Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Ben Pol Amjibu TID " Amenikosea Heshima Amnitake Radhi"

$
0
0
Ben Pol Amjibu TID " Amenikosea Heshima Amnitake Radhi"
Unalikumbuka povu la msanii mkongwe wa muziki, TID juu ya Ben Pol baada ya muimbaji huyo wa R&B kutumia kiitiko cha wimbo ‘Nyota Yangu’ cha muimbaji huyo kwenye show yake ndani ya Tamasha la Fiesta? Sasa Ben Pol amejibu mapigo tena kwa kumtaka mkongwe huyo wa muziki kumtaka radhi kutokana na kauli yake.

Jumatatu hii TID alikiambia kituo cha radio cha EA kuwa atazungumza na wakubwa wake pamoja na wanasheria wake ili kumchukulia hatua Ben Pol.

IGP Sirro Kupeleka Magari Mawili uya Polisi Pwani

$
0
0
IGP Sirro Kupeleka Magari Mawili uya Polisi Pwan
Inspekta Jenerali was Polisi IGP Simon Sirro akipokea salaam ya heshima kutoka kwa askari was Mkoa wa Pwani mara baada ya kuwasili Mkoani humo kwa ziara ya kikazi. IGP amewataka askari wa Mkoa wa Pwani kutoa huduma bora na kuendelea kuimarisha nidhamu ili wananchi waendelee kuwa na imani na Jeshi la Polisi.

Inspekta Jenerali wa Polisi, IGP Simon Sirro akikagua baadhi ya askari wa Mkoa wa Pwani mara baada ya kuwasili Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Sirro akikagua baadhi askari wa Mkoa wa Pwani mara baada ya kuwasili Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Sirro akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Eng, Evaristi Ndikilo alipowasili Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.
IKIWA ni siku chache baada ya Rais John Magufuli kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini ya dar es Salaam na kukagua magari ya polisi ambayo yaliingizwa nchini mwaka 2015, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro amesema kwamba magari mawili atayapeleka mkoani Pwani.
Rais Magufuli alibaini ukwepo kwa magari zaidi ya 50 yakiwa bado yanaendelea kubaki eneo la bandari huku ikielezwa kuwa ni ya Jeshi la Polisi na mengine ni ya Ofisi ya Rais ambapo alimwagiza IGP kuhakikisha anayakagua magari hayo na kuyatoa bandarini ili yakafanye kazi iliyokusudiwa.
“Kwa nini magari yanakuja hapa yanakaa miaka 10, wakati sheria inasema ni siku 21? alihoji Rais Magufuli.
Baada ya siku moja Sirro alitembelea bandarini hapo kuyakagua magari hayo na jana akiwa Kibaha, Pwani alisema anatarajia kutoa magari mawili ya polisi Mkoa wa Pwani ili kupunguza changamoto ya uhaba wa vyombo vya usafiri kwa askari.
“Hayo magari ni ya Jeshi la Polisi na mawili kati ya hayo natarajia kuwapa polisi Mkoa wa Pwani,” alifafanua alipokuwa kwenye ziara ya kikazi.
Sirro alisema kuimarika kwa hali ya usalama kwenye maeneo ya Kibiti, Ikwiriri na Rufiji kumetokana na ushirikiano uliofanyika baina ya jeshi hilo na wananchi wenye nia njema.
“Silaha zote ambazo wahalifu walikuwa wamezipora kwenye matukio mbalimbali wakati hali ikiwa mbaya kule Kibiti, tayari tumeshazipata zote na hali imeshaimarika vizuri hivyo napenda kuwaambia wananchi wote hivi sasa hali ni shwari,” alisema.
Aidha IGP aliwataka askari wa Mkoa wa Pwani kutoa huduma bora na kuendelea kuimarisha nidhamu ili wananchi waendelee kuwa na imani na Jeshi la Polisi.
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo aliishukuru Serikali kwa kuanzisha Mkoa wa kipolisi Rufiji akisema hali hiyo imesaidia kuimarisha usalama ndani ya Mkoa wa Pwani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shanna alisema ziara hiyo imeamsha ari ya utendaji kazi kwa askari wake na kuahidi kuyafanyia kazi maagizo yote yaliyotolewa kwake.

Mwanamke wa 73 Afungua Kesi Mahakamani Kudai Talaka kwa Mumewe

$
0
0
Mwanamke wa 73  Afungua Kesi Mahakamani Kudai Talaka kwa Mumewe
MWANAMKE ambaye yupo kwenye ndoa kwa miaka 55, amefungua kesi mahakamani kuomba mumewe ampe talaka kwa madai kuwa hamjali, na anamthamini zaidi mke mdogo.

Mwalimu huyo mstaafu, Marcella Mukami Kinyugo (73), anaiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kangema, isitishe ndoa yake na Peter Kinyugo (76) iliyofungwa Septemba 16, 1962 katika Kanisa Katoliki Kiriaini.

Bibi huyo mkazi wa mjini Kiria-ini, Mathioya, kwenye kaunti ya Murang’a, pia aliomba apewe nusu ya mali za familia yao na pia mumewe alazimishwe kulipa gharama za kesi. Katika kesi hiyo bibi huyo aliwakilishwa na Margret Nyangati kutoka kampuni ya mawakili ya Muchoki Kang’ata.

Aliieleza Mahakama kuwa, waliishi maisha ya furaha ya mume na mke tangu walipofunga ndoa, lakini miaka sita iliyopita hali ilibadilika wakati mumewe alipoacha kutimiza majukumu yake kama mume.

Mume wa bibi huyo ni mwalimu mstaafu na Chifu. Mukami alidai mahakamani kuwa matatizo yalianza baada ya Kinyugo kukaa kwa mke mdogo kwa wiki kadhaa bila kwenda kwake, na kwamba, yeye na mke mwenzake wanaishi kwenye eneo moja. Kwa mujibu wa bibi huyo, wakati mumewe anafanya hivyo, hawakuwa na ugomvi.
Chanzo; Habari Leo

Gigy Money Afunguka Chanzo cha Mwili Wake Kupukutika

$
0
0
Gigy Money Afunguka Mwili Wake Kupukutika
MWANAMUZIKI na muuza sura kwenye video mbalimbali za wasanii wa muziki wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ameeleza kuwa unene aliokuwa nao awali ulikuwa ni wa utoto hivyo kukonda kwake kwa sasa ni utu uzima.
Akizungumza na Za Motomoto News, Gigy Money alisema watu wanamsema kwa kukondeana kwake lakini anachoweza kusema ni kwamba unene wa zamani ulitokana na mwili wa kitoto lakini hivi sasa amekua mtu mzima.

Akifanya yake kwenye shoo yake Mbeya.
“Katika familia yetu hakuna mtu mnene hata mmoja, wote ni wembamba hivyo ule mwili niliokuwa nao awali ulikuwa ni wa utoto lakini sasa hivi nimekua ndiyo maana nimepukutika na siyo vinginevyo kama watu wanavyonishambulia kwa maneno mabaya,” alisema Gigy Money.

Zari Aliamsha Dude Amnanga mzazi mwenzake.

$
0
0
Mipasho! Mwanamitindo mjasiriamali, Zarinah Hassan ‘Zari The BossyLady’ ambaye aliingia katika mtafaruku wa maisha yake ya kimapenzi, kwa mara nyingine juzikati alionyesha kuwepo kwa kutoelewana kwao baada ya kuliamsha dude kwa kutoa maneno ya kumnanga mzazi mwenzake.

Awali, vyanzo vyetu vilivyo karibu na mrembo huyo mwenye watoto watano, alisema kwa sasa hana uhusiano mzuri na baba wa watoto wake wawili, kwa kile kinachosemwa kuwa ni kitendo cha mwenzake huyo kuendekeza mapenzi na wanawake wengine.

“Ni kama mchezo unaelekea mwishoni hivi sasa, maana maneno na ugomvi kati yao hauishi, jamaa anafanya kazi kubwa kuficha kuhusu huu uhusiano wake kuwa juu ya mawe, lakini ukweli ni kwamba hakuna dalili za wawili hawa kukaa tena imara kama zamani,” kilisema chanzo hicho.

Katika tukio la hivi karibuni, mwanamama huyo aliandika katika mtandao wake maneno yenye kumlenga mzazi mwenzake, akisema anaendekeza wanawake na watoto wengi na kwamba badala ya kuona anauza kazi zake nyingi za muziki, yeye amekuwa hodari wa eneo ambalo hahusiki.

Katika kumnanga huko, Zari alisema endapo mtu anatafuta ubalozi wa kondom, ambacho ni kifaa cha kinga dhidi ya magonjwa ya kuambukizwa kupitia ufanyaji mapenzi, basi hana haja ya kuhangaika kumpata, kwa kuwa tayari mtu.
Chanzo: Global Publishers

Dkt Shika Amzimia Ray C Asema Ajiwezi

$
0
0
Dkt Shika Amzimia Ray C Asema Ajiwezi
DAKTARI Louis Shika ambaye alipata umaarufu mkubwa baada ya jaribio lake la kununua nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi, ametoa mpya baada ya kudai kuwa anaguswa na muziki wa mkongwe Rehema Chalamila ‘Ray C’.

Akipiga stori na Risasi Mchanganyiko juzikati, Dr Shika alisema katika Tanzania, hakuna msanii yeyote wa Bongo Fleva ambaye anamhusudu zaidi ya mwimbaji huyo anayesifika kwa kuimba na kucheza.

Punguza Unene na Kutibu Magonjwa Kwa Kutumia Dawa za Edmark...Bonyeza Hapa

$
0
0

TUNA DAWA AMBAZO NI VIRUTUBISHO NA CHAKULA MBADALA ZIMEHAKIKIWA NA TFDA

Ni uhakika kwa afya yako, kupunguza uzito na Sumu mwilini, Mafuta/Sehemu Mbaya, Kitambi na Nyama Uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali yaliyoshindikana

Loose Weight Trainer ni Msaada wako Wasiliana Nasi Kwa WhatsApp 0713 777 470

Upate Suluhisho la Afya yako Bila Madhara
👉@looseweight_trainer

Mwanamke Mwenzangu, Usigombane na Mwanamke Mwenzako Kisa ni Mchepuko wa Mume Wako

$
0
0
Mimi kuna kitu huwa siwezi kabisa kukifanya, nimkute mwanaume wangu na mwanamke mwingine, sitomfanya chochote kabisa.

Kwani yeye amefwatwa kama mimi alivyonifata akanitongoza tu.Sasa iweje nianze kupigizana kelele na mwanamke mwenzangu.

Nitakachofanya ni kupambana na mwanaume tu. Yeye ndo atakuwa haniheshimu mpaka anaenda kumfata mwanamke mwingine.

Utakuta mwanamke anapigizana makelele na mchepuko wa mume wake, utafikiri alimfata mume wako akamwambia naomba unifanye mchepuko.

Pambana na mume wako.Mimi kuna mwanamke alinifata nilikuwa simfahamu kabisa na wala sijawahi kutembea na mume wa mtu.

Nilitukanwa matusi mazito mpaka nikashangaa, aliniudhi sana. Nikakaa nikafikiria nimfanyaje ili aumie. Nikamwambia, kwa vile nimekujibu kistaarabu mimi sitembei na mume wako ukanitukana, sasa basi ndo mda wa kumkubalia rasmi, maana alikuwa ananitongozaga mda tu.

Na ahadi alizoniahidi ngoja nikubali azitekeleze. Baada ya kusoma SMS, alipiga simu anaomba msamaha na maneno kibao. Alichoambulia ni too late na block juu. Alihaha kupiga na simu nyingine mpaka alichoka. Huku namcheka tu.

By Super women 2


Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE..

Korea Kaskazini: Tunaweza Kushambulia Eneo Lolote Marekani

$
0
0
Korea Kaskazini: Tunaweza Kushambulia Eneo Lolote Marekani
Korea Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kulifanyia majaribio kombora lake la masafa marefu ambalo linaweza kufika eneo lolote la Marekani.
Runinga ya kitaifa nchini humo imesema kuwa Pyongyang sasa imefanikiwa kuafikia azimio lake la kuwa taifa lenye nguvu za kinyuklia.
Kombora hilo kwa jina Hwasong-15 ambalo imesema ndio kombora lenye uwezo mkubwa lilirushwa katika giza mapema siku ya Jumatano.
Lilianguka katika maji ya Japan lakini liliweza kuruka juu zaidi ya kombora jingine lolote la taifa hilo .
Marekani yatishia kuiadhibu Korea Kaskazini
Kombora la Korea Kaskazini lashindwa kupaa
Marekani: Korea Kaskazini ilikusudia uchokozi
Kitengo cha habari cha taifa hilo KCNA kilisema kuwa kombora hilo liliruka katika kimo cha kilomita 4,475 na kusafiri kwa umbali wa kilomita 950 katika dakika 53.
Kombora hilo lililofyatuliwa kwa mwinuko halikupitia katika anga ya Japan kama makombora mengine hapo awali na lilianguka kilomita 250 karibu na pwani yake ya kaskazini , kulingana na maafisa wa Japan.
KCNA imeongezea kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ambaye alishuhudia kufyatuliwa kwa kombora hilo alitangaza 'kwa majivuno' kwamba sasa tumekamilisha lengo letu la miaka mingi la kuwa taifa lenye nguvu za kinyuklia.
Ripoti hiyo imesema kuwa kama taifa lenye nguvu za kinyuklia na linalopenda amani, Korea Kaskazini itafanya kila iwezalo kutekeleza lengo lake la kuleta amani na udhabiti duniani.
Imesema kuwa, silaha zake za ulinzi dhidi ya sera ya kibepari ya Marekani, hazitatishia taifa lolote duniani iwapo maslahi ya Korea Kaskazini hayatakiukwa.''Hilo ndio tangazo letu''

Mabasi ya Mwendokasi Kupanua Wigo Sasa Hadi Sinza, Masaki

$
0
0
Mabasi ya Mwendokasi Kupanua Wigo Sasa Hadi Sinza, Masaki
WAKALA wa  Mabasi Yaendayo Haraka (DART) unatarajia kupanua wigo wa usafiri huo kwa kuongeza ruti za Sinza, masaki na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Sambamba na ruti hizo, DART pia inatrajia kuongeza mabasi katika mfumo wake kutoka 140 yaliyopo sasa hadi mabasi 305 pindi awamu ya kwanza ya mfumo huo itakapokamilika.

Mtendaji Mkuu wa DART, Mhandisi Ronald Lwakatare, alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kupokea wageni sita kutoka serikali ya Rwanda ambao wako nchini kwa ziara ya siku tano ya kujifunza mradi huo unavyofanya kazi nchini.

“Tunatarajia kuwa hatua ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi huu, itaongeza idadi ya watumiaji wa mabasi ya mfumo huo kutoka 200,000 kwa siku   kufikia watumiaji 400,000 hadi 500,000 kwa siku,” alisema.

Mhandisi Lwakatare alisema mradi huo utaongeza njia  kutoka mbili zilizopo sasa hadi njia  tisa, hivyo kupanua huduma ya usafiri katika maeneo mbalimbali yaliyomo ndani ya mfumo wa DART katika awamu ya kwanza ya mradi.

“Awamu ikikamilika tutakuwa na njia tisa, kuna nyingine zitakuwa zinaenda Masaki, Sinza, Chuo Kikuu na maeneo mengine ambayo yako jirani,” alisema.

Kuhusu athari zilizotokana na mvua zilizonyesha Oktoba 26,  mwaka huu, Mhandisi Lwakatare alisema mfumo wa mabasi uliathiriwa na mvua hizo na mabasi 40  yaliharibika na kati ya hayo 20  yaliharibika zaidi.

Hata hivyo, alisema mabasi hayo  yameshatengenezwa na yameanza kutoa huduma na kwamba wamejipana kuhakikisha mitaro yote inayozunguka karakana ya Jangwani inasafishwa ili kuepuka eneo hilo kukumbwa tena na mafuriko.

“Tumefarijika kupokea ugeni kutoka serikali ya Rwanda kuja kutembelea mradi kwa lengo la kujifunza hatua tuliyofikia ukizingatia kuwa jiji la Kigali nalo lina mpango wa kuwa na mfumo kama huu,” alisema.

Timu hiyo inaongozwa na Rwagatore Etienne kutoka Mamlaka ya Jiji la Kigali akiwa na wataalamu washauri ambao ndio waliopewa kazi ya usanifu wa jiji la Kigali kuwa na mfumo wake wa mabasi yaendayo haraka.




Mastaa Walia na Utumwa Unaoendelea Nchini Libya

$
0
0
Mastaa Walia na Utumwa Unaoendelea Nchini Libya
Wakati kukiwa na taarifa za kurejea kwa biashara ya utumwa nchini Libya, wasanii mbali mbali wakubwa duniani wameonyesha kuumizwa na biashara hiyo.

Miongoni mwa wasanii hao ni pamoja na Chris Brown, T.I, Omotola, Peter wa kundi la P Square.

Kwa upande wa wasanii na watu maharufu wa kutoka bongo a,mbao wameonekana nkuguswa na utumwa unaosadikika kurudi uko libya ni pamoja  na Vanessa, Mdee Jay Dee, Aslay, Babu Tale, Eric Shigongo na wengine wengi ambapo wameambatanisha na maneno mbalimbaliu ambayo yanaonyesha kuguswa kwao ikiwemo kinachoendelea Libya si cha kufumbiwa macho.

 Hapa tumekuwekea kile walichokiandika kupitia kurasa wa zao za mtandao wa Instagram.





Mama Wema Sepetu Atua Nairobi Kumjulia Hali Tundu Lissu

$
0
0
Mama Wema Atua Nairobi Kumjulia Hali Tundu Lissu
Mama Mzazi wa msanii wa filamu Bongo na Mkurugenzi wa Endless Fame, Wema Sepetu wameenda Nairobi nchini Kenya kumjulia hali mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Lissu ambaye anapata matibabu nchini huyo.

Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amekuwa akitibiwa Nairobi tangu aliposhambuliwa kwa kupigwa risasi September mwaka huu. Viongozi mbali mbali wa kiserikali na wa chama hicho wamekuwa wakienda kumjulia hali na sasa Mama wa Wema Sepetu ameonekana kufanya hivyo.

Hapo jana Makamu wa Rais Mhe. Mama Samia Suluu alimtembelea pia Lissu hospitalini hapo. Utakumbuka Mama Wema pamoja na wanaye February 24 mwaka huu walitangaza kujiunga na Chadema.

RC Makalla Kuandika Barua Kumuomba Radhi Magufuli

$
0
0
RC Makala Kuandika Barua Kumuomba Radhi Magufuli
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amesema ataandika barua kwa mwenyekiti wa CCM Taifa na katibu mkuu wa chama hicho kuomba radhi kwa kushindwa kupata ushindi katika Kata ya Ibighi.

Kauli hiyo ya Makalla imekuja baada ya Chadema kupitia kwa mgombea wake, Lusubilo Simba kushinda kiti hicho kwa kupata kura 1,449 wakati Suma Fyandomo wa CCM alipata kura 1,205 kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika Jumapili.

“Nitaandika barua ya kukiomba radhi chama changu kwa katibu mkuu na mwenyekiti wake, lakini hapa ni lazima tujiulize ni kwa nini Mbeya,” alisema Makalla.

Makalla alisema hayo jana wakati akitoa salamu zake kwenye mkutano mkuu wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) Mkoa wa Mbeya ambao ulikuwa ni wa uchaguzi wa viongozi wa UWT ngazi ya mkoa akiwa kama msimamizi mkuu wa uchaguzi huo.

Makalla alisema kitendo cha CCM kushindwa katika uchaguzi kimeutia doa mkoa wa Mbeya na viongozi wa CCM mkoa huo wanapaswa kujitafakari upya kwa kilichotokea.

“Niseme tu hapa nimekuja tu kwenye mkutano huu kwa vile ni msimamizi mkuu wa uchaguzi huu, lakini ukweli hapa nilipo ninaumwa na jana (juzi) nilishindwa kufika kazini. Homa yenyewe inatokana na matokeo ya Kata ya Ibighi. Ni aibu kubwa kwa CCM mkoa wa Mbeya, tusidanganye hapa ni fedheha kata zote 43, halafu kata 42 zote zipo CCM na moja ndio imekwenda huko nayo ipo Mbeya,” alilalamika Makalla.

Kwa upande wake, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson alisema hali ndani ya chama hicho mkoani hapa si nzuri kutokana na kitendo cha kushindwa kunyakua kata hiyo.

“Hali si nzuri kabisa wala tusifarijiane hapa, haiwezekani mkoa mzima una kata moja ya uchaguzi, halafu nayo tukapoteza. Ni bora hii kata moja ambayo CCM imepoteza ingekuwa kata nyingine lakini si Mbeya, hii inaonyesha kuna kazi ya kufanya,” alisema.

Dk Tulia alisema kupitia uchaguzi huo ni muda mwafaka wa kujitathmini na kuhakikisha wanarejesha imani kwa wananchi wa Mbeya na si vinginevyo, huku akibainisha kwamba si bure watu wakafanya uamuzi wa tofauti wakati wanatambua fika CCM ndio iliyoshika dola.

Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Mbeya, Mary Mwanjelwa alisema kwamba baada ya chaguzi zote ndani ya CCM kufanyika kimkoa ataanza kufanya kazi ya kuzunguka wilaya zote.

Alichokisema Ridhiwani Kikwete Baada ya Mama Samia Kumtembelea Tundu Lissu Hospitali

$
0
0
Alichokisema Ridhiwan Kikwete Baada ya Mama Samia Kumtembelea Tundu Lissu Hospitali
Mbunge wa Chalinze kupitia CCM ambaye pia ni mtoto wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete, ameonehsa kuguswa na kutoa yake ya moyoni baada ya Makamu wa Rais mama Samia Suluhu kwenda kumuona Tundu Lissu hospitali.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Ridhiwani Kikwete ameandika ujumbe akisema kuwa Mama Samia ameonesha kuguswa kama mzazi kwa kitendo alichokifanya cha kwenda kumuona mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antiphas Lissu.
"Sura yake Makamu wa Rais Mama Samiah Hassan inaonyesha kuguswa kama Mzazi. Wewe ni mzazi na Mungu aibariki Tanzania", ameandika Ridhiwani.
Hapo jana Makamu wa Rais mama Samia Suluhu alikwenda hospitali hapo kumuona Tundu Lissu ambaye amelzwa tangu Septemba 7 mwaka huu, baada ya kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya


Viongozi wa CUF ya Lipumba Hapatoshi Waanza Kushikana Uchawi

$
0
0
Viongozi wa CUF ya Lipumba Hapatoshi Waanza Kushikana Uchawi
Viongozi wa (CUF) chini ya Katibu Mkuu na Lipumba wameanza kutupiana lawama na kushikana uchawi, Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF Mbarala Maharagande amefunguka na kusema Maalim Seif analindwa na haki na si ushirikina.

Mbarala Maharagande amedai kuwa Lipumba na kundi lake ni watu ambao wanaamini sana ushirikina na kutegemea ushirikina kufanikisha mpamgo wao kuivuruga na kuisambaratisha Taasisi ya CUF.
"Lipumba na wafuasi wake ni watu wanaoamini sana mambo ya ushirikina katika kufanikiwa mipango yao michafu dhidi ya Taasisi ya CUF. Mara kadhaa wameonekana kutumwa wafuasi wake kwenda kununua Mbuzi kwa ajili ya kazi hiyo katika mnada wa Vingunguti. Kamati ya ushirikina inaongozwa na Abdul Kambaya na Hamisi Hassan kwa upande wa Tanzania Bara na Mohamed Thiney na Nassor Seif kwa upande wa Zanzibar" aliandika Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF Mbarala Maharagande
Mbali na hilo Mbarala amesema kuwa Profesa Lipumba na kundi lake wameshindwa kuigawa CUF kama ambavyo walikuwa wakitegemea na kudai uchaguzi mdogo wa udiwani umeweza kutoa majibu kwani wagombea wote wa Lipumba wamepata kura chache sana na kuonekana wazi kuwa watu hao hawakubaliki katika jamii.
"Lipumba na wafuasi wake wameshindwa kuigawa CUF na mbeleko ya CCM inakaribia kukatika kutokana na kutoona faida yao hasa katika ushindani wakati wa uchaguzi. Watazania washawafahamu kuwa ni vibaraka, wasaliti na wachumia tumbo, hawapo kwa dhati ya kutaka Mabadiliko ya kweli kisiasa kutokea hapa nchini. Mgombea wa Lipumba katika Kata ya Reli, Mtwara Mikindani kushika nafasi ya nne kwa kupata kura 21 baada ya CCM, CHADEMA, na ACT katika Jimbo linaloongozwa na Mbunge kutoka ‘CUF MAKINIKIA’ ni salamu tosha kwa Maftaha Nachuma na Lipumba kuwa hawakubaliki na hawana mchango wa maana kwa CCM" alisisitiza Mbarala
Pia Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF Mbarala Maharagande amekanusha taarifa inayosema kuwa Maalim Seif anashirikiana na waganga wa kienyeji na kuwa mambo yamezidi kuwa magumu kwake.
"Eti Maalim Seif anashirikiana na Waganga na mambo yanazidi kuwa magumu kwake! Mambo yepi magumu na Spika anatakiwa atangaze rasmi lini Wabunge halali wa CUF waanze utumishi wao Bungeni kutokana na maamuzi ya Mahakama. Msemaji wa Lipumba, David Maphone kahamia kuwapigia kampeni wagombea wa UVCCM sasa"

Natamani Kufanya Kazi na Ali Kiba Katika Ujio Wangu Mpya- Sister P

$
0
0
Natamani Kufanya Kazi na Ali Kiba Katika Ujio Wangu Mpya- Sister P
Msanii mkongwe kwenye bongo fleva, Sister P ambaye amewahi kutamba kwa ngoma kama, Anakuja,  Hey Dj na zingine amefunguka na kusema kuwa katika ujio wake mpya kwenye muziki anatamani kufanya kazi na mfalme Alikiba kwani anaamini watafanya kazi kubwa.

Sister P amesema hayo leo alipokuwa akipiga stori na mwandishi wa tovuti ya EATV na kudai kuwa akifanya kazi na Alikiba lazima itakuwa kazi kubwa na bora zaidi sababu watakuwa wamekutana wanamuziki na si wasanii.
"Kwa sasa nimejipanga vya kutosha kwa ajili ya kuanza mashambulizi mwakani mwezi wa kwanza, kuna ngoma nyingi ndani nimefanya na mtayarishaji mpya kwenye muziki anaitwa Banny Music chini ya Big Sound studio, lakini kiu yangu kubwa kufanya kazi moja na Alikiba kwani naamini itakuwa kazi kubwa zaidi sababu tutakuwa tumekutana wanamuziki na siyo wasanii" alisisitiza Sister P

Sister P ambaye hivi sasa muonekano wake umebadilika tofauti na zamani ameahidi kuwashangaza Watanzania kwa kazi zake mpya na kusema anaamini kuwa atarudi kwenye nafasi yake licha ya kukaa kimya kitambo kwenye muziki.

Eto'o Afunguka Kuhusu Kutoa Fedha kwa Waliyokwama Libya Wakiuzwa Kama Watumwa

$
0
0
Etoo Afunguka Kuhusu Kutoa Fedha kwa Waliyokwama Libya Wakiuzwa Kama Watumwa
Nahodha wazamani wa timu ya taifa ya Cameroon na mshambuliaji wa FC Barceloma, Samuel Eto’o amekanusha tuhuma za kuwapatia fedha raia wa nchi hiyo ambao walikuwa wamekwama Libya na kuelezwa kuwa wamekuwa wakiuzwa kama watumwa.

Kupitia mitandao yake ya kijamii ya Instagram na Facebook Eto’o amekanusha vikali juu ya tuhuma hizo na kuwasihi watu kuonyesha upendo zaidi kwakuwa ndiyo kitu pekee kinachoweza kupambana na maovu na wala sio fedha.

“Several sites have circulated a rumor that I would have given money to every migrant returnee, in relation to a topical issue. This rumor is absolutely unfounded!”

“I would therefore take advantage of this opportunity, dear brothers and sisters, to emphasize that love prevents more evils than money can solve.”

“So let’s not waste our precious time looking for thrills at the expense of grieving people, but let us use this time to prevent other brothers from being deprived of their dignity.”

“Let us not just react when we can prevent, because among these victims are certainly people who have been our neighbours at some point, but to whom we have not daigné to look kindly. Let us build our Africa by having a positive impact on each other!.”

Uchambuzi wa Wimbo Mpya wa Diamond Platnumz Unaitwa Sikomi

$
0
0
UCHAMBUZI WA WIMBO
JINA LA WIMBO: SIKOMI
MSANII : DIAMOND PLATNUMZ

UTANGULIZI

Diamond Platnumz ni msanii wa muziki wa kizazi kipya (bongofleva) kutoka Tanzania. Anaiwakilisha nchi yake na fasihi ya kiswahili nje na ndani ya nchi kwa ufanisi. Wimbo wake mpya wa Sikomi ni mojawapo ya nyimbo zake nyingi ambazo amepata kuziimba tangu alipoanza mziki wake. Ufuatao ni uchambuzi wa wimbo wa Sikomi. Angalizo uchambuzi huu utajikita zaidi kwenye vipengele vya maudhui na wala mhakiki hajagusa vipengele vya fani.

DHAMIRA KUU
Dhamira kuu katika wimbo wa Sikomi ni mapenzi. Msanii anaeleza historia yake ya kimahusiano toka alipotoka kimuziki mpaka hapa alipofika. Amegusia visa na mikasa aliyopitia katika mahusiano yake ya kimapenzi. Msanii amepitia katika mengi katika mapenzi lakini bado haachi kujihusisha na mapenzi huu ndiyo msingi wa jina la wimbo "Sikomi". Msanii anasema kila anapoumizwa na mwanamke mmoja anatafuta mwanamke mwingine wa kumfuta machozi.

DHAMIRA NDOGO NDOGO

USALITI KATIKA MAPENZI

Msanii anaeleza jinsi alivyosalitiwa na wanawake aliowapitia msanii anasema " aliyonifanyia wa sentro siwezi Sema... ndiyo maana sikushangaa ile ghafla toka CCM kwenda CHADEMA"
Msanii anaeleza jinsi alivyoumizwa na usaliti katika mapenzi. Msanii anasema mara baada ya kutoka kimuziki alivamia tasnia ya bongo movie ambapo alisalitiwa sana.

Msanii anaeleza jinsi alivyosalitiwa na Penny aliyedai ana ujauzito wake hali iliyompelekea kumhonga gari mpenzi wake huyo ambaye mwisho wa siku alikuja kumsaliti. Msanii anasema ameshafumania na kufumaniwa pia katika mapenzi hii ni kielelezo cha usaliti katika mapenzi kwenye kazi ya msanii.

MIGOGORO
Msanii amesadifu yale yanayotokea katika jamii kwa kuonesha migogoro mbalimbali kwa kutumia wahusika katika wimbo wake baadhi ya migogoro ni hii ifuatayo;

Mgogoro wa msanii na mama yake

Mgogoro wa nafsi wa msanii kuhusu kuachana na mapenzi au kuendelea.

Mgogoro wa msanii na Esma kuhusu kuachana na mapenzi ni baada ya Esma kumwambia msanii mapenzi basi msanii hakutaka kusikia.

Mgogoro wa msanii na Zari. Msanii anasema richa ya Zari kumzalia watoto wawili wa kiume na wa kike lakini bado alimsaliti.

Mgogoro wa Msanii na wa Sentro na mgogoro wa msanii na wa sentro.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA JAMII

Msanii amemchora mwanamke kama mzazi na mlezi mfano ni mama yake na msanii na Zari.

Msanii amemchora mwanamke kama mshauri mzuri mfano ni mama yake na msanii na Esma.

Mwanamke kama mtu mwenye mapenzi ya dhati mfano Zari aliyempenda msanii mpaka kumzalia watoto wawili, mama yake msanii na Esma.

Msanii amemchora mwanamke kama mtu aliyekosa msimamo na msaliti, mfano wa Sentro na Penny.

KUFANIKIWA KWA MSANII KIMAUDHUI

Msanii ameweza kusawiri ipasavyo mambo yanayotokea katika jamii ya kitanzania na hasa katika ulimwengu wa mapenzi.

UDHAIFU WA MSANII
Msanii amekuja na hitimisho jumuishi kuwa wasanii wa sinema (bongo movie) siyo wa kuaminiwa jambo ambalo siyo la kweli kwenye uhalisia kwani kuna wasanii wengi wa tasnia ya filamu wanajiheshimu na wengine ni watu wazima wenye kujiheshimu pia na kuaminika na jamii.

Je mama Samia Amefungua Milango ya Kwenda Kumtazama Tundu Lissu Hospitalini?

$
0
0
Siku ya jana ilikuwa ya kipekee sana baada ya Makamu wa Rais, Samia Hassan kuamua kumtembelea hospitalini Nairobi kwenda kumpa pole, mbunge huyo wa Singida Mashariki, baada ya kupigwa risasi zaidi ya 30, mchana kweupe, zaidi ya miezi 2 na nusu iliyopita.

Nimesema ni tukio la kihistoria kwa kuwa huyo ni kiongozi wa kwanza wa juu, kutoka Chama Cha Mapinduzi kwenda kumtembelea Tundu Lissu.

Tanzania ya sasa tumejenga utaratibu mpya, ambapo janga kama limekukuta mtu wa upinzani, inakuwa kama hairuhusiwi kwa viongozi wa upande
wa CCM kwenda kumuona, na ukienda kumwona utahesabika ndani ya Chama chako kama msaliti!

Tulishuhudia wakati mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema alipokuwa rumande kwa miezi 4 mfululizo ambapo hakuna kiongozi yeyote kutoka CCM aliyekwenda kumwangalia gerezani Kisongo.

Najua kibinadamu wapo wanaccm wengi wanaumia sana kwa yaliyomkuta Tundu Lissu, lakini kwa msimamo wa Chama chao, wanahofia kwenda kumwona Tundu Lissu, kwa kile kinachoonekana kuwa wataitwa wasaliti!

Kwa kweli siyo utamaduni wa mtanzania, kubaguana kiasi hiki, kwa janga linalokukuta mtu wa upinzani iwe ni "marufuku" kwa kiongozi kutoka Chama Cha Mapindizi kwenda kumfariji.

Ndiyo maana nimesema, je kutokana na Makamu wa Rais, Samia Suluhu kwenda kumwona Tundu Lissu, atakuwa amefungua njia kwa viongozi wenzake wa CCM kwenda kumwona Tundu Lissu hospitalini Nairobi?
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images