Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Binti Asimulia Jinsi Wasichana Watanzania Wanavyotumikishwa Kwenye Madanguro ya Umalaya China

$
0
0
Wakati wanawake kwa wanaume wengi huenda barani Asia, hasa China kununua bidhaa kwa ajili ya kuja kuzichuuza, hali sasa ni tofauti kwa kuwa kuna wasichana ambao huenda huko kwa ahadi za ajira, lakini huishia kufanya ukahaba kwenye madanguro, gazeti hili linaweza kukuthibitishia.

Wasichana hao hutafutwa na mawakala wa hapa nchini ambao kazi yao huwa ni kutafuta wasichana wazuri na baadaye kuwashawishi kwa kuwaeleza fursa za ajira za hotelini zilizo barani Asia.

Msichana akikubali, wakala huchukua jukumu la kumtafutia viza ya kuingia China na baadaye kuwasiliana na mwenyeji wake, maarufu kama Lady Boss, ambaye hutuma tiketi ya ndege kwa ajili ya kumsafirisha ‘mwajiriwa’ mpya.

Hata hivyo, hali hubadilika mara wafikapo huko kwa kuwa ‘mwajiri’ huyo humpokonya hati ya kusafiria na baadaye kumpa maelekezo kuwa atatakiwa kulipa Dola 200 kila siku ambazo atakuwa akizipata kwa kufanya umalaya kwenye klabu na maeneo ya biashara.

Tayari wasichana kadhaa wa Kitanzania wamenaswa katika mtego huo na kujikuta wakilazimika kuuza miili yao ili wamudu ada ya Dola 200 pamoja na fedha za kujikimu, akiwemo Munira Mathias mwenye umri wa miaka 23 ambaye alimudu kuvaa ujasiri wa kuweka bayana uovu huo katika mazungumzo yake na gazeti hili.

Binti huyo Mtanzania aliyesafiri kwa saa 18 kwenda Guangzou, China alitakiwa kupumzika kwa saa mbili tu kabla ya kupelekwa kuanza ‘kazi’ ambayo hakuitarajia.

 “Baada ya kupumzika kwa saa mbili tu, nilipelekwa kwenye klabu,” anasema Munira wakati akisimulia mkasa wake.

 “Sikuwa na kazi nyingine zaidi ya kucheza muziki na wanaume ambao licha ya kwamba sikuwahi kuwaona, walinichangamkia kama vile wananifahamu.”

Munira aliondoka Januari mwaka huu kwenda China ambako aliahidiwa kuwa angeajiriwa hotelini, lakini alikutana na ‘ajira’ ya ukahaba, huku akilazimika kuwalipa ‘waajiri’ wake Dola za Marekani 200 kila siku.

 Binti huyo, ambaye alifanikiwa kuchomoka mikononi mwa waajiri hao baada ya viza yake kuisha, alisema kwa siku 91 alizokaa China, alipata mateso ambayo hatayasahau ikiwamo kupigwa, kubakwa na kundi la wanaume raia wa Nigeria, pia kulazimika kutoa mimba aliyoipata kwa kubakwa.

 “Nilifika Guangzhou kama saa 9.00 alasiri za China na kulikuwa na baridi sana,” anasema Munira akisimulia jinsi alivyokanyaga kwa mara ya kwanza ardhi ya nchi hiyo akiwa na matumaini ya kuanza maisha mapya.

“Wakati huo nilikuwa nikijaribu kupata mawasiliano na mwenyeji wangu ambaye niliagizwa kutoka Magomeni, Dar es Salaam.

Alisema alipotoka Dar es Salaam aliambiwa angepokewa na mtu anayeitwa Jacky ambaye hakumkuta kwa kuwa alikuwa safarini Malaysia, lakini alikuwa ameacha maagizo apokewe na mwanamke mwingine.

 “Nilielekezwa nikodi taksi hadi kwenye hoteli inayoitwa Nairobian. Kutoka hapo uwanja wa ndege hadi  kwenye hiyo hoteli ni sawa na umbali wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam hadi Bagamoyo,” anasema Munira.

 Anasema alitakiwa kulipa Yuan 200 (Sh60,000) na alipofika katika hoteli hiyo alipokewa, akaoga na kupewa chakula.

 “Nilipomaliza kula nilipumzika kwa saa mbili hivi. Jacky alikuwa amesharudi na alinifuata chumbani na kuniambia natakiwa kwenda saluni. Hivyo tuliondoka pamoja hadi kwenye jengo kubwa lenye maduka makubwa linaloitwa Tin- shu,” anasimulia Munira.

Watanzania lukuki

Katika jengo hilo alishangaa kuwaona Watanzania wengi, wakiwamo wanawake kadhaa ambao aliwahi kukutana nao Magomeni wakati akifuatilia safari yake.

Munira anasema miongoni mwa watu aliowaona ni binti mmoja ambaye wanafahamiana ambaye alistaajabu kumwona sehemu hiyo.

 “Aliniuliza kwa mshangao, ‘mbona umekuja huku? Umekuja kufanya nini?’ Wakaanza kunishangaa. Yule msichana akaniambia ‘huku msala ndugu yangu, umekuja kufanya nini?” alimnukuu na kuongeza kuwa kabla hawajamaliza mazungumzo yao, mwenyeji wake alitokea hivyo waliyakatisha.

Anasema waliingia saluni ambako aliwakuta Watanzania na Wakenya wakifanya kazi humo na wakati yeye akiendelea kusukwa nywele kwa umaridadi, Jacky alikwenda kumnunulia nguo na viatu dukani.

 “Baada ya hapo niliambiwa nivae nguo niende klabu kwa sababu huo ni msimu wa sikukuu za mwaka mpya wa Kichina,” alisema Munira.

Anasema alishangaa kuambiwa aende klabu usiku huo wakati alikuwa amechoka kwa safari ndefu.

 “Kilichokuwa kinanipa moyo usiku ule ni kuwa niliwaona wasichana wa Magomeni, lakini nilihisi wameambiwa wasiwe karibu na mimi.”

Anasema alipoingia klabu, pia alishangaa zaidi kukutana na Watanzania wengi wa rika tofauti ambao baadhi yao aliwatambua kwa sura na pia kulikuwa na raia wengi wa Nigeria.

 “Kiasi fulani nilifarijika kuwaona Watanzania na nilijisikia kukua kiakili baada ya kuwaona Wanigeria ambao nilizoea kuwaona kwenye filamu peke yake,” anasema.

Hata hivyo, alishangaa kuona pale klabu alichangamkiwa na watu wengi, lakini hakutaka kudadisi zaidi bali alidhani ndiyo hali halisi au alikuwa na bahati ya kupendwa.

 “Baada ya kumaliza kucheza muziki kwenye klabu hiyo, walipelekwa kwenye klabu nyingine ya asubuhi.

“Tuliporudi hotelini, nilijitupa kitandani na kulala kwa sababu ya uchovu mwingi. Miguu ilikuwa imevimba kwa sababu nilikuwa nimevalishwa viatu virefu na kucheza muziki mfululizo. Nikalala bila ya hata kuoga,” anasema.

Mwanzo wa mateso

Baada ya saa moja kupita na akiwa amelala fofofo mchana ule, mara aliamshwa na Jacky, ambaye alimwamuru amkabidhi pasipoti yake.

 “Nikampa, pasipoti yangu nilikuwa nimeiambatanisha na tiketi na kila kitu. Akanishangaza kuniambia kuwa kuanzia siku hiyo niwe nampelekea Dola 200 mezani kila siku. Nilishangaa na nikaanza kulia,” anasema.

 Kwa hasira na mshtuko alioupata, Munira anasema alitoka nje na kuanza kulia na wenzake walipomuuliza kinachomliza, aliwaeleza. Waliamua kumwambia ukweli kwamba hata wao walipelekwa kwa miadi ya kupata ajira za hoteli, lakini hawafanyi hivyo.

 “Waliniambia kuwa nao walirubuniwa na wakanyang’anywa hati za kusafiria kama mimi na wakaishia kuambiwa wafanye biashara ya kuuza miili ili watafute fedha,” anasema Munira.

 Munira anasema alichanganyikiwa, hasa pale alipoambiwa na wenzake kwamba kazi kubwa ni kwenda klabu kujiuza au kuzurura eneo la Chambu Chambu.

Chambu Chambu  ni soko la bidhaa ambako wasichana hujifanya wananunua vitu, lakini kimsingi huwa wanakwenda kutafuta wateja wa ngono.

“Kule wanaume wameshajijengea picha kuwa wanawake wa Kitanzania wapo kwa ajili ya kujiuza, basi wakikuona tu wanakufuata na mnaongea biashara, mnakwenda kumalizana,” anasimulia.

 Wasichana wenzake wa Kitanzania walimwambia kuwa hayo ndiyo maisha yenyewe, hivyo aliporejea ndani, mwenyeji wake (Jacky) alimwambia ajiandae kuanza kazi mara moja na Munira akawa hana budi kufuata maelekezo.

Baada ya hapo aliingia bafuni akaoga, kisha akaenda eneo la Chambu Chambu kutafuta wateja.

  “Nikakubaliana na hali halisi nikawa nafanya kazi kama nilivyoambiwa. Niliona nikubali lakini akili kichwani mwangu ilikuwa nifanye mbinu ili nirudi nyumbani,” anasema.

Brazil ni Kilio Kila Kona, Wengi Hawaamini Kilichotokea Jana Baada ya Aibu ya Kichapo

$
0
0
Michuano ya kombe la dunia leo imechukua sura nyingine kabisa baada ya mchezo wa kwanza wa nusu fainali kati ya wenyeji Brazil dhidi ya Ujerumani.
Kwenye mchezo uliopigwa kwenye dimba la Belo Horizonte – Ujerumani wameweka historia ya mbili kubwa – kutinga fainali ya 8 ya kombe la dunia – hii ni mara nyingi kuliko timu zote duniani, pili kuifunga Brazil nyumbani kwao ikiwa ni mara ya kwanza kwa Brazil kupoteza mechi ya ushindani kwenye ardhi yao tangu mwaka 1975.
Magoli ya Ujerumani yalifungwa na Muller, Toni Kroos mawili, Sami Khedira, Ander Schurrle nae akafunga mawili huku Oscar akiifungia Brazil goli moja la kufutia machozi katika mechi iliyoishwa kwa ushindi wa 7-1.
Ujerumani sasa anamsubiri mshindi wa kati ya Argentina vs Uholanzi hapo kesho ili kupata kujua mpinzani wake wa fainali itakayopigwa jumapili hii.

Bob Junior Akubali Kutumia Rangi za Kupaka Midomoni (Lipstick)

$
0
0
Kwenye picha mbalimbali za Bob Junior kwa wafatiliaji wamedai kuwa anapaka rangi ya mdomo [Lipstick] Soudy Brown kaongea na Bob Junior na amekubali kusema sababu kubwa ya yeye kupaka rangi hizo za mdomo, Bob Junior Amesema yeye hupaka ili midomo iweze kung'aaa na amesema kuwa hupaka lip shine, na amesema Lips zake ni tamu Balaaaa ...Kazi Kwenu Ladies

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Ukweli Kuhusu Kipa Mwenye Vidole Sita Kwenye Kombe la Dunia 2014

$
0
0
Katika michuano ya kombe la dunia kumeibuka wachezaji wengi ambao wameonyesha uwezo mkubwa kiasi cha kuteka hisia za watu wengi, mmoja wapo ni golikipa wa Mexico Guillermo Ochoa.
Golikipa huyu alionyesha uwezo mkubwa katika mechi alizoichezea Mexico kwenye michuano ya kombe la dunia inayoendelea nchini Brazil, kabla ya timu yake kutolewa na Uholanzi katika hatua 16 bora – lakini pamoja na kuondolewa kwa timu yake bado uwezo wake umeacha gumzo kubwa sana kwenye michuano hii.
Uwezo aliouonyesha Ochoa ulipelekea kuzuka kwa taarifa kwamba golikipa huyo wa Mexico aliumbwa akiwa na vidole sita vya mkononi. Zikatolewa mpaka picha kupitia vyombo vya habari mbalimbali ambavyo vilimuonyesha Ochoa akiwa na vidole sita.
Lakini ukweli ni kwamba kipa huyo ambaye kwa sasa anawindwa na vilabu vingi hana vidole sita. Picha zilizoonyeshwa na kusambazwa kwenye vyombo vya habari ni za kutengeneza.

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Sitta Ateua Masheikh, Maaskofu Kuwarejesha Ukawa Bungeni

$
0
0
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta ameanza mkakati mpya wa kunusuru mchakato wa Katiba Mpya kwa kuitisha kikao cha wajumbe 27 wa Kamati ya Mashauriano ili kuondoa mpasuko kati ya wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na wajumbe wengine.

Katika wajumbe hao wamo maaskofu wawili na masheikh wawili ambao Sitta amewateua kutoka katika Bunge la Katiba.

Sitta ameitisha kikao hicho jijini Dar es Salaam Julai 24 wakati kukiwa na matamko tofauti kuhusu mustakabali wa katiba hiyo, mengi yakieleza kuwa Rais Jakaya Kikwete ndiye aliyeshikilia hatima ya mchakato na wapinzani wakisema mkuu huyo wa nchi ndiye aliyesababisha suala hilo kwenda mrama.

Pia, Sitta ameitisha kikao hicho wakati viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakieleza kuwa suala la serikali mbili kwenye muundo wa Muungano, ambalo liligawanya wajumbe, ndiyo msimamo wa chama na wapinzani wakisema suala hilo halimo kwenye Rasimu ya Katiba na ndiyo sharti lao la kurejea bungeni.

Akizungumza  jana katika mahojiano na gazeti hili, Sitta alisema miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja kutazama mwenendo wa majadiliano katika Bunge hilo na sura 15 za katiba ili kujua yapi muhimu yanayotakiwa kupewa kipaumbele kabla ya Bunge la Katiba kuanza tena vikao vyake Agosti 5.

“Sisi tumeshapeleka barua kwa wajumbe, tumehakikisha zimekwenda na katika mkutano huo tutaelewana kuhusu masuala hayo na mengine. Wasiotaka kuhudhuria wananchi watawaelewa na wataamua iwapo nia ni kususa pekee au wenzetu wana ajenda ya siri,” alisema Sitta.

Alisema katika mkutano huo, kutakuwa na utaratibu maalumu ambao utahusisha viongozi wa dini walio ndani ya Bunge kutoka madhehebu tofauti na baadhi ya wajumbe wengine kutoka kada tofauti ndani ya Bunge hilo.

“Kutakuwa na watu karibu 27, mimi nikiwa mwenyekiti. Atakayevimba kichwa na kudharau, wananchi watajua kuwa nia yake ni tofauti na katiba,” alisema.

Sitta alisema tatizo kubwa katika Bunge hilo litakalosababishwa na kutokuwapo kwa Ukawa ni  namna ya upigaji kura, lakini iwapo theluthi mbili ya wajumbe itatimia basi watakwenda  kwa mwenendo huo.

“Yapo mambo muhimu zaidi katika rasimu hii kama vile tume huru ya uchaguzi, orodha ya haki za binadamu, uongozi wa asilimia 50 kwa 50 kijinsia na kuwapa Zanzibar nafasi zaidi katika Serikali ya Muungano, mambo ambayo ni makubwa kuliko muundo...ya nini kuyapiga teke yote haya na kujikita katika muundo pekee,” alihoji.

Sitta ambaye pia alipingwa kwa kumpanga Rais Kikwete kuhutubia Bunge hilo baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kuwasilisha Rasimu ya Katiba tofauti na kanuni, alisema kuwa kuususia mkutano huo wa Bunge katika kipindi chote hicho siyo hasara kwa CCM, bali kwa wananchi kwa kuwa nia ni kupata katiba bora na wala siyo kukomoana.

“Iwapo Ukawa watasusia kila kitu, basi wataonyesha kuwa siyo wakomavu wa kisiasa,” alisema mbunge huyo wa Jimbo la Urambo Mashariki.


Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Joyce Kiria Anangwa Baada ya Kuingilia Sakata la Flora Mbasa

$
0
0
SOO! Mtangazaji anayedili zaidi na mambo ya haki za wanawake Bongo, Joyce Kiria amenagwa na watu mbalimbali mitandaoni kwa kile kinachoonekana kuingilia sakata la mwimbaji wa Injili nchini, Flora Mbasha na mumewe Emmanuel Mbasha, akionekana zaidi kumtetea Flora.

Mmoja wa watoa maoni katika mtandao wake aliandika: “Joyce acha kujidhalilisha, huoni kama unapoteza utu wako? Naanza kuamini kuwa na wewe ni miongoni mwa wasioheshimu ndoa zao kutokana na kuwashauri wenzako upumbavu!

“Kwa mantiki hiyo hustahili hata kuwepo kwenye Kipindi cha Wanawake Live, ikiwa unatetea upumbavu. Acha kuingilia mambo yaliyopo mahakamani, utapoteza mashabiki wako bure.”

Licha ya kunangwa kwa maneno makali mara kwa mara, Joyce ameendelea kuandika kila wakati kuhusiana na ishu hiyo, akionyesha hisia zake waziwazi kuwa yupo upande wa Flora jambo ambalo limepingwa vikali na wachangiaji walio wengi, wakimtaka asijadili suala lililopo mahakamani.

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Martin Kadinda:Nilitamani Wema Sepetu Awe Mpenzi Wangu Ila Nilihairisha Baada ya Kugundua Hili

$
0
0
Stori: Mayasa Mariwata

MWANAMITINDO maarufu Bongo, Martin Kadinda amesema kabla hajawa kiongozi wake, awali aliwahi kumtamani kimapenzi mcheza filamu Wema Sepetu, lakini alighairi baada ya kugundua ni mwanamke wa kudekadeka.

Kadinda alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati akipiga stori na paparazzi wetu kuhusu masuala mbalimbali yanayomhusu msichana huyo ambaye ana uhusiano wa kimapenzi na mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz.

Kuhusu maisha wanayoishi nyota hao wawili wapenzi, Kadinda alisema kwa jinsi wanavyoishi ni kama watu wanaoigiza, akitolea mfano wa kipindi walichorudiana wakiwa nchini China, ambako wenyewe walisema wanaigiza filamu wakati ndiyo kwanza walikuwa wanarejesha penzi lao lililovunjika mara ya kwanza.

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Tanzania Haipaswi Kuongozwa na Wanyoa 'Unga' Maarufu Kama 'Vipara'.

$
0
0
Akizungumzia sakata la kuibuka kwa watu wanaojitangaza kuwania urais, Askofu mstaafu ndugu Valentine Mokiwa amesema kuwa nchi ya Tanzania bado ni changa sana hivyo haipaswi kuongozwa na wanyoa 'unga' maarufu kama 'vipara'.

"Nchi yetu bado ni changa sana hivyo sii busara kuongozwa na wanyoa 'unga'.Tunahitaji damu iliyokomaa kutuongoza". Alisema Mokiwa huku akionekana dhahiri kumlenga mmoja wa watu ambaye ametangaza nia ya kuwania urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania hivi karibuni kupitia kituo kimoja maarufu duniani cha runinga ya idhaa ya Kiswahili.

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Mabomu ya Arusha: Ni vita ya Biashara ya Utalii Au Al-Shaabab?

$
0
0
Mpaka sasa serikali haijatoa maelezo yanayo tosheleza juu ya mabomu yanayoendelea kulipuliwa Jijini Arusha.

Wananchi wengi kwa kweli sasa wameanza kuingia hofu, na hofu hii inakuja maana hatujui adui ni nani.

Hata hivyo hii vita haiwezikufanikiwa bila kuwashirikisha wananchi, ili waweze kutoa habari za nyendo zisizo za kawsida.

Jiji la Arusha ni kitovu cha biashara ya utalii,na kwa hivi karibuni biashara imeendelea kukua na kukaribisha hata viongozi wakubwa duniani.

Kuna umuhimi wa serikali na vyombo vyake vya dola ku-pursue line hiyo kama ndiyo moja wapo wa sababu za mabomu ya Arusha.

Quote of The Day:

Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Mambo Yanayokera Wafanyayo Wanaume Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi

$
0
0
Kutokubali majukumu , mwanaume umeamua kuwa na mpenzi kuwa responsible na take care of your famili kama ukibahatika kupata mtoto. kwa wadada ukiona mwanaume hayupo responsible ukiwa nae jua hadi kitandani ni mvivu wa kutupa ndio wa kwanza kulalama mmh ujui kukata kiuno. Kukiss ujui akilalamika hivyo kaa kimya uone kama anaweza kazi..... utasikia wanawake wanachuna tutaachaje kuchuna wakati kutoa kwa hiyari amtaki mjifunze.

Kujinunisha hovyo hovyo hivi mwanaume unasusa ili iweje ... he he susa wenzio wala.

Kuwa mchoyo.. unakuta mwanaume ni mchoyo kiasi kwamba hata kuhudumiana ni tatizo...
mwanume pesa yako vitu vyako ni tatizo sasa maana ya mimi kuwa mpenzio au mwili mmoja ni ipi kama unaniwekea demacation kwenye vitu vyako... yani hawa hadi kutoa mawazo ni kazi anaona utafaidi...

Mwanume mbahili yani hadi anaumwa au unaumwa kutoa hela ya kutosheleza matibabu hato ... yani sasa huyu wimbo wake wa kila siku utasikia sina hela.. hivi kutokuwa na hela ni sifa au ni uvivu basi tuone unafanya jambo la maana upuuzi mtupu

Mwanume kuendekeza pombe na marafiki yani unatoa kipao mbele rafiki zako kuliko mpenzio ukiona hivyo ujue huna future nzuri.... baadhi ya maandiko yanasema "ajifanyie rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe though rafiki anweza kuwa kama ndugu" tafakari.

Wivu uliopitiliza hapa wengi ni 25 na 30 sana hawa ndio tatizo utasikia baby tuma picha ... tuma picha unatuma bado tena tuma picha ... hivi niwaulize mnatengenezea movie hizo picha ni nini tatizo?...

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.



Al-Shabaab Noma Sana Washambulia ikulu Somalia Ndani ya nchi yao Wenyewe

$
0
0
Vikosi vya serikali Somalia vimefanikiwa kuidhibiti upya ikulu ya rais katika mji mkuu Mogadishu baada ya wapiganaji wa Al Shabaab kuishambulia.
Maafisa wanasema washambuliaji wapatao watano kutoka kundi la al-Shabab - waliuawa walipoingia katika eneo la ikulu hiyo.
Taarifa zinazohusiana
Somalia
Washambuliaji hao wanadaiwa kulipua bomu lililotegwa kwenye gari karibu na langu kuu la Ikulu hiyo.

Waziri wa habari na mawasiliano wa Somalia Mustaf Dhuhulow ameambia BBC kuwa tayari mmoja wa washambuliaji hao amekamatwa na anahojiwa na polisi.
Waziri Mustaf amesema, '' Walishambulia ikulu ya rais saa za jioni. Alikuwa watu washambuliaji watatu pamoja na dereva wao.
Washambuliaji hao waliuawa lakini dereva wao alipata majeraha madogo na anazuiliwa na polisi na kuhojiwa.
Walijaribu kuvamia Villa Somalia lakini wakakomeshwa. Tutawapa maelezo zaidi baadaye. Na tutaweza kutoa maelezo zaidi kwa raia wa Somalia na dunia nzima.''

Hii ni mara ya pili kwa Al Shabaab kuvamia ikulu ya rais mjini Mogadishu mwaka huu japo mara ya kwanza walifanikiwa kuingia ndani.
Rais Hassan Sheikh Mohamoud hakuwepo wakati wa shambulio hilo.
Kundi la wapiganaji wa kiislamu Al shabaab limefukuzwa kutoka mjini Mogadishu tangu mwaka wa 2011 lakini limekuwa likifanya mashambulio ya kuvizia tangu wakati huo.
Wanamgambo hao wanaaminiwa kufanya mashambulio kadhaa pia katika nchi jirani ya Somalia kama vile Kenya, Uganda na Tanzania kama njia ya kulipiza kisasi kwa kuingia majeshi ya Umoja wa Afrika nchini Somalia.
Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Flora Lymo Amnanga Wiliam Malecela Aka Lemutuz Kwa Kulazimisha Kupiga Picha na Mademu

$
0
0
LEMUTUMBAZ'' BILA HATA AIBU KAPOST HII PICHA YAKE YA PAMOJA NA SHILOLE KWENYE KILE KIBLOGNUKA CHAKE'' AIBUUUU'' SASA WEWE NA AKILI ZAKO TIMAMU UTAPOST VIPI PICHA KAMA HII? NA KUJIRINGISHIA YOU ARE LIVE''' AND SO ON AND ON? IKIWA WATU aka MABEBEZ WAKUJILAZIMISHIA PICHA ZA PAMOJA HAWATAKI ''WEWE KAJIDONDOSHE BAHARINI''MBUTA NANGA'' NI SHIDA!!YANI HAPA HII PICHA HAITAKIWI WALA NIIONGEZEE MANENO MAANA INASEMA WAZI KWAMBA SHILOLE HATAKI KUMSIKIA WALA KUMUONA NA TENA PICHA HII ALIDHANI KWAMBA ANGE DELETE MAANA KAFUNGA MACHO''LAKINI MLAZIMISHAJI YEYE BADO BILA AIBU KAIRUSHA LIVE MITANDAONI '' ILI MRADI AONEKANE NAE YUMO'' ACHIANGAZI BABU TAFUTA NAMNA YA KURUDI MAREKANI UKATUNZE MKEO NA WATOTO ''ULOWAKIMBIA KULE'' YANI NI LAANA TUPU LIJIBABU KUKIMBIA WATOTO WAKE ALOWAZAA''I WONDER WHO WILL EVER TAKE THAT SERIOUS RISK YAKUOLEWA AU HATA KUZAA NA WEWE JIBABU LAKUKIMBIA WATOTO WAKE'' HUKU HATA KAZI HALINA NA BADO LINAISHI KWA BABA '''KYINDO KYA KITE MCHO''
FLORA LYIMO FASHION POLICE BLOG

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Le Mutuz Amjibu Flora Lymo 'Kazi Kuvaa machupi ya Wanaume na Kujiweka Mtandaoni'

$
0
0

Le Mutuz amepost hii kwenye blogu yake
Makelele yamekuwa mengi sana nimesema hivi ninapata taabu sana kubishana na na hicho kimama kizee huko UK kinachopiga mapicha ya uchi kikiwa kimevaa machupi makubwa ya wanaume.

I mean kwanza elimu hatufananani mimi nina Degree 3 hicho kizee ni darasa la Saba, halafu ninasema hivi hii ni picha yangu ya leo asubuhi bila kunawa wala kuoga sasa hebu kiambieni na chenyewe hicho kibibi kizee kipige picha kama hii asubuhi kama hayakuwa majanga ya ajabu! ha! ha! ha! ha! ha!.

Ndio maana wengine tulienda majuu tukasoma shule masikini ya Mungu kibibi hiki kizee kimeenda majuu kujifunza kulilia kubakwa hata bila kubakwa, kuvaa machupi ya wanaume na kujiweka mitandaoni kwa sababu hakuna binadam mwenye akili timamu anaweza vaa yale machupi kinavaa.

Sasa naomba tukate mzizi wa fitina kiambieni kipige picha asubuhi kama mimi muone majanga, wewe kibibi rudi nyumbani ukalime maana hayo machupi hakuna wa kununua yanakufanana wewe wenyewe tu! ha! ha! ha! ha!.

Majuu miaka 20 umeshindwa hata kwenda shule ya kufagia sasa unaishia kulea wazee na matahira le mburulazzzz kwenu wamekusahau huwezi kurudi.

Sasa utaishia kutukana matusi watu ambao hamfanani wenzako humu online tunatafuta pesa wewe unatafuta matusi na michupi mikubwa ya wanaume kimama kizee huzuni sana, U know jipime hapa mimi na wewe U know! ha! ha! ha! - Le Big Show

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Mtangazaji Mwingine wa Clouds FM Anyakuliwa na BBC Idhaa ya Kiswahili

$
0
0
Anyway I saw This coming :Kijana Anorld Kayanda Aliyekuwa Mtangazaji wa Clouds FM Kipindi cha Jahazi Sasa Yupo BBC Swahili :
Hivi Ndivyo Alivyoandika kwenye Ukurasa wake wa Facebook
"Watu hawa (wengine hawapo pichani) walinipokea vizuri hadi nikaogopa pengine wameshanitafutia mteja wanasubiri nilale waniuze. Hii ni familia yangu mpya. Shukrani sana Dada Liz Massinga, John Solombi, Dada Halima Nyanza, Leonard Mubali, Dada Regina Mwalekwa, Hassan Mhelela, Dada Regina Joseph, Ben Mwang'onda, David Eric Nampesya, Baruan Muhuza na wengine wote. Mungu ameshanifikisha nchi ya ahadi kilichobaki ni kumtumikia. Sasa vijana waambie vijana wenzenu nao wawaambie wenzao katika ratiba zao watenge muda wa kuisikiliza Idhaa ya Kiswahili ya #BBC." Anorld Kayanda

Quote of The Day:
Don't judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

Mapacha Walioungana Wazibitisha Kushare Mpenzi Mmoja

$
0
0
Mapacha hawa walioungana, Ganga and Jamuna Mondal  ni raia wa INDIA  wanampezi mmoja anaeitwa Jasimuddin Ahmad ambae ni mwalimu..Mapacha hao wamehojiwa na kusema wanafuraha sana kwa vile mpenzi wao anawapenda jinsi walivyo na wanampenda sana huyu jamaa

Boko Haram waieleza BBC kuhusu hali na afya ya wasichana waliowateka

$
0
0
Mmoja wa wanajeshi wa Boko Haram ambaye hakutaka kujitambulisha jina alizungumza na BBC jana (July 8) na kueleza hali na afya ya wasichana zaidi ya 200 wanaoshikiliwa na kundi hilo, taarifa ambazo zilikuwa tofauti na zile za awali zilizokuwa zikitolewa na maafisa wa Nigeria.

Mtu huyo alisema kuwa wasichana hao wako katika hali salama na wana afya njema tofauti na ripoti alizozitoa Senator kuwa walikuwa wakibakwa wakichukuliwa video na wengine wakiuawa endapo wangekaidi.

Hata hivyo mtu huyo aliweka wazi msimamo wa kundi hilo kuwa watawaachia wasichana hao siku moja baada ya serikali ya Nigeria kuwaachia wafungwa wa kundi hilo wanaowashikilia.

Hivi ndivyo alivyoeleza:

“Kweli tunataka serikali ya Nigeria kuwaachia watu wetu. Kama kiongozi wetu Abubakar Shekau alivyoahidi kwenye vyombo vya habari, kama leo serikali itaawaachia watu wetu, kesho au siku inayofuata tunaahidi mtawaona wasichana wote. Tutaweza kuwaachia kesho ama siku inayofuata. Ninawaambia ukweli, wako katika hali nzuri wakisubiri kuachiliwa. Hawana tatizo. Baadhi wamebadili dini na kuwa waislam, wengine hawakubadili dini lakini hatukuwatofautisha, tunawatunza kwa usawa...”

Alichokisema RAY C baada ya TID kumwagia matusi ya Nguoni

$
0
0
Siku za karibuni, Nyota wa muziki nchini Tanzania Ray C pamoja na TID waliingia kwenye headlines kutokana na kauli za kupishana katika mtandao wa Instagram.

TID alionekana kuja juu kutokana na comment iliyotolewa na Ray C instagram kwenye moja ya post zake.

Baada ya kukaa kimya akimuuguza mama yake hatimaye mwanadada Ray C amejibu kile kilichosemwa na TID.

Hii ndio kauli ya Ray C, Namnukuu “Hi everyone!!!Asanteni kwa maombi yenu!mama anaendelea vizuri Mungu ni Mwema.(na kuhusu @tidmnyama -Nimeona post yako,Asante kwa matusi yako ila sikuwa na nia mbaya tofauti na ulivyofikiria anyway Nakuombea kwa Mungu akuepushe na majanga ya dunia!ubarikiwe sana babaa.

Matokeo ya Mechi ya Uholanzi vs Argentina Kombe La Dunia

$
0
0
Baada ya jana kushuhudia kalamu ya magoli kwenye mechi ya kwanza ya nusu fainali ya kombe la dunia kati ya Brazil na Ujerumani, leo hii imepigwa nisu fainali ya pili kati ya Argentina na Uholanzi.
Matokeo ya mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Sao Paolo ni ushindi uliotokana na mikwaju ya penati wa 4-2 kwa Argentina.
Mechi hiyo ilikuwa ya kukamiana na kucheza kwa kujihami kwa timu zote mbili iliisha kwa sare tasa katika dakika 120 na hivyo ikaamuriwa ipigwe mikwaju ya penati.
Waliopata penati kwa Argentina ni Messi, Aguero, Garay, na Rodriguez wakati Robben na Dirk Kuyt wakifunga penati mbili za uholanzi huku Vlaar na Sneijder wakikosa.
Argentina sasa itaenda kucheza na Ujerumani fainali jumapili hii, wakati Uholanzi wakikutana na Brazil jumamosi kugombea medalinya mshindi wa 3.

Quote of The Day:
I hope everyone that is reading this is having a really good day. And if you are not, just know that in every new minute that passes you have an opportunity to change that.

Jakaya Kikwete: January Anataka Mambo Makubwa Lakini Hajanishirikisha

$
0
0
Rais Jakaya Kikwete amezungumzia nia ya Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba kutaka kuwania urais mwakani, akisema mwanasiasa huyo kijana “anataka mambo makubwa, lakini hajamshirikisha”.

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kutoa maoni yake kuhusu wanachama wa CCM wanaotaka kuwania urais, baada ya chama hicho kuwaonya makada sita kwa tuhuma za kuanza mapema kampeni za kutaka nafasi hiyo kubwa.

Akiwa jijini London, Makamba alitangaza nia yake ya kuwania urais mwaka 2015, akisema huu ni wakati wa fikra mpya ambazo zinahitaji vijana na kwamba wazee wakae kando.

Jana, Rais Kikwete, ambaye alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Soni Bumbuli mkoani Tanga anakoendelea na ziara ya siku tano, alimtaka Makamba “asilazimishe” kwa kuwa wakati ukifika atapata kile anachokitaka.

“Nasikia kuwa bwana mdogo January anataka mambo makubwa. Mie hajaniambia, na mie nasikia. Hata alipogombea ubunge hakuniambia nilisikia baadaye... asilazimishe, wakati ukifika atapata, na akikosa asilete nongwa,” alisema Rais Kikwete.

Rais Kikwete alitoa mfano wake mwenyewe aliposhindwa katika uteuzi wa mgombea urais wa CCM mwaka 1995, wakati akiwa na miaka 45 (miaka minne zaidi ya umri wa Makamba ifikapo 2015), akisema kuwa hakukata tamaa na aliendelea kusikiliza ushauri wa wazee hadi alipofanikiwa kukalia nafasi hiyo ya juu mwaka 2005.

Mwenyekiti huyo wa CCM, ambaye pia ushawishi wake unaweza kuamua mteule wa chama, alimtaka mbunge huyo wa Bumbuli asikilize ushauri wa wazee.

Pamoja na ushauri huo kwa mwandishi wake wa zamani wa hotuba, Rais Kikwete alimpongeza kwa kazi nzuri ya ubunge jimboni humo na akaeleza kuwa anamsaidia katika wizara yake.

Alinukuu maneno ya aliyekuwa katibu mkuu wa Afro Shiraz na swahiba wake, Thabit Kombo aliyemwambia Kikwete kuwa “wakati ukifika utapata”, hasa kutokana na kiu yake ya muda mrefu ya kuwatumikia Watanzania.

“Nilipokosa mwaka 1995 sikukata tamaa, ndipo 2005 nikaingia, na huo ndio ulikuwa wakati wangu wa kushika wadhifa huu. Wakati ukifika watu watake wasitake utakuwa wewe tu,” alisema Kikwete.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete imekuja takriban wiki moja baada ya Makamba kueleza nia yake ya kuwania urais akisema kwa asilimia 90 ameshaamua kuingia katika kinyang’anyiro hicho.

Mbunge huyo wa Bumbuli, ambaye ni mtoto wa Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba, alitangaza uamuzi huo akiwa Uingereza alikokuwa akihudhuria mkutano wa sekta ya mawasiliano baada ya kuhojiwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na baadaye kufafanua nia hiyo katika mahojiano na gazeti hili.

Quote of The Day:
I hope everyone that is reading this is having a really good day. And if you are not, just know that in every new minute that passes you have an opportunity to change that.

LOWASSA kuanza Kampeni Waziwazi, ni Baada ya January Makamba Kutangaza Nia

$
0
0
Kuna tetesi kuwa Edward Lowassa anatarajia kuanza kampeni ya kutangaza nia waziwazi baada ya kuona January Makamba amefanya hivyo wakati ni miongoni mwa waliopewa karipio kali na CCM kwa kampeni za kabla ya wakati muafaka na hajachukuliwa hatua yoyote. Pia ameona Membe akitumia UVCCM kuimarisha kambi yake harakati za kinyang'anyiro cha urais 2015

Quote of The Day:
I hope everyone that is reading this is having a really good day. And if you are not, just know that in every new minute that passes you have an opportunity to change that.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>