Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Katika Kutimiza Miaka 20 ya ndoa yao, Lissu Ampa Ujumbe Mzito Mkewe

0
0
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu leo ametimiza miaka 20 ya ndoa akiwa bado hospitalini Nairobi akijiuguza  ambapo pia amemshukuru mke wake Alicia na kusema kwamba ni mke ambaye anaishi katika kiapo cha siku walichofunga ndoa.

Kwa mujibu wa Diwani wa Sombetini-Arusha, Ally Bananga amesema kwamba Mh Lissu amemtaja Alicia kama kipande chake sahihi kwa upande wake.

"Leo Tundu Lissu na mkewe Alicia wametimiza miaka 20 ya ndoa yao. Mume yuko kitandani na mke amebaki pembeni yake kumuhudumia. Ndoa yenye baraka hii,  na Mh Lissu amemtaja Alicia kama kipande chake sahihi"  Bananga.

Aidha Diwani Bananga ameongeza kwamba "Lissu amesema mkewe anakiishi kiapo chao siku walipofunga ndoa kuwa watayakabili maumivu na vikwazo pamoja mpaka mwisho".

Zimbabwe: Mpinzani wa Mugabe Afutiwa Kesi

0
0
Mchungaji mwanaharakati Evan Mawarire aliyeshtakiwa mahakamani kwa jaribio la kutaka kumpindua Robert Mugabe wakati wa mgomo uliodhoofisha usafiri katika miji yote mikubwa amefutiwa mashtaka.

Uamuzi huo umekuja wiki moja tangu Mugabe, aliyetawala Zimbabwe tangu ilipopata uhuru mwaka 1980, alipojiuzulu kutokana na shinikizo la jeshi.

"Hakuna ushahidi kuthibitisha kwamba yeye (Mawarire) alihimiza machafuko ya kuiondoa serikali," alisema katika hukumu yake Jaji wa Mahakama Kuu Priscilla Chigumba.

Jaji alisema Mawarire alihimiza mgomo usio na machafuko yakiwa ni majibu kutokana na mgogoro wa kiuchumi.

Mawarire aligeuka na kuwa taswira ya maandamano ya kumpinga Mugabe mwaka jana aliposambaza video yake katika wavuti akiwa amejifunga bendera ya taifa huku akilalamikia matatizo ya Zimbabwe.

Video hiyo ilitumika kushawishi vuguvugu lililoitwa BenderaHii na kusababisha migomo nchi nzima. Serikali ilijibu kwa kupiga marufuku maandamano ya mitaani jijini Harare katika kile ilichoita ni “matumizi mabaya” ya bdenera.

"Safari nzima imekuwa upuuzi," Mawarire aliwaambia wanahabari.

"Sikuwa mtu wa kupandishwa kizimbani. Sikutakiwa hata kutumia miezi 11 nikijaribu kujitetea juu ya haki zangu kikatiba,” alisema.

Pia Manawire amemuonya rais mpya Emmerson Mnangagwa, veteran wa chama tawala cha Zanu-PF kwamba asithubutu kukaba koo haki za watu.
 Facebook  T

Rais wa Nigeria Aingilia kati Waafrika Kuuzwa Libya

0
0
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ameingilia kati suala ambalo sasa limeigusa dunia nzima kwa kitendo cha raia wa Libya kuwauza kama watumwa wahamiaji wanaoingia nchini humo.

Kwenye ukurasa wake wa twitter Rais Buhari amesema vitendo hivyo havikubaliki, na kwamba wako tayari kufanya lolote kuwalinda raia wake ambao pia ni miongoni mwa wahanga wa biashara hiyo, yenye ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

“Hali ya Libya ya watu kuuzwa ni ya kutisha na haikubaliki, tutafanya kila kitu kuwalinda raia wetu popote walipo, na pia tumeshaanza kuwarudisha nyumbani wanigeria wote waliopo Libya na sehemu nyingine, tutahakikisha wote wanarejea nyumbani salama na kuhudumiwa”, ameandika Rais Buhari.

Kitendo cha raia wa Libya kuwauza wahamiaji wanaoingia nchini humo ambao wengi wao ni raia wa mataifa ya Afrika Magharibi, kimeishtua dunia nzima ambapo mpaka watu maarufu mbali mbali duniani, wamekuwa wakipost kwenye mitandao ya kijamii kukemea vitendo hivyo.


Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Ferooz Afunguka Prof Jay , Chege Kumtenga

0
0
Ferooz Afunguka Prof Jay , Chege Kumtenga
Msanii wa muziki wa bongo fleva, Ferooz ambaye anafanya vyema na wimbo wake 'Nakaza roho' ameweka wazi kuwa alichoimba kwenye wimbo huo ni ukweli mtupu na kusema kuna watu wake wa karibu kama Prof Jay, Chege wamempa kisogo.

Ferooz akipiga stori na mwandishi wa tovuti ya EATV amesema kuwa watu wake wa karibu wengi wao walimtenga na kumuweka pembeni na kudai hata alipojitahidi kuwatafuta lakini mawasiliano hayakuwa mazuri, jambo ambalo anasema hakutegemea kutokana na namna alivyokuwa akiishi na watu hao.
Mbali na hilo Ferooz anasema katika kipindi ambacho aliyumba kimaisha alizidi kukatisha tamaa na watu wengi mbalimbali lakini alijipa matumaini na kupigana jambo ambalo anaona limeanza kuleta matumaini kutokana na watu kumpokea vyema na wimbo wake huo mpya 'Nakaza roho' 
"Kiukweli namshukuru Mungu kwani wimbo huu umepokelewa vizuri na mashabiki wangu kila kona na sasa naanza kuona mtaani umeanza kufanya vizuri, kiukweli wimbo huu umenipa matumaini mapya kuwa naweza kufanya mambo makubwa kwani bado mashabiki wanapenda kazi zangu, sikutegemea kabisaa kama ningepeta mapokeo haya hivyo imenipa nguvu sana" alisema Ferooz. 
Video ya Ferooz imeongozwa na director wa video anayechipukia nchini Tanzania anayefahamika kwa jina la Kilonzo. Itazame hapa zaidi 

Trump Ajibu Mapigo 'Tutaiangamiza Korea Kaskazini Iwapo Vita Itatokea

0
0
Trump Ajibu Mapigo 'Tutaiangamiza Korea Kaskazini Iwapo Vita Itatokea
Marekani imeyataka mataifa yote kukatiza uhusiano wa kidiplomasia na ule wa kibiashara na Korea Kaskazini baada ya taifa hilo kufanyia jaribio la kombora lake la masafa marefu.
Akizungumza katika baraza la usalama la umoja wa kimataifa ,mjumbe wa Marekani katika baraza hilo Nikki Haley amesema kuwa rais Trump amemtaka mwenzake wa China kukata usambazaji wa mafuta kwa Pyongyang.
Amesema kuwa Marekani haitaki mzozo lakini Korea Kaskazini itaangamizwa iwapo vita vitazuka.
Onyo hilo linajiri baada ya Pyonyang kufanyia majaribio kombora lake la kwanza katika kipindi cha miezi miwili.
Marekani: Korea Kaskazini ilikusudia uchokozi
Marekani yailalamikia Korea Kaskazini
Marekani yatishia kuiadhibu Korea Kaskazini
Korea Kaskazini imesema kuwa kombora hilo lililorushwa siku ya Jumatano ambalo inasema liliruka kimo cha kilomita 4,475, ikiwa ni mara kumi zaidi ya kimo cha kituo cha angani.
Madai hayo hayakuthibitishwa na wataalam wametiliashaka uwezo wa taifa hilo kuwa na teknolojia kama hiyo.
Hatahivyo kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesema kuwa uzinduzi wa kombora hilo ulikuwa wa kufana.
Jaribio hilo likiwa mojawapo ya majaribio yaliofanywa na taifa hilo limeshutumiwa na jamii ya kimataifa na tayari baraza la usalama la umoja wa kimataifa limeitisha kikao cha dharura.
Bi Haley alionya kuwa kuendelea kwa uchokozi kunalenga kuliyumbisha eneo hilo.
''Tunahitaji China kuchukua hatua zaidi'', alisema.
Rais Trump alimpigia simu rais Xi Jinping mapema siku ya Jumatano , Ikulu ya Whitehouse ilisema kuwa rais Trump alizungumza na Xi Jinping kwa simu akimtaka kuchukua hatua zozote kuishawishi Korea Kaskazini kusitisha uchokozi na kusitisha mpango wake wa kinyuklia.

Baraka Da Prince Awaduwaza Mashabiki wa Alikiba

0
0
Baraka Da Prince Awaduwaza Mashabiki wa Alikiba
Kwa muda mrefu sasa wadau wengi wa muziki wa Bongo Fleva wamekuwa wakiamini kuwa Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Barakah The Prince na mfalme wa Bongo Fleva, Alikiba wana bifu au tofauti miongoni mwao baada ya Baraka The Prince kujitoa kwenye lebo ya RockStar4000 ambayo ipo chini ya Alikiba na Meneja wake Seven Mosha.

Ukweli ni kwamba Barakah The Prince hana tofauti/bifu  yoyote na Alikiba kama ambavyo mashabiki wengi wa Alikiba na wadau wa muziki walivyokuwa wakidhania kwani  Hitmaker huyo wa Sometimes kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibitisha hilo kwa kumtakia Kheri ya siku yake ya kuzaliwa Alikiba .

Alikiba leo Novemba 29, 2017 anasherehekea siku yake ya kuzaliwa na mastaa kibao wamemposti kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii kumtakia maisha kheri akiwemo Ommy Dimpoz, Mwana FA, na wengineo.

Waombolezaji Watimua Mbio na Kulitelekeza Jeneza Lenye Mwili wa Marehemu

0
0

Watalii Wakamatwa kwa Kuonyesha Makalio Hekaluni

0
0
Watalii Wakamatwa kwa Kuonyesha Makalio Hekaluni
Raia wawili wa Marekani wamekamatwa nchini Thailand baada ya kuchapisha picha yao mtandaoni wakionyesha makalio yao katika hekalu.
Watalii hao walipiga picha hiyo katika hekalu maarufu nchini Bangkok Wat Arun na kuichapisha katika mitandao ya Twitter na instagram.
Mamlaka ya uhamiaji iliambia BBC kwamba wawili hao Joseph na Travis Dasilva wote wakiwa na umnri wa miaka 38 watapigwa faini na kurudishwa kwao.
Thailand ina sheria kali kuhusu tabia zinazoonekana kutokuwa na heshima na zinazoingilia dini yake ya Buddha.
Watalii hao walikamatwa jioni Jumane wakati walipokuwa wakiondoka nchini humo katika uwanja wa ndege wa Bankok Don Mueang.
Naibu msemaji wa idara ya uhamiaji nchini Thailand, kanali Choengron Rimpadee aliambia BBC kwamba wawili hao walikuwa katika orodha ya watu waliokuwa wakichunguzwa baada ya mamlaka kuona picha hizo zenye utata katika mitandao ya kijamii.
''Wakati watakaposhtakiwa maafisa wa polisi wa uhamiaji wa Thailand watafutilia mbali visa zao na kutaka warudishwe makwao'', alisema.
Watalii wa Marekani wakamatwa kwa kupiga picha za utupu hekaluni ThailandHaki miliki ya
Watalii wa Marekani wakamatwa kwa kupiga picha za utupu hekaluni Thailand
Pia watapigwa marufuku kurudi nchini Thailand.
Alielezea kwamba wawili hao waliwasilishwa katika kituo cha polisi cha Yai nchini Bangkok ili kushtakiwa kwa kuonyesha utupu katika eneo la umma, makosa ambayo mtu anapopatikana na hatia anaweza kupigwa faini ya dola 153.
Hatahivyo, serikali ya Thai na maafisa wa polisi wameambia vyombo vya habari kwamba mashtaka hayo yanaweza kuwa mabaya zaidi.

Hii Hapa Tiba Mbadala ya Ganzi Mikononi, Miguuni

0
0
Hii Hapa Tiba Mbadala ya Ganzi Mikononi, Miguuni
GANZI mikononi na miguuni, ni tatizo linaloashiria kukosekana kwa fahamu katika sehemu hizo. Hisia ndiyo inakosekana kwa sababu hakuna damu na neva zinakosa mawasiliano ya moja kwa moja na ubongo.

Ni jambo la kawaida linalowapata watu wengi sana katika miaka ya hivi karibuni, lakini pasipo kujua nini chanzo chake wala tiba.

Vyanzo vya ganzi mwilini

Vifuatavyo vinatajwa kuwa vyanzo vya ganzi mwilini mwa binadamu:

1. Shinikizo la muda mrefu kwenye miguu na mikono.2. Kuwa karibu na vitu vyenye baridi sana kwa kipindi kirefu.3. Mabadiliko ya muda mfupi kwenye neva/mishipa.4. Ajali kwenye neva.5. Kunywa pombe kupita kiasi.6. Uvutaji sigara na bangi.7. Uchovu usioisha.

8. Kutokujishughulisha na mazoezi ya viungo kila mara.9. Ukosefu wa vitamini B12 na Magnesiamu mwilini,10. Ugonjwa wa kisukari n.k

Kwa kawaida, ganzi inayotokea kwa dakika kadhaa na kupotea huwa haina shida yoyote.

Inaelezwa, ni vyema kuonana na daktari mapema, iwapo ina kawaida ya kutokea kila mara na inadumu muda mrefu. Inaweza kuwa ishara ya ugonjwa fulani unaohitaji matibabu ya haraka.

Kuumwa ganzi miguuni na mikononi, kunaweza kuwa jambo linaloudhi sana kwa mgonjwa.

Kuna dawa kadhaa za asili. Hata hivyo, hapa mimi leo nimekuandalia dawa za asili unazoweza kuzitumia kuondokana na tatizo hili.

Matibabu mbadala mwilini:

1. Massaji; Kufanya mazoezi ya massaji wakati unapopatwa na ganzi ni namna nzuri ya kutibu ganzi.

Massaji inaongeza msukumo na mzunguko wa damu jambo ambalo mwisho ni tiba kwa tatizo la ganzi. Zaidi masaji inasaidia kusisimua neva na misuli na hivyo kuimarisha na kuongeza mzunguko wa damu kwa ujumla.

*Kwa matokeo ya uhakika weka mafuta ya nazi au ya zeituni au ya mharadali (mustard oil) kwenye viganja vya mikono yako .

*Pakaa sehemu unapopata ganzi

*Massaji maeneo hayo na mikono yako kwa wastani wa dakika tano mpaka saba.

*Fanya mara tatu hata tano kwa siku.

2. Mazoezi ya viungo; Hayo husaidia kuimarisha mzunguko wa damu na kuongeza oksijeni katika sehemu zote mwilini, hivyo kuzuia kupata ganzi.

Mazoezi ndiyo namna pekee ya bure ya kujikinga na kujitibu na magonjwa mengi ikiwamo tatizo la mwili kupatwa na ganzi.

Mazoezi maalum; hapo inajumuisha kulala chali, kunyoosha mikono chini. Kisha nyanyua mguu mmoja juu unyooke, shusha chini mguu na unyanyue wa pili hivyo hivyo juu kisha chini. Endelea hivyo hivyo kwa mara kumi kumi kwa mizunguko mitano, zoezi lichukue wastani wa dakika 10

Kisha, anyanyuke na ajipigie saluti mwenyewe, akianzia mkono wa kulia mara 15, kisha unahamia mkono wa kushoto mara 15 tena mizunguko mitano.

Hatua inayofuata ni; simama,- chuchumaa, simama, chuchumaa, simama, hivyo hivyo mara 15 kwa mizunguko mitano.

Pia, unasimama wima, nyoosha mikono yote juu na uishushe mabegani. Hivyo, mikono juu na kisha mikono mabegani mara 15 kwa mizunguko mitano.

Fanya hivi mara nne mpaka tano kwa wiki. Mazoezi ya kukimbia, kuendesha baiskeli, kuogelea ni mazuri pia.

3. Bizari; Bizari au manjano inayojulikana kwa Kiingereza kama ‘Turmeric’ ina kitu muhimu ndani yake kijulikanacho kama ‘curcumin’ kinachosaidia kuongeza msukumo wa damu katika sehemu zote ya mwili.

Pamoja na hayo, bizari inasaidia kuondoa maumivu na hali ya kutojisikia vizuri mwilini.

Kinachofuata ni kuongeza kijiko kidogo kimoja cha chai cha unga wa bizari ndani ya kikombe cha maziwa ya vuguvugu, ongeza kiasi kidogo cha asali na unywe kutwa mara moja;

Mtu anaweza kutengeneza uji mzito (paste) wa bizari na maji na utumie kufanya massaji sehemu unapopata ganzi.

4. Mdalasini; Mdalasini ina kemikali na viinilishe mbalimbali, ikiwamo manganizi na potasiamu na vitamini nyingi za kundi B.

Faida zake za kiafya zinajumuisha kuongeza msukumo wa damu kwenye miguu na mikono yako na hivyo kusaidia kutibu tatizo la ganzi.

Wataalamu wa tiba asili wanashauri gramu mbili mpaka nne za unga wa mdalasini, zitumike kila siku kwa ajili ya kuhamasisha, mzunguko mzuri wa damu mwilini.

Changanya kijiko kidogo kimoja cha chai ya mdalasini ya unga katika glasi ya maji ya moto na unywe yote mara moja kwa siku.

Au changanya kijiko kimoja kidogo cha chai cha mdalasini ya unga na kijiko kidogo kingine cha asali na ulambe mchanganyiko huo kila siku asubuhi, kwa wiki kadhaa.

Angalizo la mdalasini feki; Ni muhimu sana kuelewea kuhusu mdalasini hasa ambao hutumika kama dawa.

Siyo kila mdalasini unaouona unaweza kukupa maajabu haya, mwingine ni sumu kabisa mwilini. Na watu wengi hawajui hili jambo.

(a) Ceylon cinnamon

Mdalasini ambao hutumika kama dawa hujulikana kwa kitaalamu kama ‘Ceylon cinnamon’ na kwa kawaida wenyewe huuzwa gharama sana.

Kwa kawaida zina ladha tamu na harufu ya kuvutia zaidi na zinatoka katika nchi ya Sri Lanka katika mmea ujulikanao kama Cinnamon Zeylanicum. Hujulikana pia kama mdalasini wa India.

Huwa na rangi ya kahawia (light brown), mwembamba na mlaini.

(b) Cassia cinnamon; wakati mdalasini feki ni sumu, pia inajulikana kama ‘Cassia cinnamon’ ni mdalasini huu ambao katika baadhi ya nchi umepigwa marufuku kutumika wala kuingizwa nchini mwao. Hujulikana pia kama mdalasini wa China na wengine huuita Saigon.

Mdalasini huo unatoka katika nchi za China, Vietnam na Indonesia. Wenyewe huwa una joto zaidi na huwa na ladha kali na ya kuwasha ukiutumia. Madhara yake ni pamoja na kudhuru ini na figo ukitumika kwa kipindi kirefu.

Cassia cinnamon huuzwa bei rahisi sana na mwingi unaopatikana huko masokoni. Huwa na rangi inayokaribia na uweusi.

Kwa kawaida ni vigumu kutofautisha aina hizi mbili za mdalasini ukishakuwa tayari katika mfumo wa unga tofauti na ukiwa bado katika fimbo au magome. Nunua kutoka kwa mtu unayemuamini zaidi.

5. Kula vyenye vitamini B; ili kuzuia ganzi mwilini hasa kwenye mikono na miguu ni muhimu kwamba unakula vyakula zaidi vyenye vitamini B kwa wingi hasa vitamini B6 na B12.

Vitamini hizi ni muhimu kwa ajili ya afya nzuri kuzipa neva uwezo wa kufanya kazi vizuri na upungufu wake unaweza kusababisha ganzi katika sehemu mbalimbali za mwili kama kwenye mikono, vidole na miguu.

Vyakula hivyo ni pamoja na mayai (mayai ya kuku wa kienyeji), parachichi, nyama, maharage, samaki, maziwa, mtindi, mbegu mbegu nk

Unaweza pia kutumia vitamini B-complex mara 2 kwa siku kila siku. Kwa dozi sahihi zaidi muulize daktari wako wa karibu.

6. Ongeza matumizi ya magnesiamu

Usawa mdogo wa magnesiamu katika mwili ni moja ya sababu ya kutokea kwa ganzi katika sehemu mbalimbali za mwili. Magnesiamu ni madini muhimu katika kuwezesha ufanyaji kazi ulio mzuri wa neva za mwili na mzunguko mzuri wa damu mwilini.

Kula vyakula vyenye magnesiamu zaidi kama vile mboga za majani zenye rangi ya kijani, mbegu mbegu, siagi ya karanga, soya, parachichi, ndizi, chokoleti nyeusi, na mtindi wenye mafuta kidogo.

Unaweza pia kutumia viinilishe vya magnesiamu gramu 350 kila siku ila ongea kwanza na daktari wako wa karibu.

Vingine muhimu vya kuzingatia

1. Kuwa ‘bize’ na mazoezi kila siku.2. Usikae muda mrefu kwenye kiti.3. Epuka chai ya rangi, kahawa, soda nyeusi na vinywaji vyote vyenye kaffeini.4. Kula zaidi matunda na mboga za majani5. Kunywa maji mengi kila siku kidogo kidogo kutwa nzima6. Epuka sigara na bidhaa nyingine za tumbaku.7. Vaa viatu ambavyo ni saizi yako pia epuka viatu vyenye visigino virefu zaidi8. Hakikisha una uzito sahihi na siyo uliozidi

Wasiliana na Fadhili Paulo, Tabibu wa Tiba Asilia kwa ushauri zaidi; WhatsApp +255769142586.


Mwanamke Kukaa Bila Kuolewa Aileti Picha Nzuri Nami Naolewa Ili Kutoa Nuksi- Sasha

0
0
Mwanamke Kukaa Bila Kuolewa Aileti Picha Nzuri Nami Naolewa Ili Kutoa Nuksi- Sasha
MWANADADA mwenye mvuto wa aina yake Bongo, Sasha Kassim ambaye anatarajia kufunga ndoa mwanzoni mwa mwaka kesho amesema kuwa, ameamua kuolewa ili kutoa nuksi.

Sasha ambaye hujulikana sana mitandaoni kwa picha zake za kihasara, alisema hadi sasa bado hajaenda kutambulishwa ukweni na wala hakuna mpango huo, ila amekuwa akiwasiliana na wakwe zake kwa njia ya simu, baada ya ndoa ndipo ataenda kupata baraka zao lakini makazi yake yataendelea kuwa Bongo.

“Naolewa kutoa nuksi si unajua mwanamke kukaa bila ndoa haileti picha nzuri, wakwe zangu wamenikubali japo hawajawahi kuniona laivu zaidi ya kwenye simu, nimeshaongea na mume wangu mtarajiwa kwamba akinioa nitaendelea kuishi Bongo, sababu napapenda sana huko Italy nitakuwa naenda kwa muda mfupi na kurudi na amekubali,” alisema Sasha ambaye anatarajia kuolewa na Bonphace, raia wa Italy.

Mhalifu wa Kivita Afariki Baada ya Kunywa Sumu Mahakamani

0
0
Mhalifu wa Kivita Afariki Baada ya Kunywa Sumu Mahakamani
Kikao cha kusikiliza rufaa iliyowasilishwa na washtakiwa wa uhalifu wa kivita mjini The Hague, Uholanzi kimesitishwa ghafla baada ya mmoja wa washtakiwa kusema amekunywa sumu baada ya kusikiliza hukumu.
Slobodan Praljak, 72, alikuwa mmoja wa viongozi sita wa zamani wa kisiasa na wa kijeshi wa Bosnia wa asili ya Croatia ambao walikuwa wamefika mahakamani.
Amefariki akitibiwa hospitalini na Umoja wa Mataifa umesema sasa mahakama hiyo ni "eneo la uhalifu".
Alikuwa amehukumiwa kufungwa jela miaka 20 mnamo 2013 kwa makosa ya uhalifu wa kivita yaliyotekelezwa katika mji wa Mostar.
Baada ya kusikiliza hukumu kwamba majaji walikuwa wamedumisha kifungo hicho, alimwambia jaji, "Nimekunywa sumu".
Sita hao walikuwa wanasikiliza uamuzi wa mwisho wa rufaa uliokuwa unatolewa na mahakama maalum ya kimataifa ya UN iliyokuwa inashughulikiwa makosa yaliyotekelezwa Yugoslavia (ICTY).
Ingawa walikuwa washirika dhidi ya Waserbia wa Bosnia wakati wa vita hivyo vya 1992-95, Wacroatia wa Bosnia na Waislamu walipigana wenyewe kwa wenyewe kwa miezi 11.
Mji wa Mostar ulishuhudia mapigano makali zaidi.
Mhalifu wa kivita raia wa Austria akamatwa Poland
Waathiriwa wa uhalifu wa kivita DR Congo kufidiwa $1m
'Usiondoe gilasi'
Praljak alisimama na akainua mkono wake hadi kwenye kinywa chake, kisha anainamisha kichwa chake nyuma na kuonekana kunywa kitu kutoka kwenye gilasi ndogo.
Jaji mwandamizi Carmel Agius mara moja alisitisha shughuli na gari la kuwabeba wagonjwa likaitwa.
"Sawa," jaji alisema. "Tunaahirisha ki...Tunaahirisha...Tafadhari, pazia. Usiondoe gilasi ambayo ameitumia alipokunywa kitu."
Kabla ya pazia kurejeshwa, ukumbi wa mahakama umeonekana kujawa na mkanganyiko, anasema mwandishi wa BBC Anna Holligan kutoka The Hague.
Gari la kuwabeba wagonjwa lilionekana baadaye likifika nje ya ukumbi wa mahakama huku helikopta ikipaa juu angani.
Wafanyakazi kadha wa uokoaji wameingia ukumbini na vifaa vyao.

Punguza Unene na Kutibu Magonjwa Kwa Kutumia Dawa za Edmark...Bonyeza Hapa

0
0

TUNA DAWA AMBAZO NI VIRUTUBISHO NA CHAKULA MBADALA ZIMEHAKIKIWA NA TFDA

Ni uhakika kwa afya yako, kupunguza uzito na Sumu mwilini, Mafuta/Sehemu Mbaya, Kitambi na Nyama Uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali yaliyoshindikana

Loose Weight Trainer ni Msaada wako Wasiliana Nasi Kwa WhatsApp 0713 777 470

Upate Suluhisho la Afya yako Bila Madhara pia unaweza kujiunga nami ili ufanye Biashara hii Nicheki


Intagram napatikana kwa jina @looseweight_trainer

Ukiwa na Mpenzi Mwenye Haiba hii, Kujenga Uhusiano Imara ni Mashaka

0
0
Wataalamu wa tabia na mienendo ya binadamu wanasema, kuna Makundi kadhaa ya haiba. Wana maana kwamba, binadamu wamegawanyika katika Makundi kitabia.

Je, wewe uko kwenye kundi lipi?

Hiki ndicho ninachotaka kuwasaidia siku ya leo.

Lakini leo ningependa kuwazungumzia watu wenye haiba ya ukamilifu. Hawa ni wale watu ambao wanaamini kwamba, hawapaswi kukosea. Kwao, wanaamini kuwa, mtu anatakiwa afanye kwa usahihi na ukamilifu na kukosea kuna maaana ya udhaifu mkubwa na unyonge.

Nguvu kubwa ya watu hawa iko kwenye usahihi, ukamilifu na kurekebisha makosa. Iko kwenye kufanya ambavyo mtu angetakiwa kufanya, na kufanya mambo kwa usahihi.

Watu hawa wenye haiba ya usahihi huko ndani mwao kuna sauti (little voices) ambazo zina nguvu sana kwao, zenye kuwaamuru wafanye mambo bila kukosea. Lakini, sauti hizi zinakosoa na kuwadhibiti wahusika kwa njia yenye kuwaumiza. Huwa ni sauti zenye kuzalisha mashaka. Kushtakiwa na dhamira na hofu.

Kwa sababu ni watu wanaoamini katika “nzuri na sahihi,” inakuwa ni vigumu sana kwao kuishi na watu wengine kwa amani. Mbaya zaidi ni kwamba, wapenzi wao hupata shida sana kuendana nao. Hii ni kwa sababu, wanataka mambo yaende kwa njia yao, yawe sahihi. Kuna, “ingetakiwa iwe hivi,” nyingi sana.

Watu hawa huwafanya wengine wanaohusiana nao kuhisi kama vile wanatembea juu ya maganda ya mayai.

Kwa nini?

Ni kwa sababu hawa watu wenye haiba hii, hujiona wanaweza kuliko wengine na wanastahili kuliko wengine. Watu hawa wana tabia ya kusema au kumwambia mtu ukweli moja kwa moja kwa njia yenye kukera sana. Hali hii huwasononesha watu wanaoambiwa ukweli.

Watu ambao wameoa au kuolewa na wenye haiba hii, huwa wanatamani kuona mambo yakiwa tofauti kidogo. Wanajihisi kufungwa pumzi, kukaliwa kooni, kufungiwa kwenye dema na kushindwa kuona nafasi yao kama watu huru. Huhisi kuwa wao ni watoto, wanaokosea kila kitu, kwani ndivyo sauti za wapenzi wao zinavyowaambia kila wakati.

Inabidi mtu wa haiba hii ajifunze kukubali makosa, kwamba, kukosea siyo udhaifu, bali kujifunza. Ajue kwamba, kuna njia nyingi za kujifunza mambo, siyo njia moja tu ya “usahihi.” Kuna ya kukosea na kujifunza makosa, halafu ndiyo usahihi ufuate.

Tabia za Mama Mkwe Ndio Tabia za Mkeo..Chukua hiyo Kubali Au Kataaa

0
0
Kwa utafiti wangu mdogo niliofanya nimegundua kwamba tabia za mama mkwe ndio tabia za mkeo upende usipende.kwahiyo kama una mpango wa kuoa usiishie kumchunguza mchumba wa kike ambaye wakati wa uchumba anakuwa anaishi maisha ya kuigiza bali pia angaika kumchunguza mama mkwe.

Kwanini mama mkwe?

1. Mama mkwe ndie aliyemlea mkeo mtarajiwa kwahiyo mchumba wako atakuwa ameiga na kufundishwa kuwa na tabia kama mama yake

2.Mara mwanamke anapoolewa Mshauri mkuu ni mama yake mzazi(napenda uamini hili) kwahiyo maisha yake kwenye ndoa yatategemea ushauri wa mamaye

3.ikitokea mfarakano kwenye ndoa na kama mwanamke ndio tatizo mama mkwe ndie mtu pekee anayeweza kumbadilisha mkeo katika njia sahihi.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE..

Albert Msando Afunguka Kuhusu Video Yake na Gigy Money Wakiwa Kwenye Mahaba Mazito

0
0
Albert Msando Afunguka Kuhusu Video Yake na Gigy Money Wakiwa Kwenye Mahaba Mazito
MWANASHERIA maarufu nchini aliyekuwa Chama cha ACT Wazalendo na hivi karibuni akahamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Albert Msando, kwa mara ya kwanza amefunguka LIVE kuhusu video yake akiwa na mwanamuziki na modo Gigy Money iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii mwezi Mei mwaka huu.

Video hiyo ilimuonyesha Msando na Gigy Money wakiwa ndani ya gari, huku Msando akipitisha mkono wake juu ya mwili wa Gigy, wakati huo Gigy Money akikata kiuno huku anacheza muziki.
Akifanya mahojiano leo  kwenye Kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa kupitia Clouds TV, Msando amesema;

“Kuhusu video na Giggy sikuwa namfahamu na kusema kweli tukio lile lilitokea wakati nimekunywa pombe,  sikuwa namfahamu Giggy na hata juzi nilikutana nae kwenye ndege sikumkumbuka.

Ile ni moja kati ya sehemu zilizonisaidia katika maisha yangu, ilinisaidia kujua jamii inanichukuliaje na nini inategemea kutoka kwangu. Video ile haikutengenezwa kwa sababu zozote, mimi sikuwa namfahamu Giggy.

“Tukio lile lilitokea wakati nimekunywa kilevi, sikuwa nikitambua kilichokuwa kinaendelea. Zaidi ameeleza kuwa video ile ni funzo kwa jamii nzima kuwa responsible hata kama hujakamatwa, usisubiri uwe ‘caught on camera’ ili uwajibike,” alisema Msando.

Hata hivyo, baada ya video hiyo kusambaa watu mbalimbali walionyesha kuchukizwa na wanavyomfahamu Mwanasheria Albert Msando mtu wanayemwona ana  heshima kubwa na umaarufu katika jamii,  ambapo aliomba msamaha kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Kuhusu kuacha kusimamia kesi ya wema Msando Amesema “Niliacha kuwa Wakili wa Wema Sepetu baada ya Kibatala na Lissu kuanza kumtetea, bado ni mshikaji wangu, na nimekua nikiona hiyo habari inayozunguka kuhusu Wema Sepetu kujiandaa kurudi CCM, namkaribisha”

Faiza Aeleza Sababu ya Kumuanika Mzazi Mwenzake

0
0
Faiza Aeleza Sababu ya Kumuanika Mzazi Mwenzake
MSANII wa filamu Bongo, Faiza Ally amesema kuwa, japo mwanzoni aligoma kumuanika baba mtoto wake lakini siku chache zilizopita aliamua kumueka wazi baada ya mwanaume huyo kuridhia.

Akipiga stori na paparazi wetu, Faiza alisema, awali mwanaume huyo ambaye hakupenda kumtaja jina lake, alikuwa hataki kujulikana mitandaoni lakini sasa ameridhia wamjue yeye ndio baba halali wa mtoto wake aitwaye Li na kufunika uvumi wa kwamba mtoto huyo ni wa baba mwingine.

“Baba mtoto wangu mwanzo hakupenda watu wamjue, lakini maneno yamekuwa mengi mara nimezaa na Sugu (Joseph Mbilinyi) wengine wanasema Gabo (Salim Ahmed) wengine mwanaume mchina, jambo hilo limemkera akaona bora nimuweke wazi na jamii imjue,” alisema Faiza.

Video: Tazama Hii ya Ali Kiba na Abdu Kiba 'Single'

0
0
Video: Tazama Hii ya Ali Kiba na Abdu Kiba 'Single'
Msanii Abdu Kiba ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao ‘Single’ ambao amemshirikisha kaka yake Alikiba. Video ya ngoma hiyo imeongozwa na Hanscana, tazama hapa chini video hiyo.

Tundu Lissu Afunguka Mazito Hali Ilivyokuwa Siku ya Tukio la Kushambuliwa

0
0
Tundu Lissu Afunguka Mazito Hali Ilivyokuwa Siku ya Tukio la Kushambuliwa Kwake
 Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amesimulia hali ilivyokuwa siku ya tukio na pia kueleza ujumbe aliompa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan alipomtembelea hospitalini jijini hapa juzi.

Mbunge huyo, ambaye alishambuliwa kwa risasi akiwa ndani ya gari lililoegeshwa nje ya makazi yake mjini Dodoma Septemba 7, pia amesema amepitia majaribu mengi, lakini “hili ndilo kubwa”.

Amesema hali yake inaendelea vizuri na madaktari wanamuelezea kuwa ni “muujiza unaoishi” baada ya kufanikiwa kuunganisha vipande vya mwili ulioharibiwa kwa risasi.

Lissu alisema hayo alipofanya mahojiano na Mwananchi, ikiwa ni mara ya kwanza kwa chombo cha habari cha Tanzania tangu ashambuliwe.

Lissu amelazwa Hospitali ya Nairobi jijini hapa tangu Septemba 7 na huenda akahamishiwa nje ya bara la Afrika kwa matibabu zaidi, ambayo yatahusu mazoezi, kabla ya kurejea nchini.

Akizungumza na Mwananchi hospitalini hapo, Lissu alisema sasa anaamini kuwa Rais John Magufuli anajua kuna mgonjwa Nairobi na hivyo kufungua milango kwa wengine waliokuwa na hofu.

“Mimi namuamini na naendelea kuamini kwamba kwa sababu sasa Makamu wa Rais amekuja kwa niaba ya Rais, ametambua tuna mgonjwa yupo Nairobi. Milango itafunguka kwa wale wengine wote waliokuwa na hofu ya kuja,” alisema Lissu.

“Sasa Rais mwenyewe kamtuma makamu wake kuja kunipa pole, kwa hiyo hao wengine wa taasisi zote hawana hofu ya kuja kuniona.”

Akizungumzia mazungumzo yake na Suluhu, Lissu alisema yalikuwa mazuri.

“Mama Samia ni kiongozi wa kwanza wa Serikali ya Tanzania pamoja na mihimili yake kuja kunitembelea,” alisema Lissu.

“Spika wa Bunge hajaja, katibu wake na uongozi mzima wa Bunge haujaja. Jaji Mkuu au Jaji Kiongozi hawajaja pamoja na kwamba mimi ni Rais wa TLS.

“Na kwa kawaida mila na desturi za mahakama zetu, bila mawakili hakuna mahakama na kama Rais wa TLS nimekuwa nikialikwa na kuhudhuria vikao mbalimbali vya kiutendaji, lakini tangu nimeshambuliwa Jaji Mkuu au uongozi mzima wa Mahakama hata kutoa salamu za pole, hakuna.

“Rais Magufuli alikuwa hajawahi kusema lolote kuhusu kushambuliwa kwangu kama nakumbuka, lakini leo (juzi) amekuja Makamu wa Rais na amenieleza na napenda kuamini ni kweli ametumwa na Rais kama sehemu yake ya shughuli zilizomleta Kenya apitie kunisalimia na kunipa pole.”

Alisema Makamu wa Rais, ambaye waliwahi kufanya naye kazi wakati akiwa waziri anayehusika na Muungano na Lissu akiwa waziri kivuli wa eneo hilo, alimuuliza kama ana jambo lolote la kumweleza Rais, naye akamweleza kuhusu gharama za matibabu.

“Mimi bado ni mbunge, ujumbe ambao nataka aupeleke ni Bunge liko wapi? Bunge ambalo lina wajibu wa kisheria wa kunihudumia nikiwa naugua?” aliuliza Lissu akirejea mazungumzo hayo na Suluhu juzi jioni.

“Nilimpa ujumbe huo na napenda kuamini ataufikisha na ujio wake peke yake unatakiwa kufungua milango kwa wale waliokuwa wanafikiri wamefungiwa.”

Alisema suala la Bunge kuwa mbali naye ni mfano mwingine unaotia shaka kuhusu kushambuliwa kwake.

“Mimi ni mbunge na ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, ninatambuliwa na Sheria za Tanzania, Sheria inayohusika ni ya uedeshaji wa Bunge. Sheria inaeleza kwamba mbunge anapoumwa atapata matibabu pamoja na gharama nyingine kutoka bungeni,” alisema.

Lissu alisema kila mbunge anayeumwa analipiwa gharama zote na Bunge na vile vile kama itabidi, alazwe nje ya Dodoma iwe Dar es Salaam, Afrika Kusini, India Marekani au Kenya.

“Analipwa posho na Bunge na mtu anayemuuguza analipwa posho vile vile, nusu ya posho ya mbunge ili kumudu gharama za maisha,” alisema.

“(Lakini) Tangu nimeumizwa, Spika anajua, alitangaza bungeni mbunge mwenzetu anaumwa. Tangu wakati huo mpaka leo Spika hajaja, Katibu wa Bunge, Tume ya Bunge haijaja,” alisema Lissu, ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema.

Alisema  kuna wabunge wawili CCM, Mary Chatanda (Korogwe Mjini) na  Fakharia Shomar Khamis (viti maalum na mmoja wa watumishi wa Bunge walifika siku ya Jumapili, siku ambayo si ya kazi.

“Walikuja kunipa pole, walikaa hapa wakanipa nipa pole, halafu wakaniaga. Nikawauliza mmetumwa chochote, wakasema hapana,” alisema.

“Nikamuuliza ofisa wa Bunge, ‘kuna ujumbe umetumwa uniletee, akasema hapana. Kwa hiyo hao wawili walikuja kibinafsi tu.

“Tume ya Huduma za Bunge inayoshughulikia mambo haya, haijaja mpaka leo. Kwa hiyo ukiachilia mbali matangazo ya Spika, Bunge halijaja kabisa, halijanishughulikia kwa lolote.

“Hakuna anayeomba fadhila, nataka haki, nitendewe haki, anayetendewa mbunge yoyote anayeumwa. Hakuna anayelilia fadhila hapa, hakuna anyeomba ufadhili. Nataka Bunge litimize wajibu wake wa kisheria. Hili nitalipigania, kama siwezi kudai haki yangu ya kisheria ambayo iko wazi, kama ya kwangu naona inakanyangwa kwa makusudi tu, nitapigania ya nani?”

Lissu alisema Bunge halina sababu za maana za kutomgharimia, bali ni kupiga chenga tu.

“Wameandikiwa barua na ndugu yangu mara hawajaiona, kwa hiyo lazima nipiganie haki yangu ili nipiganie haki za wengine,” alisema.

Niliona watu wawili wenye silaha

Katika mahojiano hayo na Mwananchi yaliyochukua takriban dakika 60, Lissu pia alielezea jinsi shambulio dhidi yake lilivyofanyika Septemba 7, lakini tofauti na kauli ya ndugu zake kuwa anawajua watu hao, alisema hawafahamu watu hao na kusisitiza suala la wachunguzi kutoka nje.

“Nilitoka bungeni muda wa saa saba hivi,” alisema.

“Kabla sijatoka nilichangia mjadala wa mkataba kati ya Malawi na Tanzania kuhusu Mto Songwe. Baada ya kumaliza kuzungumza nikakaa kidogo kisha nikatoka na kwenda nyumbani kwa chakula cha mchana.

Alisema alivyofika nyumbani, wakatokea watu eneo la kuegesha magari katika nyumba hizo za Serikali, ambako anaishi jengo moja na Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani, mbunge wa Ulanga Magharibi (CCM), Dk. Haji Mponda na mmoja wa makatibu wakuu wa wizara.

“Kwa hiyo nakaa katika nyumba za Serikali. Watu wameingia katika nyumba za Serikali zinazolindwa saa 24, block inayotazamana na nyumba yangu, anakaa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson na huwa kuna polisi nje saa 24,” alisema.

“Lakini watu wameingia wenye silaha, wakaja kunishambulia. Sikuwatambua kwa sababu nilishambuliwa nikiwa katika gari sikutoka nje. Dereva wangu aliniambia kuna watu wako nyuma wananifuata nisifungue mlango.”

Alisema alijaribu kuwaangalia kwa kutumia kioo cha pembeni ya gari na kuwaona watu wawili wakitoka na bunduki. Yaliyofuata nimekuja kujikuta nipo hapa nilipo leo wiki moja baadaye.

“Kwa hiyo, siwezi kusema ninawafahamu walionishambulia. Sikutambua hata mmoja wao ila najua nilishambuliwa na watu wawili katika gari iliyokuwa na vioo vyeusi.”

Lissu alisema wiki tatu kabla ya shambulio hilo alilalamika hadharani kwamba anafuatiliwa kila anapokwenda na siku moja aliwasimamisha watu hao katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro na kuwauliza sababu za kufanya hivyo.

“Niliwauliza kwa nini wananifuata na kama kuna mtu kawatuma, mwambieni mimi si mhalifu. Lakini sikupewa ulinzi wowote,” alisema.

Wachunguzi kutoka nje

Kama ilivyo kwa familia yake na Chadema, Lissu anataka uchunguzi wa tukio hilo ufanywe na taasisi ya nje.

“Serikali inakosea sana,” alisema.

“Hili ni tukio la mbunge kushambuliwa akiwa maeneo ya Bunge. Kisheria hayo maeneo yanayoitwa ya Bunge ni pamoja na makazi ya wabunge wanapokuwa bungeni.”

Alisema huwezi kuwa bungeni kama huna sehemu ya kulala, kwa hiyo makazi yangu ni sehemu ya Bunge.

“Kitendo cha mbunge kushambuliwa wakati vikao vinaendelea-- na mbunge mwenyewe ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na anajulikana kwa kuikosoa Serikali mara nyingi kwa muda mrefu, inatia shaka,” alisema.

“Kitendo hicho peke yake kingetosha kutilia shaka uchunguzi wowote utakaofanywa na wale ambao mbunge huyo amekuwa akiwasema mara kwa mara. Kitendo hicho kingetosheleza kualika watu kutoka nje kuja kufanya uchunguzi.

“Wanakataa kwa sababu zao, tunaelekea miezi mitatu, polisi hawajasema wanamshuku nani. Hakuna mtuhumiwa hata mmoja halafu kuna jitihada kubwa imefanywa na Jeshi la Polisi kuzuia raia kumsaidia huyu mbunge.”

Alisema polisi imewazuia watu wasisali, wasimwombee Mungu apone, watu wasimchangie damu, kusiwe na dalili zozote za wazi za kumuunga mkono na huyu ambaye ameshambuliwa na watu wanasemekana hawajulikani.

“Kumekuwa na jitihada kubwa sana kuzuia watu wasimsaidie huyu kuliko kufanya upelelezi, hiyo inatoa picha kwamba bila uchunguzi huru ukweli hautajulikana, utafichwa na pengine ndivyo wanavyotaka,” alisema.

Akizungumza huku akisisitiza kwa mikono yake, Lissu alisema katika mlango wa Waziri Kalemani, kuangalia block ya Naibu Spika Dk Tulia, kuna camera za CCTV zinazofanya kazi Saa 24 hivyo kwa mtu yeyote ambaye yupo eneo hilo anaonekana, lakini akasema kuna vitu vinaashiria kuwa kunahitajika jicho la pili kuangalia hili.

Alipoulizwa nafasi ya Rais Magufuli katika suala hilo la uchunguzi, Lissu alisema: “Rais anaweza akitaka kuelekeza. Polisi ndio wenye mamlaka ya kiuchunguzi, waalike wataalamu kutoka nje.

“Haitakuwa mara ya kwanza, hatutakuwa wa kwanza kufanya hivyo na haitakuwa aibu ila ni namna nzuri zaidi ili kuondoa wingu lililotanda juu ya kushambuliwa kwangu, ukweli utajulikana na hiki kimya si kizuri.”

Lissu pia alizungumzia hali yake kiafya na matarajio yake.

“Nafikiri kiafya Lissu anaendelea vizuri na matibabu, hajapona bado lakini anaendelea vizuri, madaktari wanasema hali yangu inakuwa inatengamaa kila siku,” alisema.

“Huko tulikotoka ni kurefu zaidi kuliko tunakokwenda, vidonda vyote vya risasi vimepona, sina bandeji mwilini, sina bandeji kabisa. Maana yake vile vidonda vyote vilivyotokana na kupigwa risasi vimepoma.”

Hata hivyo, Lissu, ambaye chama na familia yake imesema ataenda kumalizia matibabu nje ya bara la Afrika, alisema bado hajajua ataruhusiwa lini, ingawa anajiona yuko katika hali nzuri.

“Madaktari hawajanipa muda, na nafikiri hawajanipa muda kwa sababu nzuri tu, majeraha niliyokuwa nayo nilipoletwa hapa, yalikuwa makubwa sana, madaktari wenyewe wamekuwa wakiniambia mimi ni muujiza unaoishi,” alisema.

“Kwa hali niliyoletwa hapa ni muujiza unaoishi. Kazi kubwa walioifanya ya kwanza ilikuwa kuhakikisha wanaokoa maisha na wameokoa maisha. Kazi ambayo inafuata ni kuniwezesha kurudi sasa katika hali yangu ya kawakida, kuweza kujitegema kimwili.”

Alisema madaktari wamemuwekea vyuma, wameunganisha mifupa.

Alisema mikono ilikuwa haifanyi kazi, lakini sasa anaweza kuichezesha na kula na kwamba tiba hiyo inachukua muda lakini tuko katika hatua ambayo si ya kuokoa maisha, bali ya kurudisha mwili katika hali ya kawaida.

“Kimawazo nafikiri sijabadilika sana, Lissu wa kabla ya Septemba 7 na Lissu wa leo kimsimamo wa kisiasa hajabadilika kabisa. Lazima tupiganie demokrasia, hiyo ndiyo salama yetu,” alisema.

“Tuwe na utawala wa kidemokrasia unaojali haki za binadamu, tuwe utawala wa sheria, tuwe na mfumo wa uongozi unaojali maisha ya wananchi, unaowajibika kwa wananchi au kwa wawakilishi wake na huu ni msimamo wangu unajulikana na bado uko vile vile.

Aadhimisha miaka 20 ya ndao wodini

Wakati akiendelea kutibiwa hospitalini hapo, jana Lissu na mkewe, Alicia walitimiza miaka 20 tangu walipofunga pingu za maisha Novemba 29, 1997 na kama kawaida walikuwa pamoja wodini.

“Mke wangu nikuzungumzieje?” alimuuliza.

“Kazi kwako,” Alicia alijibu.

“Mke wangu mpenzi anaishi kiapo chake tulipooana na kesho (jana) tunatimiza miaka 20. Tulipooana nilimsikia anasema ‘katika shida na raha’ nitampenda, nitafanya nini na nini’. Kwa hiyo mke wangu mpenzi anaishi katika kiapo chake,” alisema Lissu huku Alicia akitabasamu.

“Katika miaka hii 20, tumepitia majaribu mengi sana, lakini hili ndilo kubwa kuliko yote na nafikiri kama ni mtihani, mke wangu ameufaulu kwa daraja la juu kabisa kwa sababu amekuwepo hapa muda wote na mara nyingine ukimsikia anavyozungumza ana msimamo mkali kuliko mimi niliyeumizwa.”

Lissu alisema Alicia “ni mke wa kweli, aliyekubali kuchukua majukumu ya kuwa mke”, na kwamba anajisikia faraja na furaha ya kipekee kuwa naye na angepende wawe pamoja miaka 20 mingine.

“Najisikia mwanamme mwenye bahati sana kuwa naye. Ni mwanamke wa kipee sana kuwa naye. Tumetoka mbali sana na hii miaka 20 imekuwa mizuri sana katika maisha yangu kwa sababu ya kuwa naye,” alisema.

Alicia pia alikuwa na lake moyoni.

“Miaka 20 ni mingi, lakini nikifikiria kama ni juzi tu. Halafu nilikuwa sitaki kumkummbusha nilitaka kumfanyia ‘surprise (kumstua),” alisema huku Lissu akimsikiliza kwa makini na kutabasamu

“Lazima niwe mkweli. Kuna miaka mingine alikuwa busy (na kazi nyingi), anasahau hata siku. Tundu ni mme wangu, kikubwa naweza kusema ni rafiki yangu wa karibu sana wa miaka mingi sana, nikiwa msichana mdogo, mrembo na smart. Tumekuwa tukiishi hivyo.”

“Ujumbe wangu, Tundu siku zote aendelee kuwa Tundu tu. Tundu wa kabla ya tukio na baada ya tukio awe ni Tundu niliyemjua siku zote.”

Je, utagombea Urais 2020

Mbunge huyo wa Singida Mashariki hakutaka kuzungumzia uchaguzi wa mwaka 2020 na hata alipoulizwa kuhusu kugombea urais alistuka.

“Nafikiri huu ni mjadala unaohitaji kusubiri wakati mwafaka,” alisema.

“Si mjadala unaoweza kufanyika katika kitanda cha Hospitali ya Nairobi, Kenya. ni mjadala unaohitaji tukae, tushauriane. Kwa sababu ni chama lazima tukae tushauriane. Nafikiri hiki kitanda changu si mjadala wa kuanzisha, kama watu wananitajataja huko waendelee tu lakini mimi mjadala huu unisubiri nje ya hospitali.”Lakini Lissu alisema kwa sasa atakuwa wa tofauti kwa kuwa amepitishwa tanuru la moto na amepata uzoefu wa kutosha baada ya kujifunza mengi kutokana na tukio la Septemba 7.

“Nikitoka hapa kama Mungu amenipa pumzi ya kuendelea kuishi, haya mafunzo yatakuwa sehemu ya Lissu huyo baada ya Septemba 7. Nimejifunza kuwa Watanzania ni watu wa upendo sana. Pamoja na propaganda zote, uongo wote na ubaya wa watu, lakini Watanzania ni watu wa upendo sana,” alisema Lissu

“Wanafahamu nani anawapigania. Kuna rafiki yangu wa Dodoma ameniambia baada ya kupigwa risasi kuwa mji mzima ulihamia hospitali. Ingawa siku zote CCM wanashinda pale, siku hiyo walihamia pale (hospitali). Watanzania kila mahali walienda makanisani, misikitini, nafikiria huo upendo nitaulipaje.

“Nafikiria ni upendo ni kwa sababu ya kazi niliyoifanya bungeni na nje ya Bunge na hiyo kazi kama imewafanya wawe na upendo namna hiyo, basi nitaizidisha na nitawafanyia kazi iliyo bora zaidi.
Chanzo: Mwananchi
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images