Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumanne


Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo...

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Tupo Mbagala Rangi Tatu

Orodha ya Wasanii Katika Tamasha la Fiesta Dar Waanza Kupunguzwa Lulu Diva Afunguka Sababu ya Kuondolewa

$
0
0
Wasanii Waliokua Katika Orodha ya Tamasha la Fiesta Dar Waanza Kupunguzwa Lulu Diva Afunguka Sababu ya Kuondolewa
Mwimbaji mpya wa Bongofleva Lulu Diva ambae mwaka huu umekua mwaka wake wa kwanza kupanda kwenye jukwaa la Tamasha la FIESTA, ameiambia Amplifaya ya CloudsFM kwamba amepewa taarifa za kuondolewa kwenye orodha ya Dar es salaam.

Mwanzoni alikuwepo kwenye orodha ya watakao-perform Jumamosi November 25 lakini kutokana na tamko la Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kutoruhusu muziki kupigwa maeneo ya wazi Dsm kuanzia saa sita usiku na kuendelea, Lulu amesema jina lake limekatwa katika orodha hiyo na kurudishwa kwake ni iwapo FIESTA itaongezwa muda.

Lulu alisema imefanyika hivyo sababu orodha iliyoandaliwa awali ilipangwa kama ilivyopangwa kwenye mikoa mingine mwaka huu ambako tamasha hilo lilifanyika mpaka alfajiri na ndio maana anaiomba Serikali isaidie ili FIESTA ifanyike mpaka asubuhi.

“Mwaka huu ndio mwaka niliotimiza ndoto yangu na kutumbuiza kwa mara ya kwanza kwenye FIESTA, ujira wangu ninaopata pale ninagawana na kila mtu alie nyuma yangu, Dereva, Makeup Artist, Dancers wangu na wengine ndio maana naiomba Serikali kutufikiria tena sisi Wasanii” – Lulu Diva

Baada ya Kifo Chenye Utata cha Mwanafunzi Mkoani Kilimanjaro Polisi Wamshikilia Mkuu wa Shule

$
0
0
Baada ya Kifo Chenye Utata cha Mwanafunzi Kilimanjaro Polisi Wamshikilia Mkuu wa Shule
Kamanda wa Polisi kwenye Mkoa wa Kilimanjaro Hamisi Issah anaethibitisha kwamba tarehe 10 November 2017 ndio Polisi walipata taarifa rasmi kuhusu kifo cha utatanishi cha Mtoto ambae ni Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Scolastica iliyopo Himo Moshi Kilimanjaro.

Kamanda Issah ameendelea kwa kusema “Tulifanya mahojiano tukianzia na Mmiliki wa Shule, Walinzi na Majirani na baadhi ya Wanafunzi,  katika mahojiano hayo kuna baadhi ya watu tuliwazuia ili kuendelea na uchunguzi”

“Tukishirikiana na Familia ya mtoto ambae alipotea ilikuja na plan B ambayo ilitusaidia na walisema mtoto wao tayari ameshafariki na moja kwa moja wanahusisha kifo hicho na Mmiliki wa hiyo shule” – Kamanda Issah

Makundi ambae ni Baba Mdogo wa Marehemu amesema “Tulipata taarifa ya mtoto kupotea tarehe 7 japo hatukua tunajua alipotea lini, tulivyopata taarifa tukatoka Dodoma kuja kufatilia na kwenda shuleni kwao na kiukweli taarifa tulizozipata shuleni zilikua haziridhishi kutokana na mazingira tuliyoyakuta”

“Wakati tunafatilia kwa kushirikiana na Shule na watu wengine na kituo cha Polisi cha Himo tukawa tumepata taarifa kwamba kuna Mwili uliokotwa mtoni karibia na shule ya Scolastica” – Makundi

Polisi Kilimanjaro bado inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na inamshikilia Mkuu wa shule hiyo ya Scolastica,

Nape Aweka Wazi Kuhamia Upinzani

$
0
0
Nape Aweka Wazi Kuhamia Upinzani
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nauye amesema hana mpango wa kuhama CCM kwenda upinzani na badala yake ametaka vyama hivyo visipoteze muda kudhania atahama.

Nape ametoa kauli hiyo jana Jumatatu jioni wakani wa kampeni za kumnadi mgombea udiwani wa Kata ya Reli, Genfrid Mbunda katika uwanja wa Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Alisema wapinzani wasipoteze muda wakimsubiri kuwa atahama CCM kutokana kwamba CCM ni chama bora kuliko vyama vyote vya siasa hivyo hawezi kutoka ndani ya chama hicho.

“Unajuwa wapinzani wasipoteze muda wa kusubiri mimi lini nitahama CCM badala yake wafanye kazi ya kuvijenga vyama vyao kwa sababu walitamani sana muziki huu uhamie kwao ndio maana wanabaki wanapiga kelele za kuwapa presha wanaCCM hivyo sitahama kwa sababu ukinikata mwili wangu damu yangu unakuta CCM,” alisema Nape.

Alisema kuwa CCM hakwenda kwa bahati mbaya kutokana kwamba anakijua chama hicho hivyo hakuna namna yoyote itakayoweza kumtenganisha na chama hicho.

“Kupitia changamoto katika mabonde na mawimbi ndio unaandaliwa kuwa mkomavu na kupanda juu kwa sababu ukikimbia mapema unaonekana haufahi lakini ukibaki na kuvulimia milima na mabonde ndio unaokana ni mkomavu na ukizingatia ndani ya chama hiki kuna fursa za kutosha,” alisema.

“Kupitia mabonde na milima bila kuyumba nitaendelea kusimama imara ndio maana nikaaminiwa sasa wanaodhani Nape anapitia milima na mabonde kwa sababu hata mbegu ili iote ni lazima upande chini ili iweze kuota na hiyo ndio fomula ya maisha sasa wakati mbegu inaoza watu wanaanza kuongea siji ng’o,” aliongeza Nape.

“Mimi bado sijaona mawimbi yanayoweza kumkimbiza  CCM bado nimesimama imara kwa ajili ya kupambana na mawimbi hakuna mabadiliko yasiyo na machungu hata mama mjazito hupata machungu lakini hufurahi kupata mtoto baada ya kuvumilia kwa muda mrefu,” alisema Nape.

 0     

BOT Yaeleza Kuwa Tanzania Miongoni mwa Nchi za Afrika Ambazo Uchumi Wake Unaokua kwa Kasi

$
0
0
BOT Yaeleza Kuwa Tanzania Miongoni mwa Nchi za Afrika  Ambazo Uchumi Wake Unaokua kwa Kasi
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeeleza  kuwa, Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika zenye uchumi unaokua kwa kasi barani Afrika katika kipindi cha muongo mmoja uliopita yaani kuanzia mwaka 2007  hadi  2016.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchumi BoT, Johnson Nyella jana jumatatu kwenye sherehe ya Siku ya Takwimu Afrika (2017), iliyofanyika kitaifa jijini Dar es Salaam ambapo alieleza kuwa  uchumi wa Tanzania ulikua kwa wastani wa asilimia 6.7 mwaka 2016, wakati pato la taifa lilikua kwa wastani wa asilimia 7, sawa na ilivyokuwa mwaka 2015 na 2014.

Bw. Nyella amesema  kwa miaka minne mfululizo, mfumuko wa bei wa Taifa umeendelea kupungua na kubaki katika kiwango cha tarakimu moja.

“Mwaka 2016 mfumuko wa bei ulipungua na kufikia wastani wa asilimia 5.2 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 5.6 mwaka 2015 na asilimia 6.1 mwaka 2014.” amesema Nyella huku akielezea umuhimu wa Takwimu bora.

Takwimu bora za uchumi zinahitajika katika kupanga mipango ya maendeleo na utungaji wa sera kwa ajili ya kuboreshamaendeleo endelevu ya mwaka 2030.

Kwa mujibu wa Nyella, takwimu bora za kiuchumi zinasaidia kuongeza tija serikalini katika kupanga mipango ya maendeleo na kukabiliana na changamoto kadri zinavyojitokeza.

Amesema takwimu bora pia zinawasaidia watunga sera na watekelezaji wa programu mbalimbali na kupanga mikakati mipya ya kuboresha maisha ya wananchi.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa amesema kwenye sherehe hizo kuwa, takwimu bora za uchumi ni muhimu katika kufikia ajenda ya Bara la Afrika ya mwaka 2063 inayosisitiza ukuaji wa uchumi.

Katika kufikia ajenda hiyo, baadhi ya mambo yanayosisitizwa ni amani, utulivu, kuboresha uchumi wa Afrika, kukusanya mapato ya Afrika ili Afrika iweze kujitegemea.

Dk Chuwa, amesema Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi ya Afrika (UNECA) kwa kushirikiana na Ofisi za Takwimu za Afrika, ina kaulimbiu isemayo “Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora” ikisisitiza umuhimu wa takwimu za kiuchumi katika kuleta maendeleo endelevu hivyo kuboresha maisha ya wananchi.

Kaulimbiu hiyo inaakisi juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli kwa kuwa na dhamira ya kutengeneza uchumi wa viwanda. Amesema kwa sababu hiyo, takwimu rasmi za uchumi za serikali lazima zitolewe kwa weledi na kwa kufuata kanuni na sheria.

“Takwimu bora za uchumi kwa nchi yetu ni za muhimu sana, hasa wakati huu ambao Serikali yetu inaimarisha uchumi wa viwanda ili Tanzania iweze kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 na kuboresha zaidi maisha ya wananchi. Takwimu hizi za uchumi ni pamoja na takwimu za kilimo, viwanda, ujenzi, usafirishaji, nishati, biashara, mazingira, mfumuko wa bei na uwekezaji.”amesema Dkt. Chuwa.

Dkt. Chuwa amesema takwimu bora ni takwimu zilizo sahihi, zinazotolewa kwa wakati, linganifu na za kina, zinazozalishwa mara kwa mara na zenye ufanisi. Dk Chuwa alisema, sifa hizo zote zinaendana na kanuni za msingi za takwimu rasmi za Umoja wa Mataifa na Mkataba wa Takwimu wa Afrika, ambazo maisha ya wananchi, hasa kutekeleza ajenda.

Chanzo:HabariLeo

Mwanasheria Alberto Msando Ahamia CCM

$
0
0
Mwanasheria Alberto Msando Ahamia CCM
Mwanasheria maarufu nchini Alberto Msando ambaye amewahi kuwa mwanachama wa Chadema pamoja na ACT-Wazalendo amehamia Chama cha Mapinduzi.

Msando ameomba ridhaa ya kujiunga na CCM leo kwenye mkutano mkuu wa Halmashauri kuu ya NEC unaoendelea jijini Ikulu Dar es salaam na kukubaliwa na wanachama chini ya mwenyekiti wa chama hicho Rais John Pombe Magufuli.
“Nimeona harakati nyingi za serikali na Chama cha Mapinduzi katika kuwaletea maendeleo wananchi hivyo nimekaa nakajitathimini nimeamua kujiunga na CCM ili nisaidie kusukuma gururudumu la maendeleo.

Msando pia ameeleza kuwa alikuwa anaona anachelewa kujiunga na vijana wenzake kama Mbunge wa Dodoma Mjini Antony Mavunde ambao mara zote amekuwa akiwaona wapo mstari wa mbele katika kupigania maendeleo ya vijana na taifa kwa ujumla.
Aidha Msando ambaye amewahi kuwa mshauri wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema hii ni mara yake ya kwanza kuingia CCM kwa kuwa kwa sasa si aibu tena kwa mtu kujitambulisha kuwa ni mwana CCM kwani imesafishika kuliko ilivyokuwa awali ambapo ulikuwa ukionekana na nguo za CCM unazomewa mitaani.

CCM Yavuna Wanachama Hawa Kutoka Upinzani

$
0
0
CCM Yavuna Wanachama Hawa Kutoka  Upinzani
HALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) ambayo inaendelea na vikao vyake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo iliwapokea na kuwarudisha katika chama hicho wanachama kadhaa kutoka vyama vya upinzani ambao walijitokeza mbele ya kujieleza na hatimaye kuomba kujiunga na chama hicho.

Miongoni mwa wanachama walipokolewa ni Profesa Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba, Edna Sunga (wote kutoka ACT-Wazalendo) (kutoka ACT-Wazalendo), Lawrence Masha na Patrobas Kitambi (Chadema) na wengineo.

Mwenyekiti wa CCM Taifa, John Pombe Magufuli amewapongeza kwa kujiunga na kila alichosema chama bora na kinachowatetea wanyonge.  Alisisitiza pia kwamba hatua yao ya kujiunga na chama hicho isije ikawa majaribio bali wahakikishe uamuzi wao huo uwe wa kudumu na wakitetee chama hicho kwa muda wote wa maisha yao.

Wakati huohuo, baada ya Magufuli kuisomea NEC barua ya kuomba msamaha kutoka kwa aliyekuwa mwanachama wa chama hicho, Sophia Simba, ambaye alifukuzwa uanachama mwaka huu, halmashauri hiyo ilimrudisha kwa kauli moja.

Mwenyekiti wa BAVICHA Aibwaga Chadema Ahamia CCM

$
0
0
Mwenyekiti wa BAVICHA Aibwaga Chadema Ahamia CCM
Mwenyekiti  wa Bara la Vijana Chadema Taifa , (BAVICHA)  Patrobas Katambi ameomba ridhaa ya kujiunga na ChamaCha Mapinduzi CCM, leo kwenye kikao cha Halmashauri Kuu Taifa NEC  kwa madai kwamba siyo kwa sababu ya  madaraka bali

kwa ajili ya maslahi ya taifa.
Akizungumza mbele ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Ndg John Pombe Magufuli, Katambi amesema kwamba yupo tayari kuitwa msaliti kwa kusaliiti ubinafsi na kundi la mabinafsi kwa ajili ya maslahi ya taifa.
Akizidi kuomba ridhaa ndani ya Chama hicho Katambi amesema kwamba siasa za upinzani zimegubikwa na ubinafsi, umimi pamoja na makundi ya hapa na pale.
"Naomba ridhaa ya kuwa mwanachama siyo kwa sababu ya madaraka bali kwa ajili ya maslahi ya taifa pamoja na kusaidiana na wenzangu kukiendeleza chama. Natambua harakati zilizofanyika kwenye awamu iliyopita. Watu wengi wanapenda lakini Hatupendi kubadilika na Mabadiliko yabnapoanza misuguano ndipo inapoanzia....." Katambi
Kwa upande mwingine Katambi amesema kwamba ameona CCM inawapatia vijana nafasi na fursa za kuongoza tofauti na alipotoka kwamba vijana wakishatumiwa wanaonekana kama takataka yaani karai baada ya ujenzi.


Emmerson Mnangagwa Amtaka Mugabe Ajiuzulu Mara Moja

$
0
0
Emmerson Mnangagwa Amtaka Mugabe Ajiuzulu Mara Moja
Makamu wa rais wa zamani , ambaye kufutwa kwake kazi kulisababisha jeshi kuchukua mamlaka ya nchi , amemtaka rais Robert Mugabe ajiuzulu mara moja.
Emmerson Mnangagwa amesema alitoroka nje ya nchi wiki mbili zilizopita wakati alipobaini kuwa kuna njama za kumuua na hatarejea nchini hadi atakapohakikishiwa usalama wake.
Chama cha rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kinatarajiwa kuanza mchakato wa kupiga kura ya kutokuwa na imani nae.
Afisa wa Zanu-PF amesema kuwa hoja ya kumnyang'anya urais itawasilishwa bungeni leo Jumanne na mchakato wa kumg'oa madarakani unaweza kuchukua siku mbili tu.
Mashtaka yaliyomo kwenye hoja hiyo ni pamoja na kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 "kumpa madaraka makubwa ya kikatiba mkewe Grace, na kushindwa kuheshimu katiba''.
Viongozi wa kijeshi , ambao wiki iliyopita waliingilia kati kuchukua mamlaka ya nchi walisema atakutana na makamu wake wa rais wa zamani aliyeuhamishoni karibuni.
Jeshi limesema kuwa lina mpango na Mugabe kuhusu hali ya baadae.
Jumapili , licha ya shinikizo kubwa Bwana Mugabe aliwashangaza wengi kwa kukataa kujiuzulu, na badala yake katika hotuma yake kupitia televisheni alisema kuwa ataongoza mkutano mkuu wa chama Zanu-PF.

Sophia Simba Aiangukia CCM Arejea Rasmi kwenye Chama Hicho

$
0
0
Sophia Simba Aiangukia CCM Arejea Rasmi kwenye Chama Hicho
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Wanawake CCM (UWT), Sophia Simba aomba radhi na kuomba kurejea CCM baada ya kufukuzwa uanachama.

Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli amesoma barua ya Sophia kuomba radhi mbele ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na kuwahoji wajumbe kama wanakubali kumsamehe jambo lililokubaliwa.

"MwanaCCM aliyefukuzwa uanachama amekuwa akiandika barua nyingi za kuomba radhi lakini tumekuwa tukinyamaza,  kikao hiki ndiyo kilimfukuza," amesema Rais Magufuli katika kikao hicho kinachofanyika leo Jumanne.

Baada ya kuwahoji wajumbe na kukubaliwa Rais Magufuli aliandika kwenye barua hiyo kuwa amekubaliwa kurudi CCM.

Ruge Uso kwa Uso na Makonda Kuhusu Tamasha la Fiesta

$
0
0
Ruge Uso kwa Uso na Makonda Kuhusu Tamasha la  Fiesta
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, Jumatatu hii amefunguka kuzungumzia tetezi ya kwamba Tamasha la Muziki la Fiesta litaishia 6 usiku tofauti na miaka iliyopita kutokana na hali ya usalama.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda hivi karibuni akiwa katika kituo cha redio cha EFM kuzungumza juu ya matukio ya burudani kutotakiwa kufanyika zaidi ya saa sita usiku kwenye maeneo ya wazi Dar es salaam.

Tamasha la FIESTA 2017 linatarajiwa kufanyika Leaders Club Jumamosi hii November 25 huku ticket tayari zikiwa zimeshazagaa mitaani.

Ruge ambaye ni Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group amesema “Tunafanya juhudi za kujaribu kuona kama tunaweza tukampata Mkuu wa Mkoa”

Masha, Msando Wapewa Onyo Kali na Rais Magufuli

$
0
0
Masha, Msando Wapewa Onyo Kali na Rais Magufuli
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais John Pombe Magufuli amewaonya wanachama wapya ambao wamehamia ndani ya chama hicho leo kwenye mkutano mkuu wa NEC unaoendelea Ikulu jijini Dar es salaam.

Wanachama hao ambao wamehamia na kutangazwa leo ni Mwanasheria Alberto Msando aliyekuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo, Mbunge wa zamani wa Nyamagana Laurent Masha aliyekuwa mwanachama wa Chadema pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema taifa Patrobas Katambi.
Wengine ni Profesa Kitila Mkumbo ambaye naye alikuwa mwanachama wa ACT-Wazalendo pamoja na Sophia Simba ambaye ameomba kurejeshewa uanachama baada ya kufukuzwa kwa muda.

Akiongea baada ya kuwapokea wanachama hao Rais Magufuli amesema, “Nawaomba msije mkabadilika tena, mmekuja huku na wanachama wamewakubali msirudi tena kule, hiki ni chama cha wote hata watoto watazaliwa watakikuta na watajiunga kwasababu kina misingi imara, kwahiyo msije huku kujaribu”.
Rais Magufuli amemaliza kwa kuwapa ruhusa ya kugombea nyadhifa mbalinmbali ndani ya chama na kwenye maeneo yao. “Nyie sasa mmepitishwa na mkutano mkuu wa NEC hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kuwapinga na kama kuna nafasi ya kugombea huko nendeni mkagombee ili mje mshiriki kuijenga nchi na Chama”.

LEMUTUZ Afurahia Alberto Msando Kuhamia CCM Afunguka Haya

$
0
0
LEMUTUZ Afurahia Alberto Msando Kuhamia CCM Afunguka Haya:
.
From @lemutuzsuperbrand_ - KARIBU JEMBE Mwanasheria Msomi na maarufu Duniani @albertomsando karibu sana CCM ....KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!.....karibu ufurahie matunda ya Uongozi Shupavu wa Rais Magufuli yaani "UONGOZI UNAOACHA ALAMA".....kuondoka kwa JEMBE HILI kunaacha Pengo kubwa sana maana huyu alikuwa ndiye NGOME HASA YA UPINZANI AT SOCIAL MEDIA ........KARIBU JEMBE HILOO @albertomsando ......HAHAHAHA KIDUMU CHAMA TAWALA! - le Mutuz

Pata Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za Full Power

Ni Dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,
Dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin E pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30

ZAT 50 inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.

Kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende tunapatikana daresalaam na mikao wasiliana nasi DR Oshinda Namba za simu 0755505099/0714126118

Karibuni kwa hunduma bora

Hamisa Mobeto Adaiwa Kumfanyia Mwanae Aliyezaa na Diamond Ukatili

$
0
0
SIKU chache baada ya kutoswa malezi ya mwanaye, Abdul Nasibu ‘Prince Abdul’ ambapo alimfungulia kesi mahakamani ya madai ya malezi mzazi mwenziye ambaye ni msanii wa Bongo Fleva, lakini Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar, upande wa Watoto ukatupilia mbali shitaka hilo, mwanamitindo maarufu Bongo, Hamisa Hassan Mobeto anadaiwa kumfanyia ukatili mwanaye huyo.



TUJIUNGE NA CHANZO

Chanzo makini kilicho karibu na familia ya Mobeto kililimwagia ubuyu Ijumaa Wikienda kuwa, mrembo huyo, licha ya kuwa mtoto wake bado mdogo ana umri wa miezi minne, amekuwa akimtelekezea mama’ke mzazi, Shufaa Lutigunga na kusafiri mara kwa mara nje ya nchi.

“Yaani kwa kweli inatushangaza sana, kweli mtoto ana umri wa miezi minne, unaanzaje kumuacha na kwenda mbali kiasi hicho? “Mara utasikia leo yupo Nairobi, mara utasikia yupo Dubai sasa hapo unategemea nini?,” kilimwaga ubuyu chanzo hicho.

CHANZO CHAZIDI KUTIRIRIKA

Chanzo hicho makini kiliendelea kutiririka kuwa, Mobeto tangu ajifungue, amekuwa akisafiri mno na kumwacha mtoto, jambo ambalo linawapa maswali watu wengi kwamba, ina maana hamnyonyeshi hivyo
anaweza kumfanya mtoto adumae kwani maziwa ya mama ni muhimu kwa mtoto mchanga katika miezi sita ya kwanza.

“Kila mtu anafahamu umuhimu wa maziwa ya mama kwa mtoto mchanga hususan katika kipindi cha miezi sita ya awali, tunatilia shaka sana anaweza hata kumbemenda mtoto maana hatujui kule anaenda kukutana na wanaume tofauti, akishiriki nao je?” Kilihoji chanzo hicho.

NI SIKIO LA KUFA?

Chanzo kiliendelea kutiririka kwamba huenda Mobeto ni sikio la kufa kutokana na mambo anayoyafanya kwani kwa mtu mwingine alivyoshambuliwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu suala la kuzaa na Mbongo Fleva ambaye anajua kabisa yupo kwenye uhusiano na Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, pamoja na kuanika picha zao wakiwa faragha, hakukoma, bado anaendelea tu na mambo hayo.

“Hamisa (Mobeto) ni sikio la kufa maana kuna habari kwamba juzikati alikuwa Dubai alikokwenda kujirusha na huyo baba mtoto wake wakati ameshamtosa kwenye malezi ya mtoto. “Kwa mtu ambaye anasikia asingekubali kwenda kujirusha na mtu wa hivyo. “Kuna picha ambazo zimesambaa akiwa amepiga na mrembo mmoja huko Dubai ambapo mrembo huyohuyo
ameonekana akiwa amepiga picha na msanii huyo wa Bongo Fleva, jambo ambalo linaashiria walikuwa pamoja,” kilidai chanzo hicho.

MOBETO ANASEMAJE?

Ili kuujua ukweli wa habari hizo, Ijumaa Wikienda kama ilivyo desturi yake ya kupata mzani (balance), lilimtafuta Mobeto ambapo mazungumzo yalikuwa hivi;
Ijumaa Wikienda: Habari yako, ninaongea na Mobeto?

Mobeto: Ndiyo, nani mwenzangu?
Ijumaa Wikienda: Unaongea na Gazeti la Ijumaa Wikienda hapa.
Mobeto: Okey, sema…
Ijumaa Wikienda: Kuna habari kwamba umekuwa ukimtelekezea mama yako mtoto na kusafiri mara kwa mara na juzi tu ulikuwa Dubai ulikokwenda kujirusha na baba mtoto wako, msanii wa Bongo Fleva, unazungumziaje?
Mobeto: No coment…. (akakata simu).

KUTOKA KWA MHARIRI Ni vyema Mobeto akawa makini na suala la malezi kwani kwa kawaida, katika miezi sita ya awali, mtoto anahitaji zaidi maziwa na malezi ya ukaribu ya mama na baba licha ya kwamba baba mtoto anadaiwa kugomea malezi, kinyume na hapo ni ukatili mkubwa kwa mwanaye huyo.

GPL

Maneno ya Mama Lulu baada ya Mwanae Kwenda Jela

$
0
0
SIKU tano baada ya mwanaye ambaye ni staa wa Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ mama yake mzazi, Lucresia Karugila, kwa mara ya kwanza amefunguka baada ya mtoto wake huyo kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kumuua bila kukusudia staa mwenzake, Steven Kanumba aliyekuwa pia mwandani wake.

Awali, kulienea lawama nyingi mitandaoni baada ya Lulu kuhukumiwa kuwa huenda kuna mahali wazazi walikosea malezi ndiyo sababu ya mtoto wao huyo kujihusisha na masuala ya kimapenzi akiwa na umri wa chini ya miaka 18 ambao hakubaliki.

Kufuatia hali hiyo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta mama Lulu ili kujua mtazamo wake juu ya mwanaye kwenda jela na madai ya mitandaoni ndipo akafunguka mazito. Mama Lulu aliliambia gazeti hili kuwa, kwa sasa hapendi kuzungumza hovyo na watu na anahitaji muda mwingi wa kupumzika kwa kuwa hayuko vizuri. “Nafikiri kwa kipindi hiki nahitaji zaidi kupumzika kwa muda mwingi na sipendi kuzungumza hovyohovyo, siko vizuri kabisa,” alisema mama Lulu kwa sauti ya unyonge.

Lulu akiwa na mama yake Lucresia Karugila.
Akiendelea kuzungumza, mama huyo alisema kuwa, tangu apate majanga ya mtoto wake huyo hadi kwenda jela hayupo vizuri na wala hapendi kuongea kwa sababu hajisikii kufanya hivyo kwani anahisi anaiona dunia chungu. “Najua watu watanishangaa sana, lakini ndiyo nimeamua kuwa hivyo, siko sawa na sijisikii vizuri kabisa. “Sidhani kama kuna mzazi yeyote anaweza kupata usingizi wakati mwanaye yupo kwenye mateso kama ilivyokuwa zamani, kiukweli ninaumia sana,” alisema mama Lulu.

DAKTARI NAYE ANENA!

Naye daktari wa magonjwa ya binadamu, Dk Godfrey Chale, akizungumzia hali ya Lulu baada ya hukumu hiyo alisema kuwa, kuna magonjwa ambayo huweza kumpata mtu mwenye matatizo ya kimaisha ikiwemo kufungwa jela ikiwa ni pamoja na kuwa kichaa kutokana na msongo.

Dk Chale alisema mara nyingi watu ambao hupatwa na majanga makubwa kama la Lulu, huwa kwenye uwezekano mkubwa wa kukumbwa na msongo ambao husababisha mpangilio mbovu wa homoni kiutendaji na mhusika kuchanganyikiwa endapo atashindwa kukubaliana na mazingira ya tatizo.
Alisema kuchanganyikiwa kwa watu wenye matatizo kama ya Lulu, hutokana na kuzidiwa na huzuni na mgandamizo wa hisia (depression) hivyo kushindwa kabisa kuzuia mfumo wa kufikiri na kutafakari na ndiyo maana unakuta mtu anaongea peke yake au kufanya vitendo vya ajabu kama kuokota vitu mbalimbali kama sehemu ya kujifariji na hapo ndipo tatizo la kuchanganyikiwa huanzia.

Tatizo kubwa jingine ambalo linaweza kumpata Lulu ni kupoteza popularity momentum (nguvu ya umaarufu) na kushuka kwa uchumi atakapomaliza kifungo kwani kwa kipindi ambacho yuko jela atapoteza mikataba yake ya kikazi kama matangazo na uigizaji, vitega uchumi ambavyo vilikuwa vikimuingizia kipato cha kuyaendesha maisha yake

JE Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo ya Kiume?

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?
Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.


Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

Alichokisema Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bavicha Baada ya Kuhamia CCM

$
0
0
Alichokisema Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bavicha Baada ya Kuhamia CCM

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bavicha, Patrobas Katambi ambaye amehamia CCM amesema kama ataitwa msaliti basi atakuwa kundi la wasaliti wa nchi hii.

Akizungumza leo Jumanne mbele ya Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Katambi  amesema, “mambo mengi yalikuwa mrama  na watu tunapenda mabadiliko ila hatutaki kubadilika.”

"Kama nitaitwa msaliti basi nitakuwa msaliti kundi la wasaliti wa nchi hii, ukombozi ulishapatikana, siyo tunachokisema majukwaani ndiyo tunachokiishi,"

"Maisha tunayoyahubiri siyo tunayoishi, ukienda jimboni kwake, vijana kama nguvu kazi ya Taifa, tunajadili ‘personalities’ badala ya ‘issues’ mawazo mbadala," amesema.

"Niwaombe nijiunge na CCM siyo kwa sababu za madaraka ila tuijenge, CCM inatoa nafasi kwa vijana, vijana kwa upinzani ni sawa na karai katika ujenzi.”

Katika kikao hicho Rais Magufuli amesema karibu wanachama 200 wameomba kujiunga na chama hicho. Amesema kwa sasa hawatatambulishwa hadi mkutano mwingine.

Masha Aomba Kutumiwa Pale Atakapohitajika

$
0
0
Masha Aomba Kutumiwa Pale Atakapohitajika
Aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA Lawrence Masha ambaye ametangaza kukihama chama hiko hivi karibuni, ameomba kurejea CCM na kutumiwa pale atakapohitajika.

Akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri Kuu cha CCM kinachoendeshwa na Mwenyekiti wake Rais Magufuli, Masha amesema yeye ni kada wa CCM kwani amezaliwa na kukulia kwenye CCM, hivyo anaomba uongozi wa CCM umkubalie aweze kurudi nyumbani na kuitumikia CCM.
"Mwaka 2015 nilifanya maamuzi ambayo sina sababu ya kueleza sana, nimezaliwa ndani ya chama hiki, nilipohama ilibidi nimfiche mzee Masha, akanipigia simu akanuliza umefanya? nikamuuliza kwani wewe chama gani? akaniambia mimi nilifukuzwa we umehama, amefurahi sana juzi nilipomwambia narejea CCM, Mheshimiwa Mwenyekiti na kamati yako, naomba mnikubali, naahidi nitakuwa mwaminifu kwa chama cha Mapinduzi na serikali yake, ukinihitaji nitumie", amesema Lawrence Masha.
Hivi karibuni Lawrence Masha alitangaza kukihama chama cha CHADEMA akisema chama hiko hakina nia madhubuti ya kushika dola kama malengo ya vyama vya upinzani vingi duniani.
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images