Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

WANAWAKE WA DAR NA MAPENZI ACCORDING TO MONEY LEVEL

0
0
Wanawake wa Dar wana Viwango
vyao vya Hela..
Ukiwa unampa 50,000-90,000
utakuwa unaitw aJina lako tu,
Goodmorning Kelvin..Hallow Kelvin
How is your Day...Goodnite Kelvin

Ukiwa unampa kati ya 100,000 na
150,000 utakuwa unaitwa
DEAR...Morning Dear..Umeamkaje
Dear..Dear Umekula??Usiku mwema
Dear usisahau kuniamsha Asubuhi

Ukiwa unatoa kati ya 200,000-300,000 hapa utakuwa
unaitwa BABY...Baby Hows ur
day..Baby naumwa kweli leo...Baby
naenda Mwenge see u later.

Ukihonga 300,000 na kuendelea
hawa ndo wanaitwa HUBBY AKE...Utapendwa wewe hadi
ushaangae...Kila kitu Hubby
Ake...Hubby nimejikwaa...Hubby ndo
nafunga mlango...Hubby kuna
Mende chumbani njoo tulale
wote...Hubby hivi unanipenda??NA swali lao KUU,Hubby hivi utanioa
lini??

Chagua jina unalotaka...Mahaba ya
siku hizi ni kama MENU ya MPESA,
Unajihukumu mwenyewe
Wengi mtakuwa mnaishia kuitwa DEAR na BABY tu...Tikisa Wallet
kidogo na wewe kabla hujafa uitwe
HUBBY AKE

NB:KAMA HUNA HELA,WANAWAKE WAZURI UTAISHIA KUWAITA SHEMEJI

KUTANA NA CHACHA MAKANGE KIJANA ANAE ISHI KWENYE HANDAKI JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Chacha Makenge (36) akiwa amepozi ndani ya chumba chake 'handaki'.
 Akitoka katika handaki lake.

...Akiwa nje ya handaki lake.

Chacha akifunika mlango wa handaki lake.

Akizidi kufunika handaki lake.
Akimalizia kufunika nyumba yake.
Na Makongoro Oging’/GPL
DUNIA haiishi vituko! Chacha Makenge (36) mzaliwa wa Kijiji cha Kisangula, Mtukula, Serengeti mkoani Mara anaishi jijini Dar lakini ndani ya handaki aliloligeuza chumba kwa miaka minne sasa, ni ajabu lakini ni kweli.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni nje ya handaki hilo lililopo mita chache kutoka majengo ya biashara ya Mlimani City, Makenge alisema alichukua uamuzi huo baada ya rafiki yake (jina linahifadhiwa) kumchomea nyumba na kuteketeza samani zote.

“Ilikuwa mwaka 2009 mwanzoni rafiki yangu huyo ndiye alinipa sehemu ya kiwanja chake nijenge nyumba. Nikawa  naishi hapo huku nikiendelea na shughuli zangu za kila siku.

“Siku moja akabadili mawazo, akanitaka nihame katika eneo lake bila kunipa sababu, nilimwomba anipe muda nitafute pa kwenda.

“Julai 2009 akaja na polisi, akanikamata na kunipeleka Kituo cha Polisi cha Stakishari, nilipowauliza kosa langu, hawakunieleza.

“Baada ya siku mbili majirani walikuja kuniona na kuniambia kwamba nyumba yangu imechomwa moto na kila kitu kilichokuwa ndani kimeteketea, aliyefanya hivyo ni rafiki yangu. Nilijisikia vibaya sana.

“Siku iliyofuata majirani walikuja tena kituoni wakaniwekea dhamana. Nilipofika kwangu nilikuta majivu tu, iliniuma sana, nililia lakini sikupata ufumbuzi. Kwa vile nilikuwa sina pa kwenda ilibidi niwe nalala palepale nilipochomewa nyumba nikisaidiwa chakula na majirani.

“Siku iliyofuata, saa nne usiku nilivamiwa na watu wanne, wakiwa na mapanga na marungu, nilipambana nao mpaka wakaondoka. Kesho yake nilikwenda kwa mwenyekiti wetu wa serikali ya mtaa, Jumanne Malima kumweleza yaliyonipata, alisikitika, akaniandikia barua kwenda Polisi Stakishari.

“Nilipofika kituoni sikusikilizwa, badala yake walinikamata tena na kuniweka ndani wakidai kwamba nimefunguliwa kesi ya kumjeruhi mtu kwa panga. Hawakukubali niwekewe dhamana.

“Julai 31, 2009 nilifikishwa Mahakama ya Mwanzo Ukonga na baadaye nilipelekwa Mahabusu ya Gereza la Keko, nikawa napelekwa mahakamani hadi Septemba mwaka huo ambako nilihukumiwa kwenda jela miezi 9.

“Nilitumikia maisha ya jela hadi Desemba 10, 2009 nikatolewa kwa msamaha wa Rais Jakaya Kikwete. Nilikwenda kuishi kwa ndugu zangu huku wakifuatilia sababu ya kufanyiwa vitendo hivyo bila mafanikio.

“Maisha ya kwa ndugu hayakunifurahisha kwani hata wao walikuwa na majukumu mengi, niliamua kuendelea na kazi zangu za sanaa pia utunzaji wa mazingira na bustani kwa watu wakawa wananilipa fedha.

“Ndipo nilipoamua kutafuta sehemu iliyotulia ili niweze kuishi, nikapata hapa, ni jirani na Mlimani City. Nilichimba handaki kubwa kama unavyoliona, kwa chini kuna kitanda ninacholalia.

“Kwa hakika hapa sipati shida, wala kelele. Kwanza ni tulivu sana, nimefikia hatua ya kuishi kama mnyama kutokana na mateso na bugudha nilizopata, wengi hawajui nilipo, nipo katika pori hili kwa miaka minne sasa,”alisema Makenge.CHANZO GPL

HALIMA KIMWANA'S FAB BIRTHDAY PARTY

0
0















Muda wa zawadi ukafika


Hatari sana kaka mtu alifanya yake


Mambo ya nyekundu nyekundu hatari tupu



Ommy Dimpoz nae alifanya yake na ilikuwa hatari tupu




Habari ndo hiyo mambo ya nyekundu 


Chegge nae hakubaki nyuma




Dolar nazo zilihusika
Diamond akitoa burudani









THE END

PICHA:KIBAO KATA KWENYE BIRTHDAY YA HALIMA KIMWANA

LULU AOGOPA UBONGE AAMUA KUINGIA GYM KUPUNGUZA MWILI, TAZAMA PICHA HAPA

0
0

Baada ya Kuona Mwili unazidi Kuongezeka na Kuwa Bonge Nyanya Msanii wa Filamu Lulu Michael sasa Ameamua kuingia Gym Kupunguza huo mwili ..Hizo ni Picha Alizoshare na Mashabiki zake

MCHUNGAJI GWAJIMA NDANI YA KASHFA NZITO, WASAIDIZI WAKE WAMPIGA MWANDISHI WA HABARI HADI KUTENGUA KIUNO

0
0

Mchungaji Josephat Gwajima na wasaaidizi wake wameingia kwenye kashfa nzito ya kumshambulia mwandishi wa habari Mkoani Tanga Ndugu Eliasi Mokiwa hadi kumtengua kiuno chake kisa kikiwa kuwapiga picha misukule wake aliodai kuwagomboa mikononi mwa wachawi wa Tanga.

Habari za uhakika zilizothibitishwa na mwandishi wetu aliyekuwepo eneo ya tukio huko Mkoani Tanga ambako Gwajima na wafuasi wake waolikuwa wakifanya hudia misukule.

Akizungumzia tuki hilo mwandish huyo ambae anaripotia gazeti la Jibu la Maisha lakini ni mwanafunzi wa chuo cha Royal College ngazi ya Cheti kilichopo Mkoani humo alisema ilikuwa siku ya tarehe moja desemba 2013 saa kumi za jioni aliwa na mwandishi wa gazeti hili Mkoani Tanga  Bwa Sadiki Amidu na wakiwa kwenye viwanja vya Tangamana wakati mchungaji huyo akitangaza kuwa kuna msukule amedondoka katikati ya watu.

Mwandishi huyo anasema alisogea na yeye ili kushuhudia msukule huyo pamoja na kumpiga picha lakini katika hali isiyotarajia baada ya kupiga picha moja alishtuka amepaishwa juu kumbe kuna msaidizi wa Gwajima ambae alimpiga mtama ulimpaisha kimo cha ng’ombe na kudondoke kiuno.

Mara baada ya kutua nchini mwandishi huyo anasema alisikia kitu flani kimelia kwenye kiuno chake kumbe nyonga ilikuwa imeshateguka ambapo wakati akigragara chini walikuwa wasaidiz wanne na walimbeba juu hadi nyuma ya jukwaa na kuanza kumsurubu, wakati huo Mchungaji Gwajima alikuwa anashuhudia mchezo mzima bila kutoa kauri yeyote.

Mwandishi huyo aliendelea kueleza “ Nilipigwa sana huku wakinisachi mifukoni na kunichukulia pesa yangu yote ambayo ilikuwa ni shilingi elfu tano ya nauli huku wengine wakiniuliza kama pesa nyingine nimeweka wapi lakini kiwajibu kuwa sina pesa nyingine na kuwaeleza mimi ni mwandishi wa habari hivyo wasinidhalilishe kiasi hicho lakini hawakutaka kusikia” Alisema Eliasi

Hata hivyo Eliasi aliendelea kusema kuwa “ Mwandishi mwezangu baada ya kuona vile alitimua mbio kuokoa maisha yake kwani walishashtukia kuwa tuko wawili hivyo huenda wangetukamata wote, baadae alikuwa mchungaji mmoja mwanamke ambae sikufahamu labda huenda alikuwa mke wa Gwajima kutokana na heshima waliyompa muda ule kwani wakiwa bado wananishambulia kwa ngumi za chembe na walipomuona mama huyo waliniacha haraka na kuganda” Alisema mwandishi huyo

Baada ya mama huyo kuuliza kosa langu nini wakamueleza kuwa kuwa mimi nimepiga picha misukule na nilikuwa navizia watu waliokaa uchi na kuwapiga pamoja na misukule yao, ambapo mama huyo aliamuru niachiwe huru lakini kama hizo picha za misukule zipo kwenye kamera yangu zifutwe halafu wanirusu na mama huyo aliangalia kwenye kamera na kukuta hamna picha yoyote ya aina hiyo.

Hata hivyo  Eliasi aliendelea kusema “Nilivyoachiwa huku nikiwa nyang’anyang’a nilijisogeza kidogo kidoga hadi kituo kikuu cha Polisi na kutoa taarifa na wakampatia Jarada la Upelelezi PE namba 71 -2013 pamoja PF3 ambapo alikwenda kwenye Hospitali ya Jiji ambako walimpatia matibabu hadi siku iliyofuta ambapo alirudi na ile PF3  tena Polisi.

Aidha kutokana na mkutano huo kuwa isku ya mwisho kwenye viwanja hivyo na wakahitaji kuongeza siku za mkutano lakini walizuiwa kibari badara yake walihamishia mkutano huo kwenye viwanja vya  Ridochi. Na baada ya siku mbili Polisi wakiwa na Deffender walikwenda kuvamia mkutano huo kwa lengo la kuwakamata wale wote walihusika na tukio la kumpiga na kujeruhi mwandishi huyo, lakini kwa bahati mbaya mwandishi huyo akiwa ameandamana na Askari hakuwata wale walimpiga hivyo na kufanya Polisi kuendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Baada ya taarifa hizo Maskani Bongo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga “RPC” Masawe ili kuzungumzia ishu hiyo ambapo alipatikana lakini kwa bahati mbaya akajibu kuwa yuko kwenye mafunzo Moshi hiyo tumtafute Kaimu wake ambae nae alipopigiwa simu simu hiyo iliita tu bila kupokelewa.

Misukule ya mchungaji Gwajima imekuwa na utata mkubwa sana kwenye jamii kutokana na wengi kuamini kuwa ni propaganda tu za kujizolea waumini, kwa mfano misukule wote aliowatoa Mkoani Tanga wanadaiwa ni wa kutengenezwa ndiyo maana amekuwa mkali kwa waandishi ili wasije kuripoti uwongo huo.

Hata hivyo kwa wakazi  mji wa Tanga wamesikitishwa na tukio hilo na kupigwa kwa mwandishi huyo maarufu ambae ni ndugu moja na mtangazaji wa TBC1    Domonic Mokiwa.

MBUNGE AMPONDA MISS TANZANIA KWA KUTOKUJUA KUONGEA KISWAHILI

0
0
Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred hajui Kiswahili? Well, tuliowahi kukaa naye kidogo tunaweza kumtetea kuwa anakijua haswaa, sema hupendelea zaidi kuongea kimombo. Pengine ndio maana mbunge wa viti maalum kutoka Zanzibar, Rukia Ahmed anahisi mrembo huyo haijui lugha yake ya taifa.

Akiongea bungeni leo, Bi. Rukia amesema Brigitte Alfred hafai kuiwakilisha Tanzania kwakuwa hawezi kuzungumza Kiswahili. Mbunge huyo alienda mbali zaidi kwa kupendekeza mashindano ya Miss Tanzania yafutwe na badala yake yawekwe mashindano ya Sayansi kwa manufaa ya taifa.
Akijibu kauli hiyo, Brigitte amesema: Meanwhile as our county suffers from 3rd world problems this is what is being discussed bungeni. I would love to meet this this woman! Asante mama,” ameandika mrembo huyo kwenye Instagram. “All of your comments give me hope that there’s still sensibility out here,” aliongeza.
“Mh.Rukia amekosa mada bungeni?*rollingmyeyesoutloud*,” alitweet.
“Anko in the office must be jumping for joy right now-they love to say ‘I told you so’-In Kiswahili ofcourse.”
Hata hivyo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara alisema serikali haiwezi kuyafuta mashindano hayo kwakuwa yana umuhimu mkubwa kwa taifa na yamekuwa yakiitangaza nchi na shughuli za utalii.

WEMA JEURI YA FEDHA KWISHA!, KIGOGO ANAYEMUWEKA MJINI AFILISIKA

0
0

Stori: Oscar Ndauka na Richard Manyota
NI kweli hakuna marefu yasiyokuwa na ncha? Kama ni kweli, basi ile jeuri ya fedha ya Miss Tanzania mwaka 2006 ambaye pia hufanya vyema kwenye gemu la sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu inadaiwa imefikia nchani, Risasi Mchanganyiko limepashwa ‘ei tu zedi’.

Kwa mujibu wa chanzo makini, hali ya kifedha ya staa huyo si nzuri kiasi kwamba kwa sasa amekuwa mtu wa kushinda ndani kwa kuwa hana mpunga unaomuwezesha kwenda kujirusha kama zamani. 
SABABU NI NINI HASA?
Chanzo kilidai kwamba, binadamu aliyekuwa akimmwagia manoti staa huyo aliyetajwa kwa jina moja la Clement ambaye ni mwajiriwa wa Ikulu jijini Dar, yu hoi kwa kipato baada ya kunyofolewa kwenye kitengo kilichokuwa na uwezeshaji mwingi wa fedha.

Inadaiwa kuwa, baada ya Clement ambaye ni mume wa mtu, kuondolewa kwenye kitengo hicho amepelekwa sehemu nyingine ambayo mchana kutwa ni kupiga miayo mpaka muda wa kutoka kazini. 
MKONO WA MKEWE WATAJWA
Katika madai hayo, inasemekana mke wa Clement (jina tunalo) ana mkono wa kile kilichompata mumewe, kuondolewa kwenye kitengo chenye ulaji na pia amekuwa akiwawinda wawili hao ili awafanyie fumanizi kwa sababu Clement ni mumewe wa ndoa.

KILICHOTOKEA SASA
Chanzo kikaendelea: “Baada ya kuondolewa kwenye sehemu yenye fedha na kutupwa kwenye ukame, jamaa akaanza kupata tabu kwani fedha alizokuwa akimpa Wema zamani zikawa hazipo.
“Hilo likamwathiri na Wema mwenyewe kwani ile jeuri mliyokuwa mnamuona nayo akiifanya kwa rungu la fedha, mara sherehe, mara kumlipia Kajala (Masanja) makahamani (Kisutu), mara kwenda baa na wapambe imekatika ghafla.
“Siku hizi Wema ndani na yeye, yeye na ndani. Naamini hata mkienda kwake muda huu (juzi Jumatatu saa 5 asubuhi) mtamkuta.” 
INADAIWA AMEUZA MAGARI MAWILI
Habari zaidi kutoka chanzo hicho, hali ilipozidi kubana sana, Wema aliamua kuuza magari mawili kati ya matatu anayomiliki ili apate fedha za kuendelea kujikimu katika maisha ya kila siku.
Magari hayo mawili yanasemekana ni Toyota Mark II GX 110 na Toyota Harrier na kubakiwa na Audi Q7. 
YALIYOMPATA CLEMENT 
Habari zinazidi kudai kwamba hali ikazidi kuwa mbaya kwa Clement kiasi kwamba alijikuta akikabwa koo na benki moja ya jijini Dar es Salaam ambayo aliiomba mkopo wa Shilingi mil. 120 akitumia hati ya nyumba ambayo pia si yake.
Benki hiyo ilipozidi kumbana, mkewe (sasa wametengana) ambaye naye anadaiwa kuwa ‘mzuri’ kwenye fedha alikwenda kulipa fedha hizo benki ili nyumba ya watu isinadiwe na benki hiyo iliyokuwa haitaki mambo ya utani kwenye marejesho. 
Madai mengine ambayo hayajathibitishwa yanasema kuwa, mtikisiko huo wa kifedha kwa Clement umesababisha awe ‘choka mbaya’ kiasi cha sasa kuanza kupiga mizinga kwa rafiki zake. 
WEMA ASAKWA ASEME UKWELI WAKE
Baada ya kupokea ishu hiyo, Risasi Mchanganyiko liliamua kumsaka Wema ili aseme lolote kuhusiana na tuhuma hizo.
Saa 4:32 Wema alipigiwa simu yake ya mkononi ambayo iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa hata pale iliporudiwa tena na tena.
Baada ya jitihada hizo kugonga mwamba, gazeti hili liliamua kumwendea hewani meneja wake Martin Kadinda ambaye naye hakupokea simu licha ya kupigiwa zaidi ya mara tatu.
Risasi Mchanganyiko halikukata tamaa, kwani ni haki ya msingi kwa Wema kuongelea suala hilo. Likampigia msaidizi wake wa karibu anayeitwa Pat Man, yeye alipokea, akaulizwa kuhusu bosi wake huyo, akasema:
“Wema anaumwa (hakutaja ugonjwa), ametoka hospitali sasa hivi  (hakusema hospitali gani) yuko nyumbani.”
Mapaparazi wetu wakafunga safari kutoka Bamaga – Mwenge, Dar yalipo Makao Makuu ya Nyumba ya Magazeti Pendwa Bongo, Global Publishers hadi nyumbani kwa Wema - Makumbusho (lakini ni Kijitonyama).
Getini alikutwa mlinzi mahiri kwa mwonekano ambapo alipoombwa kumwita Wema au kumwambia kuna waandishi wa Global wapo nje, alisema:
“Mh! Kwa kweli si rahisi kutoka, amelala anaumwa... alikwenda hospitali amerudi muda si mrefu.”
Alipochombezwa kwa maneno ya ‘kisiasa’ kwamba awaambie wasaidizi wake wa ndani wakamwamshe, alikataa akisema litazuka timbwili ambalo yeye hakuwa tayari kuliona.
“Bosi akilala huwa hapendi kuamshwa, hasa kama hayuko sawa. Watu wanaomwamsha ni wale wenye ahadi naye,” alisema mlinzi huyo. 
WEMA ATUMIWA MESEJI
Baada ya kuondoka nyumbani kwa Wema, Risasi Mchanganyiko lilimtumia ujumbe mfupi (SMS) ‘mreeefu’ wenye madai yote na ikaonesha ‘delivered’ kwenye simu ya Wema, lakini pia haikujibiwa. 
TUNARUDI KWA CLEMENT  
Simu yake haikuwa ikipatikana hewani alipopigiwa ili na yeye apewe nafasi ya kusema lolote kuhusu sakata hilo. 
MKE WA CLEMENT AVUNJA UKIMYA
Risasi Mchanganyiko liliamua kumsaka kwa simu ya mkononi mke wa Clement ambapo alipopokea na kusomewa mashitaka ya mumewe na nafasi yake kama shahidi muhimu alikiri hali ya jamaa kuwa tete kimfuko.
“Kuhusu hilo la nyumba ni kweli ilikuwa inadaiwa na benki (aliitaja jina) na walitaka kuinadi ili wapate fedha zao, lakini nikaingilia kati ili kulinda heshima ya familia.
“Unajua ile nyumba kuna mtu alituuzia, kwa hiyo Clement alitoa kiasi cha fedha lakini hakumalizia na akatumia hati ya nyumba kwenda kuombea huo mkopo. Kwa sababu benki walikuja juu nilitafuta mtu akainunua, kiasi cha fedha nikammalizia aliyetuuzia na kulipa benki,” alisema mwanamke huyo. 
KUHUSU KUMFANYIA FITINA MUME AKAHAMISHWA KITENGO
Huyu hapa mke wa Clement: “Hilo si kweli bwana. Kwanza mimi ndiyo nilimfikisha pale alipofika. Sasa mtu nimuinue mwenyewe nitamfanyiaje fitina?
“Kwanza mimi siko naye siku hizi. Nilipoona anachukua magari ya nyumbani na kuyapeleka huko kwa nani sijui (Wema) nikaamua kukaa pembeni na kunyamaza kimya.
“Kama ni mabalaa anayapata hukohuko aliko, nisisingiziwe mimi kwa lolote lile.”
KUHUSU KUMWANDALIA FUMANIZI WEMA
“Aaa wapi! Nimwandalie fumanizi la nini? Yeye ana maisha yake mengine mimi niko na mambo yangu, muda huo sina kabisa, yaani niko bize sana,” alisema mwanamke huyo huku akidai muda huo alikuwa akidraivu. 
PRODYUZA WA WEMA ALIJUA HILI?
Wiki mbili zilizopita, gazeti damu moja na hili, Ijumaa Wikienda liliandika katika ukurasa wake wa mbele habari yenye kichwa; MAGARI YA WEMA YAGEUZWA GESTI.
Katika habari hiyo, Wema alidaiwa kumtimua kazi prodyuza wake katika Kampuni ya Endless Fame, Rashid Mohammed ‘Chid Classic’ kwa sababu ya kumtuhumu kufanya ufuska kwenye magari yake maeneo ya Ufukwe wa Coco, Dar.
Siku chache mbele, prodyuza huyo alifunguka katika gazeti lingine pendwa ndani ya mjengo, Amani kuwa, Wema ‘amechoka’ siku hizi, halipi mishahara wafanyakazi wake na alitaka yeye awe kuwadi ndiyo wangeendana jambo ambalo yeye hakuwa tayari. 

Baadhi ya habari zilizowahi kuandikwa na magazeti ya GPL kuhusu jeuri ya fedha ya Wema.
HABARI NYINGINE YA MJINI
Yapo madai kuwa, kutokana na maswahibu hayo ya kuwa kwenye wakati mgumu kifedha, kampuni yake imeanza kudoda na mbaya zaidi, marafiki zake anaokuwa nao kwenye raha, wamemkacha na kumwacha akihangaika mwenyewe.
“Msiniandike gazetini lakini ukweli ni kuwa, huu ndiyo wakati wake wa kujifunza kuchagua marafiki. Ona sasa, wale wote aliokuwa akila nao raha, wamekaa pembeni. Ni tatizo sawa, lakini pia ni funzo kwa upande mwingine,” alisema mpambe mmoja anayefanya naye kazi kwa karibu sana.
GPL

SINEMA ZA KIBONGO LINI ZITABADILIKA?

0
0
KWENU,
Watayarishaji wa sinema za Kibongo. Hongereni sana na kazi. Mimi nipo sawa na mishe zangu zinaendelea vyema kabisa. Leo nimewakumbuka kwa barua kwa lengo la kuwekana sawa kidogo.
Ni kweli kuna tofauti kubwa sana katika sinema zetu za sasa na zile za miaka mitano iliyopita lakini kiukweli bado kuna changamoto nyingi.  Kuna makosa mengi madogomadogo ambayo yanaachwa na yanaweza kuondolewa na kufanya sinema kuwa nzuri ya kuvutia.

Huko nyuma makosa yalikuwa mengi sana; taa, picha, hadithi na mengine lakini sasa kidogo  yamepungua kwa kiasi kikubwa. 
Ndugu zangu, soko la sinema hivi sasa limepanuka. Ni ajira inayojitosheleza, tujitahidi kuondoa kasoro ndogondogo ambazo zinaweza kuondolewa na kuifanya sinema kuwa bora. Nimeona mengi lakini yenye umuhimu zaidi ni haya;

UHUSIKA/UHALISIA
Bado kuna makosa ya msanii kuvaa uhusika katika uhalisia wa tukio sawasawa. Makosa haya, zaidi yameonekana katika namna ambavyo stori inavyomhitaji msanii. Utakuta msanii anaigiza yupo kijijini lakini eti ameweka nywele wave au ametokelezea na pamba za kijanja.

Tabia ya kuwafanya walinzi wa getini kama machizi, bado inaendelea. Aliyewaambia kuwa kila mlinzi anayekaa getini ni komediani ni nani? Bado kuna tatizo hapa.

MWENDELEZO
Hata mastaa kabisa wanashindwa namna ya kudhibiti hili. Msanii amecheza amevaa nguo fulani, siku ileile kwenye tukio lingine anaonekana amevaa nguo nyingine, tena akiwa na mtindo mwingine wa nywele!
Lakini pia kumekuwa na tatizo la msanii kurudia nguo moja mara nyingi, hata kama stori inaeleza kuwa tukio linalofuata ni BAADA YA MIAKA MITATU! Hii siyo sahihi. Halafu inawezekana vipi msanii akaigiza akiwa amenyoa nywele staili moja mwanzo hadi mwisho?

Hilo linawezekana, lakini ni kwenye visa vinavyoonesha kweli kiliisha ndani ya siku moja. Mfano mzuri ni Sinema ya Swahiba. Ni kisa kizuri, kinaanzia mchana wa siku moja na kuishia asubuhi ya siku inayofuata. 
Mwanamke amesuka rasta katika mtindo fulani, basi ataonekana hivyohivyo, mwanzo hadi mwisho wa filamu. Hiyo siyo sahihi hata kidogo. Jitahidini muwe makini katika eneo la mwendelezo (continuity) ili kufanya sinema zenu kuwa zenye ubora.

MATUKIO YA KUCHOSHA!
Hili limelalamikiwa sana. Kwanza, sinema nyingi utakuta zina sehemu mbili (Part 1 & 11), lakini ukiingia sehemu ya pili, hakuna kitu. Ni marudio tu ya kilichoonekana sehemu ya kwanza au kurefusha matukio bila sababu.
Mfano, unaweza ukakuta kipande kinachukua mpaka robo saa. Mtu anaonekana anaamka. Anajinyoosha. Anajiangalia kwenye kioo. Anakwenda bafuni, unasikia maji yakimwagika. Anatoka. Anajikausha. Anavaa kisha anatoka nje na kuingia kwenye gari.

Hii haiko sawa. Kwani lengo la kufanya hayo yote ni nini? Lazima kila onesho (scene) liwe na sababu. Mfano, kama unataka kumuonesha mhusika akiamka, basi kuna sababu, kama kuangalia saa na kugundua amechelewa kazini, kumkosa mwenzake kitandani n.k.

Lazima kuwe na sababu. Wengine mnafurahisha kweli! Mhusika ataingia kwenye gari na bado ataonekana akiendesha barabara nzima mpaka anaingia ofisini... ni robo saa nzima! Yapo mengi lakini haya machache mkiyarekebisha mtapaisha filamu za Kibongo.

Uamuzi wa kupokea au kuacha, uko mikononi mwenu wenyewe! Kazi kwenu.

Yuleyule,
Mkweli daima,
GPL

CANDY & CANDY KUZINDUA FILAMU MPYA YA BABY MADAHA "THE GAL BLADDER"

0
0

Candy  & Candy are launching their new movie which they say will be the biggest Blockbuster of the year entitled The Gal Bladder.

The premiere is going to be a type of motion pictures in a red ca rpet affair with an enduring influence whereby major Tanzanian artistes are expected to walk the red carpet. The premiere will be happening this Sunday 22nd December 2013 from 6pm to 11pm at Golden Tulip Hotel Dar es Salaam Tanzania.

This comes just days after trouble was reported to be brewing in Candy & Candy Records  after they signed a new artiste Lil Gee from Nigeria and released a new single “one of a kind” with him and immediately wanted to follow it up with a video, but another artiste had a problem with this.

That aside, we are looking forward to seeing this new movie.

MAWAZIRI MIZIGO WALIKWEPA RUNGU LA JK

0
0
Wengi wakana kuhojiwa na Kamati Kuu udhaifu wao
*Nape awasuta, Lema amlipua Waziri Medeye
HOFU ya mawaziri wanaodaiwa kuwa mizigo imezidi kuongezeka, baada ya wengi wao kujaribu kukwepa rungu la Rais Jakaya Kikwete la kutupwa nje ya Baraza la Mawaziri.

Hofu ya mawaziri hao ambao wiki iliyopita walihojiwa na Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma, wameibuka na kudai hawakuitwa mbele ya kamati hiyo kutokana na kushindwa kutimiza majukumu yao kama inavyodaiwa.

Wakizungumza na RAI kwa nyakati tofauti mjini Dar es Salaam jana, baadhi ya mawaziri hao walisema wao si mawaziri mizigo, bali ni mawaziri kamili wanaofanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.

WATU SABA MBARONI KWA MAUAJI YA ALIYE KUWA MWENYEKITI WA CCM MWANZA

0
0
JESHI la Polisi mkoani Mwanza, linawashikilia watu saba kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), marehemu Clement Mabina (57). Akizungumza na RAI jana ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola alisema hadi sasa Jeshi la Polisi linaendelea kufanya msako mkali ili kubaini wahusika wengine.

Alisema kwa mujibu wa taarifa za mashuhuda wa tukio hilo, wameeleza mauaji hayo yalifanywa na watu zaidi ya saba, hivyo jeshi hilo bado linaendelea kuwasaka wengine.

“Ni kweli tukio lilitokea jana (juzi) kati ya saa 6 na 7 mchana, ambapo marehemu alifika hapo kuweka mipaka katika eneo hilo, ambapo wananchi walitaharuki kuona mipaka ikiwekwa wakati bado kuna mgogoro wa muda mrefu.

“Baada ya hapo wananchi walivamia eneo hilo na kumhoji marehemu ndipo mvutano ulipoibuka ndipo marehemu alipojaribu kujihami kwa kutumia bastola yake na kupiga risasi juu.

“Lakini katika vurugu hizo, risasi moja ilimpata kijana mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Temeri Malimi (12) na kufariki papo hapo.

“Kutokana na kifo hicho, wananchi waliendelea kumshambulia marehemu kwa kutumia silaha za jadi hadi mauti yalipompata, ambapo miili yote imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando,” alisema.

Hata hivyo, Kamanda Mlowola alikataa kutaja majina ya watuhumiwa kwa kile alichodai bado jeshi hilo linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili hatua za kisheria ziweze kuchukulia.

Kwa upande wa msemaji wa familia ambaye ni kaka wa marehemu, Timoth Mabina alisema wamesikitishwa na kifo hicho.

Baadhi ya viongozi waliofika nyumbani kwa marehemu ni pamoja na Meya wa Ilemela, Henry Matata (Chadema), Katibu wa CCM Wilaya ya Magu, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Desdery Kiswaga na viongozi wengine.

Taarifa hii imeandaliwa na John Maduhu, Benjamin Masese na Peter Fabian, Mwanza

CCM MKOA WA ARUSHA WAHAHA KUTAFUTA MGOMBEA WA KUSHINDANA NA CHADEMA

0
0
CCM mkoa wa arusha hasa jimbo la arusha mjini, wanahaha kutafuta cha kufanya hasa kipindi cha uchaguz mdogo.katika uchaguz uliotangazwa wa madiwan kwa kata zilizowazi kote nchini mwakanin,ccm mkoa wa Arusha wanahaha kutafuta mgombea wa kushindana na upinzan hasa chadema katika kata ya sombetini kwan wengi wanaogopa kuaibika kama ile 4 bila.
Nmebahatika kutembelea kata hyo ya sombetin nakubain kuwa asilimia kubwa ya wananchi hawatak kusikia ccm,huku wagombea wengi wakitaka kujinad chadema.ofisi za ccm nyngi zmefungw.,mfn kule ngusero nje kdg na jiji bendera za chadema zipo kwa wingi na kila vikund vya watu 10 ukiwauliuza vp siasa huku, 9 wanakuambia siasa ni chadema tu huku mmjoa akiitaja ccm..
Ccm mnajiaribia wenyew kadr manavowafanyia vituko zaid upinzn na kukaa muda mrefu kwa kuiba pesa za wananchi

URAHISI WA WANAWAKE WA SIKU HIZI UNAFANYA WANAUME TUENDELEE KUWA VIWEMBE

0
0
It was yesterday bana mida ya jion, jirani kanipigia simu akanishtua kuna bonge la Foleni kuelekea Home. Yeye alinishauri nibadilishe njia ila mimi, Well nka decide ku waste time kwa office kwanza ques ziishe. Ilipofika mida ya kama 1800 hivi nkamuona dada mmoja wa makamo kiasi akiondoka peke yake. Jengo letu lilivyo ni kuwa kama unatumia mlango wa nyuma kutoka lazma upitie department yetu.

As usual, boys will always be boys nkaanzisha story na kumsihi kuwa mida hii mafoleni makubwa avute hata 15 mins hivi ndo aende. Pamoja na kuwa alikataa kusubiri kwa kisingizio kuwa kesha chelewa sana lakini alisimama kunisikiliza. Here I was alone na bidada kwenye mazungumzo ambayo hata hayakuwa na aim yeyote ya maana. Kiufupi huyu dada mi huwa namuona tu na najua anafanya kazi pale ofisini ila sijawahi hata kuongea nae. 

Waswahili wanasema Mbuzi akifia kwa muuza supu kinachofuata kinajulikana. Basi na mimi when I ran out of things to say kwa huyu mrembo nkamuingia. Ingawa nia yangu haikuwa kumtongoza na nili expect akatae kabisa na aondoke ila aliendelea kunisikiliza huku akijichekesha. Sio kwamba ninampenda au nimevutiwa naye ila niliishiwa tu story na maneno ya kusema kwa wakati ule. Nlivyomuuliza kuwa ombi langu analipokeaje jibu lilinishangaza zaidi. Baada ya kuona hana dalili ya kukataa nkamfungukia kuwa nina mchumba wangu nategemea kumuoa hivyo this relationship ni Non-official. Hili pia halikumfanya akatae and she was up for it huku akijitamba kuwa yeye ni bingwa wa kutunza siri and no one will know. 

I was Flabbergasted, sijui ni ushamba au ndo maharage ya mbeya ila how can you possibly say yes? The conversation lasted for abt 40 mins. Tukabadilishana contacts with a promise kuwa tutawasiliana. To be honest ningeendelea na hata kumuomba tukapate vinywaji na baadae guest angekubali kabsaaaaa 100%. Unajua nimeamini kuwa hakuna mwanaume M.alaya ila tatizo wanawake wanatuwekea K mezani kirahisi mno. Wengine hatupendi ku cheat ila kama wanawake hawabadiliki sidhani kama tutafanikiwa. As for the time being, I'm keeping her number just incase. Who knows she may be a very good friend after all.

BEYONCE NOMA: AVUNJA RECORD YA ITUNES NDANI YA WEEK BAADA YA KUTOA ALBUM KWA KUSHTUKIZA

0
0
Beyonce broke iTunes record for most albums sold in the first week of release after selling 828,773 copies of her self titled 5th studio album 'Beyonce' in just three days.

She celebrated the milestone by releasing two full videos, XO and Drunk in Lovewatch Here:

ABIRIA YOYOTE ATAKAYE KUTWA AMESIMAMA KWENYE DALADALA KUTOZWA FINE...KAMA KENYA VILEE

0
0
POLISI Kikosi cha Usalama Barabarani, inaandaa sheria itakayosaidia kudhibiti ujazaji wa watu kwenye magari ya abiria, ambayo abiria atakayekutwa amesimama, atatozwa faini.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Alisema kabla ya sheria hiyo kutungwa na kutekelezwa, watatafuta njia ya kutatua tatizo la usafiri kwanza.

“Ni kweli kuna maeneo ambayo kuna tatizo la usafiri, kwa maana hiyo kabla ya sheria hii kuanza kutekelezwa, ni lazima itafutwe dawa ya tatizo la usafiri na baada ya hapo ndiyo sheria ianze kutumika,” alisema Mpinga.

Akizungumzia usalama katika msimu wa siku kuu za mwishoni mwa mwaka, Kamanda Mpinga alisema matukio ya ajali ya kutisha yametokea ndani ya mwezi huu.

Alitaja ajali ya mkoani Tanga katika eneo la Kwalaguru katika barabara ya Chalinze – Segera, ambako basi la Kampuni ya Burudani lilipinduka na kusababisha vifo vya watu 12 na majeruhi 76.

Pia mkoani Arusha gari aina ya Noah ilisababisha vifo vya watu sita na majeruhi 12, Tanga katika eneo la Segera magari yaligongana na kusababisha vifo vya watu nane na majeruhi 17.

Alitaja pia ajali ya mkoani Dodoma, ambako basi la Kampuni ya Simiyu Express lilipata ajali na kusababisha vifo vya watu wawili na majeruhi 14.

“Haya ni baadhi ya matukio yaliyotokea kwa mwezi huu wa Desemba, mwaka huu katika mikoa mbalimbali nchini, ambayo yamesababisha majonzi miongoni mwetu na vyanzo vya ajali hizi ni mwendo kasi,” alisema.

>>Habari leo

LULU 'SITAKI KUTUMIA SIMU TENA KWANI KERO TU..ANAE NITAFUTA ANITUMIE BARUA"

0
0
 
MWANADADA anayetamba katika filamu za Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema kero yake kubwa ni utumiaji wa simu za mkononi na anasumbuliwa sana na watu wasiokuwa na mambo ya msingi.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Lulu alisema simu zinasumbua sana na anatamani irudi enzi ya kutumiana barua posta.
“Sitaki kabisa kutumia simu ya mkononi kwa sasa, mwenye shida na mimi atanitumia barua, yaani sijui hata nisimame wapi, kwani hata nikibadili namba ya simu inasambaa kwa kasi sana,” alidai Lulu.

Lulu alibainisha kuwa kwa siku anapigiwa simu zisizo na faida kwake na kwamba, idadi kubwa wanaompigia ni mashabiki wake, lakini wanakuwa na maneno yasiyo na msingi.
Kwa siku napigiwa simu nyingi sana ambazo ni kero kwangu. Nafurahi sana ninapopigiwa simu na shabiki wangu, lakini wapo wanaopiga simu kutaka mambo ya ajabu, nakubali kwamba wengi wao ni mashabiki wangu, lakini simu kwangu ni kero kubwa, ingawa ni msaada mkubwa pia kwangu kwani ni sehemu ya kitendea kazi,” aliongeza Lulu.

MKE WA OBAMA NOMA..CHECK ALICHOFANYA KUMCHUNGA MME WAKE ASIMSALITI KWENYE MSIBA WA MANDELA(PHOTOS)

0
0
Nelson Mandela’s memorial service saw a hundred presidents from around  he globe head to South Africa to take part in this historical event. Among them was our president Uhuru Kenyatta who was well applauded by the crowd upon introduction.
Being a big event, many activities were taking place, paparazzi were on their toes to capture every moment, some of which have come in handy, like U.S.A’s first lady showing the ladies how to guard their men. Check out the step by step pictorial guide below:
ANGALIA HIZI PICHA CHINI MOJA BAADA YA MOJA ....ALAFU UNIAMBIE UMEELEWA NINI
1. Watch him closely to see how he relates..628x471
2. Make sure to read his every move..2013-12-10T113028Z_01_KAI33_RTRIDSP_3_MANDELA-1024x588
3. Sound your warning and leave him and the enemy in shock..ap_barack_obama_4_wy_131210_4x3_992
4. If he gets the hint let him be in peace..ARP3741789-1024x634
5. But if he forgets the rules as fast..heres-obama-taking-a-selfie-with-david-cameron-and-denmarks-prime-minister-at-mandelas-memorial-service
6. Let him enjoy the final moments then strike..south-africa-mandela-memorial (1)
7. Occupy your rightful position..
1489075_10151877653746997_1783077992_n8. Problem solved and everyone is happy..
mitch

GARI AINA YA TOYOTA GAIA INAUZWA KWA BEI NAFUU ..BEI MAELEWANO PIGA SIMU 0686129299

0
0

 Toyota Gaia, Silver ,1900 cc, 4WD, 8 Seater,  Alloy Wheels, Low mileage, Six month valida insuarance , 1 year Road tax...Bei kuanzia Milion 10 Maelewano yapo piga simu 0686129299

Udaku Specially Blog

WAKALA WA KUSIMAMIA UEGESHAJI WA MAGARI JIJINI AVUNJA SHERIA LIVE LIVE

0
0
Kwa mujibu wa Sheria hairuhusiwi kufunga gari la mtu wakati yumo ndani ya gari
.Zaidi ya hapo ni Rushwa tu
.Usawa wa kijinsia uzingatiwe pia
Askari wa Manispaa ya Ilala wakiwa wanafunga gari aina ya Rav 4 huku mwenye gari akiwa ndani ya gari bila hata ya kumpa nafasi ya kujitetea kama walivyokutwa na (Mpiga Picha Wetu) katika makutano Morogoro Road na Mali Street.
Wakazi wengi wa jiji la Dar es Salaam wamekuwa na malalamiko ya muda mrefu kwa askari na wafanyakazi wa manispaa ya Ilala kwa kuwa wasumbufu endapo tu wataegesha magari yao.
Watu mbalimbali walihojiwa na MOblog bila kuwa tayari kutaja majina yao wameeleza kwa masikitiko makubwa usumbufu mkubwa wanaopata kutoka kwa askari hao wa manispaa kwa kuombwa rushwa kwa kila kosa wanalotenda wakati manispaa haina nafasi ya kutosha kwa ajili ya maegesho  ya magari ya wakazi wanaoingia na kutoka kati kati ya jijini la Dar es Salaam hasa maeneo ya mjini.
DSC_0933
DSC_0935
Bila hata aibu na huruma jamaa akiendelea kulifunga gari la mwanadada huyo ambaye jina lake halikweza kupatikana mara moja.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images