Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Atoa Siku Tatu kwa Waziri Kuwatimua Watoa Vibali kwa Waingizaji Sukari

0
0
Rais Magufuli Atoa Siku Tatu kwa Waziri Kuwatimua  Watoa Vibali kwa Waingizaji Sukari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amempa siku tatu Waziri wa Kilimo, Dkt. Tizeba kuwaondoa mara moja maafisa wote wanaotoa vibali kwa waingizaji wa sukari katika kitengo hicho.

Akizungumza na wananchi wa Missenyi mkoani Kagera alikotembelea kiwanda cha sukari Kagera, Rais Magufuli amesema watu hao wakapangiwe kazi nyingine tofauti na kutoa vibali.

“Kuna watu pale wizara ya kilimo kazi yao ni kutoa vibali tu, na nina fikiri wale uwafukuze wote tu there useless kazi zao ni kutoa vibali ndivyo wamekuwa wakiishi, vibali vya sukari bado wapo hao watu? Wale ukawatoe wahamishie kwingine ambako hawatoagi vibali kama kuna vibali vya chanjo za mbwa wakatoe huko, kila siku ni vibali na vibali ni vya fojari vya ajabu, wanapewa vibali watu wa ajabu hata wale ambao hajawahi kusafirisha hata sukari, alafu wakishapewa wanaenda kuuza vibali wanapewa wengine wanachama wa CCM wengine wa vyama vingine chukua hiki kibali nae anaenda kuuza kwa wale wana supply, na fikiri huo mtindo ni mbaya,” alisema Rais Magufuli.

“Waziri kawatoe wale wote wanaotoaga vibali pale wizarani kwako ndani ya siku 3 kawatoe wapangie kazi nyingine kama walisomea kutoa vibali mbona vipo vibali vingi kama vya kulima haiwezekani wamekaa pale there so specialized na wale ndio special wa kutoa rushwa kwahiyo waziri nakuachia hiyo kazi na wizara wa biashara kasimamie hilo waziri wa kilimo na nini kafanye hiyo kazi tunataka twende mbele mambo ya kudekezana haya na hawa watoa vibali hawawezi kufurahia wakiona vibali vinafanya kazi.”

Sibagui Msanii Hata Kama Hajui Kuimba Mimi Nitamuandikia tu- Barnaba

0
0
Sibagui Msanii Hata Kama Hajui Kuimba Mimi Nitamuandikia tu- Barnaba
Barnaba amedai kuwa hana kasumba ya kubagua wasanii wa kuwaandikia nyimbo. Ameiambia Dizzim Online kuwa kila msanii hata asiyejua kuimba anaweza kupata huduma yake.

“Mimi akija msanii hata kama hajui kuimba mimi nitamuandikia tu,” amesema. “Kwasababu ninachoamini  nyimbo nitakayomuandikia Maua ni tofauti na nitakayomuandikia Gigy Money na nyimbo nitakayomuandikia Vanessa ni tofauti na nitakayomuandikia Shilole. S najua uwezo wa kila msanii,” amesisisitiza.

Barnaba kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ya ‘Nampaga.

Makamu wa Rais wa Zimbabwe Aliyefutwa Kazi Atoroka

0
0
Makamu wa Rais wa Zimbabwe Aliyefutwa Kazi Atoroka
Aliyekuwa makamu wa rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ambaye alifutwa kazi siku ya Jumatatu amelitoroka taifa hilo kufuatia vitisho vya kifo , kulingana na washirika wake.
Rais Mugabe mwenye umri wa miaka 93 amemshtumu aliyekuwa makamu wake kwa kupanga njama za kuchukua mamlaka kutoka kwake.
''Alienda katika kanisa moja na Apostolic kujua ni lini Mugabe atafariki. Lakini aliambia kwamba atafariki wa kwanza'' , Mugabe aliwaambia wafuasi wake sikju ya Jumatano.

Bi Mugabe amekuwa akipigania kung'atuliwa kwa makamu huyo katika mkutano maalum wa chama tawala cha Zanu-PF mwezi Ujao.
Chama cha Zanu PF kilimfurusha Mnangagwa katika chama hicho siku ya Jumatano.

Bwana Mugabe alimtaja naibu wake wa zamani kuwa miongoni mwa waliopanga njama na akaonya kuwa atawachukulia hatua maafisa wengine wa chama hicho walioshirikiana na Mnangagwa.

''Tulimjua kitambo bwana Mnangagwa .Lakini hatukutaka kuwalezea. Alidhani kwamba kwa kuwa mwandani wangu nitambeba na kumpatia urais. Lakini sikufariki, na sikujiuzulu'', aliwaambaia wafuasi wake katika makao makuu ya chama cha Zanu PF mjini Harare.
''Tunatumai tutakabiliana na wengine ambao pia walikuwa na njama kama hiyo'' , aliongezea.

Askari Waliotembeza Kipigo Ukonga Washtakiwa Bungeni

0
0
Askari Waliotembeza Kipigo Ukonga Washtakiwa Bungeni
MBUNGE wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), ameliomba Bunge kuitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) cha Jeshi la Polisi wanaotuhumiwa kutembeza kichapo kwa siku mbili jimboni kwake mwishoni mwa mwezi uliopita.

Aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana alipoomba Mwongozo wa Kiti cha Spika akikiomba pia chombo hicho cha kutunga sheria kiitake serikali ifanye tathmini ya uharibifu wa mali za wananchi kutokana na tukio hilo ili iwafidie.

Akiwasilisha hoja yake hiyo, Waitara alidai kuwa Oktoba 24 askari wa FFU walifunga mitaa wa Mongo la Ndege, Mombasa, Mazizini na Gongo la Mboto na kuwapiga wananchi.

"Wakawapiga watu sana, wakavunjavunja meza za kinamama, wakapiga vijana wa bodaboda," alisema, hiyo haikutosha, Oktoba 25, wakaamkia tena kazi ileile, wanasimamisha magari kutoka hapo magereza, unashushwa unatembezwa kichurachura.

"Tunapozungumza kuna watu wamevunjika miguu, wameporwa fedha zao halafu wakachukua watu kama mia moja wakawasambaza vituo tofauti tofauti.

"Tumeuliza wale watu hawajulikani walipo. OCD anasema hajui, lakini mpaka leo (jana) hakuna kauli ya serikali."

Waitara alikiomba Kiti cha Spika kitoe mwongozo kuhusu suala hilo akidai kuwa kwa sasa hali ni tete jimboni kwake kutokana na uhasama uliopo kati ya wananchi na askari polisi.

"Askari waliokuwa wamepanga kwenye nyumba za wananchi, hapo nyuma walikuwa na mahusiano mazuri, lakini sasa kuna uhasama mkubwa kweli kweli," alisema.

Waitara aliongeza: "Mheshimiwa Mwenyekiti, unisaidie mambo mawili -- kwanza madhara yaliyotokea, tathmini ifanyike, waliopigwa, wakaporwa mali zao, mamalishe wale, wana vikoba wanadaiwa, nani anawafidia? Pili, Wizara yenye dhamana wamechukua hatua gani?"

Katika mwongozo wake, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu, aliyekuwa anaongoza kikao cha jana, aliitaka serikali kulifanyia kazi suala hilo na kumpatia majibu mbunge huyo.


SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Breaking News: Rais Magufuli Amtumbua Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (DED) Tunduru

0
0
Breaking News: Rais Magufuli Amtumbua Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (DED)
Rais John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (DED) ya Wilaya ya Tunduru, Abdallah Mussa kwa kushindwa kumudu majukumu yake.

Kutenguliwa kwa uteuzi wa mkurugenzi huyo leo Alhamisi Novemba 9,2017 kumefanyika siku tatu baada ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wa wakurugenzi wengine wawili.

     


Kutana na Mtaalam na Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Pumu, Vidonda vya Tumbo, Kisukari na Mengine Mengi

0
0
MTALAAM NA BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU NAYALIYOSHINDIKANA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI,MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni SUPER SAYI 3,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

SUPER SAYI 4 Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR ULIMWENGU ANAPATIKA DAR ES SALAAM MAGOMENI MOROCO

HUDUMA HIZI UTAZIPATA MAGOMENI

SIMU NO 0745387469, 0652121197

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Waziri Mkuu Afunguka Kuhusu Suala laTundu Lissu

0
0
Waziri Mkuu Afunguka Kuhusu Suala laTundu Lissu
Imeelezwa kuwa Serikali bado inaendelea na uchunguzi wa matukio kadhaa ya uhalifu yanayoendelea kutokea nchini ikiwemo shambulio lililofanywa dhidi ya Mbunge wa Singida mashariki, Tundu Lissu.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, wakati akijibu swali la kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Freeman Mbowe ambaye alihoji ni kwanini Serikali imekataa kutoa kibali cha wao kuleta wachunguzi wa kimataifa ili kufatilia matukio ambayo yamekuwa yakitokea nchini na kuhatarisha amani ikiwemo suala la Lissu
“Mheshimiwa Mbowe bado tuna imani na vyombo vya dola nchini, hivyo basi tuvipe muda ili wakamilishe upepelezi wa matukio hayo na mengine mengi nchini ili wakamilishe kazi yao kwa ufanisi”. Alisema Waziri Mkuu
Mbowe aliendelea kuhoji swali la nyongeza kuwa anaomba Waziri mkuu amueleze kuna ugumu gani kuruhusu uchunguzi kwa vyombo vya kimataifa na kudai kuwa si kwamba hana imani na vyombo vya ndani bali anahisi kuwa havina dhamira ya kuchunguza tukio hilo na upande wake ndio wenye maumivu.
Waziri mkuu amejibu kuwa hakuna aliyefurahishwa na tukio la mbunge Lissu kupigwa risasi, na kama Mbowe akitaka majibu zaidi ya hayo, asubiri ripoti ya vyombo vya dola kwani ndio vyenye jukumu hilo.
Aidha Waziri Mkuu ameongeza kuwa Amani ndio tunu ya Tanzania ni wajibu wa  kila mmoja kuhakikisha anailinda kwa manufaa ya wote hivyo basi uchunguzi huo hauwezi kuwa wa jana na leo Jeshi lipewe muda lije na taarifa yenye manufaa.


Mapya Yaibuka Ndoa ya Dogo Janja, Irene Uwoya Wema Ahusishwa

0
0
Mapya Yaibuka Ndoa ya Dogo Janja, Irene Uwoya Wema Ahusishwa
Nyuma ya sarakasi ya kile kinachosemekana ni ndoa kati ya staa wa Bongo Movies, Irene Pancras Uwoya na dogo wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ kuna mengi, Amani limeibuka na jipya.

DILI LA MIL. 400 LA WEMA
Ilifahamika kuwa, dili hilo lilikuwa liende kwa Wema Isaac Sepetu ambaye miezi kadhaa aliripotiwa na gazeti ndugu la hili, Ijumaa Wikienda kuwa alikuwa amelamba shilingi milioni 400 kwa ajili ya kuandaa tamthiliya hiyo.
Ilidaiwa kwamba, baada ya sakata la Uwoya na Dogo Janja likishika kasi ndipo kukaibuka ubuyu kwamba, dili hilo aliporwa Wema la sivyo ndiye angeolewa na Dogo Janja ndani ya tamthiliya hiyo.
“Wema alihakikishiwa kabisa kushikishwa shilingi milioni 400 na akaanza kufanya usaili wa mastaa zaidi ya hamsini atakaowatumia na kuwaahidi kuwalipa dau nono.
UWOYA ANUKA FEDHA
“Lakini ghafla ilidaiwa kwamba, Uwoya alifanya ‘umafia’ ndipo dili likahama kwa Wema na kutua mikononi mwake kisha kukamata huo mkwanja na sasa ananuka fedha maana zimemtembelea bidada.
“Ilikuwa rahisi kushinda tenda hiyo maana wakati Wema anataka ashikishwe shilingi milioni 400, yeye alidaiwa kukubali kufanya kazi hiyo kwa shilingi milioni 200 na ushee.
“Unaambiwa sasa hivi bifu la Uwoya na Wema linafukuta na ukizingatia kwamba huwa hawaivi chungu kimoja.
“Nakwambia inasubiriwa siku watakutana uso kwa uso watu waone itakuwaje maana hawajaonana tangu kutokea
kwa ishu hiyo.
“Unaambiwa Wema ana hasira maana tonge lilimponyoka mdomoni hivyo Team Wema wanamuomba Uwoya akae mbali nao,” kilimaliza kumwaga ubuyu chanzo na kulipisha Amani liwatafute wahusika.
MDHULUMIWA WEMA
Jitihada za kumpata Wema ziligonga mwamba baada ya simu yake kuita bila kupokelewa, lakini alipotafutwa Neema Ndepanya ambaye ni prodyuza na mwandishi wa miswada wa Wema alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli Wema alikuwa na dili kama hilo lakini siwezi kusema ndilo hilo unalolizungumzia (la Uwoya).”
UWOYA ASHTUKA
Alipotafuta Uwoya na kuulizwa juu ya kupora dili la Wema alishtuka na kudai kwamba, ndiyo kwanza anasikia ishu hiyo kutoka kwa mwandishi wetu.
“He! Ndiyo kwanza nasikia kutoka kwako (mwandishi) na sina maoni juu ya hilo maana sielewi chochote.”
Chanzo: Global Publishers

Baraka Da Prince Atupa Shutuma Kubwa kwa Meneja wa RockStar4000 Kuhusu Akaunti Yake ya You Tube

0
0
Baraka Da Prince Atupa Shutuma Kubwa kwa Meneja wa RockStar4000 Kuhusu Akaunti Yake ya You Tube
Baada ya kufungua account mpya ya YouTube na kupotea tena, msanii Barakah The Prince amedai kuwa wanaofanya mchezo huo ni Seven Mosha ambaye ni meneja RockStar4000 pamoja na mfanyakazi wa Mx Carter ambaye hakutaka kumtaja jina.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Sometimes’ ameiambia E-Newz ya EATV kuwa watu hao wawili ndio anawashuku kufanya hivyo kwani wao ndio walikuwa na password za account zote mbili.

“Nilijaribu kutengeneza channel mpya ya YouTube achana na ile mwanzo iliyokuwa na matatizo na watu wa Rockstar4000 walikuwa wanaing’ang’ania. Kwa hiyo baada ya ku-upload video kuna jamaa moja hivi mfanyakazi ya Mx Carter akaniomba password zangu za YouTube kwa maana kuna kitu walikuwa wanataka kunisaidia baada ya hapo tukio likawa linajirudia ni lilelile” amesema Barakah.

“Kwa hiyo inavyooneka hapa hapa kati ya watu wa Mx Carter na Seven wanaofanya huo mchezo moja kwa moja nawalenga wao kwa sababu hamna mtu yeyote alikuwa na access zangu za YouTube za mwanzo mpaka za pili tofauti na wao” amesisitiza.

Pia ameongeza kuwa suala hiyo tayari limeshafunguliwa kesi mahakamani. Barakah aliwahi kuwa chini ya usimamizi wa RockStar4000 na baadae kujitoa.


Mwasiti Afunguka Kinachomfanya Kuwa Kimya Katika Game

0
0
Mwasiti Afunguka Kinachomfanya Kuwa Kimya Katika Game
Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Mwasiti ameeleza sababu za ukimya wake katika game kwa kueleza kuwa yupo katika utaratibu wa kukamilisha albamu.
Endapo muimbaji huyo wa ngoma ‘Kaa Nao atafanikiwa kuitoa kwa mwaka huu ataungana na wasanii kama Lady Jaydee, Chege, Ben Pol na Navy Kenzo ambao wameshakwisha kufanya hivyo.

“Nakumbuka last time nilitoa Kaa Nao, nimekaa kimya kidogo lakini nafikiri kimya changu watu huwa wanakiulizia na watu watengemee kazi nzuri kwa sababu najipanga kumalizia albamu pengine nafikiri inanibana sana nakuwa nawaza vitu viwili kwa wakati mmoja” amesema Mwasiti.

“Lakini watu watengemee kazi nzuri kama siyo December nafikiri January mwanzoni na watafurahi kiukweli” ameongeza.

Si Mwasiti pekee yake aliyezungumzia suala la albamu kwa mwaka huu, kuna Fid Q, Izzo Bizness, Diamond, Roma na Stamina (Rostam), Wakazi na wengineo

Yanga Yawakuta ya Simba Yapigwa Faini na Kamati ya Uendeshaji Ligi Kuu

0
0
Yanga Yawakuta ya Simba Yapigwa Faini na Kamati ya Uendeshaji Ligi Kuu
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara imeipiga faini ya sh. 500,000 (laki tano) mabingwa watetezi klabu ya Yanga baada ya kitendo cha mashabiki wake kurusha uwanjani chupa zinazosadikiwa kuwa na mikojo katika mchezo wao dhidi ya watani zao wa jadi Simba SC.

Kamati hiyo imeikuta klabu ya Yanga na hatia baada ya kupitia ripoti za michezo yote ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL).

Yanga SC inakabiliwa na hadhabu hiyo kwa mujibu wa kanuni ya 42(1) kuhusu udhibiti wa klabu.

Katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara namba 58, mabingwa watetezi klabu ya Yanga ilishuka dimbani Oktoba 28 kukabiliana na Simba SC Uwanja wa Uhuru.

Katika mchezo huo wa watani wa jadi uliamuliwa kwa sare ya1-1, wakati Simba SC ikiwa ya kwanza kujipatia goli kupitia kwa Shiza Ramadhani Kichuya huku wenyeji Yanga wakisawazisha  bao hilo kupitia Obrey Chirwa.

Albamu ya 'A Boy From Tandale' ya Diamondi Kuachiwa Desemba Mwaka Huu

0
0
Albamu ya 'A Boy From Tandale' ya Diamondi Kuachiwa Desemba Mwaka Huu
A Boy From Tandale inatoka Disemba 1 ya mwaka huu? Basi unaweza kukaa mkao wa kula kwa ajili ya kuisubiri albamu hiyo kutoka kwa Diamond Platnumz.
Japo msanii huyo kutoka WCB ameonekana kufanya siri kwenye hilo, lakini Dj na mtangazaji wa The Beat1036 FM, Ellie Prohan ameonekana kupenyezewa taarifa hizo na Diamond mwenyewe.
Kupitia mtandao wa Instagram, mrembo huyo ameweka picha akiwa na msanii huyo wakati alipotembelea katika kituo hicho cha radio na kuandika ujumbe unaosomeka, “When the Persian Power Met The POWER HOUSE @diamondplatnumz 🔥🔥 #blessed #hallelujah @thebeat1036fm 💥 BIGGGGGG BANGER DROPPING 1st Dec #ABoyFromTandale #Hero !!! 😱😱.”

Taarifa hizo zinaweza zikawa na ukweli ndani yake kwa kuwa hit maker huyo wa Hallelujah aliwahi kuahidi kuachia albamu yake ndani ya mwaka huu na itawakutanisha wasanii wakubwa duniani.

UN Yaonya Hali Mbaya ya Binadamu Yemen

0
0
UN Yaonya Hali Mbaya ya Binadamu Yemen
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeuambia Muungano wa Jeshi linaloongozwa na Saudi Arabia nchini Yemen ni lazima kuruhusu misaada ya kibinadamu kupelekwa tena nchini humo.
Muungano huo wa jeshi umefunga njia zote za ardhini, anga na za maji tangu siku ya Jumatatu,kufuatia mashambulio ya makombora yaliyorushwa katika mji wa Riyadh na waasi wa Houthi walioko Yemen.
Baada ya mkutano wake wa ndani Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeagiza kuondolewa kwa vizuizi hivyo kwa kusema kwamba hali ya kibinadamu ni ya kutisha.

Mkuu wa shirika la misaada la Umoja wa Mataifa Mark Lowcock ameonya kutokea kwa kubwa la njaa, iwapo misaada haitapelekwa Yemen.
Hata hivyo Muungano huo wa Jeshi umedai kuwa vizuizi vinahitajika kuweza kuizuia Iran kuwapatia silaha waasi wa Ki-Houthi.

Uongozi Ubungo Plaza Limitedi Wafunguka Kuhusu Kufungiwa kwa Hotel ya Brue Pearl

0
0
Uongozi Ubungo Plaza Limitedi Wafunguka Kuhusu Kufungiwa kwa Hotel ya Brue Pearl
Uongozi wa Ubungo Plaza Limited umesema mpangaji wake, hoteli ya Blue Pearl alikoma kulipa kodi ya pango tangu Mei, 2014.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 9,2017, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Ubungo Plaza, Harun Mgude amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kushinda kesi Mahakama ya Ardhi.

"Blue Pearl amekuwa mpangaji wetu tangu mwaka 2006 na mkataba wake ulikuwa wa miaka 15 ambao ungeisha 2021. Alikuwa akilipa vizuri lakini tangu Mei 2014 aliacha kulipa," amesema Mgude.

Amesema kutokana hilo walikwenda kufungua kesi Mahakama ya Ardhi na Blue Pearl wameshindwa, hivyo kutakiwa kulipa au kutoka ndani ya jengo.

"Kama mnakumbuka tuliwahi kumtoa na akarudi kwa amri ya Mahakama ili kupisha kesi kuendelea, lakini Novemba 3,2017 kesi iliisha na ameshindwa na kutakiwa kulipa deni la Sh5.7 bilioni," amesema.

Amesema uongozi wa Blue Pearl umeomba kufanya kikao Jumatatu Novemba 13,2017 ili kujadili jinsi ya kulipa deni hilo.

"Baadhi ya wateja wamehamishiwa hoteli nyingine sijui ni wapi. Ila ieleweke kuwa robo tatu ya mali zilizokuwamo Blue Pearl ni za Ubungo Plaza Limited kama vile fenicha na vitu vingine," amesema Mgude.

Uongozi wa hoteli hiyo ulikuwa ukishughulikia kuwahamisha wateja na haukuwa tayari kuzungumzia suala hilo.


Familia ya Tundu Lissu Yataka Bunge Kutokwepa Majukumu Yake ya Matibabu ya Ndugu Yao

0
0
Familia ya Tundu Lissu Yataka Bunge Kutokwepa Matibabu ya Ndugu Yao
Familia ya mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu imeibuka kwa mara nyingine ikiliomba Bunge kutokukwepa wajibu wa kugharimia matibabu ya ndugu yao kwa kuwa si hisani bali ni stahiki anazopaswa kupewa.

Pia, familia hiyo imesisitiza wito wake kwa Serikali wa kuruhusu uchunguzi kutoka nje ili ukweli ujulikane kuhusu waliohusika kumjeruhi kwa risasi Lissu Septemba 7, mjini Dodoma.

Imesema haiwezekani miezi miwili imepita tangu aliposhambuliwa lakini hakuna taarifa za kukamatwa kwa mtu yeyote.

Vincent Mughwai, ambaye ni mdogo wa Lissu alisema hayo jana katika ofisi za Mwananchi, Tabata- Relini jijini Dar es Salaam.

Kwa mwezi wa pili sasa Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya.

“Miezi miwili imepita gharama za matibabu ziko juu na ni wananchi wa Tanzania ndiyo wamezilipa. Mshangao wetu ni kuwa, Lissu ni mbunge na kama kiongozi ana haki ya kutibiwa na si kubaguliwa,” alisema Mughwai.

Alisema, “Lissu ana bima, bado hajaweza kupata msaada na sisi tunasema kulikoni, kama viongozi wengine wakiugua gharama zao zinalipwa na Bunge, huyu pia ni mbunge kwa nini kunakuwa na double standard kwa ndugu yetu.”

Mughwai alisema kikao walichokaa na uongozi wa Bunge, Oktoba 2 kujadili matibabu kilikwenda vizuri na wao kama familia walieleza kutokuwa na pingamizi la ndugu yao kugharamiwa lakini tangu siku hiyo mpaka sasa hakuna taarifa zozote kutoka kwa Bunge.

“Familia hatujajulishwa ingawa tuliandika si barua bali ujumbe kwamba familia haina tatizo Bunge kulipa gharama za matibabu ya Lissu lakini kimya, Bunge wanajua huyu mgonjwa anaishije huko? Tunaomba apate stahiki zake kama anavyostahili,” alisema.

Kauli hiyo ililifanya Mwananchi kumtafuta Spika wa Bunge, Job Ndugai lakini hakuweza kupatikana huku Katibu wa Bunge, Stephen Kigaigai akisema ‘’mimi sijui na sijapata taarifa kuhusu suala hilo kwani mazungumzo yalipofanyika mimi sikuwapo.”

Mdogo huyo wa Lissu alisema ‘’sisi tunaendelea kuwashukuru Watanzania kwa kujitoa, Chadema kikiongozwa na Mbowe (Freeman Mbowe-Mwenyekiti wa Chadema) ambao mpaka sasa wapo Nairobi, hatuna cha kuwalipa, tunaomba muendelee kumwombea na kutoa michango kupitia akauti za Chadema ili ndugu yetu aweze kupona.”

Kuhusu uchunguzi, Vicent alisema, “Tunaendelea kusisitiza Serikali iruhusu uchunguzi kutoka nje, waje washirikiane na jeshi letu la polisi, huu uvumi kwamba anayehusika ni fulani utamalizika, kama ni Chadema wamehusika watajukikana, kama ni nani watajulikanani hofu iko wapi,” alihoji Vicent

Alitolea mfano, Meja Jenerali mstaafu Vicent Mribata aliyepigwa risasi maeneo ya Ununio- Tegeta jijini humo kuna watuhumiwa walikamatwa lakini tukio la Lissu mpaka sasa hakun taarifa zaidi ya magari kumi aina ya Nissan kukamatwa nayo haijulikani yalipo.

Hata hivyo, Jeshi la Polisi limekuwa likieleza kwamba uchunguzi wa suala hilo unaendelea na hauwezi kuwekwa hadharani kila hatua na mara baada ya kukamilika wataueleza umma.


Badili Mwonekano wake na Kuweka Mwili Safi Kwa Kutumia Kessy Products

0
0

*PENDEZA NA KESSY PTODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA* 🍇🌾🌳
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATAKS)KUNADAWA AINA TATU (@)JELI KUPAK_100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI NA MAPAJAN_80,000/
5)TOA KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE NA MANYAM YOTE
@) DAW YA MAJINI_100,000/NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME BILA KUVAA SIDIRIA_80,000/
8)KUONGEZA MAZIWA NA SAIZI NZURI_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA (kifaru)_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO YAKAWAIDA NA UZAZ_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_70,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA KWA DAW(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWLINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA JELI PAMOJA NA VIDONGE VYAAIN ZOT _100'000
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_ 120,000 /
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_80,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _80,000/
20)ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA MGUU_80,000/🍍🍉🌾 *TUNAPATIKAN DAR E SALAAM* *NAKWA *MIKOANKOTE* UTAPATA *PIA* *NA NCHI ZOTE PIGA CM* (+255)0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product*
*Delivery POPOTE ULIPO,*

Mh. Mbowe ambana Waziri Mkuu tukio la kushambuliwa kwa Mh. Lissu

0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema matukio yanayoendea nchini yakiwemo yale ya Mkuranga, Kibiti na kupigwa risasi kwa mbunge wa singida Mashariki, Tundu Lissu ni matukio ambayo vyombo vya dola vinaendelea kufanya uchunguzi huku akieleza na uchunguzi huo hauwezi kufanyika kwa siku moja kwasababu wanaotenda matendo hayo wanatumia mbinu nyingi za kujificha hivyo vyombo hivyo vinatakiwa kutumia mbinu za kuwatambua waliotenda.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma katika Mkutano wa 9 kikao cha 3 kinachoendelea baada ya Mbunge wa Kambi rasmi bungeni, Freeman Aikaeli Mbowe kuhoji serikali inachukuwa hatua gani kwa matukio yanayoendelea nchini likiwemo la Mbunge huyo na kupotea kwa msaidizi wake Ben Saanane.

“Nataka nieleze kwamba amani yetu utulivu ndani nchi ni jambo ambalo Watanzania wote tunatakiwa tushikamane katika kulidumisha, ndilo ambalo linaendelea zidi kutupa heshima duniani kwasababu Watanzania wote tunashirikiana katika hili, yapo matukio yanayojitokeza Mh. Mbowe umezungumzia kwa upande wa siasa matukio haya yapo kwa ujumla wake nchini kwenye maeneo kadhaa kwenye ngazi ya familia lakini pia na maeneo mbalimbali ya mkusanyiko na watu pia wengine wako watu ambao hawana nia njema nchini wanajitokeza katika kutenda matendo hayo, na hata hili unalolisema la Mh. Tundu Lissu sio Mh Tundu Lissu pekee ingawa hatupendi mambo kama haya yatokee lakini pia tumepoteza Watanzania wengi unakumbuka wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji tumepoteza watu wengi lakini pia hivi karibuni Kamanda wetu wa Jeshi la ulinzi nchini JWTZ nae alipigwa risasi pia kwa hiyo tuyazungumze haya kwa ujumla wake na tunapoyazungumza haya kwa utamaduni tulioujenga wa nchi hii katika kujilinda wenyewe kuhakikisha nchi hii inaendelea kuwa salama nataka nikuhakikishie kwamba vyombo vyetu vya dola vinaendelea kufanya uchunguzi wa haya na uchunguzi huu hauwezi leoleo ukapata ufunguzi kwasababu wanaotenda matendo haya wanatumia mbinu nyingi kujificha na sisi lazima tutumie mbinu za kutambua hao waliotenda matendo hayo katika kila eneo ili baadae tuweze kutoa taarifa ya jibu,” amesema Majaliwa.

“Nataka nikuhakikishie kuwa vyombo vya dola haviko kimya vinaendelea, nataka nikuhakikishie vilevile vyombo vya dola vina uwezo wa kusimamia usalama ndani ya nchi, ni suala la muda na ni muda gani wana kamilisha utaratibu hatua gani zichukuliwe sasa hilo linategemea na waliotenda matukio na ni namna gani wamejificha, na sisi tunatumia njia mbalimbali kuweza kuyapata haya na kuweza kujua na kutoa taarifa kwa Watanzania nataka nikusihi na familia zote ambazo zimepata athari ambao wameripoti polisi na vyombo vya dola vinaendelea kwamba pale tutakapo kamilisha uchunguzi tutatoa taarifa kwa ngazi za familia ambazo zimepata athari au ndugu, jamaa waliopata athari hiyo na kuwaambia hatua ambayo sisi tunachukua ,” ameongeza Waziri Majaliwa.

Breaking News: Aliyenunua Nyumba ya Lugumi Akamatwa na Polisi

0
0
Nyumba mbili za aliyekuwa mmiliki wa Kampuni ya Lugumi Enterprises, Said Lugumi, zilizopo maeneo ya Mbweni- JKT zimepigwa mnada leo, Alhamisi, Novemba 9, 2017.
Katika mnada huo ulioanza majira ya saa 5 za asubuhi na kudumu kwa dakika tano kwa kila nyumba, Dk Louis Shika ndiye aliyenunua nyumba hizo zenye kila kitu ndani huku zikiwa umbali wa takribani mita100 kutoka moja hadi nyingine.

Hata hivyo baada ya mnada huo, Dk Louis aliyeuziwa kwa shilingi milioni 900 na nyingine bilioni 1.1, alidakwa na polisi kwa madai ya kuharibu mnada baada ya kushindwa kutoa asilimia 25 ya fedha inayohitajika.
Mnada huo umeendeshwa na kampuni ya udalali ya Yono, baada ya mnada wa mara ya kwanza uliofanyika Septemba 7, 2017 kukwama kutokana na wateja waliojitokeza kutofikia bei iliyohitajika.
Akizungumza na Gazeti la Ijumaa, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yono, Scholastica Kevela alisema lengo la mnada ni kufidia Sh14 bilioni ambazo mfanyabiashara Lugumi anadaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Nyumba hizo mbili ni kati ya tatu ambazo zitapigwa mnada. Nyingine ikiwemo nyumba iliyopo Upanga,  jijini hapa.

Aliyenunua Nyumba za Lugumi Kwa Tsh. 1.9 Bilioni. Dk. Shika Agundulika Kuwa ni 'Tapeli'

0
0
Taarifa kutoka YONO zinasema mnada wa nyumba ya Lugumi iliyopo Upanga unarudiwa na kudai kuwa Dkt. Louis Shika aliyenunua nyumba hiyo na mbili zilizopo Mbweni ni ‘TAPELI’.


Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images