Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live

Tazama video ya Diamond Platnumz ft Rick Ross – Waka (Official Video)

$
0
0
Mwanamuziki Diamond Platnumz ameachia video ya wimbo wake ambao amemshirikisha mwanamuziki Rick Ross kutoka nchini Marekani.

Wimbo huu ulikuwa unasubiriwa kwa hamu kubwa na watu mbalimbali, kwani hata wakati wa utayarishaji wa video hii, picha mbalimbali za Diamond akiwa na Rick Ross zilisambazwa mitandaoni, kila mmoja akiwa na lake la kusema.

Tazama video hiyo hapa chini:

Video: Prezzo ni Baba Mwenye Nyumba – Amber Lulu

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Amber Lulu amesema penzi lake na rapper Prezzo kutoka nchini Kenya bado lipo pale pale wala si kiki kama wengi wanavyodhani.

Muimbaji huyo ameendelea kwa kusema Prezzo kwake ni baba mwenye nyumba, hivyo lolote analofanya ni lazima kupata ruhusa kutoka kwake. VIDEO:

Breaking News: Anna Mgwira Ajitoa ACT Wazalendo Rasmi na Atangaza Kujiunga na CCM

$
0
0
Anna Mngwira Ajitoa ACT Wazalendo Rasmi na Kujiunga na CCM
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT Wazalendo ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimajaro, Mhe. Anna Mgwira amehamia Chama cha Mapinduzi (CCM) akitokea Chama cha ACT.

Mhe. RC Mgwira aliwahi kuwa Mwenyekiti wa ACT Wazalendo kabla ya kuteuliwa na Rais Dkt. John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa na kuachana na nafasi hiyo ndani ya chama hicho na mwanachama wa kawaida.

Mhe. RC Mgwira ametangaza uamuzi huo leo hii wakati wa Mkutano Mkuu wa UWT uliofanyika mjini Dodoma ambapo amesema baada ya kujitakari kwa muda na kufanya kazi na serikali ameona ni muda muhafaka kutamka kuwa anahamia CCM.

“Kwa muda mfupi nimeiona CCM inayobadilika, nimeona juhudi za kila mtu, ninaiona CCM inayoanza kukataa rushwa, nimeiona CCM inayoanza kulipeleka taifa letu mbele” amesema Mhe. RC Mgwirwa

Kutana na Mtabibu wa Nyota Duniani Maalim Fadhil Rashid Kutoka Comoro Kwa sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436

Ronaldo Awakimbiza Mess, Neymar Atwaa Tuzo ya Ballon d' Or

$
0
0
Ronaldo Awakimbiza Mess, Neymar Atwaa Tuzo ya Ballon d' Or
MSHAMBULIAJI wa klabu ya Real Madrid, na Timu ya Taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo ametwaa tuzo ya Ballon d’Or kwa mwaka wa pili mfululizo usiku wa kuamkia leo huku akiwabwaga mpinzani wake wa karibu Lionel Messi.
Ronaldo ameitwaa tuzo hiyo kwa mara ya tano na kuwa sawa na Messi ambae pia ametwaa kwa mara tano.
Nyota wa Barcelona Lionel Messi, na Timu ya Taifa ya Argentina amekuwa wa pili huku mchezaji mahiri wa PSG ya nchini Ufaransa, Timu ya Taifa ya Brazil, Neymar Jr, akitwaa katika nafasi ya tatu.
Msimu uliopita Ronaldo aliisaidia timu yake ya Real Madrid kutwaa ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya na ubingwa wa la Liga kwa mara ya kwanza toka toka mwaka 2012.
Ballon d’Or ni tuzo ambayo imekua ikitolewa na jarida la nchini Ufaransa toka mwaka 1956 na kura hupigwa na waandishi wa habari wapatao 173, duniani kote.

Walimu Wamfungia Mkuu wa Shule Ndani ya Ofisi

$
0
0
Walimu Wamfungia Mkuu wa Shule Ndani ya Ofisi
Walimu wa Shule ya Sekondari Bondeni iliyopo jijini hapa, wamemfungia ndani ya ofisi mkuu wa shule hiyo, Rahim Massawe kwa kushindwa kushughulikia malimbikizo  ya mishahara yao inayofikia kiasi cha Sh 10 milioni kwa kipindi cha miezi mitatu mfululizo.

Wakizungumza leo Ijumaa na waandishi wa habari ofisini hapo, walimu hao wamesema kuwa wamefikia hatua ya kufanya hivyo kama sehemu ya kushinikiza madai yao ya kulipwa malimbikizo ya mishahara yao ambayo wamekuwa wakiidai kwa kipindi kirefu bila mafanikio.

Mwalimu Rose Sechume amesema kuwa shule hiyo hapo awali wakati ikiendeshwa na Bakwata mkoani hapa walikuwa wakilipwa mishahara yao bila shida yoyote ila tangu wameingia ubia na mwekezaji wa kampuni ya Zaim Education Development ambayo ilikabidhiwa shule hiyo tangu Septemba mwaka huu mambo mengi yamekuwa hayaendi likiwemo suala la malipo yao.

Kwa upande wake mwalimu Shaban Hungo amesema tangu kukabidhiwa shule hiyo mikononi mwa kampuni hiyo kumekuwa na mapungufu mbalimbali ikiwemo kukusanya ada za wanafunzi na kushindwa kulipa wafanyakazi, kufukuzwa shule kwa wanafunzi wasiomaliza ada na kunyimwa kufanya mitihani, pamoja na kuongeza ada mara mbili zaidi, kutoka wastani wa Sh 600,000 mpaka Sh 1.2 milioni.

Hungo amesema kuanzia Shule hiyo ikabidhiwe mikononi mwa kampuni hiyo imechangia kiwango cha elimu kushuka huku wanafunzi wakipoteza motisha wa kusoma kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu kwa kipindi hicho cha miezi mitatu mfululizo.

"Tumejaribu kukaa na mwalimu mkuu ili tuzungumze kila wakati anatupa majibu yasiyoeleweka sasa tumeamua kumfungia ndani mpaka huyo mwajiri wake atakapofika hapa na kutupa jibu juu ya hatima ya malipo yetu," amesema mwalimu Hungo.

Mkuu wa shule hiyo, Rahim Massawe aliyefungiwa ndani ya ofisi akizungumzia suala hilo kupitia dirisha la ofisi hiyo amesema yeye binafsi aliwaita walimu hao ofisini kwake kuzungumzia suala hilo lakini ameshangaa wanashindwa kufikia muafaka na kuamua kumfungia ndani ya ofisi.

Wafanyakazi Waliondolewa Kazini kwa Vyeti vya Dalasa la Saba Wadai Mafao Yao

$
0
0
Wafanyakazi Waliondolewa Kazini kwa Vyeti vya Dalasa la Saba Wadai Mafao Yao
Wafanyakazi 66 walioondolewa kazini katika Hospitali ya Rufaa KCMC mjini hapa, kutokana na kuwa na vyeti vya darasa la saba wamemtaka mwajiri kuwalipa mafao yao. Miongoni mwa waliositishiwa ajira ni aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (Tughe) Mkoa wa Kilimanjaro, Paul Mhumba.

Pia, wamemtaka mwajiri kuwalipa mishahara ya miezi saba tangu waachishwe kazi mwezi Juni, wakidai utaratibu wa kuwaondoa haukufuatwa, hivyo wao bado ni wafanyakazi halali.

Mhumba alidai hawakuajiriwa na Serikali, bali KCMC ambayo alisema ina uwezo wa kuwalipa fedha kutokana na mapato yake.

Alidai KCMC inakwepa jukumu la kuwalipa na badala yake inasema inasubiri mwongozo kutoka serikalini.

Mhumba alisema hayo jana mbele ya msuluhushi na mwamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi Mkoa wa Kilimanjaro, Godwin Migire.

Aliyekuwa mlinzi wa hospitali hiyo, Petro Shaluo alisema kwa miaka zaidi ya 10 aliyoitumikia hospitali hiyo alilinda mali kwa uaminifu, lakini leo anashangaa kuonekana hafai.

“Nimeitetea KCMC, niling’atwa vidole vyangu kwa ajili ya kumkamata daktari feki aliyekuwa akila fedha za wagonjwa, leo hii naonekana si kitu,” alisema mlinzi huyo.

Mkurugenzi wa rasilimali watu wa hospitali hiyo, Steven Kolimba alisema KCMC haina uwezo wa kuwalipa wafanyakazi hao, badala yake wanategemea Serikali itoe mwongozo.

Mwanasheria wa hospitali, Rachel Mboya alisema Serikali ndiyo inayohusika na malipo ya watumishi hao kwa kuwa ilikuwa inawalipa mishahara na ndiyo iliyowasitishia ajira.

Msuluhishi na mwamuzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, Migire aliagiza kuwa ifikapo Desemba 12, mkurugenzi mtendaji wa hospitali hiyo afike akiwa na jumla ya madai ya wafanyakazi hao.

Atumia Sumu ya Panya Kuwaua Ndugu Zake Akidai Wao si Wasafi

$
0
0
Atumia Sumu ya Panya Kuwaua Ndugu Zake Akidai Wao si Wasafi
Polisi nchini Italia wamemkamata mwanamume ambaye anadaiwa kutumia sumu ya kuua panya kuwaua watu wa familia yake kwa sababu hawakuwa "wasafi".
Mattia Del Zotto, 27, analaumiwa kwa kuweka sumu kwenye chakula cha babu ya nyanya yake na cha shangazi ambao walifariki
Watu wengine watano katika familia wanaendelea kupata matibabu hospitalini.
Sumu ya buibui, tiba ya kiharusi
Aliyesema Hitler hakutumia sumu aomba radhi Marekani
Awapa sumu na kuwaua watu 20 kwenye madhabahu Pakistan
Bw. Del Zotto alikamawa eneo la Mozna karibu na Milan baada polisi kupata risiti kwenye kompiuta yake.
Baada ya kukamatwa alikiri kuwa alitaka kuwaadhibu watu wasio wasafi.
Mama yake aliwaambia wachunguzi kuwa hivi karibuni alikuwa amejiunga na dhehebu.

Jerry Muro Ajipima Uwezo na Chadema “Mimi Jerry Muro Mmoja ni Sawa na Wabunge 10 wa Chadema"

$
0
0
Jerry Muro  Ajipima Uwezo na Chadema “Mimi Jerry Muro Mmoja ni Sawa na Wabunge 10 wa Chadema"
Aliyekuwa Msemaji wa Yanga SC, Jerry Muro amesema kutokana na uwezo wake katika mambo mbali mbali anaweza kujilinganisha na wabunge 10 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Katika mahojiano na kipindi cha Maisha Mseto cha Times Fm, Jerry amesema kutokana na uwezo wake suala la ubunge kwake ni jambo rahisi tu sawa na kubofya button.

“Mimi Jerry Muro mmoja ni sawa na wabunge 10 wa Chadema, nimewazidi kifikra, kinguvu, kipesa, maadili, kihoja na mambo mengine mengi sana” amese Jerry.

Katika hatua nyingine Jerry amesema mwaka 2020 si ajabu kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Edward Lowassa wakirejea katika Chama cha Mapinduzi (CCM).

Bright Amwombea Msaada wa Kuandikiwa Nyimbo Baraka Da Prince

$
0
0
Bright Amwombea Msaada wa Kuandikiwa Nyimbo Baraka Da Prince
Msanii wa muziki Bongo, Bright amesema Barakah The Prince asaidiwe kwa namna yoyote ile katika uandishi wa ngoma zake kutokana na baadhi ya maneno kujirudia.

Muimbaji huyo ametolea mfano neno ‘Moyo’ kwa kusema limekuwa likijirudia mara nyingi katika ngoma za Barakah hadi anashindwa kuelewa iwapo ana tatizo la moyo.

Kila msanii ana matatizo lake lakini kwa baraka ni kujirudia rudia kwa maneno kama moyo labda anatatizo la moyo ndomana anapenda kulirudia mara kwa mara navyoona ninachomshauri  anachotakiwa amtafute mtu wa kumtungia anaweza kumtoa mahali alipo.


Jimbo la Nyalandu Lagombamiwa Wagombea 17 Wajitokeza

$
0
0
Jimbo la Nyalandu Lagombamiwa Wagombea 17 Wajitokeza
Vikumbo vya kuwania ubunge katika majimbo ya Singida Kaskazini, Longido na Songea Mjini vimeanza kwa idadi kubwa ya makada wa CCM kujitokeza kuchukua fomu.

Katika jimbo la Singida Kaskazini ambalo liko wazi baada ya Lazaro Nyalandu kujiuzulu na kujivua uanachama wa CCM kisha kuomba kujiunga na Chadema Oktoba 30 kwa madai ya kutoridhishwa na mwenendo ndani ya chama hicho tawala, tayari wagombea 17 wameshachukua fomu akiwamo aliyekuwa msaidizi wake.

Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) majimbo hayo yatafanya uchaguzi Januari 12 mwakanina mchakato wa kupata wagombea ndani ya CCM ulianza Desemba 5 na unatarajiwa kukamilika kesho.

Katibu wa CCM Wilaya ya Singida Vijijini, Grace Shindika alisema jana kuwa miongoni mwa wanachama waliojitokeza kuwania nafasi hiyo ni Elia Digha ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo.

“Watu wamejitokeza kwa wingi kuwania nafasi hii kuliko ilivyokuwa katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa 2015. Karibu wote wamechukua na kujaza kisha kurejesha isipokuwa wanachama wawili tu ndio hawajarejesha fomu zao,” alisema.

Alisema hakuwa katika nafasi ya kutaja majina ya watu wote walioomba kukiwakilisha chama na kwamba miongoni mwao pia ni aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya wa Singida Vijijini, Narumba Hanje.

Mwingine aliyejitosa kutaka kupewa ridhaa ya CCM kuwania jimbo hilo ni Haidel Gulamali ambaye aliwahi kuwa Katibu wa Uchumi wa chama hicho Mkoa wa Dodoma. Pia, Gulamali aliwahi kuwania kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge wa Jimbo la Dodoma Mjini mara mbili bila mafanikio.

Kwa mara ya kwanza, Gulamali aliingia katika mchakato wa ndani ya CCM kuwania ubunge wa Dodoma Mjini kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 ambako alishika nafasi ya saba kati ya wagombea kumi na moja na katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambako alishika nafasi ya pili.

Songea na Longindo

Katika jimbo la Songea Mjini, tayari wanachama wanne wa CCM wameshachukua fomu za kugombea ubunge kuziba pengo lililotokana na kifo cha Leonidas Gama aliyefariki dunia Novemba 23.

Akizungumza na Mwananchi jana, Katibu wa CCM wilaya ya kichama ya Songea Mjini, Juma Mpeli alisema wanachama hao wamechukua fomu tangu juzi na jana mchana huku akibashiri kwamba wanachama wengi zaidi watajitokeza kuwania nafasi hiyo.

Waliochukua fomu ni John Nchimbi, Gideon Ole Lairumbe ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Veta, Mussa Ndomba pamoja na Kayoya Fuko.

Pamoja na kutangazwa kwa tarehe ya uchaguzi katika Jimbo la Longido, kujaza nafasi ya aliyekuwa mbunge wake kupitia Chadema, Onesmo ole Nangole, hadi jana hakuna mwanaCCM aliyekuwa amejitokeza kuwania nafasi hiyo. Ole Nangole alivuliwa ubunge baada ya Mahakama Kuu kutengua ushindi wake kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi wa mwaka 2015. 

Ujumbe wa Diamond kwa Mwanaye Wawakera Wanawake... Atuhumiwa Kuwadhalilisha Wanawake

$
0
0
Ujumbe wa Diamond kwa Mwanaye Wawakera Wanawake... Atuhumiwa Kuwadhalilisha Wanawake
Msanii Diamond Platnumz anayetamba na Ngoma ya Sikomi ameingia matatani baada ya  watu mbalimbali kumtuhumu kuwadhalilisha wanawake kupitia ujumbe wake aliouandika katika ukurasa wake wa Instagram.

Ujumbe huo ambao ulikuwa ni maalum kwa ajili ya kumtakia heri ya kuzaliwa mtoto wake wa kiume, Nillan, ulimtaka mtoto huyo akue salama ili aje awatumie wanawake vyovyote atakavyo kwa sababu  anajituma ili amwandalie pesa ya kutumia vyovyote atakavyo atakapokuwa mkubwa.

“Nasemaje! Kua Uje kuwatembezea Baba... We swala la Kutafta ela niachie mie... Jukumu lako ni moja tu, Kupita nao.....Happy 1st Year Lanny!!!” Unasomekla ujumbe huo wa Diamond.

Polisi Wakwama Kumuhoji Lissu Kuhusu Shambulio Alilofanyiwa na Watu Wasiojulikana

$
0
0
Polisi Wakwama Kumuhoji Lissu Kuhusu Shambulio Alilofanyiwa na Watu Wasiojulikana
Jeshi la Polisi limekwama kumhoji Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), akiwa hospitalini Nairobi, Kenya baada ya kiongozi huyo kusema kwamba polisi wa Tanzania hawawezi kumhoji akiwa nchini Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya nchi.

Kauli ya Lissu imekuja siku 10 tangu Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro, kuiambia Nipashe kuwa wametuma askari wawili kwenda Nairobi kuchukua maelezo ya Lissu, baada ya Mbunge huyo kukubali kuhojiwa.
"Hadi sasa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania hajamwomba Mwanasheria Mkuu mwenzake wa Kenya ruhusa ya mimi kuhojiwa na Polisi wa Kenya juu ya shambulio hilo kama inavyotakiwa na sheria husika za nchi yetu," amefafanua Lissu ambaye ni mwanasheria kwa taaluma.
Aidha kwa upande wa IGP Sirro Alipoulizwa maoni yake juu ya kauli hiyo ya Lissu kuwa polisi hawawezi kumuhoji nje ya mipaka ya nchi, aliiambia Nipashe “Mimi sina jibu.”
Wiki iliyopita, IGP Sirro alisema ametuma wapelelezi Nairobi baada ya kusikia Lissu amekubali kuhojiwa juu ya tukio hilo na matarajio yao pia ni kuwapata dereva na mlinzi wake.
“Tumetuma watu wetu kwenda kuchukua maelezo yake (Lissu). Mwanzo tuliomba kwenda lakini chama (Chadema) walikataa. Juzi tumesikia wamesema wapo tayari". Sirro
Allifafanua kwamba  lengo kubwa ni kujua mazingira ya shambulio yalikuwaje na kwamba ikiwezekana wampate dereva na msaidizi huyo wa Lissu ili kurahisisha upepelezi wa tukio lenyewe.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo Ijumaa

$
0
0

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Tupo Mbagala Rangi Tatu

Tume ya Haki za Binadamu Yaitaka Polisi Kufanya Uchunguzi wa Haraka Ili Kusaidia Kupatikana Mwandishi wa Mwananchi Aliyepotea

$
0
0
Tume ya Haki za Binadamu Yaitaka Polisi Kufanya Uchunguzi wa Haraka Ili Kusaidia Kupatikana Mwandishi wa Mwananchi Aliyepotea
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bahame Nyanduga amelitaka jeshi la polisi nchini kufanya uchunguzi wake kwa haraka ili kuwezesha kupatikana kwa mwandishi wa habari wa kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, Azory Gwanda.

Azory ametoweka siku ya 18 sasa huko Kibiti ambako anaishi na familia yake.

Akizungumza na Mwananchi baada ya kufungua kongamano la maadhimisho ya siku ya haki za binadamu leo Ijumaa, Nyanduga amesema kupotea kwa mwandishi huyo kuna viashiria vya uvunjifu wa haki za binadamu.

"Matukio haya sasa yamekuwa mengi na yameanza kuzoeleka, tunaliomba jeshi la polisi lifanye uchunguzi wake haraka ili mwandishi huyu apatikane," amesema Nyanduga.

Amesisitiza kwamba kila mtu ana wajibu wa kulinda haki za binadamu lakini Serikali ndiyo ina wajibu mkubwa kwa sababu ina wajibu wa kulinda maisha ya watu wake.

Nyanduga amesema tume yake inalaani vitendo vyote vya ukiukwaji wa haki za binadamu na mara nyingi wanaunda kamati kwa ajili ya kuchunguza matukio hayo na kutoa ripoti.

Rais Magufuli Kuufumua Uongozi wa Benki ya Wanawake

$
0
0
Rais Magufuli Kuufumua Uongozi wa Benki ya Wanawake
Rais John Magufuli, amesema watapitia upya na kuchambua uongozi wa Benki ya Wanawake nchini (TWB), ili benki hiyo iweze kufanya kazi kiushindani.
Rais Magufuli amesema hayo leo Desemba 8, mjini Dodoma wakati akizindua mkutano wa tisa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kuongeza kuwa benki hiyo imekuwa ikimkandamiza mwanamke hasa katika mikopo kwa kulipia riba kubwa na wakati huo huo wanufaika wengi wa mikopo hiyo ni wanaume.
“Tutapitia upya na kuichambua Benki ya Wanawake, hatuwezi kuwa na benki inayowaumiza wanawake tutaiangalia ili iende vizuri kiushindani, hatuwezi kuwa na benki ambayo inafanya ufisadi tu isiwe chombo cha kuleta hasara kwa fedha ambazo zingeweza kwenda kwenye kilimo lakini wanaokopa pale ni wanaume,” amesema Rais Magufuli.
Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli ameutaka uongozi mpya atakaouchagua kumsaidia kufanya mabadiliko katika benki hiyo ili ifanye kazi kwa ufanisi na ushindani.
“Kumekuwa na kawaida kuwa benki hii kila anapokuwa mwanamke haifanyi vizuri badala yake imekuwa ya kuwanyonya wanawake, nimesema haya na ni matumaini yangu mmenielewa,” amesema.

Kesi ya Uhujumu Uchumi ya Sethi na Rugemarila Yaahirishwa

$
0
0
Kesi ya Uhujumu Uchumi ya Sethi na Rugemarila Yaahirishwa
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo ijumaa Desemba 8, 2017, imeahirisha kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Singh Sethi na Mfanyabiashara, James Rugemarila hadi Desemba 22, 2017, kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika.

Harbinder Singh Sethi pamoja na Mfanyabiashara James Rugemarila, kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya zaidi ya Bilioni 3.

Mvulana wa Miaka 13 Amuua Mama Make na Kumkata Kichwa

$
0
0
Mvulana wa Miaka 13 Amuua Mama Make na Kumkata Kichwa
Mvulana wa miaka 13 huko China amekamatwa kufuatia madai kuwa alimuua mama yake na kisha kumkata kichwa.
Mvulana huyo kisha akachukua video ya mauaji hayo na kuwatumia marafiki kupitia mtandao wa kijamii wa WeChat.
Alikamatwa siku kadhaa baadaye, baada ya rafiki yake mmoja kumuonyesha mama yake video hiyo.
Kisa hicho kilitokea katika mji wa Wenxing kwenye mkoa wa Sichuan.
Polisi walithibisha kisa hicho kwa BBC lakini hawakutoa taarifa zaidi wakisema kuwa bado kinachunguzwa.
Mvulana huyo alimuua mama yake baada ya kugombana siku ya Jumapili, iliripoti Radio Free Asia.
Kisha akamkata kichwa na kukiweka kwenye mfuko kabla ya kukitupa, kwa mujibu wa ripoti.
Mvulana huyo anaripotiwa kukamatwa akiwa shuleni

Kesi ya Madabida Yahamishiwa Mahakama ya Mafisadi

$
0
0
Kesi ya Madabida Yahamishiwa Mahakama ya Mafisadi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeruhusu kesi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida na wenzake watano wanaokabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi kuhamishiwa Mahakama ya Mafisadi kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo.

Madabida na wenzake wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ikiwamo kusambaza dawa bandia za kufubaza virusi vya Ukimwi ‘ ARV’s ‘ na kusababisha hasara ya Sh.Mil 148 ambayo ipo chini ya bilioni moja ambapo walifunguliwa kesi hiyo mpya namba 80 ya 2017, baada ya mahakama kuwafutia kesi kama hiyo iliyofunguliwa mwaka 2014.

Watuhumiwa wengine katika kesi hiyo ni Seif Shamte (mkurugenzi wa uendeshaji), Simon Msoffe (meneja masoko) na Fatma Shango (mhasibu msaidizi) wa Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd, Sadick Materu na Evans Mwemezi ambao ni maofisa wa Bohari Kuu ya Dawa. ambapo washtakiwa hao wanadaiwa kuisambazia Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kopo 4476 za ARV.

Pia washtakiwa wanadaiwa kujipatia Dola za Marekani 98,506.08 (sawa na Sh 148,350,156 za Tanzania kwa udanganyifu baada ya kuonyesha kwamba fedha hizo ni malipo ya makopo 12252 ya dawa hizo za ARV’s.

Kesi hiyo ilikuwa ikisikilizwa mbele ya hakimu Mkazi, Victoria Nongwa na Wakili wa Serikali, Pius Hilla Wakati ambapo upande wa utetezi wa watuhumiwa wanawakilishwa mawakili Denis Msafiri, Makaki Masatu na Nehemiah Nkoko ambapo wakili wa utetezi, Msafiri alidai kuwa Mahakama ya Kisutu inayo mamlaka ya kuisikiliza hiyo kwa sababu kiwango chake cha fedha kipo chini ya Sh.1 bilioni.
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live


Latest Images