Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..


JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU.

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.

Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Kweli Dunia Inafikia Mwisho...Mchungaji Atumia Pombe Kubatiza

$
0
0

Mchungaji mmoja huko Afrika Kusini amekuwa akikosolewa vikali baada ya kuanza kubatiza washirika kwa kutumia vilevi ambavyo wanavipenda kitendo ambacho ni kinyume na utaratibu.

Askofu Tsietsi Makiti, (52) ambaye pia  ni Mwanzilishi wa kanisa hilo linalojulikana kama 'Gabola', amesema kuwa ameongozwa na maandiko katika Biblia ambapo Yesu alibadilisha maji kuwa divai.
"Watu wanao kunywa na kubatizwa na bia wana furaha na amani. Hii inamaanisha kuwa wanaishi katika kivuli cha Mungu, "alisema Makiti.
Kanisa hilo lenye jina 'Gabola' jina likimaanisha 'Kunywa' limesema linakubali kuwapokea waumini waliotoka makanisa mengine huku likiweka wazi kwamba idadi ya watu wameongezeka kufikia 500 ndani ya miezi miwili tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo.
Waumini pia wanaruhusiwa kunywa wakati huduma za kanisa zikiendelea.
Aidha Askofu huyo ameweka wazi kwamba ana mipango ya kuanzisha matawi ya kanisa lake hilo katika miji mbali mbali

Harmorapa Nae Aamua Lazima Amuoe Wema Sepetu...Aanza Mikakati

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Harmorapa ambaye hakauki kwenye mitandao kwa vitendo vyake vya kiki, amesema na amini naye ipo siku atatimiza ndoto zake na kumuoa Wema Sepetu kama alivyofanya Dogo Janja kwa Uwoya.

Kwenye ukurasa wake wa instagram, Harmorapa ameandika ujumbe akisema kwamba hatokuja kukata tamaa juu ya ndoto yake ya kumng'oa 'Tz Sweetheart'Wema Sepetu na hatimaye kumuweka ndani kama mke wake.

“Naamini sana katika ndoto kua ipo siku ndoto unayoota itatimia na kuwa kweli, sina cha kusema zaidi ya kumpa hongera Dogo Janja, naamini ushupavu na kutovunjika moyo kumemfanya leo akawa mume wa mwanamke wa ndoto zake, nami sivunji imani naamini Wema Sepetu ipo siku atakua wangu, ugumu alioupata Janjaro umenipa matumaini, kikubwa ni kutulia na ndoto yangu na kulenga ipo siku itatimia... One day you will be mine Wema Sepetu”, ameandika Harmorapa.

Yanga Yapaa Kileleni Ligi Kuu

$
0
0
Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara Yanga SC wamelazimishwa sare ya 0-0 na Singida United kwenye mchezo wa raundi ya 9 uwanja wa Namfua mjini Singida.

Mchezo huo umeweka historia kwa klabu ya Singida United kucheza kwa mara ya kwanza kwenye uwanja wake wa nyumbani baada ya miaka 15 kupita ambapo mara ya mwisho ilikuwa ni mwaka 2012.

Katika mechi za raundi 8 zilizopita msimu huu Singida United walikuwa wakitumia uwanja wa Jamhuri Dodoma ambapo Namfua ulikuwa unafanyiwa marekebisho kabla ya Bodi ya ligi kuupitisha rasmi uwanja huo mapema mwezi uliopita.

Katika mchezo wa leo timu zote mbili zimeshambuliana kwa zamu lakini hakuna ambaye alifanikiwa kupachika bao hadi dakika 90 zinamalizika. Eneo la ushambuliaji kwa kila timu walifanya makosa kadhaa huku uimara wa walinda milango Manyika Jr wa Singida na Youthe Rostand wa Yanga kikiwa ndio chanzo kikubwa cha sare ya leo.

Yanga sasa imepaa kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na alama 17 huku ikisubiri mchezo wa leo ambapo Azam FC yenye alama 16 itacheza na Ruvu Shooting Azam Complex saa 1:00 usiku. Kesho Simba yenye alama 16 itakuwa ugenini kucheza na Mbeya City

VIDEO:Rais Magufuli Akisikiliza Wimbo wa Kisukuma na Mama na Dada Yake

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa anasikiliza wimbo wa kabila la wasukuma pamoja na Mama yake mzazi, Suzana Magufuli na Dada yake Mkubwa Monica Joseph Magufuli.

Rais Dkt Magufuli yupo mapumzikoni kijijini kwake Lubambangwe, Chato Mkoani Geita.

Aidha, Rais anatarajia kufanya ziara Mkoani Kagera kuanzia tarehe 06 hadi 09 Novemba, 2017.

Dhumuni la ziara ya Mhe. Rais Magufuli ni kuwatembelea wananchi wa Mkoa wa Kagera pia kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo Mkoani hapa.

Vilevile  Mhe. Rais Magufuli atapata fursa ya kuongea na wananchi  kwenye Mkutano wa Hadhara Uwanja wa Ndege wa Bukoba.

Uchambuzi: Kama Urais Ungekuwa Wa Miaka Miwili..

$
0
0
Uchambuzi: Kama Urais Ungekuwa Wa Miaka Miwili..
Ndugu zangu,

Niliandika makala mara ile Rais John Pombe Magufuli alipotimiza Mwaka Mmoja akiwa madarakani.

Itakumbukwa, mwaka jana, na kwenye siku yake ya kuzaliwa, Rais wa Awamu ya Tano, Dr John Pombe Magufuli aliacha kula keki yake ya kusheherekea siku yake hiyo na kuamua kuwa kazini.
Zikatujia taarifa kubwa mbili katika siku hiyo; utenguzi wa uteuzi wa DCI na ziara ya kushtukiza wizara ya Maliasili na Utalii.

Niliandika, kuwa nataka niwe mkweli kwa nafsi yangu, kuwa hata kama tungekuwa, kama nchi, na utaratibu wa kuwa na Rais wa kipindi cha mwaka mmoja, basi, huyu tuliye naye sasa, John Pombe Magufuli, angekuwa amemaliza muda wake wa mwaka mmoja akiwa ameacha alama nyuma yake. Alama za kudumu muda mrefu.

Nikasema, kuwa ukweli nchi yetu imeanza kubadilika na fikra za watu wake pia zimeanza kubadilika. Maana, ilifika mahali, kuna walioacha kazi kwenye NGO- Mashirika yasiyo ya Kiserikali na kwenda kufanya kazi Serikalini ikiwamo kwenye Halmashauri zetu wakitamka wazi kuwa kwenye NGO kazi ni nyingi, wanarudi Serikalini na kwenye Halmashauri kupumzika na kula posho za safari na nyinginezo.

Nchi haiwezi kusonga mbele ikiwa na watu wenye mitazamo kama hiyo. Ni lazima kuwe na nidhamu ya utendaji kazi na kuheshimu sheria, kanuni na taratibu. Na wenye kukiuka hayo, ni lazima wajue kuna adhabu yenye kuendana na matendo yao maovu. Ndiyo siri kubwa ya nchi za wenzetu zilizoendelea.

Novemba 30, 2015 niliandika kwenye jarida la Raia Mwema, kuwa Magufuli ana uwezo wa kumwona bata na sungura kwa wakati mmoja.

Hii ni dhana kongwe ya kimtazamo iliyojengeka kifalsafa. Ni uwezo wa mwanadamu katika taswira moja kuwaona viumbe wawili wenye kufanana. Hivyo, inahusu uwezo wa kuliona jambo hilo hilo katika sura tofauti.

Ndio, kuna kuona kikiwa na kuona kama. Kuliangalia jambo kwa mtazamo tofauti.
Mwanafalsafa Thomas Kuhn yeye anazungumzia dhana ya ' Paradigm Shift'. Ni ile hali ya uwepo wa mapinduzi ya kifikra na ya kisayansi yenye kupelekea mabadiliko ya kimsingi katika jambo lile lile tulilokuwa na mazoea nalo.

Captain Thomas Sankara, kiongozi mwanapinduzi aliyeuawa wa Burkina Faso, katika wakati wake, alizungumzia umuhimu wa kuwa na ujasiri wa kuyapa mgongo mazoea ya kale.

Sankara aliacha hiba njema ya kuenziwa ndani ya nchi yake, Afrika na duniani. Mwanamapinduzi huyu alikuja kuawa kwa kupigwa risasi na wapinga mapinduzi na maendeleo ya Burkina Faso.
Sankara alipata kukaririwa akisema: “Ningependa kuacha nyuma yangu, imani ya kuwa, kama tunaimarisha kiwango fulani cha uangalifu na oganaizesheni, basi, tunastahili ushindi.

Kamwe huwezi kuleta mabadiliko ya kimsingi bila ya kuwa na kiwango fulani cha uwendawazimu. Hali hii inatokana na kutoshinikizwa na taratibu zilizozoeleka, kuwa na ujasiri wa kuzipa mgongo kanuni za kizamani, ujasiri wa kuanzisha mustakabali. Ni wendawazimu wa jana waliotuwezesha kuyafanya tuyafanyao leo. Ninataka kuwa mmoja wa wendawazimu hao.” (Hayati, Kapteni Thomas Sankara)
Yumkini tunachokishuhudia kwenye nchi yetu ni Magufuli's paradigm shift'. Hali ya kuwa na mabadiliko ya msingi.

Nimeona nini kwa Rais Magufuli baada ya miaka miwili?
Kama Urais ungelikuwa wa miaka miwili, basi, Rais tuliye naye, Dr John Pombe Magufuli, angeondoka akiwa ameacha alama chanya za kudumu milele.
Maana, akiingia mwaka wake wa pili, ninachoona ni upepo chanya wa Magufuli wenye kuendelea kuvuma, ndani na nje ya mipaka.

Huo ndio ukweli mwingine ningependa kuusema. Nimepata bahati ya kusafiri sehemu mbali mbali za nchi. Nimekuwa na mazoea ya kuzungumza na waananchi kupata mitazamo yao.
Mahali pengi kabisa, John Magufuli yumo kwenye midomo ya Watanzania wa kawaida walio wengi ikiwamo vijana ma-bayaye wanaoongezeka kwenye miji yetu.
Kwanini?

Naamini, John Magufuli amefaulu kufanya kile watangulizi wake hawakufaulu, ukimwacha Mwalimu. Magufuli sio tu amebeba ajenda ya vita dhidi ya ufisadi, rushwa na uhujumu uchumi, Magufuli anaifanyia kazi ajenda hiyo na watu wanaona ikifanyiwa kazi.
Ni kwa kiwango kile ambacho Hayati Sokoine alikuwa anakwenda nacho na akawa kipenzi cha umma.

Nimeandika huko nyuma, kuwa kero nambari moja kwa Watanzania kuelekea Uchaguzi Mkuu uliopita ilikuwa Rushwa na Ufisadi, kero nambari mbili ilikuwa Rushwa na Ufisadi, na kero nambari tatu ni Rushwa na Ufisadi. Hivyo, hiyo ndio ilikuwa ajenda kuu.
Huko nyuma upinzani, tofauti na CCM, ndio ulibeba ajenda hiyo, wakaipoteza njiani, sasa upinzani unahangaika kutafuta ilichokuwa nacho.

Ndio maana, tofauti na huko nyuma, maeneo mengi nilimopita, huwezi sasa kuona tofauti za wananchi za kiitikadi, wote wanajadili ajenda moja, ya kupiga vita ufisadi na hali zote zenye kurudisha nyuma maendeleo yao. Wanamuunga mkono Rais John Magufuli. Hao ni Wana CCM na Wana- Chadema.

Jipya jingine ndani ya miaka hii miwili ni kitendo cha Rais Magufuli kuruhusu wananchi kutoa kero zao hadharani kwa kuandika kwenye mabango. Hali hii inaongeza uwajibikaji na kuwatia kiwewe viongozi warasimu na wenye kuwanyanyasa wananchi. Hawa huko nyuma walijificha kwenye risala kwa Rais ambayo ilikuwa na maana ya kumsomea Rais taarifa ya kumfurahisha na wananchi hawakuwa na pa kumsomea Rais risala inayotokana na wao wananchi. Siku hizi inawezekana kupitia mabango.

Wananchi wanamuunga mkono pia Rais Magufuli kwa nia yake ya dhati ya kusimamia rasilimali za taifa hata kuwa tayari kugombana na matajiri wamiliki wa makampuni makubwa ya uchimbaji madini.

Haijawahi kutokea wala kufikiriwa , kuwa, kama nchi, tungeweza kutunisha misuli na kufanikiwa kushinda kwenye meza ya majadiliano, kwenye kudai kipande kikubwa cha keki kwa maana ya kinachopatikana kutokana na uchimbaji wa madini yetu. Vita hivi vya kupigania rasilimali zetu. Vita hivi anavyoviongoza Rais John Magufuli vimemsogeza karibu zaidi kwenye mioyo ya wananchi ambao huko nyuma walianza kukata tamaa.

Kimataifa, Rais John Magufuli ametolewa mfano wa kuwa kiongozi mwenye kusimamia uwajibikaji. Nimepata kuongea na maafisa wawili waandamizi wa Balozi za Kimagharibi walioniambia wazi kuwa Rais Magufuli anafanya vema sana kwenye eneo la uwajibikaji na kukuza uchumi.
Mwingine akafikia kuniambia kuwa, haijawahi kutokea kwa Serikali ya Tanzania kurudisha fedha za misaada ambazo hazikutumika au zimepotea kutokana na ufisadi. Ndani ya miaka hii miwili, kwa mshangao wa afisa yule wa Ubalozi niliyeongea nae, ameniambia kuwa Balozi yao imepokea fedha ambazo Tanzania ilikuwa inadaiwa irudishe.
Nini tafsiri ya jambo hilo?

Kwa mujibu wa afisa yule wa Kibalozi, kubwa kabisa Serikali inayoongozwa na Magufuli sasa inaaminika na wahisani na mabenki yenye kukopesha. Kwamba kuna usimamizi na ufuatiliaji wa fedha za miradi ya maendeleo. Kwamba sasa si rahisi fedha kuliwa na wajanja na kwamba zitafanya yale yenye kuwaletea wananchi maendeleo.

Nini siri kubwa ya hatua hii mpya? Nilimwuliza afisa yule wa Ubalozi;
" Ukiwa na Rais aliye juu na anayesimamia kwa vitendo yale yanayotakiwa kufanyika, basi, huku chini watendaji hubadilika haraka na kufanya kilicho sahihi na hata kuwa na hofu ya kufanya ufisadi." Alianiambia afisa yule wa Ubalozi.
Nini faida na hatari ya mafanikio haya ya Rais Magufuli ?
Kwa nchi, hii ni fursa pekee ya kuungana na kumkabili adui aliye mbele yetu na aliyetufikisha hapa tulipo. Waliotufikisha mahali ambapo akina mama na watoto wetu wakakosa dawa na huduma nyingine.

Wananchi wakakosa mabomba ya maji na mengineyo, huku wachache wakichota fedha za umma kwa rushwa na ufisadi.
Baada ya miaka hii miwili, hatusomi tena habari za ufisadi mkubwa ukifanyika kwenye halmashauri na kwengineko Serikalini.

Hatari ninayoiona mbele yetu ni pale tunapokuwa na Rais mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa na kiuongozi ndani ya Chama chake na Serikali. Rais anayekubalika na wananchi wengi.
Kwamba akitumia vema ushawishi huu, na kwa kutanguliza hekima na busara, nchi yetu itakuwa mfano katika bara hili, ikiwamo pia kuimarisha misingi ya kidemokrasia na utawala wa sheria.
Lakini, kama Rais mwenye haya, akaja akaota mapembe, basi, hapo itabaki kuomba majaaliwa ya maanani.

Maggid Mjengwa.

Mawaziri wa Zamani Wanavyogeuka Bubu..Soma Magazeti ya Leo Jumapili

$
0
0

Mawaziri wa Zamani Wanavyogeuka Bubu..Soma Magazeti ya Leo Jumapili

Kutana na Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed Kutoka Bagamoyo...Ana Dawa za Kurudisha Mapenzi na Zingine Nyingi

$
0
0
MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

USHAURI: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.


Aunt Ezekiel Afunguka Bongo Movie Kukimbilia Siasa, ‘ni Kukosa Kazi’

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo, Aunt Ezekiel ameeleza sababu za baadhi ya wasanii wengi wa Bongo Movie kukimbilia katika matukio ya kisiasa.

Muigizaji huyo amesema kukosa kazi kunapelekea hilo kwa asilimia kubwa pamoja na umaarufu ambao una sababisha msanii akifanya kidogo tu inaonekana amejitoa sana upande huo.

“Ni kutokana na kukosa kazi kwa sababu mwisho wa siku kazi zetu zimekuwa hazina ushindani, tumesimama katika kazi zetu, so tunajikuta hata yale ambayo hayatuhusu tunaenda kuyaingilia” Aunt Ezekiel ameiambia Times Fm.

Ameendelea na kuongeza kuwa, ‘na kwanini unaona ni Bongo Movie ndio wanashiriki, siyo kwamba ni wao tu, unaweza kukuta wananchi wengi wanashiriki lakini sisi ni puplic figure ukishiriki hata kidogo inaoneka umeshiriki kikubwa”.

Hata hivyo amesema kwa upande wake kwa sasa amejitenga mbali kidogo na mambo ya siasa kwa vyama vyote na hajafanya hivyo tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

MOBETTO: “Nimeviona Vya Diamond Kuliko yeyote”

$
0
0

Mrembo Hamisa Mobetto usiku wa October 13 2017 alifanya Party ya mtoto wake ambae amezaa na Mwimbaji Diamond Platnumz ambapo kwenye hiyohiyo party Hamisa alikubali kuhojiwa na Soudy Brown na kujibu maswali mbalimbali.

Miongoni mwa maswali aliyoyajibu ni kama anamchukia Zari ambapo alisema hamchukii na wala haoni kama chuki zinasaidia, anatambua kwamba watoto wao ni ndugu ambapo pamoja na yote wanayopitia kama Wazazi anaamini kuna siku watapatana.

Mengine yote aliyosema Hamisa yako kwenye hizi video hapa chini unaweza kujionea mwanzo mwisho na party ilivyokwenda.

TAZAMA VIDEO:

Abiria Wakumbwa na Taharuki Baada ya Daladala Kuzima Ghafla Katikati ya Reli

$
0
0
Abiria wa daladala inayofanya safari kati ya Gongo la Mboto na Makumbusho jijini Dar es Salaam, jana walikumbwa na taharuki baada ya basi hilo kuzimika katikati ya reli.

Hatua hiyo ilisababisha abiria hao kuruka kupitia madirishani ili kujinusuru huku treni ikiwakaribia.

Tukio hilo lilitokea jana majira ya asubuhi, eneo la kituo maarufu kama Bakhresa, Buguruni, barabara ya Mandela na kuwafanya abiria kusukumana na baadhi wakigombea kupita katika mlango.

Chanzo cha kuaminika kilisema  kuwa daladala hiyo yenye namba za usajili T 499 BGU na ubavuni namba S 108648 D ilizimika ghafla katikati ya reli huku kwa mbali wakiiona treni ya kutoka ubungo kwenda Stesheni katikati ya jiji, maarufu kama ‘treni ya ‘Mwakyembe’ ikikaribia eneo walilokwama.

“Abiria walikumbwa na taharuki huku wakiruka madirishani na wengine kugombea kupita mlangoni kujinusuru kugongwa na treni,” alisema mmoja wa abiria walionusurika.

Alisema kilichowasaidia kutopatwa na maafa ni kitendo cha dereva kusimamisha treni ili kupisha daladala hiyo kuondolewa katika njia yake.

Baadhi ya abiria waliokuwamo kwenye daladala hiyo, walisema tangu wakitoka Gongo la Mboto, ililonekana kuwa na matatizo na kwamba baada ya tukio hilo, abiria walioruka kwenye daladala hilo hawakurejea tena kupanda kwa kupatwa na hofu.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo Jumapili..

$
0
0

Kwa Nini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo?

$
0
0
KWA NINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE  MADOGO?

Matatizo haya yame kuwa yakiwaathiri watu wengi sana kisaikolijia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wenzao kwa kawaida mwanaume ana takiwa awe na uume kuanzia inch(6_8)  vinginevyo mtu huyo atakuwa na matatizo.



Zipo sababu nyingi zinazo sababisha tatizo hilo  baadhi ni upungufu wa  vichocheo (Hormones za Getrogen) Ambazo  mwanaume akisha balehe vichocheo hivi huchochea  ukuaji wa  uume, chango husababisha NEVA ambayo huathiri misuri ya uume.

Ngiri ambayo Huleta maumivu ya tumbo kuunguruma  na kujaa guess, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri , miguu kufa ganzi, maumivu ya kiuno,upigaji wa punyeto sababu hizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembaba na mara kwa mara hipelekea kupunguka kwa nguvu za kiume na ham ya tendo la ndoa hukosekana na kuisha kabisa

NSUMBU:__Ni dawa dawa inayo zalisha hormones za Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.

NZAGI :--Ni dawa bora ya kurudisha  nguvu za kiume na kukupa hamu ya kurudia tendo la ndoa mara dufu utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4)bila hamu kuisha (kuchoka) dawa hii ni tiba kamili kwa matatizo hayo. Dawa hii pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk(15_30)kwa tendo moja la ndoa dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji kuanzia miaka(18_90)wana ruhusiwa kuzitumia

Pia tunatibu KISUKARI, PRESHA, PUMU, MALARIA SUGU, MIMBA KUHARIBIKA(Chango)

POWER :__Ni dawa ya mitishamba inaongeza hips, (makalio), miguu, ina punguza maziwa (chuchu). Ina toa harufu mbaya sehem  za siri Nk. Pia anazo dawa za  mvuto wa mapenzi,biashara, kurudishwa kazini, kumuita aliye mbali kwa mda mfupi tu OSTADH JUMA ANAPATIKANA MALARIA ZAKHIEM SIMU:_0769-597778 au 0784-002216 au 0627457957 Wote mnakaribishwa

"Kuichagua CCM ni Kufurahia Mateso" - Tundu Lissu

$
0
0
Mbunge Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu ametuma ujumbe kwa wapiga kura kwenye kata zenye uchaguzi ya kwamba kuwapatia kura za ushindi Chama Cha Mapinduzi ni kufurahia na kuruhusu mateso.

Ujumbe huo kutoka kwa Lissu kwenda kwa wapiga kura umefikishwa na Diwani wa Sombetini  Arusha, Ally Bananga ambaye amefika hospitali ya Nairobi nchini Kenya anakopatiwa matibabu mbunge huyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Bananga ameandika, "Nendeni mkawaambie watu kwenye kata zenye uchaguzi kuipa kura ccm ni kufurahia na kuruhusu mateso yetu yaendelee!!...."  Ujumbe alioutoa Lissu kupitia diwani Bananga

Ameongeza kwamba 'Hawa watesi wetu wako katika hatua za mwisho, kama wanajiamini kwa nn wanawawekea mizengwe wagombea wetu ili wao wapite bila kupingwa"

JE ni Kweli Kufanya Mapenzi Wakati Unanyonyesha Kunabemenda Mtoto? Jibu Lipo Hapa

$
0
0
Kumbemenda mtoto ni mtoto kutokua vizuri ikidhaniwa kutokea kutokana na mama anayenyonyesha mtoto kukutana kimapenzi na mwenzi wake hasa kipindi mtoto bado ni mchanga na ananyonyeshwa.

Hii ni dhana iliyopo katika jamii mbalimbali, na inadhaniwa hutokea kwa sababu mtoto kunyonya maziwa yenye mbegu za kiume zilizoingia kwenye maziwa baada ya kufanya mapenzi.

Je, kuna ukweli wowote?
Hapana. kiukweli na kiutaalamu dhana hii si sahihi kabisa!
kufanya mapenzi na mwenzi wako baada ya kujifungua hakuwezi kusababisha afya ya mtoto kuzorota. mwanamke anapokutana na mwanaume kimapenzi, shahawa huingia kwenye tumbo la uzazi na kubaki huko. haziingii kwenye damu wala haziwezi kufika kwenye maziwa. dhana ya kuwa shahawa huingia kwenye maziwa na kumuathiri mtoto sio sahihi.

Ni baada ya muda gani mwanamke aliyejifungua anaweza kufanya mapenzi?
unaweza kuanza kufanya mapenzi tena baada ya maji maji yenye damu ya uke (lochia) kuacha kutoka ambayo ni kama wiki 3 mpaka 4 baada ya kujifungua, na wewe kujisikia vizuri na kuwa tayari kushiriki katika mapenzi. pia, mnaweza kusubiri mpaka wiki 6 zipite toka ulivyojifungua.

Je, kuna athari yoyote ya kufanya mapenzi baada ya kujifungua?
Kufanya mapenzi baada ya kujifungua hakuwezi kuleta madhara kwa mtoto endapo hamna maambukizi ya magonjwa kama virusi vya ukimwi (vvu). ikiwa mwanaume ana vvu anaweza kumuambukiza mama na kisha mtoto kuambukizwa kupitia maziwa ya mama.

Ikiwa mnafanya mapenzi kabla ya damu damu ya ukeni kukata, maambukizi ya bakteria yanaweza kutokea kwenye tumbo la uzazi (endometritis). pia kuna uwezekano wa mama kupata ujauzito miezi 6 ya kwanza ya kunyonyesha.

Nini kinasababisha afya ya mtoto kuzorota?
Kama tulivyoona, kufanya mapenzi hakusababishi mtoto kubemendwa. afya ya mtoto inaweza kuzorota kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo;

Kukosa maziwa ya mama ya kutosha
Mtoto kushindwa kunyonya vizuri
Kuanzishiwa vyakula vya ziada mapema, kabla mtoto hajafikisha miezi 6 au vyakula visivyo na viritubisho vya kutosha.
Homa, nimonia na maambukizi ya mfumo wa mkojo (uti) za mara kwa mara.
Maambukizi ya magonjwa kama virusi vya ukimwi (vvu) au kifua kikuu.
Matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo (congenital heart diseases).

Kufanya mapenzi na mwenzi wako hakusababishi mtoto kubemendwa. baada ya kujifungua mtoto hutegemea kupata lishe bora kutoka kwenye maziwa ya mama, hivyo nyonyesha mtoto wako vizuri. ukiona ukuaji wake unazorota, onana na daktari.

Hii inakuaje...Hapa Mjini Jirani Mrembo Anakuja Kwako zaidi ya Mara Mbili Anakuuliza Kama una Mchi/Mtwangio?

$
0
0
Nmeshangaa sana kwa huyu dada mrembo ambaye anakaa kwenye apartment za hapa karibu nami. Si za mwanzao tulionana tulikuwa tunafanya jogging kishkaji tu. Akanisalimia nami nikamjibu kwa pozi za ki jentroman maana alivaa track suit mwili wake tipwa tipwa ulikuwa umechoreka hasa.

Basi tukawa smetme tunaonana asub tunapoenda kazini na weekend pia mara chache sana.siku moja nkasikia alarm getini nikaenda kutaka kujua ni nani. Nikamkuta amevaa kaptula nyepes sana nlishtuka sana maana allahamdulilah mtoto ana mwili wake.

Akaniuliza eti nina mchi?anataka amejisikia hamu ya kisamvu anataka kutwanga. Nikamwambia hapana mi huwa sina vitu vya kutwanga.akashangaa akacheka nakosaje mchi wakat vya kutwanga ving tu. Basi tukabadilishana mawazo akaaga.

Siku nyingne tena akaja akanambia anataka mchi anataka kutwanga viungo anataka pika sijui chakula gani.nikamwambia sina.akasema " na wewe sasa ununue Mchi mi nina kinu... ili tuwe tunasaidiana maana na wewe hujaoa...." Nikamwambia sawa. Akanambia "promise utanunua" nikamwambia i promise.

Leo asubuh hii kaja kunipitia twende jogging tumekimbia kimbia kishkaj tumerudi akanambia ataniandalia breakfast ila pia nikumbuke ahadi ya kumpatia mtwangio.

Wadau mi hata sijui hivyo vitu vinauzwa wapi. Sikuwah kuwaza kama ntahitaj kuwa na kitu cha kutwanga.na huyu dada why aone tu mi ndo wa kumpatia mtwangio?nikimwambia asage na blender anasema hatak anataka mchi na mimi ndo nikatwange.

Sasa jaman mjini hapa hayo mambo ya kutwanga wapi na wapi?tulishawekewa blender na wazungu kurahisisha yeye anataka tu mtwangio wangu.nawaza hapa nafanyaje nimpatie hitaj lake maana anaweza ona kama si keep promise.

Ananambia akinitizamana anapata picha kama nitatwanga vizuri mpaka vitu vyake vilainike hasa.

Wadada mnapenda kuomba vitu ambavyo ni weird sana. Mjini hapa dar haya maisha yetu unang'ang'ania mtwangio toka kwa bachelor?nawaza au ni njia tu ya kuwa anaongea ongea na mimi baada ya kuona ni mpole sana?

Nikakumbuka mimi kipindi flan nliwah mng'ang'ania dada mmoja anipatie kitumbua. Nlimkuta ameshika kitumbua anakula.basi nikawa nmependa nikamwambia anipatie kitumbua chake akanipa kidogo.nikamwambia anakitumbua kitamu sana.alicheka akaniuliza nimejuaje.nikashangaa ananiona nmekula na anauliza nmejuaje kama ana kitumbua kitamu.basi nikamwambia tu" nmeona kilivyo"

Basi akanambia siku moja ntakupa halaf unambie.basi nikawa namsumbua kila mara "Fatma ahadi yako ya kitumbua" akawa anacheka sana "we mkaka hutaniwi heeehh king'ang'anizi kama ruba" nami nikashikiria hapo hapo mpaka siku alipokuja home kuniletea kitumbua chake kilikuwa kimepikwa vizuri kina ng'aa kimevimba. Aisee.... Mi sihami Mjini. Hata nchi ihamishiwe Dodoma mi ntabak dar maeneo yangu ya Kijitonyama, kinondoni na Mwenge.siendi Mbali sana na Jiji.

By GuDumeF
Jamii Forums

Ubuyu Exclusive: Inasemekana Eti Tunda Abeba Mimba ya Diamond

$
0
0
Kwa habari za kunyapia nyapia zinadai kuwa video vixen mwenye mvuto wa hali ya juu nchini Tanzania na Africa kwa ujumla Tunda Sabasita amebeba ujauzito wa msanii Diamond Platinums

Wawili hao inadaiwa kuwa wameanza uhusiano wa kimapenzi muda mrefu sana ila wanajitahidi sana kujificha ili penzi lao lisigundulike haraka mpaka pale muda muhafaka utakapo wadia kuweka wazi uhusiano wao.

Lakini siku zote bwana mapenzi ni kikohozi hakiwezi kufichika ,mwanadada Tunda ameonesha dalili zote za kushindwa kuvumilia suala hilo na kwa namna moja au nyingine amekuwa akionesha mahaba yake ya dhati kwa msanii diamond platinums.

Na ameenda mbali zaidi kwa kuamua mpaka kuweka dp ya diamond platinums kwenye account yake ya Instagram Screenshot_2017-11-05-00-15-50.jpg

Haya sasa vita ya Zari vs Hamisa Mobeto tupa kule

Habari ya mujini kwa sasa ni Zari vs Tunda

Je Zari ataweza tena kuvuka changamoto hiii????


Maoni ya Wadau Baada ya Tundu Kupost Picha ya Diamond:




Nnape Nauye Amjia juu mtu Kwenye Twitter yake..Amwita Mchawi

$
0
0
 Mbunge wa jimbo la Mtama (CCM) Nape Nnauye ameonyesha kukasilishwa na moja ya shabiki katika mtandao wake wa Twitter ambaye amemzihaki na kumwita mnafiki kutokana na ujumbe alioweka, Nape amedai watu wa namna hiyo ni zaidi ya wachawi.

Leo asubuhi Nape aliweka ujumbe kupitia mtandao wake unaosomeka "Usivunje mtungi kwa sababu ya panya aliyemo ndani ya mtungi, inamisha taratibu, fanya 'timing', utaua panya na mtungi utabaki salama"

Baada ya kuandika ujumbe huo ndipo moja ya mtu akaja na kumwambia kuwa kiongozi huyo amekua mnafiki baada ya kuvuliwa nafasi ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na kudai kuwa kiongozi huyo amekuwa akiomkosoa boss wake, jambo ambalo Nape Nnauye wiki iliyopita alisema anachukizwa kuona watu wakichukua mambo yako na kuyahusisha na kumsema au kumkosoa Rais jambo ambalo si la kweli.

"Mkuu we mnafiki sana yote hayo umeanza baaada ya kuvuliwa uwaziri 'come on' kiongozi bora si  yule anaonekana mkosoaji kwa boss wake" aliandika Majdy Wiliam

Mawaziri wa Zamani Wanavyogeuka 'Bubu'

$
0
0
Kila wakati Rais anapofanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, kuna uwezekano wa kuingiza sura mpya, lakini pia kuacha baadhi.

Katika hali hiyo, idadi ya wabunge waliowahi kuwa mawaziri inazidi kuongezeka ndani ya Bunge, ambalo ni chombo cha kuisimamia Serikali, kuiwajibisha na kutunga sheria.

Mabadiliko yaliyofanywa na Rais John Magufuli hivi karibuni, yameongeza idadi ya mawaziri wanaorudi katika viti vya kawaida, na kumrudisha mmoja, George Mkuchika katika Baraza la Mawaziri.

Ndani ya muhimili huo wa nchi, sasa kuna takriban wabunge 30 waliopata kuwa mawaziri na manaibu katika tawala zilizopita zilizokuwa chini ya Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na sasa wa Rais John Magufuli.

Wakiwa ndani au nje ya Bunge, wamekuwa hawaonekani kuwa wakosoaji katika mijadala ya Bunge, ingawa wanaweza kutoa maoni yao kwa maandishi bila ya kuzungumza bungeni.

Kati yao ni wachache ambao wameonekana kusimama na kuikosoa Serikali, wakiongozwa na Charles Kitwanga, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Hawa Ghasia, ambaye alikuwa Waziri wa Tamisemi hadi Novemba 2015.

Baadhi wanapoamua kukomaa huelekeza vita yao kwa mawaziri binafsi, kuonyesha kuwa ndio wanaoishauri vibaya Serikali.

Idadi hiyo ya wabunge, waliokula kiapo kutotoa siri za Serikali, inaongeza nguvu katika hoja ya wananchi katika mchakato wa kuandika Katiba mpya kuwa mawaziri wasitokane na Bunge.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Richard Mbunda alisema wabunge hao wanashindwa kutekeleza kikamilifu majukumu yao ya kibunge kutokana na kuwahi kuwa ndani ya Serikali.

Alisema baadhi ya matatizo kama mikataba mibovu, sheria zisizojali rasilimali za nchi zimepitishwa na mawaziri na manaibu ambao walikuwapo katika baraza la mawaziri, hivyo kukosoa ni sawa na kujivua nguo.

“Unajua unaweza kukuta, kipindi akiwa ndani ya Serikali kuna makosa aliyafanya, hivyo anashindwa kuwa na uwezo wa kuikosoa kwa kuwa anajua kabisa akifanya hivyo yanaweza kumgeukia,” alisema. “Anayeweza ni yule aliyetekeleza majukumu yake vizuri.”

Miongoni mwa wabunge waliowahi kuwa mawaziri na kukosolewa sana kila mijadala inapoibuka na William Ngeleja, Andrew Chenge, Anna Tibaijuka, Ezekiel Maige na hivi sasa George Simbachawene.

Mbunda alisema ili kuwepo na Bunge imara, mawaziri wasitokane na Bunge.

Aliyewahi kuwa Naibu Waziri katika Serikali ya Awamu ya Nne, Dk Makongoro Mahanga alisema “wanashindwa kuikosoa Serikali kwa kuwa wanaogopa wanaweza kutumia fursa hiyo kutoa siri za Baraza la Mawaziri hivyo inabidi watumie mbinu nyingine.

Dk Mahanga, ambaye amehamia Chadema, alisema si mawaziri au manaibu tu hata wabunge wengine wa CCM ambao hawajawahi kushika nyadhifa hizo, wamekuwa waoga kutokana na chama kuwabana. “Ndio maana mtu kama (aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro) Nyalandu ameamua kutoka huko kwani ukiikosoa Serikali, unachukuliwa hatua za kichama. Wapo wachache wanaofanya hivyo ila wengi wao ni waoga,” alisema

Baadhi ya wabunge hao ni Dk Mary Nagu (Hanang’), Chenge (Bariadi), Sospeter Muhongo (Musoma Vijijini), Profesa Jumanne Maghembe (Mwanga), Charles Kitwaanga (Misungwi), Mhandisi Gerson Lwenge (Wanging’ombe), George Simbachawene (Kibakwe),

Wengine waliobahatika kushika uwaziri au unaibu ni Nape Nnauye wa Mtama, Mhandisi Isack Kamwelwe (Katavi), Anastazia Wambura (viti maalum) na Ramo Makani (Tunduru Kaskazini).

Wengine ni Ezekiel Maige (Msalala), Profesa Anna Tibaijuka (Muleba Kusini), Hawa Ghasia (Mtwara vijijini) na Shamsi Vuai Nahodha (Kijitoupele).

Pia wapo Dk Shukuru Kawabwa (Bagamoyo), Stephen Masele (Shinyanga Mjini), Saada Mkuya (Welezo), Janeth Mbene (Ileje), William Ngeleja (Sengerema), Anne Kilango Malecela (kuteuliwa) na Daniel Nsanzugwanko (Kasulu Mjini).

Wengine ni Margaret Sitta (Urambo), Dk Diodorus Kamala (Nkenge), Juma Nkamia (Chemba), Philipo Mulugo (Songwe), Dk Haji Mponda (Malinyi) na Mahmoud Mgimwa wa Mufindi Kaskazini.

By Ibrahim Yamola, Mwananchi iyamola@mwananchi.co.tz

Mange Kimambi Ampa Hamisa Mobetto Mbinu Kabambe za Kumshughulikia Diamond Kuhusu Kulea Mtoto Wake

$
0
0
By Mange Kimambi

"Nimepitia kidogo sheria ya matunzo ya mtoto ya Tanzania. It seems sheria hiyo ipo sawa na sheria ya Marekani . Wanaangalia kipato cha wazazi na matunzo yanatolewa kulingana na kipato cha mzazi. I think Tatizo lililoko TZ ni kwamba wanawake wengi huwa wanashindwa kuprove mahakamani kipato cha mwanaume.
.
Hamisa don’t take it for granted kuwa umezaaa na Diamond. Kama utashindwa kupeleka ushahidi wa kipato chake unaweza pewa matunzo ya laki kwa mwezi... So please be very careful.
.
.
Kwanza ujue Diamond hawezi kusema kipato chake cha kweli mahakamani, you have to force him. Ila mwache kwanza aidanganye mahakama kuhusu kipato chake ndo wewe utoe ushahidi.... Je unapataje ushahidi? Ushahidi wa kwanza ni uombe mahakama ikupe order ya bank account zake zoooooote. Bank zooote unazozijua Dai anaweka pesa zake wapelekee order ya mahakama kuwa wawakilishe mahakamani statement za Diamond from 1Jan 2015 mpaka sasa hivi.
.
Kampuni zooote zilizoratibu show zake the last one year wapelekee order ya mahakamani watoe contract . Pamoja na kampuni zilizompa matangazo,kwa mfano Danube, Vodacom na wale Diamond Karanga. Wooote wachape barua za mahakamani wawasilishe mikataba. .
.
Then peleka order ya mahakama kwa kampuni ya WCB na ile ya website wanayouza nyimbo za wasaniii ambayo yuko share ya Kusaga. Pamoja na Chibu Perfume ambazo pia yuko share na kusaga. Mchape barua kusaga na hizo kampuni waonyeshe ownership na income.
.
.
Ukitoka hapo wachape barua TRA kutoa record ya malipo yake ya TRA
.
.
Ila cha kwanza ni statement za benki pesa zake im sure haziwekagi chini ya uvungu.
.
.
You need a good family lawyer sio lawyer ilimradi lawyer jina. Personally I recommend Mama Tenga, Huyu mama wa kipare hana mchezooooooo Diamond atatoa matunzo ya maana. Babangu hakuacha will ila Mama Tenga alinipigania nikapata haki yangu.
.
.
Cha mwisho kabisa, please usisusie matunzo, ukisusa watafanya sherehe, ndio wanachotaka ufanye. fight for your son. Huyo Bi sandra hata aposti nini mdharau mtu mzima hovyo yule. Kama ulifight mpaka Dai akamkubali mtoto hadharani basi fight mpaka mtoto apewe matunzo yanayoendana na kipato cha babake"
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live


Latest Images