Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Gigy Money: Young Dee Punguza Mitandao ya Wanawake Tulia na Amber Lulu Anakupenda Sana

$
0
0
Gigy Money: Young Dee Punguza Mitandao ya Wanawake na Kumtaka Atulie na Amber Lulu
Muuza nyago katika video mbalimbali za Bongo aliyejitosa katika muziki wa Bongo Flava, Gigy Money amemshauri Young Dee kupunguza mitandao ya wanawake.

Gigy Money ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ‘Papa’ ameiambia E-Newz ya EATV kuwa kutokana na umri wake ni vema angetulia na aliyekuwa mpenzi wake, Amber Lulu.

“Kiukweli apunguze mitandao ya wanawake unajua ina mchanganya halafu ukiangalia umri wake mdogo angetulia tu na Amber Lulu kwa sababu anampenda sana,” amesema Gigy Money.

Ameongeza kuwa katika wanawake mia wanaompenda Young Dee Lulu ndio anampenda sana na wengine majina tu, huku akieleza kuwa wawili hao hawajahi kuachana kama inavyokuwa ikiripotiwa.

Mugabe Afanya Mabadiriko ya Baraza la Mawaziri na Kumshusha Cheo Makamu Wake wa Rais

$
0
0
Mugabe Afanya Mabadiriko ya Baraza la Mawaziri na Kumshusha Cheo Makamu Wake wa Rais
Rais Robert Mugabe amefanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri ambalo amewaondoa baadhi na kuingiza sura mpya lakini habari kubwa ni kushushwa kwa makamu wa rais wake, Emerson Mangagwa.

Katika mabadiliko hayo, Mangagwa sasa atakuwa waziri wa utalii hali ambayo imetafsiriwa kwamba ameshushwa cheo.

Shirika la habari la ZimNews, likinukuu chanzo cha uhakika kutoka ndani ya serikali limesema Mnangagwa alikwishadokezwa kujiandaa kwa makubwa yanayotarajia kumfika na sasa amepokonywa nafasi zote za makamu wa rais na ile ya makamu wa rais katika chama tawala cha Zanu-PF.

Wakati fulani Mnangagwa alikuwa anapewa nafasi ya kumrithi Mugabe ikiwa atafariki dunia au kuamua kung’atuka. Lakini katika siku za hivi karibuni alianza kutopikika na wenzake hususan mke wa Raus Mugabe, Grace Mugabe.

Mnangagwa aliwahi kushutumiwa na mwanamama huyo kwamba anashirikiana na watu waliofukuzwa Zanu PF. Pia,  alishutumiwa na Grace kuwa alikuwa anafanya njama za kutaka kumpindua rais ili arithi nafasi yake.

Kilichomponza zaidi ni king’ang’anizi chake kwamba alikula sumu iliyokuwemo kwenye Ice Cream kutoka kampuni ya maziwa inayomilikiwa na Grace na akapelekwa Afrika Kusini kwa matibabu. Rais Mugabe alisema aliambiwa na madaktari waliokuwa wanamtibu makamu huyo wa rais kwamba kuugua kwake hakukutokana na sumu, lakini yeye alishikilia kwamba alilishwa sumu hali iliyoonekana ni kumdhalilisha Rais Mugabe.

Haya yakiwa hivyo, ndani ya Zanu PF kuna makundi makubwa mawili yanayonyukana kuwania uteuzi wa kugombea urais; la kwanza linaitwa G40 ambalo kuna makamu wa Rais Phelekezela Mphoko huku likiungwa mkono na Grace, na la pili linaitwa Lacoste ambalo linaongozwa na Mnangagwa. Kwa mabadiliko haya ni kama makamu huyo wa rais amepunguzwa kasi.

Aliyekuwa Waziri wa Fedha Patrick Chinamasa nafasi yake imechukuliwa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Ignatius Chombo, ambaye ni katibu mkuu wa Zanu PF anayehusika na masuala ya utawala. Wadadisi wa masuala ya siasa wameshtushwa na uteuzi huo wakihoji atafanya nini kuhusu sarafu ya Zimbabwe ambayo inaendelea kushuka.

Chinamasa amepewa wizara mpya isiyofahamika ya Usalama wa Mitandao. Muda mfupi baada ya kupewa nafasi hiyo, mwigizaji maarufu Carl Joshua Ncube alitania: "Jamani Patrick Chinamasa anawafuatilia kwenye Twitter ".

Aliyekuwa Waziri wa Utalii, Walter Mzembi sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje.

Mpwa wa Mugabe, Patrick Zhuwao anayeonekana kuwa mfuasi mkuu wa kundi la G40 linalopigiwa upatu na Grace ameteuliwa kuwa Waziri wa Kazi akitokea Wizara ya Vijana na Utamaduni.

Hatua ya kupandikwa kwake ni ushahidi wa kutosha kwamba umelenga kulipa nguvu kundi la G40 dhidi ya lile la Mnangagwa linaloitwa Lacoste.

LHRC Yazidi Kuikomalia Serikali Kufuta Adhabu ya Kifo

$
0
0
LHRC Yazidi Kuikomalia Serikali Kufuta Adhabu ya Kifo
Ikiwa dunia leo inaadhimisha siku ya kupinga adhabu ya kifo, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeitaka Serikali kuifuta adhabu hiyo.

Pia, Serikali na mamlaka husika zimetakiwa kufuta vipengele na sheria zinazoelekeza adhabu hiyo.

Kituo hicho kimeshauri mamlaka husika kuweka adhabu mbadala wa kifungo cha maisha ili kuthamini uhai ambao ni haki ya kila binadamu.

Akizungumza leo Jumanne, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Ana Henga amesema adhabu ya kifo inaondoa uwezekano wa mkosaji kujirekebisha na badala yake ni kuendeleza ukatili na kuondoa ubinadamu.

Henga amesema adhabu ya kifo inavunja misingi ya tamko la kimataifa la haki za binadamu la mwaka 1948 ambalo linasema kila mtu ana haki ya kuishi.

Amesema Tanzania inapaswa kujifunza kutoka kwa mataifa mengine duniani ambayo hayatekelezi adhabu ya kifo na badala yake kutoa adhabu mbadala kama vile kifungo cha maisha na kazi ngumu kwa watuhumiwa wa mauaji ili kulinda haki ya msingi ya kuishi.

Henga amesema harakati za kupinga adhabu ya kifo hazimaanishi kuwa ni kutetea uhalifu, hasa mauaji ila ukweli ni kwamba, hakuna ushahidi kuwa uwepo wa adhabu hiyo unaweza kupunguza uhalifu badala yake umekuwa ukiongezeka.

Tanzania ni miongoni mwa nchi chache duniani kama vile China, Korea Kaskazini na Marekani ambazo zinaruhusu na kutekeleza adhabu ya kifo katika sheria zake.

Sheria ya Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 ya Sheria za Tanzania, kifungu cha 197 kinaeleza mtu yeyote anayepatikana na   hatia ya kuua atahukumiwa adhabu ya kifo.

Henga ameitaka Serikali itekeleze pendekezo la mpango wa kujitathmini wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2016 kwa kuridhia mkataba wa nyongeza wa haki za kiraia na kisiasa na kutangaza kuwa haitekelezi adhabu hiyo.

Amesema kwa mujibu wa ripoti ya haki za binadamu ya mwaka 2016 takwimu zinaonyesha hadi mwaka 2015 kulikuwa na watu 472 waliohukumiwa kunyongwa kati yao wanaume wakiwa 452 na wanawake 20.

Pia, kati ya hao wanaosubiri kunyongwa ni 228, huku 244 wakisubiri uamuzi wa rufaa zao.

"Hii ni adhabu ya kibaguzi maana mara nyingi wanaopatikana na hatia na kupewa adhabu ni masikini wasioweza kuwa na uwakilishi na ushauri wa kisheria," amesema Henga.

Zitto Kabwe: Uchumi wa Nchi Unazidi Kudidimia Thamani ya Bei Inashuka Huku Mfumuko wa Bei Unazidi Kupaa

$
0
0
Zitto Kabwe: Uchumi  wa Nchi Unazidi Kudidimia Thamani ya Bei Inashuka Huku Mfumuko wa Bei Unazidi Kupaa
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa uchumi wa nchi unazidi kudidimia na thamani ya shilingi inazidi kushuka huku mfumuko wa bei ukizidi kupaa.

Zitto Kabwe anasema kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ambayo jana ametoa taarifa yake juu ya hali ya uchumi nchini ni kwamba hali si nzuri kwani uchumi umeonyesha kusinyaa na kudidimia huku wananchi wa hali ya chini wakiwa wahanga wakubwa zaidi.

"Taarifa hiyo inaonyesha namna hali ya uchumi wetu inavyozidi kuwa mbaya zaidi kwa wananchi wa hali ya chini , kwa mfumuko wa bei umepanda mno tangu kuanza kwa utekelezaji wa bajeti ya 2017/18, ongezeko ambalo limechangiwa zaidi na kupanda kwa bei ya bidhaa za chakula (bidhaa ambazo wananchi wengi zaidi wanazitumia)" alisema Zitto Kabawe
Aidha Zitto Kabwe amedai kushuka kwa thamani ya sarafu ya Tanzania kumezidi kuongeza maumivu kwa wananchi na ili kusaidia kupunguza ukali na gharama za maisha mishahara ilipaswa kupanda kwa asilimia 8 zaidi.

"Thamani ya sarafu ya Tanzania imeshuka, uwezo wa Tsh. 100 kununua bidhaa umeshuka hadi Tsh. 92.18. Maana yake ni kuwa mwaka 2016 shilingi 100,000 ilikupa bidhaa za shilingi 100,000. Mwaka huu 2017 shilingi 100,000 inakupa bidhaa za shilingi 92,000. Kwa hiyo ili upate bidhaa za shilingi laki moja inakubidi uongeze shilingi elfu 8 zaidi. Kiuchumi, ili kulinda hali za wananchi, mishahara ilipaswa kupanda kwa asilimia 8 ili kuwapunguzia maumivu ya gharama za maisha. Lakini hali hiyo inatokea katika wakati ambao mishahara haijapanda, na Rais wa nchi yetu kasema Serikali anayoingoza haitapandisha kabisa mishahara. Hali ni mbaya mno mtaani, mijini uzalishaji wa bidhaa za viwanda umeshuka kwa zaidi ya nusu, kutoka trilioni 1.5 mpaka bilioni 700 tu" alisisitiza Zitto Kabwe
Mbali na hilo Zitto Kabwe ametoa ushauri wa nini serikali inapaswa kufanya ili kukabiliana na hali hiyo na kupunguza ukali wa maisha kwa wananchi, Zitto amedai Serikali inapaswa itazame namna inatekeleza mipango yake ya Maendeleo, Serikali isikilize na kufanyia kazi mawazo ya sekta binafsi katika kuweka sawa mazingira ya uwekezaji bila kupoka haki ya nchi kufaidi na rasilimali zake na pia ameitaka serikali ifanyie kazi haswa uchumi wa vijijini kwa kurekebisha mapungufu yote yanayoshusha uzalishaji kwenye sekta ya kilimo.

Mahakama Yawahukumu Watu Wawili Miaka 30 Jela na Adhabu ya Viboko 12

$
0
0
Mahakama Yawahukumu Watu Wawili Miaka 30 Jela na Adhabu ya Viboko 12
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewahukumu watu wanne kifungo cha miaka 30 jela na adhabu ya kuchapwa viboko 12; viboko sita wakati wa kuingia na sita wakati wa kutoka kwa kosa la wizi wa kutumia silaha.

Waliohukumiwa ni Donald Nzweka, Michael Pascal, Ally Akili na Kurwa Mwakagenda.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Respicious Mwijage alisema hakuna shaka washtakiwa walishiriki kutenda kosa chini mwanga wa kutosha na kwamba washtakiwa walitambuliwa ipasavyo.

”Nimeridhika Jamhuri imethibiisha kosa bila kuacha shaka dhidi ya washtakiwa hivyo nawatia hatiani kwa kosa la kutumia silaha kama walivyoshtakiwa.”

Kwa pamoja July 7, 2013 maeneo ya Boko Magengeni, DSM washtakiwa waliiba simu nne aina ya Nokia Sumsung na Tecno zenye thamani ya Tsh Milioni 1,300,000, pesa taslimu Tsh 150,000, cheni za dhababu mbili zenye thamani ya Tsh 750,000, vyote vikiwa na thamani ya Tsh 2,050,000 mali ya Hobokela Mwakijambile.


Upande wa Mashtaka ulikuwa na mashahidi 11 na washtakiwa walijitetea wenyewe ambapo baada ya Hakimu kupitia ushahidi wa pande zote mbili Mahakama ilijiuliza kwamba kosa la kutumia silaha ili lithibitike Jamhuri wana wajibu wa kuthibitisha bila kuacha shaka kwamba washtakiwa kabla ya kutenda awe na kifaa hatari au wawe zaidi ya mmoja na kwamba baada ya tukio hilo walitumia nguvu kwa mtu aliyeporwa.

Katika shauri hilo, mlalamikaji na mashahidi wengine walieleza kuwa usiku wa July 7 majambazi walivunja mlango mkuu wa nyumba yao kwa kutumia bomu ambalo lilitambuliwa na Polisi kuwa baruti.

Alidai waliendelea kuvunja milango mingine na baadaye waliingia katika chumba walichokuwa wamekaa, wakiwa katika chumba hicho chenye mwanga, mshtakiwa wa nne alishika panga na alianza kuwapiga nalo kwa kutumia ubapa.

Aidha, Hakimu alisema kwa kuzingatia ushahidi huo hakuna shaka kwamba mashahidi waliweza kuwatambua  majambazi hao na kwamba ni washtakiwa katika kesi hiyo ambapo alisema kwa kuangalia maelezo yao waliyotoa Polisi yanaonyesha jinsi walivyoshiriki katika tukio na kwamba washtakiwa ndio walioiba vifaa hivyo kwa kutumia silaha kali.

Utetezi wa washtakiwa kwamba walikamatwa maeneo tofauti na kupelekwa Oyster bay Polisi na kupigwa na kunyanyaswa, Mahakama ilisema ushahidi huo hauaminiki na hauwezi kupewa uzito wowote.

Utetezi wa washtakiwa wa kukanusha kutenda kosa haukutikisa kwa aina yoyote ushahidi wa upande wa mashtaka.

”Nimeridhika na upande wa mashtaka umethibitisha kosa bila kuacha shaka dhidi ya washtakiwa wote nawatia hatiani kwa kosa la wizi wa kutumia dilaha kama walivyoshtakiwa.”

Jamhuri iliwakilishwa na Wakili wa Serikali Gloria Mwenda, ambaye alidai  aliwashtaki wakosaji wa mara ya kwanza na akaomba wapewe adhabu kali ili iwe fundisho kwa jamii.

Walionusurika wa Ajali ya Daladala Iliyotumbukia Ziwa Victoria Wasimulia na Kumtupia Lawama Dereva

$
0
0
Walionusurika wa Ajali ya Daladala Iliyotumbukia Ziwa Victoria Wasimulia na Kumtupia Lawama Dereva
Walionusurika ajali ya daladala iliyotumbukia Ziwa Victoria, wamesema iwapo dereva angesikiliza ushauri madhara yasingekuwa makubwa.

Akizungumza katika Hospitali ya Bukumbi Mission wilayani Misungwi alikolazwa, Yohana Ngabula (28) mkazi wa Kijiji cha Buyagu wilayani Sengerema amesema amepoteza mama na dada katika ajali hiyo.

Ngabula amesema walikuwa wakitoka jijini Mwanza kufuatilia mafao ya baba yao katika ofisi za Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

“Nilimshauri dereva agonge hata gari lililokuwa mbele yake badala ya kulielekeza ziwani lakini hakusikia mwisho wake ndiyo hayo yaliyotokea,” amesema.

Amesema baada ya gari kutumbukia ziwani alipasua kioo na kutoka ndipo walipofika vijana wakamuokoa.

Majeruhi mwingine mkazi wa Ibisabageni, Paulo Lazaro ambaye ni mwalimu wilayani Sengerema amesema, “Tulimshauri dereva agonge vitu nchi kavu kuliko kuipeleka gari majini lakini hakusikiliza ushauri wetu, pengine tungepona wengi zaidi.”

Mwalimu huyo amesema alipita dirishani baada ya gari kutumbukia ziwani na kwamba, ana maumivu mabegani na mgongoni.

Mwingine aliyenusurika katika ajali hiyo, Sophia Biambina (32) amesema amepoteza watoto wawili katika ajali hiyo.

Amesema walikuwa wakitoka kwenye msiba wa baba yake wilayani Magu na alikuwa akielekea nyumbani kwake Nyapande wilayani Sengerema.

“Baada ya ajali nilijikuta nimeshatoka nje sikujua nimetokaje, najihisi maumivu makali kwa sababu nilikunywa maji mengi. Kinachoniuma ni kuwapoteza watoto wangu, tulitoka msibani kumzika baba yangu,” amesema.

Soma: Waliokufa Ziwa Victoria wafikia 12

Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Bukumbi, Dk Robert Shija amesema walipokea maiti 12 na majeruhi hao watatu.

Amesema walipokea miili ya Joseph Paulo, Rehema Makalanga, Mariamu Kagosha, Pendo Msafiri, Salome Msafiri, Joyce Hamadi, Martha Makenzi, Gwanchele Mswagi na Kazungu Lukuba wote wakazi wa Wilaya ya Sengerema.

Wengine ni Martine Kamlamo mkazi wa Bukumbi, Hamadi Zahalaki wa Bukoba na Ally Abdul wa Kayenze wilayani Ilemela.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda ameuagiza uongozi wa hospitali kuwa, ndugu watakaoshindwa kusafirisha miili wawasiliane na ofisi ya wilaya kwa ajili ya kupata msaada.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole amesema walipanga kuisafirisha miili hiyo lakini tayari ndugu wameshaichukua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema hakuna miili mingine ambayo imeopolewa lakini Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji kimerudi eneo la tukio.

Msangi alisema jana Jumatatu kuwa hawajapata idadi kamili ya watu waliokuwemo kwenye gari hilo.

 

Nyumba ya Mchezaji Yavamiwa na Mashabiki kwa Kushindwa Kufunga Mabao

$
0
0
Nyumba ya Mchezaji Yavamiwa na Mashabiki  kwa Kushindwa Kufunga Mabao
Polisi nchini Zambia wamewakamata mashabiki watano kwa madai kuwa walivamia nyumba ya mwanasoka wa timu ya taifa ya kandanda Alex N'gonga.
Mashabiki hao walishikwa na hasira kuwa Ng'onga. alikosa nafasi wazi za kufunga wakati wa mechi muhimu ya kufuzu kwa kombe la dunia ambapo Nigeria iliishinda Zambia bao 1-0
Mambo muhimu kuhusu nchi ambazo tayari zimefuzu Kombe la Dunia 2018
Mashabiki walitoa hasira zao kwa kuvamia nyumba yake iliyo mji wa Kitwe ambao waliitupia mawe, kwa mujibu wa kamishina wa polisi Charity Katanga.
"Tumekamata watu watano kwa makosa ya kuharibu mali na sasa wanazuiliwa ns polisi."
Kushindwa kwa Zambia kuliipokonya fursa ya kufuzu kwa kombe la dunia nchini Urusi ambapo Nigeria walifuzu.

Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

$
0
0

THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)
MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)
Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.
ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..
Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Auwawa kwa Kupigwa Risasi na Wahalifu Wenzake Akiwa Chini ya Ulinzi wa Polisi

$
0
0
Auwawa kwa Kupigwa Risasi na Wahalifu Wenzake Akiwa Chini ya Ulinzi wa Polisi
Mkazi wa jijini Dar es Salaam, Robert Massawe (51), ambaye polisi wanadai ni mtuhumiwa wa uporaji na mauaji, ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa ni wahalifu wenzake.

Kabla ya kuuawa katika majibizano ya risasi, mtuhumiwa huyo anadaiwa alikamatwa akiwa na SMG yenye risasi 24, simu 19 zilizoporwa maeneo mbalimbali na laini za simu 58.

Taarifa iliyotolewa leo Jumanne na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamisi Issah imesema mtuhumiwa aliuawa na wenzake saa tisa usiku wa kuamkia jana wilayani Rombo.

Amesema mtuhumiwa pamoja na mkewe walikamatwa jijini Dar es Salaam na baada ya kuhojiwa na polisi inadaiwa alieleza matukio ya ujambazi aliyoshiriki na alikubali kuwaonyesha mahali alipoficha bunduki.

Polisi imesema simu tatu kati ya 19 wamegundua ziliporwa Moshi na moja alikuwa akiitumia mkewe ambaye anashikiliwa Dar es Salaam.

Kamanda Issah amesema aliwaeleza polisi kuhusu mpango wa kufanya tukio la ujambazi katika Kijiji cha Chilio, Kata ya Holili wilayani Rombo jana alfajiri.

Amesema askari walifuatana naye chini ya ulinzi hadi Moshi kwenye dampo lililopo jirani na kiwanda cha ngozi ambako bunduki ilifukiwa ardhini ikiwa na risasi 24.

“Chini ya ulinzi wa askari kanzu, alipowaona wenzake alipiga kelele kuwajulisha polisi walikuwepo eneo hilo,” amesema.

Kamanda Issah amesema kelele ziliwafanya watuhumiwa hao kukimbia huku wakifyatua risasi hovyo na baadhi zilimpiga Massawe mkono wa kushoto, mgongoni na mguuni hivyo kusababisha kifo chake.

Polisi imesema mtuhumiwa alishiriki matukio manane ya uporaji wa fedha na mauaji kwa kutumia silaha na amewahi kufungwa kwa ujambazi lakini aliachiwa baada ya kukata rufaa.

Ali Kiba: Najisikia Vizuri Watu Maarufu Kupenda Kazi Zangu na Nina Haki Kupendwa na Mange Kimambi

$
0
0
Ali Kiba: Najisikia Vizuri Watu Maarufu Kupenda Kazi Zangu na Nina Haki Kupendwa na Mange Kimambi
Alikiba ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake wa 'Seduce me' amefunguka na kusema kuwa Tanzania kila mtu ana haki na uhuru wake hivyo hata yeye anajisikia vizuri kuona watu maarufu wanapenda kazi zake na kudai ana haki ya kupendwa na Mange Kimambi

Alikiba amedai kuwa Mange Kimambi ni moja kati ya mashabiki zake na kusema anashukuru sana kuona anapenda kazi zake na kumpa nguvu katika kazi zake hizo kwa kutoa 'support'.
"Ni kama shabiki wangu na 'appreciate' anapenda muziki wangu kwa sababu mimi namuheshimu kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anani 'support' kwenye kazi zangu lakini pia kutokana na uhuru hivyo kila mtu ana haki na vilevile mimi nina haki ya kupendwa na mtu yoyote yule, hivyo nina haki ya kupendwa na Mange Kimambi pia" alisema Alikiba

Mbali na hilo Alikiba alisema anajisikia vizuri kuona muziki wake unazidi kufika mbali zaidi duniani na kuendelea kufanya vizuri nyumbani Tanzania na Afrika Mashariki kiujumla.
"Najisikia furaha zaidi pale napoona watu wanaojulikana na maarufu nao wanafurahi na muziki wangu na si kusikia muziki tu bali ni mashabiki wangu pia, hivyo kwangu mimi ni raha sana, nawapenda sana mashabiki zangu wote duniani kwani nyinyi mnanipa furaha na amani" alisema Alikiba 

Klabu ya Ndanda Yavurugana Kamati Yatokomea na Mikataba

$
0
0
Klabu ya Ndanda Yavurugana Kamati Yatokomea na Mikataba
Klabu ya soka ya Ndanda FC imesema haitambui mikataba iliyosainiwa na Kamati iliyokuwa ikiendesha timu kabla ya kuirejesha kwenye bodi takribani miezi miwili iliyopita.

Msemaji wa Ndanda FC Idris Bandali amesema kuwa tangu kamati hiyo irudishe timu haijawasilisha mikataba waliyoingia na makampuni mbalimbali ikiwemo Maxcom Limited na Kiboko.
“Klabu ya Ndanda haina nia mbaya na wadhamini lakini tunachotaka sisi wale watu walioingia nao makubaliano watuletee hizo taarifa walete mikataba”, amesema Bandali.
Aidha Bandali ameongeza kuwa taarifa ya Mhasibu wa Ndanda imesema akaunti ya timu haina pesa yoyote iliyoingia kutoka kwa hao wadhamini hivyo hawawezi kuendelea kukaa na mabango ya makampuni hayo uwanjani hivyo lazima wayatoe ili yasije kuleta utata baadae.

Kamati hiyo pia imedaiwa kusajili wachezaji na kuwapeleka Ndanda bila kuwasilisha mikataba yao kwa timu na shirikisho kitu ambacho ni kinyume na sheria za soka. Kwa mujibu wa Bandali kamati hiyo imeitwa mara nyingi na kuombwa kuwasilisha mikataba lakini imekuwa haitaki kuitikia.

Kamati ya Bodi ya Uendeshaji Ligi Yaishushia Klabu ya Simba Adhabu

$
0
0
Kamati ya Bodi ya Uendeshaji Ligi Yaishushia Klabu ya Simba  Adhabu
Kamati ya Bodi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi  imeipiga faini klabu ya Simba sh 500,000 (laki tano) kwa kosa la kuingia uwanjani kwa kutumia mlango usio rasmi katika mechi dhidi ya Mbao FC iliyofanyika Septemba 21 Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

Simba imevunja Kanuni ya 14(14) ya Ligi Kuu, na adhabu dhidi yao ni kwa mujibu wa Kanuni ya 14(49) ya Ligi Kuu. Pia Kamishna wa mechi hiyo, Maliki Tibabimale amepewa Onyo Kali kwa kutoripoti kitendo hicho cha Simba.

Kwa upande mwingine kamati imeiadhibu Singida United sh. 500,000 (laki tano) kutokana na mashabiki wa timu hiyo kuingia uwanjani kushangilia ushindi baada ya mechi dhidi ya Kagera Sugar iliyofanyika Septemba 23 mwaka huu Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Wakati huo Stand United imepigwa faini ya jumla ya sh. 1,500,000 (milioni moja na laki tano) kutokana na makosa mawili kwenye michezo miwili tofauti ambayo ni Wachezaji kuvaa jezi zenye namba tofauti na zilizosajiliwa kwenye mechi dhidi ya Simba pamoja na mashabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi dhidi ya Mbeya City na Simba.

Kamati imeionya klabu ya Stand United endapo vitendo hivyo vitatokea tena haitasita kuichukulia hatua kali zaidi za kikanuni.

Kesi ya wa Ethiopia Waliokua Wakienda Afrika Kusini Kupitia Tanzania Yaahirishwa

$
0
0
Kesi ya wa Ethiopia Waliokua Wakienda Afrika Kusini Kupitia Tanzania Yaahirishwa
KESI ya raia 40 wa Ethiopia waliokuwa wanakwenda Afrika Kusini wakipitia Tanzania imeahirishwa leo hadi Oktoba 13 mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Kesi hiyo ilikuwa imekuja kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali.

Watuhumiwa hao walikamatwa wakisafirishwa na madereva wa kampuni ya Dangote Cement inayomilikiwa na mfanyabiashara tajiri Afrika, Aliko Dangote. Watu hao ni Hussein Hassan na Juma Mtambo na Sadick ambao wiki iliyopita dhamana yao ilikuwa wazi.

Awali kesi hiyo ilipofikishwa mahakamani hapo Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Novatus Mlay, alimueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa, kuwa washtakiwa hao wanakabiliwa na makosa matano ambayo ni kuingia nchini kinyume na sheria. Ilidaiwa Septemba 25 mwaka huu watuhumiwa walikutwa maeneo ya Mbagala-Kongowe, wakiishi bila kuwa na kibali.

Kosa jingine ni usafirishaji usio halali linalowakabili madereva Watanzania waliowasafirisha ambapo inadaiwa Septemba 20 mwaka huu, maeneo ya Mbagala, Kongowe, na Mtoni Mtongani walikutwa wakisafirisha Waethiopia hao kwa kutumia gari ambalo ni mali ya Dangote Cement kuelekea Afrika Kusini.

Baada ya kusomewa makosa hayo, raia hao wa Ethiopia walikiri makosa yao ambapo Watanzania walikana na Wakili Mlay alisema upelelezi wa kesi hiyo unaendelea.

Hakimu Nongwa alisema washtakiwa waliokana makosa wanaweza kupata dhamana kwa kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili waaminifu ambapo washtakiwa waliokiri kosa walitakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Zaidi ya Walimu 20,000 Waliofeli Mtihani Iliyotakiwa Kufanywa na Wanafunzi Wao Kufutwa

$
0
0
Zaidi ya Walimu 20,000 Waliofeli Mtihani Iliyotakiwa Kufanywa na  Wanafunzi Wao Kufutwa
Mamlaka katika jimbo lililo kaskazini mwa Nigeria la Kaduna zinasema kuwa zaidi ya walimu 20,000 wa shule za msingi watafutwa baada ya wao kufeli mtihani unaotahili kufanywa na wanafunzi wao.
Hii inafuatia madai kuwa nyingi ya shule za msingi na sekondari nchini Nigeria huzalisha wanafunzi wasiohitimu vyema.
Gavana wa jimbo la Kaduna el-Rufai alisema kuwa walimu waliohitimu wataajiriwa kuchukua mahala pa wale watakaofutwa.
Haijulikani hatua hii itachukuliwa lini.
Marufuku nguo za kubana chuoni Lagos
Wasichana waonywa dhidi ya kupotoshwa na mitandao ya kijamii Nigeria
Afisa mmoja wa cheo cha juu katika jimbo la Kaduna aliambia BBC kuwa mitihani zaidi itatolewa siku zinazokuja kwa walimu wa sekondani.
Wadadisi wanasema kuwa idadi hiyo ni ishara ya viwango duni vya elimu nchini Nigeria ambapo inadaiwa kuwa walimu huajiriwa kwa misingi ya kisiasa.

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778.

Alikiba Afunguka Mahusiano yake na Mange Kimambi

$
0
0
Hitmaker wa Seduce Me, Alikiba amefunguka juu ya mahusiano yake na Mange Kimambi.

Mara kadhaa Mange amekuwa akimpa support kubwa msanii huyo huku akimtetea kwa kila hali endapo hali ya mashambulizi kutoka kwa wapinzani inaonekana kuwa kubwa.

Akiongea na Bongo5, Ali amesema, “Nimeshawahi kuonana na Mange nimepiga naye picha, ni kama shabiki wangu na nina appreciate kwamba anapenda muziki wangu kwa sababu ninamuheshibu kila mtu anayeni support.”

“Pili nina u-free nina haki na kila mtu, mimi nina haki ya kupendwa na mtu yoyote. Nina haki ya kupendwa na Mange na nina haki ya kupendwa na mtu yoyote yule,” ameongeza.

KENYA: Raila Odinga(NASA) Ajitoa Kugombea Urais wa Kenya Uliokuwa Ufanyike 26 Oktoba 2017

$
0
0
Raila Odinga ajiondoa kugombea urais wa Kenya, kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 26, 2017

Miongoni mwa sababu kubwa za kujitoa ni;
Wamehisi kuwa IEBC haina nia ya kuhakikisha yale makosa yaliyosababishwa kufutiliwa mbali matokeo ya urais Augost 8 kuwa hayatajirudia tena.
Pia wameona wapianzani wa Jubilee wataka kufanyia Katiba mapinduzi na kurudisha udikteta, wanaona kuwa Jubilee wanataka tu kuwe na uchaguzi ila wao wanataka uchaguzi bora
Pia IEBC kutokufuata masharti waliyotoa ambayo yangeakikisha kuwepo kwa uchaguzi bora na wa haki


“Kwenye demokrasia ya Kikatiba, hatakiwi kulumbana kuhusu uchaguzi huru na wa haki. Tulitakiwa tushirikiane kwa kufanya kazi pamoja kuhakikisha tunashikilia maadili haya ambayo sio tu maadili ya taifa letu bali pia ni msingi wa mfumo wa uchaguzi wa kuaminika”

"Tumeshinda vita ya demokrasia ya vyama vingi na ya Katiba mpya. Tutashinda vita ya uchaguzi huru na wa haki"

Wakati huo huo, Raila Odinga amewataka wafuasi wake nchi nzima kuandamana kesho kupinga kitendo cha Tume ya Uchaguzi kugoma kubadili uongozi wake.

Baada ya Tamko hilo, Mbuge Ndindi Nyoro amesema;
Kwanza mimi nafurahi sana vile amejiondoa kwa sababu ni kuonyesha wakenya ya kwamba vile tumekuwa tukisema kama watu wa Jubilee, NASA haijawahi kuwa ready kwa elections. Tulianza 8 august even before that walikuwa wanashinda kortini kulalamika huko.

Hii ni kwa sababu hawa-take any chance ya ku-face wakenya.

Maoni yangu ni kumuapisha rais wetu Uhuru, kwa sababu hatuwezi kuwa na mtu mmoja kwa sababu ya greedy yake ya kuongoza watu anazungusha nchi yetu kila siku

VIDEO:

Unapenda Habari za Siasa? Download App ya Mchambuzi Hapa Kusoma Matamko ya Viongozi

$
0
0

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako


Hapa Ndipo Mapenzi Yanapokuwa Magumu...Nimegundua Mpenzi Wangu Ametembea na Marafiki zangu Watatu Kabla yangu

$
0
0
Nimeona tu hili niliseme mana week ya 2 hii akili haijakaa sawa, nina mchumba ambaye huyu dada nlimpenda toka tukiwa natukua hapa hapa mtaanibasi ikafikia hatu sasa tumekua nataka kuoa. Nikamtafuta nikamwelekeza akanikubalia now ni mchumba wangu.

Ikatokea nimetembelewa na jamaa yangu wa mtaani katika maongezi nikamwambia nataka kuoa akasema ni jambo zuri akapenda amwone shemeji. Nikamwonesha picha akachea sana yaani akacheka mpaka machozi yakamtoka akanambia unataka kumwoa huyu kicheche? Nikashtuka kidogo, anasema anamfahamu vizuri huyo msichana, yeye alishapiga kipindi msichana yupo form 2 amechezea sana mpaka alipofika form 3 ndo akaachana naye alipogundua anatoka na jamaa yetu wa mtaani mwingine ambaye walikuwa wanapenda kumuita Etoo sababu yeye alikuwa anajiita ni striker kwa wasichana, akanambia anamfahamu ndani nje ana alama kidogo chini ya kalio la kushoto aliumia siku moja wakiwa wote kwenye jumba bovu, yule dada kweli anayo hii alama.

Nikamtafuta striker kwa maongezi ya kawaida nikamuuliza anamfaham x akasema anamfahamu yule msichana ana mwili flani hivi, macho na nikasema ndo yeyeakanambia alimdate kama mwaka hivi na nusu akampiga chini hajui kwa sasa yupo wapi.

Sasa juzi juzi hapa yule mchumba wangu aliweka picha yangu kwenye prof yake whatsapp kumbe kuna jamaa yangu ananifaham aliiona. Akanipigia kuwa kuna mtoto mmoja anaweka picha yangu kwneye prof yake ni nani yangu. Nikasema ni mchumba akanambia niache masikhara, nikamwambia ni kweli akasema "anyway kama umeamua ni sawa anadai yeye mara ya mwisho alikuwa na yule binti ni mwaka jana May walikuwa wote Zanzibar kwenye training wakawa wanatoka toka siku mbili tatu basi akamkamatia room kwake akala baadaye yule msichana akahamia roo ya hotel aliyofikia jamaa kwa week 2 jamaa analala naye kama mkewe naye akanambia anamfahamu na anajua sana kukatika ni kweli yule dada anajua sana tena akaenda mbali kuwa akiwa na hamu huwa yote ni kweli kabisa.

Nikaanza kumchunguza yule dada nikakuta namba mbili za wale wahusika anazo kwenye simu yake nikamuuliza ni akina nani akajibu ni marafiki alikataa kabisa kuwa hawajahi kuwa nao kimapenzi. Nilipoendelea kumbana akakubali mmoja mwingine akasema hajawah nikaendelea kumbana sana akaja akasema ni kweli ila hakukaa naye sana nikamwambia habari za Zanzibar akakiri ni kweli alifanya naye mara mbili tu, nikamwambia aniambie ukweli akaja akakiri walilala wote week moja na nusu ila walikuwa wanatumia kinga, jamaa anasema ni siku moja tu walitumia kinga siku nyingine zote hawakutumia.

Nimembana ameamua kunieleza kuwa ni kweli wote watatu aliwa date ila anasema ni issues za zamani hata mimi nli date watu so wala si big dea ila kiukweli naona kuna kitu kimebadilika hawa jamaa zangu watakujaje home? Watakujaje kwenye harusi? Nitawatizamaje? Hata hamu ya ku do naye imekatika kabisa maana napokuwa naye naona hao jamaa hasa huyo etoo. namfahamu ni mwaribifu sana hafai.

Huwa anawatumia hata maeneo yasiyo rasmina nikimwangalia huyu mchumba naye nyuma ana mzigo mi sijawahi kumnanii kwa nyuma imani yangu hairuhusu na hata mimi sijiruhusu ila kuna siku kama nilikosea kidogo ielekee huko hakushtuka sana.ilikuwa kiasi kawaida tu.akanambia "wewee unapeleka wapi huko "akaniuliza kama napenda nikamwambia hapana sijawahi akanambia "kama ungenambia unapenda ningeichapa hii dudu yako."

Sasa sijui kama etoo hakuwa amemwaribu huko pia sina amani huyu dada, jamaa watatu ninaowafahamu wamepita. Je nisio wafahamu? Hata kama ameacha ila historia haifutiki nimeingiwa na doa kubwa sana, najiuliza nifanye nini? Huyu kwao mama yake ananifahamu rasmi bado ile kutangaza hasa hasa kwa familia nzima.

By Chizi Maarifa

Rais Kenyatta Amjia Juu Raila Odinga Baada ya Kutangaza Kujitoa

$
0
0
Rais Uhuru Kenyatta amemjia juu Kiongozi wa NASA Raila Odinga baada ya kutangaza kutoshiriki uchaguzi wa marudio ambao unatarajiwa kufanyika Oktoba 26 mwaka huu nchini Kenya na kusema hata kama amejitoa Katiba ya Kenya haizuia uchaguzi kutofanyika

Kenyatta amesema kuwa Odinga alitaka uchaguzi urudiwe jambo ambalo limeigharimu nchi ya Kenya fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika kujenga barabara, zingeweza kutumika kujenga mahospitali na kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi, lakini anashangaa mtu ambaye ametaka uchaguzi kurudiwa anajiengua tena.

"Rafiki yangu nasikia sasa umesema umejitoa baada ya kutupeleka peleka zaidi ya shilingi bilioni 12 hivi sasa zinatumika ili tufanye uchaguzi, pesa ambazo zingeweza kutumika kujenga barabara, zingetumika kujenga hospitali ya wananchi sasa zinatumika kwa uchaguzi ambao yeye ndiye aliitisha na sasa anasema hataki, kuna haki hapa jamanii, si mahakama ilisema IEBC haina makosa hayo masharti yote unatoa lakini tume hii si ndiyo imefanya viongozi hawa wengine wote kupatikana" alihoji Kenyatta

Mbali na hilo Kenyatta amesema kuwa wao wataendelea na mchakato wa uchaguzi kama kawaida na kusema huenda awepo au asiwepo Odinga uchaguzi utafanyika kama kawaida kama ambavyo tume ya uchaguzi ilitangaza.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images