Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live

Pata Muonekano wa Shape Bomba na Rangi ya Ngozi Kwa Kutumua Products za Natural Beauty

$
0
0
OFFER SPECIAL
NATURAL BEAUTY ndiyo kampuni pekee inayotoa bidhaa ORIGINAL zenye GARANTII NA RISITI
Sasa ni wakati wako wa kupendeza na bidhaa hizi zisizo na kemikali wala madhara kwa mtumiaji.
       Pata bidhaa hizi upate matokeo mazuri kwa haraka na uhakika zaidi. Bidhaa zetu zote zimetengenezwa kwa mimea na matunda.

          BIDHAA ZETU:-

1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @150,000/=
2.Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge  @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:-
 (1)Mafuta  @150,000/=
(11)Vidonge @170,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a)SHARK POWER gely ya kupaka @150,000/=
(b)Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari @150,000/=
(C) VigRX CREAM- Ni dawa mpya ya kuongeza maumbile hadi nchi 7.5 inapatikana kwa @200,000/=
(C)Handsome up original ni kifaa kinachoongeza maumbile kwa %99 size uipendayo  @250,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150,000/=
7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula  @150,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=
(b)Mkanda wa kawaida @150,000/=
(c)Micro-computer belt wa umeme @200,000/=
9.Kupunguza  maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @150,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @150,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @150,000/=
12.Kurudisha usichana  (bikra) @150,000/=
        Wasiliana nasi :- (+255)
             0759029968 au.   
                0659618585
  TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ...............
     Follow us on instagram  @natural2162
@natural2162
@natural2162

Aliyekuwa Kiongozi wa Catalonia Anaweza Kugombea Tena

$
0
0
Aliyekuwa Kiongozi wa Catalonia Anaweza Kugombea Tena
Serikali ya Uhispania inasema kuwa inakaribisha kushiriki kwa kiongozi aliyefuwa wa Catalonia Carles Puigdemont kwenye uchaguzi mpya.
Serikali ya Madrid imeamrisha kuwa uchaguzi mpya kwa bunge la eneo la Catlonia utafanyika mwezi Disemba.
Madrid ililivua eneo la Catalonia utawala wake baada ya bunge la Catalonia kupiga kura ya kujitangazia uhuru,
Bwana Puigdemont amewashauri watu kukataa udhibiti kamili kutoka Madrid.
Waziri mkuu wa Uhispania avunja bunge la Catalonia
Barcelona watakuwa wapi Catalonia ikiwa huru?
Alilaani kufutwa kwa utawala wa Catalonia na kuahidi kuendelea kufanya kazi ya kujenga nchi ili huru.
Wakati huo huo mamia ya raia wa Uhispania wamekusanyika katika mji mkuu Barcerlona kuunga mkono umoja wa Uhispania.
Aidha Uhispania inaendelea kushinikiza kuchukua udhibiti wa nguvu dhidi ya serikali ya jimbo la Catalonia, iliyofutiliwa mbali.

Yaya Toure Adai Furaha Yake ni Kushinda Taji la Ligi Kuu ya Mabingwa Barani Ulaya

$
0
0
Nyota wa Manchester City Yaya Toure amesema anatamani kutwaa ubingwa wa UEFA akiwa na timu hiyo ili kukamilisha ndoto yake.

Toure amedai furaha pekee anayoitamani ndani ya kikosi cha Manchester City ni kushinda taji la Ligi ya mabingwa barani Ulaya kwani  ndio kombe pekee ambalo hajafanikiwa kutwaa akiwa Etihad.
Yaya Toure hadi sasa ametwaa makombe mawili ya EPL, mawili ya EFL pamoja na moja la FA hivyo anaona kama hadaiwi chochote kutoka nchini England zaidi ya ubingwa wa Ulaya.

Raia huyo wa Ivory Coast ameshawahi kutwaa ubingwa wa UEFA akiwa na FC Barcelona mwaka 2009, hivyo anahitaji taji lake la pili la Ulaya.

Vikosi Vya Usalama Vyaokoa Hotel ya Nasa-Halblod Iliyovamiwa na Al-Shabaab

$
0
0
Vikosi Vya Usalama Vyaokoa Hotel ya Nasa-Halblod Iliyovamiwa na Al-Shabaab
Vikosi vya usalama vimefanikiwa kuikomboa Hoteli ya Nasa-Hablod iliyokuwa imetekwa na Wapiganaji watano wa Al-Shabaab. Wanamgambo hao waliivamia hoteli hiyo baada ya kulipua mabomu wliyoyatega katika gari dogo nje ya lango la kuingilia.

Kufuatia shambulio hilo watu 23 wameripotiwa kuuawa. Vikosi vya usalama vilifanikiwa kuikomboa Hoteli hiyo baada ya kufanikiwa kuwauwa Wapiganaji hao pamoja na kuwakamata wawili.

Tusimtupie Fundi SPANA Wakati Anakarabati Mtambo

$
0
0
Na mwandishi Maalumu, Mtanzania
Nianze ‘Tafakuri Yangu’ kwa kukushirikisha usemi wa Kiingereza ninaoutafsiri kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili, kwamba mtambo au mashine inapoharibika fundi mkuu anapoikarabati baada ya kuifanyia tathmini, ndiye anayejua ilivyoharibika sanjari na aina na namba za spana zinazohitajika katika kuikarabati.

Kwa Kiingereza usemi: “Throwing spanners at works” ni nahau inayotumika kubainisha uvurugaji wa jambo linalokarabatiwa, kwamba kila anayedhani ni fundi zaidi ya anayekarabati hujiona anafaa kuliko aliyekasimiwa jukumu hilo, lakini heri mwenye mawazo kama hayo, kuna ambao humrushia fundi spana asizozihitaji kwa makusudi ili kuharibu lengo la kukarabati. Nadhani utakuwa umeelewa mashiko ya dhana hiyo inayoshadadia tukio adhimu lililotokea hivi karibuni, ambapo Rais Magufuli alitunuku vyeti wajumbe wa Kamati Maalumu za uchunguzi na majadiliano kuhusu rasilimali za nchi yetu.

Awali wakati mchakato umeanza kuhusu uthibiti wa makinikia, kisha baadaye dhahabu hata kutathmini upya sheria zetu zinazosimamia masuala ya madini jopo la mafundi lilianza kutupiwa spana na waliodhani ni mafundi zaidi ya waliokasimiwa kazi hiyo.

Mengi yalisemwa na kama isingekuwa ukimya na usiri wa kazi hiyo pengine hata hatua iliyofikiwa isingefikiwa ingawa pia ni kidato kimoja tu katika kuelekea kukamilisha mchakato kamili na kuzuia ‘utapia tija’ kwa jisi tulivyokuwa hatufaidiki na rasilimali tulizokirimiwa na mwenyezi Mungu.

Hata sasa pamoja na kwamba hatua imefikiwa katika suala hilo chapuo kubwa limeanza kupigwa kwa kushabikia zaidi kutupisha spana kwenye baadhi ya makubaliano ikiwemo fidia ya dola milioni 300. Ukiachana na hulka za watupishaji spana kuna mambo ya msingi yamefanyika na kubadili mwelekeo kutoka mdororo na kuzuia mporomoko wa upatikanaji tija, kuelekea hali chanya kwamba badala sasa ya sisi kusalia na asilimia tano tu ya madini ambayo hayapatikani kokote duniani isipokuwa hapa kwetu ndiyo maana yanaitwa ‘Tanzanite’ tutajizolea asilimia tisini na tano.

Hii inanikumbusha usemi kwamba maisha ni sawa na kupanga mstari mkiambiwa geukeni nyuma wa mbele atakuwa nyuma na wa mwisho atakuwa wa mbele, hii ndiyo ile ya kibao kugeuka ghafla japo hiki tulikigeuza baada ya kustukia kuwa tunaibiwa.

Fundi mkuu (Rais Magufuli) aliifanya kazi hiyo kwa mchakato wa kujiamini ndiyo maana tumefikia tulipo sasa katika suala hilo, ingawa spana nyingine alizotupishiwa yeye mwenyewe binafsi na kamati alizoziteua alifafanua kwamba zilisababisha mtikisiko mkubwa ambao yeye mwenyewe anafahamu namna ulivyomtesa ingawa kwa kuwa aliamini analolifanya ni sahihi basi aliamua kukomaa liwalo na liwe.

Kitakachopatikana ni kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo kwa maslahi ya Tanzania ambayo kila mmoja wetu anazaliwa ndani yake lakini anaiacha anapofarikiana na dunia.

Nadhani kwenye mafanikio hayo spana hazitarushwa tena japokuwa bado kuna hali ya kurusha kwa bezo, kwamba kuna yaliyokubaliwa ambayo hayawezi kutekelezeka kama taarifa za Acacia iliyoko chini ya Barrick Gold kudai kuwa haina uwezo wa kulipa dola ambazo kampuni mama inayoisimamia kampuni hiyo tanzu imekubali kufanya hivyo. Kwa hili lililotimizwa ‘Tafakuri Yangu’ inalipa Kongole kwani litaongeza mapato na hatutafanya tu kwa kiwango cha miradi inayoendelea sasa, mathalan, ujenzi wa barabara na elimu bure lakini pia ununuzi wa meli na uimarishaji mfumo wetu wa umeme kwa kutangaza kandarasi ya bwawa kubwa la kufua umeme la Strigler’s Gorge pamoja na ujengaji wa Reli ya kisasa na usambazaji umeme vijijini bali tutafanya zaidi.

Ingawa matumaini ni makubwa kwa hatua tuliyofikia lakini safari bado inaendelea kwani kuna mengi tunayopaswa kuyapata, kwa kuwaacha mafundi wataje spana zinazohitajika katika kukarabati mfumo ingawaje nao pia wanapaswa kuzingatia taarifa za wadau, ambao mfumo haukuwa ukiwatendea haki wakiwemo wananchi na viongozi pinzani wa siasa.

Ni katika maudhui ya ujenzi wa nyumba moja bila kugombea fito kama tunadhamiria vizazi vijavyo vifaidi matunda ya uhuru kama kauli mbiu za miaka ya mwanzoni zilivyobainisha kuwa: ‘Uhuru ni kazi’ na baadaye kubadilishwa kidogo na kuwa: ‘Uhuru na kazi’ na hakika maendeleo hayatakuja kwa kuruhusu rasilimali kutokomea kwa kuchukuliwa kirahisi kutokana na makosa ya kiutendaji kwa mikataba mibovu.

Hata hivyo kila wingu jeusi lina upapi wa mn’garo wa fedha kama ambavyo baada ya kuwekwa wazi mabadiliko ya nafasi ya juu ya BOT tashwishwi nyingi zinazowakereketa wahafidhina wa tija ya nchi yetu, zimepelekea wabainishe vipaumbele vya kugudua vimeo ambavyo kutokana na usimamizi duni vinatatanisha mfumo wetu wa fedha ikiwemo utakatishaji fedha, kulinda mfumo wa mzunguko wa fedha ili kuimarisha thamani ya shilingi yetu isidorore zaidi na ushirikishwaji wa sekta rasmi na binafsi katika ujenzi wa uchumi. Ushauri kama huu ndiyo spana anazohitaji fundi sio anazotupishiwa!

Acha Yanga Washangilie Suluhu,Simba Wanahitaji Mchumi Kuliko Manara

$
0
0
Na Thadei Ole Mushi.

Simba wanashangaa kwa nini Yanga wanashangilia kutoa Sare na Simba. Waacheni washangilie kwa nguvu zote. Hii ni match ya tatu msimu huu Yanga wanatoa sare na Simba katika dakika 90 za mchezo achana na match zilizoamuliwa kwa mikwaju ya penalt.

Simba Vs Yanga kwenye mapinduzi CUP walitoka sare ndani ya dk 90. Simba vs Yanga kwenye ngao ya hisani walitoka Sare ndani ya dakika 90. Simba vs Yanga kwenye match ya raund ya kwanza msimu wa 2017/2018 nayo wametoka sare.

Hapa ndipo napoona umuhimu wa kuwa na mchumi mwenye uelewa mkubwa pale Simba kuliko Haji Manara mpiga domo na mwenye mpira wa propaganda.

Kwa wale waliosoma course za uchumi na biashara watakuwa wanafahamu kitu kinachoitwa “Value for Money”. Ni kipengele kinacho deal na kuangalia thamani ya pesa iliyotumika kununulia bidhaa flan. Hapa tunafanya ulinganisho wa fedha zilizotumika na bidhaa iliyonunuliwa au huduma iliyonunuliwa.

Kwenye value for money tunaangalia pia effectiveness na efficiency kwamba je huduma au bidhaa hii niliyowekeza ina uwezo wa kufanya kazi kwa kiwango gani? Je input tulizoweka zinatuletea output tarajiwa?

NINI NAMAANISHA?

Nimeaangalia uwekezaji wa Simba kwa msimu huu kwa Mujibu wa taarifa zao wanadai walisajili kwa kiasi cha shilingi Bilion 1.3. Simba inaweza kuwa ndio timu pekee iliyosajili kwa Dau kubwa kuliko club zote za Afrika mashariki.

Nimeangalia kambi waliyoweka Simba kujiandaa na msimu huu, walienda South Africa kwa takribani mwezi mmoja. Walienda timu nzima usafiri wa ndege kwenda na kurudi na huduma zote walizopatiwa south Africa kwa kadirio la chini kwa timu kama simba ni bilioni 1.5.

Nimeangalia kambi ya Simba katika kujiandaa na match za yanga ni za kiwango cha juu. Huwezi kulinganisha Kambi za simba na za yanga wanaochamgisha mashabiki ili wapate kula yao. Match ya jana Haji Manara anatuambia kuwa walilala Hotel ya Nyota tano Serena Hotel kikosi kzima hapa ni mamilioni ya shilingi yalitumika.

Nimeangalia mishahara ya wachezaji wa Simba jumla ya mishahara ya wachezaji wote ni milioni 100.4. Mfano Haruna Mwenyewe anakunja milioni 8.7 pale Simba kazidiwa Laki 3 na Rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania anayelipwa shilingi milioni 9. Kwa kiwango hiki Haruna anaenda kuzurura na kubutua tu uwanjani.

Hamjanielewa tu kwa nini nalazimisha Simba wawe na mchumi anayeweza kuzipangia fedha za Simba matumizi sahihi ili zilete matokeo tarajiwa?

Mnajua Pius Buswita analipwa shilingi ngapi pale Yanga? Ni chini ya Nusu mshahara wa Niyonzima halafu bado anamfunika uwanjani. Mnajua shilingi ngapi analipwa Pato Ngonyani?

 Kelele za Haji Manara hazitaweza kuwafanya Simba kuchukua Ubingwa mwaka huu. Simba kwa uwekezaji wake walitakiwa kuwa na tofauti ya point kumi na timu nyingine si utofauti wa magoli.

Simba isitegemee kuwa mwaka huu watachukua ubingwa kwa kuwa na idadi kubwa ya magoli. Ni mara chache sana Bingwa huamuliwa kwa tofauti ya Magoli. Inaweza kupita misimu 4 ndio mkapata msimu unaoamuliwa kwa tofauti ya magoli.

NINI NAKIONA MBELE.

Simba ilianza ligi kwa kishindo kikubwa ila imeaanza kuchoka. Ni tofauti na wenzao Yanga walianza Ligi wakiwa wamechoka sasa wanaanza kuimarika.

Kama Trend itaendelea hivi bingwa atakuwa Yanga. Hili halina ubishi…..

Acheni Yanga washangilie jamani fedha yao ni ndogo ila inafanya kazi kubwa sana. Nafikiri mnaona Brevis aliyopewa Ajibu inavyofanya kazi ya kuwalaza kina Mwanjale na viatu.

Acheni washangilie watu wanatokea Lodge za Kihonda Morogoro wanakuja kuwasumbua watu waliolala kwenye Hotel ya Nyota tano…..

Tuangalie Value for Money tuachane na Kelele za Manara.Simba iamue kufanya Biashara ya mpira kwa kutumia Fedha zao kwa usahihi.

Simba ijitafakari.

Zitto Kabwe Amewasaliti Au Amesalitiwa na Wenzake??

$
0
0
Novemba  22, mwaka 2016, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, aliweka picha yake mtandaoni ikimwonyesha akiwa ndani ya Ikulu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwa miongoni mwa wageni walioalikwa kwenye tafrija ya rais mpya wa nchi yetu, John Magufuli.

Katika picha waliyopigwa inaonyesha dhahiri kuwa, kazi ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete ilikuwa kumtambulisha Zitto Kabwe kwa Rais Magufuli. Ni heshima.

Mara kadhaa Zitto amesema picha hiyo inaonyesha ‘Rais wa 6” akiwa na marais wa awamu ya nne (Kikwete) na tano (Magufuli). Ni ndoto ya kila mwanasiasa kuwa kiongozi mkuu wa nchi. Lakini kuna sura tofauti kati ya Zitto Kabwe wa serikali ya awamu ya nne na awamu ya tano ya John Magufuli.

Katika utawala wa Kikwete, Zitto amepitia katika matukio mbalimbali ya kusisimua na kushangaza, huku mengine yakitawaliwa na utata machoni pa wanasiasa wenzake. Hata hivyo, hizo si hoja za msingi kwa leo. Swali kubwa la leo ni kwanini baadhi ya wanasiasa wa chama chake cha ACT-Wazalendo wanamkimbia Zitto?

Si vibaya kuuelezea uzuri wa Zitto. Kwanza amejitahidi kufanya mbinu za kuwa hodari na kileleni.

Mwaka 2012 Zitto aliungana na wabunge kupaza sauti kutaka mawaziri nane wang’oke kutokana na ufisadi. Zitto alikusanya saini za wabunge, kutimiza 70, ili awasilishe hoja ya kumng’oa aliyekuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Baadaye Rais Kikwete aliwang’oa mawaziri waliokuwa wanatakiwa kuwajibishwa, hivyo akafanikiwa kumwokoa Pinda.

Mwaka huo huo, Kamati ya POAC ilivunjwa na Spika wa Bunge la 10, Anne Makinda, ambapo aliunganisha na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto akashinda uenyekiti wake.

Aidha, ni Zitto Kabwe ambaye alihakikisha anapigania masilahi ya Watanzania baada ya kukubali kutimuliwa bungeni kutokana na tuhuma zake dhidi ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, ambaye alidaiwa kusaini mkataba wa Buzwagi akiwa hotelini huko jijini London, nchini Uingereza. Kutokana na tuhuma hizo, aliyekuwa Spika wa Bunge 2005-2010, Samuel Sitta, alimfukuza bungeni.

Zitto pia amechangia pakubwa kupatikana kwa sheria ya Capital Gain kwenye sekta ya madini nchini.

Mapito ya Zitto

Zitto ni mwanasiasa aliyeibuliwa na Chadema chini ya uenyekiti wa Freeman Mbowe.

Ndicho kipindi ambacho Zitto aliibuka kuwa mwanasiasa mahiri na aliyetikisa kwa matukio mbalimbali. Tuhuma za usaliti wa Zitto dhidi ya Chadema zilijiri zaidi wakati akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali, ambapo alimwagiza Msajili wa Vyama vya Siasa kufanya ukaguzi wa hesabu zao za fedha.

Zitto aliagiza hilo akiwa Naibu Katibu Mkuu Chadema, hali ambayo ililalamikiwa kuwa anakisaliti chama, kwani alitakiwa “kuwatonya” juu ya mpango huo wa ukaguzi. Wapo walioudhika juu ya mpango huo na kudai Zitto ni msaliti.

Pili, mwaka 2009 Zitto alitangaza bayana kumuunga mkono mgombea wa NCCR- Mageuzi katika Jimbo la Kigoma Kusini, David Kafulila, licha ya chama chake hicho cha zamani, Chadema kuweka mgombea wao.

Tatu, uamuzi wa Zitto Kabwe kugombea uenyekiti mwaka 2009 dhidi ya Freeman Mbowe lilikuwa jaribio ambalo Chadema kilitakiwa kukabiliana nalo na kulitatua. Zitto akiwa na kambi yake ya kisiasa ndani ya Chadema, alichukua fomu na kugombea uenyekiti, hali ambayo iliibua malumbano makali, na kuitwa msaliti.

Kambi ya Zitto Kabwe ilikuwa pamoja na Samson Mwigamba na Profesa Kitila Mkumbo. Kwa muda mrefu Zitto alituhumiwa kutoshiriki majukumu mbalimbali ya kichama, hali ambayo ilitokana na jaribio lake la kugombea uenyekiti.

Inaelezwa kuwa, Zitto hakuwa karibu tena na Chadema, ingawa mwaka 2010 aliruhusiwa kugombea ubunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya chama hicho. Kuutaka uenyekiti kulitajwa kama usaliti ndani ya Chadema.

Nne, M4C ni moja ya operesheni inayotumiwa na Chadema ambayo Watanzania wanahamasishwa kujiunga katika chama ili kuleta mabadiliko. Zitto alidaiwa kutoshiriki kikamilifu katika operesheni hiyo.

Mwishowe Zitto na Chadema wakapelekana mahakamani, licha ya katiba ya chama kukataza wanachama wake kutokwenda mahakamani kwa suala la chama. Ndiyo kusema Zitto alikuwa amekiuka katiba ya Chadema, ndipo mwaka 2015 akafukuzwa uanachama na baadaye akajiunga na chama cha ACT-Wazalendo.

Ndani ya Chadema, Zitto Kabwe anatafsiriwa kama msaliti ambaye alikuwa anakihujumu chama. Kwa Chadema, Zitto, Profesa Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba, walitajwa kuwa wasaliti na walikihujumu chama hicho. Mtazamo wa Chadema ulijengwa zaidi na matukio yote ambayo yalisababisha malumbano ndani ya chama, hata kama yalikuwa ya kidemokrasia. Hujuma yao kubwa ilitajwa kuandaa mkakati wa ushindi ambao ungemwondoa Mbowe madarakani kupitia sanduku la kura.

Ndani ya chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alikuwa na washirika wake wa karibu, Profesa Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba na wakili maarufu Alberto Msando. Zitto alijiunga ACT- Machi 20, 2015 na kukabidhiwa kadi na Mwenyekti wa Tawi la Tegeta.

Cha kustaajabisha ni kwamba, Zitto amekimbiwa na washirika wake ndani ya chama kutokana na sababu mbalimbali, ikiwamo kutoeleweka kwa miongozo ya Kiongozi Mkuu wa Chama (Party Leader).

Profesa Kitila Mkumbo aliteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji. Kitila alikuwa mshauri wa ACT-Wazalendo na mshirika wa karibu wa Zitto kwa muda mrefu. Kitila na Zitto walifukuzwa pamoja ndani ya Chadema sambamba na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson  Mwigamba.

Aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Anna Mghwira, ameteuliwa na Rais Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Mara baada ya uteuzi huo, chama cha ACT-Wazalendo kilitangaza kumwengua katika nafasi yake ya uenyekiti.

Sasa hali imekuwa mbaya zaidi, kwani Samson Mwigamba ambaye alikuwa Kiongozi wa Kamati ya Uchaguzi ya chama hicho, naye amemkimbia Zitto Kabwe na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi – CCM.

Mwigamba amekimbilia CCM ambako aliwahi kukibeza na kuishambulia kwa lugha kali ambazo baadhi zilimfikisha mahakamani kwa madai ya kuwachochea askari kuasi. Awali Mwigamba alijiuzulu wadhifa wake wa Katibu Mkuu kwa sababu alikuwa akielekea masomoni na kufanya kazi mjini Arusha katika Chuo Kikuu cha Kenyatta.

Sasa Mwigamba amekikimbia ACT-Wazalendo na kwenda CCM, huku akiacha shutuma mbalimbali dhidi ya viongozi wenzake.

Uamuzi wa Mwigamba ulitokea siku chache baada ya Profesa Kitila Mkumbo kujivua uanachama wa ACT-Wazalendo, kwa madai anashindwa kuaminiwa na kutekeleza vizuri majukumu yake ndani ya wizara kwa kudhaniwa kuwa mpinzani.

“Mnamo Aprili 25, 2016, nilipokuwa nang’atuka ukatibu mkuu, nilipotoa nasaha zangu mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama nilisema, salama ya chama chetu ni kubaki kwenye misingi ya uanzishwaji wake.

“Hii haikuwa bahati mbaya, bali nilimaanisha kwa kuwa nilishaanza kuona mwelekeo wa baadhi ya viongozi kuchepuka nje ya misingi ya chama. Na kutokea hapo nimekuwa nikiwalalamikia sana viongozi juu ya kuacha misingi na mambo ya msingi yaliyotufanya tuanzishe chama hiki, mara nyingine nikifikia kutofautiana sana hata na wewe binafsi (Kiongozi Mkuu wa Chama).

“Kwa kuwa hali hiyo kwa sasa inazidi kuongezeka na jambo ambalo binafsi naamini ndiyo sababu hasa ya Prof Kitila Mkumbo kujivua uanachama,” ilisema barua ya Mwigamba kwenda kwa Kiongozi Mkuu wa Chama, Zitto Kabwe.

Swali la kujiuliza hapa je; Zitto Kabwe amesalitiwa na washirika wake au yeye amewasaliti? Kwa sababu washirika wake wamekuwa wakilalamika, huku yeye akiwa ndiye kiongozi mwenye sauti ya mwisho ndani ya chama.

Hii inaleta mantiki juu ya malalamiko ya Chadema kuwa mwanasiasa huyo alikuwa akikihujumu chama, na sasa anakiongoza chama ambacho yeye ndiye taswira kuu, huku wengine wakikosa umuhimu. Udhaifu huu umechochea ACT-Wazalendo kuonekana kama chama cha mtu mmoja na kufifisha umahiri wa wengine.

Ahukumiwa Miaka 24 Jela Kwa Kuambukiza Ukimwi Wanawake 30

$
0
0
Mwanaume mmoja nchini Italia ambaye pia ni muathirika wa UKIMWI, amehukumiwa miaka 24 jela kwa kuambukiza virusi vya ugonjwa huo wanawake takriban 30, licha ya kujua hali yake.

Mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la Valentino Talluto mwenye umri wa miaka 33, alikuwa akiwashawishi wanawake hao kufanya nao ngono bila kujikinga, kwa madai kwamba amepima karibuni na ana 'allerg' na condom.

Valentino alikuwa akiwapta wanawake hao kwa kutumia mitandao ya kijamii na kuwarubuni, huku akiwa na mahusiano na wanawake zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja.

Waendesha mashtaka wa mjini Roma Italia, waliomba apewe kifungo cha maisha jela, lakini baada ya majadiliano ya masaa 12 mahakama iliamua kumfunga miaka 24 jela.

Akiwa mahakamani Talluto alielezea kujuta kwake kwa kufanya kitendo hicho, na kusema kwamba hakujua madhara ya vitendo hivyo.

Wanawawake wengi walikutwa na HIV kutokana na matatizo ya kiafya baada ya kufahamu juu kukamatwa kwa Talluto, na miongoni mwa wanawake hao mmoja ni binti aliyekuwa na miaka 14

Baba Joti Amwambia Joti, ‘Mimi Navituko Kukuzidi’

$
0
0
Baba mazazi wa Joti amemtaka mwanaye kuwa mtulivu katika maisha yake ya ndoa huku akidai yeye alikuwa navituko hata mkuzidi mtoto wake huyo lakini aliamua kutulia ili kuendesha maisha yake.

Mzee huyo amesema hayo wakati wa sherehe ya ndoa ya mtoto wake huyo iliyofanyikia Mlimani City Dar es salaam ambapo  pia amemtaka Joti kuomba msamaha pindi anapomkosea mke wake. VIDEO:

RC Makonda 'Sitaki Kusikia Viongozi wa Dini Wakisumbuliwa'

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda amewataka Viongozi wa Dini  zote Waislam na Wakristo wenye matatizo yanayohitaji msaada wa Serikali ikiwemo Migogoro na Kesi kufika Ofisi kwake ili yaweze kupatiwa ufumbuzi.

RC Makonda amesema hayo wakati wa Ibada ya uzinduzi wa Kanisa la KKKT Ubungo iliyoenda sambamba na Jubilee ya Miaka 500 ya Ujenzi wa Kanisa.

Amesema kuwa Viongozi wa Dini wanafanya kazi kubwa ya kiroho katika kuijenga Jamii Bora hivyo hawapaswi kuzungushwa na Watendaji wa Serikali pale wanapohitaji kuhudumiwa kwakuwa thamani ya kazi wanayoifanya ni kubwa.

"Mimi sio Mkuu wa Mkoa bali mimi ni Mtumishi wa Mungu katika Ofisi ya Mkoa wa Dar es salaam, Niwaombe Viongozi wote wa Dini Dar es Salaam sasa hivi msiangaike mkiwa na kesi kwenda kwa Wenyeviti wa Mtaa au Watendaji wa Mtaa, mkiwa na tatizo lolote njooni Ofisin kwangu, mimi ndio nitawatafuta hao, nisingependa kuona Kanisa au Msikiti wanasumbuliwa na Migogoro isiyoeleweka kwa misingi ya watu fulani, njoo kwenye Ofisi yangu matatizo yenu nitayamaliza mimi kwa niaba ya Rais" Alisema MAKONDA.

Aidha RC Makonda amepongeza kanisa la KKKT Ubungo na washarika kwa Ujenzi wa Kanisa la Kisasa na kuwaomba kushirikiana katika kuijenga Dar es Salaam Mpya.

RC Makonda  amewasihi Viongozi wa Dini kuendelea kuombea Taifa na Viongozi wake akiwemo Rais DR. MAGUFULI.

Kwa upande wake Askofu wa kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani DR ALEX MALASUSA amesema kazi anayofanya RC Makonda ni njema na inampendeza Mungu na kumtia moyo aendelee kuwatumikia Wananchi wa Dar es Salaam.

Katika ibada hiyo RC Makonda ameahidi kumnunulia Seti nzima ya Vifaa vya Mziki kwa mmoja wa Watoto katika kwaya ya Watoto katika kanisa hilo kwa kuonyesha kipaji cha kutumia vifaa hivyo kitendo kilichombariki RC Makonda

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..


JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.

Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Gharama za Kumtunza Faru Fausta Kupunguzwa

$
0
0
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), imeanza kulima majani aina ya lusini ambayo ni chakula cha Faru Fausta ili kupunguza gharama za kumtunza mnyama huyo.

Faru Fausta mwenye miaka 54 anahifadhiwa kwenye banda ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro ikiwa ni hatua ya kumlinda asiliwe na wanyama wengine kutokana na jicho lake kutoona.

Amekuwa akitumia bandali 250 za majani kila baada ya miezi minne yanayoigharimu mamlaka hiyo Sh5 milioni. Majani hayo hununuliwa kutoka nchi jirani ya  Kenya.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Idara ya Malisho na Usimamizi wa Wanyama NCAA, Hillary Mushi amesema mamlaka imeandaa shamba lenye ukubwa wa eka mbili na imepanda mbege za lusini. Amesema ndani ya miezi saba majani hayo yataanza kuvunwa.

Mushi amesema NCAA imechukua hatua hiyo ili kupunguza gharama za kumtunza faru huyo, ambaye amekuwa moja ya kivutio cha watalii na watafiti kutokana na kuwa ndiye faru mwenye umri mkubwa kuliko wote duniani kati ya wanaoishi maeneo ya wazi hifadhini.

Akimzungumzia Faru Fausta, daktari wa wanyama katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Athanas Nyaki amesema ililazimika kumhifadhi kutokana na kuanza kushambuliwa na fisi.

Amesema kutokana na jicho la faru huyo kutoona na kukabiliwa na uoni hafifu katika jingine, alishambuliwa na fisi na kupata majeraha.

Dk Nyaki amesema tangu faru huyo amehifadhiwa afya yake imeimarika na majeraha yamepona.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ni moja ya hifadhi chache nchini ambazo zina faru wengi, ambao wanalindwa kwa saa 24 kwa mitambo maalumu ili kuzuia wasiuawe na majangili.

Majangili wamekuwa wakiwaua faru ili kuchukua pembe zao ambazo huuzwa zaidi katika nchi za Mashariki ya Kati.

Chadema, CUF Wampa Mtihani Zitto, Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Octoba 30

$
0
0

Chadema, CUF Wampa Mtihani Zitto, Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Octoba 30

Zitto Kabwe Amwaga 'Sumu' Mbagala, Dsm

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amezindua kampeni za chama hicho za uchaguzi mdogo wa udiwani akiahidi iwapo kitachaguliwa kitaondoa hali ngumu ya uchumi na ukiukwaji wa haki.

Zitto akizungumza katika Kata ya Kijichi mkoani Dar es Salaam leo Jumapili Oktoba 29,2017 amesema wananchi watumie uchaguzi mdogo katika kata 43 nchini utakaofanyika Novemba 26,2017 kutuma salamu kwa CCM kwamba hawaridhishwi na jinsi nchi inavyoendeshwa.

Amesema mtu akitaka kujua uchumi unasinyaa, aangalie alikuwa akipata shilingi ngapi na sasa anapata ngapi.

Zitto amewaomba wananchi wa Kijichi kumchagua mgombea udiwani wa ACT Wazalendo, Edgar Mkosamali ili kuwe na mabadiliko kwenye baraza la madiwani la Halmashauri ya Temeke.

Kiongozi huyo amelalamikia kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara akidai ni ukiukwaji wa Katiba na sheria za nchi na pia kuwanyima wananchi haki ya kukusanyika kwenye vyama vyao.

"Leo hii tunasubiri uchaguzi mdogo ndiyo tufanye mikutano ya hadhara. Kama hupendezwi na haya yote, onyesha chuki yako kwa kumchagua Mkosamali," amesema.

Zitto amesema chama hicho kikipewa ridhaa ya kuongoza Kata ya Kijichi kitaifanya kuwa ya mfano katika kutatua kero zinazowakabili wananchi.

"Kwa udogo na uchanga wetu tutawapa utumishi uliotukuka. Tunataka kuifanya Kata ya Kijichi kuwa ya mfano," amesema Zitto.

Akizungumzia uongozi, Kaimu Mwenyekiti wa chama hicho, Yeremia Maganja amewaeleza wananchi kwamba Jeshi la Polisi limekuwa likiwanyanyasa jambo ambalo ni ukiukwaji wa Katiba na sheria za nchi.

Maganja amesema lazima nchi iongozwe kwa misingi ya Katiba na sheria ili kuleta haki kwa jamii.

Mgombea udiwani katika kata hiyo, Mkosamali amesema anatambua matatizo yaliyopo na amejipanga kuhakikisha anayatatua.

Amesema hatalala bali atazunguka kila mahali kutafuta wafadhili kwa ajili ya kuleta maendeleo kwenye kata hiyo.

Kutana na Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed Kutoka Bagamoyo...Ana Dawa za Kurudisha Mapenzi na Zingine Nyingi

$
0
0

MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

USHAURI: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.

Baada ya Flora, Miss Tanzania..Skendo ya Mbasha na Mke wa Mtu Yatikisa

$
0
0
Baada ya kumwagana na mzazi mwenzake, Flora Mbasha kisha kudaiwa kuanzisha uhusiano na Mshiriki wa Miss Tanzania 2008, Jacqueline Chuwa na kumwagana, muimbaji wa Nyimbo za Injili, Emmanuel Mbasha amejikuta akitikisa kwa skendo ya kuhusishwa na mke wa mtu.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo, kwa muda mrefu Mbasha amezua minong’ono na mwanamke huyo ambaye inasemekana ni rubani wa ndege kutokana na picha na jumbe za mafumbo ambazo Mbasha amekuwa akiziweka mitandaoni. “Mbasha kwa kweli ametikisa kwa muda mrefu. Tumefuatilia sana picha anazoposti mtandaoni hususan akiwa na huyo mdada ambaye inadaiwa ni mke wa mtu, anaonekana kabisa kuna kitu lakini pengine hataki kukiweka wazi,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:


“Kuna siku alimweka huyo mdada katika Insta (Instagram) yake, akamtakia heri ya kuzaliwa lakini watu walikuwa na maswali mengi kutokana na sifa alizompa mdada huyo japo kuna watu wengine walisema ni rafiki yake wa kawaida tu.”

Risasi Jumamosi liliperuzi katika ukurasa huo wa Instagram na kushuhudia maoni mbalimbali ya wafuasi wa mtandao huo ambao walionesha kumtilia shaka mwanamke huyo wakihoji kama kweli ni mke wa mtu iweje ajianike hadharani na mwanaume mwingine Hata hivyo, wapo wengine ambao waliwataka wale wanaotilia shaka ukaribu wao, waache kuropoka mambo wasiyoyajua kwani ‘kumuwishi’ mtu bethidei ni jambo la kawaida.

Katika mazungumzo mengine na mwanahabari wetu, chanzo chetu kilieleza kuwa, ukiachana na picha ya kumtakia bethidei mwanamke huyo, ilivuja picha nyingine ambayo ndiyo imewafanya watu wazidi kumtilia shaka Mbasha na mwanamke huyo ambaye anatajwa pia kuwa na mkwanja mrefu. “Hiyo picha ndiyo balaa.


Mbasha anaonekana yupo ndani ya gari upande wa dereva huku mke wa mtu akiwa upande wa kushoto lakini safari hii, huyo mke wa mtu kajisogeza hadi kifuani kwa Mbasha wakawa very close kama mtu na mtuwe. “Katika hali ya kawaida, marafiki tu wa kawaida au mtu ambaye mnaheshimiana, hamuwezi kugandana kwa staili ile, itakuwa kuna kitu cha ziada tu kinaendelea,” kilidai chanzo hicho. Baada ya picha hiyo kutua dawati la Risasi Jumamosi, mwanahabari wetu alijaribu kumtafuta mke huyo wa mtu bila mafanikio kwani simu yake ya mkononi haikuweza kupatikana.

MBASHA ANASEMAJE?
Alipoulizwa Mbasha kuhusu mwanamke huyo na kutumiwa picha yake, alikiri kumfahamu kama rafiki yake lakini akaweka wazi kuwa hana uhusiano wowote mbaya. “Tafadhali sana jamani naomba muwe waungwana, huyo dada tunaheshimiana sana na siwezi kufanya kitu chochote kibaya na ukizingatia mumewe pia tunaheshimiana, ngoja nikutumie picha ya yeye na mumewe.

Nawaheshimu sana jamani hao,” alisema Mbasha na kumtumia mwandishi wetu picha mwanamke huyo akiwa na mumewe. Hata hivyo Mbasha hakuwa tayari kumuelezea kwa undani mwanamke huyo, mwandishi wetu alipotaka kumfahamu zaidi.


TUMEFIKAJE HAPA?
Kabla ya kuzagaa skendo hiyo ya mke wa mtu, awali Mbasha aliishi kwenye ndoa na muimbaji wa muziki wa Injili, Flora na kufanikiwa kupata mtoto mmoja kisha wakaachana baada ya Mbasha kudaiwa kumbaka shemeji yake ambapo kesi iliunguruma na hatimaye kukutwa hana hatia. Walipomwagana, Flora aliolewa na mtu mwingine lakini kwa upande wa Mbasha, hakuwahi kutangaza mchumba wake rasmi licha ya kudaiwa kuanzisha uhusiano na Jacqueline Chuwa ambaye pia inadaiwa hawakudumu

Ndoa ya Joti Yamponza Padri.....

$
0
0

DAR ES SALAAM: Wakati ndoa ya mchekeshaji Lucas Lazaro Mhuvile almaarufu Joti ikitikisa katika Jiji la Dar, wikiendi iliyopita, padri aliyefungisha ungano hilo ameingia matatani baada ya baadhi ya waumini kuhoji kiduku cha bwana harusi kanisani.

Joti, mmoja wa wachekeshaji wa Kundi la Orijino Komedi, alifunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi aitwaye Tumaini Salehe katika Kanisa Katoliki-Magomeni jijini Dar, Jumamosi iliyopita huku akiwa amenyoa kiduku (nywele zinazobaki katikati ya kichwa huku za pembeni zikiwa zimenyolewa), kitendo ambacho kiliwafanya baadhi ya waumini waliojazana ukumbini hapo kupigwa na butwaa. “Sasa hivi ndiyo nini tena jamani? Yaani kweli padri anaruhusu hili jambo linafanyika kanisani?

Huu si mtindo wa vijana wa kihuni wanaouonesha huko mitaani, unaruhusu hili jambo au kwa sababu huyu ni kijana maarufu?” Alihoji mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mama Baby.

Licha ya Mama Baby, muumini mwingine ambaye naye alikuwepo kanisani hapo, alisema kuwa, kitendo cha kuruhusu watu kuoa wakiwa na nywele za mitindo ya kihuni kama vile siyo sawa, kwani ni rahisi kuruhusu vitu vingine visivyo vya kimaadili kufanywa na vijana hasa wa kizazi cha sasa.
Ijumaa Wikienda lilikuwepo kanisani hapo hivyo lilimfuata padri aliyefungisha ndoa hiyo, Father Paul Sabuni ili kuzungumzia shaka hiyo ya baadhi ya waumini, ambapo alisema kuwa, kiduku hakijawahi kuwa tatizo kwa Kanisa Katoliki.

“Kanisa haliangalii mavazi au namna mtu alivyo, kanisa linaangalia moyo wa mtu, kama roho yake iko safi hicho ndicho tunachokitaka, suala la kiduku halina nafasi kwetu, tunashughulika na imani yake, si muonekano wala mavazi yake, hao wanaofikiri hivyo wanapaswa kupewa somo.

“Nachukua nafasi hii kumpongeza sana Joti kwa uamuzi sahihi aliofikia, kitendo chake cha kuamua kufunga ndoa ni cha kupongezwa na kinachopaswa kuigwa na mastaa wengine.

“Kwa ustaa wake angeweza kuendelea kuishi maisha ya bila ndoa na kila kitu kingekwenda, lakini amefanya jambo la busara sana kuchukua uamuzi wa kuoa ili atulie na mkewe,” alisema padri huyo.

Vinginevyo, mamia ya watu waliohudhuria harusi hiyo walipagawa na jinsi muigizaji huyo alivyokuwa kivutio machoni mwao, kwani wengi wa waliosikia kuhusu harusi hiyo, walijua ni matangazo kama ambavyo imewahi kutokea mara kadhaa huko nyuma.

Kwa muda wote wa shughuli hiyo kanisani hapo na hata kwenye Ukumbi wa Mlimani City, watu hao walionekana kufurahia na mara kadhaa, Joti alifanya vituko vya hapa na pale katika kukoleza tukio hilo, akiwa ni memba wa pili wa kundi hilo kupata jiko, baada ya Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ kufanya hivyo miezi kadhaa iliyopita.

Stori: Imelda Mtema, Ijumaa WIKIENDA

Ushindi wa Anthony Joshua dhidi ya Takam wazua utata

$
0
0
Jana usiku kulikuwa na pambano kubwa la masumbwi kati ya Bondia Muingereza, Antony Joshua na bondia  Carlos Takam kutoka Cameroon. Ambapo Joshua alimaliza pambano kwa kumtwanga Takam kwa TKO iliyoleta utata kwa mashabiki.

Joshua alipata ushindi wa TKO kunako raundi ya 10 kwa refa kusimamisha pambano hilo baada ya Takam kuvuja damu nyingi usoni.

Watu wengi waliohudhuria kwenye pambano hilo walimzomea mwamuzi wa pambano hilo wakidai Takam alikuwa bado ana nguvu ya kupambana japokuwa alikuwa amepasuka usoni.

Mashabiki wengi wa Takam wanasema refa angempa muda bondia huyo kufutwa damu ili aendelee na pambano kwani alikuwa bado na nguvu za kurusha ngumi hivyo wanaamini mwamuzi huyo alimaliza pambano kwa matakwa.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya mpambano huo, Anthony Joshua amesema kama pambano lingeendelea angemuumiza zaidi Takam hivyo maamuzi ya refa yalimuokoa .

Huu unakuwa ni ushindi wa 20 mfululizo kwa Antony Joshua (28) baada ya kufanikiwa kutetea ubingwa wake wa mkanda wa IBF hapo jana.

Kiduku cha Joti Chazua Utata Chamuweka Matatani Padri Aliyefungisha Ndoa Yake

$
0
0
Kiduku cha Joti Chazua Utata Chamuweka Matatani Padri Aliyefungisha Ndoa Yake
Wakati ndoa ya mchekeshaji Lucas Lazaro Mhuvile almaarufu Joti ikitikisa katika Jiji la Dar, wikiendi iliyopita, padri aliyefungisha ungano hilo ameingia matatani baada ya baadhi ya waumini kuhoji kiduku cha bwana harusi kanisani.
Joti, mmoja wa wachekeshaji wa Kundi la Orijino Komedi, alifunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi aitwaye Tumaini Salehe katika Kanisa Katoliki-Magomeni jijini Dar, Jumamosi iliyopita huku akiwa amenyoa kiduku (nywele zinazobaki katikati ya kichwa huku za pembeni zikiwa zimenyolewa), kitendo ambacho kiliwafanya baadhi ya waumini waliojazana ukumbini hapo kupigwa na butwaa. “Sasa hivi ndiyo nini tena jamani? Yaani kweli padri anaruhusu hili jambo linafanyika kanisani?
Huu si mtindo wa vijana wa kihuni wanaouonesha huko mitaani, unaruhusu hili jambo au kwa sababu huyu ni kijana maarufu?” Alihoji mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mama Baby.

Licha ya Mama Baby, muumini mwingine ambaye naye alikuwepo kanisani hapo, alisema kuwa, kitendo cha kuruhusu watu kuoa wakiwa na nywele za mitindo ya kihuni kama vile siyo sawa, kwani ni rahisi kuruhusu vitu vingine visivyo vya kimaadili kufanywa na vijana hasa wa kizazi cha sasa.
Ijumaa Wikienda lilikuwepo kanisani hapo hivyo lilimfuata padri aliyefungisha ndoa hiyo, Father Paul Sabuni ili kuzungumzia shaka hiyo ya baadhi ya waumini, ambapo alisema kuwa, kiduku hakijawahi kuwa tatizo kwa Kanisa Katoliki.
“Kanisa haliangalii mavazi au namna mtu alivyo, kanisa linaangalia moyo wa mtu, kama roho yake iko safi hicho ndicho tunachokitaka, suala la kiduku halina nafasi kwetu, tunashughulika na imani yake, si muonekano wala mavazi yake, hao wanaofikiri hivyo wanapaswa kupewa somo.

“Nachukua nafasi hii kumpongeza sana Joti kwa uamuzi sahihi aliofikia, kitendo chake cha kuamua kufunga ndoa ni cha kupongezwa na kinachopaswa kuigwa na mastaa wengine.
“Kwa ustaa wake angeweza kuendelea kuishi maisha ya bila ndoa na kila kitu kingekwenda, lakini amefanya jambo la busara sana kuchukua uamuzi wa kuoa ili atulie na mkewe,” alisema padri huyo.

Vinginevyo, mamia ya watu waliohudhuria harusi hiyo walipagawa na jinsi muigizaji huyo alivyokuwa kivutio machoni mwao, kwani wengi wa waliosikia kuhusu harusi hiyo, walijua ni matangazo kama ambavyo imewahi kutokea mara kadhaa huko nyuma.

Kwa muda wote wa shughuli hiyo kanisani hapo na hata kwenye Ukumbi wa Mlimani City, watu hao walionekana kufurahia na mara kadhaa, Joti alifanya vituko vya hapa na pale katika kukoleza tukio hilo, akiwa ni memba wa pili wa kundi hilo kupata jiko, baada ya Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ kufanya hivyo miezi kadhaa iliyopita.
Chanzo Global Publishers

Kidato cha Nne Waanza Kufanya Mtihani wa Taifa Leo

$
0
0
Kidato cha Nne Waanza Kufanya Mtihani wa Taifa Leo
WATAHINIWA wapatao 385,938 wameanza kutafanya mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne leo Jumatatu, Oktoba 30, 2017 kote nchini. Akizungumza jana Jumapili, Oktoba 29,2017 Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde alisema kati ya watahiniwa hao, 323,513 (School candidates) ni wa shule na 62,425 ni wa kujitegemea (Private candidates).
Dk Msonde alisema mitihani hiyo itaanza leo Oktoba 30, 2017 na kumalizika Novemba 17, 2017 huku akieleza kuwa maandalizi ya mitihani yameshakamilika na mitihani imeshafika kwenye vituo.
Aidha Msonde alizitaka kamati za mitihani za mikoa na halmashauri kuhakikisha utaratibu wa uendeshaji wa mitihani hiyo unafuatwa huku akiwataka wanafunzi kuacha vitendo vya udanganyifu wakati wa kufanya mitihani kwa kuwa wanaweza kufaulu bila kufanya hivyo.
“Mliyojifunza yanatosha fanyeni mitihani kwa kufuata utaratibu uliowekwa, baraza halitasita kuwafutia mitihani wote watakaojihusisha na udanganyifu, wasimamizi wa mitihani wajiepushe na vitendo vya udanganyifu, atakayekiuka atachukuliwa hatua za kisheria.” alisema Msonde.
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live




Latest Images