Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtaalam na Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Pumu, Vidonda vya Tumbo, Kisukari na Mengine Mengi

$
0
0

MTALAAM NA BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU NAYALIYOSHINDIKANA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI,MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni SUPER SAYI 3,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu 

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

SUPER SAYI 4 Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR ULIMWENGU ANAPATIKA DAR ES SALAAM MAGOMENI MOROCO

HUDUMA HIZI UTAZIPATA MAGOMENI 

SIMU NO 0745387469, 0652121197

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Mwigulu Akanusha Madai ya Rais Magufuli Kupendelea Kanda ya Ziwa

$
0
0
Mwigulu Akanusha Madai ya Rais Magufuli Kupendelea Kanda ya Ziwa
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema kuwa si kweli kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli anapendelea Kanda ya Ziwa kama alivyozungumza Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa.

Nchemba ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma baada ya Mbunge huyo wa Iringa kuibuka hoja hiyo . Ambapo Waziri huyo amesema kuwa amekuwa Rais huyo amekuwa akisikiliza vilio vya wananchi pale anapokuwa eneo husika moja kwa moja.

“Kuna hili suala la kusema Rais anapendelea kanda ya ziwa,nataka niweke kumbukumbu sawa Mh. Rais si kwamba anapendelea Kanda ya Ziwa, ila Rais amekuwa anasikiliza vilio vya wananchi pale anapokuwa eneo husik,a moja ya jambo ambalo nataka nitumie kumbukumbu Mh. Rais alipokuwa Bagamoyo wananchi walipolilia eneo la Magereza alilitoa hapo hapo, huku sheria ikiwa inataka eneo lile litumike kwaajili ya Magereza,”amesema Waziri Nchemba.

“Lakini kwakuwa kilio cha wananchi kilikuwa kikubwa, na huko sio Kanda ya Ziwa ni Pwani alilitoa hapo hapo hata akusubiri maelekezo ya Wizara kukaa kama alivyosema Kanda ya Ziwa, pale aliamua hapo hapo alisema wananchi wapewe eneo hilo na hivyo ndivyo anatolea utatuzi wa changamoto za wananchi na hicho ndicho kilichomfanya achaguliwe.”

Idadi ya Wanafunzi Waliokufa Kutokana na Bomu la Kutupa kwa Mkono Mkoani Kagera Yaongezeka

$
0
0
 Idadi ya wanafunzi waliopoteza maisha  kutokana na bomu la  kutupwa kwa mkono katika shule ya msingi Kihinga wilaya ya Ngara mkoani Kagera imeongezeka na kufikia sita huku kukiwa na majeruhi  42 ambao wamelazwa Hospitali ya misheni Rulenge.


Mganga Mkuu  Hospitali ya Rulenge Sr Goleth Fredrick amesema idadi hiyo imeongezeka baada ya wengine kutolewa katika kituo cha afya Bukiriro na kwamba wanafunzi watatu wamefariki na kufikisha idadi ya vifo vya wanafunzi sita.

Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Agustino Olomi amesema chanzo cha wanafunzi hao kujeruhiwa kwa bomu ni baada ya mmoja wao kuliokota akidhani ni chuma chakavu.

“Mmoja wapo aliliokota akidhani kwamba ni chuma chakavu hivyo akaamua kuja nalo shuleni baadaye  alipeleke kwa mnunuzi  ili aweze kununua  madaftari’’amesema

Hata hivyo kamanda wa Kikosi cha Kulinda mipaka cha jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ wilaya ya Ngara meja Mutaguzwa amesema bomu hilo lilikuwa na vipande 36 na lingelipukia ndani ya darasa lingeleta athari zaidi .

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Misheni Rulenge, Goreti Francis amethibitisha kupokewa miili  ya wanafunzi hao  waliopoteza maisha.

“Majeruhi wana majeraha sehemu mbalimbali za mwili, tunafanya kila jitihada kuokoa maisha yao,” amesema Dk Francis.

Akizungumza kwa simu akiwa eneo la tukio, zaidi ya kilomita 50 kutoka Ngara mjini, diwani wa Kibogora, Adronis Bulindoli amesema wanafunzi waliofariki wana umri kati ya miaka minane na tisa.

Syria Yaitenga Marekani Kutokana na Msimamo Wake

$
0
0
Marekani inakaribia kutengwa kutokana na msimamo wake kuhusu makubaliano ya tabia nchi baada ya Syria kusema kuwa iko tayari kuunga mkono makubaliano hayo.

Makubaliano hayo ya Paris yanaunganisha mataifa duniani katika kukabiliana na hali ya tabia nchi.

Syria na Nicaragua yalikuwa mataifa ya pekee nje ya makubaliano hayo wakati yalipotiwa saini 2015.

Nicaragua ilitia saini yake mnamo mwezi Oktoba.

Mnamo mwezi Juni Marekani ilisema kuwa itajiondoa , lakini sheria za mkataba huo zinasema kuwa hatua hiyo haiwezi kufanyika hadi 2020.

Wakati huohuo maafisa wa Ufaransa wamesema kuwa rais Donald Trump hakualikwa katika mkutano wa wa Disemba kuhusu hali ya tabia nchi utakaofanyika mjini Paris.

Zaidi ya mataifa 100 yamealikwa katika mkutano huo ambao unalenga kujenga miungano ya kifedha na kibishara ili kuimarisha mkataba huo kulingana na msaidizi wa rais Emmanuel Macron.

Akitangaza uamuzi huo wa Marekani mnmao mwezi Juni, rais Trump alisema kuwa ni wajibu wake kuilinda Marekani na kwamba atakubaliana na mkataba mpya ambao hautaathiri biashara za Marekani.

Alidai kwamba mkataba huo utagharimu kazi milioni 6.5 za Wamarekani na dola trilioni 3 za uchumi wake, huku washindani wake wakuu kama vile China na India wakipendelewa na makubaliano hayo.

Taarifa ya Marekani iliotolewa mwezi Oktoba baada ya Nicaragua kutia saini makubaliano hayo ilisema kuwa Marekani itajiondoa hadi pale mkataba huo utakapoipendelea.

Msemaji wa Ikulu ya Whitehouse Kelly Love amesema kuwa hakuna mabadiliko yoyote kuhusu msimamo huo.

Hii Hapa Hoteli ya Kifahari Ambayo ni Gereza kwa Wanawafalme Saudi Arabia

$
0
0
Hii Hapa Hoteli ya Kifahari Ambayo ni Gereza kwa Wanawafalme Saudi Arabia
Ni jina la mahoteli ya kifahari yaliyo maarufu kote duniani.
Marais, mawaziri wakuu na wafalme wamekaribishwa katika mahoteli ya Ritz-Carlton.
Lakini kwa mujibu wa ripoti kadhaa, mahoteli hayo katika mji mkuu wa Saudi Arabia yamekuwa gereza.
Miezi michache baada ya kumkaribisha Rais wa Marekani Donald Trump wakati wa ziara yake ya kwanza kama rais, watu kadhaa mashuhuri nchini Saudi Arabia sasa wanaripotiwa kuwa wageni wa serikali huku hoteli hiyo ikitajwa kuwa gereza la kifahari zaidi duniani.
Wanawafalme 11, mawaziri wanne na watu wengine kadhaa wamekamatwa katika kile mamlaka za saudi Arabia zinasema kuwa ni kampeni ya kupambana na ufisadi nchini humo.
Bilionea maarufu duniani Prince Alwaleed bin Talal anaripotiwa kuwa miongoni mwa wale waliokamatwa.
Mtandao wa gazeti la The New York Times ulichapisha kanda ya video iliyoonyesha wajibu mpya wa hoteli ya Ritz-Carlton Riyadh.
Katika video hizo walinzi wanaonekana wamelala kwenye mikeka katika chumba kimoja cha hoteli, watu wenye sare pia nao wanaonekana huku bunduki zikionekana zikiegeshwa kwenye ukuta.
Gazeti la Guardian liliripoti kuwa wageni waliombwa siku ya Jumatano jioni wakusanyike sehemu moja na mizigo yao, kabla ya kusafirishwa kwenda kwa hoteli zingine mjini Riyadh.
The Guardian inamnukuu afisa mmoja wa Saudi Arabia akisema kuwa mamlaka hazingeweza kuwaweka watu hao gerezani na hilo lilikuwa suluhu bora.
Jitihada za kulipia vyumba katika hoteli hiyo siku ya Jumannwe hazikuzaa matunda.

Farid Musa kuikosa Taifa Stars vs Benin Kutokana na Tatizo la Goti

$
0
0
Farid Musa kuikosa Taifa Stars vs Benin Kutokana na Tatizo la Goti
Ikiwa imepita siku moja tu toka jopo la madaktari club ya KRC Genk ya Ubelgiji inayochezewa na nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Mbwana Samatta, watoe taarifa kuwa Mbwana Samatta hatokuwa uwanjani hadi mwanzoni mwa kipindi cha majira ya baridi kufuatia kuumia kwa goti lake la kulia.
Leo taarifa mpya zimetolewa kuhusiana na mtanzania Farid Musa anayecheza soka la kulipwa nchini Hispania akiichezea Tenerife B, Farid Musa ambaye jina lake lilikuwa sehemu ya kikosi cha Taifa Stars kitakachocheza dhidi ya Benin November 12 2017, zimetoka taarifa kuwa ameumia goti.
Farid Musa anaripotiwa kuwa ameumia ligament za goti na anasubiri kufanyiwa vipimo vya mwisho ambayo vitatoa taarifa rasmi kuhusu muda atakaokaa nje staa huyo wa Tanzania lakini taarifa za awali zinaelewa kuwa kwa mujibu wa jeraha lake anaweza kukaa nje ya uwanja kwa kipindi chote cha msimu kilichosalia.

Ali Choki Atoa ya Moyoni Kuhusu Muziki wa Dansi

$
0
0
Ali Choki Atoa ya Moyoni Kuhusu Muziki wa Dansi
MUZIKI wa Dansi, ambao miaka kumi iliyopita ulikuwa ndiyo habari ya mjini katika burudani, hivi sasa unaonekana kupoteza mvuto, kiasi kwamba wengi wanaamini upo njiani kuelekea kaburini, ambako tayari tasnia nyingine, Bongo Movie, inasubiri kufukiwa.
Mmoja wa wanamuziki wa dansi la kizazi kipya, Ali Choki ambaye alikuwepo wakati muziki huo ukishika hatamu na anashuhudia wakati huu mgumu, ni Ally Choki mwenye majina mengi ya kisanii, yakiwamo Kamarade, Mzee wa Farasi, Mzee wa Kijiko, Mzigo na mengine kibao.

Katika mahojiano maalum, Choki anapingana na hisia za kudondoka kwa muziki huo, akisema kinachotokea ni kuwepo kwa kundi la watu wenye uwezo ambao hawataki kuiona dansi ikitamba.

Mkongwe huyo anaamini kuwa baadhi ya vituo vya redio, ambavyo ndivyo vilikuwa chachu kubwa ya kukua kwa muziki huo, vimechangia kuukosesha msisimko kwa kuacha kupiga kama ilivyokuwa ikifanya siku za nyuma.

“Zamani kulikuwa na chati mbalimbali kwenye redio, vipindi kama nani zaidi katika muziki wa dansi, top ten na nyimbo zetu zilipigwa mara kwa mara, nyimbo mpya zilizinduliwa na kufanya kuwa na hamasa kubwa miongoni mwa wanamuziki, lakini angalia hivi sasa.

“Hata hizo nyimbo za dansi zimepangiwa vipindi vya usiku sana, wakati ambao watu wameshachoka wamelala, nani atasikiliza nyimbo usiku mkubwa, hata hao wazee ambao unaweza kusema eti ndiyo muziki wao, wameshalala.

“Dansi bado ipo na ina watu, isipokuwa kuna kundi flani la watu hawaupendi huu muziki, wanatamani utoweke, lakini haitawezekana, utakuwepo tu na utarejea enzi zake, katika hili ni lazima tuwashirikishe wadau, hasa vyombo vya habari kama magazeti, redio na televisheni, maudhui ya muziki huu bado ni mazuri,” anasema Choki, ambaye kwa mara nyingine, amerejea African Stars ‘Twanga Pepeta’ baada ya kuwa nje kwa miaka kadhaa.

Anasema tatizo kubwa linaloukabili muziki wa Dansi ni kuondoka kwa kizazi chake katika maeneo muhimu ya redio, televisheni na magazeti na kuwepo kwa wale aliowaita, vijana wa Bongo Fleva.

“Kuna watu wapo katika hizo sehemu hawaujui huu muziki, wao wameikuta Bongo Fleva, ndiyo maana kila redio ina chati za muziki wa kizazi kipya, dansi hawana muda nao, lakini pia kuna hawa mapromota nao, wapo tayari kumlipa msanii mmoja shilingi milioni tano, lakini bendi wanataka kwa laki tano, wakati kundi lina watu wengi, hawa nao wanatakiwa kubadilika.

“Sasa hivi hakuna anayehangaika kutaka kujua bendi gani imetoa wimbo gani mpya, tofauti na zamani, kila bendi ilipotoa wimbo mpya, ulipata ‘airtime’ ya kutosha, hapa kuna tatizo la makusudi ambalo linawezekana kabisa kupatiwa majibu,” anasema.

Juu ya mustakabali wake kimuziki, Choki anasema mkataba wake na bendi hiyo utamalizika mwakani, hivyo huu ni wakati wa yeye kutambua nini kitafuata baada ya hapo.

“Kuna vitu vingi vya kufanya kuelekea kumalizika kwa mkataba wangu, sijajua kama nitarejesha bendi yangu au nitatafuta kazi sehemu nyingine, lakini kuna kitu kinapita akilini mwangu ili nijue cha kufanya,” anasema.

Kuhusu kushuka kwa ushindani wa kimuziki baina ya bendi na bendi kama ilivyokuwa miaka iliyopita, alisema hali hiyo inachangiwa na sababu alizotoa mwanzo, kwani kama ni kwenda na wakati, wapo baadhi ya wanamuziki ambao wanabadilika kulingana na mazingira.

“Muziki wa Dansi ni kama jeans tu, miaka nenda rudi ipo, tumez-aliwa tumeikuta na sasa tunazeeka yenyewe ipo tu, inabadilika staili tu, mara pana, mara nyembamba, inayobana na sasa imekuja kwa staili ya kuchanwa, lakini ipo tu.

“Wanamuziki pamoja na wadau wanatakiwa kubadilika kidogo ili urejee, lakini nina uhakika hautakufa na mimi kama mwanamuziki, nitasimama kuhakikisha dansi inarudi na kutesa kama zamani,” anasema Choki, ambaye licha ya African Stars, amewahi pia kupigia Bendi za Bantu Group, Mchinga Sound, TOT Plus, Double Extra na ile aliyokuwa akiimiliki, Extra Bongo.

Kutana na Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed Kutoka Bagamoyo...Ana Dawa za Kurudisha Mapenzi na Zingine Nyingi

$
0
0
MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

USHAURI: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.

Kesi Mbili Zawasilishwa Mahakamani Kupinga Ushindi Wa Kenyatta

$
0
0
Kesi mbili zimewasilishwa katika mahakama ya juu nchini Kenya, zikitaka kufutwa kwa ushindi wa rais Uhuru Kenyatta kufuatia uchaguzi wa tarehe 26 mwezi Oktoba.

Kesi hizo ziliwasilisha mahakamani Jumatatu saa chache kabala ya siku ya mwisho.

Aliyekuwa mbunge wa kilome Harun Mwau na mawakili Njonjo Mue na Khelef Khalifa, wanasema kuwa katiba ilikiukwa wakati wa maandalizi ya uchaguzi huo.

Kesi ya mwau ambayo inawashtaki IEBC, mwenyekiti wake na Rais Uhuru Kenyatta ambaye alitangazwa mshindi kwenye uchaguzi wa mwezi Oktoba, inasema kuwa kushindwa kwa IEBC kuruhusu vyama kuandaa uchaguzi wa vyama, kuliwanyima wale ambao walitaka kugombea fursa ya kufaya hivyo.

Mwau alijumuisha kipengee cha uamuzi wa mahakama, kuwa mgombea kwa chama cha United Democratic Cyrus Jirongo alikuwa amefilisika kwa hivyo hakustahili kuwania urais.

Kesi iliyowasilishwa na mawakili Mue na Khalifa nayo kwa upande mwngine ilizunguzia ukiukaji wa katiba ikiwemo kuchapisha picha za watu wasiostahili kwenye makaratasi ya urais akiwemo mgombea wa muungano wa NASA Raila Odinga, ambaye alikuwa ametangaza kuwa hangegombea urais.

Akiongea na vyombo vya habari wakati wa kuandika kesi hiyo, wakili wa Mue na Khalifa, Harun Ndubi, alisema kwa tume ya uchaguzi haukustahili kuandaa uchaguzi kwa hivyo wanataka uchaguzi huo kuandaliwa upya.

Ndubi alisema kuwa tume ya uchaguzi ilikuwa na upendeleo kwa hivyo haikustahili kuandaa uchaguzi.

Ndubi aliwaambia waandishi wa habari kuwa kumjumuisha Odinga kwenye makaratasi ya kura licha ya yeye kujiondoa kuliwachanganya wapiga kura.

CHANZO:BBC SWAHILI

Kingu Awaahidi Wanasingida Kama Watachagua Diwani Wa CCM Basi Atabeba Majukumu Yote Ya Tundu Lissu

$
0
0
Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu amewaahidi wananchi wa Kata ya Siuyu jimbo la Singida Mashariki kuwa endapo watamchagua mgombea udiwani wa CCM, atakuwa mlezi wao na kwenda kuwasemea bungeni kuhusu matatizo ya maji waliyonayo, jukumu ambalo linapaswa kufanywa na Lissu ambaye ndiye mbunge wa hapo.

Mh. Kingu ametoa ahadi hiyo wakati akimnadi mgombea wa Udiwani kata ya Siuyu Wilayani Ikungi Mkoani Singida ambapo mbali na kuahidi kuwa mlezi wa kata hiyo amewaahidi wakina mama kuwapatia Milioni 15 katika mfuko wa VICOBA endapo watafanikisha kumpatia ushindi mgombea huyo wa CCM Mgonto Juma Ramadhani

"Mimi kama Mbunge wa Singida Magharibi naahidi na nitayatekeleza baada ya uchaguzi wa tarehe 26. Nitatoa milioni 15 kwa ajili ya kata ya Siuyu peke yake na Ofisi za chama mmesema kwamba hamna viti nitawapatia Milioni moja kwa ajili ya viti. Nimepewa taarifa kuna vijiji havina maji hii agenda ya Siuyu nitaibeba na nitaipeleka Dodoma kuiwasilisha na baada ya hapo nitamleta Waziri wa Maji kuja kutatua hiyo changamoto", amesema Kingu

'Nimeogopa kuja na hizo fedha hapa kwa sababu watasema nahonga  hivyo nitasubiri mpaka uchaguzi upite ndiyo nilete  ili nisije kuchafua hali ya hewa kwa sasa" Kingu.

Kwa upande wa Mgombea wa Kata hiyo amewaomba wananchi kumchagua ili aende kuwawakilisha katika baraza la madiwani katika kutatua tatizo la maji ambalo lipo kwa mda mrefu na tatizo la barabara ambayo ni mbovu.

Uchaguzi katika kata ya Siuyu unafanyika baada ya Diwani Gerald Mahami aliyekuwepo kutoka (CHADEMA) kuvuliwa udiwani kutokana na kuwepo madai ya kushindwa kuhudhuria vikao vya baraza la madiwani.

"Magufuli ni Mpango wa Mungu" - Godbless Lema Afunguka Arusha

$
0
0
Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amekiri kwa wakazi wa Murieti Mkoani Arusha kwamba Rais John Magufuli ni Mpango wa Mungu kwani Mpango wa Mungu siyo lazima uwe mzuri.

Akizungumza wakati wa kumuombea kura mgombea wa udiwani kata ya Muriet, Mh. Lema amesema kwamba maisha watanzania wanayoyapitia ni kutokana na serikali ya awamu ya tano.
"Rais Magufuli mimi nasema ni Mpango wa Mungu. Ugumu huu wa Maisha umesababishwa na serikali ya awamu ya tano wafanyabiashara hawana kazi, hivyo ninaposema ni mpango wa Mungu mkumbuke siyo lazima uwe mzuri lakini pia naombeni nikisema mpango wa Mungu mjue anawakumbusha nini cha kufanya" Lema.
Mh Lema katika Kata hiyo ambaye amemnadi mgombea Mosses amesema kwamba vitisho vya Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo haviwashtui kwani yeye anachojua ni kwamba CHADEMA itashinda na wao watashindwa hivyo mpango wa kugoma klumtangaza mshindi wa cchadema utawapa nafasi ya kutambua namna ya kuishi nao wakati mwingine.

Pamoja na hayo Mbunge Lema amewataka wananchi wa Murieti kumpigia kura mgombea huyo wa Chadema Simon Moses Mollel. kwani ndiye atakayeweza kuwatetea katika kutafuta maendeleo na siyo CCM ambayo imekuwa ikisababisha maisha magumu.

Hata hivyo Lema amewaweka wazi wana Muriet kwamba pamoja na kuwa bunge limekwishaanza hataweza kuondoka mkoani hapo mpaka atakapohakikisha amewachosha CCM vya kutosha.

EATV

RPC Kagera Afafanua Bomu lilivyoua Wanafunzi

$
0
0
Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani kagera Agustino Olomi amesema chanzo cha wanafunzi kupoteza maisha na kujeruhiwa kwa bomu ni kutokana na Mwanafunzi kuokota bomu hilo akidhani chuma chakavu ili aweze kwenda kuuza.

Katika taarifa aliyoitoa akizungumza na Wanahabari Kamanda Olomi amesema kwamba katika kijiji hicho kumekuwa na tabia ya kuuza vyuma chakavu ambapo mnunuzi huwa akiwapatia malipo ya madaftari.

Kwa upande wa Kamanda wa Kikosi cha kulinda mipaka cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ wilaya ya Ngara Meja TR Mutaguzwa amesema Bomu hilo lilikuwa na vipande 36 na lingelipukia ndani ya darasa lingeleta athari zaidi .

Mjadala wa Tundu Lissu Waibuka Bungeni

$
0
0
Kambi rasmi ya upinzani bungeni imelaani na kupinga vitendo viovu alivyotendewa Mnadhimu wa Kambi hiyo, Tundu Lissu, ambaye alinusurika kifo baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana Septemba 7, mwaka huu mjini Dodoma

Lissu ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema, anaendelea kupatiwa matibabu katika   hospitali moja ya Nairobi,   Kenya.

Akiwasilisha bungeni maoni ya kambi rasmi ya upinzani bungeni jana kuhusu mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2018/2019 kwa niaba ya Msemaji Mkuu wa kambi hiyo,  Halima Mdee, David Silinde alisema vitendo hivyo vinatakiwa vikemewe kwa uzito unaostahili.

Silinde  ambaye ni Mbunge wa Momba (Chadema), alisema vitendo hivyo vikiachwa viendelee bila kukemewa kuna hatari ya kundi linalohisi kuonewa likakosa uvumulivu na hivyo kuathiri amani ya nchi.

“Ingawa  miezi miwili sasa imepita tangu Lissu anusurike kifo baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi wakati mkutano  wa nane wa bunge ukiwa unaendelea na vikao vyake hapa Dodoma na mpaka sasa hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na serikali juu ya kukamatwa kwa watu waliohusika na tukio hilo.

“Ikiwa polisi wameshindwa kufanya uchunguzi na kuwakamata wahalifu hao ndani ya miezi miwili, Kambi Rasmi ya upinzani bungeni  haioni muujiza wowote unaoeweza kutendeka ili watu hao wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria hata kama polisi wataongezewa miezi mingine miwili.

“Tafsiri ya ukimya huo wa serikali ni rahisi, kwamba hakuna dhamira ya dhati wala utayari wa kushughulikia jambo hilo. Hili la kuanza kutuwinda kwa lengo la kutuua, hatuwezi kamwe kulinyamazia,” alisema.

Alisema Kambi Rasmi ya Upinzani inatoa wito kwa wananchi wote kupaza sauti zao kupinga uonevu na ukandamizaji wa haki, kupinga matukio ya utekaji, utesaji na umwagaji wa damu katika nchi.

Tibaijuka Atangaza Kung'atuka Nafasi ya Ubunge

$
0
0
Tibaijuka Atangaza Kung'atuka Nafasi ya Ubunge
Mbunge wa Muleba Kusini kupitia CCM, Prof. Anna Tibaijuka, ametangaza kung’atuka nafasi ya ubunge kwa kutogombea tena kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020.

Mheshimiwa Tibaijuka alitangaza uamuzi huo walipokuwa wakizungumzia miaka miwili ya Rais John Pombe Magufuli tangu aingie madarakani ambaye alikuwa kwenye ziara mkoani Kagera.
Mama Tibaijuka amekuwa mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 2010, na alishawahi kukumbwa na kashfa kubwa ya pesa za Escrow.
Hivi karibuni Mbunge wa SIngida Kaskazini Lazaro Nyalandu pia ametangaja kujiuzulu ubunge wake na kuomba kujiunga na chama cha CHADEMA.




Sidhani Kama Nitakuwa na Mwanaume Hapa Tanzania- Chuchu Hansy

$
0
0
Sidhani Kama Nitakuwa na Mwanaume Hapa Tanzania- Chuchu Hansy
Muigizaji wa filamu bongo Chuchu Hansy ambaye pia ni mzazi mwenzake Vicent Kigosi (Ray) amesema iwapo akiachana na Ray hatokuwa na mwanaume wa Tanzania tena.

Chuchu Hany ameyasema hayo alipokuwa akipiga Story na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwamba iwapo ataachana na mwenza wake huyo, hatakuwa kwenye mahusiano tena na mtu yeyote hususan wa hapa Tanzania.
"Kuachana kupo kwa sababu kila kitu Mungu ndio anapanga, kwa hiyo mimi siwezi kushindana na Mungu, kama ikitokea itakuwa imefikia mwisho wetu, sidhani kama nitakuwa tena na mwanaume tena hapa Tanzania, sidhani, yaani sijui kama nitaingia kwenye mahusiano, nitakaa muda mrefu bila mahusiano", amesema Chuchu Hansy.
Pamoja na hayo muigizaji huyo amekanusha tetesi za kuachana na mzazi mwenzake Ray Kigosi, baada ya kuwa na tetesi kuwa wawili hao wameachana.

Bodi ya Ligi Yaipiga Faini Timu ya Simba

$
0
0
Bodi ya Ligi Yaipiga Faini Timu ya Simba
Bodi ya ligi nchini TPLB imetoa onyo kali kwa klabu ya Simba pamoja na kuipiga faini baada ya kubaini makosa kadhaa ambayo yalifanywa na klabu hiyo kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Njombe Mji.
Mkurugenzi mtendaji wa bodi hiyo Boniface Wambura amesema Simba imeonywa kwa kosa la kumsimamisha kwenye benchi la ufundi kocha wao msaidizi Masoud Juma raia wa Rwanda kwenye mchezo wao na Njombe Mji bila kuwa na vibali vya kufanya kazi nchini.
Mbali na onyo hilo klabu ya Simba imeadhibiwa kwa kupigwa faini ya Tsh. 300,000 kwa kosa la kuchelewesha kuwasilisha orodha ya majina ya wachezaji waliocheza mchezo wa siku hiyo. Wambura amesema Simba waliwasilisha majina saa 9:00 mchana ikiwa ni saa moja kabla ya mchezo kitu ambacho ni kinyume na kanuni.
Aidha Wambura amesema kikao cha bodi ya ligi bado kinaendelea kujadili mambo mbalimbali yanayohusu ligi kuu pamoja na ligi daraja la kwanza na daraja la pili ambapo baadhi ya dosari wamezipeleka kwenye kamati ya nidhamu kwaajili ya hatua zaidi.

Hoteli ya Blue Pearl Yafungwa kwa Kudaiwa Kodi ya Bilioni 5.7

$
0
0
Habari zilizotufikia ni kwamba Kampuni ya udalali ya Yono asubuhi ya leo November 9, 2017 imeifunga Hotel ya Blue Pearl iliyopo kwenye jengo la Ubungo Plaza eneo la Ubungo kutokana na mmiliki wake kudaiwa kodi ya pango Tshs bilioni 5.7.

Mpaka muda huu baadhi ya wageni waliokuwa wako hotelini hapo wameanza kutolewa kutokana na kufungwa kwa hoteli hiyo.

Inaelezwa pia kuwa magari zaidi ya 20 yanayomilikiwa na hoteli hiyo nayo yamefungwa kutokana na mmiliki kudaiwa kodi hiyo ya pango na tayari kampuni hiyo ya udalali imekwisha anza kufuta maandishi ya ‘Blue Pearl Hotel’ kwenye mlango wa kuingilia.

Mahakama Yamuongezea Kifungo Oscar Pistorius Hadi Miaka 15

$
0
0
Mahakama Yamuongezea Kifungo Oscar Pistorius Hadi Miaka 15
Serikali ya Afrika Kusini imeiomba Mahakama ya juu nchini humo kumwongezea kifungo mwanaridha mlemavu, Oscar Pistorius ‘Blade Runner’ aliyekutwa na hatia ya kumuua mpenzi wake, Reeva Steenkamp, Februari 2013.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Pretoria, Thokozile Masipa, alimhukumu Pistorius kifungo cha miaka sita baada ya kumtia hatiani kwa mauaji ya bila kukusudia, uamuzi ambao haujawaridhisha watu wengi.

Hivi karibuni, serikali hiyo kupitia Wakili, Andrea Johnson, ilirejea mahakamani na kuomba uamuzi wa Jaji Masipa ubatilishwe na mwanaridha huyo aliyejipatia umaarufu kwa kushiriki mbio akitumia miguu ya bandia kwa kuwa ni mlemavu, aongezewa muda zaidi wa kukaa jela.

“Jaji aliyeisikiliza kesi alikosa kabisa kuweka wazi sababu za kutotoa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka 15 (Kwa mujibu wa sheria za Afrika Kusini) alipomhukumu Oscar Pistorious kwa mauaji ya Reeva Steenkamp,” wakili huyo aliiambia mahakama hiyo ambayo bado inaisikiliza rufaa hiyo.

Trump na Xi Waanza Mazungumzo Baada ya Makaribisho ya Kifahari

$
0
0
Trump na Xi Waanza Mazungumzo Baada ya Makaribisho ya Kifahari
Rais wa Marekani Donald Trump ameanza mazungumzo na kiongozi wa China Xi Jinping mjini Beijing kufuatia makaribisho ya kkifahari katika mjihuo wa taifa hilo.
Bwana Trump anatarajiwa kuzungumzia kuhusu vile China inaweza kukabiliana na mipango ya kinyuklia ya Korea Kaskzini swala amblo litatawala ziara yake ya rasi ya Korea.
Marekani inaitaka China ,ambaye ni mshirika mkuu wa Pyongyang kuishinikiza zaidi lakini Beijing imesema kuwa imefanya ya kutosha.
Viongozi hao wa mataifa yenye uwezo mkubwa duniani pia wanatarajiwa kujadiliana kuhusu mapungufu yao ya kibiashara .

Mapema katika zaira hiyo ya mataifa matano, bwana Trump aliitaka Korea Kaskazini kuingia mkataba ili kumaliza mipango yake ya utengenezaji wa silaha za kinyuklia, huku pia akiionya dhidi ya uchokozi zaidi dhidi ya Marekani na dunia nzima , akisema ''musitujaribu''.
Pia ameitaka China kufutilia mbali ushirikiano wao na Pyongyang na kusisitiza wito wa Beijing kulishinikiza taifa hilo.
China imesema kuwa inafanya kila iwezalo na kusisitiza kuwa inatekeleza vikwa vya Umoja wa matiafa kwa ukamilifu.

Ndege Yatua kwa Dharura Baada ya Mke Kumfumania Mumewe

$
0
0
Ndege Yatua kwa Dharura Baada ya Mke Kumfumania Mumewe
Ndege ya Qatar Airways ambayo ilikuwa ikitokea Doha kuelekea Indonesia ililazimika kutua kwa dharura India usiku wa manane kufuatia abiria mmoja mwanamke kuanza kumpiga mumewe akimtuhumu kumsaliti baada ya kufungua simu ya mumewe huyo wakati amelala.

Unaambiwa simu ya mume huyo ilikuwa na password ya fingerprints ambapo mwanamke huyo alitumia kidole cha mumewe akiwa amelala na kuifungua simu na kugundua mumewe huwa anamsaliti.
Baada ya vurugu hizo kuendelea Ndege ilitua Chennai, India kwa dharura kisha wakaamriwa kuteremka na kuwekwa kizuizini katika Airport kabla ya kusafirishwa kuelekea Kuala Lumpur.

Viewing all 104698 articles
Browse latest View live


Latest Images