Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live

Sikiliza Jinsi Adamu Mchomvu, DJ Fetty na B 12 Walivyokuwa Wanapigana Huku Wakio Live Redioni

$
0
0
Leo Kwenye Kipindi cha XXL Watangazaji wa Clouds Walipiga Ngumi Live Live Huku wakiwa wamesahau Kuzima Mike Ambapo wasikilizaji tulisikia kila kitu jinsi walivyokuwa wakirushiana mangumi....
Sikiliza Hapa Jinsi ilivyokuwa:


Balozi wa Libya Ajiua kwa Risasi Ofisini Dar

$
0
0
 Balozi wa Libya nchini Tanzania, Ismail Nwairat, amejiua kwa risasi jana ofisini kwake, katika tukio la kwanza la aina yake nchini kwa kigogo wa ubalozi kuondoa uhai wake.

Hadi sasa haijafahamika sababu za kujiua kwa balozi huyo ambaye alikuwa akipingana waziwazi na sera za utawala ulioondolewa madarakani wa Kanali Muhamar Gaddafi, aliyeuawa wakati wa mapinduzi Oktoba 2011.

Habari zilizopatikana jana na kuthibitishwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa zilisema kuwa Nwairat alijifungia kwenye ofisi yake iliyopo Mtaa wa Mtitu, Barabara ya Umoja wa Mataifa na kujifyatulia risasi upande wa kushoto wa kifuani.

Msemaji wa wizara hiyo, Mkumbwa Ally alisema baada kusikia mlio wa bunduki majira ya saa 7:00 mchana, maofisa ubalozi walivunja mlango wa ofisi hiyo na kumkuta Nwairat ameanguka chini.

“Tumepata taarifa hizo na kubaini kuwa lilikuwa ni tukio la kujiua, marehemu alikutwa na risasi moja kifuani,” alisema Ally.

Alisema baadaye walimpeleka balozi huyo Hospitali ya AMI, Oysterbay ambako ilielezwa kuwa alikuwa ameshafariki dunia. Kwa sasa mwili wa balozi huyo umehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuhifadhiwa kabla ya kusafirishwa kwenda kwao Libya.

Ally alisema hadi sasa hawajafahamu sababu za balozi huyo kujiua kwa kuwa hakuacha ujumbe wowote.

Nwairat anajulikana kwa kuwa mpinzani wa wazi wa utawala wa Gaddafi, ambaye alikuwa kiongozi wa kijeshi wa Libya tangu alipoingia madarakani kwa mapinduzi mwaka 1969.

Katika hafla ya kuadhimisha miaka mitatu ya mapinduzi ya Libya iliyofanyika Machi 9 jijini Dar es Salaam, Balozi Nwairat aliuelezea uongozi wa Gaddafi kuwa wa ukandamizaji, wa kiimla, usiotumia katiba na ambao uliwanyima wananchi wake haki ya kujieleza ndani na nje ya nchi hiyo.

Kuhusu taratibu za mazishi, Ally alisema kwa sasa Wizara inafanya inafanya jitihada kushirikiana na wafanyakazi wa ubalozi huo pamoja na ubalozi wa Tanzania Libya kuangalia taratibu za kusafirisha mwili huo.

“Serikali itawapa ushirikiano wote watakaohitaji ili kufanikisha mwili wake kusafirishwa na atapewa heshima zote za kidiplomasia kama inavyotakiwa na kama wafanyiwavyo mabalozi wote,” alisema.

Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, pamoja na kueleza kufahamu tukio hilo, alisema angetoa maelezo ya kina leo katika mkutano maalumu na wanahabari.

Ray' Sasa Nimerudi Kazini Nitarudisha Bongo Movies Kama Enzi za Marehemu Kanumba'

$
0
0
MUONGOZAJI na mwigizaji mahiri katika tasnia ya filamu Swahilifilamu Vincent Kigosi ‘Ray’ amesema kuwa hajatoweka katika tasnia ya filamu bali alikuwa akijipange kwa ajili ya kuangalia soko la kimataifa kwani soko la ndani tayari wamelishika.

Ray anasema kuwa wapenzi wa kazi zake wajiandae kupokea kazi mpya ambazo zipo tayari zinakuja huku akiwa ameendelea na mpango wake wa kuendelea kuibua vipaji vipya ambavyo vitakuwa nyota baada ya kazi hizo kutoka.

Samahani sana wadau wangu, naombeni sana mnisamehe kwa kupotea kwa kipindi kirefu, na yote haya yanatokana na majukumu ya kufanya kazi kimataifa zaidi, soko la ndani tumefanikiwa, nisingependa kuja kwenu na mikono mitupu, hivyo mtarajia kazi zenye ubora”anasema Ray

Video Nzima Edzen Jumanne Akeleza Jinsi Ndoa Yake na Dida Ilivyovunjika, Kumbe Big Brother Ndio Tatizo

$
0
0


Stori: Deogratius Mongela na Chande Abdallah

SIKU chache baada ya kuvunjika kwa ndoa ya Khadija Shaibu ‘Dida’, aliyekuwa mumewe, Mtangazaji wa TV1, Ezden Jumanne ameibuka na kutoa sababu kuu tatu za kutengena kwao, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi.

Akizungumza na waandishi wetu katika nyumba aliyohamia kwa sasa, Kijitonyama, Dar, Ezden alisema mgogoro kati yake na Dida ulianza zamani ambapo Dida alikuwa na tabia ya kurudi usiku mnene, Ezden alidai kadiri siku zilivyozidi kusonga mbele, tabia hiyo ilizidi kuonekana ingawa alikuwa akimuonya mara kwa mara.

BIG BROTHER NDIYO TATIZO
Pamoja na sababu hizo, Ezden aliitaja sababu kuu iliyoanza kuzua mgogoro uliosababisha kuvunjika kwa ndoa hiyo ni Shindano la Big Brother Africa linalotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu nchini Afrika Kusini.


Alisema siku moja mtalaka wake huyo alimweleza kuwa kuna rafiki yake aliyemtaja kwa jina la Furaha amempa mchongo wa kuwa mgeni staa (celebrity guest) ndani ya Jumba la Big Brother na kumuomba ampe ridhaa ya kwenda huko.

Akizidi kumwaga data mbele ya kinasa sauti cha Risasi Mchanganyiko, Ezden alisema:
“Nilimruhusu kwa moyo mmoja ambapo pia aliniomba nimsaidie kumpa uzoefu juu ya lugha ya Kiingereza ili akaendane na kanuni za Big Brother.

“Kama mume nilimsapoti kwa nguvu zote, siku nyingine kama nikiwa nimerudi nyumbani mapema mimi mwenyewe nilikuwa nikimfundisha ‘tense’ mbalimbali.”
Katika aya nyingine, Ezden alisema kuna siku Dida alimfungukia kuwa hatakwenda Big Brother kama mgeni staa kwani anatakiwa kuingia kama mshiriki na kumwambia kuwa alikuwa akiogopa kumwambia ukweli mapema.

“Nilimkatalia ndipo alipocharuka, huwezi amini alifikia hatua  ya kusema nambania zali lake. Niliumia sana siku ile ikabidi nimuulize kama anaithamini Big Brother kuliko ndoa yake, hakunijibu.
“Kama mume ilibidi niwaulize wazazi na mashemeji zangu kama wamemruhusu Dida kushiriki shindano hilo kama alivyoniambia, walidai aliwaambia kuwa mimi ndiye niliyemruhusu ndiyo maana nao hawakuwa na pingamizi.

“Baada ya kuwaelewesha waliniambia hawakupenda mambo hayo ya Big Brother kwa kuwa yana udhalilishaji ndani yake,” alisema Ezden.
Siku ya tukio, Ezden alisema alikuwa akioga bafuni na simu yake ilikuwa kitandani, ghafla Dida alimfuata na kumuuliza kwa nini aliweka password!

“Alipiga kelele mpaka majirani wakaanza kujaa nyumbani kisa ‘password’ niliyoiweka kwenye simu yangu. Nikamuuliza yeye si ndiye aliyesema kuwa kila mtu awe na simu yake! Akaanza kunipa maneno ya kejeli.
“Hapo nikaona heshima yangu inashuka. Kiukweli nilimpiga mpaka nikamuumiza. Baadaye akaondoka kwa hasira kumbe alikwenda kuwachukua ndugu zake.

“Walipokuja tukajitahidi kusuluhisha lakini kila nilipopewa nafasi ya kuzungumza, Dida aliniingilia. Kwa kuwa tulishawahi kukaa vikao vingi sana kabla lakini hakuna tulichoweza kusuluhisha, niliona hakuna  haja ya kuendelea naye,” alisema Ezden na kuongeza kuwa kikao hicho kiliisha kwa ahadi kwamba angetoa talaka kwa Dida ambaye naye alionekana kuikubali.

Ezden alisema, Juni 28, mwaka huu  alimpa Dida talaka tatu na kuongeza kuwa hategemei kurudiana naye wala kuoa hivi karibuni.Kwa upande wake, Dida alipopewa nafasi ya kuzungumza alisema: “Mimi sina la kusema na wala sitaki kulumbana na mtu.
GPL

Breaking News:Mchezaji Athmani Idd Chuji Amesajiliwa na Azam FC

$
0
0
Aliyekuwa kiungo wa Yanga SC, Athumani Iddi 'Chuji' akiwa mzoezini na klabu bingwa ya Tanzania Bara, Azam FC asubuhi ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Njama chafu za kuidhoofisha CHADEMA: ‘Tatizo ni Mbowe, Dk. Slaa’

$
0
0
ILI kudhibiti nguvu ya upinzani na kujihakikishia ushindi katika uchaguzi ujao, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeamua kuwekeza katika mikakati michafu dhidi ya viongozi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hasa Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa.

Wachambuzi kadhaa wa mwenendo wa siasa nchini wameliambia gazeti hili jana kwamba njia ya kuihakikishia CCM ushindi mwakani ni kuhakikisha Mbowe na Dk. Slaa hawawi sehemu ya uongozi wa chama hicho kikuu cha upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Kwa mujibu wa watoa habari wetu, ambao hawakupenda kutajwa gazetini, hata chokochoko za wanachama wasaliti na waliofukuzwa ambao bado wanaona fahari kujihusisha na kile wanachoita jitihada za “kusafisha CHADEMA”, ni sehemu ya mkakati mzito wa CCM kutumia watu wanaoonekana kuwa ndani au karibu ya chama hicho, ili kuonyesha umma kwamba kina migogoro.

“Imewachukua CCM muda mrefu kutambua uwezo wa Mbowe kuongoza na kupanga chama kimkakati. Kama wangejua zamani wangeshammaliza kabla hajaonyesha makali. Hata hivyo, bado wanasema wana muda, na wana vijana wanaoweza kuifanya kazi hii kwa malipo kidogo tu,” alijitapa mmoja wa wachambuzi hao, akidai anajua kwa karibu mipango ya baadhi ya vigogo wa CCM.
Alisema kwamba awali walijaribu kutumia mbinu zile zile walizotumia kuua au kudhoofisha vyama vya upinzani huko nyuma, hasa NCCR-Mageuzi, Chama cha Wananchi (CUF) na Tanzania Labour Party (TLP), lakini wamegundua kuwa haziwezi kufanya kazi kwa CHADEMA kwa sababu kina viongozi wasio wepesi.

Kwa mujibu wa mchambuzi huyo, CCM walitumia ruzuku na ushushushu kama silaha ya kuua vyama kwa kupandikiza migogoro. Mahali pengine walitumia pesa, na hisia za udini, ukabila na ukanda, lakini kwa CHADEMA wamegundua hoja hizo hazina mashiko kwani chama kimekuwa kinakua kila sehemu ya nchi.

“Kwa NCCR-Mageuzi ilikuwa rahisi kusema wanagombania ruzuku. Wakati huo ruzuku kwa vyama lilikuwa jambo jipya, na ni kauli ambayo iliaminika kirahisi. Hata pale walipoanza kushambuliana kwamba mashushushu wamevamia chama, ilikuwa rahisi kwa umma kuamini.
“Viongozi waligombanishwa bila kujua, chama kikameguka. Mwenyekiti akaondoka na pande lake, na katibu akabaki na lake. Kwa CHADEMA imeshindikana kuwatenga mwenyekiti na katibu mkuu, hivyo chama kimebaki kimoja.

Hata hawa walioondoka, wameondoka na makundi ya watu, lakini hayana nguvu ya kubomoa chama. Mbinu kuu iliyobaki sasa ni kuhakikisha Mbowe na Dk. Slaa wanaondoka kwenye uongozi. Hapo hutaona CHADEMA tena,” alidokeza.

Mchambuzi mwingine ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Mzumbe, alisema kinachowatisha CCM ni kwamba Mbowe na Dk. Slaa hawatingishiki kwa pesa wala kwa vitisho.
Alisema: “Hata hii mbinu ya kutumia akina Zitto imeshindwa kuleta matunda waliyotaka. Sasa hapa kuna mambo kadhaa ya kuchunguza. Tazama vijana waliokimbilia kwenye chama kipya kilichoanzishwa na kusajiliwa haraka haraka. Sikiliza lugha wanayotumia kujenga chama chao. Wanashambulia viongozi wa CHADEMA.

“Ukitazama juhudi kubwa za kujenga na kukuza CHADEMA katika kipindi cha uongozi wa Mbowe na Dk. Slaa, utaelewa kwanini CCM na baadhi ya wasiotakia mema CHADEMA, wanawashambulia viongozi hawa kwa kishindo.

“Kumbuka kauli na tambo za Wassira na Mwigulu kwamba CHADEMA itakufa. Wanajua kuwa CHADEMA chini ya Mbowe na Slaa haiwezi kufa. Kwa hiyo, ili ife inabidi wawili hawa waondoke, ishikiliwe na wengine ili CCM wabahatishe tena.
“Si kwamba chama hakina watu wengine wenye uwezo, lakini ukweli ni kwamba uongozi wa Mbowe na Slaa umeijenga CHADEMA ikawa tishio ambalo CCM wasingependa kuliona likisitawi hadi uchaguzi mkuu ujao.”

Kumbukumbu zinaonyesha kwamba wakati Mbowe anapewa dhamana ya kuongoza chama hiki mwaka 2004, CHADEMA ilikuwa na wabunge wanne tu wa kuchaguliwa na mmoja wa viti maalumu. Madiwani hawakuzidi 100.

Mwaka 2005 kilipata wabunge 11, na mwaka 2010 kilipata wabunge 49, na mamia ya madiwani. Kinaongoza mamia ya mitaa, vitongoji na vijiji. Kinazidi kuaminiwa na kupata maelfu ya wanachama. Hamasa na umaarufu wa CHADEMA vimeongezeka nchi nzima.
Wasomi na wafanyabiashara wamezidi kujiunga na CHADEMA, ujasiri wa wananchi umeongezeka, na chama tawala kimeyumba katika maeneo mengi.

Wafuatiliaji wa masuala ya kisiasa wanasema kwamba Mbowe na Slaa hawahongeki. Kwa hiyo, CCM imedhamiria kuwachonganisha na wanachama, na kuhakikisha wanaondolewa kwenye uongozi kwa mbinu zozote zile.

Mbinu ya sasa inayotumiwa ni kutumia makundi ya waasi ndani ya CHADEMA, na waliokwishapoteza uanachama kudai kwamba Mbowe hastahili kugombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Wiki hii baadhi ya vyombo vya habari vilimnukuu ofisa mwandamizi kutoka Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa akisema maneno hayo hayo, ingawa Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa CHADEMA, John Mnyika alitoa kauli haraka haraka kupinga kauli hiyo, akisema mtoa kauli amekurupuka, na hizo ni dalili za ofisi hiyo kutumika vibaya.

Wakati Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imesema uongozi wa CHADEMA uliondoa kipengele cha ukomo wa muda wa uongozi bila kufuata utaratibu wa kikatiba, gazeti hili limegundua jambo tofauti.
Mawasiliano ya kimaandishi kati ya Ofisi ya Msajili wa Vyama, Jaji Francis Mutungi na CHADEMA, yanaonyesha kuwa mambo yote yalifuata utaratibu.
Kwa mujibu wa barua ya Januari 15, 2014 (Kum.Na.DA.112/123/16A/19), Msajili alidai kuwa Ibara ya 6.3.2c ya Katiba ya CHADEMA ilichomekwa kinyemela bila kupitishwa na mkutano mkuu wa chama.

Lakini barua ya CHADEMA kwenda kwa makatibu wa wilaya na mikoa nchi nzima, Julai 13, 2006 (Kumb. C/HQ/ADM/CIR/15/139), inaeleza wazi maeneo yaliyokuwa kwenye mchakato wa kufanyiwa maboresho.

Aya ya mwisho inasomeka hivi: “Pia pendekezo la Ibara ya 6:3.2 (c) ya rasimu inasomeka: ‘Kiongozi aliyemaliza muda wake wa uongozi ana haki ya kugombea na kuchaguliwa tena, ilimradi awe ametimiza masharti ya kuchaguliwa kuwa kiongozi.’ Badala ya Ibara ya 6:3.2 (c) iliyokuwa inaweka kikomo cha muda wa awamu mbili kwa viongozi kuwa madarakani katika cheo kimoja kwa ngazi moja ambacho kimeondolewa.”
Barua hiyo ilisainiwa na Shaibu Akwilombe aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, ambaye sasa ni katibu wa CCMMkoa wa Mtwara.

Mwezi mmoja baadaye, Agosti 13, 2006, Mkutano Mkuu wa CHADEMA ulipitisha maboresho hayo na mengine yaliyokuwa yamependekezwa na kupitiwa na wajumbe.
Mkanganyiko Ofisi ya Msajili

Juzi CHADEMA ilisema Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ilikurupuka kutoa tamko kuhusu ukomo wa viongozi wao pasipo kuzingatia kwa ukamilifu maelezo na vielelezo vilivyopelekwa kwenye ofisi yake baada ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2006.
Tanzania Daima imeona barua nyingine, Kumb. DA/112/123/01/125, iliyosainiwa na Msajili Msaidizi Sisty Nyahoza. Inasema, “Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inatoa ufafanuzi kuwa vipindi vya uongozi katika vyama vya siasa huwekwa na katiba za chama husika.
“Msajili wa Vyama vya Siasa anaviasa vyama vya siasa kuzingatia katiba zao na si kumwomba msajili kusogeza mbele chaguzi zenu za ndani, kwani sheria haimpi msajili mamlaka hayo.

Kwa mujibu wa barua hiyo, msajili amesema kuwa anaelewa changamoto zinazovikabili vyama vya siasa.

chanzo: Tanzania daima

Enyi Wanaume Acheni Sifa Wafikisheni Wenzi Wenu Kwenye Kitanda

$
0
0
Ndugu zangu  katika hali ya mazoea ni nadra kusikia mwanaume akijisifia kuwa kamfikisha mwenzi wake bali wengi hujisifia wamefika kati ya mara 3 mpaka 5, wengine wanathubutu kusema wamefika mara8.

Niliwahi kusoma kitabu cha tendo la ndoa, tafiti za mtunzi wa kitabu kile zilionesha kuwa kati ya wanawake asilimia 100 ni 35 tu wanaofika kileleni na 75 hawafiki mpaka ukomo wa uhai wao. Hii inatokana na ukweli kwamba wanaume wengi hawajui jinsi ya kuwaandaa wenzi wao yaani kuanza na kumaliza, badala yake wanajijari wenyewe. Yaani mtu anakula hajui kama na mwenzake anahiji ashibe.

Je tunahitaji elimu juu ya jambo hili ili kutimiza wajibu wetu?

Cathy' Jamani Ustaa Kwenye Ndoa ndio Chanzo cha Kuvunjika kwa Ndoa Nyingi za Mastaa Hapa Mjini'

$
0
0
MSANII maarufu katika tasnia ya filamu Bongo, Sabrina Rupia ’Cathy’ amewataka wasanii wenzake kutofanya ustaa kwenye ndoa zao kwani ndiyo chanzo cha kuvunjika kwa ndoa nyingi.

Akipiga stori na paparazi wetu, Cathy alisema kabla ya kuolewa lazima uwe na utayari wa kuolewa na kujuana kwa undani zaidi na mwenzio kabla ya kufanya uamuzi pia usiweke neno kuachika katika ndoa kwa sababu tu unaweza kupata mwingine.

“Uvumilivu ndiyo nguzo muhimu katika ndoa, unapojifanya staa na kuishi maisha ya kistaa katika ndoa, mambo yanaharibika kabisa,” alisema Cathy huku akikataa kutoa mifano ya walioachika kwa kuendekeza ustaa katika ndoa akidai wanajijua.

Uhuni Unaofanywa na Adam Mchomvu, Fetty na B12 Hatutaweza Kuuvumilia

$
0
0
Kitendo walichokifanya vijana wa xxl jana ni muendelezo wa lile tukio lililotokea kipindi cha nyuma kidogo kusema kwamba "adamu mchomvu, fetty na b12 wamefukuzwa clouds fm" mnakumbuka?, huu ni moja ya uhuni unaofanywa na hawa vijana pamoja na menejiment yao.

Ujue kwa mwaka huu namba ya wasikilizaji wa XXL imepungua kwa kiasi kikubwa hivyo wanataka kuipandisha na kwaakili zao wanadhani hiyo njia itasaidia.

Vijana hawa waliamua kuigiza jana ili wazungumziwe kwenye mitandao ikiwa ni sambamba na kuandikwa kwenye magazeti, wanataka kujiongezea umaarufu kinguvu.

Last time walisambaza taarifa kuwa vijana hao wamefukuzwa, leo wanasema wamegombana. Kama hicho kitendo menejiment haija kipenda, kwanini wanaisambaza hiyo clip ya ugomvi wao maana ukiisikiliza ile clip ina quality ya ofisini kwao na si kwamba mtu amerekodi kwa simu.na kusambaza.

Acheni kutafuta Kicks Kinguvu....

EFM ndio Habari ya Uswahilini ....Hahah

Picha ya Kwanza Ikionyesha Jinsi Ofisi ilivyoharibika Baada ya Watangazaji wa Clouds Kupigana Ngumi

$
0
0
Picha ya Kwanza Ikionyesha Jinsi Ofisi ilivyoharibika Baada ya Watangazaji wa Clouds Kupigana Ngumi kwenye Kipindi cha XXL ......

Ni Ukweli Usio Pingika Kuwa Kwasasa Penye Davido Diamond Hakai

$
0
0
Dah kiukweli huyu DAVIDO (miaka21) anamtesa sana kaka yake Diamond Platinuma(miaka26)

1.Tuzo za MTV Africa Music Awards zilizofanyika KwaZulu-Natal Davido alifanikiwa kuchukua tuzo mbili ikiwemo ya mwimbaji bora wa kiume na pia akachukua tuzo ya mwanamuziki bora wa mwaka kwa ila upande wa Diamond platnumz kwa bahat mbaya diamond alishindwa kupata hata tuzo moja

2.Tuzo za B.E.T zilizofanyika majuzi Davido alidhihirisha unyama wake tena baada ya kuchukua tuzo kubwa zabet kipengele cha best international act ila cha kusikitisha Kwenye hizo hizo tuzo za B.E.T. Davido aliwaita Nominees wote wa Africa waende stage wajumuike naye ila kaka yake alikataa kabisa kwenda nahisi diamond alikuwa na hasira sana za kushindwa na dogo Davido

3.DAVIDO huyu dogo ni mjanja sana kwenye kutafta pesa na umaarufu alivyoona tu diamond anashine sana kwenye my number one alimtumia diamond ili nae afahamike east africa na apate shows huku bongo, DAVIDO akaitwa kufanya remixkwenye remix ya namber one na kaka yake remix ilivotoka nyota ya davido ilingaa maana hata huku tz aliitwa kufanya show na clouds na alipewa pesa nyingi sana kuna mstari aliimba "from Dar 2 Lagos i gona make u famous" kuweka wazi yeye ndio Top

Video ya Shetta 'Kerewa' Yaanza Kuoneshwa MTV Base

$
0
0
Bajeti kubwa aliyokuwa anaitaja Shetta katika video ya wimbo wake wa ‘Kerewa’ imeanza kuzaa matunda baada ya video hiyo kuanza kuoeneshwa na kituo cha MTV Base.

Shetta haujutii ushauri aliopewa na Diamond kutumia kiasi cha Milioni takriba 30 za kitanzania kuhakikisha mzigo unatoka vizuri na kwa kiwangu cha juu.


Hii ni hatua kubwa kwa msanii huyo kwa kuwa inakuwa video yake ya kwanza kuanza kuonekana katika channel hiyo ya kimataifa na bila shaka matunda zaidi yanakuja.

Hatimaye Gwajima Naye Afunguka Sakata la Mbasha Baada ya Mengi Kusemwa Mitandaoni

$
0
0
MCHUNGAJI Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la jijini Dar es Salaam, Josephat Gwajima, amefunguka na kuuweka hadharani uhusiano wake na familia ya waimbaji wa nyimbo za Injili nchini, Flora Mbasha na mume wake, Emmanuel Mbasha.

Gwajima amekuwa akitajwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Flora na kwamba hatua hiyo inadaiwa kuchangia mvurugano kwenye ndoa ya wanamuziki hao.

Mbali ya kutajwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Flora, pia anatajwa kuwa nyuma ya kesi ya ubakaji inayomkabili Mbasha ambapo kumekuwa na taarifa mbalimbali


zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikimuhusisha mchungaji huyo na kesi hiyo iliyoanza kutajwa Juni 17 mwaka huu.

Akizungumza kwa mara ya kwanza kuhusu sakata hilo kwenye mahojiano maalumu na gazeti hili, Gwajima akiwa katikati ya madhabahu ya kanisa lake lililopo Kawe jijini Dar es Salaam huku akiwa na wasaidizi wake pamoja na watoto wake wawili, alisema taarifa zinazoenezwa ni za kijinga na hazina ukweli wowote.

Alisema mgogoro wa Mbasha na Flora unaonekana kuwa ni wa muda mrefu na kwamba umekuja kujitokeza kanisani kwake baada ya kuanza kufanya nao kazi ya kutoa huduma ambapo wawili hao walikuwa waburudishaji kwenye mikutano yake.

“Nilimfahamu Flora na Mbasha mwezi wa tisa mwaka jana… kipindi hicho nilikuwa na mkutano Arusha. Wote wawili niliwaalika tukaenda nao kwenye mkutano na pindi mkutano ulipomalizika walirudi nyumbani tukaenda tena katika mikoa mingine ya Moshi, Tanga, Morogoro na Kilombero wote wawili walikuja kushiriki mikutano hii kama waimbaji na wote walirudi nyumbani kwao.

“Nimekuwa nikiona kwenye mitandao wakisema kuwa nilikwenda na Flora peke yake katika baadhi ya maeneo kama Morogoro… si kweli, muda wote walikwenda wote wawili na walirudi wote wawili, pia sina uhusiano wa kimapenzi na Flora kama inavyodaiwa.

“Kwanza watu wote waliokwenda kwenye mkutano walikuwa 300, kila mkoa walikuwa watu 300. Naamini kuna mtu ana hoja zake binafsi anataka kuudanganya umma kwamba Gwajima ana uhusiano na Flora.

“Nataka niwakumbushe Watanzania kuwa baada ya kumaliza hii mikutano hawakuwa washirika wetu kanisani, kwa maana kuwa hawakuwa wakisali kanisani kwangu kwa sababu tuliwaalika kuja kuimba na walikuwa wanalipwa kwa sababu ya kuimba pekee,” alisema.

Aidha alisema baada ya kumaliza mikutano hiyo na kukaa kwa muda, Flora aliamua kwa mapenzi yake kwenda kusali kanisani kwake na baadaye mumewe naye akajiunga na mke wake kushiriki ibada kwenye kanisa lake.

Akizungumzia suala la kuwa nyuma ya kesi inayomkabili Mbasha na kuwa amekuwa akimpatia fedha Flora ili kufanikisha dhamira ovu dhidi ya mumewe, Gwajima alisema si la kweli.

“Hili suala la kumpatia fedha Flora ili amuangamize mume wake halina ukweli, ukweli ni kwamba baada ya Mbasha kutuhumiwa kubaka alitoweka nyumbani, mke wake hakuwa na sehemu ya kupata msaada, kutokana na hali hiyo ndipo Flora alikuja kanisani kwetu kuomba msaada wa fedha na kwa vile ni mshirika wetu tulimsaidia.

“Nilizungumza na wachungaji wenzangu tukaona ni vyema tuitishe harambee ili waumini wamchangie kama wanavyochangia watu wengine wenye matatizo mbalimbali kwa sababu Flora alisema jamani hana fedha na mume wake amemkimbia na hana chochote, watu wakamchangai!

“Sasa nadhani zipo fikra kwamba, Gwajima anachangisha fedha za Flora ili apate fedha za kuendelea kumshtaki mumewe, pia zipo fikra kwamba kanisa langu ndilo limemzuia Flora kurudi kwake.

“Zikianza kusambazwa picha mbaya za Gwajima kwenye mitandao ya kijamii ili nichukue uamuzi wa kumfukuza Flora kanisani kwangu ili akapate matatizo, siwezi kumfukuza Flora kanisani kwangu wala hilo halitatokea… nimechukua hatua mbalimbali ikiwamo kumshauri Flora arudi kwa mume wake lakini alikataa mwenyewe,” alisema.

Aidha, Mchungaji huyo pamoja na kukanusha kuwa yeye sio chanzo cha mgogoro huo pia alisema hajamsomesha wala hakuwahi kutoa fedha za kufadhili masomo ya Flora nchini Uingereza.

“Unaweza kumpeleka ng’ombe kisimani lakini jukumu la kunywa maji ni lake, akikataa ni mwenyewe, akinywa ni mwenyewe, mimi siku zote nawashauri Flora na Mbasha wawe na uhusiano mzuri, warudishe uhusiano wapatane, hata kesho (leo) nitampigia simu baba yake mzazi Mbasha na wadogo zake ili nijaribu kuwaita tena kujaribu kuona kama tunaweza kuwasaida kuwarejesha kwenye ndoa yao.

“Hata hivyo uamuzi wa kurudiana bado utakuwa ni wa kwao wao mimi siwezi kuwalazimisha,” alisema.

Mbasha (32) alipandishwa kizimbani Juni 17 mwaka huu katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala akikabiliwa na mashtaka mawili ya ubakaji na kusomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Wilberforce Luago.

Akisoma mashtaka Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga, alidai mshtakiwa ambaye pia ni mfanyabiashara alitenda makosa hayo mawili maeneo ya Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam.

Kesi ya Mbasha inatarajia kusomwa tena Juni 17, mwaka huu kwenye Mahakama hiyo ambapo mshtakiwa huyo yuko nje kwa dhamana.

Kagame Ajirudi Na Kusema Rwanda na Tanzania ni Ndugu Hatupaswi Kugombana

$
0
0
BAADA ya mgogoro wa muda mrefu wa diplomasia kati ya Tanzania na Rwanda, Rais Paul Kagame, amesema nchi hizo mbili ni ndugu na yanayotokea yasingepaswa kutokea.

Kagame aliyasema hayo alipozungumza na waandishi wa habari, akifafanua kuwa mataifa hayo yataendelea kuwa ndugu.

Akijibu swali la mwandishi mmoja kuhusu uhusiano wa nchi yake na Tanzania kwa sasa, Rais Kagame alisema hakuna sababu yoyote inayoweza kufuta au kuharibu uhusiano wa wananchi wa nchi hizo mbili jirani.

Kagame alisema matatizo yanayowakabili wananchi wa Rwanda yanafanana na yanayowakabili Watanzania kwa sababu wote ni Waafrika wenye changamoto sawa za maisha.

“Matatizo yanayowakabili Watanzania ni sawa na yale yanayowakabili Wanyarwanda… hawa ni ndugu zetu ni kaka zetu ni dada zetu, Waafrika wenzetu ambao tunachangia mengi,” alisema.

Alipoulizwa kama angezuru Tanzania kutokana na kuwapo msuguano wa diplomaisia baina ya nchi mbili hizo, Rais Kagame alisisitiza yote yanayotokea sasa yasingepaswa kutokea.

“Hii haipaswi kusubiri nifanye ziara au nisifanye ziara hiyo, ukweli unabaki palepale… sisi ni ndugu na ujumbe wangu ungekuwa hakupaswi kuwapo au kusingepaswa kutokea matatizo yoyote kati ya Rwanda na Tanzania,” alisema.

Rwanda na Tanzania zilikabiliwa na wakati mgumu kuanzia mwaka jana kutokana na kutofautiana mtazamo kuhusu jinsi ya kukabiliana na kundi la waasi wa Kihutu la FDLR linaloendesha mapambano dhidi ya Rwanda kutokea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Baadhi ya mitandao ya nchi hiyo imemnukuu Rais Kagame akisema kuwa ni vema masilahi ya mataifa hayo pamoja na Afrika yakaangaliwa zaidi kuliko kutazama watu wenye muono wa karibu ambao lengo lao ni kusababisha matatizo.

Akizungumzia FDLR alisema baadhi ya watu wameamua kulifanya kuwa ni tatizo kubwa lakini ni kati ya vitu rahisi.

Tanzania na Rwanda ziliingia katika mgogoro wa diplomasia hadi kufikia hatua ya kutunishiana misuli baada ya Rais Jakaya Kikwete kuzishauri Rwanda na Uganda kuzungumza na waasi wa nchi zao waliopo DRC.

Ushauri huo ulipingwa vikali na Rwanda ikidai kwamba Rais Kikwete aliingilia mambo ya ndani ya nchi hiyo kwa kushauri wawe na mazungumzo na watu wanaoua raia wa nchi hiyo.

Katika mazungumzo yake hayo na waandishi wa habari juzi, Kagame, aliviomba vyombo vya habari, wanasiasa na mitandao ya jamii kusaidia kuziba ufa wa uhusiano uliobomolewa.

Naye Rais Kikwete alipolihutubia taifa mwisho wa Juni mwaka jana alisema mgogoro baina ya Tanzania na Rwanda ulikuwa umemalizika rasmi.

Alisema hatua hiyo ilitokana na mazunguzo kati yake na Kagame yaliyofanyika Uganda.

Ingawa hakusema mgogoro huo ulimalizika vipi, Rais Kikwete alisema hatua ya mazungumzo baina yake na Kagame ndiyo chanzo cha mafanikio hayo yote.

Wakati hali ikionekana kutulia, Mei mwaka huu, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema uhusino wa Tanzania na Rwanda haukuwa mzuri.

Pamoja na mambo mengine, alisema lilikuwapo suala la watu kupenyeza maneno kati ya pande hizo mbili na kusababisha ziangaliane kwa jicho la shaka hasa kila mmoja anapomuana mwenzake akizungumza na adui yake.

Alisema pia kuwa waasi wa kundi la M23 walioondolewa DRC ni raia Rwanda.

Hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania kusema hadharani kuwa inao uhakika waasi hao ni raia wa Rwanda.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizopeleka majeshi DRC ambayo kwa kushirikiana na yale ya Umoja wa Mataifa yaliwaondoa waasi hao DRC.

Al Shabaab Yamuua Mbunge na Mlinzi Wake Nchini Somalia

$
0
0
WANAMGAMBO wa Al Shabaab wamedai kuwa wamemuua kwa kumfyatulia risasi mbunge maarufu mjini Mogadishu. Taarifa zinasema, Ahmed Mohamud Hayd (Mb) aliuawa baada ya kutoka hotelini ambapo katika tukio hilo, mlinzi wake pia aliuawa huku Katibu wa Bunge akibaki amejeruhiwa.

Kundi la Al-Shabaab, ambalo lina uhusiano na lile la al-Qaeda, limeapa kuendelea na mashambulizi zaidi katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani. Wanamgambo hao walipoteza ngome yao mjini Mogadishu na kuchukuliwa na Vikosi vya Umoja wa Afrika mwaka 2011, lakini wameendelea na mashambulizi ya mabomu na mauaji mjini humo.

Msemaji wa kundi hilo, Abdulaziz Abu Musab alisema kuwa kundi lake limemuua kama ilivyopangwa na kuwa wataendelea kuwafuatilia wabunge wengine ikiwa hawataachana na Bunge nchini humo. Al-Shabaab imekua ikipigania kuunda taifa la kiislamu nchini Somalia.

Kumbe Mwigulu Akiweka Siasa Pembeni ni Mwelewa na Mjuzi wa Mambo

$
0
0
Kwa muda mrefu nilikuwa nikimuona Mwigulu bungeni na michango yake, nilikuwa nimeshamuweka kwenye kundi la watu wazandiki, wafitini, wahafidhina, mchochezi na vitu vingine kama hivyo. Leo nimemsikia kupitia Clouds Fm nimependa ufafanuzi wake kuhusu kukopa na kulipa deni la taifa. Ingawa hii haina maana kwamba hizi tabia zimeisha lakini amenifanya niamini kabisa kwamba kumbe siasa inatakiwa uvae joho jingine kuifanya...Kwa Waliopata Nafasi ya Kumsikiliza Leo  Clouds FM Najua Mtakuwa Mmeliona Hilo Kaongea Vizuri Sana Tofauti na Anavyoropokaga Akiwa Jukwaani ama Bungeni.

Utabiri wa Kifo Chake Aunty Ezekiel Amwaga Machozi

$
0
0
SIKU chache baada ya Nabii wa Huduma ya Ufufuo, Buza jijini Dar, Yaspi Paul Bendera kutabiri kuwa vifo vya mastaa vitaendelea, staa wa sinema Bongo, Aunt Ezekiel amemwaga machozi baada ya kuhusishwa kuwa yeye ndiye anayefuata kufa.

Kupitia gazeti la Ijumaa, Juni 13, mwaka huu, Nabii Bendera alisema ameoneshwa kwamba wasanii 20 wangekufa hivyo kama wanataka kujinusuru, wafike kanisani kwake na kupakwa mafuta.
Wakati gazeti hilo lilipoingia mtaani, ukurasa wa mbele uliambatanisha picha mbalimbali za baadhi ya wasanii waliofariki pamoja na wengine ambao wapo hai akiwemo Aunt Ezekiel (pichani) ndipo utata ulipoanzia.

Chanzo kilicho karibu na staa huyo, kilipenyeza habari kuwa, ndugu zake walimpigia simu Aunt ambapo walionesha kuwa na hofu ya kifo ambayo ilimfanya mwigizaji huyo naye aangue kilio mara kwa mara.
“Ndugu zake walilia sana kwani baada ya kuona picha ya Aunt katika gazeti, waliamini maneno ya nabii huyo kwa kujua pengine anayefuata kufa kati ya hao kumi ni ndugu yao.

“Aunt alilia sana siku hiyo na Wema (Sepetu) ndiye alisimama kumsihi asiendelee lakini kama haitoshi, bado amekuwa akiteseka mara kwa mara kila anapokumbuka tu, anakosa amani na kujikuta analia,” kilisema chanzo.

Hata hivyo, chanzo kimeeleza kuwa baada nguvu kubwa kutoka kwa marafiki wa karibu wa Aunt akiwemo Wema wamekuwa wakimsihi amuombe Mungu kwani si kwamba picha yake kutumika gazetini ndiyo atakufa wala maneno ya nabii huyo si sababu ya kuamini kwamba kweli vifo hivyo vitatokea.

“Wamemtaka amuombe Mungu na kutosikiliza maneno ya watu maana kuna watu ambao wamekuwa wakishadadia ishu hiyo katika mitandao na kumfanya Aunt aingiwe na hofu ya kifo, kidogo ameanza kuwaelewa,” kilisema chanzo.

Baada ya kupata habari hizo, gazeti hili lilimtafuta Aunt, alipopatikana aliweka wazi kuwa suala hilo limemkosesha amani sana pamoja na ndugu zake.

“Walijua ndiyo nakufa, na mimi pia niliposikia harakaharaka niliamini nimetajwa mimi hususan waliponiambia picha yangu imetumika gazetini, nililia sana siku hiyo na siku zilizofuata pia watu walizidi kuniliza mitandaoni, mwisho wa siku nimemwomba Mungu anisimamie, atakaponichukua ni kwa mapenzi yake kama maandiko yanavyosema,” alisema Aunt.

Kwenye utabiri huo, nabii huyo alinukuliwa kuwa ndani ya mwezi Juni, idadi ya wasanii 20 wangefariki lakini hadi sasa hakuna kifo chochote kilichotokea hali ambayo inawafanya baadhi ya watu kuamini kwamba masuala ya kifo ni Mungu pekee anayejua nani atakufa lini.

Umewahi Kufanya Mapenzi kwa Bahati Mbaya Bila Kutegemea?

$
0
0
Nimewahi kupata experience ya matukio mawili ambayo yalinipa maana halisi ya "UNEXPECTED SEX" .
Tukio la kwanza lilitokea mwaka 2009 ambapo nilipanda basi nikielekea Tabora kwenda kumuona ndugu yangu wilayani Uyui lakn ndani ya gari nilikutana n mdada ambaye she was 25 by then na baada ya stori mbili tatu tukafahamiana na tuliposhuka stend nikamwambia mi nitalala hapa town then asubuhi niende wilayani nikaamua kumjaribu kwa kumuomba tulale wote she didn't mind it at all.
Kilichofuata ilikua ni shoo ya kufa mtu ambayo I never had it before na ilipofika asubuhi tukaagana na hatukuwahi kuwasiliana tena till now.
Tukio la pili limetokea last year kipindi cha mwezi wa february;Shemeji yangu mmoja alikuja kuleta mzigo wa kaka yangu sasa cha ajabu alipoingia ndani mvua ikaanza kunyesha kwa nguvu mpaka nikaamua kufunga milango.
Baada ya hapo nikakaa na shemeji na baada ya stori mbili tatu nikaona ananiambia "shem cku hizi unaonekana mrefu",nilipomuuliza kwanini akaniambia naona kama unanizidi vile,ndipo tulipoaamua kupima kwa kusimama huku yeye akiwa mbele yangu na niliposhika her WAIST nikaona anavuta mikano basi ikabidi nimpe mamboz na mvua ilipoisha akaondoka and we never did it again coz it was a good sex to a wrong person. 


Sasa wanajamvi naomba kupata experiences zenu katika hili.
Nani amewahi kufanya mapenzi kwa bahati mbaya???? And how did it happen??????
Na kuna ukweli wowote kwamba UNEXPECTED SEX NI TAMU ZAIDI KULIKO ILE INAYOKUA PLANNED?

January Makamba Atangaza Nia ya Kugombea Uraisi 2015 Licha ya Kuonywa Kuto Fanya Hivyo

$
0
0
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ametangaza nia yake ya kuwania urais akisema huu ni wakati wa kupisha fikra mpya kuongoza dola, licha ya chama hicho kuzuia kutangaza nia na kupiga kampeni kabla ya muda.

Makamba, mmoja wa makada wa CCM walioonywa na chama hicho baada ya kutuhumiwa kuanza kampeni mapema, alijipigia debe kuwa iwapo atapitishwa na chama hicho, ataelekeza nguvu kwenye vipaumbele vyake vinne ambavyo ni ajira, huduma za jamii, uchumi imara na utawala bora.

Mbunge huyo wa Bumbuli alisema hayo akiwa Uingereza anakohudhuria mkutano wa sekta ya mawasiliano baada ya kuhojiwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza na baadaye kufafanua nia hiyo katika mahojiano na Mwananchi jana.

Kafulila "I’m Ready to Go to jail. I’m Not Afraid of Telling the Truth, Kikwete to Intervene in IPTL Sale Saga..

$
0
0
Kigoma South MP David Kafulila yesterday appealed to President Jakaya Kikwete to intervene in the controversy surrounding the payment of Sh201 billion to Pan African Power Solutions Ltd (PAP).

The NCCR-Mageuzi lawmaker said the scandal could damage Mr Kikwete’s legacy if he did not take it seriously.

“Honourable Kikwete is now heading towards the end of his two terms.  I’m appealing to him to take this matter seriously otherwise it will  tarnish his leadership’s image,” he said.

Mr Kafulila, who has been vocal both inside and outside Parliament over the sale of Independent Power Tanzania Limited (IPTL) and subsequent payment of tens of billions of shillings from an escrow account under the custodian of the Bank of Tanzania, vowed that he would not be silenced.

“I’m ready to go to jail. I’m not afraid of telling the truth just because some people are threatening to eliminate me,” he said.

Mr Kafulila spoke a few days after exchanging harsh words with Attorney General Fredrick Werema in Parliament, where  Mr Werema branded the MP a “monkey”.  Mr Kafulila responded by calling the AG a “thief”.

NCCR-Mageuzi Secretary-General Mosena Nyambabe said yesterday that the party supported Mr Kafulila’s crusade against grand corruption.

“He is playing his role as an MP and the party fully supports him,” he said.

Mr Nyambabe urged other lawmakers from the opposition to support Mr Kafulila.

He said security agencies should not take threats against Mr Kafulila lightly, and called on the government to guarantee his safety.

The official said  it should not be lost on Tanzanians that there were people who had been brutally attacked after daring to question the underhand dealings of powerful individuals.

He accused Mr Werema, Energy and Minerals minister Sospeter Muhongo and Permanent Secretary Eliakim Maswi of misleading Parliament and the public on the escrow account.
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live




Latest Images