Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Lulu Diva Awatupia Dongo Waliokuwa Wanamwita Gume Gume.....

0
0
VIDEO Queen aliyegeukia kwenye Bongo Fleva, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’, amefunguka kuwa, wale wote waliomuita gumegume kipindi cha nyuma, sasa anawacheka kwa dharaaau!

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Lulu Diva alisema kuwa, wakati anaanza kujiingiza kwenye masuala ya uhusiano wa kimapenzi na jamaa yake aliyeko naye sasa hivi (hakumtaja), wengi walijua hawezi kuwa na mwanaume huyo muda mrefu.

“Waliokuwa wakiniita gumegume, siwezi kukaa na mpenzi mmoja kama nilivyodumu na mpenzi wangu, nawacheka tu kwa dharau,” alisema Lulu Diva.
Stori: Imelda Mtema, Dar

Ndoa ya Dogo Janja na Irene Uwoya Yamnyima Ndikumana Usingizi....Ona Utoto Anaofanya

0
0
Siku chache baada ya kusambaa kwa picha za harusi za aliyekuwa mke wake ambaye ni Queen wa Bongo Muvi, Irene Uwoya, kuonekana amefunga ndoa na mwanamuziki nguli wa Bongo Fleva, Dogo Janja, msakata kabumbu Hamad Ndikumana ‘Kataut’, ameonekana kuumizwa na ndoa hiyo. Licha ya kuwa kwa sasa ana mpenzi mwingine, lakini kutokana na maneno yake mitandaoni mashabiki wanadai anaumwa homa ya wivu.

Posti za Ndikumana Kwenye Ukurasa Wake wa Instagram
Ndikumana ambaye hasira za kumuanika mpenzi wake mpya zilianza baada ya kumuona mzazi mwenziye kafunga ndoa na Janja, ambapo mashabiki walitarajia baada ya kila mmoja kupata pumziko lake hakutakuwa na maneno tena. Lakini imekuwa tofauti kwani mwanasoka huyo ameendelea kuposti picha kupitia mtandao wake wa Instagram na kuiambatanisha na ujumbe unaoelezea jinsi ambavyo mama yake anamhurumia kwa jinsi alivyokuwa amepotea njia kumuoa Uwoya, na sasa amepata jiko jipya anampongeza.


Irene na Ndikumana walifunga ndoa mwaka 2009 na kufanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume waliyempa jina la Krish, lakini ndoa yao haikudumu kwa muda mrefu wakatengana, ambapo hivi karibuni kumeenea taarifa kwamba Diva huyo amefunga ndoa na Dogo Janja, kutokana na picha zao za harusi zinazosambaa mitandaoni, lakini Uwoya mwenyewe amekanusha ishu hiyo na kusema hajafunga ndoa na Janja, badala yake ni Muvi inayotarajiwa kutoka hivi karibuni.

NA ISRI MOHAMED/GPL

Leo Ndio Leo....Hatma ya Lulu kubaki uraiani au Gerezani Kujulikana

0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania leo Novemba 13, 2017 inatarajia kutoa hukumu katika kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili muigizaji wa filamu Tanzania Elizabeth Michael maarufu Lulu.

Kesi hiyo iliendelea mara ya mwisho Oktoba 26 mwaka huu chini ya Jaji Sam Rumanyika, ambapo baada ya kufunga kupokea ushahidi wa upande wa mashtaka, na utetezi kwa upande wa mtuhumiwa alitangaza kuwa hukumu ya kesi hiyo itatolewa mahakamani hapo Novemba 13.

Katika kesi ya msingi, Lulu anatuhumiwa kumuua bila kukusudia kinyume na kifungu cha 195 cha Kanuni za Adhabu (PC) aliyekuwa mwigizaji mwenzake wa filamu, Steven Kanumba Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu Sinza Vatcan, jijini Dar es Salaam.

Wazee wa Baraza ambao hutoa ushauri kwa hakimu anayeendesha kesi za mauaji walisema kuwa, Lulu alimuua Kanumba bila kukusudia.

Hukumu hii imevuta hisia za watu wengi hasa waigizaji na wapenzi wa tasnia ya filamu nchini huku wengi wakimuonea huruma Lulu na kuomba ashinde au kupewa adhabu iliyo nyepesi kwa sababu hukumu itakayosomwa leo itafungua ukurasa mpya katika maisha yake.

Kisheria kwa mujibu wa kifungu cha 198 cha kanuni za adhabu, mshtakiwa anayepatikana na hatia ya kuua bila kukusudia adhabu ya juu kabisa huwa ni kifungo cha maisha jela.

Aidha, adhabu ya chini huwa ni kuachiwa huru kwa masharti maalumu au kifungo cha nje, ambapo ama mshtakiwa huonywa asifanye kosa jingine ndani ya muda maalumu unaopangwa na mahakama au anaweza kuamuriwa kufanya shughuli za jamii.

Zitto Kabwe..Jambo Moja Linanisumbua Sana. Nisaidieni Tafadhali

0
0
Anaandika Mbunge wa Kigoma Zitto Kabwe.
Jambo moja linanisumbua sana. Nisaidieni tafadhali

Inawezekanaje Serikali ikasaini mkataba wa shilingi Trilioni 7 kujenga Reli bila kuweka vifungu vya kufungamanisha na sekta nyengine nchini? Yani kweli hata misumari ( screws) nchi hii haiwezi kutengeneza mpaka iagizwe kutoka Uturuki? Yani hata kampuni ya kuchimba kokoto itoke Uturuki? Hivi Viwanda vya Chuma nchini vinafanya kazi gani sasa? CTI, TPSF nielezeni hili, hamuwezi kuzalisha kitu chochote kulisha ujenzi wa Reli ya Kati ya SGR? Katika BOQ ya Mradi wa SGR, hamna muwezalo? Serikali iliwapa BOQ mkashindwa? Ukiwauliza watu wa Wizara hawana majibu, wanasema Mkataba ali negotiate Rais mwenyewe. Inawezekana kweli? Siwezi kumwuliza Rais. Anasema sisi kazi yetu kukosoa tu. Amekasirika. Siwezi kumwuliza mtu aliyekasirika, tena Amiri Jeshi Mkuu.

Wakati wa Mdororo wa Uchumi Asia mwaka 1997-1998 Waziri Mkuu wa Malaysia Tun Mahathir Mohammed alifanya miradi mikubwa sana ikiwemo kujenga Mji Mpya, barabara kubwa na Jengo la Petronas. Kwanini? Ili kuingiza fedha kwenye uchumi na kuchochea shughuli nyengine za uchumi na kukuza mahitaji ( aggregate demand). Malaysia ikawa nchi ya kwanza kuibuka kutoka Asian Financial Crisis.

Sisi Watawala wetu wamekwenda madarasa tofauti na kusoma vitabu tofauti vya Uchumi? Unajenga Reli kwa pesa yako ( inavyodaiwa), kwa hiyo unakusanya kodi kutoka kwa watu wako, unanunua US$, unamlipa Mkandarasi. Mkandarasi ananunua kila kitu kutoka nchini kwao Uturuki, mataruma ya Reli, Chuma, Screws na Misumari na hata mchimba kokoto Mturuki. Kwenye uchumi hii inaitwa leakages. Uchumi wetu unahitaji more inflows.

Unajengaje Reli kwa kutumia Chuma kutoka nje the wakati una hazina ya chuma Ludewa? Unamwaga TZS 7 Trilioni bila kuhakikisha offsetting? Natamani kuiona hiyo BOQ ya Reli ya Kati.
Hili linanisumbua sana. Siamini kuwa watawala waliokwenda shule na wenye uzoefu Serikalini hawakuona faida kubwa ya offsets. Baraza la Mawaziri limejaa PHDs, kweli wameshindwa kuona hili? Fedha zetu wenyewe tunatengeneza ajira nje? Kwamba sisi tuwe vibarua tu na wagonga reli? Trilioni 7 zingechochea sana uchumi ( multipliers).

Tunaambiwa sisi tupo negative mno. Hebu watetezi wa Serikali, mnaojua kuitafsiri Serikali, nisaidieni. Hili mnaona lipo sawa?

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Tetemeko Nchini Iran na Iraq Lawaua Zaidi ya Watu 100

0
0
Tetemeko Nchini Iran na Iraq Lawaua Zaidi ya Watu 100
Tetemeko la ukubwa wa 7.3 katika vipimo vya richa limekumba eneo la kaskazini mwa Iran na Iraq na kuua watu kadha.
Takriban watu 129 waliuawa katika mkoa ulio magharibi mwa Iran wa Kermanshah, kwa mujibu wa maafisa.
Tetemeko hilo lilizua hofu hadi kusababisha watu kukimbia kutoka manyumbani mwao kwenda barabarani.
Misikiti kwenye mji mkuu wa Iraq Baghdad, imekuwa ikifanya maombi kwa kutumia vipasa sauti.
Saudia yadai Iran ilihusika katika shambulio la kombora
Wengi wa waathiriwa walikuwa ni kwenye mji wa Sarpol-e Zahab, kilomita 15 kutoka mpakani.
Kulingana na kituo cha Marekani USGS tetekemo hilo lilitokea umbali wa kilomita 33.9 chini ya ardhi la lilisikika nchini Uturuki, Israel na Kuwait

Uharibifu umeripotiwa kuetka katika vijiji vinane kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu nchini Iran Morteza Salim.
Baadhi ya vijiji vimekumbwa na matatizo ya nguvu za umeme na mawasiliano yamevurugwa
Iran kulipiza kisasi dhidi ya vikwazo vipya vya Marekani
Makundi ya uokoaji yanatatizwa na maporomoa ya ardhi.
Tetemo hilo lilitokea kilimita 30 kusini magharibi mwa mji wa Halabja karibu na mpaka wa Iran.
Lilitokea umbali wa kilomita 33.9 na lilisikika nchini Uturuki, Israel na Kuwait.

Ali Kiba, Nandy Wang'aa Nigeria Washinda Tuzo za AFRIMA

0
0
li Kiba, Nandy Wang'aa Nigeria Washinda Tuzo za AFRIMA
Ni tukio jingine lililosubiriwa sana na Watanzania pia wakitaka kujua matokeo yatakuaje kwa Watanzania walioshiriki kwenye tuzo hizo za ALL AFRICA MUSIC AWARDS 2017 ( AFRIMA)

Good news ni kwamba Mwimbaji wa Tanzania staa wa hit single ‘wasikudanganye’ ameshinda tuzo ya Msanii Bora wa kike upande wa Afrika Mashariki wakati Mtanzania mwingine Alikiba ameshinda tuzo mbili.

Tuzo za Alikiba ni Best Artist or Group in African RnB and Soul ambayo ameshinda pamoja na Rapper wa Nigeria M.I ambae walifanya pamoja Smash Hit ya ‘Aje” na tuzo nyingine ni Kolabo Bora ya Afrika ambapo smash hit ya “Aje” imechukua…….. List kamili ya Washindi wote itakujia soon hapahapa



Majirani Wafunguka Kuusu Dkt. Luis Shika Mnunuzi Feki wa Nyumba za Lugumi

0
0
Majirani Wafunguka Kuusu Dkt. Luis Shika Mnunuzi Feki wa Nyumba za Lugumi
Jina la Dr. Luis Shika lilianza kupata umaarufu mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kushiriki mnada wa nyumba za Lugumi na kushinda nafasi ya kuzilipia nyumba 3 ambazo gharama zake ni zaidi ya BILIONI 2.

Gumzo lilikua kubwa sana baada ya kugundulika kwamba Dr. Shika hakuwa na pesa yoyote mfukoni hivyo akakamatwa kupelekwa Polisi kwa kuvunja masharti ya mnada ambapo hata hivyo baadae alisema hawezi kutembea na pesa nyingi hivyo.

Watu wengi wamekua na shauku ya kutaka kujua kama kweli Dr. Shika ni Bilionea kama alivyojitokeza kununua Majumba ya Bilioni, anaishi wapi? maisha yake ni yapi? majirani wameongea kila kitu kwenye hii video hapa chini.

Cristiano Ronaldo Aongeza Mtoto wa Nne

0
0
Cristiano Ronaldo Aongeza Mtoto wa Nne
Mchezaji bora wa dunia kutoka Real Madrid, Cristiano Ronaldo ameongeza mtoto wanne katika familia yake.
Ronaldo amefanikiwa kupata mtoto huyo kupitia kwa mpenzi wake ambaye ni mwanamitindo wa nchini Hispania, Georgina Rodriguez.

Kupitia mtandao wa Instagram, mchezaji huyo ameandika jina la mtoto huyo ni Alana Martina.

Watoto wengine wa mchezaji huyo ni Cristiano Ronaldo Jr mwenye miaka saba na mapacha wake aliwapata mwaka huu Eva Maria na Mateo ambao mama yao bado hajafahamika.

Bodi ya Mikopo Yatoa Orodha Nyingine ya Wanafunzi Waliofanikisha Mikopo

0
0
Bodi ya Mikopo Yatoa Orodha Nyingine ya Wanafunzi Waliofanikisha Mikopo
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha nyingine yenye wanafunzi 1,775 wa Mwaka wa Kwanza waliofanikiwa kupata mikopo.

Hivyo idadi hiyo kufanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo hadi sasa kufikia 31,353. Katika Awamu ya Kwanza, wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza walipangiwa mikopo, Awamu ya Pili (11,481), Awamu ya Tatu (7,901).
“Tumekua tukifanyia kazi orodha za udahili ambazo tumekuwa tukipokea, na kila tunapokamilisha, tunatoa orodha za wanafunzi waliopangiwa mikopo ambao wana sifa – leo tumetoa hao 1,775”, amesema Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru
Badru, katika taarifa yake kwa vyombo vya habari pia amekumbusha kuwa kiasi cha shilingi 427.54 bilioni zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka 2017/2018 na tayari Serikali imeshatoa shilingi 147.06 bilioni kwa ajili ya robo ya kwanza ya mwaka huu wa 2017/2018.

Lulu Awasili Mahakamani Kusikiliza Hukumu Yake

0
0
Lulu Awasili Mahakamani Kusikiliza Hukumu Yake
Tayari mwigizaji wa filamu nchini, Elizabeth Michaeli maarufu kama Lulu amewasili mahakamani kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya kesi inayomkabili, ya kumuua Steven Kanumba bila kukusudia.

Amewasili mahakamani akiongozana na wakili wake Peter Kibatala kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya kesi yake.

Lulu anakabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia msanii mwenzake Steven Kanumba.

Watu mbalimbali wamejitokeza kufuatilia huku hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.

Familia ya Dkt Shika Aliyevuruga Mnada wa Nyumba za Lugumi Yafunguka Kuhusu Kumtenga Ndugu Yao

0
0
Familia ya Dkt Shika Aliyevuruga Mnada wa Nyumba za Lugumi Yafunguka Kuhusu Kumtenga Ndugu Yao
Wakati utata ukizidi kugubika kushikiliwa, maisha na mwenendo wa Dk Louis Shika anayetuhumiwa kuvuruga mnada wa nyumba za bilionea Said Lugumi, imebainika kuwa ndugu zake walishamtenga baada ya kutoweka kijijini na kutojihusisha na familia.

Dk Shika alipata umaarufu kwa muda mfupi baada ya kushiriki katika mnada wa nyumba tatu za kifahari jijini Dar es Salaam na kuibuka mshindi, akiwa ameweka dau la takriban Sh2 bilioni, lakini akashindwa kufanya malipo ya awali ya asilimia 25.

Umaarufu wake ulitokana na hali ya kujiamini aliyoonyesha wakati akipandisha bei ya nyumba hizo na wakati fulani, akitaja bei ya juu kwa kusema kuwa ndiyo “900 ingependeza”, lakini akashindwa kufanya malipo kama ilivyotakiwa, hali iliyomfanya aanze kufuatiliwa na vyombo vya dola na baadaye vyombo vya habari.

Kutokuwa na fedha kulingana na mahitaji ya mnada huo, makazi, maisha na maelezo yake yalishangaza wengi waliofuatilia maisha yake.

Na waandishi wa habari wa Mwananchi waliofika kijijini kwao mkoani Mwanza, walikuta hadithi mpya.

Mwananchi ilipokutana na kaka mkubwa wa Dk Shika anayeitwa Pelanya Lunyalula mwenye umri wa miaka 84, ilimkabidhi gazeti lenye picha ya “bilionea’ huyo. Alipoiona alibubujika machozi akisema ni mdogo wake anayeitwa Shika.

“Kwetu wana ukoo, Shika tunamhesabu kwenye kundi la ndugu wasiokuwepo (tumetumia neno letu kuepusha makali), maana hajawahi kurejea nyumbani licha ya baba, mama na ndugu wengine kufariki na yeye kupata taarifa,” alisema Lunyalula akiwa nyumbani kwake kitongoji cha Misheni, Kijiji cha Chamugasa jana.

“Uamuzi wa kumtenga Shika ulifikiwa katika kikao cha wana ndugu wakati wa msiba wa baba yetu mkubwa, Mzee Kisula Buselele. Hilo lililomfika atalimaliza mwenyewe kama alivyolianzisha kwa sababu hatumhesabu kama ndugu.”

Lunyalula, baba wa watoto tisa anasema mara ya mwisho alionana na Dk Shika wakati akiwa kijana na wakati huo mdogo wake alikuwa hajaenda masomoni nchini Urusi.

“Sikumbuki mwaka. Ila ni miaka ile ya operesheni ya wahujumu uchumi (miaka ya themanini mwanzoni). Tangu wakati huo hajarudi nyumbani wala kuwa na mawasiliano na familia,” alisema Lunyalula ambaye ni mtoto wa pili kuzaliwa kwenye familia ya Mzee Lunyalula Kidola na Mama Wile Ngongo.

“Kwa kipindi chote hicho, huwa tunasikia tu kuwa amerudi likizo kutoka Ulaya, lakini anaishia Dar es Salaam na kurudi bila kufika nyumbani,” alisema Lunyalula ambaye anafuatiwa na wadogo watatu kabla ya Dk Shika. Aliwataja waliomtangulia Dk Shika kuwa ni Dk Jeremiah, Mpelwa na mwingine anayesema alifariki kabla ya kupewa jina.

“Kama unavyoiona hii nyumba inakaribia kuanguka. Hii kweli inaweza kuwa nyumbani kwao mtu anayejiita daktari bingwa aliyesoma Ulaya? Hailingani, na hata wenzake wakija kuona picha ya nyumbani kwao, watashangaa,” alisema.

Nyumba ya familia hiyo ya matofali ya udongo na kuezekwa kwa mabati, ilijengwa na Dk Shika na ndugu yake Jeremiah aliyefariki Desemba 19, 1992 kwa mujibu wa maandishi kwenye kaburi lake lililo pembeni mwa makaburi ya wazazi wake.

Kwa mujibu wa Lunyalula, Dk Jeremiah aliyewahi kufanya kazi hospitali za Bugando ya Mwanza na KCMC mjini Moshi, ndiye alikuwa wa kwanza kwenda kusoma Urusi na kufuatiwa na Dk Shika.

Mwenyekiti wa Kitongoji

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Emmanuel Wakenya alieleza kushangaa taarifa kwamba Dk Shika ni mmoja wa watu kutoka eneo hilo.

“Tumeshtuka kujua kumbe mtu anayeitwa Dk Louis Shika ni ndugu yetu hapa kijijini aliyepotea muda mrefu tangu tukiwa watoto na hajarejea hadi leo,” alisema.

Wakenya, ambaye ni  mpwa wa Dk Shika, alisema alimfahamu ‘bilionea’ huyo akiwa mtoto, lakini hajawahi kumwona wala kupata taarifa zake.

Mwenyekiti huyo aliyeishukuru Mwananchi kwa kuwapelekea nakala ya gazeti lenye habari na picha ya Dk Shika, alisema licha ya kutorudi nyumbani, ‘daktari’ huyo hajawahi kuoa wala kupeleka mke au watoto kijijini hapo.

Kauli hiyo iliungwa mkono na Lunyalula.

“Mimi sina mke kwa sasa,  lakini nimewahi kuoa na kuzaa watoto tisa kabla ya kutengana na mke wangu mwaka 2004. Shika yeye hatujui habari zake kuhusu ndoa na familia,” alisema Lunyalula.

Ndugu wengine wa Dk Shika, kwa mujibu wa kaka yake Lunyalula ni dada yao mkubwa Cecilia, Jeremiah (marehemu), Mpelwa, Pius, Kefline, Hellen, Dotto na Paulo.

Jirani hamfahamu Dk Shika

Jirani wa familia ya Dk Shika kijijini, Ng’washi Kabukabu hamjui mtu mwenye jina hilo.

“Mimi huyo Shika simfahamu wala sijawahi kumsikia hadi leo mnaponiuliza habari zake. Ila familia hii ni kati ya majirani tunaoishi nao vizuri,” alisema mama huyo.

Makazi yalivyo

Jijini Dar es Salaam, jirani zake eneo la Tabata Mawezi, takriban mita 700 kutoka kituo cha daladala cha Tabata Mawenzi, walikuwa na hadithi nyingine zinazoendelea za kusisimua.

“Unajua mambo mengine yanashangaza. Mtu anapozeeka akili zinarudi kama za mtoto na huyu ni babu ujue. Hata suala la umeme au maji hapa huwa halipi atatoa wapi hela?” alisema mama mmoja mpangaji mwenzake aliyeomba jina lake lisitajwe.

Mama huyo aliwaonyesha waandishi wa gazeti hili chumba ambacho anaishi Dk Shika.

Kwa kutokea dirishani ambako hakuna pazia, unaweza kubaini kuwa aliondoka mapema siku ya mwisho, mithili ya mtu aliyekuwa anawahi sehemu; kitanda cha ukubwa mita 4x6 kikiwa hakijatandikwa, juu yake kukiwa na magazeti, karatasi, nguo na vitabu na chandarua hakijashushwa vizuri.

Pembeni kuna kabati likiwa na mabegi mawili ya nguo, kuna mabeseni matatu madogo, dumu moja la maji, kikaango cha mayai au chapati, kikombe kimoja cha plastiki na jiko la mafuta ya taa.

Pembeni kuna vitanda na chaga zimeegeshwa nusu ya chumba chote, kandambili, nguo baadhi zimetundikwa na mifuko myeusi.

“Hivyo vitanda ni vya baba mwenye nyumba na wakati akija alivikuta. Si unajua babu hana vitu vingi kama ulivyoona, ndiyo maana anatumia vivyo hivyo,” alisema jirani mmoja.

‘Bilionea’ ni mtu wa kawaida

Mmoja wa kina mama wanaouza chakula eneo la jirani na ambaye alijitambulisha kwa jina la Mama Glory alisema Dk Shika “ni mtu wa kawaida sana”.

“Huwa anakuja hapa kunywa chai ingawa anapenda maharage na chapati mbili au moja,” alisema.

“Nilikuwa namjua kama babu, hilo la dokta ndiyo nimelijua sasa. Babu akija hapa hana tatizo, atakula na akimaliza ataondoka. Si msumbufu kabisa ni mtu wa kawaida kabisa.”

Kauli ya Mama Glory inafanana na ya mama lishe mwenzake aliyejitambulisha kwa jina moja la Rose.

“Kumbe babu ana hilo jina! Nilivyosikia nilishangaa ila huwezi kumjua mtu kama ana hela kwa kumuangalia,” alisema.

“Ni mteja wetu hapa na anapenda kula ugali, ila nilishtuka nilivyoona katika mitandao na baadaye kwenye taarifa ya habari usiku. Huwezi kumjua mtu kama ana hela kwa kumuangalia, labda ni kweli.”

Mmoja wa watoa huduma za kifedha kwa simu za mikononi ambaye hakutaka kutaja jina kwa kuhofia kutafutwa kutoa ushahidi, alisema huwa anamuona mtaani ‘bilionea’ huyo.

“Mara nyingine huwa anakuja kutoa hela katika simu na nilishangaa nilipoona katika mitandao kwamba kanunua majumba ya Lugumi kwa kuwa huwa akija kutoa hela, haizidi Sh5,000,” alisema.

“Utakuta anatoa Sh4,500, Sh3,500 na wakati mwingine anatoa Sh2,500. Kutokana na chenji kusumbua huwa namkwepa.”

Asaidiwe, asiwekwe ndani

Hashim Said, anayeuza duka karibu na eneo hilo, alisema tangu alipomfahamu miezi minne iliyopita hakuwahi kununua kitu chochote dukani kwake.

“Hapa anaweza akaja na akakuulizia kitu ambacho hakipo na ukikileta hanunui. Hiyo ndiyo ilikuwa kawaida yake,” alisema na kuongeza kuwa huwa anawadokezea kuwa alikuwa akienda Urusi.

“Inavyoonekana mwanzoni alikuwa vizuri kiuchumi japo nasikia anapokaa kawekwa tu. Kwa mazingira yake mwenyewe na maisha anavyoishi hapa mtaani, sijui kama anaweza kuwa na fedha. Wewe mtu kama anapitisha siku mbili bila kula atakuwa na hela?” alihoji Said.

“Ninachokiona huyu mzee hapaswi hata kuwekwa ndani. Ukifuatilia hata mazungumzo yake kuna vitu kama viliwahi kumtokea kwani katika mazungumzo yetu hapa aliwahi kusema alifungwa ila ukimuuliza wapi hasemi. Huyu anapaswa kusaidiwa na si kuwekwa ndani.

“Kwa hiyo anapaswa kutafutiwa wataalamu wa saikolojia wakazungumza naye na si kumuweka ndani au kumpeleka mahakamani. Ujue hana wasiwasi kabisa kwani juzi alipokuja na polisi hapa kama wanne alikuwa akitembea kwa kujiamini kabisa.”

Habari hii imetayarishwa na Peter Saramba,Ngollo John na Ibrahim Yamola

Taifa Stars Yaonesha Ubavu kwa Benin Bila Samatta

0
0
Taifa Stars Yaonesha Ubavu kwa Benin Bila Samatta
Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imelazimisha sare ugenini dhidi ya Benin kwenye mchezo wa kirafiki wa kalenda ya FIFA uliomalizika jioni hii.

Tanzania ambayo imecheza bila ya nahodha wake Mbwana Samatta ambaye ni majeruhi, ilijikuta ikilazimika kusubiri hadi kipindi cha pili ili kusawazisha bao la Benin lililofungwa na Stephan Sessegnon dakika ya 30.
Baada ya kurejea kutoka mapumziko Taifa Stars ilirudi na nguvu mpya ambapo walifanya mashambulizi kadhaa kupitia kwa washambuliaji wake Simon Msuva, Shiza Kichuya na Elias Maguli.
Jitihada binafsi za Shiza Kichuya zilizaa matunda dakika ya 51 baada ya kuwapita walinzi akitokea pembeni kushoto, kisha kupiga krosi ambayo ilitendewa haki na Elias Maguli kwa kuiandikia Taifa Stars bao la kusawazisha.
Baada ya bao hilo timu zote ziliendelea kushambuliana lakini hakuna timu ambayo iliona lango la mwenzake hadi mwamuzi alipomaliza mchezo huo matokeo yakabaki kuwa sare ya 1-1.

Breaking News: Lulu Michael Kwisha Habari yake...Apigwa Mvua Miaka Miwili

0
0

HUKUMU: Mahakama Kuu imemhukumu Mwigizaji wa Filamu, Elizabeth Michael maarufu Lulu kwenda jela miaka 2 kwa hatia ya kuua bila ya kukusudia.
.
Lulu alikuwa akikabiliwa na kesi ya kumuua bila ya kukusudia mwigizaji mwenzake, Steven Kanumba mwaka 2012.
.
Elizabeth Michael kwa Mara kwanza alipelekwa Mahakama ya kisutu iliyopo Dar es salaam, akishtakiwa kuua bila kukusudia tarehe 7 mwaka 2012""Ushahidi wa mazingira ni ushahidi ambao mstakiwa alikubali kwamba yeye ni MTU wa mwisho kuwa na marehemu ambapo mshtakiwa alikuwa na mahusiano na marehem kwa miezi 4"
.
Ushahidi wa mazingira unaweza kutumika kama msingi pekee wa kumtia hatiani mshtakiwa tena mshtakiwa pekee, Sasa ninapokwenda kuangalia maelezo ya mshtakiwa kama yanakidhi vigezo nilivyosema awali""Kwa mujibu wa mshtakiwa alisema alianza kupigwa na marehem, Mshtakiwa alisema kuwa marehemu alilewa lakini kuhusu mshtakiwa anatakiwa kutoa Maelezo yanayo jitosheleza kwa hili mshtakiwa alijikanganya"
.
Mshtakiwa katika maelezo yake hakueleza kuwa marehemu alianguka au laah!! wakati anamkimbiza, Maelezo ya Dkt. Josephine siyo maelezo ya cheti cha hospitali hayakuwa na hadhi ya hospitali""Inakinzana na hekima ya kawaida kwamba hata pale marehemu alipoendelea kumpiga na kumshambulia na akaenda kiwango cha kumtishia kumuua, mstakiwa hakuthubutu hata kumpiga..." Muigizaji wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu' amekutwa na hatia ya kuua bila kukusudia na hukumu itatolewa baada ya mawakili wake kujitetea.

Mange Kimambi Afunguka baada ya Lulu kupigwa mvua ya Miaka Miwili

0
0

From @mangekimambi_ - Breaking newzzzzzzzz..... Lulu amekutwa na hatia ya kuuwa bila kukusudia na amehukumiwa miaka miwili jela.......
.
.
.
Dah huyu jaji anawaza kama mimi posti yangu niliyoposti masaaa mawili yaliyopita nilisema ningekuwa jaji ningemkuta na hatia ila ningempa adhabu ndogo mwaka mmoja au miwili jela.......
.
.
Jaji ametenda haki....
.
.
Sio kama nimefurahi Lulu kafungwa nilichotaka ni kuona hakuna double standards, nilitaka kuona haki inatendeka. Na Lulu ana deserve hiyo miaka 2 jela labda itampa muda wa kufikiria how her actions affected Mama Kanumba na familia yake. Labda akitoka atakuwa more humble......
.
.
.
Lakini still mwanasheria wa serikali achukulie hatua za nidhamu na afukuzwe kazi!! Alijaribu sana kusabotage kesi ili amsaidie mtuhumiwa......
.
.
PS: December Magu anatoa misamaha kwa wafungwa, sidhani kama atawasahau wafungwa wa kumpa kiki ya kufungia mwaka kama Lulu na kina Babu Seya maana ile barua ya kina Baba Seya had Bashitel written all over it."

Alichoandika Wema Sepetu Baada ya Lulu Kuhukumiwa

0
0

Wema Sepetu - Dah... Speechless... 😔😔😔 Pole my baby... This too shall pass... 😔😔😔 Dah...

Kutana na Mtaalam na Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Pumu, Vidonda vya Tumbo, Kisukari na Mengine Mengi

0
0
MTALAAM NA BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU NAYALIYOSHINDIKANA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI,MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni SUPER SAYI 3,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

SUPER SAYI 4 Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR ULIMWENGU ANAPATIKA DAR ES SALAAM MAGOMENI MOROCO

HUDUMA HIZI UTAZIPATA MAGOMENI

SIMU NO 0745387469, 0652121197

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.


TAZAMA Video Mpya ya Rosa Ree Ambayo Imekuwa Gumzo Mtaani:

Kutana na Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed Kutoka Bagamoyo...Ana Dawa za Kurudisha Mapenzi na Zingine Nyingi

0
0
MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

USHAURI: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.

Sababu za Mbowe Kutomuheshimu Lipumba Hizi Hapa

0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe amedai kwamba Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF anayetambuliwa na msajili wa vyama Prof. Ibrahim Lipumba kuwa ni Profesa wa ajabu ambaye anaweza kubomoa chama alichokijenga.

Akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo Mtwara, Mh. Mbowe amesema kwamba hana ugomvi wowote na Prof Lipumba ingawa amekiri atakuwa muongo akisema kwamba anamuheshimu kwani anatumika katika kukivuruga chama alichokuwa akikiongoza kwa muda mrefu.

Mh. Mbowe amesema kwamba wakati CUF ikishirikiana na UKAWA kwa ujumla kutafuta kura na kuongeza wabunge wa chama hicho bungeni, yeye Prof Lipumba alikuwa mafichoni na anamshanga sasa hivi anavyorudi ndani ya chama hicho na kutaka kukisambaratisha.

"Sina ugomvi na Prof Lipumba lakini nikisema namuheshimu nitakuwa muongo sana. Prof Lipumba ni msomi sana tena msimchezee kwenye elimu lakini usomi ni jinsi unavyotumia elimu yako lakini siyo wingi wa vyeti. Ni Profesa wa ajabu kweli kweli. Mimi simuogopi mtu nitazungumza straight. Amesema Mbowe

Pamoja na hayo Mbowe amedai kwamba Spika wa Bunge pamoja na Msajili wa vyama vya siasa wanatumika katika kuibomoa CUF na kuongeza kwamba hataacha kusema ukweli kwani hakuna mtu yoyote anayemuogopa isipokuwa Mungu pekee.

Ameongeza kwamba kasi inayotumika kuibomoa CUF inatumika pia kuibomoa CHADEMA na kuweka wazi kwamaba siku chama cha Chadema kikiuliwa labda awe amefariki lakini siyo wakati huu ambao bado anapumzi.

Zitto Kabwe Aizungumzia Bombadier Bungeni....

0
0
Serikali imekiri kujitoa kwenye Mpango wa Kimataifa wa uendeshaji wa shughuli za serikali kwa uwazi (OGP), ambao serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilijiunga Septemba 21 mwaka 2011.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Mh. George Mkuchika wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe lililohoji kwanini serikali imejitoa kwenye Mpango wa Kimataifa wa uendeshaji serikali kwa uwazi (OGP).

Mh. Mkuchika amesema baada ya serikali kushiriki kwenye utekelezaji wa mpango huo kwa muda wa miaka minne imeamua kujitoa, ambapo ameongeza kuwa sio nchi ya kwanza kujitoa kwenye mpango huo.

“Baada ya serikali kushiriki utekelezaji wa mpango huo kwa muda wa miaka minne imeamua kujitoa, na Tanzania sio nchi pekee iliyojitoa, zipo nchi kama Hungury na Urusi zilijiunga na baadae kujitoa”, amesema Waziri Mkuchika.

Kwa upande mwingine Mh. Zitto ameshauri kuwa serikali ingeendelea kuwa mwanachama wa (OGP) ingefaidika kwa sulaa la ndege za Bombadier ambazo zimekwama nchini Canada kutoka na nchi huyo kuwa ndiyo mwenyekiti wa sasa wa OGP.

Hata hivyo Waziri amesisitiza kuwa mahusiano ya Tanzania na Canada ni mazuri bila hata ya Tanzania kuwa mwananchama wa (OGP) ambapo masuala ya Bombadier yatashughulikuwa na balozi wa Tanzania nchini humo.

Mpango wa kuendesha serikali kwa uwazi ulizinduliwa Septemba 20 mwaka 2011 na rais wa zamani wa Marekani Barack Obama ikiwa kama taasisi binafsi. Hadi sasa umoja huo una nchi wanachama 70 ambapo nchi 10 pekee ndio zinatoka barani Afrika.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images