Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live

Kubenea Awachoma Mafisadi

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage amesema wafanyakazi wa kiwanda cha nguo cha Urafiki waliobinafsisha kiwanda hicho na kuiingizia hasara serikali watashughulikiwa ipasavyo.

Mwijage ameyasema hayo bungeni leo wakati akijibu maswali mawili ya nyongeza yaliyoulizwa na mbunge wa Ubungo Mh. Said Kubenea aliyetaka kujua hatua watakazo chukuliwa wafanyakazi walioshiriki kubinafsisha kiwanda cha urafiki kwa mwekezi kutoka China ambaye ameshindwa kuleta faida.
“Ukiiona ripoti ya mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG utalia Kubenea, kwahiyo kila mtu aliyehusika kutuingiza kwenye dhahama hii rungu litamshukia kama Mwewe”, amesema Waziri Mwijage
.
Aidha Waziri amesema kuwa tayari serikali ipo mbioni kumaliza makubaliano na mwekezaji mpya kutoka China ambapo kiwanda hicho kitajengwa upya vizuri na serikali itanufaika kwa takribani asilimia 75.
Waziri Mwijage ameongeza kuwa kiwanda cha Urefiki ni cha kihistoria hivyo watakijenga upya na kitakuwa na wafanyakazi zaidi ya elfu nane.

OFA! OFA!OFA! Wahi ofa yetu ya kufunga mwaka tuna punguzo kubwa la bei kwanzia leo wahi OFA: Punguza unene, tumbo Na nyama zembe !

$
0
0

OFA! OFA!OFA! Wahi ofa yetu ya kufunga mwaka tuna punguzo kubwa la bei kwanzia leo wahi OFA hii ! Products kutoka malysia! Punguza unene, tumbo Na nyama zembe ! Uta loose kilo 10 mpaka 15 mabadiliko utayaona week ya kwanza uta punguza kilo 3 mpaka 5! Virutubisho vina kufanya ujione kushiba na wala usi tamani kula vyakula vengine Na Hamna haja ya gym wala mazoezi una pungua vizuri! bila madhara Tuna tuma mzigo kokote ulipo wasiliana nami
Call / whatsapp
#0653745074
Au Instagram
Follow @lilito_edmark
Follow @lilito_edmark
Follow @lilito_edmark

Mugabe Aonekana Hadharani kwa Mara ya Kwanza

$
0
0
Mugabe Aonekana Hadharani kwa Mara ya Kwanza
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza tangu jeshi la nchi hiyo lichukue madaraka siku ya Jumatano.
Alihudhuria sherehe za kufuzu kwenye mji mkuu Harare.
Bwana Mugabe amekuwa chini ya kuzuizi cha nyumbani kwa siku siku kadhaa huku kukiwa na mvutano kuhusu ni nani atamrithi.
Jeshi lilisema Ijumaa kuwa lilikuwa kwenye mazungumzo na Mugabe na litaujulisha umma kuhusu matokeo ya mazunngumoz hayo haraka iwezekanavyo.

Serikali Kuwatetea Wapangaji wa Nyumba Kuja na Mpango wa Kulipa Kodi kwa Mwezi Mmoja Mmoja

$
0
0
Serikali Kuwatetea Wapangaji wa Nyumba Kuja na Mpango wa Kulipa Kodi kwa Mwezi Mmoja Mmoja
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema kuwa iko kwenye mchakato wa kuanzisha mamlaka itakayo simamia masuala ya kodi ya nyumba itakayo fanya ukomo wa kodi kulipwa kwa mwezi mmoja na si miezi sita wala kumi na mbili.

Hayo yamezungumzwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Angelina Mabula wakati akijibu swali la Mbunge Halima Bulembo aliyehoji

Je, ni lini sasa serikali itafuta utaratibu wakulipa kodi kwa miezi 6 au mwaka na sisi kama bunge tutunge sheria itakayo walazimisha wamiliki wote kupokea kodi ya kila mwezi badala ya mwaka au miezi sita kama ilivyo sasa?

“Naomba nimtaarifu Mhe. Mbunge pamoja na wabunge wizara tayari imekwisha liona hilo, na tayari tuko kwenye mchakato wa kuanzisha mamlaka itakayo simamia masuala yote ya nyumba na katika sheria, na hiyo sheria italetwa hapa bungeni. Tumeangalia suala la ukomo wa kutoa kodi za nyumba hiyo ya miezi sita na mwaka mmoja haita kuwepo,amesema Mabula.

“Tumeona inaumiza watu wengi kwahiyo kodi itakuwa inalipwa kwa mwezi mmoja mmoja na wakati huo huo utatakiwa kuweka kama amana ya miezi mitatu kwaajili ya shughuli zingine ambazo zinaweza kuwa, kwahiyo suala hilo limelisikia na tunalifanyia kazi ,” amesema Mabula.

Chuchu Hans Ageuka Mbogo Baada ya Kuachana na Ray

$
0
0
Chuchu Hans Ageuka Mbogo Baada ya Kuachana na Ray
STAA wa filamu Bongo, Chuchu Hans kwa mara ya kwanza amegeuka mbogo ‘amewaka’ baada ya kuulizwa madai ya kuachana na msanii mwenzake aliyezaa naye mtoto mmoja, Vincent Kigosi ‘Ray’.

Chuchu ameiambia Star Mix kuwa, kila kukicha anasikia madai ya kuachana na mzazi mwenzie huyo na mpaka sasa hajajua ni nani anayeendelea kuzusha habari hizo.

“Najua wazi watu wengi hawapendi kabisa kuniona na Ray. Naanza kuingiwa na wasiwasi huenda wanaosambaza habari hizo ni watu wa karibu yetu na siku nikiwabaini ama zake au zangu,” aliwaka Chuchu.

Taifa Stars Kufundishwa na Kocha wa UEFA

$
0
0
Taifa Stars Kufundishwa na Kocha wa UEFA
Shirikisho la soka nchini TFF limemtangaza mchezaji wa zamani wa Tanzania Ammy Ninje kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania bara maarufu kama Kilimanjaro Stars.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam afisa habari wa shirikisho hilo Alfred Lucas amesema kocha huyo mwenye leseni A ya ukocha kutoka shirikisho la soka barani Ulaya UEFA ataiongoza Kilimnjaro Stars kwenye michuano ya CECAFA Challenge mwaka huu.
Katika hatua nyingine Alfred amesema kocha Ammy kesho anatarajia kutangaza wachezaji wa kikosi hicho watakaokwenda nchini Kenya kuiwakilisha Tanzania bara kwenye michuano hiyo.
Ammy Conrad Ninje ni mchezaji wa zamani wa Tanzania ambaye amecheza soka na kujifunza ukocha katika nchi za Ulaya na Amerika. Hatua kubwa ambayo amewahi kufikia ni kuwa kwenye benchi la ukocha la timu ya Hull City ya nchini England.
Michuano ya CECAFA Senior Challenge inatarajiwa kuanza Desemba 3 hadi 17 mwaka huu. Kilimanjaro Stars imepangwa kundi A na nchi za Kenya, Libya, Rwanda na Zanzibar.

Odinga Atinga Nairobi Polisi Watumia Nguvu Kuwatawanya Wafuasi Wake

$
0
0
Odinga Atinga Nairobi Polisi Watumia Nguvu Kuwatawanya Wafuasi Wake
Pamoja na ulinzi mkali uliowekwa kuzuia wafuasi wa Nasa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyetta (JKIA) baadhi wamemudu kufika ili kumpokea kiongozi wao Raila Odinga akitokea katika ziara ya siku 10 nje ya nchi.

Raila aliyekwenda Marekani kulalamikia jinsi ulivyofanyika uchaguzi mkuu wa marudio kwa kura ya urais nchini Kenya alitua JKIA saa 5:00 asubuhi.

Ndege iliyokuwa imembeba Raila ilitua wakati polisi wakipambana na wafuasi wake ambao walikuwa wakihaha kuingia ndani ya kiwanja hicho kilichokuwa chini ya ulinzi mkali hali iliyosababisha kupambana na polisi.

Licha ya ulinzi huo na moshi wa mabomu ya machozi wafuasi wa Nasa wapatao 200 wakiwemo wanawake walifanikiwa kupita utepe uliowekwa na vyombo vya usalama na wakaingia hadi ndani ya uwanja.

Helikopta ya polisi ilikuwa ikizunguka juu ya uwanja huo huku magari ya maji ya kuwasha na magari ya maalumu ya kusafisha njia yalikuwepo uwanjani hapo na yalitumika kuzima moto wa matairi.

Jana Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino na mwenzake wa Rauaraka TJ Kajwang na mwanasiasa wa Starehe Steve Mbogo walikamatwa na polisi.

Viongozi wa Chama cha Zanu PF Wajipanga Kumuondoa Mugabe Madarakani

$
0
0
Viongozi wa Chama cha Zanu PF Wajipanga Kumuondoa Mugabe Madarakani
Viongozi wa chama tawala cha Zanu PF wanakutana leo kuandaa rasimu ya uamuzi wa kumwondoa madarakani Rais Robert Mugabe mwishoni mwa wiki hii.

Pia, wataandaa mazingira ya kumfungulia mashtaka wiki ijayo ikiwa ataendelea kukataa kuachia madaraka, kiongozi wa ngazi ya juu amesema.

"Hakuna kurudi nyuma," kiongozi huyo aliliambia shirika la habari la Reuters. "Ikiwa atazidi kuwa mkaidi, tutaandaa mazingira ili afukuzwe Jumapili. Hilo likifanyika atafunguliwa mashtaka Jumanne."

Hatima ya Mugabe bado haijulikani hadi leo kwani imeelezwa amekataa juhudi zote za kumtaka ajiuzulu baada ya jeshi kutwaa mamlaka ya nchi ambalo hadi wiki hii lilikuwa nguzo muhimu katika utawala wake wa miaka 37.

Jeshi lilisema kupitia televisheni ya taifa kwamba lilikuwa linafanya mazungumzo ili kupata ufumbuzi na kwamba litaliarifu taifa kuhusu matokeo haraka iwezekanavyo.

Marekani, mkosoaji wa miaka mingi wa Mugabe kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu na wizi wa uchaguzi inataka “enzi mpya” Zimbabwe, alisema ofisa wa ngazi za juu wa mambo ya nje wa Marekani kuhusu masuala ya Afrika ukiwa ni wito uliowazi wa kumtaka mzee huyo aondoke.

Mkanganyiko umejitokeza pale Mugabe alipoonekana jijini Harare kwenye picha akiwa mtu mwenye tabasamu na akisalimiana na mkuu wa majeshi wa Zimbabwe, mtu ambaye yuko nyuma ya mapinduzi na kuibua maswali kuhusu kukaribia mwisho wa enzi zake.

Katika hali isiyotarajiwa Mugabe aliondoka kwa msafara kwenye nyumba yake ya kifahari maarufu kama "Paa la Bluu" alikokuwa amezuiliwa na jeshi na akaenda hadi Ikulu ambako alipigwa picha zilizosambabzwa kwenye vyombo vya habari alikutana na mkuu wa majeshi, Jenerali Constantino Chiwenga na wapatanishi kutoka SADC.


Dully Syskes Afunguka Kuhusu Ulithi Alioachiwa na Babaake

$
0
0
Dully Syskes Afunguka Kuhusu Ulithi Alioachiwa na Babaake
Msanii Dully Sykes ambaye hapo jana ameachia wimbo wake mpya wa 'Bombadier', amesema marehemu baba yake amemuachia urithi mkubwa ambao ni muhimu sana maishani mwake.

Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Dully Sykes amesema anajivunia kitendo cha baba yake kumuachia urithi wa 'nguvu', kwani ameweza kuwa na watoto wengi.
"Kitu ambacho mzee ameniachia na najivunia ni kuwa na nguvu za kuwa na watoto wenGi, tayari nina watoto wengi na bado wengine watakuja”, amesema Dully Sykes.
Baba Mzazi wa Dully Sykes ,ambaye pia alikuwa msanii na kipenzi cha watu, Mzee Abby Sykes alifariki dunia Februari 15, 2015, baada ya kuugua muda mrefu.

Kauli ya Mama Kanumba Kushukuru Mahakama Kumtendea Haki Yawaibua Wengi Atumiwa Ujumbe Huu

$
0
0
Kauli ya Mama Kanumba Kushukuru Mahakama Kumtendea Haki Yawaibua Wengi Atumiwa Ujumbe Huu
Mwanamuziki na Muigizaji nchini, Patcho Mwamba ameifungukia kauli ya Mama Kanumba ya kushukuru kitendo cha Muigizaji Lulu kufungwa miaka miwili kwa kosa la kumuua bila kukusudia muigizaji Kanumba na kusema kwamba hakuna haja ya kuendelea na 'beef' kwani hakuna haki inayoweza kumrudisha Kanumba hai.
Patcho ambaye alikuwa muigizaji na rafiki wa karibu na Marehemu Steven Kanumba amesema kwamba Mama kanumba anapaswa  kuwa na moyo wa kusamehe kwa sababu binti huyo akimaliza kifungo atarudi mtaani na ataendelea na maisha yake hivyo kujengeana chuki siyo jambo jema.
"Sina la kusema juu ya jukumu ya Lulu, lakini Mahakama imeamua kama ilivyoamua, kwa upande mmoja kuna unafuu kwani kwa kesi ile kufungwa miaka miwili ni bahati, ukija upande wa pili inaumiza sana kwani jela siyo sehemu nzuri sana kwa mtu kuwepo kila mtu anajua hilo hasa ukizingatia   bado ni mdogo hivyo tumuombee Mungu ampe nguvu, uwezo naamsaidie aweze kustahimili hiyo hali" Patcho.
Aidha Patcho ameongeza "Nimemuona mama anasema anashukuru (Mama Kanumba) haki imetendeka, mimi sidhani kama kunahitajika kuwepo na ma Beef. Mwanaye, ambaye pia ni rafiki yetu ameondoka lakini tunaamini ni mipango ya Mungu. Hakuna haki inayoweza kumrudisha Kanumba aishi. kusema naenda kumzika Kanumba upya sidhani kama kuna haja ya kuendeleza ma beef japo yapo. End of the day Lulu atatoka wataongea vizuri?. Sidhani yule mama yangu hivyo simshauri aendee kuwa na kinyongo".
Patcho amemalizia na kusema kwamba "Kusema kufungwa kwa Lulu kutampatia unafuu sidhani  ni uongo yeye aendelee kuwa mama maana ninachoamini Lulu hakumuua Kanumba bali alikuwa shahidi wakati Kanumba anakufa  ndichi ninachokiamini. Baadaye Lulu atatoka jela je  ukimuon utamgonga na gari? au Mama Lulu utaweza kuongea naye na wale ni Wahaya ni kabila moja. Sidhani kama Lulu alikuwa akikaa na kufikiria ipo siku atamuua Kanumba".

Wasiliana na The Great Maalim Hussein Mtaalam wa Kutatua Matatizo Yaliyoshindikana Kwa Kutumia Nyota na Dua

$
0
0
THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)
MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)
Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.
ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..
Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107 WhatsAPP tu.
+255 746 757 102 Kupiga tu.

Prezo Afunguka Uhusiano Wake wa Kimapenzi na Amber Lulu

$
0
0
Prezo Afunguka Uhusiano Wake wa Kimapenzi na Amber Lulu
Rapper wa Kenya, Prezzo ameonesha kuthibitisha rasmi uhusiano wake na video model aliyegaukia uimbaji, Amber Lulu.

Akiweka picha kwenye Instagram akiwa na Lulu, Prezzo ameandika, “Wacha waongee Lulu wangu, cha msingi we jua niko na wewe. President hatakuwacha uzame kamwe. Ngechu got u mia mia mia #Rapcellency #GodsSon #TheMakiniTeam #MamaCandy.”

Siku kadhaa zilizopita pia aliweka picha nyingine na kuandika, “Pili pili msioila inawawashia nini?? Tuko freshi ka chungwa #LuluMafia #Rapcellency #TheMakiniTeam.”

Hata hivyo kwenye interview na Dizzim Online wiki kadhaa zilizopita, Prezzo alidai kuwa Lulu ni rafiki yake tu.

Wanafunzi 6 wa Chuo Kikuu UDSM Watimuliwa kwa Utovu wa Nidhamu

$
0
0
Wanafunzi 6 wa Chuo Kikuu UDSM Watimuliwa kwa Utovu wa Nidhamu
Wanafunzi sita kati ya 100 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliokuwa kwenye mpango wa mafunzo ya vitendo kwenye taasisi na kampuni mbalimbali wameondolewa kwenye mpango huo kutokana na utovu wa nidhamu.

Mpango wa majaribio ya mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa UDSM unatekelezwa na Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (Taesa) kwa kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani (ILO).

Akizungumza leo Ijumaa Novemba 17,2017 wakati wa kikao cha tathmini, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taesa, Boniface Chandaruba amesema baadhi ya wanafunzi hao hawajitambui na hawaoni umuhimu wa mafunzo hayo.

Amesema kati ya wanafunzi hao sita, baadhi waliwatukana wasimamizi wa programu hiyo na wengine kuwarekodi viongozi wao na kuwaweka kwenye mitandao.

"Wanafunzi wa aina hii hatutawavumilia tunawaondoa kwenye programu hii," amesema.

Amesema programu hiyo inawawezesha wanachuo kwenda kufanya mafunzo kwenye taasisi za Serikali, mashirika ya umma na kampuni binafsi ili kupata ujuzi na maarifa ya kazi wanazosomea.

Amesema sababu za kuanzisha programu hiyo ni kutokana na baadhi ya waajiri kulalamika kwamba wamekuwa wakiajiri wahitimu wa vyuo vikuu ambao hawajui kazi.

"Baadhi ya waajiri wanasema wanatoa ajira kwa watu ambao wanatakiwa kufundishwa kazi kwa zaidi ya mwaka mmoja," amesema.

Amesema wanachuo hao wataendelea na mafunzo kwa miaka mitatu watakayokuwa chuoni.

"Wakifanya kazi vizuri na kuwavutia waajiri wanaweza kuajiriwa moja kwa moja watakapomaliza masomo," amesema

Mshauri wa Wanafunzi wa UDSM, Paulina Mabuga amesema licha ya wanafunzi hao kuondolewa katika mpango huo, pia uongozi wa chuo utachukua hatua za kinidhamu.

Ameipongeza Taesa na ILO kuanzisha mafunzo hayo kwa vitendo na kuichagua UDSM kuwa chuo cha kufanya majaribio.

Amependekeza mpango huo uwe endelevu ili kuwapa wahitimu uzoefu wa kazi wanazosomea.

Mmoja wa wanafunzi, Adelaide Mwasyoghe amesema anafanya mafunzo kwa vitendo katika Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Amesema kwa muda mfupi ameweza kujifunza kazi na kufahamiana na wafanyakazi wenzake.

"Nikimaliza masomo sitahitaji kuelekezwa kwa sababu nitakuwa nafahamu mazingira ya kazi ya  kampuni," amesema.

Makonda Awaomba Wadau Kutoa Misaada ya Vifaa kwa Walemavu wa Viungo

$
0
0
Makonda Awaomba Wadau Kutoa Misaada ya Vifaa kwa Walemavu wa Viungo
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo amewatembelea wagonjwa 21 kati ya 35 waliotakiwa kupewa miguu ya bandia katika Hospitali ya CCBRT iliyopo Msasani jijini Dar es Salaam na amewaomba wadau kuendelea kusaidia.
Makonda amewatembelea wagonjwa hao Ijumaa ya Novemba 17, mwaka huu ikiwa ni muendelezo wa kampeni yake aliyoianzisha Agosti 15 hadi 18, mwaka huu wakati Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ilipokuwa imeandaa kliniki ya huduma tengamao ambayo ilihudhuriwa na takribani watu 650 waliokuwa na mahitaji mbalimbali.
Akizungumza katika hafla hiyo, amewaomba wadau na mashirika mbalimbali kujitokeza kuwasaidia wagonjwa wenye ulemavu wa viungo hasa miguu ili kuwawezesha kutembea hasa katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka.
Katika kipindi cha kampeni hiyo, CCBRT kwa kushirikiana na Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) na Taasisi ya MoveAbility walikubali kutoa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu wa viungo 21 walioelekezwa kufika katika hospitali hiyo kwa ajili ya matibabu na kupewa miguu bandia.
Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alipotembelea wagonjwa hao, Mkuu wa Idara ya Utengamao CCBRT, Ruth Mlay alisema kuwa Idara ya Utengamao inao uzoefu mkubwa wa kuzalisha na kutengeneza viungo saidizi kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa viungo saidizi kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa viungo hasa kwa waliopatwa na kiharusi, polio na matatizo ya kuzaliwa nayo.
Wakati huohuo, kampuni ya usanifu wa majengo ya Spectrum Design imechangia kiasi cha milioni kumi kwa ajili ya kampeni hiyo ya kuwawezesha walemavu wa miguu kununua miguu bandia.

Malinzi Wenzake Wakwama Mahakamani Kesi Yao Hadi Novemba 30

$
0
0
Malinzi Wenzake Wakwama Mahakamani Kesi Yao Hadi Novemba 30
Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka nchini (TFF) Jamal Malinzi (wa pili kulia) akifuatiwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Selestine Mwesigwa, wakirudishwa rumande baada kesi yao kutajwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar jana na kuahirishwa mpaka Novemba 30 mwaka huu.

Jeshi la Polisi Limepokea Msaada wa Vifaa Tiba vya Bilioni 2 Kutoka Marekani

$
0
0
Jeshi la Polisi Limepokea Msaada wa Vifaa Tiba vya Bilioni 2 Kutoka Marekani
Jeshi la Polisi limepokea vifaa tiba kutoka shirika la Project Cure la nchini Marekani vyenye thamani ya Sh2 bilioni.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Siro akizungumza alipopokea vifaa hivyo katika Hospitali Kuu ya Polisi Kilwa Road leo Ijumaa Novemba 17,2017, amesema vitasambazwa katika vituo vya tiba vya polisi 20.

IGP Siro amesema wanalenga kuhakikisha askari wanapata huduma bora na kuwafanya wawe imara katika kutekeleza majukumu yao.

“Tutajitahidi kuwasomesha wataalamu wetu wa afya ili waweze kufanya kazi kwa weledi. Hospitali kuu ya polisi ipo vizuri, hivyo tunawakaribisha kwa yeyote atakayehitaji kutibiwa hapa kwa kuwa ina vifaa bora,” amesema IGP Siro.

Pia, amezindua majengo matatu katika hospitali hiyo ambayo ni kwa ajili ya  wagonjwa mahututi, stoo kuu ya dawa na jengo la kuhifadhia maiti.

Kamanda wa Afya, Paul Kasabago amesema wanakabiliwa na changamoto ya vifaa tiba katika wodi ya wagonjwa mahututi itakayofunguliwa.

Kasabago amesema wanahitaji mashine za CT- scan na MRI ili kuendelea kuboresha hospitali hiyo iweze kutimiza vigezo vya kuwa hospitali ya rufaa.

Ameishukuru Serikali ya watu wa Marekani kupitia shirika la misaada la USAID kwa kufadhili juhudi za Serikali ya Tanzania katika kupambana na Ukimwi kupitia shirika lisilo la kiserikali la JSI na AIDSfree Tanzania linalofanya kazi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika majeshi ya Polisi na Magereza.

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la JSI, Peter Maro amesema mradi wa AIDSFree umetoa mafunzo kwa watumishi wa afya katika nyanja mbalimbali za utoaji wa huduma za Ukimwi na Kifua Kikuu.

UVCCM Wamvaa Mbowe, Wasema Rais Magufuli Hajawahi Kutamka Mahali Popote Kama Serikali ni ya Kwake

$
0
0
“Rais Dk John Pombe Magufuli hajawahi kutamka mahali popote kama Serikali ni ya kwake na si ya CCM kama ilivyodaiwa na kiongozi wa upinzani Bungeni Freeman Aikael Mbowe” – Shaka

“Pamoja na Serikali kuongozwa na Rais Magufuli bado iko chini ya Chama Cha Mapinduzi na kumtaka Mbowe kuacha maneno ya upotoshaji na uchochezi wa kitoto” - Shaka

“Rais Dk Magufuli tokea alipoingia madarakani miaka miwili iliopita amekuwa akihimiza shime ya kukuza fikra mpya na kudumisha uzalendo ulioporomoka na kuzaa kundi la mafisadi, wezi wa mali za umma bila kujali itikadi za kisiasa kwasababu uzalendo hauna alama ya siasa au chama” - Shaka

“Matamshi ya Mbowe hayana msingi wala mantiki yoyote bali anaonekana kama mtu anayeweweseka usingizini baadaa ya kuona utendaji wa Serikali ya CCM kwa miaka miwili ukiendeshwa kwa uwajibikaji, ufanisi, umakini na kuweka pembeni mitazamo hafifu ya kisiasa huku ikijali zaidi nchi na utaifa” – Shaka.

"Mbowe ni mwanasiasa mnafiki na profesa wa kuzua. Amesahau alipowakusanya wananchi pale Mwembeyanga Temeke na kutaja orodha ya viongozi wa Serikali aliodai ni mafisadi likiwemo jina la Edward Lowassa aliyehamia Chadema na kuteuliwa kuwa mgombea urais " - Shaka.

“Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 /2020 ni miliki ya ya CCM na Rais Dk Magufuli hana ilani binafsi ya uchaguzi hivyo Mbowe aache kumlisha maneno Rais kwa kusaka kwake umaarufu dhaifu wa kisiasa.” - Shaka

"Mbowe aache kufuatilia mambo ya CCM kwasabahu hayatamsaidia yeye au chama chake. Hana sifa ya kuwa kiongozi mkweli mbele ya Watanzania kwa sababu ni wakala wa mafisadi na chama chake kimekuwa maficho ya viongozi wasiotamanika katika jamii " - Shaka.

“Serikali ya awamu ya tano haijawahi kukataa kupokea ushauri au maoni ndiyo maana Rais Dk Magufuli amekubali hata kupokea ilani ya uchaguzi ya ACT Wazalendo na madai ya kuteua viongozi kwa mtazamo wa udini, ukabila au ukanda huo ni upuuzi usiohitaji kusikilizwa.” - Shaka

“CCM itaendelea kuamini na kufuata itikadi ya siasa ya Ujamaa na Kujitegemea kama ilivyoanishwa kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani ujamaa si utitiri wa vibanda vya nyasi na kadhia ya umasikini bali ni imani na utekelezaji.” - Shaka

“Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kwa umakini na uangalifu mpya ili kukwepa yaliotokea nyuma yasijirudie tena na kukuta faida au tija ya rasilimali za Taifa zikiwanufaisha Mabepari na Mafisadi.” - Shaka

“Ninachokiamini kwa mujibu wa ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020, Serikali haijaibeza sekta binafsi, kupuuzia uwekezaji na wawekezaji au kutofungua milango ya ushirika wa maendeleo bali kinachowatatiza baadhi ya Mafisadi na Wanasiasa uchwara ni kuzibwa kwa mirija na mianya ya wizi wao.” - Shaka

"Kiongozi yeyote anayekuwa wa kwanza kuumwa au kuthubutu kuutaja udini na ukabila hadharani huyo ndiye mkabila na mdini halisi. Hatuwezi kuteua viongozi kwa kutazama idadi ya makabila, dini au ukanda kwasababu Serikali si kilenge cha mizimu na matambiko" - Shaka.

“Nasikitishwa na matamshi ya Mbowe kudai hali ya uchumi ni mbaya wakati takwimu za uchumi katika taasisi za kitaifa na kimataifa zikiutaja uchumi wa Tanzania kukua kwa kasi.” - Shaka

"Huwezi kuwahimiza waumini wa Kikristo au Waislam kufanya ibada ikiwa hakuna Misikiti au Makanisa. Tunajenga viwanda, tutazalisha ili kupata masoko ya ndani na nje kutokana na ubora wa bidhaa. Hata Wachina, Waingereza na Wamarekani hatukukubaliana kama tutanunua bidhaa zao" - Shaka.

“Rais Magufuli na Seikali inayoongozwa na CCM itaendelea na mikakati yake katika dhamira ya kujenga uchumi imara wa viwanda kuelekea uchumi wa kati, kuziba mifereji ya wizi na ufisadi bila kuyumbiswa na mayowe ya wapinzani.” – Shaka

Shaka Hamdu Shaka ni Kaimu Katibu Mkuu UVCCM ameyasema hayo alipozumgumza na waandishi wa habari ofisini kwake huko Upanga jijini Dar es Salaam kufuatia madai ya Mbowe dhidi ya Rais na utawala wake.

Dogo Aslay Hizi Sasa Sifa Zimezidi Kipimo..Umetuzalilisha Wanawake

$
0
0
Mimi binafsi ni shabiki mkubwa wa nyimbo za dogo aslay ukweli ni kwamba dogo anajitahidi ila kilonifanya niandike hii thread kuna wimbo wa Aslay umetoka sijui kautoa mwenyewe au umevuja au vipi maana wimbo wenyewe una verse moja tu lakini mashairi ya wimbo huo hayajawafurahisha wanawake wengi ikiwemo Mimi.

Ni wimbo ambao unamdhalilisha mwanamke huyu dogo anapaswa atambue kwamba mashabiki wa mziki wake wengi ni wanawake hata kama umeachana na mwanamke huwezi kumtolea matusi kama ya kwenye wimbo wa aslay so aslay kama umo humu Jf acha kudhalilisha wanawake ambao ndo mashabiki zako wakubwa including Ray 4 real.

Baadhi ya mashairi katika huo wimbo;

Kiuno kizito kama engine ya fuso ,
Hauna lolote kitandani yaani upopo,
Unashindwa hata kufua vichupi vyako,
Unanuka jasho makwapani kama choo cha soko..

Hayo ni baadhi ya mashairi kwa kweli hayajatufurahisha wanawake na ni udhalilishaji

So aslay  metudisappoint 90% ya wanawake Tz.
Yangu ni hayo sema nimeshindwa kuapload hiyo audio.

 VIDEO:

Rais Mugabe Amtunuku Shahada Mke wa Jenerali Aliyemzuia

$
0
0
Rais Mugabe Amtunuku Shahada Mke wa Jenerali Aliyemzuia
Rais wa Zimbabwe's Robert Mugabe amewatunuku shahada zaidi ya wanafunzi 3,300 katika chuo kikuu cha Zimbabwe, akiwemo mke wa jenerali aliyemzuia siku ya Jumatano.
Marry Chiwenga alipata shahada ya MBA kulingana na shirika la habari la Zimbabwe.
Awali Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza tangu jeshi la nchi hiyo lichukue madaraka siku ya Jumatano.
Alihudhuria sherehe za kuhitimu kwa mahafala kwenye mji mkuu Harare.
Bwana Mugabe amekuwa chini ya kuzuizi cha nyumbani kwa siku kadhaa huku kukiwa na mvutano kuhusu ni nani atamrithi.
Jeshi lilisema Ijumaa kuwa lilikuwa kwenye mazungumzo na Mugabe na litaujulisha umma kuhusu matokeo ya mazunngumoz hayo haraka iwezekanavyo.
Mtu moja aliyeshuhudia alinukuliwa na Reuters akisema kuwa Mugabe alishangiliwa wakati wa sherehe baada ya kuzungumza.
Jeshi lilichukua madaraka baada ya Mugabe kmfuta kazi makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa wiki iliyopita, na kuashiria kuwa alimpendelea mkewe kuweza kuchukua ungonizi wa Zanu-PF na urais.

Kutana na Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed Kutoka Bagamoyo...Ana Dawa za Kurudisha Mapenzi na Zingine Nyingi

$
0
0

MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

USHAURI: kama unahitaji msaada ni  bora kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate  msaada kwa haraka.
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live




Latest Images