Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Waziri Kairuki Aweka Wazi Vipaumbele vyake

0
0
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ameeleza vipaumbele  vyake katika Wizara kuwa ni pamoja na  udhibiti wa utoroshaji wa madini nchini, maslahi kwa wafanyakazi huku akiwataka watumishi kufanya kazi kwa uadilifu na weledi wa hali ya juu.

Kairuki ameyasema hayo mapema leo tarehe 10 Oktoba, 2017 jijini Dar es Salaam  alipozungumza na  watumishi wa Wizara ya Madini pamoja na taasisi zake, waliopo Dar es Salaam na Makao Makuu  ya Wizara Dodoma. Lengo La kikao hicho lilikuwa ni kufahamiana na kupanga mikakati  ya kushirikiana ili kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa Uchumi wa nchi.

Taasisi zilizoshiriki katika kikao hicho ni pamoja na  Wakala wa Jiolojia  Tanzania (GST), Shirika la Madini la  Taifa (STAMICO), Chuo cha Madini Dodoma (MRI) pamoja na Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini na Mpango wa Kuongeza Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia ya Uziduaji (TEITI).

Amesema kuwa Sekta ya Madini  inatarajiwa kuwa na mchango mkubwa wa ukuaji wa uchumi wa nchi na kuwataka wataalam wa madini kubuni mbinu za ukusanyaji wa maduhuli pamoja na kuboresha mazingira ya uwekezaji kwenye uchimbaji madini.

Katika hatua nyingine aliwataka wataalam hao kubuni mikakati  ya kuzuia utoroshaji wa madini nchini ili nchi ipate mapato stahiki.Amewataka watumishi kuepuka kufanya kazi kwa mazoea na kuwa wabunifu ili  sekta hiyo iwe na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi.

Naye Naibu  Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amewakumbusha  watumishi kuzingatia Dira na Dhima ya Wizara  ikiwemo kufanya kazi kwa tija ili hatimaye  sekta ya madini iweze kuchangia katika uchumi wa nchi kwa kuwa mchango wa sekta husika bado ni kidogo.

Freeman Mbowe Ashauriwa Kumtafuta Dr Slaa ili Kuokoa Jahazi Kwenye Chama

0
0
Mmoja wa Madiwani ambao wamehamia CCM wakitoka CHADEMA mkoani Arusha waliokumbwa na skendo ya kununuliwa, amemtaka Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, kumtafuta aliyekuwa katibu wake Mkuu Wilbroad Slaa, ili kuokoa jahazi kwenye chama.

Kwenye video ambayo anaonekana akizungumza,  aliyekuwa diwani wa kata ya Kimandolu Mchungaji Rayson Ngowi, amesema kuna haja ya kutafuta hekima za Wilbroad Slaa, ili kukisaidia chama hicho kukaa kwenye mstari unaofaa, kwa kuwa sasa kimeanguka kwa kiasi kikubwa.

Bwana Ngowi amesema hata yeye kutoka CHADEMA ameondoka kwa kutaka mwenyewe na sio kununuliwa kama inavyodaiwa, na kwamba kuna wengine watakaofuata nyuma yao baada ya wao kuondoka kwenye chama hicho.

“CHADEMA ya leo sio ile ya Dkt Slaa, CHADEMA ya leo ni  ya maslahi, CHADEMA ganganjaa, na wakikataa mimi nitasema, sikiliza Mbowe, chama chako kina matatizo makubwa, huna viongozi, kamtafute Dkt. Slaa nafikiri ataokoa jahazi, kama mnataka kurudisha imani, kwa sababu sio mimi tu nimeondoka watakuja wengi”, amesema diwani huyo.

Hali ya Uchumi ni Mbaya- Zitto Kabwe

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa uchumi wa nchi unazidi kudidimia na thamani ya shilingi inazidi kushuka huku mfumuko wa bei ukizidi kupaa.

Zitto Kabwe anasema kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ambayo jana ametoa taarifa yake juu ya hali ya uchumi nchini ni kwamba hali si nzuri kwani uchumi umeonyesha kusinyaa na kudidimia huku wananchi wa hali ya chini wakiwa wahanga wakubwa zaidi.

"Taarifa hiyo inaonyesha namna hali ya uchumi wetu inavyozidi kuwa mbaya zaidi kwa wananchi wa hali ya chini , kwa mfumuko wa bei umepanda mno tangu kuanza kwa utekelezaji wa bajeti ya 2017/18, ongezeko ambalo limechangiwa zaidi na kupanda kwa bei ya bidhaa za chakula (bidhaa ambazo wananchi wengi zaidi wanazitumia)" alisema Zitto Kabawe

Aidha Zitto Kabwe amedai kushuka kwa thamani ya sarafu ya Tanzania kumezidi kuongeza maumivu kwa wananchi na ili kusaidia kupunguza ukali na gharama za maisha mishahara ilipaswa kupanda kwa asilimia 8 zaidi.

"Thamani ya sarafu ya Tanzania imeshuka, uwezo wa Tsh. 100 kununua bidhaa umeshuka hadi Tsh. 92.18. Maana yake ni kuwa mwaka 2016 shilingi 100,000 ilikupa bidhaa za shilingi 100,000. Mwaka huu 2017 shilingi 100,000 inakupa bidhaa za shilingi 92,000. Kwa hiyo ili upate bidhaa za shilingi laki moja inakubidi uongeze shilingi elfu 8 zaidi. Kiuchumi, ili kulinda hali za wananchi, mishahara ilipaswa kupanda kwa asilimia 8 ili kuwapunguzia maumivu ya gharama za maisha. Lakini hali hiyo inatokea katika wakati ambao mishahara haijapanda, na Rais wa nchi yetu kasema Serikali anayoingoza haitapandisha kabisa mishahara. Hali ni mbaya mno mtaani, mijini uzalishaji wa bidhaa za viwanda umeshuka kwa zaidi ya nusu, kutoka trilioni 1.5 mpaka bilioni 700 tu" alisisitiza Zitto Kabwe

Mbali na hilo Zitto Kabwe ametoa ushauri wa nini serikali inapaswa kufanya ili kukabiliana na hali hiyo na kupunguza ukali wa maisha kwa wananchi, Zitto amedai Serikali inapaswa itazame namna inatekeleza mipango yake ya Maendeleo, Serikali isikilize na kufanyia kazi mawazo ya sekta binafsi katika kuweka sawa mazingira ya uwekezaji bila kupoka haki ya nchi kufaidi na rasilimali zake na pia ameitaka serikali ifanyie kazi haswa uchumi wa vijijini kwa kurekebisha mapungufu yote yanayoshusha uzalishaji kwenye sekta ya kilimo.

Je,una Upungufu Wa Nguvu Zakiume,kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa,kufika Kileleni Mapema Na Kushindwa Kurudia ?

0
0

Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa na mambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA nk.

Upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa, mahusiano mengi kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,
1 KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA
2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA
3 KUWAHI KUFIKA KILELENI
4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI
5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO LA NDOA KABISA.

TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.

PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK

WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha vidonda vya tumbo,korodani kuvimba,na anatoa dagu za utajiri kwa wanaohitaji bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM, NAUTALETEWA POPOTE ULIPO TIBA HII

SIMU; NO 0767145357/0629034550.
WHATS APP 0759030343 

Freeman Mbowe Ashauriwa Kumtafuta Dr Slaa ili Kuokoa Jahazi Kwenye Chama

0
0
Mmoja wa Madiwani ambao wamehamia CCM wakitoka CHADEMA mkoani Arusha waliokumbwa na skendo ya kununuliwa, amemtaka Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, kumtafuta aliyekuwa katibu wake Mkuu Wilbroad Slaa, ili kuokoa jahazi kwenye chama.

Kwenye video ambayo anaonekana akizungumza,  aliyekuwa diwani wa kata ya Kimandolu Mchungaji Rayson Ngowi, amesema kuna haja ya kutafuta hekima za Wilbroad Slaa, ili kukisaidia chama hicho kukaa kwenye mstari unaofaa, kwa kuwa sasa kimeanguka kwa kiasi kikubwa.

Bwana Ngowi amesema hata yeye kutoka CHADEMA ameondoka kwa kutaka mwenyewe na sio kununuliwa kama inavyodaiwa, na kwamba kuna wengine watakaofuata nyuma yao baada ya wao kuondoka kwenye chama hicho.

“CHADEMA ya leo sio ile ya Dkt Slaa, CHADEMA ya leo ni  ya maslahi, CHADEMA ganganjaa, na wakikataa mimi nitasema, sikiliza Mbowe, chama chako kina matatizo makubwa, huna viongozi, kamtafute Dkt. Slaa nafikiri ataokoa jahazi, kama mnataka kurudisha imani, kwa sababu sio mimi tu nimeondoka watakuja wengi”, amesema diwani huyo.

Fuvu na Viungo Vingine vya Binadamu Yyaokotwa

0
0
Akiongea na waandishi wa habari Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Simon Haule amedai kuwa jana watu walipoona viungo hivyo vya binadamu ilibidi kutoa taarifa kwa jeshi la polisi na wao walifika na kukuta viungo hivyo.

 "Fuvu la kichwa limepatikana hapo bwawani, taya ya binadamu, mbavu za binadamu kumi na nne, baada ya kupatikana kwa taarifa hizo jeshi la polisi lilichukua hatua za haraka kufika eneo la tukio kwa ajili ya uchunguzi wa awali tukishirikiana na daktari mtaalam wa viungo vya binadamu katika tukio hilo tulikuta viungo hivyo ikiwa pamoja na mfupa mmoja wa sehemu ya paja, mifupa ya mikono na mifupa ya sehemu ya bega ya binadamu" alisema Simon Haule 

Aidha Kamanda Haule amesema kuwa uchunguzi wa tukio hilo unaendelea ikiwa pamoja na kufungasha mifupa yote na kupeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kufanya vipimo kubaini vinasaba na jinsia ya mtu ambaye amefariki.

Rais Magufuli Azushiwa Taarifa ya Uongo Mtandaoni

0
0
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa amekanusha taarifa zinazosambazwa mitandaoni kumhusu Rais Dkt John Pombe Magufuli na kutaka wananchi kuzipuuza.

Msigwa, kupitia ukurasa wake wa Twitter amekanusha taarifa zinazodai kuwa leo Oktoba 10 ni siku ya kuzaliwa ya Rais Magufuli, huku akisema kuwa tarehe sahihi ya kuzaliwa ya kiongozi huyo wa nchi ni Oktoba 29.

 “Taarifa zinazoenezwa kuwa leo tarehe 10.10 ni siku ya kuzaliwa kwa Rais Magufuli sio kweli. Mhe. Dkt John P.J. Magufuli alizaliwa 29.10.1959.”



Watu wengi waliotoa maoni yao kuhusu kanusho hilo, wamesema kwamba hawajaiona taarifa yenyewe inayosema leo ni siku ya kuzaliwa ya Rais, lakini wengine wakaeleza kwamba, hiki hakikuwa kitu cha msingi cha kukanusha kwani tarehe ya kuzaliwa ya Rais inaweza kupatikana kirahisi mtandaoni.

Chadema Yapata Pigo Lingine

0
0


Chama cha mapinduzi (CCM) manispaa ya Iringa kimeendelea kujiimarisha kwa kuvuna wanachama watano kutoka chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) manispaa ya Iringa wakiwa na mikakati ya kuja kulikomboa jimbo la Iringa mjini ambalo lipo chini ya chama cha CHADEMA.

Akizungumza wakati wa kuwapokea wanachama hao kutoka kata ya kitwiru mwenyekiti wa CCM manispaa ya Iringa Said Rubeya aliwapongeza wanachama kwa kutambua kazi inayofanywa na chama cha mapinduzi chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano DR John Pombe Magufuli.

“Mimi nimefurahi sana nyie kurudi nyumbani maana mtakuwa na msaada mkubwa sana katika kukijenga chama hapa manispaa ya Iringa ili tuweze kulikomboa jimbo hili katika uchaguzi ujao na hii ndio mikakati yetu” alisema Rubeya.

Rubeya aliwaambia wanachama hao kuwa sasa wapo katika mikono salama ya kisiasa tofauti na walipokuwa kwenye chama cha awali na kuwasihi wasiwe waoga katika kufanya kazi za kukijenga chama cha mapinduzi.

“CCM ndio chama tawala hivyo ondoeni hofu na mzidi kutupa maarifa mliyotoka nayo huko na kukisaidia chama hiki kuzidi kupata wananchama wengi kutoka vyama vya upinzani na mkiwa CCM mtapikwa vizuri na kuwa viongozi wazuri” alisema Rubeya.

Aidha Rubeya aliwaambia kuwa CCM hutoa madaraka kwa mtu yeyote yule mwenye weledi katika nafasi aliyogombea, hivyo huku hakuna kuteuana huku kuna nafasi za kugombea na kuchaguliwa na wanachama wa chama cha mapinduzi tofati na kule mlikokuwa mnateuna kwa maslai ya mtu mmoja.

Naye katibu wa chama cha mapinduzi manispaa ya Iringa Marko Mbaga aliwataja wanachama waliohamia chama hicho kutoka CHADEMA ni Baraka Kimata aliyekuwa katibu mwenezi na Diwani wa kata ya Kitwiru,Theodora Mbata aliyekuwa matroni wa wanawake kata ya Kitwiru, Erick Muyungo na  Raymond kimata aliyekuwa kiongozi wa redbrigad manispaa ya Iringa na katibu mwenezi wa kata ya kitwiru.

“Hii ni mwanzo tu watakuja wengi mno kwa kuwa CCm manispaa ya Iringa wanachapa kazi hata kama halmashauri ipo kwa wapinzania lakini wao wataendelea kufanya kazi kwa kutekeleza ilani ya chama chetu ili kuwamaliza wapinzani wetu wote warudi kwenye chama tawala” alisema Mbaga

Edwin bashir ni katibu wa chama cha mapinduzi manispaa ya Iringa alisema kuwa sasa ni wakati wa kufanya kazi kwa wananchi na wananchi waendelee kuwa na Imani na chama cha mapinduzi ili waje kufanikiwa kulikomboa hili jimbo ambao lipo upinzani.

“Mimi najua vijana wengi muda sio mrefu wataanza kurudi nyumbani kwao kwenye chama wananchokipenda na kuondokana na siasa za maji taka kwa kuwa CCM ni tanuli za kuwahoka viongozi bora na sasa manispaa tutafanya kazi kweli kweli na kuwamaliza wapinzani kwa nguvu zote” alisema Bashir.

Baraka Kimata,Theodora Mbata, Erick Muyungo na  Raymond kimata walisema kuwa watakitumikia ipasavyo chama cha mapinduzi kama walivyokuwa wanakitumika chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA na kuhakikisha CCM wanashinda chaguzi zote watakazo kuwa wanashiriki katika manispaa ya iringa.

Kwa upande wake mbunge wa viti maalumu mkoa wa iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Ritta Kabati aliwapongeza viongozi wote wapya waliochaguliwa hivi karibuni na kuanza kufanya kazi inayoonekana machoni mwa wakazi wa manispaa hiyo.

“Juzi mmechaguliwa lakini kazi imeanza kwa kuwapata wananchama wapya wanaotoka upinzani kurudi CCM hiyo sio kazi ndogo kwa kweli hiyo ni kazi kubwa sana ambayo mmeanza nao nichukue nafasi hii kuwapongeza kwa mnachokifanya kuhakikisha tunapata wanachama wengi kutoka upinzani” alisema Kabati.

Tatizo la kukosa au Upungufu wa Nguvu za kiume Limekuwa Kubwa Sana Duniani kote..Hili Hapa Suluhisho

0
0

[BIG OFFER]
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA  (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k.
           Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

 BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
     Kwa kutumia mimea na matunda NATURAL BEAUTY PRO Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-

1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7  @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=
      BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
      @natural2162

     Wasiliana nasi Popote
  ulipo duniani kwa (+255)
           0759029968 na
              0659618585

        UTAPATA HUDUMA
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Siri ya Profesa Kitila Kun'goka ACT-Wazalendo

0
0
Siri ya Profesa Kitila Kun'goka ACT-Wazalendo
Wakati Profesa Kitila Mkumbo akitangaza kung’atuka rasmi uanachama wa ACT-Wazalendo siri kubwa imefichuka kuhusu hatua yake hiyo.

Hata hivyo, mwenyewe anasema kuwa sababu za yeye kufanya hivyo ameziweka wazi na kwamba anayetaka kusema lolote aseme.

Juzi, barua iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha imesainiwa na Profesa Kitila, ikiandikwa kwenda kwa Dorothy Semu, Kaimu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo ilimnukuu ikisema kuwa ameamua kung’atuka kwa hiyari yake.

Kwa mujibu wa barua hiyo, Profesa Kitila ilisema, “Utakumbuka kuwa nilipoteuliwa kuwa katibu mkuu wa wizara katika Serikali ya CCM nilijiuzulu nafasi yangu ya ushauri wa chama na tukakubaliana kuwa ningeendelea kuwa mwanachama wa kawaida.”

Hata hivyo, Profesa Kitila alisema uzoefu wa miezi sita wa kutumikia nafasi yake serikalini umeonyesha ni vigumu kwake kuendelea na uanachama na kutekeleza majukumu yote mawili.

Mara baada ya barua hiyo, mjadala wa sababu hasa ya kiongozi huyo ambaye alipata kuwa pia mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema kabla ya kufukuzwa uanachama ulipamba moto huku wengine wakienda mbali zaidi kwa kusema kuwa hizo ni harakati zake za kujiweka sawa kuwania kiti cha ubunge mwaka 2020 kwa tiketi ya chama tawala cha CCM.

Hata hivyo, wachunguzi wa masuala ya kisiasa walilidokeza gazeti hili sababu nne za kiongozi huyo kuamua kung’atuka uanachama wake kuwa ni pamoja na kutoaminika serikalini.

Mmoja wa watumishi wa wizara hiyo alilimbia Gazeti la Mwananchi kuwa tangu kuteuliwa kwa katibu mkuu huyo wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji amekuwa akikumbana na wakati mgumu serikalini kwani watumishi pamoja na viongozi wenzake hawamuamini na kumuona mtu hatari kufanya naye kazi.

“Hali hii ina mkwaza kikazi, wakati viongozi wenzake wakifanya maamuzi ya pamoja yeye wanamtenga, amekua kama yatima. hana uwezo wa kupata taarifa hata wanapokutana kwani wanamuona si mmoja wao,” kilisema chanzo cha habari.

Sababu nyingine ni kutoonekana timu Magufuli na kushindwa kupata fursa ya kuwa karibu naye kwa kuwa hawaoni kama ni mmoja wao licha ya kuwa katika Serikali.

Walisema kutoka kwake upinzani kulimnyima fursa kubwa ya kuwa karibu na Rais hivyo kujikuta akishindwa kupata fursa hiyo na kujikuta mpweke.

Inaelezwa pia kuwa hali hiyo imesababisha kiongozi huyo katika kipindi cha miezi sita alichokaa katika wizara hiyo kujikuta akiwa muathirika kwa kukosa nyaraka mbalimbali muhimu kutokana kutoaminika kwake na kujikuta yatima.

Sababu nyingine inayotajwa ni hatua ya Zitto Kabwe kuchukua nafasi kukosoa utawala kama alivyokuwa akifanya Mbunge wa Singida Mjini, Tundu Lissu ambaye hivi karibuni alijeruhiwa kwa risasi na watu wasiofahamika.

Inaelezwa hatua ya Zitto kuhoji na kukosoa utawala wa Serikali pamoja na Bunge katika mitandao ya kijamii na katika hotuba zake imesababisha katibu mkuu huyo kuonekana wazi kuwa ameshindwa kumdhibiti kiongozi huyo mkuu wa ACT- Wazalendo.

Inasemekana kwamba hatua hiyo ya Zitto imemuweka katika wakati mgumu Profesa Kitila ambaye ameonekana wazi hawezi kuisaidia Serikali na kwamba hata baada ya kujaribu mara kwa mara kumnyamazisha ilishindika hivyo akaona ni vyema kukaa pembeni ili asinoekane ni mmoja wao.

Sababu nyingine inayotajwa ni uamuzi wake wa kugombea nafasi ya ubunge katika jimbo la Ubungo kwa tiketi ya chama tawala.

Wachunguzi wa masuala ya siasa wanasema kuwa kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo ameamua kuwekeza nduvu zake kugombea nafasi hiyo ya ubunge ili kupambana na mbunge aliyekuwepo Saed Kubenea.

Mwenyewe afunguka

Mwananchi ilipomtafuta kujibu taarifa hizo, Profesa Kitila alisema hawezi kuzuia watu kuzungumza ila ukweli utabaki pale pale.

“Watu wana mengi yakuzungumza, wana haki ya kufanya hivyo lakini ukweli sababu ziko wazi nimeziweka katika barua yangu ya kung’atuka waisome wataielewa,”alisisitiza Profesa Kitila.

Profesa Kitila alisema kwa upande wake hakufikia uamuzi huo peke yake na kwamba aliwashirikisha viongozi wenzake na wote kwa pamoja walikubaliana.

“Tulikaa na viongozi wenzangu, tukajadili na kuwaeleza sababu za mimi kufikia uamuzi huu nao bila hiyana walikubaliana na mimi na wakabariki kitendo hiko ndipo nilipoandika barua. Kwahiyo ninachotaka watu wajue tu siyo uamuzi wangu mwenyewe.”

Alisema kilicho msukuma zaidi baada ya kupata ugumu pale anapotekeleza na kusimamia mipango na mafanikio ya Serikali ambayo yeye ni sehemu yake hivyo ili kuepuka mgongano wa wazi wa masilahi (confilict of interest), ameamua kung’atuka uanachama wake.

Hata hivyo, kiongozi mkuu wa chama hicho Zitto Kabwe alipoulizwa na gazeti hili hakuwa tayari kulizungumzia hilo.

Awali ofisa habari wa chama hicho, Abdallah Khamis alipotafutwa na Mwananchi kuzungumzia suala hilo alisema kujiondoa kwa mtu kwenye chama au kubaki ni utashi wake.

Profesa Kitila Mkumbo ni nani?

Alizaliwa 21 Juni 1971 katika Kijiji cha Mgela wilayani Iramba mkoani Singida.

Elimu

Alisoma katika Shule ya Msingi Mgela iliyoko Wilaya ya Iramba kati ya mwaka 1981-1987 kisha akajiunga Shule ya Sekondari Mwenge (Singida) na kusoma kidato cha kwanza hadi cha tano mwaka 1988-1991 na elimu ya Juu ya Sekondari akaipata pale Shule ya Sekondari Pugu kati ya mwaka 1992-1994 akijikita katika mchepuo wa PCB (Fizikia, Kemia na Bailojia).

Baada ya kuhitimu kidato cha sita alifanya kazi ya kuvua samaki katika Bwawa la Mtera huko Iringa kwa sababu ya kuwa na hali mbaya ya kiuchumi na baadaye alipata nafasi ya kwenda kujiunga na mafunzo ya polisi kwenye Chuo cha Polisi(CCP) Moshi kwa muda wa miezi miwili lakini alikatisha mafunzo baada ya kuchaguliwa kujiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM)

Alihitimu shahada yake ya kwanza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1999 akisomea Sayansi ya Elimu.

Baada ya kumaliza alianza kazi hapo hapo chuo kikuu kama Ofisa Utawala, aliifanya kazi hiyo kwa miaka minne (1999 – 2003) na wakati anafanya kazi aliendelea kusoma Shahada ya Uzamili (M.A) akibobea katika Saikolojia, alihitimu shahada hiyo mwaka 2002.

Profesa Kitila alifanya vizuri katika shahada ya uzamili na baada ya kufundisha chuo kikuu kwa miaka michache alipewa udahili katika Chuo Kikuu cha Southampton kilichoko nchini Uingereza ambako alitunukiwa Shahada ya Uzamivu akibobea pia katika saikolojia, hii ilikuwa ni mwaka 2008.

Kati ya mwaka 2009 – 2012, Profesa Kitila amefanya kazi kama mratibu wa kamati ndogo ya ufundi ya masuala ya ukimwi Mwaka 2010 hadi 2012 amekuwa Makamu Mwenyekiti wa UDASA (Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam) na kisha akachaguliwa kuwa mwenyekiti wake.

Mwaka 2009 alikuwa Ofisa anayesimamia mitihani katika Shule ya Elimu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Pia, amekuwa mkuu wa Idara ya Elimu ya Saikolojia na masomo ya Mtaala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia mwaka 2009 – 2012, amekuwa Mkuu wa Kitivo cha Elimu katika Chuo Cha Elimu cha Dar es Salaam (DUCE) na kuwa Profesa Mshiriki katika Shule ya Elimu ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam kuanzia Julai 2014.

Siasa

Profesa Kitila alianza siasa kama mwanachama wa CCM, baadaye alijiunga Chadema kawa mshauri muhimu wa chama hicho.

Mwaka 2014, Profesa Kitila alifukuzwa katika chama chake cha Chadema kwa tuhuma za kuandaa waraka wa mapinduzi na kukihujumu chama hicho, Kitila alitangaza kuwa angeshirikiana na Zitto Kabwe kuanzisha chama kipya ambacho hivi sasa kinajukana kama ACT – Wazalendo.

Mwaka 2017 Rais John Magufuli alimteua Profesa Kitila kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji nafasi ambayo anahudumu mpaka sasa.

Mke wa Sheikh Jumuiya ya Uamsho Ambaye Mumewe yuko Mahabusu AJINYONGA

0
0
Mke wa Sheikh Suleiman Othman mmoja wa wafuasi wa Jumuiya ya Uamsho wanaoshikiliwa mahabusu Tanzania Bara amejiua kwa kujinyonga.

Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja imesema Rahma Mussa Koki (28) alijiua kwa kujinyonga Jumapili

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Hasina Ramadhan Taufiq amesema watu watano wamehojiwa wakiwemo wazazi wake kuhusu tukio hilo.

Amesema katika mahojiano bado hawajatambua sababu za mwanamke huyo kujinyonga.

“Katika hatua za awali tumesikia alianza kuugua maradhi ya akili na huenda yakawa chanzo cha yeye kuijua,” amesema Taufiq.

Amesema licha ya watu hao kuhojiwa, hakuna wanayemshikilia.

Kamanda Taufiq amesema kazi ya Jeshi hilo ni kuhakikisha wanaendelea na upelelezi na utakapokamilika watatoa taarifa.

Wakati huohuo, Safia Kombo Sheha, mama mzazi wa Rahma amesema kabla ya kifo chake alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya akili na alipatiwa matibabu mara kadhaa.

“Kabla ya kifo chake kama wiki nzima alikuwa akisema nitajinyonga nasi tukawa karibu naye kila wakati kwa kujua ni
mgonjwa. Jumapili asubuhi tulikuwa pamoja ila niliondoka kidogo. Niliporudi nilikuta mlango wa chumbani kwake umefungwa, tulipouvunja tulikuta akiwa amejinyoka kwa kutumia kamba,” amesema.

Safia amesema baada ya ndugu na majirani kufika walibaini alishafariki. Tukio hilo amesema lilitokea saa nne asubuhi, eneo la Kigunda, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Rahma ameacha watoto watatu, wawili wakiwa wa kike.

Diamond Platnumz Ameingia Kwenye Maandalizi ya Kazi Mpya na Rick Ross.

0
0
Diamond Platnumz Ameingia Kwenye Maandalizi ya Kazi Mpya na Rick Ross.
Msanii wa muziki nchini ambaye anafanya vizuri kimatiafa, Diamond Platnumz Jumanne hii ameingia location kwaajili ya maandalizi ya kazi mpya akiwa na msanii mkubwa wa Hip Hip kutoka Marekani, Rick Ross.


Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo, Hallelujah ameonekana katika video na picha wakishoot Kazi hiyo ambayo haijajulikana ni kazi na namna gani.

Meneja wa kimataifa wa muimbaji huyo, Sallam amethibitisha kwamba wawili hao wameingia location kwaajili ya maandalizi ya Kazi hiyo.



“Diamond Platnumz x Rick Ross On set now somewhere in Miami #BlackBottleBoys and we never stop!!,” aliandika Instagram Sallam.

Rick Ross na Diamond wote ni mabalozi wa kinywaji cha Belaire ndio maana wanajiita BlackBottleBoys.

Ndege za Kivita za Marekani Zapaa Rasi ya Korea

0
0
Ndege za Kivita za Marekani Zapaa Rasi ya Korea
Marekani kwa mara nyingine imefanya mazoezi ya kijeshi kwa pamoja na Korea Kusini, ambapo ndege zake mbili za kivita za kuangusha mabomu zimepaa juu ya rasi ya Korea.
Ndege hizo za kutekeleza mashambulizi aina ya B-1B zimepaa angani pamoja na ndege za kivita za Korea Kusini aina ya F-15K.
Ndege hizo zimetekelesha amzoezi ya kurusha makombora kutoka angani hadi ardhini katika maji ya bahari ya KOrea Kusini.
Mazoezi hayo yamefanyika huku wasiwasi na uhasama kati ya Marekani na Korea Kaskazini kuhusu mpango wake wa nyuklia ukizidi.
Pyongyang majuzi ilitekeleza jaribio lake la sita la silaha za nyuklia na pia imerusha makombora kupitia anga ya Japan mara mbili miezi ya karibuni.
Ndege hizo za Marekani zilipaa kutoka kisiwa chake cha Guam katika Bahari ya Pacific Jumanne usiku kabla ya kuingia anga ya Korea Kaskazini na kufanya mazoezi katika Bahari ya Mashariki na Bahari ya Manjano, jeshi la Korea Kusini limesema.
Trump: Ningependa kukutana na Kim Jong-un
Trump na Kim Jong-Un waitana ''wenda wazimu''
Rais wa K.Kaskazini asema Trump atalipia kauli zake
Mazoezi hayo yalikuwa sehemu ya mpango mkubwa "wa kuzuia kupitia vitisho" vitendo vya Korea Kaskazini, jeshi hilo lilisema.
Marekani imesema jeshi la wana anga la Japan pia limeshiriki mazoezi hayo.
Rais wa Marekani Donald Trump alikutana na maafisa wakuu wa usalama Jumanne usiku kujadili njia za kukabili vitisho vya Korea Kaskazini, ikulu ya White House ilisema.
Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un wamejibizana wiki za karibuni.
Donald Trump na Mike Pence in Bedminster, New Jersey, on 10 August 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image caption
Trump Agosti alisema Kim Jong-un atajuta sana, na upesi sana, iwapo atatishia kisiwa cha Guam tena
Akihutubu Umoja wa Mataifa Septemba, Trump alisema Bw Kim yupo kwenye "safari ya kujiandamiza".
Kim naye alimweleza Trump kama mzee aliyepungukiwa na uwezo wake wa kiakili na kuahidi kumfunza adabu kwa moto.
Jumatano, mbunge wa Korea Kusini alisema wadukuzi kutoka Korea Kaskazini walidukua mitambo na kuiba shehena kubwa ya nyaraka za siri za jeshi la Korea Kusini, ikiwa ni pamoja na mpango wa kumuua Kim Jong-un.
Trump: Korea Kaskazini watakuwa kwenye 'shida kubwa'
Marekani na Korea Kaskazini nini kimebadilika?
Korea Kaskazini yasema itazamisha meli ya Marekani
Aidha, kulikuwa na mpango wa hatua za kukabili Korea Kaskazini wakati wa vita ambao ulikuwa umeandaliwa an Marekani na Korea Kusini kwenye nyaraka hizo.
Wizara ya Ulinzi ya Korea Kusini ilikataa kuzungumzia madai hayo ambayo yalikanushwa na Korea Kaskazini.
Mambo sita unayofaa kufahamu kuhusu kisiwa cha Guam
Mambo 42 aliyoyafanya Donald Trump akiwa likizoni
Mambo muhimu kuhusu hali ya kijeshi rasi ya Korea

Watumishi na Madiwani Waingia Kwenye Mgogoro na Mkuu wa Wilaya ya Gairo

0
0
Watumishi na Madiwani Waingia Kwenye Mgogoro na Mkuu wa Wilaya ya Gairo
Watumishi na madiwani wameingia kwenye mgogoro na Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Nchembe kutokana na hatua yake ya kuwaweka rumande.

Hatua hiyo imesababisha baadhi ya watumishi na madiwani kuiomba Serikali kuchukua hatua kutatua mgogoro huo wa utendaji.

Nchembe anatuhumiwa kuagiza kukamatwa na kuwekwa ndani Diwani wa Msingisi, Stephano Mganga baada ya wananchi kupasua bomba na kuchota maji kwa ajili ya kuyauza.

Ilielezwa kuwa mkuu wa wilaya aliamuru diwani huyo kukamatwa kwa kushindwa kudhibiti tatizo hilo, lakini baada ya kuhojiwa aliachiwa.

Mganga alisema alikamatwa kwa agizo la mkuu wa wilaya akidaiwa kuchochea wananchi wasitoe mchango wa Mwenge.

Pia, Mganga alisema tayari ameitwa mara ya tatu polisi kuhojiwa kuhusu kutoa maelekezo ya ratiba ya mgawo wa maji tofauti na aliyotoa mkuu wa wilaya.

Alisema ratiba waliyojipangia ni kupata maji kila baada ya saa mbili, lakini mkuu wa wilaya aliagiza badala ya muda huo wapate kwa saa sita jambo ambalo diwani huyo hakuliafiki kwa kuwa lingesababisha wananchi wengine kukosa huduma.

“Mara zote tatu nilizohojiwa na kuachiwa ni kwa busara za mkuu wa kituo cha polisi, kwa kuwa DC alitaka nilazwe rumande,” alisema.

Mwingine ambaye ameonja ‘kibano’ cha mkuu wa wilaya ni Meneja wa Maji wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Gairo, Herman Mundo aliyewekwa rumande kwa saa 13 kutokana na majibu yake ya barua kwa Nchembe.

Mundo alisema alipokea barua ya mkuu wa wilaya ikimtaka aongeze muda wa mgawo wa maji kutoka saa mbili hadi sita kwa siku.

“Nilipokea barua hiyo nikamjibu kitaalamu kwamba suala hilo ni gumu kwa kuwa maji yanayopatikana ni kidogo ndiyo maana tunagawa kwa saa mbili, lakini baada ya kupokea barua alisema nimemjibu jeuri, nilikamatwa na kuwekwa ndani,” alisema.

Alikamatwa Agosti 6 na kushikiliwa kwa saa tatu kabla ya kuachiwa ili akahudhurie mkutano wa wahandisi ulioitishwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Morogoro (Moruwasa).

Mundo alisema aliporejea hakuripoti polisi, Agosti 11 alikamatwa ili kukamilisha muda wa saa 48 kama ilivyokuwa imeagizwa na mkuu wa wilaya.

Alisema alishikiliwa saa tatu asubuhi na kuachiwa saa tano usiku kutokana na agizo kutoka mamlaka za juu.

Orodha ya walioonja joto

Wengine waliowekwa ndani na kulala siku moja ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Magoeko, Daudi Mbena (40) kutokana na kutoitisha mikutano ya kitongoji.

Pia, mwandishi wa Mbena wa mihtasari ya vikao vya wananchi, Chitemo (61).

Kauli ya DC, mkurugenzi

Nchembe alisema aliagiza Mbena na Chitemo wawekwe ndani ili kuwanusuru wasipigwe na wananchi kwenye mkutano.

“Siku hiyo nilikwenda kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa ili kutatua mgogoro kati ya wananchi na mwenyekiti huyo, vurugu zilipotokea wananchi wakisema hawamtaki na walitaka kuwapiga nikaita polisi wakawachukua,” alisema.

Kuhusu tuhuma za madiwani na watumishi wengine wa halmashauri, Nchembe alisema zimeshaundwa kamati za kufuatilia migogoro hiyo, hivyo hawezi kuzizungumzia.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Agnes Mkandya hakuwa tayari kuzungumzia hilo kwa madai kuwa imeundwa kamati.

“Jamani hatuwezi kuzungumzia tena haya mambo kwenye vyombo vya habari, ebu tuacheni tayari kamati ilishatuhoji,” alisema Mkandya.

Matokeo ya kamati

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Rachel Nyangasi aliziomba mamlaka kuwapatia taarifa ili waweze kuzifanyia kazi. “Tumehojiwa na kamati mbili zilizoundwa na Serikali kufuatilia mgogoro huo, tunaomba zilete majibu kama tunatakiwa tujirekebishe tufanye hivyo ili mambo yaende,” alisema.

Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari alisema kuwa tayari kamati zimekamilisha kazi na ripoti zimeshawasilishwa kwa mamlaka husika kwa hatua zaidi.

Hivi karibuni Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby alimuomba aliyekuwa Naibu Waziri wa Nchi (Tamisemi), Suleiman Jafo kutatua mgogoro uliopo kati ya mkuu wa wilaya, mkurugenzi wa halmashauri na baadhi ya wakuu wa idara.

Aslay Afunguka Bifu Lake na Beka Asema Wao ni Washkaji Mashabiki ndo Wanakuza

0
0
Aslay Afunguka Bifu Lake na Beka Asema Wao ni Washkaji Mashabiki ndo Wanakuza
HUKU kukiwa na fununu za kuwepo kwa bifu zito kati ya Aslay na mwanamuziki mwenzake Beka Flavor, ambao walifanya kazi pamoja katika Yamoto Band, msanii huyo amefunguka kuwa hakuna bifu lolote kati yao.
Akizungumza na Risasi Vibes, Aslay alisema kwa muda mrefu amekuwa akihusishwa kuwa katika msigano na Beka Flavor kitu mbacho si kweli kwani wao ni washkaji licha ya kutofanya kazi pamoja kwa sasa.
“Mimi na Beka ni washkaji vibaya sana, tena mara ya mwisho kuwasiliana naye ilikuwa jana (juzi), mashabiki ndiyo wanakuza mambo hayo lakini ukweli ni kwamnba sina bifu na Beka,” alisema Aslay.

Simbeye Anusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali ya Gari

0
0
Simbeye Anusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali ya Gari
Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), Edward Simbeye amepata ajali ya gari.

Simbeye alikuwa akitokea Dar es Salaam kwenda Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano asubuhi, Simbeye amesema ajali hiyo ilisababishwa na tairi la mbele kushoto kufyatuka hivyo gari kupoteza mwelekeo na kuanguka kando mwa barabara eneo la Kawawa mjini Moshi.

“Namshukuru Mungu nimetoka salama mimi na mdogo wangu… nilikuwa nakwenda nyumbani kwa sababu za kifamilia,” amesema Simbeye.

Zitto Kukimbilia Mahakamani Kupinga Uteuzi wa Rais Magufuli

0
0
Zitto Kukimbilia Mahakamani Kupinga Uteuzi wa Rais Magufuli
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) amesema Jumatano hii ataenda Mahakamani kupinga uteuzi wa nafasi ya Katibu wa Bunge uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli Jumamosi iliyopita.


Uteuzi huo ulienda sambamba na uteuzi wa Mawaziri ambapo baadhi ya mawaziri walibadilishwa na wengine kuongezwa.

“Katika kulinda utawala wa sheria nchini kwetu, pia Uhuru na Hadhi ya Mhimili wa Bunge, Leo tarehe 11/10/2017 tunawasilisha mahakamani ombi la kutengua uteuzi wa Katibu wa Bunge na kutaka mchakato wa kisheria ufuatwe katika kumpata Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” aliandika Zitto Facebook.

Rais Magufuli alimteua Katibu mpya wa Bunge na yule ambaye alikuwa akifanya shughuli hiyo kuahidi kumpangiwa kazi nyingine.

Zitto alisema uteuzi wa Katibu wa Bunge uliofanywa na Rais John Magufuli ni batili Kwa mujibu wa Sheria ya Utawala wa Bunge, sheria namba 14 ya mwaka 2008 ikisomwa pamoja na Katiba ya JMT ibara ya 87.

Alisema Katiba inatoa Mamlaka Kwa Rais kuteua na sheria inaweka utaratibu Wa kutekeleza mamlaka hayo ya Katiba.

TPSF: Serikali Inapaswa Kuufanyia Kazi Ushauri wa Dngotena Si Kuupuuza

0
0
TPSF: Serikali Inapaswa Kuufanyia Kazi Ushauri wa Dngotena Si Kuupuuza
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imesema Serikali inapaswa kuufanyia kazi na si kuupuuza ushauri uliotolewa na bilionea namba moja barani Afrika, Aliko Dangote.

Juzi, Dangote alimtahadharisha Rais John Magufuli kuwa vitendo vyake vinaogofya na kukimbiza wawekezaji nchini.

Dangote alilaumu sera za Serikali akisema, “zinawatisha wawekezaji wengi. Kuwatisha wawekezaji si kitu kizuri. Mmoja akitishwa wengine watakimbia bila hata kuhitaji maelezo.”

Malalamiko hayo aliyatoa jijini London, Uingereza anakohudhuria kongamano la wawekezaji wa Afrika lililoandaliwa na gazeti la Financial Times.

Akitoa maoni yake jana kuhusu kauli hiyo ya Dangote, mkurugenzi mkuu wa TPSF, Godfrey Simbeye alisema mwekezaji huyo ni mkubwa na anapozungumza anasikika ndani na nje ya Afrika hivyo kutoufanyia kazi ushauri wake kunaweza kuligharimu Taifa.

“Alichokisema ni ushauri tu, Dangote ni mwekezaji mkubwa, amewekeza ndani na nje ya Afrika. Sidhani kama ushauri wake unaweza usifanyiwe kazi na mimi nashauri ufanyiwe kazi si kuupuuza,” alisema Simbeye na kuongeza:

“Serikali iufanyie kazi kama ana hoja zifanyiwe kazi si kuzipuuza na kama hana hoja ajibiwe, yule si mtu wa kumbeza. Mtu kama huyu mwekezaji mkubwa anapozungumza kitu tunapaswa kukiona na kukifanyia kazi, ni wakati wa Serikali kuupokea ushauri wake.”

Simbeye alisema kwa uzoefu wake katika nchi mbalimbali anachokizungumza mfanyabiashara huyo kina tija hivyo ni wakati sasa Serikali kupokea ushauri huo.

Kwa upande wake, kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Kabwe Zitto alisema Serikali isikilize na kufanyia kazi mawazo ya sekta binafsi katika kuweka sawa mazingira ya uwekezaji bila kupoka haki ya nchi kufaidika na rasilimali zake.

“Kwa mfano hoja aliyotoa ndugu Dangote si ya kupuuza kwani kwa kawaida mitaji huona aibu. Serikali ijiondoe kwenye mentality (dhana) kuwa uwekezaji ni kupata kodi tu, la hasha,” alisema Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Mjini na kuongeza:

“Kwa demografia ya Tanzania, ambapo watu milioni 1.6 huingia kwenye soko la ajira kwa mwaka, ajira yapaswa kuwa lengo kubwa la Serikali katika kuvutia mitaji kutoka nje na vilevile ndani.”

Zitto pia aliitaka Serikali ifanyie kazi uchumi wa vijijini kwa kurekebisha upungufu wote unaoshusha uzalishaji kwenye sekta ya kilimo ikianza na pembejeo, masoko na viwanda vidogo vya kuongeza thamani ya mazao.

Mtaalamu wa uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Humphrey Moshi alisema ufike wakati wawekezaji wasigeuke miungu watu wadogo huku akiishauri Serikali kuendelea na mikakati yake ya kuimarisha uwekezaji.

“Tumpuuze tu, mazingira ya sasa ya biashara yanahitaji uwazi na ili uwe wazi lazima upinge rushwa na dhana ya ‘win win situation’. Unapomuona mwekezaji kaja kwako kuna kitu kakiona sasa ukiona anaanza kusema vikwazo kuna jambo,” alisema Profesa Moshi.

Alisisitiza kuwa, “sisi tuendelee na tunayoyafanya, wao wanatafuta faida na sisi tunatafuta, ndiyo dhana ileile niliyoisema win win situation. Inawezekana huko nyuma kulikuwa na njia za namna namna ambazo sasa hazipo.”

Hata hivyo, akizungumza na Mwananchi jana, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alisema: “Mimi sina ubishi na Dangote na hatuwezi kupuuza ushauri wake kwani uwapo wake nchini umefanikisha kubadili hata bei ya saruji.”

“Nimezungumza na Dangote na amekwisha kuzungumza pia na viongozi wangu wa juu na tunatambua uwekezaji wake hapa nchini,” alisisitiza Mwijage.

Waziri huyo alisema kinachotakiwa kufanyika kwa sasa ni kusubiri kuhitimishwa kwa majadiliano ya sakata la mchango wa madini (makinikia) kati ya Serikali na wawekezaji wa kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo yatafungua mlango mpya wa sekta hiyo. Dangote amewekeza nchini Dola 500 milioni za Marekani (zaidi ya Sh1.1 trilioni) na anaona sheria hiyo haitendi haki na itawakimbiza wawekezaji.

Malalamiko ya Dangote yanatokana na sheria mpya ya usimamizi wa rasilimali za Taifa iliyopitishwa na Bunge mwezi Julai inayopendekeza Serikali kuwa na walau asilimia 16 kwenye miradi yote iliyowekezwa kwenye sekta ya madini.

Mkemia Mkuu Ato Siri ya Kupimwa Mkojo kwa Wahalifu

0
0
Mkemia Mkuu Ato Siri ya Kupimwa Mkojo kwa Wahalifu
Mkemia Mkuu wa serikali Profesa Samuel Manyele ametoa sababu inayowafanya kupima mkojo wa watu wanaotuhumiwa uhalifu mbali mbali, jambo ambalo liliibua mzozo mkubwa lilipotakiwa kufanyika kwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Prof. Manyele amesema mpelelezi ana haki ya kutaka kitu ambacho kitamuongoza kwenye upelelezi wake, hivyo yeye kama mkemia mkuu huhitaji mkojo kwa kuwa mkojo ndio husafisha mwili, na ndio sampuli pekee ambayo utaipata kwa muhusika bila kutoboa mwili wake, ili kugundua iwapo mtuhumiwa amefanya kosa kutokana na matatizo ya akili.
"Wapelelezi wana haki ya kuchukua kielezo chochote, kama mtu amefanya kosa kwa kutumia kitu ambacho kinaharibu akili mfano dawa za kulevya, bangi au mirungi, maana yake ni kwamba uthibitisho wake utapatikana kutoka mwilini mwake, na sampuli ambayo mkemia mkuu anaitumia ambayo haihusiani na kutoboa mwili wa mtu ni mkojo, mkojo ndio unasafisha mwili, kemikali zote tata zinapita kwenye mkojo, kwa hiyo sisi tukiipata tunachunguza kuna nini, lengo hasa ni kuangalia matumizi ya vitu ambavyo huenda vinampelekea kufanya uhalifu", amesema Prof Manyele.
Hivi karibuni kumekuwa na mzaha unaofanyika kwa wananchi kwa kuitisha kipimo cha mkojo, baada ya baadhi ya watu wanaotuhumiwa kufanya uhalifu akiwemo Tundu Lissu, muigizaji Wema Sepetu, Mfanya biashara Yusuph Manji kutakiwa kupimwa mkojo.

Madiwani wa Chadema Waonywa

0
0
Madiwani wa Chadema Waonywa
Diwani wa kata ya Sombetini Arusha Ally Bananga (CHADEMA) amewataka madiwani waliopo ndani ya chama chao wanaotaka kuhama ndani ya chama waondoke mapema kwani wakija kuwagundua kipindi cha uchaguzi kwamba ni wasaliti watawatawanya viungo.

Bananga amelazimika kutoa kauli hiyo baada ya wimbi la madiwani Arusha kuhama chama hicho kwa tuhuma za kupokea rushwa, ambapo ameweka wazi kwamba anaamini kwamba hakuna tatizo la madiwani kuhama vyama kwani ni uhuru kama ilivyo kwa mashabiki wa simba kwenda Yanga kwa ajili ya maslahi yao lakini wasiondoke kwa kununuliwa kwani haitakuwa busara na mwisho wa siku itakuwa ni matatizo.
"Sina tatizo kwa madiwani kuhama hata kidogo. Lakini kama ni kuhama kwa kununuliwa kama hivi tunavyoona hili ni tatizo. Kama huna imani yetu ondoka mapema kwa amani. Tupishe kwa sababu tunaelekea kwenye uchaguzi na tunaamini tutashinda kata zote,  sasa isije ikatokea mbeleleni tukakugundua kwamba wewe ni msaliti maana tutatawanyana viungo kitu ambacho siyo kizuri. Ondokeni kwa amani yote sasa hivi mapema" - Bananga.
Aidha Bananga amesema kwamba amesikia maneno yaliyozungumzwa na aliyekuwa Diwani wa Kimandolu, Mchungaji Rayson Ngowi na kueleza kwamba hawezi kumsemea neno baya kwani ni rafiki yake lakini pia amemtaka  asifanye madhabahu ya Mungu kama kaunta ya 'bar' kwani ni mtu anayemfahamu na wanajuana ni mangapi wamefanya pamoja hivyo asijisahaulishe.

"Namheshimu sana Ngowi. Lakini amekubali kufika bei mimi nilishajua siku nyingi na nilimwambia. Hata watu waliokuwa wakiongea naye waliniambia. Ametafuta laana ya Mungu, yeye anajiita Mchungaji jambo ambalo nina wasiwasi nalo. Lakini kwa maneno aliyoyasema kwenye mkutano Soko kuu lakini ndiyo ameshanunuliwa, Mungu siyo mjomba yake na Madhabahu asiigeuze kama kaunta. Bananga ameongeza
Ameongeza kwamba "Adhabu ya Mungu inamfuata kabla ya adhabu yetu sisi Chadema tutakayompatia wakati atakapogombea. Kama yeye ni mwanaume asogeze pua yake kwenye uchaguzi huu mdogo aone tutakavyomfanya".
Pamoja na hayo Bananga amesema anaamini ushindi katika uchaguzi mdogo lazima watashinda kwani wamekuwa bora chini ya uongozi wa Mbunge Godbless Lema na Meya Calist Lazaro na kutokana na ushahidi wa Nassari kuonyesha wabunge walikuwa wakinunuliwa kama maandazi safari wamejiandaa kupeleka keki kwenye chaguzi.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images