Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Nyaya za umeme zenye thamani ya sh. milioni 70.7 zakamatwa

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, tarehe 07  Novemba maeneo ya Tegeta IPTL lilifanikiwa kukamata gari lenye namba za usajili T. 897 ARF aina ya Fusso likiwa limebeba nyaya za umeme Roller/Drum 05 zikiwa ndani ya gari hilo zenye thamani ya Tsh Milioni 70.7.

Dereva wa gari hilo aliwaelekeza askari watuhumiwa wenzake na baada ya upekuzi zilikamatwa Roller/drum 02, mashine ya kupaka, rangi na makopo matatu (3)matupu ya rangi yaliyotumika kubadilisha uhalisia wa Roller/drum, zote zilikutwa kwa mtu aitwaye Zawako Kasiba na mke wake, mkazi wa IPTL Tegeta na watuhumiwa wengine wanne.

Aidha watuhumiwa wote wamekamatwa na mawasiliano yalifanyika na Shirika la umeme (TANESCO) na walipofika kuzitambua nyaya hizo na kugundua kuwa ni mali za Shirika ambazo ni DRUM 07 zikiwa na mita 21,000 zenye thamani ya sh. Milioni 70.7

Jumla ya watuhumiwa sita wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo akiwemo mwanamke mmoja. Watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa ili kubaini mtandao mzima wa watu wanaotuhumiwa kuhujumu miundo mbinu ya TANESCO.

RC Mongella apanga kutatua kero za ardhi kila mwezi

$
0
0
Mwanza. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella ametenga siku moja kila mwezi kwa ajili ya ziara za kikazi katika wilaya zote saba mkoani hapa kusikiliza na kutatua kero za migogoro ya ardhi zinazowakabili wananchi.

Mongella alisema jana kuwa ziara hizo zitaanza Novemba 20, katika wilaya za Ilemela na Nyamagana.

“Nitaanza na jiji la Mwanza ambalo ni kinara kwa kuwa idadi kubwa ya migogoro ya ardhi ambayo hutokana na utendaji mbovu wa baadhi ya maofisa wa idara ya ardhi,” alisema Mongella.

Alisema mwaka jana 2016, jiji hilo linaloundwa na Manispaa za Ilemela na Nyamagana lilikuwa na migogoro ya ardhi zaidi ya 1, 040 iliripotiwa.

Lamar Awatolea Mfano Diamond na Alikiba katika jambo hili

$
0
0
Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakisema muziki wa Bongo Flava umekosa utambulisho ukilinganisha na ule wa Nigeria, sasa Bongo5 tumemtafuta Producer Lamar kuzungumzia suala hilo.

Producer huyo kutoka studio za Fish Crab amesema si sawa kusema muziki wa Bongo hauna utambulisho na kila msanii ana kitu chake ambacho kinatambulisha kuwa muziki husika unatoka Bongo.

“Kwanza huyo anayesema muziki hauna utambulisho hathamini cha nyumbani kwa sababu muziki wetu una utambulisho, unajua kila muziki una utambulisho wake ila unajaribu kuchukua vitu fulani kutoka sehemu fulani kuleta ladha tofauti, so ukisema muziki wetu hauna utambulisho unakosea sana” amesema.

“Kina Diamond wana identity zao, kina Alikiba na wasanii wote wanaofanya hip hop, Bongo Flava wana utambulisho wao, unajua kabisa huu muziki unatoka Bongo” ameongeza.

Lamar ameshafanya kazi na Diamond katika ngoma ‘Moyo Wangu’ na Alikiba kupitia ngoma ‘My Everything’.

Sugu amchana Ndalichako, anamaliza miti kwa kujaza karatasi na kuleta ujangwa

$
0
0
Mbunge wa Mbeya mheshimiwa Joseph Mbilinyi alimtolea uvivu waziri wa elimu prof Ndalichako kufuatia ripoti yake aliyoitoa kuhusu mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu hapa nchini

Sugu amesema taarifa ya Ndalichako imejaza karatasi nyingi pasi na point ya msingi ya kutatua tatizo sugu la mikopo, hivyo anatumia karatasi nyingi na kusababisha matumizi holela ya miti inayotumika kutengeneza karatasi

Ameongeza, Ndalichako anasababisha ujangwa kwani anaongeza matumizi ya karatasi kwa kuandika na kujaza vitu viso maana

JE, Unasumbuliwa na Upungufu wa Nguvu, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE, UNASUMBULIWA NA UPUNGUVU WA NGUVU, HAMU YA TENDO LA NDOA AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?
      SOMA HAPA
    Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.

      BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
     Kwa kutumia mimea na matunda🍅🍍🍓🌿🍉🍒🍎 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=
      BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA

    KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
      @markson_beauty_pr

Mawasiliano (+255)
           0767447444 na
              0714335378

        UTAPATA HUDUMA
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Ajali Mbaya ya Basi na Gari Dogo Yaua Wawili......

$
0
0
Watu wawili wamefariki dunia wilayani Ikungi, Singida baada ya gari dogo kugongana na basi la abiria. Polisi wamesema kuna kila dalili kuwa dereva wa gari dogo alikuwa amelala.

Diamond Ataja Kilichomsukuma Kuingia Kwenye Muziki

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo Fleva mwenye mafanikio makubwa nchini Tanzania, Naseeb Abdul, maarufu kwa jina la kisanii ‘Diamond Platinumz’ ameeleza kuwa licha ya kuupenda muziki, ari ya kutaka kuuonyesha umma kwamba muziki unaweza kuwa msaada kwa jamii ndiyo sababu iliyomsukuma kuingia katika tasnia hiyo.

Diamond ameyaeleza hayo alipokuwa akifanya mahojiano na mtangazaji, Salim Kikeke, wa kituo cha kurusha matangazo cha Uingereza, BBC ambapo ameeleza kuwa lengo lake ni kutaka kuwafumbua akili vijana kuwa muziki unaweza kutumika kutengeneza fursa mbalimbali pamoja na kuwa chanzo cha mapato.

“Napenda kuutumia muziki kwa njia nzuri, kuwaonyesha vijana wenzangu kama unaweza kuwa mwanamuziki na ukautumia katika misingi bora ukatengeneza ajira, ukatengeneza kitu ambacho kitakusaidia hata utakaposhindwa muziki,” alisema Diamond.

Vilevile Diamond alieleza kuwa yuko mbioni kuachia albam yake mpya ambayo amewashirikisha wasanii kutoka nchi mbalimbali duniani huku akitaja wimbo mpya wenye jina ‘Waka’ aliomshirikisha msanii kutoka nchini Marekani ‘Rick Ross’ ma kusema kuwa utatoka Disemba mosi, mwaka huu.

Mbali na muziki, Diamond ameeleza kuwa anajihusisha na biashara nyingine ili aweze kujiingizia kipato na kuendesha maisha yake. Biashara alizozitaja ni pamoja na ‘Diamond Karanga’ na ‘Chibu Perfume’ ambazo zimejipatia umaarufu mkubwa sana hapa nchini.

Taarifa ya Mamlaka ya Chakula Kuhusu Usalama wa Matumizi ya Maziwa ya Nido

$
0
0
Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) ni Wakala wa Serikali chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambayo imeundwa chini ya Sheria ya Dawa, Chakula na Vipodozi sura 219.

TFDA imebaini uwepo wa taarifa inayosambazwa katika mitandao ya kijamii kwa lengo la kuogofya wananchi juu ya usalama wa maziwa ya Nido. Taarifa hiyo ina picha ya kopo la maziwa ya Nido na Inasema kuwa katika maziwa hayo kumewekwa vionge vya kulewesha.

Mamlaka inapenda kuutaarifu umma kuwa uchaguzi wa awali umeonyesha kuwa taarifa hii kwa sasa haina ukweli wowote.

TFDA kupitia mifumo yake ya ufuatiliaji wa usalama wa bidhaa katika soko inaendelea kufuatilia bidhaa hii ikiwa ni pamoja na taarifa zinaazosambazwa.

Rai yetu kwa wananchi ni kuacha kusambaza taarifa zozote zinazohusu usalama, ubora na ufanisi wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendanishi bila kupata ufafanuzi na uthibitisho kutoka TFDA.

Imetolewa na;

Mkurgenzi Mkuu,

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA),

Barabara ya Mandele- Mabibo External,

S.L.P 77150, Dar es Salaam.

Kutana na Mtaalam na Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Pumu, Vidonda vya Tumbo, Kisukari na Mengine Mengi

$
0
0
MTALAAM NA BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU NAYALIYOSHINDIKANA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI,MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni SUPER SAYI 3,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

SUPER SAYI 4 Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR ULIMWENGU ANAPATIKA DAR ES SALAAM MAGOMENI MOROCO

HUDUMA HIZI UTAZIPATA MAGOMENI

SIMU NO 0745387469, 0652121197

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.


TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Press Play:




Godbless Lema Amshauri Spika Ndugai Kuhusu Wabunge

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amemshauri Spika wa Bunge la Tanzania Mh. Job Ndugai kutumia busara kuwaondoa bungeni wabunge nane walioingia Bungeni kuziba nafasi za wabunge nane waliokuwa wamevuliwa uanachama wa chama cha CUF Julai 24.

Lema aetumia nafasi yake kuandika ujumbe huo ikiwa ni siku moja baada ya Mahakama Kuu kutengua kufukuzwa kwa Wabunge 8 na Madiwani 2 wa Chama cha Wananch CUF mpaka pale shauri la msingi litakaposikilizwa.

Lema kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika   "Mh Spika anapaswa, kuzingatia kwa busara uamuzi uliotolewa na mahakama kwa kuwaondoa wale Wabunge wa Lipumba ndani ya Bunge na kuwarejesha Wabunge halali sasa . Mpaka hapo haki itakaposhinda zaidi"

Wabunge hao nane walivuliwa uanachama Julai 24 Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi, CUF linaloongozwa na Profesa Lipumba  kwa madai ya utovu wa nidhamu, yakiwemo kukisaliti chama hicho.



TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Press Play:

Rais Magufuli Na Museveni Walaani Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) Kuanza Kuichunguza Burundi

$
0
0
Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni ametoa tamko la kulaani uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) ambayo imemuagiza mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo kuanzisha uchunguzi dhidi ya mgogoro wa Burundi.

Rais Museveni ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki amesema ICC inaingilia mambo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki bila kuwahusisha viongozi wa Jumuiya hiyo jambo ambalo sio sahihi na linarudisha nyuma juhudi za kutafuta amani ya Burundi.

Rais Museven amezungumza hayo kabla ya kuagana na Rais Magufuli ambaye jana amemaliza ziara rasmi ya kiserikali ya siku 3 nchini Uganda na kurejea nchini Tanzania.

Akizungumzia uamuzi huo wa ICC Mh. Magufuli amesema hatua hiyo inarudisha nyuma hatua zilizochukuliwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo iliunda Kamati ya usuluhishi wa mgogoro wa Burundi inayoongozwa na Mhe. Rais Museveni na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa.

Rais Magufuli aliagana na Rais Museveni katika Mji wa Masaka na baadaye kusindikizwa na Makamu wa Rais wa Uganda Mhe. Edward Kiwanuka Sekandi hadi Mutukula, mpakani mwa Tanzania na Uganda.

TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Press Play:

TAWA, Polisi wakamata jangili, meno ya Tembo

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro kwa kushirikiana na Maafisa wa Uhifadhi wa Wanyamapori wamefanikiwa kumkamata jangili akiwa na meno ya Tembo 5 yenye thamani ya MIL 100 na mshitakiwa yuko kituo cha Polisi morogoro.

Taarifa kutoka kwa jeshi la Polisi morogoro mshtakiwa anategemea kufikishwa mahakamani. Aidha, Afisa Habari wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania – TAWA Bw. Twaha Twaibu ameeleza kuwa walipata taarifa kutoka kwa raia wema juu ya kuwepo kwa jangili huyo wa meno na kutuma maafisa wanyamapori kutoka Makao Makuu ya TAWA wakishirikiana na jeshi la Polisi na kuweza kumkamata jangili huyo.

Nae Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Ulrich Matei akiongelea tukio hilo, amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo aliejulikana kwa jina la Nehemiah Nashon akiwa katika chumba namba 104 cha Hoteli ya BZ iliyopo maeneo ya Nane-nane Mjini Morogoro, na kwamba vipande hivyo vina thamani ya zaidi ya shilingi Mil. 100.

TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Press Play:

Majina ya Wanasoka 5 Wanaowania tuzo ya Mwanasoka bora Afrika(BBC) Yawekwa Hadharani

$
0
0
Jopo la wataalamu wa soka wakiongozwa na mkongwe wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria Emmanuel Emunike wamekaa chini na kujadili majina ya wachezaji watano wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika msimu huu.

1.Naby Keita. Amekuwa gumzo kubwa katika ligi ya Ujerumani Bundesliga kutokana na kiwango alichokionesha akiwa na Rb Leizpg na msimu huu alikuwepo katika kikosi cha Bundesliga. Keita pia anahusishwa na kujiunga na Liverpool.

2.Sadio Mane. Alikuwepo katika kikosi cha Epl cha waandishi wa habari za michezo, alichaguliwa mchezaji bora wa klabu ya Liverpool msimu uliopita huku pia hapo jana akiisaidia Senegal kufuzu kwa fainali za kombe la dunia.

3.Pierre Aubameyang. Msimu uliopita alifanya makubwa Ujerumani akifunga mabao 35 na kuweka rekodi kuwa mchezaji wa 4 kuwahi kufunga mabao 30 nchini Ujerumani huku akiwa Muafrika wa kwanza kufikisha mabao hayo katika Bundesliga.

4.Mo Salah. Ameiwezesha Misri kushiriki michuano ya kombe la dunia lakini msimu uliopita alikuwa na kiwango kizuri sana alipokuwa Fiorentina huku msimu huu akiwa amefunga mabao 7 katika ligi ya Epl.

5.Victor Moses. Kama ilivyo kwa Salah na Mane huyu naye tayari timu yake imefuzu kuelekea Urusi, Victor Moses tangu kocha Antonio Conte ajiunge na Chelsea amekuwa akimpa sana nafasi japokuwa msimu huu ameandamwa na majeraha yanayomuweka nje hadi sasa. Jopo la wataalamu wa soka wakiongozwa na mkongwe wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria Emmanuel Emunike wamekaa chini na kujadili majina ya wachezaji watano wanaowania tuzo ya mchezaji bora Afrika msimu huu.

TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Press Play:

Aliyetaka Kununua Nyumba za Lugumi Anaishi Nyumba ya Kupanga Chumba Kimoja

$
0
0
Dr. Luis Shika aliyetaka kununua nyumba za Lugumi anaishi katika nyumba ya kupanga ambapo amepanga chumba kimoja na anadaiwa malimbikizo ya kodi

Kutana na Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed Kutoka Bagamoyo...Ana Dawa za Kurudisha Mapenzi na Zingine Nyingi

$
0
0

MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

USHAURI: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.

Haya Hapa Mambo Yaliyotikisa siku Nne za Bunge

$
0
0
Mambo yaliyotikisa siku nne za Bunge;

1. Uwanja wa Ndege Chato
2. Kupaa deni la Taifa
3. Sekta Binafsi
4. Wabunge wa Zanzibar
5. Kushambuliwa kwa Lissu
6. Hoja ya Mbowe

TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Press Play:

Uhuru Kenyatta Ajitapa "We Are a True Democracy"

$
0
0
Rais Kenyata amesema

"kama sio kukomaa kwa democrasia Kenya, nisingelikuwa hapa sasa hivi eti nasubiri Supreme court itoe maamuzi kwa mara ya pili. Tungelikuwa na shida sana sasa hivi.
Tuheshimu democratic Institutions tulizoziweka zifanye kazi yake, nchi zingine wasingelikubali".

TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Press Play:

Comment ya Waziri January Makamba Instagram kwa Mange Kimambi

$
0
0
Mitandao ya kijamii ni sehemu nyingine ambayo inayofikisha ujumbe kwa urahisi zaidi, ni sehemu ambayo ukiweka chochote ndani ya dakika 10 kinakua kimesambaa sehemu mbalimbali za dunia kutokana na watu wengi kujiunga na mitandao mbalimbali.

Mmoja wa Wakazi wa Mwanza alimtumia Mwanadada Mange Kimambi video fupi ikionyesha Kiwanda ambacho bomba lake linatoa moshi na akasikika akiongea kwenye hiyo video “huo moshi unaoonekana hapo kuna kiwanda kinaitwa Nyakato Steel kinachafua hali ya hewa ni hatari, Wananchi wa Igoma afya zinaumiza huku”

Baada ya kupost video hiyo Mange aliandika watu wamtag Waziri January Makamba ambae ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anaeshughulikia Muungano na Mazingira ili ajionee malalamiko hayo.

Dakika kadhaa baadae Waziri January Makamba alijibu kwenye hiyo post kwa kuandika kuwajulisha wote waliolalamika kwa kuandika 

“jmakamba @mangekimambi_ nimeona. Tutatuma watu. Asante“
January Makamba ni miongoni mwa viongozi wa Tanzania ambao hujibu sana maoni au comment za Wananchi kwenye mitandao ya kijamii na kufanya iwe rahisi kwa watu wenye madukuduku yao kuyafikisha au kusikilizwa kwa urahisi zaidi kuliko kutumia mifumo mingine ambayo ni ngumu kumfikia.


Baadhi ya comments za Wananchi baada ya kuona comment ya Waziri January Makamba

Miongoni mwa Viongozi wengine ambao hutumia mitandao yao binafsi kuweka kazi wanazofanya au kujibu comments au post za Wananchi ni pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii Dr. Kigwangalla, Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe, Waziri wa Uchukuzi Profesa Mbarawa, RC wa Dar es salaam Paul Makonda, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu n.k

Wema Sepetu aendelea kuwa kimya baada ya Lipstick zake kufungiwa na Serikali

$
0
0
Ni miaka mitatu imepita tokea Wema Sepetu Miss Tanzania 2006 azindue lipstick zake ziitwazo “Kiss By Wema Sepetu” na zikaingia sokoni na kufanya vizuri kwenye mauzo sehemu mbalimbali za Tanzania.

Leo November 11 2017 Serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imetangaza kuzifungua lipstick hizo na kueleza kwamba wamebaini kuwa hazijakidhi viwango vya matumizi kwa binadamu.



Tulizoea kuona Wema Sepetu akijibu haraka au kuzungumzia matukio yake pindi tu yakitokea kama hivi lakini kwenye hili la leo bado ameendelea kuwa kimya na kutoandika chochote kulihusu kwenye mitandao yake.

Kwenye mitandao yake leo Wema ameichunia habari ya kufungiwa na badala yake ameendelea kuipigia debe APP yake mpya ya kulipia ambayo itakua ikionyesha mambo yake mbalimbali ikiwemo movie anazoigiza pamoja na maisha yake ambapo kwenye moja ya post zake alizopost jioni ya November 11 2017 imesomeka hivi hapa chini.

“Najivunia Kuwa The First Female in AFRICA to own my Very Own Application, Mnadhani naskia sifa wala… Sioni hata sifa… (LoveDove🤗🤗🤗 Download WemaApp now on Playstore… Soon itafika mpaka App Store… Inshallah“

BASATA yaongea kuhusu Msondo Ngoma kumdai Diamond Milioni 300

$
0
0
Baada ya Band ya Msondo Ngoma kutaka ilipwe shilingi milioni 300 na kundi la WCB kwa kutumia bila ruhusa vionjo vya wimbo wake kwenye wimbo wa “Zilipendwa”  Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Godfrey Mngereza ameongea yafuatayo.

“Unaweza kuitazama katika mitizamo mbalimbali lakini unapoangalia kwamba wanaanza kushtakiana kimsingi ni taratibu ambayo inagusa sana mambo ya haki miliki, kabla ya kuitumia kazi ya mtu ni vizuri ukamuona mwenye kazi mkubaliane”

“Ukitumia kazi ya mtu bila utaratibu hiyo moja kwa moja ni kosa, cha msingi hata kabla ya kumuweka Mwanasheria ili kudai haki yako ni vizuri ukawafata au ukawasiliana na alietumia kazi yako bila ruhusa…. katika hili linalojitokeza sasa hivi ni swala la kuamshana kwamba kazi ya sanaa ya mtu flani haina tofauti na mali ya mtu ya aina nyingine, huwezi kutumia gari la mtu bila ridhaa yake” – Mngereza
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images