Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Hivi Ndivyo Rayvanny Alivyowachana Diamond, Ali Kiba, Ommy Dimpozi na Nay

0
0
Hivi Ndivyo Rayvanny Alivyowachana Diamond, Ali Kiba, Ommy Dimpozi na Nay
Msanii wa Bongo Flava kutoka label ya WCB, Rayvanny ameachia ngoma mpya ‘Tabia’ ambayo amewachana wasanii wengi kuhusu tabia zao.

Ngoma hiyo ambayo Rayvanny amerap, baadhi ya wasanii waliopitiwa na punch line zake ni Diamond, Nay wa Mitego, Ommy Dimpoz, Young Dee, Shilole, Joh Makini Juma Nature na wengineo kibao. Hapa chini ni baadhi lines hizo.

Ila Juma Nature muda mwingi yupo tungi, Alikiba wa Kariakoo yeye ni shisha na Mirungi/

Diamond akiongea kidogo katukana, Love Boy hupenda wasichana/

Ommy Dimpoz kwa vijembe huyo bwana hachoki, dogo mtoboa siri ni Young Killer Msodoki/

Ukikutana na FA kama hakujui haongei, yuko bize na simu kama Bongo Movie Ray/

Nay wa Mitego yeye ni bifu na kuchonga, utasikia yule mtoto bishoo nitamgonga/

Wanao-act kishua Gosby na Young Dee, wasiogopa wajua mengi Kimbunga na Nash Mc/

Shilole, Shishi mitusi kwa mkupuo, sijui stajini ana sweat maana sizioni nguo/

Nikki wa Pili ha-act kiki-crazy, ila kaka yake Joh anamkopi Jay Z/

Twaweza: Asilimia 67 ya Watanzania Wanataka Katiba Mpya

0
0
Wananchi wawili kati ya watatu wanasema Tanzania inahitaji katiba mpya, huku nusu ya wananchi wanasema mchakato wa Katiba uanze upya na tume mpya.

Matokeo haya yametolewa na Twaweza katika utafiti uitwao Zege imelala? Maoni ya wananchi kuhusu kukwama kwa mchakato wa kuunda katiba mpya.

Imesema muhtasari unatokana na takwimu kutoka Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia simu za mikononi. Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze amesema, “Wananchi wanataka katiba mpya. Wengi wao wanataka mchakato uanze upya na tume mpya katika ukurasa mpya. Hata hivyo, wapo wananchi ambao wapo tayari kusonga mbele kwa kutumia rasimu iliyoandaliwa na tume iliyotangulia.”

Amesema leo Alhamisi Oktoba 19,2017 kuwa, cha msingi ni kwamba, wananchi wanaunga mkono kipengele kilichoongeza madaraka ya Bunge katika suala la kuwapitisha mawaziri walioteuliwa, na kinachowapa wananchi haki ya kuwaondoa wabunge wanaozembea kazini.

Eyakuze amesema utafiti umedhihirisha uwajibikaji wa siasa kwenye uhalali wa mchakato wa katiba.

Amesema, “Matokeo yameonyesha dhahiri kwamba wananchi wengi wanatatizwa katika kutofautisha kitendo cha Ukawa kugomea Bunge la Katiba na migomo mingineyo. Ushabiki wa kisiasa huwafanya watu wengi kutozingatia uhalali wa jambo husika.”

Eyakuze amesema, “Hivyo basi; vyovyote tutakavyofufua mchakato wa katiba, ni muhimu kwa wahusika wakuu kuheshimu na kutambua kwamba sheria mama ya nchi ni ya thamani zaidi kuliko tofauti za kisiasa. Tanzania inahitaji mchakato wa katiba utakaozingatia uhalali na ujumuishi wa Watanzania wote.”

Twaweza: Asilimia 67 ya Watanzania Wanataka Katiba Mpya
Taarifa ya Twaweza kwa vyombo vya habari imesema asilimia 67 ya Watanzania wanasema ni muhimu kwa Tanzania kupata Katiba mpya na asilimia 56 wanasema toleo la mwisho la rasimu ya Katiba lipigiwe kura na wananchi.

Hata hivyo, asilimia 48 ya wananchi wanasema kwa maoni yao, Katiba mpya haitapatikana ndani ya miaka mitatu ijayo.
Taarifa hiyo imesema wananchi wanaendelea kuunga mkono kwa nguvu kubwa uundwaji wa Katiba mpya inayotilia mkazo suala la uwajibikaji.

Imesema asilimia 79 wanataka mawaziri wanaoteuliwa wapitishwe na Bunge na asilimia 64 wanataka wawe na uwezo wa kuwaondoa wabunge katikati ya uchaguzi iwapo hawatatekeleza majukumu yao ipasavyo.
Hata hivyo, wananchi wamegawanyika kwenye baadhi ya hatua za uwajibikaji zilizopendekezwa ikiwemo kuzuia viongozi na watumishi wa umma kuwa na akaunti nje ya nchi (asilimia 52 wanaunga mkono), kuwepo kwa ukomo wa ubunge (asilimia 52 wanaunga mkono) na kuweka kanuni za uwazi na uwajibikaji kuwa sehemu ya tunu za Taifa (asilimia 48 wanaunga mkono).

Hivi vyote ni vipengele vya rasimu ya Katiba ambavyo viliondolewa na Bunge Maalumu la Katiba.

Twaweza imesema wananchi pia wanaunga mkono kuondolewa kwa kipengele kinachotaka kuchunguza na kudhibiti Ofisi ya Rais (asilimia 55) na mawaziri kuchaguliwa kutoka nje ya Bunge (asilimia 62).
Matokeo hayo Twaweza imesema yanatokana na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,745 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara (Zanzibar haihusiki kwenye utafiti huu) Juni hadi Julai 2017.
Kuhusu muundo wa Serikali ni moja kati ya vipengele vilivyoibua mjadala mzito wakati wa mchakato wa kuunda Katiba Mpya na hatimaye kuwagawa wananchi. Asilimia 42 ya wananchi wa Tanzania Bara waliunga mkono muundo wa Serikali mbili.

Twaweza imesema muundo wa Serikali moja ulikubalika kwa asilimia 25 tu na muundo wa Serikali tatu uliopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba ulipendwa na asilimia 16 tu.

Kampuni ya Barrick Yakubali Masharti Yote ya Sheria Mpya ya Madini

0
0
Kampuni ya Barrick Yakubali Masharti Yote ya Sheria Mpya ya Madini
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuwa kampuni ya Barrick imekubali masharti yote ya sheria mpya madini mazungumzo yao.

Profesa Kabudi amesema hayo leo Alhamisi wakati akitoa taarifa kwa Rais John Magufuli kuhusu majadiliano kati ya Serikali na kampuni ya Barrick.

“Pia wamekubali Serikali kuwa na asilimia 16 kwenye migodi yote ya Barrick na kwamba kwenye mgawanyo itakuwa ni asilimia 50 kwa 50.

Amesema mbali na hilo pia mapato yote ya kampuni hiyo yatawekwa kwenye akaunti zilizopo hapa nchini na kwamba makao makuu yao yajengwe Mwanza.

Amesema mbali na hilo pia kampuni hiyo imekubali kuwa kila kampuni inayoendesha migodi kuachana na wafanyakazi wa mikataba bali waajiriwe wazawa na wasiwe wanakaa kambini.

“Hii ni kuachana na mtindo wa sasa wa kuwaweka watu wazima kwenye makambi,”amesema Profesa kabudi.

Awali Mwenyekiti Mtendaji wa Barrick, John Thonton amesema makubaliano hayo yataenda kuidhinishwa na Bodi nchini Uingereza ambayo ina hisa asilimia 64.

Amesema wamekubaliana pande hizo mbili watakuwa wanagawana faida asilimia 50 kwa 50 kama alivyosema Profesa Kabudi.

Simba Yamtangaza Kocha Mpya Masoud Djuma Atakayeziba Pengo la Jackson Mayanja

0
0
Simba Yamtangaza Kocha Mpya Masoud Djuma Atakayeziba Pengo la Jackson Mayanja
Klabu ya Simba leo  imemtambulisha aliyekuwa kocha wa Rayon Sport ya Rwanda Masoud Djuma kuchukua nafasi ya Jackson Mayanja ambaye jana ametangaza kuachana na klabu hiyo.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba SC, Haji Manara mchana wa leo amemtangaza Masoud Djuma kuchukua nafasi ya kocha msaidizi katika klabu yao hiyo ya Simba na kuwaomba wanachama wa mashabiki wa Simba kumpa ushirikiano kocha huyo.
"Tunawaomba wanachama na mashabiki wa klabu ya Simba mumpe ushirikiano kocha wetu Masoud Djuma yeye ndiye atakuwa msaidizi wa Kocha Omog kuanzia leo Oktoba 19, 2017 na pia tumeboresha benchi la ufundi kwa kumteua meneja mpya Richard Robert yeye anachukua nafasi ya Dkt Kapinga ambaye alikuwa meneja kwa muda tuliokuwa naye mfupi lakini amerudi kwa mwajiri wake nasi klabu tumeona turidhie" alisema Haji Manara.
Mbali na hilo Manara amekanusha taarifa zinazoendelea kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kocha wao Mkuu Omog ameondoka klabuni hapo kwa sababu hajalipwa mshahara na kusema kuwa wao Simba hawajawahi kuwa na njaa na kusema kuwa kocha mkuu wao anaendelea na mazoezi na kikosi chao hivyo huo unaosambaa ni uzushi.

China Yajipanga Kupambana na Vita ya Rushwa

0
0
China Yajipanga Kupambana na Vita ya Rushwa
Moja ya mikakati ambayo Chama cha Kikomunisti China (CPC) imeipa kipaumbele ni vita dhidi ya rushwa, na katika mkutano wake mkuu unaoendelea jijini hapa, kimetangaza kufuatilia uozo huo katika milango ya watu.

Naibu Katibu wa Tume Kuu ya CPC ya Nidhamu na Ukaguzi, Yang Xiaodu akizungumza na waandishi wa habari amesema chama hicho kitaendelea kupambana na rushwa kwa nguvu zote na hakitamvumilia yeyote atakayebainika kushiriki katika rushwa.

Amesema leo Alhamisi Oktoba 19,2017 kuwa licha ya kufuatilia vitendo vya rushwa katika kona mbalimbali ikiwemo majumbani, wataendelea kuwafuatilia waliokimbilia ng’ambo na kutwaa mali walizochuma isivyo halali.

Kigwangala Atoa Siku Saba kwa Wavamizi wa Pori la Tengeru Loliondo

0
0
Kigwangala Atoa Siku Saba kwa Wavamizi wa Pori la Tengeru Loliondo
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Hamisi Kigwangalla amefunguka na kuwapa siku saba wavamizi ambao wapo kwenye pori tengefu la Loliondo kuondoka mara moja ndani ya siku hizo kwani wasipofanya hivyo baada ya hapo mali zao zitataifishwa na serikali.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla.
Kigwangalla amesema uwepo wa wavamizi hao ambao wana ng'ombe zaidi ya 6,000 na matrekta zaidi ya 200 kutoka nchi ya jirani imekuwa sababu kubwa ya chanzo cha mgogoro wa ardhi baina ya vijiji na hifadhi hiyo.
"Kuna taarifa kwenye eneo lenye mgogoro la Pori Tengefu la Loliondo, kuna ng'ombe zaidi ya 6,000 na trekta zaidi ya 200 toka nchi jirani, yote kinyume cha sheria! Uwepo wao siyo tu unahatarisha uhai wa mfumo wa ikolojia ya Serengeti-Mara, bali pia unapunguza eneo la kuchungia kwa wenyeji wa Loliondo. Hivyo kuleta kiu ya wananchi wa Loliondo kuingia ndani zaidi ya eneo la hifadhi kutafuta malisho na hatma yake kuhatarisha uhai wa Serengeti. Uvamizi huu wa wenzetu kutoka nchi jirani ni moja ya sababu kubwa (zilizojificha) za mgogoro wa ardhi baina ya vijijj na hifadhi kukolea moto" alisema Waziri Kigwangalla
Aidha Waziri huyo amesema wakati wanaendelea kutafuta ufumbuzi wa kudumu wamewataka wavamizi hao kuondoka katika maeneo hayo
"Wakati tukiendelea kutafuta suluhisho la kudumu, tutaondoa makando kando kama haya haraka. Leo tumetoa siku saba kwa wavamizi wote toka nchi jirani waliopo eneo la Loliondo bila kufuata taratibu za kisheria waondoke na mali zao la sivyo tutazitaifisha" alisisitiza Kigwangalla.

Mvua Kubwa Yaua, Yaezua Nyumba

0
0
Mvua Kubwa Yaua, Yaezua Nyumba
MTU mmoja amekufa na nyumba mbili zimeezuliwa mapaa yake na kuanguka kutokana na mvua kubwa iliyonyesha ikiwa ni msimu wa mvua za vuli ambao umeanza mkoani Kigoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Martin Otieno alisema hayo mjini Kigoma na kumtaja aliyekumbwa na mkasa huo ni Jumanne Masudi (54) ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nyarubanda, Tarafa ya Kalinzi Kigoma Vijijini na kwamba alikumbwa na mauti saa 10:30 jioni juzi akiwa nyumbani kwake.

Kamanda Otieno alisema wakati mvua ikinyesha, Masudi alikuwa nyumbani kwake na kwamba mvua hiyo iliyoambatana na upepo, iliezua paa la nyumba aliyokuwemo na kusababisha ukuta kuanguka, ambao ulimuangukia kichwani na kusababisha kifo chake.

Maafa hayo yamekuja siku moja baada ya juzi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk Agnes Kijazi kuzungumzia mwelekeo wa mvua za msimu, akisema kutakuwa na mvua za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mengi yanayopata msimu moja wa mvua kwa mwaka, na kwamba mvua kubwa inatarajiwa Januari mwakani.

"Msimu huu ni mahsusi katika maeneo ya magharibi mwa nchi, Kanda ya kati, nyanda za juu Kusini Magharibi, Kusini mwa nchi, maeneo ya Kusini mwa mkoa wa Morogoro pamoja na Ukanda wa Pwani ya Kusini. Mvua inatarajiwa kuanza wiki ya kwanza ya Novemba na kuisha wiki ya nne ya Aprili, 2018,” alieleza Dk Kijazi.

Katika tukio lingine, Kamanda Otieno alisema dereva wa pikipiki ya abiria maarufu bodaboda, William Nashon (22) ameuawa kwa kuchomwa kisu shingoni na mtu asiyefahamika aliyekuwa abiria wake, aliyemtoa eneo la Ujenzi manispaa ya Kigoma Ujiji na kumpeleka eneo la Burega.

Otieno alisema Nashon alikufa akiwa anakaribia Hospitali ya Mkoa ya Kigoma ya Maweni, akifanya jitihada za kuokoa maisha yake na kwamba alianguka baada ya kupoteza damu nyingi kutokana na jeraha alilolipata na hivyo kufariki dunia. Hata hivyo, licha ya mauaji hayo muuaji hakuchukua kitu chochote kutoka kwa mtu huyo na polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusu kadhia hiyo.

Haji Manara: Njaa Aijamuondoa Jackson Mayanja Simba

0
0
Haji Manara: Njaa Aijamuondoa Jackson Mayanja Simba
Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kwamba taarifa ambazo zinasambazwa mitandaoni kuhusu aliyekuwa Kocha Msaidizi, Jackson Mayanja kuondoka kikosini hapo kwa sababu ya kukosa mshahara siyo za kweli.

Pia alisema tayari magazeti mawili ya michezo yamekanusha habari hizo (siyo Mwanaspoti) kutokana na kuandika habari hiyo isiyo ya kweli.

Alisema anaiomba Serikali kufuatilia mtandaoni watu wanaozusha na na kuichafua klabu hiyo.

Kocha Msaidizi wa Yanga Awaahidi Mashabiki wa Timu Hiyo Kutetea Ubingwa Msimu Huu

0
0
Kocha Msaidizi wa Yanga Awaahidi Mashabiki wa Timu Hiyo Kutetea Ubingwa Msimu Huu
Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa “Fusso” amewatoa hofu mashabiki wa timu hiyo kwa kuwaahadi kutetea ubingwa wao msimu huu.

 Yanga ipo mjini Tabora ikijiandaa na mchezo wake dhidi ya Stand United utakaopigwa Jumapili ijayo mjini Shinyanga.

Juzi timu hiyo ilitoka suluhu na Rhino Rangers katika mchezo wa kujipima nguvu uliopigwa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Fusso alisema awaangalia mchezo moja moja  wa Ligi Kuu kwani wao kila mchezo kwao ni muhimu katika safari yao ya kutetea ubingwa.

“Siwezi kuzungumzia mchezo mmoja wa Stand United na wakati tuna mechi nyingi tu za Ligi Kuu hivyo sisi tumejipanga kushinda mechi zote ili malengo tuliyojipangia yatimie,”alisema Fusso.

Alisema mashabiki wa soka wasipate hofu kwani chama lao lina wachezaji wazuri  wenye kiwango kikubwa ambao wataweza kutetea ubingwa msimu huu.

“Tumejipanga imara tuna wachezaji wazuri na wenye morali hivyo tuko katika mapambano  na mashabiki wetu wasiwe na wasiwasi tutabeba tena Kombe”alisema Kocha huyo Msaidizi.

Yanga ina pointi 12 ikiwa katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu mpaka sasa.

Mess Afumwa Akila Dawa Uwanjani na Kuificha Kwenye Soksi

0
0
Mess Afumwa Akila Dawa Uwanjani na Kuificha Kwenye Soksi
 Lionel Messi ameonekana kitia mdomoni kitu alichokificha katika soksi kabla ya kuweka rekodi mpya katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa.

Nyota huyo wa Barcelona alifunga bao lake la 100 katika mashindano yote ta Uefa akiiongoza klabu yake kushinda 3-1 dhidi ya Olympiakos kwenye Uwanja wa Nou Camp  na alionekana ameficha siri ya mafanikio yake katika soksi.

Katika dakika ya 10, kwenye Uwanja wa Nou Camp, kamera za uwanjani zilimuonyesha Messi akichukua kidoge chake kutoka katika soksi na kukitia mdomoni.

Nyota huyo wa Argentina alitafuta kabla ya kwenda kuandika rekodi yake mpya.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Hispania, Messi alikuwa akitafuta kidonge cha glukozi ili kujiongezea nguvu.

Messi alifunga bao moja na kutegeneze lingine la Lucas Digne huku mchezaji wa Olympiakos, Dimitris Nikolaou akijifunga mwenyewe na kufanya kadi nyekundu aliyopewa Gerard Pique kukosa maana usiku huo.

Kabla ya mapumziko Pique alikuwa ametolewa kwa kadi ya pili ya njano, wakati akijaribu kwenda kushambuliaji.

Sababu, Dalili na Tiba ya Tatizo la Nguvu za Kiume Pamoja na Maumbile Madogo ya Uume..Soma Hapa

0
0
 SABABU, DALILI NA TIBA YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME  PAMOJA NA MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA


       Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA  (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k.
     Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

      BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
     Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7  @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 7  hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=
      BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.


Wasiliana nasi (+255)
           0767447444 na
              0714335378

        UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Kufanya Mapenzi Mara kwa Mara Kunaboresha Afya yako

0
0
Kufanya mapenzi ni mojawapo ya vitu vichache ambavyo watafiti wanasema vinamfanya mtu aburudike huku mwili wake ukifaidika kutokana na tendo hilo.

Utafiti umeonyesha kwamba kufanya tendo la ndoa mara kwa mara kunatibu mafua, kuepusha magonjwa ya moyo, kunazuia kansa na hata kuongeza urefu wa maisha.

Watafiti katika chuo kikuu cha Nottingham University nchini Uingereza wamegundua kwamba wanaume wenye umri zaidi ya miaka 50 wanaofanya tendo la ndoa mara kwa mara wana uwezekano mdogo sana wa kupata kansa ya kibofu.

Watafiti hao walikanusha madai kwamba kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara 20 kwa mwezi kunaongeza uwezekano wa kupata matatizo ya moyo.

Madaktari wamekubaliana kwamba mapenzi ni kama shughuli zingine za kawaida na ni mazoezi bora kwa afya.

"Kwa kulinganisha na mazoezi, kufanya mapenzi ni sawa na kutembea zaidi ya kilomita moja au kupanda na kushuka ngazi za majengo mawili marefu" alisema Dr Graham Jackson wa hospitali ya St Thomas.

Utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Queens University cha Belfast umesema kwamba kufanya mapenzi zaidi ya mara tatu kwa wiki kunapunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo.

Tendo la ndoa pia linasaidia kulinda mifupa. Dr Sarah Brewer alisema: “kiwango cha Testosterone kimeonekana kuongezeka wakati tendo la ndoa na baada ya tendo la ndoa".

Utafiti huo ulibainisha kwamba kwa wanaume na wanawake ili waweze kupata faida za tendo la ndoa inawabidi wafanye tendo hilo mara kwa mara.

"Itumie au ipoteze" ndiyo ushauri uliokuwa ukitolewa kwa wazee na wanasayansi toka nchini Finland.

Pamoja na faida za tendo la ndoa ,tendo hilo pia lina hasara zake kama vile kupata magonjwa ya zinaa iwapo kinga haitatumika.

Mambo yatakayokusaidia Kudumisha Mahusiano ya Mapenzi

0
0
Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.”

Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi.

Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana.

1. Uaminifu
Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako.

Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli mara zote. Ongeeni juu ya mipango na mawazo yenu bila kufichana.

Watambulishe kwa mpenzi wako ndugu ,jamaa na marafiki wakaribu ili kumpa mwenza wako amani.

2. Weka muda kwajili ya Mwenza wako
Mahusiano mazuri kati ya wapenzi yanahitaji muda wa wapenzi hao kukaa pamoja. Wapenzi wasio na muda wa kukaa wana hatari ya kupoteza mvuto wa mahusiano yao na hivyo kuhatarisha uhai wa mapenzi kati yao.

Kama wapenzi wapo mbali mbali basi wanahitaji kuweka muda wa kuongea kila inapowezekana. Tafuta muda wa kutoka pamoja, hata kama mtaenda mgahawani kunywa chai au juisi tu inatosha sana na inawaweka karibu zaidi.

3. Mawasiliano
Mawasiliano ni muhimu sana baina ya wapenzi. Hata kama umebanwa na kazi pata dakika chache za kuongea na mpezi wako na kumtaka hali. Andika hata ujumbe wa maneno au barua pepe. Mwambie mpenzi wako ulipo kila mara inapobidi ili kumjengea imani na wewe na kumpa amani moyoni. Tuma ramani ya mahali ulipo kama unatumia simu ya “Smart” (Tuma location kwenye whatsapp)
Mawasiliano ni ufunguo wa kudumisha upendo.

Wakati kuwasiliana na mpendwa wako, kumbuka kwamba upendo ni muhimu. Ongea toka moyoni na si kwa ajili ya kutimiza wajibu tu, kwani mpezi wako atajua tu kama hakuna mahaba katika mawasiliano yenu hivyo kutoleta faida ile inayotegemewa.

Mawasiliano mengine ni yale ya kuelezana yaliyo moyoni. Mweleze mwenza wako linalokusibu ili kupata ufumbuzi wa pamoja. Wapenzi wanaoongea kwa utulivu siku zote watakuwa pamoja.

4. Zawadi
Tafuta kitu cha kumpa mpenzi wako. Si lazima kiwe na thamani kubwa. Inaweza ikawa pipi au matunda tu. Mnunulie zawadi kila inapowezekana hasa unaposafiri au katika siku yake ya kuzaliwa.

5. Onyesha Upendo Wako
Kila mtu anajinsi yake tofauti ya kuonyesha upendo, lakini vyovyote itavyokuwa ni jambo la muhimu sana kuonyesha hisia zako kwa mpenzi wako. Mara nyingi wapenzi wa muda mrefu wanasahau juu ya hili.

Maneno kama “Nakupenda”au majina ya mahaba kama “Mpenzi” au ”La-azizi” yanachangia sana kuonyesha mapenzi na kumfanya mwenza wako kujisikia vizuri. Maneno haya yanaposemwa kwa hisia halisi na toka moyoni yana mchango mkubwa katika kuboresha mahusiano.

Sababu kuu 7 za Kwanini Kila Mwanaume Anahitaji Mwanamke Sahihi

0
0
Kwangu kipindi ambacho kilinivutia sana ni kipindi cha kampeni za uchaguzi nchini Marekani.

Ni pale Obama akiwa katika kampeni kwenye moja ya majimbo kugombea duru ya pili ya uraisi aliposimamisha hotuba yake na kutambua uwepo wa mkewe Michelle.

Obama alisema, "Mke wangu amekuwa bega kwa bega na mimi tokea niko chuo, kuna kipindi nilishindwa kulipa ada ila yeye ndiye aliyenilipia"

Obama akaenda mbali zaidi na kukiri mbele ya jamii ya kimataifa kwamba asingekuwepo hapo alipo kama sio mke wake Michelle.

Hivyo basi, nashauri kwamba mwanamke ambae mwanaume atakua nae huenda akawa chachu ya mafanikio na baraka kwake au anaweza akamrudisha nyuma kabisa katika mipango yake.

Sababu kuu 7 za kwanini iwe isiwe mwanaume lazima upate mwanamke alie sahihi.

1. Kila mwanamke anao uwezo wa kukuridhisha kimapenzi ila mwanamke sahihi na bora pekee ndiue anaeweza kuku-challenge kiakili na kuwa 'intellectually inspired'.

2. Mwanamke yeyote anaweza kukuteka kihisia, ila yule sahihi pekee ndiye mwenye uwezo wa kukuteka kiroho na ukamtumikia Mungu wako.

3. Mwanamke yeyote anaweza akakushawishi muandike mpango wa harusi (wedding plan), ila mwanamke sahihi peke yake ndie mwenye uwezo wa kukuandikia na kukushauri mpango wa biashara (business plan)

4. Kila mwanamke anaweza akakubusu tena 'French kiss' ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukutamkia maneno yaliyojaa busara na hekima.

5. Kila mwanamke anaweza akakupenda sana tu tena kama una pesa, ila mwanamke aliye bora pekee ndiye anaeweza kusimama na wewe hata kukuinua pale utakapokuwa huna kitu.

6. Mwanamke yeyote anao uwezo wa kukushibisha kwa kukupikia chakula kitamu, ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukulisha chakula cha ubongo.

7. Kila mwanamke anao uwezo wa kukushawishi chumbani ila mwanamke bora pekee ndio mwenye uwezo wa kukushawishi umrudie Mungu wako.

Mwisho ngoja nihitimishe kwa kusema hivi ukisoma vitabu vya kihistoria kuhusu Winstom Churchhill mpaka Abraham Lincoln, na kutoka kwa Nelson Mandela mpaka kwa Martin Luther King Jr lao moja kwamba “No matter how strong a Man is, he is only as strong as the Woman he marries” Kwa tafsiri yangu ya kuunga unga isiyo sahihi sana Wanamaanisha "haijalishi ni kwa kiasi gani mwanaume una nguvu, nguvu zako zina athiriwa kwa kiasi kikubwa na mwanamke utakaemuoa"

Kutana na Bi Khadija na Kamgambile ni Watabibu wa Tiba za Asili na Kusafisha Nyota

0
0
KUTANA NA BI KHADIJA NA KAMGAMBILE NIWATIBABABU WATIBA ZA ASILI KUSAFISHA NYOTA PETE YA MALI

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANAO UWEZO MKUBWA WAKUJUWA JAMBOLAKO NA KUKU SAIDIA

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANA TIBU MARADHI KAMA HAYA MIGUU KUUMA NAKUEAKA MOTO

PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIEPOTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE)  KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA LIMBWATA KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM  ANOTOA PETE YA BAHATI ITAKAYO KUKETEA PESA BILA YAMASHARITI

NA KUMILIKI MALI UNAZO TAKA DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KU DHULUMIWA

UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO

DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE KUSAFISHA NYOTA NA KUTOWA MIKOSI KARIBU

CALLING +255719866726/

KWA WHATSAPP IMO +255768455841/

Zitto Afunguka Makubwa Baadam ya Rais Magufuli Baada Ya Kukamilisha Majadiliano Kati Ya Tanzania Na Barrick

0
0

Ameandika Zitto Kupitia Ukurasa wake wa Facebook:

Mwezi Machi 2017 niliwaambia Watanzania kuwa tumepoteza TZS 1.8 trilioni za kodi ya capital gains kwa maamuzi ya papara ya Rais kuhusu mchanga. Nilitukanwa Sana.
Leo tumeishia kupata TZS 640 bilioni ( 1/3 ya tulichokosa ). Mnashangilia Sana.
Nikiwaita Mazwazwa mnasema nawatukana.
Niliandika Machi 2017

" Amri ya Rais kuhusu 'Mchanga wa Dhahabu' imepotezea nchi Tshs 1.8trn Capital Gains Tax
Jana nilipokuwa natoa mada kuhusu miaka 50 ya Azimio la Arusha niliongelea pia suala la umakini wa viongozi katika kauli zao. Kwamba Kiongozi lazima ujue unatoa kauli gani wakati gani. Niliwaeleza wanachama na wageni wengjne katika mkutano wa ACT Wazalendo kuwa Amri ya kiholela aliyoitoa Rais John Magufuli kuzuia usafirishaji wa Mchanga wa Dhahabu imepelekea nchi yetu kupoteza USD 880m Kama kodi ya ongezeko la Mtaji kutokana na mauzo ya Acacia Mining.

Hivi sasa nchini kwetu kuna sheria ya kutoza 20% ya thamani ya mauzo iwapo kampuni zinauziana hisa. Tozo inayotozwa inaitwa Capital Gains Tax. Kodi hii mpya ilitungwa mwaka 2012 ili kukabili wawekezaji waliokuwa wanauziana makampuni juu Kwa juu bila Tanzania kupata lolote. Tanzania imeshafaidika na kodi hiyo Kwa mauzo mbali mbali ambayo yamekwisha fanyika kwenye sekta mbalimbali.

Wakati Rais anatoa AMRI kuhusu Mchanga wa madini kusafirishwa kwenye nje ya nchi kulikuwa na mazungumzo yanaendelea kati ya Kampuni ya Acacia mining ( yenye Assets zinazozalisha nchini Tanzania tu kwa sasa - Buzwagi, Bulyanhulu na North Mara) na kampuni nyengine ya nchini Canada kuhusu Acacia kununuliwa Kwa USD 4.4bn. Mara baada ya amri hiyo mazungumzo yalivunjika na hivyo mauzo kutofanyika.

Iwapo Rais angechelewa kutoa kauli yake Kwa wiki moja tu mazungumzo yale yangepelekea mkataba wa mauzo kusainiwa na hivyo Serikali ingepata 20% ya thamani ya Mauzo Kama kodi ya Ongezeko la Mtaji ( capital gains tax ). Hivyo kauli ya Rais imesababisha hasara Kwa nchi yenye thamani ya USD 880m sawa sawa na shilingi 1.8 trilioni".
Watanzania amkeni huu usingizi wa pono.

VIDEO:Hakika Kwa Hili Alilofanya Magufuli ni Ushindi Mkubwa Kwa Taifa Letu.....

0
0
Majadiliano kati ya Tanzania na timu ya wawakilishi wa kampuni ya Barrick Gold inayomiliki migodi ya madini hapa nchini yamekamilika na makubaliano kati ya pande hizo yametiwa saini jana tarehe 19 Oktoba, 2017 mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu, Jijini Dar es Salaam.

Timu ya Barrick Gold Corporation ilikuwa imeongozwa na Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni hiyo Prof. John Thornton wakati timu iliyowakilisha Serikali ya Tanzania imeongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi.

Miongozi mwa mambo waliyokubaliana ni kutekeleza mwelekeo mpya wa biashara ya madini ambapo kutakuwa na mgawanyo sawa wa faida (yaani Tanzania kupata asilimia 50 na Barrick Gold Corporation kupata asilimia 50 ya faida) na kuundwa kwa kampuni ya ubia wa usimamizi wa migodi ya madini iliyopo Tanzania ambayo itakuwa na makao makuu yake Mwanza na ofisi ndogo Dar es Salaam nchini Tanzania badala ya nchini Uingereza.

Mengine ni kufunga ofisi za uhasibu na fedha zilizopo Johannesburg Afrika Kusini na kuhamishia Tanzania na kutekeleza masharti yote ya mabadiliko ya sheria mpya ya madini na rasilimali za nchi ya mwaka 2017.

Aidha, Barrick Gold Corporation imekubali kuwepo kwa wawakilishi wa Serikali katika bodi za migodi yake yote hapa nchini, kazi mbalimbali za kwenye migodi kufanywa na kampuni za Kitanzania, Migodi kutoa ajira za kudumu kwa wachimbaji, wachimbaji hao kuishi majumbani kwao badala ya kuishi kwenye makambi ya migodi na mashauri yote ya kesi mbalimbali kufanywa hapa nchini.

Kampuni ya Barrick Gold pia imekubali kutoa Dola za Kimarekani Milioni 300 sawa na takribani Shilingi Bilioni 700 kama malipo ya kuonesha nia njema ya kufidia fedha zilizotokana na upotevu wa mapato kupitia biashara ya kampuni hiyo.

Akizungumza baada ya kutia saini makubaliano hayo Prof. Thornton amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa msimamo wake unaojenga misingi ya biashara ya kuaminiana na uwazi, ambayo ni muhimu na ya namna yake kwa biashara katika karne hii ya 21.

Prof. Thornton amesema Barrick Gold Corporation watazingatia makubaliano haya na wanaamini kuwa yamefungua ukurasa muhimu utakaowezesha kufanya biashara kisasa.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amezipongeza timu zote mbili yaani Tanzania na Barrick Gold Corporation kwa kazi kubwa ziliyofanya kufikia makubaliano hayo na kwa kipekee amempongeza Prof. Thornton kwa nia yake thabiti ya kukubali kufanyika kwa mazungumzo na kukubali mambo yaliyofikiwa.

Mhe. Rais Magufuli amesema makubaliano hayo yataisaidia nchi kuzalishaji ajira zaidi, kupata manufaa mbalimbali yanayostahili ikiwemo fedha za kugharamia huduma za kijamii kwa wananchi na yanajenga msingi imara ambao utaiwezesha Tanzania kunufaika na rasilimali zake za madini.

Mhe. Dkt. Magufuli amemuagiza Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Kabudi kuunda timu zitakazoshughulikia biashara ya madini ya Tanzanite na Almasi pamoja na migodi mingine ya dhahabu haraka iwezekanavyo ili nchi iweze kunufaika ipasavyo.

“Nataka machimbo yote ya dhahabu mchakato kama huu ufanyike, pia nakuagiza Prof. Kabudi biashara ya madini ya Tanzanite na Almasi nako ni lazima kufuate utaratibu huu, asiyetaka aondoke” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Pia Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania kuunga mkono juhudi hizi badala ya baadhi yao kuzibeza kwa kuwa zina manufaa kwa taifa na wananchi wake.

Msikilize  Hapo Chini

Usome Ushahidi Uliotolewa Mahakamani wa Kesi ya Lulu ya Kuua Bila Kukusudia

0
0
Kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili mwigizaji wa filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu, imeendelea leo Oktoba 19 katika Mahakama Kuu ya Dar es Salaam ambapo upande wa mashtaka umeanza kuwasilisha ushahidi katika kesi hiyo.

Kesi hiyo ikiendelea mahakamani, mdogo wa marehemu Kanumba, Seth ambaye alikuwa akiishi na kaka yake na alikuwepo siku ya tukio, alitoa ushahidi kwa namna alivyoweza kushudia tukio zima lililopolekea kifo cha ndugu yake.

Akitoa ushahidi, Seth alisema, “Siku ya tukio marehemu Kanumba alinambia nisitoke nyumbani anataka tutoke wote kuanzia saa sita usiku, akaja Lulu na Kanumba ndiye aliyemfungulia mlango Lulu, alipofika ndani nikasikia akimuuliza Lulu kwanini anaongea na boyfriend wake mbele yake? Katika malumbano yao Kanumba alikuwa akimvuta Lulu arudi ndani na Lulu naye alikuwa anataka kutoka nje, wakati wakiendelea kugombana mlango wa chumba changu sikuufunga.”

Aliendelea kuiambia mahakama kuwa, “Baada ya ugomvi Lulu alikuja chumbani kwangu akilia, akanambia Kanumba kadondoka amejaribu kummwagia maji haamki. Na ilikuwa mara ya kwanza kuona ugomvi kati yao, nilipoingia chumbani nilimkuta Kanumba chini kaegemea ukuta nikamlaza chali nikamtafuta daktari wake, Dk Kageiya, alipofika alimfanyia chek up akanambia ameshafariki ila akashauri tumpeleke Hospitali ya Taifa Muhimbili.”

Baada ya kutolewa kwa ushahidi huo wa upande wa mashtaka, kesi hiyo imeahirishwa hadi kesho Oktoba 20, 2017.

Steven Kanumba ambaye alikuwa mmoja wa waigizaji wakubwa nchini Tanzania na Afrika, alifariki dunia Aprili 7, 2012 akiwa nyumbani kwake, Sinza jijini Dar es Salaam.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta Amfungulia Mashtaka Odinga

0
0
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta Amfungulia Mashtaka Odinga
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amemfungulia mashtaka ya kudharau Mahakama kiongozi wa Muungano wa Upinani Nchini humo, Nasa, Raila Odinga.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation, Rais Kenyatta amefungua mashtaka hayo katika Mahakama ya Juu, ambapo Katibu Mkuu wa chama tawala cha Jubilee, Raphael Tuju, ameushutumu upinzani wa Nasa, kwa kutatiza mafunzo ya maafisa wa uchaguzi kwenye ngome kuu za Odinga magharibi mwa nchi hiyo.
Kesi hiyo ni mfululizo wa hali ya sintofahamu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa marudio wa Urais Oktoba 26.
Upinzani umekuwa ukishinikiza kufanyika kwa mabadiliko ndani ya Tume ya Uchaguzi na Mipaka, hasa ukiwalenga maafisa wa tume hiyo wanaotuhumiwa kuvuruga uchaguzi uliobatilishwa wa Agosti nane mwaka huu.

Tunda Afunguka Kuhusu Kuficha Mimba yake

0
0
Tunda Afunguka Kuhusu Kusicha  Mimba yake
Muuza nyago wa Bongo,Tunda Sebastian ametoa sababu ya kudanganya kuwa hakuwa na ujauzito kwamba kuonesha tumbo la mimba ni kuwapa nafasi watu wabaya. Akizungumza na Star Mix, Tunda alisema kuwa, mara nyingi anawakatalia watu kama ni mjamzito kwa sababu anaona siyo vizuri kumtangazia kila mtu kuhusiana na hali hiyo.
“Nimeamua kuwa tofauti kidogo na watu wengine kwani siyo lazima mtu ajue upo kwenye hali hiyo, ujue watu wengine siyo wema, kwenye macho wanakuchekea kumbe moyoni wanaumia,” alisema Tunda.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images