Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Picha za Lissu Zamuumiza Haji Manara Atoa Neno

0
0
Picha za Lissu Lamuumiza Haji Manara Atoa Neno
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Instragram ameweka picha ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ambaye kwa sasa yupo Jijini Nairobi nchini Kenya kwa matibabu nakuandika kuwa anamuombea apone licha ya kutokuwa shabiki wake wala chama chake cha siasa.

Haji Manara ambaye ni mwanachama wa CCM amesema hayo leo baada ya kuona picha ya kwanza ya Mbunge huyo wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa hospitali nchini Kenya ambapo anapatiwa matibabu kufuatia kupigwa risasi Septemba 7 mwaka huu na watu wasiojulikana.

“Ohhh God,,,mm sijawah kukushabikia ww wala chama chako,,ila nakuombea kwa Mungu upone haraka kaka,,urudi ktk harakati zako,,nikiamini bila uwepo wenu chama changu kitalala.”





Majengo ya Serikali Yachomwa Moto na Waandamanaji

0
0

Majengo ya Serikali Yachomwa Moto na Waandamanaji
Majengo kadhaa ya serikali katika mji wa Sokode ambao ni wa pili kwa ukubwa yamechomwa moto na waandamanaji Jumatatu usiku wakipinga kukamatwa kwa imam na mpinzani mkuu.

Hali hiyo imesababisha Serikali za Canada na Marekani kutoa tahadhari kwa raia wao kuhusu hali ya usalama siku moja kabla ya maandamano makubwa ya siku mbili mfululizo yaliyoitishwa na upinzani kuanzia leo.

Marekani ikikariri amri ya serikali ya kupiga marufuku maandamano imetaja ngomo huo kuwa “hauna kibali” hivyo imewataka raia wake kuchukua hatua za kiusalama popote wanapokuwa. Canada pia imetoa onyo kama hilo ikizingatia hali ilivyochafuka Sokode.

Majengo ya polisi, posta na sehemu ya shirika la mawasiliano ni miongoni mwa yaliyolengwa na waandamanaji waliopambana na maofisa usalama, vyombo vya habari vimeripoti.

Imam Alpha Alhassane kiongozi mashuhuri wa kiroho katika mji huo ni mshauri anafahamika wa chama cha upinzani cha Pan-African National Party kinachoongozwa na Tikpi Atchadam.

Sababu za kukamatwa kwake hazijulikani lakini anahusishwa na mfululizo wa maandamano dhidi ya serikali yanayoratibiwa na upinzani. Polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya maandamano ambayo yanaripotiwa kusambaa hadi Lome.

Vyama vya upinzani vimeitisha maandamano ya siku mbili dhidi ya serikali nchi nzima kuanzia Jumatano ya Oktoba 18 hadi Alhamisi ya Oktoba 19.


Hudda Avutiwa Kutoka Kimapenzi na Jux Asema Yupo Single Hata na Mimi Ninapatikana

0
0
Hudda Avutiwa Kutoka Kimapenzi na Jux Asema Yupo Single Hata na Mimi Ninapatikana
Mwanamitindo na Mfanyabiashara kutoka Kenya, Huddah Monroe, amefunguka na kusema kwamba anadhanii Msanii Juma Jux wa Tanzania ni mwanaume ambaye yeye anaweza kuwa naye kimahusiano huku akimmwagia sifa kuwa anamuonekano mzurii kwenye mavazi.

Akifanya mahojiano maalumu na kipindi cha Nirvana kinachorusha kila Jumanne saa tatu usiku chini ya Mtangazaji Deogratius Kithama, Huddah alijibu swali la mtangazaji huyo kama anaweza kuwa kwenye mahusiano na Jux baada ya kumsifia kuwa ana muonekano wa tofauti na wenye kuvutia.
"Aaah, Nafikiri ni mwanaume ambaye naweza kuwa naye kwenye mahusiano...... Yupo 'single? hata mimi nitapatikana....." amesema Huddah
Aidha Huddah amemshauri Jux kufanya kolabo na wasanii wakubwa zaidi wa kimataifa ili azidi kuwa msanii kubwa zaidi ndani na nje ya kimataifa kwani anamuonekano wa kuwa mtu maarufu.
Mbali na hayo Huddah amekiri kwamba alishawahi kumcheki Jux kupitia mtandao na kumwambia jinsi gani anapenda muonekano wake wa mavazi na jinsi ambavyo anavaa tofauti na jinsi jamii zinavyomfikiria.

Vigogo UVCCM Walia na Usugu wa Tatizo la Rushwa

0
0
Vigogo UVCCM Walia na Usugu wa Tatizo la Rushwa
Licha ya sifa nyingi anazomwagiwa Rais John Magufuli katika mapambano ya rushwa na ufisadi, Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) umesema bado lipo tatizo la rushwa nchini.

Kutokana na tatizo hilo, mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya na Songwe, Aman Kajuna amemtaka Rais Magufuli kutumia nguvu kubwa katika mapambano hayo kwa kuwa Taifa linaendelea kutafunwa kila uchwao.

Kajuna, ambaye aliongozana na mwenyekiti mwenzake wa Kagera, Yahaya Katema walikuwa wakizungumza kwa niaba ya wajumbe wa Baraza Kuu la UVCCM na walimsifu Rais kuwa amekuwa kiongozi wa mfano kwa kazi nyingi lakini wakatilia shaka maeneo matatu. Aliyataja maeneo hayo kuwa ni rushwa, kilimo na ukosefu wa maji aliosema bado wananchi wengi vijijini wanalia kukosa maji na kumtaka Rais kutupia macho katika maeneo hayo. “Ni kweli bado tuna changamoto kubwa kwa baadhi ya maeneo; kwanza rushwa bado inatutafuna naomba Rais aongeze nguvu, kilimo nacho kinaonekana kusahaulika lazima tuangalie na pia ilani yetu ilitaja upatikanaji wa maji, kweli bado ni tatizo kubwa,” alisema Kajuna.

Akizungumzia mchujo wa vijana waliojitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika ndani ya umoja huo, alisema mchakato ulikwenda vizuri na kulikuwa na hoja zenye nguvu ambazo zilitolewa majibu bila ya kuwaathiri.

Mwenyekiti wa Kagera, Katema alisema kuna mambo mengi ambayo hayajatekelezwa, lakini akasisitiza kuwa ni mapema kutoa majibu kwa sasa kwa kuwa ilani inatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano.

Katema alimpongeza Rais kuwa anafanya kazi nzuri ambayo CCM ingetamani iwe na mtu wa aina hiyo hivyo ni vyema Watanzania wakawa wavumilivu kwa sasa ili wapatiwe maendeleo.

Pia, mwenyekiti huyo alimpongeza naibu katibu mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka kuwa amekuwa nguzo imara ndani ya umoja huo ikiwamo kujibu hoja za wapinzani kwa wakati na kusababisha utulivu mkubwa.

Umri kigezo muhimu

Shaka akizungumza na waandishi wa habari jana alisema asilimia 98 ya wagombea walijitokeza katika usaili ambao umechukua siku nne.

“Wengine walituma barua na dharura zao kwa nini hawakuja katika zoezi la usaili. Wengine pia wamejitoa, lakini wametuma barua za kujitoa,” alisema.

Kaimu katibu mkuu huyo alisema taarifa ya mchakato huo zitapelekwa kwenye Sekretarieti ya Kamati Kuu kwa ajili ya kuendelea na vikao vingine vya kuwajadili kabla ya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho ndicho kikao cha mwisho kwa nafasi za uwakilishi wa chama.

Katika nafasi ya uenyekiti wa Taifa, wanachama 113 walijitokeza, makamu mwenyekiti 23 na nafasi tano za ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa kupitia vijana wajitokeza 118.

Bila kueleza sababu za kujitoa, Shaka alisema mgombea mmoja wa nafasi ya uenyekiti aliandika barua ya kujitoa katika kinyang’anyiro cha kuomba nafasi hiyo inayoachwa wazi na mbunge wa Donge, Khamis Juma Sadifa.

“Msingi wa umoja wa vijana ndani ya kanuni ni umri, kwa hiyo tulijiridhisha kupitia kwa mamlaka, vyanzo vyetu sisi wenyewe kupitia mamlaka zinazohusika lakini kupitia kwa mhusika mwenyewe na vielelezo vyake,” alisema Shaka.

“Tutakwenda kusimamia haki baada ya kujiridhisha kuwa huyu ndiye mgombea mwenyewe na hivi ndivyo vielelezo vyake. Kwa sababu amepata nafasi ya kusalimia wajumbe (kamati ya utekelezaji) na tukapima capacity (uwezo) yake katika ku-face audience (kukabiliana na hadhara) lakini pia na kujenga hoja, kwa hiyo ni mafanikio kwetu tumeona uwezo wa wanachama wetu walionao,” alisema.

Shaka alisisitiza kuwa wagombea wa nafasi zote za jumuiya hiyo wanatakiwa hadi kumaliza muda wao wa kuongoza iwapo watachaguliwa wawe chini ya miaka 35.

Alisema usaili huo utawaweka katika nafasi nzuri ya kukishauri chama kwa kuwa miongoni mwao wapo watakaofanikiwa na wapo watakaosubiri.   

Picha:Famous Furniture watua Dar, Wakali wa Wagodoro ya Sealy na Masofa ya La-Z-Boy

0
0
Mwandishi wa Habari Akijaribu moja ya Vitanda vinavyouzwa katika Duka hilo


Kampuni ya Famous Furniture imefungua duka lake Mlimani City, Dar es salaam, Tanzania kwa ajili ya wanaopenda kuishi maisha yasiyo na karaha na kwa starehe.


Famous Furniture watakuwa ni wasambazaji rasmi magodoro na vitanda vya Sealy Posturepedic pamoja na sofa na viti vya La-Z-Boy nchini.



Akizungumza na waandishi wa habari jioni ya leo katika ufunguzi wa duka hilo,  ,alisema Sealy ina vitanda na magodoro ya aina mbalimbali yanayokidhi mahitaji ya kiafya na starehe na yanayodumu kwa muda mrefu.

“Sealy ina uzoefu wa utengenezaji wa magodoro na vitanda kwa zaidi ya miaka 100, na kwa sasa ndiyo chapa inayoongoza kwa kutengeneza vitanda na magodoro bora kabisa duniani kote. Vitanda vya Sealy vimetengenezwa na wabobeaji wa afya ya mfupa ili kukupatia starehe, mfumo bora wa egemezi yote haya yakiwa kuhakikisha unapata usingizi mzuri na wenye afya,” alisema Dhaesee.



Mwandishi wa Habari akijaribu moja ya kiti katika Duka Hilo
Aliongeza “Zaidi ya watu miloni 40 duniani wanapata usingizi mzuri na kuamka wenye afya kwa sababu ya kutumia bdhaa za Seay Tunahakksha usiku wako unakuwa wenye pumziko na amani. Usingizi mzuri hupoza mwili, unakupa nguvu, unahakikisha unakua vyema na afya nzuri huku akili yako ikizidi kujenga vizuri. Kumbuka, unatumia theuthi ya maisha yako yote kwenye usingizi. Leo hii, kuna bidhaa mbalimbali za Sealy unazoweza kuchagua lakini lengo letu ni moja; kuhakikisha tunakuwa sababu ya wewe kuwa na maisha yenye starehe,”

Alisema Fenicha za La—Z—Boy zinatengenezwa na kusambazwa kwa leseni katika nchi nyingi duniani.

“La—Z— Boy ina haki miliki za US na kimataifa kwenye miundo zaidi ya 200. Dizaini ya kwanza ilitengenezwa mwaka 1928 na tangia hapo, wamekuwa ni mabalozi ”maisha ya starehe” wanaoongoza duniani,” alisema Dhaesee.

Naye  Ryan Beattie kutoka Bravo Group, msambazaji wa La—Z—Boy kutoka Famous Furniture alisema binadamu hutumia muda mwingi wakiwa wamekaa chini, hii ndio ya sababu ya wabunifu, watafiti na wataalamu wa afya kuumiza vichwa kutoa bidhaa zitakazoleta starehe katika mikao.

Waandishi wakiwa Bize kupata matukio katika uzinduzi wa duka la Famous Furniture

“Unahitaji kukaa kwenye viti bora na vizuri vinavyokujenga kiafya.  Starehe ya mkao sio katika muonekano tu hata aina ya kitu unachokalia kinakupa starehe ya mwili na mfumo bora wa egemezi, hasa kama unakaa kwa muda mrefu,” alisema Beattie.

Kuhusu Famous Furniture Ltd

Famous Furniture Limited (iliyosajiliwa na namba 135127) iliona umuhimu wa kutambulisha bidhaa bora za nyumbani ili kukidhi soko linalokuwa la Tanzania. Bidhaa bora za La-Z-Boy zitaboresha mwonekano wa nyumba yako na starehe yako ya mkao wakati magodoro ya Sealy posturepedic yatahakikisha usingizi wenye afya. Na sasa vyote hivi vinapatikana katika duka namba 47, Mlimani City. Wataalamu wetu wapo tayari kusikia mahitaji yako na kuyafanyia kazi. Famous Furniture inatarajia kufungua maduka mengine matano (5) nchini kote kabla ya mwisho wa mwaka 2018.

Famous Furniture ni kampuni iliyo chini ya Bravo Group Manufacturing (Pty) Ltd yenye viwanda 7 Afrika Kusini na inayoongeza kwa kuwa na bidhaa bora za chumbani na sebuleni.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Alhamisi

0
0

Kutana na Bi Khadija na Kamgambile ni Watabibu wa Tiba za Asili na Kusafisha Nyota

0
0

KUTANA NA BI KHADIJA NA KAMGAMBILE NIWATIBABABU WATIBA ZA ASILI KUSAFISHA NYOTA PETE YA MALI

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANAO UWEZO MKUBWA WAKUJUWA JAMBOLAKO NA KUKU SAIDIA

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANA TIBU MARADHI KAMA HAYA MIGUU KUUMA NAKUEAKA MOTO

PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIEPOTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE)  KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA LIMBWATA KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM  ANOTOA PETE YA BAHATI ITAKAYO KUKETEA PESA BILA YAMASHARITI

NA KUMILIKI MALI UNAZO TAKA DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KU DHULUMIWA

UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO

DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE KUSAFISHA NYOTA NA KUTOWA MIKOSI KARIBU

CALLING +255719866726/

KWA WHATSAPP IMO +255768455841/

Chadema Wamkataa Mkerugenzi wa Halmashauri ya Meru Kusimamia Uchaguzi

0
0
Chadema Wamkataa Mkerugenzi wa Halmashauri ya Meru Kusimamia Uchaguzi
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeweka wazi kwamba hakimuhitaji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru Bw. Christopher Kazeri kuwa msimamizi wa uchaguzi mdogo kwa madai hawana imani naye pia hana sifa kwani anaweza kusababisha umwagikaji wa damu.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeweka wazi kwamba hakimuhitaji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru Bwana Christopher Kazeri kuwa msimamizi wa uchaguzi mdogo kwa madai kwamba hawana imani naye pia hana sifa kwani anaweza kusababisha umwagikaji wa damu.
Akiitoa taarifa hiyo Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini Amani Golugwa amesema kwamba Mkurugenzi huyo alipoteza sifa za kusimamia uchaguzi tangu Juni, 24 walipokuwa kwenye uchaguzi wa vitongoji na vijiji  kwa kufoji matokeo katika vijiji kadhaa na kuwalazimisha wasimamizi wabadilishe namba kwenye fomu.
Golugwa amesema kwamba vitendo ambavyo Mkurugenzi huyo alivifanya anavitafsiri kama mambo ya kihuni kwani yalipelekea kugombanisha watu ambao ni ndugu hivyo hofu yao ni kwamba anaweza kusababisha umwagikaji damu katika uchaguzi mdogo wa marudiano Arumeru Mashariki.
"Tumeishauri Tume iweze kuwasiliana na mamlaka ya uteuzi kwamba hatumtaki ndg Kazeri awe msimamizi wa uchaguzi huu mdogo Arumeru Mashariki, kwanza aliingilia uchaguzi wa vitongoji na vijiji na kulazimisha kubadilishwa matokeo ambayo yalionyesha Chadema wameshinda, jambo ambalo lilileta ugombanishi kwa wagombea, na hata wagombea wa CCM walikataa matokeo kwa kukubali kwamba walishindwa na hata wasimamizi na askari waliokuwepo hapo walithibitisha kwamba Chadema walikuwa wameshindwa" Golugwa
Ameongeza  "Kama uchaguzi wa vitongoji Mkurugenzi ametumia mabavu na kufanya uhuni ambao tumeumbatanisha kwa Tume, kwenye uchaguzi huu wa madiwani si ataleta hata vifaru au kusababisha umwagaji wa damu? Kwa busara na hekima ya kawaida matendo aliyoyafanya Kazeri hayampi sifa ya kuwa msimamizi.
Hata hivyo Golugwa amefafanua na kusema kwamba wamewasilisha ushahidi wa wagombea wa CCM wakikataa kupokea ushindi huo wa vitongoji kwa madai kwamba hawawez kupokea ushindi wa  mtutu wa bunduki.

Kangi Lugola Afunguka Kuhusu Kashfa Yake ya Rushwa

0
0
Kangi Lugola Afunguka Kuhusu Kashfa Yake ya Rushwa
Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Kangi Lugola amesema kashfa ya rushwa iliyokuwa inamkabili kipindi cha serikali ya awamu ya 4, ilikuwa ni zengwe alitengenezewa baada ya kutaka kufichua vitendo vya rushwa.

Kangi Lugola ameyasema hayo leo alipokuwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba wakati yupo kwenye mchakato wa kufichua vitendo viovu vilivyokuwa vikifanywa na serikali, ndipo akatengenezewa zengwe na mtu ili aache kufanya hivyo.
Kangi Lugola ameendelea kusema kwamba inafahamika wakati wa awamu ya nne alikuwa kinara kwenye kuikosoa serikali ya CCM ambayo pia ndio chama chake, na alikuwa wa kwanza kutia saini ya kutokuwa na imani na waziri mkuu wa awamu ile.

Ridhiwani Kikwete: Mungu Utenda Wema Siku Zote Ashukuliwe Yeye kwa Kurejesha Tabasamu Katika na Afya kwa Lissu

0
0
Ridhiwani Kikwete: Mungu Utenda Wema Siku Zote Ashukuliwe Yeye kwa Kurejesha Tabasamu Katika na Afya kwa Lissu
Mbunge mpya wa Jimbo la Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete amefunguka na kusema kuwa amefurahi kumuona Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu akiwa mwenye tabasamu na furaha na kuzidi kumuombea apone kabisa na kurudi kupambana.

Ridhiwani Kikwete amesema hayo kupitia mtandao wake wa Instagram na kusema Mungu siku zote anatenda wema kwa watu kufuata kushambuliwa kwa risasi nyingi Tundu Lissu na hatimaye kuweza kupona na sasa furaha yake kuanza kurejea.
"Mungu utenda wema siku zote. Ashukuliwe yeye kwa kazi ya kurejesha tabasamu katika sura yako na afya kwa wanaokuuguza. Nimefurahi kukuona tena msomi, Kiongozi wangu na mwana kamati mwenzangu wa Bunge ukitabasamu na mwenye Afya njema. Mungu akulinde na akusimamie katika matibabu yako .Looking forward to see you back into your good shape" aliandika Ridhiwani Kikwete

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana mnamo Septemba 7, 2017 akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma na kisha baadaye kusafirishwa na kupelekwa jijini Nairobi Kenya kwa matibabu ambapo mpaka sasa yupo nchini Kenya akiendelea kupatiwa matibabu.

Mkutano wa Wagombea Urais na IEBC Kenya Waahirishwa

0
0
Mkutano wa Wagombea Urais na IEBC Kenya Waahirishwa
Tume ya Uchaguzi Kenya imeahirisha mkutano ambao ulikuwa umepangwa kufanyika leo kati ya mwenyekiti wa tume hiyo na wagombea wa urais.
Mkutano huo ulikuwa umepangiwa kufanyika saa nane unusu adhuhuri lakini tume hiyo imetoa taarifa na kusema umeahirishwa.
Uchaguzi mpya umepangiwa kufanyika Alhamisi wiki ijayo.
Hata hivyo, ingawa Rais Uhuru Kenyatta amesisitiza yuko tayari kwa uchaguzi huo na utaendelea, mgombea wa upinzani Raila Odinga alijiondoa wiki iliyopita.

Jana, Bw Odinga, ambaye ni mgombea wa muungano wa National Super Alliance (Nasa) alitangaza kwamba siku hiyo badala ya kushiriki uchaguzi, wafuasi wake watafanya maandamano makubwa kote nchini.
Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati siku ya Jumatano alikuwa amewalaumu wanasiasa wa kusababisha kuwepo kwa mazingira yanayoifanya vigumu kuandaa uchaguzi huru na wa haki.
Alisema alikuwa anawapa "kadi ya manjano".

Bw Chebukati alikuwa ameahidi kuhudumu kama mpatanishi kati ya wanasiasa hao.
Tume hiyo Jumatano ilipata pigo baada ya mmoja wa makamishna Dkt Roselyn Akombe kutangaza kujiuzulu akiwa Marekani na kusema hana mipango yoyote ya kurejea Kenya hivi karibuni.
Kenyatta kupinga mazungumzo
Rais Kenyatta today alionekana kupinga mkutano Jumatano alipotangaza kwamba hatafanya mazungumzo yoyote na upinzani.
Akihutubu Saboti, Trans Nzoia magharibi mwa nchi hiyo, alisema wale ambao hawataki kushiriki uchaguzi wa 26 Oktoba hawafai kuwazuia watakaotaka kushiriki uchaguzi huo kupiga kura.
"Vile hakuna anayelazimisha mtu kushiriki uchaguzi wa 26 Oktoba, vile vile hakuna aliye na haki ya kuzuia wengine kushiriki," alisema.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi IEBC ilimtangaza Rais Kenyatta kuwa mshindi wa uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti, akiwa mbele ya mpinzani wake Raila Odinga wa muungano wa upinzani Nasa kwa zaidi ya kura 1.4 milioni.

Bw Odinga alipinga matokeo hayo mahakamani na Mahakama Kuu ikaamua ulijaa kasoro nyingi na kuagiza uchaguzi mpya ufanyike katika kipindi cha siku sitini.
Tume ya uchaguzi ilitangaza tarehe mpya ya uchaguzi kuwa 26 Oktoba lakini Bw Odinga alijiondoa wiki iliyopita akisema mageuzi ambayo yalifaa kutekelezwa kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki hayajatekelezwa.

Mahakamani:Shahidi wa Kwanza Seth Bosco Atoa Ushahidi wa Kifo cha Kanumba

0
0
Mahakamani:Shahidi wa Kwanza Seth Bosco Atoa Ushahidi wa Kifo cha Kanumba
Mahakama kuu chini ya Jaji Sam Rumanyika imeanza kuisikiliza shauri la kesi ya jinai namba 125 ya mwaka 2012, Inayomkabili  Msanii Elizabethi Michael ya kumua msanii mwenzie Steven Kanumba bila kukusudia mbapo leo upande wa jamhuri ulikuwa na Mashahidi 2 na shahidi namba moja alikuwa ni Mdogo wake Steven Kanumba Aliyejitabulisha kama Seth Bosco, lakini shahidi wa pili aliomba udhuru wa kutofika leo.

Katika maelezo ya Shahidi Seth Bosco akiongozwa na wakili wa Jamhuri Faraja George ameieleza mahakama kuwa Kanumba ndiye aliye mfungulia mlango Lulu, na alipofika ndani baada ya muda kidogo yeye akiwa chumbani kwake alianza kusikia mvutano wa sauti ya Kanumba ikimwambia Lulu

"kwanini Unaongea na 'Boyfriend' wako mbele yangu?" Mabishano yalianzia kwenye korido, na baada ya kuingia chumbani zilianza kusikika kelele

Baada ya muda mfupi Lulu aliinita na kuniambia Kanumba ameanguka najaribu kumwagia maji naona haamki, nilipoingia chumbani nikweli nilikuta yuko chini akiwa ameegemea ukuta, nikamchukua nikamlaza chali na ndipo nilipoanza kumtafuta Daktari wake anayeitwa Paplas Kageiya, daktari alipofika alimfanyia 'Chek up' akasema ameshafariki, akashauri tumpeleke Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, niliendesha gari mpaka muhimbili, tulipofika muhimbili kwenye kitengo cha dharura walituambia tukatafute utaratibu wa kipolisi, wakati wao wanaandaa vibali vya kuruhusiwa apelekwe mochwari, Baada ya mahojiano ya Polisi katika kituo cha urafiki Ubungo, niliondoka na Askari kurudi nyumbani kwaajili ya uchunguzi, baada ya polisi kufika pale wakiwa chumbani wanaendelea na uchunguzi walikuta Panga chini ya kitanda" Alisema shahidi Seth Bosco

Baada ya ushahidi huo, mahakama imeahirisha shauri hilo hadi kesho Oktoba 20, 2017 kwaajili ya kuendelea kusikiliza mashidi wengine Wanne kutoka upande wa Jamhuri.

Upande wa mstakiwa unaongozwa na Wakili Msomi Peter Kibatala.

Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa kwa siku tatu mfulilizo, ingawa Jaji Rumanyika ameelekeza upande wa mstakiwa na Jamhuri kuona kama wnaweza kutumia hata siku mbili kuisikiliza na siku ya tatu ikatumika kuandika hukumu.

Bi Mugabe Amshtaki Mfanyibiashara kwa Kutomuuzia Pete ya $1.35m

0
0
Bi Mugabe Amshtaki Mfanyibiashara kwa Kutomuuzia Pete ya $1.35m
Mke wa rais nchini Zimbabwe Grace Mugabe amemshtaki mfanyibiashara mmoja kwa kushindwa kumpatia pete ya almasi yenye thamani ya $1.35m kulingana na chmbo cha habari cha Herald.
Jamal Ahmed alidaiwa kumpatia pete yenye thamni ya $30,000 badala ya ile aliyoagiza.
Ni mgogoro wa hivi karibuni kuhusu pete hiyo yenye Carat 100 iliotarajiwa kuwa zawadi ya rais Mugabe kwa mkewe wakati wa maadhimisho ya miaka 20 ndoa yao.
Mwaka uliopita, bwana Ahmed aliwashtaki Bi Grace Mugabe na mwanawe wa ndoa yake ya kwanza mahakamani baada ya kuchukua mali zake katika mgogoro wa pete hiyo.
Alisema katika nakala za mahakamani kwamba bi Mugabe alitaka kurudishiwa fedha zake baada ya pete hiyo ya almasi ilionunuliwa Dubai kukabidhiwa yeye baada ya kusafishwa na mtu mwengine.
Wakati aliposhindwa kulipa fedha hizo kwa akaunti moja huko Dubai, licha ya kusema kuwa fedha hizo zilitumwa kupitia benki moja ya Zimbabwe mke huyo wa rais alichukua kwa lazima nyumba zake.
Bwana Ahmed alisema kuwa alinyanyaswa, kutukanwa na kutishiwa na kuambia hawezi kuchukua hatua yoyote kwa kuwa walioshtakiwa ndio 'Zimbabwe'.
Disemba iliopita jaji mmoja alimuagiza bi Mugabe kurudisha mali hiyo.
Na sasa anamshtaki bwana Ahmed , ambaye ana kibali cha kuishi nchini Zimbabwe na biashara katika taifa hilo kwa $1.23m ili kulipa deni hilo.

Aliyekuwa Katibu Mkuu ACT- Wazalendo Samsoni Mwigamba na Wanachama Wengine 10 Wajiunga na CCM Rasmi Leo

0
0
Aliyekuwa Katibu Mkuu ACT- Wazalendo Samsoni Mwigamba na Wanachama Wengine 10 Wajiunga na CCM Rasmi Leo
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Samsoni Mwigamba na wanachama wengine 10 wametangaza kujiunga na chama cha CCM baada ya kujivua uanachama wa ACT Wazalendo leo.

Taarifa za Mwigamba kujiunga na CCM zimetolewa leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, na kusema kwamba wameamua kufanya hivyo ili kujitenga na upinzani unaokerwa na maendeleo ya nchi, na pia kuunga mkono juhudi za serikali za mapambano dhidi ya rushwa.
“CCM ya sasa ndicho chama kinachotekeleza kwa karibu itikadi, falsafa na sera za ACT Wazalendo ambazo mimi na wenzangu tulishiriki kukiasisi, nchi yetu ndio kinara wa mapambano dhidi ya rushwa sasa hivi, sera ambazo ndio misingi ya ACT Wazalendo, tumeamua kujitenga na upinzani unaokerwa na mafanikio ya nchi ili tuendelee kuwa sehemu ya mapambano katika kurejesha nchi kwenye misingi yake”, amesema Mwigamba.
Samson Mwigamba atakuwa kiongozi wa pili ACT Wazalendo kujivua uanachama wa ACT Wazalendo kwa mwaka huu baada ya Prof. Kitila Mkumbo ambaye naye alifanya hivyo wiki kadhaa zilizopita.

Zitto Kabwe Afunguka Mazito Baada ya Kuona Picha na Kusikia Sauti ya Tundu Lissu

0
0
Zitto Kabwe Afunguka Mazito Baada ya Kuona Picha na Kusikia Sauti ya Tundu Lissu
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Mhe. Zitto Kabwe amefunguka mambo ambayo yanaendelea nchini hivi sasa na kusema serikali ya CCM inahangaika kuhamisha mjadala wa watu ambao wameshambulia Tundu Lissu.

Zitto Kabwe amesema kuwa jana alipoona picha za Tundu Lissu na kusikia sauti yake alifarijika kwani sasa anaamini kuwa kiongozi huyo siku za karibuni ataungana na wao katika kuendelea kupambana kujenga Demokrasia ya nchi.
Aidha Mbunge huyo amedai kuwa kitendo cha madiwani kununuliwa na viongozi wengine wa upinzani ni ajenda ya serikali ya CCM kuhakikisha wanazima mazungumzo juu ya watu ambao walifanya shambulio kwa lengo la kutaka kumuuwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.
"Yote hayo yanayoendelea, CCM inafanya juhudi kubwa kuhamisha mjadala kuhusu waliokushambulia kwa kununua madiwani na wanachama wa vyama vya upinzani kila siku, wakiubana zaidi Uhuru wa habari, na wakiuzima uhuru wa vyama vya siasa, hawataki kabisa mawazo mbadala ya kututoa katika hali tuliyonayo. Utakaporudi naamini utakuta mengine mengi mapya. Ninafuraha kuwa unaendelea vizuri sana tofauti na nilipokuja kukuona. Tutazidi kumwomba Mola afya yako iimarike zaidi. Tuna kazi kubwa sana mbele ya safari, na kwa hakika ni lazima tuifanye kwani tusipoifanya Nchi yetu itaanguka Kiuchumi na Kidemokrasia, na watu wetu kuendelea kuwa masikini zaidi kuliko ilivyo sasa" alisema Zitto Kabwe

Mbali na hilo Zitto Kabwe aliendelea kusema "Kupigwa risasi wewe ilikuwa ni lengo la waliokushambulia kutunyamazisha. Tumewaambia kuwa hatutanyamaza kamwe. Kama ulivyoniambia ukiwa kitandani kuwa "tumeshashinda. Tutashinda". Hakika ushindi ni dhahiri na ndio maana wanatapatapa kuzuia Uhuru wa mawazo na fikra. Lakini Shambulio la kutaka kukuua limetuonyesha watu wanaoumizwa na 'INJUSTICE' na wasioumizwa nayo. Wengi wasioumizwa na 'Injustice' wanadiriki hata kuhoji kwanini eti tunapaza sauti kuhusu suala lako" alisema Zitto Kabwe
Zitto Kabwe ni kati ya Wabunge ambao waliweza kufika jijini Nairobi kwenda kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu wiki kadhaa zilizopita.

Pendeza na Products za Kessy...Kutengeneza Shape, Makalio, Kutoa Mvi na Mengine

0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA


1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/
(21) ENGEZA  MGUU_80,000/

 TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM

(+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO

Chadema Yawataka CCM Kumtumia Lowassa

0
0
Chadema Yawataka CCM Kumtumia Lowassa
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu amefunguka na kusema kwamba wanawaruhusu Chama cha Mapinduzi watumie nafasi ya Lowassa kuwepo Chadema kuwaita wao mafisadi kama jinsi wao walivyofanya kwa miaka mingi.

Salumu amesema kwamba kuwataja watu ambao waliwaita vinara wa ufisadi na leo wapo nao kwenye chama chao ulikuwa ni wajibu wao kama chama cha upinzani kutumia upenyo wa udhaidfu wa chama cha mapinduzi kuonyesha wananchi madhaifu ya serikali.
"Lazima ukubali kwamba ni wajibu wetu kuonyesha madhaifu ya serikali, Kama tulikuwa tunampinga Lowassa kwamba ni fisadi ulikuwa ni wajibu wetu Chadema. Sasa kama leo hii Lowassa yupo kwetu ni wajibu wao CCM kuwaambia watanzania kuwa Chadema kina mafisadi. Kwa sababu Lowassa amekuja Chadema ni yule yule wala hajawa malaika kama jinsi ambavyo kelele zinavyopigwa," Mwalimu amefunguka
Akizungumzia kuhusu chama kupwaya na kumtegemea mtu mmoja kuwa mkosoaji wa serikali iliyopo Madarakani, Mwalimu amesema kupanga ni kuchagua hivyo wao kama Chadema wanauwezo mkubwa wa kukosoa  lakini  huamua kuchagua nani atoe hoja kwa wakati gani na siyo kwamba wameishiwa.

"Hata kwenye timu ya mpira wapo mastaa wengi wanaofanya vizuri lakini huangaliwa ni nani wa kuibeba timu, ndivyo hata Chadema ilivyo, mnaweza kuwa wengi lakini kupanga ni kuchagua, Tundu ni Mwanasheria Mkuu wa chama hivyo chama kinaanda ajenda lakini atachaguliiwa mmoja wa kuifikisha ajenda hiyo huku wengine tukitoa sapoti, inategemea ajenda hiyo pia inatolewa wakati gani, mbona hapa katikati mengine yametokea kwani tumemuinua Lissu kitandani atusaidie kusema. si tulisema wenyewe. ? hivyo hakuna mtu mmoja anayeibeba Chadema bali tunashirikiana pamoja", Mwalimu ameoneza.
Huu ni utaratibu wetu hata kipindi cha kina Mh. Zitto Kabwe pamoja na Dkt. Slaa wote agenda zilikuwa ikitengenezwa na watu ndani ya chama na wanaozipeleka mbele huwa ni wachache siyo kwamba eti chama kimepwaya.
Katika hatua nyingine Mwalimu amesema lengo la chama cha upinzani ni kushika dola na siyo kusikiliza jinsi ambavyo watu wengine wanavyokosoa na kusisitiza kwamba Chama chao kilianzishwa kwa malengo ya kuja kushika dola.

Nyarandu Ajitoa Mhanga Akusudia Kuwasilisha Mswada wa Sharti la Kurejea Katiba Mpya Bungeni

0
0
Nyarandu Ajitoa Mhanga Akusudia Kuwasilisha Mswada wa Sharti la Kurejea Katiba Mpya Bungeni
Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM), Lazaro Nyalandu amesema anakusudia kuwasilisha hoja mswada binafsi kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai utakaoweka sharti la kurejea upya mjadala wa Katiba mpya.

Nyalandu  ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii katika Serikali ya awamu ya nne , ameeleza hayo katika akaunti zake mitandao ya kijamii ya Instagram, Twitter na Facebook huku akisema mswada huo atauwasilisha kwenye kikao kijacho cha Bunge.

Katika akaunti hizo Nyalandu ameandika: “Nakusudia kuwasilisha kwa Spika wa Bunge , Mheshimiwa  Job Ndugai, azma yangu ya kuleta muswada  binafsi wa sheria  katika kikao kijacho cha Bunge  itakayoweka sharti la kurejea upya  mjadala wa Katiba Mpya ya Tanzania, kwa kuzingatia Rasimu ya Katiba ilivyowasilishwa na Tume ya Jaji Warioba,” .

Kujiuzulu kwa Kocha Mayanja Kwawavuruga Simba

0
0
Kujiuzulu kwa Kocha Mayanja Kwawavuruga Simba
Sakata la kocha msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja kutangaza kubwaga manyanga limeibua mshangao huku kaimu rais wa Simba, Salum Abdallah ‘Try again’ akizungumza chemba na kocha huyo Mganda jana mchana bila kuwa na taarifa.

Habari za kocha huyo msaidizi wa Simba kujiuzulu zilianza kusambaa jana asubuhi kwenye mitandao ya kijamii, huku mabosi wa Simba wakiwa hawafahamu chochote.

Gazeti hili lilimtafuta kaimu rais wa Simba, Salim Abdallah kama wamepewa taarifa rasmi na kocha huyo lakini, alionyesha sintofahamu juu ya taarifa hiyo.

Wakati akionyesha kutofahamu, Abdallah alikuwa na Mayanja wakati huo wakizungumza bila kujua kuwa anayezungumza naye ana mpango wa kuachia ngazi.

“Mayanja kujiuzulu? Mbona niko naye hapa, unataka nikupe umsalimie?,” Aliuliza bosi huyo wa Simba na mwandishi alikubali na kaimu rais huyo alimpa Mayanja simu.
Mayanja, licha ya kuwa hadi wakati huo hakuwa amemwambia bosi huyo uamuzi wake, alikiri mbele yake kuwa anadhamiria kubwaga manyanga, jambo lililomshitua Abdallah, ambaye ana kaimu nafasi ya Evans Aveva.

Licha ya kwamba inaelezwa Mayanja ametangaza kujiuzulu kutokana na maneno kuzidi kwenye timu yao, mwenyewe hakuwa tayari kuzungumzia chanzo cha kuachana na timu hiyo.

“Ni kweli kinachozungumza ndicho kipo, lakini siwezi kulisemea hilo mimi, uongozi utatoa tamko,” alisema Mayanja kupitia simu ya rais wa Simba, ambaye naye alisisitiza suala hilo litatolewa ufafanuzi na msemaji wao Haji Manara.

“Sikuwa najua chochote hadi wakati huu licha ya kuwa na Mayanja hapa, lakini ngoja nimsikilize kisha ufafanuzi wote utatolewa na ofisa wetu wa habari, Manara,” alisema Abdallah.

Alipotafutwa Manara baadaye kwa ajili ya kufafanua hilo, alisema taarifa aliyoitoa Mayanja katika ukurasa wake wa Instagram ilijitosheleza na wao kama uongozi utakaa kabla ya kutoa ufafanuzi.

Kama ulivyoona alichoandika katika Instagram, amefikia uamuzi huo yeye, nasi hatuna cha kuongeza hapo kwa sasa ila tutatoa taarifa yetu,” alisema Manara bila kusema siku atakayotoa taarifa hiyo Katika ukurasa huo wa Mayanja, kocha huyo raia wa Uganda aliandika kwa kifupi juu ya kuachia ngazi akitaja sababu binafsi ndizo chanzo cha kuchukua uamuzi huo.

Makocha washangazwa

“Hii kama hadithi, Mayanja kaondoka Simba! daaah! Lakini ndiyo mpira wa kibongo ulivyo,” alisema kocha wa Stand United, Athuman Bilal ‘Bilo’.
Kocha wa Njombe Mji, Mrage Kabange alisema anashangazwa na uamuzi huo kwani Simba haipo katika nafasi mbaya kwenye msimamo kiasi cha kufanya uamuzi mgumu.

“Unajua kama ingekuwa ya mwisho au inaning’inia kwenye msimamo sawa, lakini mmmh! Tuwaachie wenyewe,” alisema Kabange kwa kifupi.
Wakati kocha wa Mtibwa Sugar, Zuber Katwila akisema timu hiyo iachwe kama ilivyo kwani Simba na Yanga katika soka hazitabiriki.

Jackson Mayanja alizaliwa Julai 27, 1969 nchini Uganda, ni fulubeki wa kulia kuwahi kushuhudiwa nchini humo kwa wakati wake.

Mayanja ni maarufu kwa jina la Mia Mia (100%) nchini kwao, ambalo alipewa wakati anacheza El Masri ya Misri 1992.

Jina hili lilitokana na kila alichokuwa akifanya uwanjani alikuwa hakosei, alikuwa na pasi sahihi fupi na ndefu na kuwashawishi Waarabu kumpa jina hilo kama mtu sahihi kwa kila afanyacho uwanjani kinafanikiwa kwa asilimia 100.

Mkuu wa Tume ya Uchaguzi Wafula Chebukati Akutana na Raila Odinga

0
0
Mkuu wa Tume ya Uchaguzi Wafula Chebukati Akutana na Raila Odinga
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya Wafula Chebukati akutana na mgombea urais wa upinzani Raila Odinga.
Bw Chebukati amesema anatarajia kukutana na mgombea wa chama tawala cha Jubilee Uhuru Kenyatta baadaye.

"Mkutano huo utafuatwa na mkutano wa pamoja wa wawili hao," ameandika kwenye Twitter.
Mkutano wa wagombea urais na IEBC Kenya waahirishwa
Gazeti la kibinafsi la Nation limesema wawili hao walikutana kwa takriban dakika 40 katika makao makuu ya tume hiyo Nairobi.
Mwenyekiti huyo alikuwa awali ameitisha mkutano wa wagombea urais wote leo adhuhuri lakini akauahirisha mapema leo asubuhi.

Hata hivyo, ingawa Rais Uhuru Kenyatta amesisitiza yuko tayari kwa uchaguzi huo na utaendelea, mgombea wa upinzani Raila Odinga alijiondoa wiki iliyopita.
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya awalaumu wanasiasa
Jana, Bw Odinga, ambaye ni mgombea wa muungano wa National Super Alliance (Nasa) alitangaza kwamba siku hiyo badala ya kushiriki uchaguzi, wafuasi wake watafanya maandamano makubwa kote nchini.

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati siku ya Jumatano alikuwa amewalaumu wanasiasa wa kusababisha kuwepo kwa mazingira yanayoifanya vigumu kuandaa uchaguzi huru na wa haki.
Alisema alikuwa anawapa "kadi ya manjano".
Waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang'i tayari ametangaza Alhamisi kuwa siku ya mapumziko.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images