Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Wasitegemee Jipya Toka kwa Okwi Anaziweza Timu Ndogo Tu si Yanga- Ray

$
0
0
Wasitegemee Jipya Toka kwa Okwi Anaziweza Timu Ndogo Tu si Yanga- Ray
MSANII wa Bongo Movie’s, Vincent Kigosi ‘Ray’ amewaambia mashabiki wenzake wa Yanga kuwa, wasihofi e mabao ya Emmanuel Okwi wa Simba, kwani huwa anazifunga timu ndogo tu. Yanga leo Jumamosi inacheza na Simba kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam mechi ya Ligi Kuu Bara raundi ya nane.
Mpaka sasa Okwi ndiye kinara wa mabao akiwa nayo nane.

Ray alisema: “Yanga ipo vizuri kila idara hivyo na ninaamini haitatuangusha kwenye mchezo huu ingawa wapinzani wanapiga kelele za Okwi, watambue kuwa huyo haiwezi Yanga.
“Okwi anaonekana katika mechi ndogo lakini katika mechi kubwa anafunikwa hivyo wasitegemee jipya kutoka kwake.”
Chanzo Global Publishers

Hivi Ndivyo Hamormonize Alivyofumguka Kuhusu Kuhama WCB

$
0
0
Hivi Ndivyo Hamormonize Alivyofumguka Kuhusu Kuhama WCB
Msanii wa muziki wa Bongo Flava kutoka label ya WCB, Harmonize amejibu iwepo anaweza kuondoka katika label hiyo.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Shulula’ ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa hawezi kufanya hivyo kwa sasa.

“Hapana kwa sababu unapozungumzia Harmonize inaizungumzia WCB, so bila WCB hakuna Harmonize, yaani kama baba kama mama” amesema Harmonize.

Alipoulizwa ni msanii yupi anamkubali katika label hiyo alijibu, “ndani ya WCB nawakubali wote kwa sababu kikubwa kila msanii unayemuona pale hajaja kwa bahati, kila mtu ana kipaji japokuwa wanatofautiana”.

Ruby Aelezea Kolabo Yake na Yemi Alade

$
0
0
Ruby Aelezea Kolabo Yake na Yemi Alade
Msanii wa muziki Bongo, Ruby amefunguka kuhusu tetesi za ujio wa kolabo yake na msanii wa Nigeria, Yemi Alade.

Muimbaji huyo ameeleza kuwa hawezi kuweka sana hilo wazi kwani mipango yake sasa ni kuvunja ukimya wake kwa upande nyumbani.

“Siwezi nikasema tayari kila kitu kimemalizika lakini vitu vipo, sitaki kusema kabisa kwenye kolabo za kimataifa natamani iwa surprise kwa sababu nimekaa muda mrefu kimya I need talk about home kwanza” amesema Ruby.

Mwanamume Aliyewaambukiza Watu 30 Virusi vya Ukimwi Makusudi Afungwa Miaka 24 Jela

$
0
0
Mwanamume Aliyewaambukiza Watu 30 Virusi vya Ukimwi Makusudi Afungwa Miaka 24 Jela
Mhasibu mmoja nchini Italia amefungwa jela miaka 24 kwa kuwaambukiza makusudi wanawake 30 virusi vya Ukimwi.

Valentino Talluto anadaiwa kushiriki mapenzi bila kinga na wanawake angalai 53 baada yake kupatikana na virusi vya Ukimwi mwaka 2006, mwanamke mdogo zaidi miongoni mwa hao alikuwa na miaka 14 wakati wa kuanza uhusiano wao.

Mawakili wa Talluto walikuwa wametetea mteja wao wakisema vitendo vyake vilikuwa "visivyo vya busara, lakini havikuwa makusudi."

Hata hivyo, aliwaambia wale waliomwambia avalie mpira wa kondomu aliwaambia kwamba alikuwa na mzio, au kwamba muda mfupi awali alikuwa amepimwa na kupatikana hana Ukimwi, shirika la habari la AFP linasema.

Baadhi ya wanawake walipomkaripia baada ya kugundua kwamba walikuwa wameambukizwa, alikanusha madai kwamba alikuwa na virusi hivyo ambavyo husababisha Ukimwi.
Kutokana na vitendo vyake, watu wengine wanne waliambukizwa virusi hivyo kando na wanawake ambao aliwaambukiza moja kwa moja: wanaume watatu na mtoto mmoja.
Mwendesha mashtaka Elena Neri aliambia mahakama mwezi uliopita kwamba: "Vitendo vyake vilikusudiwa kupanda mauti."

Mwanamume huyo aliwaambia kwamba iwapo angekuwa anawaambukiza wanawake hao virusi makusudi, badi hangelikuwa ameunga uhusiano halisi nao.
"Wengi wa wasichana hao wanawafahamu marafiki zangu na jamaa zangu," amesema.
"Wanasema kwamba nilitaka kuwaambukiza Ukimwi watu wengi zaidi. Kama hiyo ingekwua ndiyo hali, ningeenda basi kwenye baa na kushiriki ngono kiholela, singeliwaingiza katika maisha yangu."
Majaji mjini Roma walijadiliana kuhusu hukumu dhidi yake kwa zaidi ya saa 10 kabla ya kutangaza hukumu hiyo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari Italia, mhukumiwa alilia hukumu ilipokuwa inasomwa.
Hata hivyo, adhabu hiyo haikufikia hukumu ya kufungwa jela maisha ambayo viongozi wa mashtaka walikuwa ameomba mahakama ahukumiwe.

Milioni 300 Zamponza Mfanyabiashara Yusuph Manji Ofisi Zake Zafungwa

$
0
0
 Milioni 300 Zamponza Mfanyabiashara Yusuph Manji Ofisi Zake Zafungwa
Mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji amekuwa katika kipindi kigumu tena baada ya kuandamwa na mambo mengi ambapo kwa sasa Kampuni ya Udalali ya Yono imezifunga  ofisi zake zilizopo Barabara ya Pugu akituhumiwa kudaiwa kodi ya zaidi ya Sh300 milioni na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)



Uchaguzi wa Rais Kuendelea Kenya Kurudiwa Vituo Vitano Leo

$
0
0
Uchaguzi wa Rais Kuendelea Kenya Kurudiwa Vituo Vitano Leo
Uchaguzi wa marudio ambao ulipangiwa kufanyika leo nchini Kenya katika maeneo ambayo shughuli hiyo haikufanyika Alhamisi utafanyika katika vituo vya kupigia kura vitano pekee.
Vituo hivyo ambavyo vina jumla ya wapiga kura 696 vinapatikana katika eneo bunge la Turkana ya Kati, kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi IEBC Wafula Chebukati alisema tume hiyo haingeweza kuendelea na uchaguzi katika vituo vingine 3,635 ambavyo vinapatikana katika maeneo bunge 27, mengi yakiwa ngome ya muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa).
Kiongozi wa muungano huo, waziri mkuu wa zamani Raila Odinga, alisusia uchaguzi huo na alikuwa amewataka wafuasi wake kutoshiriki.
Mengi ya maeneo bunge hayo yanapatikana katika majimbo manne - Kisumu, Migori, Homa Bay na Siaya.
Bw Chebukati alisema tarehe ambayo uchaguzi utafanyika maeneo hayo itatangazwa baadaye ingawa hakusema ni lini.

"Jana, baadhi ya wafanyakazi wangu walitekwa na kuteswa. Baadhi nyumba zao zilivunjwa na kuporwa. Wengine waliamrishwa kutofika na kuzuiwa kwa nguvu kufika vituo vya kupigia kura ambapo walifukuzwa. Baadhi wametafuta hifadhi katika vituo vya polisi," alisema Bw Chebukati katika taarifa Ijumaa jioni.
"Katika baadhi ya visa, hata polisi zaidi waliotumwa kuimarisha usalama hawakuweza kuzuia ghasia kwani fujo kutoka kwa waandamanaji pia zilizidi."
Wasifu wa Raila Odinga, kiongozi wa upinzani Kenya
Mfahamu rais 'wa kidijitali' Uhuru Kenyatta
Mwenyekiti huyo wa tume aliwalaumu wanasiasa na kutoa wito kwao kuhakikisha "watu kutoka maeneo yaliyoathiriwa hawanyimwi haki yao ya kupiga kura na pia kuhakikisha haki ya kuishi inaheshimiwa."
"Uchaguzi wa kufana ni matokeo ya watu mbalimbali wakifanya majukumu yao na bila ubinafsi na kwa njia njema. Hii ni pamoja na viongozi wa kisiasa, maafisa wa usalama na wanahabari."
Siaya Migori
Tume ya IEBC ilikuwa awali imekadiria kwamba asilimia 48 ya wapiga kura 19.6m waliosajiliwa kupiga kura walishiriki uchaguzi huo.
Hii iliashiria kuwa huenda hadi watu 9.4m walijitokeza kushiriki, idadi ambayo ni ya chini mno ukilinganisha na uchaguzi wa tarehe 8 Agosti ambapo waliojitokeza walikuwa asilimia 78.9 ambao ni wapiga kura 15m.
Lakini Bw Chebukati baadaye alifafanua kwamba takwimu halisi kutoka maeneo bunge 267 zilikuwa zinaonesha waliokuwa wamejitokeza maeneo hayo walikuwa 6.6m.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa..Jibu Lipo Hapa

$
0
0

JE,UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZAKIUME,KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA,KUFIKA KILELENI MAPEMA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA UA MAUMBILE MADOGO YA UUME?


Tatizo la kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya kiume husababishwa namambo mengi kama,KISUKARI,NGIRI,CHANGO,TUMBO KUUNGURLUMA,MAUMIVU YA KIUNO,UNENE KUPITA KIASI,KUJICHUA(MASTER BLASHION)HOMON Hishindwa kufanya kazi inavyotakiwa nk.upungufu wa nguvu za kiume husababisha tendo la ndoa kutofanyika kwa kujiami nakwa usahihi nahivyo husababisha ndoa mahusiano mengi kuvunjika.BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI,1KUKOSA HAMU YA TENDOL LA NDOA 2 UUME KISIMAMA KWA KULEGEA 3 KUWAHI KUFIKA KILELENI 4 KUSHINDWA KURUDIA TENDO LA NDOA WAKATI 5 KUCHOKA SANA BAADA YA ROUND YAKWANZA NAKUKINAI TENDO NDOA KABISA.TUMIA 3 POWER KWA TATIZO LA UKOSEFU(UPUNGUFU)WA NGUVU ZA KIUME NAHAMU YA TENDO LA NDOA.FINA HUBORESHA MAUMBILE YA KIUME KWA KUNENEPESHA KWA SAIZI UIPENDAYO HAIJARISHI UMRI.PIA KUNA DAWA ZA KURUDISHA MPENZI KWA MUDA MFUPI SANA NAZAKUPATA KAZI,KESI,KUDHULUMIWA,NK WASILIANA NA SHEIKH OMARY AKUTATULIE MATATIZO YAKO HATA KAMA UMEHANGAIKA SANA PASIPO MAFANIKIO UMEFANIKIWA LEO

Pia sheikh omary anatibu busha bila opresheni,kisukari,ngiri,presha,vidonda vya tumbo,korodani kivimba nakuuma,na anatoa ndagu za utajiri kwa wanaohitaji utajiri bila masharti yoyote magumu.ANAPATIKANA DAR ES SALAAM NAUTALETEWA POPOTE ULIPO TIBA HII UKIWA HAUNA NANAFASI YAKUFIKA OFISINI,

PIGA SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 5

Hashim Lundenga Ailalamikia Serikali Kufungia Fungia Kazi za Sanaa

$
0
0
Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waendeshaji wa mashindano ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga amefunguka na kutoa lawama kwa serikali kuhusu sakata la kufungia fungia wasanii na kazi za sanaa na kusema jambo hilo linadidimiza sanaa.

Ludenga amesema hayo leo alipokuwa akihojiwa kwenye Jukwaa la sanaa ambalo limeandaliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambapo leo limefanyika katika wa Taifa Dar es Salaam, na kusema kitendo cha serikali kufungia wasanii na kazi za sanaa kimekuwa kikwazo na kudidimiza sanaa nchini.

"Mimi leo nimekuja hapa hakuna ajenda maalum ila nikipata nafasi nitatoa yangu ya moyoni, suala la kufungia sanaa au wasanii huko si kuendeleza sanaa  bali ni kudidimiza sanaa yetu, ingependeza msanii anapofanya kosa fulani kuwe na faini fulani ambayo mtu analipa lakini siyo kumfungia, anapokiuka utaratibu au sheria kuwe na faini tu kama kwa wenzetu wa mpira wa miguu" alisema Ludenga

Ludenga anasema msanii anapofungiwa kwa wakati fulani anapokuja kurudi inamchukua muda na anakuwa anaanza upya katika sanaa jambo ambalo linarudisha nyuma sanaa na maendeleo ya sanaa kiujumla.

"Unapomfungia msanii kuja kuanza tena mpaka aje kusimama kama alivyokuwa wakati unamfungia inachukua muda na gharama zaidi hivyo unakuwa unadidimiza sana badala ya kuboresha, mfano sisi tumefungiwa mwaka 2014, na sababu za kufungiwa ni kutokana na makosa ya mawakala wetu, kumbuka wakati tunafungiwa tulikuwa na wadhaamini kabisa huku ni kurudishana nyuma" alisisitiza Ludenga.

Christina Shusho Afunguka Kuhusu Viongozi Tanzania

$
0
0
Msanii wa muziki wa Injili Tanzania Christina Shusho, amewataka watanzania kuwaombea viongozi wetu wa kitaifa, kwani tuna kila sababu ya kujivunia watu hao kutokana na uongozi wao uliotukuka

Christina Shusho ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa East Africa Radio, na kusema kwamba Tanzania tuna bahati kupa viongozi wenye hekima ambao wanaliongpoza taifa kwa amani, tofauti na nchi zingine za jirani kwa Afrika Mashariki.

"Najivunia sana viongozi wetu, tena niwaambie tu watanzania tuwaombee sana, tuna bahati ya kupata viongozi wenye upendo, na pia tudumishe upendo wetu tuwe na subira kwenye mambo yetu tudumishe hii amani, Mungu ametupendelea sana nchi za wenzetu wanalia na amani yao", amesema Christina Shusho.

Kauli hiyo ya Shusho imefuatia baada ya kuporomoshewa matusi na wakenya, kutokana na mihemko waliyonayo kipindi hiki cha uchaguzi, na kusema kwamba Wakenya wanahitaji  maombi pia kwani wanapitia kipindi kigumu.

Ukipata Mwanamke Mwenye Sifa Hizi 16 Usimwache

$
0
0
Hizi ni sifa halisi za mwanamke wa kweli

1. Ni nguvu ya mwanaume
2. Ni jasiri
3. Mchapakazi
4. Mwenye kujiamini
5. Tegemeo la familia
6. Mwalimu wa watoto na familia yake kiujumla
7. Mlinzi wa mwanaume.
8. Chanzo cha baraka ya familia.
9. Adui wa maadui wa familia.
10. Sauti ya familia.
11. Mponyaji wa familia yake na taifa.
12. Mlezi wa huduma.
13. Mkombozi wa familia na taifa.
14. Msaidizi wa Mungu tumfanyie msaidizi wa kufanana naye.
15. Mwombezi wa familia, huduma na taifa.
16. Mficha siri wa Mungu

Kutana na Mtabibu Wanyota za Binadamu Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka Comoro Kwa Sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU WANYOTA ZABINADAMU    DUNIANI KOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAUWEZO WAKUBAINI JAMBOLAKO NAKULITATUA MAALIM FADHILI RASHIDI ANATIBU MARADHI YA FUATAYO KAMA VILE

KAMA MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WA KURUDISHA MTU ALIEPOTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKEMUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYAWAKO LIVE KWASABABU MAALUM ANA TOWA PETE YA BAHATI ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI UNAZOTAKA

DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVUZAKIUME PIA ANAYO DAWA YA KUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIA CHUMAULETE KWENYE BIASHARA KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI TIBAHII NI KWADINI ZOTE MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKASANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO NCHI YEYOTE DUNIANI UTAPATA HUDUMAYANGU ACHAKUTESEKA NA MATATIZO ULIONAYO MAALIM FADHILI RASHIDI YUPO TANZANIA KWA AJILIYAKO


CALLING +255719362806/+255763276239/

KWA WHATSAPP IMO +255785786436

Uvuvi Haramu Kusababisha Waziri Mpina Kuahidi Kujiuzulu

$
0
0
Uvuvi Haramu Kusababisha Waziri Mpina Kuahidi Kujiuzulu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina ameahidi kuachia madaraka endapo tatizo la uvuvi haramu litaendelea kuwa sugu nchini.

Waziri Mpina amethibitisha hilo wakati akiteketeza nyavu zinazotumika katika uvuvi haramu zilizokamatwa mkoani Kigoma zenye thamani ya shilingi Milioni thelathini na moja.
Kama nitashindwa kushughulia suala zima la uvuvi haramu, nitaachia dhamana hii niliyopewa na Mheshimiwa Rais, lakini hadi nafikia hatua hiyo lazima wengi watakuwa wamejuruhiwa”, amesema Mpina.

Zoezi hilo la kuchoma nyavu haramu ni mwendelezo wa hatua ambazo amewahi kuzichukua rais wa jamahuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jonh Magufuli kipindi akiwa waziri wa wizara hiyo. Mpina ameahidi kuwa huo ni mwanzo tu wa zoezi hilo katika serikali ya awamu ya tano ambapo hatua zaidi zitaendelea kuchukuliwa ili kukomesha uvuvi haramu.
Aidha waziri Mpina ametoa maelekezo kwa viongozi wa Mikoa ambayo shughuli hizo zinafanyika kwa kuwataka wahakikishe wanasimamia na kulinda rasilimali za taifa ikiwa ni mapoja na Mito, Ziwa na Bahari.

Penda Kujijali Kwanza Yanini Kumng'ang'ania Asyekupenda?

$
0
0
Penda Kujijali Kwanza Yanini Kumng'ang'ania Asyekupenda?
Ili mapenzi yaweze kuwa bora kwa kila aliye katika mahusiano, huwa ni vyema kila mmoja kuiona thamani ya mwenzake. Ukipenda kujiangalia mwenyewe  si ajabu mwenzako kupata hisia za kuwa humthamini wala humjali.
    Muunganiko wenu katika mapenzi maana yake tayari mmekuwa kitu kimoja. Katika mimi unaweka sisi.

   Ila pia ni vyema ikakumbukwa ladha na maana halisi ya mapenzi ipo kwa anayekupenda na kukuthamini. Unapokuwa na uhakika kama anakupenda na kukuthamini hapo ndipo nafsi yako itatulia na kuwa na amani. Ndani ya mapenzi na mtu wa aina hii ni amani na utulivu kwa kwenda mbele. Hakuna majuto wala majonzi ya kila siku.

    Unapoamua kuwa katika mahusiano na mtu ambaye hakupendi, bali unakuwa naye kwa kuwa tu unampenda jua umejiingiza katika utumwa. Mapenzi ni suala la kihisia zaidi. Mwenzako anapokosa hisia na wewe maana yake hata uwepo wako hauthamini inavyopaswa. Na hapo ndiyo tunaona yale mahusiano ya kingono yanapozaliwa na si ya kimapenzi kwa maana halisi.

    Yaani mwenzako anapokuwa na mihemko ya kingono ndipo anapokutafuta na si vinginevyo. Niliwahi kuongea na msichana mmoja aliyewahi kuniambia anampenda kijana mmoja ambaye anauhakika kabisa yeye hampendi. Alinambia uhakika huo kaupata kutokana na kijana huyo kumtakia  kuna msichana yupo anampenda na kumjali ila si yeye.

   Kuonesha zaidi kumpenda msichana yule mwingine, jamaa aliwahi kumwambia kama ikitokea hata huyu msichana akagombana na yule mpenzi mwingine wa yule jamaa, kijana yule alikuwa radhi kumdhuru huyu msichana.

   Hata kwa matazamo wa haraka hapo unaweza kugundua ni kwa namna gani huyu msichana alikuwa haitajiki. Ila cha kushangaza msichana huyu(aliyeongea na mimi) alimwambia mvulana husika yuko radhi kuwa naye hivyo hivyo.

    Aliamua kuwa hivyo akiamini ipo siku jamaa atamuelewa. Kweli walikuwa pamoja. Ila  unajua kinachomkuta sasa?

   Kila jamaa anapogombana na yule msichana mwingine anamtumia huyu kingono na mambo mengine yasiyo ya kimapenzi, na bila kutafakari mara mbili huyu msichana anafanya kwa kile anachoamini hali hiyo itamfanya huyu jamaa amfikirie zaidi. Kuna kitu cha kuangalia hapa.
   Suala la mapenzi si suala la kuoneana huruma wala aibu. Mapenzi ni hisia. Unapojitoa kwa mwenzako kwa kila jambo na unamuona haelekei ujue hana hisia na wewe. Kwanini unakubali kuteseka na kuumia kila siku kwa kumuangalia yeye tu?

     Ndiyo, unampenda sana, unamjali sana na unamuhitaji sana, ila kama yeye hakutaki wa kazi gani? Ni muda wa kujiangalia na wewe sasa.
    Ona thamani yako kama binaadamu, jionee huruma jinsi unavyoteseka kila siku kwa mtu asiyeona thamani yako.

  Wewe ni binaadamu mwenye hadhi na thamani, bila kujali muonekano wala rangi yako. Unahitaji mwenye kukuthamini na kukujali na si anayekufanya kama mdoli wake ngono au kadi yake ya pesa. Kataa utumwa wa mapenzi kwa kuiona thamani yako.
   Ni vyema ukalia kwa kumkosa kuliko kuonekana unaye wakati moyoni siyo wako. Hakuna sifa ya kuwa na mtu mwenye fedha au muonekano mzuri ikiwa hakujali wala haupo moyoni mwake. Mapenzi ni amani na raha.

  Mapenzi hufanya watu wafurahi na kusahau shida zao. Ila jiulize kwanini kwako hayako hivi? Unaenda kwa mwenzako badala afurahie uwepo wako, yeye anaona unajipendekeza. Unampigia simu na kumpa maneno mazuri ya faraja, yeye anaona unamsumbua. Sasa wa kazi gani? Siku njema wapendwa.

Rais Magufuli Amewaagiza Watendaji wa Wizara ya Elimu Kuhakikisha Wanatoa Mikopo kwa Wanafunzi

$
0
0
Rais Magufuli Amewaagiza Watendaji wa Wizara ya Elimu Kuhakikisha Wanatoa Mikopo kwa Wanafunzi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli amewagiza watendaji wa Wizara ya Elimu kuhakikisha wanatoa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu wenye sifa ya kupata mikopo kabla ya vyuo kufunguliwa ili kuepuka kupata usumbufu wakati wa masomo yao.

Rais Magufuli ameyazungumza hayo baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua Ikulu jijini Dar es Salaam,amesema tarehe 29 mwezi uliopita.

“Tarehe 29 mwezi uliopita wizara ya fedha imetoa Shilingi bilioni 147, zimepelekwa Wizara ya Elimu, ni mikopo ya wanafunzi wenye sifa, nitashangaa kama watakuwepo wanafunzi ambao hawatapata mkopo, nitashangaa” amesema Magufuli.

Rais Magufuli amewaapisha Makatibu Wakuu wapya, Naibu Makatibu Wakuu wapya na Wakuu wa Mikoa wapya baada ya kuwateua juzi, waliapisha jana Ikulu jijini Dar es salaam.

Natamani Sana Kuwa Mama na Ikitokea Siwezi Kupotea Kwenye Muziki- Ruby

$
0
0
Natamani Sana Kuwa Mama na Ikitokea Siwezi Kupotea Kwenye Muziki- Ruby
MWANADADA kutoka kiwanda cha muziki wa Bongo Fleva, Hellen George ‘Ruby’ amefunguka kuwa hawezi kupotea kimuziki kisa kuzaa.
Ruby aliiambia Mikito Nusunusu kuwa, anatamani sana kuitwa mama na haofii kuwa atapotea kimuziki kama inavyotokea kwa wasanii wengine kwa sababu amejipanga kikamilifu.
“Natamani sana kuitwa mama kwa kweli na ikitokea muda wowote nitamshukuru Mungu na nitazaa maana sina kipingamizi, siwezi kupotea kimuziki maana mtoto ni moja ya baraka pia,” alisema Ruby
Chanzo Global Publishers

Bobi Wine Amekataa Fedha Milioni 29 Alizohongwa na Serikali

$
0
0
Bobi Wine Amekataa Fedha Milioni 29 Alizohongwa na Serikali
Mwanamuziki Uganda, ambaye ni Mbunge Kyadondo East , Bobi Wine amekataa fedha milioni 29 za Uganda alizohongwa na serikali ili aweze kukubaliana na mapendekezo ya kufanyia marekebisho kipengele cha katiba na kuondoa ukomo wa miaka 75 kuongoza nchi.

Bobi Wine ameiamuru benki ambayo amewekewa fedha hizo kuzirudisha kwa watu ambao wameziweka na kusema kutokana na taarifa ya mawasiliano wabunge wote wa Uganda 449 wamepewa fedha hizo ili waweze kukubaliana na hoja hiyo na kuoandoa ukomo wa miaka 75 ili kuweza kumpa nafasi tena  Yoweri Kaguta Museveni (73) kugombea nafasi ya Urais tena kwa awamu ya sita 2021.

"Oktoba 24, 2017 Milioni 29 wa Uganda ziliwekwa kwenye Account yangu ya benki, pesa hizo walipewa wabunge wote wa Uganda kwa mujibu wa taarifa rasmi pesa hizo walizopewa wabunge ni ili kukubaliana na pendekezo la kufanyia marekebisho kipengele cha 102 (b) cha Katiba ya Uganda na kuondoa ukomo wa miaka 75 kama sifa ya kusimama kama Rais wa Uganda" alisema Bobi Wine

Bobi Wine aliwapa taarifa watu wa benki yake kuwa wazirudishe hizo fedha zote zilizotumwa kwa mtu ambaye amezituma kwake na kusema amefanya maamuzi hayo kutokana na ukweli kwamba yeye haungi mkono Katiba yao kuchezewa kwa ajili ya mtu mmoja na kusema hawapo tayari kwa mtu kuwa Rais kwa wakati wote ndiyo maana Katiba iliweka ukomo wa miaka.

Profesa Jay Afunguka Kinachomsababisha Kuwa Kimya

$
0
0
Profesa Jay Afunguka Kinachomsababisha Kuwa Kimya
BAADA ya mashabiki wake wengi kutaka kujua kwa nini yupo kimya kwenye anga la muziki, mkongwe Bongo Fleva ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Morogoro, Joseph Haule ‘Profesa Jay’ ameibuka na kuwaeleza kinachomsibu.
Akipiga stori na baada ya kuulizwa sababu za kuwa kimya, Profesa Jay alisema bado anaweka mambo ya kifamilia sawa na yakishakuwa vizuri ndipo atakaporejea tena.
“Kuna mambo mengi ya kifamilia yananiweka bize, najitahidi kuyaweka sawa yakikamilika mashabiki wangu watarajie muziki mzuri kutoka kwangu. Niwaombe tu wawe na subira kwani mambo mazuri hayataki haraka,” alisema Profesa Jay.

Pata Muonekano wa Shape Bomba na Rangi ya Ngozi Kwa Kutumua Products za Natural Beauty

$
0
0

OFFER SPECIAL
NATURAL BEAUTY ndiyo kampuni pekee inayotoa bidhaa ORIGINAL zenye GARANTII NA RISITI
Sasa ni wakati wako wa kupendeza na bidhaa hizi zisizo na kemikali wala madhara kwa mtumiaji.
       Pata bidhaa hizi upate matokeo mazuri kwa haraka na uhakika zaidi. Bidhaa zetu zote zimetengenezwa kwa mimea na matunda.

          BIDHAA ZETU:-

1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @150,000/=
2.Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge  @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:-
 (1)Mafuta  @150,000/=
(11)Vidonge @170,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a)SHARK POWER gely ya kupaka @150,000/=
(b)Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @150,000/=
(C) VigRX CREAM- Ni dawa mpya ya kuongeza maumbile hadi nchi 7.5 inapatikana kwa @200,000/=
(C)Handsome up original ni kifaa kinachoongeza maumbile kwa %99 size uipendayo  @250,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150,000/=
7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula  @150,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=
(b)Mkanda wa kawaida @150,000/=
(c)Micro-computer belt wa umeme @200,000/=
9.Kupunguza  maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @150,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @150,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @150,000/=
12.Kurudisha usichana  (bikra) @150,000/=
        Wasiliana nasi :- (+255)
             0759029968 au.     
                0659618585
  TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............
     Follow us on instagram  @natural2162
@natural2162
@natural2162

Zari, Mobeto Wawekwa Kitimoto Kuhusu Kutupiana Vijembe Mitandaoni

$
0
0
Zari, Mobeto Wawekwa Kitimoto Kuhusu Kutupiana Vijembe Mitandaoni
Warembo waliokuwa kwenye vita ya maneno, Hamisa Mobeto na Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wamedaiwa kuwekwa kitimoto ili waache kurushiana maneno kwenye mitandao ya kijamii.
Risasi Jumamosi limeelezwa kuwa, kwa nyakati tofauti wawili hao waliwekwa kitimoto na ndugu wa msanii wa Mzazi Mwenzao na kutakiwa waache malumbano hayo mitandaoni kwani hayaleti picha nzuri kwao na ukizingatia kosa limeshafanyika na msanii kukiri hadharani.
“Walichoelezwa tu ni kwamba, waache kutupiana vijembe mitandaoni maana wao sasa hata kama hawatakuwa wake wenza lakini tayari msanii ana damu yake kwa Mobeto. Amekiri kwamba aliteleza na kujikuta ameingia kwenye uhusiano naye hadi kufikia hatua ya kupata mtoto.

Zarinah Hassan.
“Mtoto ameshazaliwa na ni damu ya msanii na mwisho wa siku msanii atalazimika kumpa mahitaji yake kama mwanaye hata kama yeye hataendeleza uhusiano na mama wa mtoto. Zari ni mama wa watoto wake wawili, wamedumu muda mrefu hivyo yeye ataendelea tu kushikilia usukani kama mke,” kilisema chanzo cha ndani kutoka katika familia ya msanii.
Chanzo hicho cha ndani kilizidi kueleza kuwa, wanamshukuru Mungu kwamba mwanamitindo Mobeto na Zari ambaye ni mjasiriamali maarufu, kila mmoja kwa wakati wake ameelewa vizuri somo hilo hivyo kuacha kutupiana manenomaneno katika mitandao ya kijamii.
“Tunashukuru Mungu kwani kila mmoja ameelewa somo. Hawarushiani tena maneno kama ilivyokuwa awali. Zamani ilikuwa hazipiti siku mbili utasikia kuna jipya wame-sababisha lakini sasa hivi kama unafuatilia hata mitandaoni, watu hawawa-zungumzii tena.,” kilisema chanzo hicho
Chanzo Global Publishers
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images