Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

0
0

Gari Aina ya Toyota Land Cruiser (Prado) Ladaiwa Kuserereka Kwenye Ferry na Kuzama Baharini

0
0
TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa gari dogo aina ya Toyota Land Cruiser (Prado) linadaiwa kuseleleka kutoka kwenye pantoni (Ferry) na kuzama baharini eneo la Posta jijini Dar es Salaam mapema leo asubuhi, Desemba 1, 2017.

Inadaiwa kwamba katika gari hilo binafsi kulikuwa na watu wanne ambao wote walizama nalo na mpaka tunaenda mitamboni ilikuwa haijajulikana kama wamenusurika au wamekufa.

Video hiyo inaonesha watu wakishangaa eneo la tukio huku mmoja wao akijitolea kwenda kulifunga kamba gari hilo ili livutwe na kuokolewa lakini kabla ya kulifikia, lilizama baharini na kupotea.

Mtandao wa Global Publishers umemtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Emmanuel Lukula kuzungumzia tukio hilo ambapo amesema hana taarifa kwa kuwa alikuwa kwenye kikao hivyo anakwenda kufuatilia na atatoa ufafanuzi kuhusu tukio iwapo limetokea.

Pendeza na Kessy Product: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Safi Kwa Product za Asili

0
0

PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA*
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATAKS)KUNADAWA AINA TATU (@)JELI KUPAK_100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI NA MAPAJAN_80,000/
5)TOA KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE NA MANYAM YOTE
@) DAW YA MAJINI_100,000/NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME BILA KUVAA SIDIRIA_80,000/
8)KUONGEZA MAZIWA NA SAIZI NZURI_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA (kifaru)_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO YAKAWAIDA NA UZAZ_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_70,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA KWA DAW(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWLINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA JELI PAMOJA NA VIDONGE VYAAIN ZOT _100'000
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_ 120,000 /
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_80,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _80,000/
20)ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA MGUU_80,000/🍍🍉🌾 *TUNAPATIKAN DAR E SALAAM* *NAKWA *MIKOANKOTE* UTAPATA *PIA* *NA NCHI ZOTE PIGA CM* (+255)0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product*
*Delivery POPOTE ULIPO,*

Nyalandu Aguswa na Biashara ya Utumwa Libya Ameutaka Umoja wa Mataifa Kuchukua Hatua

0
0
Nyarandu Aguswa na Biashara ya Utumwa Libya  Ameutaka Umoja wa Mataifa Kuchukua Hatua
Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa wa Singida Kaskazini aliyejiuzulu, Lazaro Nyalandu ameutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua zaidi juu ya kinachoendelea nchini Libya.

Mh. Nyalandu amesema kwamba ni lazima hatua zichukuliwe kwa kile kinachoendelea nchini Libya kwa vile  kinachoshuhudiwa kwa sasa ni matusi kwa wanadamu.
Kupitia kwenye mtandao wake wa Twitter Mh. Nyalandu ameandika
"Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika lazima uchukue hatua dhidi ya Libya sasa. Tunachoshuhudia ni matusi kwa wanadamu" Nyalandu
Hivi karibuni kumekuwa na taarifa zikiripotiwa kutoka Libya kwamba kumekuwa na biashara ya utumwa ikifanyika ikihusisha Libya kuuza waafrika wengine nchi za Ulaya.
Siku ya jana Ubalozi wa Libya nchini Tanzani umesema Waafrika wanaosemwa wanauzwa kutoka Libya, yawezekana walikuwa wanakabidhiwa kwa watoroshaji ili wawapeleke Ulaya na sio kuwauza kama watumwa.

China Yaahidi Kufadhili Ujenzi Wa Reli Kwa Kiwango Cha Kimataifa (SGR)

0
0

Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
BALOZI wa China hapa nchini, Wang Ke amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na kuahidi kuwa nchi yake iko tayari kushawishi taasisi za fedha ikiwemo Benki ya EXIM ya nchini humo kushiriki ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa baada ya kufanyika kwa upembuzi yakinifu wa mradi huo.

Alisema kuwa kutokana na ukubwa wa mradi huo, unaokadiriwa utagharimu Dola za Marekani bilioni 7.6 hadi kukamilika kwake, utahitaji kufanyiwa upembuzi yakinifu ili kukidhi masharti ya kupata mkopo kupitia Benki ya Exim na taasisi nyingine zitakazotaka kujenga mradi huo muhimu.

“Mradi huu ni muhimu na wa kihistoria kwa nchi hizi mbili, China ingependa kuona mradi huo unaboreshwa ili uweze kutoa huduma ya kusafirisha mizigo na abiria na kwamba kuimarika kwake kutaokoa miundombinu ya barabara kwa kuwa shehena kubwa ya mizigo itasafirishwa kupitia reli hiyo.

Aidha, Balozi Ke alisema kuwa nchi yake inasubiri pia kukamilika kwa taratibu za ndani kati yake na Tanzania ili mradi wa reli ya TAZARA uanze  ili kuboresha usafiri na usafirishaji wa mizigo na abiria kati ya Tanzania na Zambia pamoja na nchi za maziwa makuu.

Balozi Ke alitumia fursa hiyo kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kukusanya kodi, kusimamia matumizi adili ya fedha za umma, kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kupambana na rushwa.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo na mgeni wake, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango alisema kuwa Serikali imeridhia uamuzi wa China wa kufanya upembuzi yakinifu wa mradi huo wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) ili China kupitia taasisi zake iweze kujenga sehemu ya mradi huo.

“Tayari mradi umeanza kujengwa kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, kwahiyo kujitokeza kwa China kutaka kufadhili ujenzi wa mradi huo kutasaidia kukamilisha mradi huo muhimu kwa haraka na kwa wakati” Alisema Dkt. Mpango.

Alisema pia kuwa China imeonesha nia ya kusaidia kuujenga na kuupanga mji wa Dodoma kutokana na nchi hiyo kuwa na uzoefu wa kupanga miji ambapo nchi hiyo imeonesha nia ya  kujenga miundombinu ya elimu, barabara, uwanja wa ndege wa kimataifa-Msalato, kujenga mfumo wa maji safi na maji taka pamoja na majengo ya kisasa.

Kuhusu biashara, Dkt. Mpango alisema wamekubaliana kuwa China itaisaidia Tanzania kukuza kiwango cha biashara ambapo takwimu zilizoko zinaonesha kuwa urari wa biashara kati ya nchi hizo unaonesha kuwa Tanzania imekuwa ikinunua bidhaa nyingi kutoka nchini humo kuliko inavyo uza bidhaa na huduma zake.

“Mwaka 2016 Tanzania iliuza China bidhaa na huduma zenye thamani ya Dola za marekani milioni 460 wakati China iliuza hapa nchini bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.2, kiwango ambacho ni kikubwa karibu mara 5 ya kile tulichowauzia” Alisema Dkt. Mpango.

Ili kuvutia Sekta ya utalii, Tanzania imeiomba China kuanzisha safari ya ndege wa moja kwa moja kutoka China hadi Tanzania ili kuvutia watalii wengi kutoka nchini humo na kwamba utaratibu utafanyika ili Mamlaka ya usafiri wa anga iweze iratibu na kusaini makubaliano ya ushirikiano na hivyo kufanikisha jambo hilo.

“China imeandaa maonesho makubwa ya uwekezaji na biashara ya bidhaa na huduma mbalimbali mwezi Novemba, 2018, hivyo wafanyabiashara wa Tanzania pamoja na  Bodi ya Utalii nchini wahakikishe wanashiriki kikamilifu kwenye maonesho hayo ili kutumia nafasi hiyo kujitangaza” Alisistiza Dkt. Mpango.

Aidha, Dkt. Mpango alieleza kuwa Balozi Wang Ke, amesema kuwa Nchi yake itashiriki katika ujenzi wa miradi ya bandari ili kukuza masuala ya usafiri kwa kuboresha bandari za Tanga, Bagamoyo, Kigoma, Bagamoyo, Dar es Salaam, Mtwara na katika Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika.

Waziri huyo wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango alitoa wito kwa wawekezaji kutoka China na nchi nyingine kuja kuwekeza nchini katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaipeleka nchi katika uchumi wa viwanda.

Miradi mikubwa ambayo China imewekeza na kufadhili hadi sasa hapa nchini ni Reli ya TAZARA, Kiwanda cha Urafiki, ujenzi wa barabara, majengo, ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi dar es Salaam, Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dare Salaam, Ujenzi wa Mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na miradi mingine kadha wa kadha.

TFF Yajibu Hoja ya Zitto ya Kususia Mechi ya Jumapili

0
0
TFF Yajibu Hoja ya Zitto ya Kususia Mechi ya Jumapili
Shirikisho la Soka Tanzania TFF limejibu hoja iliyotolewa na Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe, kuitaka Tanzania isusie kucheza mechi na Libya ili kupinga vitendo vya biashara ya utumwa inayoendelea nchini humo.

Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, afisa habari wa TFF Alfred Lucas amesema suala hilo limefikishwa kwa uongozi wa TFF na litatolewa majibu hivi karibuni.
"Msimamo utatolewa na viongozi wangu mara baada ya kukaa na kutafakari hali halisi kwa sasa, na wenye uwezo wa kukaa na kutafakari ni viongozi wa juu, itakapokuwa tayari mtajulishwa", amesema Alfred Lucas.
Hapo jana Zitto Kabwe ametoa wito kwa TFF kuitaka timu ya Kilinajaro Stars isusie mechi inayotarajiwa kuchezwa na Libya, ili kuonyesha kutokubaliana na vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kuendeleza biasha ra utumwa.

Tanesco Yatoa Ufafanuzi Kuhusu Kukatika Kwa Umeme

0
0
Tanesco Yatoa Ufafanuzi Kuhusu Kukatika Kwa Umeme
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetoa tamko juu ya katizo la umeme la siku ya pili mfululizo baada ya siku ya jana Novemba 30, 2017 shirika hilo kutangaza kuwa kutakuwa na katizo la umeme kwa watumiaji wa umeme wa gridi ya taifa kwa mikoa yote.

Katika hali ya kushangaza watu walijua katizo hilo ni la jana tu kama ilivyotangazwa lakini leo pia, Umeme umekatika ghafla na TANESCO tayari wametolea maelezo ya katizo hilo la umeme kwa siku ya pili kupitia kwenye tovuti yao taarifa hiyo imesomeka kama ifuatavyo.

Shirika la Umeme Tanzania linawataarifu Wateja wake kuwa wakati Wataalamu wetu wanaendelea kurekebisha mifumo yetu ya grid kutokana na hitilafu iliyotokea jana, Imegundulika mifumo ya Gridi haijatengemaa vizuri na hivyo wanaendelea na kazi kuhakikisha huduma ya umeme inarejea.

Hivi Ndivyo..Saluni za Masaji Zinavyovunja Ndoa Dar es Salaam

0
0
MIONGONI mwa vilio vya wanandoa wengi jijini Dar, mbali na hali ngumu ya kimaisha inayosababishwa na vyuma kukaza, matatizo ya kiafya na majanga mengine mengi, ni suala zima la uaminifu kwenye uhusiano wa kimapenzi na magonjwa ambukizi kwa njia ya ngono.

Uchunguzi uliofanywa na Gazeti la Ijumaa ulibaini kwamba, masuala ya kusalitiana yanazidi kushamiri siku hadi siku.
Imebainika kwamba, wengi waliopo kwenye uhusiano wa kimapenzi, wanalia kutokana na mateso ya usaliti.

Uchunguzi huo ulibaini kwamba, kati ya watu mia mbili, wanaoishi maeneo ya Sinza, Mwananyamala, Buguruni, Temeke, Mbagala na Kimara waliofikiwa kwenye utafiti huu, asilimia 75 (watu 151), waliweka wazi kuwahi kusalitiwa.

Ni asilimia 25 (watu 49), pekee walidai kulisikia suala la usaliti kutoka kwa jirani zao.
Pamoja na sababu nyingi ambazo Ijumaa limeelezwa kwenye utafiti huu, lakini saluni ambazo zinatoa huduma za masaji zinatajwa kuwa ni chanzo kikubwa cha usaliti na magonjwa ambukizi.
Katika maeneo hayo yaliyofikiwa, imebainika pia kuwa kati ya mitaa mitatu mpaka minne, kuna saluni moja inayotoa huduma hizo.

UTAZITAMBUAJE SALUNI ZA MASAJI NA HUDUMA ZITOLEWAZO HUMO?

Ijumaa lilikwenda mbele zaidi na kuchimba saluni hizo zinazotoa huduma za masaji. Lilibaini kwamba, zipo saluni za aina nyingi zinazotoa huduma hizo.
Zipo ambazo huandikwa jina fulani alafu mbele yake zinatambulishwa kwa maneno ‘MASSAGE’. Hizi unakuta ni katika nyumba fulani ambazo tofauti na kibao cha utambulisho unaweza kufikiri ni makazi ya mtu.

Mfano; utakuta kibao kimeandikwa Q Massage ambapo ukiingia katika nyumba hizo utapokelewa na akina dada warembo, wanaovutia ambao watakukaribisha na kukueleza aina za huduma za masaji wanazotoa.

Aina hizo ni pamoja na masaji ya kawaida. Hapa mteja anakuwa amevaa nguo zake, lakini analala kitandani, mezani au kwenye kibaraza maalum cha kufanyia masaji na anapewa huduma.

BODY TO BODY
Aina nyingine ya masaji ya mwili kwa mwili (body to body.) Katika aina hii ya masaji mteja anavua nguo zake zote na anayemhudumia anakuwa hana nguo au pengine amevaa nguo ya ndani tu!
Lakini huduma hii pia hutolewa kwenye saluni za kawaida za kiume zilizopo mitaani.

Katika saluni hizi, nyingi, bila kuwa na mteja unaweza usifahamu kama kuna huduma ya masaji inayotolewa ndani yake.

Unakuta tofauti na huduma ya kunyoa, kuremba nywele kwa mafuta ya aina tofautitofauti, ndani ya saluni hizo, kuna kichumba maalum chenye kitanda, meza kubwa au kibaraza kilichojengewa vizuri kwa ajili ya kufanyia masaji.

NGONO HUFANYIKAJE KWENYE SALUNI HIZO?
Ijumaa lilizungumza na baadhi ya watoa huduma hizo za masaji ambazo kwa jijini Dar, hutolewa kwa watu wote, wanaume kwa wanawake;

“Mteja anapokuja unaweza kumwambia kuwa masaji ni kiasi fulani, labda ile ya mwili kwa mwili. Sasa mnapoingia huko chumbani na kuanza kufanya masaji, kwa kuwa mnakuwa wawili tu na hamna nguo, baadaye anageuka na kudai kuwa amezidiwa.

“Anakutaka mfanye mapenzi na anakuongezea pesa. Kwa hiyo wengi wetu unakuta tuna shida na kiukweli kwenye sehemu za masaji, wengine wanalipwa posho za siku tu na wengine hawalipwi kabisa, ni juhudi za kila mtu kupata pesa kwa njia yoyote unapopata mteja.

“Unakuta tunashawishika na kufanya mapenzi kwa sababu ya pesa. Mtu akikolea, anachukua mawasiliano yako na mara kwa mara anakuwa anakuja kwa ajili ya kupata huduma, wakati huu unakuta hataki masaji tena, bali ngono tu,” anasema Amina, mtoa huduma ya masaji kwenye nyumba moja iliyopo maeneo ya Sinza-Kwa Remmy.

Je, ni kwa kiasi gani huduma hii ya ngono imeshamiri kwenye saluni hizi? Ni kweli kuwa machangudoa kwa sasa wamekimbilia kwenye saluni hizi? Hayo na mengine mengi usikose toleo lijalo.

GPL

Mkoa wa Njombe Waongoza kwa Maambukizi ya Ukimwi

0
0
Mkoa wa Njombe Waongoza kwa Maambukizi ya Ukimwi
 Mkoa wa Njombe umetajwa kuongoza kuwa na asilimia 11.4 ya watu wanaishi na virusi vya Ukimwi huku Zanzibar wanaoishi na virusi hivyo ni chini ya asilimia 1.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk Albina Chuwa ametoa takwimu hizo leo Desemba 1 katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani ambayo Kitaifa imefanyika viwanja vya Mnazi Mmoja.

Dk Chuwa amesema mkoa wa Lindi umekuwa wa mwisho kwa watu wenye virusi  vya ukimwi na  idadi ya asilimia  0.1 huku maambukizo kwa Jiji la Dar es Salaam yamepungua hadi kufikia asilimia 4.7 ikiwa na maana watu 133,971 wanaishi na ugonjwa huo.

Mkurugenzi huyo amesema kwa ujumla watu 1.4 milioni nchini Tanzania wanaishi na virusi vya Ukimwi na takwimu hizo ndiyo rasmi hivyo asitokee mtu au kikundi cha watu kupotosha.

"Nasema kwa sababu kuna watu wanakurupuka na kuja na takwimu zao. Naomba watambue takwimu ni fani kama fani nyingine na zina miiko yake," amesema Dk Chuwa

Hata hivyo, Dk Chuwa amesema Serikali haimzuii mtu au kikundi kufanya utafiti ila ni lazima awasiliane na ofisi ya takwimu wapitie dodoso zake kabla ya kuruhusiwa kufanya.

Amesema atakayekiuka na kupotosha takwimu adhabu yake iliyowekwa kisheria ni kifungo cha miaka mitatu au faini Sh10 milioni au vyote kwa pamoja.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi, Justin Mwinuka ameiomba Serikali kutengeneza Sheria zitakazoratibu upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya ukimwi (ARV).

Mwinuka amesema uwepo wa sheria hiyo utasaidia kuwabana watu wanaofanya biashara kupitia dawa hizo.Amesema wagonjwa wengi hawapati dawa kutokana na kushindwa kumudu gharama.

"Tuna changamoto ya uhaba wa dawa na zinazopatikana zinauzwa sasa wagonjwa wanashindwa kupata fedha za kununua,"

Mwinuka pia ameomba watu wanaoishi na virusi vya ukimwi kuingizwa kwenye mpango wa kaya maskini Tasaf ili waweze kutatua changamoto ya uhakika wa lishe.

Katibu wa Bunge Ahoji Stahiki za Tundu Lissu

0
0
Katibu wa Bunge Ahoji Stahiki za Tundu Lissu
Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema amemwandikia barua kaka wa mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, akimtaka alieleze ni stahiki zipi ambazo ndugu yao anastahili apewe na chombo hicho.

Kauli hiyo inayoweza kuibua malumbano mapya katika matibabu ya mwanasheria huyo mkuu wa Chadema, imetolewa siku mbili baada ya Lissu kuhoji sababu za Bunge kutojihusisha na matibabu yake tofauti na sheria zinavyotaka.

Lissu yuko Hospitali ya Nairobi nchini Kenya ambako anatibiwa tangu Septemba 7 aliposhambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana wakati waki ndani ya gari lililoegeshwa nje ya makazi yake mjini Dodoma.

Kauli ya Lissu ilikuwa ni mwendelezo wa kilio kilichotolewa awali na ndugu yake, Alute Mughwai Lissu ambaye alisema alishaiandikia ofisi ya Bunge kutaka ilipie gharama za matibabu ya mbunge huyo.

Katika mahojiano na Mwananchi hospitalini jijini Nairobi, Lissu alisema alimwambia Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ahoji “Bunge liko wapi” kutokana na kutofanya juhudi za kwenda kumuona tangu alazwe takriban miezi mitatu iliyopita.

Pia alieleza kushangazwa na kitendo cha chombo hicho kutogharimia matibabu ambayo anastahilki kisheria iwe anatibiwa ndani au nje ya nchi.

Lakini jana, alipoulizwa kuhusu hatua waliyofikia baada ya kupokea barua ya familia hiyo iliyotaka Bunge lizingatie haki za msingi za ndugu yao, Kagaigai alionekana kutaka maelezo kutoka kwa familia.

“Sisi tumewajibu hizo haki ni zipi kwa sababu kuna allowance (posho) kuna mshahara zote hizo ni haki za mbunge. Hajajibu haki anazoongelea ni zipi,” alisema Kagaigai ambaye alimtaka mwandishi wa Mwananchi asimrekodi sauti yake na baadaye kuandika maelezo hayo katika daftari lake.

Kigaigai alisema barua hiyo imeandikwa na Bunge Jumatatu (Novemba 27) na kwamba bado wanasubiri majibu kutoka kwa Alute kuhusu haki anazotaka Bunge izingatie.

Alipotafutwa azungumzie majibu hayo ya katibu wa Bunge, Alute ambaye kitaaluma ni wakili wa kujitegemea, alisema hajapata barua hiyo ya ofisi ya Bunge.

“Mpaka sasa (saa 7:00 mchana) sijapokea barua yoyote.”

Kuhusu haki hizo, Alute alisema kama ambavyo alizungumza huko nyuma kwamba sheria inamtambua Lissu na hivyo anatakiwa agharimiwe matibabu yake.

“Lissu si wa kwanza au wa mwisho kutibiwa nje. Matibabu ya mbunge kwani ndio yanaanzia Lissu?” alihoji.

“Yanatambulika kisheria kwa hiyo sijajua hiyo barua imetutaka kufanya nini. Ngoja tuisubiri.

“Hivi (aliyekuwa mbunge wa Songea Mjini-CCM, marehemu) Leonidas Gama alivyokwenda India, alijipia au aligharamiwa na Bunge?”

Katika mahojiano kati na Mwananchi jijini Nairobi, Lissu alisema kwa wadhifa wake wa ubunge na Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni anatambuliwa na sheria za Tanzania hususan Sheria ya Uedeshaji wa Bunge na kugharamiwa matibabu si hisani bali ni stahiki zake.

Alisema sheria hiyo inaeleza mbunge anapoumwa atapata matibabu pamoja na gharama nyingine kutoka bungeni pamoja na mtu anayemuuguza ambaye hulipwa nusu ya posho ya mbunge ili kumudu gharama za maisha.

Alisema hilo hufanyika baada ya mgonjwa kuwa amelazwa nje ya eneo la Bunge, akimaanisha Dodoma na bila ya kujali anatibiwa Dar es Salaam, Afrika Kusini, India Marekani au Kenya.

Lissu alisema Spika wa Bunge, Job Ndugai anajua kwamba aliumizwa na ndiyo maana aliwahi kulitangazia Bunge na akaendesha shughuli ya kumchangia ingawa alishangazwa na ukimya wa yeye kutopewa stahiki zake na kuahidi akitoka atazipigania kwani ni haki zake.

Septemba 21, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga kuhusu gharama za matibabu ya Lissu, alisema Serikali haijashindwa wala haijakataa kumhudumia.

“Lissu ni Mtanzania na ni mbunge,” alisema.

“Hata sasa hivi anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Nairobi, lakini kidogo tunaona kunafanyika mambo tusiyoyaelewa kama dhamira ya kufanyika kwa mambo hayo.

“Muwaeleze Watanzania na familia kwamba Serikali iko tayari kumhudumia Lissu popote anapotaka kupelekwa duniani iwapo tutapata maombi rasmi kutoka kwa familia.”

Ufafanuzi wa Waziri Mwalimu ulitofautiana na ule alioutoa Spika wa Bunge, Job Ndugai Septemba 15 bungeni mjini Dodoma wakati akijibu tuhuma za wabunge, hususan wa upinzani waliodai Bunge limeshindwa kumgharamikia Lissu.

Ndugai alisema baada ya kueleza kwamba utaratibu wa bima wanayotumia ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ni wa kutibiwa katika hospitali za Serikali.

“Sisi wote tuna bima pamoja na mawaziri na bima yetu inafanana na ni NHIF. Bima yetu tunatibiwa katika hospitali hii yetu ya mkoa au hospitali nyingine za Serikali, rufaa yetu ni Muhimbili. Baada ya hapo ni kupelekwa India Hospitali za Apollo,” alisema Spika.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Punguza Unene na Kutibu Magonjwa Kwa Kutumia Dawa za Edmark...Bonyeza Hapa

0
0
TUNA DAWA AMBAZO NI VIRUTUBISHO NA CHAKULA MBADALA ZIMEHAKIKIWA NA TFDA

Ni uhakika kwa afya yako, kupunguza uzito na Sumu mwilini, Mafuta/Sehemu Mbaya, Kitambi na Nyama Uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali yaliyoshindikana

Loose Weight Trainer ni Msaada wako Wasiliana Nasi Kwa WhatsApp 0713 777 470

Upate Suluhisho la Afya yako Bila Madhara pia unaweza kujiunga nami ili ufanye Biashara hii Nicheki


Intagram napatikana kwa jina @looseweight_trainer

Watu 6 Washikiliwa kwa Kukutwa na Mifupa ya Albino, Ulimi wa Simba

0
0
Watu sita wanashikiliwa na polisi mkoani Songwe kwa tuhuma za kukutwa na vipande vitatu vya mifupa ya mtu wanayedai kuwa ni albino, pamoja na mafuta na ulimi unaodhaniwa kuwa wa simba.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, Mathias Nyange alisema jana kuwa watu hao walikamatwa juzi saa 7:00 mchana katika mji wa Tunduma wilayani Momba na askari waliokuwa doria.

Alisema watuhumiwa hao walikutwa na mafuta ya simba, mifupa mitatu ya albino, mfupa mmoja wa mnyama ambaye hajajulikana, na vipande viwili vya ulimi, vitu vinavyosadikiwa kuwa ni vifaa vya tiba asili.

Kamanda Nyange alidai kuwa baada ya kuhojiwa, watuhumiwa walikiri kuwa mifupa waliyokutwa nayo ni ya albino waliyemkata mkono mkoani Morogoro.

Alisema kati ya watuhumiwa hao wawili ni wakazi wa Morogoro, wawili wakazi wa Mbozi, mmoja ni mkazi wa Wilaya ya Momba na mwingine ni kutoka Nakonde nchini Zambia.

Nyange alisema watuhumiwa hao wanatarajia kupelekwa mkoani Morogoro ambako ndiko wanakotuhumiwa kutenda kosa.

Wakati huohuo, Nyange amesema watu watatu wanaokadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 25 na 30 wamefariki dunia baada ya kupigwa risasi na askari waliokuwa doria saa 4:00 usiku wa Novemba 30 baada ya kukaidi amri ya kusimama ya polisi ambao waliwatilia shaka.

Baada ya kukataa kutii amri ya kusimama, polisi waliwafuatilia na baadaye watu hao walianza kuwafyatulia risasi, jambo ambalo kamanda huyo alisema liliwalazimisha askari kuanza kujibizana nao.

Alisema baada ya kuwapekua walikutwa na silaha moja aina ya bastola iliyotengenezwa kienyeji inayotumia risasi za short gun ikiwa na risasi moja na pia walikutwa na mapanga mawili pamoja na kipande kimoja cha nondo.

Kimenuka..Polisi Wamshikilia Mwanamke Aliyemvika Mwenzake Pete ya Uchumba Baada ya Video Kusambaa

0
0
Geita. Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mtumishi wa mgodi wa GGM, Milembe Suleiman anayetuhumiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsi moja.

Mfanyakazi huyo ambaye ni ofisa ugavi kitengo cha manunuzi anashikiliwa baada ya ‘video’ inayomwonyesha akimvisha pete ya uchumba mwanamke mwenzake kusambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

Video hiyo ambayo imezua mijadala hasa ikizingatia kwamba iko kinyume cha utamaduni wa Kitanzania na Serikali ambayo imekuwa ikikemea na kupiga marufuku vitendo vya mapenzi ya jinsi moja.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo amesema wanamshikilia kuwa uchunguzi kwa kuwa nchi hairuhusu mambo hayo.

Ofisa Habari wa GGM, Dili Tenga amesema hayo ni masuala binafsi ya mfanyakazi hivyo wao kama mgodi hawawezi kuyazungumzia lakini wanaviachia vyombo vya dola viendelee na uchunguzi wake.

By Rehema Matowo, Mwananchi rmatowo@mwananchi.co.tz

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Tupo Mbagala Rangi Tatu


Simba SC Yabadirisha Ratiba Kuanza Mazoezi Yake Jumatatu

0
0
Simba SC Yabadirisha Ratiba Kuanza Mazoezi Yake  Jumatatu
Vinara wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2017/18 Simba SC, imebadili ratiba yake ya kuanza mazoezi baada ya kuwapa mapumziko wachezaji wake kufuatia kusimama kwa ligi.

Kikosi cha Simba SC sasa kitaanza mazoezi yake rasmi siku ya Jumatatu kwenye viwanja vya Polisi Jijini Dar es Salaam. Awali taarifa ya klabu ilieleza kuwa timu ingeanza mazoezi ijumaa hii.
Simba itakuwa inajiandaa na mchezo wake wa raundi ya 12 ligi kuu soka Tanzania Bara, ambapo itakuwa mgeni wa Ndanda FC kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara.
Ligi kuu soka Tanzania Bara (VPL) imesimama kwa muda kupisha michuano ya kombe la CECAFA Challenge inayotarajiwa kuanza Desemba 3 hadi 17 mwaka huu.

Siwezi Kuomba Support Kutoka Team Diamond- Abdukiba

0
0
Siwezi Kuomba Support Kutoka Team Diamond- Abdukiba
Msanii wa Bongo Flava, Abdu Kiba amesema hawezi kuomba support kutoka team Diamond ingawa hana tatizo nao.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Single’ aliyomshirikisha Alikiba ameiambia Planet Bongo, East Africa Radio kuwa kufanya hivyo atakuwa ameenda kinyume na label yake ya sasa ‘King’s Music’.

“Sidhani, siwezi kufanya hicho kitu, mimi ni Abdu Kiba kama Abdu Kiba ila siwezi kuanza kufanya hivyo kwa sababu kwanza nitakuwa nimewakwaza mashabiki wangu, cha pili nitakuwa nimeruka miiko ya label yangu” amesema.

Alipoulizwa iwapo team zina umuhimu katika muziki, ajilibu; “kitu kama hicho lazima kiwepo kwa sababu ili aweze kupatikana bora ni lazima awepo mpinzani kuweza kumpata bora, s o kitu kama hicho kinatakiwa kiwepo lakini siyo kiwe too much”.

“Still bado naona kawaida, nahitaji kuona mapambano bado yanendelea ili tuweze kujua nani bora” alisisitiza.

Mtuhumiwa wa Mauaji Ajilipua Wakati wa Kesi Yake Ikiendelea Mahakamani

0
0
Mtuhumiwa wa Mauaji Ajilipua Wakati wa Kesi Yake Ikiendelea Mahakamani
Mtuhumiwa wa kesi ya mauaji amejilipua kwa kutumia maguruneti mawili katika mahakama moja mashariki mwa Ukraine.

Mtuhumiwa huyo amejilipua yeye na mtuhumiwa mwenzie wakati kesi yao ya kuua kwa kukusudia ikisikilizwa katika mahakama mjini, Nikopol katika jimbo la Dnipropetrovsk, Ukraine.

Kwa mujibu wa Polisi mjini Nikopol wamesema watu wawili wamefariki dunia na tisa kujeruhiwa kwenye tukio hilo wakiwemo washtakiwa wawili , walinzi wawili na mawakili watatu wa serikali na raia wawili waliokuywa wanasikiliza kesi mahakamani hapo.


Ndani ya mahakama hiyo baada ya mlipuko kutokea.

Mtuhumiwa huyo na wenzake watatu wanatuhumiwa kulifyatulia risasi gari moja na kuwaua abiria wawili mnamo mwezi Februari 2016.

Kwa mujibu wa mtandao wa Ukrainska Pravda taarifa zinasema mtuhumiwa mmoja alitoa maguruneti mawili wakati kesi ikiendelea mahakamani hapo na kuyalipua.

Gazeti hilo likimnukuu Msemaji wa Jeshi la Polisi mjini Nikopol, Yaroslav Trakalo amesema kuwa mtuhumiwa huyo alichukua hatua hiyo baada ya kusikia kwamba kesi hiyo inaahirishwa na kwamba watuhumiwa wanarudishwa rumande.

Rihana Akabidhiwa Mtaa Wenye Jina Lake Katika Kisiwa cha Barbados

0
0
Rihana Akabidhiwa  Mtaa Wenye Jina Lake Katika Kisiwa cha Barbados
Kisiwa cha Barbados, kilichopo nchini Marekani kimemtunusu mwanamuziki Rihanna kwa kumpa mtaa yenye jina lake.

Uongozi wa eneo hilo umetoa jina la mtaa huo kwa msanii huyo anayetoka katika kisiwa hicho siku ya uhuru wa kisiwa hicho.

Baada ya kupewa jina la mtaa, Riri ameushukuru uongozi wa kisiwa hicho kwa kumpatia heshima hiyo.

“My home. My whole life was shaped on this very road. I was just a little island girl riding bikes, running around barefoot, and flying kits in the cemetery, but I had BIG dreams. Dreams that were born and realized right here,” amesema Riri

Akaongeza “Thank you to my family, my country, and the people of Westbury New Road,” she continued. “You will forever be a part of who I am, and for that, I am honored to have this place named after me.”

Kwa miezi miwili mfululizo Rihanna amekuwa akipata dili za kutokea katika majarida makubwa kama Vogue Arabia, Vogue Paris,na Dazed.





Ligi Kuu Yasimama Kupisha Kombe la Chalenji la CECAFA

0
0
Ligi Kuu Yasimama Kupisha Kombe la Chalenji la CECAFA
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa sasa imesimama kwa takribani majuma mawili sababu kubwa ni kupisha Kombe la Chalenji la CECAFA michuano inayoratibiwa na Baraza la Soka kwa nchi za Afrika Mashariki (CECAFA).

Kutokana na michuano hiyo kuingilia ratiba, kwa mujibu wa Shirikisho la soka nchini (TFF), Desemba 22, 23, 24 na 26, zitakuwa siku za mechi za kuwania Kombe la Shirikisho la Azam yaani Azam Sports Federation Cup (ASFC).

Mechi zitakazochezwa katika siku hizo zitafahamika Desemba 5, mwaka huu ambako imepangwa droo ya timu 64 zitakazocheza Raundi ya Tatu ya ASFC.

Timu 64 maana yake ni kuwa timu 16 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara; timu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na timu 24 ambazo zimefuzu kutoka hatua awali; ya kwanza na pili.

Baada ya michezo hiyo, ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom itaendelea tena kwa michezo ya raundi ya 12 itakayofanyika Desemba 29, 30 na 31 kabla ya ligi tena kusimama kupisha michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Michuano ya CECAFA itafikia ukomo Desemba 17, mwaka huu na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa ratiba mara baada ya michuano hiyo.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images