Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live

Je Wajua Kwanini Baadhi ya Wanaume wana Maumbile Madogo?

$
0
0


KWANINI BAADHI YA WANAUME WA NA MAUMBILE MADOGO?
Tatizo hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia ,hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wenzao,kwakawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6_8 vinginevyo mtu huyu ana matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni,upungufu wa vichocheo (hornes) za gestrojen ambapo mwanaume anapobalehe vichocheo hivi (hormones)huchochea ujuaji wa uume.chango ambalo hushambulia nerve ambapo huharibu kabisa ukuaji wa uume, Punyeto ambayo huasili misuli ya uume,pia ngiri ambayo huleta maumivu ya tumbo kuunguluma na kujaa gesi,korodani moja kuvimba,kutopata choo vizuri,sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kisinyaa nakuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu zakiume (hamu ya tendo landoa hupungua au kuisha kabisa).NSUMBU,Nidawa inayozalisha hormones za gestrogene na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.NZAGI,Ni dawa ya kurudisha nguvu za kiume ,hutia hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila hamu kuisha nakuponya kabisa tatizo hilo. Pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk 15 nakuendelea kwa tendo la kwanza.kumbuka dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji.Natunatibu kisukari,bp,ngiri,miguu kuwaka moto,namengine mengi.

WASILIANA OSTADHI JUMA KWA SIMU NO,0784002216 AU 0769597778

Mmiliki wa Shule Amefikishwa Mahakamani Kusomewa Shitaka la Mauaji.

$
0
0
 Mmiliki wa Shule  Amefikishwa Mahakamani Kusomewa Shitaka la Mauaji.
Mmiliki wa Shule ya Msingi na Sekondari ya Scolastica iliyopo mji wa Himo wilayani Moshi, Edward Shayo amefikishwa mahakamani leo Jumatatu kusomewa shitaka la mauaji.

Mmiliki huyo, pamoja na watu wengine wawili wanatarajiwa kusomewa shitaka la mauaji ya mwanafunzi wa shule hiyo, Huphrey Makundi (16) aliyekuwa kidato cha pili.

Shayo ametolewa hospitali ya rufaa ya KCMC alikolazwa na kupelekwa moja kwa moja Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini Moshi chini ya ulinzi mkali wa polisi.

Muda wowote kutoka sasa anatarajiwa kusomewa shtaka hilo pamoja na mlinzi wa shule na mwalimu mmoja ambao tayari nao wapo chumba cha mahabusu cha Mahakama.

Mtoto huyo alitoweka shuleni Novemba 11 na baadaye kubainika ameuawa baada ya maiti yake iliyozikwa kama ya mtu asiyefahamika, kufukuliwa Novemba 17

Papa Yuko Myanmar Inayotuhumiwa kwa Mauaji ya Waislamu wa Rohingya

$
0
0
Papa Yuko Myanmar Inayotuhumiwa kwa Mauaji ya Waislamu wa Rohingya
Papa Francis amewasili nchini Myanmar kwa ziara ya wiki nchini humo na Bangladesh, wakati wasiwasi unaendelea wa kimataifa kuhusu usalama na ulinzi kwa wasilamu wa Rohingya.
Lengo ni kuona iwapo atatumia neno "Rohingya" kuwaita kundi la watu wanaosema wamenyanyaswa.

Maafisa nchini Myanmar wanakataa kulitumia jina hilo, jambo ambalo linaongeza wasiwasi kwamba huenda kukazuka ghasia za Mabudda walio wengi nchini humo iwapo Papa atalitumia jina hilo.
Hata kabla ya kuondoka Roma, Papa Francis alikuwa anakabailiwana kitendawili cha kidiplomasia: iwapo kuliita kundi dogo la waislamu Myanmar - Rohingya.
Ni jina lisilo tumika na serikali ya kiraia na jeshi - wakieleza kuwa ni wahamiaji haramu kutoka Bangladesh na kwahivyo hawapaswi kuorodheshwa kama mojawapo ya makabila nchini humo.

Lakini mashirika ya kutetea haki za binaadamu wanamuomba awaite hivyo, yakieleza kuwa nilazima Papa Francis aoneshe huruma kwa watu walionyimwa uraia na tangu Agosti wamekabiliwa na kile kamishna wa haki za binaadamu katika Umoja wa mataifa amekitaja kuwa 'kinachoonekana kuwa mauaji ya kikabila'.

Zaidi ya WaRohingya 600,000 wamekimbilia mpakani - na wakimbizi wakielezea kukabiliwa na mauaji, ubakaji na kuteketezwa moto kwa vijiji - jeshi imekana tuhuma zote.
Papa atakutana na kiongozi wa Myanmarr - Aung Sun Suu Kyi - Jumanne - huenda ni jukumu zito kidiplomasia katika miaka yake minne kama kiongozi wa kanisa katoliki.

Mwanamfalme Prince Harry Kumuoa Mpenzi Wake Meghan Markle

$
0
0
Mwanamfalme Prince Harry Kumuoa Mpenzi Wake Meghan Markle
Mwanamfalme Harry atafunga ndoa na mpenzi wake Mwigizaji Mmarekani Meghan Markle, Jumba la Clarence limetangaza.
Mwanamfalme huyo, wa tano kwenye msururu wa warithi wa ufalme wa Uingereza, atafunga ndoa na Bi Markle majira yajayo ya kuchipua.
Harusi yao itafanyika katika Nottingham Cottage, Kensington Palace jijini London.
Mwanamfalme Harry athibitisha mpenziwe
Wawili hao, ambao wamekuwa wakichumbiana tangu Julai 2016, walitangaza rasmi uchumba wao Novemba.
Taarifa imesema Mwanamfalme Harry ana furaha sana kutangaza taarifa hizo na kwamba amepokea baraka na idhini kutoka kwa wazazi wa Bi Markle.
Wawili hao walionekana hadharani mara ya kwanza Septemba mwaka huu.

Miss Afrika Kusini Avishwa taji la Miss Universe 2017

$
0
0
Miss Afrika Kusini Avishwa taji la Miss Universe 2017
NEL-PETERS (22) mrembo aliyeshika nafasi ya kwanza nchini Afrika Kusini amevishwa taji la Mrembo wa Dunia (Miss Universe 2017) akiwashinda Miss Colombia, Laura Gonzales (mshindi wa pili) na Miss Jamaica, Davina Bennett (mshindi wa tatu) katika mchuano uliofanyika jana Jumapili jijini Las Vegas, Marekani.
Mrembo huyo ametunukiwa taji hilo ambapo pia hivi karibuni alitunukiwa shahada katika menejimenti ya biashara kwenye Chuo Kikuu cha North-West cha Afrika Kusini. Akihojiwa wakati wa mashindano hayo, Nel-Peters ambaye ni mzaliwa wa Western Cape nchini humo, alisema kuna wakati aliwahi kutishwa kwa kushikiwa bunduki na watu ambao hakuwataja, akaongeza kwamba tukio hilo limemfanya kuwa na mpango wa kuwafundisha wanawake jinsi ya kujilinda.
Akijibu maswali zaidi, mrembo huyo alisema suala kubwa zaidi kwake linalomkera ni wanawake kulipwa asilimia 75 ya mshahara kwa kazi ileile ambapo wanaume hulipwa asilimia 100. “Kuna sehemu za kazi wanawake hulipwa asilimia 75 kwa kazi ileile, saa zilezile za kazi wafanyazo wanaume. Sidhani kama hii ni haki, lazima tuwe sawa duniani kote,” alisema Nel-Peters.
Washindi 13 walioingia fainali walitoka nchi za Thailand, Sri Lanka, Ghana, Hispania, Ireland, Croatia, Uingereza, Marekani, Brazil, Canada, Philippines, Venezuela na China.

Kocha Mkuu wa AC Milan Atimuliwa

$
0
0
Kocha Mkuu wa AC Milan Atimuliwa
Klabu ya AC Milan imetangaza kuachana na Kocha wake Mkuu, Vincenzo Montella na nafasi yake kuchukuliwa na Gennaro Gattuso.

Kibarua cha Montella kilizidi kuwa kigumu wakati timu yake ya Milan ilipokubali kutoka sare dhidi ya Torino siku ya mchezo uliyopigwa hapo jana siku ya Jumapili.

Kablu hiyo yenye maskani yake nchini Itali,imetoa taarifa hiyo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter.

“Milan inatangaza kuachana na Vincenzo Montella kama Kocha Mkuu . Benchi la ufundi lanaimani na Gennaro Gattuso kuziba nafasi ya Montella.” ujumbe ndivyo ulivyosomeka kupitia mtandao wa Twitter.

Gattuso ambaye ni straika wazamani wa Itali na klabu ya AC Milan anarudi kuchukua nafasi hiyo akitokea timu ya Primavera team.



Aliyekuwa Kocha wake Mkuu wa AC Milan, Vincenzo Montella (kushoto) na Gennaro Gattuso (kulia)

Montella ameanza kuitumikia Milan wakati wa majira ya joto mwaka 2016 baada ya kuziongoza klabu za Roma, Catania, Fiorentina na Sampdoria.

Licha ya kupatiwa wachezaji wengi wapya ndani ya kikosi chake na mmiliki wa klabu hiyo, kocha huyo mwenye umri wa 43, amepoteza michezo sita kati ya 11 aliyocheza katika Serie A, na kuiacha ikiwa na alama 20 huku ikishika nafasi ya saba katika msimamo wa ligi.

Mwakyembe Ametembelea Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid

$
0
0
Mwakyembe Ametembelea Uwanja wa Kumbukumbu ya  Sheikh Amri Abeid
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe leo ametembelea uwanja wa kumbukumbu ya  Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Waziri Mwakyembe akiwa ameambatana na Rais wa TFF Wallace Karia pamoja na Kaimu Katibu mkuu wa TFF Kidao Wilfred amejionea maendeleo ya marekebisho yanayofanyika kwenye Uwanja huo.
Uwanja huo upo kwenye marekebisho ili kuboresha eneo la kuchezea (Picha) pamoja na majukwaa na maeneo mengine ya uwanja kama ubora wa vyoo na mabafu.

Waziri Mwakyembe na viongozi hao wa TFF wameambatana na wenyeji wao ambao ni viongozi wa chama cha soka mkoani humo ARFA na wamewaonesha maeneo mbalimbali ya uwnaja huo ambayo tayari yameshaekebishwa na yake ambayo bado.
Mwakyembe yupo mkoani Arusha tangu jana akiwa ameenda kwenye shughuli mbalimbali ikiwemo ufunguzi wa ligi kuu soka ya wanawake Tanzania bara. Katika mchezo wa uzinduzi Allience Queens ya Mwanza ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Panama FC.

Serikali Kununua Kondom Milioni 500 na Kusambazwa Nchini Bure

$
0
0
Serikali Kununua Kondom Milioni 500 na Kusambazwa Nchini Bure
Serikali inatarajia kununua kondomu milioni 500 zitakazosambazwa nchi nzima bure kwa lengo la kupunguza maambukizi ya Ukimwi ifikapo mwaka 2030.


Kondomu hizo zitasambazwa bila malipo ambapo kutakuwa na mashine maalumu zitakazofungwa kwenye maeneo ya baa, nyumba za kulala wageni, migodini na katika kumbi za burudani.

Akizungumza leo wakati wa uzinduzi wa mkakati wa kitaifa wa kondomu, Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Neema Rusibamaila, amesema kondomu hizo zitanunuliwa kupitia fedha za Global Fund.

“Takwimu za mwaka 2011/12 zinaonyesha asilimia 69 ya wanawake na asilimia 77 ya wanaume wanafahamu kwamba kondomu inaweza kuzuia VVU lakini ni asilimia 27 tu ya watu wenye wenza zaidi ya mmoja walitumia kondomu walipofanya ngono mara ya mwisho,” amesema.

Ulinzi Waimarishwa Nairobi Kenyatta Akitarajiwa Kuapishwa Kesho

$
0
0
Ulinzi Waimarishwa Nairobi Kenyatta Akitarajiwa Kuapishwa Kesho
Ulinzi umeimarishwa katika jiji kuu la Kenya, Nairobi pamoja na miji mingine mikuu Rais Uhuru Kenyatta akitarajiwa kuapishwa kuongoza nchi hiyo kwa muhula mwingine hapo kesho.
Muungano wa upinzani umetangaza kwamba hautambui sherehe hiyo na haumtambui Bw Kenyatta kama rais aliyechaguliwa na wananchi.
Kiongozi mkuu wa upinzani Raila Odinga amepanga kuandaa mkutano mkubwa wa kuwakumbuka watu waliofariki wakati wa makabiliano kati ya wafuasi wa upinzani na polisi.
Bw Odinga na muungano wake wa National Super Alliance (Nasa) wamesisitiza kwamba mkutano huo utafanyika katika uwanja wa Jacarada, Nairobi, takriban kilomita kumi hivi kutoka uwanja wa Kasarani ambapo sherehe ya kuapishwa kwa Bw Kenyatta itakuwa inaendelea.
Polisi hata hivyo wamesisitiza kwamba hakutakuwa na mkutano mwingine Nairobi ila sherehe ya kumuapisha Bw Kenyatta.
Bw Odinga alisusia uchaguzi wa marudio uliofanyika 26 Oktoba baada ya kufutiliwa mbali kwa uchaguzi wa kwanza uliokuwa umefanyika tarehe 8 Agosti.
Mahakama ya Juu ilifutilia mbali uchaguzi huo wa kwanza kutokana na kesi iliyokuwa imewasilishwa na Bw Odinga.

Bw Kenyatta alipata asilimia 98 ya kura katika uchaguzi wa marudio, ushindi ambao uliidhinishwa na Mahakama ya Juu iliyofutilia mbali kesi mbili zilizokuwa zimewasilishwa na wanaharakati wawili na mbunge wa zamani kupinga uchaguzi huo.
Serikali imesema viongozi 20 wa mataifa mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria sherehe hiyo ya kuapishwa kwa Bw Kenyatta, akiwemo kiongozi wan chi jirani ya Tanzania Dkt John Magufuli.
Mwezi uliopita, ripoti ya Tume ya Taifa ya Haki za Binadamu ilisema watu 37 waliuawa tangu kutokea kwa uchaguzi wa tarehe 8 Agosti.
Tume hiyo iliwatuhumu polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi wakikabiliana na wafuasi wa upinzani.
Idara za usalama nchini Kenya zimekanusha tuhuma hizo.

Sakaya Aweka Msimamo Wake CUF 'Sipo Tayari Kuondoka CUF'

$
0
0
Sakaya Aweka Msimamo Wake CUF  'Sipo Tayari Kuondoka CUF'
Naibu Katibu wa CUF Tanzania Bara, Magdalena Sakaya  amedai hayuko tayari kuondoka Chama cha Wananchi CUF na kwenda katika vyama vingine hata kama chama chake kina mgogoro na iwapo na ikitokea Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ikiamua kukifuta

chama hicho yeye atastafu siasa
Akifanya mahojiano maalumu na Nipashe, Sakaya amesema kwamba Mgogoro unaoendelea ndani ya chama chao ni wa Kikatiba na unafahamika kwa msajili wa vyama na kuongeza kama ikitokea kwamba CUF inafutwa basi yeye atastaafu siasa na siyo kuhama chama.
"Kwanza naamini CUF haiwezi kufutwa. Yaani hilo halipo pamoja na changamoto ya mgogoro iliyopo. CUF ina misingi yake na mgogoro uliopo ndani yake ni wa kikatiba. Kwa hiyo, mimi nikiamua kwamba sasa sitaki kuendelea kuwapo CUF, ninaacha siasa. Ninaendelea na mambo yangu mengine, eeeh" Sakaya
Sakaya ameongeza kwamba "Kwanza mimi sijawahi kuwa na kadi ya CUF pekee. Nakumbuka wakati tunaripoti Shule yaSekondari ya Wasichana Kibosho (mwaka 1986) tuligawiwa kadi za kijani (CCM) wakati ule nchini kulikuwa na chama kimoja. Baadaye nikiwa na akili yangu timamu kadi niliyoichukua ni ya CUF ambayo niliichukua mwaka 1995 na ninayo mpaka leo na nitaendelea kuwa nayo. .

Mbunge Leonidas Gama Kuzizikwa Leo Kijijini Kwao

$
0
0
Aliyekuwa mbunge wa Songea Mjini, Leonidas Gama anazikwa leo kijijini kwao Likuyu Fusi wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Ibada ya mazishi imefanyika leo Jumatatu Novemba 27,2017 nyumbani kwao kijijini Likuyu Fusi umbali wa kilomita 25 kutoka Songea mjini. Mazishi hayo yamehudhuriwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Gama alifariki dunia usiku wa kuamkia Alhamisi Novemba 23,2017 katika Hospitali ya Misheni ya Peramiho alikopelekwa baada ya hali yake kubadilika akiwa nyumbani kwake.

Taarifa ya Bunge iliyotolewa baada ya kifo cha Gama ilisema mbunge huyo alirejea nchini Novemba 11,2017 akitokea India alikokuwa akipatiwa matibabu.

ZIMBABWE: Rais Mnangagwa Ampa Shavu Mugabe..

$
0
0
Rais wa Mpito, Emmerson Mnangagwa aidhinisha rasmi tarehe ya kuzaliwa ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe (21 Februari) kuadhimishwa kama Sikukuu ya Kitaifa

Itatambulika kwa jina la "Robert Gabriel Mugabe National Youth Day" kama ambavyo ilipendekezwa na chama tawala mnamo mwezi Agosti mwaka huu!

Je unasumbuliwa na Upungufu wa Nguvu, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0

JE, UNASUMBULIWA NA UPUNGUVU WA NGUVU, HAMU YA TENDO LA NDOA AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?
SOMA HAPA👇👇.
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
Kwa kutumia mimea na matunda🍅🍍🍓🌿🍉🍒🍎 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
🍉🍒🍓🌿🍍🍅🍀🍉
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Mjue Charlie Chaplin, Mwigizaji Mchekezaji wa zamani

$
0
0
Leo tunamuongelea mchekeshaji wa zamani ambaye aliacha historian duniani kwa kazi yake ya sanaa iliyowavutia watu wengi kipindi icho mpaka sasa

Charlie Chaplin ni miongoni mwa watu waliokuwa na vipaji hasa mpaka kuna baadhi ya watu wanasema hajatokea kama yeye mpaka sasa

Charlie Chaplin alizaliwa London, 16 Aprili 1889, wazazi wake waliofanya kazi katika sekta ya burudani alipokuwa na umri mdogo baba yake aliekuwa mlevi alipotea na baadaye mama yake alipata matatizona na akapelekwa kwenye hifadhi
Hii ilisababisha Charlie na nduguye kujilea wenyewe Mwaka 1910 Charlie alisafiri na kuelekea Amerika na kupata ujuzi katika sekta ya filamu kutokana na kipaji alichokuwa nacho alibuni alama mtindo wake wa uvaaji uliokuwa ukimtambulisha ni kofia ya bakuli, masharubu na nguo zinazofaa,


Charlie Chaplin akawa nyota kubwa na umaarufu wake ulienea duniani kote Charlie Chaplin alikuwa na uwezo mkubwa alitumia fedha, kuandika na kuelekeza filamu zake mwenyewe baadhi ya filamu zake maarufu zaidi ni pamoja na lights city ya Mwaka (1931) greater dictator ya Mwaka (1940)
Kutokana na uchekeshaji wake kuna watu wakiona picha yake tu wanacheka

Filamu yake ya Greater dictator ilikuwa inaongelea juu ya udikteta wa kikatili wa Hitler na Mussolini. Chaplin mwenyewe alicheza majukumu mawili alicheza kama myahudi aliyechaguliwa Pia alicheza kama "Adenoid Hynkel - dikteta wa Tomania ufahamu wazi wa Adolf Hitler Filamu hiyo ilifanyika mwaka mmoja kabla ya Marekani kuingia katika vita dhidi ya Ujerumani Hatimaye mamlaka ya Marekani waliamua kumruhusu kutumia visa yake ya kuingia Marekani baada ya kuzuiliwa kwa mda kwa sababu za kuukuunga mkono ukomunisti

Charlie Chaplin baadaye alisema hakuwa Mkomunisti lakini alikataa kuhukumu Wakomunisti kwa sababu hakupenda asili ya zama za McCarthy

Chaplin alikuwa na vipaji vya ajabu hii ilikuwa ni talanta iliyopatikana kupitia filamu zake za kimya Charlie Chaplin pia kutokana na kazi zake nzuri alipewa tuzo mwaka 1972 kwa alama yake ya muziki katika filamu ya 1952 Limelight Pia alipewa tuzo ya heshima mwaka 1972 ambayo picha ya mwendo aina ya sanaa ya karne hio
Charlie Chaplin alikuwa na watoto 11 kwa wanawake watatu tofauti na alikuwa na wanawake wengine kwa kibongo tunaita (michepuko) alikufa katika usingizi huko Vevey Uswisi siku ya Krismasi 1977

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo


Aslay Hajawahi Kuniandikia Nyimbo, Wala Kunisadia Chochote- Beka Flavour

$
0
0
Aslay Hajawahi Kuniandikia Nyimbo, Wala Kunisadia Chochote- Beka Flavour
Msanii Beka Flavour ambaye ni moja ya zao la Yamoto Band, amesema kwamba baada ya kundi hilo kusambaratika hapati msaada wowote kutoka kwa wenzake kama ilivyokuwa awali.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Beka amesema kwenye kazi zake za sasa msanii mwenzake Aslay hajamsaidia kitu chochote, na hata yeye hajampa msaada wowote Aslay kwani kila mtu anapamba ili kuweza kusimama.
“Sijawahi kumuandikia nyimbo Aslay na wala yeye hajawahi kuniandikia, wala hajawahi kunisadia chochote, kila mtu anapambana na hali yake, ila mtu akiwa na kazi mpya tunasikilizishana, jana Aslay kanisikilizisha ngoma zake mbili ambazo hazijatoka”, amesema Beka Flavour.
Hivi karibuni Beka Flavour ameachia kazi mpya ambayo inajulikana kwa jina la 'Sarafina' na kuwa msanii wa pili kutoka Yamoto Band kuachia kazi mara kwa mara wakiwa kama 'Solo Artist'.

CCM Yaifanyia Kitu Mbaya Upinzani Yakamata Kata 42 Kati ya 43 za Uchaguzi wa Udiwani

$
0
0
CCM Yaifanyia Mbaya Upinzani Yakamata Kata 42 Kati ya 43 za Uchaguzi wa Udiwani
Chama cha mapinduzi CCM kimeibuka na ushindi katika kata 42 kati ya 43 zilizofanya uchaguzi mdogo wa udiwani jumapili ya Novemba 26 kwenye mikoa 19 nchini.

Hayo yamebainishwa leo na katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Ndugu Humphrey Polepole, wakati akitoa tathmini ya uchaguzi mbele ya waandishi wa habari kwenye ofisi ndogo ya makao makuu ya chama hicho Lumumba jijini Dar es salaam.
Polepole amesema kuwa Chama chake kimeibuka na ushindi huo katika kata hizo ikiwa ni matokeo ya kazi nzuri inayofanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya CCM.

Polepole ameitaja kata ambayo chama chake kimekosa ushindi kuwa ni Ibigi iliyopo wilayani Rungwe mkoani Mbeya ambayo imechukuliwa na mgombea wa CHADEMA. Aidha Polepole amedai kuwa chama kimeumia kwa kuikosa kata hiyo lakini kimekubali matokeo.
Kwa upande mwingine Polepole amezitaka mamlaka kushughulikia haraka baadhi ya dosari zilizojitokeza kwenye baadhi ya maeneo, ambayo chama hicho kimeripoti kutoridhishwa na mwenendo wa mchakato wa uchaguzi ikiwemo vitendo vya vurugu vilivyofanywa na watu wasiokuwa na nia njema.

Susan Kiwanga na Wengine 41 wakamatwa na Polisi, Lijuakali Asakwa

$
0
0
Susan Limwaga na Wengine 41 wakamatwa na Polisi, Lijuakali Asakwa
Polisi mkoani Morogoro inawashikilia watu 41 akiwemo mbunge wa Mlimba (Chadema), Susan Kiwanga.

Pia inawashikilia madiwani wawili, huku mbunge wa Kilombero (Chadema), Peter Lijualikali akitafutwa na jeshi hilo wakidaiwa kufanya fujo na kuchoma moto ofisi ya mtendaji baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Sofi wilayani Malinyi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Urlich Matei katika taarifa leo Jumatatu Novemba 27,2017 amesema tukio hilo lilitokea jana Jumapili Novemba 26,2017 saa tano usiku ambako walikwenda kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa udiwani.

Kamanda Matei amesema wabunge hao na madiwani wawili wa Chadema kutoka Ifakara walionekana kuhamasisha baadhi ya wafuasi wao kufanya vurugu.

Amesema watuhumiwa wanadaiwa kuchoma majengo ya umma ambayo ni ofisi shule ya msingi Sofi, nyumba ya walimu wa shule hiyo na ofisi ya mtendaji kata.

Kamanda Matei amesema fujo na uharibu huo ulitokea baada ya msimamizi wa uchaguzi kutangaza matokeo kuwa mgombea wa CCM ndiye alishinda kwa kupata kura 2,099.

Mgombea wa chama alipata kura 1,684 jambo lililopingwa na wafuasi wa chama hicho na kuanza  vurugu.

Amesema baada ya kuchoma majengo hayo kwa kutumia petroli, walidhamiria pia kwenda katika zahanati lakini askari waliwakamata.

Kamanda Matei amesema polisi inaendelea kuwatafuta watu wengine waliohusika na vurugu hizo, akiwemo mbunge Lijualikali.

Amesema watuhumiwa 41 wamepelekwa wilayani Ulanga kwa ajili ya kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Mbunge Lijualikali akizungumza na MCL Digital kwa simu kuhusu vurugu hizo amesema wakati matokeo yakitangazwa alikuwa Ifakara.

Amesema taarifa za kutafutwa na polisi ndiyo kwanza anazisikia kutoka kwa mwandishi wa habari wa MCL Digital.

 “Baada ya kumalizika kampeni Jumamosi nilirejea Ifakara kwa hiyo sijui chochote kuhusu hizo vurugu na nashangazwa kuhusishwa na tuhuma hizo, lakini kama kweli natafutwa nitakwenda kujisalimisha polisi,” amesema Lijualikali.

Kajala Aonyesha Umairi Wake wa Kumtega Shemeji Yake

$
0
0
Kajala Aonyesha Umairi Wake wa Kumtega Shemeji Yake
Video mpya ya 'Omulilo' ambayo ni kazi yake mwanamama Saida Karoli imeachiwa rasmi, huku Kajala akiigiza muhusika aliyeimbwa kwenye wimbo huo.

Video hiyo inamuonyesha Kajala akiwa anaishi kwa shoga yake kipenzi, lakini licha ya kumsitiri anafanya kitendo kibaya cha kumtaka shemeji yake kimapenzi kwa kumtega kwa kumvalia mavazi ya kumshawishi.
Kazi hiyo ambayo imefanywa na mikono ya Hanscana, ni moja ya kazi zilizoachiwa hivi karibuni na Saida karoli tangu arudi rasmi kwenye game, baada ya kishindo cha wimbo wa 'Orugambo'.

Tanesco Yaanza Kubomoa Sehemu ya Jengo Lake

$
0
0
Tanesco Yaanza Kubomoa Sehemu ya Jengo Lake
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeanza hatua ya ubomoaji kwenye sehemu ya jengo lake kama utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli  alilotoa mwanzoni mwa mwezi huu ili kupisha ujenzi wa daraja la juu la ubungo.

“Uongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) unawafahamisha Wateja wake wote na Wananchi kwa ujumla kuwa TANESCO imeanza utekelezaji wa  Agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Joseph Magufuli, kuhusu kubomolewa  kwa Jengo la Ofisi za TANESCO Makao Makuu, liliopo Ubungo Jijini Dar es salam. Kuanzia Jumatatu Novemba 27, 2017. Ukuta wa mbele ya jengo umesha vunjwa, pia  baadhi ya Watumishi wa Shirika wameanza kuhamishiwa katika ofisi nyingine za TANESCO zilizopo jijini Dar es salaam ili kupisha shughuli za ubomoaji kufanyika kwa usalama  zaidi. Uongozi wa Shirika   pamoja na Wakala wa Majengo TBA wanaendelea kufanya taratibu zitakazo wezesha zoezi la ubomoaji wa Jengo kufanyika bila kuathiri huduma kwa Wateja wa Shirika. Katika kipindi hiki cha utekelezaji wa Agizo la Mheshimiwa Rais. Tunapenda kuwahakikishia Wateja wetu na Watanzania wote kwa ujumla kuwa Huduma za Umeme zitaendelea kupatikana kama kawaida ikiwemo huduma ya manunuzi ya LUKU. Uongozi wa Shirika utaendelea kutoa taarifa kwa kadri zoezi hili linavyo endelea.”

Mapema mwezi huu Rais Dkt John Pombe Magufuli wakati akikagua ujenzi wa daraja la ghorofa tatu barabara ya Ubungo, aliamuru sehemu ya jengo la TANESCO na jengo la Idara ya maji kwenye eneo la barabara kuvunjwa ili kupisha ujenzi huo.
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live




Latest Images