huu wa Mbunge Nassari na Lema, Watanzania Tuwe Wakali...Tutapoteza Taifa

0
0
Anaandika Jerry C. Muro
Dar es Salaam, Tanzania
October mosi, 2017


Nimetazama mkutano na waandishi wa habari wa Mbunge wa Arumeru Mashariki Mhe. Joshua Nasari ambao alimualika pia Mbunge wa Arusha Mjini Mhe. Godbless Lema, nikaishia kuvuna hasira kubwa sana. Na kwa hili kwa kweli naomba watakaokasirika wanisamehe.

Mimi ni kijana ninayefanya kazi za upigaji wa picha na utengenezaji wa vipindi na makala mbalimbali (Audio Visual Production). Kwa mara ya kwanza baada ya Mhe. Rais Magufuli kuwapokea madiwani walioamua kuondoka CHADEMA na kuhamia CCM pale Sheikh Amri Abeid Arusha niliposikia kuwa Nasari anasema anaushahidi usio na mashaka na ambao ameupata kwa vifaa maalum alivyovipata nchini Uingereza nilivutiwa sana kwamba nguvu ya teknolojia sasa itamaliza ubishi juu ya biashara ya kununua wanasiasa ili wahame upande mmoja kwenda mwingine.

Nilikatishwa tamaa na Nasari akiwa na mwenzake Lema waliposema hawatatoa ushahidi huo kwa yeyote isipokuwa wakikutana na Rais, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ama viongozi wa juu waliokuwa wanawataja. Niliona hawa ni wababaishaji kama kawaida yao.

Leo nikabonyezwa kwamba kuna mkutano wa waandishi wa habari na uthibitisho unatolewa, nimefuatilia mwanzo mpaka mwisho na nimeogopa sana, nimeogopa kwa sababu naona tunakokwenda sasa watanzania wote tunafanywa watoto.

Tunaigeuza nchi kuwa ya maigizo na sinema, tunaleta mzaha na taharuki badala ya kujielekeza katika ujenzi wa taifa letu ambalo kwa kweli linahitaji mikono na akili zetu ili litokea hapa lilipo.

Sasa twenda kitaalamu.
Picha zilizotolewa na Nasari zinaonesha zimerekodiwa na kamera ya kificho na kwa hakika aliyekuwa anarekodi anaoneka kabisa ama alitumia kalamu zenye kamera ambazo zinapatikana madukani popote Dar es Salaam hata mikoani ama katumia kamera zilizopandikizwa kwenye vishikizo vya shati.
Hivi vifaa vya kawaida sana na kila anayehitaji anaweza kuvipata, wafanyabiashara wengi wanavyo na huvitumia pale wanapofanya makubaliano na watu mbalimbali ili wasije wakawageuka baadaye. Hata bei yake ni ndogo, mimi nina kalamu yangu nilinunua kwa shilingi 23,500 na inarekodi vizuri.

Ama laa aliyerekodi anaweza kuwa ametumia simu ya mkononi.
Matokeo yake ni kuwa ubora wa picha dhaifu sana na sauti haisikiki kabisa kwa uthibisho wa kila kinachozungumzwa. Lakini pia eneo lililotumika kurekodi kuna mwangwi mwingi sana kiasi kwamba ngumu kujua sauti ya aliyekuwa anazungumza.

Kibaya zaidi kwa sababu ya kutumia vifaa dhaifu hata picha zilizorekodiwa hazioneshi sura ya mtu zaidi ya kuonesha traki suti na mikono na kwa kupitapita inaonesha sura ya mtu ambayo ni vigumu kujua ni nani kutokana na mwanga hafifu.

Mbinu hii hutumika lakini hutumika kwa weledi unaokuwezesha kutokuwa na mashaka na Yule unayemrekodi.
Kwa sisi tunaofanya kazi za Audio visual production kuchukua picha Fulani ukaipandikizia sauti ni jambo rahisi sana na mchezo huu unafanywa sana na watengeneza sinema na movie.

Unaweza kuchukua sauti ya Juma ukaipandikiza kwenye picha ya Hamis.
Sasa nataka kumwambia hivi Nasari, taharuki aliyoitengeneza kwa watanzania kwa kutegemea ataonesha vipicha hivyo vilivyopigwa na simu ya mchina ama vikamera vya kalamu ni utoto mkubwa sana. Hao anaosema ni akina Mnyeti na Mkurugenzi na Katibu Tawala wa Meru hakuna mahali wanapoonekana kwa uhakika kwamba wamesema unachodai, lakini pia hata hizo sauti zao hazisikiki kwa uthibitisho wa uhakika kuwa wasemaji walikuwa wanasema nini.

Kwenye mkutano na waandishi wa habari Nasari anafanya janja ya nyani eti anapandisha sauti za hizo video halafu anazima na kuzungumza yeye kwamba wamesema hivi na hivi na hivi. Utoto na ujinga wa hali ya juu.

Mhe. Nasari na mwenzako Lema, tupeni huo ushahidi usio na mashaka, hizi takataka mnazotaka kupanda ndege kuja kuzileta kwa Kamishna Mkuu wa TAKUKURU ni upuuzi na usanii wa kupigiwa mfano, na I wish ningekuwa mimi ndio Kamishna Mlowola mkikanyaga tu ofisini kwangu nawakamata na kuita vyombo vya dola ili muthibitishe madai yenu.

Kwa sababu nina hakika mnajua mnafanya, fanyeni siasa za kileo jamani. Siasa za kuwafanya watanzania watoto ama wajinga sio leo.

Hizo video zenu zinaweza kutengenezwa na mtu yeyote, tunataka utuoneshe video kama zile alizozionesha Jerry Muro alipowapiga wale askari wa barabarani wanapokea rushwa. Picha iwe clear na ambayo mtu akiona anapata uhakika kwamba ile ni hela. Ama tunataka kuona video kama ile ya yule askari aliyepokea rushwa kwa watalii kule Zanzibar.

Nilitarajia kumuona DC Mnyeti akigawa hela kama mlivyodai, nilitarajia kuwaona madiwani wakipokea hiyo hela kama mlivyotuaminisha. Badala yake mnatuletea picha za mashati ya watu na sauti za kupandikiza.
Hakuna hata diwani mmoja mliyemuonesha hapo, na ningekuwa mimi ni diwani ningewafungulia mashitaka ya kunichafua. Ili mkathibitishe hiyo rushwa nilichukua wapi.
Kama ushahidi ndio huu, Nasari anastahili kukamatwa mara moja ili taharuki aliyeijenga kwa jamii aithibitishe. Ama achukuliwe hatua.

Na kwa kweli mimi sielewi, hivi kweli tunajenga nchi kwa mtindo huu? Kwani Diwani ama mwanachama wa chama cha siasa kuhamia chama kingine tatizo nini? Mbona wanasiasa wanahama kila siku? Wapo wanaokwenda Chadema akina Sumaye, Lowassa, Mgeja, Masha, Ester Bulaya na wengine wengi. Hawa ni wakubwa wakubwa tu. Halikadhalika wapo wanaohama Chadema na kwenda CCM wengi tu wakiwemo hao madiwani kuna shida gani?
Manaake tunatengeneza mazingira kwamba chama kinachostahili kuhamwa ni CCM tu, Chadema hapana.

Wakihama wamehongwa, wamenunuliwa.
Sasa hebu angalia, mkutano wa kuangalia ushahidi wa rushwa ya kuwanunua madiwani yameanza kuzungumzwa na mengine ya miradi, anashambuliwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo.

Sasa wote tunajua hapa kuwa kutokana na changamoto anazokumbana nazo Nasari kwenye Jimbo amebaki kupambana na Mkuu wa Wilaya, anaona kabisa hataweza kurudi. Kwa hiyo kamfanya Mkuu wa Wilaya ndio adui yake, halikadhalika sote tunajua kuwa Mhe. Lema nae anaugomvi na Mkuu wa Mkoa Bw. Gambo sasa wanadhani watatumia tuvideo hutu kuwadhohofisha. Childish!!!!!

Na niseme ukweli watumishi wa serikali katika mkoa wa Arusha mnagombanishwa bila sababu, maana hawa jamaa wanasema nyinyi ndio mnaowapa taarifa, naamini wanawasingizia.
Nimalizie kwa kusema tukiendelea kulea michezo hii ya kitoto ya Lema na Nasari tutakuja kujuta.

Hii nchi imejengwa kwa juhudi kubwa za mababu zetu, who is Nasari aje kuibomoa, who is Lema?
Yaani mmefikia mahali pa kutengeneza sinema za kuwavuruga wananchi, mnatengeneza movie za kulivuruga taifa. Mimi naamini vyombo vya dola havitaacha hili lipite hivi hivi.

Ndugu Nasari pambana na hali yako kwenye Jimbo, kama ulipoteza muda wa kuhudumia wananchi wa Arumeru Mashariki ukidai unakwenda kusoma ili ukatengeneze sinema hii ya kukubeba kisiasa unakosea sana.

Unatafuta huruma ya wananchi. Unataka sinema hii ndio ikupe ushindi?
Nitashangaa sana kama vyombo vya dola vitaachia hili jambo lipite. Zipo nchi zilizofanya mageuzi makubwa ya uchumi na maendeleo kwa ujumla ililazimu watu kama hawa wapotezwe kabisa, maana kuendelea kupoteza muda na watu wa aina hii ni sawa na kuchezea shilingi chooni.

Haiwezekani watu wale wale kila siku wanaleta taharuki nchini, halafu wanachekewa tu.

Nimesoma Majibu ya Mhe Mnyeti, yeye amesema vizuri sana kuwa amechangia Harusi ya Diwani kama alivyoombwa na Muhusika na kama alivyoombwa kuchangia matibabu ya Mhe Lissu, na Amekwenda mbali zaidi kwa Kusema Katika matukio ya filamu hii ambayo producer alikuwa Lema na Director alikuwa Nasari ni filamu ya kuokota matukio ya kazi anazofanya kama Mkuu wa Wilaya.

Uchaguzi umekwisha 2015, badala ya kujenga nchi sisi kila siku kutiana hamaki tu.

Wasalamu katika UZALENDO
Jerry C. Muro
Dar es Salaam
Tanzania

DC Mnyeti Kujibu Tuhuma za Nassari na Lema Baada ya Kurekodiwa Akishawishi Rushwa

0
0
DC Mnyeti aahidi kujibu tuhuma zilizotolewa na Wabunge Nassari na Lema kuwa alihusika kushawishi Madiwani wa CHADEMA kujiuzulu- MTANZANIA

Ushahidi wa Kujua Alipo Ben Saanane na Aliyefanya Shambulio la Lissu Kuwa Hadharani

0
0
Ushahidi wa Kujua Alipo Ben Saanane na Aliyefanya Shambulio la Lissu Kuwa Hadharani
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amefunguka kwamba ikiwa wamefanikisha kuupata ushahidi wa rushwa unavyotumika katika ofisi za umma Arusha anauhakika pia wataupata pia ushahidi wa kujua Ben Saanane alipo pamoja na aliyefanya  Shambulio la Lissu.

Akizungumza leo kwenye mkutano alioufanya na wanahabari yeye pamoja Mbungea Joshua na Nassari wa Arumeru Mashariki, wakati walipokuwa wakiuonyesha baadhi ya ushahidi walionao
"Kama ambavyo hili jambo limekuwa 'revealed kwa kiasi hichi huko mbele ya safari tunapoenda mambo ya Ben Saanane yatakuwa wazi pamoja na shambulio la Tundu Lissu. Hivyo tunapeleka ushahidi wote kwa Mkurugenzi wa Takukuru na tunamtaka achukue hatua kama jinsi alivyochukua  hatua kwa Rugemalila na wengine" Lema

Aidha Mh. Lema amesema kuwa matukio yanayoendelea ndani ya Mkoa wa Arusha hayawezi kufichika kwa kuwa wao ndiyo wenye mkoa na wanajua namna gani ya kucheza michezo yote hivyo ni vyema watu hao wakachukuliwa hatua ili wasiendelee kukaa ofisini.

Kwa upande wa Mbunge Joshua Nassari amesema kwamba anajua jambo analolifanya linahatari kubwa lakini tayari ameshajitolea hata kufa kwa ajili ya kusema ukweli na kulitetea taifa
"Nimeondoka Nairobi  Lissu bado  ni Mgonjwa sana hawezi kufanya lolote.  Najua hata sisi ndipo tunapoelekea lakini tumeshajitolea ma tupo tayari. Mimi mke wangu amelia sana leo wakati nikiwa  nakuja kuutoa  ushahidi huu" Nassari amesema

Mbali na ushahidi walioutoa Lema pamoja na Nassari wamesema kwamba kwa siku ya leo wametoa sehemu ndogo ya ushahidi wao na kwamba sehemu nyingi watakwenda kuzitoa Takukuru kwani ni aibu na fedheha kutoa ushahidi huo ambao wanaamini utaichafua nchi pamoja na Rais kwa ujumla.
Pamoja na hayo Mh. Lema amesema kwamba pamoja na kwamba ametoa ushahidi huo hadharani hana uhakika kama kuna hatua za kisheria zinaweza kuchukuliwa ingawa ana uhakika na amani kwama ameshatimiza wajibu wake.


Rais Magufuli Kutoshiriki Kumbukumbu ya Baba wa Taifa

0
0

Rais Magufuli Kutoshiriki Kumbukumbu ya Baba wa Taifa
Taasisi mbalimbali za umma na zisizo za umma zinazomualika Mhe. Rais katika shughuli za kumbukumbu ya Mwl. Julius Nyerere zinakumbushwa kutokutangaza ushiriki wa Mhe. Rais Magufuli katika shughuli zao mpaka zipate uthibitisho kutoka Ofisi ya Rais.

Taarifa iliyotolewa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais imesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli hatakuwa mgeni rasmi katika kongamano la maadhimisho ya kumbukizi ya Mwalimu Nyerere kama inavyotangazwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Aidha taarifa hiyo imeongeza kwamba Oktoba 11, 2017 ambayo inatangazwa kuwa ndio siku ya kufanyika kwa kongamano hilo, Mhe. Rais atakuwa na majukumu mengine ya Kitaifa kulingana na ratiba yake ya kazi na kuwataka watu wote kuzingatia utaratibu.

Sheik Ponda Amkosoa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Sakata la Wasiojulikana

0
0
Sheik Ponda Amkosoa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Sakata la Wasiojulikana
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda amemkosoa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Boaz akieleza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimeshindwa kuchunguza matukio ya uhalifu yanayotokea nchini.

Akiwa nchini China kuhudhuria mkutano mkuu wa 86 wa Taasisi ya Polisi ya Kimataifa (Interpol), Boaz alikaririwa na gazeti moja la Serikali akisema kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vina uwezo wa kuchunguza matukio ya uhalifu, yakiwamo mauaji na utekaji bila kusaidiwa na vyombo vya nje.

Hata hivyo, Sheikh Ponda aliyempigia simu jana mwandishi wetu, alisema kauli iliyotolewa na DCI haina ukweli.

“Kuna matukio mengi ya mauaji na maiti zimekuwa zikiokotwa, kuna utekaji hadi sasa wengine hawajulikani walipo,” alisema Sheikh Ponda na kuongeza:

“Tunashangaa kumsikia DCI akizungumzia uhodari wa Jeshi la Polisi katika kuchunguza matukio ya uhalifu, wakati tuna maswali mengi tunajiuliza.”

Alisema hadi sasa wananchi hawafahamu alipo Ben Saanane, ambaye ni Mkuu wa Idara ya Sera na Utafiti wa Chadema aliyetoweka tangu Novemba mwaka jana.

Sheikh Ponda alisema China ni nchi yenye maendeleo katika masuala ya ulinzi na usalama, hivyo ni vizuri wawakilishi wa Tanzania kwenye mkutano huo wakaeleza changamoto za usalama zinazotokea nchini ili wasaidiwe kuongeza ujuzi wa kukabiliana na uhalifu.

Kauli ya Sheikh Ponda imekuja wakati viongozi wa Chadema wakiitaka Serikali iruhusu vyombo vya nje kuchunguza tukio la kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Kauli ya Mwigulu

Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alisema matukio mengi ya uhalifu yanaendelea kuchunguzwa na akataka jamii kutoa taarifa ambazo zitasaidia kukamatwa kwa wahusika.

Pia, Nchemba alisisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vina uwezo wa kuchunguza matukio yote, hivyo wachunguzi kutoka nje ya nchi hawahitajiki.

Lwandamina Afunguka Pengo la Tambwe

0
0
Lwandamina Afunguka Pengo la Tambwe
KOCHA Mkuu wa Yanga, Mzambia, George Lwandamina, amefungukia pengo la straika wake, Amissi Tambwe, raia wa Burundi. Tambwe ambaye msimu uliopita alifunga mabao 12 katika Ligi Kuu Bara, msimu huu kwake umeanza vibaya baada ya kushindwa kucheza hata mechi moja kati ya tano za ligi walizocheza wenzake.

Kukosekana kwa Tambwe ambaye alikuwa akiuguza majeraha ya goti, inaonyesha kwamba inachangia uhaba wa mabao ndani ya kikosi hicho kwani katika mechi hizo tano, Yanga imefunga mabao manne pekee tofauti na msimu uliopita ambapo katika mechi kama hizo, timu hiyo ilikuwa imefunga mabao nane huku Tambwe akifunga matatu.

“Ni kweli Tambwe tumemkosa katika mechi hizi za mwanzo, lakini kukosekana kwake haiwezi kuwa tatizo kwa sababu kuna wengine wanacheza nafasi yake kama Obrey Chirwa.

“Anapokosekana mchezaji mmoja kikosini huwa hakuna pengo kutokana na kwamba hapa wote wanaelewana vizuri na kila mmoja anajua majukumu yaike, hivyo akipewa nafasi anafanya vizuri,” alisema Lwandamina.

Daktari wa Yanga, Edward Bavu, alisema leo Jumatatu Tambwe anaanza mazoezi ya nguvu na atakuwa fiti kucheza mchezo ujao dhidi ya Kagera Sugar utakaochezwa Oktoba 13 kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Stori: Omary Mdose

Manara Awatupia Lawama Waamuzi wa Mchezo wa Jana Asema 'Awakawii Kunifungia'

0
0
Manara Awatupia Lawama Waamuzi wa Mchezo wa Jana Asema 'Awakawii Kunifungia
Afisa Habari wa Klabu ya Simba, Haji Manara amefunguka na kuwarushia lawama waamuzi wa mchezo wa uliyochezwa jana kati ya Stand United dhidi ya Simba SC kuwa walichokifanya siyo sahihi kwa kulikataa goli la wazi na kisha kutoa penati yenye utata.

Manara amesema hayo kupitia ukurasa wake maalum wa instagram baada ya kumalizika mchezo huo ambao Simba walitoka kifua mbele kwa ushindi wa mabao 2-1 na hatimaye kuweza kupata alama tatu za mchezo huo.
"Hii ndiyo ligi ya Bongo na hao ndiyo marefa wetu. Unatoa penati tata kisha unakataa goli halali, fowadi anamkimbia beki unasema kaotea!. Acha nipige kimya hawakawii kunitia 'lock up", amesema Manara.
Simba SC kwa sasa inashikilia usukani wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa alama 11 ikifuatiwa na Mtibwa Sugar pamoja na Azam FC kwa alama hiyo huku wakitofautiana idadi ya magoli ya kufungwa na kufunga.


Rais Paul Biya Alaani Vurugu, Cameroon

0
0
Rais Paul Biya Alaani Vurugu, Cameroon
Rais wa Cameroon, Paul Biya amelaani ghasia zilizotekelezwa na pande zote baada ya polisi kuwapiga risasi na kuwauwa watu nane wakati wa maandamano ya raia wa nchi hiyo wanaozuungumza kiingereza wanaotaka kujitenga kuwa na eneo lao.Watu wanane wamejeruhiwa katika ghasia hizo.
Ghasia hizo zimetokea wakati wa maadhimisho ya miaka miaka hamsini na sita tangu kujumuishwa kwa jimbo la wazungumzaji wa kiingereza ndani ya Cameroon.
Wazungumzaji wa lugha ya Kiingereza ambao ni wachache wamekuwa wakiandamana takriban mwaka sasa kwa kile wanachosema kubaguliwa katika mfumo wa elimu na sheria.

Tanroad Yabomoa Nyumba ya Prof. Jay

0
0
Tanroad Wabomoa Nyumba ya Prof. Jay
NYUMBA ya Mbunge wa Mikumi (Chadema), Joseph Haule maarufu kama Prof. Jay, katika eneo la Mbezi Kimara imebomolewa na Wakala wa Barabara Nchini (Tanroads), kwa kile kilichoelezwa imejengwa kwenye hifadhi ya barabara ya Chalinze Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiwa ni maandishi kwenye akaunti ya Instagramu ya mbunge huyo, nyumba hiyo ilibomolewa bila yeye kupewa taarifa.

Nipashe ilimtafuta Profesa Jay kwa simu zake, lakini hazikupatikana na hata kwa WhatsApp iliita bila kupokelewa na alivyotumiwa ujumbe wa maandishi haukujibiwa.

Taarifa za kubomolewa alizipokea kutoka kwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), waliompigia baada ya saa 24 nyumba kubomolewa wakimtaarifu wanakwenda kukata umeme na kuchukua mita yao.

Meneja wa Tanesco Mkoa wa Magomeni, Frank Chambua, akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu, alithibitisha nyumba ya Mbunge huyo kubomolewa Ijumaa na Tanesco walikwenda kuchukua mita na nyaya zao zilizokuwapo na kuzirejesha ofisini.

“Jana (juzi) tulikwenda kwenye eneo na kukuta nyumba yote imeshabomolewa, tulichukua mita na nyaya zetu na kuzirejesha ofisini, nasi tulijulishwa baada ya nyumba kubomolewa,” alieleza.

Meneja huyo alisema kwa mujibu wa utaratibu Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), wanapokwenda kubomoa nyumba huwajulisha, ili wakate umeme, nao huwajulisha wateja, ili waruhusiwe kuingia kuchukua mita na nyaya.

“Kuna maeneo mengine mazingira yanakuwa magumu sana kwamba ni lazima kuwajulisha wateja wetu watusaidie tuchukue nyaya na mita, maana nyingine zinabomolewa nusu na nusu inabaki na nyingine zinakuwa ndani ya ukuta, huwezi kuingia bila ruhusa ya mwenye nyumba,” alifafanua Meneja huyo.

Katika ujumbe wake Prof. Jay ambaye pia ni Msanii wa Bongo Flavor, alisema: “Mimi ni mmoja wa waathirika wa hili zoezi la kubomolewa nyumba zetu huku Mbezi Kimara Septemba 29, mwaka huu.”

Aliongeza: “Jana (siku alipoandika ujumbe) nikiwa katika majukumu jimboni Mikumi majira ya saa 12 jioni, nilitaarifiwa kwamba watu wa Tanroads wakiwa wameambatana na greda mbili na magari mawili ya polisi (defender) yenye askari waliokuwa na silaha mbalimbali za moto walikuwa wanabomoa nyumba yangu (sijawahi kuumia kiasi hiki).”

“Nimesikitishwa sana jinsi Tanroads wanavyoweza kujichukulia maamuzi bila kujali mhimili muhimu wa mahakama, wametoa maagizo gani. Na taratibu zilizotumiwa kubomoa nyumba yangu bila ya mimi na Tanesco kupewa taarifa na kubomoa huku umeme unawaka kilikuwa ni kitendo kinachohatarisha maisha ya wabomoaji wenyewe, familia yangu na majirani zangu.”

Haule alisema Tanesco walimpigia saa 24 au zaidi baada ya ubomoaji wakimtaarifu wanakwenda kukata umeme kabla ya ubomoaji, lakini aliwajulisha kuwa imeshabomolewa.

“Niliwaambia imeshabomolewa kabisa, sijaweza kuokoa kitu chochote hata mita yenu mnayoiulizia mkaitafute kwenye kile kifusi cha nyumba yangu kilichokusanywa na Tanroads. Tanesco walishangazwa sana kuvunjwa nyumba yangu kwa taratibu hizo,” alisema.

“Lakini naamini kila kitu kinatokea kwa sababu maalum. Nimejifunza kumtegemea Mungu na kumshukuru kwa kila jambo, na hili moja ya mitihani ya hapa duniani, nimepokea na kumsikiliza Mungu ana mpango gani juu yetu katika familia yangu mbeleni. Tumelipokea na naamini tutashinda,” alisema zaidi.

Meneja huyo alisema: “Tanroads walitupa taarifa tukatoe mita za umeme, na mara nyingi wanaweza kupiga na tukifika eneo la tukio tunakuta wanaendelea kubomoa nyumba,” alisema na kuendelea:

“Kama nyumba itavunjwa nusu na nusu kubaki tunamrejeshea mita mteja baada ya kujiridhisha kutoka Tanroads, ila kama inavunjwa yote huwa tunawahi kuchukua mita na nyaya zetu na haiamishwi kwenda eneo jingine hata akijenga nyumba kwingine.”

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

JE Una Tatizo la Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kushinwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo?

0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇 Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. @natural beauty pro. Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-

1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.VIG RX CREAM-Ni dawa mpya ya kuongeza maumbile inayoongeza hadi nchi 7.5 inapatikana kwa @200,000/= 3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @150,000/= KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- @natural2162 @natural2162 @natural2162 

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0759029968 na 0659618585 

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

Godbless Lema Adai Gari lake Limechomolewa nati 13 na Watu Wasiojulikana

0
0
Gari la Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema  limechomoka matairi leo Jumatatu baada kudaiwa kuwa limefunguliwa nati 13 kati ya 20 na watu wasiojulikana.

Lema amesema walikuwa wamepanga na Mbunge wa Arumeru Mashariki(Chadema), Joshua Nassari kuondoka na gari hilo jana usiku kuelekea Dar es Salaam kuwasilisha ushahidi wa tuhuma za rushwa za madiwani waliohama Chadema.

Hata hivyo amesema majira ya mchana alipokuwa na gari alihisi mlio kwenye tairi ndipo alikwenda kuliegesha hoteli ya Equator.

Amesema kutokana na kulitilia shaka gari aliomba lifti kwenye gari la Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli, Isack Joseph kwenda naye Dar es Salaam.

"Asubuhi leo (Jumatatu) nikamtuma dereva wangu akachukue gari Equator hoteli alipeleke gereji na baada ya kutoka mita chache tairi zilichomoka," amesema.

Amesema tayari amemuagiza dereva kwenda kutoa taarifa polisi lakini ameiomba kampuni ya  ulinzi ya inteligence inayolinda nyumba yake kufanya uchunguzi kubaini watu walioingia ndani na kufungua nati.

"Pia nimeomba wataalam kupitia kamera za nyumbani kwangu kuona kilichotokea kwani kuna uwezekano wa watu kuingia ndani kufanya uhalifu huo.”

Wanawake wa Kichagga na Kihaya Mtatumaliza Wanaume

0
0

Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Wanawake wa kichagga na kihaya wanatumalizia ndugu zetu. Yaani hawa wanawake ni so strategic, wananyatia wanaume (hata simba na ufundi wake wa kuwinda hawafikii) wenye mafanikio au dalili ya kufanikiwa tu! Wanaume waliosoma, wenye hela au biashara kubwa kubwa. Mbaya zaidi wakishaolewa wanawaendesha hao wanaume mpaka wengine wanakufa vifo vya ghafla kama vile kwa presha! Mrengo wao kimaisha ni kujenga kwao.

Ndugu zangu na rafiki zangu asilimia kubwa wenye mafanikio na elimu wote wameoa wachagga au wahaya, yaani badala ya kuwapenda hawa wanawake kwa sababu ni shemeji zangu, badala yake sina amsha amsha nao kabisa. Mwaka jana kulikuwa na harusi kama 18 hivi ambazo nilihusishwa kwa sababu ya ukaribu au undugu, yaani kati ya hizo 16 mchagga au mhaya anaolewa! Niligoma mgomo baridi, vikao wala michango sikutoa! Mbaya zaidi kuna jamaa nimesom naye UDSM rafiki wa damu, tuliapa viapo vyote, tukae mbali na wanawake wa kichagga na kihaya, cha ajabu juzi ananitumia ujumbe wa simu kuwa anaoa na nilivyohoji shemeji ni wa wapi, akaniambia mchagga. Yaani anamezwa na zimu tulilolikwepa kwa zaidi ya miaka kumi!

Wakuu hii hali ikoje kwa jamaa/ndugu zenu? Wanawake wa kihaya na kichagga muwe na uungwana japo kidogo.

By Simplicity.

Mwanamuziki Maua Sama Afunguka Kuhusu Kuolewa

0
0
WIKI chache baada ya kuchumbiwa na Mzungu, staa wa Muziki wa R&B, Maua Sama amefunguka kuwa ataolewa mwakani.

Akichonga na Over Ze Weekend, Maua alisema kuwa kila kitu kinakwenda kwa utaratibu wake na kwamba suala la ndoa huenda likawepo mwakani na siyo mwaka huu.

“Bado sana mipango ya ndoa labda mwakani. Sasa hivi naangalia muziki zaidi na nashukuru nimeweza kukaa kwa muda mrefu bila kuchuja na hii ni kutokana na msanii unavyojiweka,” alisema Maua.

Imelda Mtema | Ijumaa Wikienda

Kijana Ukitaka Kuoa Tafuta Mwanamke Mwenye Nyota..Mengine ni Mbwembwe tu..

0
0

Kuna kitu kipo lakini watu hawajui au hawjawahi kukifikiria!! Nacho ni Nyota ya mwanamke!!
Leo nimeambiwa kisa kimoja ambacho kimelipua mawazo yangu yaliyolala kwa kitu ambacho nilikuwa nakiona

STORY
Kuna jamaa yangu anataka kuoa mke wa pili baada ya kuombwa na mke wa kwanza afanye hivo!!Jamaa kamuoa mke wa kwanza miaka michache iliopita na alikua mambo safi kwa sababu bahati ya hela anayo!! Ila baada ya kumuoa bidada mambo mengi yakawa yanadolola na ameshuka kawa kapuku kila analofanya linabuma!!

Sasa Siku chache zlizopta mke wake huyo kamshauri aongeze mke mwingine labda yeye hana nyota ya mafanikio!! Kwani toka waoane mambo ndo yamekua upside down!!"

Hapo ndipo nilpokuja kukubali Yale ambayo nimewashuhudia kuna baadhi ya wanawake ukiwa nao tu mambo yanakuwa yanakunyokea sana hadi unahisi tofauti ( imenitokea)

Pia kuna jamaa mwingine alioa mwanamke mambo yakawa yananyokaa alipomuacha mambo yake yakawa hayaendi walivorudiana nae mambo yakawaka tena!!

Nilishasikia hata mahubiri ya dini nanukuu "kama Kijana unahangaika kufanikiwa hufanikiwi basi subiri ukioa hapo nyota yako yaweza ng'arishwa"

HITIMISHO
Mwanamke utae muoa ndie anadetermine nyota yako ing'ae,au ififie

Prof. Kitila: Wizara yangu itamsaidia Rais Magufuli kupata kura nyingi bila kampeni katika uchaguzi wa 2020

0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo ameahidi kuwa wizara yake itakuwa mfano bora wa kumsaidia Rais John Magufuli ili apate kura za kutosha bila kufanya kampeni mwaka 2020.

Profesa Mkumbo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wawakilishi wa viongozi wa mamlaka 19 za maji kuhusu mipango mbalimbali ya kuboresha sekta ya maji nchini.

Amesema ahadi yake haitakwenda bure kwani mwaka 2020 Rais Magufuli ataanzia Dar es Salaam hadi Kigoma akipunga mkono tu bila kusema neno lakini kura zitakuwa za kishindo.

Katibu huyo amesema Wizara ya Maji ndiyo kila kitu kwani inawagusa wananchi wa hali ya chini na juu na ndiyo maana kuna ulazima wa kuwa na usimamizi wa kutosha.

Kutokana na hilo Profesa Kitila amekemea tabia ya vyama vya wafanyakazi kutengeneza majungu ya wivu na kugeuza mamlaka za maji kuwa vichaka vya majungu na umbea ambapo matokeo yake ni kuumiza na kuwabambikizia tuhuma viongozi wakiwemo wakurugenzi wa mamlaka hizo.

Amewataka wafanyakazi kupigania haki zao huku wakitimiza wajibu wao kwani bila wao kufanya kazi kwa tija hawawezi kuwa na haki ya kudai maslahi bora.

Katibu wa kikao hicho Robert Chilewa amesema mamlaka hizo zimekuwa na changamoto kubwa kutokana madeni yanayofikia Sh 15 bilioni kutoka taasisi na mashirika ya umma.

Amesema mamlaka zimeanza kuyumba kwa utendaji kazi kutokana na kuondolewa kwa watumishi wasiofikia elimu ya kidato cha nne ambao walikuwa nguzo imara huku Wilaya ya Wanging'ombe anakotoka Waziri wa Maji ikiwa na watumishi asilimia 72 wote wa darasa la saba na akamwomba Profesa Kitila awasaidie watumishi hao warudishwe kazini.

CHANZO: Mwananchi

Pendeza na Products za Kessy...Kutengeneza Shape, Kutoa Mvi na Mengine

0
0
PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA🌺🍌🍍
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/🍍🍉🍊                                                                                     TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM                                         (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO,

Nuh Mziwanda amesema kwa sasa hataki kabisa kusikia suala la mapenzi.

0
0

Msanii wa muziki Bongo, Nuh Mziwanda amesema kwa sasa hataki kabisa kusikia suala la mapenzi.



Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Bao la Ushindi’ ameiambia FNL ya EATV kuwa kwa sasa anajielekeza zaidi katika kazi na si vinginevyo.

“Sasa hivi sipo kabisa katika suala la mapenzi, kama nina ganzi, sasa hivi na-relax kidogo nafanya kazi, yeah! wanawake wapo ila akitoea yule ambaye nahisi Mungu amenileta fresh,” amesema Nuh.

Alipoulizwa iwapo ana mipango ya kuja kuoa siku za mbeleni baada ya hivi karibauni ndoa yake kuvunjiaka alisema itatengemea kwa sababu yeye ni binadamu pia.

“Pia mimi ni mtoto wa kiume na ndoa ni jambo jema kwa hiyo siwezi kusema sitakuja kuoa kwa sababu huwezi kujua nini kitatokea mbele yangu,” amesema.

Nuh Mziwanda ambaye ana historia ya kuwa katika mahusiano na msanii Shilole mwaka huu ameachana na aliyekuwa mke wake wa ndoa ambaye pia walijaliwa kupata mtoto mmoja.

Maskini..Mtoto Aungua Moto Akiwa Amelala

0
0
Mtoto wa miaka miwili wa kike aliyefahamika kwa jina la Brightness Barnabas amefariki dunia akiwa amelala ndani ya nyumba baada ya nyumba kuungua moto kutokana na hitilafu ya umeme mkoani Shinyanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema chanzo cha moto huo ilikuwa ni hitilafu ya umeme.

"Nyumba ya Barnabas Saimoni (35) ambaye ni Msukuma anajishughulisha na kilimo mkazi wa kijiji cha Kakolo iliungua moto na kusababisha kifo cha mtoto binti aitwaye Brightness Barnabas mwenye umri wa miaka miwili" alisema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images