Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.


Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

Madereva wa Daladala Waendeleza Mgogomo Tanga

0
0
Madereva wa Daladala Waendeleza Mgogomo Tanga
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, amethibitisha kuendelea kwa mgomo wa madereva wa daladala zinazofanya kazi katikakati ya jiji hilo ulioanza jana asubuhi.

Madereva hao wamegoma kufanya kazi kwa kile kinachodaiwa kupinga uonevu unaofanywa na Askari wa kikosi cha usalama barabarani ambapo wamekuwa wakiwatoza faini na kuwakamata bila makosa.
“Ni kweli madereva wamegoma tangu jana lakini wengine kwenye baadhi ya maeneo wameanza kazi leo na wengine bado wamegoma na tunatarajia kukutana nao asubuhi hii kwaajili ya kuzungumza namna ya kutatua mgomo huo”,  amesema RPC Wakulyamba.
Mapema wiki jana RPC Wakulyamba alithibitisha kukamatwa kwa madereva kumi wa mabasi na daladala kwa tuhuma za kuendesha vyombo vyao bila kufuata sheria na kanuni za usalama barabarani.

Bunge Kuanzisha Uchunguzi wa Ufisadi Mkubwa Afrika Kusini

0
0
Bunge Kuanzisha Uchunguzi wa Ufisadi Mkubwa Afrika Kusini
Bunge la Afrika leo linaanzisha uchunguzi unaohusu madai ya ufisadi wa kiwango cha juu zaidi serikalini.
Wale waliopiga ramli kuhusu ufisadi huo na maafisa mashuhuri wanatarajiwa kuitwa kutoa ushahidi wao.

Muda huu huenda ukawa wa kukosa amani miongoni mwa watu wenye ushawishi nchini Afrika Kusini.
Mawaziri, watu matajiri, mtoto wa rais na mashahidi wengine wengi, wanatarajiwa kuitwa mbele ya wabunge wanaochunguza madai ya ufisadi mkubwa nchini humo.

Inadaiwa kuwa familia moja yenye nguvu ya Gupta, imekuwa na ushawishi wa viwango vya juu serikalini, ili kuweza kujishindia kandarasi za serikali.

Familia hiyo ya Gupta imekana madai hayo sawa na rafiki wao Rais Jacob Zuma
Katika kipindi hiki cha misukosuko ya siasa kuhusu ni nani atakaye mrithi Zuma, uchunguzi wa wiki hii huenda ukawa na athari za aina yake.

Vijana Wamng'ang'ania Mugabe Wamtaka Awe Rais wa Maisha

0
0
Vijana Wamng'ang'ania Mugabe Wamtaka Awe Rais wa Maisha
Umoja wa Vijana wa chama cha Zanu PF unataka Rais Robert Mugabe, licha ya umri wake mkubwa, aruhusiwe kufia ofisini hali inayoibua fununu kwamba mzee huyo hana mpango wa kuachia madaraka kwa sasa.

Pendekezo hilo limekuja wakati huu ambao wanachama wengi katika chama hicho tawala kwenye majimbo nchi nzima walikutana mwishoni mwa wiki na kuamua kuitisha mkutano wa dharura Desemba kushughulikia mgawanyiko uliosababishwa na Mugabe kushindwa kumwandaa mrithi wake kwa miaka 37 aliyokaa madarakani.

Mikutano ya kwenye majimbo iliitishwa siku chache baada ya uamuzi toka juu uliofanywa na mkutano mkuu na kamati kuu kutaka uitishwe mkutano mkuu maalumu ili ushughulikie migogoro ya ndani inayotishia kuisambaratisha Zanu PF kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.

Mmoja wa makamu wa Mugabe, Emmerson Mnangagwa anadaiwa kuongoza kundi linaloitwa "Team Lacoste" linalohaha kumpigia kampeni aweze kumrithi Mugabe akiondoka madarakani.

Kundi jingine la vijana zaidi linalojiita "Generation 40" linaloungwa mkono na Memsapu Grace Mugabe limeelekeza mashambulizi dhidi ya Mnangagwa wakati jina la Waziri wa Ulinzi Sydney Sekeramayi limeingizwa kwenye vita ya urais na Waziri wa Elimu ya Juu Jonathan Moyo anayemwona kuwa anafaa.

Katikati ya mnyukano huu wa kuwania kumrithi Mugabe, mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Zanu PF, Mubuso Chinguno amesema chama hakina mgombea mwingine zaidi ya mzee huyo mwenye umri wa miaka 93.

"Rais Mugabe ni rais wetu wa maisha. Hatuna tatizo naye hata akifia ofisini kwa hiyo tunakaribisha mapendekezo haya mapya ya kuwepo Kongamano la Mwaka Desemba ambalo litageuzwa kuwa mkutano mkuu maalumu,” alisema Chinguno.

Janeth Museveni Afunguka Njia Alizotumia Kutunza Bikra za Watoto Wake Hadi Siku ya Ndoa Zao

0
0
Janeth Museveni Afunguka Njia Alizotumia Kutunza Bikra za Watoto Wake Hadi Siku ya Ndoa Zao
Mke wa Rais Yoweri Museveni, Janet Museveni amesema kuwa aliwatunza mabinti zake vizuri hadi wanaolewa wakiwa bikira kwa kutumia njia asilia za Kiafrika za kumlea mtoto wa kike.

“Niliwataka mabinti zangu wote kusaini kadi za ‘kusubiri upendo wa kweli’ na walijizuia kufanya ngono hadi usiku wa harusi ambao walionyesha kadi zao kwa wenza wao,” alisema mama Janet na kuongeza kuwa “jambo hili linaweza kufanikishwa hata leo.”

Janet alikuwa akizungumza katika wilaya ya Kyenjojo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike Alhamisi iliyopita.

Aliongeza: “Hivyo ndivyo sisi, hapo zamani, tulilelewa na wazazi wetu, hakukuwa una ukosefu wa maadili kama ilivyo sasa.”

Siku hiyo ilifuatiwa na mjadala uliofanywa na wadau waliokuwa na utayari wa kulinda haki za vijana wa kike.

Mabinti wa mama Janet ni pamoja na Diana aliyeolewa na Geoffrey Kamuntu, Natasha aliyeolewa na Edwin Karugire, na Uvumilivu aliyeolewa na Odrek Rwabwogo.

“Mwanamume awe mkubwa au mdogo, sema hapana na kimbia, mwanamume anaweza kutumia lugha tamu kukushawishi, usimruhusu mwanamume yeyote kukuchezea wakati wewe ni binti mdogo, mwanamume asikuingize kwenye ngono hadi pale utakapoolewa, penzi la kweli husubiri,” Janet alitoa ujumbe huo kuwalenga wasichana

Marekani Yataka Utulivu Baada ya Iraq Kuteka Mji wa Kirkuk

0
0
Marekani Yataka Utulivu Baada ya Iraq Kuteka Mji wa Kirkuk
Marekani imeombakuwepo utulivu baada ya wanajeshi wa serikali ya Iraq kuteka mji wa Kaskazini mwa Iraq wa Kirkuk na vituo muhimu kutoka kwa wakurdi.
Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani Heather Nauert amezitaka penda zote kuzuia makabiliano zaidi.
Wanajeshi wa Iraq walielekea Kirkuk wiki tatu zilizopita, baada ya eneo la Kurdistan kuandaa kura ya maoni ya uhuru iliyokumbwa na utata.
Wanajeshi wa Iraq waingia Kirkuk, Wakurdi watoroka
Lengo lao ni kuteka sehemu zilizo chini ya udhibiti wa wakurdi tangu Islamic State wadhibiti eneo hilo.
Wenyeji wa maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa wakurdi ukiwemo mji wa Kirkuk, kwa wingi waliunga mkono kujitenga kutoka Iraq wakati wa kura ya tarehe 25 mwezi Septemba.

Licha ya mji wa Kirkuk kuwa nje ya eneo la Kursistan, wapigaji kura wa Kurdistan walio mjini humo waliruhusiwa kushiriki kura.
Waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abadi aliitupilia mbali kura hiyo na kuitaja kuwa iliyo kinyume na katiba.
Wakurdi wa Iraq wanasema wako tayari kujitenga na kuwa na taifa lao
Huku hayo yakijiri, wapiganaji wanaoungwa mkono na serikali wamechukua udhibiti wa mji wa Sinjaar Kaskazini magharibi mwa mkoa wa Nineveh.
Hatua hiyo katika mji unaodaiwa na wakurdi na pia mamlaka za Iraq, ilifanyika bila ya kuwepo mapigano baada ya wanajeshi wa wakurdi wa Peshmerga kuondoka eneo hilo.

Katika taarifa Bi Nauert alisema kuwa Marekani ina wasi wasi kutokana na ripoti za kuendelea mapigano katika mji wa Kirkuk.
Bi Nauert alisema kuwa Marekani ilikuwa ikishirikiana na maafisa kutoka pande zote, kushiriki mazungumzo ikionya kuwa bado kuna kazi kubwa ya kulishinda kundi la Islamic State nchini Iraq.
Mapema Rais Donald Trump alikuwa amesema kuwa maafisa wa Marekani hawapendelei upande wowote.

TMA Yatahadharisha Kuanza kwa Mvua za Masika Zinazotarajia Kuanza Novemba

0
0
TMA Yatahadharisha Kuanza kwa Mvua za Masika Zinazotarajia Kuanza Novemba
MAENEO ya kusini-magharibi mwa nchi yanategemewa kuanza kupata mvua za masika kuanzia mwezi Novemba mwaka huu hadi Aprili mwaka kesho (2018).
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini, Dkt. Agnes Kijazi, aliyesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo alisema kutokana na mifumo ya hali ya hewa, mvua zitakuwa ni za wastani hadi juu ya wastani.
Kwa upande wa Kanda ya Magharibi ambayo inajumuisha mikoa ya Tabora, Rukwa, Katavi na Kigoma, mvua zitaanza wiki ya kwanza ya Novemba na kuendelea hadi wiki ya nne Aprili mwaka kesho. Kwa Kanda ya Kati inayojumuisha mikoa ya Singida na Dodoma, mvua zitaanza wiki ya kwanza ya Novemba hadi Desemba mwaka huu ambapo zitaendelea na kwisha wiki ya nne ya Aprili mwaka kesho.
Kwa Nyanda za Juu Magharibi zinazojumuisha Mbeya, Songea, Iringa, Njombe, Ruvuma na kusini mwa Morogoro, mvua zitaanza Novemba hadi Desemba na kuendelea hadi wiki ya nne ya Aprili mwaka 2018. Dtk. Kijazi alitoa wito kwa wananchi kuyavuna maji yanayotokana na mvua hizo na kuweka chakula kwa ajili ya mifugo kwa vile mvua zitakuwa za wastani.

Shahidi Akwamisha Kesi ya Meno ya Tembo

0
0
Shahidi Akwamisha Kesi ya Meno ya Tembo
Kesi ya uhujumu uchumi kwa kujihusisha na meno ya tembo yenye thamani ya Sh13 bilioni itaendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kesho, Oktoba 18, 2017.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi leo Jumanne amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa ilipaswa kuendelea kusikilizwa lakini shahidi wa upande wa mashtaka amepata udhuru.

Baada ya kueleza hayo, wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko amesema alitarajia upande wa mashtaka ungeandaa mashahidi wawili au watatu ili mmoja akipata udhuru wengine waendelee.

Soma: Kesi malkia wa ndovu kusikilizwa siku nne

Nkoko ameutaka upande huo kuandaa mashahidi watatu ili hali kama hiyo isijitokeze kesho.

Hakimu Shaidi ameuagiza upande wa mashtaka kuzingatia suala hilo na ameahirisha kesi hadi kesho kwa ajili ya kuendelea na usikilizwaji.

Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mfululizo kuanzia Oktoba 18, 19 na 20, mwaka huu.

Washtakiwa Salvius Matembo, Philemon Manase na raia wa China anayedaiwa kuwa Malkia wa Pembe za Ndovu, Yang Feng Glan (66), wanakabiliwa na kesi ya kuhujumu uchumi kwa kujihusisha na meno ya tembo yenye thamani ya Sh13 bilioni.

Washtakiwa wanadaiwa kati ya Januari Mosi, 2000 na Mei 22, 2014  walijihusisha na biashara  ya nyara za Serikali kinyume cha sheria.

Washtakiwa wanatetewa na mawakili Nkoko, Hassan Kihangio na Jeremiah Mtobesy

Shuhudia Maajabu ya Chief Sultan Mzee...Mtaalamu wa Nyota za binadamu

0
0
Ona Maajabu ya Chief Sultan Mzee

 Mtaalamu wa Nyota za binadamu Africa Mashariki na dunia nzima,
Amewasaidia watu wengi kujua nyota zao na jinsi ya kuzing'arisha,
Anarudisha Mpenzi,Mume,Mke mliyeachana NDANI ya masaa manne(4) tu,
Anaweza kuongeza ROMANCE na MAHABA kwa Mwenzi wako
Anatoa pete ya BAHATI pamoja na kukupa uwezi wa Kupata faida kubwa katika biashara yako,
Kwa wale mnaosumbuliwa na Chuma ulete tatizo hilo analiondoa kabisa,
Anakuwezesha kushinda kesi iliyodumu siku nyingi nk.


KWA USTAA,UMARUFU UTAPATA UTAJIRI WA MAISHA NA BILA MASHARTI YOYOTE, UTAPEWA NGUVU ZA KUJILINDA NA UTAJIRI, MALI NA AFYA YAKO,Karibu kwa CHIEF SULTAN MZEE akupatie Pete za Bahati na utajiri.Wachungaji wengi duniani, Wanasiasa na Wasanii Maaarufu duniani Tayari wamejiunga pia wamefaidika na wamebadirisha  Maisha yao toka umasikini mpaka utajiri,kujua m

Tundu Lissu Kusafirishwa Nje ya Nchi kwa Matibabu

0
0
Tundu Lissu Kusafirishwa Nje ya Nchi kwa Matibabu
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Freeman Mbowe amesema kuwa hali ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu sasa imezidi kuimarika na kusema atasafirishwa kwa matibabu ya awamu ya tatu siku za karibuni.

Mbowe amesema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya chama hicho, alipokuwa akitoa taarifa ya maendeleo ya Tundu Lissu na kusema mpaka sasa Mbunge huyo anaendelea vizuri na kudai amefanyiwa upasuaji mara 17.
"Tundu Lissu mpaka sasa amefanyiwa upasuaji mara 17 amewekewa damu nyingi kuliko mgonjwa yoyote katika hospitali ya Nairobi lakini Mungu ameendelea kutenda miujiza kwake, saizi mashine zote zilizokuwa zinamsaidia zimeondolewa, saizi hapumulii mashine tena, mirija yote aliyokuwa anatumia kwa ajili ya chakula imeondolewa na juzi kwa mara ya kwanza aliweza kukaa" alisema Mbowe

Mwenyekiti wa CHADEMA aliendelea kueleza kuwa "Matibabu ya awamu ya tatu ya Tundu Lissu yatafanyika nje ya nchi haitakuwa tena Kenya wala Tanzania, lakini kwa sababu za usalama hatuwezi kusema atakwenda sehemu gani au nchi gani, ukifika wakati sahihi tutasema hiyo awamu ya tatu ya matibabu itakuwa ya muda mrefu kidogo" alisema Mbowe
Mbali na hilo Mbowe ameendelea kusema kuwa serikali inafahamu watu ambao wameshambulia Tundu Lissu na kudai wao hawana imani na vyombo vya dola nchini na kusema vyombo hivyo vimekuwa tawi la Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo hawana nia ya dhati katika kufanya uchunguzi juu ya sakata la Tundu Lissu kupigwa risasi mnamo Septemba 7, 2017.

Tundu Lissu Afanyiwa Upasuaji Kubwa Mara 17, Atolewa ICU

0
0
Tundu Lissu Afanyiwa Upasuaji Kubwa Mara 17, Atolewa ICU
 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ametoka ICU na sasa anaweza kukaa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne, Mbowe amesema afya ya Lissu inaimarika kwa kuwa alihitaji upasuaji mwingi sana kutokana na risasi zilizoingia kwenye mwili wake.

“Amefanyiwa upasuaji mkubwa mara 17 mpaka sasa. Ameongezewa damu nyingi kuliko mtu yeyote miaka 20 iliyopita ametoka ICU wiki iliyopita,” amesema Mbowe.

Soma: Mbowe: Lissu anaweza kuongea na kula kidogo

Amesema Lissu hatumii oxygen tena wala mirija na kwamba anakula chakula anachokitaka.

“Juzi kwa mara ya kwanza alikaa, anatembea Wheel Chair na aliliona jua kwa mara ya kwanza,” amesema Mbowe.

“Tunawashukuru madaktari wa Dodoma na Nairobi. Hospitali ya Nairobi imefikisha awamu ya pili ya kutibu. Tunavyozungumza baada ya wiki moja kadri madaktari watakavyoshauri atamaliza matibabu ya pili,”

“Ataanza awamu ya tatu nje ya Nairobi yatakayokuwa ya muda mrefu. Kwa usalama wake hatutataja wapi anakwenda. Siyo Tanzania na sio jirani. Hiyo ndio hali halisi ya mgonjwa.”

Juma Nature Afunguka Kuhusu Kuacha Muziki

0
0
Juma Nature Afunguka Kuhusu Kuacha Muziki
Msanii Juma Nature ambaye ni mkongwe kwenye game ya bongo fleva Juma Kassin Nature, amesema wasanii wanaotangaza kuacha muziki na kuendelea kuwepo wanatafuta huruma ya mashabiki, au wanawapima watapokeaje.

Juma Nature ameyasema hayo alipokuwa akiongea na mwandishi wa East Africa Television, na kusema kwamba ni vigumu kwa mwanamuziki kuacha kufanya muziki, hivyo wasidanganye watu na kutafuta kiki kwa kujaribu kuacha muziki.

Simba Yakanusha Kuliondoa Benchi Lake la Ufundi

0
0
Simba Yakanusha  Kuliondoa Benchi Lake la Ufundi
Klabu ya soka ya Simba imeendelea kukanusha taarifa za kutaka kuliondoa benchi lake la ufundi chini ya kocha Mcameroon Joseph Omog na msaidizi wake Mganda Jackson Mayanja.

Hayo yamesemwa leo na afisa habari wa klabu hiyo Haji Manara ambapo amesema taarifa zozote zinazoenezwa si za kweli na klabu inaendelea na benchi lake kama kawaida.
“Kuhusu makocha Simba bado inaendelea na benchi lake la ufundi chini ya mwalimu Omog na Mayanja hakuna mabadiliko yoyote yaliyofanyika”, amesema Manara.
Aidha Manara amesema kikosi cha Simba kinaingia kambini leo kuanza maandalizi ya mchezo wao wa ligi kuu wikiendi ijayo dhidi ya Njombe Mji kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Aidha Manara amempongeza Mwenyekiti mpya wa Bodi ya ligi TPLB ambaye pia ni Katibu wa Yanga Clement Sanga ambapo amesema klabu ya Simba itampa ushirkiano ili kutatua changamoto zilizopo kwenye ligi kuu.

Nassari Awajibu Takukuru, 'Sitokaa Kimya Endapo Sioni Hatua Zinazochukuliwa'

0
0
Nassari Awajibu Takukuru, 'Sitokaa Kimya Endapo Sioni Hatua Zinazochukuliwa'
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari amesema kuwa hatokaa kimya endapo haoni hatua zinazochukuliwa.

Nassari amesema hayo leo Jumanne muda mchache baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola kumtaadharisha Nassari kuacha kugeuza taarifa anazoziwasilisha kwenye taasisi hiyo kuwa ni za kisiasa.

Hata hivyo Nassari amesema, “Mlowola inabidi asome sheria ya ‘Whistle blower’ ili nikae kimya lazima nione jitihada zinazofanyika kama hakuna nitaendelea kuongea. Sitokubali kutishwa ili nisiendelee kupeleka ushahidi ninachotaka kuona ni wahusika wanachukuliwa hatua sio madiwani, wahusika wakuu ni mkuu wa wilaya na mkurugenzi,”

Awali akizungumza leo Jumanne asubuhi, Mlowola ametoa tahadhari hiyo kwa Nassari leo Jumanne, Oktoba 17, 2017 alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema endapo Nassari ataendelea kuingiza siasa kwenye suala hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mlowola amesema kitendo cha mwanasiasa huyo kuweka hadharani taarifa za uchunguzi ni kinyume cha sheria kwa kuwa kazi hiyo inatakiwa kufanyika kwa siri na Mahakama ndiyo yenye jukumu la kuchukua hatua.

Amesema Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa lakini jukumu hilo linakuwa tofauti kwa Nassari ambaye ameamua kujitokeza hadharani.

Soma: Takukuru yamtaka Nassari kuacha kuingiza siasa katika taarifa zake

"Alicholeta Nassari kwetu ni taarifa si ushahidi. Ameleta tumezipokea na tunazifanyia kazi, inashangaza anapozungumza na vyombo vya habari na kutuelekeza namna ya kufanya kazi," amesema.

Mlowola amesema, "Tulishampa angalizo kuwa mambo tunayoongea ni siri lakini mwenzetu inaonekana anafanya siasa kama anavyosema mwenyewe kuwa ataendelea kuleta ushahidi kama series ya Isidingo."

Mkurugenzi mkuu huyo amemtaka Nassari kuacha kukiingiza chombo hicho kwenye siasa ili kifanye kazi kwa uhuru kama sheria inavyoelekeza.

"Nitoe rai kwa Nassari na wengine wote, ukishaleta taarifa kwenye chombo husika kama hiki kiache kifanye kazi. Hakuna sababu ya kukishinikiza au kukiingiza kwenye malumbano ya kisiasa. Ukweli wa mambo utajulikana mahakamani," amesema.

Mimi Nimefika Kituoni Naibu Waziri Nakukabidhi Kijiti Endelea na Safari- Anastazia Wambura

0
0
Mimi Nimefika Kituoni Naibu Waziri Nakukabidhi Kijiti Endelea na Safari- Anastazia Wambura
Aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura ameufananisha utumishi wa umma na chombo cha usafiri ambacho abiria hushuka kituoni baada ya kufika na dereva kuendelea na safari.

“Mheshimiwa waziri, viongozi wenzangu na ndugu zangu watumishi wa wizara, mimi nimefika kituoni, naibu waziri nakukabidhi kijiti endelea na safari, endelea kuwatumikia Watanzania kama ambavyo ilani ya chama tawala inavyoeleza,” amesema Wambura.

Amesema hayo leo Jumanne, Oktoba 17,2017 baada ya mrithi wake Juliana Shonza kuwasili katika ofisi za wizara mjini Dodoma na kupokewa na Waziri wa wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe, viongozi wa wizara na watumishi wengine.

Wambura amempongeza Shonza kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo. Pia, amemshukuru Rais John Magufuli kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kuwatumikia Watanzania.

Kwa upande wake, Shonza ameahidi kushirikiana na watendaji wa wizara, wadau na wananchi kwa jumla kusimamia maadili ya Mtanzania.

“Wizara hii ni muhimu kwa kuwa inajenga taswira ya Taifa kupitia sekta zake za habari, utamaduni, sanaa na michezo hivyo nitahakikisha tunashirikiana kwa karibu katika kuwatumikia wananchi,” amesema Shonza.

Amesema atahakikisha maadili bora kwa jamii yanazingatiwa ili kuendelea kujenga Taifa imara kwa kuzingatia mavazi yenye heshima na nyimbo zenye kujenga.

Shonza katika taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari (Maelezo) amesema ni wajibu wao wakiwa watumishi wa umma kuhakikisha wanatekeleza ilani ya chama tawala kilichoahidi kuwatumikia Watanzania ili kuhakikisha malengo ya Serikali yanafikiwa kwa wakati.

Waziri Mwakyembe amemuahidi ushirikiano wa hali na mali Shonza katika kuwahudumia wananchi kupitia sekta za habari, utamaduni, sanaa na

Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

0
0
THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Madiwani Waliojiuzulu Chadema Wahojiwa kwa Zaid ya Saa Sita

0
0
Madiwani Waliojiuzulu Chadema Wahojiwa kwa Zaid ya Saa Sita
Maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam, wamewahoji kwa zaidi ya saa sita, madiwani waliojiuzulu Chadema wanaotuhumiwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kuwa walipewa rushwa.

Waliofika Takukuru ni Catherine Mtui, aliyekuwa diwani wa viti maalumu, Japhet Jackson (aliyekuwa diwani wa Ambuleni) na Bryson Isangya (aliyekuwa diwani wa Maroroni). Baada ya kuhojiwa hawakutaka kuzungumza chochote wakisema wanaacha uchunguzi uendelee.

Pamoja nao, diwani wa Mbuguni, Ahimidiwe Rico anayedaiwa kuwa ndiye alirekodi sauti na picha wakati akishawishiwa na viongozi wa Serikali na wa Halmashauri ya Meru amehojiwa kwa zaidi ya saa tatu leo Jumanne Oktoba 17, 2017.

Rico amesema amewaeleza Takukuru kila kitu ambacho anakifahamu katika sakata hilo, ikiwemo kuwarekodi viongozi ambao walimshawishi kujiuzuru udiwani.

"Msimamo wangu ni kwamba, nachukia rushwa. Nimewaeleza kila kitu na wao waliniuliza kuhusu vifaa nilivyotumia kuwarekodi nikawaambia ni mali ya mbunge, alivitoa nchini Uingereza," amesema.

Rico aliyesindikizwa na diwani wa  Nkwanankore, Wilson Nanyaro amesema  ana imani na Takukuru kwamba watafanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua.



Soma: Nassari, Lema waitupia zigo Takukuru

"Nimewaeleza wazi kuwa hata shauri hili likienda mahakamani nipo tayari kwenda kutoa ushahidi na kuthibitisha sauti za watu ambao niliwarekodi," amesema.

Amesema baada ya mahojiano yaliyoanza saa tatu hadi saa sita mchana, maofisa wa Takukuru wamemwambia aondoke na watamuita watakapomuhitaji.

Hakuna ofisa wa Takukuru aliyekuwa tayari kuzungumzia mahojiano hao wakisema wasemaji ni makao makuu ya ofisi hiyo Dar yaliyoko jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, mbunge Nassari amekiri kumpatia vifaa vya kurekodi diwani Rico ili kufichua njama za kujiuzulu madiwani.

Nape Nnauye: Watu Hawatakiwi Kuiogopa Serikali Yao Bali Serikali Inapaswa Kuogopa Watu Wake

0
0
Nape Nnauye: Watu Hawatakiwi Kuiogopa Serikali Yao Bali Serikali Inapaswa Kuogopa Watu Wake
Mbunge wa Mtama, Nape Moses Nnauye amefunguka na kusema kuwa watu hawapaswi kuogopa serikali yao bali serikali ndiyo inapaswa kuogopa watu wake.

Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo ametumia maneno ya mwandishi wa vitabu maarufu kutoka nchini Uingereza Alan Moore ambaye mpaka sasa ameshaandika vitabu vingi vikiwepo Watchmen, V for Vendetta na From Hell.
Ujumbe huo alioweka Mbunge wa Mtama uliwekwa kwa lugha ya kiingereza "“People shouldn't be afraid of their government. Governments should be afraid of their people”  ukiwa na maana ya kuwa Watu hawapaswi kuogopa serikali yao bali Serikali inapaswa kuogopa watu wake.

Kufuatia ujumbe huo baadhi ya watu wameungana naye na kusema ndiyo ambavyo inapaswa kuwa huku wengine wakimpa changamoto kiongozi huyo


Ujangili wa Kutumia Waya Wasababisha Kupungua Nyumbu Serengeti

0
0
Ujangili wa Kutumia Waya Wasababisha Kupungua Nyumbu Serengeti
Ujangili wa kutumia waya katika hifadhi za Taifa, Mapori ya Akiba na Hifadhi za Jamii (WMA), umechangia kupungua kwa wanyama wakiwamo nyumbu kwa asilimia 40 katika ikolojia ya Serengeti.

Nyumbu ni kati ya vivutio vinavyoifanya Hifadhi ya Serengeti kuwa kwenye maajabu ya dunia kutokana na jinsi wanavyohama kwa kuvuka Mto Mara kwenda Maasai Mara nchini Kenya na kurudi.

Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Wanyamapori (Tawiri) cha Hifadhi ya Serengeti, Dk Robert Fyumagwa alisema juzi kuwa hali si nzuri.

Dk Fyumagwa alitoa kauli hiyo katika mdahalo wa wadau wa hifadhi ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya miaka 18 ya kifo cha Mwalimu Julius Nyerere, chini ya uratibu wa Frankfurt Zological Society, Serengeti Media Centre na Chuo cha Utalii (Setco).

“Nyumbu wamepungua kutokana na ujangili wa nyaya unaofanywa na jamii inayozunguka ikolojia hiyo ambayo inasema inamuenzi Mwalimu Nyerere, ikumbukwe yeye alikemea ufujaji wa mali za umma na kila mwananchi ana wajibu wa kulinda maliasili zetu,”alisema.

Meneja wa Mradi wa Frankfurt Zological Society, Masegeri Tumbuya alisema kuwa tangu Aprili hadi Septemba mwaka huu, mitego 6,837 ya nyaya iliteguliwa katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti kupitia kitengo maalumu kinachoshughulika na udhibiti wa ujangili huo.   

Mange, Wema Wang'aa Matibabu ya Lissu Wakusanya Zaidi ya Milioni 60

0
0
Mange, Wema Wang'aa Matibabu ya Lissu Wakusanya Zaidi ya Milioni 60
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amedai Wema Sepetu, Mange Kimambi pamoja na team yao ya mtandaoni wamefanikisha kupatikana kwa pesa zaidi ya milioni 60 kwaajili ya matibabu ya Mh Tundu Lissu ambaye amelazwa nchini Kenya kwaajili ya matibabu. Amedai warembo hao pamoja na wadau wengine mitandaoni waishio nchi za nje waliweza kuchanga kupitia mitandao na kufanikisha kupatikana kwa hela hizo.

Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images