Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Nimejiunga Chadema Baada ya Kufuata Ushauri wa Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere Aliwahi Kusema Chadema Ifae- Nyarandu

0
0
a Baada ya Kufuata Ushauri wa Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere Aliwahi Kusema Chadema Ifae- Nyarandu
Lazaro Nyalandu amefunguka na kusema kuwa yeye aliviangalia vyama vya upinzani nchini na kuamua kujiunga na CHADEMA baada ya kuachana na CCM kwa kufuata ushauri wa marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambaye aliwahi kusema CHADEMA ifae.

Nyalandu amesema hayo alipokuwa akihojiwa na DW na kusema mpaka sasa bado hajajiunga na CHADEMA lakini amefikiria kujiunga nao baada ya kuvitazama vyama vingine vya siasa na kuona huko ndiko kunaweza kuwa sehemu sahihi kuwepo kwa sasa.
"Mpaka sasa bado sijafanya hatua yoyote ile ila nimeviangalia vyama vyote vya upinzani na kuangalia chama kimoja kimoja kwa sababu ilikuwa ni lazima niamue kuwa kwenye chama fulani nikakumbuka ushauri wa Baba wa Taifa alivyoitazama na yeye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere marehemu Mwenyezi Mungu ailaze mahali pema peponi, alisema CHADEMA ifae na mimi nimevitazama vyama vingine ni vizuri vinajitahidi na vipo kwenye hatua mbalimbali katika kukomaa kwao lakini kwa kweli nimeona chama ambacho mimi ningependa kuongeza nguvu ni CHADEMA" alisisitiza Nyalandu.
Lazaro Nyalandu toka alipotangaza kujivua uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge aliondoka nchini Tanzania na kwenda nchini Kenya ambapo mpaka sasa yuko nchini Kenya.



Nyalandu Hakua Analazimika Kuandika Barua kwa Spika Wala CCM Kujiunga Chadema Kulitosha Kulithibitisha- Msekwa

0
0
Nyarandu Hakua Analazimika Kuandika Barua kwa Spika Wala CCM Kujiunga Chadema Kulitosha Kulithibitisha- Msekwa
Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge wala CCM kwani kuonyesha kwake nia ya kujiunga na Chadema kulitosha kuthibitisha hilo.

Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana, Msekwa ambaye ni makamu mwenyekiti wa CCM mstaafu, alisema kilichomwondoa Nyalandu CCM ni kifungu cha 13 (f) cha Katiba ya CCM kinachoeleza kuwa mtu aliyejiunga na chama kingine chochote cha siasa anapoteza sifa ya kuwa mwana CCM.

“Kilichomwondoa Nyalandu ni kujiunga na chama kingine kinyume na kifungu cha 13 (f). Kuandika barua ni utaratibu tu wa kutoa taarifa kwa chama au Bunge ili wajue,” alisema Msekwa.

Alisema mbali na katiba ya CCM, hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema mtu aliyejivua uanachama wa chama cha siasa anapoteza sifa ya kuwa mbunge.

“Kuandika barua ni utaratibu tu... Chama pia kinaweza kumwandikia Spika ili ajue kwamba yule siyo mwanachama wake,” alisema.

Mbali na mazungumzo ya simu, baadaye Msekwa alituma ujumbe wa maandishi (sms) kupitia simu yake ya mkononi akisisitiza suala hilo.

“Nathibitisha tu maneno niliyoyasema kwenye simu kuhusu Nyalandu na mambo yake. Ni kwamba Nyalandu amepoteza uanachama wake wa CCM kutokana na ibara ya 13(1)(f) ya Katiba ya CCM. Na amepoteza ubunge wake kutokana na Ibara ya 71(1)(f) ya Katiba ya nchi. Hakuna haja ya yeye kuandika barua kwa chama au kwa Spika.

Aliongeza: “Kwa mfano, wakati mimi nikiwa Spika, Mhe. (Augustino) Mrema alikuwa Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi. Halafu akaamua ghafla kuhamia TLP. Hakuna barua niliyoandikiwa kuhusu jambo hilo. Lakini tamko lake lilitosha kuniwezesha kuiarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwamba nafasi ya Mrema bungeni ilikuwa wazi kwa hiyo Tume ikachukua hatua za kuijaza. Hakuna utata wowote kuhusu Nyalandu,” alisema Msekwa.

Utata wa barua

Msekwa ametoa ufafanuzi huo wakati kukiwa na sintofahamu kuhusu barua ya Nyalandu kama imepokewa na Ofisi ya Bunge au la.

Wakati Ofisi ya Spika ikisema haijapokea barua hiyo, Nyalandu ameibuka na kuonyesha barua aliyoituma katika mhimili huo.

Nyalandu alimwandikia Spika Ndugai barua hiyo ambayo Mwananchi limeiona Oktoba 30, siku ambayo alitangaza kujiuzulu nafasi zote ndani ya chama hicho ukiwamo ubunge.

Lakini juzi, Ofisi ya Bunge katika taarifa yake ilisema haijapokea barua hiyo badala yake imepokea ile ya CCM Oktoba 30 ikieleza kuwa Nyalandu amepoteza sifa ya kuwa mwanachama wake.

Siku hiyo, Spika wa Bunge, Job Ndugai alihojiwa na Azam TV na kusema kuwa alikuwa hajapokea barua ya Nyalandu lakini hakusema kama alikuwa amepokea ile ya CCM. Alisema endapo angeipata (Barua ya Nyalandu) na kuthibitisha kujiuzulu kwake, angeshauriana na wasaidizi wake kabla ya kuchukua uamuzi.

Ikinukuu barua ya CCM, Taarifa ya Bunge inasema kuwa chama hicho kimekuwa kikifuatilia vitendo na kauli za Nyalandu zisizoridhisha kinyume cha misingi, falsafa na itikadi ya CCM.

“Hivyo, Chama cha Mapinduzi kuanzia tarehe ya barua yao kimemjulisha Mheshimiwa Spika kuwa Lazaro Nyalandu amepoteza sifa za uanachama wa Chama cha Mapinduzi na hivyo kupoteza nafasi zote za uongozi wa ndani wa chama hicho na ubunge kwa mujibu wa ibara ya 13 ya chama hicho,” inasema taarifa hiyo ya Bunge.

Taarifa hiyo inasema kutokana na barua hiyo, Nyalandu amekoma kuwa mbunge na hatua stahiki za kuiarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi zinaendelea kuchukuliwa.

Hata hivyo, mara baada ya mbunge huyo kutangaza kujiuzulu, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole alikaririwa akisema Nyalandu ametumia haki yake ya kikatiba inayompa haki kila Mtanzania kuwa mwanachama wa chama chochote.

“Ibara ya 20 ya Katiba ya Jamhuri inaeleza kuwa kila Mtanzania ana haki ya kuwa na chama. Ninachoweza kusema ni kwamba kuna jambo la kawaida kabisa lililotokea na wala siyo kubwa kama linavyodhaniwa.”

Polepole alisema wameondoka wazito kwenye chama na kimebaki kimoja na kwamba Nyalandu si sehemu ya wazito, bali ni mwananchi wa kawaida mwenye haki na si mara ya kwanza jambo hili kutokea.

Barua ya Nyalandu

Katika barua yake kwa Spika Ndugai ambayo Mwananchi imeiona pamoja na mambo mengine, alimjulisha kuwa kama alivyotangaza kupitia mkutano wake wa wananabari ameamua kujiuzulu nafasi yake ya ubunge wa jimbo Singida Kaskazini kupitia CCM.

Mwanasiasa huyo anasema licha ya kuondoka CCM na bungeni, bado anaamini kwamba Tanzania inahitaji kupata Katiba Mpya itakayoweka bayana ukomo wa mamlaka ya mihimili ya utawala (Bunge, Serikali na Mahakama) ili kuondoa mwingiliano unaonekana kufanyika kwa wazi sasa.

“Kwa sasa dola haionekani kuwa na mipaka katika dhana ya uongozi wa nchi na hivyo kufanya uwakilishi wetu wa wananchi bungeni kuwa legevu kuliko ilivyokusudiwa kikatiba.”

Nyalandu anawashukuru wabunge wenzake, Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani bungeni Freeman Mbowe, maspika wastaafu, Pius Msekwa, Samuel Sitta na Anne Makinda pamoja na Ndugai kwa ushirikiano waliomuonyesha katika vipindi vinne alivyokuwapo bungeni hapo ambako “Alifanya kazi kwa mapenzi makubwa, dhamira ya dhati na moyo mkunjufu.”

Katika barua yake hiyo, Nyalandu anadai kwamba dola imeingilia kwa kiasi kikubwa mfumo wa utendaji na uendeshaji wa CCM hadi kukosa uelekeo, jambo ambalo alisema linawaondolea au kuwapunguzia wabunge wake uwezo wa kufanya uamuzi binafsi wakati wa mijadala au katika kupiga kura kwa kadri ya dhamira zao zinavyowaongoza kama ilivyokuwa wakati wa mchakato wa Katiba Mpya.


Huu Hapa Ukweli Kuhusu Ndoa ya Msanii Enock Bella wa Yamoto Band

0
0
Huu Hapa Ukweli Kuhusu Ndoa ya Msanii  Enock Bella wa Yamoto Band
Msanii wa muziki wa kizazi kipya na mkali wa ngoma ‘Natamba’ Aslay ameonekana kuwa msanii aliyediriki kuwadanganya mashabiki kwa mgongo wa ndoa kama njia pekee ya kuutetea ujio wa kazi mpya ya msanii mwenzake Enock Bella.

Itakumbukwa kuwa kati ya wasanii waliounda kundi la Yamoto Bendi, ukiachana na Aslay, Beka Flavour na Marombosso pia Enock Bella alikamilisha idadi ya wanakikundi hicho kipindi ambacho walifanya kazi za pamoja. Baada ya maneno maneno yenye tetesi na uvumi wa hapa na pale juu ya kuvunjika kwa kundi hilo, basi kila mmoja alionekana kujitawala katika sura ya kuachia kazi ya pekee yake ambapo utaratibu huo uliongozwa na Aslay.

Wengi walionekana kumpokea vyema Aslay ambapo Beka Flavour naye alipokelewa vyema kupitia kazi yake ya ‘Libebe’ na ‘Sikinai’ huku wengi wakiutamani ujio wa Enock Bella, ukiachana na Maromboso aliyekwisha anza kufanya kazi chini ya usimamizi wa lebo ya Muziki ya WCB Wasafi.

Oktoba 23 mwaka huu wa 2017, Aslay aliutumia ukurasa wake wa Instagram kuwadanganya mashabiki kwa bashasha za pongezi kwa hatua ya msanii mwezake Enock Bella kuchukua jiko(Yaani kupata mke/Kuoa). Katika picha Enock alionekana akiwa ni mwenye kujistili kwa suti ya gharama akiwa kamkaribiria mrembo mmoja kwa jina maarufu ‘Mami’ aliyejipamba kwa nakshi ya vazi la heshima mithiri ya Bibi Harusi.

Kilichokuja kugundulika usiku wa kuamkia tarehe 3 ya mwezi Novemba, Enock ameachia video ya wimbo wake mpya ‘Sauda’ uliotayarishwa chini ya Studio za WCB Wasafi kwa mkono wa Lizer Classic huku video ikiongozwa na Director Ivan ambapo mrembo aliyetumika katika video hiyo ndo yule ambaye alitajwa kama mke wa Enock Bella katika picha aliyopost Aslay mrembo akiwa sambamba na Enock Bella.

Hata hivyo kingine ambacho kimetambulishwa rasmi kwa wengi ambao wanamfahamu na kumfatilia Enock Bella ni kusikika akijiita Enock Bella ‘Base’ kutokana na haina ya sauti anayoitumia katika uimbaji wake.

Mimi Mars: Ammwagia Sifa Jux Asema 'Natamani Warudiane na Vanessa Mdee'

0
0
Mimi Mars: Wanaosema Natoka Kimapenzi na Jux Wananikosea Heshima
Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Mimi Mars amesema kwa sasa anatamani Jux na Vanessa Mdee warudiane.

Muimbaji huyo ambaye ni ndugu wa damu na Vanessa, katika mahojiano na kipindi cha Clouds E pia alielezea kuchukizwa na taarifa zinazodai kuwa anatoka kimapenzi na Jux baada ya kuachana na Vanessa.

“Kwanza nilikasirika kwa sababu ni kukoseana heshima, ina maanisha watu wananionaje kwanza, mnanichukuliaje kwamba mimi naweza nikafanya tendo na mtu wa dada yangu haileti maana kabisa, niliipuuzia ndio maana sijaizungumzia” amesema Mimi Mars.

“Mungu akijalia kweli I wish warudiane maana yake walikuwa poa, (Jux) ni mtu mcheshi, ana upendo, mtu mkarimu na ni mtu anayempenda Vanessa Mdee” ameongeza.

Alipoulizwa anauchukuliaje ukaribu wa sasa kati ya Jux na Vanessa, alijibu; “kama mimi naona ni marafiki kama walivyotuambia ambao wanaendelea kuwa na uhusiano mzuri, maana tumejiwekea watu wakiachana lazima wawe maadui siyo lazima iwe hivyo, kwa hiyo wao wanatuonyesha njia tofauti”


Mahakama Imewahukumu Watu Wawili Kifungo cha Maisha Jela kwa Kubaka Mpwa Wao wa Miaka 10

0
0
Mahakama Imewahukumu Watu Wawili Kifungo cha Maisha Jela kwa Kubaka Mpwa Wao wa Miaka 10
Mahakama moja nchini India imewahukumu watu wawili kifungo cha maisha jela kwa kumbaka mpwa wao mwenye umri wa miaka 10 ambaye alijifungua mtoto wa kike mnamo mwezi Agosti.
Wanaume wote wawili walikuwa wajomba wa smichana huyo.

Walihukumiwa kwa kumbaka msichana huyo siku ya Jumanne.
Uja uzito wa msichana huo ulibainika katikati ya mwezi Julai wakati alipopelekwa hospitalini baada ya kulalamikia maumivu ya tumboni.

Mjombake wa pili alikamatwa baada ya chembechembe za DNA za mtoto huyo kutofanana na kakake mkubwa ambaye ndio mshukiwa wa kwanza .
Kesi ya mshukiwa wa kwanza ilichukua mwezi mmoja huku mjombake mdogo akihukumiwa baada ya kesi hiyo kuchukua siku 18.
Kesi hiyo ya msichana wa miaka 10 imegonga vichwa vya habari kwa wiki kadhaa nchini India na kote duniani.

Alikuwa na uja uzito wa wiki 30 wakati mahakama moja ya Chandigarh ilipokataa ombi la kuavya mimba, kwa sababumimba hiyo ilikuwa kubwa.
Jopo la madaktari lilisema kuwa kutolewa kwa mimba hiyo ni hatari .
Baadaye mahakama ya juu ya India pia ilikataa kutolewa kwa mimba hiyo kwa sababu kama hizo za kimatibabu.

Sheria ya India hairuhusu kutolewa kwa mimba baada ya wiki 20 hadi pale daktari aweze kubaini kwamba maisha ya mama yapo hatarini.
Mtoto huyo hakujua kwamba alikuwa akibeba uja uzito na kwamba alielezewa kwamba tumbo lake likuwa na jiwe, kulingana na mwamndishi wa BBC Geeta Panday mjini Delhi.
Alijifungua mwezi Agosti na mtoto huyo kukabidhiwa mamlaka ya kuangalia watoto ili kulewa.
Awali msichana huyo aliwaambia maafisa wa polisi na wanaharakati wa maslahi ya watoto kwamba alibakwa mara kadhaa katika kipindi cha miezi saba iliopita na mjombake mkubwa ambaye yuko katika umri wake wa 40.

Wasimamizi wa Uchaguzi Wameambiwa Wasitangaze Ushindi wa Wetu Tukishinda- Mashinji

0
0
Wasimamizi wa Uchaguzi Wameambiwa Wasitangaze Ushindi wa Chaadema Tukishinda- Mashinji
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Mashinji amefunguka na kusema kuwa baadhi ya wasimamizi wa Uchaguzi mdogo wa udiwani ambao unatarajiwa kufanyika karibuni katika Kata 48 katika mikoa 18 nchini wamepewa maelekezo kutowatangaza Madiwani CHADEMA wakishinda.

Dkt. Vincent Mashinji amesema hayo leo kupitia mtandao wake wa Twitter na kudai kuwa hiyo itakuwa ni fursa kwao wao CHADEMA kuwaonyesha na kuwafundisha ustaarabu mpya.
"Wasimamizi wa uchaguzi wana maagizo ya kutowatangaza madiwani wa CHADEMA watakao shinda. Hii ni fursa kwetu kuwafundisha ustaarabu mpya. Na imani maneno haya utayakumbuka nikupe mshahara, nyumba na gari halafu umtangaze mpinzani kashinda" alisema Katibu Mkuu wa CHADEMA
Mbali hilo Mashinji amejibu hoja ya Rais ambayo aliitoa akiwa Mwanza kuwa wezi ambao walikuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikimbilia CHADEMA na kudai kuwa watu hao ambao wanatoka CCM na kwenda CHADEMA wameamua kuokoka.
"JPM kusema wapo watu waliokuwa ni wezi katika CCM na kusema saizi watu hao wamekimbilia CHADEMA. Lazima JPM ajue kuwa “Wameamua kuokoka” Alisema Mashinji.

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Ijumaa

0
0

Dogo Janja Aeleza A-Z Kuhusu Ndoa Yake Asema Uwoya Alibadiri Dini Wiki Tatu Kabla ya Ndoa

0
0
Dogo Janja Aeleza A-Z Ndoa Kuhusu Ndoa Yake Asema Uwoya Alibadiri Dini Wiki Tatu Kabla ya Ndoa
Mwanamuziki wa Bongo Fleva anayetamba na ngoma ya Ngarenaro, Dogo Janja akifanya yake muigizaji wa filamu, Irene Uwoya, ambaye kwa sasa anaitwa Sheila.

Eh! Bwana kweli! Mwanamuziki wa Bongo Fleva anayetamba na ngoma ya Ngarenaro, Dogo Janja,  amethibitisha kumuoa muigizaji wa filamu, Irene Uwoya, ambaye kwa sasa anaitwa Sheila.
Akifanya mahojiano na Redio ya Clouds katika Kipindi cha Leo Tena, Dogo Janja amesema kwamba aliamua kumuoa mwanamke huyo kwa kuwa tu moyo wake ulimsukuma kufanya hivyo kutokana na  upendo mkubwa aliokuwanao kwake.
“Sikulazimishwa! Niliamua kwa moyo wangu kumuoa Sheila. Nilipeleka posa, ikakubaliwa na hatimaye kufunga ndoa,” alisema Dogo Janja ila baada ya kuulizwa mahali ndoa ilipofungwa, hakuwa wazi kulijibu hilo.
Akiendelea kufanya mahojiano kwenye kipindi hicho kuhusu kuoa mtu ambaye tayari ni mke wa mtu aliyefunga ndoa kanisa Katoliki na mumewe Ndikumana ‘Katauti’ raia wa Burundi ambaye hawajawahi kutalikiana, Dogo Janja alisema yeye si mtu sahihi wa kujibu hilo ambapo alisema mtu sahihi wa kulijibu ni Irene.

Dogo alimsifia mkewe huyo akisema wakati anamfuata hakutia maanani kwamba ni staa, alimchukulia tu kwamba ni mtu wa kawaida ambaye ana matunzo ya kawaida si ya gharama kama wanavyodhani watu wengine.
Aliendelea kumsifia mrembo huyo akisema anampenda na angemshirikisha mambo yake yote ambayo hawezi kumwambia mtu mwingine na kwamba anamwamini.
Kuhusu kuthohudhuria kwa mama yake kwenye harusi hiyo, alisema alimwambia mama yake anayeishi Arusha ambaye alimjibu kuwa jambo hilo alisimamie mwanamuziki wa Bongo Fleva, Hamad Ali   ‘Madee’ ambaye amemleta mwanamuziki huyo hapa mjini tangu anatokea jijini Arusha miaka kadhaa iliyopita hadi sasa.
Ndoa hiyo alidai ilifungwa Ijumaa iliyopita wakati wa sala ya adhuhuri huko Mikocheni, jijini Dar es Salaam ambapo miongoni mwa watu maarufu waliohudhuria ni Madee, msimamizi wa ndoa hiyo, Kassim Mganga, mwigizaji wa filamu, Blandina Chagula ‘Johari’ waigizaji Monalisa, Natasha na wengineo kibao.
Ndoa hiyo imeendelea kuleta mkanganyiko katika mitandao ya jamii ambapo watu wengi hawaamini wakidhani kwamba ni maigizo kama anavyosema Irene Uwoya kwamba yote hayo yalikuwa ni maigizo ya muvi.
Baada ya kuthibitishiwa kwa asilimia zote kwamba ni kweli Dogo Janja na Irene Uwoya wamefunga ndoa sasa ni wakati wa kujua ilikuaje na waliwezaje?

Kuhusu Uwoya Kubadiri Dini
 “Uwoya alibadili dini na kuwa Muislamu wiki tatu kabla ya ndoa, nilijaribu kuongea nae sababu tulikua tuna imani tofauti yeye ni Mkristo na mimi ni Muislamu, aliridhia kwa nafsi yake wala hakushawishiwa na mtu“
Kwenye hii Interview Dogo Janja amesema mambo mengi ikiwemo kutaja jina jipya la Irene Uwoya baada ya kubadili dini ambapo kwa sasa anaitwa Sheila, bonyeza play hapa chini kumsikiliza Dogo Janja zaidi akizungumzia pia ishu ya umri, yeye kuwa mdogo zaidi kuliko Uwoya


Ndugai Awatumia Barua NEC Kuwataarifu Jimbo la Nyalandu Lipo Wazi

0
0
Ndugai Awatumia Barua NEC Kuwataarifu Jimbo la Nyalandu Lipo Wazi
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai leo Novemba 3, 2017 amemuandikia barua Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) kumtaarifu kuwa jimbo la Singida Kaskazini lipo wazi kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Taarifa ya Bunge iliyotolewa leo inasema kuwa jimbo hilo lipo wazi kutokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumfuta Uanachama Lazaro Nyalandu toka Oktoba 30, 2017 siku ambayo Mbunge huyo alitangaza mwenyewe kupitia vyombo vya habari kujivua nafasi zake ndani ya chama hicho na kusema kuwa ameandika barua kwa Spika kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge kupitia CCM.


Keisha, Dogo Janja Wajichanganya Ukweli Kuhusu Mahali Ndoa Ilipofungwa

0
0
Keisha, Dogo Janja Wajichanganya Ukweli Kuhusu Mahali Ndoa Ilipofungwa
Mwanamuziki Keisha amejichanganya kuhusu suala la ndoa kati ya Dogo Janja na mwigizaji, Irene Uwoya akitoa maelezo tofauti kuhusiana na ushiriki wake katika kufanikisha shughuli hiyo.

Awali Keisha akihojiwa mwanzoni mwa kipindi cha Leo Tena cha leo Ijumaa kinachorushwa na kituo cha Redio Clouds amesema alishiriki kumfuata bibi harusi nyumbani kwao baada ya watangazaji kutaka kufahamu kwa nini ndoa haikufungwa huko.

Keisha akimsaidia Dogo Janja kujibu swali hilo alisema: “Nilikuwa mmoja wa waliokwenda nyumbani kwa kina Irene kumfuata kisha tulimpeleka katika eneo la siri ilipofungwa ndoa, unajua mimi ni kama mama au dada mkubwa wa Abdul ( Dogo Janja) kwa sababu Madee ni kama baba yake asingweza kwenda peke yake.”

Lakini watangazaji walipoendelea na mahojiano Keisha alibadilisha kauli yake akisema hata yeye hakuwa akifahamu anayeolewa ni nani na pia hakuamini iwapo ni tukio la kweli mpaka aliposhuhudia tendo zima.

“Nilipofika nilimuuliza Johari (mwigizaji) ambaye alikuwa mmoja wa mashahidi iwapo ni ndoa kweli na siyo filamu. Johari alisema siwezi kukudanganya hii ndoa kweli. Mimi nimeolewa kwa hiyo niliposhuhudia tukio zima nikajiridhisha kuwa ile ndoa haswa,” amesema Keisha.




       


Kitilia na Wenzake Mambo Bado Magumu Mahakamani

0
0
Kitilia na Wenzake Mambo Bado Magumu Mahakamani
Upelelezi wa kesi ya utakatishaji fedha wa Dola za Kimarekani Milioni 6 inayomkabili aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Harry Kitilya na wenzake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu bado haujakamilika ikiwa ni mwaka mmoja na nusu sasa.

Mbali ya Kitilya, Washtakiwa wengine ni aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 1996 ambae pia ni Ofisa wa Stanbic Bank, Shose Sinare na Sioi Graham Solomon ambao walifikishwa Mahakamani hapo kwa mara ya kwanza April 1,2016 kwa kukabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha.

Wakili Mwandamizi wa Serikali Mutalemwa Kishenyi amemueleza Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba wanasubiri awamu ya pili ya upelelezi kutoka Uingereza hivyo akaomba kesi hiyo iahirishwe hadi tarehe nyingine.

Baada ya kuelezwa hayo, Mwambapa ameahirisha kesi hiyo hadi November 10,2017 ambapo kwenye kesi hii, Washtakiwa wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya March 2013 na September 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani 550 milioni kwa serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard Uingereza.

Pia wanadaiwa kuwa March 2013 Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani Milioni 6 wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo na zililipwa kupitia Kampuni ya Egma T Ltd.




.

Mtandao wa Whatsap Umekwama Kufanya Kazi Dunia Nzima,

0
0
Mtandao wa Whatsap Umekwama Kufanya Kazi Dunia Nzima,
Mtandao wa kutuma mafaili mbalimbali kama Picha, Video na Sauti wa WhatsApp umekwama kufanya kazi kwa masaa kadhaa kwenye baadhi ya nchi duniani ikiwemo Tanzania.

Ripoti zinasema tatizo hilo limeanzia nchini Uingereza kisha kuendelea katika nchi za Marekani, Italia, Ujerumani India na sasa nchi za Afrika Mashariki nazo zimepitia changamoto ya kukosa huduma ya mtandao huo.
Tatizo hilo limeelezwa kuanza majira ya saa mbili asubuhi ambapo maelfu ya watumiaji wa WhatsApp wameeleza kukosa huduma. Wengi wao wamelalamika kukwama kwenye baadhi ya majukumu yao kutokana na kutegemea mtandao huo kwaajili ya kuhamisha na kupokea mafaili yao.
Hadi sasa bado wamiliki wa mtandao huo ambao ni kampuni ya Facebook chini ya Mkurugenzi Mark Zuckerberg hawajatoa tamko juu ya tatizo hilo.
Update
WhatsApp imerejea kwenye hali ya kawaida hapa Tanzania, wakati huo nchi zingine kama Uingereza bado zinalalamika kukosa huduma hiyo ambapo watumiaji wanasema inafunguka na kuonesha kuwa kuna ujumbe umeingia lakini hauwezi kuufungua ili kuusoma au kuona kama ni Picha au Video.

Deni la Milioni 32.5 Zaiweka Hatarini Hoteli DC Atoa Ziku Saba Kulipa Deni Hilo

0
0
Deni la Milioni 32.5 Zaiweka Hatarini Hoteli  DC Atoa Ziku Saba Kulipa Deni Hilo
Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama wilaya ya Kahama Fadhil Nkurlu ametoa siku saba kwa uongozi wa hoteli ya Mongo kulipa deni la mapato ya serikali shilingi milioni 32.5 na kuwalipa fidia waandishi wa habari walioibiwa vifaa vya kazi wakati wamelala hotelini hapo.

Nkurlu ametoa maagizo hayo leo Ijumaa baada ya kutembelea hoteli hiyo kutokana na uongozi kukaidi agizo la Mamlaka ya Mapato(TRA) la kulipa kiasi hicho kabla au ifikapo Julai 5.

Meneja wa TRA Mkoa wa Kodi wa Kahama, Jacob Mtemang’ombe amethibitisha hoteli hiyo kudaiwa Sh30 milioni inayotokana na kodi ya asilimia 10 ya mauzo yaliyofanyika zaidi ya mwaka mmoja uliopita.

Morinyo Anusurika Jera Afutiwa Kesi Baada ya Kulipa Faini

0
0
Morinyo Anusurika Jera Afutiwa Kesi Baada ya Kulipa Faini
Kocha Jose Mourinho amelipa faini na kufutiwa kesi iliyokuwa inamkabili ya kukwepa kodi nchini Hispania kati ya mwaka 2011 na 2012 akiwa kocha wa Real Madrid.

Mourinho alikuwa anatuhumiwa kukwepa kodi ambayo ni kiasi cha Euro milioni 3.3 zaidi ya bilioni 8,100 za Kitanzania. Kesi yake imemalizika leo kwenye mahakama ya Pozuelo de Alcarcon jijini Madrid.
Baada ya kutoka mahakamani mchana huu Mourinho ameongea na wanahabari ambapo amesema kuwa kesi yake imemalizika baada ya kulipa faini na sasa yupo huru.

"Kesi imeisha na sijajibu lolote kwasababu sikuwa na hoja ila nimelipa na kusaini na serikali kuwa sina tena tuhuma na kesi imefungwa ndiyo maana niko hapa, hakuna kitu kingine chochote", Mourinho amewaambia Wanahabari.
Mourinho anatarajiwa kusafiri mchana huu kwa ndege binafsi kurejea jijini Manchester kwaajili ya kusafiri na timu kuelekea jijini London ambapo Jumapili timu yake itacheza na Chelsea kwenye mchezo wa EPL.


Hivi Ndivyo Joti na Mkewe Wanavyokula Raha Katika Fungate Yao

0
0
Hivi Ndivyo Joti na Mkewe Wanavyokula Raha Katika Fungate Yao
Mara baada ya kufunga ndoa weekend iliyopita, mchekeshaji Joti na mkewe wameamua kusherekea fungate yao katika mbuga ya wanyama ya Serengeti.

Kwenye ukrasa wake wa instagram aliposti video mbili na kuandika maneno haya

"Baba anapotafuta furaha yake ni kuona Familia inakula pamoja,ila hii familia hapana kwa kweli,🤣🤣#FarufaruSerengeti @juma_jux @vanessamdee @bernabeu_madrid @missmandoza
Kwenye maisha sio kila vita ni ya kwako,Na sio kila vita inakuhusu,Jifunze kuzitazama na kuzikagua kwanza ili kuzipima vita zinazokujia tokea mbali,ili ufanye maamuzi ya kuingia au kutokuingia,ukiparamia kila vita mwishoni utagundua kuwa umepoteza nguvu nyingi na akili kupambana na maadui ambao wala hawakuwahi kuwa adui zako,ukiingilia vita isio yako utashindwa kirahisi hata kama ulikuwa mtu wa kushinda,Chagua vita unayoweza kupambana nayo..🙏🙏#saboracamp#OurSingita#SingitaSaboraCamp

Beka Flavour Afunguka Chanzo cha Kuporomosha Mvua ya Matusi Kwenye Instagram Yake

0
0
 Beka Flavour Afunguka Chanzo cha Kuporomosha Mvua ya Matusi  Kwenye Instagram Yake
Msanii Beka Flavour ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Sikinai' amefunguka na kuomba radhi kwa Watanzania baada ya kushusha matusi kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram baada ya mtu mmoja kumkorofisha juu ya mpenzi wake.

Beka Flavour amesema kuwa yeye kama binadamu alipoona mtu huyo ameandika mambo ambayo hakupendezwa nayo kuhusu mpenzi wake huyo aliamua kumjibu na kwa kuwa alikuwa na hasiri alijikuta ameandika matusi pasipo yeye mwenyewe kutegemea.
Mtazame hapa akifunguka zaidi.


Kwa Nini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo?

0
0
KWA NINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE  MADOGO?

Matatizo haya yame kuwa yakiwaathiri watu wengi sana kisaikolijia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wenzao kwa kawaida mwanaume ana takiwa awe na uume kuanzia inch(6_8)  vinginevyo mtu huyo atakuwa na matatizo.


Zipo sababu nyingi zinazo sababisha tatizo hilo  baadhi ni upungufu wa  vichocheo (Hormones za Getrogen) Ambazo  mwanaume akisha balehe vichocheo hivi huchochea  ukuaji wa  uume, chango husababisha NEVA ambayo huathiri misuri ya uume.

Ngiri ambayo Huleta maumivu ya tumbo kuunguruma  na kujaa guess, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri , miguu kufa ganzi, maumivu ya kiuno,upigaji wa punyeto sababu hizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembaba na mara kwa mara hipelekea kupunguka kwa nguvu za kiume na ham ya tendo la ndoa hukosekana na kuisha kabisa

NSUMBU:__Ni dawa dawa inayo zalisha hormones za Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.

NZAGI :--Ni dawa bora ya kurudisha  nguvu za kiume na kukupa hamu ya kurudia tendo la ndoa mara dufu utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4)bila hamu kuisha (kuchoka) dawa hii ni tiba kamili kwa matatizo hayo. Dawa hii pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk(15_30)kwa tendo moja la ndoa dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji kuanzia miaka(18_90)wana ruhusiwa kuzitumia

Pia tunatibu KISUKARI, PRESHA, PUMU, MALARIA SUGU, MIMBA KUHARIBIKA(Chango)

POWER :__Ni dawa ya mitishamba inaongeza hips, (makalio), miguu, ina punguza maziwa (chuchu). Ina toa harufu mbaya sehem  za siri Nk. Pia anazo dawa za  mvuto wa mapenzi,biashara, kurudishwa kazini, kumuita aliye mbali kwa mda mfupi tu OSTADH JUMA ANAPATIKANA MALARIA ZAKHIEM SIMU:_0769-597778 au 0784-002216 au 0627457957 Wote mnakaribishwa

Download Wimbo Mpya wa Mwanamuziki Rosa Ree

0
0

Bonyeza Hapa Chini Kudownload Wimbo Mpya wa Rosa Ree


Mashinji "Wasimamizi wa Uchaguzi Wameagizwa Wasitangaze Chadema Tukishinda"

0
0
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Mashinji amefunguka na kusema kuwa baadhi ya wasimamizi wa Uchaguzi mdogo wa udiwani ambao unatarajiwa kufanyika karibuni katika Kata 48 katika mikoa 18 nchini wamepewa maelekezo kutowatangaza Madiwani CHADEMA wakishinda.

Dkt. Vincent Mashinji amesema hayo leo kupitia mtandao wake wa Twitter na kudai kuwa hiyo itakuwa ni fursa kwao wao CHADEMA kuwaonyesha na kuwafundisha ustaarabu mpya.

"Wasimamizi wa uchaguzi wana maagizo ya kutowatangaza madiwani wa CHADEMA watakao shinda. Hii ni fursa kwetu kuwafundisha ustaarabu mpya. Na imani maneno haya utayakumbuka nikupe mshahara, nyumba na gari halafu umtangaze mpinzani kashinda" alisema Katibu Mkuu wa CHADEMA

Mbali hilo Mashinji amejibu hoja ya Rais ambayo aliitoa akiwa Mwanza kuwa wezi ambao walikuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikimbilia CHADEMA na kudai kuwa watu hao ambao wanatoka CCM na kwenda CHADEMA wameamua kuokoka.

"JPM kusema wapo watu waliokuwa ni wezi katika CCM na kusema saizi watu hao wamekimbilia CHADEMA. Lazima JPM ajue kuwa “Wameamua kuokoka” Alisema Mashinji.

VIDEO: Daladala Lashika Moto Likiwa Barabarani, Abiria Wajirusha

0
0
Ilikua hali ya taharuki baada ya abiria waliokuwemo kwenye daladala kuambiwa na watu wa nje barabarani kwamba gari walilopanda limeshika moto, abiria wakaanza kuruka hata gari halijasimama ambapo hakuna aliejeruhiwa, bonyeza play kwenye hii video hapa chini kutazama ilivyokua VIDEO:
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images