Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live

JE Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?
Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

Nilijiona Mkosaji Wakati Ndikumana Anapambana na Ndoa Yake na Irene na Sikutaka Kumuumiza Mwanaume Mwenzangu- Msami

$
0
0
Nilijiona Mkosaji Wakati Ndikumana Anapambana na Ndoa Yake na Irene na Sikutaka Kumuumiza Mwanaume Mwenzangu- Msami
Mwanamuziki wa bongo fleva nchini Msami Baby amefunguka na kusema wazi kwamba aliwahi kujuta kuwa na mahusiano na Irene Uwoya baada ya kujua kwamba anamuumiza aliyekuwa Mume wa muigizaji huyo, Marehemu Hamadi Ndikumana aliyefariki

usiku wa kuaMkia jana huko Rwanda.
Msami amefunguka na kusema kwamba hakuwahi kumchukia Mwanaume huyo (Ndikumana)  na kwamba kutokana na heshima aliyokuwa anampatia ndikumana ilimfanya aamua kuvunja mahusiano  hayo.
Msami amesema kwamba baada ya kugundua kwamba Ndikumana anapambania Ndoa yake na Irene Uwoya alijihisi mkosaji kitendo kilichomfanya ajisikie vibaya na hata lugundua kwamba nikitendo kisichopendeza mbele za Mungu.
"Kuna kitu kiliniambia nachokifanya siyo sahihi, nilimwambia Irene wewe umefunga ndoa ya kikristo na mimi nimetumikia kanisani kwa muda wa miaka saba hivyo naijua vizuri dini,  kuendelea kumuumiza mwanaume mwenzangu sikuona kama kuna maana ndiyo maana nilirudi kwa Mungu wangu na kujutia makosa niliyoyafanya" Msami.
Ameongeza "Sikuwahi kumfuata Ndikumana kumuomba msamaha kwa sababu nilikuwa na mahusiano na mwanamke wake, lakini nilienda luongea na Mungu wangu kisha nikaungama dhambi zangu ndiyo maana mimi na Irene tukaendelea kuwa Marafiki lakini kusikia tena jamaa amefariki imeniumiza sana.
Msami ni mwanaume ambaye alitajwa kuwa na mahusiano na Irene Uwoya kwa muda mrefu ingawa wao walikuwa wakikanusha na baada ya kuachana Msami alikiri kwenye FNL ya EATV kwamba aliwahi kuwa kwenye  mahusiano na muigizaji huyo

Inasikitisha Mwanaume Auawa Kikatili na Kunyofolewa Sehemu za Siri Kisa Kukutwa na Mipira ya Kiume Mifukoni Mwake

$
0
0
Mwanaume Auawa Kikatili na Kunyofolewa Sehemu za Siri Kisa Kukutwa na Mipira ya Kiume Mifukoni Mwake
Mwanaume mmoja nchini Thailand ameuawa kikatili na mke wake kwa kukatwa na kisu sehemu zake za siri baada ya kukutwa na mipira ya kiume mfukoni.

Mwanaume huyo aliyetambulika kwa jina la Amnuay Wensila (62) alikutwa na kondom kwenye mifuko yake na mkewe baada ya kurejea nyumbani akitoka kazini. Ndipo alipoulizwa na kushindwa kutoa maelezo.

Taarifa kutoka gazeti la Post Today la nchini humo zimeeleza kuwa mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina la Nittaya Saengdeuan (22) alianza kumchoma kisu kwenye mwili wake kabla ya kumuua kwa kumkata sehemu zake za siri.

Baada ya kutekeleza mauaji hayo, Bi. Nittaya aliuchukua mwili wa marehemu na kuufunika kwenye pipa nje ya nyumba yao.

Awali, Nittaya alikataa kutoa ushirikiano na polisi akidai kuwa hajahusika na chochote kuhusu kifo cha mmewe akidai kuwa hata yeye alikuwa anamtafuta.

Hata hivyo, baada ya mahojiano marefu na kamanda wa polisi mjini Udon Thani,  Peerapong Wongsaman ambako tukio hilo lilikotokea alikubali kutekeleza mauji hayo.


Bi Nattaya kwenye mahojiano na Kamanda wa Polisi.

Nittaya kwenye maelezo yake amesema alichukua maamuzi ya kumkata uume mumewe baada ya kukuta kondomu kwenye mifuko yake kwani aliamini kuwa ameshasalitiwa.

“Tulifanya nae mahojiano kwa muda mrefu na mwanamke wa Amnuay Wensila (62) na amekiri kutekeleza mauaji ya mumewe kwa kumchoma sehemu zake za siri kutokana na wivu wa mapenzi na tayari taratibu za kumpeleka mahakamani zinafanywa.“amesema Kamanda Peerapong Wongsaman.

Nittaya atakamiliwa kwa kesi ya kuua kwa kukusudia na hii inakuwa sio mara ya kwanza kutokea nchini Thailand kwani mwaka 2015 liliripotiwa tukio kama hilo ambapo mwanamke mmoja alimuua mumewe kwa kumwagia tindikali akiwa usingizini baada ya kukuta meseji ya mahaba kuingia kwenye simu yake wakiwa wamelala.

Chanzo : Today Post & Linda Ikeji

Mugabe Awa King'ang'anizi Akataa Wito wa Kuondoka Madarakani

$
0
0
Mugabe 'Akataa Wito wa Kuondoka Madarakani
Rais wa miaka mingi nchini Zimbabwe anaripotiwa kukataa kuandoka madarakana mara moja licha ya kuongezeka wito wa kumtaka ajiuzulu.
Mugabe, 93 aliwekwa chini ya kuzuizi cha nyumbani wakati jieshi lilichukua madaraka siku ya Jumatano kufuatia mvutano kuhusu ni nani atamrithi.
Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu mazungumzo yaliyofanywa Muganbe na ujumbe kutoka kanda hiyo pamoja na mapema.
'Mamba' ambaye amegeuka kumuuma Mugabe
Lakini taarifa zinasema kuwa amekataa kuondoka madarakani.
Kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai alisema mapema kuwa kwa manufaa ya watu Mugabe anastahili kujiuzulu mara moja.

Jeshi lilichukua hatua baada ya Rais Mugabe kumfuta makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa, wiki iliyopiya, na kuashiria kuwa alimpendelea mke wake Grace Mugabe, kuchukua uongozi wa chama cha Zanu-PF na kuwa rais.
Taarifa zinasema kuwa Mugabe ambaye alikuwa madarakani tangu nchi hiyo ipate uhuru mwak 1980 anakataa kuondoka kwa hiari kabla ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kuandaliwa mwaka ujao.
Watu wasubiri hatua za jeshi Zimbabwe
Baadhi ya wadadisi wanasema kuwa Bw. Mugabe anaweza kujaribu kujihakikishia usalama na familia yake kabla ya kuondoka madarakani.
Maafisa wa Zanu PF mapema walikuwa wamesema kuwa Bw. Mugabe atasalia madarakani hadi ufanyika mkutano mkuu wa Chama mwezi Disemba wakati Bw. Mnangagwa atakiongoza chama na hatimaye kuwa rais

Kifungo cha Lulu ni Pigo Kubwa kwa Muna Asema "Ntafunga na Kumuombea Usiku na Mchana Atoke"

$
0
0
Kifungo cha Lulu ni Pigo Kubwa kwa Muna Asema "Ntafunga na Kumuombea Usiku na Mchana Atoke"
MMOJA kati ya wasanii wa karibu wa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ni Rose Alphonce ‘Muna’ ambaye tangu aanze kukumbana na tatizo hili la kesi ya mauaji bila ya kukusudia dhidi ya msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba amekuwa naye bega kwa bega.

Muna ni miongoni mwa wasanii wa filamu zao la Kaole ambaye amejitolea kuwa kama dada wa hiari kwa Lulu, ameonyesha moyo wa kipekee kuliko msanii yeyote Bongo ambapo amekuwa karibu kuanzia siku ya kwanza ya kesi ya Lulu mpaka siku ya hukumu.

Ijumaa limemtafuta Muna na kuzungumza naye mengi juu ya ukaribu huo ambapo amesema kuwa amepokea hukumu ya Lulu ya miaka miwili jela kwa masikitiko makubwa sana lakini kitu anachoamini hilo ni jaribu tu itafika wakati litapita na ataendelea na maisha yake mengine.

Muna akitoka mahakamani baada ya rafiki yake Lulu kuhukumiwa kifungo cha mika miwili jela.
“Unajua mimi namuamini sana Mungu,naamini kabisa hilo ni jaribu na ipo siku litapita na Lulu ataendelea na maisha yake ya zamani kama kawaida,” anasema Muna.

Muna anaongeza kuwa, atakumbuka sana kipindi chote alichokuwa na Lulu, katika mambo mbalimbali waliokuwa wakifanya pamoja kwenye shida na kwenye raha ambapo walipita naye pamoja lakini kubwa atakalolifanya ni kufunga na kumuombea usiku na mchana. “Nitakumbuka nyakati zote nilizokuwa naye pindi yupo uraiani. Kuanzia siku aliopewa huku kazi yangu moja tu sasa kufunga na kuomba kwa ajili yake,” anasema Muna.
Chanzo: Global Publishers

Haipaswi Kumuhukumu Lulu na Kumcheka Ila ni Kujifunza Kitu kwenye Mapenzi Kupitia Yeye- Penny

$
0
0
Haipaswi Kumuhukumu Lulu na Kumcheka Ila ni Kujifunza Kitu kwenye Mapenzi Kupitia Yeye- Penny
MTANGAZAJI wa Kipindi cha Harusi Yetu kinachorushwa kupitia Televisheni ya Magic Swahili, Penniel Mungilwa ‘Penny’ amewaasa watu wajifunze kupitia muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’.

Akizungumza na Star Mix Penny alisema kuwa, haipaswi kumuhukumu Lulu na badala yake kujifunza kwani jambo kama hilo linaweza kumpata mtu yeyote. “Jamani hakuna sababu

Elizabeth Michael ‘Lulu’.
ya kumsema Lulu vibaya au kumcheka ila ni kujifunza kuwa tukio kama hilo linaweza kumpata mtu yeyote hivyo mwenzio akipatwa na jambo kama hilo ni vyema kumuombea,” alisema Penny.
Stori zinazo husiana na ulizosoma

Balozi Afunguka Ukweli Kuhusu Dkt Shika Atoboa Siri Alivyomsafirisha Kijasusi Kutoka Urusi

$
0
0
Siku mbili zikiwa zimepita tangu Dk Louis Shika kuelezea siku 28 za mateso aliyoyapata nchini Urusi, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini humo wakati huo, Patrick Chokala amefichua siri jinsi walivyomsafirisha kijasusi ‘bilionea huyo wa nyumba za Lugumi’ kurudi Tanzania.

Balozi Chokala aliyekuwa Urusi kati ya mwaka 2002 na 2008 katika kipindi ambacho sakata la utekwaji wa Dk Shika lilijitokeza, amethibitisha kuwa ni kweli Mtanzania huyo ni daktari na kwamba ni kweli amewahi kutekwa.

Dk Shika anatuhumiwa kuvuruga mnada wa majumba ya mfanyabiashara maarufu, Said Lugumi uliofanywa na kampuni ya Yono baada ya kufika bei ya kuzinunua nyumba hizo tatu kwa Sh3.2 bilioni, lakini akashindwa kutimiza sharti la kulipa asilimia 25 ya fedha hizo.

Kushindwa huko kulipa kulisababisha awekwe rumande katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam kwa siku sita hadi alipoachiwa kwa kujidhamini mwenywe Novemba 14 na kutakiwa kuripoti kila siku.

Mara baada ya kutoka polisi kwa dhamana, Mwananchi lilifanya mahojiano maalumu na Dk Shika nyumbani kwake Tabata Mawenzi na alieleza mambo mbalimbali ikiwamo kutekwa na kuteswa akiwa Urusi Juni 2004, ikiwa ni pamoja na kukatwa vidole viwili mkono wa kushoto na kimoja mkono wa kulia.

Pia alieleza jinsi alivyofanikiwa kuwatoroka watekaji hao.

Balozi Afunguka Ukweli Kuhusu Dkt Shika Atoboa Siri Alivyomsafirisha Kijasusi Kutoka Urusi
Jana, Mwananchi lilizungumza na Balozi Chokala ambaye alisema analikumbuka vizuri tukio la kutekwa kwa Dk Shika na jinsi ubalozi ulivyomsaidia asipatwe na kadhia kubwa zaidi. “Ni kweli huyo jamaa ni daktari wa binadamu. Alisoma Chuo Kikuu cha Lumumba kilichopo Moscow, Urusi,” alisema Balozi Chokala.

Alisema kutokana na upekee wa yaliyomsibu Dk Shika, ubalozi ulilazimika kuingilia kati ili kunusuru maisha yake.

Kwa kumbukumbu zake, balozi huyo alisema Dk Shika alitekwa na majambazi waliokuwa wanataka fedha ambazo yeye mwenyewe (Dk Shika) alikuwa anajigamba kuwa nazo na kuwashawishi watekaji hao kumfuatilia. “Majigambo ya kumiliki fedha nyingi hajayaanza leo. Tangu akiwa Urusi alikuwa anasema anamiliki fedha nyingi. Watu walimuamini kwa sababu alikuwa daktari anayetambulika, matokeo yake alitekwa,” alisema Chokala, ambaye amewahi kuwa mwandishi wa Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi.

Balozi huyo alisema baada ya kufanikiwa kuwatoroka majambazi hao ambao baadaye walikamatwa na polisi nchini humo kisha kufunguliwa mashtaka, Dk Shika alipelekwa hospitali kwa matibabu akiwa amepoteza vidole kadhaa vya mikono yote miwili.

Alisema majambazi hao walimtesa kwa muda mrefu kwa kuwa mpaka anapatikana vidole hivyo vilikuwa vimeanza kuoza.

“Walimshikilia kwa muda mrefu kwa kuwa walihitaji fedha ambazo Dk Shika hakuwa nazo,” anakumbuka balozi huyo aliyestaafu mara baada ya kurudi nchini.

Alisema baada ya ubalozi kupewa taarifa zake, ulifuatilia na kugundua kwamba alipelekwa nchini humo na Wizara ya Afya, na alikuwa amelipiwa kila kitu ikiwa ni pamoja na tiketi ya ndege.

Wakati anatekwa, alisema Dk Shika alikuwa ameshahitimu lakini hakuwa na nauli ya kurudi nyumbani, hivyo akawa anahangaika kupata nafasi ya kuendelea na shahada ya uzamili. “Tulipowasiliana na wizara walithibitisha kuwa ni mtu wao. Tuliandaa utaratibu wa kumrudisha bila yeye kujua kwa sababu hakuwa anataka kufanya hivyo,” alisema.

Akiwa anaendelea kuhudumiwa, ubalozi ulimuandalia safari ya kurudi bila yeye kufahamu kuepuka asitoroke. Balozi Chokala alisema ilikuwa ni lazima Dk Shika arudishwe kuepusha janga jingine linaloweza kumkuta endapo angeendelea kuishi nchini humo. “Kujirudia kwa tatizo kama hilo kungeupa ubalozi lawama. Hatukutaka kujiweka kwenye nafasi hiyo,” alisema.

Baada ya mipango yote kukamilika, askari wa ubalozini walimpeleka uwanja wa ndege na kumkabidhi kwa wahudumu wa ndege iliyokuwa inakuja Tanzania wakiwaelekeza wasimshushe popote isipokuwa Dar es Salaam ambako Wizara ya Afya ilikuwa inamsubiri.

Mpango huo ulitekelezwa kama ulivyopangwa na wizara ikathibitisha kumpokea mtumishi wake huyo ambaye balozi Chokala anasema alipewa nyumba na akawa anaendelea na majukumu yake. “Akiwa Urusi, nilielezwa kuwa alikuwa ana matatizo ya kijamii ambayo yaliendelea kumuandama hata aliporudi. Nasikia kuna wakati alienda kwao na hakurudi tena kazini,” alisema.

Kwa muda wote wa kushughulikia sakata la ‘bilionea’ huyo, balozi alisema hakuonana naye na alipomsikia kwenye vyombo vya habari akawa hana uhakika ingawa jina lilikuwa lenyewe. “Siwezi kumsahau. Tukio lake lilikuwa la kipekee,” alisema na kufafanua kuwa ubalozi haukuendelea kufuatilia kesi yake kwa kuwa walichokipa kipaumbele ni usalama wa Mtanzania huyo.

Kuhusu Dk Shika kuwa ni Rais wa kampuni ya Lancefort aliyoianzisha akiwa Urusi ambayo Serikali ya nchi hiyo ilitilia shaka mwenendo wake, hivyo kuifuatilia, Balozi Chokala alisema hafahamu chochote.

“Siwezi kulizungumzia hili. Kwa wakati huo, usalama wake ulikuwa muhimu zaidi na ndio tulioupa kipaumbele,” alisema.
Chanzo: Mwananchi

Tundu Lissu Afanyiwa Upasuaji Mwingine Nairobi Sasa Kufikia Upasuaji wa 18

$
0
0
Tundu Lissu Afanyiwa Upasuaji Mwingine Nairobi Sasa Kufikia Upasuaji wa 18
 Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu amefanyiwa upasuaji wa 18.

Upasuaji huo ulifanyika jana katika hospitali ya Nairobi nchini Kenya ambako Lissu anaendelea na matibabu tangu Septemba 7, baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa katika makazi yake, area D mjini Dodoma.

Akizungumza na Mwananchi jana kwa simu, kaka yake Lissu, Alute Mughwai alisema, “Lissu leo (jana) amefanyiwa upasuaji ambao ulianza asubuhi na umemalizika salama. Nimeambiwa muda mfupi uliopita (ilikuwa saa 9.32 alasiri wakati akizungumza na Mwananchi) kuwa ameshatoka chumba cha upasuaji.”

Alute alisema, “Nimeambiwa upasuaji ulikwenda vizuri na sasa atapaswa kupumzika kama siku nne kisha ataendelea na mazoezi kama kawaida.”

Ingawa Alute hakueleza huo ni upasuaji wa ngapi, Oktoba 17 mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari alisema Lissu alikuwa amefanyiwa upasuaji mara 17 hivyo kama hakufanyiwa mwingine huo wa jana utakuwa ni wa 18.

“Lissu mpaka sasa amefanyiwa upasuaji mkubwa mara 17, ameongezewa damu nyingi kuliko mgonjwa yeyote aliyewahi kutibiwa hospitali hiyo ya Nairobi kwa miaka 20 iliyopita,” alisema Mbowe siku hiyo.

Alute alisema mpaka sasa bado hawajaanza mipango ya kushughulikia matibabu ya awamu ya tatu ambayo yalielezwa na Mbowe kuwa yatafanyikiwa nje ya Kenya.

“Nilisema nitazungumza na waandishi, lakini sijafanya hivyo kwani hakuna taarifa zaidi ya hizi na utaratibu wa matibabu ya awamu ya tatu bado hayajaanza ndio maana niko kimya,” alisema Alute

Pata Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za Full Power

Ni Dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,
Dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin E pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30

ZAT 50 inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.

Kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende tunapatikana daresalaam na mikao wasiliana nasi DR Oshinda Namba za simu 0755505099/0714126118

Karibuni kwa hunduma bora

Mshambuliaji wa Azam FC Waziri Junior Apata Pigo Mama Yake Mzazi Afariki Dunia

$
0
0
Mshambuliaji wa Azam FC Waziri Junior Apata Pigo Mama Yake Mzazi Afariki Dunia
Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Azam FC Wazir Junior amefiwa na mama yake mzazi usiku wa kuamkia leo nyumbani kwao wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Taarifa kutoka klabu hiyo zimethibitisha msiba huo ambapo tayari mchezaji huyo amepewa ruhusa ya kwenda nyumbani kwaajili ya kushiriki msiba huo wa mama yake.
Klabu ya Azam FC imepokea kwa masikito makubwa msiba huo mzito wa mama yake Wazir hivyo imeungana na familia nzima kwenye kipindi hiki kigumu.
Wazir alikuwa amesafiri na timu kuelekea Njombe kwaajili ya mchezo wa ligi wikiendi hii dhidi ya Njombe Mji lakini tayari ameenza safari ya kurejea Dar es salaam asubuhi hii ambapo ataunganisha hadi Lushoto Tanga.
Uongozi wa Azam FC kwa niaba ya mashabiki na klabu kwa ujumla, umetoa salamu za rambirambi kwa ndugu, jamaa na marafiki pamoja na familia ya Junior.

Rich Mavoko Awakana Gigy Money na Lulu Diva " Sijawahi Kutoka Kimapenzi na Gigy Labda Yeye Ameamua Kutangaza"

$
0
0
Rich Mavoko Awakana Gigy Money na Lulu Diva " Sijawahi Kutoka Kimapenzi na Gigy Labda Yeye Ameamua Kutangaza"
Msanii wa Bongo Flava kutoka label ya WCB, Rich Mavoko amesema hakuna ukweli wowote kuhusu yeye kutoka kimapenzi na Gigy Money na Lulu Diva.

Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha The Playlist, Times Fm kuwa hasa ishu ya Gigy Money ni stori za kutengeneza tu hasa pale alipomuimba katika ngoma ya ‘Mpe Habari’ abaymo alifanya na Stereo.

“Sema mimi sijawahi kusema natoka naye labda yeye atangaze kwa kuamua kuongea lakini nafikiri ni vitu ambavyo vimeshapita hata kuviongelea huwa staki” amesema.

Kuhusu Lulu Diva, Mavoko amesema wao ni marafiki tu wa kawaida na hivi karibuni hawajaonana kutoka Lulu alikuwa bize na show zake.

Tena sijaonana naye muda huwezi amini, nimekuja kuonana naye hivi karibuni kwa sababu na yeye alikuwa yupo bize alikuwa na show, ndivyo anavyoweza kulizungumzia.


Snura Ajipongeza Kulea Familia Bila Mzazi Menzie "Lazima Nijiandalie Tuzo Kulea Familia Mwenyewe si Jambo Dogo"

$
0
0
Snura Ajipongeza Kulea Familia Bila Mzazi Menzie "Lazima Nijiandalie Tuzo Kulea Familia Mwenyewe si Jambo Dogo"
MWANAMUZIKI aliyejizolea jina kubwa kupitia wimbo wake wa ‘Majanga’ Snura Mushi amefunguka kuwa anatarajia kujipa tuzo ya kupambana mwenyewe kwenye maisha akiwa kama baba na mama kwa wakati mmoja.

Akizungumza na Showbiz Snura alisema kuwa, wanawake wengi siku hizi wamekuwa wapambanaji peke yao hivyo basi siyo vibaya kujitukuza.

“Kulea familia mwenyewe siyo kazi ndogo na siku hizi wanawake wengi tunapitia hili hivyo mimi mwenyewe najiandalia tuzo kabisa angalau nijipe moyo nizidi kutafuta kwa ajili ya wanangu,” alisema Snura

Kamati ya Maadili Yamuweka Kikaangoni Kubenea Ahojiwa kwa Kosa la Kutoa Kauli ya Kudharau Bunge

$
0
0
Kamati ya Maadili Yamuweka Kikaangoni Kubenea
Kamati ya  Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, imemhoji  Mbunge wa Ubungo Mheshimiwa Saed Kubenea kwa kosa la kutoa kauli ya kudharau Bunge.

Akizungumza mara baada ya kumhoji Mbunge huyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mheshimiwa Almasi Athuman  Maige (Mb) alisema, Mheshimiwa  Kubenea amefikishwa mbele ya Kamati  hiyo kujibu tuhuma inayomkabili kutokana na kauli aliyotoa kitendo ambacho   ni kinyume na kifungu cha 26 (e) na 34 (1) (a)   ya Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge, Sura ya 296.

Mheshimiwa Maige alisema mahojiano hayo yamefanyika  leo (jana) baada ya kuahirishwa mara mbili kutokana na Mheshimiwa Kubenea kutokua katika hali nzuri kiafya na hivyo kuomba mahojiano yaahirishwe.

Mheshimiwa Maige aliongeza kuwa  baada ya kumsikiliza Mhe. Kubenea itaandaa Taarifa yake na kuiwasilisha kwa Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai kwa hatua zaidi.

“Kanuni zimeweka masharti kuwa shughuli za Kamati hii zinazofanywa zitabakia kuwa ni siri hadi hapo itakapomaliza kazi yake na kuwasilisha taarifa Bungeni,” alisema.

Singapore Yasitisha Biashara na Korea Kaskazini

$
0
0
Singapore Yasitisha Biashara na Korea Kaskazini
Singapore imesitisha shughuli zote za biashara na Korea Kaskazini wakati ambapo Umoja wa Mataifa na Marekani wanataka kuiwekewa vikwazo vikali.
Forodha nchini Singapore zilisema kuwa bidhaa za biashara kutoka Korea Kaskazini zilipigwa marufuku kuanzia tarehe 8 Novemba.
Wale watakiuka marufuku hiyo watafungwa kwa hadi miaka miwili.
Marufuku hiyo inachukuliwa baada ya Umoja wa Mataifa kuiwekea vikwazo Korea Kaskazini kufuadtia jaribio ya sita ya nyuklia.
Singapore ilichukua nafasi ya nane kama mshirika wa kibiashara wa Korea Kaskazini.
Asilimia kubwa ya biashara za korea kaskazini ni pamoja na China, mshirika mkubwa wa kiuchumi wa taifa hilo.
Awamu ya hivi karibu ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa ililenga makampuni na watu binafsi pamoja na makampuni mawili nchini Singapore.
Mwezi Januari mwaka 2016 kampuni moja nchini Singapore ilipigaw faini ya dola 125,000 kwa kusaidia kusafiridsha silaha kutoka nchini Cuba kwenda Korea Kaskazini baada ya mahakama kupata kuwa kampuni ya Chinpo wa usafiri wa baharini ilikiuka azimio la Umoja wa Mataifa.

Lema- “Toka Nimekuwa Mbunge Sijawahi Kupata Raha Katika Uongozi Wangu"

$
0
0
Lema- “Toka Nimekuwa Mbunge Sijawahi Kupata Raha Katika Uongozi Wangu"
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kupitia CHADEMA, ameweka wazi matatizo anayoyapata kama mbunge wa wananchi wake anaowatumikia, na kusema kwamba kama viongozi wao wanaumia zaidi wanapoona hawawaelewi wanachokifaya.

Lema ameyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara akifanya kampeni kwa ajili ya chaguzi ndogo ndogo za udiwani katika kata ya Muriet mkoani Arusha, na kueleza kwamba wao kama wabunge wao wanajitoa muhanga kuwatetea wananchi wao, lakini huwa wanaumia zaidi pale wananchi hao kuonekana hawajali wala hawaoni jitihada zao.
“Mimi ni mbunge ambaye nimekaa hospitali kumuuguza mbunge mwenzangu ambaye amepigwa risasi. Tundu Lissu amepigwa risasi kwa sababu ya kutetea uhuru wenu, tukiona hamuelewi mnatuumiza kuliko hao wanaotupiga, kama kuna kuna mateso tunapata kama viongozi wenu ni wakati nyie ambao tunawapigania hamtuelewi, tunaumia kuliko maelezo”, amesema Godbless Lema.
Godbless Lema ameendelea kwa kusema kwamba yeye binafsi anakumbana na changamoto nyingi kwani tangu apate wadhifa huo hajawahi kupata raha, kutokana na misuko suko anayoipata kutoka kwa jeshi la polisi na kudhalilishwa.
“Toka nimekuwa mbunge wenu sijawahi kupata raha katika uongozi wangu, mimi ni mbunge ambaye nimepigwa sana, nimedhalilishwa sana na polisi, ni mbunge ambaye nyumbani kwangu polisi wamesachi mpaka nguo za ndani za mke wangu, kunidhalilisha na kutisha, nimekwenda jela miezi minne na siku 12, nimetekwa ili kuuawa, nimefukuzwa bungeni, kesi nilizonazo ni nyingi, nina kesi mbili dhidi ya Rais na siogopi, na haya yote kwa ajili yenu nyinyi”, amesema Godbless Lema.
Godbless Lema amekuwa mbunge ambaye mara kwa mara anakabiliana na jeshi la polisi kwa makosa mbali mbali anayotuhumiwa, ambapo mpaka sasa bado ana kesi zinazomkabili mahakamani.


Kubenea Awachomea Wafanyakazi wa Kiwanda cha Urafiki, Waziri Ahaidi Kuwashughulikia

$
0
0
Kubenea Awachomea Wafanyakazi wa Kiwanda cha Urafiki, Waziri Ahaidi Kuwashughulikia
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage amesema wafanyakazi wa kiwanda cha nguo cha Urafiki waliobinafsisha kiwanda hicho na kuiingizia hasara serikali watashughulikiwa ipasavyo.

Mwijage ameyasema hayo bungeni leo wakati akijibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na mbunge wa Ubungo Mh. Said Kubenea aliyetaka kujua hatua watakazo chukuliwa wafanyakazi walioshiriki kubinafsisha kiwanda cha urafiki kwa mwekezi kutoka China ambaye ameshindwa kuleta faida.
“Ukiiona ripoti ya mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG utalia Kubenea, kwahiyo kila mtu aliyehusika kutuingiza kwenye dhahama hii rungu litamshukia kama Mwewe”, amesema Waziri Mwijage
.
Aidha Waziri amesema kuwa tayari serikali ipo mbioni kumaliza makubaliano na mwekezaji mpya kutoka China ambapo kiwanda hicho kitajengwa upya vizuri na serikali itanufaika kwa takribani asilimia 75.
Waziri Mwijage ameongeza kuwa kiwanda cha Urefiki ni cha kihistoria hivyo watakijenga upya na kitakuwa na wafanyakazi zaidi ya elfu nane.

Simu Aina ya Samsung Galaxy Note 4 Inauzwa Kwa Bei Nafuu Kabisa

$
0
0

Samsung Galaxy Note 4 mpya kabisa na haina matatizo
Bei Shillingi 600,000.

Piga namba ya simu:
0718785554 /0786424272

Inapatikana Tabata Segerea

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo...

$
0
0

MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Tupo Mbagala Rangi Tatu

Manchester United Hawakuwa Wakimhitaji Di Maria Bali Waliitaka Jezi yake tu

$
0
0
Kati ya usajili ambao Luis Van Gaal aliufanya na ukawa gumzo dunia nzima ilikuwa ni usajili wa Angel Di Maria kutoka Real Madrid ambaye baada ya msimu mmoja tu waliamua kuachana naye akaenda PSG.

Wakati Di Maria akiondoka kwenda PSG hakuna bosi wa United alihangaika kumbembeleza abaki katika timu yao na walionekana walikuwa tayari kumuacha mchezaji huyo aondoke ndani ya muda mfupi.

Imebainikwa kwamba Manchester United walikuwa wakihitaji zaidi mauzo ya jezi ya Di Maria kuliko walivyokuwa wakihitaji uwepo wake katika timu hiyo na hilo lilimkera Muargentina huyo.

Msemaji wa mchezaji huyo amethibitisha kwamba United hawakumhitaji Di Maria ili kushinda makombe na walikuwa wakiambiana kwamba wakimnunua atawasaidia sana katika mauzo ya jezi.

Debora Gomes amesema Di Maria hakuwa na furaha ndani ya United na mabosi hawakuwa na habari naye huku akisema baada ya Fergie kuondoka sasa United imekuwa klabu ambayo haiwazi kuhusu soka tena bali jinsi ya kuingiza pesa tu.

Mwaka 2014 ndio mwaka ambao United walitoa kiasi cha £59m kwa Real Madrid ili kumnunua na inasemekana hadi anaondoka United walishauza jezi za Di Maria ambazo ziliwaingizia zaidi ya £75m.

Paul Makonda "Nimarufuku Kupiga Mziki wa Wazi Jijini Dar es Salaam zaidi ya Saa Sita Usiku....

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo akihojiwa na Katika kituo cha radio cha E-FM ametoa onyo kwa watu wa Wenye Wanaomiliki Bars na Watoa Burudani kutokupiga mziki baada ya saa sita usiku...ametoa agizo kwa askari kufanya kazi yao kwa yoyote atakae piga mziki baaada ya muda huo

Hii inakuja ikiwa Tarehe 25 Nov kuna Tamasha kubwa la Fiesta Ambalo mara nyingi huwa linafanyika mpaka asubuhi....Sasa Je Tamasha Hili Pia litaishia saa sita au?
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live




Latest Images