Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Mateso Yamwandama Madam Rita Atembelea Magogo Mwaka Mzima Sasa

$
0
0
MATESO! Mkurugenzi wa Kampuni ya  Benchmark Productions inayoendesha shindano la kusaka vipaji vya muziki, Bongo Star Search (BSS), Rita Paulsen ‘Madam’ amesimulia mateso aliyopitia takriban mwaka sasa (siku 365) baada kuvunjika mguu mwaka jana alipopata ajali ya gari katikati ya Jiji la Dar.


 Akizungumza na Ijumaa Wikienda kwenye mahojiano maalum hivi karibuni aliponaswa na gongo linalomsaidia kutembea, Madam Rita alisema kwa kusikitisha kwamba, baada ya kupata ajali alitibiwa kwenye Hospitali ya Muhimbili lakini madaktari walimwambia aliteguka tu kumbe alikuwa amevunjika mfupa.

“Nimepitia mateso makubwa. Mwaka jana baada ya kupata ajali na kuvunjika mguu nilipopelekwa Muhimbili waliniambia nimeteguka tu, na wakaamua kunifunga hogo ambalo baadaye walinifungua na kuniambia nimepona,” alisimulia Madam Rita na kuongeza:

 “Baada ya pale nilianza kujiachia hata niliposikia maumivu na kuwaambia walisema niukanyagie tu kwamba hali hiyo ingebadilika kwa sababu ulielekea kupona, kumbe nilikuwa nimevunjika kabisa mfupa na kama ningejua siku nyingi hata nisingejiumiza kiasi hicho.

“Ujue baada ya kuambiwa hivyo, nilishangaa kuona maumivu yanazidi, nikaamua kwenda nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kuuangalia zaidi mguu wangu kwa sababu maumivu yalikuwa yakiongezeka kila siku.

“Nilikwenda kwenye Hospitali ya Morning Site ya Afrika Kusini ambapo nilifanyiwa upasuaji na kugundulika nilivunjika mfupa na kwamba tayari nilipokuwa nikitembea ilikuwa ikipandiana.

“Ona sasa nilivyoteswa na mguu huu maana ajali nilipata mwaka jana na huu upasuaji nimefanyiwa mwaka huu Afrika Kusini.

“Naona bora pale Fame Centre (Dar) maana wao waligundua tatizo na kunishauri kwenda Sauzi ambapo nimefanyiwa upasuaji na mguu unaelekea kupona kwa sababu mwanzo nilikuwa natumia magongo mawili lakini ona leo ninajikongoja kwa gongo moja ambalo nalo si muhimu sana sasa.”

Al-Shabab washambulia tena Kenya na kuua watu 29 wasio na hatia

$
0
0
Watu 29 wameripotiwa kupoteza maisha baada ya watu wenye silaha za moto kufanya mashambulizi mawili katika eneo la Lamu, Pwani ya Kenya, Jumamosi (July 5).

Mashuhuda wa tukio hilo wameeleza kuwa watu hao waliokuwa na silaha nzito walivamia kituo cha biashara katika kijiji cha Hindi, Lamu na pia Kituo cha Polisi cha Gamba Jumamosi usiku.

Shambulizi hilo liliwalenga wananchi wasio na hatia na kuharibu magari na nyumba.

Kundi la kigaidi la Al-Shabab limedai kuhusika moja kwa moja na mauaji hayo kwa sabababu za kulipiza kisasi kwa kuwa wanajeshi wa Kenya wanalisaka kundi hilo nchini Somalia.

Kundi hilo lilidai kuhusika pia na mashabulizi mengine yaliyofanyika awali kwa sababu kama hizo.

Jumapili, July 6, Makamo wa rais wa Kenya, William Ruto alilitembelea maeneo yaliyoshambuliwa..
Funny Quote of the Day
If you can't convince them, confuse them.

Wasichana 63 waliotekwa na Boko Haram watoroka na kurejea Nyumbani

$
0
0

Wasichana 63 waliotekwa na kundi la Boko Haram mwezi mmoja uliopita wamefanikiwa kutoroka kutoka kwenye kambi waliyokuwa wamefichwa na kurejea makwao.

Kwa mujibu wa maafisa wa Nigeria, idadi hiyo inawajumuisha wanawake waliotekwa na Boko Haram kutoka kwenye kijiji cha Kummabza, Borno wiki mbili zilizopita.

Ingawa serikali kuu haikutoa taarifa rasmi juu ya tukio hilo, Gavana wa Borno, Alhaji Kashim Shittima alitoa maelezo juu ya taarifa hizo.

Vyanzo vya ulinzi, wakazi wa maeneo hayo na watu waliowashuhudia wanawake hao wamewaambia waandishi wa habari kuwa waliwashuhudia wanawake zaidi ya 60 waliorejea makwao Jumamosi.

Inaelezwa kuwa wanawake hao walitoroka Ijumaa usiku, wakati ambapo wanajeshi wa Boko Haram walienda kushambulia kambi za jeshi la Nigeria ambapo maafisa wanadai waliwauwa wanajeshi wa Boko Haram zaidi ya 50 katika mashambulizi hayo.

Hata hivyo, bado Boko Haram wanawashikilia wasichana wengine zaidi ya 200 waliowateka kati ya April na July mwaka huu..

Funny Quote of the Day
If you can't convince them, confuse them.

Lulu Michael Awafungukia Wabaya Wake Wanao Mchafua Kila Siku

$
0
0
Stori: shakoor jongo
Kumbe! Sexy lady wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kwamba amewajua wabaya wake wanaomfuatilia na kumsakama kwa ubaya katika maisha yake, amewaonya kuwa dawa yao ipo jikoni.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda wikiendi iliyopita jijini Dar, Lulu alisema kuwa kila kukicha lazima watu hao waibuke na jipya linalomhusu yeye, mbaya zaidi ni kwa ajili ya kumchafua.

“Mara utasikia Lulu kagombania bwana, mara Lulu kafanya sijui kitu gani lakini ukiangalia hakuna hata cha ukweli kwa kuwa nimekuwa staa basi kila mtu ana lake la kuongea, kifupi nimeshawajua wabaya wangu na kwamba ni wengi sana, nawaambia niko njiani kuwaandalia dawa yao ambayo naamini itakuja kuwa fundisho kwao na kwa wengine,” alisema Lulu.

Hii ni mara ya kwanza kwa muigizaji huyo kufunguka kuhusu suala hilo lakini Ijumaa Wikienda linamuomba asichukue sheria mkononi kwani kibao kinaweza kumgeukia.
GPL
Funny Quote of the Day
If you can't convince them, confuse them.

Nani Kasema Nimehongwa Gari ? Acheni Umbeya Mwenzenu Najituma

$
0
0
Mafanikio! Taarifa ikufikie kuwa staa wa Bongo Fleva, Estalina Sanga ‘Linah’ amekanusha stori za madai ya kuhongwa gari jipya analosukuma mjini kwa sasa aina ya Toyota Mark X.

Akizungumza na mwanahabari wetu, Linah ambaye hivi karibuni alitokea nchini Afrika Kusini kufanya video ya wimbo wake mpya alisema mkoko huo amepewa na kampuni anayofanya nayo kazi ya NFZ.

“Nani kasema nimehongwa gari? Siwezi kuhongwa gari kwani najituma sana kwemye kazi yangu,” alisema Linah.Mbali na kumiliki ndinga hilo, miezi kadhaa iliyopita aliwajengea nyumba wazazi wake na sasa anajenga ya kwake.

Funny Quote of the Day
If you can't convince them, confuse them.
Post Sponsored By Kenyangossip.com

Picha za Wema Sepetu, Aunty Ezekiel na Martin Kadinda Zatibua Swaumu

$
0
0

OOHOO! Picha ambazo hazijakaa poa katika kipindi hiki cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani za mastaa, Aunt Ezekiel, Wema Sepetu na Martin Kadinda zimetibua swaumu za Waislamu waliofunga.

Picha hizo zinazoonesha ni za kipindi cha Wema cha In My Shoes kinachorushwa kupitia EATV, zinawaonesha sehemu ya juu wakiwa wazi.

“Huyu aliyeachia hizi picha ametutibua sana sisi tuliofunga, alilenga kutuharibia swaumu zetu, haijakaa poa sana,” ilisomeka sehemu ya maoni ya picha hizo kwenye mitandao ya kijamii.

Funny Quote of the Day
If you can't convince them, confuse them.

Tazama Video Mpya Iliyosubiriwa Kwa Hamu Ya Diamond Platnumz-Mdogo Mdogo

$
0
0

Video Mpya ya Wimbo wa Diamond unaotamba kwa sasa Mitaani-Mdogo Mdogo Bro Hata sijalala just been on Your youtube Channel..But One thing its worth my Sleep..Such an Amazing Hit..Brother Your the best na kweli watajiuliza kama kunamwingine kaibiwa....Gud Stuff Diamond Video Hii Hapa Chini:

New Video:Diamond Platnumz Feat Iyanya - Bum Bum (Official Video)

$
0
0
Well done Diamond , though wanted to see more shakes from that lady with red gown and those dancers... am in love with your creativity but make sure hupotezi ladha ya mziki wetu wenye ladha ya kikwetu, wanaiger wasikuchote sanaaaaaa...... Nice voice, You are the best Diamond.....You are an international artist ..Proudly to have You as my Tanzanian artist...GOOOOOOO Diamond

Video Hii Hapa:

Chris Brown and Karrueche Tran Call it Quits...Again?

$
0
0

What are these two up to again? Just last week, it was all good between them with Chris posting butt pics of Karrueche on his instagram page. But it looks like they may have called it quits....again!

Over the weekend, fans noticed that Chris and his long-suffering girlfriend Karrueche had deleted all photos of each other from their respective Instagram accounts...and then Karrueche posted cryptic posts right after deleting Chris Brown from her Instagram life.


Chadema:Tumeshtuka Hatuchukui Tena Makapi ya Kutoka CCM

$
0
0
 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakitasubiri wanachama watakaoachwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uteuzi wa wagombea katika uchaguzi mkuu ujao.

Kutokana na tamaa ya kuingiza watu wengi kwenye Bunge, vyama vya upinzani vimekuwa na tabia ya kuwapokea wanachama wa CCM wanaoshindwa kwenye kura za maoni na baadaye kuwapa nafasi ya kugombea ubunge, lakini Dk Slaa anasema safari hii hawatakuwa tayari kufanya hivyo.

 “Tulishasema kwamba kwa ngazi zozote hata ngazi za udiwani au ubunge hatusubiri mabaki, makapi yatakayotokea CCM ndiyo yaje kwetu,” alisema Dk Slaa katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam.

“Safari hii hatusubiri. Tulishasema kuwa wagombea wetu tunawaandaa mapema ili tusitegemee mtu anayekuja dakika za mwisho kuwa ndiyo atuokoe.”

Kauli ya Dk Slaa inaweka msisitizo katika ile iliyowahi kutolewa na mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwamba hawatapokea wanasiasa watakaoihama CCM ili kupata nafasi za uongozi kwa tiketi ya Chadema.

Katika mahojiano hayo, Dk Slaa alisema: “Huwezi kuzuia kupokea mwanachama kokote alikotokea, lakini unapofika wakati wa kuweka watu katika nafasi, lazima ufikirie.”

Mwaka 2010, Chadema ilipokea wagombea wawili walioshindwa kwenye kura za maoni za CCM, John Shibuda aliyeshindwa katika kura za maoni za Maswa Magharibi na Freddy Mpendazoe ambaye alienguliwa kwenye kura za maoni za CCM Jimbo la Segerea.

Shibuda alifanikiwa kurudi bungeni baada ya kushinda uchaguzi wakati Mpendazoe alishindwa katika hali ya kutatanisha na juhudi zake za kutengua matokeo hayo mahakamani ziligonga mwamba.

“Tatizo hilo lilitokana na ugeni wetu,” alisema Dk Slaa akizungumzia kitendo cha Chadema kupokea wagombea walioshindwa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

“Lakini kwa wakati huu, Chadema ina wanachama wengi wenye sifa za kugombea hivyo hatuhitaji kusubiri mtu,” aliongea katibu huyo mkuu ambaye aliwahi kutangaza kuwa nafasi za wagombea ubunge wa Chadema katika majimbo yote nchini zitatangazwa kwenye magazeti na watakaojitokeza, watafanyiwa usaili.

Kuhusu uchaguzi mkuu wa chama hicho, Dk Slaa alisema utafanyika Desemba mwaka huu baada ya kuridhiwa na kikao cha Kamati Kuu kitakachofanyika Julai 18.

Alisema wanahakikisha uongozi unapatikana kuanzia ngazi za chini na watachukua hatua kwa maeneo ambayo watabaini viongozi wamepeana nyadhifa bila chaguzi madhubuti kufanyika.

Quote Of The Day:
We can't help everyone, but everyone can help someone.

USAJILI: Yanga Sasa Yakubali Kumuuza Mrisho Ngasa Afrika ya Kusini

$
0
0


Uongozi wa klabu ya Yanga umetoa ruksa kwa klabu ya Free State Stars ya Afrika Kusini kufanya mazungumzo kama wanataka kumsajili mchezaji wao nyota, Mrisho Ngasa.

Awali klabu hiyo ilishangazwa na hatua ya klabu hiyo kubwa inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini kumchukua mchezaji wao kinyemela na kumfanyisha majaribio kinyume na taratibu na kanuni za mpira wa miguu duniani.

Ngassa alikwenda kufanya majaribio na timu hiyo ya Afrika Kusini takribani wiki mbili zilizopita, na uongozi wa timu hiyo ulikuwa tayari kutoa Sh132 milioni ili kumsajili mchezaji huyo.

Hata hivyo, mpango huo uligonga mwamba kutokana na ukweli kuwa viongozi wa Free State Stars walifanya mpango huo na Ngassa kinyemela.

Hatua hiyo iliufanya uongozi wa Yanga kulishutumu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kuhusika moja ka moja na mpango huo kwani haukuridhishwa na jinsi Ngassa alivyoondoka nchini kwenda Afrika Kusini wakati alikuwa kwenye Kambi ya Taifa Stars.

Katibu Mkuu wa Yanga, Benno Njovu alisema kuwa wametoa fursa kwa uongozi wa timu hiyo ya Afrika Kusini kuja nchini na kufanya mazungumzo mezani ili kufanikisha suala hilo.

Njovu alisema kuwa Yanga haina haja ya kumzuia Ngassa kwenda kucheza soka lake Afrika Kusini kwani hiyo ndiyo kazi yake.

“Tutakuwa hatufanyi haki kumzuia Ngassa, lakini cha ajabu ni kwamba mpaka sasa sijamwona Ngassa kuja kuzungumzia suala hilo, nimemwona kwa mbali sana na wala hakuja kuonana na mimi, pamoja na hayo yote, sisi tupo tayari kuzungumza na timu hiyo aliyokwenda kufanya mazoezi,” alisema Njovu.

Alisema kuwa hata fedha ambazo klabu hiyo imeahidi kuzitoa kwa Yanga, wao wanazisoma kupitia mitandao tu kwani hakuna mawasiliano yoyote. “Nasisitiza waje kuonana na sisi ili kufanikisha suala hilo, hatuna kinyongo  kuhusiana na mpango wake mpya, wasituogope kwani klabu yetu ipo eneo la wazi na kila mtu anaijua, ila ‘njia za panya’ hatutaki katika masuala haya makubwa yanayohusu usajili na ustawi wa wachezaji wetu,” alisema Njovu.

Ngassa alionyesha kuridhishwa na mwenendo wa suala hilo baada ya hatua hiyo ya uongozi wake.

“Sina la kuongezea, si unajua kuwa soka ni kazi yangu na masilahi ndiyo kila mtu anataka, Free State Stars wamenikubali na wapo tayari kutoa fedha kwa Yanga ili wanisajili, kinachotakiwa ni makubaliano tu kati ya Yanga na Free State Stars, sasa sijui awali ilishindikana nini,” alisema Ngassa.

Quote Of The Day:
We can't help everyone, but everyone can help someone.

Maiti Zalazwa Vitanda vya Wagonjwa Badala ya Kuifadhiwa Motuari

$
0
0
Wananchi wanaopata huduma za afya katika kituo cha afya Murongo wilayani Kyerwa mkoani Kagera, wameuomba uongozi wa kituo hicho kujenga chumba cha kuhifadhia maiti ili kuwaondolea adha wananchi wanayokumbana nayo baada ya kushuhudia maiti zikilazwa kwenye vitanda vya wagonjwa.

Wakizungumza na gazeti hili jana, wananchi hao walisema kuwa kutokana na kituo hicho kutokuwa na chumba cha kuhifadhia maiti wameiomba bodi ya afya ili kusaidia ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti, kuondoa adha wanayokumbana nayo ya kushuhudia maiti zikilazwa kwenye vitanda vya wagonjwa.

Mmoja wa wananchi hao, Sebastiani Katunzi alisema wanapopata msiba katika hospitali hiyo wanakumbana na changamoto nyingi, kwani maiti zinalazwa kwenye vitanda vya wagonjwa jambo linalowatia wasiwasi wagonjwa waliopo wodini.

“Tumeiomba bodi ya afya wilayani hapa isaidie kujenga chumba cha kuhifadhia maiti, kwani watu tunapopata misiba tunakuwa na wasiwasi, kwani tunashuhudia maiti zikilazwa kwenye vitanda vya wagonjwa jambo ambalo siyo jema,” alisema Katunzi

Mganga Mkuu wa kituo hicho, Alobogasti Nkabyemanyira alisema kituo hicho cha afya Morongo tangu kianzishwe wagonjwa waliokuwa wanalazwa walikuwa ni wachache, hivyo ingetokea mgonjwa akafariki alikuwa anasafirishwa siku hiyo.

Nkabyemanyira alikiri kuwapo  kwa tatizo hilo la kutokuwa na chumba cha kuhifadhia maiti na kueleza kwamba wagonjwa wameongezeka  kiasi kikubwa na kusababisha kuwapo kwa upungufu wa vitanda pia.

“Ni kweli kuna tatizo, lakini tutawasilina na uongozi wa wilaya ili bajeti ya mwaka ujao iweze kukidhi mahitaji kama hayo,” alisema Dk Nkabyemanyira.

Quote Of The Day:
We can't help everyone, but everyone can help someone.

Kwanini Wanawake Wanawahi Kusahau Shida Walizopitia

$
0
0
Unamkuta binti kijijini kachoka, kapigika hata mafuta ya kujipaka hana anavaa kandambili za kuunga lakini kwa kumuangalia tu ana sura nzuri japo haina matunzo ukioa ukaja nae mjini ukamfungulia kamradi akaanza kupata hela anasahau shida zote za kijijini na kuanza dharau kwa mmewe na akumbuki tena alipotekea, ipo mifano mingi sana ambayo inafikia hata wanaume kujiua kutoka na usaliti wa Aina hii , Sio la kutoka kijijini tu pia hili la unakuta mdada hana hili wala lile anatokea jamaa anajitolea kumsomesha mpaka chuo ila akishamaliza tu chuo na kupata kazi jamaa aandike maumivu ndo basi tena......Dharau mtindo mmoja kashasahau alipotoka......

Diamond Amzawadia Mama Yake Gari Siku ya Birthday Yake Jana (Video)

$
0
0
Ingawa hayupo Tanzania lakini hakungoja mpaka arudi ndipo akabidhi zawadi hii badala yake alichokifanya ni mara baada ya kukamilisha kila kitu kinachoihusu gari hii Diamond Platnumz aliwapatia mameneja wake kwa ajili ya kuiwasilisha kwa mama yake.
Ni Toyota Harrier Lexus New Model ambapo Babu Tale amesema imegaharimi milioni 38.1 ambapo milioni 35 imetumika kulinunulia gari hilo mpaka kuingia Tanzania na Milion 3.1 imetumika kulipamba na kuweka Music System pamoja na seat Cover.
Zawadi hii ameitoa Diamond kwa mama yake kama zawadi kwa ajili ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa mama yake ambaye amesema ametimiza miaka 55, mama yake amesema hakutegemea zawadi hii na anamuombea mwanae kwa Mungu afanikiwe zaidi.

Mama Diamond Was Surprised When She Cerebrating Her Birthday…Wema Sepetu Gave Her
Car Keys

Majina ya Watanzania Waliofungwa Nje ya nchi Baada ya Kukamatwa na Madawa ya Kulevya

$
0
0
Majina 403 ya Watanzania waliokamatwa, kufungwa au kushikiliwa katika magereza mbalimbali duniani kwa makosa ya madawa ya kulevya ‘unga’.

Baadhi ya watuhumuiwa wa kiume waliokamatwa kwa makosa ya kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya ‘unga’.

Hivi karibuni, serikali ilikiri kukamatwa kwa Wabongo hao nje ya nchi na kusema baadhi yao wanasubiri kunyongwa baada ya kupatikana na hatia. Hata hivyo, serikali ilificha majina ya watu hao.

Ifuatayo ni orodha ya majina hayo na maeneo wanayotoka nchini Tanzania. Kwenye mabano ni hukumu zao.

Abdallah Ally Rashid Mbonde Fredue, Dar (miaka 15 jela), Mzia David Michael, Dar (22), Rashid Mzonge, Magomeni, Dar (maisha), Salum Jumbe Pigigi (maisha), Ramadhan Iddi Juma, Kinondoni, Dar (7), Saleh Happy Hambona, Dar (18), Michael Dalasi Taraja, Temeke, Dar (19) na Juma Omar Mgeni (kunyongwa).

Wengine ni Masumbuko Salum Hassan, Dar (kunyongwa), Luka Joseph Urio, Dar (maisha), Masome Frorian Anthony, Dar (maisha), Salum Mohammed Kitupura, Dar (kunyongwa), Begge Hemed Ahmed, Tanga (15) na Mwanjati James Simon, Dar (maisha).

Wengine ni Mohammed Musa Mohammed, Dar (maisha), Omalla Donald Nyowino, Dar (15), Yahya Ally Seif, Kinondoni, Dar (maisha), Chande Mohammed Chande, Kinondoni, Dar (maisha), John James Amandus, Kinondoni, Dar (kunyongwa), Bantulaki Isihaka Ally, Tanga (kunyongwa), Zungiza Mohamed Ally, Dar (kunyongwa), Rashid Bakari Mzonge, Kimara Suka, Dar (maisha), Mende Katija Mikidadi, Ilala, Dar (maisha), Shame Shame Udai, Dar (maisha) na Mlenzi Mangala Hamisi, Dar (maisha).

Baadhi ya watuhumuiwa wa kike waliokamatwa kwa makosa ya kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya ‘unga’. Farida Sarboko Makarani, Zanzibar (kunyongwa), Adam Hariri Mohammed, Magomeni, Dar (18), Said Mfaume Said, hajatajwa wa wapi (kunyongwa), Mohammed Bakari Mkemi, haijatajwa wa wapi (kunyongwa), Mariam Ramadhan Mahimbo, hajatajwa wa wapi (kunyongwa), Julieth Jonathan Jaspher, haikusemwa anakotoka (kunyongwa), Halifa Matumla Ally, haijaandikwa atokako (kunyongwa), Rajabu Salum Mwanyenza, haijaandikwa atokako (kunyongwa), Ismail Mohammed Rajabu Mapusa, Magomeni Dar (maisha) na Hamisi Kombo Ally (kunyongwa).

Waliopo mbaroni ambao pia hawajaandikwa watokako ni: Sephu Abdulrahman, Alfredy Thomas Singini, Lawrence Mbogoni Oni, Mohammed Ibrahimu Kilima, Wilfred Casmir Mushi, Shakira Ahmed Mumba, Jackline Benedict, Rajabu Rashidi Mshare, John Peter Martin, Abdallah Mwalimu Mbaruk, Rashid Mzee Mrisho, Juma Ismail Nayopa, Tsakiris Costa Achelis na Faith Michael Kabambe.

Wengine waliohukumiwa ni Bakari Badi Omari Mneko, Sinza, Dar (17), Masomi Thomas Joseph, Dar (17), Abdallah Iddi Ally, Tabata, Dar (17), Kondo Ally Mohammed (20), Mohammed Abubakar Nazzir (24), Abdallah Anwar Abasi (24), Makuti Al- Jaribu Hassan, Kilwa, Lindi (25), Abdallah Iddi Athuman (24), Mnyamani Hamad Ally, Tanga (22), Mtalu Rajabu Ally Rajabu, Kariakoo, Dar (17) na Shughuli Kibaya Bakari, Tanga (8).

Wengine ni Mfaume Omar Ng’anzi Msuya, Kariakoo, Dar (21), Steven Robert Onay (9), Omar Juma Mang’enge (8), Steven Simon Kanul, Dar (8), Iddi Haji Fumo, Unguja (9) na Seleman Hamisi, Unguja (8).

Pia wapo Athuman Hassan Nash, Magomeni, Dar (8), Seleman Hussein Msimbe (8), Abdallah Farid Twalib, Dar (17), Salim Ally Amani, haikutajwa anakotoka (22), Calist Wilson Mosha, Arusha (18) na Saleh Abdul Omar, Kigogo, Dar (21).

Wengine ni Bugingo Sweetbert Rwezaura, Kijitonyama, Dar (21), Mohammed Omari Ally, Zanzibar (19), Sayula Rashid Paul, hajatajwa atokako (16), Koshuma Geofrey Gabriel, Kijitonyama, Dar (30) na Salim Mrisho Hussein, Tanga (21).

Orodha inaendelea kama ifuatavyo: Riziki Riziki Hamduni, Kinondoni, Dar (19), Bashir Rajabu Kafune, Magomeni, Dar (19), Kharim Mohammed Omar, Ilala, Dar (19), Abubakar Abdul Ligalwike, Kinondoni, Dar (8).

Wengine waliofungwa na miaka yao katika mabano ni Pendo Ernest Kessy, Ilala, Dar (9), Anna Kiula, Kijitonyama, Dar (9), Nuru Shebe Maftah, Mwananyamala, Dar (9), Fatma Rashid, Dar (9) na Naima Abdulhafidh Rashid, Mwananyamala, Dar (9).

Pia wapo Mariam Madaresa, Arusha na Dar (9), Mohammed Omar Ally, Wete, Zanzibar (19), Faidhi Mohammed Abdallah, Kijitonyama, Dar (14), Mohammed Ijumaa Rashid, Mbezi Beach, Dar (10), Omari Musa Abdallah, Tanga (10), Zahra Ayubu Mwila, Korogwe na Kibaha (25) na Shamsa Gulum Shambe, Magomeni Mwembechai, Dar (16).

Wengine waliopo mbaroni ni Jeniffer Kessy, Mwananyamala, Dar, Shadia Issa, Mbezi Beach, Dar, Rosemary Asakwe Kionaumela, Mapipa, Dar na Samir Sandra Khalid.

Orodha ya waliohukumiwa inaendelea: Tatiana Bakari Chambo, Temeke, Dar (11), Ramadhan Maneno Mtumwa, Kijitonyama, Dar (14), Yusuf Herold John, Magomeni (18), Hassan Hiza Sebudu, Tanga (22), Halfa Abdallah Ng’anga, Ilala, Dar (19) na Nelson Anthony Dhinner, Kigogo, Dar (14).

Wengine waliohukumiwa ni Awadh Salehe Awadh, Kinondoni, Dar (24), Hasim Paul Syula, Mapipa, Dar (16), Fussy Abdu Mussa, haijatajwa anakotokea (17), Mtwanzi Carlos Adam, haijatwaja anakotoka (17) na Yusuf Abbas Kilima, Dar (5).

Wafuatao wametiwa mbaroni; Salum Mhibu Mkwawira, Tunduma, Mbeya, Juma Musa Juma wa Zanzibar, Nassor Mohammed Ayub wa Tanga, Jimmy Joseph Kivelege wa Dar, Kilugage Joram Masembo wa Kahama, Shinyanga, Manengelo Abdurahman wa Dar na Hamud Ali Mohammed (mji haukutajwa).

Wengine ni Eric Charles Mkude wa Tanga, Makame Khatibu Ali wa Kiembesamaki, Zanzibar, Abdulwahid Hamisi Mashauzi wa Singida, Said Ally Makame wa Zanzibar, Peter George Gyellah wa Tegeta, Dar, Said Abdallah Mzee wa Dar na Yusuf Chombo Khalid wa Dar.

Wafuatao wamehukumiwa na miaka yao kwenye mabano; Salehe Mohammed Aboubakar, Tanga (20), Abdul Omar Salehe, Dar (14), Omari Hussein Ally, Tanga (14), Kaliro Samson Majani Busagaga, Tarime, Mara (9), Mohammed Salum Mbaraka, Moshi, Kilimanjaro (9), Zuberi Musa Zuberi, Zanzibar na Dar (9), Adam Athumani Udindo (alikataa kutaja anakotoka, 14).

Wafuatao pia wapo mahabusu katika nchi mbalimbali, kesi zinaendelea; Frank Thomas Frank (Moshi), Nasra Hassani Masogoa (Dar), Nice Saidi Mbwana (Tanga na Dar), Josephine Raymond Malibanga (hakutaja atokako), Sara Yuga Mtinda (Singida), Amina Khamisi Bwanga (hakutaja atokako), Flora Frederick Siyame (Dar) na Zawadi Aloyce Henjewele (Songea).

Wengine ni Upendo Eric Shayo wa Moshi, Mariam Haruna Feruzi (Dar), Yusta Riwa (Moshi Kilimanjaro), Watende Sudi Kiwamba (Tabora), Elizabeth Yoram Kwambaza (Korogwe, Tanga), Mariam Shabibi (Dar) na Zahoro Mohammed Nassoro (Tanga).

Wengine waliokamatwa na wako mahabusu ni Rashid Nassoro Maumba (Mpanda), Mohamed Said Mrisho (Tanga), Suleiman Said Mpetula (Dar), Shaban Salum Mnyimani (Dar), Abood Yasser Ali (Tanga), Juma Shabani Ngoma (Tanga), Juma Akida Yusufu (Tanga) na Miraji Yusufu Semahimbo (Tanga).

Wengine ni James Christopher Lukio (Tanga na Dar), Rabin Issa Mbaba (Mafia), Abdallah Rajabu Dole (Dar), James Sakaya Henry (Dar), Bakari Kheri Nassoro (Dar), Faraji Juma Lota (Dar), Gervas Anselm Muganda Matura (Musoma), Rawe Waikama Magarya (Tarime) na Abdulraheem Sadiki Mohamed (Dar).

Wafuatao wamehukumiwa na miaka yao kwenye mabano ila miji waliyotoka Bongo haikutajwa; Rashid Habib Muhsin (9), Abdallah Saidi (16), Hiridi Mamdadi Issa (12), Juma Mohammed Mapande (16), Mwatadi Kulwa Hamisi (16), Hamisi Abdallah Mohammed (9), Erick John Ibrahim (16) na Abdallah Farid Salum (9).

Thuweni Hamadi Suleiman, Kileo Walter Exaudy na Jacqueline Clifford Fitzpatricque (Jack Patrick) hawa bado hawajahukumiwa.

IDADI YA NCHI

Katika orodha hiyo, China wapo Wabongo 65, Brazil 108, Kenya 34, Hong Kong 118, Pakistan 16, Falme za Kiarabu 12, Japan 7, Morihsaz 6, Uingereza 5, Malawi 5, Uganda 4, Oman 3, Uswisi 2, Italia 2, Marekani 2, Argentina 2, Uturuki 1, Ureno 1, Botswana 5, Chile 1, Afrika Kusini 3 na Msumbiji 1.

paparazi aliongea na Kaimu Kamishna wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya, Aida Tesha (pichani) kuhusu kukamatwa kwa watu hao ambapo alikiri na kusema kuwa serikali inaendelea kufuatilia takwimu za Watanzania wengine ambao wamekamatwa nje ya nchi.

Bomu Lingine Larushwa Hotelini Arusha na Kujeruhi Watu Kadhaa (Picha)

$
0
0

Bomu limerushwa na watu waliokuwa kwenye pikipiki nakujeruhi watu zaidi ya wanane waliokuwa wakipata chakula cha jioni katika mgahawa wa Vema.



Quote Of The Day:
We can't help everyone, but everyone can help someone.

RACHEL wa T.H.T achanganyiwa Bangi na UNGA…Juhudi za haraka zatakiwa kumnasua

$
0
0
Kama  ilivyotokea  kwa  msanii nyota  wa  kike  wa  bongo  fleva, Rehema  Chalamira  ‘Ray C’  kuingizwa  katika  matumizi  ya  dawa  ya  kulevya  na  mtu  ambaye  alitokea  kumwamini  sana, ndivyo  ilivyotokea  sasa  kwa   msanii  anayefuata  nyendo  zake, Winfrida  Josephat ‘Rachel’  ambapo  anadaiwa  kuvutishwa  unga  bila  kujua….

Kwa  mujibu  wa  chanzo  chetu  cha  karibu  na  msanii  huyo,Rachel  amewekewa  dawa  hizo  kupitia  kwenye  bangi  na  wakati  mwingine  kwenye  sigara hivyo  inakuwa  vigumu  kubaini  hila  iliyofanyika….

Habari  ambazo  tumezipata  zinadai  kwamba msanii  wa  kiume  nyota  wa  bongo  fleva ambaye  amewahi  kutuhumiwa  kutumia  dawa  za  kulevya  ndiye  anayemtengenezea  kokuteli  hiyo  inayotarajiwa  kumwangamiza  siku  za  usoni….

“Huyu  mtoto  ameshaanza  kutumia  dawa  za  kulevya.Huwezi  amini, hata  Ray C ameshapewa  taarifa,  hivyo  anamsaka  kuhakikisha  anamtoa  katika  kifungo  alichojiingiza…

“Unajua  Ray C anampenda  sana  kutokana  na  namna  anavyopenda  kujiweka  kama  yeye na  hata  jinsi  anavyoimba  nyimbo  zake, hivyo  aliposikia  madai  hayo  alianza  kumsaka  kila  kona  lakini  bado  hajafanikiwa  kwani  Rachel  anamkimbia,” kimesema  chanzo  hicho.

Hata  hivyo  habari  zaidi  zinasema  kuwa  kutokana  na  namna  Rachel  anavyomuamini  msanii  huyo  wa  kiume  hajakubali  kama  anachanganyiwa  dawa  za  kulevya  kwenye  bangi  na  sigara.

“Mwenyewe  anajiona  yupo  sawa, lakini  sisi  tunaona  tofauti, hakika  Rachel  anapotea  na  sijui  nani  atamuokoa.

“Tumeshamwabia  kwamba  anapotea  lakini  haamini, tunaweza  kusema  kwamba  Ray C aliponea  bahati, sasa  sijui  kama  na  yeye  atapata  bahati  kama  alivyopata  mwenzake, “ kilisema  chanzo  hicho

Rachel  ambaye  anatamba  na  wimbo  wa  ‘upepo’  hakuweza  kupatikana  kuzungumzia  tuhuma  hizo


Quote Of The Day:
We can't help everyone, but everyone can help someone.

Exclusive: Video za Bum Bum na Mdogo Mdogo zimemgharimu Diamond shilingi milioni 130!

$
0
0
Wakati unafurahia kuangalia video kali mbili za Diamond Platnumz, Bum Bum na Mdogo Mdogo zilizoachiwa kwa pamoja jana, tungependa kukufahamisha kuwa ubora huo unaouona haujaja kwa pesa za nyanya.

Bum Bum na Mdogo Mdogo zimemgharimu Diamond dola 78,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 130 za Tanzania.

“Video ambayo tumefanya Uingereza imetucost dola 38,000 video ambayo tumefanya South Africa ambayo ni mdogo mdogo imetucost elfu 40,000,” amesema Tale. Akizungumza kuhusu kuwapata waigizaji kwenye video ya Mdogo Mdogo, Tale amesema walimlipa Godfather kulingana na kile walichohitaji.
Bongo5


Quote Of The Day:
We can't help everyone, but everyone can help someone.

Soma Majibishano ya Watanzania Waishio Nje ya Nchi Kuhusu Video ya Mdogo Mdogo

$
0
0
Utake ustake, wiki hii na wiki nyingine zijazo jina la Diamond litakuwa likizungumzwa sana si tu Tanzania bali sehemu nyingi duniani kwa watu wanaoufuatilia muziki wa Afrika. Kitendo chake cha kuachia video mbili kwa mpigo na tena alizotumia gharama kubwa mno kuzikamilisha, kumemfanya bila ubishi kuwa msanii namba moja na hatari zaidi Afrika Mashariki.

Pamoja na asilimia zaidi ya 90 ya watu kuipenda video ya Mdogo Mdogo, kuna asilimia nyingine ya watu wenye mtazamo tofauti. Haya ni majibizano ya watanzania wawili kwenye Youtube kuhusiana na wanavyoiona video hiyo.

KZ SLP alianza kwa kuandika:

This reminds me of Tanzania b4 1961 nuthin new here no hate music is good video is still way back mentality and reality ..Back 2 Slave time.. Kila ki2 hapa was suppose 2b the other way not this way.. What the music got 2 do wit all this. Show ur ppl be proud of ur women. And u get plenty likes cos of mzungu anacheza mchiriku.. Wazungu wenyewe huku wanashangaa why have to be like this..So next time do better.. Good music reminds back home I love it. Video? bruh I don’t think so..

Natasha M Shyrose akajibu:

It has nothing to do being proud or not proud of African women. This video shows love is pure it see no color or tribe. It is against racism and support of interrational marriage/relationship or difference. It is 2014 be loving all people of all colors and background are worthing like you and your African brother or Sister. We are all one thing. Love is the answer!

KZ SLP akajibu tena:

Miss/Mrs Natasha .. I was expecting someone 2 think or thought that am racist well am so not.. Got 4 beautiful kids with ex black and two more with my previous white wife and I got white blood in my family as ma grandpa is European.. As u say this is 2k14 well nothin has change as the time goes by. Am from Tanzania gru up in Europe .. When u say love does not have color I agree but color do have a value .. U c! Last time I was in my beautiful land was 2k13 after 14yrs and still it’s whiteman got more respected than myself .. As I was with my wife and the saddest part was she could enter places that I couldn’t if I didn’t have proper cloths.. Where I am now is way far from that.. We already pass that in edges.. This video does have memories that I c on Hollywood Slave movies everyday a white as a king and princes a dark shall bow.. So it’s a bit disappointed kinda clip. But am no racist. Jus would wanna c things changes.. Which will never so I wait till 2k50 when we will be a ruler till then let us c things on diff perspective. Jus my opinion .

Natasha M Shyrose akaandika tena:

Value is within yourself my friend. If you go to a place whereby people feel you are worthless is better to go away from such places. If some people try to undeevaluate you because of your color then know they are not right people. We should not be tired to remind people that we worth despite what they think about us most especially if they want to interact with us. Try to select everything from places, friends, people and you will see beautiful side of life. Unfortunately they are people who would rather cheer crappy characteristics than great quality just because they are supporting certain color or tribe. I think we should think of personality and qualities people have and be color blind. Those who cares of features instead of qualities have more problems than what they try to express. The are the ones who are actually weak not the one who assume oneself to be a victim.
“Let people treat you the way you want to be treated”

Greetings from Norway.
Bongo5

Je wewe Unasemaje Kuhusu Hiyo Video ?


Quote Of The Day:

We can't help everyone, but everyone can help someone.
Post Sponsored By Kenyangossip.com

Alichokisema WEMA siku ya birthday ya Mama DIAMOND PLATINUMZ

$
0
0
Mara kadhaa mama Wema Sepetu alikaririwa akisema hamkubali Diamond kuwa katika uhusiano na mwanae. Na kwa upande mwingine habari  zilidai mama Diamond hamkubali Wema bali anamkubali VJ Penny.

Sasa basi  jana ilikuwa  ni birthday ya mama Diamond ambapo Wema ameweka picha katika mtandao mmoja wa kijamii akiwa  amekumbatiana  na  mama  Diamond  kuonyesha  kuwa  hakuna  ugomvi  tena  kati  yao…..

Picha  hizo  ziliambatana  na  ujumbe  huu:

Today is this amazing woman’s birthday…naanzaje kutokumpenda na kumtakia kila lenye kheri mama’ngu kipenzi …Mungu akutangulie mummy….akuweke na azidi kukufungulia milango ya baraka mzaa chema wangu…..love you mama’ke

Quote Of The Day:

We can't help everyone, but everyone can help someone.
Post Sponsored By Kenyangossip.com

Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images