Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

I Need a Tanzanian Matured Man to Love Me

0
0
Mambo! Mimi ni binti,umri wangu ni miaka Ishirini na tano,mrefu,mweusi na mwembamba ni mkristo pia,elimu yangu ni chuo kikuu na ni mfanyakazi. Lengo langu hapa natafuta mwanaume,wa kuanza naye urafiki,mapenzi na mengine tukielewana.Awe mrefu,mwembamba,mwenye afya bora,mwonekano mzuri wa sura na mtanashati,asiwe mnywaji wa kilevi kupitiliza wala asivute sigara! Awe ana chanzo cha mapato cha kueleweka,matured,broadminded na alietayari kuingia kwenye mahusiano ya mapenzi na mwanamke,sexually active kwa njia ya kawaida ya kimaumbile!Elimu chuo kikuu...karibuni,alie tayari awache Mawasiliano yake! Sitaki mzaha,kebehi wala nyodo...!kama unajua hayakuhusu usinivuruge!
I Used to live in USA now Am Back
Note:I only Need Tanzanian Man Not Otherwise...
Call Me Sandra Kileo

Dudu Baya Akanusha Kutishia Kumkata Masikio Mpenzi Wake

0
0
Rapper Godfrey Tumaini aka Dudu Baya amekanusha taarifa zinazosambazwa na mpenzi wake kuwa anamtishia kumkata masikio pamoja na kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja na kijana anayetambulika kwa jina la Aunt Bilal.

Akizungumza na Bongo5 leo, Dudu Baya, amesema kuwa mpenzi wake huyo ambaYe pia ni mganga wa kienyeji anatapatapa kutokana na maumivu ya kuachwa.

“Huyu demu ameachwa mara tano, ana matatizo ya wivu, pia huwa anatishia ukimwacha atakuroga, alishawai kuwa na mzungu na wakazaa huyo mzungu alimkimbia bila hata kuaga akaenda Marekani,” amesema Dudu. “Mimi hajanifukuza kwake nimeondoka mwenyewe na nilimuaga nikamdanganya naenda Morogoro, hata mimi nashangaa nimkate masikio kwa sababu gani? Siwezi kufanya hivyo, eti nina mahusiano na Aunt Bilal, haiwezekani! Polisi wamemuambia asikimbilie kwenye vyombo vya habari haya ni mapenzi, achana na hasira tuwasuluhishe, mimi nikasema haiwezekani niambie mimi nawachukua mademu nafanya nao mapenzi chooni? Haya ni mambo ya kuchaufana tu, hakuna ukweli wowote, nimezunguka kwenye tour nyingi nimewahi kuandikwa kuhusu tuhuma kama hizi, mimi nawaomba watu waangalie ukweli uko wapi, mimi siwezi fanya vitu kama hivyo,” aliongeza.

Tazama HAPA video ya aliyekuwa mpenzi wa Dudu Baya, Mary Kapalisya akiongelea suala hilo

Must Read: Barua ya Emmanuel Mbasha ikieleza jinsi Mkewe Anavyochepuka na Mchungaji wake na Walivyopanga Kumfunga

0
0
Muimbaji wa muziki wa injili na mfanyabiashara, Emmanuel Mbasha anayetuhumia kumbaka shemeji yake, ameandika barua ndefu kwa mchungaji maarufu nchini, Gwajima anayemtuhumu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wake, Flora Mbasha kiasi cha kupanga njama za kuhakikisha anafungwa jela;


Isome:

“Mchungaji …yapata kama wiki mbili zilizopita nilihoji kupitia vyombo vya habari juu ya ‘utajiri’ wa ghafla wa mkewangu Mara baada ya mgogoro kutokea kati yangu na yeye, bila kupoteza muda mkewangu akanijibu kupitia gazeti moja la udaku kuwa amechangiwa fedha kiasi cha milioni 9 na waumini kanisani kwakoMchungaji, naomba uelewe kuwa nafahamu juu ya mipango yote mnayoipanga kuliko unavyodhani!!

Kwanza ni kweli kuwa mlipitisha harambee ya kumchangia mkewangu, lakini kiwango kilichopatikana kilikuwa ni milioni 2 na laki tatu na si milioni tisa kama mlivyotangaza!! Lakini mlitangaza uongo huo makusudi iwe rahisi kutimiza malengo yenu ya kidhalimu mliyoyapanga juu yangu!!Mnamo tarehe 3 mwezi juni mwaka huu, mlifungua akaunti mpya kwa jina la mkewangu katika benki ya crdb morogoro, na siku nne baadae mkewangu aliingiziwa fedha kiasi cha milioni 18 kutoka akaunti ya MWANAMAPINDUZI FOUNDATION ambayo hyo accnt ipo nmb mwanza! Ambapo asasi hii inamilikiwa na mchungaji wako msaidizi Maximilian Machumu pamoja na mbunge wa viti maalumu kutoka mikoa ya kaskazini!

Nashukuru kama ulimpa fedha hizi kwa nia ya kumsaidia, lakini hofu yangu ni kuwa kwanini kitendo hiki kifanyike kwa kificho?? Kwanini mtumie njia za siri ambazo si rahisi watu kujua kama mmempa fedha??

Pia napatwa na mashaka zaidi kwani siku moja baada ya fedha hizi kuingizwa taarifa ya benki inaonyesha kuwa kiasi cha milioni sita cash zilitolewa na siku hiyo hiyo wapo waandishi watatu wa magazeti ya udaku ambao wanaonekana waliingiziwa fedha kiasi cha milioni moja kila mtu na aliyedeposit hizo fedha ni moja ya viongozi wako hapo kanisani!! Kuna nini hapo??

Mchungaji, naomba tusizunguke mbuyu! Ni dhahiri shahiri kuwa umekuwa na uhusiano wenye utata na mkewangu kwa muda mrefu sasa!
Binafsi nilianza kupata wasiwasi mwaka jana mwezi desemba tulipoenda katika mkutano wako wa injili pale morogoro! Mimi na mkewangu tulifikia hoteli ya kingsway msamvu na wewe ulifikia Nashera Hotel maeneo ya forest hill!! Baada ya siku tatu za mahubiri mkutano wako ulipigwa marufuku na serikali kwasababu ya maneno yakichochezi uliyokuwa unahubiri, hvyo ikatulazimu waimbaji wote turejee dar es salaam!!

Lakini uliniomba mkewangu abaki na wewe kwani ulipanga uwe unawafanyia watu maombi pale kanisani kwako kihonda kwa muda wa siku nne!! Nilikubali na nikamuacha mkewangu nyumbani kwa dada yako pale mazimbu!! Lakini kesho yake dada yako alisafiri kwenda mwanza na ikabidi mkewangu arudi hotelini kingsway!!

Kwaa taarifa nilizonazo na nimezithibitisha kupitia wahudumu wa pale hotelini ni kuwa mkewangu hakuwahi kulala pale hata siku moja ingawa chumba kililipiwa kwa siku zote zile!! Unaweza kunijibu alikuwa analala wapi?? Je unaweza kunieleza kwanini mkewangu alikuwa analetwa nashera hoteli na taxi kila siku usiku!! Sibahatishi katika hili kwani hata namba ya dereva taxi ninayo!!

Yote haya nilivumilia, na hapa kati kati kuna mengi sana yametokea lakini nikajifanya mjinga nikajishusha nikavumilia kwa lengo la kulinda ndoa yangu isiharibike lakini naona wenzangu hambadiliki wala hamjishitukii sana sana mapenzi ndio yanzidi kuwa motomoto kati yenu!! Ulikuwa unategemea nivumilie mpaka lini, nijishushe kiasi gani, niwe mjinga kiasi gani Nilikuvumilia sana mchungaji lakini sasa imefika point hapana, imetosha lazima nikuondelee uvivu watanzania na dunia ikufahamu jinsi ulivyo na kitendo ulichonifanyaia na unataka kuniziba mdomo kwa kunitishia jela miaka 30!!!

Wewe ni mpuuzi na shetani anaishi ndani yako… na nataka nikuahidi kitu kimoja kuwa NITAKUSHINDA! Najua utanisumbua sana kutokana na hela zako but at the end, I will be the last man standing!! Narudia tena, nitakushinda.!! Bila kusahau naomba niongee na wewe pia mkewangu, hivi ni nini kilichokukuta ndani ya moyo wako How did we get here?? Je ni fedha zilizokufanya ukengeuke kiasi hicho au kuna kingine?? Kama unanichukia mimi kiasi hiki je, uwahurumii hata watoto wetu?? Mbona tunawatengenezea mikosi wakiwa wadogo hivi?? Hivi unadhani watoto wanajisikiaje watakaposikia kuwa baba ameenda jela kwa kosa la kubaka lakini aliyechongesha muvi yote hiyo ni mama?? Hivi kisaikolojia hawa watoto watakuwaje Si watakuwa huku wanatuchukia sisi wote wawili kwa aibu na mikosi hii tunayowatengenezea Kwanini tunataka kuwataabisha watoto kwa dhambi ambayo hawajaitenda.

Yes nafahamu nimekukosea mengi and am very sory for that, lakini basi embu kumbuka mkewangu nimekuvumilia mambo mangapi mkewangu, kumbuka makosa mazito uliyonifanyia lakini nikakusamehe ni sijamsimulia hata ndugu yako ama ndugu yangu ili kulinda heshima yako!! Kumbuka jinsi tulivyopogana na changamoto mbalimbali mpaka leo hii umefikia kuwa moja ya icons wa muziki wa injili hapa nchini?? Kumbuka shida, manyanyaso, dhuluma, kuchekwa na kudharauliwa ambako tumepitia mpaka leo hii tuko hapa!!!

Mkewangu, kwa miaka yote hii nimekubali nionekane bushoke tu huku watu hawajui kuwa mimi ndiye ninayechora ramani ya kila ishu yako!! Mimi ndiye nimekuwa nafatilia na kufanikisha kila kitu chako from scratch!!! Lakini nimekubali jamii inione bushoke kwani nilikuwa najua nini mimi na wewe tunatengeneza kwa maisha yetu ya sasa na baadae!!! Nini kilichokubadilisha mkewangu Fedha Au huyo mchungaji mwanamazingaombwe.

Hivi kweli kabisa umefikia hatua ya kulipa waandishi wa habari ili wanikandamize nionekane sifai katika jamii Ni nini kilichokuoata mkewangu?? Naomba uelewe kuwa binafsi siogopi kwenda jela kwasababu ya hiyo muvi mliyonizushia, kwani ni bora nikakae jela kuliko kuishi huru huku mkininyanyasa kiasi cha kuondoa utu wangu kama bidamu, lakini kinachoniuma ni familia yetu!! Kwanini watoto wateseke kwa sababu ya tamaa zetu binafsi!! Nikifikiria hilo naumia sana!

Najua kwa sasa inaonekana kama vile ni impossible kwa mimi na wewe kurudiana tena, lakini binafsi naamini tunaweza!! Najua haitakuwa rahisi kwani tumeharibu mno, lakini ni heri ya kujaribu kuliko kuendelea kufanya huu upuuzi tunoufanya sasa!! Kumbuka hiki tunachokifanya sasa hatujajipaka matope sisi tu pekee, bali mziki wote wa injili Tanzania, na tusipotubu tukajirudi Mungu atatuhukumu kwa dhambi hii!!

Kumbuka kuwa hakuna kati yenu atakayeshinda katika hii vita, vyombo vya habari pekee ndivyo vitakavyo nufaika lakini mimi, wewe na mchungaji wote tuta loose!! Mwisho nimalizie na wewe mchungaji, tulipokutana mara ya kwanza nilikuchukulia kama kaka na kama mlezi wetu wa kiroho!! Lakini umegeuka shetani mwenye pembe saba, umeparaganyisha familia yangu, umeleta maumivu makali kwenye ukoo!!
Nakuonya tena kwa mara nyingine, muache mkewangu!! Huyo ni mkewangu, nilimtolea mahali mimi mwenyewe na wazazi wake waliniamini na kunikabidhi!!! Nasema niachie mkewangu!!

Wewe ni nyoka, imefika time watanzania wakujue ukweli wako wewe mbwa mwitu mkali uliyevaa ngozi ya kondoo!!! Umedanganya watu vya kutosha na umefarakanisha ndoa nyingi sana kwa sababu ya kiburi cha pesa zako chafu za sembe!! Umeudhalilisha ulokole kiasi cha kutosha imefika time tuwaeleze watanzania ukweli na wakufahamu kuwa wewe ni nyoka!!

Sitakubali kuona ukiendelea kuitesa familia yangu, nitapambana na nitakushinda!!! Siogopi fedha zako wala connection ulizonazo, ni bora nife nikiwa nimesimama kuliko kuishi nimepiga magoti! Nitapambana na wewe mpaka mwisho ili historia isomeke vizuri ili hata wanangu wakiwa wakubwa wajue kuwa baba yao sikuwa lofa kiasi cha kupiga magoti na kuelekeza shingo kibla kuruhusu mdhalimu kama wewe uichinje familia yangu, bali licha ya umasikini wangu nilisimama kiume na kupigana kutetea familia yangu!!!

Narudia tena mchungaji, nitapambana na nitakushinda..” Kwako – Mchungaji Gwajima
-------------------
Post Sponsored By Kenyangossip.com, The kenyan House of Gossip News

Mama Amchoma Kisu na Kumuua Mwalimu Mbele ya Wanafunzi Wake

0
0
Mwanamke mmoja ameripotiwa kumchoma kisu na kumuua mwalimu wa kike wa shule ya msingi mbele ya wanafunzi wake katika mji wa Albi ulio kusini mwa Ufaransa.

Muendesha Mashtaka wa Albi, Claude Derens ameiambia AFP kuwa tukio hilo limetokea jana (July 4) majira ya asubuhi kwa saa za Ufaransa na kwamba uchunguzi unafanyika ili kubaini sababu zilizopelekea mwanamke huyo kufanya tukio hilo la kikatili.

“Mama huyo alionekana akiwa na kisu na akamchoma mwalimu wa kike mwenye umri wa miaka 34 mbele ya wanafunzi wake, sababu itafahamika baada ya uchunguzi kukamilika.” Claude Derens aliiambia AFP.

Aliongeza kuwa baada ya tukio hilo, rais wa Ufaransa Francois Hollande alimtuma waziri wa elimu, Benoit Hamon haraka katika shule hiyo ili kuhakikisha anachukua hatua kama mwakilishi wa serikali.
------------------
Post Sponsored By Kenyangossip.com, The kenyan House of Gossip News

WEMA akimbilia TCRA kumsaka mtu aliyetengeneza Picha Chafu ya Mama yake Mzazi

0
0
Miss  Tanzania  2006/2007  Wema  Sepetu  ameiomba  Wizara  ya  Sayansi  na  Teknolojia  kupitia  Mamlaka  ya  Mawasiliano  Tanzania  ( TCRA )   kumsaka  mtu  aliyetengeneza  picha   chafu  ya    mama  yake  mzazi, Mariam  Sepetu  na  kisha  kuisambaza  kwenye  mitandao  ya  kijamii…

Akizungumza  na  mwanahabari  wetu, Wema  alisema  anaamini  kuwa  TCRA  wanao  uwezo   wa  kumbaini  mtu  huyo  ambaye  bado  hajamfahamu  ili  sheria  iweze  kuchukua  mkondo  wake  kwani  amemdhalilisha  mzazi  wake  bila  sababu  yoyote….

“Nafanya  utaratibu  wa  kwenda  TCRA  ili  wamsake  aliyefanya  kitendo  hicho  kwani  uwezo   huo  wanao,” alisema  Wema

Mrembo  huyo  alisema  serikali  isisubiri  mpaka  tukio  hilo  limkute  kiongozi  wa  serikali  ndo  waanze  kuhaha  kwani  tabia  hiyo  inaonekana  kuota  mizizi  baada  ya  hivi  karibuni  kufanyiwa  hivyo  wabunge.

The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) is a statutory regulatory body responsible for regulating the communications and broadcasting sectors in Tanzania. 

Kibaka Atundikwa Juu ya Mti baada ya Kunaswa Akiiba Funguo za Daladala Gereji Jijini Mbeya.

0
0
Kijana mmoja  ambaye hakujulikana jina   mara  moja   amejikuta  akionja  machungu  ya  hasira  za  wananchi  baada  ya  kutundikwa  mtini  na  kuning’inizwa  akituhumiwa  kukwapua  funguo  za  daladala  moja  iliyokuwa  ndani  ya  Gereji  moja  iliyoko  mitaa  ya  Soweto  jijini  Mbeya.

KAJALA Akana Tuhuma za Kuchepuka Ovyo Ovyo

0
0
BAADA ya kuzagaa kwa taarifa mbalimbali kwamba mwigizaji wa Bongo, Kajala Masanja anachepuka nje, ameibuka na kukanusha madai hayo akisema hayana ukweli wowote.

Mitandao mbalimbali ya kijamii imekuwa ikiposti taarifa mbalimbali zinazomhusisha Kajala kutembea na wanaume tofauti kitu ambacho mwenyewe amesema hakina ukweli na wanaosambaza uvumi huo, wakome.

Akizungumza na mwanahabari wetu Julai 3, mwaka huu alisema wanaoeneza habari za yeye anachepuka wanamtafuta ubaya kwani hana mpango wowote wa kuolewa wala kuishi na mwanaume kwa sasa.
“Waniache, mtu akisema nina mwanaume alishawahi kuniona? Sina mwanaume mwingine zaidi ya mume wangu,” alisema Kajala.

Kwenye mahojiano hayo, Kajala alisisitiza kuwa, haoni sababu ya yeye kuchepuka wakati mumewe Faraja Augustino yupo hai na anaamini ipo siku atatoka gerezani na ataendelea na maisha ya ndoa yake kama ilivyokuwa zamani.

Kiukweli sioni haja ya kuolewa na mwanaume mwingine tena wakati ni wazi ipo siku mume wangu atakuwa huru, naomba ieleweke kwamba sina mpango na mwanaume yeyote na sasa namgonjea atoke tuendelee na maisha yetu,” alisema Kajala.

Mume wa Kajala, Faraja Agustino anatumikia kifungo cha miaka 7 baada ya kushindwa kulipa faini ya shilingi milioni 200 kufuatia kesi ya kutakatisha fedha iliyokuwa ikimkabili.
Kwenye kesi hiyo, Kajala ambaye naye alihusishwa, alilipiwa faini ya shilingi milioni 13 na mwigizaji Wema Sepetu, kifungo cha miaka mitano kikamuepuka.

Wema, Mama Yake Kuwasomea ALBADILI Waliosambaza Picha Chafu

0
0
SIKU chache zimekatika tangu kusambazwa kwa picha feki inayodaiwa ni ya mama wa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu, Mariam Sepetu, wawili hao wako kwenye mkakati mzito wa kuwasomea kisomo cha Albadili wale wote waliohusika kwa namna yoyote ile kuitengeneza picha hiyo na kuitupia mitandaoni, Risasi Jumamosi linakumegea.

Picha hiyo iliyosambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwa na kichwa cha mama Wema, lakini sehemu ya kuanzia shingoni kwenda chini si yeye na mhusika alikuwa hana nguo, ilizua gumzo kwa wiki mbili sasa huku watu wanaojiita Timu Dengue wakitajwa kuhusika.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, mama Wema na mwanaye wameamua kusoma Albadili ili kuwaadabisha wale wote waliohusika na sakata hilo lenye kufedhehesha.
“Mama Wema na mwanaye walikasirishwa sana na watu waliotengeneza ile picha na kuitupia kwenye mitandao ya kijamii kama Instagram.

“Wiki iliyopita baadhi ya wasamaria wema walikwenda nyumbani kwa mama Wema na kumtajia majina ya wahusika, lakini hawakuwa na ushahidi hivyo yeye na Wema wameamua kujiunga kiimani zaidi kwa kusoma Albadili.

“Wamesema kwanza kabla ya tukio hilo la Abdadili wametoa siku saba kwa yeyote anayejijua amehusika na picha zile za kutengeneza aende mwenyewe kwa mama Wema, nyumbani kwake, Sinza-Mori (Dar) ili kuomba msamaha.

Quote Of The Day:
Spread love everywhere you go. Let no one ever come to you without leaving happier.






Daraja Laua na Kujeruhi Katika Mji yanapofanyika Mashindano ya Kombe la Dunia

0
0
Watu wawili wanaripotiwa kufa na 22 wamejeruhiwa baada ya daraja linalopita juu ya barabara kuvunjika katika mji wa Belo Horizonte ambako baadhi ya mechi za kombe la dunia zinafanyika.

Daraja hilo limeripotiwa kuvunjika Alhamisi ya iliyopita na kuvunja sehemu ya basi huku gari lingine likiwa limenaswa ndani.

Wajenzi wa daraja hilo walipaswa kuwa wamemaliza ujenzi kabla mashindano ya Kombe la Dunia kuanza.

Mji wa Belo Horizonte umesha-host mechi 5 za kombe la dunia hadi sasa na ndipo mocha nyingine ya nusu fainali itafanyika.

Quote of the Day:
Spread love everywhere you go. Let no one ever come to you without leaving happier.

Utafanya Nini Ukimfumania Mpenzi Wako Katika Hali Kama Hii?

0
0
Kila Mtu anajua Kutendwa katika Mapenzi ni Jambo Linalouma Sana kupita maelezo yahitaji moyo wa ziada kuvumilia ..Je endapo ikakutokea ukamfumania mke ama mume akiwa katika hali hiyo hapo juu nini cha kwanza utafanya?

When your heart is broken it is the saddest thing in the world. All your energy leaves you and everything in your life seems to lose all meaning. You gave your heart and soul to this love, and now it is no more. How can your heart ever be whole again?

Picha za Kutisha za Sheikh wa Arusha Aliyelipuliwa Bomu Wakati Akila Daku

0
0

Sheikh wa Msikiti wa Qiblatan,Sood Ally Sood (37) uliopo Kilombero jijini hapa amejeruhiwa kwa bomu la kurushwa kwa mkono alipokuwa akila daku nyumbani usiku wa kuamkia jana.

Pamoja na Sheikh Sood, mtu mwingine aliyekuwa nyumbani kwake,aliyetajwa kwa jina la Muhaji Kifea (38) mkazi wa Sinza jijini Dar es Salaam pia amejeruhiwa katika tukio hilo na wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru kwa matibabu.

Sheikh alijeruhiwa miguu yake yote na mapajani huku Kifea akipata majeraha makubwa miguuni na kupoteza baadhi ya vidole vya miguu yote.

Akizungumza hospitalini hapo, Sheikh, Sood alisema tukio hilo lilitokea nyumbani kwake eneo la Majengo ya chini, usiku wa kuamkia jana saa 5:00 wakati yeye pamoja na mgeni wake walikuwa wakila chakula sebuleni.

“Nikiwa sijui hili wala lile nilishtushwa na mlipuko ulioambatana na vyuma mbalimbali vilivyokuwa vikiruka hewani ambapo bomu hilo linaelezwa kuwa ni guruneti lililorushwa kupitia dirishani baada ya watu wasiofahamika kufanikiwa kuvunja kioo cha dirisha la chumba tulichokuwamo,” alisema Sheikh Sood.

Alidai anawajua waliotekeleza shambulio hilo kwa sababu amekuwa akipokea vitisho kutoka kwa watu anaowafahamu na tayari alikuwa ametoa taarifa kwa vyombo vya dola.

Alisema kuwa siku tatu kabla ya tukio hilo alikoswakoswa kupigwa risasi na watu wasiofahamika wakati akitoka msikitini na akatoa taarifa Kituo Kikuu cha Polisi jijini Arusha kuhusu tukio hilo. Sood anasema kuna baadhi ya vijana anawatuhumu juu ya matukio hayo.

Sheikh huyo ambaye ni Kiongozi wa dhehebu la Answar sun Kanda ya Kaskazini amekuwa akitofautiana na waumini wenzake kutokana na msimamo wake wa kutokukubaliana na baadhi ya waumini wenye msimamo mkali wa msikiti huo.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,  Magesa Mulongo alikemea matukio ya mabomu yanayolitikisa Jiji la Arusha katika siku za karibuni na kuviagiza vyombo dola kufanya uchunguzi wa kina kubaini wahusika wote ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

“Uchunguzi wa awali unaonyesha tukio hili limetekelezwa na watu walio karibu na Sheikh. Polisi wanaendelea na uchunguzi kwa sababu baadhi ya watu wanaotajwa kuhusika kwenye tukio hili pia ni miongoni mwa watuhumiwa kwenye matukio mengine ya milipuko ya bomu Arusha,” alisema Mulongo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatusi Sabasi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa majeruhi wanaendelea vyema huku polisi wakiendelea na uchunguzi wa kina kuwabaini wahusika.

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alielezea kusikitishwa na matukio ya milipuko ya mabomu Arusha na kuliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina kuwakamata wahusika bila kujali vyeo, nyadhifa, dini, itikadi wala rangi zao.
“Arusha tunapita katika kipindi kigumu sana. Kwanza tulishuhudia mlipuko wa bomu kanisani, ikafuatiwa na lile la mkutano wa hadhara wa Chadema, kabla ya mwingine kulipuka kwenye baa na sasa nyumbani kwa Sheikh,” alisema Lema.

Quote of the Day:
Spread love everywhere you go. Let no one ever come to you without leaving happier.

CHADEMA Imehama Kwenye Reli, Imebaki Kuishambulia ACT Badala ya CCM. Imeporomoka 77%

0
0
Kwa lugha rahisi ya sasa hivi ni kwamba chadema imechepuka na mchepuko wake ni ACT. Nakihurumia sana hiki chama. Makada wake wanatumia muda mwingi sana kuishambulia ACT na viongozi wake huku wakiacha masuala nyeti ya taifa hili yakiwa "untouched". ...maadui wao wakubwa hivi sasa ni mwigamba,zitto,na kitila et al.

Agenda sensitive kama vile uchaguzi wa serikali za mitaa wameiacha.kuboreshwa Daftari la mpiga kura,ufisadi nk sasa sio agenda yao tena...wamehama kwenye reli.

Hizo hoja hapo juu ndio zimekiporomosha hiki chama kwa 77%, hivi sasa kimebaki hapa jf na kwa viongozi wake. Leo hii huwezi ukapita mtaani ukamwambia mtu peoplesss!!!! Akajibu confidently..poweeeeerrrrr!!!! ! Haipo tena hususan tangu the zitto et al saga imeanza..imekolezwa chumvi na ukawa na hivi karibuni na wajumbe 82 na the most currently na msajili..kwa sababu kila chadema wanapojitahidi kujibu hoja kwenye media zinakuwa nyepesi,zilizojaa matusi,kejeli na uwongo mwingi, hawajikiti kwenye mada husika.

Ushauri kwa chadema 2015 ileeee kwenye kona
Ushauri kwa ACT enezeni sera za chama chenu,fanyeni ziara mikoani,ile ajali isiwadhoofishe
Ushauri kwa ccm...adui muombee njaa..tumieni hii fursa ipasavyo
Ushauri kwa cuf/nccr ....pigeni ndogondogo,chadema inasinyaa.

By Utaifakwanza Via JF

Mtoto Aliyezaliwa na Miguu Mitatu Anayetarajia Kufanyiwa Upasuaji.

0
0
Mtoto mdogo ambaye amezaliwa na miguu mitatu amesafirishwa kwenda nchini Marekani kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji kuondoa miguu miwili
Ana Paula mwenye miezi 22 alikuwa ni pacha aliyeungana ambapo dada yake hakuweza kupona wakati wa upasuaji wa kuwatenganisha.

Ni mguu mmoja tu wa mtoto huyo unaofanya kazi hivyo upasuaji atakaofanyiwa katika moja ya hospitali za watoto ni kuondoa miguu miwili ambayo haifanyi kazi na kumwongezea uwezo wa viungo vyake kufanya kazi.
Ana na mama yake walisafirishwa kutoka Panama kwa msaada waliopatiwa na wasamaria ili zoezi zima liweze kukamilika.

Quote of the Day:
Spread love everywhere you go. Let no one ever come to you without leaving happier.

Hiki Ndicho Kitu Kikubwa Atakachofanya Diamond siku ya Birthday ya Mama Yake.

0
0
Mama yake Diamond amezaliwa tarehe 7/7 na siku hiyo Diamond amepanga kufanya kitu kikubwa akiwa  anasherekea. Mwaka huu anafanya kitu ambacho hadi mashabiki zake watafurahia siku hiyo na hii ni nafasi yako kukijua.
Quote of the Day:
Spread love everywhere you go. Let no one ever come to you without leaving happier.

Slaa: Rais Kikwete ana Rungu la Katiba Mpya Sio Maaskofu wala Taasisi

0
0
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemtaka Rais Jakaya Kikwete kujitokeza hadharani kutafuta suluhu ya kupata mwafaka wa mchakato wa Katiba Mpya kwa kuwa hakuna mamlaka nyingine zaidi inayoweza kuunusuru.

Pia, amewatahadharisha viongozi wa dini kuwa makini na kauli zao wanazozitoa za kuwataka wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kurejea bungeni Agosti 5.

Dk Slaa aliyasema hayo juzi katika mahojiano maalumu na gazeti hili, makao makuu ya Chadema Mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

“Mwenye rungu la kuweza kutengua kitendawili hiki ili turudi bungeni ni Rais (Kikwete) mwenyewe, hakuna mwingine,”alisema Dk Slaa.

“Tatizo aliyesaini waraka uliowasilishwa na Warioba ni Rais mwenyewe, alisaini ukurasa wa kwanza na wa mwisho, kwa taarifa rasmi za kina Warioba, Rais alishirikishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba hatua kwa hatua na kwa kila hatua alisema sawa mchakato uendelee,”alisema Dk Slaa.

Alikumbusha kuwa wakati akipokea Rasimu ya Pili ya Katiba, Rais Kikwete alisema: “Mtapata rasimu, ijadilini na itapitishwa na Bunge. Kwa mwanasheria yeyote, lugha kujadiliwa na kupitishwa haitoi ruhusa ya kubadilishwa, inatoa ruhusa kuboreshwa. Ndiyo utaratibu wa sheria zote duniani.”

“Sasa anapofika mahali anayeleta wazo ni Rais, lakini kwa bahati mbaya anayekwenda kupindua pia ni Rais na amekwenda mbali zaidi kiasi cha kusema kwamba kama Serikali tatu ile ile ambayo yeye ameisaini itapatikana, jeshi litapindua nchi.

“Anayezungumza ni Rais, hakuna mamlaka nyingine inayoweza kutengua kitendawili hiki. Wanaweza kuja maaskofu, ...masheikh, asasi mbalimbali... hatimaye hakuna anayeweza kutengua kwa sababu aliyeufanya ni mwenye mamlaka ya juu,”alisema.

Vanessa Mdee Adai Aliachia ‘Hawajui’ Baada ya Baadhi ya Watu Kuponda Ushindi Wake wa Kill Awards

0
0
Vanessa Mdee amesema aliachia wimbo wake ‘Hawajui’ ulioandikwa na Barnaba baada ya baadhi ya watu kudai hakustahili kushinda tuzo ya wimbo bora wa rnb (Closer) kwenye tuzo za Kili mwaka huu.

Vee Money amesema hayo kwenye mahojiano na gazeti la Daily Nation la Kenya.

“Hawajui unawahusu ‘wasema hovyo’. Hivi karibuni nilishinda tuzo za Kilimanjaro kwa wimbo bora wa R-n-B wa mwaka ambao ni wazi mashabiki wangu waliniwezesha na walifurahi sana. Lakini watu wengine wengi walisema “Oh hayuko tayari, hastahili’. Hilo lilinihuzunisha. Ulikuwa ukosoaji mkubwa wa kwanza kwangu kama mwanamuziki. Hivyo hiyo ilinisukuma kuandika kitu kuhusu watu wenye chuki lakini sio katika hali ya kawaida kwamba na wewe pia unawachukia wale wanaokuchukia,” alisema.
By Bongo5

Is Diamond Platnumz’s success a superstitious yield?

0
0
By Haji Said (Twitter: @Despicabledude)

Within the last couple of years, we have witnessed some Tanzanian artists transitioning before our very eyes into becoming regional and global superstars. Diamond Platnumz particularly has become a household name in undoubtedly many East, West, Central and South African countries. His recent BET (Best International Act: Africa) nomination amongst many others from different awards shows like MTV MAMA and AFRIMMA has created a stand-out lane for him as an artist and this cannot be taken for granted.

Amidst hearing all sorts of rumors and hear-says revolving around him being associated with superstition and nepotism such as the scandalous allegation of the star’s entanglement with the Freemason secret society; it’s only fair at times to put the cynicism aside and look rationally on what has turned an artist like Diamond Platnumz the megastar that he is.

Since we’re all allowed to have different opinions, this is a positively-angled, non-superstitious take on what might have contributed to Diamond’s successes:

Being at the right place at the right time; what most “naysayers” fail to understand is the fact that the music industry in Tanzania has been steadily growing, the recent social media revolution has provided a platform for artists like Diamond to showcase their work, engage with fans and promote his work within the country and globally.

Putting out good performances on stage and visuals is another thing which has made Diamond stand-out as a performer. Not that the industry never had or do not have artists who (can) perform well but Diamond embodies this aspect amongst others hence making him an all-around entertainer. His choreographed dance moves and back-up dancers have always been part of his spectacle on stage guaranteeing him invitation to perform in many concerts and events. To top it all off, he set a new bar for music videos in East Africa with his Number One number which is a comparatively a high-budget and undisputedly high quality video.

Having a decently good singing voice and a whole lot of catchy songs which speak and seduce many girls/ladies/women has also definitely made him the most-sought-after bongo flavor crooner. Most of Diamond’s songs are about love and relationships. His chat-topping singles like Mbagala, Kamwambie, Ukimwona and Number One have enabled him to garner such a loyal and big female fan base.

Diamond has also been romantically involved with other celebrities to which if anything, has just given him more buzz and coverage on national and international tabloids and blogs. It’s not easy to recall exactly how many popular female celebrities Diamond has dated but the recent Wema Sepetu, Jokate Mwegelo and Penny Mungilwa involvements with the star might have received more coverage on entertainment media than any other celebrity in Tanzania and possibly elsewhere in the last 2 years.

Any artist who has all these qualities and limelight-provoking situations/experiences at his/her together with a great management steering team behind him/her supporting and help to promote his/her work is definitely deemed to be the biggest pop star. The situation is alike anywhere else in the world. Diamond just happens to be the one in Tanzania right now.
By Bongo5

UFISADI Mwinge: Magufuli Awajia Juu Maofisa Tanroads

0
0
Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli amewajia juu maofisa wa Wakala wa Barabara (Tanroads) mkoani Mwanza baada ya kubaini wanataka kulipa fidia ya zaidi ya Sh100 milioni kutokana na uamuzi wao wa kupitisha barabara kwenye eneo lisilo katika mipango.

Hayo yalitokea jana wakati Waziri Magufuli akihitimisha ziara ya ukaguzi wa barabara ya Usagara-Kisesa yenye urefu wa kilometa 17.8. Magufuli alieleza kushangazwa na Tanroads kupitisha barabara katika eneo la Halmshauri ya Wilaya ya Magu, hivyo  kutakiwa kulipa fidia na kuacha eneo la wazi ambalo halihitaji malipo.

Waziri Magufuli alisema kuna mbinu za kutaka kujenga kituo cha mafuta kwenye eneo ambalo limeachwa wazi na Tanroads, hivyo kuamuru barabara hiyo irejeshwe kwenye eneo lililopangwa.

Waziri Magufuli alisema hawezi kuvumilia kuona barabara inachelewa  kwa madai ya ulipaji fidia, huku   maeneo ambayo hayatakiwi kulipiwa fidia yanachwa wazi bila sababu za msingi.

“Ucheweshaji huu wa kipande hiki cha kilometa tano, ni jambo la ajabu kuona mnaacha kupitisha barabara kwenye eneo ambalo halina vikwazo vyovyote,” alihoji Dk Magufuli.

Dk Magufuli alisema anatambua kila kitu kinachoendelea katika ujenzi wa barabara hiyo na suala la fidia halifanywi kwa bahati mbaya.

 “Hivi nyie mnadhani fedha za Serikali zinachotwa tu… naomba majibu kwanini mmekuja kwenye eneo la halmashauri na kutaka kulipa fidia wakati barabara ya zamani kuna eneo kubwa ambalo linatosha bila kulipa hata senti tano? Mtambue kwamba barabara hii inajengwa na fedha za Serikali zaidi ya Sh17 bilioni,” alisema na kuongeza:

“Au hizi nyumba mnazotaka kulipa fidia ni za ndugu zenu. Nafahamu kuna mbinu ya kutaka kupitisha huku ili kule muache eneo la ujenzi wa kituo cha mafuta. Kuanzia sasa naomba ujenzi huu urudi kule.”

Awali, akisoma taarifa ya ujenzi, mkandarasi wa madaraja, Elias Boniface alisema ujenzi wa barabara hiyo unaofanywa na kampuni ya Nyanza Road Work Limited umekamilika kwa asilimia 37.5

Alisema barabara hiyo itakuwa kiunganishi cha magari yanayotoka nchi jirani kwenya Mkoa wa Mara na nchini Kenya.

Funny Quote of the Day
If you can't convince them, confuse them.

Zambi: Serikali Mbili ni Maagizo ya Jakaya Kikwete

0
0
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya, Godfrey Zambi amefichua sababu za chama hicho kushikilia msimamo wa muundo wa serikali mbili katika mjadala wa Katiba Mpya, akisema ni “maagizo ya mwenyekiti wa CCM”.

Mjadala wa Katiba Mpya ulikumbwa na mtikisiko baada ya Rais Jakaya Kikwete kueleza kitu alichokiita maoni yake binafsi wakati akizindua Bunge la Katiba kwa kueleza kuwa angependa muundo wa Muungano wa serikali mbili tofauti na Rasimu ya Katiba iliyopendekeza serikali tatu.

Mjadala huo ulivurugika kabisa baada ya kundi la wajumbe kutoka vyama vya upinzani waliounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao likidai mjadala umepoteza mwelekeo kwa kuweka kando maoni ya wananchi ya kutaka muundo wa serikali tatu.

Akifungua mkutano wa Baraza la Utendaji la Umoja wa Vijana wa CCM wa Mkoa wa Mbeya juzi jioni, Zambi alisema mwenyekiti wa CCM alishawaambia kwamba msimamo wa chama ni kuhakikisha zinabaki serikali mbili kwenye Katiba Mpya.

 ‘’Vijana sasa lazima niwaeleze ukweli kuhusu muundo wa serikali, ni kwamba piga ua, CCM inataka kuimarisha muundo wa serikali mbili na hili ni agizo la mwenyekiti wetu Rais Jakaya Kikwete,” alisema huku akishangiliwa.

Alisema suala la Muungano ni maelewano na kwamba baadhi ya shughuli muhimu za Zanzibar zimehamishiwa Bara wakati nyingine za Bara zimehamishiwa Zanzibar.

 Hata hivyo, alisema kero iliyopo kwa sasa kwenye Muungano huo ni namna ya kugawana mapato makubwa ambayo alisema Serikali inaendelea kuyafanyia kazi.

 “Rais Kikwete katika kutueleza msimamo wa chama, pia alifafanua vizuri suala la serikali tatu kuongeza gharama za uendeshaji, jambo ambalo hata mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba aliliona, ingawa alifafanua kwamba halina namna,” alisema.

 Zambi, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, alisema anamshangaa Mwenyekiti wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe anapotamka kwamba serikali tatu ni lazima.

“Vijana wote na wanaCCM mkoani Mbeya naomba muelewe kwamba sisi chini ya mwenyekiti wetu wa CCM, Rais Kikwete, tumeamua muundo wa serikali mbili tu,” alisema.

Alisisitiza kwamba kama wachache hawataafiki msimamo huo kwa busara, Serikali ya CCM itaendelea na katiba iliyopo.

Akieleza sababu za msimamo wake wa serikali mbili wakati akizindua Bunge la Katiba, Rais Kikwete alizungumzia gharama za uendeshaji wa serikali tatu akisema katika muundo wa serikali tatu, Serikali ya Muungano haitakuwa na vyanzo vya uhakika vya fedha na kwamba hilo linaweza kusababisha kushindwa kulipa mishahara kama ya wanajeshi na hivyo kusababisha chombo hicho cha dola kuchukua serikali.

Kiongozi wa CHADEMA kanda ya Magaharibi Ashambuliwa

0
0
WATU wasiojulikana wamemvamia na kumpiga pamoja na kumjeruhi sehemu mbalimbali za mwili kwa kutumia vitu vyenye ncha kali Makamu Mwenyekiti wa uenezi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kanda ya Magaharibi,Deogratius Liyunga na kupelekea kulazwa katika Hospita ya Mkoa wa Kigoma (Maweni).

Tukio hilo limetokea jana majira ya  saa tano usiku katika eneo la Mlole Manispaa ya Kigoma Ujiji,wakati kiongozi huyo akiwa njiani kurudi nyumbani kwake akitokea eneo la Mwanga kuangalia mechi za  kombe la Dunia.

Akiongea na mtandao huu wodini na alipolazwa juu ya tukio hilo,kiongozi huyo alisema kuwa alibakiza hatua 25 iliaweze kuingia nyumbani kwake ghafla walitokea watu wanne,mmoja alimvamia na kumkaba shingo huku wale wengine wakimshambulia kwa kisu,nyembe na ubao.

Alisema mbali ya watu hao kumpiga na kumjeruhi lakini walimpora fedha kiasi cha shilingi 63,000 ingawa hawakufanikiwa kumpora simu yake ya mkononi iliyokuwa mfukoni.

Baada ya watu hao waliomvamia kuondoka alifanya mawasiliano kwa watu wake wa karibu wakiwemo wanachama wa CHADEMA ambao walifika eneo la tukio na kumkimbiza Hospital kwaajili ya matibabu.

 Makamu Mwenyekiti alisema kuwa tukio hilo lililomkuta linahusiano mkubwa na masuala ya kisiasa kwani kabla ya tukio hilo amekuwa akipokea ujumbe mfupi wa maneno ya vitisho  kwenye simu yake ya mkononi kutoka kwa watu wanaodaiwa kuwa ni wananchama wa chama kipya cha ACT.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kigoma,Frasser Kashai alipopigiwa simu na mtandao huu kuthibitisha juu ya tukio hilo alisema hana taarifa zozote kuhusiana na tukio hilo.

”Mimi hiyo taarifa sijaipata ofisini kwangu bado ndo nina isikia kutoka kwako ngoja nifuatilie nitakujulisha”alisema Kashai.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images