Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Gigy Money Adai Ngoma yake ‘Papa’ ni Kali Kuzidi Seduce Me

$
0
0
 Video Vixen na Msanii Muziki Bongo, Gigy Money amedai kuwa ngoma yake Papa ni nzuri kuzidi ngoma ya Alikiba Seduce Me.

Akizungumza na Planet Bongo ya EA Radio amesema ngoma yake kwa sasa ina miezi minne na bado inaendelea kufanya vizuri kitu ambacho anaamini ni kutokana ukali wake.

“Papa ni kali kuliko Seduce Me sema Alikiba ni msanii mkubwa na watu walimmiss sana, huwezi kusikiliza Seduce Me zaidi ya mara tano lakini Papa unaweza kusikiliza siku nzima” amesema Gigy Money.

Wimbo wa Gigy Money ‘Papa’ hadi sasa una views 381,008 katika mtandao wa YouTube wakati ule wa Alikiba ‘Seduce Me’ uliotoka August 25 una views milioni 6.3.

Paul Makonda Ajibu Baada ya Kutajwa Mfano wa Kuigwa na Rais Magufuli

$
0
0
Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kutaka Wakuu wa mikoa wengine kuiga utendaji kazi wa Paul Makonda ambaye ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam. Mkuu wa mkoa huyo amemshukuru Rais Magufuli na wananchi wa Dar es salaam kwa kumpa ushirikiano.



RC Makonda ametoa shukrani hizo leo, kupitia ukurasa wake wa instagram huku akitaka pongezi za Rais Magufuli ziwaendee wale wote waliomuunga mkono.

Utukufu na heshima apewe Mungu aketie mahali patakatifu.Asante sana Mh Rais asante watumishi wa Mkoa wa Dar es salaam. Asante sana wadau na Wananchi wote wa mkoa wa Dar es saalam kwa mshikamano wenu,Upendo wenu na Umoja wenu katika kuleta maendeleo ya mkoa wa Dar es salaam.Pongezi za Mh Rais ziende kwenu nyote mnaoendelea kuunga mkono Kwa hali na mali maendeleo ya Mkoa wa Dar es salaam.

Soma Nafasi za Ajira zilizotangazwa Leo

$
0
0

Breaking News:Mwimbaji Maromboso wa Mkubwa na Wanawe Ajiunga WCB ya Diamond Platnumz

$
0
0
Breaking News:Mwimbaji Maromboso wa Mkubwa na Wanawe Ajiunga WCB ya Diamond Platnumz
Ikiwa leo ni siku ya Kuzaliwa ya Mwimbaji Maromboso wa Mkubwa na Wanawe Diamond Platnumz ametoboa siri ambayo wengi tulikuwa hatuijui, Akimtakia siku ya kuzaliwa Diamond Platnumz ameandika haya:

"DiamondplatnumzHappy birthday @mbosso_ words can't Express how big fan of yours i am.... i can't wait, to officially introduce you as the Member of @wcb_wasafi Artists & Family.... i can't wait for the world to hear the special and unique Talent that you have, that makes me be your Number One fan...... Happy Birthday Young Khan" Diamond Platnumz

Jack Wolper Hana Bahati...Penzi lake na Kiben Ten Brown Laota Mbawa...

$
0
0
Duniani kuna mambo, Ile couple ya Amber Rose na 21 Savage ya Bongo inayomuhusu muigizaji wa filamu  Jackline Wolper na Brown dezaini kama limekufa hivi.

Wawili hao ambao walionekana wakiwa wameshibana kimahaba sasa kunonyesha kama kuna hali ya kutokuwa sawa hii ni kutokana na kuwa  mrembo Wolper hakuonekana na mpenzi wake huyo aliyerithi mikoba ya Harmonize,  katika private party ya Diamond Platnumz usiku wa Jumatatu(02/10/2017) katika hotel ya Hyatt Regency.

Pia ukiitazma akaunti ya mtandao wa kijamii wa Instagram, ya Bff wa Wolper  amemu-unfollw mrembo huyo na kufuta picha zote walizowahi kupiga pamoja  ama kumpost.

Pendeza na Products za Kessy...Kutengeneza Shape, Kutoa Mvi na Mengine

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA🌺🍌🍍
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/                                  TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM                      (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO,

Nimemkuta Mpenzi Wangu Anafungasha Manii zangu Anataka Kuondoka Nazo

$
0
0
Nina mpenzi wangu ni mwezi sasa toka tumejuana, jumapili tulipanga kukutana kufanya yale mambo yetu basi tukameet cha kushangaza baada ya kumaliza akaomba kuondoka basi nikwamwambia tukaoge kwanza. Tulipomaliza kuoga yy katangulia kutoka mm nikabaki nafuta futa mwili kdg, ile narudi namkuta anafunga zile condom zenye manii anataka kuweka kwenye mkoba wake. Asee nilishikwa na butwaa, nikajaribu kumuuliza anapeleka wapi akasema alitaka akatupe nje cuz hapendi kuziacha hotel.

Basi nikiwaza nikajaribu kufikiria kuna siku aliwahi kuniambia habari za kichawichawi nikamwambia azirudishe kwenye kile kidust bin. Usiku nikampgia simu nikajaribu kumuuliza kwa upole aniambie ni wap alikua anapeka akanijibu jibu lile lile. Basi nikaamua kumchunia nikidhamiria kumuacha sasa jana akaomba tukutane nikagoma, usiku akanipigia simu siku analia eti anasema alinipenda sana alitaka nimuoe na zile manii kuna rafiki zake wa kazini kwao ndio walimwambia kuna mganga anaweza anaweza kunifanya nimuoe kama atawapelekea zile manii.

Wakuu ni mara ya pili tumefanya hili tendo sasa sijui ile siku ya kwanza napo aliondoka nazo, huyu binti ni mnyamwezi wa huko tabora naogopa sana atakua anataka kuniloga. Nimewahi kumpeleka home kwangu mara moja but nashangaa alikua anainsist tukafanyie hili tendo hotel.

Naombeni mwenye kuelewa hili ananipe ushauri, nimeshindwa kuomba ushauri kwa watu cuz limekaa kiaibu aibu sana.
Asante.

Nuh Mziwanda Aitamani Ndoa ya Mr. Blue na mkewe

$
0
0
Msanii wa bongo fleva Nuh Mziwanda ameibuka na kusema kwamba hana mpango wa kurudi nyuma na kurudiana na aliyekuwa mke wake Nawal kwa kuwa bado ana utoto mwingi, na kusema kwamba anayatamani maisha ya ndoa ya Msanii Mr. Blue na mkewe

kwani wanaheshimiana
Nuh amelazimika kusema maneno hayo baada ya kukubali kufunguka juu ya kuachana na mke wake ambaye pia ni mama wa mtoto wake na kusema kwamba mke wake huyo bado ana akili za kitoto sana na  ndizo zilizompelekea  kupiga picha na mwanaume mwingine na kudai amefunga ndoa kisha kuwatumia marafiki zake, kitu ambacho amedai mke wa Mr. Blue hana mambo hiyo
"Mimi naangalia sana maisha ya Mr. Blue na mke wake, Mke wa Byser hana michongo hii.

Wanaheshimiana  lakini mimi na sijui nimemkosea wapi Nawal na kusema kama ningekuwa nimemkosea angeniambia hata chumbani. Nashangaa kwa nini tulidumu kwenye uchumba halafu kwenye ndoa ndiyo tusidumu. amesema

"Nawali bado ana utoto mwingi sana mpaka sasa hajaamua kuwa mke wa mtu na kumuheshimu mume wake kama mke ninachoamini ni kwamba mungu alimleta Nawal kwenye maisha  yangu kwa ajili ya kuzaa naye mtoto na sio kuishi naye. Kama pia familia yake inaangalia matendo ya mtoto wao akienda kwenye media na kuzungumza vitu visivyokuwa na ukweli basi  familia  inakuwa siyo staha kwani ilipaswa wamshahuri vyovyote "aliongea Nuh.

Aidha Nuh ameongeza  kuwa yeye kuamua kurudi kwenye dini yake aliamua kumpa sababu mke wake ya kuachana kwani alikuwa akihangaika kutafuta sababu kwa muda mrefu hadi kuchangia kutokuwa na amani.

"Mke wangu alikuwa akitafuta sababu za kuachana na ndiyo maana niliamuakurudi kwenye dini yangu. Yeye sasa hivi kusema hajaolewa ni 'Too Late' kwani siwezi kurudi nyuma. Mama yangu na muziki wangu ndiyo vinanifariji sana. Mke mwema nitaletewa ambaye nikimkosea ataniambia na tutavumiliana ili maisha yaendelee

Rais Magufuli Ataja Mshahara wake kwa Mwezi

$
0
0
Rais  Dk. John Magufuli amesema tangu alipoingia madarakani hajapandisha mishahara ya watumishi wa umma na  hatapandisha kwa sababu  anawatumikia Watanzania kwanza.

Kauli hiyo aliitoa   Dar es Salaam jana alipofungua Mkutano Mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) ambao uliwakutanisha mameya na wenyeviti wa halmashauri nchini.

Rais Magufuli alieleza umuhimu wa ALAT katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM na mikakati yake kwa Watanzania.

Aliahidi kushughulikia changamoto za uhaba wa watumishi katika halmashauri na ucheleweshwaji wa ruzuku ya miradi ya maendeleo.

Aweka wazi mshahara wake
Katika mkutano huo, Rais Magufuli pia alitaja mshahara wake anaolipwa kuwa ni Sh milioni tisa kwa mwezi.

“Watu walikuwa wanafanya ‘board meeting’ Dubai na wakienda kule wanapandisha mshahara mpaka Sh milioni 40, mimi mshahara wangu ni Sh milioni tisa. Naeleza ukweli. Watu walikuwa wanafanya kufuru,” alisema.

Akihutubia kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika mkoani Kilimanjaro, Mei Mosi mwaka huu, Rais Magufuli aliahidi nyongeza ya kawaida ya mishahara na kuwapandishia madaraja wafanyakazi wanaostahili.

“Watumishi 9,932 walikuwa na vyeti feki, watumishi hewa walikuwa 19706, hivyo kama Serikali ingeongeza mishahara ina maana watumishi hawa pia wangefaidika na fedha ambazo hawakustahili kuzipata,”  alisema Rais Magufuli.

Pia alisema wafanyakazi 12,000 ‘waliotumbuliwa’ kwa vyeti feki hawawezi kumpenda na ndiyo maana wanapiga kelele kupitia mitandao ya  jamii kwa sababu  naye hahitaji kupendwa nao.

“Watu 12,000 waliotumbuliwa kwa vyeti feki hawawezi kunipenda na hao ndiyo wanaopiga kelele kwenye mitandao huko. Tanzania ina watu milioni 52 sasa hawa (12,000) hata hawanisumbui, nikiwaona ‘I just enjoy them’ hata sishtushwi na wanaolalamika.

“Ukimtumbua mtu jipu hawezi kufurahi akipona ndiyo ataanza kuelewa,”alisema.

Pensheni za watumishi hewa
Rais Magufuli aliagiza Sh bilioni 38 zilitokana na waliokuwa watumishi hewa zirudishwe serikalini.

“Zile pensheni zote za watumishi hewa zirudishwe serikalini, Sh bilioni 38 zirudishwe serikalini. Likizo hewa, likizo za uzazi hewa. Tunachukua hatua lakini ni kwa Taifa la Watanzania. Tulikuwa tunaenda kubaya, kuzimu,” alisema.

Benki Ufisadi
Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli alisema kulikuwa na benki moja   nchini ambayo ilipata hasara ya asilimia sita na hata ilipoongezewa fedha ilipata hasara zaidi.

“Ikapata hasara zaidi ikaongezewa hela sasa ikapata hasara ya asilimia 11 ikaongezewa hela ikapata hasara zaidi asilimia 22. Sasa tumeifunga.

“Watu kama hawa hawawezi kutupenda na mimi sitaki wanipende ilimradi napendwa na watanzania. Sikuja kuuza sura, nimependwa na mke wangu inatosha,”alisema.

Alisema kuna  benki makao makuu yake yalionekana Dar es Salaam lakini imefunguliwa Marekani na   hata wataalamu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) hawakuligundua hilo.

“Kuna benki makao makuu yake yako Dar es Salaam lakini ikafunguliwa kule Marekani. Wataalamu wa BoT hawakugundua haya na fedha ambayo ipo kwenye hiyo benki haizidi asilimia tano,” alisema Rais Magufuli.

Pembejeo hewa
Alisema kwenye halmashauri 140, kulikutwa na pembejeo hewa za kilimo zenye thamani ya Sh bilioni 57.9.

“Hata Chato kwetu kulikuwa na huu uozo pembejeo hewa za thamani ya Sh bilioni 1.5.

“Wanafunzi hewa 65,000 kutoka elimu ya msingi mpaka chuoni. Wanafunzi hewa wanaopokea mikopo walikuwa 8500.

“Ungekuwa mimi umekuta li-Tanzania liko hivi, uozo kila kona ungefanyaje? Ningekuwa Mhehe ningejinyonga, ningesema “Swela,”  alisema.

Alisema wakati anaingia madarakani alikuta mikoa mingi inasumbuliwa na kipindupindu lakini baadaye yalipelekwa madawa.

Pia alisema   bei ya mbolea ya kupandia imeweza kushuka, mathalani katika Mkoa wa Lindi kutoka Sh 100,00 hadi  Sh 51,000.

Alisema wapo watu ambao wanalalamika fedha imepotea na kwamba wanaolalamika ni wale ambao walizoea vya bure.

“Apartment zilikuwa zimepangishwa mtu ana washikaji 10 na wote anawatunza, wengine hadi baa walikuwa wanalipia viti kwamba kila siku lazima akae hapo. Watumishi wengine walikuwa wanasafiri kila wiki, wanabadilishana mabegi pale airport,”alisema Magufuli.

Waziri Ndalichako Aanika MADUDU Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)

$
0
0
Serikali  imeeleza kwamba matatizo ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ni kulipwa kwa wanafunzi hewa, ubadhirifu wa fedha na kuwepo kwa watendaji wanaohusika kuweka fedha za wanafunzi wanne kwa mwanafunzi mmoja.

Kadhalika imeeleza tabia ya HESLB kujiona ‘Mungumtu’, kuwaona watoto wa Watanzania kama ni shida kwao na wasiostahili kupewa mikopo na hata kuwa na majibu ya mkato yasiyokuwa na chembe ya kazi ya utoaji huduma.

Waziri wa Elimu, Sayansi ya Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako  alisema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizindua Bodi mpya ya HESLB na kuitaka kujitenga na menejimenti wakati wa utekelezaji wa majukumu yake na kuhakikisha matatizo hayo yote ambayo yapo katika taarifa aliyowakabidhi, yanakaguliwa upya, kuhakikiwa na kufanyiwa kazi.

Pia alisema taarifa hiyo imeambatanisha taarifa ya fedha za HESLB zilizochezewa.

Alikabidhi taarifa hiyo kwa Makamu Mwenyekiti wa bodi mpya, Madina Mwinyi akiagiza ifanyiwe kazi kuhakikisha na kujiridhisha pamoja na kuwajua wadeni wa HESLB huku ikiepuka kuiamini menejimenti kama ilivyokuwa kwa bodi ya awali badala yake kuisimamia.

“Ninakabidhi taarifa yenye changamoto za Bodi ya Mikopo kwenu Bodi ya Wakurugenzi ambayo inaainisha uwepo wa wanafunzi hewa na ambao wanalipwa mikopo wakiwemo waliomaliza au kuacha chuo,” alisema.

Pia alisema taarifa hiyo inahusisha kuwepo kwa watendaji wanaohitajika kujieleza ambao walikuwa wakiweka fedha za wanafunzi wanne kwa mwanafunzi mmoja ambapo ushahidi upo na eneo hilo bado kuna shida.

Kadhalika, aliiagiza Bodi mpya kutazama upya na kujiridhisha kuhusu vigezo vya utoaji mikopo kwani kumekuwa na matatizo, na hata kutizama utoaji wa mikopo kama taratibu na sheria zinazingatiwa.

“Malalamiko ya Bodi ya Mikopo yapunguzwe ama kuondolewa kabisa ili kukidhi matarajio ya wadau wa elimu nchini, endeleeni kukagua na hata majina ya wanaohitajika kupata mikopo kabla ya kutolewa rasmi,” alisema Profesa Ndalichako.

Kuhusu Bodi mpya aliitaka isimamie zaidi urejeshwaji wa mikopo kwani hadi sasa serikali imetoa Sh trilioni 3.1 tangu kuanzishwa kwa bodi, lakini ni Sh milioni 217 pekee zilizorejeshwa huku Sh bilioni 588 zikiwa zimefikia muda wake zikitakiwa kulipwa.

 Akizungumza baada ya bodi hiyo kuzinduliwa, Makamu Mwenyekiti, Madina Mwinyi alisema katika kufanyia kazi changamoto za HESLB wataanza kwa kujipanga wao wenyewe katika taasisi wanamotoka ili kila mmoja kujua ni kiwango gani cha mikopo kinachotakiwa kurejeshwa.

Kadhalika alisema bodi hiyo itahuisha taswira ya HESLB pamoja na kuiaminisha jamii kuwa suala la mkopo wa elimu ya juu ni lazima kurejeshwa kwa wakati.

Wajumbe wa bodi hiyo na taasisi wanazotoka katika mabano ni Profesa Caroline Nondo (Mwakilishi kutoka Tume ya Vyuo Vikuu), Susan Urio (Mwakilishi wa Wanafunzi), Madina Mwinyi ambaye ni Makamu Mwenyekiti (Mwakilishi wa Wizara ya Elimu Zanzibar).

Wengine ni pamoja na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Gerson Mdemu (Mwakilishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali), Dk Dalmas Nyaoro (Mwakilishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia), Frank Mgeta (Mwakilishi wa Wizara ya Fedha na Mipango), Dk Francis Masika (Mwakilishi wa Baraza la Elimu ya Ufundi) na Mjumbe mmoja ambaye ni Mwakilishi wa Wizara ya Fedha Zanzibar hajateuliwa.

Nassari:Hakuna Dhamira ya Dhati ya Kuchunguza Shambulio la Tundu Lissu

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joshua Nassari ameeleza kuwa vyombo vinavyohusika na uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu havina dhamira ya dhati ya kuufanya uchunguzi huo.

Nassari ameongea hayo kufuatia na kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kusema kuwa, Tundu Lissu atakuwa msaada mkubwa katika upelelezi wa tukio hilo pale atakaporudi nchini.

“Mtu ameshambuliwa yuko kitandani, hatujui atapona siku gani, hatujui atarudi lini nchini, hatujui atarudi katika hali gani, eti wanamsubiria aje kufanya upelelezi. Akirudi baaada ya miaka miwili?”

“Na huo Upelelezi utakaokuja kufanyika baada ya miaka miwili ni upelelezi wa aina gani!…. Kwa hiyo mimi nafikiri dhamira ya dhati haipo,” alieleza Joshua Nassari.

Alieleza kuwa amesikitishwa na kitendo cha waziri anayesimamia wizara nyeti nchini kusema kuwa, wanamsubiri Tundu Lissu apone ndipo uchunguzi uendelee.

“Waziri huyo huyo amezungumza kwamba wanamsubiri Tundu Lissu apone ili aweze kuwasaidia kufanya upelelezi. Tundu Lissu angekufa maana yake upelelezi usingekaa ufanyike?” alihoji Nassari.

“Nilipomsikia Mwigulu akiongea nikiwa Nairobi, nilisikitika kidogo kwa sababu ni kijana msomi na mtu wa umri mdogo ambae anajua teknolojia zilizopo duniani kwa sasa hivi. Kwa hivyo ni aibu kusema kwamba watafanya upelelezi kwa vyombo vya ndani na wanamsubiri Tundu Lissu apone ndipo aje awasaidie kufanya upelelezi.”  aliongeza.

“Angekufa maana yake upelelezi usingefanyika. Kwa maana hiyo watanzania hatuko salama…”

Tunafanya Haya Kutengeneza Tanzania Mpya- Rais Magufuli

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. John Pombe Magufuli amesema serikali ya Tanzania imenunua ndege sita ikiwepo ndege moja yenye uwezo wa kutoka Dar es salaam hadi Marekani moja kwa moja na ndege hizo zitakuja mwakani 2018, huku akiwataka watanzania kuunga mkono juhudi zake kwani anafanya hivyo kwa ajili ya kutengeneza Tanzania mpya.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. John Magufuli

Rais Magufuli amesema hayo kwenye Mkutano wa 33 wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) ambao umefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

“Tumenunua ndege sita ndege mbili zimeshawasili Tanzania, lakini ndege zingine ikiwepo Bombardier zitawasili mwakani 2018 mwanzoni. Tunafanya haya kwa ajili ya kutengeneza Tanzania mpya, nchi ambazo zina ndege zake idadi ya watalii wanaoingia kwenye nchi hiyo ni kubwa zaidi, nchi yetu ni ya pili kwa kuwa na vivutio vingi duniani lakini idadi ya watalii wanaoingia ni ndogo kutokana na kukosa ndege zetu”amesema Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine Rais Magufuli amewaonya watumishi wa umma wakiwemo wakurugenzi wenye tabia za ulevi na kuwambia waache tabia hiyo mara moja kabla ya kuwatumbua.

Makonda Ameondoa Uhalali wa Rais Kusimamia Matendo yake..Chadema Wafunguka

$
0
0
Chama cha Demokrsia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kwamba, Rais Magufuli amepoteza uhalali wa kusimamia kile alichokifanya kipindi cha nyuma baada ya kumtetea kiongozi anayedaiwa kuwa ameghushi vyeti.

Tamko la CHADEMA limekuja ikiwa ni saa chache tangu Rais aliposema kuwa, baadhi ya watu wanasema kuwa Makonda hajasoma, lakini kwake hata kama hajasoma na hajui A lakini anakamata dawa za kulevya, huyo ni msomi mzuri.

“Je! Rais anajua kuwa kauli yake ya leo (jana) kuonesha kuwa ‘vyeti’ si suala muhimu, ameondoa uhalali wowote ule uwe wa kisheria au wa kisiasa wa agizo lake la kuwafukuza watumishi wale waliodaiwa kutokuwa na vyeti?” walihoji CHADEMA katika taarifa yao walioitoa jana.

CHADEMA wamesema kuwa, miezi kadhaa iliyopita kinyume na sheria na taratibu, Rais aliagiza kuondolewa kwenye utumishi wa umma watumishi zaidi ya 9,000 baada ya kudaiwa walikuwa na vyeti vya kughushi, lakini leo anasimimama na kuonyesha kuwa, suala la vyeti si la msingi kama mtu anaweza kufanya kazi.

Aidha, wamehoji kama kweli Rais Magufuli alimaanisha aliposema kwamba serikali yake haitalea vilaza (watu wasio na sifa stahiki) alipokuwa akizungumzia sakata la wanafunzi waliodahiliwa kusoma programu maalum ya ualimu katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

“Je! Rais Magufuli anajua kuwa kauli yake ya leo (jana) inaonesha kuwa hakuwa na nia ya dhati kupinga ‘vilaza’ kwenye serikali yake? Na kwamba hakuwa mkweli kwa sababu wapo vilaza anaowatetea?

Baada ya madai ya utata wa majina anayotumia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaama na elimu yake kutopatiwa majibu wala ufafanuzi, Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob, alifungua shauri mbele ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, ili mamlaka hiyo ishughulikie suala hilo kwa kadri ya sheria za nchi na kumaliza utata uliopo.

CHADEMA wameeleza kuwa kauli ya Rais Magufuli inaingilia shuari hilo ambalo bado halijapatiwa ufumbuzi na kwamba inaiweka Sekretairieti ya Maadili katika wakati mgumu.

Katika taarifa yao, CHADEMA wameonyesha kushangazwa na kauli ya Rais Magufuli kuwa hajapandisha na wala hatopandisha mishahara ya wafanyakazi kwani bado anayokazi kubwa ya kuwaletea wananchi maendeleo, lakini kwenye sherehe za Mei Mosi, Rais aliahidi kuwa katika bajeti ya 2017/18, kungekuwa na nyongeza ya mishahara ya watumishi.

Hata hivyo, CHADEMA wamemkumbusha Rais kwamba, amekuwa akisema yeye ni mtetezi wa wanyonge, ni vyema akajua kuwa miongoni mwa wanyonge ni pamoja na wafanyakazi hao wanaoomba kuongezewa kima cha chini cha mshahara.

By Swahili Times

ACT Wazalendo Wamjibu Magufuli Kuhusu Mishahara...Wadai Imesikitishwa

$
0
0
CHAMA cha Act-Wazalendo kimesikitishwa  na kauli ya Rais Magufuli aliyoitoa jana kwenye ufunguzi wa mkutano wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) kuhusu mishahara ya wafanyakazi aliposema  alipoingia madarakani hakusema ataongeza mishahara kwa vile hakuchaguliwa kuongeza mishahara na kwamba ana jukumu la kuwahudumia wananchi.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi ACT Wazalendo,  Ado Shaibu, alisema:

“Swali la kujiuliza baada ya kauli hiyo ni, je, wafanyakazi wa Tanzania wanastahili kufanyiwa hivi na serikali wanayoihudumia? Jibu bila shaka ni hapana.  Serikali inatoa wapi ujeuri wa namna hii dhidi ya wafanyakazi nchini wakati kiuzalishaji na kimapato inawategemea wafanyakazi?
“Licha ya mchango wao madhubuti katika ujenzi wa taifa kwenye sekta mbalimbali, kwa utumishi wao wa kutukuka, ukweli wa mambo ni kuwa wafanyakazi ndiyo wanaochangia zaidi mapato ya serikali kuliko waajiri wao.
“Kwa mfano, kitabu cha mapato cha mwaka 2016/17 kinaonyesha kuwa wafanyakazi wote wa sekta ya umma na sekta binafsi watachangia jumla ya Sh. Trilioni 3 kwenye mapato yote ya serikali kulinganisha na wenye mitaji (waajiri) ambao watachangia jumla ya shilingi bilioni 900 tu kutoka kwenye kodi za faida/gawio, ongezeko la mitaji na riba.”
“Ni kwa nini serikali inawadharau na kuwahadaa wafanyakazi?   Wakati wa kampeni za kugombea urais, Magufuli alijipambanua mbele ya Watanzania kuwa akichaguliwa kuingia madarakani, serikali itahakikisha kuwa inasimamia maslahi bora ya wafanyakazi ikiwemo mishahara bora,” alisisitiza.

BREAKING NEWS: Mbunge Nasari Arudi Tena TAKUKURU

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari akiwasili Makao makuu ya Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Jijini Dsm, kuendelea mahojiano ya kile wanachokiita ushahidi wa Picha za Video zilizonaswa zikionesha Jinsi madiwani wa CHADEMA katika baadhi ya kata Mkoani Arusha walivyorubuniwa kwa Pesa ili kujivua kujiuzuru na kujivua Uanachama.

TTCL Yaomba Radhi Kufuatia Ujumbe Tata Ulioonekana Kwenye Ukurasa wake wa #Twitter

$
0
0
TTCL yaomba radhi kufuatia ujumbe ulioonekana kwenye ukurasa wake wa #Twitter mapema leo asubuhi.


Mahakama Yakwama Kutoa Uamuzi Kesi ya Wema Sepetu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imekwama kutoa uamuzi wa ama kupokea au kutopokea kielelezo cha hati ya ukamataji mali nyumbani kwa Wema Sepetu katika kesi ya kutumia dawa za kulevya kwa sababu Hakimu hajamaliza kuandaa uamuzi huo.

Uamuzi huo ulitarajiwa utolewe leo October 4, 2017 na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, lakini amesema bado hajamaliza kuandaa uamuzi huo ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi November 1, 2017.

Awali, Wakili wa Wema, Peter Kibatala aliiomba Mahakama isipokee hati hiyo kwa kuwa haikukidhi vigezo.

Mbali ya Wema, washtakiwa wengine ni Angelina Msigwa na Matrida Abbas ambao wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kutumia dawa za kulevya.

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) Kutoa Msimamo wao Kauli ya Rais Magufuli

$
0
0
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), limesema linatarajia kutoa msimamo wao hivi karibuni kufuatia kauli ya Rais Magufuli ya kutoongeza mshahara, mara baada ya vikao vyao na serikali kufanyika.

 Akizungumza na mwandishi wa habari wa East Africa Television, Katibu Mkuu wa TUCTA, Yahya Msigwa amesema wanakusudia kuonana na uongozi wa serikali ili kujadili suala hilo, na ndipo watatoa msimamo wao kama hawatafikia makubaliano mazuri.

“Tunahitaji kuonana na uongozi wa serikali tujadili, kuna mambo mengi ya kujadili sio la mishahara tu, kwa muda mrefu vikao vimekuwa havikaliwi, hata vikikaliwa havina majibu, sasa hivi lazima tulitafutie ufumbuzi kwa sababu changamoto ni nyingi, wafanyakazi hawana hali nzuri kabisa, malalamiko ni mengi mno”, amesema Yahya Msigwa.

Hapo jana Rais Magufuli ametoa kauli ambayo imeibua sintofahamu nyingi kwa wananchi, baada ya kusema hajaongeza mishahara na hatoongoze mishahara kwa wafanyakazi kwa kipindi chote atakachokuwepo madarakani.

Madee Amchana Roma Mkatoliki..Adai ni Muongo Hakwenda Zimbabwe

$
0
0
MSANII wa Bongo Fleva, Ahmadi Alli ‘Madee’ anayefanya vizuri na wimbo wake mpya wa ‘Sema’ ametoa povu juu ya wimbo wa Roma Mkatoliki wa ‘Zimbabwe’ akisema ni mzuri ila haamini kama kweli alienda nchini Zimbabwe kama alivyodai wakati wimbo huo unatoka.

Ameyasema hayo katika kituo kimoja cha radio hapa nchini kuwa kituo cha radio kilijaribu kumhoji Roma mambo kadhaa lakini hakuwa na majibu yenye ushawishi, kitu ambacho kinamfanya kutoamini juu ya safari hiyo.

“Tulijaribu kumhoji juu ya uwanja wa ndege wa Zimbabwe unaitwaje akaingia chocho, hajatutajia hadi leo. Kwa hiyo ni muongo, muongo sana lakini wimbo wake ni mkali kinoma ila yeye simuamini hata kidogo,” alisema Madee na kuongeza:

“Ila la Zimbabwe siliamini, hilo la kutekwa muache mwenyewe, inaweza kuwa kweli au si kweli. Kuna kitu kimoja ananichanganya, yeye kaumia mkono halafu eti anachechemea si uongo huu?” alisema Madee.

Hata hivyo, amesema kuwa muda mwingi yeye na Roma huwa wanapiga stori za kifamilia na utani mwingi, na watu wanapoona kitu chochote kwenye mitandao kati yao wasikichukulie kama kweli kwani huwa ni utani.

NA : SAMSON JEREMIAH/GPL

Duma Afunguka Kufanya Uchafu Hadharani na Irene Uwoya

$
0
0
MUUZA nyago kwenye muvi za Kibongo, Daud Michael ‘Duma’ juzi kati alipobanwa juu ya kufanya uchafu na muigizaji mwenziye Irene Uwoya kwenye muvi ya Bei Kali kwa kunyonyana ndimi na midomo hadharani alisema kuwa huo si uchafu bali walikuwa kazini na walitakiwa kuonesha uhalisia zaidi.


Akipiga stori na gazeti hili, Duma aliendelea kuwa muvi hiyo ni kwa ajili ya watu wazima lakini hata wandani wao, kwa upande wa kila mmoja wao yeye pamoja na Uwoya wanatakiwa kuelewa kwamba pale ni kazini na wawasamehe kwa walichokifanya.

“Kiukweli mimi sioni ubaya wa kilichofanyika pale. Sanaa ni kazi na unapokuwa kwenye scene unatakiwa kuonesha uhalisia zaidi, hicho ndicho kilichotokea na kikubwa muvi ile ni ya watu wazima,” alimaliza Duma.

Stori: UWAZI SHOWBIZ
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images