Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live

Zitto Kabwe Atoa Kauli Hii Kuhusu Matibabu ya Bure Kwenye Meli ya Wachina Iliyopo Bandarini

$
0
0
Zitto Kabwe Atoa Kauli Hii Kuhusu Matibabu ya Bure Kwenye Meli ya Wachina Iliyopo Bandarini
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Zuberi Kabwe, amesema kitendo cha watu kujazana kufuata matibabu kwenye meli ya wachina iliyopo bandarini, inadhihirisha ni namna gani wananchi wanashindwa kumudu gaharama za matibabu, na iwe somo kwa Taifa

Zitto Kabwe ameyasema hayo kwa kuandika ujumbe kwenye ukurasa wakewa facebook na kusema kwamba taifa lenye hali kama hii haliwezi kupiga hatua kimaendeleo, hata kama wakijenga miundombinu ya kisasa, na kuitaka serikali kuweka misingi imara kwenye jamii yake.
"Nimepita kituo cha reli ya kati Dar na kuona msururu wa watu. Nimeambiwa wanakwenda kwenye meli ya madaktari wa wachina. Hii ni ishara kuwa watu wetu wanaumwa na hawana uwezo wa kuhudumia afya zao. Taifa lenye hali hii haliwezi kamwe kusonga mbele hata lijenge fly overs kila kona. Maendeleo ni watu, hili liwe somo. Tujenge Hifadhi ya Jamii ya Taifa ili tuwe na Taifa lenye afya bora na Uchumi shirikishi", ameandika Zitto Kabwe.
Hivi karibuni meli kutoka china yenye madktari bingwa imetia nanga kwenye bandari ya Dar es salaam, na kutoa huduma ya matibabu kwa wakazi wa jiji hilo bila gharama zozote.


Tamasha la Fiesta Mwisho Saa Sita Ruge Afunguka Kupunguza Wasanii 20 Kwasababu ya Muda

$
0
0
Tamasha la Fiesta Mwisho Saa Sita Ruge Afunguka Kupunguza Wasanii 20 Kwasababu ya Muda
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, Alhamisi hii katika kipindi cha Clouds360, amesema amepunguza wasanii 20 katika list ya wasanii ambao walipanga kuwepo kwenye show ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Jumamosi hii katika viwanjwa Leaders Club.

Ruge alisema miongoni mwa wasanii hao walioondolewa kisa muda ni pamoja na Lulu Diva, Zaiid, pamoja na ChinBeez.

‘’Tulikaa kama kamati jana tunatumia nguvu kubwa mno kwenye suala la muda wakati tuna shoo kubwa iliyokamilika, kwahiyo tumeamua kuachana na suala la muda,tumeamua tukae kwenye muda tulioupanga sisi na kuhakikisha tuna ‘six hours’ za entertainment ambazo zimepangwa na kupangika,” alisema Ruge.

Aliongeza, “Kitakachokosekana ni wale wasanii zaidi ya 20, kama, Bright, Mimi Mars,Lulu Diva, Zaiidyao, ChinBeez,hao bahati mbaya ni lazima tuwaondoe kwa sababu ya ratiba kubana kutokana na muda, tungeweza kuwaingiza lakini hatuna muda’’

Wema Apokelewa Mapokezi Makubwa Rwanda Afunguka Kilichompeleka Huko

$
0
0
Wema Apokelewa Mapokezi Makubwa Rwanda Afunguka Kilichompeleka Huko
Msanii maarufu wa Filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu jana jumatano usiku aliwasili nchini Rwanda ambako alieleza kuwa ameenda kikazi kwenye Tamasha la KFM Instagram Party.

Wema Sepetu amesema ameenda nchini Rwanda kwa ajili ya tamasha la KFM Instagram Party, Tamasha linaloandaliwa na kituo cha Radio cha KFM lenye lengo la kuwakutanisha watumiaji wa mtandao wa Instagram nchini humo, na litafanyika Novemba 24, 2017, katika ukumbi wa Chillax Lounge, Nyarutarama jijini Kigali.

“Ndio mara yangu ya kwanza nimekuja (Rwanda) ndege imegusa ardhi saa mbili na nusu naweza kusema sina hata lisaa tangia nimefika, vile nimekuwa nikisikia kuhusu Rwanda nimeviona, najua bado ni usiku kesho nitaweza kuona mengi zaidi, nimesikia kwamba Rwanda ni nchi ambayo ni ndogo lakini ni nzuri, nilikuwa niko na kaka yangu tunapisha barabarani napigwa na butwaa ‘oh my God hii sehemu ina usafi mwingi.”amesema Wema Sepetu kwenye mkutano na Waandishi wa Habari mapema jana usiku baada ya kuwasili nchini Rwanda na kueleza kilichompeleka.

“Ni jambo jema kwamba nimekuwa Queen of Social Media, siyo kwamba nimejipa mwenyewe, watu wamenipa hicho cheo, naamini itakuwa ni muda mwafaka wa watu kukutana nami ana kwa ana, kwa sababu kuonana kwenye ‘ma-social media’ tu mtu anakuwa anatamani kukuona, eti huyu Wema natamani nikae naye nipige naye picha, tupige naye stori mbili tatu, sitaweza kufanya hivyo na watu wote ila angalau watu waweze kupata taswira halisi kuhusu mimi kipenzi cha wengi kutoka Tanzania. Mimi ni mcheshi, napenda burudani napenda matamasha naamini nitafurahi kuwa na watu wangu wa Rwanda hasa ukizingatia huu mwaka unaelekea ukingoni, 2017 ni mwaka ambao kwangu mimi umekuwa ni mrefu sana, pia nashukuru Mungu unaisha.”amesema Wema Sepetu.

Hatimaye Kampuni ya Udalali Yono Yatoa Masharti Mnada wa Nyumba za Lugumi Kesho

$
0
0
Kampuni ya Udalali Yono Yatoa Angalizo Kwenye Mnada wa Nyumba za Lugumi Kesho
ILI kuhakikisha mnada wa nyumba mbili za Lugumi huko JKT Mbweni na Upanga jijini Dar es Salaam unakwenda vizuri, watu watakaofika na kushiriki mnada huo kesho, watabidi kutimiza masharti kadhaa.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya udalali ya Yono, Scolastica Kevela, wote watakaofika maeneo hayo watabidi kutoa vitambulisho vyao vya kazini, vya udereva na vya upigaji kura.

Isitoshe, kwa mujibu wa Kevela, wote watakaoingia mnadani hapo  itabidi watoe Sh. Milioni mbili kama uhakikisho wao wa dhamira ya kushiriki  na kununua  mali husika, hii ikiwa kwa washangiliaji na watazamaji.

Kevela alisema wale watakaoshinda mnada huo, Sh.milioni mbili walizotoa zitakuwa sehemu ya malipo yao, na kwa wale watakaoshindwa, watarudishiwa fedha hiyo baada ya mnada.

Alisisitiza pia kwamba washindi wa mnada huo watatakiwa kulipa asilimia 25 ya bei ya nyumba husika waliyoshinda na asilimia 75 iliyobaki itabidi ilipwe ndani ya siku 14 ambapo atakayeshindwa kufanya hivyo hatarudishiwa fedha iliyotangulizwa ya asilimia 25.

Pia alionya kwamba watu wasiohusika kwa lolote na mnada huo kwamba ni vyema wasifike maeneo hayo ili kukwepa kupambana na sheria pindi wakijikita katika kuharibu mchakato wa mnada huo.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo...

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Tupo Mbagala Rangi Tatu

Lema Ataka Mwigulu Nchemba Kupimwa Mkojo

$
0
0
Lema Ataka Mwigulu Nchemba Kupimwa Mkojo
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amemjia juu Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt Mwigulu Nchemba na kufikia hatua ya kusema waziri huyo apimwe mkojo ili kuangaliwa kama anashiashiria vya matumizi ya dawa za kulevya. 

Lema amesema hayo baada ya kauli ya waziri huyo kuwakosoa upinzani kutumia tukio la kushambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kama ajenda katika kampeni za uchaguzi wa marudio na kusema kwamba chama hicho kimefilisika.

Lema aliandika hivi " Nafhamu Mh Mwigulu atumii madawa ya kulevya au kilevi, lakini kauli zake kwenye mikutano ya hadhara ya kampeni za udiwani zinaleta wasiwasi nakuona ni vyema nikashauri apimwe mkojo. Anayesema eti kupigwa Lissu risasi hakuna mahusiano na kuomba kura?"

Jokate Amfananisha Magufuli na Nabii Musa Aliyewakomboa Wana Israel Canaan

$
0
0
Jokate Amfananisha Magufuli na Nabii Musa Aliyewakomboa Wana Israel Canaan
Kaimu Katibu Idara Ya Uhamasishaji, Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ leo ameandika ujumbe mrefu mtandaoni ambao unasifia kazi na majukumu kadhaa aliyoyafanya Rais John Magufuli katika kipindi cha miaka miwili tangu aingie madarakani.

Katika ujumbe huo, Mwegelo ameifananisha kazi hiyo ya Magufuli na jukumu alilolifanya Nabii Musa la kuwatoa wana wa Israel kwenda Canaan, nchi ya ukombozi wao.  Ufuatao ndiyo ujumbe kamili aliouandika:
Musa alipitia vitu vingi ikiwemo kejeli, kujaribiwa na hatimae kufanikiwa kuwavusha Wana wa Israeli kuelekea nchi ya ahadi. Lakini kuna wakati wafuasi wake hao walipojaribiwa kidogo tu wakaanza kunung’unika na kumkebehi Musa kwamba ni kheri maisha waliyokuwa wanaishi Misri kwa Farao.

Rais John Pombe Magufuli ameianza safari yake nyingine baada ya Novemba 5 mwaka huu kufikisha miaka miwili madarakani. Napenda kuifananisha safari yake hiyo iliyosheheni mageuzi makubwa sawa na ile ya Wana wa Israeli walipokombolewa na Nabii Musa kutoka kwenye mikono ya utumwa chini ya Farao wa Misri.

Uwajibikaji, Uzalendo, Utendaji
Kumekuwa na tatizo tatizo la watumishi wa Serikali kutokuheshimu misingi ya kazi zao katika utumishi wao wa umma, nidhamu ya kazi ilikuwa haipo. Ilifikia wakati watu walitunga safari za nje ilimradi tu wapate posho za kujiendeleza wao na familia zao.

Uzalendo wa nchi ukageuka kuwa uzalendo unaokimu mtu na familia yake na watu wake wa karibu. Fedha nyingi zikawa zinapotea angani na hata matunda ya safari tulikuwa hatuyaoni. Bado barabara na miundimbinu muhimu ilikuwa kasi yake ya kuimarishwa haikuwa nzuri sana.

Utendaji na ubunifu ulikuwa wa chini kwani hakukuwa na kitu kipya katika utendaji wa kazi kwa wengi zaidi ya kujitajirisha kupitia kodi za wananchi bila sababu zozote zile za msingi. Manung’uniko yalikuwa mengi juu ya rasilimali za taifa. Kulikuwa na makundi mengi yakizungumza kwa lawama namna rasilimali zilikuwa zinatumika vibaya. Makundi haya yakihusisha Wanasiasa, Wasomi na hata baadhi ya Wananchi wenye kufuatilia maslahi na rasilimali za taifa. Nchi yetu pendwa ya Tanzania ‘kuibiwa’ umekuwa ni mjadala wa muda mrefu bila utatuzi au hatua yoyote kuchukulliwa.

Kuna wakati, nikiamini kwa nia njema na uchungu wa nchi yao na si siasa, baadhi ya wanasiasa walipaza sauti kusema kuwa ni aibu kubwa kwa nchi yetu kushindwa hata kumiliki ndege yetu. Walihoji: “Tutatangazaje utalii bila ya kuwa na ndege yetu?” Kwa ufupi kila kitu kilikuwa kikionekana kwenda sivyo. Na hapa sijagusia issue ya “mafisadi”
Kuingia kwa Magufuli madarakani miaka miwili iliyopita, ukiyatazama maisha yake, utakubaliana nami kuwa huyu ni kiongozi anayeishi na kujituma kwa ajili ya maslahi ya wananchi. Hii inanikumbusha nilipokuwa masomoni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam miaka kadhaa ya nyuma, niliwahi kumuona Rais wetu ambaye kipindi kile alikuwa ni Waziri akila sehemu mmoja wanafunzi katika kijiwe maarufu cha misosi kiitwacho “Harvard”.

Pale chakula ni cha bei ya chini kabisa, mlo kamili mzuri ulikuwa hauzidi elfu 1000. Ilikuwa ni sehemu ya sisi wanafunzi wa kawaida kula kwa sababu ya bajeti zetu ndogo. Kumuona yeye kama waziri pale kulipelekea mimi kuanza kuelewa Dkt. Magufuli ni mtu wa aina gani. Ni wazi kwamba ni mtu wa watu, hana makuu, hajikwezi na anapenda “ku-budget.”

Mageuzi na Mabadiliko
Sishangai miaka miwili tu ya uongozi wake akiwa ameacha tayari alama na mageuzi makubwa ya kukumbukwa. Kwa kifupi tu ametenda yafuatayo ya kukumbukwa:
· Kuwezesha elimu bure kuanzia shule ya Msingi hadi Sekondari;
· Kufufua shirika la ndege la ATCL kwa nunua ndege mpya sita;
· Kuongeza mapato ya ndani toka trilioni 9.9 kwa mwaka hadi trilioni 14 kwa mwaka;
· Kurejesha nidhamu na uwajibikaji kwa watumishi wa umma;
· Ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania
· Kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma;
· Kutimiza ahadi ya Serikali kuhamia Dodoma;
· Kukamilisha miradi mikubwa wa umeme wa Kinyerezi I-extension na Kinyerezi II;
· Kuanza ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge;
· Uzalendo kusimamia raasilimali za taifa yakiwemo madini;
· Kuanza ujenzi wa barabara za juu Tazara, Ubungo na daraja la wapiti kwa miguu Furahisha;
· Ujenzi wa madaraja ya kisasa mfano la daraja la Kilombero;
· Kusimamia uhakika wa madawati maabara na maktaba katika shule zote nchini;
· Ujenzi wa maduka ya kisasa ya dawa za ndani ya kila hospitali ya Serikali;
· Kupambana vikali dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya nchini;
· Kutoa bima za afya za matibabu ya bure kwa wazee
· Kuhakikisha wanafunzi wanaostahili kupata mikopo ya elimu ya juu wanapatiwa
· Kuhakikisha Tanzania inakuwa na viwanda vya kutosha nchini
· Kufuta kodi na urasimu kwenye kilimo na uwekezaji nchini
· Kuhakikisha serikali inasimamia uuzwaji wa mazao ya wakulima masokoni na kupata faida. Mfano wakulima walikuwa wakiuza korosho zao kwa tsh 800 kwa kilo mpaka tsh 4000 kwak kilo.
Nimesukumwa kuzungumzia na kuorodhesha mafanikio haya kwa ufupi ili tujue shabaha ya rais wetu. Rais wetu anataka kurudhisha heshima. Heshima hailetwi kwa blah blah, heshima huletwa kwa vitendo na kufanya vitu kwa njia ya kuwa “disruptive”-kutokufanya vitu kikawaida au kwa mazoea.

Msimamo mkali wa rais
Rais Magufuli anataka kuona watu wakijituma na kuleta matokeo chanya. Hata ukiangalia safu zake za uongozi ni viongozi walioshiba kwenye nafasi zao. Na wanaonekana hawafai wanaondolewa. Ila bado kuna makundi ya watu kwenye jamii wanaona anachofanya ni kazi bure na kufikia hatua ya kuaminisha umma kuwa Serikali hii ya Awamu ya Tano imefanya hali imekuwa ngumu na eti haina malengo na kuwa imepoteza dira.
Hakuna ukombozi uliofanyika bila kutoa jasho, kutokwa damu na kutumia mbinu za kujifunga mikanda. Mheshimiwa Rais anafanya hilo, ni lazima kujitoa mhanga kwa kipindi hiki kwa ajili ya mafanikio ya muda mrefu. Nilifikiria viongozi wetu hasa wa upinzani wangefurahia mabadiliko haya kwa maana ndio kitu hasa walichokuwa wakikitamani na wakishiriki kikamilifu katika kutoa mawazo yenye kujenga ila hali imekuwa ni tofauti.
Hapa ndio maana nimekikumba kisa cha safari ya Mussa-maana nalifananisha hili na kadhia ya wale Wana wa Israeli kufikia hatua mpaka kumkufuru Mwenyezi Mungu na wakaona kuwa ni kheri wangebaki kule Misri. Kama kumbukumbu ya kuku, nao walisahau walipotoka.

Ushauri
Natambua ni vigumu kumuaminisha kila mtu ukweli kama tayari anaamini uongo, kama ilivyo vigumu kumuaminisha uongo yule ambaye anaamini ukweli. Ila kama vijana na taifa lililo la vijana, imefika wakati wa kila mmoja kusimamia kila anachokiamini, LAKINI asiamini kile alichoaminishwa. Vijana tuache siasa za kupikwa na kuungaunga, tusimame katika ukweli na mambo yale ambayo yana maslahi kwa taifa letu na si maslahi binafsi. Tujiulize: Inakuwa vipi, wanasiasa na wanaharakati wale wale ambao walikuwa wanapigania vitu flani vifanyiwe kazi, sasa vinafanyiwa ndiyo wa kwanza kununa na kufanya ‘confusion’ mbele ya Jamii?
Ndani ya chama cha Mapinduzi tunaamini Umoja ni Ushindi. Huu ni wakati wa kuungana na Mheshimiwa Rais katika ukombozi wa Watanzania, lazima tuelewe shabaha ya Rais wetu kuwa ana nia njema na maendeleo ya nchi yetu.
Hii safari sio rahisi, hakuna aliyemkamilifu ila wote tunaitumainia Tanzania yenye neema. Vijana tuache kupokea mapokeo ya wanasiasa wasio na nia njema na nchi yetu, tufanye kazi kwa kushirikiana katika kuiletea nchi hii neema.
Chanzo: Global Publishers

Siku Nikihama Chadema Mimi na Familia Yangu Tutauwawa- Issaya Mwita

$
0
0
Siku Nikihama Chadema Mimi na Familia Yangu Tutauwawa- Isssaya Mwita
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam, Issaya Mwita amefunguka kuwa kamwe hafikirii kuhama Chama cha Demokrasia na Maendeleo kwa kusema kwamba hafikirii kuhama chadema kwani familia yake itateketezwa kwa mapanga na wananchi akiwepo yeye pia.

Akizungumza leo asubuhi kupitia kipindi cha EABreakfast,  ndani ya East Africa Radio, Mwita amesema kwamba amekitumikia Chadema kwa muda mrefu ikiwepo kutumia fedha zake binafsi kwenye kukijenga chama hivyo hadhani kama anaweza kuhamia chama kingine kwani hata madaraka aliyonayo anaamini yanamtosha kabisa.
Mwita amesema kwamba amesikitika sana kuona kuna baadhi ya watu waliohama vyama na kuongeza kwamba yeye ameaminiwa na wana Dar es salaam ndiyo maana akapewa dhamana kubwa ambayo ni kubwa kuliko hata nafasi ya Waziri.
"Nchi hii tumeanza kuitumikia tangu tupo majeshini. Hatukuwahi kununuliwa, lakini nawashukuru wana Dar es salaam kwa kuniamini pia nafasi niliyonayo ni kubwa. Nahama Chadema naenda wapi na nikienda huko nitafanya kazi gani? Najua kuna 'Cheap' Politics ambayo inafanyika ili kubomoa chama chetu lakini sisi tunaamini hapa tutavuka jambo hili na tutafika pazuri". Meya Mwita
Mwita amesema kwamba sifa moja ya kabila analotoka siyo watu wa kuyumbishwa hivyo siku atakapobadili msimamo ndiyo siku ambayo ataipoteza familia na yeye mwenyewe.
"Nipo ndani ya chama hiki tangu 1999. Nimekijenga kwa nguvu na pesa zangu. Hivyo naanzaje kufanya upumbavu kama huo. Nikuambie siku nikifanya uamuzi huo utasikia mama yangu amekufa, kaka zangu na hata mimi mwenyewe, Siku nikihama labda wanihamishie mbinguni lasivyo wataniua. Unataka mimi nife....aaah siwezi". amesema Mh. Mwita
Aidha, Mh. Mwita amesema kwamba aina yake ya kuliongoza jiji la Dar es salaam imekuwa tofauti sana kwani ameamua kuwa mkimya ili kuleta maendeleo kwa wananchi hivyo suala la kupiga kelele halitakuwa na tija kama hakutakuwa na maendeleo.

Katambi Awajia Juu Chadema "Nimekaa Kimya Kuficha Haiba Yao Wasiponiomba Radhi Nitasema Kilichonitoa Kule"

$
0
0
Katambi Awajia Juu Chadema "Nimekaa Kimya Kuficha Haiba Yao Wasiponiomba Radhi Nitasema Kilichonitoa Kule"
Aliyekuwa mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Patrobas Katambi amewataka viongozi wakuu wa Chadema kuthibitisha tuhuma za kununuliwa kwake na CCM la sivyo atatoa sababu za kina za uamuzi wa kuhama chama hicho.

Katambi Jumanne Novemba 21,2017 alitangaza kujiunga CCM katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam akidai upinzani hauna dhamira ya dhati ya kupambana na ufisadi.

Akizungumza na Mwananchi  leo Alhamisi Novemba 23,2017, Katambi amesema, “Inaniuma kuona nazushiwa uongo, natishwa kwa uamuzi wangu, nilikaa kimya kulinda staha za watu, nimetoa muda  wathibitishe wanachokisema.”

Amesema, “Unajua hekima na busara zangu zilinilazimisha kuondoka Chadema na kuhamia CCM bila kufafanua yaliyonitoa ili kuacha haiba yao waendelee kwa amani na mfumo wao wa siasa mpya, lakini wameshindwa sasa nitasema ukweli kama watashindwa kudhibitisha hadharani.” Katambi amesema hakukurupuka kufikia uamuzi wa kuondoka Chadema na wala hakuwashirikisha wazazi wake, kwa hiyo anayepaswa kulaumiwa au kutishwa ni yeye si wazazi au mke wake.

“Nimekuwa nikipokea vitisho vya kila aina, wazazi wangu na mke wangu, niseme tu kwamba mlinzi wa kwanza wa maisha yangu ni Mungu. Namwachia Mungu maisha yangu niliyoyatoa katika ukweli kwa faida ya Watanzania,” amesema.

Amesema kama watashindwa kutoka hadharani kukanusha taarifa hizo, ataitisha mkutano na waandishi wa habari na kusema ukweli wa kile kilichomfanya akaondoka Chadema.

Jana Jumatano Novemba 22,2017 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akizungumza na Mwananchi alisema Katambi hakuondoka hivihivi bali kuna hila ilifanyika ambayo ilitumia saa 48 kukamilisha mchakato na kujiondoa.

"Badala ya nguvu na fedha kuzielekeza kujenga viwanda wao nguvu wamezielekeza kushawishi viongozi wetu, wamewashawishi wengi na Katambi ni miongoni ingawa wengine wamekataa."

Odinga Amaliza Mapumziko Yake Zanzibar Arejea Nairob

$
0
0
Odinga Amaliza Mapumziko Yake Zanzibar Arejea Nairob
Kiongozi wa muungano wa upinzani wa Nasa nchini Kenya, Raila Odinga amerejea nyumbani baada ya kujichimbia kwa siku nne Zanzibar nchini Tanzania.

Mwanasiasa huyo ambaye amegoma kuutambua ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta alikuwa visiwani Zanzibar kwa mapumziko baada ya kumaliza ziara ya siku 10 nchini Marekani.

Taarifa za kurejea nyumbani kiongozi huyo zimethibitishwa na msemaji wake, Dennis Onyango ambaye aliliambia gazeti la Nation kuwa Odinga amerejea Kenya.

Pia, mkurugenzi wa mawasiliano wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM), Philip Etale amezungumzia kuwasili kwa Odinga mjini Nairobi.

Ingawa baadhi ya picha zimekuwa zikimuonyesha mwanasiasa huyo akiwa mapumzikoni katika hoteli moja Zanzibar lakini ziara yake imehusishwa na hali ya kisiasa nchini mwake.

Mapokezi ya Odinga mwishoni mwa wiki aliporejea Kenya baada ya kuwa nje ya nchi kwa siku 10 yalikumbwa na taharuki baada ya kutokea ghasia zilizohusisha wafuasi wake na polisi.

Mtu Mmoja Aiomba Mahakama Kumfunga Jela

$
0
0
Mtu Mmoja Aiomba Mahakama Kumfunga Jela
Baada ya kupigwa marufuku kuomba na kulala ovyo ovyo kwenye veranda za maduka katika mji wa Middlesbrough, Bradley Grimes alimuomba jaji wa mahakama ammpeleke gerezani kuliko kumuacha bila makazi .
Itakuwa na athari gani? " Kile walichokifanya ni kunifanya nisipende kuishi katika jamii kujaribu kunizuwia nisiwe omba omba.
Lakini lazima niombe ili kuweza kuishi," Bradley Grimes alimueleza mwandishi wa BBC.
Alikosa makazi ya kuishi baada ya kuondoka kwenye mfumo wa misaada ya jamii akiwa na umri wa miaka 17.
Bradley Grimes mwenye tatizo la kigugumizi na ''akili ya kitoto'' hakuweza kupata kazi na mara kwa mara amekuwa omba omba- akiwaomba wasafiri chakula na pesa kando ya mtaa wenye shughuli nyingi.
Lakini hii ilimfanya jaji katika mahakama ya Middlesbrough kumuamrisha kuacha tabia hiyo
Amri hiyo iliambatana na amri ya kumzuwia " kuzurura" nje ya majumba ya biashara.
Bradley anasema amri hiyo ilimzuwia "kukaa nje ya duka " na kulala kwenye bveranda za maduka ambako alikuwa akipata joto, na hilo lilimfanya kuendelea kukamatwa na maafisa wa usalama.
" mitambo ya kamera ya CCTV inachukua picha na kuituma moja kwa moja kwa polisi au walinzi wa mitaa. Polisi wakija, unakamatwa ," alieleza Bradley, ambaye sasa ana umri wa miaka 23.
Anasema kilichomfanya maafisa wa usalama ni kukaamkabala ni kituo cha basi.

"Nilifika kwenye kituo ambako walinifunga mara moja ama mara mbili kwa siku, katika kipindi cha miezi michacheg
"Nilikuwa nafungwa zaidi nyakati za mwishoni mwa juma.
"Siwezi hata kukaa kwenye kiti cha umma bila kutiwa nguvun. Inabidi nishinde nikizurura ."Kutokana na kuchoshwa na hali hii, aliamua kuomba msaada usio wa kawaida at his situation, he decided to seek .
Alipokuwa mahakamani, akishtakiwa kwa kukiuka hukumu ya kifungo cha nyumbani cha miezi minne- kosa mabalo alikiri kulifanya - alimuomba jaji kumuweka jela,.

Waziri wa Elimu Amsimamisha Kazi Ofisa Mikopo wa Chuo Kikuu

$
0
0
Waziri wa Elimu Amsimamisha Kazi Ofisa Mikopo wa Chuo Kikuu
Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako amemsimamisha kazi ofisa mikopo wa Chuo Kikuu Ardhi, Rajabu Kipango kwa kushindwa kukamilisha mchakato wa kutoa mikopo kwa wanafunzi waliopatiwa mkopo licha ya Serikali kuwasilisha fedha kwa wakati.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya wanafunzi  kulalamika kutoingiziwa mikopo na kusababisha kushindwa kujikimu.

Baada ya malalamiko hayo, imebainika ofisa huyo kutofanya uhakiki wa wanafunzi waliopewa mikopo, huku Serikali ilishatoa fedha kwa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).

Profesa Ndalichako amesema leo Alhamisi Novemba 23,2017 kuwa, Serikali haiwezi kukwamishwa na watu wachache.

Ameagiza vyuo vingine kukamilisha mchakato wa mikopo ili kuondoa malalamiko ya wanafunzi kushindwa kupata fedha kwa wakati.

Pia, ameagiza wakuu wa vyuo vyote nchini kukaa na wanafunzi na kutatua matatizo yao badala yakukaa ofisini.

"Haingii akilini ofisa mikopo eti mwanafunzi anakufuata kazi yako ni kumzungusha badala ya kulifanyia kazi," amesema.

Profesa Ndalichako amesema kumekuwa na lawama kwa wanafunzi kwamba hawalipi ada kwa wakati, wakati Serikali ilishatuma fedha kwa ajili ya kuwapatia mikopo

Nimehama Chadema Lakini Sijahamua Chama cha Kujiunga Nacho- Kafulila

$
0
0
Nimehama Chadema Lakini Sijahamua Chama cha Kujiunga Nacho- Kafulila
ALIYEKUWA mbunge wa Kigoma Kusini tangu 2010-15 na baadaye kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) David Kafulila, amesema kwamba pamoja na kutangaza kukihama chama chake hicho, bado hajaamua chama ambacho atajiunga nacho, lakini akasisitiza kwamba ajenda ya ufisadi aliyokuwa anaipigania upande wa upinzani imetoweka na sasa anatafuta sehemu ya kuiendeleza.

Kafulila aliyasema hayo wakati akihojiwa  jijini Dar es Salaam leo, ikiwa ni siku moja tangu atangaze uamuzi wa kuondoka Chadema.

“Hilo ni jambo la kawaida kwa wanasiasa duniani kuhama wakati wanatetea ajenda zao,” alisema Kafulila ambaye alipata tuzo akiwa mbunge wa kwanza kuendesha harakati  dhidi ya ufisadi  Aprili 29, 2015.

Aliongeza kwamba msimamo wake wa kupiga vita ufisadi tangu utotoni hadi kuingia bungeni uko palepale na atauendeleza akiwa katika chama chochote.

Kuhusu madai  kwamba hana imani na upinzani ambako umeshindwa kupambana na ufisadi, wakati ndipo alipopatumia kujiimarisha katika vita hiyo, mwanasiasa huyo machachari alisisitiza kwamba  ajenda ya kupiga vita ufisadi imekufa katika vyama hivyo na ameona hakuna tena matumaini ya kuifufua ajenda hiyo ambayo awali ilikuwa ndiyo nembo ya upinzani.

Pia Kafulila alikanusha mawazo kwamba ameondoka chama hicho baada ya kukosa maslahi kwa kutopata cheo,  ambapo amesema kama ni vyeo bado nafasi zipo Chadema na watu wanajitokeza kuvigombea, jambo ambalo yeye hakulifanya wakati akiwa huko.  Kwa hiyo, akasisitiza kwamba suala la kutopata cheo katika chama hicho siyo lililomfanya ajivue uanachama.

Hata hivyo, wakati akisubiri chama cha kujiunga nacho, alimsifia  Rais John Magufuli kwamba  amejipambanua katika suala la kuupiga vita ufisadi na anakubalika ndani na nje ya nchi na kwamba watu wengi wanakubaliana na hatua anazozichukua.

Kafulila alikuwa mwanachama wa Chadema baadaye akajiunga na NCCR-Mageuzi, akarejea tena Chadema hadi alipojivua uanachama jana.

Wasiliana na The Great Maalim Hussein Mtaalam wa Kutatua Matatizo Yaliyoshindikana Kwa Kutumia Nyota na Dua

$
0
0
THE GREAT MAALIM HUSSEIN
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
Maalim Hussein ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

MAALIM HUSSEIN ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.

Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
Maalim Hussein Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
+255 674 835 107 WhatsAPP tu.

Lissu Kusafirishwa Nje ya Nchi kwa Matibabu

$
0
0
Lissu Kusafirishwa Nje ya Nchi kwa Matibabu
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu anatarajiwa  kusafirishwa nje ya nchi kwa matibabu mwezi mmoja kuanzia sasa.

Familia yake imesema Lissu baada ya kupata matibabu nje ya nchi amepanga kufanya mambo matano akirejea salama .

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 23, kaka wa Tundu Lissu, Wakili Alute Mughwai alisema taratibu za kumsafirisha  nje ya nchi zimeanza.

Lissu, ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu na mwanasheria mkuu wa chadema amelazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 alipokuwa akirejea nyumbani kwake Area D mjini Dodoma Septemba7.

Soma: Lissu afanyiwa upasuaji wa 18

"Awamu ya tatu ya matibabu yake ni maalumu sana kwani itahusu pia mazoezi ambayo kama haitafanyika vyema ataweza kupata ulemavu wa kudumu,"alisema.

Hata hivyo, alisema  Lissu atapelekwa nje kwa ndege ya kawaida tofauti na hali yake ya awali alipotakiwa kusafirishwa  na ndege maalumu za wagonjwa.

"Itatolewa taarifa ni lini ataondoka kwa matibabu na atakwenda nchi gani, hasa baada ya kupata ushauri wa mwisho wa madaktari katika hospitali Nairobi," alisema.

Mambo matano ya Lissu akirejea nchini

Mughwai alisema amezungumza na Lissu akiwa Hospitali Nairobi na amemueleza kuwa  akirejea tu nchini, kuna mambo makubwa matano ambayo atafanya.

Alisema jambo la kwanza, ambalo atafanya ni kwenda katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kuwashukuru madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo kwa kuokoa maisha yake siku aliyopigwa risasi.

Wakili Mughwai alisema Lissu amemwambia baada ya hapo atakwenda kanisani na msikitini kumshukuru Mungu kwa kuokoa maisha yake kwa kufanya ibada maalumu.

"Baada ya ibada, tutaangalia utaratibu kifamilia kama itawezekana  kwenda kufanya matambiko  kwenye makaburi ya wahenga wetu 76 waliofariki katika vita miaka 200 iliyopita," alisema.

Alisema  baada ya hapo, anatarajia kuendelea kufanya kazi zake za siasa na uwakili pale alipoishia kwa ari kubwa .

Wakili Mughwai alisema  jambo la tano atahakikisha  anasimama na kupambana kisheria na watu waliotaka kukatisha maisha yake baada ya kumpiga risasi.

"Amesema atahakikisha anasimamia jambo hili kwa uwezo wake wote ili kuhakikisha wanafikishwa katika vyombo vya sheria waliohusika na uovu huo," alisema.

Familia yataka Lissu akahojiwe Nairobi

Akizungumzia juu ya upelelezi wa shauri la Lissu, Mughwai alisema bado msimamo wao upo palepale wanaomba wapelelezi kutoka nje ya nchi washirikiane na wapelelezi wa ndani kuwakamata watuhumiwa.

Alisema ingawa familia ya Lissu iliandika barua tangu Septemba 16, kutaka wapelelezi wa kimataifa na kujibiwa na mwanasheria mkuu Septemba 20  kuwa jukumu la upelelezi ni la polisi.

 "Tunataka wapelelezi wa nje kushirikiana na wa ndani kwa sababu hatuna imani na upelelezi kutokana na kasi ndogo kwani hadi sasa wamekuwa wakieleza kukwama upelelezi kutokana na kutomuhoji dereva wa Lissu,"alisema.

Hata hivyo, alisema kwa sasa Lissu anaweza kuongea mwenyewe hivyo, jeshi la polisi linaweza kwenda Nairobi kumuhoji na atawapa maelezo yote ikiwepo watu ambao aliwatambua.

"Bila shaka Lissu atawaeleza watu hao, walimshambulia kwa sababu gani,"alisema.

Familia yaelezea gharama

Katika hatua nyingine, Mughwai alisema Oktoba 2, familia ya Lissu ilikutana na viongozi wa bunge kujadili matibabu yake ambayo ni haki yake kisheria.

Alisema baada ya mazungumzo hayo, Oktoba 8, familia iliandika barua rasmi kwa katibu wa bunge kwa kuzingatia sheria ya bunge namba 14 kifungu cha 24 kuhusu stahiki za mbunge.

Alisema barua hiyo, ilipelekwa bungeni kwa kutumia shirika la kubeba mizigo na vifurushi la DHL na kupokelewa Oktoba 19 na baadaye aliwasiliana na Spika Job Ndugai na kumweleza juu ya barua hiyo na aliahidiwa kuwa suala hilo litashughuliwa.

Hata hivyo, alisema familia haijapata mrejesho tangu wakati huo hadi Novomba 11, alipoamua kumpigia katibu mpya wa bunge baada ya kushauriwa na Spika Ndugai ambaye aliahidi kufuatilia.

"Hivyo hadi sasa bado Bunge halijaanza kugharamia matibabu ya Lissu kama sheria inavyosema na Lissu amekuwa akitibiwa kwa michango ya watu mbali mbali," alisema

Alisema michango hiyo ambayo inakusanywa katika akaunti maalumu ya Chadema  na pia kupitia chama cha mawakili(TLS) ndio hadi sasa inatumika.

"Tutaendelea kulitaka Bunge kugharamia matibabu kwani sio suala la hiari, ni haki ya mbunge lakini pia tunaomba wananchi waendelee kuchangia matibabu ya Lissu kupitia akaunti iliyotolewa na Chadema, chama cha TLS na kwa familia"alisema

Katika hatua nyingine, Mughwai alisema, familia ya Lissu, Chadema na chama cha Mawakili wa Tanganyika(TLS), hawana mgawanyiko wowote juu ya matibabu ama hatua zinazoendelea za kumtibu Lissu.

Wakili Mughwai alisema wanasikitishwa na taarifa kuwa familia imegawanyika juu ya uamuzi wa kuliomba bunge kugharamia matibabu ya Lissu.

"Tupo kitu kimoja wote familia yetu tupo pamoja kwa yote na Lissu anajua hatua zote kwani hata makamishna wa bunge walipomtembelea Oktoba 23 aliwauliza kuhusu stahiki zake kama mbunge,"alisema.

Tundu Lissu alipigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nje ya nyumba yake akirejea kutoka vikao vya bunge Dodoma, Septemba 7 na kukimbizwa hospitali ya Nairobi kwa matibabu ambapo hadi sasa anapatiwa matibabu.

Emmerson Mnangagwa Aweka Wazi Mipango Yake Mipya Zimbabwe

$
0
0
Emmerson Mnangagwa Aweka Wazi Mipango Yake Mipya Zimbabwe
Aliyekuwa Makamu wa Rais Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa amesema kwamba anatarajia kuona ukurasa mpya wa demokrasia nchini Zimbabwe ikiwani pamoja na kuapa kutengezeza ajira nchini humo.

 Mnangagwa ametoa kauli hiyo mara baada ya kurejea nchini Zimbabwe akitokea Afrika Kusini ambako alikimbilia baada ya kufukuzwa kazi na aliyekuwa rais wa nchi hiyo Robert Mugabe.
Mnangangwa ametumia nafasi hiyo kuhutubia umati mkubwa uliofika kumlaki katika uwanja wa ndege wa Harare ambapo alisema kwamba anataka kukuza uchumi, amani na ajira.
Inakadiriwa kuwa asilimia 90 ya watu nchini Zimbabwe hawana ajira.
Mnangagwa, anatarajiwa kuapishwa kuwa rais wa nchi hiyo asiku ya ijumaa kulingana na taarifa iliyotolewa na Television ya Taifa. Kufukuzwa kwa kiongozi huyo kulifanya jeshi la nchi hiyo pamoja na chama tawala kuingilia kati na kumaliza utawala wa Mugabe uliodumu kwa miaka 37.
Aidha kiongozi huyo amelishukuru jeshi kwa kuendesha mchakato wa kumuondoa Mugabe kwa amani kwa madai kwamba alishawahi kukabiliana na matukio kadhaa ya kutaka kuuwawa.
Msemaji wa chama tawala cha Zanu-PF amesema Mnangagwa, mwenye umuri wa miaka 71, ataliongoza taifa hilo mpaka mwakani mwezi Septemba utakapo fanyika uchaguzi mkuu nchini humo

Nyota ya Dkt Shika Yazidi Kung'aa Atunukiwa Kuwa Mgeni Rasmi Katika Mahafali ya Chuo Kahama

$
0
0
Nyota ya Dkt Shika Yazidi Kung'aa Atunukiwa Kuwa Mgeni Rasmi Katika Mahafali ya Chuo Kahama
DKT Louis Shika ambaye amekuwa maarufu kwa muda mfupi kama ‘bilionea wa nyumba za Lugumi’ wakati wa kunadi nyumba za Said Lugumi jijini Dar es Salaam, ametunukiwa heshima ya kuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya Chuo cha Afya  kilichoko Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga,  ambako amepokelewa kama mfalme.
Mapokezi hayo ya kipekee yameanzia uwanja wa ndege wa mjini Kahama alipowekwa kwenye gari la wazi huku msafara mkubwa uliokuwepo ukijumuisha na bodaboda,  magari na mamia ya watu mbalimbali waliojitokeza kumwoma na kumlaki.
Ziara hiyo ya Dkt. Shika mkoani humo itamalizika jioni hii chuoni hapo ambapo anatarajiwa kurejea kwa ndege Dar es Salaam usiku.

Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi kwa Familia ya Aliyekuwa Meya wa Jiji Dar

$
0
0
Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi kwa Familia ya Aliyekuwa Meya wa Jiji Dar
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mzee Kleist Sykes kilichotokea jana.


Lema AMtaka kafulila Kumshauri Mkewe Kuhama Chadema

$
0
0
Lema AMtaka kafulila Kumshauri Mkewe Kuhama Chadema
Mbunge wa Arusha Mjini kupitia CHADEMA Godbless Lema, amefunguka kuhusu kitendo cha David Kafulila kuhama CHADEMA na kusema ana amini atamshauri mke wake naye afuate nyayo zake.

Kwenye ukurasa wake wa twiter Godbless Lema ameandika ujumbe akisema Kafulila ni rafiki yake wa karibu, lakini kwa namna alivyoamua hana shaka atamshauri mke wake ambaye ni mbunge kupitia chama cha CHADEMA, kufanya kama yale aliyoyafanya.

"David Kafulila ni rafiki yangu, nafikiri kwa namna hii alivyoamua ataweza bila shaka kumshauri Mbunge wa Chadema, Jesca Kishoa (mke wake) kufikiri kama yeye, hii inaweza kusaidia maoni yake juu ya uamuzi aliouchukua leo na kuthibitisha ukweli huu kama hupo", ameandika Godbless Lema.

Jana David Kafulila ametangaza kukihama chama cha CHADEMA akidai vyama vya upinzani havina nia ya kupambana dhidi ya ufisadi, lakini mke wake Jesca Kishoa ambaye ni mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA bado hajazungumza chochote.




Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live




Latest Images