Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Haya Hapa Madhara ya Kujichubua Ngozi

$
0
0
Katika baadhi ya sehemu duniani watu wanaamini kuwa ngozi angavu huashiria uzuri, utajiri na uwezo(kifedha) alionao mtu.Katika baadhi ya sehemu watu wenye ngozi nyeusi huchukuliwa kuwa wapo chini ya kiwango,

hii hupelekea watu hawa kutumia ving´arisha ngozi kama krimu, vidonge au nyenzo zingine kubadilisha ngozi zao.

 Tafiti zinaonyesha kwamba wavulana na wasichana hupendelea kutumia bidhaa zinazong´arisha ngozi ili waweze kupata hadhi nzuri katika kundi la familia zao, na jamii. Kwa kweli,hata matangazo yanayoonyeshwa kwenye televisheni mbalimbali huonyesha kitu hiki. Mambo hayo yote huwa na athari kubwa juu ya mawazo ya vijana wa kiume na wakike ambayo hupelekea kuwafanya wachague chochote wanachomudu kati ya krimu au vidonge.


Madhara ya kujichubua ni yapi?
Mtu anaeyejichubua anaweza kupata kansa ya ngozi, chunusi, uvimbe katika ngozi, ngozi kuwa nyembamba,Kuongezeka kwa hamu ya kula na uzito,kutokwa na mabaka, pumu, kupata watoto wenye kasoro, kupata matatizo ya akili, kuharibika kwa ini, kuharibika kwa mishipa ya fahamu pamoja na figo kutokana na kiwango kikubwa cha zebaki(mercury) kilichomo katika krimu,Osteoporosis(kupungua kwa uzito wa mifupa ambapo huongeza hatari ya kuvunjika kwa mifupa)

Baadhi ya madhara haya huonekaa mara moja na mengine hujitokeza kadri mtu anavyotumia ving´arisha ngozi.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo...

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Tupo Mbagala Rangi Tatu

Mkewe Tundu Lissu Afunguka Waliofanya Shambulio..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Novemba 20

$
0
0


Mkewe Tundu Lissu Afunguka Waliofanya Shambulio..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Novemba 20

Mke Amuombea Kura Mume Aliye Mahabusu...Mbowe Amsaidia

$
0
0
Mke wa mgombea udiwani Kata ya Mhandu (Chadema), Godfrey Misana amelazimika kupanda jukwaani kumwombea kura mume wake aliye mahabusu kutokana na kukabiliwa na shtaka la kujeruhi.

Katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika leo Jumapili Novemba 19,2017 katika uwanja wa Shule ya Msingi Mhandu, mwanamama huyo, Rose aliitwa jukwaani na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ili kuomba kura kwa ajili ya mume wake.

Rose aliwaomba wakazi wa kata ya Mhandu kumpa kura mume wake ili aweze kuwatumikia na kutatua changamoto zote zilizopo katani hapo zikiwamo za barabara, zahanati na maji.

Misana (46), mgombea udiwani wa Chadema katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Novemba 26,2017 na kampeni meneja wake, Charles Chinjibela (37) Ijumaa Novemba 17,2017 walipandishwa kizimbani

wakidaiwa kumjeruhi meneja wa kampeni za CCM katika kata hiyo, Thomas Warioba.

Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza, mbele ya hakimu Ainawe Moshi wanadaiwa kutenda kosa hilo Novemba 14,2017. Mahakama itatoa uamuzi kuhusu dhamana Novemba 21,2017.

Akiomba kura, Rose amemuomba Warioba ambaye ni mlalamikaji katika kesi hiyo kuiomba Mahakama imwachie mume wake kwa kuwa amemkumbuka pamoja na familia yake.

"Nikuombe Warioba uwaambie Mahakama wamwachie mume wangu kwa kuwa mimi na familia yangu tumemkumbuka sana ni siku ya tano sasa hatujamuona, kitanda kimekuwa kikubwa jamani niko chini ya miguu yako mwache mume wangu,” alisema Rose huku akishangiliwa na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano huo.

Mbali ya Rose kuomba kura, wananchi walijitokeza na mabango yaliyoandikwa “Hata kama upo gerezani kura tutakupa tulia hivyo hivyo."

Imeandikwa na Kalunde Jamal, Ngollo John na Johari Shani.

Hizi Hapa Tabia za Msichana Anayekupenda Kimapenzi ila Anashindwa Kukueleza!

$
0
0
1. Atakutega kupata attention yako. Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda au lah! Mf wa mambo hayo ni kujifanya anaumwa na kuangalia respond yako kwake ni kiasi gani unamjali na kiasi gani utahangaika kwa ajili yake au

2. Haoni aibu kugusa sehemu yako ya mwili. Msichana anayependa haoni aibu kukushika mkono ama kukutomosa au hata kukumbatia. Kwa kufanya hivyo hujua kuwa kwa asilimia kubwa hisia za kushikana kwenu kutamrahisishia kazi ya kuwa na wewe

3. Kucheka kwa nguvu hata kwa kitu kisicho chekesha endapo wewe umezungumza. Mara nyingi ataonesha uso wa furaha hata kama si furaha ya kweli

4. Wivu.
Hujisikia wivu anapokuona na wasichana wengine. Ukiwa unachart nao na ukiwaita majina ya kimahaba. Hapendi.

5 anakumbuka siku zako muhimu. Hukumbuka kama vile siku yako ya kuzaliwa hatowez kuisahau kufanya ipite bila kukutakia heri ya siku ya kuzaliwa kama sivyo ukifaulu mtihani au chochote katika maisha yako atakuwa mbele kukupongeza

6. Eye contact anapenda kukuangalia machoni muda wote ambao mtakuwa mkizungumza pamoja akidhani kuwa utaelewa ni kiais gani anakupenda kupitia vile ambavyo anakuangalia.
Ila wengine huona aibu kuwatazama wavulana wanaowapenda si wote wana ujasiri wa kuwatazama wapenzi wao.

7. Hupenda kukaa mmuda mwingi na wewe. Hawezi kupoteza hata sekunde ukimuhitaji kwa mazungumzo. Anajisikia furaha kukaa na wewe muda mrefu bila kuchoka. Anaweza akaacha kila kitu anachokifanya ili ajumuike na wewe.

8. Yupo tayari kuangamiza. Kama msichana anakupenda yupo tayari kusacrifice. Ni kitu ambacho hakuna mtu ambaye anaweza akafanya kwa mtu mwingine. Utaona vipi huyo msichana alivyo kwako na wa wengine. Yaani yupo tayari yeye akose lakini wewe upate na kwa mwingine anaweza akamwamba hana alichoombwa lakini akakupa wewe kama pesa na vitu vingine.

9. Anachukulia matatizo yako kama ni yake. Unapomueleza kuwa ana tatizo anajali tatizo lako kama vile ni lake na hujisikia vibaya sana na kuhuzunika na atafanya lolote ili aweze kukusaidia utoke katika hilo tatizo.

10. Mikwaruzano ikitokea katika urafiki wenu hayupo tayari kukupoteza kabla hajakuambia anakupenda. Kwa kuwa anakupenda endapo ikatokea mikwaruzano basi atafanya juu chini kuyaweka mambo sawa ili asikukose

OFA!OFA! Wahi ofa yetu ya Kufunga Mwaka Tuna Punguzo Kubwa la Bei Kwanzia Leo Wahi OFA: Punguza Unene, Tumbo Na Nyama zembe !

$
0
0
OFA! OFA!OFA! Wahi ofa yetu ya kufunga mwaka tuna punguzo kubwa la bei kwanzia leo wahi OFA hii ! Products kutoka malysia! Punguza unene, tumbo Na nyama zembe ! Uta loose kilo 10 mpaka 15 mabadiliko utayaona week ya kwanza uta punguza kilo 3 mpaka 5! Virutubisho vina kufanya ujione kushiba na wala usi tamani kula vyakula vengine Na Hamna haja ya gym wala mazoezi una pungua vizuri! bila madhara Tuna tuma mzigo kokote ulipo wasiliana nami
Call / whatsapp

#0653745074

Au Instagram
Follow @lilito_edmark

Nyalandu Rasmi Chadema Aanza Kuonekana Kwenye Kampeni ya Udiwani

$
0
0
Nyalandu Rasmi Chadema Aanza Kuonekana Kwenye Kampeni ya Udiwani
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amemkabidhi kadi ya uanachama wa chama hicho aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu, Jijini Mwanza katika uwanja wa Shule ya Msingi Mhandu kwenye kampeni ya kumnadi mgombea udiwani Godfrey Mahame

Godfrey Mahame.
"Nimeisubiri kwa shauku kubwa siku hii ya leo ili nipate fursa ya kupigania mageuzi ya kisiasa na ya kiuchumi Tanzania," amesema Nyalandu baada ya kukabidhiwa kadi.
Amesema ana shauku, furaha na heshima kukaribishwa rasmi kuwa mwanachama wa Chadema. Nyalandu ameongeza kuwa katika majira na nyakati ambazo Taifa linapitia, mabadiliko ya kisiasa nchini Tanzania ni lazima.
"Naungana na chama hiki pendwa ili tutembee pamoja mtaa kwa mtaa kijiji kwa kijiji tuwaambie wananchi wakati wa ukombozi ni sasa," alisema Nyalandu.
"Saa ya mabadiliko imefika kwa mtu yeyote miongoni mwetu, tumepewa utayari wa kubadilisha mwelekeo wa nchi," amesema.

Mahakama ya Kenya Kuamua Juu ya Kesi ya Urais Leo

$
0
0
Mahakama ya Kenya Kuamua Juu ya Kesi ya Urais Leo
Mahakama ya juu zaidi nchini Kenya Jumatatu inatarajiwa kutoa uamuzi katika kesi zilizowasilishwa kwenye mahakama hiyo kupinga uchaguzi wa marudio wa tarehe 26 Oktoba ambapo rais wa sasa Uhuru Kenyatta alitangazwa kama mshindi.
Katika Kesi majaji watatakiwa kutoa uamuzi kuhusu masuala yafuatayo:
Wataamua iwapo tume huru ya taifa ya chaguzi na mipaka (IEBC ) ilifaa kuteuwa upya wagombea urais au la.
Uamuzi pia utatolewa na mahakama hiyo juu zaidi juu ya ya ikiwa kujiondoa kwenye uchaguzi huo kwa kiongozi Muungano wa upinzani Raila Odinga na Makamu wake Kalonzo Musyoka kuliathiri uchaguzi huo.
Majaji pia watatoa uamuzi kuhusu ikiwa baada ya tume ya IEBC kushindwa kuendesha uchaguzi katika ameneo bunge 25 kati ya 290 kunahalalisha ama kubatilisha matokeo ya uchaguzi.
Aidha Mahakama hiyo itawaeleza waKenya ikiwa tume ya uchaguzi (IEBC) ilikuwa na uwezo wa kuandaa uchaguzi wa haki na huru baada ya kugubikwa na mgawanyiko miongoni mwa wajumbe wake.
Kwa upande mwingine Wakenya watasubiri kusikia uamuzi wa mahakama kuhusu kama ghasia zilizotokea kabla na baada ya uchaguzi wa marudio wa urais ziliathiri ama hazikuathiri matokeo ya uchaguzi na kuufanya kuwa usio wa haki na huru au la.
Mahakama itatoa ufafanuzi juu ya dosari ya karatasi za kupigia kura, maarufu kama form 34A ziliathiri matokeo ya uchaguzi.
Hukumu hii inasubiriwa kwa shauku kubwa na raia wa Kenya pamoja na kwingineko duniani, huku wengio wakijiuliza hatma ya Kenya.
Tangu kufanyika kwa uchaguzi wa marudio wa urais tarehe 26 Oktoba, baadhi ya miji mikuu nchini Kenya ukiwemo mji mkuu Nairobi, pamoja na mji wa magharibi wa Kisumu imekuwa ikikumbwa na ghasia za maandamano ambazo zilizosababisha mauaji ya watu na wengine kujeruhiwa.

Ireni Uwoya Anusurika Kubigwa Rwanda Familia ya Ndikumana Yamtetea

$
0
0
Ireni Uwoya Anusurika Kubigwa Rwanda Familia ya Ndikumana Yamtetea
FAMILIA ya aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Timu ya Rayon Sports ya Rwanda, Hamad Ndikumana ‘Katauti’ (39), imezuia staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya ambaye alikuwa mke wa jamaa huyo asifanyiwe fujo baada ya kutinga nchini Rwanda jioni ya Ijumaa iliyopita. Hatua hiyo ilikuja baada ya Ndikumana kupoteza maisha huku Uwoya akishushiwa tuhuma za hapa na pale na kwamba huenda alichangia kifo hicho.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichoambatana na Uwoya, familia ya Ndikumana ilichukua uamuzi huo baada ya watu mbalimbali nchini humo kuwa na hasira na Uwoya. Kutokana na kifo cha Ndikumana, Uwoya alilazimika kwenda Rwanda kuhani msiba akiwa na mwanaye aliyezaa na jamaa huyo, Krish, mama na baba yake na mabaunsa wa kumpa ulinzi.

Chanzo hicho kilieleza kwamba, watu mbalimbali nchini humo walikuwa na hasira juu ya Uwoya kwamba ndiye aliyesababisha kifo cha Ndikumana kwani alikuwa na msongo wa mawazo akimfikiria yeye kwa kuwa alimpenda na kutaka wairudishe ndoa yao, lakini mwanamama huyo akawa anang’ang’ania apewe talaka ambayo hadi Ndikumana anafariki dunia alikuwa hajaitoa.

Staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya.
“Mashabiki wa Ndikumana walitaka kumfanyia fujo Uwoya kwa kuwa wanadai ndiye chanzo cha kifo cha mpendwa wao, lakini familia iliwazuia wasifanye hivyo kwa kuwa walishamsamehe Uwoya ndipo hali ya amani ikawepo,” kilisema chanzo hicho. Kiliendelea kueleza kuwa, Uwoya aliwasili nchini Rwanda Ijumaa iliyopita kwenda kuona kaburi la mumewe ambaye alizikwa Jumatano iliyopita ambapo alipokelewa vizuri na mama wa Ndikumana pamoja na familia kwa jumla.

“Zile tofauti waliziweka pembeni na mama Ndikumana akamwambia wamemsamehe hivyo ikawa ni kuomboleza upya kwani Uwoya na mama’ke alikuwa akilia sana hadi kushindwa kutembea,” kilisema chanzo hicho. Hata hivyo, alisaidiwa kwa kushikwa mkono na wenyeji kwani mama huyo alikuwa akimpenda sana mkwewe Ndikumana kama mtoto wake.

Baada ya chanzo kutiririka, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Uwoya ambaye alikiri kupokelewa vizuri na familia pamoja na mama Ndiku ambaye alipomuona tu alimkumbatia huku akilia kwa uchungu akimuita ‘mwanangu’. Naye msanii wa filamu, Michael Sangu ‘Mike’ ambaye ni mmoja wa watu waliosafiri alikiri kuwa walipokelewa vizuri na hakuna tofauti yoyote iliyojitokeza.

“Uwoya, baba, mama na Krish walitangulia na ndege na walipokelewa vizuri kabisa na hakuna mtu aliyewafanyia fujo wala nini, familia imewapokea kwa ukarimu na sisi ambao tulifika baadaye maana tulisafiri kwa basi tulipokelewa vizuri sana,” alisema Mike Sangu.
Chanzo: Global Publishers

Mtoto wa Mugabe Amtetea Babaake na Kukitukana Chama cha Zanu-PF

$
0
0
Mtoto wa Mugabe Amtetea Babaake na Kukitukana Chama cha Zanu-PF
Mtoto wa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe na mkewe Grace, Chatunga Bellarmine Mugabe amemsifu baba yake na kukitukana chama cha Zanu-PF.


Rais Robert Mugabe akiwa na mkewe Grace pamoja na mtoto wao wa tatu Chatunga

Mtoto huyo ambaye ni watatu katika familia ya Rais huyo ametoa maneno hayo kupitia mtandao wake wa Facebook kwa kukiambia chama hiko kuwa hakiwezi kufanya lolote bila Rais Mugabe. Kupitia mtandao huo, Chatunga ameandika:

“You can’t fire a Revolutionary leader ! Zanu Pf is nothing without President Mugabe ✊ Gushungo will always remain the champion of champions! Proud of you Gushungo Proud of Dad. Gushungo always and forever to death✊ People like Wellence Mujuru celebrate and march became of Jealous and ruchiva acting as if he cares for the people and unnecessary attacks !
We all grow up in life and take up our responsibility to serve our country. We all have a responsibility to keep this country safe and guard our sovereignty. God bless all who sacrifice for our nation Zimbabwe

Chama cha Zanu-PF kimemtaka Mugabe kujiuzulu Urais wa nchi hiyo mpaka kufikia leo mchana.

Kalan Jeremiah Kumsaka Dkt Shika "Nitamtafuta kwaajili ya Kujifunza"

$
0
0
Kalan Jeremiah Kumsaka Dkt Shika "Nitamtafuta kwaajili ya Kujifunza"
Msanii wa muziki wa hip hop, Kala Jeremiah amedai atafanya jitihada za kumtafuta Dk Louis Shika ili apate madini kutoka kwa mzee huyo ambaye anadaiwa kuwa  ni msomi wa udaktari.

Akiongea na Bongo5 weekend hii, Kala alisema mzee huyo anaonekana kuwa ni msomi mkubwa na tayari ana mambo mengi amejifunza akiwa nje ya nchi alipokuwa alisoma na kufanya kazi enzi za ujana wake.

“Binafsi nitamtafuta kwaajili ya kujifunza, yule ni mzee mwenye mambo mengi, aliyopitia, ni mafunzo tosha kwa vijana kama mimi na wengine. Kwahiyo nitamtafuta ili nijifunze,” alisema Kala.

Kala alidai kwa kuwa nyimbo zake ni za kijamii zaidi, ataangalia uwezekano wa kumtumia katika baadhi ya project zake kama akipata nafasi.

Pia rapa huyo aliitaka serikali kumtumia mzee huyo katika Tanzania ya Viwanda kwa kuwa anaonekana ana mambo mengi ambayo anayafahamu.

Dk Louis Shika hivi karibuni aliingia kwenye headline baada ya kushindwa kutoa asilimia 25 ya mnada wa nyumba za Lugumi muda mchache baada ya kushinda mnada huo na kudai pesa zake zipo Urusi.

Dkt Shika Apata Shavu la Matangazo na Huu ndo Muonekano Wake Mpya

$
0
0
Dkt Shika Apata Shavu la Matangazo na Huu ndo Muonekano Wake Mpya
Maisha ya Dk Louis Shika ambaye hivi karibuni aliingia kwenye headline baada ya kushindwa kutoa asilimia 25 ya mnada wa nyumba za Lugumi muda mchache baada ya kushinda mnada huo, yameanza kubadilika taratibu kutokana na kupata deal kadhaa za matangazo.

DK Shika ambaye alikuwa katika muonekano ambao haufananii na utajiri anaoutangaza kuwa nao, weekend hii ameonekana akiwa amevaa suti kali.


Wadau wa mambo wanadai kuwa mzee huyo mashuhuri mitandaoni amepata deal kubwa katika kampuni moja kubwa la michezo ya kubashiri.

Huwenda akapata deal nyingi zaidi kutoka na umaarufu alionao kwa sasa

Mali Kubwa Toka China Yatua Dar Tayari kwa Matibabu ya Bure

$
0
0
Mali Kubwa Toka China Yatua Dar Tayari kwa Matibabu ya Bure
Mkuu Wa Mkoa Wa Dar Es Salaam Paul Makonda ameipokea meli kubwa toka China iliyofika kwa ajil ya kuanza zoezi la utoaji wa huduma ya vipimo vya afya pamoja na matibabu ambayo yatatolewa bure kabisa kwa muda wa siku tano.
Ambapo Rc makonda ametoa wito kwa wakazi wote wanaoishi Dar es salaam kuanza kujitokeza kwa wingi kuanzia leo ili waweze kupewa huduma ya vipimo pamoja na matibabu bure hasa kwa wale wenye matatizo mbalimbali.
Aidha ameongeza kuwa anaushukuru ubalozi wa china hasa kwa kitendo cha wao kuruhusu meli hiyo itoe huduma katika nchi ya Tanzania hususan Dar es salaam kwan hiyo inaonyesha kuwa nchi ya china inaunga mkono hasa katika jitihada za Rais Maguful Za Kumtetea Mtanzania Wa Kipato Cha Chini Na Kuhakikisha Kuwa Wanapata Huduma Zote Muhimu.
Meli hiyo ambayo imepokelewa siku ya jana imekuja na madaktari pamoja na wahudumu wapatao zaid ya 381,huku madaktari 30 kati yao siku ya jana tayari wamekwisha fanya ziara ya kuitembelea hospital ya Muhimbili,Amana,Mwananyamala pamoja na Hospital ya Temeke kwa ajili ya kukagua vifaa ambayo vitakuwa vimepoteza umakini wake wa kutoa huduma na kabla ya kuondoka watakabidhi msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajil ya hospital hizo. Angalia picha.

  

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatatu

$
0
0

Breaking News: Mahakama ya Juu Nchini Kenya Yatupilia Mbali Kesi ya Kupinga Ushindi wa Kenyatta

$
0
0

Chama cha Zanu- PF Kumbuluza Mahakamani Mugabe

$
0
0
Chama cha Zanu- PF Kumbuluza Mahakamani Mugabe
Mtandao wa Twitter unaofuatilia taarifa za vyombo vya habari nchini Zimbabwe unaripoti kuwa Kiongozi wa chama tawala Cha ZANU PF anaamini mchakato wa kumshtaki Bwana Mugabe utaendelea kama ilivyopangwa Jumanne , wakati ambapo chama bunge linatarajiwa kukaa.

Hii ni kama muda wa makataa uliowekwa wa kujiuzulu kwake ambao ni Jumatatu saa sita adhuhuri utakwisha kabla Bwana Mugabe hajajiuzulu.
Mamlaka ya Mugabe yalidhoofishwa tangu jeshi lilipoingilia kati Jumatano, wakati ulipoibuka mzozo juu ya nani anayepaswa kumrithi .

Mzozo huo uliibuka wiki mbili zilizopita wakati kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93- alipomfuta kazi makamu wake Emmerson Mnangagwa, jambo lililowakasirisha makamanda wa kijeshi walioona kuwa ni jaribio la mkewe Grace kutaka kuwa rais.
Halikuwa tangazo ambalo baadhi ya waZimbabwe walilisubiri. Bwana Mugabe bado ni rais na haijawa wazi ikiwa bunge sasa litaanza mchakato wa kumshitaki.

Watu wa Zimbabwe walikuwa wanatarajia kusikia mugabe akijiuzulu kulingana na madai yao.
Baadhi ya wale waliokusanyika kufuatilia hotuba yake kwenye vilabu waliiambia BBC kuwa wamekatishwa tamaa na kutojiuzulu kwa rais Mugabe.
Hata hivyo hali ya imeendelea kuwa tulivu katika maeneo mengi ya Zimbabwe, huku wengi waliendelea kusubiri mchakato utakaofuata.

Duru kutoka ndani ya mazungumzo ya hatma ya Mugabe zimeiambia BBC kuwa Mugabe mwenye umri wa miaka 93 alikuwa amekubali kuondoka madarakani , lakini baadae akabadili mawazo yake
Jeshi linatarajiwa kuwa na mkutano na waandishi wa habari Jumatatu asubuhi pamoja na Muungano wa Wapiganaji waliopigania Uhuru wa Zimbabwe.

Katika hotuba yake ya kwanza kwa taifa tangu jeshi lichukue madaraka Jumatano, Mugabe hakujiuzulu na alisema kuwa ameazimia kuongoza kongamano lijalo la Zanu-PF.
Hatma yake sasa iko mashakani kwani kulingana na mbunge wa Zanu-PF Terence Mukupe anasema kongamano hilo ni mahala panopofaa kumuidhinisha kiongozi mpya anayependelewa na chama cha Zanu-PF

Kaburi Lafukuliwa Chini ya Usimamizi wa Polisi

$
0
0
Kaburi Lafukuliwa Chini ya Usimamizi wa Polisi
Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro kwa kushirikiana na madaktari wa hospital ya rufaa ya KCMC limesema linaendelea na uchunguzi wa mwili uliofukuliwa kwenye makaburi ya Karanga mji mdogo wa Himo mjini Moshi.

Mwili huo ulifukuliwa jumapili chini ya usimamaizi wa Jeshi la Polisi na kufuatia utata uliojitokeza baada ya mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Scholastica iliyopo Himo kupotea kwa siku kadhaa bila kuonekana.

“Tunaendelea na uchunguzi juu ya mwili huo na tayari kuna watu tumewakamata hivyo kila kitu kitakapokuwa sawa tutatoa ripoti kamili ya tukio hilo na wenzetu wa KCMC wanaendelea na uchunguzi wa mwili tulioufukua ili kujiridhisha kama ni wenyewe au sio”, amesema Kamishna Msaidizi wa Polisi Hamis Issa.
Humphrey Makundi, mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Scolastica anatajwa kupotea tangu Novemba 7 mwaka huu akiwa shuleni.

Kutokana na kuwepo kwa taarifa za kuokotwa kwa mwili katika mto Ghona uliopo mita 300 kutoka shule hiyo na kukosekana kwa ndugu walioutambua, mahakama ililazimu kukubali ombi la familia ya Humphrey la kufukua kaburi hilo ili kuweza kutambua kama mwili huo ni wa mtoto wao.

Hii Hapa List ya Wachezaji Wanaoongoza kwa Magoli Ligi Kuu

$
0
0
Hii Hapa List ya Wachezaji Wanaoongoza kwa Magoli Ligi Kuu
Ligi Kuu soka Tanzania Bara iliendelea tena wikiendi hii iliyopita, ikiwa ni mzungumko wa 10 kwa kushuhudiwa michezo saba ikipigwa katika viunga mbalimbali hapa nchini.

Katika michezo hiyo iliyoanza Novemba 18 mwaka huu wababe wa ligi Simba SC, Azam FC na Yanga SC zote zilifanikiwa kuchomoza na pointi tatu muhimu hali inayopelekea wachezaji wanao cheza katika klabu hizo kuongeza idadi ya mabao

Klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba mpaka sasa inaongoza ligi hiyo kwa kuwa na jumla ya pointi 22 ikifuatiwa na Azam FC wenye alama 22 ikiwa na tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa wakati Yanga SC baada ya ushindi wake wajana wa mabao matano dhidi ya Mbea City unaifanya kuwa na pointi 20 kwa kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi hiyo ya VPL.


Chama cha CCM Kina Dhambi Kubwa na Mshahara wa Dhambi ni Mauti- Lema

$
0
0
CCM Kina Dhambi Kubwa na Mshahara wa Dhambi ni Mauti- Lema
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amesema kuwa kitu cha msingi ambacho wananchi wanatakiwa wajue ni kwamba Chama cha Mapinduzi (CCM) kimefika mwisho huku akisema mshahara wa dhambi ni mauti na Chama hicho kina dhambi kubwa sana iliyokaribia mauti.

Lema ameyasema hayo Jumapili hii katika uwanja wa Shule ya Msingi Mhandu mkoani Mwanza ambako Mbowe alikuwa anahutubia mkutano wa hadhara wa kampeni za udiwani katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Novemba 26,2017.

“Tundu Lissu yuko hospitali ana uguza majeraha ya risasi si kwasababu alifumaniwa, si kwasababu ni mwizi ni kwasababu ya kupigani haki zenu, dhambi kubwa kuliko dhambi zote duniani ni uoga na sasa kitu cha msingi sana mjue tu kwamba CCM imefika mwisho. Mmesikia Zimbabwe waliompindua Rais Mugabe sio Wapinzani aliokuwa ana wapiga mabomu ni Wanajeshi aliwavalisha yeye vyeo, walewale machinga waliokuwa wanamshangilia Mugabe leo wameandamana kusema Mugabe toka, nitamshukuru Mungu sana siku nikiona hiyo siku inafika mahali hapa, mshahara wa dhambi ni mauti na dhambi ya CCM ni kubwa sana imekaribia kwenye mauti kwasababu leo yupo Mwenyekiti wetu hapa na Katibu wetu Mkuu yuko mahali hapa na Lazaro Nyalandu yuko hapa,” alisema Lema.

“Ila niwaombe watu wa Kata hii, ukiibiwa kura unaenda nyumbani mwanaume una mwambia mke wako tumeibiwa kura mama mtafutie sketi huyo baba kama ambavyo Katiba inaruhusu kuzuia uhalifu wa aina yoyote kwa mwananchi yoyote ndivyo ambavyo Katiba ina ruhusu kulinda kura zako viongozi wameandaa mawakala wazuri sana kwahiyo ukishaa piga kura kaa mita 100.”

Msajili wa Vyama Atoa Onyo kwa Vyama vya Siasa

$
0
0
Msajili wa Vyama  Atoa Onyo kwa Vyama vya Siasa
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amevionya vyama vya siasa na kutaka vifanye kampeni kwa kufuata sheria, vikijiepusha na vitendo vya matusi na uchochezi.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Jumapili hii Novemba 19,2017 na Jaji Mutungi amesema maneno ya uongo, matusi na uchochezi kwenye kampeni ni kinyume cha sheria.

Sina shaka na mwitikio wa ushiriki wa vyama vya siasa katika kampeni za Uchaguzi mdogo wa madiwani unaendelea nchini katika kata 43 zilizoanza Oktoba 26 na zinazotarajiwa kuhitimishwa Novemba 25 mwaka huu, hata hivyo, zimebainika kasoro ndogo ndogo ambazo si ishara nzuri kuelekea uchaguzi wa amani.

Siyo jambo lenye tija kuacha kasoro hizi ziote mizizi, tunastahili kukemea kasoro hizi kwa nguvu zote, hivyo naviasa vyama vya siasa na wagombea wote wanaoshiriki katika uchaguzi huu mdogo wa madiwani kujiepusha na yafuatavyo:-

a) Kuepuka kutumia maneno ya uongo na yenye kuudhi, matusi, uchochezi, kashfa, na mambo yanayofanana na hayo kwani ni kinyume na sheria na , badala yake vyama vinadi sera zao;

b) Kuepuka vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani na kuepuka propaganda ambazo zinawatia hofu wananchi na wapiga kura.

c) Kutochukua hatua za kisheria mkononi na kutojihusisha na vitendo vya uchokozi mfano kuingilia mikutano ya kampeni ya chama kingine, kuchoma ama kuchana bendera/ mabango ya chama kingine ;

d) Kutojihusisha na vitendo vyovyote vya rushwa, mfano kununua wapiga kura au kuuza shahada ya mpiga kura;
e) Kuepuka propaganda ambazo zinawatia hofu wananchi na wapiga kura.

Aidha ni vyema vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi huu pia kuelewa kuwa, vina wajibu wa kisheria wa kuwaasa na kuwadhibiti wanachama na wagombea wao kuheshimu na kufuata Sheria zote zinazohusika. Hivyo, kila chama kitekeleze wajibu wake, ili uchaguzi huu ufanyike kwa amani na utulivu.

Pia ninawaomba sana Waandishi wa habari kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia maadili ya kazi zenu wakati huu wa kampeni na uchaguzi ili kuwasaidia wananchi kupata taarifa sahihi.

Ifahamike kwa wadau wote kwamba, maafisa kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa wapo katika kata zote 43 wakifanya uangalizi wa karibu kubaini ukiukwaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Gharama za uchaguzi.

Lengo kuu ni kuhakiksha kuwa kunakuwepo uwanja sawa wa ushindani katika uchaguzi, hakuna chama chochote kinachoingilia mikutano ya chama kingine kwa kufanya vurugu, kuepusha matumizi makubwa ya fedha na kuweka uwazi katika matumizi ya fedha na rasilimali nyingine katika kampeni. Hivyo kila chama cha siasa ambacho kinashiriki katika uchaguzi kinapaswa kuwashawishi wananchi kwa sera zake na si vinginevyo.

Miongoni mwa majukumu ambayo yanatekelezwa na maafisa wa ofisi yangu kwa sasa katika kata hizo 43 ni pamoja na kutoa mafunzo elekezi kwa vyama vya siasa, wagombea wa Udiwani, viongozi wao na wananchi kwa ujumla juu ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi na matendo yaliyokatazwa wakati wa kampeni na uchaguzi na kutoa taarifa juu ya mwenendo wa kampeni. Naamini elimu hii itaendelea kuwaongezea Umma ufahamu wa dhamira nzuri ya Serikali katika kukuza demokrasia nchini.

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ina jukumu la kisheria la kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa namba 5 ya mwaka 1992 na Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya mwaka 2010 na Kanuni zake katika chaguzi zote ikiwamo chaguzi ndogo za wabunge na madiwani.

Jaji Francis S.K. Mutungi

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA

19 Novemba, 2017
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images