Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Viongozi wa Makundi ya What's App Kitanzini

$
0
0
Jeshi la polisi kitengo cha makosa cha makosa ya mtandaoni limewatahadharisha viongozi wa makundi ya What's App na kuwataka kutoa taarifa pindi uhalifu unapofanyika kwenye makundi yao.

Kufanya hivyo kutasaidia polisi kuchukua hatua dhidi ya mhusika aliyefanya uhalifu huo ili kukabiliana na ongezeko la vitendo vya uhalifu mtandaoni.

Hayo yameelezwa leo Ijumaa na naibu mkuu wa kitendo hicho, Joshua Mwangasa wakati wa semina iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano(TCRA) na kuwakutanisha viongozi wa dini wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema makosa ya kimtandao yameendelea kuongezeka kwa kasi kubwa huku makundi ya What's App yakionekana kuwa kichocheo kikubwa.

Mwangasa amesema viongozi wa makundi hayo hawatakiwi kuvumilia makosa hayo hivyo wanatakiwa watoe taarifa polisi.

"Usikubali umeanzisha kundi kwa nia nyingine halafu mtu au watu wanaweka mambo yasiyofaa, toa taarifa hatua zichukuliwe kinyume na hapo hata wewe utahusika,"

Amesema kwa kiasi kikubwa makundi hayo yamekuwa yakitumika kusambaza taarifa za uongo na uchochezi.

Mwangasa ametumia fursa hiyo kuwaomba  viongozi wa dini kuwahubiria waumini wao juu ya matumizi sahihi ya mitandao ili kujiweka mbali na uhalifu.

"Ukosefu wa maadili ndio unachangia haya yote haya, ndiyo sababu narudi kwenu viongozi wa dini wasisitizeni waumini wenu watumie mitandao kwa maendeleo," amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TCRA, Mhandisi James Kilaba amesema mamlaka hiyo inaendelea kuchukua hatua kuimarisha ulinzi wa mawasiliano mtandaoni.

Amesema simu za mkononi kwa sasa zimekuwa kama silaha hivyo matumizi yake yanapaswa kuangaliwa kwa umakini zaidi.

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.


Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

Polepole adai Chadema ‘walikurupuka’ kumuunga mkono Rais Kenyatta

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilikurupuka kuchukua uamuzi wa kuunga mkono Chama cha Jubilee kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta.


Polepole amesema Chadema walikosea kushabikia uchaguzi wa Kenya kwa kuonesha upande fulani kati ya vyama vinavyoshindana kuomba dhamana kwa wananchi wake kuongoza nchi hiyo na kudai kitendo hicho sio cha kikomavu kwenye siasa.

“…Walikurupuka kuchukua upande kwa sababu katika diplomasia na mashirikiano ya nchi huwa ni dhambi kubwa kwa nchi moja au chama cha kuanza kuingilia uchaguzi wa nchi nyingine na kuchukua upande katika pande zile zinazoomba dhamana kwa wananchi katika nchi nyingine ambayo siyo ya kwenu.“amesema Polepole kwenye mahojiano yake na Times FM huku akielezea madhara ya kitendo hicho.

“Fikiria mfano unachukua upande kwenye uchaguzi wa Kenya halafu wewe ni chama kilichopo madarakani hapa Tanzania halafu upande kule wanashinda wengine sio wale uliowaunga mkono. Tafsiri yake nini nini? umeharibu mahusiano ya diplomasia utakuwa umejenga uadui..kwa sababu katika siasa watu wanatafuta dhamana kwa wananchi. Sasa hapa (Tanzania) kama kuna chama cha upinzani kilicho makini kinatakiwa kifahamu diplomasia na uhusiano ya kimataifa unatutaka sisi kuheshimu matakwa ya wananchi wa Kenya wao waamue watakayeona anafaa kuiongoza Wakenya, Kisha sisi tutalazimika kushirikiana na yeyote atakayepewa dhamana ya kuiongoza nchi hiyo.”amesema Polepole.

Hata hivyo, Humphrey Polepole amedai kuwa Chama chake cha Mapinduzi hakiwezi kuonesha kipo upande gani kwenye uchaguzi huo kwani kinajua fika kuwa dhamana ya kuongoza nchi hiyo ipo mikononi mwa Wakenya.


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilitangaza mapema mwaka huu kabla ya Uchaguzi nchini Kenya kuwa kinamuunga mkono Rais Kenyatta katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu nchini Kenya.

Wanaume Wenye Umri Mkubwa Hatarini Saratani ya Kinywa Kwa Kunyonya Sehemu za siri

$
0
0
Imebainika wanaume wengi hasa wenye umri mkubwa wapo katika hatari ya saratani ya kinywa zaidi kuliko wanawake kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo tabia ya wanaume kufanya mapenzi ya kunyonya sehemu za siri za wanawake.

Akibainisha, Dk. Alex Eliakim kutoka chuo cha madaktari wa meno amesema pamoja na tabia hiyo ya kujamiiana kupitia kinywa pia sababu nyingine ni utumiaji wa kileo na tumbaku. Alisema wanaume wananyonya sehemu za siri za mwanamke huchukua bakteria ambao wanaleta msuguano na bakteria wa kinywa na kusababisha magonjwa.

'Awamu ya Tano Imeanza Kurejesha Mtizamo wa Nyerere

$
0
0
NAIBU Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha, amesema Serikali ya awamu ya tano imeanza kurejea katika mtazamo wa Mwalimu Julius Nyerere juu ya uchumi wa viwanda aliouanzisha.

Akizindua Kongamano la Kumbukumbu ya Kifo cha Mwalimu Nyerere lililofanyika katika  Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere  jijini Dar es Salaam juzi, Ole Nasha alisema Mwalimu Nyerere alijenga viwanda vingi hapa nchini.

Alivitaja viwanda ambavyo Mwalimu Nyerere alivijenga kuwa ni viwanda vya nguo kama Urafiki, Mbeya Tex, Mwatex, Mutex, viwanda vya ngozi, viwanda vya zana za kilimo, viwanda vya kutengeneza vipuli pamoja na viwanda vinavyotegemea malighafi za mazao yanayolimwa hapa nchini.

Alisema Taifa linahitaji viongozi wazalendo na waadilifu kama alivyo Rais Dk. John Magufuli ambaye ameonesha nia ya dhati ya kufuata nyendo za Mwalimu Nyerere kwa kuhimiza maendeleo ya kiuchumi yanayotegemea viwanda.

“Serikali ya awamu ya tano kwa muda wa miaka miwili iliyokaa madarakani, imejitahidi kurejea na kuweka kwenye vitendo dhana ya Mwalimu Nyerere ya uchumi wa viwanda, kwani kwa sasa  inatekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa, mwaka  2016/2017-2020/2021 unayojikita katika ujenzi wa viwanda kama njia ya maendeleo ya kiuchumi na maisha ya watu,”alisema Ole Nasha.

Alisema mtazamo wa Mwalimu Nyerere ulikuwa ni kutumia viwanda vya ndani kama njia ya kujinasua kutoka kwenye unyonyaji wa muda mrefu.

Kama Taifa huru kuna haja ya kuondoa tofauti za kisiasa na kuishi katika misingi ya usawa, umoja, ushirikiano ili kujiletea maendeleo ya uchumi kwa mtu mmoja na taifa kwa ujumla, ikiwemo kuhimiza uzalendo kwa kila mtanzania ili kujenga Tanzania ya viwanda na uchumi wa kati ifikapo 2025.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Kumbumbuku ya Mwalimu Nyerere, Profesa Shadrack Mwakalila, alisema kuwa ili kufikia Tanzania ya viwanda taifa linahitaji viongozi wazalendo wenye uchu wa maendeleo na wasio na misingi ya ukabila wala udini.

“Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne ambavyo ni watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora, hivyo ustawi wa uchumi wa viwanda  unahitaji viongozi na watendaji ambao ni wazalendo, watiifu na wenye kutanguliza mbele masilahi ya taifa,”alisema Profesa Mwakalila.

Kongamano la maadhimisho ya siku ya  Mwalimu Nyarere hufanyika kila mwaka ili kujadili busara, fikra na hekima zake katika kujenga usawa, maendeleo, umoja na ustawi wa uchumi wa taifa letu.

Maadhimisho ya mwaka huu ni ya 18, tangu Mwalimu Nyerere afariki mnamo Oktoba 14, 1999, ambapo kauli mbiu ya kongamano la mwaka huu inasema “Mtazamo wa Mwalimu Nyerere katika Uchumi wa Viwanda na Maendeleo ya Jamii”.

Maadhimisho hayo yatafanyika visiwani Zanzibar ambapo shughuli ya kuzima mwenge wa uhuru itafanyika.

Hakuna Kitu Kinachanganya Kama Kuwa Kwenye Mahusiano na Mtu Asiyejua Nini Haswa Anataka

$
0
0
Hakuna kitu kinachoudhi na kuchanganya kama kuwa katika ndoa au mahusiano na mtu ambae hana uhakika ni nini haswa anataka. Unakuta kuna muda anaonesha kukupenda kweli, then baadae unakuta mtu huyohuyo anakufanya ujihisi hupendwi. Mtu anakuacha halafu baada ya kujitahidi kuendelea na maisha yako anarudi na kukuomba mrudiane.

Mtu anakwambia kabisa it's over, lakini baadae anakuita eti muyajenge. Mtu yuko na ndoa kabisa ila anajifanya yuko Single. Mtu kwa muda mfupi tu anabadilika kutoka "Nakupenda sana" kwenda "nakuchukia sana". Anakufanya unajisikia vizuri kidogo tu anakunadilikia..ni mbaya zaidi kama umezaa na mtu wa aina hiyo ambae haeleweki.

Huu upuuzi wa kutokueleweka kwenye mahusiano ni utoto. Mtu ambae amekua kiakili anahitaji uhakika. Mtu aliyekua kiakili anaeleza wazi kama mahusiano yapo au hayapo. Kuwa na uhakika na maamuzi yako kuliko kupotezeana muda.

Acha kumchezea michezo ya kitoto mwenzako. Chagua moja kama upo kwenye uhusiano nae au laa. Usiwe mguu mmoja ndani mguu mmoja nje. Mapenzi sio moody. Mapenzi ni kitu ambacho kipo constant. Mapenzi yanatabirika na yanayotegemeana. Mapenzi ni facts sio theory. Mpe mtu clarity kuhusu mahusiano yenu.

Ndoa imara na Mahusiano imara hayajengwi kwa misingi ya mapenzi yasiyo na uhakika. Mtu uliyenae anaweza kabisa kukubaliana na matokeo. Kama haumtaki tena mweleze wazi ili afahamu amesimama wapi. Ni bora kukataliwa sasa hivi ukaendelea na maisha yako huku ukijitahidi kutibu moyo, kuliko kuendelea kusalitiwa na mtu ambae hafahamu ni nini anachokitaka.


From Tweve Hezron

Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

$
0
0
THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Serikali yakanusha Kukataa Kuongeza Mishahara, Yadai Taarifa hiyo ilizushwa na Chadema

$
0
0
Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. John Pombe Magufuli hakuna sehemu ambayo alitamka kutotekeleza ongezeko la mwaka la mishahara ya watumishi wa Umma na kuitaka TUCTA kuachana na masuala ya siasa.

Hayo yamesemwa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas  kuwa hoja ya Rais Magufuli kutokuwaongezea mishahara watumishi wa Umma ilizushwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kusema Rais Magufuli hakusema jambo hilo .



“Hakuna mahali Rais Magufuli alipokataa kutekeleza ahadi ya ongezeko la mwaka la mishahara ya watumishi wa umma, Serikali imetenga Bil. 487.7 kuwalipa wafanyakazi wanaopanda madaraja kwa mwaka huu wa fedha”amesema Dkt. Abbasi .

Soma taarifa kutoka serikalini kwa vyombo vya habari.


Video: Nimekuja Dar kwaajili ya Danube sio Diamond – Zari

$
0
0
Mama watoto wa Diamond, Zari The Bosslady ametua jijini Dar es salaam jioni ya leo akitokea nchini Afrika Kusini kwaajili ya kuzindua duka jipya la bidhaa za nguo, Danube.



Mrembo huyo ametua katika Uwanja wa JK Nyerere International akiwa bila mtoto wake mdogo Nillan kitendo ambacho kimeonyesha huwenda mrembo huyo ajafika kwaajili ya Diamond na ni kwa muda mchache.

Akiongea na waandishi wa habari muda mchache baada ya kuwasili, Zali alisema amekuja nchini kwaajili ya uzinduzi wa duka la Danube sio kitu kingine

“Nimekuja Tanzania kama balozi wa Danube sio Diamond. Kwahiyo nashukuru kwa upendo wetu, na tuendelee kutumia bidhaa za Danube,” alisema Zari.

Zari amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi Mlimani City jijini Dar es salaam siku ya kesho kwaajili ya uzinduzi wa duka hilo.

Wawili hao waliingia kwenye mgogoro mzito wa mapenzi baada ya Diamond kuchepuka na mwanamitindo, Hamisa Mobetto na kufanikiwa kupata mtoto mmoja.

Dar, Kilimanjaro, Mwanza yaongoza Kwa Wagonjwa wa Akili

$
0
0

Matumizi ya vilevi mbalimbali ni moja ya vichocheo vinavyosababisha ongezeko la wagonjwa wa akili, huku mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro na Mwanza ikiwa ndio vinara vya wagonjwa hao.

Mratibu wa Taifa magonjwa  ya akili na dawa za kulevya kutoka Wizara ya Afya, Shadrack Buswelu amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani Morogoro leo Ijumaa.

Biswalu amesema magonjwa ya akili au afya ya akili bado yamekuwa ni tatizo kubwa katika jamii, hivyo ni mzigo kwa Taifa na duniani kwa ujumla jambo linalosababisha kurudisha nyuma maendeleo katika nyanja mbalimbali.

Amesema huduma ya afya ya akili kwa sasa inatakiwa kupewa kipaumbele mahala pa kazi, waajiri wanapaswa kuhakikisha wanawahudumia wafanyakazi wao pindi wanapoona kuna tatizo linajitokeza kwenye maeneo ya kazi.

“Mikoa ya Lindi na Mtwara inaonyesha kuwa ya mwisho kwa kuwa na wagonjwa wa akili na hii sio sababu kwamba hawapo bali idadi katika mikoa inayoongoza wamekuwa wakiripotiwa na mikoa hiyo ya mwisho ripoti yake imekuwa ni ndogo,”amesema.

Mratibu huyo ambaye hakutaka kutanja tawimu kwa namba amesema uelewa wa wananchi bado umekuwa mdogo kutokana na asilimia kubwa kukimbilia kwa waganga wa jadi badala ya kufika katika vituo vya kutolea huduma.

Amesema kwa mujibu wa taarifa ya afya akili na dawa za kulevya zinazopatikana kwenye vituo vya kutolea huduma za mwaka 2015/2016 wagonjwa 6,072 walilipotiwa, huku 2016/2017 wagonjwa waliouzuria kupatiwa matibabu ni 7,084 hivyo takwimu hizo zimekuwa zikiongezeka kila mwaka.

Alitaja baadhi ya vichocheo vya ugonjwa huo kuwa ni pamoja na unywaji pombe, matumizi ya dawa za kulevya, ugumu wa maisha unaochangiwa na msongo wa mawazo, balaa la njaa, ubakaji, mafuriko, mtu kupoteza kazi, kufukuzwa shule, vita na wamama wajawazito kutumia vilevi husababisha mtoto kuzaliwa na ugonjwa huo.

Vile vile amesema Serikali ilitoa sheria ya afya ya akili ya Mwaka 2008 ambayo imekuwa ikitoa maelekezo ya namna gani huduma zitakavyotolewa nchini,akasisitiza kauli ya wanajamii kumuita mtu kichaa ni kosa kisheria.


Idriss Sultan Hana ‘Ngoma’ Aweka Majibu Hadharani

$
0
0

Mshindi wa Big Brother Africa 2014 Idris Sultan ameweka wazi vipimo vinavyoonyesha kuwa hana virusi vya ukimwi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Idris ameweka picha inayoonyesha karatasi yenye majibu ya vipimo ya afya yake alivyovifanya leo Ijumaa.

Karatasi hiyo inaonyesha kuwa hana virusi vya ukimwi wala homa ya ini.

Picha hiyo ilibebwa na ujumbe uliosomeka, "Barua ya wazi kwa  mwanamke ninayemtongoza ni matumaini yangu  hii itakufanya unipe moyo wako wote. Nimejaribu kufaulu lakini kama unavyoona vipimo vyote nimefeli na hakuna mtihani ninaoupenda kama kufeli.”

Serikali Kununua Vichwa Visivyo na Mmiliki Bandarini

$
0
0

Serikali imesema ipo katika mchakato wa kuvinunua vichwa 13 vya treni ambavyo vilitelekezwa kwenye Bandari ya Dar es Salaam.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema hayo leo Ijumaa wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa mashine za ukaguzi wa mizigo(Scanners) zenye thamani ya Sh27 bilioni kwa ajili ya kuongeza ulinzi na udhibiti wa mapato kwenye bandari hiyo.

Profesa Mbarawa amesema Serikali imeunda timu ya wataalamu 11 kwa ajili ya kufanya tathmini ya ubora pamoja na thamani ya fedha  ya vichwa hivyo na baada ya kukamilika watafanya makubaliano na mmiliki wa vichwa hivyo ili kuvinunua.

Julai mwaka huu katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi kwaajili ya upanuzi wa bandari hiyo Rais John Magufuli alisema ana taarifa ya vichwa vya treni vilivyoshushwa bandarini hapo lakini mmiliki
wake hajulikani huku akisisitiza kuwapo kwa mchezo mchafu.


Utata huo uliibuka kufuatia  Shirika la Reli Tanzania(TRL) kununua vichwa hivyo kupitia mkataba wake na kampuni ya EMD ya Marekani na utengenezaji ukafanywa na kampuni ya DCD ya Afrika Kusini huku taratibu za ununuzi zikidaiwa kukiukwa.

Hata hivyo tayari Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko alishaeleza kuwa vichwa hivyo vina nembo ya TRL lakini vilizua mgogoro baada ya kubainika kuwa mchakato wa ununuzi haukuwa sahihi.

Lakini kwa mujibu wa taarifa iliyowahi kutolewa kwa vyombo vya habari na TRL Machi 23, 2015 ilibainisha kuwa vichwa viwili kati ya 15 vya treni vilivyonunuliwa na shirika hilo vilipokelewa katika Bandari ya Dar es Salaam Machi 21, 2015.

Taarifa hiyo ilisema vichwa hivyo vimetengenezwa nchini Afrika Kusini na kwamba ununuzi huo umegharimu kiasi cha Sh70.9 bilioni ambazo zote zilishalipwa.

Mdee Mdee Noma Amjibu IGP Sirro Sakata la Sheik Ponda na Polisi

$
0
0
Mbunge wa Kawe kupitia CHADEMA, Halima James Mdee, amejibu kauli ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Nyakoro Sirro ya kutojadili suala la Tundu Lissu, na kusema hawatoacha kufanya hivyo.

Kwenye ukurasa wake wa twitter Halima Mdee ameandika ujumbe akisema kwamba hakuna sheria inayokataza mtu kujadili jambo fulani, na IGP hana mamlaka ya kukataza hilo.

“Hakuna popote katika sheria za nchi IGP ana mamlaka ya kunyamazisha watu wasijadili jambo, tutaendelea kujadili ya Lissu mpaka haki itendeke”, ameandika Halima Mdee.
Pia Halima Mdee ameendelea kwa kuandika kuhusu kukamatwa Sheikh Ponda, akisema ni mipango ya kuwafunga mdomo watu watakaojadili suala hilo.

“Najaribu kutafakari alichokisema Ponda na kwa namna gani kinaashiria uchochezi, sikioni! ni namna ya kutisha na kufunga midomo watu”, ameandika Halima Mdee.

Hivi karibuni IGP Sirro aliwataka wanasiasa kuacha kufanya mijadala ya kumjadili Tundu Lissu, na waliache jeshi la polisi lifanye kazi zake bila kuingiliwa na jana Jeshi la polisi lilitoa agizo kwa Shekh Ponda kufika kituo cha polisi kutokana na kauli alizozitoa juu ya sakata la Tundu Lissu.

Mapenzi Yamtesa Lady Jay Dee...Kafunguka Kutokutaka Ndoa na Mnigeria

$
0
0
Msanii Lady Jaydee amesema sasa hivi hafikirii kufunga ndoa na mchumba wake Mnigeria ambaye pia ni msanii, kwa sababu haamini kila mahusiano ni lazima yaishie kwenye ndoa.

Jaydee ametoa siri hiyo leo alipokuwa akipiga stori na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kuwataka watu wasitegemee jambo hilo kwake na wasikariri kila mahusiano yataishia kwenye ndoa, kwani wapo waliokimbilia ndoa na zikawashinda.

Nilianza Mziki Kwa Kuiba - Mr Blue Afunguka

$
0
0
Msanii wa Hip hop, Kheri Sameer Rajabu alimaarufu kama Mr Blue amefunguka na kusema kuwa yeye alianza muziki kwa kuiba 'verse' ya mtu kipindi alichokuwa mdogo na hivyo alipoimba na kupata shangwe sana kwa watu ndiyo kitu kilichomsukuma kufanya muziki

Mr Blue amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio ambapo leo alipewa Heshima ya Bongo fleva, Mr Blue amedai kuwa yeye alikuwa anaishi Kariakoo lakini nyumbani kwao kulitokea matatizo ya kifamilia hivyo alihama na kwenda kukaa Tandale na huko ndiko anadai kulikuwa chimbuko lake la muziki kwani watu aliowakuta huko walikuwa wanafanya muziki.

"Kwa hiyo nilipohamia huko ndiko kulikuwa nyumba ya muziki, nikajikuta nawasikiliza sana na kukariri 'verse' hivyo kuna siku nilikwenda sehemu na kuchana verse ya mtu nilishangiliwa sana, kwa hiyo mimi naweza kusema nimeingia kwenye muziki kwa kuiba 'verse' ya mtu ambaye naye nilimkuta huko nilikohamia" alisema Mr Blue.

Aidha Mr Blue amesema kuwa katika maisha yake ya muziki amekosa mengi ambayo alikuwa anastahili kuyapata kwenye muziki wake kama tuzo mbalimbali na jasho lake kwenye album zake alizotoa kipindi cha nyuma kwani hakunufaika nazo.
Itazame hapa video ya Mr Blue akimshukuru Mungu

Emmanuel Mbasha Afurahia Kutongozwa na Wanawake Wanaomtamani Kimapenzi

$
0
0
Msanii wa muziki wa Injili, Emanuel Mbasha ambaye wengi humsifia kwa utanashati wake, amesema anamshukuru Mungu kwa kuonyeshwa kupendwa, baada ya mabinti wengi kumtamani kimapenzi.

Akiongea na eNewz ya East Africa Television, Emmanuel Mbasha amesema ingawa wanawake wengi wanafunguka hisia za mapenzi juu yake, lakini anamuomba Mungu ampe mtu sahihi zaidi ili yasije yakajirudia yaliyomkuta awali.

"Wadada wengi wananipenda wa kila aina na hiyo iko wazi, ukiangalia DM yangu kila siku inajaa meseji, kuna kila aina, na ninamshukuru Mungu kwa kipaji hicho, maana yake kupendwa nako ni kibali na ni baraka za Mungu, sasa nikikurupuka tu kuchukua nitaingia majanga, natamani nipate mtu sahihi, nifanye naye maisha tupate watoto tuendelee mbele, maana yake sitawaza kukaa hivi milele ila kwa sasa sina sababu ya kukurupuka", amesema Emmanuel Mbasha.

Mbasaha ambaye amesema amechoshwa na  upweke, ameendelea kusema kwamba..."mimi nimetokea kwenye changamoto kubwa sana ya mahusiano, angekuwa mwengine angedata angeanza kunywa pombe, kuvuta bangi na kufanya mabaya, lakini nilisimama na Mungu, hivyo nimetulia nikisubiria Mungu aniletee mtu sahihi".

Emmanuel Mbasha ameachana na aliyekuwa mke wake ambaye pia ni mwanamuziki wa nyimbo za Injili, Flora Mbasha, huku akimshtaki kwa kosa la kumbaka mdogo yake, kesi ambayo Emmanuel aliachwa huru kutokana na kukutwa hana hatia.

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.



Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

Calisah Kufungua Duka la Kuuza Mimba Kwa Wanawake Wahitaji

$
0
0
Akizungumza kwenye eNewz ya East Africa Television, amesema anakusudia kufanya hivyo ili awasaidie wanawake wanaotaka kuzaa watoto wenye muonekano mzuri kama yeye, na wale ambao waume zao hawawezi kuzalisha kutokana na umri kuwa mkubwa (vibabu).

“Suala la kuzaa mimi mwenyewe ni kitu ambacho nilikuwa na plan nacho kwa sababu nimeshatoka na wanawake wengi, sema sikuwa tayari kuzaa mi bado kijana mdogo, hawa wote nilikuwa nao tu kwa mambo mengine, lakini kama kuna mtu atataka tuzae, naweka tu bao langu napiga inatoka pair flan kali, najua mtoto wangu atakuwa na maisha mazuri”, amesema Calisah.

Calisah ameendelea kwa kusema kwama...”Tunawajua wanawake wengi sana wazuri ambao wanaishi na wazee wana mapengo lakini ana hela, anajikuta anazaa naye kisa hela, tusijidharau wanaume, kwa hiyo mtu anakuja na mpunga wake nafanya chochote kwa pesa, mi kidume nanyoosha tu, aje tu na hela, kama wanawake wazuri wanatembea na watoto wazuri, kwa nini sisi wanaume tusifanye hivyo? Anakuja anatoa hela, tunapiga tunatoa pair yetu”.

Itazame vdeo yote hapa chini akizungumza hilo.

VIDEO: Hamisa Mobetto Atishiwa Kifo yeye na Mwanae

$
0
0
Mrembo Hamisa Mobetto amekua akipokea vitishio juu ya maisha yake na ya mwanae

Kuona vitishio alivoviweka wazi angalia hii video hapa VIDEO

Mwarab Fighter Bodyguard wa Diamond ni Mmoja Wapo wa Wafanyakazi Bora wa WCB.. Anajua Sana Kutimiza Majukumu

$
0
0
Habari wadau.

Mimi ni shabiki mkubwa wa diamond platnumz.. na wcb kwa ujumla..

Kuna mtu hasikiki sana anaitwa mwarab fighter.. huyu jamaa anajua sana kutimiza majukumu yake..

Niliangalia video leo akiwa anampokea zari.. jinsi anavyomuongoza kuhakikisha anakuwa safe... mpaka raha.. kuna muda zari anashangaa shangaa mwarab anamshtua tembea mama...

Hata diamond kipindi anazindua karanga mwarab anavyohakikisha bosi wake yupo safe mpaka raha yaani..

Jamaa ni mtu mzima na anajua sana anachofanya.. anatimiza majukumu kiutu uzima kabisa..

Hongera sana mwarab fighter kwa kufanya kazi yako kwa ubora.. na hongera sana diamond kwa kutoa ajira kwake..

Swali hivi hapatagi mzuka wa kiume.. maana kuna picha wapo dubai diamond na zari wamepakatana.. huku mwarabu yupo pembeni analinda.. najiuliza mashine haipataki ukakasi mazingira hayo kulinda wapendanao...

Jamaa ni jembe sana.

Najua diamond unamtembeza sana duniani.. kila unapoenda nae anaenda... safi sana kwa upendo wako... usisite kuhakikisha unamlipa vizuri na kumshauri pia awekeze ili watoto wake nae wajue baba yao alikuwa ni jembe.... asisishie kuendesha magari tu

By FRESHMAN
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images