Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live

Mdogo wa Marehemu Ndikumana Awashushia Mvua ya Matusi Bongo Movie

$
0
0
Mdogo wa Marehemu Ndikumana Awashushia Mvua ya Matusi Bongo Movie
Mdogo wa marehemu Hamadi Ndikumana ambaye alikuwa mume wa muigizaji wa filamu Tanzania Irene Uwoya, anayeitwa  Laddy Ndikumana, amesema waigizaji wa filamu wa bongo (bongo movie ) ni wajinga, kutokana na mambo yao wanayoyafanya.


Laddy ameyasema hayo alipokuwa akiongea na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwamba waigizaji hao ni wajinga na wanafiki kwa kuwa wameshindwa kufika kwenye msiba wa kaka yake Ndikumana, ambaye wakati wa uhai wake walijifanya kuwa rafiki yao na kumpenda.
Laddy ameendelea kwa kusema kwamba wakati marehemu Ndikumana alipokuwa na pesa, wasanii hao walikuwa marafiki na kula naye bata, lakini wameshindwa kujitokeza kwenye msiba, na kumuacha Irene Uwoya peke yake kwenda Rwanda.

Wema Sepetu Afunguka Msimamo Wake Kuhusu Kurudi CCM

$
0
0
Wema Sepetu Afunguka Msimamo Wake Kuhusu Kurudi CCM
Malkia wa filamu nchini, Wema Sepetu amemwambia muigizaji mwenzake wa filamu ambaye ni kada wa CCM, Steve Nyerere kwamba hana mpango wa kurudi tena CCM.

Wema amesema hayo baada ya kuona ujumbe wa Steve Nyerere kumpongeza Alberto Msando kwa uamuzi wake wa kukihama chama cha ACT Wazalendo ya kwenda Chama Cha Mapinduzi, CCM.

“HAHAHAHAHAHAHAHAHAHA SASA UTAKUWA MZALENDO WA KWELI , MSANDO NAESHIMU MAAMUZI YAKO MAANA NI MAAMUZI SAHIHI, KWAKO PAMOJA NA FAMILY YAKO , RAFIKI ZAKO NASI TUPO PAMOJA NAWE, SOON NA YULEEEEEEEEE RAFIKI YETU , DADA ETU , MSANII MWENZETU , NAYE YUPO NJIANI KURUDI NYUMBANI, COMING BACK TIVU , WELCOME MSANDO,” aliandika Steve Nyerere.

Baada ya kauli hiyo, Wema Sepetu aliamua kuweka mambo sawa juu ya kauli hiyo huku akidai kwamba hana mpango wa kuhama Chadema na kurudi CCM.

“I hope hauniongelei mimi… Maana mawazo hayo sina,” aliandika Wema Sepetu.

Muigizaji huyo alikihama chama hicho baada ya kudai kuna mambo ambayo hayaendi sana ndani ya chama hicho.

Madereva Walevi Kupewa Adhabu ya Kufanya Kazi Mochwari

$
0
0
Madereva Walevi  Kupewa Adhabu ya  Kufanya Kazi Mochwari
Mamlaka ya Usalama wa Uchukuzi nchini Kenya NTSA imependekeza adhabu mpya miongoni mwa madereva walevi.

Madereva walevi sasa watalazimika kufanya kazi katika vyumba vya kuhifadhia maiti ili kupunguza idadi kuu ya ajali za barabarani.

”Hatuwezi kuwa na madereva wengi walevi wanaofanya ajali na wanapofikishwa mahakamani wanapewa adhabu hafifu.Tutakapokamilisha kutengeza sera hiyo mpya tutahakikisha kuwa inakuwa sheria”, alisema mkurugenzi wa mamlaka hiyo Francis Meja.

Na Wakenya wengi katika mitandao ya kijamii waliunga mkono mpango huo na kusema kuwa utawafanya madereva kuwa makini.

Je una hisi sheria hii ikija Tanzania itasaidia kupambana na madereva walevi?.


Hamisa Mobetto Atikisa na Filamu Yake ya Zero Player

$
0
0
Hamisa Mobetto Atikisa na Filamu Yake ya Zero Player
FILAMU ya mwanamitindo Hamisa Mobeto iliyozinduliwa wiki iliyopita, katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Suncrest Cineplex uliopo ndani ya Quality Center, uliopo Barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam, hivi sasa inatikisa jiji kwa kile kinachotajwa kuwa ina kiwango kikubwa cha ubora.

Kwa mujibu wa wadau waliozungumza na Risasi Mchanganyiko juzikati, filamu hiyo iitwayo Zero Player, imechukuliwa kwa viwango bora kabisa kuliko kazi nyingi zilizotolewa siku za hivi karibuni na zaidi ya hapo, pia hata waigizaji wake waliifanya kwa ubora wa hali ya juu.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, mwanamitindo huyo ambaye alicheza filamu hiyo na wasanii wengine kutoka nchi mbalimbali zikiwemo  Afrika Kusini, Ghana, Cameroon, Nigeria na Tanzania na pia filamu hiyo imerekodiwa katika kiwango kizuri sana na kila mmoja amecheza inavyopaswa katika nafasi yake.

“Kwa kweli ni filamu ambayo nimecheza lakini hata mimi mwenyewe naifurahia jinsi nilivyoitendea haki nafasi yangu, imenionyersha kiasi gani nimekua katika tasnia hii,” alisema Mobetto, mama wa watoto wawili. Baadhi ya wasanii walioudhuria uzinduzi huo walipongeza filamu hiyo na kusema kuwa imechezwa katika kiwango kizuri sana na chenye ubora wa uhakika huku wakiwapongeza wasanii ambao wamecheza filamu hiyo.

“ Yaani kiukweli nimeangalia filamu hii nimependa sana jinsi walivyocheza wameonekana wako makini na wanajua ni kitu gani wanakifanya katika uigizaji huo na pia wameweza kuwafunika hata wakongwe” alisema Ester Kiama
STORI: Imelda Mtema, Risasi Mchanganyiko

Simba Yapania Kuwaonyesha Kazi Lipuli Jumapili

$
0
0
BAADA ya kuishuhudia Yanga ikiichapa Mbeya City kwa mabao 5-0, hivyo kuzidi kupunguza wigo wa mabao dhidi yao, vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba wamepania kuibuka na ushindi mnono kwenye mchezo wao ujao dhidi ya Lipuli ya Iringa, imeelezwa.

Simba inayodhaminiwa na Kambuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, itakuwa mwenyeji wa Lipuli kwenye mchezo wao wa Jumapili utakaochezwa katika Uwanja wa Azam Complex unaomilikiwa na klabu ya Azam.

Kocha Msaidizi wa Wekundu hao wa Mismbazi, Masoud Djuma, alisema baada ya michezo migumu ya mikoani, sasa wanaelekeza nguvu kwenye mchezo huo na lengo ni kuhakikisha wanapata ushindi mzuri ili kuendelea kukaa juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu.

“Ligi ni ngumu, unaona kila timu inajitahidi kupata ushindi, tupo juu ya msimamo kwa tofauti ya mabao ili kuendelea kufanya hivyo ni lazima tujitahidi kupata ushindi, lakini ushindi wa mabao mengi,” alisema Djuma.

Alisema baada ya michezo miwili ya mkoani Mbeya, kwa sasa nguvu zao wanazielekeza kwenye mchezo dhidi ya Lipuli huku wakijipanga kuhakikisha wanapata ushindi mnono.

“Tunaendelea na program yetu ya mazoezi…, tunajua kila mchezo utakuwa mgumu, lakini ni lazima tujipange na kujiandaa kupambana kwa ushindi hicho ndicho kitu cha muhimu,” aliongezea kusema.

Simba wanaendelea kuongoza ligi wakiwa na pointi 22 sawa na Azam, lakini ikiizidi kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Baada ya michezo ya mwishoni mwa wiki hii ikiwa ni mzunguko wa 11, Ligi Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kusimama kwa muda kupisha michuano ya Chalenji itakayofanyika Nairobi, Kenya.


Lwandamina: Uwepo wa Tshishimbi, Tambwe Kutaongeza Makali Mechi ya Jumamosi

$
0
0
Lwandamina: Uwepo wa Tshishimbi, Tambwe Kutaongoza Makali Mechi ya Jumamosi
KOCHA wa Yanga, George Lwandamina, amesema kurejea kwa mshambuliaji wake Amisi Tambwe na kiungo Papy Tshishimbi kunampa uhakika wa kuibuka na ushindi kwenye mchezo ujao dhidi ya Tanzania Prisons.

Baada ya ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Mbeya City Jumapili iliyopita, Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, sasa imeelekeza nguvu zake kwenye mchezo huo ujao utakaochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza na Nipashe jana, Lwandamina alisema timu yake imezidi kuimarika na ushindi dhidi ya Mbeya City unadhihirisha, hivyo kuwapo kwa nyota hao walioukosa mchezo uliopita, kunampa matumaini ya kufanya vizuri.

“Kwangu kurejea kwao kuninapa faraja na kunifanya kuwa na wigo mpaka wa kupanga kikosi, Tambwe hajacheza tangu kuanza kwa ligi na Tshishimbi hakucheza mchezo uliopita, kuwa nao wote kwa pamoja kutaongeza zaidi nguvu kuelekea kwenye mchezo dhidi ya Prisons,” alisema Lwandamina.

Tshishimbi ambaye amekuwa sehemu ya muhimili wa kikosi cha Yanga msimu huu, aliukosa mchezo uliopita kutokana na kuwa majeruhi baada ya kuumia kifundo cha mguu.

Tambwe alikuwa akisumbulia na goti, lakini amepona na Lwandamina amethibitisha kuwa anaweza akamtumia kwenye mchezo ujao.

Katika hatua nyingine, Lwandamina alisema kuwa alitegemea kupata ushindi kwenye mchezo uliopita dhidi ya Mbeya City, lakini si kwa idadi kubwa ya mabao kama waliyoyapata.

“Sikutegemea ushindi mkubwa vile, Mbeya City ni timu nzuri na inawachezaji wanaojituma, nashukuru tulitumia vizuri mapungufu yao kuweza kupata ushindi ule, ila sikutegemea kupata idadi kubwa ya mabao hasa mbele ya timu kama ile,” alisema Lwandamina.

Yanga inaendelea kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikifikisha pointi 20, mbili nyuma ya vinara Simba wanaoongoza ligi na Azam FC inayoshika nafasi ya pili ikiwa na pointi sawa na Simba, lakini ikizidiwa kwa tofauti kubwa ya mabao ya kufunga na kufungwa.


Irene Uwoya Aondoka na Baraka Zote Kutoka kwa Baba Mzazi wa Marehemu Ndikumana Aagwa kwa Maombi

$
0
0
Irene Uwoya Aondoka na Baraka Zote Kutoka kwa Baba Mzazi wa Marehemu Ndikumana  Aagwa kwa Maombi
MSANII wa filamu za Kibongo, Irene Uwoya ameagwa kwa maombi na baba mzazi wa aliyekuwa mumewe, Hamad Ndikumana,….. na kushukuru kwa baraka hizo jambo lililovuta na kuteka hisia za watu wengi.
Katika maombi hayo mafupi, baba mzazi wa marehemu Ndikumana alimtakia safari njema Uwoya ikiwa ni pamoja na baraka tele kwake na mwanaye, Krish ambapo Uwoya aliahidi kushirikiana na familia hiyo kila atakapohitajika kwani tayari ni sehemu yao.

Baba mzazi wa aliyekuwa mumewe, Hamad Ndikumana akimfanyia mambi Irene Uwoya.
“Nenda na baraka zote na hakika nakupa baraka zangu zote wewe na mjukuu wangu Krish na tambua kwamba tunakupenda sana,” alisema baba mkwe wa Uwoya katika maombi hayo mafupi.
“Nawashukuru sana jamani na hakika Mungu awabariki, asante sana Burundi na Mungu awabariki,” alisema Uwoya.
Aliyoyasema kupitia akaunti yake ya Instagram
Asante baba kwa baraka zako …nashukuru mmenipokea vzuri na baraka juuu…MUNGU akubariki sanaaa…tutaonana tena nawapenda sana Mbaki salama…MUNGU ni mwema!!!asante Burundi…

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
MIUJIZA YA SHARIFU SEIF MOHAMED KUTOKA BAGAMOYO.

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,
(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Isome Hapa Barua ya Kujiuzulu Aliyoandika Rais Robert Mugabe

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Robert Mugabe, jana alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo baada ya kuongoza taifa hilo kwa miaka 37 tangu lilipopata uhuru mwaka 1980.

Mugabe katika barua aliyoiandika kwenda wa Spika wa Bunge, alisema uamuzi huo ni wa kwake binafsi na kwamba hajashinikizwa na mtu yeyote.

Katika barua yake ya kujiuzulu, Mugabe aliiandika jana Novemba 21 na kuielekeza kwa Spika wa Bunge, Jacob Mudenda.

Mugabe aliandika kuwa, kwa mujibu wa kufungu cha 90(1) cha Katiba ya Zimbabwe marekebisho ya namba 20 ya mwaka 2013.

“Kufuatia mazungumzo yangu na Spika wa Bunge, Wakili Jacob Mudenda majira ya saa 7:53 mchana, Novemba 21, 2017 kuhusu kutangaza kujiuzulu kama Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mimi Robert Gabriel Mugabe, kwa mujibu wa kifungu cha 90(1) cha Katiba ya Zimbabwe natangaza rasmi kujiuzulu kwangu kama Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe mara moja.”

“Uamuzi wa kujiuzulu ni wangu kwa chama, na nimefanya hivi kwa maslahi ya watu wa Zimbabwe na nia yangu ya kuona makabidhiano ya madaraka yenye amani ambayo yatashikilia amani, utulivu na umoja wa taifa.”

Aidha, Rais Mugabe alisema, “Tafadhali utangazie umma kuhusu kujiuzulu kwangu haraka iwezekanavyo kama inavyotakiwa na kifungu cha 96(1) cha Katiba ya Jamhuri ya Zimbabwe.

“Wako Mwaminifu, Robert Gabriel Zimbabwe, Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe,” alihitimisha Rais Mugabe.

Kufuatia kujiuzulu kwa Mugabe, wananchi katika Mji Mkuu wa Zimbabwe, Harare walitoka katika mitaa mbalimbali na kushangilia huku wakisema kuwa ni awamu mpya kwa Zimbabwe sasa kuendelea kiuchumi.


Paul Makonda Aibuka Ofisi za Clouds Media Kuwapa Pole

$
0
0

Clouds Wameandika haya Baada ya Paul Makonda Kuwatembelea Kuwapa Pole:
...
"Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam, ikiongozwa na RC Paul Makonda wamefika hapa #Mjengoni - #CloudsMediaGroup kutupa pole na kujionea athari zilizosababishwa na moto uliozuka jana asubuhi katika Ofisi zetu hapa Mikocheni. .
.
Tunashukuru kwa yote, tuko salama"

Hizi ndizo Sababu za Mke wa Mugabe Kuchukiwa

$
0
0
Wakati mwisho wa utawala wa miaka 37 wa mume wake Aliyekuwa Rais Robart Mugabe wa Zimbabwe ukiwa wa aibu, sababu tano za wananchi wa taifa hilo kumchukia Grace Mugabe zimeanikwa.

Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali ya kijamii na magazeti ya nchi hiyo, Grace Mugabe alisababisha watu kumchukia kutokana na tabia yake ya kupenda kufanya manunuzi ya gharama ambayo yalisababisha kupewa jina la utani la First Shopper, badala ya first Lady. Manunuzi hayo yanadhaniwa kutumia fedha za umma.

Sababu nyingine inayotajwa kumfanya achukiwe ni ubabe, ambao aliounyesha katika matukio mbalimbali ya hadhara, alipokuwa akiongozana na mume wake katika shughuli za kisiasa. Katika hafla nyingi, Grace aliweza kuwafokea maofisa wa serikali hadharani na kumfanya kuogopwa kupita kiasi.

Licha ya sifa hizo, pia mwanamke huyo aliyezaa na Mugabe akiwa bado kwenye ndoa yake, anadaiwa kuwa mgomvi, kwani mara kadhaa ameripotiwa kuwapiga watu, wakiwemo waandishi wa habari na watu wa kawaida, kama ilivyokuwa mapema mwaka huu, alipompiga na kumuumiza msichana mmoja wa miaka 20 nchini Afrika Kusini, baada ya kumkuta akiwa na watoto wake wa kiume hotelini.

Jambo lingine lililomfanya kuchukiwa na wananchi wengi wa nchi hiyo ni tamaa yake ya madaraka, kwani licha ya kuwa kiongozi wa Jumuia ya wanawake wa Zanu PF, pia kwa nyakati tofauti alionyesha kutamani kuchukua nafasi ya mume wake, kitu kilichofanya wananchi wake kuona kama nchi inataka kuendeshwa kifamilia.

Inadaiwa hata kuondolewa kwa Makamu wa Rais Emmerson Mnangangwa, kulifanywa na Mugabe kwa shinikizo lake. Kitu kingine kinachowaudhi wananchi wa nchi hiyo ambayo fedha yake haina thamani kutokana na vikwazo kutoka nchi za Magharibi, ni kitendo chake cha kukosa heshima za kike, hasa tabia yake ya kuropoka hovyo katika hafla mbalimbali zinazohitaji staha kwa wanawake.

Hadi wakati gazeti hili likienda mtaani, bado haikujulikana alipo mwanamke huyo mzaliwa wa Afrika Kusini, baadhi ya habari zikisema amekimbilia Namibia, lakini wengine wakisema amedhibitiwa nchini Zimbabwe

Pata Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za Full Power

Ni Dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,
Dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin E pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30

ZAT 50 inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.

Kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende tunapatikana daresalaam na mikao wasiliana nasi DR Oshinda Namba za simu 0755505099/0714126118

Matapeli Waibuka Kuuza Namba za Kadi Kwenda Kutibiwa Bure Meli ya Wachina

$
0
0
Matapeli Waibuka Kuuza Namba za Kadi Kwenda Kutibiwa Bure Meli ya Wachina
WAKATI upimaji wa afya bure ukiendelea katika meli maalumu kutoka China, baadhi ya wananchi jijini Dar es Salaam wamegeuza shughuli hiyo kuwa mtaji baada ya kuanza kuuza namba za kadi wanazopatiwa.

Aidha, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Grace Maghembe amesema tayari watu 6,000 wamepata namba kuwawezesha kuwaona madaktari hao kwa utaratibu unaofaa.

Dk Maghembe alitoa mwito kwa wananchi ambao hawajapewa namba, kusubiri hadi waliopata namba hizo watakapohudumiwa. “Tunawaomba msiendelee kusongana; tumeshagawa namba hadi 6,000, hivyo subirini hawa wapate huduma ndipo tutaangalia kama tutaendelea kugawa namba nyingine kulingana na uwezo wa madaktari hawa,”alisema Maghembe.

Meli hiyo yenye madaktari na wataalamu wa afya zaidi ya 380 iliwasili nchini Novemba 19 na inatarajiwa kutoa huduma hiyo kwa siku tano kwa wagonjwa 600 kwa siku. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema amepata taarifa juu ya uwepo wa watu hao wanaofika kwenye meli hiyo kama wagonjwa wanaotaka kuhudumiwa, lakini wakipatiwa namba hizo hugeuka na kuziuza kwa Sh 5,000 hadi Sh 50,000, jambo ambalo ni kosa na kinyume na makusudio.

“Upimaji huo tulisema ni bure na ni makosa kwa mtu kununua au kuuza namba,” alisema. Alibainisha kuwa, baadhi ya wagonjwa wamebainika kutakiwa kusafirishwa kwenda China kupatiwa huduma zaidi hivyo ofisi yake itaandaa utaratibu wa kuwawezesha kusafiri.

Akaongeza, “wagonjwa hawa wanaotakiwa kusafirishwa tutaangalia utaratibu wa kuwasaidia baada ya kupata idadi kamili tutawasaidia kupata hati za kusafiria pamoja na kuangalia utaratibu wa kuwawezesha wakiwa huko kwa matibabu.”

Zitto Kabwe Amwita Niki wa Pili Kujiunga na ACT- Wazalendo

$
0
0
Zitto Kabwe Amwita Niki wa Pili Kujiunga na ACT- Wazalendo
Msanii Nikki wa Pili ambaye ni miongoni mwa wasanii wasomi nchini, ameitwa kujiunga na chama cha ACT Wazalendo, ili kuongeza nguvu na kukijenga zaidi chama hiko.

Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Zuberi Kabwe amemuandikia ujumbe kwenye ukurasa wake wa twitter kumuomba kufanya hivyo.
"Njoo ujenge Chama cha kijamaa bana acha mambo yako", ameandika Zitto Kabwe kwenye ukurasa wa Nikki wa pili.
Baada ya tweet ya Zitto Kabwe kumuomba Nikki, Nikki alimjibu kuwa chama cha kijamaa kinajengwa na watu wanyonge, bali yeye  kama mtu wa vyombo vya habari sio wa kuaminika kwani hawachelewi kuwauza.
"Chama cha kijamaa hujengwa na vugu vugu la wanyonge wenyewe, ni muwe tu na mkakati wa kuwaunganisha ki ideologia, umoja zao hizo za boda boda, machinga, wakulima, sisi watu wa media hatu kawii kuwauza sokoni kama nyanya", ameandika Nikki wa Pili.
Mpaka sasa haijulikani msanii huyo ni mfuasi wa chama gani kutokana na kuonekana kuwa mwanaharakati wa masuala ya kisiasa na uchumi, na hajawahi kuonekana kwenye jukwaa la chama chochote kufanya kampeni.

Fedha Siyo Kigezo Changu cha Kutoka Kimapenzi na Mwanaume - Nandy

$
0
0
Fedha Siyo Kigezo Changu cha Kutoka Kimapenzi na Mwanaume
MWANA-DADA anayefanya vizuri katika Bongo Fleva Faustina Charles ‘Nandy’ ameeleza kuwa hampendi mwanaume kwa sababu ya mkwanja isipokuwa anataka mapenzi ya kweli.

Akipiga stori na Risasi Vibes, Nandy ambaye anatamba na ngoma ya Kivuruge alisema anachopenda yeye ni mwanaume mcha Mungu na mchapakazi, haijalishi kama hiyo kazi inamuingizia kipato kikubwa au la.

“Fedha siyo kigezo cha mwanaume kuwa na mimi, muhimu mtu awe na hofu ya Mungu, asiwe mtu wa kujibweteka awe anajish-ughulisha kwa kazi yoyote ile, tutapambana wote kutafuta maisha hadi mambo yatakapokuwa vizuri na kujivunia kwa pamoja,”alisema.

Mwakyembe Atuma Salamu za Pole Clouds Media Group kwa Kupatwa na Ajali ya Moto

$
0
0
Mwakyembe Atuma Salamu za Pole Clouds Media Group kwa Kupatwa na Ajali ya Moto
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe atuma salamu za pole kwa kituo cha redio cha Clouds kwa ajali ya moto > Aagiza taasisi zinazohusika kufanya uchunguzi wa kina kubaini chanzo cha tatizo

Polepole Afunguka Kuhusu Wanachana wa CCM Wanaohamia Upinzani

$
0
0
 Polepole Afunguka Kuhusu Wanachana wa CCM Wanaohamia Upinzani
Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Humphrey Polepole, amesema chama hicho kwasasa kimeweka misingi ambayo inawabana viongozi wasiotosheka lakini hakina tabia ya kuwasema vibaya wanachama wake wakihama.

Akiongea kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari Ndg. Polepole amesema kuwa Chama chao kinalinda misingi na Itikadi zake ambazo ni kuheshimu utu wa mtu pamoja na kuwatumikia raia hivyo kwa kiongozi ambaye hawezi kufanya hayo lazima atakimbia.
"Mimi kama Katibu wa Itikadi na Uenezi sijawahi kutoa tamko la kumsema vibaya mwanachama anayehama chama chetu kwasababu sio misingi na Itikadi zetu". Pia ameongeza kuwa ni dhambi kubwa kumhukumu mtu anapohama chama kimoja kwenda kingine.
“Hatuna tabia ya kuwasema vibaya wale wanaokihama chama, lakini tumegundua kwamba raia wa kawaida ndio wamekuwa na tabia ya kuwasema kwa sababu wanayaona matendo yao ya kutotosheka”, amesema Polepole.
Aidha Polepole amesisitiza kuwa CCM kwasasa imeweka misingi migumu itakayowabana wasiotosheka na wasio na kiasi ndio maana tumeamua kuweka sheria ya mtu mmoja, cheo kimoja. Sheria ambayo itawabana wenye kutaka vyeo vingi kwa wakati mmoja.

Chadema Hakiwezi Kutetereka au Kufa Kwasababu ya Katambi Kuondoka

$
0
0
Chadema Hakiwezi Kutetereka au Kufa Kwasababu ya Katambi Kuondoka
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema chama hicho hakiwezi kutetereka au kufa kwa kiongozi au mwanachama wake kuondoka.

Amesema kuna mkakati mkubwa unaotumia fedha unaofanywa kuwalaghai viongozi na wanachama wake kukihama chama hicho.

Kauli hiyo ameitoa leo Jumatano baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa vijana wa chama hicho, Patrobas Katambi kutangaza kujiunga na CCM.

Akizungumza leo Jumatano na Mwananchi, Mbowe ambaye pia ni amesema, "Tuko ‘strong enough’ sio mara ya kwanza watu kuondoka hivyo wanachama wetu wasiogope waendelee kujenga chama na kuendelea na kampeni za udiwani,"

"Huiwezi kututeteresha, kuondoka kwa Katambi si hivi hivi, ushawishi wa fedha umetumika...ingawa ni haki yao ila hao hawaondoki kwa mapenzi yao na hilo halina ubishi,"

"Badala ya nguvu na fedha kuzielekeza kujenga viwanda wao nguvu wamezielekeza kushawishi viongozi wetu, wamewashawishi wengi na Katambi ni miongoni ingawa wengine wamekataa."

Mbowe amesema, "Katambi alikuwa katika majukumu ya chama na aliwaaga wenzake anakwenda kumuguza mama yake mgonjwa hivyo akakatiwa tiketi ya ndege, kumbe alikuwa anakwenda kukamilisha dili ambalo naambiwa limetumia saa 48 kukamilika."

Amesema Chadema ilipofika haiwezi kufa kwani imejijenga na hapo walioondoka lakini mpaka sasa kimeendelea kuwapo.

Mbowe amesema mwitikio wa wananchi katika kampeni za udiwani kwenye kata 43 umeishtua CCM ikiwamo kuhama kwa aliyekuwa mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu.

Lucy Komba Amtete Irene Uwoya “Kiukweli Mwacheni Alie tu Hata Kama Walikuwa Wametengana"

$
0
0
Lucy Komba Amtete Irene Uwoya “Kiukweli Mwacheni Alie tu Hata Kama Walikuwa Wametengana"
MKONGWE wa filamu nchini anayeishi Denmark, Lucy Komba amemtetea msanii mwenzake Irene Uwoya aliyefiwa na aliyekuwa mumewe, Hamad Ndikumana ‘Katauti’ na kuwataka watu kumuacha alie.

Akizungumza na Za Motomoto News, Lucy alisema watu wanaomponda Uwoya kuhusiana na kifo cha Ndikumana wanakosea kwani hakuna mtu ambaye amewahi kufiwa na mume au aliyekuwa mzazi mwenzake na asilie.

“Kiukweli Uwoya mwacheni alie tu hata kama walikuwa wametengana, lakini unaposikia mtu ambaye aliwahi kuwa mume, mpenzi au baba watoto wako amefariki lazima uumie, tena sana kwani kifo ni kitu kingine kabisa, wanaomshambulia wamwache maana wanamuonea tu,” alisema Lucy.

Mwigulu Awajia Juu Chadema Kuhusu Tundu Lissu

$
0
0
Mwigulu Awajia Juu Chadema Kuhusu  Tundu Lissu
Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt Mwigulu Nchemba amewakosoa upinzani kutumia tukio la kushambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kama ajenda katika kampeni za uchaguzi wa marudio na kusema kwamba chama hicho kimefilisika.

Akiwa Masasi katika kampeni za kumnadi mgombea wa udiwani wa tiketi ya CCM, Dkt Nchemba amesema kwamba kitendo hicho cha Chadema kufanya kila mahali tukio la Lissu kama ndiyo ajenda atakwenda kuwaambia wakazi wa Singida wawaangalie vizuri watu hao.
"Mimi nitaenda kuwaambia wana Singida kwamba tuwaangalie vizuri hawa watu. Wao  ni mwenzao kwenye Chama sisi ni ndugu yetu na tunatoka sehemu moja. Inawezekanaje wawe wanafurahia tukio hilo? Kama kuna kitu walikuwa wanataka kitokee ili warushe maneno kwa serikali" amesema Dkt Nchemba.
Aidha akiendelea Nchemba amesema Chadema wanamuona kama Lissu mtaji ndiyo maana hata polisi walipomtaka dereva wake ili kuweza kumhoji wameamua kukaa naye huko.
Pamoja na hayo Nchemba amewata watu wakapige kura bila kuhofia fujo zinazoweza kufanywa na wanachadema kwani serikali ipo kwa ajili ya kusimamia sheria.
 "Wamezoea kufanya fujo. Nendeni mkapige kura akitokea mtu atakayethubutu kukughasi wewe mkariri sura alafu sisi tutamfundisha ustaarabu wa vyama vingi. Anayefanya fujo atakutana na mkono wa sheria. Na uzuri vijana wangu wapo hapa atakayethubutu kufanya fujo, Muwaonyeshe kwamba mmepitia mafunzo" Nchemba
Hata hivyo Nchemba amewataka wananchi hao kuichagua CCM kwa kazi nzuri inayofanya na kuwaamba kuuchagua upinzani wakitegemea itashinda ni sawa na kujeruhi nafsi.

Viewing all 104667 articles
Browse latest View live




Latest Images