Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Aslay Atamba 'Trending 'You Tube Aishusha Hallelujah ya Diamond

0
0
Aslay Atamba You Tube  Aishusha Hallelujah ya Diamond
Ikiwa siku moja imepita toka meneja wa msanii Aslay, Mx kutoa taarifa kuwa ngoma ya ‘Natamba’ imeripotiwa kushushwa katika mtandao wa YouTube hatimaye ngoma hiyo ilirejea hapo jana jioni na kushika namba mbili kama ilivyokuwa awali na hivi sasa imeshika nafasi ya kwanza katika trending ya YouTube.

Hii ni good news kwa mashabiki wa Aslay kwani ngoma hiyo imefanikiwa kushika namba moja katika mtandao wa YouTube kwa kuishusha ngoma ya Diamond Platnumz ft Morgan Heritage ‘Hallelujah’, iliyokuwa imeshika namba moja kwa takribani siku tano mfululizo.

‘Natamba’ ni ngoma nyingine kutoka kwa msanii huyo baada ya kuongeza meneja wake na ina watazamaji 446,213 mpaka sasa.

Maandamano ya Kupinga Kujitenga kwa Catalonia Kufanyika

0
0
Maandamano ya Kupinga Kujitenga kwa Catalonia Kufanyika
Wale wanaopinga juhudi za jimbo la Catalonia kujitenga leo wamepanga maandamano makubwa huko mjini Madrid wakisema Uhispania ni taifa moja na hawataki ligawanyike.
Sintofahamu hiyo imetokana na kufanyika kwa kura tata ya juzi ambapo Catalonia ilisema kura ndiyo ingeamua iwapo wajitenge .

Japo wanasema asilimia kubwa ya waliopiga kura waliunga mkono, bado hawajatangaza uhuru wao wala hakuna dola yoyote ya nje na ndani ya Uhispania inayoitambua.
Utawala wa serikali kuu ulitumia nguvu na mbinu tofauti tofauti kujaribu kuzuia kura hiyo .
Mzozo huo umesababisha wasiwasi mkubwa sio tu wa kisiasa bali pia wa kibiashara.
Mapema leo benki ya pili kuu Caixabank, imetangaza kuondoa makao yake makuu kutokana na wasiwaasi unaoendelea kuligubika eneo hilo

Shirika la fedha dunia ,IMF limesema mzozo huo unaharibu mazingira ya uwekezaji wa Catalonia.
Ni dhahiri pande zote mbili na hata jamii ya kimataifa zingependa kuona mzozo huo umesuluhishwa kwa majadiliano lakini bado hamna dalili zozote kwamba yatafanyika hivi karibuni.

Simba Kumekucha Mauzo ya Hisa

0
0
Simba Kumekucha Mauzo ya Hisa
Kamati ya kusimamia mchakato wa zabuni ya klabu ya Simba, imeandaa mwaliko wa awali kwa ajili ya wanachana na taasisi zenye nia na sifa za kushiriki katika mchakato wa zabuni.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jaji mstaafu Thomas Mihayo amesema nyaraka za mwaliko wa awali zipo tayari na wawekezaji kwenye sifa na vigezo wanaweza kuzipata.

"Mwaliko wa kuchukua nyaraka hizi, utatangazwa kupitia vyombo vya habari kwa siku  kumi ili kuwapatia fursa za kutosha wazabuni watarajiwa kujiandaa na kukamilisha nyaraka muhimu.
Pia wazabuni watatumia muda huo kufanya mashariano kabla ya kuwasilisha Oktoba 18 ndiyo itakuwa Siku ya mwisho ya kuwasilisha nia ya kushiriki katika mchakato wa uwezekaji.
Alisema hatua hii itafuatiwa na uchambuzi wa mawasilisho yatakayopokelewa ila kutambua wzabuni watakao kuwa wamekidhi sifa na vigezo.

CUF Yakataa Kushirikiana na Ukawa Uchaguzi wa Madiwani November 26

0
0
CUF Yakataa Kushirikiana na Ukawa Uchaguzi wa Madiwani November 26
Chama cha Wananchi(CUF), upande wa Profesa  Ibrahim Lipumba kimesema kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi wa madiwani uliopangwa kufanyika Novemba 26 lakini kimesisitiza kutoshirikiana na Ukawa.

Hii ni mara ya kwanza kwa chama hicho kuweka msimamo wake katika uchaguzi tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambapo CUF ilikuwa miongoni mwa vyama viliunda umoja huo kwa kuweka wagombea waliokubaliana.

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Abdul Kambaya amesema leo Jumamosi jijini kuwa chama hicho hakioni sababu yoyote ya kushirikiana na vyama vingine kwenye uchaguzi huo ambao unahusisha halmashauri 34.

“CUF tunashiriki kwenye uchaguzi huu lakini hatututegemei kushirikiana na umoja wowote ule, sisi hatuitambui Ukawa lakini tunajua kuna chama kama Chadema, CUF na vyama vingine,” amesema Kambaya wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za chama hicho zilizopo Buguruni.

Amesema chama hicho kimejipanga vilivyo kuelekea kwenye uchaguzi huo na kwamba ili kuwaletea maendeleo wananchi wa maeneo hayo kunahitajika kuwa na viongozi wenye utulivu wa akili.

“Sisi tuko tayari kuelekea kwenye uchaguzi huo bila kuhusishwa na chama kingine chochote tunaamini tutafanya vizuri,” amesema.

Awali, mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho, Jafari Mneko aliwataka wana CUF kujitokeza kwa wingi katika kinyang’anyiro hicho. Amesema chama chake kimepokea taarifa kutoka ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ikiwaarifu kuhusu uchaguzi huo.

“Tumepata barua kutoka tume ambayo imetueleza kuhusu tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo na sisi tumeanza kujiandaa na ndiyo maana tunawaomba wanachama wetu wanaohisi wana uwezo wajitokeze kuomba nafasi na baadaye viongozi wa chama watachuja majina yao,” amesema.

Katika hatua nyingine mkurugenzi huyo alionya kile alichokiita mali ya chama kutumika kinyume na sheria na akawataka wanachama kutetea maslahi ya chama chao.

“Kuanzia sasa hatutapenda kuona mali ya chama kama mihuri, bendera ikiendelea kuchezewa ovyo, tunawataka wanachama kuzingatia katiba ya chama ibara ya 12 ambayo inamtaka kila mwanachama kulinda katiba na imani ya chama,” amesema.

Zitto Kabwe Atoa Neno Baraza Jipya La Mawaziri

0
0
Zitto Kabwe Atoa Neno Baraza Jipya La Mawaziri
Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama cha ACT -Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe, ametoa maoni yake juu ya Baraza jipya la Mawaziri lililofanyiwa mabadiliko hii leo, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Kwenye ukurasa wake wa Facebook Zitto Kabwe ameandika ujumbe akiwapongeza Mawaziri hao walioteuliwa ambao wengi wao ni vijana, huku akiwataka kuchapa kazi kwa bidii.

"Uteuzi wa vijana kushika nafasi za juu ni hatua nzuri, naona vijana wengi wamepewa majukumu makubwa, ninawaombea watekeleze majukumu kwa weledi mkubwa", ameandika Zitto Kabwe.

Leo Rais Magufuli amefanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na kuongeza wizara mpya mbili, baada ya kuzivunja baadhi ya wizara ambazo zilikuwa na vitengo vingi.


Majibu ya Saratani ya Utumbo Yawafanya Wapenzi Wafunge Ndoa

0
0
Majibu ya Saratani ya Utumbo Yawafanya Wapenzi Wafunge Ndoa
Mwanamke mmoja Marekani ajulikanaye kwa jina la Katie Sutterby, 29, amefariki siku tatu tu baada ya kufunga ndoa kutokana na saratani ya utumbo.

Imeelezwa kwamba mwanadada huyu alipimwa na kukutwa na ugonjwa huo wiki tano zilizopita jambo lililopelekea mchumba wake Will Arnold aliyekuwa amepanga kumvalisha pete ya uchumba binti huyo mwishoni mwa mwaka huu kuamua kumchumbia binti huyo na kuanza mipango ya harusi.

Arnold, 38, alieleza kuwa kila kitu kilitokea haraka sana na daktari aliwaambia kuwa Katie kutokana na ugonjwa huo alikuwa amebakiza miezi michache tu ya kuishi kama sio mwaka mmoja hivyo ilibidi waandae harusi ili kumalizia siku hizo za Katie kama mume na mke na hata mpango wao wa kwenda Paris kwenye honeymoon haukufanikiwa kwasababu ya hali yake kiafya.

Waziri Mwakyembe Atoboa Siri ya Kutibu Saratani

0
0
Waziri Mwakyembe Atoboa Siri ya Kutibu Saratani
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amewaomba watanzania kutambua kwamba saratani ya matiti inaweza kutibika hivyo ni wajibu wao wa kuhakikisha kwamba wanajiwekea utamaduni wa kuchunguza afyaili waweze kupata matibabu mapema kama watagundulika kuwa nayo.

Dkt. Mwakyembe amesema hayo leo jijini Dar es salaam wakati alipoongoza matembezi ya hisani ya kuchangisha fedha kiasi cha shilingi milioni mia moja zitakazosaidia matibabu kwa wagonjwa wenye saratani ya matiti hususani wakina mama ambapo matembezi hayo yameandaliwa na Tanzania Breast

Aidha Dkt. Mwakyembe amebainisha kwamba serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kutibu saratani ya matiti kutokana na wengi waliokuwa wakisumbuliwa na ugonjwa huo kushindwa kufanya uchunguzi wa afya zao mara kwa mara.

Wapiga Vita Silaha za Nyuklia Wapewa ‘Tuzo ya Heshima’

0
0
Wapiga Vita Silaha za Nyuklia Wapewa ‘Tuzo ya Heshima’
Kundi la kimataifa linalopigania kupigwa marufuku kwa silaha za nyuklia duniani limezawadiwa Tuzo ya Amani ya Nobel ya mwaka huu.

Imeelezwa kuwa kundi hili limekuwa na mchango mkubwa katika kupinga na kupiga marufuku matumizi ya silaha za nyuklia kutokana na madhara yake chini ya sheria za kimataifa hivyo linastahili tuzo hiyo.

Kamati ya maandalizi ya tuz hizo ambazo pia ni waamuzi wa kuu wa mshindi wa tuzo hiyo, imehimiza mataifa mengine yenye silaha za nyuklia kutafuta namna ya kuachana na silaha hizo polepole.


Tume Yaridhia Masharti ya Nasa

0
0
Tume Yaridhia Masharti ya Nasa
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), Wafula Chebukati ametangaza timu ya maofisa watakaosimamia shughuli za uchaguzi wa marudio Oktoba 26 huku jina la ofisa mtendaji mkuu, Ezra Chiloba likikosekana.

Chebukati, wakati anatangaza majukumu ya maofisa hao Ijumaa alisema Chiloba, ambaye muungano wa National Super Alliance (Nasa) unataka aondolewe, hatakuwa na mkono katika uchaguzi huo. Mbali ya Chiloba, pia maofisa wengine saba hawamo.

Hatua hiyo imekuja muda mfupi baada ya maandamano makubwa kufanywa na wafuasi wa Nasa mjini Kisumu, Nairobi na Homabay wakishinikiza kuondolewa na Chiloba na wenzake 10.

Vilevile, mabadiliko hayo yamefanyika wakati Nasa wakitangaza kuongeza siku ya Jumatano katika siku za maandamano. Katika barua yao waliyopeleka polisi sasa Nasa watakuwa wakiandamana kila Jumatatu, Jumatano na Ijumaa kushinikiza maofisa 11 waondolewe, na zifutwe zabuni kwa kampuni ya kuchapisha makaratasi ya kupigia kura na inayosambaza vifaa vya utambuzi wa mpigakura na kutuma matokeo kwa njia ya kielektroniki.

Baada ya shinikizo kali la maandamano ya ghasia, Chubukati ameonekana akikubali yaishe kwa upande wake akianza kwa kuondoa majina ya Chiloba na maofisa wengine saba.

Mabadiliko haya yanafanana na yale yaliyotangazwa siku chache baada ya Mahakama ya Juu kubatilisha matokeo yaliyompa ushindi Rais Uhuru Kenyatta, lakini Tume ilikanusha.

Gazeti la The Nation limefahamishwa kwamba Chebukati alifanikiwa kuwashawishi makamishna wote na wakaridhia timu mpya ambayo itawajibika katika maandalizi na kujibu maswali yote yanayohusu uchaguzi wa marudio.

Timu mpya ni ya Marjan Hussein atakayekuwa msimamizi wa timu; David Towett atahusika na operesheni, Albert Gogo atasimamia teknolojia ya uchaguzi, Dk Sidney Namulungu atasimamia vituo vya kujumlishia kura, Tabitha Mutemi atasimamia mawasiliano, Agatha Wahome atahusika na fedha, manunuzi na utawala, na Salome Oyugi atahusika na masuala ya sheria.

Kadinali Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi Siyo Msimamo wa Katoliki

0
0
Kadinali Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi Siyo Msimamo wa Katoliki
Mwadhama Kadinali, Polycarp Pengo amesema kwamba kauli iliyotolewa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo la Rulenge mkoani Kagera, Severine Niwemugizi kwamba Katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi ni maoni binafsi siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Pengo alisisitiza hilo wakati akitoa ufafanuzi juu ya sintofahamu iliyojitokeza miongoni mwa Watanzania na waumini wa kanisa hilo kutokana na kauli ya Askofu Niwemugizi.

“Napenda kutamka moja kwa moja kwamba huo siyo msimamo wa kanisa na hauwezi kuwa msimao wa kanisa kwa sababu sisi tuna taratibu zetu za kuishauri Serikali au kuzungumzia masuala ya jamii,” alisema.

Alifafanua zaidi kwamba  kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara lakini kimsingi kauli ile imekosa vigezo vya kuichukulia kama msimamo wa kanisa au jimbo anakotoka.

Kadinali Pengo alisema yeye binafsi kipaumbele chake ni kuona huduma za jamii kama zile elimu na afya zinaendelea kuboreshwa kwa kasi kama ambavyo Serikali ilivyoanza kufanya.

“Mtu akiniambia priority (kipaumbele) ya Tanzania ni Katiba mpya inabidi anithibitishie huo ukipaumbele maana siwezi kuona mtoto anakufa kwa njaa au kwa kukosa dawa eti kwa sababu ya Katiba mpya. Kwangu mimi Katiba ni kitu ambacho kije baadaye, si cha haraka.

“Wanasiasa wasiache watoto wetu wafe kwa njaa kisa malumbano ya Katiba. Wasiache watoto wakose shule kwa sababu hela zote zimeishia kwenye malumbano juu ya Katiba,” alisisitiza Kadinali Pengo.

Kwa upande wake Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Marek Solczynski hakutofautiana na kauli ya Kadinali Pengo kwa kusema  pamoja na kwamba Askofu Niwemugizi ana haki ya kutoa maoni yake lakini tatizo linakuja pale watu wakaposhindwa kung’amua kuwa ni maoni binafsi au ni ya kanisa.

Amesisitiza kwamba kanisa lina taratibu zake za kutoa maoni kwa masuala ya kijamii na kwa Serikali. “Hayo ni maoni yake binafsi na wala yasihusishwe na kanisa katoliki,” alisema Balozi Askofu Merek.

Hivi karibuni Askofu Niwemugizi alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kipaumbeke cha kwanza cha Watanzania ni Katiba mpya na kuongeza yeye binafsi ni miongini mwa watu walioipinga Katiba Inayopendekezwa.

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo walisema, pamoja na mjadala mkubwa ulioibuka na baadhi ya wanasiasa kususia mchakato wa kukamilisha Katiba mpya, wataalamu wa sheria wanasema Katiba inayopendekezwa ilikuwa ni bora kuliko ya sasa ikiwemo kuruhusu wagombea kuhoji mahakamani matokeo mbalimbali ikiwemo ya urais.

“Hata mimi ukiniuliza leo tuache kufanya mageuzi ya msingi katika jamii ili kuwa na uchumi imara au tuanze kushughulika na Katiba mpya, nitakwambia tuachane na Katiba.

“Nakumbuka ile Katiba Inayopendekezwa ilikuwa na masuala makubwa yenye maslahi kwa nchi ikiwemo kipengele cha kupinga matokeo ya urais lakini kwa kuwa kuna watu walikuwa na maslahi yao binafsi, wakatoka nje ya Bunge na kukwamisha mchakato ule sioni uharaka wa leo tuache mengine yote turejee kwenye mchakato huu,” alisema Wakili wa Mahakama Kuu, James Nandonde.

     

Maaskofu Wajitokeza Kukemea Mapepo Yanayoelekea Kuchafua Hali ya Hewa ya Siasa Amani

0
0
Maaskofu Wajitokeza Kukemea Mapepo Yanayoelekea Kuchafua Hali ya Hewa ya Siasa Amani
Watumishi wa Mungu, baada ya kuona yanayoendelea Cameroon na Uganda, wamejitokeza na kupaza sauti zao kukemea pepo anayeelekea kuchafua hali ya hewa ya siasa na amani.

Kutoka Yaounde, maaskofu wa Kikatoliki wamelaani “unyama” na “matumizi yasiyo ya lazima” ya nguvu dhidi ya waandamanaji katika eneo la wanaozungumza Kiingereza wiki iliyopita yaliyosababisha kuuawa watu 19.

Mapambano hayo yalitokea wakati viongozi wa eneo hilo walipoashiria kujitangazia uhuru wakidai kwamba Wanaozungumza Kiingereza kwa miongo mingi wamekuwa wakikosa usawa kiuchumi na kukosa haki za kijamii mbele ya wenzao walio wengi wanaozungumza Kifaransa.

"Tunalaani kwa nguvu zetu zote unyama na matumizi ya silaha za moto yasiyo ya lazima dhidi ya raia ambao wala hawakuwa na silaha yaliyofanywa na vikosi vya sheria na usalama hata kama walichokozwa,” ilisema taarifa ya Baraza la Maaskofu jimbo la Bamenda.

Watu 14 waliuawa katika mapambano na vikosi vya usalama wiki iliyopita, na wafungwa watano walipigwa risasi na walinzi walipojaribu kuvunja gereza la Kumbo.

Baadhi ya waombaji walipigwa mabomu ya kutoa machozi walipokuwa wakiondoka katika misa wakati wengine “walikamatwa, kujeruhiwa na baadhi (wakiwemo vijana wasio na silaha na wazee) walipigwa risasi kutoka kwenye helikopta.”

Lakini serikali imejitetea kwa kusema askari wake walilazimika kujihami baada ya kuweka amri ya kutotemba katika eneo hilo. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres na shirika la kutetea haki za binadamu la and Amnesty International wametoa wito ufanyike uchunguzi.

Kutoka Kampala Uganda, waumini wapatao 100 wakiongozwa na mchungaji Julius Oyet, walikwenda bungeni ambako walifanya ibada, wakalitakasa Bunge kwa damu ya Jesu kisha wakamwekea mikono kichwani Spika wa Bunge Rebecca Kadaga.



Watumishi hao wa Mungu waliombea utakaso ili Bunge lirejea katika hali yake ya kawaida baada ya wiki iliyopita kukumbwa na vurugu zilizosababisha wabunge kadhaa kujeruhiwa na wengine wa upinzani kukamatwa na polisi.

Wabunge 24 wa upinzani walisimamishwa Septemba 27 baada ya vurugu kuibuka huku wakimtuhumu Waziri wa Maji Ronald Kibuule kuingia na bunduki. Mgawanyiko mkubwa ulijitokeza wakati wa mjadala wa ukomo wa umri wa rais.

“Tunaomba hekima na mwongozo wenye mwelekeo. Tunatangaza kwamba hakuna silaha itakayofanya kazi dhidi yake na wala hatakufa mapema,” alisema Oyet akiwa amemwekea mikono Spika.

Katika sala zake, Mchungaji Tony Okot kutoka Kaskazini mwa Uganda alisema: “Tunaombea amani katika bunge hili na mzunguko wa viongozi wakati tukiomba utulivu wa wabunge wanapojadili muswada na kunyamazisha mapepo mengine yasifike hapa. Tunaomba kuwa chochote wanachofanya wafanye kwa hofu, amani, upendo, umoja na kuheshimiana.”

Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

0
0

THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)
MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)
Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.
ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..
Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Kweli Vyuma Vimekaza...Nay wa Mitego Akiri Kufulia na Kuuza Magari yake yote.......

0
0
VYUMA vimekaza! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya utajiri wa staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kudaiwa kwisha baada ya magari ya thamani aliyokuwa akiyamiliki kupukutika, Risasi Jumamosi linakupa mkanda kamili.
Kwa mujibu wa mnyetishaji wetu ambaye ni mmoja wa watu wa karibu wa Nay, kwa sasa mwanamuziki huyo ana hali ngumu kimaisha kwani ule utajiri aliokuwa nao awali, kwa sasa haupo tena, umepukutika.
“Kiukweli mambo ni magumu sana kwa Nay kwa sababu magari yote aliyokuwa nayo ameuza na sasa amebaki na moja tu, ndiyo maana hata huoni akiwa na mbwembwe kama zamani, hapana chezea hali ngumu ya sasa wewe,” kilisema chanzo hicho.

VIPI KUHUSU STUDIO YAKE?
Mnyetishaji huyo alizidi kutiririka kuwa, hata kwenye studio yake iliyopo Sinza-Kijuweni, Dar, kwa sasa wapo wakurugenzi wawili na kila mmoja ana timu yake ambapo mmojawapo ni Nay na mwingine alitajwa kwa jina moja la Isihaka.
“Studio kwake kwenyewe siku hizi hata hapaeleweki maana kuna uongozi wa watu wawili na kila mmoja ana watu wake. Kuna kipindi wanashindwa kuelewana katika mambo f’lani ya kiutendaji na vikao vimekuwa vikiwekwa kila kukicha,” alisema mtoa habari wetu.

NAY ANASEMAJE?
Ili kuujua ukweli, gazeti hili lilimtafuta Nay ambapo mahojiano yalikuwa hivi;
Risasi Jumamosi: Kuna habari kwamba umefulia na ule utajiri wako wote umepukutika, hili likoje?
Nay: Ni kweli nimefulia.
Risasi Jumamosi: Vipi kuhusu ishu ya kuuza magari na kubaki na moja tu?
Nay: Hata hilo gari moja sina kabisa, yote niliyauza tangu mwaka jana!
Risasi Jumamosi: Nini kisa cha kuyauza?
Nay: Nimefulia jamani.
Risasi Jumamosi: Kutokana na hali hiyo ngumu, inaelezwa kwamba hata kwenye studio yako mko wakurugenzi wawili, wewe na Isihaka ili kumudu gharama za uendeshaji, hili likoje?
Nay: Duh! Siyo kweli, aliyewaambia amewadanganya.
Risasi Jumamosi: Vipi kuhusu hii ishu kwamba magari yanayoonekana kwenye video za nyimbo zako siyo yako ni ya huyo Isihaka?
Nay: Duh! Hiyo kali sana, sasa kwenye video kuna msanii anayetumia magari yake binafsi? Huwa tunakodisha, huyo mmbeya wenu amewadanganya.
Baadhi ya magari ambayo Nay aliwahi kuripotiwa kuyamiliki ambapo kwa sasa hana ni pamoja na Range Rover Sport, Toyota Prado, Nissan Murano, Toyota Mark X, Toyota Brevis, Toyota Noah na mengineyo. Pia alikuwa na daladala kadhaa, Bajaj na bodaboda.

Polepole: Magufuli Hakuwa na Nafasi Yoyote CCM, Lakini Kafanya Mageuzi Makubwa

0
0
Humphrey Polepole amefunguka na kusema Rais Magufuli hakuwahi kuwa na nafasi ya uongozi ndani ya Chama hicho na kudai ndiye alikuwa mtu sahihi 2015 kwani alipoingia ndani ya chama na serikali ameweza kuona matatizo ambayo wengine hawakuweza kuyaona.

Polepole amesema kuwa kwa jinsi ambavyo chama hicho kilivyokuwa kipindi cha nyuma kilihitaji mtu ambaye hayupo ndani ya mfumo wake ili aweze kuona mapungufu mbalimbali ndani ya chama na serikali.

"Ndugu Magufuli kama Mwenyekiti ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) amekuwa ni kiongozi wa kawaida na duniani kote unaposoma elimu ya mageuzi huwa inataka upate mtu ambaye ni wa kawaida labda huenda asiyetoka katika eneo ambalo linafanyiwa mageuzi ili aweze kuwa na jicho la nje, kwa sababu gani wewe unayekaa ndani unaona kama mambo yako sawa hivi, sasa ndugu Magufuli ndani ya CCM hajawahi kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu, hajawahi kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, hajawahi kuwa Mjumbe wa Sekretarieti sasa CCM ilipotafakari ni nani atakayeweza kufanya mageuzi makubwa ndani ya chama hivyo hakukuwa na mtu mwingine zaidi ya John Pombe Magufuli" alisema Polepole

Aidha Polepole amesema kuwa Rais Magufuli alipoingia serikalini na ndani ya Chama Cha Mapinduzi hakuona haya kusema madudu na uozo uliopo ndani yake

"Magufuli hajaona haya kusema kwanini dhahabu inaondoka mnaitazama, Kwanini hii Almasi inakwenda na kwanini tunashindwa kuichakata hapa, kwanini bandarini mnaruhusu mizigo inaingia bila kulipa kodi, na nyinyi CCM kwanini mali zenu zinahodhiwa na watu na fedha haziji kwenye chama, hii yote ni kwa sababu anajicho la nje ambaye anaona tofauti na nyinyi mliopo ndani ya ambao mshazoe" alisema Polepole

Mbali na hilo Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amesema kuwa anapomsikia Rais Magufuli akisema kuwa nafasi ya Urais ni kazi ngumu anamuelewa kweli na kusema kuwa yeye anajua uongozi si kazi ya furaha bali ni mzigo mkubwa.

Video: Jerry Muro aivaa CHADEMA ajibu tuhuma

0
0
Jerry Muro amejibu tuhuma zilizotolewa na mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema kwamba yeye ndiye aliyehusika katika kufungua taili ya gari na pia ni mmoja wa watu wanaoshabikia ndoa za jinsia moja.

Amesema hayo leo jijini Dar es salaam alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari huku akisema tuhuma hizo kwake hazima kwani yeye sio mwanasiasa hivyo asubiri aingie kwenye siasa alafu wapambane vizuri.
                                                TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI


Haya Hapa Majina ya Mawazili Wanne Waliotemwa Uwazili

0
0

Rais John Magufuli amefanya mabadiliko ya baraza la mawaziri kwa kuwatema mawaziri wanne waliokuwepo kwenye baraza la awali.

Mawaziri walioachwa ni aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na nafasi yake kuchukuliwa na Hamis Kigwangwala aliyekuwa Naibu Waziri Wizara ya Afya.

Mwingine aliyeachwa ni aliyekuwa Waziri Maji na Umwagiliaji,  Mhandisi Gerson Lwenge ambaye nafasi yake imechukuliwa na Mbunge wa Katavi,  Mhandisi Issack Kamwele aliyekuwa naibu waziri wa wizara hiyo.

Panga hilo limempitia pia aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura ambaye nafasi yake imechukuliwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM, Juliana Shonza.

Aliyekuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani naye ametupwa nje na nafasi yake kuchukuliwa na Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga.

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kufanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri tangu aingie madarakani.

Habari mbaya kwa mashabiki wa Manchester United

0
0
Hakuna habari zenye uhakika kuhusu Paul Pogba, tetesi ni nyingi. Zipo habari kwamba amebakisha wiki mbili kurudi uwanjani huku wengine wakisema amebakisha mwezi mzima kurudi uwanjani.

Lakini chanzo kimoja cha habari ambacho kinaaminika kimekuja na habari mbaya kuhusu Pogba, inasemekana kiungo huyo wa Ufaransa anaweza kukosa michezo mingi zaidi na asirejee hadi mwisho wa mwaka.

Habari hizo zinasema Paul Pogba atakuwepo nje ya uwanja hadi msimu wa sikukuu za Christmass na anaweza kuikosa Chelsea, Tottenham na pia anaweza kukosa mchezo wa Manchester Derby dhidi ya City.

Sasa wakati mashabiki wa United walishaanza kumsahau Paul Pogba kutokana na kiwango kizuri sana cha Mourruane Fellaini kumekuja taarifa kwamba Fellaini ni majeruhi na anaweza kukaa nje kwa miezi kadhaa.

Fellaini ameumia wakati akiitumikia timu yake ya taifa ya Ubelgiji huku kocha wake Roberto Martinez akisisitiza kwamba wana mashaka makubwa kuhusu majeraha ya Fellaini, hii leo taarifa kamili ya majeraha ya Fellaini inaweza toka lakini inatarajiwa kuwa mbaya sana kwa United.

Manchester United wamekuwa na msimu mzuri sana tangu msimu wa 2017/2018 kuanza lakini sasa jinamizi lililowaandama msimu uliopita la majeruhi linaonekana limerudi tena Old Traford kwa mara nyingine.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ?

0
0
Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM, NAUTALETEWA POPOTE ULIPO TIBA HII

SIMU; NO 0767145357/0629034550.
WHATS APP 0759030343

Zari Hassan Aanika Ukweli Wote Kuhusu Diamond Platnumz

0
0
Mpenzi wa Diamond Platnumz, Zarina Hassan maarufu kama Zari The Boss Lady amefunguka na kudai kuwa yeye na mpenzi wake huyo hawajaachana.

Akiongea katika U-Heard ya Clouds FM, Zari amedai kuwa hawajaachana kama inavyodaiwa  na watu hii ni kutokana na kuwa hakumu-wish happy birtday katika mitandao  ya kijamii kama ilivyozoeleka.

“Hakuna lolote baya linaloendelea kati yake na Diamond, na wanaheshima mikataba aliyonayo na kampuni pia hakuna chochote kibaya kinachoendele,” ameema mrembo huyo.

Pia akaongeza kuwa “Nilimu-wish siku yake ya kuzaliwa sema nilitumia njia ya kawaida,na tunajaribu kuhamisha maisha yetu katika mitandao kuwa ya kawaida.”

Vile vile mrembo huyo alisisitiza kuwa stori zinazoenezwa kuwa Nillan sio mtoto wa Diamond sio za kweli na kuhusu DNA pia sio kweli.

Aslay Aishusha ‘Hallelujah’ Trending Kwenye Youtube

0
0
Ikiwa siku moja imepita toka meneja wa msanii Aslay, Mx kutoa taarifa kuwa ngoma ya ‘Natamba’ imeripotiwa kushushwa katika mtandao wa YouTube hatimaye ngoma hiyo ilirejea hapo jana jioni na kushika namba mbili kama ilivyokuwa awali na hivi sasa imeshika nafasi ya kwanza katika trending ya YouTube.

Hii ni good news kwa mashabiki wa Aslay kwani ngoma hiyo imefanikiwa kushika namba moja katika mtandao wa YouTube kwa kuishusha ngoma ya Diamond Platnumz ft Morgan Heritage ‘Hallelujah’, iliyokuwa imeshika namba moja kwa takribani siku tano mfululizo.

‘Natamba’ ni ngoma nyingine kutoka kwa msanii huyo baada ya kuongeza meneja wake na ina watazamaji 446,213 mpaka sasa.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images