Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Kitilia Afunguka Sababu ya Kukubali Kuteuliwa na Rais

0
0
Kitilia Afunguka Sababu ya Kukubali Kuteuliwa na Rais
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo, ameweka wazi sababu ya yeye kukubali kuteuliwa kushika wadhifa huo, licha ya misimamo ambayo alikuwa nayo awali, dhidi ya wasomi wanaoteuliwa kushika wadhifa mkubwa serikalini.

Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, Prof. Mkumbo amesema kilichofanyika kwake ni kupandishwa cheo kutoka nafasi aliyokuwa nayo awali, na asingeweza kukataa kwani ni heshima kubwa aliyopewa na Rais.
“Wakati nimeteuliwa na Rais, mimi nilikuwa mtumishi wa umma, nilipandishwa cheo kutoka chuuo kikuu mpaka ukatibu mkuu, nani huyo akipandishwa cheo atakataa!!? Mimi nilikuwa mtumishi wa umma, hiyo ni heshima kubwa niliyopewa”, amesema Kitila Mkumbo
Prof. Mkumbo ameendelea kwa kusema kwamba baada ya kuteuliwa huko hakuchelewa kuachia wadhifa ambao alikuwa nao kwenye chama cha ACT- Wazalendo, kwa kuwa aliona dhahiri asingeweza kuendeleza harakati alizokuwa anafanya kwenye chama.
“Katika nafasi ya Katibu mkuu, mimi sio tu mtumishi wa umma, mimi ni serikali nawajibika kwa serikali kuisimamia, kutekeleza mipango ya serikali, tofauti kabisa na uhadhiri, kwenye chama nilikuwa nafanya harakati, nikaona hili sasa haliwezekani, ikabidi niwaombe wenzangu kwamba hapa nilipofika majukumu haya siwezi kuchanganya na uanachama wangu, ikabidi niweke uanachama pembeni”, amesema Kitila Mkumbo.
Hivi karibuni Kitila Mkumbo amejiondoa unachama wa ACT- Wazalendo, akisema kwamba hatoweza kutumikia serikali akiwa mwananchama wa chama hicho, kwani kuna mgongano wa maslahi.

Nambamba ya Aslay Aishikiki You Tube Yafikia Watazamaji Milioni Moja

0
0
Nambamba ya Aslay Aishikiki You Tube Yafikia Watazamaji Milioni Moja
Licha ya kuwekewa kikwazo cha umri,  video ya wimbo Natamba imeendelea kufanya vizuri Youtube na kufikisha watazamaji milioni moja.

Video hiyo ya Aslay iliwekwa mtandaoni Oktoba 4 ambapo hadi leo Alhamisi inafikisha siku saba na inaendelea kushika namba moja kwa siku tatu mfululizo kuwa video inayotazamwa zaidi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram siku chache zilizopita Aslay alilalamikia kuwepo kwa watu waliotoa taarifa mbaya kuhusu video hiyo na kusababisha kuwekewa kikwazo cha umri.

Video hiyo inaangaliwa na watu wenye umri usiopungua miaka 18.

Katika kurasa mbalimbali za mtandao wa Instagram zimetapakaa video za watu wanaojirekodi wakiimba wimbo huo ambao umepata umaarufu siku chache baada ya kuachiwa.

Natamba ni miongoni mwa mfululizo wa zaidi ya nyimbo 10 nkali kutoka kwa Aslay alizoziachia ndani ya mwaka huu baada ya Yamoto Band kusambaratika.

Mutukufu Agha Khan Kusaidia Sekta ya Afya, Elimu Pamoja na Vyombo vya Habari

0
0
Mukufu Agha Khan Kusaidia Sekta ya Afya, Elimu Pamoja na Vyombo vya Habari
Rais John Magufuli na Kiongozi wa madhehebu ya Ismailia duniani, Mtukufu Aga Khan wamezungumzia mambo matatu yatakayosaidia maendeleo ya Tanzania.

Mambo hayo ambayo yaliwekwa wazi na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ni sekta ya afya, elimu na vyombo vya habari.

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu jana Mtukufu Aga Khan alimweleza Rais Magufuli kwamba taasisi yake imedhamiria kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kwa kupanua Hospitali ya Aga Khan iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mtukufu Aga Khan aliwasili nchini jana kwa ziara ya siku mbili akitokea Uganda ambako alihudhuria sherehe za Uhuru wa nchi hiyo kwa mwaliko wa Rais Yoweri Museveni. Baada ya kuwasili, alikwenda moja kwa moja Ikulu na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli.

Katika mazungumzo yao, Mtukufu Aga Khan alimweleza Rais Magufuli kwamba upanuzi wa Hospitali ya Aga Khan utahusisha kuongeza idadi ya vitanda vya wagonjwa kutoka 72 vya sasa hadi kufikia 172.

Pia, alimweleza kuwa itaimarisha matibabu ya moyo na kansa na kuongeza ufundishaji wa madaktari na wataalamu wengine wa afya.

Akizungumza baada ya mazungumzo yao, Rais Magufuli alimshukuru Mtukufu Aga Khan kwa jinsi taasisi zake zinavyotoa huduma za kijamii hapa nchini, lakini akatoa wito kwa taasisi hizo kupunguza gharama za huduma zake kwa wananchi ili waweze kumudu.

“Wanatoa huduma nzuri na mimi kwa niaba ya Watanzania na Serikali kwa ujumla nimeshukuru sana, nimemshukuru sana mzee Aga Khan na watu wake wote kwa kazi kubwa wanazozifanya kwa ajili ya Watanzania,” alisema Rais Magufuli.

Alisema “wame-create (wametengeneza) employment (ajira), wamefanya mambo makubwa. Kwa mfano, kwenye hospitali wanatoa training (mafunzo) ya bure, nafikiri kila mwaka huwa wanatoa watu karibu 100 kwa ajili ya kuwafanyia training.”

Rais Magufuli alisema Serikali ya Awamu ya Tano ipo tayari kuendeleza na kuimarisha ushirikiano na Aga Khan na alimuomba kiongozi huyo kuendelea kupanua wigo wa huduma za taasisi zake ikiwa ni pamoja na kuwekeza mjini Dodoma yaliko makao makuu ya Serikali.

Elimu

Kuhusu elimu, Rais Magufuli alisema Mtukufu Aga Khan na taasisi yake wataanzisha ujenzi wa chuo kikuu kikubwa huko Arusha na tayari wameshapata eneo. Rais Magufuli alisema Mtukufu Aga Khan alimweleza kwamba ujenzi huo utaanza ndani ya miezi sita.

Kama ilivyokuwa katika afya, pia Rais alisema kuna changamoto chache ambazo ni bei kubwa katika huduma za elimu zinazotolewa na taasisi za Aga Khan lakini akasema Mtukufu Aga Khan ameahidi kulishughulikia suala hilo na tayari ameshatoa maelekezo kwa watu wake.

Vyombo vya habari

Baada ya mazungumzo na Rais Magufuli, Mtukufu Aga Khan alisema haamini kwamba kipaumbele cha vyombo vya habari ni kujikita kwenye habari za siasa pekee, badala yake alisema anaamini vyombo hivyo vina wajibu mpana zaidi wa kujikita katika masuala ya maendeleo hususan katika nchini zinazoendelea.

Alisema taasisi ya Aga Khan ipo katika mchakato wa kujikita katika wajibu huo kwa kuwa na waandishi wa habari na wachambuzi mahiri waliobobea katika fani mbalimbali licha ya kwamba hilo linachukua muda mrefu kuwaandaa.

“Tunahitaji weledi kwenye hii tasnia. Tunahitaji watu wanaoweza kuzungumzia mambo ya afya; wanaoweza kuzungumzia uchumi; wanaoweza kuzungumzia masuala ya dini; wanaoweza kuzungumzia siasa wanaoweza kuchangia kwenye mambo ya Katiba. Tunahitaji yote haya,” alisema Mtukufu Aga Khan

Kuhusu AKDN

Mtukufu Aga Khan pia ni kiongozi wa mtandao wa maendeleo wa Aga Khan (AKDN) ambao unatoa huduma mbalimbali duniani.

Kwa hapa nchini, mtandao huo unatoa huduma za afya, bima, elimu, mikopo kwa wajasiliamali na kusaidia kilimo hasa kwa wakulima wa vijijini.

Ziara ya Aga Khan inalenga kuimarisha ushirikiano baina ya serikali na taasisi yake ambayo ina uwekezaji mkubwa hapa nchini ambazo ni pamoja na sekta ya afya, elimu, mawasiliano, taasisi za fedha na viwanda.

Siri za Kijeshi za Australia Zaibwa Kupitia Udukuzi

0
0
Siri za Kijeshi za Australia Zaibwa Kupitia Udukuzi
Habari za siri kuhusu mpango wa jeshi la serikali ya Australia zimeibwa katika udukuzi wa mtandaoni.
Takriban GB 30 za data zilizokuwa na mwanakandarasi wa serikali zilidukuliwa ,ikiwemo maelezo kuhusu ndege mpya za kijeshi na manuwari.
Data hiyo ilikuwa na siri kubwa lakini haikutajwa kiwango chake kulingana na serikali hiyo.
Maafisa wa kukabiliana na maswala ya usalama wa mitandaoni nchini Australia walimtaja mdukuzi huyo kwa jina 'Alf' baada ya jina la muigizaji wa kipindi cha runinga cha 'Home and Away'.
Udukuzi huo ulianza mnamo mwezi Julai mwaka uliopita lakini idara ya ishara nchini Australia haijkujulishwa hadi mwezi Novemba

Wananchi, Vongozi wa Loliondo WafurahiaKupigwa Chini kwa Maghembe

0
0
Wananchi, Vongozi wa Loliondo WafurahiaKupigwa Chini kwa Maghembe
Wananchi pamoja na viongozi wa maeneo mbalimbali katika tarafa ya Loliondo wamefurahia kupigwa chini aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe huku wakimsubiri kwa hamu waziri mpya Dk Hamis Kingwangala.

Wamemtaka Dk Kigwangala akutane na wakazi wa eneo hilo ili waweze kumweleza kiini cha mgogoro wa eneo la pori tengefu.

Wananchi hao wamesema kupigwa chini Profesa Maghembe kimewapa faraja na matumaini ya kubaki katika ardhi wanayoipigania.

Wakizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana Jumatano katika eneo la Ololosokwan baadhi ya wakazi wa tarafa hiyo walimshauri Dk Kingwangala kutosikiliza majungu bali anapaswa kufika eneo la mgogoro na kupata ukweli.

Diwani wa Kata ya Ololosokwani, Yannick Ndoinyo amesema kwamba Dk Kingwangala anapaswa kukutana na wakazi wa eneo hilo ili waweze kumweleza kiini cha mgogoro unaofukuta mpaka sasa huku akimshauri ajiepushe na wapiga majungu.

“Waziri Kingwangala tunaomba akutane na sisi aje tumweleze kiini cha mgogoro na akitusikiliza hapa nawahakikishia hakuna mgogoro,” alisema Ndoinyo.

Hata hivyo, alisisitiza kwamba wateule katika wizara ya maliasili na utalii wanapaswa kutambua ya kwamba ardhi wanayoipigania ni mali yao kisheria na kusema kwamba kinachofanyika kwa sasa ni uvamizi na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Diwani wa Kata ya Soitsambu, Boniphace Kanjwel alisema wanamshukuru Rais Magufuli kusikia kilio cha wakazi wa eneo hilo kupitia ujumbe wa mabango mbalimbali waliyomwonyesha wakati akiwa katika uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid.

Kanjwel amesema Dk Kingwangala anapaswa kutambua kwamba jamii ya wamasai ni wahifadhi wazuri wa mazingira tofauti na uvumi unaoenezwa kwa sasa kwamba wao ndio chanzo cha uharibifu wa mazingira katika eneo la Loliondo.

“Baada ya kubeba mabango tunamshukuru Rais Magufuli alisikia kilio chetu lakini tunaomba kumwambia waziri Kingwangala kwamba jamii ya wamasai ni wahifadhi wazuri wa mazingira,” amesema Kanjwel

Kwa upande wake diwani wa viti maalumu kupitia CCM wilayani Ngorongoro, Tina Timan alipinga baadhi ya propaganda zinazoenezwa kwamba wakazi wa eneo hilo ni raia kutoka nchini Kenya na kusisitiza kwamba wao ni Watanzania halali na kumwomba Dk Kingwangala kukutana nao.

Katibu wa CCM Kata ya Ololosokwan, Saibulu Letama amesema kwamba wao kama chama tawala wanampongeza Rais Magufuli kwa mabadiliko ya baraza la mawaziri aliyofanya na kudai kwamba wananchi wa eneo hilo wamekuwa wakitegemea shughuli za ufugaji kama njia mojawapo ya kuwaingizia kipato kiuchumi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Olorien, Nektayo Ledidi kwa upande wake amesema wao kama jamii ya wamasai wanaiomba Serikali kutambua ya kwamba wao ni Watanzania wanaostahili haki ya kupatiwa makazi na sio kunyanyaswa.

Katika operesheni ya kuwaondoa wakazi wanaoishi katika  eneo la pori tengefu iliyoendeshwa na Serikali  hivi karibuni  jumla ya maboma 463 yameteketezwa kwa moto, mifugo 300 imefariki kwa kukosa chakula baada ya kukamatwa, mifugo 618 imetaifishwa baada ya kukamatwa na mifugo 590 inashikiliwa kizuizini kwa muda wa miezi mwili mpaka sasa.

Tuapambana Nao kwa Umakini- Omog

0
0
Tuapambana Nao kwa Makini- Omog
KUELEKEA mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam Jumamosi, Kocha Mkuu wa Simba Mcameroon, Joseph Omog, amesema “tutapambana nao kwa umakini”.

Akizungumza na gazeti hili jana, Omog, alisema kazi yake sasa ni kurekebisha makosa machache aliyoyaona katika mechi zilizopita, lakini amewaambia wachezaji wake wajiandae kukutana na ushindani kwa sababu Mtibwa Sugar wameonyesha kiwango kizuri kwenye michezo yao yote iliyotangulia.

Omog ambaye klabu yake inadhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo ya SportPesa, alisema Mtibwa Sugar ni moja ya timu zinazofanya vizuri katika Ligi Kuu Tanzania Bara licha ya kikosi chake "kubomolewa" na klabu mbalimbali zinazoshiriki ligi hiyo kila msimu unapomalizika.

"Tunajiandaa kwenda katika mazoezi ya jioni (jana jioni), soka ni mchezo ambao kila siku unatakiwa kujifunza, ila kikubwa tunawafahamu Mtibwa Sugar, ni moja kati ya timu ngumu na bora Tanzania, tunaiheshimu na tutaingia kuwakabili huku tukifahamu tuko kwenye hadhi inayofanana," alisema Omog.

Kocha huyo alisema pia anataka kushinda mechi hiyo na ile dhidi ya Njombe Mji itakayopigwa Oktoba 21, mwaka huu kwenye Uwanja wa Uhuru ili kujiweka kwenye nafasi "huru" ya kujiandaa kuikabili Yanga wakiwa na ari na kasi iliyoimarika.

Naye Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Zuberi Katwila, ametamba kuwa tangu arithi mikoba ya Salum Mayanga, ambaye aliteuliwa kuwa kocha mpya wa timu ya Taifa (Taifa Stars) katikati ya msimu uliopita, hajawahi kupoteza mchezo wowote wa Ligi Kuu dhidi ya timu za Dar es Salaam.

Katwila alisema kuwa mechi hiyo itakuwa na ‘tensheni’ kwa sababu atakayeshinda atafanikiwa kuongoza katika msimamo wa ligi kwa kuwa timu zote zina pointi 11, lakini Simba ikiwa juu kutokana na kuwa na mabao mengi ya kufunga.

" Mechi yetu itakuwa na ushindani mkubwa wa kila mmoja kutaka kumshusha mwenzake katika mbio za kuongoza ligi, nashukuru tangu nipewe timu sijawahi kufungwa na Simba au Yanga, ninajivunia rekodi yangu na ninataka kuilinda," aliongeza mchezaji huyo wa zamani wa timu hiyo.

Simba na Mtibwa Sugar zitashuka dimbani kila moja ikiwa na kumbukumbu ya kushinda mechi tatu na kutoka sare mara mbili katika mechi zao tano walizocheza msimu huu.

CUF Yampongeza Sheik Ponda Kwa Kuwaunganisha Watanzania Kushikamana Kutetea Haki za Binadamu

0
0
Chama cha CUF ChampongezSheik Ponda Kwa Kuwaunganisha Watanzania  Kushikamana Kutetea Haki za Binadamu
Chama Cha Wananchi (CUF) kimetoa pongezi kwa Sheikh Ponda baada ya jana kuwataka Watanzania bila kujali itikadi zao na imani zao za dini kwa pamoja kushikamana kutetea na kulindwa kwa haki za binadamu, uhuru wa Kidemokrasia na utawala wa sheria.

Sheikh Ponda alisema hayo jana baada ya kumtembelea Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu jijini Nairobi anakopatiwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi mnamo Septemba 7, 2017 mjini Dodoma.

Kufuatia kauli hiyo wa Sheikh Ponda Chama Cha Wananchi CUF kimempa pongezi kiongozi huyo kwa uthubutu wake wa kusema ukweli na kukemea maovu mbalimbali ambayo yanaendelea nchini.
"Tunampongeza kwa kujitokeza katika kipindi hiki ambacho Watanzania na Viongozi wengi wa dini na kisiasa wamejazwa woga, wale waliokuwa mstari wa mbele kukemea maovu katika awamu zilizopita hivi sasa wamejitia upofu, ububu na uziwi. Tunampongeza kuelezea Umuhimu na Ulazima kwa Watanzania kuungana pamoja kutetea uwepo wa mfumo wa Haki, Demokrasia na Utawala wa Sheria kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" alisema Mbarala Maharagande
Aidha Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa CUF, Mbarala Mharagande amedai kuwa wao CUF wanatarajia viogozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, wasomi mbalimbali, waandishi wa Habari na wananchi kwa ujumla hawapaswi kukaa kimya bali wanapaswa kukemea mambo mabaya ambayo yanaendelea nchini, huku wakivitaka vyombo vya dola kutekeleza wajibu wao.

Miili ya Wanajeshi wa JWTZ Waliouawa DRC Yaagwa

0
0
Miili ya Wanajeshi wa JWTZ Waliouawa DRC  Yaagwa
Miili ya askari wawili wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliouawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) imeagwa tayari kwa kurejeshwa nchini.

Askari hao walikuwa kwenye operesheni ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa (UN). Habari zilizopatikana zilisema miili ya askari hao iliagwa jana.

JWTZ katika taarifa kwa umma juzi iliwataja askari hao kuwa ni Koplo Maselino Paschal Fubusi na Praiveti Venance Moses Chimboni. Taarifa ilisema askari wengine 12 walijeruhiwa katika shambulio lililofanywa na kundi la wapiganaji la ADF.

Taarifa ya Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya JWTZ ilisema askari hao walishambuliwa kwa kupigwa risasi na kundi la waasi Oktoba 9, wakiwa umbali wa kilomita 24 mashariki mwa mji wa Beni.

JWTZ ilisema UN inaandaa utaratibu wa kuirejesha miili ya askari hao na utakapokamilisha wataujulisha umma mapokezi, kuaga na mazishi yatakavyokuwa.

Wakati huohuo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amelaani mauaji hayo yaliyofanywa na wapiganaji wa ADF wenye asili ya Uganda.

Katika mashambulizi hayo, walinda amani wengine 18 ambao wako kwenye ujumbe wa UN unaojulikana kama Monusco walijeruhiwa. Katika taarifa ya Guterres kupitia msemaji wake, Stephane Dujarric ametuma rambirambi kwa Serikali ya Tanzania na familia za wafiwa. Pia, amewatakia heri majeruhi wapone haraka.

Katibu mkuu huyo ameitaka Serikali ya DRC kuanza mara moja hatua za uchunguzi kuhusu mauaji hayo. Kuhusu vikundi vya wanamgambo, Guterres amevitaka kusitisha mapigano na kutafuta suluhu kwa njia ya amani.

Amesema mashambulizi yoyote dhidi ya walinda amani yanaweza kuwa ni uhalifu wa kivita kama inavyoainishwa katika sheria za kimataifa.

Hii ni mara ya pili kwa Tanzania kupoteza askari waliopo kwenye operesheni ya amani nchini DRC.

Katika tukio la awali, askari mmoja aliuawa mwezi uliopita baada ya kushambuliwa na waasi.


Israel Yadai Kuwaona Wadukuzi wa Urusi Wakiidukua Marekani

0
0
Israel Yadai Kuwaona Wadukuzi wa Urusi Wakiidukua Marekani
Majasusi wa Israel waliwaona wadukuzi wa Urusi wakidukuwa programu ya kuzuia virusi mitandaoni Kaspersky kulingana na vyombo vya habari vya Marekani.
Warusi hao walidaiwa kujaribu kuchukua data kuhusu mipango ya ujasusi ya Marekani kulingana na gazeti la New York Times na Washington Post.
Majasusi wa Israel walibaini hayo baada ya kuidukua programu hiyo.
Mfumo huo wa usalama kwa jina Kaspersky umesema kuwa haikushirikishwa wala haukugundua kuhusu hali hiyo na imekana kushirikiana na serikali yoyote.
Mwezi uliopita, serikali ya Marekani iliamua kusitisha udukuzi huo kupitia programu hiyo ya Urusi katika kompyuta zake.
Waisraeli hao wanadai kuijulisha Marekani , hatua iliosababisha kupigwa marufuku kwa programu ya Kaspersky.
Gazeti la The New York Times lilisema kuwa hali hiyo ilielezewa na watu kadhaa ambao walielezwa kuhusu swala hilo.
Nakala kadhaa zimedaiwa kuibwa kutoka kwa afisa mmoja wa ujasusi wa Marekani ambaye alikuwa ameweka programu ya kaspersky ili kulinda virusi katika kompyuta yake.
Hakuna matamshi yoyote yaliotolewa na Shirika hilo la ujasusi la Marekani NSA, ikulu ya Marekani na ubalozi wa Israel.

Shuhudia Maajabu ya Chief Sultan Mzee...Mtaalamu wa Nyota za binadamu

0
0
ONA MAAJABU YA CHIEF SULTAN MZEE

 Mtaalamu wa Nyota za binadamu Africa Mashariki na dunia nzima,
Amewasaidia watu wengi kujua nyota zao na jinsi ya kuzing'arisha,
Anarudisha Mpenzi,Mume,Mke mliyeachana NDANI ya masaa manne(4) tu,
Anaweza kuongeza ROMANCE na MAHABA kwa Mwenzi wako
Anatoa pete ya BAHATI pamoja na kukupa uwezi wa Kupata faida kubwa katika biashara yako,
Kwa wale mnaosumbuliwa na Chuma ulete tatizo hilo analiondoa kabisa,
Anakuwezesha kushinda kesi iliyodumu siku nyingi nk.

KWA USTAA,UMARUFU UTAPATA UTAJIRI WA MAISHA NA BILA MASHARTI YOYOTE, UTAPEWA NGUVU ZA KUJILINDA NA UTAJIRI, MALI NA AFYA YAKO,Karibu kwa CHIEF SULTAN MZEE akupatie Pete za Bahati na utajiri.Wachungaji wengi duniani, Wanasiasa na Wasanii Maaarufu duniani Tayari wamejiunga pia wamefaidika na wamebadirisha  Maisha yao toka umasikini mpaka utajiri,kujua mengi zaidi na kutatuliwa Matatizo yako yoote kwa usiri na Uaminifu piga simu namba 0762-846979 au 0672-202509

Aliyedaiwa Kununua Madiwani Chadema Akimbilia kwa Mganga wa Kienyeji

0
0
Mtuhumiw Aliyehiriki Kununua Madiwani Chadema Akimbilia kwa Mganga wa Kienyeji
Mtuhumiwa mmoja aliyeshiriki kununua madiwani wa CHADEMA Meru amejisalimisha kwa mganga wa kienyeji ili kulinda kibarua chake kisiweze kuota nyasi kufuatia uchunguzi mbalimbali ambao unaendelea.

Mbunge wa Jimbo la Arumeri Mashariki, Joshua Nassari amethibitisha hilo na kusema kuwa mtuhumiwa huyo anaishi maeneo ya Mukidoma Usa- River na kudai kuwa tayari anao ukweli wote kuhusu hilo na kuahidi kuutoa muda si mrefu.

"Mmoja wa watuhumiwa wa rushwa ya ununuzi wa madiwani Meru aishie maeneo ya Mukidoma Usa-River ameleta mganga toka kanda ya ziwa, na yupo nyumbani kwake . Lengo ni kumsaidia mtuhumiwa huyu asipoteze ajira yake. Mganga huyu ameletwa na mama wa mtuhumiwa. Tutaanika hadharani acha tuone tofauti ya Mungu na miungu" aliandika Joshua Nassari
Mbunge wa Jimbo la Arumeri Mashariki, Joshua Nassari siku kadhaa zilizopita aliachia ukweli juu ya wateule wa Rais John Pombe Magufuli jinsi ambavyo walikuwa wakipanga mipango ya kununa madiwani wa CHADEMA na baadaye alichukua ushahidi huo na kuupeleka TAKUKURU.

Mbasha Afuraishwa na Kutongozwa na Wanawake

0
0
Mbasha Afuraishwa na Kutongozwa na Wanawake
Msanii wa muziki wa Injili, Emanuel Mbasha ambaye wengi humsifia kwa utanashati wake, amesema anamshukuru Mungu kwa kuonyeshwa kupendwa, baada ya mabinti wengi kumtamani kimapenzi.

Akiongea na eNewz ya East Africa Television, Emmanuel Mbasha amesema ingawa wanawake wengi wanafunguka hisia za mapenzi juu yake, lakini anamuomba Mungu ampe mtu sahihi zaidi ili yasije yakajirudia yaliyomkuta awali.
"Wadada wengi wananipenda wa kila aina na hiyo iko wazi, ukiangalia DM yangu kila siku inajaa meseji, kuna kila aina, na ninamshukuru Mungu kwa kipaji hicho, maana yake kupendwa nako ni kibali na ni baraka za Mungu, sasa nikikurupuka tu kuchukua nitaingia majanga, natamani nipate mtu sahihi, nifanye naye maisha tupate watoto tuendelee mbele, maana yake sitawaza kukaa hivi milele ila kwa sasa sina sababu ya kukurupuka", amesema Emmanuel Mbasha.
Mbasaha ambaye amesema amechoshwa na  upweke, ameendelea kusema kwamba..."mimi nimetokea kwenye changamoto kubwa sana ya mahusiano, angekuwa mwengine angedata angeanza kunywa pombe, kuvuta bangi na kufanya mabaya, lakini nilisimama na Mungu, hivyo nimetulia nikisubiria Mungu aniletee mtu sahihi".
Emmanuel Mbasha ameachana na aliyekuwa mke wake ambaye pia ni mwanamuziki wa nyimbo za Injili, Flora Mbasha, huku akimshtaki kwa kosa la kumbaka mdogo yake, kesi ambayo Emmanuel aliachwa huru kutokana na kukutwa hana hatia.

Sheik Ponda Apewa Siku Tatu Kujislimisha Polisi

0
0
Sheik Ponda Apewa Siku Tatu Kujislimisha Polisi
Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam limempa siku 3 tu Sheikh Issa Ponda, ili kujisalimisha na kuhojiwa kuhusu tuhuma zinazomkabili, na iwapo hatafanya hivyo watamchukulia sheria stahiki.

Tarifa hiyo imetolewa leo na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Lazaro Mambosasa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari, na kusema kwamba ndani ya siku hizo 3 lazima awe amekwenda kujisalimisha, la sivyo hatakuwa salama.
“Ametenda makosa ya jinai kama uchochezi, lakini pia amekuwa anatoa lugha ambazo ni za kejeli, dhidi ya serikali, anatufutwa na kama unamjua mwambie ajisalimishe ili tuweze kumhoji, kukimbia hakutomsaidia, tukiona kuna kosa la jinai tutampeleka mahakamani kama hana tutamwachia, mimi nampa siku tatu lakini akija leo ni nzuri zaidi, nampa siku 3 ajitokeze mwenyewe aweze kuhojiwa, vinginevyo hatakuwa salama”, amesema Kamanda Mambosasa.
Hapo jana Jeshi la polisi lilivamia mkutano wa Sheikh Ponda aliokuwa nafanya na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, na kufanikiwa kukamata baadhi ya watu wakiwemo waandishi wa habari ambao walikuwepo kwenye mkutano huo.

Maandamano ya Nasa Nchini Kenya Yapigwa Marufuku Kenya

0
0
Maandamano ya Nasa Nchini Kenya Yapigwa Marufuku Kenya
Serikali ya Kenya imepiga marufuku maandamano yaliyopangwa kufanyika katika miji mitatu mikubwa ikiwamo jiji la Nairobi ikitaja kasoro zilizoonekana wakati wapinzani walipofanya maandamano hivi karibuni dhidi ya tume ya uchaguzi.

Waziri wa Usalama wa Ndani, Fred Matiangi amesema kutokana na wasiwasi wa uwezekano wa kujitokeza kwa vitendo vya uvunjifu wa amani Serikali imeamua kuyapiga marufuku maandamano ya aina yoyote yaliyopangwa kufanyika katika miji ya Nairobi, Mombasa na Kisumu.

“Kutokana na ukweli kuwa uko uwezekano wa kujitokeza kwa uvunjifu wa amani, tunatangaza kuwa Serikali haitaruhusu kufanyika maandamano yoyote katika miji ya kibiashara ya Nairobi, Mombasa na Kisumu,” amesema waziri huyo.

Amesema taarifa ya zuio la kutofanyika kwa maandamano hayo pia limetumwa kwa mkuu wa jeshi la polisi.

Kumekuwa na taarifa kuwa muungano wa Nasa umepanga kufanya maandamano katika miji hiyo kwa lengo la kushinikiza tume ya uchaguzi kufanyiwa mabadiliko kabla ya uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Oktoba 26.

Waziri Matiangi amesema waandamanaji hao walionekana wakishambulia vituo vya polisi, maofisa wa polisi na kuwajeruhi  huku wakivuruga shughuli nyingine zilizokuwa zikiendelea wakati walipoandamana hivi karibuni.

Mgombea wa Nasa, Raila Odinga ametangaza kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho.


Massogange Azidi Kukwama Mhakamani Kesi Yake Yasogezwa Mbele

0
0
Massogange Azidi Kukwama Mhakamani Kesi Yake Yasogezwa Mbele
Agnes Gerald maarufu kama ‘Masogange’ amerudi tena kwenye headlines za Mahakamani tena leo October 12, 2017 ambapo hata hivyo, kesi yake ya kutumia dawa za kulevya imesogezwa mbele katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu hadi November 14, 2017.

Masogange alitarajia kuanza kujitetea leo lakini Wakili wa Serikali, Adolf Mkini alimuomba Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri aahirishe kesi hiyo hadi tarehe nyingine ambapo kutokana na ombi hilo, Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi November 14, 2017.

Masogange ataanza kujitetea baada ya Mahakama kumkuta na kesi ya kujibu kwa upande wa mashtaka ambao ulikuwa na mashahidi watatu.

Masogange anadaiwa kuwa kati ya February 7 na 14, 2017 katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jiji la Dar es Salaam alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Diacety Imophine).

Pia anadaiwa kuwa kati ya February 7 na 14, 2017 alitumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.

Majaliwa: Serikali Itaendelea Kuimarisha Ushrikiano wa kiuchumi na Uganda

0
0
Majaliwa: Serikali Itaendelea Kuimarisha Ushrikiano wa kiuchumi na Uganda
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano wake wa kiuchumi na kidiplomasia baina yake na Uganda.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo Oktoba 12, 2017 alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Bw. Richard Kaonero jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa Tanzania na Uganda zinauhusiano ya muda mrefu na kwamba serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli inafarijika na ushirikiano huo.

“Tunaimani kubwa na ushirikiano wetu na Serikali ya Uganda. Tutaendelea kuimarisha miradi mbalimbali ya maendeleo tunayoitekeleza kwa pamoja ukiwemo ujenzi wa bomba la gesi.”

Waziri Mkuu ametumia nafasi hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Uganda ili waje kuwekeza Tanzania kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya  kilimo. Pia amewakaribisha raia wa Uganda kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko nchini Tanzania kama mlima wa Kilimanjaro, fukwe, mali kale na mbuga za wanyama.

Kwa upande wake, Balozi Kaonero  ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi wake kupitia sekta ya viwanda. Lakini pia Balozi huyo ameiomba Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kuanzisha safari ya kwenda Entebe nchini Uganda ili kuimarisha usafiri kati ya nchi hizo mbili.

Chanjo Dhidi ya Ugonjwa wa Ebola Yafanikiwa

0
0
Chanjo Dhidi ya Ugonjwa wa Ebola Yafanikiwa
Uchunguzi uliofanyiwa chanjo mbili tofauti za ugonjwa wa Ebola umebaini kuwa chanjo hizo zinaweza kumkinga mtu kutokana na virusi vya ugonjwa huo kwa takriban mwaka mmoja.
Utafiti huo uliochapiswa katika jarida la New England Journal of Medicine, ulifanyiwa nchini Liberia na kuwashirikisha wagonjwa 1,500
Wale waliopewa chanjo hiyo walifanikiwa kupata kinga yenye nguvu kwa karibu mwaka mmoja.
Chanjo ya Ebola yafanikiwa
Maziko salama yanusuru maisha Afrika Magharibi
Majaribio hayo yanaonyesha kuwa chanjo hizo zote zinaweza kutumiwa kuokoa maisha wakati wa majanga ya ugonjwa wa Ebola siku za usoni.
Ugonjwa wa Ebola uliwaua zaidi ya watu 11,000 nchini Liberia, Sierra Leone na Guinea, wakati wa mlipuko wa ugonjwa huo mwaka 2014-2015.

Wahujumu Uchumi Wafikishwa Mahakamani Kisutu

0
0
Wahujumu Uchumi Wafikishwa Mahakamani Kisutu
Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi, inayomkabili Mkurugenzi wa Tathmini, Archard Alphonce Kalugendo (49) na Mthamini wa Madini ya Almas wa Serikali, Edward Joseph Rweyemamu (50) umeileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, sehemu kubwa ya upelelezi umekamilika bado maeneo machache.

Wakili wa Serikali, Wankyo Simon amemueleza Hakimu Hakimu Mwandamizi, Godfrey Mwambapa kuwa kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya kutajwa.

Ali Hapi Afanya Usafi wa Mazingira Katika Nyumba ya Baba wa Taifa Kuazimisha Kumbukummbu Yake

0
0
Ali Hapi Afanya Usafi wa Mazingira Katika Nyumba ya Baba wa Taifa Kuazimisha Kumbukummbu
Ikiwa zimesalia siku mbili kuadhimisha Siku ya Mwalimu Nyerere, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kinondoni imefanya usafi wa mazingira katika nyumba ya Baba wa Taifa iliyopo Mikocheni jijini hapa.

Kamati hiyo imeongozwa na mkuu wa wilaya hiyo, Ally Hapi ikihusisha askari 417 kutoka Jeshi la Wananchi(JWTZ), Magereza, Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) pamoja na Jeshi la Polisi.

Akizungumza mara baada ya kufanya usafi huo leo Alhamisi, Hapi amesema katika kumuenzi muasisi wa Taifa hili usafi wa mazingira ni moja ya njia ya kuunga mkono jitihada zake kwa vitendo.

"Hatuna kitu cha kumlipa kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa Taifa hili lakini kwa hiki tulichokifanya ni sehemu ya kumuenzi kwa vitendo," amesema

Amesema kazi hiyo itakuwa endelevu ikihusisha na maeneo mengine kwenye wilaya hiyo kwa lengo la kuhamasisha wananchi kulinda mazingira.

"Kazi hii ni endelevu na itafanyika kila mwezi tukianzia hapa nyumbani na maeneo mengine ikiwamo fukwe za bahari na yale yenye vichaka," amesema Hapi.

Mjukuu wa Mwalimu Nyerere, Sophia Nyerere ameishukuru kamati hiyo na kwamba wamefarijika kushirikiana katika kuboresha mazingira.

Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

0
0

THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images