Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Serikali Yatoa Yafunguka Kuhusu Barrick

$
0
0
Serikali Yatoa Yafunguka  Kuhusu Barrick
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Waziri wa Katiba Na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi imetoa ufafanuzi kuhusu suala la faida na mgao wa asilimia 50/50 na kusema jambo hilo limekuwa halifahamiki vizuri kwa watu wengi.

Profesa Kabudi amesema kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itapata asilimia 16 ambazo zinapatikana bila malipo kwa mujibu wa sheria za madini kama ambavyo zimepitishwa huku Barrick wao wakibaki na asilimi 84.

Hiace Yawaka Moto Yaua Watu Watano

$
0
0
Hiace Yawaka Moto Yaua Watu Watano
Watu watano wamefariki dunia baada ya gari aina ya Toyota Hiace kugongana na lori kisha kuwaka moto.

Ajali hiyo imetokea katika Kijiji cha Kyamyorwa wilayani Muleba mkoani Kagera.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustino Olomi amesema ajali hiyo imetokea leo Ijumaa Oktoba 20, saa 12:00 asubuhi.

Amesema mwendo kasi wa dereva wa gari dogo la abiria ni chanzo cha ajali hiyo.

Ingawa Kamanda Olomi hakuwataja waliokufa, Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Richard Ruyango amesema miongoni mwao ni dereva wa gari dogo, kondakta na abiria watatu.

Amesema watu hao walishindwa kujiokoa kutokana na mlango wa gari kubanwa hivyo kushindwa kufunguka.

Peter Msigwa Aliamsha Dude Akusudia Kupeleka Hoja Bungeni ya Kumuondoa Ndugai

$
0
0
Peter Msigwa Aliamsha Dude Akusudia Kupeleka Hoja Bungeni ya Kumuondoa Ndugai
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kusema kuwa katika Bunge ambalo linatarajiwa kuanza Novemba 7, 2017 anakusudia kupeleka hoja ya kumuondoa Spika wa Bunge, Job Ndugai

Spika wa Bunge Job Ndugai.
Msigwa amesema hayo leo kupitia moja ya mtandao wake wa kijamii na kusema kuwa kwa kuzingatia kanuni ya 137 ya kanuni za kudumu za Bunge atapeleka hoja yake hiyo ya kumuondoa Spika wa Bungue.
"Ninakusudia kupeleka hoja ya kumuondoa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe. Job Ndungai, kwa kuzingatia Kanuni ya 137 ya kanuni za kudumu za bunge ina complement ibara ya 84 (7) (d) ya Katiba" alisema Msigwa

Mbunge Peter Msigwa ni kati ya wabunge ambao wamekuwa wakilalamika kuwa Spika wa Bunge, Job Ndugai amekuwa akiendesha bunge kwa shinikizo na upendeleo na kudai kuwa hastahili kuendelea kuongoza kiti hicho.

“Habari ya kuondoka kwa Mayanja imekuuzwa lakini ameondoka Mwambusi Nchi Yote Kimya"- Haji Manara

$
0
0
“Habari ya kuondoka kwa Mayanja imekuuzwa lakini ameondoka Mwambusi Nchi Yote Kimya"- Haji Manara
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya klabu ya Simba, Haji Manara amesema Simba SC ilimuomba kocha, Jackson Mayanja iwavumilie mpaka itakapomalizana na Irambona Juma .

Manara ameyasema hayo wakati akizungumza na vyombo vya habari alipokuwa akimtambulisha mrithi wa kocha Mayanja na meneja mpya, Richard Robert.

“Hatukupanga mwalimu Mayanja aondoke ila alikuwa na matatizo na familia yake ambayo na alituomba ruksa kwa muda mrefu ila Simba SC tulimuomba  atuvumilie mpaka tutakapo maliza mazungumzo na kocha mwingine.”Amesema Manara.

Manara ameongeza “Bahati nzuri tumempata kocha bora wa mwaka jana wa Rwanda akiwa bingwa wa klabu ya Rayon lakini stori ya kuondoka kwa Mayanja imekuwa habari kubwa.

“Habari ya kuondoka kwa Mayanja imekuuzwa lakini ameondoka M wambusi‘no bady talk, this is Simba’ yani ndo hapo muone ‘brand’ ya Simba ilivyokubwa mtakataa, mtabisha maana alivyoondoka hakuna mtu aliyesema nchi imekaa kimya kaja kocha huyu watu wanazungumzia Masoud Juma ndiyomaana nasema hii ndiyo Super Brand ya nchi.”

Klabu ya Simba imeamua kuachana na kocha wake raia wa Uganda, Jackson Mayanja hapo juzi siku ya Jumatano hali iliyozua minong’ono miongoni mwa wapenzi wa mchezo wa soka nchini kwakuonekana swala hilo kama limekuja ghafla.

Irambona Juma alikuwa alichaguliwa kuwa kocha bora nchini Burundi kupitia klabu ya Rayon Sports hivyo wacha apewe muda na kusubiri hekima na demokrasia za wakati kuweza kutoa matokeo ambayo yamefichwa nyuma ya msare wa saa

Wanawake Wajiapiza Kutofanya Mapenzi Hadi Kenyatta Atakaposimikwa Kuwa Rais

$
0
0
Kenyatta Aonya Wanaotishia Kuvuruga Uchaguzi Kenya
Jubilee wameiga kaulimbiu ya kampeni ya muungano wa Nasa baada ya kikundi cha wanawake kutoa wito wa kujizuia kufanya ngono hadi pale watakapokamilisha kumsimika Uhuru Kenya kuwa rais.

“Hakuna ngono hadi baada ya uchaguzi” ni kauli ya hamasa iliyoanzishwa na mgombea urais kwa tiketi ya Nasa, Raila Odinga kwamba wakati wa vita wanaume huwa hawalali na wake zao. Kauli hiyo ilikuwa maarufu kipindi cha kuelekea uchaguzi wa Agosti 8.

“Agosti 8 inakuja; itakuwa siku ya kihistoria na hakuna mtu atakayeachwa bila kupiga kura. Wanaume watalala nje. Siku itakapofika, hakuna mwanamume kulala na mkewe,” alikuwa akisema.

“Mnapokwenda vitani, ngono ni mkosi,” Odinga alinukuriwa akisema Juni

Safari hii kikundi cha wanawake nchini kimetoa rai ngono ipigwe marufuku kuelekea uchaguzi mkuu wa marudio ambao umeamriwa na Mahakama ya Juu.

Ingawa sintofahamu imetawala uchaguzi huo uliopangwa Oktoba 26, wanawake katika mji wa Nyeri katika mkutano na waandishi wa habari Jumatano walisema hawatashiriki ngono na waume zao hadi Uhuru Kenyatta atakapoapishwa kuwa rais kwa muhula wa pili.

Kiongozi wa kikundi hicho, Rahab Mukami, ambaye ni mwakilishi wa wanawake alisema wanawake wameimarisha kampeni kuhakikisha Kenyatta anashinda.

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imesisitiza kwamba uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa licha ya mgomo ulioitishwa na Odinga wa National Super Alliance (Nasa).

Nasa wametoa wito kwa wafuasi wao kufanya maandamano makubwa siku ya uchaguzi. Mara kadhaa wafuasi wao wamepambana na polisi katika mitaa ambayo muungano huo ni ngome zao.

Kenyatta Aonya Wanaotishia Kuvuruga Uchaguzi Kenya

$
0
0
Kenyatta Aonya Wanaotishia Kuvuruga Uchaguzi Kenya
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amewatahadharisha wanaotishia maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini humo pamoja na maandalizi ya uchaguzi mpya kwamba watakabiliwa vikali.
Aidha, ametoa wito kwa wapiga kura kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi ambao umekumbwa na utata Alhamisi wiki ijayo 26 Oktoba.
Rais huyo amesema maafisa wa usalama wa kutosha wametumwa maeneo mbalimbali kuhakikisha kuna usalama siku hiyo.
"Tunapojiandaa kwa uchaguzi wa urais tareje 26 Oktoba, ni muhimu kudumisha amani, sawa na tulivyofanya (Agosti) na nyakati nyingine awali," amesema.
"Kupiga kura kuwachagua viongozi tunaowataka ni haki ambayo ilipiganiwa na mababu zetu, na lazima tuilinde."
"Sheria itatumika kwa njia sawa bila kujali hadhi yako katika jamii au siasa, hakuna atakayesazwa. Kwa wale wanaofana wakati wa vurugu, siku zenu zinafikia ukingoni, sheria itachukua mkondo wake na mtaadhibiwa ipasavyo."
Kiongozi huyo alikuwa akihutubu wakati wa sherehe ya Siku ya Mashujaa ambayo huadhimishwa kila tarehe 20 Oktoba kuwakumbuka mashujaa waliopigania uhuru pamoja na Wakenya wengine waliotoa mchango wa kipekee kwa taifa baada ya uhuru.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga alijiondoa kutoka kwenye uchaguzi huo wa Alhamisi na amesisitiza kwamba hakutakuwa na uchaguzi siku hiyo.

Badala yake amewahimiza wafuasi wake kuandaa maandamano kote nchini humo.
Kiongozi huyo wa upinzani ameongoza mkutano wa kisiasa eneo la Bondo, magharibi mwa Kenya ambapo amewahimiza Wakenya kuwa na umoja na kudumisha amani.
Bw Odinga amekuwa akishinikiza mageuzi yafanywe katika tume ya uchaguzi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mpya.
Miongoni mwa mabadiliko hayo, alitaka afisa mkuu mtendaji Ezra Chiloba ang'atuke pamoja na maafisa wengine wakuu katika tume hiyo.
Taarifa zinasema Bw Chiloba ameamua kwenda likizo ya wiki tatu kuanzia Jumatatu, jambo ambalo litahakikisha kwamba hatakuwepo wakati wa kufanyika kwa uchaguzi.

CCM Yawateua Madiwani Waliojiuzulu Chadema Kuwania Uchaguzi Mdogo

$
0
0
CCM Yawateua Madiwani Waliojiuzulu Chadema Kuwania Uchaguzi Mdogo
Chama cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Arusha, kimewateua wagombea wanane wa udiwani, watakaoshiriki uchaguzi mdogo, watatu wakiwa ni madiwani ambao walijiuzulu Chadema ili kumuunga mkono Rais John Magufuli, lakini wakadondoshwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Shaban Mdoe amesema leo Ijumaa kuwa madiwani hao watapeperusha bendera ya CCM, katika  uchaguzi huo mdogo.

Uchaguzi unafanyika baada ya waliokuwa madiwani wa kata nane kupitia Chadema kuachia ngazi kwa hiyari yao wakiunga mkono jitihada za Rais Magufuli.

Mdoe amesema miongoni mwa waliopitishwa ni madiwani watatu waliojiuzulu udiwani Chadema na kujiunga na CCM kisha kupokelewa na mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli ambapo alishauri vikao vya kikatiba kuwarejesha katika nafasi zao kama bado wanazo sifa.

Madiwani waliokuwa Chadema na kujiuzulu ambao walishindwa kura za maoni ndani ya CCM na jana kupitishwa ni Japhet Joseph Jackson (Ambureni), Anderson Sikawa (Leguruki) na Solomon Laizer (Ngabobo).

Mdoe amesema katika kikao hicho cha leo makada wengine walioteuliwa kupeperusha bendera ya CCM na majina ya kata zao katika mabano ni pamoja na Francis Mbise (Muriet) iliyopo katika jiji la Arusha, Flora Zelothe (Mussa) iliyoko wilayani Arumeru.

Wengine ni pamoja na Prosper Damuni MeyanI (Moita), iliyoko wilayani Monduli, Samson Laizer (Makiba) na Yona Kaaya (Maroroni) halmashauri ya Meru.
Amesema katika kikao hicho wajumbe wote na kwa kauli moja walikubaliana kuhakikisha ushindi unapatikana kwa chama cha mapinduzi na kuzitwaa kata hizo ambazo zilikua zikishikiliwa na madiwani wanaotokana na Chadema.

Ajibu: Sina Mpango wa Kuwekwa Kwenye Orodha ya Wanaowania Tuzo za Mfungaji Bora

$
0
0
Ajibu: Sina Mpango wa Kuwekwa Kwenye Orodha ya Wanaowania Tuzo za Mfungaji Bora
MSHAMBULIAJI tegemeo wa Yanga, Ibrahim Ajibu ametoa kauli ambayo inaweza kutafsiriwa kuwa ni kama ‘anamzuga’ mpachika mabao wa Simba, Emmanuel Okwi.

Ajibu amedai kuwa yeye hana mpango wa kuwemo katika orodha ya wachezaji wanaowania Tuzo ya Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Bara msimu huu.

Mpachika mabao wa Simba, Emmanuel Okwi.
Kauli hiyo, imetolewa na Ajibu muda mfupi baada ya kuifungia timu yake bao kisha kumpa asisti Mzambia, Obrey Chirwa katika mchezo wa ligi hiyo dhidi ya Kagera Sugar, Jumamosi iliyopita.

Mshambuliaji huyo al­itua kuichezea Yanga kwenye msimu huu wa ligi kuu akitokea Simba kwa dau la shilingi milioni 50 mara baada ya mkataba wake wa miaka mitatu kumalizika.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Ajibu alisema yeye anachokiangalia hivi sasa ni kuifungia timu yake mabao ili wapate pointi tatu kwa ajili ya kutengeneza mazingira ya ubingwa.

Ajibu alisema, pointi tatu ndi­yo muhimu ambazo ameahidi kuendelea kufunga na kutengeneza nafasi za mabao kwa wachezaji wenzake ili wafani­kishe malengo yao kama timu waliyoji­wekea.

Aliongeza kuwa, yeye ataendelea kufunga mabao kama kawaida lakini kama ikitokea mwishoni mwa msimu ligi kuu ikamalizika na yeye akawa mfungaji bora, basi atashukuru kwani haikuwa mipango.

“Niseme kuwa, mimi sifungi mabao ili niwe mfungaji, lakini ninafunga mabao ili niiwezeshe timu yangu ushindi na mwisho wa mechi tuchukue pointi tatu.

“Kwani nimesikia tetesi kuwa ninafunga mabao kwa ajili ya kushindana na mchezaji flani (Okwi), hapana mimi ninafunga kwa ajili ya kuiwezesha timu yangu kutwaa ubingwa wa ligi kuu.
“Mimi bado nina deni kubwa na Yanga ambalo bado sijalilipa kama unavyokumbuka wakati ninasajiliwa kuja Yanga nilitoa ahadi kadhaa ikiwemo hii ya ubingwa wa ligi kuu, hivyo ni lazima niitimize.

“Hivyo, nitaendelea kufunga na kutengen­eza nafasi za kufunga mabao kama kawaida na kama ikaja kutokea mwishoni mwa msimu ninakuwa mfungaji bora, basi nitashukuru Mungu kwani haikuwa mipan­go sana,” alisema Ajibu.

Okwi, anaongoza kwenye ufungaji akiwa amefunga ma­bao 7 akifuatiwa na Mohamed Rashid wa Prisons (4), Habib Haji wa Mbao FC, Shiza Kichuya (Simba), Eliud Ambokile (Mbeya City) na Ajibu wote (3).

Weah Kuchuana Tena na Boakai Novemba 7 Katika Uchaguzi wa Marudio

$
0
0
Weah Kuchuana Tena na Boakai Novemba 7 Katika Uchaguzi wa Marudio
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Alhamisi iliweka rekodi ya kutangaza rasmi matokeo yote ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 10 ikiwa ni siku sita kabla ya tarehe ya mwisho iliyopangwa Oktoba 25.

Ikitangaza matokeo hayo, NEC imethibitisha kwamba mwanasoka nyota wa zamani duniani, George Weah aliyewania urais kupitia chama cha Congress For Democratic Change (CDC) atachuana na Makamu wa rais Joseph Boakai wa chama tawala cha Unity Party (UP)

Katika uchaguzi huo wa marudio uliopangwa Novemba 7, mshindi ataapishwa kuchukua nafasi ya Rais Ellen Johnson Sirleaf anayemaliza muda wake.

Sirleaf alishinda kwa mara ya kwanza urais mwaka 2006 kuwa rais wa kwanza barani Afrika kuchaguliwa kidemokrasia. Alishinda muhula wa pili mwaka 2011 na atakabidhi madaraka kwa rais wa pili tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe vilipomalizika mwaka 2003.

Baada ya kujumlisha matokeo yote kutoka vituo 5390 vya kupigia kura vilivyosambaa nchi nzima hakuna mgombea aliyepata asilimia 50+ ya kura za kumwezesha kuwa rais.

Weah alipata kura 596,037 sawa na asilimia 38.4, Boakai kura 446,716 sawa na asilimia 28.8, Cahles Brumskine wa LP kura 149,495 (9.6%), Prince Johnson wa MDR kura 127,666 (8.2%), Alexander Cummings wa ANC kura 112,067 (7.2%) na Benoni Urey wa ALP kura 24,246 (1.6%)

Wagombea wengine 14 waliambulia chini ya asilimia moja ya kura. Wapigakura 1,641,922 sawa na asilimia 75.2 ya waliojiandikisha walishiriki uchaguzi huo.

Mashabiki Waitia Klabu ya Roma Matatani

$
0
0
Mashabiki Waitia Klabu ya Roma  Matatani
Klabu ya Roma imeshitakiwa na UEFA baada ya baadhi ya mashabiki wake kusikika wakiimba  nyimbo zenye ujumbe wa ubaguzi wa rangi kwa kumwita Nyani mlinzi wa Chelsea Antonio Rudiger.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani aliingia dakika ya 77 kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa siku ya Jumatano ambapo mchezo huo ulimalizika kwa matokeo ya 3-3 kwenye dimba la Stamford Bridge.
Kesi hiyo itasikilizwa na kutolewa maamuzi Novemba 16 mwaka huu na Kamati ya UEFA ya Udhibiti wa Maadili na Nidhamu.

Rudiger, mwenye umri wa miaka 24, amehamia Chelsea kutoka Roma kwenye usajili wa majira ya joto mwaka huu. Kabla ya kuhamia Uingereza kwa gharama ya £ 29m, Rudiger alisema ubaguzi wa rangi katika mechi za mpira wa miguu ni tatizo kubwa nchini Italia.

Pendeza na Kessy Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa

$
0
0
*PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA* 🍇🌾🌳
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATAKS)KUNADAWA AINA TATU (@)JELI KUPAK_100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI NA MAPAJAN_80,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE NA MANYAM YOTE
@) DAW YA MAJINI_100,000/NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME BILA KUVAA SIDIRIA_80,000/
8)KUONGEZA MAZIWA NA SAIZI NZURI_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA (kifaru)_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO YAKAWAIDA NA UZAZ_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_70,000/
13) KUWA MWEUPE  WAKUPENDEZA KWA DAW(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWLINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA JELI PAMOJA NA VIDONGE VYAAIN ZOT _100'000
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_ 120,000 /
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_80,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _80,000/
20)ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/🍍🍉🌾                                                                                    *TUNAPATIKAN DAR E SALAAM*  *NAKWA *MIKOANKOTE* UTAPATA *PIA* *NA NCHI ZOTE PIGA CM*                                         (+255)0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product*
 *Delivery  POPOTE ULIPO,*

VIDEO: Mwanafunzi Achomwa Kisu Shingoni Akigombea Mwanamke

$
0
0
Mwanafunzi wa shule ya sekondari Nzasa amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu shingoni kwa kisa kinachodaiwa kugombea mwanamke.

Mwanafunzi huyo Ashiri Musa ambae alikua anasoma kidato cha nne shule ya sekondari Nzasa alikutwa na tukio hilo jana majira ya usiku ambapo alichoma kisu shingoni na kupekea kuvuja damu nyingi ambazo zilipelekea kifo chake papohapo.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Temeke alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mtuhumiwa wa tukio hilo anashikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi.

                                              TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI

Kutana na The Great Maalim Hussein Aweze Kutatua Matatizo yako Kwa Tiba za Asili, Dua na Nyota..

$
0
0
THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107

Acacia Wasema Hawana Pesa za Kuilipa Tanzania

$
0
0
Kampuni ya uchimbaji madini, Acacia (Acacia Mining) imefunguka na kusema kuwa haina uwezo wa kulipa dollar milioni 300 kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kutatua mgogoro wa kodi.

Akiongea leo Oktoba 20, 2017 kwa njia ya simu na chombo cha habari cha Kimataifa cha Uingereza (Reuters) Afisa wa Fedha wa Acacia, Andrew Wray kampuni hiyo haina uwezo wa kulipa fedha hizo kwa serikali ya Tanzania.

Washirika wakubwa wa Acacia, Barrick Gold siku ya jana Oktoba 19 walikubalina na serikali ya Tanzania kuwa watalipa dollar milioni 300 kwa serikali ya Tanzania pamoja na kugawana mapato yanayotokana na shughuli za uchimbaji wa madini nchini.

Chanzo cha habari tovuti ya Reuters.

Nilitegemea Hili Kutokea- Zitto Kabwe

$
0
0
Baada ya Kampuni ya uchimbaji madini nchini, Accacia kudai kwamba haina pesa za kuilipa serikali ya Tanzania kama ilivyodaiwa jana na kampuni ya Barrick Gold Mining,  Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amefunguka na kusema kwamba Serikali ilikosea kutangaza ushindi mapema.

Mh. Kabwe amesema alitegemea kauli kama hiyo kutoka kwenye Kampuni ya Accacia kwani siyo mara ya kwanza kwa Kampuuni ya Barrick kutoa ahadi kama hiyo (ameiita kishika uchumba) kwani hata 2016 walipobanwa na bunge kuhusu suala la misamaha ya kodi.

Mh. Zitto amesema kwamba tangu jana alishangaa sana kusikia serikali ikisema kwamba "Tumefanikiwa" kwani haikuwa ikizungumza na kampuni ya Accacia bali mmiliki wa kampuni Barrick na kutokana na sheria ya Makampuni Mmiliki kama mmiliki anasimama mwenyewe na kampuni husimama yenyewe.

"Nilitegemea hili kutokea baada ya serikali kutangaza hayo jana. Ni makosa tuliyoyafanya wenyewe. Serikali kutangaza ushindi kwenye mazungumzo waliyofanya na kampuni hiyo yalikuwa ni makosa kwani ni kawaida kwa kampuni ya Barrick kutoa ahadi kama waliyokuwa wameitoa jana na walishafanya hivyo kwa nchi ya Bolivia, na Chille. Serikali inapaswa sasa irudi kukaa mezani na Accacia wenyewe kwa ajili ya mazungumzo".

Kampuni ya uchimbaji madini, Acacia (Acacia Mining) imefunguka na kusema kuwa haina uwezo wa kulipa dola milioni 300 kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kutatua mgogoro wa kodi.

Pendeza na Kessy Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa

$
0
0

*PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA* 🍇🌾🌳
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATAKS)KUNADAWA AINA TATU (@)JELI KUPAK_100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI NA MAPAJAN_80,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE NA MANYAM YOTE
@) DAW YA MAJINI_100,000/NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME BILA KUVAA SIDIRIA_80,000/
8)KUONGEZA MAZIWA NA SAIZI NZURI_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA (kifaru)_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO YAKAWAIDA NA UZAZ_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_70,000/
13) KUWA MWEUPE  WAKUPENDEZA KWA DAW(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWLINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA JELI PAMOJA NA VIDONGE VYAAIN ZOT _100'000
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_ 120,000 /
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_80,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _80,000/
20)ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/🍍🍉🌾                                                                                    *TUNAPATIKAN DAR E SALAAM*  *NAKWA *MIKOANKOTE* UTAPATA *PIA* *NA NCHI ZOTE PIGA CM*                                         (+255)0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product*
 *Delivery  POPOTE ULIPO,*

Serikali Yamwaga Ajira 400 TRA

$
0
0
Benny Mwaipaja, Shinyanga
Serikali inatarajia kuajiri wafanyakazi 400 wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kipindi kifupi kijacho ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika Mamlaka hayo, hatua inayotarajiwa kuongeza ufanisi na makusanyo ya kodi.

Ahadi hiyo imetolewa Mjini Shinyanga na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, wakati akizungumza na viongozi na watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utendaji wa Mamlaka hayo mkoani humo.

Dkt. Kijaji amesema kuwa taratibu zote zimekamilika na wakati wowote nafasi za ajira zitatangazwa na kwamba nafasi hizo zimelenga kuiwezesha TRA kuwafikia watu wengi zaidi na kuongeza wigo wa makusanyo ya kodi.

“Tunatambua changamoto ya uchache wa watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ndio maana tumeamua kuajiri wafanyakazi hao 400 ambao ni wengi kuliko kada nyingine ili tuweze kuimarisha utendajikazi wa Mamlaka na hivyo kuongeza makusanyo ya kodi zinazotakiwa kwa shughuli za maendeleo nchini” alisema Dkt. Kijaji

Alisema kuwa pamoja na uhaba wa watumishi, anaamini kuwa lengo la mwaka huu la kukusanya shilingi trilioni 17 ambazo Mamlaka hayo imepangiwa yatafikiwa na ikiwezekana kuzidi kwa kutumia wafanyakazi waliopo.

Dkt. Kijaji alitoa rai kwa wafanyakazi wa TRA kuwa waadilifu na kwamba atakayebainika kukiuka maadili yake ya kazi atachukuliwa hatua kali za kinidhamu na kisheria.

Awali Meneja wa Mamlaka ya Mapato mkoa wa Shinyanga Bw. Jumbe Samson, alieleza kuwa mkoa wake umepangiwa lengo la kukusanya Shilingi bilioni 18 na kwamba wanauhakika wa kufikia lengo hilo kutokana na mikakati mbalimbali waliyojipangia ikiwemo kusimamia ukusanyaji kodi kikamilifu katika sekta ya madini.

Kwa upande wake, Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA Bw. Beatus Nchota alisema kuwa Mamlaka yake imejiwekea mipango ya kufungua ofisi zake kila wilaya hapa nchini ili kusogeza huduma karibu na wananchi na kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali ili lengo walilopewa la kukusanya shilingi trilioni 17 liweze kufikiwa.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Bi. Josephine Matiro, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, alisema kuwa Serikali mkoani humo itahakikisha kuwa TRA inatimiza malengo yake ya kukusanya kodi na kumhakikishia Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji kwamba watasimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Serikali Yalifunga Shirika Kwa Tuhuma za Kuchochea Ushoga na Ndoa za Jinsia Moja

$
0
0
Serikali yasimamisha shughuli za Shirika la CHESA kwa tuhuma za kuchochea vitendo vya ndoa za jinsia moja.

Zitto Kabwe Aitupia Lawama Serikali Baada ya Acacia Kusema Hawana hizo Dola Milioni 300 za Kuilipa Tanzania

$
0
0
Baada ya Kampuni ya uchimbaji madini nchini, Accacia kudai kwamba haina pesa za kuilipa serikali ya Tanzania kama ilivyodaiwa juzi  na kampuni ya Barrick Gold Mining,  Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amefunguka na kusema kwamba Serikali ilikosea kutangaza ushindi mapema.

Akifanya mahojiano maalalumu jana mchana, Mh. Kabwe alisema kwamba alitegemea kauli kama hiyo kutoka kwenye Kampuni ya Accacia kwani siyo mara ya kwanza kwa Kampuuni ya Barrick kutoa ahadi kama hiyo (ameiita kishika uchumba) kwani hata 2016 walipobanwa na bunge kuhusu suala la misamaha ya kodi waliahidi hivyo.

Mh. Zitto amesema kwamba tangu juzi  alishangaa sana kusikia serikali ikisema kwamba "Tumefanikiwa" kwani haikuwa ikizungumza na kampuni ya Accacia bali mmiliki wa kampuni Barrick na kutokana na sheria ya Makampuni Mmiliki kama mmiliki anasimama mwenyewe na kampuni husimama yenyewe.

"Nilitegemea hili kutokea baada ya serikali kutangaza hayo jana. Ni makosa tuliyoyafanya wenyewe. Serikali kutangaza ushindi kwenye mazungumzo waliyofanya na kampuni hiyo yalikuwa ni makosa kwani ni kawaida kwa kampuni ya Barrick kutoa ahadi kama waliyokuwa wameitoa jana na walishafanya hivyo kwa nchi ya Bolivia, na Chille. Serikali inapaswa sasa irudi kukaa mezani na Accacia wenyewe kwa ajili ya mazungumzo".

Kampuni ya uchimbaji madini, Acacia (Acacia Mining) imefunguka na kusema kuwa haina uwezo wa kulipa dola milioni 300 kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kutatua mgogoro wa kodi.

Kutana na Bi Khadija na Kamgambile ni Watabibu wa Tiba za Asili na Kusafisha Nyota

$
0
0
KUTANA NA BI KHADIJA NA KAMGAMBILE NIWATIBABABU WATIBA ZA ASILI KUSAFISHA NYOTA PETE YA MALI

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANAO UWEZO MKUBWA WAKUJUWA JAMBOLAKO NA KUKU SAIDIA

BI KHADIJA NA KAMGAMBILE WANA TIBU MARADHI KAMA HAYA MIGUU KUUMA NAKUEAKA MOTO

PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIEPOTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE)  KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA LIMBWATA KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM  ANOTOA PETE YA BAHATI ITAKAYO KUKETEA PESA BILA YAMASHARITI

NA KUMILIKI MALI UNAZO TAKA DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KU DHULUMIWA

UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO

DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE KUSAFISHA NYOTA NA KUTOWA MIKOSI KARIBU

CALLING +255719866726/

KWA WHATSAPP IMO +255768455841/
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images