Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live

Punguza Unene na Kutibu Magonjwa Kwa Kutumia Dawa za Edmark...Bonyeza Hapa

$
0
0
TUNA DAWA AMBAZO NI VIRUTUBISHO NA CHAKULA MBADALA ZIMEHAKIKIWA NA TFDA

Ni uhakika kwa afya yako, kupunguza uzito na Sumu mwilini, Mafuta/Sehemu Mbaya, Kitambi na Nyama Uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali yaliyoshindikana

Loose Weight Trainer ni Msaada wako Wasiliana Nasi Kwa WhatsApp 0713 777 470

Upate Suluhisho la Afya yako Bila Madhara pia unaweza kujiunga nami ili ufanye Biashara hii Nicheki


Intagram napatikana kwa jina @looseweight_trainer

Jinsi ya Kuepuka na Kujizuia Kutapika Safarini

$
0
0

Safari ni hatua na kudhihirisha hilo leo katika Afya Bongo5, tunakuletea njia kadhaa za kufanya pindi unapojisikia kutapika (kichefu chefu) uwapo safarini.


Kitendo cha kutapika kinaweza kumtokea mtu yoyote na hii huchangiwa na hali ya hewa inapoingiliana na utokea kwa wasafiri wa majini na nchi kavu, pia hutokea mara nyingi kwa mtu ambaye hakuwahi au hajawahi kusafiri umbali mrefu.

Ili uweze kuzuia hali hii uwapo sfarini basi huna budi kuepuka kula ovyo kabla ya kuanza safari na ndani ya safari, pia usile kula vitu vyenye sukari nyingi kwani vinaweza kuharibu koo lako kutoka na sukari kuzidi.

Vile vile unashauriwa kuweka njiti ya kiberiti mdomoni ili kuzuia kutapika, na kama hitoshi lamba ndimu kila wakati kwani inakata kichefuchefu na kutapika haraka.

Hivyo vyote vikashindikana na ukaona unahitaji kutapika basi muite muhudumu wa usafiri huo, ili akupatie mfuko wa rambo uweze kutapikie humo na ukimaliza hakikisha unafunga vizuri na kuweka sehemu husika na baada ya hapo safisha kinywa chako kwa maji safi na salama.

Bongo5

TANESCO Yawatoa Hofu Wateja Wake Juu Ya Mfumo Wa Ununuzi Wa Luku

$
0
0
TANESCO Yawatoa Hofu Wateja Wake Juu Ya Mfumo Wa Ununuzi Wa Luku
Shirika la Umeme Tanzania Tanesco limewatoa hofu wateja wake juu ya mfumo wa ununuzi wa Umeme kwa njia ya luku na kusema kuwa kwa sasa upo sawa na wanaweza kununua
katika mifumo iliyozoeleka.

Akizungumza jana  jijini Dar es Salaam Kaimu Meneja wa Teknolojia na Mawasiliano(TEHAMA) wa Tanesco, Demetruce Dashina alisema kuwa kulitokea tatizo dogo la mfumo wa ununuzi wa umeme kwa njia ya Luku kutokana na wataalamu wa shirika hilo walipokuwa wakihamisha mitambo hiyo kutoka ofisi ya Zamani kwenda sehemu nyingine.

“Jana tulikuwa tunafanya uhamisho wa mfumo wa luku kwenda katika ofisi zetu mpya hivyo ikawalazimu wateja wetu kupata usumbufu kidogo, lakini kuanzia saa saba(jana) mfumo huo umekaa sawa na wateja wanaweza kununua umeme kama walivyokuwa wanafanya hapo awali bila shida yoyote mara baada ya marekebisho ya kiufundi” alisema Dashina

Alisema kuwa shirika lilijipanga kuwahudumia wateja wake kama kawaida wakati wa kuhamisha mitambo hiyo lakini Wananchi wengi wakapata taharuki hivyo kufanya mfumo wa
ziada kuzidiwa kutokana na watu kununua umeme kuliko Kawaida.

Kwa upande wake Kaimu Meneja  Uhusiano wa Tanesco Leila Muhaji aliwaomba radhi wananchi kwa usumbufu uliojitokeza na kuwasisitiza kuwa sasa wanaweza kununua katika mifumo iliyozoeleka.

Muhaji alisema kuwa Tanesco inatambua umuhimu wa umeme hivyo   kuwataka watanzania kuwa na Imani na shirika lao kwani lipo kwa ajili ya kuwahudumia  kama inavyohitajika.

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Mrisho Gambo Asema Lema Yupo Mbioni Kuhamia CCM

$
0
0
Mrisho Gambo Asema Lema Yupo Mbioni Kuhamia CCM
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo jana Disemba 10,2017 ameweka picha kwenye mtandao wake wa Facebook akiwa na Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Godbless Lema na kusema kuwa yupo mbioni kurudi nyumbani.

Baada ya kuweka picha na ujumbe huo baadhi ya watu walianza kusema kuwa Mkuu wa mkoa huyo anafanya siasa rahisi huku wengine wakisema ni jambo ambalo haliwezekani Mbunge huyo wa CHADEMA kurudi CCM ili hali wapo ambao wanatamani jambo hilo litokee hata leo. 
"Msituko. Yupo mbioni kurudi nyumbani" aliandika Mrisho Gambo 
Haya ni baadhi ya maoni ya watu katika mtandao wa Facebook wa Mrisho Gambo baada ya kuweka picha akiwa na Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya CHADEMA. 

Stamina Afanya Kweli Amvalisha Pete ya Uchumba Mpenzi Wake

$
0
0
Stamina Afanya Kweli Amvalisha Pete ya Uchumba Mpenzi Wake
Rapper Stamina yupo mbioni kuuaga ukapera baada ya jana kumvisha pete mchumba wake wa muda mrefu ajulikanae kwa jina la Veronica.


Stamina akimvisha pete ya uchumba mpenzi wake.

Stamina amemvisha pete mchumba wake huyo jana mkoani Morogoro na kwa mujibu wa maelezo ya mtu wake wa karibu huenda rapper huyo akafunga ndoa mwaka huu baada ya maajirio.

Upinzani Nchini Kenya Waahirisha Kumuapisha Odinga Kuwa Rais

$
0
0
Upinzani Nchini Kenya Waahirisha Kumuapisha Odinga Kuwa Rais
Umoja wa Muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya (NASA), umetangaza kuahirishwa kwa sherehe za kumuapisha kiongozi mkuu wa umoja huo, Raila Odinga na Stephen Kalonzo Musyoka, kama Rais na Makamu wake wa Jamhuri ya Kenya.



Katika taarifa iliyotolewa jana na Muungano huo siku ya jana imeeleza kuwa imeahirisha sherehe hizo hadi itakapotangazwa tarehe hapo baadae.
Umoja wa Muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya (NASA), umetangaza kuahirishwa kwa sherehe za kumuapisha kiongozi mkuu wa umoja huo, Raila Odinga na Stephen Kalonzo Musyoka, kama Rais na Makamu wake wa Jamhuri ya Kenya.
Katika taarifa iliyotolewa jana na Muungano huo siku ya jana imeeleza kuwa imeahirisha sherehe hizo hadi itakapotangazwa tarehe hapo baadae.

Wema Aweka Wazi Mahusiano Yake na RC Makonda

$
0
0
Wema Aweka Wazi Mahusiano Yake na RC Makonda
Tangu mrembo Wema Sepetu akamatwe kwa tuhuma za kujihusisha na madawa ya kulevya kwa kutajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam mnamo mwezi Februari mwaka huu, Mrembo huyo hajawahi kumposti wala kumzungumzia kwa lolote kama alivyokuwa akifanya hivyo kipindi cha nyuma.

Watu wengi waliamini kuwa kitendo cha Wema Sepetu kutajwa na RC Makonda kwenye  orodha ya Wasanii waliotuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya kuliondoa urafiki wao waliokuwa nao awali.



Sasa, Wema Sepetu ameamua kuwaonesha mashabiki wake kuwa hayo yote yameshaisha na kwa sasa amerudisha yake ya urafiki na RC Makonda kama ilivyokuwa zamani.

Hayo, ameyathibitisha kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuweka picha akiwa na RC Makonda na kuandika kuwa “Kila lenye mwanzo lazima mwisho uwepo“.
Hatua hiyo ya Wema Sepetu imeonekana kuwafurahisha mashabiki wake wengi wakimsapoti kwa maamuzi hayo. Pitia baadhi ya maoni ya mashabiki wake baada ya uamuzi huo

irenefaith_muganda-Safi sana wema wangu safi mno….
hobokelamesson-Duuuuh, kwani kuna ubaya? Watu mapovuu tatizo nini? Safi Sana mdogo angu Wema kuishi vizuri na watu ni hazina, kiroho safi kabisa.
anastaziarug-Huyu ndo wema niliekuwa namutamani mungu akupe kila lililo jema mamy umekuwa sasa
sharifa15-Ni makosa mengi tunafanya hapa duniani lkn MUNGU anatusamehe, sa cha ajabu nn watu wanao fahamiana vzr kusameheana! Mi sijaona kosa.. Madam fanya lile linalo kupendeza km kusema walimwengu hawajaanza leo kukusema.
cynthiajustin-75% of Kenyans got your back. We endorse your decision. God bless @wemasepetu
Kwa upande mwingine, mrembo Wema Sepetu bado anakabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya bangi na kesi yake itasikilizwa alhamisi ya tarehe 14 Desemba, 2017. kunako mahakama ya Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam.

Lwandamina Ageukia Michuano ya CAF

$
0
0
Lwandamina  Ageukia Michuano ya CAF
WAKATI klabu nyingine za Ligi Kuu Tanzania Bara zikiwa kwenye mchakato wa kuimarisha vikosi vyao kwa ajili ya ligi, Kocha wa Yanga, George Lwandamina, amesema usajili watakaoufanya ni kwa ajili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf).

Yanga itashiriki michuano hiyo mikubwa Afrika kwa ngazi ya klabu kuanzia Februari mwakani.

Kikosi hicho cha Yanga kinampango wa kusajili wachezaji watatu kwenye safu ya ulinzi, kiungo na ushambuliaji.Akizungumza jijini Dar es Salaam, Lwandamina, alisema kwa sasa ni wakati wa kujipanga kwa ajili ya michuano ya kimataifa.

“Nina kikosi kizuri, lakini kwa michuano ya kimataifa ni lazima tuongeze wachezaji kwa ajili kupambana kwenye michuano hiyo, tunataka kuona tunafanya vizuri,” alisema Lwandamina.

Lwandamina, alisema kuwa yapo mapendekezo aliyoyawakilisha kwa uongozi wa timu hiyo ambapo ameeleza wachezaji wanaopaswa kuongezwa kwenye kikosi chake.

“Najua uongozi unafanyia kazi ripoti yangu, ni lazima pia kuangalia michuano ya kimataifa na ukiangalia tumebakiza Januari tu kabla ya kuanza michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika,” alisema Lwandamina.

Aidha, Lwandamina, alisema katika ripoti hiyo ameelezea pia ni wachezaji gani ambao uongozi haupaswi kuwaachia waondoke.

Kikosi cha Yanga kinaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Uhuru kujianda na michezo ya Ligi Kuu ambapo mchezo unaofuata watacheza na Mbao FC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.







Netanyahu: Jerusalem Umekuwa Mji Mkuu wa Israel kwa Miaka 3000

$
0
0
Netanyahu: Jerusalem Umekuwa Mji Mkuu wa Israel kwa Miaka 3000
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kuwa wapalestina ni lazima wakubali kuwa Jurusalem ndio mji mkuu wa Israel ili amani iweze kupatikana.
Netanyahu alisema Jerusalem umekuwa mji mkuu wa Israel kwa miaka 3,000 na haujakuwa mji mku wa watu wengine.
Aliongea huku maandamano yakiendelea kwenye ulimwengu wa kiislamu kufuatia hatua ya Marekani kuutambua Jurusalem kuwa mji mkuu wa Israel.
Ghasia zilizuka karibu na ubalozi wa Marekani nchini Lebanon na kwingineno siku ya Jumapili.

Jerusalem kwenyewe, mpalestina mmoja alikamatwa kwa kumdunga kisu na kumjeruhiwa vibaya afisa wa usalama wa Israel karibu na kituo kimoja cha basi.
Akiongea mjini Paris baada ya mazungumzo na rais wa Ufaransa Emmauel Macron, Bw Netanyahu alisema kuwa jitihada za kuwanyima wayahudi mji wa wa Jerusalem ni kitu kibaya.
"Unaweza kusoma katika kitabu kizuri zaidi, kinaitwa Biblia, alisema. Unaweza kuyaskia katika historia ya jamii wa wayahudi kote duniani… Ni wapi tena kuna mji wa Israel, isipokuwa Jerusalem?

Mradi wa Mwendo Kasi Waleta Heshima Dar Waleta Tuzo ya C40 Bloomberg

$
0
0
Mradi wa Mwendo Kasi Waleta Heshima Yaleta Tuzo ya C40 Bloomberg
JIJI  la Dar es Salaam ni miongoni mwa majiji 10 duniani ambayo yamepata tuzo ya C40 Bloomberg Philantropies 2017   kupitia Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka.

Katika tuzo hiyo  mwaka huu imepokelewa na Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Miwta aliyerejea nchini alfajiri ya Desemba 8 mwaka huu.

Jiji la Dar es Salaam limechangia tuzo hiyo  na Jiji la New York  nchini Marekani

Mradi wa Mabasi yaendayo haraka unawahudumia abiria 200,000 kila siku kwa kutumia mabasi ya kisasa ambayo yanachangia kupunguza msongamano wa magari barabarani na kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa na hivyo kuwa siri ya mafanikio ya tuzo jijini hapa.

Tuzo ya C40 Bloomberg Philanthropies hutolewa kila mwaka katika miradi inayotekelezwa kwenye maeneo mahususi matano ili kutambua jitihada za majiji wanachama wa Taasisi ya mtandao wa Majiji zaidi ya 90 duniani inayoshughulika na namna bora ya kukabiliana na Athari za mabadiliko ya Tabia ya Nchi Duniani.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatatu

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Jacqueline Wolper Ametia Aibu ya Mwaka kwa Mashabiki Wake

$
0
0
Jacqueline Wolper Ametia Aibu ya Mwaka kwa Mashabiki Wake
STAA wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe ametia aibu ya mwaka mbele ya mashabiki wake wakati akisherehekea siku yake ya kuzaliwa (birthday) kufuatia gauni alilovaa ambalo lilishindwa kumstiri maumbile yake nyeti, Ijumaa Wikienda lilikuwepo.

Tukio hilo la aina yake lilijiri wikiendi iliyopita kwenye Ukumbi wa Buckets uliopo Masaki jijini Dar ambapo katika sherehe hiyo mbali na pati hiyo pia alizindua ‘App’ yake ambayo atakuwa akiweka kazi zake zote za sanaa pamoja na biashara zake huku akipewa sapoti na mastaa wengi wakiwemo Steve Nyerere, Gigy Money, Amber Lulu, Barnaba, Aunt Ezekiel na wengine kibao.

Akizungumzia shughuli yake hiyo, Wolper aliwashukuru mashabiki wake waliohudhuria akisema: “Asanteni kwa wote mliokuja kunipa sapoti kwenye siku yangu hii.

“Nilizaliwa Desemba 6, nil­isherehekea na watoto yatima.
“Lakini leo (usiku wa kuamkia Ijumaa iliyopita), nimeamua kusherehekea pamoja nanyi mashabiki wangu. “Naombeni muendelee kuniunga mkono pia kwenye App yangu ambayo nimeizindua leo.”

Hata hivyo, mbali na sham­rashamra hizo, jambo lililo­geuka gumzo kubwa ni gauni alilovaa mwanadada huyo.
Gauni hilo lilikuwa jeusi ambalo liliacha sehemu kubwa ya mwili wake wazi hasa katika maungo yake ya mbele kiasi kwamba alionekana kwamba kwa ndani alikuwa ametinga ‘kufuli’ pekee.

Kufuatia hali hiyo, muda mwingi Wolper alionekana aki­jitahidi kujiziba eneo la mbele kwa viganja vya mikono, jambo lililowafanya baadhi ya watu kuhoji kwamba kama alikuwa akiona aibu alivyovaa nusu utupu basi asingevaa hivyo!
“Sasa anafichaficha nini? Si amevaa mwenyewe? Kwa nini asiachie tu watu tuone vitu….” Alisikika jamaa mmoja aliyeonekana kudata baada ya kujionea ‘vitu’ vya ndani ya Wolper.

Hata hivyo, mbali na wengi kuonekana kuliponda gauni hilo matata, wapo waliolisifia kwamba ni mkali wa mitindo.
Chanzo: Global Publishers

Meya wa Jiji Kujadiri Changamoto Zinazowakabili Viongozi na Umoja wa Mataifa

$
0
0
Meya wa Jiji Kujadiri Changamoto Zinazowakabili Viongozi na Umoja wa Mataifa
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam Isaya Mwita, anatarajia kuzungumza katika mkutano wa kujadili changamoto zinazo wakabili viongozi wa serikali za mitaa, ulioandaliwa na Umoja wa Mataifa jijini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Mkutano huo wa siku tatu unaanza leo na unatarajiwa kujadili na kutoa majibu ya changamoto mbalimbali ambazo wanakutana nazo viongozi wa serikali za mitaa wakiwemo Mameya.
Meya Mwita ameondoka nchini jana jioni kuelekea  Addis Ababa, ambapo katika mkutano huo atazungumza kuelezea changamoto zilizopo katika jiji la Dar es Salaam na namna ambavyo  kwa asilimia kadhaa wameweza kuzitatua.
Mbali na Mameya, mkutano huo pia utahudhuriwa na viongozi wengine wa serikali za mitaa kutoka Nchi mbalimbali duniani. Lengo kuu ni viongozi hao kujadili changamoto zinazozikabili halmshauri zao, mafanikio, lakini pia kujengeana uwezo kwenye utendaji kazi.
Miongoni mwa changamoto ambazo mkutano huo utajikita katika kuzijadili ni suala la bajeti katika halmashauri na ukusaji wa mapato ambavyo ndio msingi wa maendeleo.

Baada ya Kutoka Gerezani kwa Msamaha wa Rais Kanisa Lawaombea Nguza, Papii kwa Saa Tano

$
0
0
Baada ya Kutoka Gerezani kwa Msamaha wa Rais Kanisa Lawaombea Nguza, Papii kwa Saa Tano
Mwanamuziki wa dansi, Nguza Viking ‘Babu Seya na mwanaye Johnson Nguza, maarufu kwa jina la kisanii la Papii Kocha, wamefanyiwa maombi maalumu yaliyodumu kwa takriban saa tano baada ya kutoka gerezani kwa msamaha wa Rais.

Maombi hayo yalifanyika juzi katika Kanisa la Life in Christ Ministries Zoe, lililopo Tabata Segerea na yalianza saa 1:00 jioni hadi saa 5:00 usiku yakiongozwa na Nabii Joseph.

Nguza, ambaye ni maarufu kutokana na kibao chake cha “Seya” na Papii Kocha, ambaye walishirikiana naye kukitengeneza upya kibao hicho, walikuwa wakitumikia kifungo cha maisha, lakini walitoka gerezani baada ya Rais John Magufuli kutangaza kuwasemehe wafungwa 8,157 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa Tanganyika zilizofanyika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Wanamuziki hao walikaa gerezani kwa takriban miaka 13 na miezi minne baada ya kupatikana na hatia ya kunajisi watoto 10 wa kike ambao ni wanafunzi wa Shule ya Msingi Mashujaa ya Sinza jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti, Nabii Joseph alisema wamewaombea Nguza na Papii Kocha ili kuwajengea uwezo wa namna ya kuishi maisha mapya ya uraiani kama wananchi wengine baada ya kutoka kifungoni.

Alisema wakati maombi hayo yakiendelea, Nguza na Papii walionyesha kuwa wapo tayari kubadilika na kumtumikia Mungu.

“Mtu anapofungwa maisha na kuachiliwa huru, anaona kama akili inakataa kuamini kama ni kweli yupo huru. Ndio maana walivyotoka gerezani walikuja hapa ili tuwaweke vizuri,” alisema.

Nabii Joseph alitumia nafasi hiyo kueleza sababu ya Babu Seya na Papii Kocha kwenda moja kwa moja kanisani badala ya nyumbani walikokuwa wameandaliwa kwa mapumziko.

Alisema wakati wakiwa gerezani, kila wakati alikuwa akiwatumia ujumbe kupitia kwa ndugu yao Nabii Michael Nguza uliolenga kuwapa matumaini na moyo wa kuamini kuwa Mungu yupo na kwamba ipo siku watatoka gerezani kwa kuwa yeye alishaoteshwa.

“Ndiyo maana kama mnakumbuka Babu Seya aliwahi kusema kuwa akitoka gerezani ataishi maisha ya kumtumikia Mungu.Aliamua kusema hivi baada kupata ujumbe wa maono yangu kuwa Mungu anawahitaji wamtumikie,” alisema Nabii Joseph.

Nabii Joseph alidai kuwa kwa nyakati tofauti aliwahi kutabiri zaidi ya mara tatu kuwa Nguza na mwanae watatoka gerezani, hivyo anamshukuru Mungu na Rais Magufuli kwa uamuzi wa kuwachilia huru wanamuziki hao.

Kwa mujibu wa Nabii Joseph, baada ya kumaliza maombi hayo, Nguza na Papii Kocha walielekea sehemu maalumu bila kuitaja jina kwa ajili ya mapumziko ya utulivu wa Mungu.

Alisema wamepanga kuwapa ushauri wa kiroho kwa muda wa wiki moja kwa kutumia wachungaji na manabii watakaokuwa wakienda sehemu hiyo maalumu ya mapumziko,” alisema Nabii Joseph.

Mbali na hilo, Nabii Joseph alisema kanisa hilo limeandaa wimbo maalumu unaoitwa “Siku za Maisha Nilizokuwa Gereza” kwa ajili ya wawili hao.

“Wimbo huu niliutunga miaka mitatu iliyopita. Ndani ya wimbo tumshirikisha Papii Kocha sehemu ya kiitikio kinachosema “upendo wa Mungu kwa ajili ya maisha” na atatumbuiza siku ya ibada ya Jumapili ijayo akiambatana na baba yake,” alisema nabii huyo.

Alisema siku hiyo kutakuwa na ibada maalumu itakayoanza saa 3:00 asubuhi hadi jioni kwa ajili ya kumuomba Mungu na kumuombea Rais Magufuli kwa upendo wake na moyo wa huruma alionyesha kwa wafungwa 8,157 alioachia huru.

Mmoja wa waumini wa kanisa hilo, Mchungaji Petros alisema ni furaha kuwaona Nguza na Papii Kocha wakiwa huru na kuanza maisha mapya.

Ilivyokuwa baada ya kuachiwa

Baada ya Rais Magufuli kutangaza msamaha kwa wanamuziki hao, saa 11:00 jioni gazeti la hili lilizungumza na Mkuu wa Magereza ya Mkoa wa Dar es Salaam, (DCP), Augustine Mboje aliyesema wapo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuwaachia.

Ilipotimu saa 12:00 jioni, ungeweza kusema watu waliokuwa nga’mbo ya pili ya lango kuu la gereza la Ukonga walikuwa wanashangilia mpira, bali ni shangwe za kuziona sura za Nguza na Papii Kocha wakati wakitoka.

Kiongozi huyo wa bendi ya zamani wa Marquis du Zaire na mwanae waliwapungia mikono watu waliokuwa nje ya gereza.

Ilikuwa ni furaha kwa ndugu na marafiki waliojazana nje ya gereza kila mmoja akitaka kuwaona na wengine kuwashika mkono na kusababisha msongamano wa magari.

Watu hao walisikikia wakilitaja jina la Rais Magufuli huku wengine wakimkaribisha uraiani Nguza, ambaye ni maarufu kwa upigaji gitaa la solo na mwanae ambaye ni mwimbaji.

Hali hiyo ilililamzimu Jeshi la Magereza kuingilia kati na kuwazuia watu hao kisha kuwaingiza wasanii kwenye gari na ndugu zao wa karibu.

Wakati wanatoka Nguza na mwanaye walibeba magitaa na walionekana na nyuso za furaha na msafara wao ulianza kuelekea kanisani.

Walifika kanisa hapo saa 1:00 jioni na kuamsha furaha kwa ndugu zao wa karibu ambao baadhi walikumbatiana nao.

Miongoni mwa marafiki wa karibu walioambatana na wawili hao ni mwimbaji wa kundi la FM Academia, Nyoshi El Sadat ambaye alionekana kuwa mtu mwenye furaha.

“Namshukuru sana Mungu ndiyo maana nipo hapa,” alisema Nyoshi.

“Nilikuwa nimelala nilipoamka saa 9:00 alasiri na kuangalia simu nikakuta kuna idadi kubwa ya watu walionipigia na kunitumia ujumbe mfupi. Ikanibidi nichukue gari na kwenda gerezani na tumetangu wakati huo, tupo hapa kanisani.

“Tunamshukuru Mwenyezi Mungu na Rais Magufuli kwa kuwasemehe wote na si familii hii pekee. nikiongelea familia hii watasema napendelea ila tunamshukuru Rais kwa kuwaseheme wote.”

Mmoja wa watoto wa Nguza, Michael Nguza maarufu kama Nabii Michael alisema leo huenda wakatoa tamko la familia baada ya baba yake na mdogo wake kutoka gerezani.

Miili ya Askari Waliokufa DRC Kurejeshwa Kesho na Serikali, UN

$
0
0
Miili ya Askari Waliokufa DRC Kurejeshwa Kesho na Serikali, UN
Serikali inashirikiana na Umoja wa Mataifa (UN) kuhakikisha miili ya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliouawa na waasi katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) inarejeshwa nchini.

Akizungumzia na waandishi wa habari jana, mnadhimu mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali James Mwakibolwa alisema miili ya askari hao itarejeshwa nchini kati ya Jumanne na Jumatano. Mwakibolwa alisema askari hao walivamiwa kambini na waasi wa kundi cha ADF na mapigano yalidumu kwa takriban saa 13.

Alisema askari 14 wa JWTZ waliuawa, 44 walijeruhiwa na wengine wawili hawajulikani walipo.

Mwakibolwa alisema tukio hilo lililotokea Desemba 7 katika kambi ndogo iliyopo kwenye daraja la Mto Simulike lililopo Kaskazini Mashariki mwa Wilaya ya Beni, Jimbo la Kivu.

Alisema shambulio hilo ni kubwa zaidi kutokea tangu JWTZ ianze kushiriki ulinzi wa amani nchini DRC mwaka 2011.

“Taratibu za kusafirisha miili ya marehemu kuirejesha nchini inafanyika chini ya uratibu wa Serikali na Umoja wa Mataifa. JWTZ na Serikali tunaendelea kuchukua hatua stahiki kufuatilia tukio hili ikiwamo kufanya uchunguzi katika eneo husika,” alisema Mwakibolwa.

Alisema tukio hilo halitawavunja moyo JWTZ wala kutetereka kupeperusha bendera ya Tanzania ndani na nje ya nchi bali linawaongezea ari, nguvu, ushupavu na uhodari zaidi katika kutekeleza majukumu yao.

“Ni bahati mbaya mashujaa wetu wameuawa wakiwa wanatekeleza jukumu la ulinzi wa amani nchini DRC. Kwa umoja wetu Watanzania tuwaombee dua roho zao zipumzike kwa amani na majeruhi wapone haraka iwezekanavyo ili warejee kutekeleza majukumu yao,” alisema.

Baada ya Stamina Kumvalisha Pete ya Uchumba Mpenzi Wake Roma Ampa Maneno Haya

$
0
0
Baada ya Stamina Kumvisha Pete ya Uchumba Mpenzi Wake Roma Ampa Maneno Haya
Rapper Bonventure Kabogo maarufu kama Stamina anayeuwakilisha vyema mkoa wa Morogoro ,yuko mbioni kuachana na chama la ukapera baada ya kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa muda mrefu.

Tukio hilo la kumvisha pete mpenzi wake limefanyika mkoani Morogoro ambapo ndio nyumbani kwao Stamina na baada ya tukio hilo wasanii wenzake  wampongeza kwa hatua hiyo na kumuomba asihishie hapo amuoe kabisa mpenzi  wake huyo.
Kupitia ukurasa wake wa instagram msanii mwenzake ambae wanafanya naye kazi kwa karibu hivi sasa Roma mkatoliki amemtahadharisha kwa kumwambia " Congratulation My Brother @staminashorwebwenzi On Your #Engagement .Im Proud Of You Son....Sasa #Umuoe Sio Uishie Kwenye #Pete Tu!!Nisaidieni #Kumuwish Mdogo Wangu Marafiki!!"


Yanga Yasaini Kiungo Hatari wa Kimataifa

$
0
0
WAKATI zikiwa zimebaki siku nne pekee kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa Desemba 15, Kocha wa Yanga, George Lwandamina leo Jumatatu anatarajia kupokea jina la mshambuliaji raia wa DR Congo kutoka kwa mwenyekiti wa usajili wa timu hiyo, Hussein Nyika, ambaye alikuwa nje kwa ajili ya kusaka mshambuliaji.

Nyika alitembelea nchi za Ghana, Congo na Burundi kwa ajili ya kusaka mshambuliaji wa kimataifa ambaye atajiunga na timu hiyo kwa ajili ya kuongeza nguvu kutokana na washambuliaji wa kutumainiwa Amissi Tambwe na Donald Ngoma kuwa majeruhi jambo ambalo limesababisha wawategemee Ibrahim Ajibu na Mzambia, Obrey Chirwa pekee.

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Yanga kimesema kuwa Nyika anatarajiwa kukutana na Lwandamina kwa ajili ya kumpa ripoti juu ya aina gani ya mshambuliaji ambaye anaweza kujiunga na timu hiyo baada ya kufanya uchunguzi kwenye nchi za Congo, Ghana na Burundi ambapo alienda kwa lengo la kusaka mshambuliaji.

“Leo Jumatatu, mwenyekiti wetu wa usajili, Hussein Nyika anatarajia kufanya kikao na kocha, Lwandamina kwa ajili ya kumpa mrejesho wa kile ambacho amekutana nacho baada ya kwenda nje kusaka mshambuliaji ambaye kocha anamuhitaji kabla ya dirisha kufungwa.

“Hadi sasa kuna majina ya washambuliaji watatu kutoka nchi za DR Congo, Ghana na Burundi ambapo alienda wiki chache zilizopita kwa ajili ya kuangalia ni nani ambaye anaweza kuwa msaada katika kipindi hiki ambacho fowadi yetu imepungua makali kutokana na baadhi yao kuwa majeruhi,” kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo, alipotafutwa Nyika ili aweze kuzungumzia hilo, hakuweza kupatikana kutokana na simu yake ya mkononi kuita tu bila ya kupokelewa.

Yanga Wakwama kwa Mo, Simba Kumpa Mkataba wa Miaka Miwili

$
0
0
Yanga Wakwama kwa Mo, Simba  Kumpa Mkataba wa Miaka Miwili
KLABU ya Yanga imeshindwa kumpa kiungo Mohamed Ibrahim ‘Mo Ibra’ kile anachotaka, hivyo leo Jumatatu mchezaji huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na klabu yake ya Simba.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Meneja wa Mo, Jamal Kisongo amesema kuwa mteja wake huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na Simba baada ya kushindwana na Yanga ambao nao walikuwa wanamtaka huku Msimbazi wao wakitimiza makubaliano waliyokuwa wanataka.

Alisema walifanya mazungumzo na Yanga lakini kuna baadhi ya vitu kwenye mkataba hawakuridhika navyo na walipozu-ngumza na Simba wakakubali kurekebisha baadhi ya vipengele kwenye ule mkataba wa awali hivyo rasmi mteja wake anabaki Simba na leo atasaini kandarasi baada ya ile ya awali kumalizika.

“Kesho (leo) natarajiwa kwenda kusaini mkataba mpya wa miaka mawili na mchezaji Mohammed pale Simba baada ya ule wa awali kumalizika, hivyo tunaongeza mwingine.
“Yanga nao walionyesha kumhitaji lakini kuna vitu walishindwa kukamilisha na tulipozungumza na Simba wamekubali kurekebisha baadhi ya vipengele, hivyo atabaki huko,” alisema Kisongo.
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live




Latest Images