Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Hali si Shwari Ray na Johari sasa Kugawana Hadi Nguo za Ndani

$
0
0
Hali katika kampini ya RJ inayoongozwa kwa ubiya kati ya Vicent Kigosi ( Ray) na Blandina Chagula ‘Johari’, inazidi kuwa tete kwa kile kinachoelezwa kuwa johari hataki kufanya kazi pamoja na ‘mke mwenza’  Chuchu Hans.

Chanzo hicho ambacho kipo karibu na wasanii hao kilisema kuwa mwezi mmoja uliopita Johari na Chuchu, walikuwa katika kuelekea kuelewana ambapo johari, alishakubali yaishe kuwa Ray wake ameshapokonywa na mtoto huyo wa Kitanga .

Mnyetishaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya Johari kuwa katika hali hiyo,ndipo Chuchu alipoanza kutanua makucha yake ndani ya kampuni kwa kujifanya ni mmoja kati ya wakurugenzi wakati ukweli haupo hivyo.

Chanzo hicho kilizidi kusema kuwa imefikia hatua Chuchu, kaanza kutoa amri kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo bila ya kupata kibali kutoka kwa wakurugenzi waasisi ambao mtaji wao unadaiwa kutokana na  Johari ‘kumpiga’ changa la macho mfanyabiashara maarufu kutoka mkoani Mbeya.

Mpashaji huyo alizidi kusema kuwa bifu liliibuka upya mkoani Dodoma, ambako Ray na Johari walikwenda katika ziara ya Kilimanjaro Music Awards Tour, na mashabiki wao kuwataka wapande jukwaani kwa pamoja.

Mtoa habari hiyo alisema kuwa kuwa kutokana na hali hiyo, ndipo Chuchu alipoanzisha bifu la chinichini lililopelekea hadi sasa kwenye kampuni hiyo kuzuka mtafaruku mkubwa huku Johari, akitaka kujitenga kabisa na Ray lakini kinachomkwamisha ni pesa zake nyingi alizowekeza.

Inadaiwa  kuwa Johari amekuwa mkali sana sasa hivi akimtaka mkurugenzi mwenzake Ray, wagawane kila kitu mpaka nguo za ndani walizonunua kwa pesa za kampuni yao hiyo.

Katika kufuatilia habari hizo ili kupata ukweli kuhusiana na timbwili hili mwanahabari wetu aliwasaka wote kwenye simu zao za mkononi, lakini wote hawakutaka kutoa ushirikiano kwa kile walichokieleza kuwa wapo bize na maswala binafsi.

Hausigeli Adaiwa Kumuua Mwajiri Wake kwa Kumchoma Kisu

$
0
0
Karani wa Mahakama ya Wilaya ya Singida, Asha Juma(24), ameuawa kwa kuchomwa kisu na mfanyakazi wake wa ndani.

Tukio hilo limetokea jana saa 4:00 asubuhi eneo la Sabasaba katika kata ya Utemini mjini Singida.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alisema mauti yalimfika karani huyo mara baada ya kuchomwa kisu sehemu ya titi la kulia na mfanyakazi huyo wa ndani aitwaye Valetina Kerenge(17).
Msichana huyo ambaye ni mwenyeji wa mkoani Mwanza wilayani Ukerewe,  inasadikiwa alilifanya tukio hilo wakiwa ndani na baada ya hapo alipata kiwewe na kukimbilia nje ya nyumba aliyokuwa akikaa na kwenda kwa majirani kuomba msaada.
Inasemekana wakati juhudi za majirani za kunusuru uhai wake zikifanyika ili kumuwahisha hospitali kwa matibabu, ghafla marehemu huyo alianguka chini na kufariki papo hapo.

“Imesikitisha maana chanzo halisi hakijajulikana, maana msichana huyu alipoona mambo siyo alikimbia,” alisema Kamanda Kamwela.
Kamanda alisema tayari msako mkali wa polisi ulifanikisha kumpata majira ya saa 8 mchana akiwa katika harakati za kutoroka maeneo ya uwanja wa ndege.
Mwili wa marehemu ulipelekwa katika Hospitali ya Mkoa wa Singida kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi, na baada ya kuchunguza ndugu wa marehemu watakabidhiwa kwa taratibu za kuusafirisha mwili huo kuelekea mkoani Shinyanga kwa mazishi.
Jeshi la polisi linamshikilia msichana huyo kwa ajili ya mahojiano.

Pinda Awaagiza UKAWA Kurudi Bunge la Katiba; Asema Sio OMBI

$
0
0
Ametoa agizo hilo leo Iringa katika Jubilee ya miaka 25 ya uaskofu wa Ngalalekumtwa katika kanisaa katoliki Iringa. Amesema ukawa lazima wahakikishe wanarudi bungeni kujadili.katiba na kusisitiza sio ombi kwani wananchi wanataka hivyo.

Amesisitiza kuwa endapo ukawa watakwamisha upatikanaji wa katiba bora, ataongoza kampeni nchi nzima kuwataka wananchi kuikataa katiba wakati wa kura ya maoni na kuwanyima kura wapinzani.katika uchaguzi mkuu ujao

Maskini Yule Mwanafunzi wa Chuo Aliyechomwa Moto Kwa Kuzaniwa Mwizi Afariki Dunia

$
0
0
Daniel Anael Lema, aliyekuwa mwanafunzi wa mwaka wa nne wa shahada ya sheria katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Mt. Augustino, Tawi la Iringa (Ruaha University College – RUCO), amefariki dunia baada ya kushambuliwa kisha kuchomwa moto na wananchi wenye hasira akidhaniwa kuwa mwizi.

Tukio hilo lilitokea Juni 24, 2014, majira ya saa 5 usiku ambapo inadaiwa kuwa Daniel alikuwa ametoka kuangalia michuano ya Kombe la Dunia, akawa anatafuta chakula cha jioni ambapo alipofika kwenye mgahawa mmoja ambao ulikuwa umefungwa, aliingia ndani ambapo binti aliyekuwa amelala ndani ya mgahawa huo, alianza kupiga kelele za mwizi zilizowakusanya wananchi wenye hasira kali.

Wananchi hao walianza kumshambulia Daniel wakiongozwa na mlinzi mmoja wa jamii ya Kimasai, baada ya kuzidiwa na kichapo wananchi hao walimmwagia mafuta ya taa na kumchoma moto kisha wote wakatoweka.

Mwanafunzi huyo aliokolewa na madereva bodaboda ambao walizima moto na kumkimbiza katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa lakini siku kadhaa baadaye alifariki dunia.

Mwili wa marehemu umeagwa mapema leo katika hospitali hiyo tayari kwa safari ya kuelekea mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika kesho Jumatano.
Daniel Anael Lema, aliyekuwa mwanafunzi wa mwaka wa nne wa shahada ya sheria katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Mt. Augustino, Tawi la Iringa (Ruaha University College – RUCO) enzi za uhai wake.

Beyonce Achochea Moto Tetesi za Usaliti wa Jay Z, Abadili Mashairi ya wimbo na Kumlilia

$
0
0
Beyonce Knowles amechochea kuni katika moto wa tetesi za usaliti wa mapenzi wa Jay Z baada ya kubadili kidogo mashairi ya wimbo wake ‘Resentment’ uliopo katika albam yake ya  B’Day aliyoitoa mwaka 2006.

Wakati anaimba Resentment kwenye On The Run Tour, huko Ohio alibadili miaka inayoitaja kwenye wimbo halisi na kuitaja miaka ya uhusiano wake na Jay Z, yaani alitoa miaka 6 na kuwa 12 katika wimbo huo wenye kilio cha usaliti.

Kitendo hicho kilizua shangwe zaidi kutoka kwa mashabiki waliofahamu kabisa kuwa mwaka 2002 enzi za Bonnie&Clyde ndio mahusiano ya wawili hao yalichipua.

Wimbo halisi unasema:

"Been ridin' with you for six years why did I deserve/ To be treated this way by you.”

Lakini Beyonce alibadili miaka na akasikika akiimba:

"I know she was attractive but I was here first/ Been ridin' with you for 12 years why did I deserve/ To be treated this way by you, you/ I know your probably thinking what's up with Bee/ I been crying for too long what did you do to me."

Hata hivyo, wanandoa hao huonekana wakiwa wenye furaha na mtoto wao kila baada ya show zao.

Ndege Yaanguka Juu ya Paa La Nyumba na Kuuwa Watu Wanne Hapo Hapo

$
0
0
Taarifa kutoka Kenya naambiwa watu wanne waliokua kwenye ndege iliyokua ikipaa kutoka uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta Nairobi kuelekea Mogadishu Somalia wamefariki dunia baada ya Ndege hiyo kuanguka katika eneo la Utawala dakika chache baada ya kupaa,
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya July 02 na inaaminika kwamba ndege hiyo ilikua iondoke mapema kusafirisha zao la Mirungi na bidhaa zinginezo kuelekea Somalia.
Walinzi wawili walijeruhiwa mmoja ametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani huku mmoja amelazwa katika hospitali ya mama Lucy,kwa mujibu wa mkuu wa polisi Jijini Nairobi Benson kibue amethibitisha ajali hiyo na kusema kuwa Ndege hiyo yenye nambari 5Y-CET ilianguka kwenye paa la jengo la kibiashara likijaribu kutua ghafla na kushika moto papo hapo likiteketeza watu wanne waliokua ndani.
Polisi wanaendelea na uchunguzi kwenye mabaki ya ndege hiyo kuona iwapo kuna waasika zaidi.

Diamond Awatia Kiwewe Nelly na Chriss Brown, Wagombea number zake za Simu

$
0
0
Stori: Andrew Carlos na Musa Mateja

Next level! Staa wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa anafanya kweli kimataifa, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ameandika historia kwenye Tuzo za Black Entertainment Television (BET) 2014 huku akiwatia kiwewe mastaa wakubwa kama Cornell Iral Haynes ‘Nelly’, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ na wengine kibao.

Tukio hilo lilijiri usiku wa kuamkia Jumatatu wiki hii kwenye Ukumbi wa Nokia Theatre jijini Los Angeles, Marekani ambapo Diamond alikuwa ameteuliwa kuwania Kipengele cha Mwanamuziki Bora kutoka Afrika akiwa sambamba na mwanamuziki Davido (Nigeria), Mafikizolo (Afrika Kusini), Tiwa Savage (Nigeria), Toofan (Togo) na Sarkodie (Ghana).

TUZO YAENDA KWA DAVIDO
Tuzo hiyo haikuwa bahati kwa Diamond kwani ilikwenda kwa Davido.
Licha ya kukosa tuzo hiyo, yapo mengi ambayo Diamond ameweka historia au rekodi katika ‘event’ huku kuunganishwa na mastaa hao ikiwa topiki muhimu.

MCHUMBA WA CHRISS BROWN AMSHOBOKEA
Katika hali ya kushangaza, mwanamitindo maarufu Marekani ambaye ni mchumba wa Chris Brown, Karrueche Tran alionekana kumshobokea Diamond mara alipokutana naye uso kwa uso.
Karrueche alijikuta hajiwezi alipokuwa  akimhoji Diamond ambapo moja kwa moja alimvutia kipaza sauti na kuanza kumpiga maswali huku akionesha kuvutiwa naye kwa muonekano aliokuwa nao.

Karrueche alikuwa akijichekeshachekesha huku akimhoji kuhusiana na mwanamuziki ambaye Diamond anamkubali ambapo alijibu ni Chris Brown, wote wakajikuta wakiangua kicheko.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Karrueche muda wote aliendelea kumshangaa na mwisho wa siku wakabadilishana namba za simu.

MASTAA MACHO JUU
Ulipofika wakati wa utoaji tuzo katika kategori ya Mwanamuziki Bora kutoka Afrika, lilipotajwa tu jina la Diamond kutoka Tanzania na wimbo wake wa Number One RMX, mastaa kibao walionesha kushangaa na ndipo macho yote yakahamia eneo aliokuwa amekaa.
Wengi walionekana kutoa maneno ya chinichini sambamba na kumuoneshea vidole wakionesha kumkubali kwa kutinga mjengoni hapo.

NELLY, CHRIS BROWN WAINGIWA KIWEWE
Wakati Diamond anaingia ukumbini, mastaa mbalimbali duniani walionekana kumshangaa na kati yao alikuwa ni Nelly ambaye aliushikilia mkono wa Diamond kwa sekunde kadhaa akitaka waendelee kupiga stori.

Wakiwa katika zulia maalum jekundu, Nelly aliyewahi kutamba na wimbo wake maarufu wa Dilemma alionekana na kutaka kumfahamu zaidi Diamond.

Kila sehemu aliyokuwa akienda, Nelly hakutaka kumuacha na alionekana kuambatana naye kwa kumng’ang’ania mkono kila kona akipiga naye picha na kuzunguka eneo lote wakiwa pamoja.
Naye Chris Brown ambaye aliangusha bonge la shoo alionekana kumshangaa Diamond huku akitamani kuendelea kukaa naye.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu ukumbini humo, maswali mengi yaliibuka kuwa iweje, kwa Mtanzania kama yule kukanyaga katika mjengo mmoja na mstaa wa dunia.

TYSON, MAYWEATHER WADUWAA
Mabondia maarufu duniani akiwemo Floyd Mayweather na Mike Tyson walijikuta wakiduwaa kwa kumshangaa kwa kila hatua aliyokuwa anapiga. Macho yao hayakuwa mbali naye na hata katika zulia jekundu, Maywearher, baada ya kumaliza kupiga picha akiwa na mkewe alimfuata Diamond na kuongea naye mawili-matatu kuonesha kukumkubali.

MASTAA KIBAO WAGOMBEA NAMBA
Wakati shoo hiyo ikiendelea baadhi ya msataa waliokuwa pembeni na  Diamond walionekana kumfagilia na hata wengine kuomba namba za simu kwa malengo tofauti ikiwa ni pamoja na kutaka kufanya naye kolabo katika siku za usoni.

LUPITA, DIAMOND USO KWA USO
Staa kutoka Kenya ambaye anatingisha katika soko la filamu za Hollywood, Marekani kupitia filamu ya 12 Years A Slave, Lupita Nyng’o alikutana uso kwa uso na Diamond wakiwa wote wametokea Ukanda wa Afrika ya Mashariki.

Walionekana kuwa na furaha kwa pamoja na ikumbukwe kuwa Lupita amejizolewa umaarufu mkubwa ambapo hata Jay-Z na Rihanna waliwahi kuandika kupitia kurasa zao kwenye mitandao ya kijamii wakioneshwa kumkubali kwa kazi zake.

Mastaa wengine wakubwa aliokutana nao ni pamoja na Ashanti, DJ khalid, Jeniffer Hudson, French Montana, John Legend, Paris Hilton na wengine kibao

HABARI NYUMA YA PAZI
Duru za kibahari zilieleza kwamba mambo yote yanayokea kwa Diamond kuna nguvu kubwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye hivi karibuni alimkutanisha mtoto huyo wa Tandale na meneja wa wanamuziki wakubwa duniani, Tremaine Neverson ‘Trey Songz’ na Sean Michael Leonard Anderson ‘Big Sean’, ili kufanya nao kazi.

“Siyo jambo rahisi na bado milango itazidi kufunguka zaidi kwani JK aliahidi kumsaidia. Kwa kuunganishwa na mastaa wakubwa duniani sasa hivi utasikia amehamia Marekani kutusua mtonyo,” alisema mmoja wa wasanii wa Bongo Fleva ambaye naye anafanya vizuri.


Akizungumza na mwanahabari wetu kutoka jijini Los Angeles, Diamond alisema kuwa hakuamini jinsi alivyopokelewa na mastaa wakubwa ambao hakutarajia kukutana nao uso kwa uso.
“Sasa najua ndoto itatimia. Mastaa wakubwa lakini wamenionesha upendo wa ajabu. Naona wasanii wote duniani wanapendana sana. Jamaa hawana ubaguzi. Walinichangamkia sana utadhani tunafahamiana.

“Kuna mengi nafanya nao lakini siwezi kuwataja kwa sababu si unawajua Wabongo?
“Lakini nikidondoka tu Bongo naachia video mbili kali sana, mashabiki wangu wasikilizie.
“Kuhusu kukosa tuzo, mimi naona ni mwanzo mzuri. Inanipa hasira ya kutengeneza muziki mzuri utakaopendwa na watu wengi duniani. Tusikate tamaa, ni mwanzo mzuri. Pia asiyekubali kushindwa si mshindani,” alifunguka Diamond akimshukuru Mungu kwa yote anayomtendea kila kukicha kisha watu wanampa sapoti.

SASA LEVO ZA AKINA HASHEEM THABEET
Kwa sasa Diamond anakuwa ni staa mwingine wa Kibongo wa kimataifa akitanguliwa na staa wa NBA, Hasheem Thabeet, Modo Flaviana Matata na wengineo.

Naomba ushauri..Jamaa Ananitaka Kimapenzi Nikimwangalia Ananishinda Kila Kitu kwa Uzuri..Nimkubalie?

$
0
0

Jamani mie Mdada wa Hapa Mjini basi jamani eti huyo jamaa kanitumia Message Facebook eti anataka kuwa boyfriend wangu eti ananipenda sana baada ya kuona picha zangu, Nashindwa hata nimwambiaje maana japo ni mwanaume ila kanishinda mpaka uzuri , Lips zimeenda shule nyusi ndio usiseme...Je nimkubalie ?

Wakenya Wataka Vera Sadika Ashiriki Big Brother ila Waweze Ona Makalio yake Akiwa Anaoga(Shower Hour)

$
0
0
Wakenya Wameanzisha Kampeni Online wakitaka Vera Sadika Mrembo Ambae ni Nguzo huko Kenya kwa wakati huu Ashiriki Shindano la Big Brother Afrika Ambalo litaanza Hivi Karibuni ...

Hizi Ni baadhi ya Tweets

-Si Vera aende #bba... Will be waiting for shower hour with vaseline on ny hand.

-They should take Vera Sidika. & Rama...Lol"@JoeWMuchiri: I wonder which person will rep Kenya in BBA this year."

-Vera sidika @vee_beiby will be auditioning BBA  this year,just can't wait to watch it,this is gonna be einteresting.....

-Vera Sidika is BBA material...i Cant Wait too see Her Behind

Maximo Aanza kazi Yanga Kwa Mikwara Atangaza Week Nne za Hatari, Tegete Apewa Majukumu ya Taifa Stars

$
0
0
KOCHA Mkuu mpya wa Yanga, Mbrazili, Marcio Maximo, jana alianza kazi yake kwa mkwara mzito huku kila aliyehudhuria akionyesha kutikisa kichwa kuikubali.

Maximo majira ya saa mbili kamili asubuhi alikwishatua kwenye Ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam na kuanza rasmi mazoezi na timu hiyo ya Jangwani na kuwakusanya tena wachezaji wake saa tisa kamili kwenye Uwanja wa Bandari Tandika kwa mazoezi ya takribani saa mbili.

Maximo ambaye amekuwa akifanya mambo yake kisasa, alianza kama kawaida yake huku akiwasimamia wachezaji wake kunyoosha viungo na baada ya hapo kuanza kuwakimbiza.
Wachezaji wa Yanga ambao wengi walikuwa wametoka kwenye mapumziko, walikimbizwa kwa umbali wa kilomita 1.5 mara mbili kwenda na kurudi huku kocha huyo akiungana nao akiwa na kocha wa vijana, Salvatory Edward.

Maximo alionyesha kuwa yupo fiti pamoja na kwamba umri umeenda baada ya kuanza na wachezaji hao na kumaliza nao mbio bila kupumzika sehemu yoyote ambapo walitumia dakika 30.
Mara baada ya kumaliza kukimbia, wachezaji wa Yanga walitakiwa kupumzika kwa kunywa maji na kunyoosha viungo na kuanza zoezi la kuruka koni na kukimbia mbio fupi ambazo zilichukua dakika 30, msimamizi akiwa ni kocha msaidizi, Leonardo Neiva.

Kama ilivyo kawaida yake, Maximo aliendelea na utani wake huku akichombeza kwa maneno ya Kiswahili; tupo pamoja, harakaharaka, ongeza mwendo, usichoke na mengine mengi.
Baada ya kumaliza kuruka koni, Maximo alionyesha kuridhika na kuwaita pamoja na viongozi wengine waliokuwepo uwanjani hapo na kuzungumza nao.

Baada ya mazungumzo kocha huyo aliwakusanya wote na kuomba dua na kutawanyika ambapo aliwapa ruhusu ya kuzungumza na waandishi, lakini yeye akapanda prado lake na kutimka.
Hata hivyo, saa tisa alasiri kocha huyo alilianzisha tena na mastaa wake kwenye Uwanja wa Chuo cha Bandari, Temeke ambapo alianza kwa kuwazungusha uwanja raundi tatu huku kukukiwa na mashabiki kibao.

Mashabiki hao walishuhudia mazoezi mazuri huku kocha huyo akiwataka wachezaji wake kufanya kila kitu kwa uhakika.
Mashabiki waliofurika uwanjani hapo walionekana kushangilia kwa nguvu kubwa kila Mbrazili Coutinho alipokuwa akigusa mpira na wakati Maximo alipokuwa akiwafokea wachezaji wake pale walipofanya vibaya.

Mashabiki waliokuwepo uwanjani hapo walionekana kumsifia kocha huyo, huku wengi wakiamini kuwa kama ataendelea hivyo, Yanga itakuwa bonge la timu.
Maximo aliongoza mazoezi hayo kwa ustadi wa hali ya juu, huku msaidizi wake naye akiwa moto kwenye kila kitu ikiwa ni pamoja na kukimbia, kupiga pasi na kukaba.

Hata hivyo, Coutinho kuna muda alidondoka na kuchubuka mguuni, lakini bado aliendelea kukipiga hali iliyowafanya mashabiki washangilia.

Mazoezi ya jioni yalikamilika saa 11:45 jioni na kukamilisha saa nne za Maximo za siku ya kwanza, huku Coutinho akifunga mabao mawili.

Wachezaji wa kikosi cha kwanza waliohudhuria mazoezi ya jana ni Juma Kaseja, Ally Mustapha ‘Barthez’, Juma Abdul, Salum Telela, Hussein Javu, Said Bahanuzi, Omega Seme, Rajab Zahiri, Mbuyu Twite na  Saleh Abdallah pamoja na wa kikosi cha pili..

Ugomvi wa Ray C na TID, Ray C Umejitakia Mwenyewe Kutukanwa

$
0
0
Jana kwenye Mitandao mbali mbali hasa blogs na Insta Kulienea habari kuwa Tid Amemtukana Ray C matusi ya Nguoni Baada ya Ray C Kupost kwenye Picha aliyopost TID Instagram Akimwomba Waongee.......Ni Ukweli Usiopingika kwamba TID alikasirika baada ya Kuambiwa Hivyo Hadharani Kwani Ray C Kwa sasa anajaribu kuwashawisha wasanii mbali mbali wanaotumia Madawa ya Kulevya ili Waache kwa Kuhudhuria Hospitalini , Hivyo kauli hiyo ilikuwa ni mwiba kwa Msanii TID na Badala ya Kujibu Vizuri naye alianza kuporomosha matusi ....

My Take:
Najiuliza Kwanini Ray C hakutafuta hata number yake ya simu ama kumtafuta Face to Face na Kuongea na Kumshawishi, Ndio tunajua kwamba TID anatumia ila Si kumwambia Hadharani Kiasi Kile Tena Kwenye Profile yake ya Instagram , Hata kama Hakumwambia Direct ila Ile Kauli si nzuri kwa mtu Ambae Tayari Ameathirika...So Nadiriki Kusema Ray C Alijitakia Mwenyewe!

Kwanini Sheria Ngowi Kumvalisha Diamond Why Not Martin Kadinda?

$
0
0
Diamond At BET, Dressed by Sheria Ngowi
Kama Kumbu kumbu zangu zipo Vizuri nakumbuka Mtu wa Kwanza kabisa kumvisha Diamond na kuanza kupendeza alikuwa Martini Kadinda na zile suti zake za Single Buttons, Lakini Siku zinavyokwenda naona huyu Kardinda simsikii Tena kwenye Nguo kiivyo

Kwa nilivyotegemea kwa ukaribu aliyonao kwa Diamond kwa sasa Yeye ndio Angechukua Hiyo Fursa ya Kumtengenezea Nguo Mbongo Flava Huyo Hasa Kwenye Hizo Awards za MTV na BET lakini Katika Hizo Awards zote Mbili Amevalishwa na Sheria Ngowi ....Sikatai Sheria ni Mzuri Sana ila Najiuliza tu Kwa Huyu kaka naona Kama Umeneja Kwa Wema Umemuondolea Ndoto za Kuwa Designer Mkubwa..



Diva Loveness Ajifananisha Yeye Mwenyewe na Tony Braxton

$
0
0
Leo Diva Ameamka na Mpya Huko Instagram kwa Kupost Picha mbali mbali akijifananisha na Mwanamuziki wa Marekani Anayejulikana kama Tony Braxton , katika Picha Moja Ameandika

"Kipindi cha Slave Trade Kuna Babu au Bibi Alikuwa Tanga..Wewe ni ndugu yangu Nahisi lol"

Haya Jamani Watu Wawili Wawili ....Je wewe unafanana na nani?

Kutana na Golkipa wa Ajabu Kombe la Dunia mwenye Vidole Sita Mkononi

$
0
0
Brazil. Inawezekana kuwa Mexico imetolewa ‘kikatili’ kwenye hatua ya 16 bora ya fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil.

Visa vya winga wa Uholanzi, Arjen Robben kujiangusha na hatimaye kupata mkwaju wa penalti vilikatisha safari ya Mexico.

Hata hivyo, wakati ikirejea Mexico City, timu hiyo imeacha simulizi kubwa kwenye fainali hizo, na hasa juu ya umahiri wa kipa Guillermo Ochoa langoni.

Ochoa, ambaye ana umri wa miaka 28, aliwazuia washambuliaji wengi kutikisa nyavu zake, wakiwamo wa Brazil walioongozwa na Neymar katika mchezo ulioisha kwa timu hizo kutofungana.

Kipa huyo alikuwa kizingiti kwenye lango la Mexico, lakini ana kitu cha ziada; ni mwanadamu mwenye vidole sita vya mkono wake  wa kulia.

Ochoa, mwenye umri wa miaka 28 ambaye msimu ujao hana timu bada ya klabu yake ya sasa Ajaccio ya Ufaransa kutompa mkataba mpya, alikuwa kivutio kwa mashabiki wa nchi hiyo kiasi cha wengine kumwita “rais”

Ameichezea klabu hiyo mechi zaidi ya 100. Umahiri wake langoni utaweza kumpatia timu.

Hakuna shaka, klabu za barani Ulaya kama Arsenal na Manchester City zimevutiwa naye, ingawa yeye anapenda kubakia Ufaransa.

Safari yake ya kwenda Ufaransa mwaka 2011 ilikumbwa na kiwingu baada ya kuhusishwa na matumizi ya dawa za kulevya. Alikuwa miogoni mwa nyota watano waliokumbwa na kashfa hiyo. Alitiwa hatiani kwa kutumia dawa aina clenbuterol na kufungiwa.

Chadema: Ofisi ya Msajili inatumiwa wa Vyama Inatumiwa Vibaya na Wasaliti wa Chama

$
0
0
Mvutano mpya umeibuka baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kumvaa Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kikidai ofisi yake inatumiwa na wasaliti wa chama hicho.

Pia, chama hicho kimemtaka Jaji Mutungi ajitokeze hadharani kubainisha iwapo yeye ndiye aliyemtuma msaidizi wake, Sistyl Nyahoza kutangaza kuwa mwenyekiti wake, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa hawana sifa ya kugombea uongozi ndani ya chama hicho kutokana na kuzuiwa na katiba ya Chadema.

Jana, Nyahoza alikaririwa na vyombo vya habari akisema Mbowe na Dk Slaa hawana sifa za kugombea uongozi wa chama hicho kutokana na katiba ya chama chao kuwabana.

Alibanisha kuwa kipengele cha ukomo wa mgombea katika katiba yao ya mwaka 2006 kiliondolewa kinyemela bila idhini ya mkutano mkuu.

Nyahoza alisema katiba ya Chadema ya mwaka 2004, ilikuwa na kipengele cha ukomo wa madaraka kuwa kiongozi aliyeongoza vipindi viwili vya miaka mitano mitano, hawezi kuwania tena nafasi hiyo.

Jana, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema Jaji Mutungi hana mamlaka ya kubaini sifa za viongozi wa chama hicho, bali wenye mamlaka hayo ni wanachama wa chama hicho pekee.

Mnyika alisema mwaka 2006, katiba ya Chadema haikurekebishwa, bali iliundwa upya na kuridhiwa na mkutano mkuu wa chama na kwamba Agosti 13, 2006 ilizinduliwa na nyaraka zote alikabidhiwa Msajili wa Vyama wa wakati huo, John Tendwa.

Katika uzinduzi huo wa katiba pamoja na bendera mpya ya Chadema, Tendwa alikimwagia sifa chama hicho kwa kuonyesha mwelekeo na mwenendo mzuri na kuvishauri vyama vingine viungane nacho kuunda chama cha upinzani chenye nguvu nchini.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Mbowe alikaririwa na gazeti hili Agosti 15, 2013 akisema yalikuwa yanalenga kuimarisha mapambano ya kisiasa ya chama hicho.

Mnyika alisema: “Mkutano mkuu wa chama uliipitisha Katiba hiyo baada ya mchakato mrefu wa kukusanya maoni kutoka kwa mabaraza ya wilaya na majimbo. Hatukurekebisha katiba kama inavyoidaiwa. Ni makubaliano ya wanachama wote ambao waliafikiana na mambo yaliyotakiwa kuwamo.”

Alisema katika mchakato huo kulikuwa na makubaliano na mabishano katika baadhi ya masuala lakini suala la ukomo wa uongozi liliafikiwa na wanachama wote bila tatizo na kupitishwa kuingia katika katiba na Ofisi ya Msajili ilipelekewa fomu ya marekebisho pamoja na katiba mpya kama sheria inavyotaka... “Kama wameipoteza waseme tuwapatie katiba wairejee.”

“Tunachomtaka Mutungi ni kuheshimu katiba ya chama na kuwaheshimu wanachama wa Chadema na ayapuuze madai ya wasaliti wachache. Kama vipi asubiri aone uamuzi wa Baraza Kuu na Mkutano Mkuu ubainishe kama katiba ilivunjwa,” alisema Mnyika.

Lowassa Aweka Wazi Mali zake Aseme yeye sio Tajiri Bali ni Mfugaji tu Monduli

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema madai kwamba yeye ni tajiri hayana ukweli wowote. Amesema yeye ni mfugaji na anamiliki ng’ombe zaidi ya 800 katika Jimbo la Monduli, mkoani Arusha.

Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake wiki iliyopita mjini Dodoma.

 “Haya madai hayana hata chembe ya ukweli hata kidogo, isipokuwa mimi nadhani wananitakia mema kwa sababu ukiona jumba zuri wanasema la Lowassa, gari nzuri la Lowassa, kitu chochote kizuri wanasema cha Lowassa,” alisema na kuongeza:

“Wamesema uongo mwingi sana, mimi nasema tu nilichopata nimepata na sina utajiri kiasi hicho, lakini si mbadhirifu wa haki zangu ninazopata kama mshahara na haki nyingine.”

Alipotakiwa kutaja mali anazomiliki, Lowassa alisema: “Mimi ni mfugaji, nina ng’ombe zaidi ya 800 jimboni kwangu Monduli.”

Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli, alisema madai kwamba anamiliki utajiri uliopindukia yalianza kabla hajajiuzulu uwaziri mkuu na ilielezwa kuwa “maduka fulani” ni yake.

Alibainisha kuwa hata kampuni ya Alphatel ambayo wanamiliki kwenye familia yake iliwahi kuhusishwa na jengo kubwa lililojengwa na mtu mmoja mwenye asili ya Kiasia wilayani Kinondoni, Dar es Salaam likiitwa Alpha.

“Ikaonekana ni jengo langu, kule Mbezi kuna rafiki yangu mmoja walienda watu wakasema hii nyumba ya Lowassa. Yule bwana alitoka na bastola akawakimbiza. Mimi sina nyumba maeneo hayo,” alisema Lowassa.

Bomu la ajira

Akitaja njia za kutegua ‘bomu la ajira’ kwa vijana ambalo amekuwa akisema liko mbioni kupasuka, Lowassa alitaja maeneo mawili ambayo yanapaswa kutazamwa ili kuzalisha ajira nyingi mpya.

Alitaja kilimo akisema kinachukua watu wengi nchini. Alisema kinapaswa kutengenezewa mazingira ili vijana wanaomaliza chuo kikuu wawe tayari kuishi kwenye mazingira ya kilimo.

Breaking News:Majambazi Wavamia Basi la Mahabusu na Kuwashambulia Askari na Kutokomea

$
0
0
Breaking news: sasa hivi saa 8.15mchana.Kuna tukio hapa Tmj hospital. Majambazi wakikimbia kwa miguu wakitokea kwa Nyerere wamelishambulia basi la magereza lilobeba wafungwa na escort ya polisi kwa risasi kadhaa. Askari magereza na polisi wamejeruhiwa na majambazi yametokomea kusikojulikana. Mahabusu wanashangilia hapa na shughuli zote zimesimama hapa

Wolper 'Kuna Watoto Wanalawitiwa Majumbani Alafu Wazazi Wanayamaliza Kimya Kimya'

$
0
0
Wakati  sheria  ikizidi  kuwatia  hatiani  wale  nguli  wa  kulawiti  watoto, staa  wa  bongo  movie, Jackline  Wolper  amesema  kuwa  hata  kwa  upande  wake  huwa  anasikitishwa  na  vitendo  hivyo  kwani   kufanya  hivyo  ni  kuwatia  doa  katika  maisha  yao……

Staa  huyo  alisema  kuwa  kitendo  cha  kulawiti  mtoto  ni  cha  kinyama  na  kwamba  haoni  sababu  ya kucheka  na  watuhumiwa  bali  wanatakiwa  kufikishwa  mahakamani  ili  sheria  ichukue  mkondo  wake…

Kuna  watoto  wanalawitiwa  na  kubakwa  huko  vijijini  na  hata  hapa  mjini, lakini  unakuta  wazazi  wanazungumza  nyumbani  na  kuyamaliza  bila  kujua  yule  mtoto  ameathirika  kiasi  gani, inauma  sana, ni  lazima  wafikishwe  mahakamani  ili  sheria  ichukue  mkondo  wake”,alisema  Wolper

Majambazi Waliomuua Sista wa Kanisa Katoliki Maeneo ya River Side Ubungo Wakamatwa

$
0
0
JESHI la Polisi katika Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashikilia watu nane wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi sugu. Wawili kati yao wanahusishwa na tukio la kuuawa kwa Sista Cresencia Kapuri (50) wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam katika Parokia ya Makoka.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari, jana.

Alisema wahutuhumiwa hao, wakiwa katika utekelezaji wa uhalifu wao, walisababisha vifo, majeraha, wizi wa mali na fedha taslimu.

Alisema watuhumiwa hao, walitumia silaha za moto, ikiwa ni pamoja na bunduki aina ya SMG, bastola na vifaa mbalimbali vya uvunjaji, ikiwa ni pamoja na baruti.

Alitaja watuhumiwa wanaohusishwa na tukio la kuuawa kwa Sista Cresencia kuwa ni Manase Ogenyeka (35), maarufu kama Mjeshi, mkazi wa Tabata Chang’ombe Manispaa ya Ilala, ambaye ni dereva wa bodaboda ; na Hamisi Shaaban maarufu kama Carlos, mfanyabiashara, mkazi wa Magomeni Mwembechai Manispaa ya Kinondoni.
Sista huyo aliyekuwa pia Mhasibu wa Parokia ya Makoka na Mhasibu wa Shule ya Mwenyeheri Anwarite inayomilikiwa na Kanisa Katoliki, aliuawa kwa kupigwa risasi Juni 23, mwaka huu katika eneo la Riverside, Ubungo Kibangu, Dar es Salaam. Kova alisema licha ya kuhusishwa na kifo cha Sista huyo, watu hao wanatuhumiwa kupora Sh milioni 20.

Alisema watuhumiwa hao, pia walikuwa wakitafutwa kwa muda mrefu kwa tuhuma za uporaji wa Benki ya Barclays Tawi la Kinondoni, uliotokea Aprili 28, mwaka huu, ambapo mamilioni ya fedha yaliibwa kabla na baada ya tukio hilo.

“Jambazi Manase Ogenyeka ndiye aliyeendesha pikipiki, akimbeba mwenzake akiwa na fuko la mamilioni ya fedha na kutoroka nazo wakati Hamisi Shaaban ndiye aliyekuwa kiongozi katika tukio hilo,” alidai Kova.

Mbali ya kuuawa kwa Sista Cresencia, katika tukio hilo aliongozana na Sista Brigita Mbaga (32) na dereva wao, Mark Mwarabu, aliyekuwa akiendesha gari aina ya Toyota Hilux Pick-Up, lenye namba T213 CJZ ambaye alikatwa dole gumba lake kwa risasi baada ya kushambuliwa.

Alisema Jeshi la Polisi, bado linawatafuta watuhumiwa wengine wawili katika tukio la kuuawa kwa Sista. Mtu mwingine anayetafutwa ni Leonard Molel anayetuhimwa kwa tukio la wizi katika Benki ya Barclays.

Kamanda huyo alisema watuhumiwa wengine watatu, kati ya hao wanane, walikamatwa baada ya kutumia mbinu ya hati bandia wakiwa wanaomba kazi katika kampuni binafsi ya ulinzi iitwayo Instant Security Services Mtaa wa Makangira Msasani, Dar es Salaam.

Hao ni Elibariki Makumba (30) na Nurdin Suleimani (40), wakazi wa Buguruni Madenge na Mrumi Salehe(38), mkazi wa Kigogo Fresh.

Alitoa rai kwa kampuni za ulinzi, yanapotaka kuajiri walishirikishe Jeshi la Polisi ili wafanye upekuzi wa pamoja, utakaohusisha alama za vidole, picha na ukaguzi wa kumbukumbu muhimu za kibayolojia kama vile vipimo vya DNA.

Aidha, aliwaomba wananchi ambao wana tabia ya kutembea na fedha nyingi, kuacha kufanya hivyo, kwani kwa sasa teknolojia imepanuka, hivyo kuweza kutumia simu za mkononi kuhamisha fedha kutoka benki moja kwenda nyingine.

Clouds FM Kimenuka Watangazi wa Kipindi cha XXL Wapigana Live On Air

$
0
0
leo karibu na mwisho wa kipind cha xxl watangazaj wa kipind hiko wamegombana live kwenye kipind mpaka ray alipokuja na kuwazimia mics!
kisa ni compilation album ya fiesta.
Nini maoni yako kuhusu mwenendo wao na nani alikuwa Source au influencer wa ugomvi?
Audio ya Ugomvi huo Coming Soon
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images