Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Omog Ataka Wachezaji Wake Kutowadharau Lipuli Katika Mechi Yao Kesho

$
0
0
Omog Ataka Wachezaji Wake Kutowadharau  Lipuli Katika Mechi Yao Kesho
KOCHA wa Simba, Joseph Omog amewataka wachezaji wake kutowadharau wapinzani wao wa kesho timu ya Lipuli ya Iringa na kuwataka kuwa makini kwa dakika zote 90.

Akizungumza kabla ya kuanza mazoezi ya jana kwenye uwanja wa chuo cha Polisi Kurasini, Omog, alisema kuwa hawatakiwi kuwabeza wapinzani wao hao kwa kuwa mpira ni mchezo wa makosa.

“Hakuna timu ndogo kwenye ligi, wachezaji nimekuwa nikiwaambia hivyo, lazima nidhamu ya mchezo ifuatwe, kama wachezaji watafuata maelekezo tuna nafasi nzuri ya kushinda,” alisema Omog.

Alisema kuwa kwenye mazoezi ya timu hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Sportpesa, amekuwa akikazania wachezaji wake kucheza soka la kasi na kuhakikisha wanatumia vyema nafasi wanazozipata.

“Kwanza naangalia zaidi ushindi kabla ya kutazama wingi wa mabao, kama tutatengeneza nafasi nyingi na kuzitumia vizuri tunaweza kupata ushindi wa mabao mengi,” aliongeza kusema Omog.

Alisema kuwa licha ya ugeni wa Lipuli kwenye ligi, anaamini nao wamejiandaa vizuri kwa ajili ya kupata ushindi kwenye mchezo huo wa kesho utakaochezwa kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

“Walipata pointi moja walipokuja hapa kucheza na Yanga.., kwa hiyo si timu ya kubeza, tutapambana kwa ajili ya pointi tatu,” aliongezea kusema Omog.

Simba ipo kileleni kwa msimao wa ligi ikiwa na pointi 22 sawa na Azam FC wanaoshika nafasiya pili lakini wekundu hao wa msimbazi wana magoli mengi.



Kigwangalla Awachana Wanaosema Vyuma Vimekaza "Wanaofanya Shughuli Zao Halali Hawatoona Vyuma Vimekaza"

$
0
0
Kigwangalla Awachana Wanaosema Vyuma Vimekaza "Wanaofanya Shughuli Zao Halali Hawatoona Vyuma Vimekaza"
Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Hamisi Kigwangalla amesema maisha yataendelea kuwa magumu kwa watu wasio na shughuli maalum ambao wamezoea kuishi kwa ujanja ujanja.

Ameyasema hayo wakai akijibu maswali ya wananchi kupitia mtandao wa ‘Twitter’ ambao wengi walitaka kujua kuhusu utendaji kazi wake na hali halisi ya maisha yalivyo wakidai kuwa ni magumu.
“Wanaofanya shughuli zao halali hawatoona vyuma vimekaza, badala yake watafurahia sema watoto wa mjini, wasanii sanii na wajanja wajanja ndiyo watapata shida! Hawa wajanja wajanja ni wangapi? Na wenye shughuli halali ni wangapi?”, alisema Kigwangalla akiacha maswali kwa mmoja wa watu waliomuuliza.
Waziri Kigwangalla aliendelea kwa kutoa ufafanuzi juu ya namna ya kujenga uchumi kupitia kufanya kazi na sio kutegemea kupata pesa kwa njia rahisi rahisi.
“Mfumo wa uchumi unataka watu tufanye kazi kwa ubunifu ndipo tupate maisha mazuri siyo kufanya usanii kidogo tayari ukatajirika! Kukaza vyuma maana yake kuziba mianya ya wasanii ili walio kwenye uchumi halisi na wasanii wawe sawa siyo kuonea watu!” alimaliza.

Waziri Kigwangalla hivi sasa yupo jimboni kwake Nzega vijijini akiwa amepiga kambi kwaajili ya kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Nata.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo...

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Tupo Mbagala Rangi Tatu

Bwana Harusi Afariki, Bibi Harusi Ajeruhiwa Kwenye Ajari Wakati Wakitoka Kufunga Ndoa

$
0
0
Bwana Harusi Afariki, Bibi Harusi Ajeruhiwa Kwenye Ajari Wakati Wakitoka Kufunga Ndoa
WATU 12 wamekufa na wengine 22 kujeruhiwa katika ajali iliyotokea kijiji cha Ighuka wilayani Ikungi kwenye Barabara Kuu ya Singida – Manyoni baada ya Toyota Hiace walimokuwa wakisafiria kutoka kumchukua bibi harusi kugongana uso kwa uso na Toyota Noah iliyokuwa imepakia watu kutoka msibani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Debora Magiligimba alisema kuwa ajali hiyo ilitokea juzi saa mbili usiku kwa kulihusisha gari lenye namba za usajili T 581 BBV iliyokuwa ikitokea Singida kwenda Manyoni na T 423 CFF iliyokuwa ikitokea Manyoni kwenda Singida.

Alisema kuwa ingawa uchunguzi wa kina juu ya chanzo cha ajali hiyo bado unaendelea, taarifa za awali zinaonesha kuwa sababu kuu ni mwendo kasi na uzembe wa madereva.

“Baadhi ya majeruhi walituambia dereva wa Toyota Hiace aliyekuwa anatoka Singida mjini alihama kutoka upande wake na kwenda upande wa pili wa barabara ambako aligongana uso kwa uso na Noah iliyokuwa imebeba watu waliokuwa wakitoka msibani na kusababisha vifo vya abiria 10 hapo hapo na majeruhi 24,” alisema.

Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa mkoa wa Singida, Dk Ng’hungu Kusenza alisema kuwa majeruhi wawili waliofikishwa Hospitali ya Misheni Puma kwa ajili ya matibabu pia walikufa hivyo kufanya idadi ya watu waliokufa kuwa 12.

Aliwataja waliokufa ambao miili yao imehifadhiwa Hospitali ya mkoa kuwa ni John Duma, Jasson Nsunza, Abubakar Omari, Mary Kinku, Mwanaidi Juma na Husna Juma, Wengine ambao miili yao imehifadhiwa Hospitali ya Misheni Puma wilayani Ikungi ni Ezekiel Joseph, Mussa Daniel, Namtaki Daniel, Hamis Omari, Jumanne Mganga na Wansola Shalua.

Habari ambazo hazijathibitishwa zinadai kuwa Bwanaharusi na madereva wa magari yote mawili ni miongoni mwa watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.

Godbless Lema Ampa Onyo Mrisho Gambo

$
0
0
Godbless Lema Ampa Onyo Mrisho Gambo
Mbunge wa Arusha Mjini, Mh. Godbless Lema amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kutojaribu kufanya hila zozote za kuisababishia CCM ipate ushindi kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika hapo kesho, Nov 26.

Lema amesema kwmba anafahamu kila hatua na vikao ambavyo Mkuu huyo wa Mkoa na kwamba ana ushahidi wa kutosha wa kila kitu kunachopangwa.
"Mrisho Gambo,unapaswa kujua kwamba huna mamlaka wala  uwezo wa kushinda huu uchaguzi kwa nguvu/hila, hakuna kikao umekaa ambacho sina taarifa zake na ushahidi wa kila kitu".  Lema
Aidha Lema ameongeza kwa kumkanya kiongozi huyo asijaribu kufanya hivyo.
"Unataka kushinda uchaguzi huu kwa gharama yoyete ile ?sababu polisi wako nyuma yako ? usijaribu" Lema ameandika kupitia ukurasa wake wa Twitter asubuhi ya leo
Kesho kata 43 zinatarajiwa kufanya uchaguzi wa marudio wa kuwapata madiwani.

Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia Ajali Iliouwa Watu 12 Waliotoka Kuoa

$
0
0
Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia Ajali Iliouwa Watu 12 Waliotoka Kuoa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametumia salama za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Singida kufuatia ajali iliyosababisha vifo vya watu 12.


'Kiba 100' ya Roma na Stamina Yakimbiza You Tube Yashika Nafasi za Juu

$
0
0
'Kiba 100' ya Roma na Stamina Yakimbiza You Tube Yashika Nafasi za Juu
Muunganiko wa wakali wawili wa muziki wa Rap kutoka Tanzania, Roma na Stamina ‘ROSTAM’ umeshika nafasi ya juu baada ya sifa na pongezi kusambaa zaidi zinazowataja kuwa ni miongoni mwa wasanii wanaofanya vizuri kwa umoja wao pindi wanapokwea jukwaa lolote la kiburudani.

Kupitia taarifa rasmi inayoonekana kupitia mtandao wa YouTube, video ya ngoma ya muunganiko wa wakali hao inayokwenda kwa jina ‘Kiba 100’ wakiwa wameshirikisha Maua Sama, chini ya uongozwaji wa Director Nicklass imeendelea kufanya vizuri kwa kushika nafasi ya kwanza(#1 Trending Video) nchin Tanzania.

IGP Siro Atoa Onyo Uchaguzi wa Madiwani Kesho " Jeshi la Polisi Halitamvumilia Atakayeleta Vurugu"

$
0
0
IGP Siro Atoa Onyo Uchaguzi wa Madiwani Kesho " Jeshi la Polisi Halitamvumilia Atakayeleta Vurugu"
Wakati uchaguzi wa udiwani ukitarajiwa kufanyika kesho katika kata 43 nchini, Jeshi la Polisi limesema halitamvumilia yeyote atakayeleta vurugu.

Kauli hiyo imetolewa wakati baadhi ya wanasiasa wakitoa madai ya kuwapo mikakati iliyoandaliwa kuhujumu uchaguzi huo, huku ofisi ya ofisa mtendaji wa Kata ya Saranga jijini Dar es Salaam ikiwa imechomwa moto.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari jana alisema kuna mambo yameanza kujitokeza ya uvunjifu wa amani ikiwemo kuunguzwa ofisi ya mtendaji wa kata hiyo iliyopo wilayani Ubungo na watu kupigana wakiwa kwenye kampeni mkoani Mwanza.

IGP Sirro alisema jeshi hilo litahakikisha wale wote waliofanya matukio hayo wanachukuliwa hatua za kisheria.

Aliwataka wanasiasa kufanya siasa na si kufanya fujo na kwamba, yeyote atakayepatikana amevunja sheria ya nchi atashughulikiwa kama wahalifu wengine.

“Ninawaomba wananchi mchague madiwani walio sahihi msichague wale ambao wanatarajia kuleta vurugu kwa kuwa watashughulikiwa na tunaendelea na upelelezi ili kuwabaini wote waliohusika kuunguza ofisi ya ofisa mtendaji wa kata,” alisema IGP Sirro.

Licha ya kuungua kwa ofisi hiyo usiku wa kuamkia jana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema uchaguzi utaendelea kama ulivyopangwa. Tume imesema vifaa vingi vya uchaguzi vimeteketea.

Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC) Hamis Mkunga alisema jana katika taarifa kwa umma kuwa tayari ofisi yake imekwishafanya utaratibu mwingine ili kuhakikisha vifaa vyote vya uchaguzi vilivyoteketea vinapatikana.

Mkunga alisema chanzo cha moto huo ni hujuma kwa kuwa walioshuhudia walipofika eneo la tukio walikuta dumu la mafuta ya petroli na kwamba vyombo vya ulinzi vinaendelea na uchunguzi.

Alisema vyombo vya usalama wilayani Ubungo vimejulishwa na kuwahakikishia wananchi wa eneo hilo kuwa usalama utaimarishwa na kuwataka wajitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura.

Mkuu wa Idara ya Uchaguzi NEC, Irene Kadushi alisema Kata ya Saranga ina vituo vya kupigia kura 139.

Alisema utunzaji wa vifaa vya uchaguzi zimehamishiwa katika Ofisi ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kwa usalama zaidi.

Mikoa inayotarajiwa kufanyika uchaguzi ni Geita, Mwanza, Dodoma, Ruvuma, Tabora, Songwe, Mbeya, Rukwa, Lindi, Mtwara, Iringa, Singida, Simiyu, Arusha, Tanga, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Manyara na Morogoro.

Malalamiko Chadema

Chadema katika mikoa ya Arusha na Iringa imesema imeandika barua kwa NEC na makao makuu ya polisi kueleza kuhusu kukiukwa utaratibu wa uchaguzi na kuwepo njama za kufanywa vurugu katika uchaguzi huo.

Wakizungumza na waandishi wa habari, mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema; Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro na Kaimu Katibu wa Chadema mkoani hapa, Elias Mungure walisema wanaomba NEC na vyombo vya dola kuingilia kati ili uchaguzi uwe huru na haki.

Lema alisema tangu kuanza kampeni za uchaguzi mdogo, viongozi wa Chadema wamekuwa wakivamiwa na hakuna hatua zinazochukuliwa na kwamba kuna taarifa za njama za wengine kuvamiwa ili kuvuruga uchaguzi.

Meya Lazaro alisema wameshangazwa na viongozi wa Serikali kwenda kwenye kampeni na kutoa ahadi kitu ambacho ni kinyume cha sheria za uchaguzi.

Mungure alisema wameandika barua NEC na kwa vyombo vya juu vya Serikali kuhusu hujuma na ukiukwaji wa utaratibu unaofanyika.

Hata hivyo, Kamaanda wa polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema jana kuwa hana taarifa za mipango ya vurugu na akawataka wenye taarifa kuzipeleka polisi.

Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa akizungumza na waandishi wa habari jana ameitaka polisi kuwaacha wananchi wachague mgombea wanayemtaka akidai kuna hujuma zinafanyika na taarifa ameshazifikisha kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) .

Pia, ametaka watendaji wa Serikali waache kuingilia masuala ya siasa bali watekeleze majukumu yao, huku akitaka mkurugenzi wa Halmashauri ya Iringa kusimamia uchaguzi wa Novemba 26,2017 kwa haki.

Mratibu mwandamizi wa uchaguzi Kata ya Kitwiru wa Chadema, Edward Kinabo amedai kuna njama za kuvuruga uchaguzi usiwe wa amani, uhuru na haki.

Kinabo amesema wameonana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Julius Mjengi na kumweleza kuhusu njama hizo anazodai zinafanywa na polisi na CCM.

Amesema wanachama saba wa Chadema wako polisi kwa wiki moja sasa bila kufikishwa mahakamani jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Meya wa Manispaa ya Iringa, Alex Kimbe amewahakikishia wananchi watachagua kiongozi wanayemtaka na si kwa kulazimishwa kwa kutishwa.
Chanzo: Mwananchi

Faiza Ally Amwonyesha Mpenzi Wake Mpya Kwa Mara ya Kwanza Wakifanya Yao

$
0
0
Faiza Ally Amwonyesha Mpenzi Wake Mpya Kwa Mara ya Kwanza Wakifanya Yao
Muigizaji wa Filamu Bongo, Faiza Ally ameamua kumuweka wazi mpenzi wake mpya baada ya kuachana na Mr. Sugu aliyebahatika kupata naye mtoto mmoja aitwaye Sasha.

Mrembo huyo ametumia fursa ya mtandao wa kijamii wa Instagram kuweka picha akiwa na mwanaume huyo anayehisiwa  kuwa  baba mzazi wa mtoto wake wa pili wa kuime aliyempata miezi kadhaa iliyopita, picha hiyo imewaonyesha wawili hao wakiwa wanapigana busu zito.

“If this is not love basi sijui how love is ❤️,” ameandika mrembo huyo

Mbeya City Yalazimika Kufanya Mabadiliko ya Dharura

$
0
0
Mbeya City Yalazimika Kufanya Mabadiliko ya Dharura
Klabu ya soka ya Mbeya City imelazimika kubadili jezi yake iliyokuwa imepanga kuitumia kwenye mechi ya ugenini leo dhidi ya Singida United.

Mbeya City imefikia uamzi huo baada ya kuwepo kwa mfanano kati ya jezi yake ya Singida United ambao ni wenyeji wao katika mchezo wa leo.
Jezi hizo ni kama zinavyoonekana hapo chini ambapo kushoto ni jezi ya wenyeji Singida United na kulia ni jezi ya Mbeya City iliyokuwa imepangwa kutumika leo.

Hata hivyo bado Mbeya City hawajasema ni jezi gani ambayo watatumia lakini msimu huu jezi zao za pili kwaajili ya mechi za ugenini ni zile zenye rangi ya damu ya mzee hivyo huenda ndio zitakazotumika leo.
Singida United inayoshika nafasi ya 5 ikiwa na alama 17 inacheza leo na Mbeya City yenye alama 11 katika nafasi ya 10 kwenye mchezo wa raundi ya 11, uwanja wa Namfua mjini Sungida.


Tamasha la Fiesta Kimeeleweka Hadi Majogoo Wasanii Walioondolewa Warudishwa

$
0
0
Tamasha la Fiesta Kimeeleweka Hadi Majogoo Wasanii Walioondolewa Warudishwa
Ilitangazwa kwamba Tamasha kubwa la FIESTA 2017 Mkoa wa Dar es salaam litafanyika mpaka saa saba usiku ambapo taarifa hizo zikafanya kamati kuwaondoa Wasanii zaidi ya 15 kwenye orodha ya kutumbuiza sababu ya badiliko la muda wa kumaliza sherehe hii kubwa ya Taifa la Bongofleva.

Wasanii wote walioondolewa wamerudishwa kwenye orodha na mipango yao ya kazi itaendelea kama kawa

Tayari kupunguzwa huko kwa muda kulishafanya baadhi ya Wasanii waondolewe kwenye orodha ya Wanaotumbuiza kwenye tamasha hilo akiwemo Lulu Diva, mtazame akiongea hapa chini

Je Dada Unapenda Kuwa Mrembo na Kaka Unakosa Hamu ya Tendo au Uume Mdogo?

$
0
0
BAADA YA UTAFITI TULIOFANYA MARKSON BEAUTY  TUMEGUNDUA KUWA  WANAUME WENGI DUNIANI HUSUMBULIWA NA MATATIZO KAMA👇👇
☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa  nk.
      @markson_beauty_pr tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
1.HANDSOME UP OG_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @250,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX  CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @200,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/=
     PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
☆Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/=
☆Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
☆Kuwa mweupe bila sugu @150,000/=
☆Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @150,000/=
☆Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @130,000/=
*Kubana uke na kuzuia uchafu ukeni @130,000/=
*Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
     BIDHAA HIZI NI ZA MIMEA NA MATUNDA NA ZIMEPIMWA KTK MAMLAKA NA KUPATA KIBALI HIVYO NI SALAMA KWA 100%

    Wasiliana nasi Popote
  ulipo duniani kwa (+255)
           0767447444 au
              0714335378
        UTAPATA HUDUMA
    NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON BEAUTY CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
        Follow us
WEBSITE:- www.markworldbeauty.og
INSTAGRAM PAGE:-
@markson_beauty_pr

“Wapiga Penati Wanaangalia Chini Kama Kondoo, Enzi zangu Bwana…”-Mwakyembe Atoa Somo Upigaji Penati

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa somo kwa wanasoka wa Tanzania kuhusu namna ya upigaji wa penati baada ya kutoridhishwa na namna ya baadhi ya wachezaji wanaopiga matuta nchini.

Waziri Mwakyembe amesema enzi zake alikuwa anawatungua magolikipa kwa mikwaju ya matuta tofauti na wapigaji wa siku hizi ambao huangalia chini mithili ya kondoo anaetaka kupigana.

“Upigaji penati nchi hii nafikiri nahitaji kukaa na makocha, sisi zamani tulikuwa tunafundishwa. Pale alikuwa hakosi penati, lakini vijana wa sikuhizi pamoja na ufundi mkubwa walionao, wanapiga penati wameangalia chini. Inashangaza mtu anaangaliaje chini? Wanabahatisha.”

“Mimi sipigi penati naangalia chini, najua toka niliposimama hadi kwenye mpira ni hatua sita, namwangalia golikipa movements zake, mguu wangu unaponyanyuka akianza kwenda kulia, mimi napiga kushoto, ndio upigaji wa penati. sasa mtu anaangalia chini utafikiri kondoo anakwenda kupigana.”

“Mimi ni mchezaji wa soka wa muda mrefu hata hao unaowasikia Tukuyu Stars sisi ndio tulianzisha huko miaka ya nyuma imeenda polepole tukiwa vijana wadogo tunacheza mpira, nilikuwa napiga namba tisa (9) vizuri sana.”

Kikosi Bora cha Champions League Wiki hii hiki Hapa, EPL Watoa Wawili tu

$
0
0
1.Igor Akinfeev. Baada ya kuruhusu mabao katika michezo 43 iliyopita, mchezo wake wa jana ulikuwa mchezo wake wa kwanza kucheza bila kufungwa, lakini alionesha kiwango kikubwa sana na kuisaidia CSKA Moscow kushinda bao 2 kwa nunge.

2.Michael Lang. Aliwachefua kabisa Manchester United katika upande wa kulia, uwezo wa mlinzi huyu ulikuwa kikwazo kwa United. Alikuwa na uwezo mkubwa kupandisha mashambulizi na mara nyingi alionekana kumzidi maarifa Daley Blind.

3.Filipe Luiz. As Roma wako vizuri sana msimu huu lakini hana Atletico Madrid walionekama kuwazima kabisa, huku upande wa kushoto wa Atletico ukiwa imara zaidi kutoka na uwepo wa Fellipe Luiz.

4.Samuel Umtiti. Mlinzi wa kati wa klabu ya Barcelona alikuwa katika kiwango kikubwa na kufanikiwa kuwazuia washambuliaji wa Juventus kuwadhuru, kiwango cha Umtiti cha jana kimedhihirisha alistahili kuwa Barcelona.

5.Eric Dier. Maurcio Pochettino anaonekana anawajua haswa wachezaji wake na kwa mara nyingine anamshusha Dier katika nafasi ya mlinzi wa kati, na Dier ameonesha uwezo uliowafanya watu wengi kuamini kwamba ni kiraka haswa.

6.Ever Benega. Wengi wanajadili suluhu ya bao 3 kwa 3 kati ya Liverpool na Sevilla huku kila mmoja akitoa sababu, lakini Benega alikuwa kirusi kikubwa kwa Liverpool na kipindi cha pili aliwafanya Liverpool waonekane hawajui wanachofanya katika eneo la la kiungo.

7.Naby Keita. Uwezo wa kiungo huyu katika siku za hivi karibuni umekuwa gumzl dunia nzima, kwa mara nyingine Keita anaionesha dunia kwamba yeye ni kiungo wa kiwango cha dunia, aliwazima kabisa FC Monaco katika mchezo wao na RB Leizpg wakashinda bao 4 kwa moja.

8.Cesc Fabregas. Huyu ndiye “pass master” ana uwezo mkubwa mnoo na mchezo zidi ya Quarabag jicho lake na uwezo wa miguu yake vilitosha kwa UEFA kumuweka katika kikosi bora cha Champions League wiki hii.

9.Lorenzo Isingne. Uwezo mkubwa sana alioonesha zidi ya Shaktar Donetski umewafanya Waitaliano kuhoji sababu ya Gian Piero Ventura kumuweka nje katika mechi ambayo Italia walikatishwa ndoto zao za kwenda kombe la dunia.

10.Bas Dost. Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uholanzi alikuwa katika kiwango kikubwa sana wakati Sporting Lisbon wakiichapa Olympiakos kwa mabao 3 kwa 1 huku Bas Dost akifunga mabao mawili kwa kila kipindi.

11.Neymar. Achana na Edison Cavanni lakini mshambuliaji wa Kibrazil Neymar amezidi kuionesha dunia kwamba yeye anastahili kuwa mchezaji ghali duniani, alifunga mabao 2 wakati PSG wakishinda mabao 7 lakini alikuwa nyota katika mchezo huo.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE..

Mbowe: Tumewazidi CCM Kimkakati Katika Kampeni za Uchaguzi za Udiwani

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema wamewazidi CCM kimkakati katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani utakaofanyika kesho  katika kata 43 nchini.

Mbowe amesema chama tawala hakina mpango mkakati wa kufahamu mambo gani wananchi wanataka na shida gani zinawakabili zaidi ya kuzungumzia kwa jumla na kujinasibu kufanya mambo makubwa ikiwamo kujenga barabara, kununua ndege na kupambana na mafisadi.

Amesema leo Jumamosi Novemba 25,2017 kuwa ndiyo maana katika kampeni za kuwanadi wagombea wa uchaguzi huo alinadi ajenda tatu ambazo ni dhana ya uhuru, maendeleo na demokrasia.

Mbowe amesema maendeleo hayapimwi kwa kununua magari, kujenga viwanja vya ndege, kupambana na mafisadi bali yanapimwa kwa maisha ya mwananchi mmoja mmoja.

"Tunaaminishwa uchumi unakuwa kwa sababu nchi imenunua ndege, inapambana na mafisadi na inajenga viwanja vya ndege, hayo ni mambo mazuri hakuna anayepinga, lakini je, mwananchi wa kawaida ananufaika vipi," amesema Mbowe.

Amesema hali ya maisha ni ngumu, hivyo Serikali isijifungie na isizibe masikio kusikia wanacholalamika wananchi.

"Wananchi wana hali ngumu, sisi tuliozunguka na kuzungumza nao tunajua, biashara zinafungwa, wananchi masikini hali zao zimezidi kuwa ngumu, watumishi hawajapandishiwa mishahara hivyo hali kuzidi kuwa duni kwa wanaotegemea kuchuuza bidhaa kwa sababu hakuna anayemudu kununua," amesema Mbowe.

Amesema amani ya kudumu na demokrasia haiwezi kuwepo kama hakuna nafasi ya vyama vya siasa kufanya kazi zake bila kuonekana kama wahalifu.

Mbowe amesema wananchi wana kiu na shauku ya kuhudumia mikutano ya kisiasa.

Majimaji Yawatangazia Kihama Ruvu Shooting "Wajipange Kupokea Kichapo"

$
0
0
Majimaji Yawatangazia Kihama Ruvu Shooting "Wajipange Kupokea Kichapo"
MAJIMAJI ya Songea mkoani Ruvuma, imesema kuwa, kutokana na wachezaji wake kuwa na afya njema, leo lazima iibuke na ushindi mbele ya wenyeji wao, Ruvu Shooting.

Majimaji inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo ya Sokabet, leo Jumamosi inacheza na Ruvu Shooting mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Kocha Msaidizi wa Majimaji, Habib Kondo, alisema wamewaandaa vijana wao tayari kwa mchezo huo na kinachowapa matumaini ya kuibuka na ushindi ni kutokuwa na majeruhi hata mmoja.

“Tupo vizuri kupambana na Ruvu Shooting, hivyo wapinzani wetu wajipange kupokea kichapo kwani malengo yetu makubwa ni kuondoka na pointi tatu, haijalishi kama tupo ugenini.

“Hatuna majeruhi ndiyo maana tumekuwa na matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi kwani tutakuwa na wachezaji wote, kilichobaki ni kuchagua nani aanze ili tupate matokeo mazuri,” alisema Kondo.

Majimaji ipo nafasi ya nane katika ligi kuu ikiwa na pointi 11 ambapo katika mechi kumi, imeshinda michezo miwili, imetoka sare tano na kufungwa mara tano.

Rais Magufuli Amwagia Sifa Kikwete Kwa Kufanikisha Ujenzi wa Hospitali

$
0
0
Rais Magufuli Amwagia Sifa Kikwete Kwa Kufanikisha Ujenzi wa Hospitali
Rais wa Serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa sifa na pongezi kwa rais mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kufanikisha ujenzi wa hospitali ya Mloganzila.

Rais ametoa pongezi hizo leo wakati akihotubia wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Hospitali na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila jijini Dar es salaam.
“Wakati ujenzi wa Hospitali hii unaanza mimi nilikuwa naagizwa tu na niliambiwa nikatafute eneo kubwa nikawaza nitalitoa wapi lakini baadae mzee Jakaya akanipigia tena simu  akaniambia kuna eneo huko Mloganzila ni la serikali nenda kaangalie na ujenzi uanze haraka, ndio nikaja hapa”, amesema Rais Magufuli.
Rais magufuli ameongeza kuwa “Watu tunapenda sifa lakini hizi sifa sio zangu ni za rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwani mimi nilikuwa naagizwa tu nikiwa waziri wa Ujenzi, ndio maana nimeona niseme wazi kuwa sifa zote zimwendee mzee Kikwete”.

Aidha rais Magufuli ameweka wazi kuwa wakati anakwenda kuona eneo la Mloganzila wala hakukuwa na barabara lakini aliambiwa na rais Kikwete aanze ujenzi wa miundombinu ikiwemo barabara haraka iwezekanvyo na alifanya hivyo sambamba na waziri wa maji amnbaye naye aliagizwa kuanza ujenzi wa miundombinu ya maji.
Rais Magufuli amesisitiza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa Hospitali na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila jijini Dar es salaam ni mpango na jitihada za rais wa awamu ya nne.

Misri Yaapa Kukabiliana na Wauaji wa Watu 235 Msikitini

$
0
0
Misri Yaapa Kukabiliana na Wauaji wa Watu 235 Msikitini
Kikosi cha kijeshi cha Misri kimeanza mashambulio dhidi ya ngome za wanamgambo wanaodhaniwa ndio waliosababisha vifo vya watu wapatao 235 baada ya kuwashambulia katika eneo la rasi ya Sinai wakati walipokuwa wanatoka msikitini.
Waathiriwa wengi wa shambulio hilo lililofanywa na wanamgambo walikuwa ni wanawake, wanaume na watoto pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa wakitoka msikitini .
Serikali ya Misri imetangaza siku tatu za maombolezi kufuatia mauaji hayo.
Watu 235 wauawa katika shambulio la msikiti Misri
Rais Abdel-Fattah al-Sisi ameahidi kuchukua hatua kali dhidi ya wanamgambo hao.
Eneo hilo la Sinai hukumbwa na mashambulio ya mara kwa mara yanayofanywa na wanamgambo wanaopinga serikali ya Misri, na msikiti uliolengwa ni maarufu sana na waumini wa madhehebu ya kisufi na watu wa kabila la -Sawarka wanaosemekana kuunga mkono kikamilifu serikali ya rais rais Abdel-Fattah al-Sisi .

Ngome ya Chadema Yavamiwa na Watu Wasiojulikana Wakiwa na Siraha za Moto na Kumteka Mwanachama Wake Mmoja

$
0
0
Ngome ya Chadema Yavamiwa na Watu Wasiojulikana Wakiwa na Siraha za Moto na Kumteka  Mwanachama Wake Mmoja
Mbunge wa Iringa Mjini  Peter Msigwa amethibitisha kuchukuliwa na Mwanachadema (Linus) wa Iringa na watu wasiojulikana waliokuwa na silaha za moto.

Msigwa amesema kwamba watu hao wamefika katika ngome yaoya kuratibu Kampeni za uchaguzi wa udiwani wakiwa na aliyekuwa diwani wa CHADEMA na kisha kuhamia CCM (ambaye ni mgombea tena wa nafasi hiyo kwa sasa) ambapo yeye ndiye amekuwa akionyesha watu wa kukamatwa.
Ameongeza kwamba kwakutumia  juhudi zao binafsi imewabidi kuwasiliana na OCD pamoja na afisa upelelezi wa wa wilaya kuhusu kuvamiwa kwa watu wao ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye vituo vya polisi kwa ajili ya kuweza kufuatilia wapi mtu wao alipopelekwa.
"Kuna watu nimewatuma waende polisi kwa ajili ya kuwafatilia kama amepelekwa. Nimewasiliana na OCD ingawa ameniambia yupo kwenye ziara ya Kikwete, pia Afisa upelelezi wa wilaya na tayari kituo cha polisi tumepeleka namba ya gari moja ambalo lilionekana kwenye uvamizi huo" Msigwa.
Akizungumza kuhusu watu waliodhurika kutokana na tukio hilo Msigwa amesema kwamba "Watu walishakusanyika kwa ajili ya kuwazingira watu hao waliovamia  lakini walipoonyesha bastola zao watu wakarudi nyuma. Kwa kifupi CCM Kitwiru hawana namba sasa wanajaribu ku-'force'".
Sambamba na hayo  Msigwa amesema kwamba tangu jana walikwishamlalamikia RPC  kutokana na vitendo ambavyo vimekuwa vikifanywa na askari wa Mkoa ikiwa ni pamoja na kuwatengenezea watu wa Chadema kesi ambazo hazina ukweli na mpaka leo wengine wakiendelea kusota chini ya ulinzi kwa wiki nzima .
Aidha Mbunge Msigwa amesema kwamba kuna askari ambao ni wa Mkoa kutoka kwa RPC  wamekuwa wakivalia nguo za CCM zile 'Green Guard'  kwakushirikiana na vijana wa 'Green Guard' na kisha kuanza kuwasumbua na kuwatisha Wenyeviti wa Mtaa (Chadema) na wakati mwingine wamekuwa wakiwapiga wanachadema mawe lakini RPC mpaka sasa hajawachukulia hatua yoyote.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images