Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Viongozi wa Chadema Wapo Hatarini, Kuitwa Viherehere kwa Kushughurikia Tukio la Lissu- Mbowe

0
0
Vihongozi wa Chadema Wapo Hatarini, Kuitwa Viherehere kwa Kushughurikia Tukio la Lissu- Mbowe
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Taifa, Freeman Mbowe amedai kuwa anafahamu baadhi ya viongozi wa Chadema wapo hatarini na hata kufikia kuitwa viherere kwa kujiweka mbele kwenye tukio la Lissu


Mbowe amesema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari akielezea maendeleo ya hali ya Lissu ya kiafya ambaye anatibiwa huko Jijini  Nairobi  baada ya shambulio la risasi zaidi 30 kwenye gari lake.
Mbowe amesema kuwa kamwe hawatathubutu kurudi nyuma katika suala la kumpigania Lissu wala kukiri umauti na badala yake wataendelea kupambana kwa maombi na mikakati.
"Kuna wengine tunaitwa viherehere. Hatutarudi nyuma wa kumuogopa yeyote.Tunajua kuna nini kinapangwa, hatutakiri umauti tutaukataa kwa nguvu zote. Hatuwezi kusema tupo tayari kufa maana ulimi ukikiri umauti ndivyo itakavyokuwa" Mbowe.
Katika upande mwingine Mbowe amewaahidi wananchi na Watanzania wote kwa ujumla kuwa kuanzia leo zitaonekana picha za Mh. Lissu akiwepo hospitalini ili kuthibitisha kauli yake ya kwamba kiongozi huyo ameimarika kiafya.

Mapya Yaibuka Waraka wa Babu Seya Aliomwandikia Kwenda kwa Rais Magufuli

0
0
HIVI karibuni ulisambazwa waraka mzito na wa kushtua kwenye mitandao ya kijamii uliosemekana umeandikwa na mwanamuziki wa dansi mkongwe nchini, Nguza Viking almaarufu kama Babu Seya anayekitumikia kifungo cha maisha gerezani.
Kufuatia kusambaa kwa waraka huo, Gazeti la Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita liliingia katika Gereza la Ukonga jijini Dar anapokitumikia kifungo chake mwanamuziki huyo na kuzungumza naye ambapo alianika mambo mapya mbali na waraka huo.
WARAKA ULIOSAMBAA
Waraka huo wenye ujumbe mzito uliodaiwa uliandikwa ili umfikie Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli ‘JPM’ ulisomeka hivi:
“MFUNGWA WA MAISHA
Na Babu Seya akiwa gerezani
…NAWAOMBA Mwambieni Rais Magufuli juhudi zake nazisikia.
“Mungu azidi kumpa maarifa zaidi kuliongoza vyema jahazi la Watanzania.
“Rais huyu nimependa hekima zake.. Mimi namfananisha na mwandishi wa makala za kitabu cha methali na Mhubiri Nabii Suleiman.
“Mwambieni rais nimeiweka akiba yangu ya tumaini la mwisho kwake, kwani MUNGU NDIYE MFALME WA KWANZA AWEZAE KUMALIZA MSIBA WANGU HUU WA KUISHI KWENYE KUTA ZA GEREZA.
Wa pili ni yeye RAIS JOHN JOSEPH awezae kunitenganisha mimi na maisha ya gereza.
“Sipendi ndoto yangu ya kuja kufia gerezani…naichukia kama tawala za Herode pale Galilaya. Naumwa huku hakuna makaburi mazuri ya kuzikia wafu wetu.
“ Mwambieni anisaidie japo nije kufia kwenye mikono ya mama yangu tu aliyeteseka leba kwa kumwaga damu yake nyingi wakati wa kunizaa…
“Kama ikishindikana siyo mbaya… U can see my dead body through my window coffin.
“Mtaweza kushuhudia maiti yangu yenye pamba masikioni na puani ikiwa ndani ya jeneza langu kupitia upenyo finyu wa dirisha la jeneza hilo…
“Nimekinai na hukumu na nimeshajifunza mengi. Siku nitakayotoka ndiyo siku nitakayolivaa joho la uchungaji na kupita mitaani nikihubiri neno la Mungu mpaka jasho langu ligeuke damu!
“Natumaini katika mkono wa bwana na natumaini katika mkono wa John Joseph. Halelujah, tutaonana madhabahuni…” ni sehemu ya waraka huo unaodaiwa kuwa ni wa Babu Seya.
UWAZI LATINGA GEREZA LA KEKO
Baada ya kuuona waraka huo Gazeti la Uwazi lilifunga safari hadi Gereza Kuu la Ukonga ililopo Wilaya ya Ilala jijini hapa, ambapo lilikutana na ulinzi mkali na sheria kali za gereza hilo.
Hata hivyo, lilifanikiwa kuonana na Mkuu wa Gereza, ACP Stephen Mwaisabila ambaye alisema:
“Waraka huo haujaandikwa na Babu Seya kwa sababu kuna utaratibu maalumu wa wafungwa kuandika barua kwenda kwa viongozi au sehemu yoyote wanayotaka waraka wao ufike.
“Inashangaza kuona kuna watu wanafanya kitu kama wafungwa, kwa kuandika uzushi mbalimbali kuhusu Babu Seya, kwani kuna wakati walivumisha kuwa Babu Seya kaachiwa, wengine walimuona hospitalini akipita wakavumisha kuwa yuko hoi.”
UTARATIBU WA KUANDIKA BARUA KWA WAFUNGWA
“Mfungwa yeyote ana haki ya msingi ya kuandika barua kwenda anapotaka lakini ni lazima barua yake ipitie kwa Mkuu wa Gereza, Mkuu wa Magereza wa Mkoa (RPO), Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP), kisha inaenda kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, ndipo hupelekwa kwa kiongozi anayemtaka kama ni waziri mkuu au rais.”
Mkuu huyo wa gereza aliwaonya wanaondika uzushi huo kuwa, ni kosa kisheria kuandika mambo ya serikali wakati kuna watu walioaminiwa kwa ajili ya mambo hayo.
UWAZI ANA KWA ANA NA BABU SEYA
Uwazi lilimuona Babu Seya akiwasimamia kama kocha wafungwa wenzake ambao walikuwa wakicheza mpira wa miguu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 18 ya Kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mwandishi wetu aliomba kumsalimia Babu Seya, aliruhusiwa akaambiwa hairuhusiwi kumpiga picha.
BABU SEYA AFUNGUKA
“Nikushukuru kwa kuja kunisalimia, ujumbe ambao unasema umeenea kwenye mitandao ya kijamii, sijauandika ila nafarijika kuona kuna watu wananipigania.
“Ombi langu ukitoka nje kupitia gazeti lako mwambie Mheshimiwa Rais Dk. John Pombe Magufuli namuomba alipitie upya faili letu.
“Ni kweli mahakama ilitukuta na hatia, hatuna uwezo wa kupinga hukumu iliyotolewa na mahakama lakini ombi langu kwa Rais Magufuli ninamuomba apitie upya faili letu, nasema kwa dhati, mimi sina hatia,”alisema Babu Seya.
Hii ni mara ya pili kwa gazeti hili kuzungumza na Babu Seya akiwa gerezani tangu ahukumiwe kifungo cha maisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu zaidi ya miaka 10 iliyopita.

Mahakama: Mwenyekiti wa IEBC Hana Uwezo wa Kurekebisha Matokeo Kenya

0
0
Mahakama: Mwenyekiti wa IEBC Hana Uwezo wa Kurekebisha Matokeo Kenya
Mahakama ya upeo nchini Kenya imeunga mkono uamuzi wa mahakama ya rufaa unaomnyima uwezo mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati kurekebisha matokeo ya uchaguzi kutoka maeneo bunge.
Mahakama hiyo ya juu iliamua kwamba matokeo ya uchaguzi yaliotangazwa katika maeneo bunge ni ya mwisho.

Katika uamuzi wa mwisho , majaji watano wa mahakama hiyo walisema kuwa kulikuwa na hitilafu kati ya matokeo ya fomu 34A na 34B, mwenyekiti anafaa kutangaza matokeo ya uchaguzi na kuwaachia mahakama swala hilo kuamua.

Majaji hao walisema kuwa bwana Chebukati ana wajibu wa kukagua matokeo hayo kama yalivyopeperushwa kwa njia ya kielektroniki.
Hatahivyo kila anapokumbana na hitilafu , anapaswa kuelezea vyama vilivyopo, wachunguzi wa uchaguzi na raia na kuwachia swala hilo mahakama ya uchaguzi.
Katika uamuzi uliosomwa na naibu jaji mkuu Philomena Mwilu ,mahakama ilisema kuwa uwezo wa mwenyekiti kuchunguza matokeo sio agizo lililotolewa na mahakama bali ni sheria iliopo katika katiba na sheria za uchaguzi.

Katika kesi yake, tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC ilisema kuwa ombi hilo lilikuwa haliangazii uamuzi wa mahakama ya juu wa tarehe mosi mwezi Septemba.
Kamishna wa tume ya uchaguzi Kenya azuiwa Uwanja wa ndege
Tume ya uchaguzi Kenya yatetea uamuzi kuhusu tarehe ya uchaguzi mpya
Chama cha Kenyatta chapinga maafisa wapya wa uchaguzi Kenya
Tume hiyo iliongezea kwamba ombi hilo sio rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama ya rufaa inayojulikana kama Kesi ya Maina Kiai, ilioamuru kwamba matokeo yatakayotangazwa katika vituo vya kupigia kura ndio matokeo ya mwisho

Sababu, Dalili na Tiba ya Tatizo la Nguvu za Kiume Pamoja na Maumbile Madogo ya Uume..Soma Hapa

0
0

SABABU, DALILI NA TIBA YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME  PAMOJA NA MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA


       Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA  (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k.
     Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

      BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
     Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7  @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 7  hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=
      BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.


Wasiliana nasi (+255)
           0767447444 na
              0714335378

        UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Gigy Money Amchana Hemedy PhD Siyo Level zake, ‘Hana Hela’

0
0
Video Vixen Bongo aliyeamua kutumbukia katika muziki, Gigy Money amedai msanii Hemedy PhD siyo level zake kwa sababu hana fedha.

Kauli ya Gigy Money inakuja baada ya hapo awali kuripotiwa kupishana kauli kwa wawili hao na Hemedy alipoulizwa na kipindi cha The Playlist cha Times Fm alijibu hawezi kumzungumzia Gigy.

Gigy akipiga stori na Bongo5 amesema kuwa yeye kwanza hamjui Hemedy na hana hadhi ya kuongea na yeye. “Hawezi kuwa na hadhi ya kuniogelea mtu kama mimi kwa sababu hana hela”, amesema.

Hemedy na Gigy wote wanajihusisha na ‘vitu’ viwili katika tasnia ya burudani Bongo, Gigy anafanya muziki na video vixen, Hemedy muziki na uigizaji.

Bongo5

PICHA:Mtoto Apigwa Risasi Begani Kenya Wakati Wa Maandamano Ya Uchaguzi

0
0
Madaktari nchini Kenya wamefanikiwa kutoa risasi begani kwa mtoto iliyompata wakati wa maandamano ya uchaguzi katika Mji wa Kisumu.

Picha ya Chini Ikionyesha Risasi baada ya Kutolewa

Shonza kuanza na Wasanii Wanaovaa Vibaya na Kutumia Maneno Mabaya

0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza imetangaza kuanza kushughulika na wasanii ambao wanavaa vibaya na kutumia maneno mabaya kwenye kazi zao za sanaa.

Juliana Shonza amesema hayo leo alipokuwa anapokelewa ofisini na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harisson Mwakyembe na kusema alipoteuliwa tu aliona kuwa kwenye sanaa hususani wasanii wamekuwa wakivaa vibaya kwenye kazi zao na kutumia maneno yasiyo na maadili kwenye kazi zao hizo na kusema kama serikali lazima wahakikishe wanalifanyia kazi ili kulinda utamaduni wa Tanzania.

"Nilipoteuliwa tu ni jambo ambalo nilianza nalo ni mmomonyoka wa maadili kwa kweli imekuwa ni changamoto kubwa sana nimeshuhudia saizi hata ukiangalia kwenye nyimbo na kazi za sanaa lugha ambayo inatumika inakuwa siyo nzuri, lakini kama haitoshi kuna nyimbo ambazo zinaibwa ukifuatilia ndani unakuta maadili siyo mazuri, lakini hata katika suala la mavazi mimi nalisema wazi nitawaambia wasanii wa kike wajitahidi kuvaa vizuri, kwa sababu hatuwezi kuacha hivi vitu vikawa vinaendelea tu kila taifa na misingi yake na tamaduni zake" alisema Juliana Shonza

Mbali na hilo Naibu Waziri wa Habari amesisitiza kuwa ni jukumu la viongozi kuhakikisha utamaduni wetu unaendelezwa na kusimamia misingi ya taifa.

Serikali imesema Ufugaji Kuku, Samaki ni Uchumi wa Viwanda

0
0
Naibu Waziri wa Mifugo na Kilimo, Abdallah Ulega akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mwandege wakati wa kuhitimisha ziara yake iliyokuwa ya siku mbili.

Ulega aliyasema nayo wakati wa ziara yake  aliyoifanya Wilaya ya Mkuranga-Pwani kwenye vijiji Vinne ,ambapo  alisema hakuna sababu ya wananchi wa Mkuranga kuchukua Kuku mikoa mingine  wakati wanaweza kufuga wenyewe na kujipatia kipato na maendeleo yakapatikana na kuwawezesha kuuza hata sehem nyingine.
Amesema yuko tayari kuwasaidia wananchi wa Mkuranga mbegu za Kuku pamoja na watalaam wa kuwafundisha jinsi ya kufanya ufugaji wa Kuku na samaki wa kisasa.

Amesema ajira katika Wilaya hiyo zipo ikiwa ni pamoja na ufugaji Kuku pamoja na samaki ambayo ni ajira ya kudumu na soko ni kubwa kutokana mahitaji ya vitoweo hivyo kuhitajika kwa wingi.

"Sioni sababu wananchi wa Mkuranga kuchukua kuku kutoka mikoa mingine wakati mnaweza kufanya nyinyi wenyewe kutokana na maeneo mlionayo, haitawezekana kama nyinyi hamtaweza  kuonyesha mfano nikiwa ni Mbunge na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi"alisema Ulega.

Katika ziara yake  alitembelea Ujenzi wa Zahanati za Kibamba, Kimazichana na Mwandege na kuahidi kuwaunga mkono wananchi katika juhudi mbalimbali wanazoonyesha katika maendeleo ya huduma za jamii.

Ulega amesema kuwa wakati uliopo ni kufanya kazi za Maendeleo kwa kuunga mkono jitihada za Rais Dk. John Pombe Magufuli juu ya dhamira ya serikali ya Viwanda.

 Naibu waziri  aliaahidi kuchagiaji  sh. Milioni moja na mifuko ya saruji kwa ajili ya kikundi cha VICCOBA cha wanawake waliojenga ukumbi wa mikutano na sherehe kilichopo Mwandege.

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?
Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

Moto Waendelea Kuwaka CCM

0
0

Wakati Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole akiwataka wakuu wa wilaya nchini kuwa na hekima ya kuridhika na vyeo walivyonavyo moto umeendelea kuwaka ndani ya chama hicho, baadhi ya makada na wachambuzi wa siasa kukosoa pendekezo lake la wagombea kuwa wakazi wa majimbo husika.

Wiki iliyopita, Polepole alisema katika kipindi cha redio Times kuwa wanachama wanaotaka kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM 2020, sasa watalazimika kuwa wakazi wa eneo wanalotaka kuliwakilisha, sharti ambalo linaweza kuwaondoa takriban nusu ya wabunge wa sasa.

Tamko hilo la Polepole lilizua mjadala mzito jambo lililosababisha Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Organaizesheni, Pereira Silima alitoa taarifa kueleza kuwa hakuna mahali popote katika mabadiliko ya katiba yao palipoandikwa kuwa wagombea wa udiwani na ubunge watajadiliwa kwa sifa ya kuishi jimboni.

Ukiacha hilo juzi usiku katika kipindi cha ‘Tuambie’ kinachorushwa na televisheni ya TBC, Polepole alizungumzia suala jingine la kuwa kanuni za uchaguzi haziwakatazi wakuu wa wilaya kuwa wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa wa CCM, wanapaswa kuwa na hekima.

Kauli ya Polepole imekuja wakati tayari kukiwa na wakuu wa wilaya wanne, mkuu wa mkoa na makatibu tawala walioshinda katika chaguzi za chama hicho zilizofanyika hivi karibuni.

Walioshinda ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego ambaye aligombea ujumbe wa mkutano mkuu wa CCM baada ya kupata kura 311.

Mwingine ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Nanyumbu, Salum Palango aliyepata kura 295.

Wakuu wa wilaya walioshinda ni Simon Odunga (Chemba) aliyeshinda kwa kura 432, Christina Mndeme (Dodoma) na Elizabeth Kitundu (Bahi) wote kutoka mkoani Dodoma.

Mkoani Morogoro, walioshinda ni Alhaji Mohamed Utaly (Mvomero) na Seriel Nchembe (Gairo).

Wakuu wengine wa wilaya walioshinda ni Raymond Mushi (Babati) mkoani Manyara, Herman Kapufi (Geita), katibu tarafa wa Makuyuni (Arusha), Paul Kiteleki na mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, Alexander Mnyeti.

“Ukienda kwenye kanuni za uchaguzi za 2017 fungu la 25: Nafasi ya uongozi ni kazi ya muda wote (inazitaja hapo), Mkutano Mkuu wa Taifa haujatajwa, lakini mkuu wa wilaya ni kiongozi wetu wa Serikali pia ni kiongozi wetu wa chama,” alisema Polepole na kuongeza:

Mkuu wa wilaya ni mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ni mjumbe wa halmashauri kuu ya wilaya na ni mjumbe wa mkutano mkuu wa wilaya. Huyu pia ni kamisaa wa Serikali, ‘public officer’ anayefanya kazi zote za chama. Sasa nikasema hekima pale ituongoze, yaani mtu ujiongeze mwenyewe.”

Aliendelea kusema: “Kama wewe una dhamana zote hizi, kwa nini mkutano mkuu tusimwachie mwanachama mwingine asiye na dhama nyingine yeye ashiriki kwenye mkutano wa chama?”

Polepole aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma mkoani Mara na baadaye Ubungo jijini Dar es Salaam alisema kwa sasa kuna wakuu wa wilaya wapatao 166 na kama wote wataomba nafasi hizo, watafurika kwenye nafasi za chama hicho.

“Kama wakuu wa wilaya wote watachukua kwa pamoja wako 166, zamani mkutano mkuu tulikuwa 2400 sasa hivi tumepunguza idadi tumekuwa 1,700, hao ni wanachama walioomba dhamana halafu kati ya hao 166 ni wakuu wa wilaya,” alisema Polepole na kuongeza:

“Upande wa pili ni hekima ya kuwa na kiasi. Wewe una nafasi kadhaa, hizi nafasi nyingine tumwachie mtu mwingine. Hiyo inakuja kutokana na maelekezo yetu kwenye fungu la 22 kwamba; mtu mmoja kofia moja. Ukiwa kiongozi una dhamana tayari basi hii nyingine waachie wengine nao waweke mawazo yao katika kupeleka mbele chama chetu.”

Mbunge wa Nzega Mjini(CCM), Hussein Bashe katika maoni yake alisema dhana ya ukazi imepitwa na wakati pamoja na kuwa inaenda kinyume na Katiba, kanuni na tamaduni za chama hicho.

“Nimeisikia kauli ya katibu wangu nadhani ni kauli ambayo inahitaji mjadala mpana, binafsi naamini chama chetu kina katiba, Kanuni na maadili. Utamaduni huu ndo msingi a chama chetu ambao unatuongoza,” alisema.

Bashe alisema dhana ya aina hiyo ikipewa fursa siku moja itakuja hoja ya kwamba anayetakiwa kugombea uchaguzi ni lazima awe mchaga, ikiwa hoja ya mkazi itakosa uhalali na nguvu kisiasa.

“Fursa aina hii ya mawazo ikipewa uhalali, siku moja hoja ya mkazi ikikosa uhalali na nguvu ipo siku tutatumia ukabila, ikiisha tutasema udini kwa kuwa ukiwa muislamu utayajua sana matatizo ya waislamu,” alisema.

Bashe alisema mbunge anayo majukumu yake nayo ni uwakilishi na kwamba, mbunge kuwa mkazi haiwezi kumfanya azifahamu shida za watu yapo mambo ya msingi ambayo yanatakiwa kutazwa.

“Je Mbunge ametimiza majukumu yake? Ametimiza ahadi zake? Amekuwa muwakilishi mzuri wa wananchi wake? Dhana hii binafsi naiona kama ni dhana ‘aoutdated’ (imepitwa na wakati),” alisema.

Alisema kuwa hoja ya mkazi haimfanyi mtu kuwa mwakilishi mzuri na ifahamike kwamba wabunge wengi wanafanya shughuli mbalimbali ikiwazo zao binafsi zinazosaidia maendeleo ya wananchi wake.

“Mwalimu Nyerere alitengeneza mifumo toka Tanu mpaka CCM ya kumuandaa kiongozi kuanzia Chipukizi, Yuth Legue.Haya ni maeneo ya majaribo na makosa

Alisisitiza kuwa zipo nafasi ambazo kiongozi hatakiwi kutoa kuli yenye Taswira ya kuwagawa watanzania kwa msingi wowote ule hata kama utakuwa na nia njema.

“Tumeona kauli ya Silima, ni kauli sahihi kabisa. Hivi karibuni kumekuwa na matamko controversial ambayo unajiuliza duh hivi Katibu Mkuu yupo wapi? Hata kama tunafanya reform, hii ni njia sahihi? Vitisho vimekuwa vingi sana,”alisema Bashe.

Alieleza kuwa CCM ni wanachama na wanachama

“Leo wana CCM wameanza kuwa wanyonge na hofu ya kukosa ari. Tumeanza kujenga tabaka la watawala na watawaliwa ndani ya chama, ni muhimu sana kila kiongozi aheshimu katiba na kupima kauli zetu,”.


Hans Poppe afunguka haya baada ya kiongozi wa Yanga kuchaguliwa kuiongoza Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara

0
0
Mwenyekiti wa usajili wa klabu ya Simba Zacharia Hans Poppe amesema mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara (TPLB) Clement Sanga atende haki katika uongozi wake bila kujali kuwa yeye ni kiongozi wa Yanga.

“Yeye kuipenda Yanga hatumzuii kwa sababu ni mpenzi wa Yanga na kiongozi kule lakini atende haki asijipendelee”-Hans.

“Sasa hivi tunataka maendeleo ya soka sio mambo ya longolongo. Clement Sanga ni mtu ambae namfahamu nimezungumza nae mara kwa mara kwa mtazamo wake ni mtu ambae anapenda maendeleo nina imani atatekeleza wajibu wake vizuri.”

“Nimshauri tu kama kuna mambo anatakiwa ayasikilize wao kama rufaa basi wafanye ndani ya muda na kusimamia ratiba isibadilishwe mara kwa mara.”

Sanga ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa klabu Yanga amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara akimwangusha Ahmed Yahaya aliyekuwa madarakani awali kabla ya uchaguzi kufanyika.

Kamishna wa Tume ya Uchaguzi Kenya ajiuzulu akiwa Marekani

0
0

Kamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) nchini Kenya, Dk Roselyn Akombe ametangaza kujiuzulu nafasi yake katika tume hiyo.

Dk Akombe ametuma taarifa ya kujiuzulu akiwa mjini New York nchini Marekani  anakoishi ambapo alikuwa akiufanyia kazi Umoja wa Mataifa kabla ya kujiunga na tume ya IEBC.

Katika taarifa yake, Akombe amesema kwamba  uchaguzi wa marudio wa uraisi uliopangwa kufanyika Oktoba 26 mwaka huu haujafikia vigezo vya kuwa uchaguzi huru na wa haki.

Akombe anajiondoa kwenye tume hiyo ya IEBC ikiwa imebaki wiki moja uchaguzi wa urais kurudiwa kutokana na matokeo ya awali kufutwa na mahakama kuu na kuamuru uchaguzi mpya ufanyike.

Agosti Akombe alizuiliwa kwenye uwanja wa ndege wa JKIA akielekea nchini Marekani.

Dk Roselyn Akombe Kwamboka alizaliwa 1976 katika kaunti ya Nyamira , na kusomea katika chuo kikuu cha Nairobi kabla ya kuelekea nchini Marekani kwa masomo zaidi.

Ana shahada ya uzamifu katika masuala ya sayansi na kimataifa mbali na shahada nyengine kama hiyo katika somo hilo kutoka chuo kikuu cha Rutgers .

Hadi uteuzi wake katika tume hiyo alifanya kazi kama katibu katika Umoja wa Mataifa mjini New York, wadhfa ambao anasema ulimwezesha kuwa na uzoefu katika maswala

Uwezo wake mkuu amesema mbele ya kamati ya bunge nchini Kenya, ni kutatua migogoro na kwamba ameishi ng'ambo kwa takriban miaka 15, hatua iliomwezesha kuelewa zaidi mahitaji ya watu wanaoishi ughaibuni wakati wa uchaguzi.

 0       

Diwani wa Chadema Aliyerekodi Madiwani Wakishawishiwa Kujiuzulu Arusha Ajitokeza

0
0

Diwani aliyehusika kuwarekodi viongozi wa Halmashauri ya Meru wanaodaiwa kuwa walikuwa wakiwashawishi kwa ahadi ya fedha na mambo mengine Madiwani wa CHADEMA ili wajiuzulu, amejitokea na kusema kuwa yeye alifanya hivyo kutokana na kuchukia rushwa.

Diwani wa Kata ya Mbuguni, Ahimidiwe Rico aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka katika ofisi za Taaisisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Arusha ambao alihojiwa kwa takribani saa tatu kuhusu tuhuma hizo za rushwa.

Rico aliwaambia waandishi wa habari kuwa alifanya hivyo kutokana na kuchukia rushwa na ni kwa manufaa ya maslahi mapana ya taifa na sio kwamba ni masuala ya kisiasa.

Akizungumzia kuhojiwa na TAKUKURU, Rico alisema kuwa alifika katika ofisi hizo baada ya kupokea wito uliomtaka kufanya hivyo, na alipofika alikutana na maafisa wa TAKUKURU kutoka Makao Makuu Dar es Salaam, ambapo walimhoji na yeye alitoa ushirikiano wote wakati wa mahojiano hayo.

Alisema kuwa alipoulizwa kuhusu vifaa vilivyotumika kurekodi, alisema kuwa ni mali ya Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari ambavyo alivitoa nchini Uingereza alipokuwa akisoma, na kwamba ushahidi huo walishirikiana kuukusanya.

Rico hakuweka wazi na masuala gani aliyoulizwa au aliyowaambia maafisa hao akisema kuwa, jambo hilo lipo chini ya uchunguzi hivyo ni vyema wakaachiwa TAKUKURU wenyewe wafanye kazi yao.

Mbali na Rico, maafisa hao waliwahoji kwa zaidi ya saa sita, madiwani waliojiuzulu Chadema wanaotuhumiwa na Mbunge Nassari kuwa walipewa rushwa na si kweli kwamba walijiuzulu kwa hiar yao kama ambavyo walidai kwa nyakati tofauti.

Wengine waliohojiwa ni  Catherine Mtui, aliyekuwa Diwani wa Viti Maalumu, Japhet Jackson, aliyekuwa Diwani wa Ambuleni na Bryson Isangya, aliyekuwa Diwani wa Maroroni.

Ufafanuzi wa Polisi Kuhusu Utoaji wa Stika za Usalama Barabarani

0
0

Kikosi cha Usalama Barabarani, kimekanusha taarifa inayosambazwa mitandaoni kuhusu ugawaji wa stika za usalama barabarani na kusema hazina ukweli wowote badala yake zipuuzwe.

Hayo yamesemwa na kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Fortunatus Musilimu na kueleza kuwa ukaguzi wa vyombo vyote vya usafiri na usafirishaji umeanza leo Jumanne Oktoba 17, 2017, baada ya uzinduzi wa wiki ya nenda kwa usalama uliofanywa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, jana Jumatatu, katika mji wa Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Kamanda Musilimu amesema kuwa taarifa hizo siyo za kweli na ukaguzi wa magari ni wa lazima na utafanyika nchi nzima.

Taarifa hiyo iliyosambazwa inaeleza kuwa ukaguzi wa magari madogo utalipiwa Sh. 15,000 huku magari makubwa yakilipiwa Sh. 30,000 na stika itauzwa kwa Sh. 8,000.

Musilimu amesema kuwa ukaguzi huo utafanyika kwa awamu kwa kuhusisha magari ya abiria na ya mizigo na utafanyikia katika sehemu husika kama vile, vituo vya mabasi, gereji, vituo vya polisi na maeneo mengine yatakayotangazwa na Mkoa husika.

“Magari ya mizigo na ya abiria ndiyo yataanza kwa muda wa miezi mitatu ya ukaguzi na ubandikaji wa stika. Hapa tunajumuisha daladala, mabasi ya abiria, malori na teksi. Magari mengine madogo yatatangaziwa muda maalumu,” alisema Kamanda.

Kamanda Musilimu amesema kwamba magari yote yanayotembea barabarani ni lazima yawe salama na stika itatolewa tu baada ya Afisa atakayelikagua kuridhishwa na hali ya usalama wake na mhusika atatakiwa kulipo Sh. 5,000 tu.

“Maofisa wetu watakuwepo sehemu maalumu iliyopangwa. Kifungu cha 39 cha Sheria ya Usalama Barabarani Sura ya 168 inasema gari linalotembea ni lazima liwe salama, hivyo stika zote zitatolewa baada ya ukaguzi na kupewa fomu ya polisi namba 93 inayoonyesha chombo chako ni salama,” alisema Kamanda Musilimu.

Kuhusiana na taasisi pamoja na Kampuni binafsi, Kamanda Musilimi amesema zinaweza kuomba kupatiwa huduma ya ukaguzi katika maeneo yao na kwamba baada ya zoezi la ukaguzi kuisha operesheni kubwa itafanyika kubaini magari ambayo hayakukaguliwa kisha kuyakamata.

“Mashirika makubwa wanayo nafasi ya kuomba kukaguliwa mahali walipo nasi tutawafuata. Kipindi hicho kikipita operesheni kubwa ya kukamata vyombo hivyo itafuata,” alisema Kamanda Fortunatus.

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatano

0
0

Kutana na Bi Khadija na Kamgambile ni Watabibu wa Tiba za Asili na Kusafisha Nyota

0
0
KUTANA NA BI KHADIJA NA KAMGAMBILE NIWATIBABABU WATIBA ZA ASILI KUSAFISHA NYOTA PETE YA MALI

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANAO UWEZO MKUBWA WAKUJUWA JAMBOLAKO NA KUKU SAIDIA

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANA TIBU MARADHI KAMA HAYA MIGUU KUUMA NAKUEAKA MOTO

PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIEPOTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE)  KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA LIMBWATA KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM  ANOTOA PETE YA BAHATI ITAKAYO KUKETEA PESA BILA YAMASHARITI

NA KUMILIKI MALI UNAZO TAKA DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KU DHULUMIWA

UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO

DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE KUSAFISHA NYOTA NA KUTOWA MIKOSI KARIBU

CALLING +255719866726/

KWA WHATSAPP IMO +255768455841/

Moto Waacha Wanafunzi Bila Nguo, Bweni Lateketea

0
0

ZAIDI ya wanafunzi 70 wanaosoma katika Shule ya Sekondari ya Nandembo wilayani Tunduru Mkoa wa Ruvuma, wamekosa mahali pa kulala na kuhamishiwa eneo la kanisa, baada ya moto kuteketeza bweni lao.

Wanafunzi hao walinusurika kifo kutokana na kuwa darasani moto huo ulipoanza kuwaka Jumatatu.

Moto huo uliunguza na kuteketeza madaftari, nguo, mashuka na mali nyingine za wanafunzi.

Mashuhuda walisema bweni hilo walilokuwa wakilala wanafunzi wa kiume wa kidato cha kwanza na kidato cha nne lililipuka moto kati ya saa 1:30 na saa 2: 00 usiku.

Mkuu wa shule hiyo, Mary Ndunguru, alisema baada ya kuzuka kwa moto huo, walimu walishirikiana na wanafunzi kuuzima moto huo bila mafanikio.

Alisema wakati wa tukio hilo, wanafunzi walikuwa wakiendelea na masomo ya jioni katika madarasa yaliyopo zaidi ya mita 200, hivyo kuchelewa kubaini kilichokuwa kinaendelea.

Ndunguru alieleza baada ya kuudhibiti moto na kubaini kutokuwapo uwezekano wa wanafunzi kuendelea kulala katika bweni hilo, aliwasiliana na viongozi wa Kanisa Katoliki kijijini hapo na kuomba wanafunzi waende kulala eneo la kanisa kwa muda wakati uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ukiendelea na juhudi za kutafuta ufumbuzi wa kuwajengea bweni lingine.

Kaimu Ofisa Elimu wa Shule za Sekondari wilayani Tunduru, Habiba Mfaume, alisema takwimu zinaonyesha kuwa jumla ya wanafunzi 72 walikuwa wanalala katika bweni hilo na hakuna aliyepata madhara.

Alisema amemuagiza mkuu wa shule hiyo kuwaita wazazi wote katika kikao kilichopangwa kufanyika kesho, ili kuomba msaada wa awali kwao na kila mzazi ajitahidi kufika na nguo zitakazosaidia kuwasitiri watoto wao katika kipindi hicho cha mpito.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Chiza Marando, alisema ili kuwasaidia wanafuzni wanaojiandaa kufanya mitihani ya kuhitimu masomo ya kidato cha nne inayotarajiwa kuanza Oktoba 30 mwaka huu, ameshawatuma wataalamu kupitia masomo yote waliyosoma, ili kuwasaidia kuwatolea nakala wanafunzi wote kuwasaidia waendelee kujisomea.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tunduru ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Kaimu Ofisa Tawala wa wilaya hiyo, Agustino Maneno, alisema amemuagiza Kamanda wa Polisi wa wilaya hiyo kupeleka wataalamu wake kupeleleza chanzo cha moto huo.

Kisa Kinguo Kifupi...Mrembo Prety Kindy Azomewa Mtaani

0
0
MSANII wa filamu Bongo, Suzan Michael maarufu kama Pretykind, juzikati alionja joto la jiwe baada ya kuzomewa na wanafunzi pamoja na watu wengine kufuatia kimini alichokivaa na kukatiza katika mitaa ya Tandale jijini Dar.
Muigizaji huyo alionekana akikatiza barabarani bila woga licha ya kuwa watu walikuwa wakimshangaa na kumcheka na kibaya zaidi wanafunzi wa shule waliokuwa wakikatiza eneo hilo walikuwa wakimzomea.
Lakini katika hali ya kushangaza, Pretykind alipotafutwa na kuulizwa juu ya tukio hilo alisema; “Sioni cha ajabu hapo, maana hayo ndiyo mavazi niliyozoea, nafanya kitu roho inapenda, uzuri nilikuwa na gari nikapaki mara moja kwenda dukani, nilivyoona watu wanaanza kujaa nikakimbilia kwenye gari.”

Stori: Mayasa Mariwata.

Kisa Ndoa Ndugu Wadaiwa Kumsusa Mtangazaji Zamaradi

0
0
BAADA ya kufunga ndoa hivi karibuni na kuibua gumzo kubwa nchini, aliyekuwa mtangazaji wa Clouds TV, nyepesi vimevuja kuwa baadhi ya wanaotajwa kuwa ndugu zake wanadaiwa wamemsusa.

Akizungumza na Za Motomoto News, mmoja wa ndugu wa karibu wa Zamaradi, aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema ndugu wa upande wa baba yake hawako naye vizuri kwani wanadai hawakushirikishwa wala kualikwa katika shughuli hiyo, kitendo ambacho kiliwakasirisha.

Lakini Zamaradi alipoulizwa kuhusiana na hilo alisema; “Hakuna kitu kama hicho, kwani waliokuwa ndugu zangu wote niliwaalika na walihudhuria kwenye ndoa yangu.”

Stori Na Gladness Mallya

Waraka Mzito wa Kushtua Kwa JPM...Babu Seya Aanika Mapya

0
0
HIVI karibuni ulisambazwa waraka mzito na wa kushtua kwenye mitandao ya kijamii uliosemekana umeandikwa na mwanamuziki wa dansi mkongwe nchini, Nguza Viking almaarufu kama Babu Seya anayekitumikia kifungo cha maisha gerezani.
Kufuatia kusambaa kwa waraka huo, Gazeti la Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita liliingia katika Gereza la Ukonga jijini Dar anapokitumikia kifungo chake mwanamuziki huyo na kuzungumza naye ambapo alianika mambo mapya mbali na waraka huo.

WARAKA ULIOSAMBAA
Waraka huo wenye ujumbe mzito uliodaiwa uliandikwa ili umfikie Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli ‘JPM’ ulisomeka hivi:

“MFUNGWA WA MAISHA
Na Babu Seya akiwa gerezani
…NAWAOMBA Mwambieni Rais Magufuli juhudi zake nazisikia.
“Mungu azidi kumpa maarifa zaidi kuliongoza vyema jahazi la Watanzania.
“Rais huyu nimependa hekima zake.. Mimi namfananisha na mwandishi wa makala za kitabu cha methali na Mhubiri Nabii Suleiman.
“Mwambieni rais nimeiweka akiba yangu ya tumaini la mwisho kwake, kwani MUNGU NDIYE MFALME WA KWANZA AWEZAE KUMALIZA MSIBA WANGU HUU WA KUISHI KWENYE KUTA ZA GEREZA.

Wa pili ni yeye RAIS JOHN JOSEPH awezae kunitenganisha mimi na maisha ya gereza.
“Sipendi ndoto yangu ya kuja kufia gerezani…naichukia kama tawala za Herode pale Galilaya. Naumwa huku hakuna makaburi mazuri ya kuzikia wafu wetu.
“ Mwambieni anisaidie japo nije kufia kwenye mikono ya mama yangu tu aliyeteseka leba kwa kumwaga damu yake nyingi wakati wa kunizaa…
“Kama ikishindikana siyo mbaya… U can see my dead body through my window coffin.
“Mtaweza kushuhudia maiti yangu yenye pamba masikioni na puani ikiwa ndani ya jeneza langu kupitia upenyo finyu wa dirisha la jeneza hilo…
“Nimekinai na hukumu na nimeshajifunza mengi. Siku nitakayotoka ndiyo siku nitakayolivaa joho la uchungaji na kupita mitaani nikihubiri neno la Mungu mpaka jasho langu ligeuke damu!
“Natumaini katika mkono wa bwana na natumaini katika mkono wa John Joseph. Halelujah, tutaonana madhabahuni…” ni sehemu ya waraka huo unaodaiwa kuwa ni wa Babu Seya.

UWAZI LATINGA GEREZA LA KEKO
Baada ya kuuona waraka huo Gazeti la Uwazi lilifunga safari hadi Gereza Kuu la Ukonga ililopo Wilaya ya Ilala jijini hapa, ambapo lilikutana na ulinzi mkali na sheria kali za gereza hilo.
Hata hivyo, lilifanikiwa kuonana na Mkuu wa Gereza, ACP Stephen Mwaisabila ambaye alisema:
“Waraka huo haujaandikwa na Babu Seya kwa sababu kuna utaratibu maalumu wa wafungwa kuandika barua kwenda kwa viongozi au sehemu yoyote wanayotaka waraka wao ufike.
“Inashangaza kuona kuna watu wanafanya kitu kama wafungwa, kwa kuandika uzushi mbalimbali kuhusu Babu Seya, kwani kuna wakati walivumisha kuwa Babu Seya kaachiwa, wengine walimuona hospitalini akipita wakavumisha kuwa yuko hoi.”

UTARATIBU WA KUANDIKA BARUA KWA WAFUNGWA
“Mfungwa yeyote ana haki ya msingi ya kuandika barua kwenda anapotaka lakini ni lazima barua yake ipitie kwa Mkuu wa Gereza, Mkuu wa Magereza wa Mkoa (RPO), Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP), kisha inaenda kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, ndipo hupelekwa kwa kiongozi anayemtaka kama ni waziri mkuu au rais.”
Mkuu huyo wa gereza aliwaonya wanaondika uzushi huo kuwa, ni kosa kisheria kuandika mambo ya serikali wakati kuna watu walioaminiwa kwa ajili ya mambo hayo.

UWAZI ANA KWA ANA NA BABU SEYA
Uwazi lilimuona Babu Seya akiwasimamia kama kocha wafungwa wenzake ambao walikuwa wakicheza mpira wa miguu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 18 ya Kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Mwandishi wetu aliomba kumsalimia Babu Seya, aliruhusiwa akaambiwa hairuhusiwi kumpiga picha.

BABU SEYA AFUNGUKA
“Nikushukuru kwa kuja kunisalimia, ujumbe ambao unasema umeenea kwenye mitandao ya kijamii, sijauandika ila nafarijika kuona kuna watu wananipigania.
“Ombi langu ukitoka nje kupitia gazeti lako mwambie Mheshimiwa Rais Dk. John Pombe Magufuli namuomba alipitie upya faili letu.
“Ni kweli mahakama ilitukuta na hatia, hatuna uwezo wa kupinga hukumu iliyotolewa na mahakama lakini ombi langu kwa Rais Magufuli ninamuomba apitie upya faili letu, nasema kwa dhati, mimi sina hatia,”alisema Babu Seya.
Hii ni mara ya pili kwa gazeti hili kuzungumza na Babu Seya akiwa gerezani tangu ahukumiwe kifungo cha maisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu zaidi ya miaka 10 iliyopita.

Gabriel Ng’osha – Dar.
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images