Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Sababu ya Aslay Kupiga ‘Bandika Bandua’ Katika Ngoma zake

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Aslay ameeleza  sababu ya kutoa nyimbo mfululizo.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Natamba’ ameiambia Planet Bongo ya EA Radio kuwa anataka kuwa na nyimbo nyingi ila anapokuwa anafanya show zake asitumie nyimbo za Yamoto Band.

“Tangu nimetoka kwenye band nimekuwa nikifanya kazi peke yangu natengemea show zangu ziwe na nyimbo zangu tu siyo za Band ndio maana nafanya kutoa nyimbo nyingi ilimradi hata nikipata show niwe natumia nyimbo zangu,” amesema Aslay.
“Kingine natoa kazi nyingi kwa sababu ni nzuri, kazi nzuri ikikaa ndani huwa naogopa kwa sababu naogopa idea kugongana, kazi nuri ukitoa leo nyingine ukatoa kesho watu watapenda tu” ameongeza.

Kwa mwaka huu Aslay amefanya vizuri na ngoma kama Mhudumu, Baby, Angekuona, Tete, Pusha, Marioo, Likizo, Danga na nyinginezo.

DC Kinondoni Atoa Siku Saba Wafanyakazi Walipwe Malimbikizo yao

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapi ametoa siku saba kwa muwekezaji anaemiliki mgahawa wa Tangren uliopo Mikocheni jijini Dar es Salaam kuhakikisha kuwa wafanyakazi wa mgahawa huo wanalipwa stahiki zao za malimbikizo ya muda mrefu.

Akizuungumza jijini Dar es Salaam alipotembelea mgahawa huo DC Hapi  baada kupokea malalamiko kwa wafanyakazi wa mgahawa huo ambao wamedai kutolipwa malimbikizo yao kwa muda miaka kumi, na wamekuwa wakifanya kazi bila likizo wala ‘over time’, DC Hapi ameagiza stahiki zao zishughulikiwe ndani ya siku saba.

Pia DC Hapi ameagiza wafanyakazi hao waunganishwe kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii haraka iwezekanavyo na wapewe mafunzo ya namna inavyofanya kazi.

” Tunapenda sana wawekezaji lakini sio wawekezaji wasiofuata misingi na taratibu na sheria za nchi, namuomba muwekezaji huyu azingatie maagizo niliyotoa vinginevyo tutachukua hatua zaidi” Alsema DC Hapi.

DC Hapi ameeleza kuwa watafanya oparesheni ya kuwafutia leseni za biashara na kuwachukulia hatua wawekezaji wasiofuata sheria na taratibu za nchi, ambapo amesisitiza kuwa haitaji wafikie huko endapo watafuata sheria.

Katika hatua nyingine DC Hapi amewataka wafanyakazi kuwa na nidhamu ya kazi kwa kufanya kazi kwa bidii na kuacha kutoa visingizio visivyokuwa na sababu ya msingi kama walivyo lalamikiwa na mmiliki wa mgahawa huo Liu Deng Wei ambaye ameeleza kuwa wafanyakazi hao wamekuwa wakichelewa kufika kazini na kutoa visingizio visivyokuwa na msingi.

Pia DC Hapi katika ziara yake alitembelea kiwanda cha kutengeneza lifti cha SEC East African kilichopo Masaki na kuutaka uongozi wa kampuni hiyo kuweka mahusiano mazuri na wafanyakazi wao ili kutatua changamoto zinazowakabili.


DC Hapi amewashutumu vikali baadhi ya viongozi kutoka Wizara ya Kazi wanaoshirikiana na muwekezaji kuwanyonya watanzania wanyonge na kuhaidi atazifikisha taarifa kwa mamlaka ya juu wazifanyie kazi.

Paul Makonda Awashukuru Wananchi wa Dar Kwa Kumuunga Mkono Kwa Hali na Mali

$
0
0
Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kutaka Wakuu wa Mikoa wengine kuiga utendaji kazi wa Paul Makonda ambaye ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam,  Mkuu wa mkoa huyo amemshukuru Rais Magufuli na wananchi wa Dar es salaam kwa kumpa ushirikiano katika utendaji kazi za mkoa .

RC Makonda ametoa shukrani hizo  kupitia ukurasa wake wa instagram huku akitaka pongezi za Rais Magufuli ziwaendee wale wote waliomuunga mkono.

“Utukufu na heshima apewe Mungu aketie mahali patakatifu.Asante sana Mh Rais asante watumishi wa Mkoa wa Dar es salaam.

“Asante sana wadau na Wananchi wote wa mkoa wa Dar es saalam kwa mshikamano wenu,Upendo wenu na Umoja wenu katika kuleta maendeleo ya mkoa wa Dar es salaam.
“Pongezi za Mh Rais ziende kwenu nyote mnaoendelea kuunga mkono Kwa hali na mali maendeleo ya Mkoa wa Dar es salaam.”

Pendeza na Products za Kessy...Kutengeneza Shape, Kutoa Mvi na Mengine

$
0
0

PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA🌺🍌🍍
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/🍍🍉🍊                                                                                     TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM                                         (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO,

Timu ya Simba Kiboko...Mwendo wa Ushindi tu

$
0
0
Klabu ya soka ya Simba imeibuka na ushindi kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Dodoma FC uliopigwa leo jioni kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Kikosi hicho ambacho kinajiwinda na mwendelezo wa ligi kuu kimeshuka dimbani leo kuikabili klabu ya Dodoma FC ambapo wekundu wa Msimbazi wameondoka na ushindi wa bao 1-0.

Bao pekee katika mchezo huo limefungwa na kiungo mshambuliaji Said Hamis Ndemla ambaye aliachia shuti kali akiwa katikati ya uwanja baada ya kupokea pasi kutoka kwa Jonas Mkude.

Simba ambayo inaongoza msimamo wa ligi kwa alama 11 itashuka dimbani Oktoba 14 kuvaana na Mtibwa Sugar kwenye mechi ya ligi kuu itakayopigwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Video: Nimeingia TAKUKURU kijasusi nimetoka kijasusi – Joshua Nassari

$
0
0
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari Jumatano hii aliwasili katika Makao makuu ya Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Jijini Dsm, kwaajili ya kuwasilisha ushahidi wa awamu ya pili wa tuhuma zinazo wahusu madiwani wanane waliohama CHADEMA na kujiunga na CCM katika baadhi ya kata Mkoani Arusha.

Mbunge huyo aliwasili Ofisini hapo majira ya Saa Nane kasoro mchana, nakuruhusiwa kutoka majira ya Saa kumi na moja jioni ambapo mbali na kutoa ushahidi huo pia amefungua jarada la kesi zinazowahusu madiwani hao kama alivyoagizwa na mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU, Valentino Mlowola.

Akiwa anaingia ofisini hapo Mbunge Nasari alionekana akiwa ameshika ‘Flash’ na ‘Hard Disk’ ambavyo pia amedai vifaa hivyo alibebea ushahidi wa kutosha

Hata hivyo mbunge huyo amedai kuwa usalama wa maisha yake uko mashakani kulingana na jumbe za vitisho anazopokea baada ya kufichua sakata hilo

 VIDEO:

Mrisho Gambo: Sina Tatizo na Lema ila Inabidi Asome Alama za Nyakati

$
0
0
Mrisho Gambo amefunguka na kusema Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema anapaswa kutambua kuwa yeye kama Mkuu wa mkoa anajishughulisha na matatizo ya watu hivyo kama hatabadili aina ya siasa azifanyazo  basi anapoteza muda wake kwa miaka mitano yote.

Gambo amesema kuwa yeye hana tatizo lolote na Mbunge huyo wa Arusha mjini na kudai kwamba anapaswa kutambua na kubadili aina ya siasa anazofanya kwa kuwa yeye amelenga kutatua matatizo na changamoto za watu wa Arusha Mjini.

"Msuguano na Mbunge haupo lakini anatakiwa tu asome alama za nyakati kwamba Mkuu wa Mkoa wa sasa amedhamiria kuhangaika na shida za watu kama hatalitambua hilo atapoteza muda wake kwa miaka yake yote mitano" alisema Mrisho Gambo.

Aidha Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa yeye kama kiongozi kijana anahitaji zaidi kukosolewa kuliko kusifiwa ili aweze kujirekebisha sehemu ambayo ana mapungufu ili aweze kuwa kiongozi madhubuti na mahiri zaidi.

Imekuwaje Magari Haya Yakafanana 'Plate Number'?

$
0
0
Nimekutana na hizi picha Mtandaoni nikaona sio mbaya nikauliza hili swali...Imekuwaje Magari Haya Yakafanana 'Plate Number?
Je ni Kosa la nani ?


Unapenda Habari za Siasa? Download App ya Mchambuzi Hapa

$
0
0
Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi.....

Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako


Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ????

$
0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM, NAUTALETEWA POPOTE ULIPO TIBA HII

SIMU; NO 0767145357/0629034550.
WHATS APP 0759030343

Manji Kuwashtaki Yono Auction Mart..Adai Hawakufuata Utaratibu wa Kufunga Ofisi za Quality Group

$
0
0
Kampuni ya Quality Group (QGL) limited inayomilikiwa na Yusufu Manji imelaani utaratibu uliotumiwa na kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart kufunga ofisi zake, hivyo inakusudia kuchukua hatua za kisheria.

Ofisi hizo zilizopo jengo la Quality Plaza zilifungwa siku tatu zilizopita kwa madai kuwa inadaiwa na Mamlaka ya Mapato (TRA), Sh12.2 bilioni.

Mshauri Mkuu wa masuala ya sheria wa QGL, Stefano Alderighi alisema jana kuwa haamini kama kamishna wa TRA anahusika katika tukio hilo.

“Yono walipokuja tuliwaomba vitambulisho, lakini walitujibu kuwa hawana na hakuna haja ya kutupa,” alisema Alderighi.

“Hata tulipowaomba kibali cha TRA walituonyesha nyaraka ambazo hazijatiwa saini na kamishna mkuu wa mamlaka hiyo, jambo ambalo linatuaminisha kuwa huenda kamishna hafahamu chochote kuhusu watu hao.”

Alisema QGL inalaani utaratibu uliotumiwa na Yono kwanza kwa kutoonyesha vitambulisho na nyaraka zinazowapa mamlaka na pia kwa kutowapa muda wafanyakazi kuondoka ofisini na vitu vyao binafsi.

“Yono walitumia kama dakika tano tu, waliwalazimisha watumishi wote kutoka nje ya ofisi bila kuwapa muda wa kuchukua vitu vyao. Lakini pia hawakuwaheshimu wageni wa ndani na nje waliokuwa katika kituo cha afya cha kampuni ambacho nacho walikifunga,” alisema Alderighi.

Alisema tayari uongozi wa kampuni umeomba kuonana na kamishina mkuu wa TRA ili kumtaarifu suala hilo na kuomba ushauri wa namna ya kufanya kabla ya kufungua shauri dhidi ya Yono.

Pia alimuomba kamishna huyo kukifungulia kituo cha afya cha kampuni hiyo kwa kuwa hakihusiki na madai hayo ya kodi, lakini pia kwa ajili ya ustawi wa umma.

Hata hivyo, siku ambayo ofisi hizo zinafungwa, mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo alisema wamekuwa na mawasiliano na kampuni ya Farm Equipment ambayo inamilikiwa na Manji tangu Agosti 15, lakini kulikuwa hakuna mrejesho kuhusu deni hilo.

Lakini Alderighi alisema wamewasiliana na TRA kuhusu madai yao mara mbili kabla ya tukio hilo na hata baada ya kufungiwa ofisi, wamewaandikia barua na wataendelea kushirikiana nao.

Akijibu madai hayo, mkurugenzi wa Yono, Consolata Yono alisema wanaongozwa na utaratibu kutoka TRA.

“Ni vigumu kwenda kufunga ofisi ya mtu bila kuwa na nyaraka zote muhimu. Hao kama wanadaiwa walipe tu sio kuanza kusingizia eti wameonewa,” alisema Yono.

Viongozi wa Dini Nchini Wavunja Ukimya, Waeleza Wasiwasi Wao Juu ya Hali inayoendelea

$
0
0
Matukio ya uhalifu yanayoendelea nchini yamewaibua viongozi wa dini ambao licha ya kuelezea wasiwasi wao kutokana na kuongezeka, wameitaka Serikali ibuni mikakati ambayo itamhakikishia kila raia usalama wake.

Wamesema kuna haja kwa wananchi kuhakikishiwa usalama kwani woga na hali ya kutokuaminiana iliyoanza kujitokeza miongoni mwao inaweza kusababisha hali kuwa mbaya baadaye.

Viongozi hao wamesema hayo jana walipokutana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba katika kikao kilichofanyika jijini Dar  na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), James Mbatia.

Ingawa kikao hicho kilikuwa sehemu ya utamaduni wa viongozi wa dini zote kukutana na kujadiliana kuhusu mambo yanayohusu nchi, lakini kwa sehemu kubwa kilitawaliwa na matukio yaliyoanza kuibuka katika siku za hivi karibuni.

Matukio hayo ni pamoja na kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, vitisho vinavyotolewa kwa baadhi ya makundi ya watu pamoja na tukio la kukutwa kwa miili katika eneo la Coco Beach jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Alinikisa Cheyo alisema katika majadiliano hayo wamekubaliana kwamba suala la ulinzi wa raia linapaswa kuwa ajenda ya kudumu kwa Serikali bila kujali itikadi.

“Ni muhimu mwanachi ahakikishiwe usalama wake popote pale alipo… potelea yukoje, yuko wapi lakini ahakikishiwe ya kwamba yupo salama,” alisema.

Hii ni mara ya kwanza kwa viongozi hao wa dini kukutana na waziri Mwigulu tangu kuibuka kwa matukio hayo na walitumia fursa hiyo kufanya maombi ya pamoja kumuombea Lissu ambaye anaendelea na matibabu jijini Nairobi.

Sheikh Hassan Said Chizenga kutoka Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata) alisema mikutano ya namna hiyo inawapa fursa waumini wa pande zote kubadilishana mawazo na kisha kukubaliana njia bora zaidi ya kulinda amani ya nchi.

“Huku kukutana tu kwenyewe pia kunasaidia kufuta tofauti zilizopo baina yetu na kuweza kutupa moyo wa kushirikiana sisi kwa sisi na kujua mambo mengine ambayo tulikuwa hatujui,” alisema.

Baadaye waziri Nchemba alisema  kuwa ingawa Serikali inaendelea kuchukua jukumu la kuimarisha ulinzi na usalama, wananchi nao wanapaswa kuchukua tahadhari.

“Wananchi lazima wawe makini maana unaweza ukamkuta mtu anamtuma mtoto kwenda dukani nyakati za usiku wakati sasa kuna haya matukio ya utekaji watoto, kwa hiyo wananchi lazima wazingatie hilo,” alisema.

Alisema Serikali imezipokea hoja zilizotolewa na viongozi wa dini na kwa kuzitilia maanani, inaanza kuangalia namna ya kufanikisha ulinzi wa nyumba kumi.

“Wametupa changamoto na sisi tunazifanyia kazi na tunaangalia uwezekano wa kuanzisha ulinzi wa nyumba kumi,” alisema.  

Wagombea Wenye ‘Harufu’ ya Edward Lowassa Watoswa

$
0
0
Katika kile kinachonekana mzimu wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa bado haujatoweka ndani ya CCM, wagombea kadhaa wa nafasi za uenyekiti wa wilaya, ambao wanatuhumiwa kumuunga mkono, wameondolewa, Mwananchi imeelezwa.

Lowassa, mmoja wa watu walioonekana kuwa na nguvu kubwa ndani ya CCM, alijiondoa mwaka 2015 baada ya jina lake kutopitishwa kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho. Kuondoka kwake kulifuatiwa na wenyeviti wa mikoa, wilaya, wabunge, madiwani na wanachama waliomfuata Chadema.

Wakati wa uchaguzi, aliyepitishwa kugombea urais, John Magufuli alikuwa akilalamika kuwa kuna baadhi ya wanachama ambao wanaunga mkono Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) uliokubaliana kumpitisha Lowassa kugombea urais.

Mwishoni mwa mwaka jana, Mkutano Mkuu wa CCM uliwatimua wanachama 12, wakiwamo wajumbe wa Kamati Kuu, wenyeviti wa mikoa na wilaya kwa madai ya kukisaliti chama hicho, hasa kutokana na kushirikiana na Ukawa.

Mwenyekiti wa Wilaya ya Meru, Furahini Mungure aliwahi kukaririwa akisema kuwa nguvu ya Lowassa, aliyekuwa mgombea wa Chadema kupitia Ukawa ndiyo iliyompa ushindi mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari huku aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisema waziri mkuu huyo alisumbua uchaguzi huo

Lakini fagio hilo halikumaliza vumbi aliloliacha mbunge huyo wa zamani wa Monduli na Halmashauri Kuu ya CCM iliyokutana Ikulu jijini Dar es Salaam wiki iliyopita ilizingatia suala hilo katika mchujo wa wagombea uenyekiti.

Mbali na kigezo hicho, sera mpya ya kutaka mwanachama asiwe na nafasi mbili za utendaji pia ilitumika kuwaengua wagombea, sambamba na mambo mengine kama utumishi serikalini.

Orodha ya wagombea waliopitishwa kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama hicho iliyotangazwa juzi katika gazeti la chama hicho, inaonyesha wengi wa wenyeviti hao waliomba kupata ridhaa kutetea nafasi zao lakini wameondolewa.

Orodha hiyo iliyojumuisha mikoa 33 ya Tanzania Bara na Zanzibar, inapeleka machungu kwa baadhi ya wenyeviti hao.

Mkoani Dar es Salaam, baadhi ya watu wanaotuhumiwa kumuunga mkono waziri huyo mkuu wa zamani, wameondolewa. Wenyeviti wa wilaya za Kinondoni na Ilala walikutwa na makosa ya usaliti na kuadhibiwa na chama hicho, hivyo hawakuwa na sifa za kugombea.

Mkoani Dodoma, wenyeviti wawili wameachwa ambao ni Paulo Luhamo kutoka Wilaya ya Dodoma Mjini na Philimon Mdate kutoka Bahi.

Kwa upande wa Geita, kati ya wenyeviti watano, ni mmoja pekee kutoka Wilaya ya Chato, Ibrahim Bagula aliyeachwa huku mgombea kutoka Mbogwe, Deus Lyamkando akipitishwa.

Mkoa wa Iringa, ambako kulikuwa na mgogoro mkubwa ndani ya CCM kuhusu wagombea urais, ndiyo ulioathirika zaidi kutokana na wenyeviti wake wote kukatwa majina yao na vikao hivyo vya juu vya chama.

Waliokatwa ni pamoja na (Abeid Kiponza (Iringa Mjini), Delfina Mtavialo (Iringa Vijijini), Seth Motto (Kilolo) na Yohanes Kaguo wa Mufindi.

Juhudi za Mwananchi kupata sababu za kuondolewa kwa wagombea hao hazikufanikiwa, lakini mkoa huo ulikuwa na vuguvugu kubwa la upinzani.

Kwa upande wa Kagera, kati ya wenyeviti watano, mgombea mmoja kutoka Bukoba Mjini, Yusuph Ngaiza amekatwa. Bukoba Mjini pia ni kati ya sehemu ambazo upinzani ulikuwa na nguvu.

Mkoani Kigoma, kati ya wenyeviti saba waliojitokeza kutetea nafasi zao, wawili wamekatwa ambao ni Kassim Kasambwe (Kigoma Mjini) na Almas Mohamed Kabambe (Uvinza).

Kilimanjaro, moja ya mikoa ambayo upinzani unashika majimbo mengi, wilaya zote zinatarajiwa kuwa na sura mpya kutokana na CCM kuagiza kurudiwa kwa uchaguzi katika wilaya tatu, huku wawili wakiamua kutogombea na jina la mmoja kutoka Same, Agustino Kessy, kukatwa.

Mkoani Mara kati ya wenyeviti sita, wawili hawajapitishwa ambao ni Chacha Gimanwa (Bunda) na Rashid Bugomba (Tarime). Mara pia ni ngome ya upinzani.

Mkoani Mbeya, wenyeviti watatu kati ya sita wameachwa. Wenyeviti hao ni Ephrahimu Mwaitenda (Mbeya Mjini), Ipyana Seme (Vijijini) na Mathayo Mwangomo (Mbarali).

Mkoani Morogoro, ambako CCM ina nguvu, kati ya wenyeviti wanane, Bassor Udulete kutoka Kilosa ambaye anadaiwa kushiriki kusaliti chama hicho, ameondolewa.

Katika Mkoa wa Mtwara, wagombea watatu; Ally Chimkawene (Mtwara Mjini), Ally Kombo (Vijijini), Abdu Namtula (Tandahimba) na Kazumari Mlilo (Masasi) wameachwa.

Waliokatwa mkoani Mwanza ni pamoja na mwenyekiti wa Wilaya ya Sengerema, Chasama Kamata na wa Misungwi, Judith Mlolwa wakati mkoani Njombe, CCM imeagiza mchakato uanze upya wilayani Makete.

Waliokatwa mkoani Pwani ambako kuna wilaya nane ni Hamisi Kanesa (Kibaha Vijijini na Omary Kubwa (Mkuranga) wakati Shinyanga hakuna mgombea aliyeachwa isipokuwa kwa mwenyekiti wa Wilaya ya Kahama, Mabara Mlolwa, ambaye hakugombea.

Hali ni kama hiyo mkoani Arusha ambako mgombea mmoja, Mustapha Mbwambo (Karatu) amekatwa, lakini wengine hawakugombea kutokana na baadhi kufukuzwa na wengine kuzuiwa na kanuni inayokataza kushika nafasi mbili.

Katika wilaya sita za Mkoa wa Singida, walioachwa ni watatu ambao ni Hassan Tati (Ikungi), Barnabas Hanje (Singida Vijijini) na Hamad Hamad (Manyoni), huku aliyekuwa mwenyekiti wa Manispaa ya Singida, Hamisi Nguli akishindwa kugombea kutokana na kufukuzwa na NEC.

Mkoani Tabora, wenyeviti wawili hawakugombea; Mussa Ntimizi ambaye ni mbunge na Seleman Mbogo (Sikonge), huku Costa Olomi (Igunga) na Moshi Abdallahman wa Tabora Mjini wakienguliwa.

Mkoani Tanga ni mwenyekiti mmoja pekee kutoka Wilaya ya Tanga, Kassim Mbuguni ambaye jina lake limekatwa.

Kwa upande wa visiwani Zanzibar katika Mkoa wa Kaskazini Pemba kati ya wenyeviti 12, walikatwa ni watatu pekee ambao ni wa Micheweni (Khamis Hamad Yussuf), Chakechake (Yussuf Ali Juma) pamoja na wa Mfenesini, Mjumbe Msuri Mjumbe.

Aliyekatwa azungumza

Mmoja wa wenyeviti hao ambao jina lake limekatwa amesema hana kinyongo na uamuzi huo.

Alisema kilichofanyika ni kwa mujibu wa kanuni na taratibu cha chama hicho na kwamba hana nia ya kukata rufaa.

“Matokeo hayo nimeyapokea kwa moyo mkunjufu na sioni haja ya kukata rufaa,” alisema Ephrahim Mwaitenda wa Mbeya Mjini.

“Nitaendelea kuwa mwanachama mwaminifu katika kukitumia chama changu. Inawezekana chama kimeona ni vyema nipumzike kwa kuwa siwezi kuendana kasi wanayoitaka kwa sasa.”

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Mrembo Jack Wolper Anazomeana na Kivuli Chake......

$
0
0
MIONGONI mwa waigizaji wa kike niliowahi kufanya naye kazi kwa kipindi kirefu na kwa ukaribu zaidi ni pamoja na mrembo Jacqueline  Wolper Massawe, aliye pia na a.k.a nyingi zikiwemo za Gambe na Amber Rose wa Bongo. Mkononi nimefumbata miaka saba sawa tangu nianze kazi ya uandishi wa habari, kwenye magazeti haya pendwa.

Ninao uzoefu mkubwa kwa kuwafahamu watu wengi maarufu kwa maana ya maisha yao ndani na nje ya kazi zao, nawajua sana hususan wasanii wa filamu ambao nafanya nao kazi mara kwa mara. Hata wengi wao wananijua vyema , kwenye eneo la kazi kwamba huwa siruki sentensi kwenye kuanika ukweli. Hivi karibuni, Wolper alikaririwa na mmoja wa waandishi wenzangu akisema kitendo cha kumshika na kumbeba mtoto wa mwigizaji mwenzake, Faiza Ally kimemuondolea gundu ya kutopata mtoto hivyo na yeye kutarajia kupata wa kwake mwakani.

Sawa, Wolper yuko sahihi lakini mbona maelezo hayo yanakanganya na kuzua maswali mengi yanayoumiza ubongo? Nitafafanua. Mwishoni mwa mwaka jana (2016), nikiwa nafanya kazi kwenye ofisi zingine (jina nalipaka oili), kama mwanahabari niliwahi kufanya naye mahojiano kwa njia ya simu (kumbukumbu zipo) na miongoni mwa maswali ambayo nilimuuliza ni pamoja na hilo la kutokuwa na mtoto lakini majibu yake yalinipa picha halisi kwamba Wolper hayuko tayari kupata mtoto kwa sasa hata ndani ya miaka mitatu au mitano ijayo kwa kile alichosema umri wake bado sana. Ngoja nikumbushie kidogo sehemu fupi ya mazungumzo yangu na yeye kwa siku hiyo. Mimi: Hivi kwa nini Wolper unashindwa kuolewa na ukatulia na mume ili maisha yasonge? Wolper: Kwani wewe umeoa?

Mimi: Bado. Wolper: Sasa kama bado kwa nini unaniuliza mimi nisiolewe, inakuwaje babu wewe au unataka kunichuria (neno la kisela lenye kuonesha kuudhika). Mimi: Binafsi umri wangu bado. Wolper: Kwani wewe unajua umri wangu? Hebu niambie una miaka mingapi? Mimi: Nina miaka (nikamtajia umri wangu). Wolper: Mimi bado mdogo sana, sijapanga kuolewa kwa sasa, natafuta maisha kwanza aise. Mimi: Hivi Wolper una mtoto? Wolper: (kwa sauti ya ukali na ya juu zaidi) Bwana eeeeh hivi (akilitaja jina langu), umetumwa? Nizae kabla ya muda wangu ili iweje? Nitazaa muda ukifika lakini siyo leo wala miaka mitatu ijayo labda mitano, maisha yenyewe magumu namna hii halafu tunaleteana habari za kuzaa hapa, unakuwaje wangu? Au unataka nikujibu vibaya tuanze kuandikana vibaya? Sitaki bwana habari hizo… (anaendelea…) Tafuta maswali mengine ya kuniuliza ndipo unipigie simu sawa?

Ni kweli raha ya kila mwanamke ni kuzaa lakini kila jambo lina wakati na mimi niko fiti nikihitaji kuzaa ni wakati wowote tu, mayai yangu yako active (hayana tatizo lolote), tena nikitaka kuzaa wala sitamuuliza au kumhusisha mwingine ni mimi na Mungu wangu tu. Mimi: Sasa ukiwaona wanawake wenzako wamebeba watoto wao huwa huumii na kujisikia vibaya? Wolper: Niumie nini sasa? Kawaida na nimeshasema siyo kwamba sina uwezo wa kuzaa la hasha. Naweza na sina mkosi kwa hilo na unielewe maana naona kama unanichanganyia habari tu hapa, hebu niache nifanye shughuli zangu sawa? (anakata simu na kuizima kabisa). Nimelazimika kukumbushia sehemu fupi sana ya mazungumzo yangu na Wolper kwa siku hiyo ili kama atasoma hapa aone ni kwa namna gani niko sawia na ninachokiandika hapa.

Leo Wolper anasema amemshika mtoto wa Faiza (Li) eti ni ishara kwamba ameondoa gundu ya kutopata mtoto! Hiyo gundu imetoka wapi wakati aliwahi kukana kabisa kwamba hana gundu na hajaamua tu kuzaa kwa kuwa umri bado na wingi wa majukumu ambayo yanambana kufanya hivyo, huku akisisitiza ndani ya miaka mitano ijayo? Wolper anataka kumchezea nani akili? Wakati mwingine mimi huwa nalazimika kuandika ukweli juu ya mambo ambayo hata wahusika huwa hawapendi yaanikwe ingawa ni ukweli na ndiyo maana uhusiano wangu na wasanii wengi wasio waelewa siyo mzuri kwa sababu kwenye kazi yangu ya kuandika huwa simhofii wala kumuonea mtu.


Naamini kabisa kwamba kama Wolper angeniona kwenye shughuli hiyo ya mtoto wa Faiza, kama ana kumbukumbu nzuri asingeweza kusema kwamba nimemshika na kumbeba Li hivyo nimetoa gundu, kama angefanya hivyo ningeamini pia kwamba analo tatizo kubwa la KUSAHAU! Nimsihi tu Wolper awe makini na kauli anazotoa wakati wa mahojiano na waandishi wa habari, kwani kujichanganya kwake kwa kauli kunaweza kumshushia heshima yake kwa jamii ambayo inaaminika kwamba yeye ni kioo cha jamii kujitazamia kwa ajili ya kuwa na mienendo mizuri. Kitendo cha ulimi mmoja kuwa na kauli mbili hutafsiri jambo moja tu. Mtu husika hajiamini na hana msimamo juu ya utendaji wake wa mambo, jambo ambalo kama nilivyosema huko nyuma kwamba, hupunguza mno heshima na wakati mwingine hata thamani ya mtu kwa hadhira. Wolper kama anahisi ana tatizo kwenye suala zima la uzazi, ni bora tu akaweka wazi ili kama kuna uwezekano wowote wa kusaidiwa iwe hivyo au asimamie eneo moja kwamba bado hana mpango wa kuolewa wala kuzaa, lakini kuliko asubuhi aseme sina mpango na sifikirii kabisa kuzaa halafu kabla hata njiwa hajameza punje ya mtama anajitokeza kwa mwanahabari na kusema ametoa gundu kwa kumbeba mtoto.

Kufanya hivyo hakumsaidii kwa lolote na chochote zaidi ya kujichora na kujianika kwa watu, vinginevyo Wolper anajaribu kukizomea kivuli chake, ambapo tafsiri yake ni kwamba anajidanganya yeye mwenyewe kwani kama ana tatizo na bado anataka tuamini kwamba yuko sawa au kinyume chake, huko ndiko kujidanganya na maana yake kwa wale wajuzi wa misemo huhitimisha kwa kuainisha kwamba mtu wa namna hiyo hufananishwa kama anayekizomea kivuli chake. Nawalisilisha.

Global

List ya Mastaa wa Bongo Ambao Mapenzi Hayajawaacha Salama

$
0
0
MAPENZI sanaa tamu ya wakubwa. Lakini hugeuka kuwa chungu kama shubiri pale unayempenda mnaposhindwana, anakutenda au mnaachana. Katika ulimwengu wa leo, kutokana na utandawazi na watu wengi kutokuwa waaminifu katika uhusiano wao wa kimapenzi, kila kukicha kumekuwa na vilio vya wapenzi kusalitiana kisha kuvunja uhusiano au ndoa. Katika makala haya nakuletea baadhi ya mastaa wa kike ambao licha ya kuwa warembo na kila mwanaume rijali akiwaona, lazima awamezee mate, lakini wamejikuta wakiteswa na mapenzi na kubaki wakiumia na kulia kila kukicha kwani wanapopenda wanajikuta wakishindwana.

ZARINAH HASSAN ‘ZARI’
Mwanamama huyu raia wa Uganda ni mrembo hasa, kwani licha ya kuwa ni mama wa watoto watano, lakini bado yupo vizuri na ni miongoni mwa warembo wanaovutia kwa macho. Zari amepitia misukosuko mingi ya mapenzi hadi kuachana na aliyekuwa mumewe, marehemu Ivan Ssemwanga aliyezaa naye watoto watatu kabla ya kuangukia kwa staa wa Bongo Fleva ambaye wamejaaliwa watoto wawili. Licha ya hao, pia aliwahi kusemwa kutoka na mmoja wa marafiki wa karibu wa Ivan, King Laurence na pia hivi karibuni kudaiwa kutoka na mmoja wa vijana wanaosaidia mazoezi yake Gmy, ambaye nusura amtenganishe na baba wa watoto wake wawili. Hivi karibuni Zari amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya Mbongo Fleva huyo kuchepuka na kuzaa na mwanamitindo, Hamisa Mobeto hali iliyosababisha watu kumtukana huku wengine wakimtia moyo katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

JACQUELINE WOLPER
Mwanadada huyu mrembo amepitia misukosuko mbalimbali katika mapenzi kwani aliwahi kuvishwa pete ya uchumba na mwanaume mmoja raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kuachana. Haikuishia hapo, aliwahi kuchumbiwa na mfanyabiashara, Abdallah Mtoro ‘Dallas’, lakini
uhusiano wao uliyeyuka, akarejea kwa Mkongo mwingine kabla ya kuingia kwa msanii wa Bongo Fleva ambaye alimtambulisha hadi ukweni kwao huko Mtwara, lakini walimwagana na sasa yupo na mwanaume mwingine anayejulikana kwa jina moja la Brown.

WEMA ISAAC SEPETU
Miss Tanzania huyu wa mwaka 2016, mapenzi yamekuwa ni kitendawili kwake kwani amewahi kuwa kwenye uhusiano na wanaume mbalimbali. Huyu, pengine ndiye staa mwenye kujua hasa maumivu ya mapenzi kwa sababu orodha ya wanaume aliowahi kutoka nao, inatisha! Mr Blue, TID, Charlz Baba, Steven Kanumba, Kigogo wa Ikulu, Mkongo na wengineo ni baadhi ya watu ambao wamewahi kushiriki mapenzi na kumwagana na mrembo huyu matata. Pia aliwahi kuwa na staa mkubwa wa Bongo Fleva na baada ya hapo akaingia kwenye uhusiano na Mshindi wa Big Brother Africa, Idris Sultan kisha wakatemana. Hivi karibuni ameripotiwa kuwa kwenye uhusiano usio wa ‘matangazo’ na mfanyabishara wa Arusha.

KAJALA MASANJA
Staa huyu ni mrembo, lakini na yeye ameonja maumivu makali ya mapenzi. Baada ya kuingia kwenye uhusiano wa mapenzi na prodyuza maarufu Bongo, Paul Matthyase ‘P Funk’ na kujaliwa kupata mtoto wa kike, Paula, hatimaye walitemena licha ya kukaa kwa muda mrefu. Haikuishia hapo, aliingia kwenye ndoa na kijana Faraji Chambo lakini ndoa yao iliingia doa baada ya Chambo kutiwa nguvuni na vyombo vya dola kwa matatizo kadha wa kadha. Baada ya kuachana, akaingia kwenye uhusiano na msanii Quick Rocka, kabla ya kusemwa kuwepo katika uhusiano na mwanaume mwingine kwa sasa. Ni mwanamke ambaye ana
historia ya kusisimua katika chungu na tamu ya mapenzi.

ZUWENA MOHAMED ‘SHILOLE’
Mwanamama huyu, licha ya kuwa na watoto wawili, bado ni mrembo, amewahi kuwa kwenye uhusiano na wanaume tofauti, lakini hadi sasa hajapata wa kumuoa. Shilole amewahi kuwa kimapenzi na msanii wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda ambaye alimvisha hadi pete ya uchumba, lakini matokeo yake alikwenda kumuoa mwanamke mwingine. Pia amewahi kuripotiwa kuwa na Wabongo Fleva, Elias Barnaba, Boy Caro, Neddy Music na sasa yupo na Uchebe ambaye aliwahi kukiri kwamba amesha-mtolea posa na ndoa yao itakuja ‘soon’.

HAMISA MOBETO
Ni mrembo, mama wa watoto wa wawili ambapo mwanaye wa kwanza alizalishwa na bosi mkubwa wa kituo cha redio, akamwagwa. Hivi karibuni mwanamama huyo ameingia kwenye vichwa vya habari baada ya kuripotiwa kuzaa na msanii mkubwa wa muziki wa kizazi kipya, lakini uhusiano wao, licha ya kupata naye mtoto, unaonyesha ni mchungu kwake kwani haionekani kama atapata alichotegemea

Rais Magufuli Anapokea Mshahara Mdogo Kuliko Marais wote Afrika Mashariki

$
0
0
Baada ya Rais Magufuli kuweka hadharani Mshahara anaoupokea imekuja kubainika kuwa Mshahara wa Rais Magufuli unalingana na Mshahara na marupurupu anayepokea Diwani wa Kenya na ni Rais anayepokea Mshahara mdogo kati ya viongozi wa Africa Mashariki.

Rais Yoweri Museveni wa Uganda anapokea dola 14978.65 kwa mwezi.
Rais Uhuru Kenyattta wa Kenya anapokea dola 13539.67 kwa mwezi.
Rais Paul Kagame wa Rwanda dola 6361.8 kwa mwezi.
Rais John Magufuli wa Tanzania anapokea dola 4026.87 kwa mwezi.

Fastjet Yaleta Ndege Mpya Aina ya E190 Kukabiliana na ATCL Katika Soko la Ndani na nje ya Tanzania

$
0
0

Baada ya Air Tanzania kuibuka na ndege zake toka kampuni ya Canada,wao Fastjet wameibukia Brazil na kuleta ndege aina ya Embrer190 (E190),twin-jet engines.

Kuanzia juma lijalo,wateja wa Fastjet nje na ndani ya nchi wataanza kusafiri na ndege aina ya E190 ambazo ni "tamu" kwa usafiri wa ndani na nchi jirani(Mainlines and Regional Airlines).

Fastjet inatazamiwa kuongeza ndege mbili aina ya E190,ambazo kwa ujumla wake zitakuwa tatu pamoja na ile Airbus319 ambayo Fastjet imekuwa ikiitumia kwa miaka mitano sasa.Ujio wa E190 ni changamoto kubwa kwa Air Tanzania na DH8-Q400(Bombardier) ambazo mpaka sasa,AirTz wanazo mbili tu.

Kuna habari kuwa Fastjet,akiwa na hizo E190 ataanza kwenda kwenye "destinations" ambazo hapo awali zilikuwa zinatawaliwa na Air Tz

Kigoma,Mtwara,Mbeya,Arusha,KIA,Mwanza,Tabora,Zanzibar na nchi ya Commoro ni maeneo ambayo Fastjet anatazamiwa kwenda na kuleta ushindani mkubwa kwa shirika letu la Taifa(National Carrier)

Uzuri wa E190,ni jet engines,pia ina mwendo kasi na comfortability.Safari ya Dsm Mbeya ni dakika 35 mpaka 40,wakati ile ya Mwanza ni dakika 55,hali ambayo ni kinyume kabisa na "pangaboi" zetu za ATCL.

Jukumu la ATCL kwa sasa,ni kufanya juhudi ya "kuikomboa" hiyo bambadia moja iliyoshikiliwa,kuleta kwa haraka zile Bombardier CS300 ambazo ni "jet engines" tulizoambiwa zipo mbioni kuja ili kukabiliana na ushindani wa Fastjet.

Bila kupepesa,ujio wa E190 katika "route" ambazo ATCL anakwenda,tena katika ulimwengu wa soko huria,utaleta changamoto na ushindani mkubwa sana kwa shirika letu la ATCL.Ndege za E190 zina raha yake,hizi ndio ndege ambazo Kenya Airways anazitumia kwa safari zake za ndani ya Afrika kwa muda mrefu sasa.Ujio wake katika soko la usafiri wa anga Tanzania,ni ufunguo wa mapinduzi makubwa ya usafiri wa anga na changamoto mpya za kimaendeleo.

Juzi Rais ktk hotuba ya ALAT alisema "Tutaendelea kununua ndege nyingi mpaka shirika liimarike na Tanzania ipate maendeleo".

Ni matumaini yangu,ujio wa E190 za Fastjet,utaifanya Serikali iamke zaidi na kuimalisha shirika letu la ndege la ATCL.Tuondoke kwenye DH-Q400,tukimbilie haraka kwenye zile Bombardier CS300,kukabilana na hawa kasuku wa kijivu.

Barafu

Mbunge CHADEMA Amshangaa IGP Sirro Kuhusu Dereva wa Lissu

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Gobless Lema amemshangaa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro kwa kauli yake kuhusu dereva wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

IGP Sirro akiwa ziarani mkoani Mtwara jana alisema, “Yule kijana ukimuona kwenye picha yuko vizuri tu, sasa wanaposema anapata huduma ya matibabu ya kisaikolojia wakati kwenye magazeti anaonekana vizuri, hii inatupa changamoto.”

Alisema, “Ndugu zangu, mheshimiwa Lissu amepigwa risasi na watu tunaowatafuta, huyo kijana aje. Kuja kwake kutatusaidia kupata majibu ya mambo mengi. Mtu anasema anatibiwa kisaikolojia lakini kila siku nikiona magazeti anaonekana anawaka inanipa tabu.”

Lissu ambaye pia ni mwanasheria wa Chadema alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 akiwa ndani ya gari nje ya makazi yake eneo la Area D mjini Dodoma.

Lema katika video iliyosambaa leo Alhamisi kwenye mitandao ya kijamii ya WhatsApp na Facebook anaonekana akisema kauli ya IGP Sirro ni lugha ya mzaha na hasa kwa familia ya Lissu, dereva aliyeshuhudia tukio hilo na Chadema kwa jumla.

Amesema kauli kuwa dereva wa Lissu anachelewesha upelelezi kukamilika si kweli.

Faiza Ali Aongea Ukweli "Diamond Bado Kijana Mdogo Sana Mwacheni Aenjoy na Watoto Wenzie

$
0
0
Huku Tetesi na Stori kibao zikikamata headlines mitandaoni kuwa couple ya @diamondplatnumz Na mama watoto wake @zarithebosslady SASA IMEBAKI STORI, Faiza Ameandika ujumbe Huu :
.
By @faizaally_ - Diamond kijana mdogo sana anahitaji ku have funny na watoto wenzie na sisi wa dada watu wazima tuangalie watu wa kutoka nao... Go baba and have funny enjoy the world ndio useto down .... jiachie uwe huru ikibidi usiwe na mahusiano , bado hujaiona dunia hata robo, we ni star , hela ipo there is lot to see...nasema with clean heart no hate kwa zari au kwa yoyote , nimezurula sana duniani kabla ya kuzaa na kutulia...jiachie life is today buana
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images