Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Mahakama Yasogeza Mbele Hukumu Bob Chacha Wangwe Hadi Novemba 15

$
0
0
Mahakama Yasogeza Mbele Hukumu Bob Chacha Wangwe Hadi Novemba 15
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesogeza mbele hukumu ya kesi ya kutoa taarifa ya uongo kupitia mtandao wa Facebook, inayomkabili Bob Chacha Wangwe, November 8,2017.

Bob ambaye ni Mwanaharakati ni mtoto wa marehemu Chacha Wangwe, aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime, mkoani Mara na Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara.

Hukumu hiyo ilitarajiwa kusomwa leo na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo amesema ameshamaliza kuiandaa hukumu hiyo lakini anaona ni vyema akaisoma tarehe ijayo.

“Hukumu nimeshamaliza kuiandaa kila kitu, hivyo nitaisoma November 15,2017,”.

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi 6, upande wa utetezi ukiwa na shahidi mmoja ambaye ni mshtakiwa mwenyewe.

Awali katika ushahidi wake, Bob amedai kuwa yeye hakuandika maneno ya upotoshaji wala hajawahi kufanya hivyo.

“Mimi nilitoa maoni yangu kuhusu uchaguzi wa Zanzibar na kasoro zake za kidemokrasia kama Watanzania wengine na waangalizi wa uchaguzi huo walivyofanya,”.

Katika kesi hiyo namba 167, Chacha Wange anatuhumiwa kwa kosa la kuchapisha taarifa za kupotosha katika ukurasa wake wa mtandao wa Facebook.


Kauli ya Rais Yaleta Gumzo Bungeni, Waziri Ajibu Kauli Hiyo

$
0
0
Kauli ya Rais Yaleta Gumzo Bungeni, Waziri Ajibu Kauli Hiyo
Naibu waziri wa Mungano na Mazingira Kangi Lugola, amewataka wananchi kutoitafriri vibaya kauli ya Rais kuhusu kufanya shughuli za kilimo kwenye vyanzo vya maji, na kusema kwamba hakuna sheria inayoruhusu watu kufanya shughuli za kilimo.

Waziri Lugola ameyasema hayo leo alipokuwa akijibu swali Bungeni kuhusu kauli hiyo ya Rais ambayo imeonekana kuruhusu watu kufanya uharibifu kwenye vyanzo vya maji na mazingira, na kusema kwamba 
“Niwahakikishie kauli ya Rais isije ikapotoshwa wananchi wakaenda kuvamia maeneo ya mito na kuanza kulima, na kauli aliyoitoa Mheshimiwa Rais, Watanzania waelewe vyanzo vya maji ndio uhai wetu, hakuna anayeruhusiwa kwenda kwenye chanzo cha maji, kwa hiyo hamruhusiwi .", Amesema Kangi Lugola
Naibu Waziri Kangi Lugola ameendelea kwa kusema kwamba yeyote atakayevunja sheria na kuingia kwenye vyanzo vya maji atachukuliwa hatua, lakini pia ifahamike kwamba Rais ana mamlaka ya kuruhusu watu kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria ya mita 60. 

"Yeyote atakayevunja sheria hatasalimika, sheria niliyoisema ya 2004 Rais anaweza akatoa Kibali, Waziri anaweza akatoa kibali kwenye maeneo ya mita 60 kutokana na changamoto aliyoiona, kwa hiyo Rais hajavunja sheria, na ninyi mtakapowachochea wananchi kuvunja sheria, sheria za Rais Magufuli mtapambana nazo", amesema Kangi Lugola.
Hapo Jana Rais Magufuli alipokuwa kwenye ziara yake mkoani Kagera, ameitaka serikali kuwaacha vijana wanaofanya shughuli za kilimo kando ya mto wa maji kwani wanajiiingizia kipato.

Majaliwa Awapiga Stop Mawazili Utoaji wa Matamko

$
0
0
Majaliwa Awaonya Mawazili Utoaji wa Matamko
Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa amewataka Mawaziri kuacha kutoa matamko yasiyotekelezeka ili kuepusha mkanganyiko serikalini.

Waziri ametoa tamko hilo jana jioni kwenye kikao cha baraza la mawaziri kilichofanyika Dodoma, ambapo amewaasa mawaziri kujidhirisha na bajeti pamoja na sera za serikali kabla ya kutoa tamko ili kuepusha athari zinazoweza kujitokeza endapo tamko halitatekelezeka.
Mbali na hilo waziri mkuu amewataka viongozi hao wafanye kazi kwa kuzingatia maadili ya uongozi ili kuithibitishia jamii kuwa Rais Dkt. John Magufuli aliwateua kutokana na uadilifu na uwezo wao kiutendaji.

“Tunao wajibu mkubwa kuhakikisha kwamba kila mmoja wetu anafanya kazi kwa nguvu na bidii ili kutimiza matarajio ya Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli na wananchi wote kwa ujumla,” amesema waziri mkuu.
Aidha waziri mkuu amewataka mawaziri wafanye ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo inayohusu sekta zao kwa kuwa wao ni wasimamizi wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali.

Bahati ya Kuolewa Ninayo Ila kwa Sasa Bado Nakula Ujana- Ericah

$
0
0
Bahati ya Kuolewa Ninayo Ila kwa Sasa Bado Nakula Ujana- Ericah
MUUZA nyago kwenye video za wasanii mbalimbali Bongo, Ericah amesema hataki kuolewa kwa sasa, kwa sababu muda wake wa kufanya hivyo haujafika kwani hajamaliza starehe za ujana.

Akipiga stori na Risasi Vibes, Ericah alisema zaidi ya wanaume watatu walishamtolea barua ili wamuoe lakini aliwatolea nje sababu bado anataka aendelee kufaidi ujana wake, kwa kuamini ndoa itambana maisha yake ya kula bata, kwani atakuwa chini ya maamuzi ya mtu mwingine.
 
“Namshukuru Mungu bahati ya kuolewa ninayo, lakini kichwani mwangu siwazi hilo hata kidogo maana kila kwa wakati, naona muda wangu bado, siwezi nikajifosi kufanya kitu ambacho nafsi yangu haijaridhia, nikaenda kumpasua kichwa atakayenioa,” alisema

Serikali Yaiomba Mahakama Kumuongezea Kifungo Oscar Pistorius

$
0
0
Serikali Yaiomba Mahakama Kumuongezea Kifungo Oscar Pistorius
Serikali ya Afrika Kusini imeiomba Mahakama ya juu nchini humo kumwongezea kifungo mwanaridha mlemavu, Oscar Pistorius ‘Blade Runner’ aliyekutwa na hatia ya kumuua mpenzi wake, Reeva Steenkamp, Februari 2013.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Pretoria, Thokozile Masipa, alimhukumu Pistorius kifungo cha miaka sita baada ya kumtia hatiani kwa mauaji ya bila kukusudia, uamuzi ambao  haujawaridhisha watu

Hivi karibuni, serikali hiyo kupitia Wakili, Andrea Johnson, ilirejea mahakamani na kuomba uamuzi wa Jaji Masipa ubatilishwe na mwanaridha huyo aliyejipatia umaarufu kwa kushiriki mbio akitumia miguu ya bandia kwa kuwa ni mlemavu, aongezewa muda zaidi wa kukaa jela.

“Jaji aliyeisikiliza kesi alikosa kabisa kuweka wazi sababu za kutotoa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka 15 (Kwa mujibu wa sheria za Afrika Kusini) alipomhukumu Oscar Pistorious kwa mauaji ya Reeva Steenkamp,” wakili huyo aliiambia mahakama hiyo ambayo bado inaisikiliza rufaa hiyo.

Steve Nyerere Amekata Mzizi wa Fitina na Kusema “Hatuwezi Kuacha urafiki na Wema"

$
0
0
Steve Nyerere Amekata Mzizi wa Fitina na Kusema “Hatuwezi Kuacha urafiki na Wema"
Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza nchini lakini pia ni msanii wa Filamu, Steven Nyerere amekata mzizi wa fitin ana kudai kuwa hana tatizo lolote na malkia wa filamu Bongo Wema Sepetu.

Kauli ya Steve imekuja baada ya kuzagaa habari kuwa waili hao kwa sasa hawana mawasiliano mazuri.

“Hatuwezi kuacha urafiki na Wema coz Wema ni dada, ni mtu ambaye tume hangaika naye kuhakikisha kwamba tumafika hapa tulipo na mimi nataka kusema Wema ni mzalendo wa taifa la Tanzania labda tu tumegewajika katika vyama,” amesema Steve katika mahojiano aliofanya na Bongo5.

Akaongeza “Nachotaka kusema kuwa Wema atakuwa Wema na Stev ataendelea kuwa Steve kwa sababu wote ni binadamu hujui kesho nani atakuzika. Sasa ni dada na tuna wasiliana na bado tunaendelea kupendana kaka dada na kaka.”

Nape Aibua Hoja ya Kufungia Magazeti Bungeni Akosoa Utaratibu Unaotumika

$
0
0
Nape Aibua Hoja Bungeni ya Kufungia Magazeti Akosea Utaratibu wa Kufungia
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amekosoa utaratibu wa kufungia magazeti, akihoji kuadhibiwa chombo kizima badala ya mwandishi aliyeandika.

Nape ambaye aliwahi kuwa waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amehoji ni kwanini daktari anapompasua mgonjwa mguu badala ya kichwa haifungiwi hospitali nzima.

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu nyumbani kwake Kisasa mjini hapa juzi, Nape alisema lengo la sheria mpya ya huduma za vyombo vya habari ya 2016 si kufungia magazeti.

Septemba 29, Serikali ilisitisha uchapishaji na usambazaji wa gazeti la Raia Mwema kwa siku 90 ikisema taarifa yake moja ilijaa nukuu za kutunga zikimsingizia Rais John Magufuli.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyopingwa na baadhi ya wanazuoni na wanahabari, mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) ambaye ni msemaji mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi alisema agizo hilo linahusu pia toleo la mtandaoni.

Dk Abbasi alisema adhabu hiyo inatokana na toleo namba 529 la Septemba 27 hadi Oktoba 3 lililochapisha habari ya uchambuzi yenye kichwa cha habari “Urais utamshinda John Magufuli”.

Kwa mujibu wa Dk Abbasi, habari hiyo ilisheheni nukuu za uongo, kutungwa na zenye nia mbaya.

Oktoba 24, Serikali ililifunga kwa siku 90 gazeti lingine la Tanzania Daima kwa madai ya kuendelea kuandika habari za uongo na za upotoshaji kinyume cha sheria hiyo.

Katika taarifa yake, Dk Abbasi alisema gazeti hilo katika toleo namba 4706 la Oktoba 22, liliandika habari iliyobeba kichwa cha habari “Asilimia 67 ya Watanzania wanatumia ARVs”.

Taarifa ya Serikali ya kulifungia gazeti hilo iliorodhesha habari nyingine nne ilizosema zilikuwa na makosa na akisema Serikali imejitahidi kuwakumbusha wahusika kuzingatia maadili bila mafanikio.

Alichosema Nape

Nape aliyetimiza umri wa miaka 40 jana, alisema bado anaamini sheria ya huduma za vyombo vya habari aliyoipigania hadi ikatungwa ni bora zaidi.

Alisema sheria hiyo hailengi kufungia magazeti, bali kushughulika na mwanataaluma anayefanya makosa kama zilivyo taaluma nyingine za mawakili, madaktari, wakandarasi na wahasibu.

“Changamoto kubwa iliyopo na ambayo naamini Serikali inaifanyia kazi ni kutoanzishwa kwa zile taasisi za kusimamia vyombo vya habari. Zisipoanzishwa hizi misuguano itaendelea,” alisema Nape.

“Nimekuwa nikiwasikiliza wanahabari, nimekuwa nikisikiliza Serikali mgongano unaotokea na kelele zinazotokea za kufungia magazeti, kutishiana ni kwa sababu hizi taasisi hazijaanzishwa.” Nape alisema sheria imeeleza lianzishwe Baraza Huru la Vyombo vya Habari na limewekewa kazi zake. “Usipokuwa nalo wakati shughuli za habari zinaendelea, nani atashughulikia? Migogoro itabaki. Tumesema iwepo bodi ya Ithibati, isipokuwepo nani anashughulikia?” Alihoji Nape.

Waziri huyo wa zamani alisema sheria hiyo iliyopitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais Magufuli ililenga kusaidia kuondoa majukumu makubwa kwenye Serikali kusimamia habari.

“Wabaki (Serikali) na mambo machache ambayo yanalinda nchi yetu. Ndiyo maana kwenye ile sheria yamebaki makosa mawili peke yake ambayo Serikali inatakiwa iingilie,” alisema.

Nape alisema, “Ni public safety (usalama) na uchochezi ambayo ni lazima uyathibitishe pia na tukaweka mle kipengele kwamba mkibishana lazima muende mahakamani. Sheria ililenga kuifanya iwe taaluma.”

Katika kipindi chake cha uwaziri, Nape aliyafungia magazeti ya Mawio na Mseto na redio mbili. Alisema alifanya hivyo kwa kutumia sheria ya zamani na ndio iliyokuwapo.

Aliongeza kuwa ifike mahala sheria itekelezwe kwa kuwa kanuni zipo na taasisi zilizotajwa kwenye sheria zianzishwe. “Zile taasisi zitatuondolea mgogoro kwa sababu Baraza Huru la Habari wanahabari wataitana wenyewe na kuonyana wenyewe kama wanavyofanya madaktari, wanasheria na wanataaluma wengine,” alisema.

Sheria ya Huduma za Habari 2016

Kifungu cha 10(1) cha Sheria ya Huduma za Habari ya 2016, kimeweka sharti la kuanzishwa kwa Bodi ya Ithibati itakayokuwa na wajumbe saba ambapo mwenyekiti atakuwa ni mwandishi mwandamizi. Ukiacha mwenyekiti ambaye atakuwa mwandishi mwandamizi, bodi hiyo itamjumuisha pia mkurugenzi wa Idara ya Habari, katibu wa bodi na mwanasheria kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa Serikali.

Vifungu vya 23 hadi 31 vya sheria hiyo vimeweka sharti la kuanzishwa kwa Baraza Huru la Habari ambalo majukumu yake ni pamoja na kusikiliza malalamiko dhidi ya vyombo vya habari.


Odinga Apendekeza Serikali ya Muda Iundwe Kenya

$
0
0
Odinga Apendekeza Serikali ya Muda Iundwe Kenya
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amependekeza serikali ya muda iundwe nchi humo na kutawala kwa muda wa miezi sita kama sehemu ya kutatua mzozo wa kisiasa nchini humo.
Bw Odinga, ambaye alisusia uchaguzi wa marudio uliofanyika mwezi uliopita, amesema katika kipindi hicho kunafaa kufanyika marekebisho ya katiba kuchunguza upya mamlaka ya rais.
Kiongozi huyo ambaye ameanza ziara nchini Marekani alisema yuko tayari kufanya mazungumzo na Rais Uhuru Kenyatta kuhusu marekebisho ya kikatiba ambayo anasema yanahitajika kupunguza hatari ya kuzuka kwa fujo kutoka kwa makundi ya jamii za wachache ambao wanajiona kwamba wametengwa.
Bw Kenyatta alitangazwa mshindi wa uchaguzi huo wa marudio uliofanyika tarehe 26 Oktoba akiwa na kura 7.5 milioni ambazo ni sawa na asilimia 98 ya kura zilizopigwa.
Waliojitokeza kushiriki uchaguzi huo ni asilimia 39 ya waliojiandikisha kuwa wapiga kura nchini humo.
Uchaguzi huo ulitokana na hatua ya Mahakama ya Juu, kufuatia kesi iliyowasilishwa na Bw Odinga, kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 Agosti ambapo Bw Kenyatta alikuwa ametangazwa mshindi akiwa na asilimia 54 ya kura.
Mahakama ya Juu ilisema uchaguzi huo wa mwanzo ulikumbwa na kasoro nyingi.
Bw Odinga alisusia uchaguzi wa marudio akisisitiza lazima mageuzi yafanywe katika Tume ya Uchaguzi (IEBC).
Alisema hakuna na imani kwamba uchaguzi huo wa marudio ungekuwa huru na wa haki.
Wafuasi wa Bw Odinga wamekuwa wakiandamana mara kwa mara tangu kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa kwanza.
Watu zaidi ya 50 wameuawa katika makabiliano kati ya polisi na wafuasi wa upinzani.
"Mfumo halisi wa utawala wa urais unaendeleza ukabila kwa sababu kila kabila linahisi kwamba haliko salama ikiwa mtu kutoka kabila hilo si kiongozi," aliambia Reuters kwenye mahojiano.


Katiba mpya iliyoanza kutekelezwa mwaka 2010 iligatua baadhi ya mamlaka ya serikali kuu kwa kuunda serikali za majimbo 47 zinazoongozwa na magavana.
Serikali hizo huwa na uwezo wa kujiendeshea shughuli nyingi lakini bw Odinga anasema mamlaka mengi bado yamebaki kwenye serikali kuu na hilo linafaa kubadilika.
"Tulipata katiba mpya mwaka 2010; Tunafikiri kwamba wakati umefika tuiangalie upya," amesema.
Alieleza kuwa marekebisho ya Katiba hiyo yanafaa kuimarisha taasisi huru za serikali mfano tume ya uchaguzi na kupunguza mamlaka ya rais.
"Tunafikiri kwamba pengine miezi sita itatosha kufanikisha marekebisho haya ambayo tunayahitaji katika taifa hili," alisema.
Bw Kenyatta, baada ya kutangazwa mshindi, alisema hatafanya mazungumzo na upinzani hadi umalize njia zote za kisheria za kupinga matokeo ya uchaguzi.

JE, Unasumbuliwa na Upungufu wa Nguvu, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE, UNASUMBULIWA NA UPUNGUVU WA NGUVU, HAMU YA TENDO LA NDOA AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?
      SOMA HAPA
    Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.

      BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
     Kwa kutumia mimea na matunda🍅🍍🍓🌿🍉🍒🍎 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=
      BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
🍉🍒🍓🌿🍍🍅🍀🍉
    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
      @markson_beauty_pr

Mawasiliano (+255)
          0767447444 na
              0714335378

        UTAPATA HUDUMA
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

     

Mpambano wa Aslay na Diamond Wahamia Kwenye Magari yap....BMW 3 vs. Diamond BMW 6

$
0
0
Wazee nimepita sehemu nikakuta haters wa Diamond wanasifia kishenzi kwamba Asley kanunua gari kali kuliko msanii yoyote hapa bongo,

Sasa mimi huwa sipendi ujinga nikaingia chimbo nikafanya upelelezi wangu nikagundua kumbe ile X3 ya Asley hata Millioni 100 haijafika bana, wakati huo kaka wa bongoflavor Diamond X6 yake inagonga 130 Millioni....

Nimeamini kweli hapa bongo ukishakua namafanikio tu basi haters watakuwinda kama traffic wa posta,

Cheki mashine hii....

 VIDEO:

Agizo la Rais Magufuli Laibua Maswali Bungeni

$
0
0
Agizo la Rais John Magufuli kuhusu wananchi wanaofanya shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka vyanzo vya maji wasibughudhiwe limeibua maswali bungeni ikielezwa Rais amevunja sheria.

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Peter Msigwa katika swali la nyongeza bungeni amesema, “Kwanza niipongeze wizara mara nyingi imejitahidi kuelimisha jamii itunze mazingira, lakini sisi kama wawakilishi wa wananchi tumsikilize Rais au waziri? mara nyingi tumeambiwa akisema Rais ni sheria jana amewaambia waingie kwenye mabonde walime mpaka mvua itakapowatoa,  lakini waziri unazuia.”

Akijibu, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi Lugola amesema Rais Magufuli hajavunja sheria kuagiza mamlaka zinazohusika na mazingira kuacha kuwabughudhi wananchi wanaolima pembezoni mwa mito.

Pia, ameonya viongozi wanaochochea wananchi kuvunja sheria na wananchi waliozoea kuzivunja akisema Serikali itapambana nao.

Lugola pamoja na waziri wa wizara hiyo, January Makamba leo Jumatano Novemba 8,2017 wamesema sheria inatoa mamlaka kwa waziri kutoa kibali kwa shughuli kufanyika katika maeneo hayo.

Waziri January amesema kutokana na maelekezo ya Rais Magufuli ya jana Jumanne Novemba 7,2017 kwa eneo mahsusi kwa mujibu wa sheria wataweka mwongozo wa matumizi.

Rais Magufuli alisema busara itumike wakati wa utekelezaji wa  sheria ya mazingira inayozuia shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka kwenye chanzo cha maji ili kuwaondolea  kero wakulima wanaojitafutia chakula na kipato cha kawaida kwa ajili ya familia zao.

“Ni vyema utekelezaji wa sheria ya mazingira ya mita 60 ilenge zaidi kubana wanaotumia maeneo ya maziwa na bahari na si wananchi wanaolima mazao ya  chakula ya muda mfupi kando mwa mito,” aliagiza.

Rais Magufuli alitoa kauli hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa mwananchi aliyejitambulisha kwa jina moja la Roshi, mkazi wa Kyaka wilayani Missenyi aliyedai kuwa mazao ya  chakula yaliyokuwa kwenye shamba lake lililopo kando mwa  mto yalifyekwa na watu wa mazingira kwa madai kuwa yalilimwa ndani ya mita 60.

Rais Magufuli alisisitiza agizo hilo wilayani Karagwe na hata mjini  Bukoba akiagiza wananchi hao kuendelea na shughuli za kujiongezea kipato na wasiondolewe katika maeneo hayo.

Kuhusu wananchi wanaodaiwa kuvamia vyanzo vya maji, Rais aliagiza watu zaidi ya 200 wanaodaiwa kuvamia vyanzo vya maji watafutiwe maeneo mengine kwa sababu ni kosa la viongozi na mamlaka husika zilizozembea kuwazuia mapema kuingilia maeneo hayo.

Serikali Yaweka Utaratibu wa Upigaji Picha Daraja la Nyerere

$
0
0
Serikali imetoa utaratibu wa upigaji picha katika daraja la Nyerere lililopo kigamboni ili kuhakikisha usalama wa miundombinu mali pamoja na watumiaji wote wa barabara hiyo.

Kaimu Meneja uhusiano na Masoko wa Shirika la Hifadhi ya Jamii Tanzania (NSSF), Salim Khalfan Kimaro, ameeleza kuwa ili kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara inayopita katika daraja hilo, fedha za makusanyo, pamoja na miundombinu, wapiga picha wote watapaswa kufuata utaratibu maalumu.

“Tumetoa taratibu maalum za kupiga picha baada ya kuzingatia hali halisi ya pale darajani ili kuwe na usalama wa wapiga picha wenyewe, lakini pia wapita njia pamoja na magari yanayokatisha pale na eneo letu la makusanyo kwa maana ya usalama wa fedha za makusanyo,” alisema Kaimu Meneja Kimaro.

Kaimu Meneja Kimaro alisema kuwa wapiga picha wote watapaswa kuomba kibali kwa Mkurugenzi Mkuu ambapo wataelekezwa kwa Afisa msimamizi wa mradi wa daraja la kigamboni ili wapewe maelekezo ya mahali salama na mahususi kwa kupigia picha.

Kimaro aliongeza kuwa kwa wale wanaopiga picha maalumu kama vile za harusi, video za kwaya na wasanii wa miziki mingine, watapaswa kulipia kiwango maalumu kilichowekwa ili waweze kupata huduma hiyo.

“Wale wanaopiga picha za matukio maalum watalipia kiwango fulani ambapo kwa saa moja ni 250,000 na kwa nusu saa ni 125,000,” alisema Kimaro.

Aidha kaimu Meneja kimaro alieleza kwamba wapiga picha wanaopiga picha moja moja ama ‘selfie’ hawatolipia lakini amewataka kuhakikisha kuwa wanachukua tahadhari ya usalama wao pamoja na watumiaji wengine wa barabara katika daraja hilo.

Download Application ya MCHAMBUZI Kwenye Simu yako Kusoma Habari za Siasa Kila Baada ya Lisaa Limoja

$
0
0

Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Kwenye simu yako
BonyezaHAPA

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... 
Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako

Pendeza Kwa Kutumia Kessy Products..Kuweka Mwili Wako Sawa Kwa Products Zisizo Kuwa na Madhara

$
0
0
*PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA  MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA* 🍇🌾🌳
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE  NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATAKS)KUNADAWA AINA TATU (@)JELI KUPAK_100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI NA MAPAJAN_80,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE NA MANYAM YOTE
@) DAW YA MAJINI_100,000/NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME BILA KUVAA SIDIRIA_80,000/
8)KUONGEZA MAZIWA NA SAIZI NZURI_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA (kifaru)_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO YAKAWAIDA NA UZAZ_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_70,000/
13) KUWA MWEUPE  WAKUPENDEZA KWA DAW(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWLINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA JELI PAMOJA NA VIDONGE VYAAIN ZOT _100'000
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_ 120,000 /
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_80,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _80,000/
20)ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA     MGUU_80,000/🍍🍉🌾                                                                                    *TUNAPATIKAN DAR E SALAAM*  *NAKWA *MIKOANKOTE* UTAPATA *PIA* *NA NCHI ZOTE PIGA CM*                                        
(+255)0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product*
 *Delivery  POPOTE ULIPO,*

Kingu Awaahidi Wananchi wa Singida Mashariki Kubeba Jukumu la Tundu Lissu

$
0
0
Kingu Awaahidi Wananchi wa Singida Mashariki Kubeba Jukumu la Tundu Lissu
Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu amewaahidi wananchi wa Kata ya Siuyu jimbo la Singida Mashariki kuwa endapo watamchagua mgombea udiwani wa CCM, atakuwa mlezi wao na kwenda kuwasemea bungeni kuhusu matatizo ya maji waliyonayo, jukumu ambalo linapaswa kufanywa na Lissu ambaye ndiye mbunge wa hapo.

Mh. Kingu ametoa ahadi hiyo wakati akimnadi mgombea wa Udiwani kata ya Siuyu Wilayani Ikungi Mkoani Singida ambapo mbali na kuahidi kuwa mlezi wa kata hiyo amewaahidi wakina mama kuwapatia Milioni 15 katika mfuko wa VICOBA endapo watafanikisha kumpatia ushindi mgombea huyo wa CCM Mgonto Juma Ramadhani
"Mimi kama Mbunge wa Singida Magharibi naahidi na nitayatekeleza baada ya uchaguzi wa tarehe 26. Nitatoa milioni 15 kwa ajili ya kata ya Siuyu peke yake na Ofisi za chama mmesema kwamba hamna viti nitawapatia Milioni moja kwa ajili ya viti. Nimepewa taarifa kuna vijiji havina maji hii agenda ya Siuyu nitaibeba na nitaipeleka Dodoma kuiwasilisha na baada ya hapo nitamleta Waziri wa Maji kuja kutatua hiyo changamoto", amesema Kingu


'Nimeogopa kuja na hizo fedha hapa kwa sababu watasema nahonga  hivyo nitasubiri mpaka uchaguzi upite ndiyo nilete  ili nisije kuchafua hali ya hewa kwa sasa" Kingu.
Kwa upande wa Mgombea wa Kata hiyo amewaomba wananchi kumchagua ili aende kuwawakilisha katika baraza la madiwani katika kutatua tatizo la maji ambalo lipo kwa mda mrefu na tatizo la barabara ambayo ni mbovu.
Uchaguzi katika kata ya Siuyu unafanyika baada ya Diwani Gerald Mahami aliyekuwepo kutoka (CHADEMA) kuvuliwa udiwani kutokana na kuwepo madai ya kushindwa kuhudhuria vikao vya baraza la madiwani.

Twitter Yafanya Mabadiriko Yawaruhusu Watu Wengi Kutumia Tarakimu 280 Kuandika Ujumbe

$
0
0
Twitter Yafanya Mabadiriko Yawaruhusu Watu Wengi Kutumia Tarakimu 280 Kuandika Ujumbe
Twitter imetangaza kwamba imeanza kuwafungulia watu wanaoutumia mtandao huo wa kijamii uwezo wa kuandika ujumbe kwa kutumia tarakimu 280 badala ya 140.
Kampuni hiyo ilikuwa imewawezesha baadhi ya watu kutumia tarakimu hizo lakini kwa majaribio tangu Septemba.
Lakini sasa wamesema watu wengi wataruhusiwa kuandika ujumbe mrefu.
Watakaozuiwa pekee ni wale wanaoandika ujumbe kwa Kijapani, Kichina na Kikorea ambao wanaweza kuwasilisha maelezo zaidi kwa kutumia tarakimu chache.
Twitter wamesema majaribio yalifanikiwa.
Mabadiliko hayo ni sehemu ya mpango wa Twitter kuwavutia watu zaidi.
Wakati wa majaribio, ni ujumbe 5% ambao ulikuwa na urefu wa zaidi ya tarakimu 140 na ni 2% uliokuwa na zaidi ya tarakimu 190, wamesema.
Lakini walioandika ujumbe mrefu walipata wafuasi zaidi, walihusiana na watu zaidi na walitumia muda zaidi katika mtandao huo.
"Tuliona kwamba watu walipohitaji zaidi ya tarakimu 140, waliandika ujumbe kwa urahisi na mara nyingi. Muhimu zaidi, watu waliandika ujumbe wa chini ya tarakimu 140 mara nyingi zaidi na ufupi wa ujumbe wa Twitter ulisalia," meneja wa bidhaa na huduma wa Twitter Aliza Rosen ameandika.
Mabadiliko hayo yalipotangazwa mara ya kwanza, wengi waliyakosoa na kusema badala yake wangelipenda kuona taarifa za chuki pamoja na mashine zinazoandika ujumbe zikidhibitiwa zaidi.
Aidha, wengi walitaka ujumbe urudi kufuata historia tena, ujumbe wa karibuni zaidi ukionekana mwanzo na pia waweze kuhariri ujumbe.
Mtandao huo kwa sasa una watu 330 milioni, idadi ambayo ni ya chini ukilinganisha na 800 milioni wa Instagram na zaidi ya 2 bilioni wa Facebook.

Mahakama Yaanza Kusikiliza Ushahidi wa Kesi ya Kutoa Lugha Chafu Inayomkabili Halima Mdee

$
0
0
Mahakama Yaanza Kusikiliza Ushahidi wa Kesi ya Kutoa Lugha Chafu Inayomkabili Halima Mdee
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kuanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya kumtolea lugha ya matusi Rais John Magufuli inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee (39), December 7, 2017.

Wakili wa serikali, Leornad Challo amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa kesi imeitishwa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa lakini shahidi waliyenaye ana safari.

Baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi December 7, 2017 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa.

Awali katika kesi hiyo Mdee aliposomewa maelezo ya awali inadaiwa July 3/2017 akiwa Makao Makuu ya Chadema, maeneo ya Ufipa alitoa lugha ya matusi dhidi ya Rais Magufuli.

Inadaiwa alitukana kuwa “Rais anaongea hovyo hovyo, inabidi afungwe break”.

Baada ya kutoa lugha hiyo, July 4/2017 alikamatwa na Polisi maeneo ya Kibangu, kisha kupelekwa kwa ZCO ambapo alihojiwa na kukiri kutoa maneno hayo.

Baada ya kusomewa maelezo hayo, Mdee alikubali wasifu wake ambao ni Jina, umri, nafasi ya uongozi, mahali anapokaa, kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Lakini alikana kumtolea lugha ya matusi Rais Magufuli, pamoja kukiri maneno hayo wakati akihojiwa katika ofisi za ZCO.

Vyama Vinne Vya Siasa Vyaungana Kumpinga Weah Kuwa Rais

$
0
0
Vyama vya Siasa Vinne Vyaungana Kumpinga Weah Kuwa Rais
Vyama vinne vya siasa Jumanne vilifanya mazungumzo ili “kuungana” kwa lengo la kumpa uwezo makamu wa rais Joseph Boakai kupambana dhidi ya mchezaji soka nyota wa zamani wa kimataifa George Weah kuwania kiti cha urais wa Liberia.

Ofisa wa ngazi ya juu wa chama tawala cha Unity Party (UP) alisema mazungumzo hayo yalifanyika siku ambayo wananchi wa Liberia walipaswa kupiga kura katika uchaguzi wa marudio kati ya Weah aliyeongoza duru ya kwanza kwa asilimia 38 na Boakai aliyeshika nafasi ya pili akiwa na asilimia 28.

Uchaguzi huo wa marudio haukufanyika kama ilivyopangwa baada ya Mahakama ya Juu, Jumatatu kuiweka Liberia kwenye njiapanda ilipositisha kwa muda usiojulikana, na wadadisi wa masuala ya siasa wanasema unaweza kucheleweshwa kwa wiki kadhaa.

Mahakama iliamua uchaguzi usiendelee hadi yatakapotatuliwa malalamiko kuhusu ulaghai katika mchakato yaliyowasilishwa na chama cha Liberty Party ambacho mgombea wake ni Charles Brumskine.

Mwenyekiti wa UP, Robert Kpadeh alisema mazungumzo yalihusu vyama vinne vilivyoweka wagombea urais akiwemo Brumskine, ambaye alishika nafasi ya tatu katika uchaguzi wa Oktoba 10 na walijadili “kuunganisha nguvu katika Nyanja mbalimbali."

"Unachokiona leo ni ishara kubwa kwa ulimwengu kwamba wanakuja pamoja kwa lengo la kupigania demokrasia,” alisema Kpadeh.

"Tunaamini kabisa kwamba Weah hawezi kuongoza nchi."

Alipoulizwa ikiwa vyama hivyo vitamfanyia kampeni Boakai iwe kwa uchaguzi wa marudio ikiwa hatimaye utafanyika, Kpadeh alijibu: "Inawezekana" akasisitiza kwamba vyama hivyo vinne vimekubaliana kusimamia pamoja kesi dhidi ya ulaghai.

Oktoba 23 Brumskine alifungua kesi akilalamikia "ulaghai mkubwa na dosari" uliofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) akidai kuzikwa kwa baadhi ya makaratasi ya kupigia kura na kujaa kadi za kidanganyifu.


Ali Kiba Awaacha Watu Njia Panda Awaachia Swali Hili Mashabiki " Nini Kinafuata?"

$
0
0
Ali Kiba Awaacha Watu Njia Panda Awaachia Swali Hili Mashabiki " Nini Kinafuata?"
Staa wa muziki wa bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘AliKiba’ ameanza kuonesha dalili za ujio wa kazi nyingine baada ya ‘Seduce Me’ iliyoingia kwenye rekodi ya kazi zake zilizopokelewa vizuri zaidi ndani ya muda muda mfupi kwa mwaka 2017.

AliKiba sio mtu wa maneno mengi katika kuachia kazi zaidi ya vionjo vya kugusia gusia kwa maneno machache ya kinachopatikana katika kazi yake yoyote pindi anapoelekea kuiachia rasmi ambapo mapema leo aliweka picha yake akiuliza mashabiki kuwa nini ‘Kinafuata?? ‘What Next…?.
Muda mfupi baadae mara baada ya post hiyo iliyoambatana na swali, Kiba aliweka picha yake nyingine akiwa na muongozaji wa video mpya ya kolabo ya wimbo ‘Malo’ wa Tiwa Savage uliyowashirikisha StarBoy ‘Wizkid’ na Spellz, Director Meji Alabi. Swali likaibuka Je’ anachouliziwa kuwa nini kifuate kimeongozwa na Director Meji Alabi ambaye aliongoza video ya hitsong ya ‘Chekecha Cheketua’ ya AliKiba.

Sifungi Magoli Kwaajili ya Kushindana na Mtu Natoa Mchango kwa Timu Yangu- Kichuya

$
0
0
Sifungi Kwaajili ya Kushindana na Mtu Natoa Mchango  kwa Timu Yangu- Kichuya
BAADA ya kufanikiwa kuifungia bao la ushindi timu yake dhidi ya Mbeya City, kiungo wa Simba, Shiza Kichuya amesema kuwa sasa ameanza kazi ya kuhakikisha anaendeleza kasi ya kufumania nyavu.
Kichuya amefikisha mabao matano sawa na Ibrahim Ajibu wa Yanga huku mshambuliaji Emmanuel Okwi akiongoza kwa kuwa na mabao nane.

Aidha, kiungo huyo msimu uliopita alimaliza ligi kwa kufunga mabao 12 sawa na Obrey Chirwa na Amissi Tambwe wa Yanga, Mbaraka Yusuph aliyekuwa Kagera Sugar msimu uliopita sasa Azam FC.
Akizungumza na Championi Jumatano, Kichuya alisema kuwa kazi yake ni kufunga na anajipanga kuona anaendeleza kasi ya kufumania nyavu katika kila mechi.
“Nimejipanga kuhakikisha nafanikiwa kuifungia timu yangu katika kila mechi pale ninapopata nafasi ya kufanya hivyo kwani kila mechi ambayo tunacheza inakuwa na ugumu wa hali ya juu, hivyo tunapambana.
“Nafunga kwa ajili ya kuisaidia timu yangu iweze kufanya vizuri na kusonga mbele katika msimamo wa ligi kwa kupeana ushirikiano ipasavyo na wachezaji wenzangu.

“ Kwa upande wangu sifungi kwa ajili ya kushindana na mtu, bali ninachokifanya ni kwa ajili ya kutoa mchango wangu katika timu tu mabao nitakayomaliza nayo kwenye ligi ndiyo hayo Mungu atakayonijaalia kufunga lakini kasi yangu ya kupambana sasa inaongezeka,” alisema Kichuya.

Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images