Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Taharuku Yatanda Baada ya Mwanamke Mwizi wa Nyanya Kushindwa Kutua Tenga Yawalazimu Polisi Kutumia Mabomu Kuwatawana

$
0
0
Taharuku Yatanda Baada ya Mwanamke Mwizi wa Nyanya Kushindwa Kutua Tenga Yawalazimu Polisi Kutumia Mabomu Kuwatawana
Uvumi kuhusu mwanamke mwizi wa nyanya kushindwa kutua tenga umesababisha polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi mjini Mbalizi.

Hali ya taharuki imewakumba wananchi wa mji mdogo wa Mbalizi leo Jumatano baada ya mtu au watu wasiojulikana kuvumishwa kuwa mwanamke huyo baada ya kushindwa kutua tenga alikimbilia kituo cha Polisi Mbalizi kuomba msaada.

Uvumi huo ulieleza kuwa, mwanamke huyo aliimba nyanya sokoni Mbalizi.

Katika tukio hilo jana mchana Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi waliovamia kituo hicho ili kumuona mtuhumiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga amesema uvumi huo ulienezwa na watu au mtu asiyejulikana kwamba kuna mwanamke aliiba tenga la nyanya sokoni Mbalizi lakini alipojaribu kulishusha kutoka kichwani ilishindikana, hivyo akaamua kwenda kituo cha polisi kuomba msaada.

“Wakati wa taharuki kama ile kila mtu anakuwa na tabia na nia yake, ndiyo maana imelazimika kutumia nguvu kidogo kuwanyamazisha watu kwa mabomu. Ule ni uvumi tu ambao hata hatujamfahamu aliyeeneza alikuwa na mlengo gani kwa kuwa hakuna tukio kama hilo,” amesema.

Kamanda Mpinga amesema sasa hali ni shwari na wananchi wameelimishwa wakaondoka kwenda sehemu zao za biashara na shughuli nyingine.

Mwenyekiti wa Soko la Mbalizi A ambako kituo cha polisi kipo, Geofrey Msigwa amesema hakuna kitu kama hicho bali naye aliona watu wengi wakielekea kituoni jambo lililosababisha polisi kuwatawanya kwa mabomu.

Amesema, “Hii ni hatari kwa mtu kusikia jambo bila kulifanyia utafiti na kuanza kulizusha bila kutambua athari inayoweza kutokea.”

Amelaani kitendo hicho akisema kinahatarisha usalama na amani.

Pia, amewaonya watu kutokimbilia vitu ambavyo ni vya kusikia bila kuvifanyia uchunguzi kwa kuwa inaweza kuwagharimu.

Msigwa amesema hawana taarifa za wizi huo na wanashangazwa na uvumi huo.

UEFA Yaanzisha Ligi Mpya yaTimu za Taifa

$
0
0
UEFA Yaanzisha Ligi Mpya yaTimu za Taifa
Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA limeanzisha ligi mpya ya timu za taifa ambayo itaitwa ‘UEFA Nations League’.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tu baada ya kumalizika kwa michezo ya kuwania kufuzu kombe la dunia mwaka 2018. Ligi hiyo itaanza Septemba 2018 wakati ratiba itapangwa Januari 24 jijini Lausanne, Uswis.
Ligi hiyo mpya itakuwa na muundo wa ligi nne ambapo timu zitapangwa kutokana na uwezo wake. Ligi A itakuwa na timu 12 zinazoongoza kwa viwango vya FIFA ikifuatiwa na Ligi B ambayo nayo itakuwa na timu zinazofuata kwenye viwango baada timu 12 za mwazo huku Ligi C ikiwa hivyohivyo sambamba na Ligi D.
Katika Ligi A na Ligi B timu zitapangwa kwenye makundi matatu yenye timu nne kila kundi wakati Ligi C na B zitakuwa na makundi manne yenye timu nne kila kundi. Kwenye ligi hii timu zitakuwa zinashuka na kupanda kutoka ligi moja kwenda nyingine ikitegemeana na matokeo.

Ligi A: Germany, Portugal, Belgium, Spain, France, England, Switzerland, Italy, Poland, Iceland, Croatia, Netherlands.
Ligi B: Austria, Wales, Russia, Slovakia, Sweden, Ukraine, Republic of Ireland, Bosnia and Herzegovina, Northern Ireland, Denmark, Czech Republic, Turkey.
Ligi C: Hungary, Romania, Scotland, Slovenia, Greece, Serbia, Albania, Norway, Montenegro, Israel, Bulgaria, Finland, Cyprus, Estonia, Lithuania.
Ligi D: Azerbaijan, FYR Macedonia, Belarus, Georgia, Armenia, Latvia, Faroe Islands, Luxembourg, Kazakhstan, Moldova, Liechtenstein, Malta, Andorra, Kosovo, San Marino, Gibraltar.

VIDEO: Sheikh Ponda Aeleza Alichoteta na Tundu Lissu

$
0
0
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda amesema ameguswa na hisia za Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu.

Ponda amesema hayo leo Jumatano akizungumzia safari yake ya Nairobi nchini Kenya alikokwenda kumjulia hali Lissu hivi karibuni.

“Tulipokuwa tunabadilisha mawazo, niliguswa na hisia kubwa, badala ya mimi kumpa matumaini yeye ndiye alinipa matumaini,” amesema Ponda.

TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI

Nilikuwa na Wasiwasi Mkubwa Kufanya Kazi Peke Yangu Bila Mkubwa Fella- Aslay

$
0
0
Msanii Aslay Isihaka ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Natamba' amefunguka na kuweka wazi kuwa alikuwa na wasiwasi mkubwa kufanya kazi peke yake bila ya Meneja wake Mkubwa Fella na bila ya kuwa na uongozi wowote baada ya Yamoto Band.

Aslay amesama hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet Bongo ya EATV na kudai kutokana na woga na wasiwasi huo ndipo hapo alipoamua kumtafuta meneja wake wa sasa Chambuso na kuanza kufanya kazi pamoja.

"Nilikuwa na wasiwasi mkubwa sana kwamba tunaweza kusonga bila Mkubwa nyuma au menenjimenti yoyote baada ya hapo nikamtafuta Chambuso na yeye akaniambia kuwa tunaweza kusonga mbele, hivyo tupige kazi na kweli tukaanza kazi nakumbuka kazi yangu ya kwanza ilikuwa inaitwa 'Angekuona' hiyo niliachia kwenye TV na Radio mbalimbali, huo ndiyo wimbo ambao mimi unanigusa kutoka moyoni kwa sababu ni maisha yangu halisi kabisa" alisisitiza Aslay 

Mbali na hilo Aslay amesema kwa sasa bado hajapata mafanikio makubwa ila anaamini kuwa atapata mafanikio makubwa mbeleni na baadaye kuja kuwa kama wasanii wengine wakubwa ambao wananufaika vizuri kupitia muziki wao.

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.


Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778.

Vanessa Ashindwa Kuvumilia Kisa Jux...Amtolea Povu Kali Shabiki Alikoment Kwa Jux

$
0
0
Msanii Vanessa Mdee ameshindwa kuvumilia maneno ya shabiki mmoja kwenye account ya Instagram ya Jux na kuamua kumtolea povu juu ya maneno yake ya shombo kwa mpenzi wake wa zamani huyo.

Jux aliweka video akifanya show ya pamoja na Vanessa Mdee na moja ya shabiki wa Jux wa kike alianza kumponda Jux kuwa anajipendekeza kwa Vanessa na kwenda mbali zaidi na kusema Vanessa hana haja na yeye na hana kitu cha kumpa.

Kufuatia ujumbe huo Vanessa Mdee alishindwa kuvumilia na kuja kumjibu binti huyo kwa kumweleza kuwa yeye si msemaji wake na kudai amekuwa akitukana kila siku kwenye page hiyo ya Jux na kusema huenda akawa anamtaka Jux.



Juma Jux na Vanessa Mdee walikuwa ni wapenzi lakini baadaye ikasemakana kila mmoja kuanza maisha yake mapya, ingawa wapo watu wanadai kuwa wawili hao ni wapenzi ila wameamua kuweka maisha yao ya mapenzi chini ya kapeti ili kutoa nafasi zaidi ya kazi zao za sanaa kupata nafasi zaidi kuliko kuzungumziwa zaidi kwenye mapenzi na mahusiano. 

Mambo 6 ya Msingi ya Kufahamu Kabla ya Kupekuliwa na Polisi

$
0
0

NA  BASHIR   YAKUB –

Unapopekuliwa  yapo  mambo  ambayo  usipoyazingatia  wewe  unayepekuliwa  basi  yatakuingiza  matatani  mbeleni  au   hata  kama  umebambikiziwa  kosa  itaonekana ni  kweli    na  waweza  kwenda  jela  bila  kuwa  umetenda  kosa lolote.

Kawaida  wanaopekua  ni  askari.  Usitarajie  huyu  anayekuja  kukupekua  awe  ndiye  wa  kukwambia  haki  zako . Badala  yake wewe  unayepekuliwa  ndiye  uwe  wa  kumwambia  askari  kuwa  hiki  ndicho  hiki  hapana.  Askari  anapokuja  kukupekua  tayari  wewe  unashukiwa na  hivyo ni  rahisi   kwake  kuacha kufuata  au  kuongeza jambo lisilokubalika  ilimradi  atimize  lengo  lililomleta. Wewe  ndiye  wa  kusema  hili  ndio  na  hili  hapana.

Hivyo  basi  ni muhimu  sana kwako  kujua  kuhusu  kupekua  na  mambo  gani  ya  msingi  ufanyiwe  au  usifanyiwe  ili  kuepuka uwezekano  wa kwenda  jela  bila  kosa.

Usiseme  mimi  sina haja  ya  kujua  kuhusu  kupekua  kwasababu  ni  mwema  sana  na  hivyo si  rahisi  kutakiwa  kupekuliwa. Laa  hasha, kupekuliwa  na  kukamatwa  na  polisi  humkumba  yeyote  awe mwema  ama  vinginevyo. Kujua  ni  silaha  na  hivyo  ni  muhimu  kukaa  na silaha  hii.

Makala  yatapitia  sura  ya  20, vifungu  vya 38 hadi 45 vya  Sheria  ya Mwenendo  wa  Kesi  za  Jinai .

 ANARUHUSIWA  KUKUPEKUA.
Askari  ndiye  anayeruhusiwa kukupekua. Hata  raia  wanaweza  kumzuia  raia  mwenzao  wakampekua  ikiwa  wana  taarifa  kuhusu kuficha  au  kumiliki kitu  ambacho  ni  kosa  kwa  mujibu  wa  sheria.  Isipokuwa  ni  haramu  kabisa  kwa  raia  kumpekua  raia  mwenzake  bila   kuwa  na  kibali  maalum.

VITU  GANI  VINAWEZA  KUPEKULIWA.
Mtu  kama  mtu  anaweza  kupekuliwa,  kwa  maana  nguoni  mwake  kama  mifukoni  nk. Pia  vifaa  kama  gari,  ,meli, nk  navyo  vyaweza  kupekuliwa.  Halikadhalika  nyumba  kama  nyumba nayo  yaweza  kupekuliwa  pamoja  navyo  vifaa  vingine.

JE  WAWEZA  KUPEKULIWA  MDA  WOWOTE.
Hapana,  si  kweli  kuwa  waweza  kupekuliwa  mda  wowote  anaotaka  askari.  Sheria  niliyotaja  hapo  juu  inasema  mda  wa  kupekua  ni  kuanzia   jua  linapochomoza  na  mwisho  ni  linapozama.  Yametumika  maneno  jua  kuchomoza  na  kuzama   badala  ya  kutaja  mda labda  saa  11  za  asubuhi  mpaka  saa  12  za  jioni  kwasababu  ya utofauti wa  jiografia  ya  sehemu  na  sehemu.

Muonekano  wa  saa  12  za  jioni  wa  kanda  ya  ziwa  ni  tofauti  na  ule  wa  pwani  nk.  Kwahiyo  kutaja  saa  kwa  lengo  la  kumaanisha  usiku  unapoingia  na  unapotoka ingekuwa  kama  inapotosha.

Hata  hivyo  inawezekana  tu  kupekuliwa nje  ya  muda  huo  kwa  kibali maalum  cha  mahakama.

MPEKUAJI  KUAMBATANA  NA  SHAHIDI  MWENYEJI.     
Askari  anayepekua  aje  na  shahidi mwenyeji.  Mjumbe au  kiongozi  kutoka  serikali  za  mitaa ni  mtu  muhimu  kuwa  mwenyeji. Jirani  pia   anaweza kuwapo.  Hii  ni  kuhakikisha  wanakuwa  mashahidi  kuwa  hakuna  kilichoingizwa  ndani  wakati  kuingia  kupekua  na  pia  kushuhudia  vinavyochukuliwa.

ORODHA  YA  VITU  VINAVYOCHUKULIWA.
Ni  lazima  kila  kinachochukuliwa  kuandikwa  kwenye  orodha  maalum .  Orodha  hiyo utaisaini  wewe  uliyepekuliwa,  askari  aliyekupekua, pamoja  na  mashahidi  ambao  ni  mjumbe au  serikali  za mitaa  au  jirani  mwema.

Hii  huepusha  badae  kuambiwa  kuwa  hata  kitu fulani  ambacho  kinajenga  kosa  kuwa kilikutwa  kwako. Lakini  pia  ni  muhimu  kwa  ajili  ya  kurejesha  mali  zako  baadae  zikiwa  zimetimia.

KIBALI  CHA  KUPEKUA.
Askari  mwenye  cheo  chini  ya  Sub Inspector  haruhusiwi  kupekua  nyumba  au  eneo  la  mtu  bila  kibali  maalum aidha  kutoka  mahakamani  au  kutoka  kwa  mkubwa  wake  mwenye  cheo  cha  Sub  Inspector  kwenda  juu.   Hii  ni  kwa  kesi  ya  kupekua  nyumba.

Kwa  kesi  ya  kupekua   mtu  binafsi  pale  anaposimamishwa  au  upekuzi  wa  gari  na  vifaa  vingine  askari  yeyote    anaweza  kupekua  bila  kibali.

Magufuli Huenda Akawa Rais wa Pili Kuenziwa Zaidi Baada ya Mwalimu

$
0
0
Ni wazi kuwa kila Rais mstaafu ameacha legacy yake, ambapo baadhi yao wanakumbukwa zaidi ya wengine. Hadi sasa naweza kusema hakuna Rais aliyeacha legacy nzuri inayoishi, na itakayoishi vizazi na vizazi kuzidi ile iliyoachwa na Mwalimu Nyerere. Licha ya kuwa utawala wa Mwalimu umekuwepo wakati wengi wetu tukiwa ama wadogo sana kuweza kupambanua mambo au tukiwa hatujazaliwa kabisa, lakini kwa nguvu ya historia nzuri aliyoiacha tumekuwa tukimzunguzia as if ndiye Rais tuliyefurahia sana utawala wake. Mwalimu amekuwa ni Benchmark ya utawala ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu.

Lakini pia historia inatuambia kuwa Mwalimu huenda akawa ndiye Rais pekee aliyepitia magumu kuzidi Marais wote so far katika utawala wake. Yumkini hadi sasa akawa ndiye Rais wa kwanza kuchukiwa enzi za utawala wake kuzidi Marais wengine hadi kufikia hatua ya kutaka kupinduliwa mara kadhaa. Hali hiyo haijasikika hadi sasa kama kuna Rais yeyote aliyei-face wakati wa utawala wake, labda iwe imetokea na kuzimwa kwa siri kubwa sana. Naweza kusema kuwa nia na dhamira njema ya Mwalimu juu ya hatma ya nchi yetu ndivyo vinavyompa sifa kubwa kwa sasa, licha ya kuwa wakati wa utawala wake watu wengi hawakumwelewa na wengine kumuita dikteta.

Nikiangalia kwa upande mwingine, kwa kipindi kifupi ambacho Rais Magufuli ametawala, amekuwa ni “Talk Of The Day”. Ni Rais aliyepenya mioyoni mwa watu wengi sana, wadogo kwa wakubwa kwa kipindi kifupi kuzidi Marais wengi waliopita. Leo unaweza kumuuliza hata mtoto mdogo sana jina la Rais akakutajia, na pengine na mambo kadhaa kumhusu Rais huyo tofauti na ilivyokuwa kwa mihula kadhaa hapo awali. Ni ukweli usiopingika kuwa amepenya mioyoni mwa watu kwa namna tofauti, wapo wanaompenda sana na wale wanaomchukia pia kitu ambacho si kigeni kwani kimewatokea Marais wote waliopita.

Naweza kusema kuwa kumekuwa na tofauti kubwa ya kutafsiri dhamira au nia ya Rais JPM na hatma ya nchi yetu katika utawala wake. Kwa mtazamo wangu naona nia yake ni njema sana, pengine akitaka kutupeleka kule ambako Mwalimu Nyerere alipenda tuwepo. Kuwa katika nchi ambayo watu wote tunaifurahia, tunaheshimiana, tunathaminiana, na kunufaika kwa rasilimali zetu. Kuwa katika nchi ambayo mirija ya unyonyaji inazibwa na haki inatamalaki. Kwa kifupi ni kuwa katika nchi ya neema. Wale wasiompenda huenda ndio walikuwa wanufaika kwa njia zisizo halali, hivyo kuzibwa kwa mianya ya unyonyaji, rushwa n.k kunawafanya waishi kama mashetani.

Kwa kuwa Rais Magufuli amekuwa akionesha dhamira au nia yake hiyo wazi wazi, ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za makusudi na kwa haraka ili kuhakikisha kuwa malengo yake yanatimia, kuna uwezekano mkubwa JPM akawa ni Rais wa pili kuenziwa zaidi baada ya Mwalimu endapo Marais watakaomfuata hawatafanya vizuri sana zaidi yake.

Benmpo

Pendeza na Natural Beauty, Ongeza Hips na Makalio, Kuwa Mweupe na Softi, Ongeza Maumbile ya Kiume na Nguvu

$
0
0
PENDEZA NA NATURAL BEAUTY.  ONGEZA HIPS NA MAKALIO, KUWA MWEUPE NA SOFTI, ONGEZA MAUMBILE YA KIUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO N.K
      NATURAL BEAUTY Tunakuletea bidhaa bora zenye matokeo ya uhakika na haraka zisizo na kemikali wala madhara. Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa kiafya.
    NB. Matokeo ni uhakika na garantii.

          BIDHAA ZETU:-
 
1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @150,000/=
2.Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge  @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:-
 (1)Mafuta  @150,000/=
(11)Vidonge @170,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a)SHARK POWER gely ya kupaka @150,000/=  200,000/=
(b)Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @150,000/=
(C) VIG RX- Ni dawa mpya ya kuongeza maumbile hadi nchi 7.5 inapatikana kwa @200,000/=
(C)Handsome up original ni kifaa kinachoongeza maumbile kwa %99 size uipendayo  @250,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150,000/=
7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula  @150,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=
(b)Mkanda wa kawaida @140,000/=
(c)Micro-computer belt wa umeme @200,000/=
9.Kupunguza  maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @150,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @150,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @130,000/=
12.Kurudisha usichana  (bikra) @150,000/=
        Wasiliana nasi :- (+255)
            0759029968 au.      
                0659618585
  TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............
     Follow us on instagram  @natural2162

               

Mkuu wa Wilaya Achoma Nyumba 900 Chunya

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Chunya, Bi. Rehema Madusa ameingoza Kamati ya Ulinzi na Usalama kuteketeza nyumba zaidi ya 900 za wananchi ambao wamevunja sheria kwa kuvamia na kuishi ndani ya hifadhi ya misitu ya asili iliyopo tarafa Kipembawe Chunya.

Kufuatia zoezi hilo la kuwaondoka watu hao waliovamia hifadhi hizo lililofanywa na Kamati ya Ulinzi kwa kushirikiana na wakala wa huduma za misitu nchini, TFS, zaidi ya kaya 1000 zimekosa mahali pa kuishi baada ya nyumba zao kuchomwa moto.

Meneja wa wakala wa huduma za misitu (TFS) Grace Wille, wilaya ya Chunya amesema kuwa katika tarafa ya Kipembawe kuna misitu zaidi ya saba inayohifadhiwa, lakini misitu hiyo imevamiwa na makundi ya watu ambao wanaendesha shughuli za kiuchumi na kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira na kwamba zoezi hilo la kuwaondoa ambalo limeanza leo litakuwa ni endelevu.
Mbali na hilo wananchi ambao wamechomewa moto nyumba zao wameonyesha kus

Pius Msekwa: Suala la kuongeza miaka 7 halikubaliki, Labda iwe Minne

$
0
0
Akizungumza na AZAM TV kwenye Taarifa ya Habari ya saa mbili usiku leo. Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania Pius Msekwa anasema itakuwa ngumu sana kwa Bunge au Chama cha Mapinduzi kuongeza muda wa Rais kukaa madarakani zaidi ya miaka 5 kwa awamu kama walivyokubaliana toka zamani.Kasema hata wao Enzi zao walishajadiliana kuhusu hili na waliiona tatizo litakuwa pale Nchi ikipata Rais mbaya kwani miaka zaidi ya 5 kwa awamu italeta shida sana katika Nchi. kwahiyo akashauri utaratibu wa miaka 5 angependa uendelee.

Hawa Ndio Wanaokula Mema ya Rais Magufuli

$
0
0
Amani itawale.

Tangu kuingia madarakani kwa Rais Magufuli watu wengi wamekuwa wakihoji ni nani hasa anayenufaika na huu utawala..
Malalamiko mengi yamekuwa yakitolewa na watetea mafisadi wa ufipa kwamba zama za Rais Magufuli kila mtu anaisoma namba wala hamna mwenye nafuu.

Lakini uchunguzi niliofanya umenipa majibu tofauti kabisa.
Watu wafuatao wanakula mema ya Rais Magufuli kwa sana tu na hawataki kabisa atoke madarakani.

1. Wamachinga
Kabla ya Rais Magufuli kuwa machinga ilikuwa ni balaa tupu ,kila siku walichezea vipigo na kuchukuliwa bidhaa na mgambo.
Leo ndani ya utawala wa Rais Magufuli wamachinga wanafanya biashara ndani ya jiji bila shida yoyote.
Kwa nini wasimpende Magufuli?

2. Wakulima
Chini ya utawala wa Rais Magufuli kodi zote za ajabu ajabu zimefutwa hivyo kuongeza tija kwa wakulima.
Mazao ya chai ,korosho, Pamba, mpunga, tumbaku yalikuwa na kodi zaidi ya kumi!!!
Sasa kwa nini wasimpende Rais Magufuli??

3. Wafugaji
Kabla ya Rais Magufuli kuwa mfugaji ilikuwa adhabu tosha.
Ukipeleka kuuza Ng'ombe mnadani unakutana na kodi ya kwato na pembe!!

Chini ya Magufuli hizo kodi zote zimefutwa. Sasa wafugaji wanafanya biashara zao kwa raha na kujiongezea kipato.

Pia watu wa vijijini walikuwa wananyanyaswa sana wakienda kwenye huduma za serikali ,lakini sasa hivi wanaheshimika na kuhudumiwa vizuri.

Sasa hutaki wampende Magufuli ili wakupende wewe mtetea mafisadi?

Watetea mafisadi wote wajue kupambana na mtu ambaye siyo Mnafiki inahitaji timing na akili nyingi .

Magufuli siyo mnafiki ,nyeupe anasema nyeupe na nyeusi anasema nyeusi.

Wanasiasa wengi wamezoea kusema nyeusi ni nyeupe na nyeupe ni nyeusi.
Nawambieni watapata shida enzi ya Magufuli.

Asante Jakaya Kikwete kwa kutuachia Rais Magufuli mafisadi wanafungasha virago wenyewe na kuiacha Tanzania yetu.

Sheaik Ponda Afunguka Mikakati ya Lissu Aliyoipanga Kureaajea Katika Siasa

$
0
0
Sheaik Ponda Afunguka M ikakati ya Lissu Aliyoipanga Kureaajea Katika Siasa
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda ameelezea jinsi mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu anavyopanga mikakati ya kurejea katika siasa baada ya kupona.

Ponda amesema hayo baada ya kumtembelea Lissu aliyelazwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikopelekwa baada ya kushambuliwa kwa takriban risasi 30 akiwa ndani ya gari, nje ya makazi yake mjini Dodoma katika tukio lililotokea mchana Septemba 7.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana jijini hapa ulioishia kwa baadhi ya waandishi wa habari kukamatwa na Jeshi la Polisi, Sheikh Ponda alisema safari yake ya Nairobi ilikuwa na malengo manne.

Aliyataja madhumuni hayo kuwa ni kumjulia hali Lissu, kumuombea dua na kumjengea matumaini ya afya yake, kumjengea matumaini endelevu ya harakati zake za umma na kujenga mazingira ya kutosha kuzungumzia tukio hili.

“Katika kipengele cha tatu, tulipokuwa tunapeana na kubadilishana hoja, nilipata hisia nzito kwake,” alisema Sheikh Ponda.

“Maana yeye aliye kitandani alinipa mimi matumaini makubwa. Alisema anaamini yuko karibu kurudi jukwaani na ataanzia pale atakapokuta kasi ya mabadiliko imefikia.

“Alinieleza kazi muhimu za kuwajenga watu anazofanya akiwa pale kitandani. Alinieleza anaamini damu yake na yangu na nyingine zitakazomwagika kwa namna hii, zitawafanya Watanzania kupata uhuru wa kweli wenye thamani.”

Sheikh Ponda alisema tukio hilo na mengine ambayo yamekuwa yakitokea nchini yawe funzo na kuifanya jamii kujenga umoja na ushirikiano katika kulirudisha Taifa katika njia sahihi.

“Izingatiwe kwamba ikiwa tatizo lipo na watu hawasemi kama lipo, basi litaendelea kuwepo na wasababishaji pia wataendelea kudumu,” alisema.

“Na wale wanaoamini hali iliyopo ni kwa Serikali kushindwa kutekeleza wajibu wake, tuunganishe nguvu kuhakikisha Serikali inatekeleza wajibu huo.

“Masheikh, maaskofu, mapadri, wana vyuo, viongozi wa upinzani na hata viongozi wazuri walioko CCM waiambie ukweli Serikali. Kimya chao ni hasara na kitawanyima hadhi ya anuwani yao.”

Sheikh Ponda alisema kwa kipindi cha hivi karibuni kumekuwapo na matukio ambayo kwa namna moja au nyingine yanalichafua Taifa katika uso wa kimataifa.

Aliyataja matukio hayo kuwa ni mauaji ya kutisha, maiti za watu kuokotwa kwa wingi na zinaendelea kuokotwa, raia na viongozi kadhaa wametekwa na kupotea, viongozi mashuhuri wa vyama vya siasa vya upinzani na wa taasisi za kidini wanashambuliwa kwa silaha nzito kwa lengo la kuuawa.

Alisema kwa kuwa roho za Watanzania hivi sasa ziko juu na baadhi wamepoteza matumaini ya usalama wao, ni jukumu la Serikali kuhakikisha usalama wa raia wake unakuwapo wakati wote.

Kukamatwa waandishi

Mara baada ya mkutano huo uliofanyikia Hoteli ya Iris iliyopo Mtaa wa Livingstone Kariakoo kumalizika, na waandishi kadhaa kuondoka, askari wa Jeshi la Polisi walifika kumfuata Sheikh Ponda.

Askari hao waliokuwa wamevalia kiraia na wengine sare, walikuwa kwenye gari mbili na kuzuia mtu yeyote kutoka huku wakitaka kujua alipo Sheikh Ponda na walipoelezwa kwamba ameshaondoka, walianza kumsaka.

“Tulipowaeleza kwamba kaondoka walianza kutuomba material ya kile alichozungumza Sheikh Ponda. Mimi nilikubali na tukaanza kushuka kwenda katika gari lao,” alisema Rashid Kombo, mwandishi wa Z4News. “Wakati tunashuka na kwenda kupanda katika gari lao, mpiga picha wa Nipashe, John Badi akawa anapiga picha. Walipomwona wakamchukua na tukaondoka naye.

“Tulipofika Central (kituo kikuu cha polisi) wakanishusha mimi kwenda kuwapa material na Badi wakaondoka naye kumpeleka kituo cha Msimbazi na mimi nilipomaliza kuwapa material wakaniachia.”

Alipotafutwa na Mwananchi, Badi alisema alihojiwa kuhusu tukio hilo na baadaye kuachiwa.

“Mimi baada ya kufika pale Iris Hotel na kukuta magari ya polisi nilijiuliza kuna nini. Ndipo nikatoa kamera na kuanza kupiga picha na ndipo waliponichukua mimi na mwenzangu Suleiman Mpochi hadi Msimbazi,” alisema Badi.

“Tulivutana nao wakiuliza kwa nini tunapiga picha askari wakiwa kazini. Sisi tukawaeleza tatizo lipo wapi. Mwisho wa siku walituachia.”

Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa hakupatikana kuzungumzia tukio hilo na Mwananchi ilipomtafuta Kaimu Kamanda wa Polisi Ilala, Joseph Matuki alisema hakuwa na taarifa hizo.

“Hizo taarifa kwanza ndiyo unanipa wewe, sikuwa najua kama Sheikh Ponda alikuwa na mkutano hapo Iris.” alisema.

Alipoulizwa inawezekana polisi wakaenda pale bila yeye kujua, Kamanda Matiku alisema “kama wametumwa na bosi mimi nitaajuaje”, lakini hakutaja ni bosi gani.

Jambazi Auwawa na Wananchi WAakati Akiwatoroka Askari

$
0
0
Jambazi Auwawa na Wananchi WAakati Akiwatoroka Askari
Jambazi mmoja ameuawa na wananchi wakati akiwatoroka askari baada ya kubainika kufanya jaribio la kutenda uhalifu katika mradi wa ujenzi wa kituo cha pamoja cha forodha OSBP Tunduma mkoani Songwe.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi kamishna msaidizi wa polisi mkoa wa Songwe amesema tarehe 10 usiku wa kuamkia jumatano hii majambazi hao walipanga kufanya tukio la uhalifu katika mradi wa ujenzi wa kituo cha forodha OSBP
Tunduma na kwamba baada ya kugundulika walikimbia na kutelekeza bunduki yenye risasi 30, na zana zingine walizokuwa nazo.
Kamanda Nyange amesema majambazi wawili walifanikiwa kutoroka wakati mmoja aliyetajwa kwa jina la Isha Martin Mwampulo (20) mkazi wa Lwasho kata ya Ndalambo wilayani Momba akinaswa na wananchi, ambapo hata hivyo baada ya kushambuliwa alijeruhiwa vibaya na kufariki dunia akiwa njiani kuwahishwa hospitali.
Wakazi wa mji wa Tunduma mbali ya kupongeza jitihada za jeshi la polisi, wamesema wako tayari kushiriki kikamilifu katika kufichua wahalifu lakini wakataja kasoro ya askari kuchelewa kufika pindi wanapoarifiwa kuhusu uhalifu jambo linalowakatisha tamaa wananchi katika kushiriki kupambana na uhalifu.
Aidha jeshi la polisi limedai kuwa jambazi huyo alikuwa amevaa sare za wakandarasi na kutumia mwanya huo kutaka kutekeleza azma yake.
Kamanda nyange ameendelea kutahadharisha kuwa Mkoa wa S ongwe sio mahali salama kwa wahalifu na kupongeza ushirikiano wa wananchi kwa jeshi la polisi hadi hivi sasa

Trump Aonya Kufutillia Mbali Leseni za Vyombo vya Habari

$
0
0
Trump Aonya Kufutillia Mbali Leseni za Vyombo vya Habari
Rais Donald Trump ameendeleza mgogoro wake na vituo vya runinga nchini humo akisema kuwa vimekuwa na upendeleo na kuonya kwamba atafutilia mbali leseni zao.
Alikasirishwa na ripoti ya ktuo cha habari cha NBC iliodai kwamba kwamba aliwaagiza maafisa wake wa usalama na majenerali kwamba alitaka kuongezwa kwa kiwango kikubwa silaha za kinyuklia nchini humo.
Rais huyo alisema kuwa habari hiyo ilitungwa.
Waziri wake wa ulinzi Jim Mattis aliitaja taarifa hiyo kama isiokuwa ya ukweli.
Wiki iliopita NBC iliripoti kwamba waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson alimuita bwana Trump 'mtu mjinga' matamshi ambayo Bwana Tillerson hajayapinga lakini ambayo rais Trump ameytaja kuwa habari bandia.
Wanahabari wanasema kuwa rais huyo atapata shida kufutilia mbali lesen za vyonbo vya habari.
Zinadhibitiwa na tume ya mawasiliano nchini humo.

Gigy Money Adaiwa Kubeba Mimba ya Mtangazji Moj

$
0
0

MUUZA ‘nyago’ na msanii wa filamu Bongo, Gifty Stanford ‘Gigy Money’ anadaiwa kubeba ujauzito wa mwandani wake Moulad Alpha ‘Moj’ ambaye ni mtangazaji wa kituo cha Choice FM, ambapo za chini ya kapeti zinaeleza anafanya siri ili kuepuka kile anachokiita “kupigwa juju”.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, msanii huyo kwa sasa ana kibendi kipatacho miezi miwili ila amekuwa akihofia kueka wazi suala hilo sababu ya kuogopa kufanyiwa mambo ya kishirikina, ila watu wake wa karibu wengi wameanza kumstukia kutokana na dalili za wazi alizonazo.
Alipovutiwa waya na paparazi wetu kuhusiana na ishu hiyo alionekana kuuma maneno na kusema kuwa; “Sina mimba ila siku hizi nakula sana labda ndio maana watu wanahisi nina kibendi, pia siku hizi nimepungua mwili kwa sababu sifanyi tena mazoezi.

Wakili wa CHADEMA Amvaa IGP Sirro Sakata la Kuzuia Mjadala wa Tundu Lissu

$
0
0
Wakili wa CHADEMA, John Malya amefunguka na kuzungumzia juu ya kauli ya IGP Sirro kuhusu kuzuia wanasiasa kuzungumzia sakata la Lissu na kusema IGP hana mamlaka hayo kuzuia wananchi kuzungumzia jambo lolote na kufanya hivyo ni kuvunja sheria.

John Malya amesema hayo jana alipokuwa akiongea na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Kinondoni na kusema kuwa Sirro anapaswa kukaa kimya sasa na kuendelea na uchunguzi wa sakata hilo ila hana mamlaka ya kuzuia wananchi wasitoe mawazo yao wala kuzungumzia jambo fulani.

"Kamanda Sirro alinukuliwa akiwa Mbeya anasema amepiga marufuku wanasiasa kujadili masuala yanayomuhusu Tundu Lissu na kujadili watu ambao labda wanasadikiwa au wanashukiwa kwamba wameshiriki jaribio la kumuuwa Lissu.Nimefikiri ni muhimu kumkumbusha IGP Sirro  kuwa yeye ni kamanda wa Polisi na si kamanda wa raia hana mamlaka ya kutoa amri wananchi wajadili nini na nini wasijadili mamlaka hayo hana na nitatoa ufafanuzi.

"Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa haki na fursa ya wananchi kutoa maoni, kuzungumza mawazo yao na kubadilishana habari, ndiyo ibara ambayo inawapa wananchi na nyinyi waandishi wa habari uhuru wa kufanya kazi zenu katika nchi hii pamoja na sheria zingine lakini ibara ya 18 ndiyo msingi haswa wa kwanini wananchi wana uhuru wa kupashana habari na kuwa na uhuru wa mawazo" alisema Malya

Malya alisema kuwa IGP naye anaongozwa na sheria na kanuni mbalimbali na kusema katika hizo sheria na kanuni ambazo zinamuongoza IGP katika kutenda kazi zake za kila siku hakuna sehemu ambapo anapewa mamlaka ya kuzuia wananchi kujadili jambo fulani na kusema anaweza kufanya hivyo kwa askari lakini si kwa wananchi.

"Kamanda Sirro anaongozwa na sheria kadhaa lakini kubwa anaongozwa na sheria ya jeshi la polisi na huduma saidizi, na msaafu anaotumia unaitwa 'Police General Order' (PGO).  Kwenye jeshi la polisi hii ni sheria maarufu sana wao wenyewe wanaijua ndiyo inasema IGP anamuamuru nani na nani hawezi kumuamuru sasa huko anaweza kuwaamuru askari wake wasijadili au wasifanye kitu fulani, lakini kusema yeye amuru raia mamlaka hayo hana kwenye sheria wala kanuni" alisisitiza Malya

Aidha Malya anasema kuwa wananchi wanasubiri kusikia kauli ya IGP Sirro kuhusu upelelezi wa jambo hilo, au kusikia watu ambao wamekamatwa na kupelekwa mahakamani lakini si kuwazuia watu wasijadili shambulio alilolipata Tundu Lissu na kudai kuendelea kufanya hivyo ndiko kunapelekea hata wananchi pamoja na wao kuwa na mashaka na jeshi la polisi katika kufanya uchunguzi wa jambo hilo.

"Wakati huu ambapo wanasiasa, wapiga kura wanajadili juu ya hali ya Tundu Lissu yeye Sirro anapaswa kunyamaza, hapa yeye ndiyo anapaswa kunyamaza na siyo wanasiasa, yeye anyamaze afanye kazi ya upelelezi kitu cha pili tunachotaka kusikia amepeleka watu mahakamani, hivyo kufanya hicho anachokifanya anazidi kutufanya kukosa imani zaidi na jeshi la polisi" alisisitiza Malya

Kupata Matamko ya Wanasiasa Kila Siku Download App ya Mchambuzi Kwenye Simu yako HAPA

CHADEMA 'wacharuka' kuhusu Mange Kimambi Wamtaka IGP Sirro Kupambana na Wahalifu na Sio Wakosoaji Serikali

$
0
0
Mbunge wa Tarime Vijijini , John Heche amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro kutangaza kiama kwa wahalifu wa wanaofanya mauaji  kwa kupiga watu risasi siyo na siyo kuwatangazia wakosoaji wa Serikali.

Heche amelazimika kusema hayo baada ya hivi karibuni IGP Sirro alipokuwa mkoani Iringa kusema kwamba anafahamu makosa ya mtandaoni yanayofanywa na Mange Kimambi na kuahidi kwamba watamshughulikia.
"IGP anapaswa kuwatangazia kiama wahalifu na watu wanaofanya vitendo vya kupiga watu risasi& kutupa wengine baharini sio wakosoaji wa serikali"

Aidha Kiongozi mwingine wa Chadema aliyeingilia kauli ya IGP Sirro kuhusu Mange Kimambi ni Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema ambaye yeye alsema,
"IGPSirro shughulika na usalama wa  raia, malizia uchunguzi BenSanane, TunduLissu na maiti zinazookotwa baharini. Achana na Mange Kimambi"
Hivi karibuni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Nyakoro Sirro alisema kuwa jeshi la polisi linatambua makosa ya kimtandao yanayofanywa na mwanadada Mtanzania Mange Kimambi aishiye nchini Marekani na kusema kuwa jeshi la polisi linashughulikia suala hilo


Kupata Matamko ya Wanasiasa Kila Siku Download App ya Mchambuzi Kwenye Simu yako HAPA

Unapenda Habari za Siasa? Download App ya Mchambuzi Hapa Kusoma Matamko ya Viongozi Kila Siku

$
0
0
Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Kwenye simu yako
Bonyeza HAPA

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.



Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images