Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live

Salamu Lugha ya Kiarabu Kwenye Facebook Zazua Hofu Israela

0
0
Salamu  Lugha ya Kiarabu Kwenye Facebook Zazua Hofu Israela
Polisi wa Israel walimkamata mwanamume mpalestina wiki iliyopiwa, baada ya kuchapisha salamu kwenye mtandao wa Facebook akisema "habari za asubuhi" kwa lugha ya kiarabu, lakini salamu hizo zikatafsiriwa visivyo kumaanisha "washambulie" kwa lugha ya kiyahudi.
Polisi walithibitisha kuwa mfanyakazi huyo alikamatwa kwa muda mfupi kwa kushukiwa kuchochea lakini akaachiliwa kabla ya makosa hayo kutambuliwa.
Chapisho hilo lilionyesha picha ya mfanyakazi huyo akisimama kando ya tinga tinga katika ukingo wa magharibi.

Marekani yajiondoa Unesco ikilalamikia ubaguzi dhidi ya Israel
Magari kama hayo yametumiwa kuwashgambulia waisraeli awli.
Hakuna afisa anayezungumza lugha ya kiarabu aliombwa ushauri kabla ya mtu huyo kukamatwa

Ukawa Watoa Neno Magari ya Makonda

0
0
Ukawa Watoa Neno Magari ya Makonda
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF) upande wa Maalim Seif Shariff Hamad, Julius Mtatiro ametaka magari ya polisi ambayo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, alikabidhiwa jana yatumike kutimiza haki badala ya kukandamiza.

Akizungumza na Nipashe baada ya Makonda kukabidhiwa magari 16 yaliyokarabatiwa na kufanana na ya vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa (UN), Mtatiro ambaye pia ni mchambuzi wa masuala ya kijamii alisema:

“Kukabidhiwa magari Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ni jambo moja lakini namna ya kuyatumia ni jambo jingine.”

Mtatiro ambaye chama chake ni moja ya vinavyounda mwavuli wa kisiasa wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema magari hayo yatapaswa kutumika kukabiliana na uhalifu badala ya kudhibiti harakati za kisiasa, kwa mfano.

Mbali na CUF, vyama vingine vinavyounda Ukawa ni Chadema, NSSR Mageuzi na NLD ambavyo kwa pamoja viligawana majimbo na kuweka mgombea mmoja wa urais, Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, katika uchaguzi mkuu wa 2015.

Uongozi wa Mtatiro, ambaye ni wa kambi ya Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, upo katika mvutano mkali na Mwenyekiti Prof. Ibrahim Lipumba, anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, hata hivyo.

Aidha, Mtatiro alisema vyombo vya usalama nchini bado vina uhitaji mkubwa wa vifaa na vitendea kazi, hivyo hafla ya jana ni jambo jema.

Alitaka upatikanaji wa vitendea kazi kuwa mkakati wa nchi, badala ya mkoa.

Makonda, kwa jithada zake binafsi katika kuboresha mazingira ya kazi ya polisi wa mkoa wake aliomba kukarabatiwa na kubadilishwa mwonekano wa magari 58 chakavu ya polisi kwa karakana moja binafsi iliyopo Moshi, mkoani Kilimanjaro, mwaka jana.

"Ninachoamini pia ni kwamba kuna tatizo kubwa la upungufu wa vitendea kazi vya ulinzi nchi nzima, hivyo ni vema ukawekwa mkakati maalum na Waziri wa Mambo ya Ndani, kuhakikisha vitendea kazi vya kutosha vinapatikana hasa katika eneo la upelelezi, isiishie tu kwenye magari," alisema Mtatiro.

Makonda alikabidhiwa magari hayo katika hafla iliyofanyika Moshi, kwa mujibu wa taarifa za mitandao ya kijamii zilizopatikana jijini.

Hafla ya kukabidhi magari hayo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira.
Magari hayo yatakuwa na uwezo wa kubeba askari tisa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Makonda alisema kupatikana kwa magari hayo kutasaidia kupunguza vitendo vya uhalifu kwa wakazi wa Dar es Salaam kwa kuwa yana uwezo wa kuwasaidia askari kukabiliana na wahalifu.

Alisema magari hayo yatatumika kufanyia doria saa 24 katika mkoa wake kwa ajili ya kuhakikisha polisi wanapambana na vitendo vya uhalifu.

Familia ya Lissu Yatoa Msimamo Wake Matibabu ya Lissu

0
0
Familia ya Lissu Yatoa Msimamo Wake Matibabu ya Lissu
Familia ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu imesema ataendelea kupata matibabu kwenye Hospitali ya Nairobi, Kenya wakati taratibu za kumhamisha zikiendelea.

Aidha, familia hiyo imesema itaweka wazi kwa umma siku itakapomhamishia hospitali nyingine mtaalamu huyo wa sheria.

Akizungumza na Nipashe kwa simu jana, kaka wa Lissu, Vicent Lissu, alisema mbunge huyo atahamishwa kutoka katika hospitali hiyo kwenda kupata matibabu ya kibingwa zaidi kama ilivyoelezwa Jumanne iliyopita na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.

"Mheshimiwa Lissu bado anaendelea na matibabu kwenye hospitali ileile," Vicent alisema, "akihamishwa mtajua maana tutaeleza ila kwa sasa bado ni mapema kusema atakwenda nchi gani, itoshe kujua bado yupo Nairobi."

Alipoulizwa kuhusu gharama za matibabu ya mbunge huyo na kama kuna deni lolote katika Hospitali ya Nairobi, Vicent alisema:
"Hilo ni suala binafsi sana na sidhani kama ni wakati wake kulizungumzia, jueni anaendelea na matibabu.

"Mengine ni masuala ya kifamilia sana."

Hadi jana jioni, dola za Marekani 31,663 (Sh. milioni 69.9) zilikuwa zimechangwa na watu walio ughaibuni kugharamia matibabu ya Lissu, ikiwa ni ongezeko la dola 1,969 (Sh. milioni 4.36) kutoka zilizokuwa zimechangwa wakati Mbowe akizungumza na waandishi wa habari kwa mara ya mwisho jijini Dar es Salaam kuhusu hali ya Lissu.

Kwa mujibu wa mtandao wa www.gofundme.com/Lissumedicalcare, tangu utaratibu huo wa watu walio ughaibuni kumchangia Lissu uanzishwe Septemba 12 na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Vincent Mashinji, mtu aliyetoa mchango mkubwa zaidi ni Yasinta Massawe aliyechangia dola 3,000 (Sh. milioni 6.6).

Mbowe aliwaambia waandishi wa habari Jumanne kuwa michango hiyo imetokana na uhamasishaji unaofanywa na Watanzania walio nje wakiongozwa na Mange Kimambi anayeishi Marekani.

Katika mkutano huo na waandishi wa habari, Mbowe alisema afya ya Lissu imeimarika na ameshaanza kula na kupumua bila msaada wa mashine.

Siku moja baada ya mkutano huo, picha za mnato na video zilianza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii zikimwonyesha Lissu akifanyishwa mazoezi akiwa kwenye kiti cha wagonjwa na nyingine mbunge huyo akisikika akimshukuru Mungu na watu wote waliopambana kuhakikisha wanaokoa maisha yake.

Katika mkutano wake wa Jumanne, Mbowe alisema Lissu ambaye amefanyiwa operesheni 17 hadi Oktoba 12, gharama za matibabu yake zilikuwa zimefikia Sh. milioni 412.45.

"Tumepokea michango mingi ambayo imewezesha kwa kiwango kikubwa kusaidia matibabu ya Mheshimiwa Lissu," Mbowe alisema. "Kundi la kwanza katika kuchangia ni wabunge wa Chadema ambao walichanga Sh. milioni 48.4.

"Wananchi na viongozi wengine wa chama walichanga Sh. milioni 24.2, wanachama na viongozi na familia walichanga kupitia akaunti maalum ya CRDB Sh. milioni 90.8, michango iliyochangwa na wabunge wote Sh. milioni 43.

"Wapo Watanzania kwenye anga ya kimataifa walichangia fedha dola za Marekani 29,700 ambapo dada zetu kina Mange Kimambi walisaidia kuhamasisha kupitia mitandao.

"Hata mpaka sasa hivi bado fedha hazijatosha.

"Hapa ninazungumza gharama ya matibabu pekee yake kwa mwezi Septemba zimegharimu fedha za Kenya Sh. 10,687,316 sawa na dola za Marekani 106,875 na ilipofika Oktoba 12 jumla ya gharama ni Sh. 13,708,156 za Kenya."

Mbowe pia alisema jopo la madaktari 12 ambao walikuwa wanamtibu Lissu wamelipwa Dola za Marekani 46,440 (Sh. milioni 102.5) kwa kuwa kila daktari anapotoa huduma kwa muda fulani anahitajika kulipwa.

Lissu (49), ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria (TLS) alihamishwa kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma kwenda Nairobi usiku wa Septemba 7 baada ya kupigwa risasi 32 na watu wasiojulikana, akiwa ndani ya gari lake nyumbani kwake Area D mjini humo.

Njombe Mjini Waipigia 'Saluti' Simba Baada ya Kichapo cha Mabao 4-0

0
0
Njombe Mjini Waipigia 'Saluti' Simba Baada ya Kichapo cha Mabao 4-0
Nahodha wa Njombe Mji, Laban Kambole amesema uzoefu mdogo wa ligi umechangia kupata kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa Simba jana kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kambole alisema Simba ni timu kubwa tofauti na wao ambao wamepanda daraja msimu huu na kucheza Ligi Kuu kwa mara ya kwanza mwaka huu.

"Timu yetu wachezaji wengi ni wachanga na ukweli tulizidiwa katika mchezo huo kwani wengi hawana uzoefu wa ligi."

"Tatizo kubwa la wachezaji wengi wa Tanzania huwa tunaogopa majina ya hizi timu hivyo unakuta ukifika uwanjani unasahau kufanya uliyoelekezwa na kucheza unavyojua wewe," alisema Kambole.

Kambole alisema bado wana nafasi ya kufanya vizuri katika michezo mingine ijayo kwani wanachoshukuru wameshamaliza kucheza na Yanga na Simba kwenye mzunguko wa kwanza.

"Tumeshacheza na Yanga na Simba hivyo sasa tutashusha presha na kupambana katika michezo ijayo kuhakikisha haturudi tulikotoka," alisema nahodha huyo ambaye timu yake ilicheza kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Uhuru.

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa..Jibu Lipo Hapa

0
0
JE,UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZAKIUME,KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA,KUFIKA KILELENI MAPEMA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA UA MAUMBILE MADOGO YA UUME?Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa namambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURLUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA(MASTER BLASHION)HOMON Hishindwa kufanya kazi inavyotakiwa nk.upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa mahusiano mengi kuvunjika.BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,1KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO NDOA KABISA.TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO UMEFANIKIWA LEO 

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha,vidonda vya tumbo,korodani kivimba nakuuma,na anatoa ndagu za utajiri kwa wanaohitaji utajiri bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NAUTALETEWA POPOTE ULIPO TIBA HII UKIWA HAUNA NANAFASI YAKUFIKA OFISINI,

PIGA SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 50.
SHEIKH OMARY WHATSAP 0759030343.

Daktari: Tulifungua Ubongo wa Kanumba na Kuukuta Umevimba na Kisogo Kilikuwa na Mgando wa Damu

0
0
Daktari: Tulifungua Ubongo wa Kanumba na Kuukuta Umevimba na Kisogo Kilikuwa Mgando wa Damu
KESI inayomkabili muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’,  imeendelea kusikilizwa leo Jumatatu, Oktoba 23, katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ambapo shahidi wa nne upande wa Jamhuri anatoa ushahidi wake.
Katika ushahidi huo imeelezwa na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Binadamu  wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dtk. Innosent Mosha ambaye ni shahidi wa nne wa kesi hiyo, aliletewa oda  kutoka Jeshi la Polisi kwamba aufanyie uchunguzi mwili wa Steven Kanumba uliokuwa mochwari akishirikiana na daktari mwingine.
“Tulifungua ubongo wa Kanumba na kuukuta umevimba, mishipa midogomidogo ya ubongo ilikuwa imeingia damu, lakini kabla ya kufungua ubongo, kwenye kisogo kulikuwa na mgando wa damu.
“Baada ya kumaliza uchunguzi wetu tulipeleka sampuli kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ambapo tulipeleka pia sampuli mbalimbali za viungo vya mwili wake,” amefafanua Dkt. Mosha.
Ushahidi bado unaendelea kutolewa mahakamani

Mahakama Yamkuta na Kesi ya Kujibu Lulu Atakiwa Kujitetea

0
0
Mahakama Yamkuta na Kesi ya Kujibu Atakiwa Kujitetea
Mahakama Kuu jijini Dar es salaam, imesema muigizaji Elizabeth Michael (Lulu) ana kesi ya kujibu dhidi ya tuhuma za kuuwawa kwa msanii Steven Kanumba , hivyo anatakiwa kujitetea.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Mahakama kuu baada ya kufunga kusikiliza ushahidi upande wa mashtaka na kumtaka muigizaji huyo kuanza kujiandaa kwa ajili ya kutoa utetezi wake.
Wakili wa Elizabeth, Peter Kibatala ambaye ndiye anayemtetea muigizaji huyo, aliomba muda wa dakika 40 ili wajiandae kufanya hivyo, na kesi yake inasikilizwa tena saa 5 asubuhi hii.

Rais wa Somalia Afanya Ziara Nchini Uganda

0
0
Rais wa Somalia Afanya Ziara Nchini Uganda
Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed Farmajo yuko nchini Uganda kwa ziara rasmi .
Haijajulikana lengo la safari yenyewe lakini huenda inauhusiano na usalama wa mji mkuu wa nchi hiyo wa Mogadishu unaozidi kuzorota huku Uganda ikiwa na askari wengi kama walinda amani.
Ziara hii inafanyika wiki moja tu baada ya kutokea shambulio kubwa la kigaida nchini Somalia ambalo limesababisha vifo vya mamia ya watu.

Ingawa haijulikani lengo la safari hiyo, lakini wachambuzi wanahisi ziara hii inaweza kuwa ni moja wapo ya jitihada za Somalia kuomba usaidizi zaidi wa kijeshi kutoka Uganda hasa ikizingatiwa kwamba, Uganda ni miongoni mwa nchi zinazochangia wanajeshi wake Somalia.
Hata hivyo, swali ni je, iwapo wataongezewa nguvu inaweza kuleta tofauti yoyote? kwa sababu hivi sasa tayari Uganda ina idadi kubwa zaidi ya wanajeshi Somalia.

Uganda inachukuliwa kama mshirika wa karibu na Somalia na kuafuatia shambulio hilo rais Museveni alililaani vikali.
Hakusema ni hatua gani Museveni angefanya kuweza kuzua shambulio kama hilo lakini Uganda ina vikosi zaidi nchini Somalia vikiwa chini ya kivuli cha vikosi vya kulinda amani vya Muungano wa Afrika.

Bananga: Watanzania Nani Aliyetuloga?.. Kama Hatujalogwa Kuna Taifa Limetusomea Alibadri

0
0
Bananga: Watanzania Nani Aliyetuloga?.. Kama Hatujalogwa Kuna Taifa Limetusomesha Alibadri
Baada ya serikali kuandaa uchaguzi wa marudio kutokana na sababu mbalimbali, Diwani wa Kata ya Sombetini Arusha, Ally Bananga kupitia mtandao wa kijamii ametaka kujua  nani aliyewaloga watanzania kiasi cha kushindwa kufikiri gharama zinazotumika

kwenye uchaguzi huo zingesaidia kuboresha huduma za kijamii.
Bananga amedai kwamba Serikali inatenga fedha zingine milioni 200 kwa ajili ya uchaguzi wa marudio ikiwepo sehemu ambazo madiwani wamejiuzulu na kuhoji kwamba hivi diwani asingejiuzulu hizo fedha mil 200 kama zisingweza kununua madawa katika hospitali.
Kiongozi huyo amehoji,  "Hivi?? Watanzania nani aliyetuloga????? Siyo serikali siyo wananchi aiseeee!!! hivi Diwani asingejiuzulu hizo fedha mil 200 zisingenunua madawa hospitali? Je, zisingejenga matundu ya vyoo mashuleni? Je, zisingejenga vituo vya polisi maeneo yenye uhitaji? " Bananga
Bananga ameongeza "Kama Tanzania haikulogwa basi kuna taifa litakuwa lilitusomea alibadri siyo bure!!!!"
Oktoba 4, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza kwamba uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 Tanzania utafanyika Novemba 26 mwaka huu ambapo Mwenyekiti wa NEC  Jaji  Semistocles  Kaijage, alisema kuwa uchaguzi huo unafanyika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo baadhi ya madiwani kufariki dunia, kujiuzulu, kutohudhuria vikao na wengine ushindi wao kutenguliwa na Mahakama.

Wizara ya Ardhi Yafafanua Kuhusu Uwekaji wa Alama za X na Kuvunja Majengo

0
0
 Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo Yafafanua Kuhusu Uwekaji wa Alama za X na Kuvunja Majengo
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imetoa ufafanuzi kuhusu uwekaji wa alama za X na kuvunja majengo yanayojengwa katika miji bila kibali na katika viwanja vya watu wengine walio na hati miliki za ardhi kwa dhuluma.

Taarifa ya wizara iliyotolewa leo Jumatatu Oktoba 23,2017 imesema kwa wale waliojenga kwenye viwanja vyenye hati za watu wengine kwa nguvu na kuwadhulumu wenye hati miliki haki yao ya kisheria, hatua zitachukuliwa ili kuwarudishia haki wanaostahili.

“Hatutabomoa nyumba ya mtu bali tutaendelea na urasimishaji wa makazi kwa maeneo yaliyojengwa holela ili yawe makazi rasmi na wananchi wapelekewe huduma muhimu kama vile barabara, umeme na maji,” imesema taarifa hiyo.

Wizara imesema, “Muhimu wapewe hati miliki ili ziwasaidie kiuchumi na waweze kulipa kodi ya ardhi... lakini tutazuia ujenzi mpya holela katika miji yetu kwa mujibu wa sheria.”

Taarifa imesema viongozi wote wa wilaya na mitaa wahamasishe wananchi kushiriki kikamilifu katika urasimishaji wa makazi yao kwa faida yao na Taifa kwa jumla.

Yanga Kurejea Dar Kesho

0
0
Yanga Kurejea Dar Kesho
Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara VPL timu ya Yanga inatarajiwa kurejea jijini Dar es salaam siku ya Jumanne ikitokea Shinyanga ambako jana ilicheza mchezo wa raundi ya saba dhidi ya Stand United.

Hilo limethibitishwa na msemaji wa Yanga Dismas Ten ambaye emeeleza kuwa timu itaanza safari ya kutoka Shinyanga kurejea Dar es salaam siku ya Jumanne Oktoba 24.
“Timu inatarajiwa kurejea jijini Dar es salaam siku ya kesho Jumanne Oktoba 24 mwaka huu ambapo itapumzika na kisha taratibu zingine za maandalizi ya mchezo wa Oktoba 28 dhidi ya Simba zitaendelea”, amesema Ten.
Hata hivyo msemaji huyo hajafafanua ni wapi timu hiyo itaweka kambi kwaajili ya maandalizi hayo huku kukiwa na tetesi kwamba huenda ikaweka kambi nje ya Dar es salaam japo bado haijabainika ni wapi haswa.

Yanga jana iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya wenyeji Stand United kwenye uwanja wa CCM Kambarage na kufanya ifungane pointi na vinara Simba ambayo nayo ilishinda mechi yake dhidi ya Njombe kwa mabao 4-0 hali inayosababisha kuongezeka kwa ushindani kwenye mchezo wao wa Jumamosi.

Makonda Awatoa Hofu Wakazi wa Dar Kuhusu Bomoa Bomoa

0
0
Makonda Awatoa Hofu Wakazi wa Dar Kuhusu Bomoa Bomoa
Ndugu Zangu Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Naomba kuwatoa hofu, Mimi Paul Makonda nikiwa Mkuu wenu wa Mkoa na mtumishi wa serikali ya awamu ya tano, Napenda kuwataarifu kwamba serikali hii inayoongozwa na Mhe Rais, Dkt. John Pombe Magufuli HAIVUNJI Nyumba ya mtu Bali inaendelea kurasimisha Makazi kama ambavyo ilifanya kimara kwa kuwapatia Hati elfu Sita (6000) kwa Wananchi waliokuwa wamejenga kwenye makazi yasiyo rasmi, jitihada zinaendelea na ndivyo itakayofanyika tarehe 27/10/2017 kwa Wananchi waliojenga katika maeneo ya makongo juu.

Naomba niseme, na kama nimemuelewa vizuri alichokisema _Mhe William Lukuvi_ ambae ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi ni kuwa wananchi wasiendelee kujenga bila vibali vya ujenzi jambo ambalo linawanyima haki yao ya kukopeshwa, kulipa kodi ya majengo, na mwishoni kuwa na miji isiyopangwa vizuri.

Naomba kukiri kuwa apo awali kulikuwa na changamoto ya upatikanaji wa vibali vya ujenzi jambo ambalo haliwezi kuwa Adhabu kwa Wananchi waliojenga miaka ya nyuma iliyopita kwani ilifika hatua Mwananchi ana Hati ya Kiwanja chake na amekamikisha michoro kwa Mujibu wa Sheria na ana fedha za kuanza Ujenzi kwa ajili ya Makazi ya kuishi, unakuta Mwananchi huyo analazimika kufuatilia manispaa kwa zaidi ya miaka miwili mpaka mitatu bila kupata kibali cha ujenzi na hata akipata kibali baada ya miaka Mitatu na kuanza ujenzi, unakuta ndani ya muda mfupi watakuja baadhi ya watu wa OSHA kumsimamisha kwa madai hawana taarifa ya ujenzi jambo linalotengeneza mianya ya Rushwa, akimalizana na watu wa OSHA Wanakuja baadhi ya watu wa kikosi cha zimamoto (fire) nao inabidi atafute utaratibu wa kumalizana nao, jambo linalokera wananchi na kuwafanya wakose hamasa ya Kutafuta vibali vya ujenzi na Hatimae kujenga kiholela.

Kututokana na jambo hili, baadhi ya watu wasiowaaminifu wanatumia mwanya huu kuvamia maeneo ya watu na kujenga Kiholela na kuibua Migogoro Mikubwa ya Ardhi.

TULICHOFANYA KAMA MKOA

Kutokana na sababu hizo na changamoto nilizozielezea hapo juu, serikali ya Mkoa tulifanya kikao na wataalamu wa Ardhi na nikatoa maelekezo kuwa vitengo vyote nane vinanavyohusika na Utoaji wa vibali vya ujenzi VINAPASWA kuwa na mfumo Mmoja wa mawasiliano (one stop center) ili Mwananchi atakapoomba kibali cha ujenzi Idara zote nane zifikiwe kwa wakati Mmoja na kupunguza usumbufu wa Mwananchi kwenda kufuatilia vibali na wakati mwingine unaambiwa wahusika hawapo.

Ili mfumo huo uanze kufanya kazi wataalamu wangu walihitaji vitendea kazi ambavyo nimewawezesha vifaa hivyo zikiwemo Computer Hamsini (50) katika manispaa zote za Mkoa wa Dar es Salaam na kuwataka kutoa vibali ndani ya mwezi Mmoja tangu kupokea maombi kutoka kwa Mwananchi tofauti na awali ambapo Mwananchi alikuwa akichukua muda wa miaka miwili kufuatilia kibali cha ujenzi, lengo Likiwa kuwawezesha wananchi kufuata Sheria ili kuendana na Mpango wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na makazi Chini ya _Mhe William Lukuvi_ katika kuhakikisha tunapanga miji yetu.

Kwa maelezo Haya mafupi, Naomba niseme kwenye Mkoa wa Dar es Salaam HAPATAKUWA na bomoa bomoa ya KARNE wala Nyumba ya mtu kuvunjwa ISIPOKUWA wananchi wanaojenga sasa ni vyema wakafuata utaratibu kama alivyoelekeza Mhe William Lukuvi waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi, ili kuepuka kuvunjiwa Nyumba ambayo umeijenga kwa jasho jingi, na kujinyima uku ukikesha ili utimize ndoto ya kuwa na makazi bora.

Niwatakie kazi njema, na kwa pamoja tushirikiane katika Kupanga na kuendeleza Mkoa wetu wa Dar es Salaam kwa ajili ya Maendeleo ya Taifa na vizazi vyetu.

Mhe Paul C. Makonda
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
23/10/2017

JPM Amteua Profesa Florens Luoga Kuwa Gavana wa BOT

0
0
JPM Amteua Profesa Florens Luoga Kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli, amemteua Profesa Florens Luoga kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, baada ya aliyepo sasa, Gavana Benno Ndulu kumaliza muda wake, miezi michache baadaye.
Rais Magufuli ameyasema hayo leo wakati akiunuku vyeti kwa kamati zilizofanya uchunguzi wa kiwango, aina na thamani ya madini katika makinikia, ikulu jijini Dar es Salaam.
kabla ya uteuzi huo, Luoga ambaye kitaaluma ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alikuwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na uteuzi wake utaanza baada ya Benno Ndulu kumaliza muda wake.

Lulu Aanza Kujitetea Afunguka Mazito Siku ya Tukio Kifo cha Kanumba

0
0
Lulu Aanza Kujitetea Afunguka Mazito Siku ya Tukio Kifo cha Kanumba
Kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili muigizaji wa filamu Tanzania, Elizabeth Michael (Lulu), imeendelea leo ambapo upande wa mshtakiwa umeanza kutoa utetezi wake.

Akisimulia jinsi ilivyokuwa siku ya tukio, Lulu amesema marehemu alikuwa akimpiga na panga baada ya kutokea ugomvi uliotokana na wivu wa mapenzi, alipomuona akiongea na simu.
"Nilikuwa nataka kutoka ila marehemu 'Kanumba' alinikataza, alikuwa hataki nitoke, nilipomwambia natoka na marafiki zangu alinikimbiza na taulo na mimi nilikuwa naogopa kupigwa, mara nyingi alikuwa ananipiga kila akilewa na sio kwa akili zake, alipoona simu yangu inaita akahisi ni simu ya mwanaume akasema kwanini naongea na simu ya mwanaume mbele yake? Marehemu akaingia uvunguni akatoa panga akasema leo nakuua huku akinipiga na panga kwenye mapaja", ameelezea Lulu.
Lulu ameendelea kusimulia...."Marehemu alianguka mwenyewe na kujigonga kwa nguvu na kuinuka sehemu nyingine alikuwa kama anatapatapa, nilimwambia Seth kuwa Kanumba amedondoka na akajaribu kumuamsha hakuamka akasema anaenda kumuita daktari, alivyosema anaenda kumuita daktari na mimi nikaondoka nikiogopa anaweza akaamka akaanza kunipiga, niliondoka nikawasha gari kuelekea Coco Beach kutuliza akili".
Muigizaji huyo ameendelea kusimulia kwamba ..."Nilivyofika Coco beach meseji zilianza kusambaa kuniuliza kuwa nasikia Kanumba amefariki, nikampigia 'Kidume'  ambaye ni rafiki yake Kanumba kumuuliza Kanumba yupo hospitali gani niende kumuona, akaniambia wewe usije hospitali, niambie uko wapi, tukakubaliana tuonane Bamaga, tulivyokutana Bamaga alikuwa kama anataka kuongea na mimi ghafla wakaja askari kunikamata".
Pamoja na hayo muigizaji huyo ameithibitishia mahakama kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na marehemu (Steven Kanumba) kwa muda wa miezi minne kabla ya kukutwa na mauti.
Mahakama Kuu imeghailisha kesi hiyo mpaka siku ya kesho Oktoba 24, ambapo itasikilizwa tena.

Nasa Yatangaza Maandamano Yatakayofanyika Kesho

0
0
Nasa Yatangaza Maandamano Yatakayofanyika Kesho
 Kiongozi wa Muungano wa National Super Alliance (Nasa), Raila Odinga ametangaza maandamano ya siku mbili kuanzia kesho.

Odinga akizungumza katika Kanisa Katoliki la St Peter’s Kiminini, Trans-Nzoia amesema maandamano ya kesho Jumanne Oktoba 24,2017 na Jumatano yanalenga kushinikiza Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kufanya mageuzi kabla ya kuandaa uchaguzi wa urais wa marudio.

“Jumanne kutakuwa na maandamano, Jumatano pia tutaandamana na Alhamisi hakuna uchaguzi,” alisema Odinga ambaye amesusia uchaguzi huo wa marudio wa Oktoba 26,2017.

Wiki iliyopita Odinga alisema angetoa mwelekeo halisi Oktoba 25,2017 kuhusu hatua ambayo wafuasi wake watachukua wakati wa uchaguzi huo.

Kiongozi huyo wa upinzani amesema maandamano ni haki ya kikatiba ya Wakenya hivyo waandamanaji hawapaswi kuadhibiwa kwa kupigwa risasi na polisi.

Raila amedai ana ushahidi wa kuonyesha kuwa uchaguzi wa Oktoba 26 umesheheni udanganyifu.

“Tuna ushahidi wa kuonyesha kuwa uchaguzi wa Alhamisi una dosari. Tayari magari ya polisi yanasafirisha karatasi za kura. Ukweli ni kwamba kiasi kikubwa cha kura zilichapishwa jijini Nairobi na wala si Dubai kama mnavyoelezwa,” alisema.

Alidai kuwa kujumuishwa kwa Cyrus Jirongo katika karatasi za kura ni ithibati kwamba karatasi za kura zilichapishwa nchini Kenya.

“ Jirongo alitangazwa na korti kuwa amefilisika, mbona IEBC ilimjumuisha katika karatasi ya kura? Walijumuisha wagombea wote wanane kwa sababu karatasi zilikuwa zimechapishwa na Jubilee jijini Nairobi,” alisisitiza Odinga.

Alisisitiza kuwa hatashiriki uchaguzi wa Alhamisi ambao utawahusisha Rais Uhuru Kenyatta, Mohamed Abduba Dida,  Dk Ekuru Aukot, Cyrus Jirongo, Dk Japhet Kaluyu, Profesa Michael Wainaina na Joseph Nyagah.

“Uhuru hana mshindani, anashindana peke yake. Sisi tunahitaji uchag

Lipumba Asifu Jitihada za Rais Magufuli za Kupigania Maliasili

0
0
Lipumba Asifu Jitihada za Rais Magufuli za Kupigania Maliasili
Mwenyekiti wa (CUF) anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa, Profesa Lipumba amefunguka na kumsifia Rais John Pombe Magufuli kwa hatua mbalimbali anazochukua juu ya maliasili za nchi hii na kusema Rais amechukulia jambo hilo umuhimu.

Lipumba amesema hayo leo Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akizungumza kwenye hafla ya kupongezwa na kupewa vyeti kwa wajumbe walioshiriki kwenye kamati za uchunguzi wa madini alimaarufu kama makinikia.
"Kwa niaba ya vyama vya siasa nchini naomba kumpongeza Rais kwa juhudi alizofanya kwenye suala hili la madini, sisi viongozi wa upinzani kwa muda mrefu, kwa miaka mingi tumekuwa tukipiga kelele sana kuhusu mikataba ya madini na maliasili za nchi hii, itakuwa ajabu sana sisi tuliokuwa mstari wa mbele kupiga kelele kwamba tunaibiwa kubeza juhudu unazofanya sasa" alisema Lipumba
Aidha Lipumba ametoa ushauri kwa serikali kuwa watu ambao wanatakiwa kuingia kwenye bodi za kampuni mpya wa madini kuwa wanapaswa kuwa wazalendo kweli na kwenda kusimamia maliasili za nchi na kudai bila kufanya hivyo tutalizwa tena.
"Watanzania wanatakiwa kushiriki kwenye kampuni hizo ambazo zitakuwa na uwazi na faidi inayopatikana inapaswa kuwa nusu kwa nusu, lazima Watanzania watakaoshiriki katika kampuni wanatakiwa kuwa wazalendo kulinda masilahi ya taifa, kwa sababu tumekubaliana kugawana nusu kwa nusu lakini mkajikuta wametangaza faidi ya asilimia 0 hivyo hiyo 0 ukigawanya kwa mbili unapata 0 palepale, kwa hiyo watakaoingia ndani ya kampuni wahakikishe utaratibu wa kudanganywa haupati nafasi" alisema Lipumba
Lipumba amesema kuwa wao watamuunga mkono Rais John Pombe Magufuli na kusema kuwa katika hutua hii wanatanguliza maslahi ya Tanzania kwanza na maslahi ya Vyama Vya Siasa yatafuata baadaye.

Dada Yake Raila Odinga Kukamatwa kwa Uchochezi

0
0
Dada Yake Raila Odinga Kukamatwa kwa Uchochezi
Dada wa kinara wa upinzani nchini Kenya Raia Odinga, atashtakiwa kwa kuchochea ghasia baada ya kushambuliwa kwa wafanyakazi wa tume ya uchaguzi IEBC wiki iliyopita, kwa mujibu wa mwendesha mkuu wa mashtaka nchini Kenya.

Mwendesha mashtaka mkuu nchini Kenya Keriakor Tobiko aliamrisha Ruth Odinga akamatwe.
Bw. Odinga alikuwa anawania urais pamoja na Rais Uhuru Kenyatta kwenye marudio ya uchaguzi wa urais siku la Alhamisi, lakini aljiondoa mapema mwezi huu, akisema kuwa uchaguzi huo hautakuwa wa huru na haki

Zitto Aliamsha Dude Kuhusu Ndege za Bombardier

0
0
Zitto Aliamsha Dude Kuhusu Ndege za Bombardier
Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo amefunguka na kusema kuwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ya awamu ya tano imekopa dollar milioni 500 kutoka benki ya Uswiss na pesa hizo ndiyo zimetumika kulipa ndege za Tanzania.

Zitto Kabwe amesema hayo leo kupitia mitandao yake ya jamii na kusema kuwa riba za mkpo huo ni mkubwa sana na kudai watu wa chini wakiwepo wavuvi wa Migebuka kutoka Kigoma watahusika kulipa deni hilo kupitia kodi zao.
"Serikali ya CCM ya awamu ya Tano imekopa $500m kutoka Benki ya Credit Suisse ya Uswiss Kwa riba kubwa Sana. Sehemu ya fedha hizo zimetumika kulipia ndege ambazo Serikali inanunua. Wavuvi wa Migebuka Kigoma watahusika kulipa deni hilo kupitia kodi zao" alisema Zitto Kabwe

Rais Magufuli leo amesema kuwa uchumi wa nchi unazidi kukuwa na kudai serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina pesa za kutosha ndiyo maana imeweza kununua ndege mpya zaidi ya sita kwa mara moja na kudai watu ambao wanasema uchumi umeshuka wanaichonganisha serikali na wananchi.

Papa Aiombea Nchi ya Kenya

0
0
Papa Aiombea Nchi ya Kenya
Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amesema anaifuatilia kwa karibu Kenya na anaiombea ishughulikie matatizo yake kwa majadiliano yenye kujenga kwa masilahi ya taifa.

Papa, ambaye pia ametoa wito wa amani duniani, amewataka waumini wote kuungana naye katika sala kwa lengo hilo maalamu na hasa kwa Kenya ambako mvutano uko juu katika mkesha wa uchaguzi wa marudio wa rais wenye ushindani mkubwa uliopangwa kufanyika Oktoba 26.

“Nawaomba wote kuungana nami katika sala ya kuombea amani ya dunia,” alisema Papa alipowaambia mahujaji na watalii waliokuwa wamekusanyika kwa ibada Jumapili.

“Nafuatilia kwa karibu sana siku hizi hali ya Kenya, ambayo niliitembelea mwaka 2015, na ambayo ninaiombea, kwamba nchi nzima iweze kukabiliana na hali ngumu ya sasa katika mazingira ya majadiliano ya kujenga, wakiwa na lengo mioyoni ya kutafuta mema.”

Mgogoro nchini Kenya umefkia hali ya mkwamo tangu Mahakama ya Juu ilipofuta matokeo ya urais ya uchaguzi wa Agosti 8 ikitaja “dosari” na “ukiukwaji” wa mchakato wa uchaguzi.

Katika uchaguzi huo zaidi ya watu milioni 15 walishiriki na matokeo yalipotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), Rais Uhuru Kenyatta alipata asilimia 54 huku mpinzani wake mkuu Raila Odinga akipata asilimia 44.

IEBC imeandaa uchaguzi wa marudio Oktoba 26 kama ilivyoamriwa na Mahakama ya Juu lakini Odinga amejitoa, akisema hatashiriki hadi yafanyike marekebisho makubwa katika Tume hiyo ikiwemo kuondolewa kwa sekretarieti iliyokuwa inaongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu, Ezra Chiloba.

Katika kusisitiza msimamo wake Odinga ameitisha maandamano makubwa ya wafuasi wake nchi nzima Jumanne na Jumatano yakiwa na lengo la kuhakikisha uchaguzi haufanyiki kama ilivyopangwa.

Maswali ya Jaji Rumanyika kwa Lulu Kuhusu Kesi Inayomkabili ya Kuua Bila Kukusudia

0
0
Maswali ya Jaji Rumanyika kwa Lulu Kuhusu Kesi Inayomkabili ya Kuua Bila Kukusudia
BAADA YA Muigizaji, Elizabeth Michael ‘Lulu’kuanza kujitetea katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar, kwa tuhuma za kusababisha kifo cha Steven Kanumba bila kukusudia, msanii huyo amekana kuhusika na kifo hicho.
Lulu ameeleza siku ya tukio, Kanumba alikuwa amelewa na yeye Lulu alitaka kutoka na marafiki zake lakini alimkataza, baada ya Kanumba kuona simu ya Lulu imeita alizani anaongea na mwanamme mwingine huku ambapo alichukua panga na kumkimbiza nalo. Kanumba alianguka na Lulu kuchukua gari na kukimbilia Coco Beach ambapo baadaye alikamatwa na polisi maeneo ya Bamaga.
Jaji wa Mahakama Kuu, Samu Rumanyika amemtwanga maswali Lulu kama ifuatavyo;
Jaji Sam Rumanyika: Kipindi unaendesha gari ulikuwa na leseni halali?
Lulu: Ndiyo.
Jaji: Tufafanulie uhalali wake.
Lulu: Nilikuwa sina.
Lulu: Baada ya kukamatwa nilipelekwa kituo cha polisi Oysterbay nilikuwa nikihojiwa nikiwa sijui kama Kanumba amefariki.
Lulu ameeleza hayo leo Jumatatu akijitetea katika kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live




Latest Images