Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Ratiba ya Hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabigwa Ulaya Hii Hapa

$
0
0
Ratiba ya Hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabigwa Ulaya Hii Hapa
Droo ya Hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya maarufu kwa jina la Champions League imepangwa na kuna michezo mitatu ambayo imeonekana kuwavutia watu wengi.

Juventus wanatarajia kukutana na Tottenham Hotspur wakati ambapo wababe wa Hispania Real Madrid wao watakula sahani moja na wababe wa Ufaransa, Paris Saint-Germain.

Ratiba hiyo inamaanisha kuwa staa wa PSG, Neyamr atakutana na Real Madrid kwa mara nyingine baada ya mchezaji huyo kukuna nao mara kadhaa lipokuwa akiitumikia Barcelona.

Gumzo zito ni juu ya  Chelsea wanaonolewa Kocha Antonio Conte ambapo wanatarajiwa kukutana na Barcelona.

Manchester City wao wataanzia ugenini ambapo huko watakipiga dhidi ya Basle wakati Porto wataikaribisha timu nyingine ya England, Liverpool katika hatua hiyo.

Sevilla wao wataanza nyumban I kuikaribisha Manchester United kabla ya timu hizo kurudiana wiki moja baadaye.

Michezo ya hatua hiyo itachezwa Februari, mwakani.

Ratiba kamili ya hatua hiyo ni hii hapa:
Juventus vs Tottenham Hotspur

Basle vs Manchester City

Porto vs Liverpool

Sevilla vs Manchester United

Real Madrid vs Paris Saint-Germain

Shakhtar Donetsk vs Roma

Chelsea vs Barcelona

Bayern Munich vs Besiktas

Gauni la Harusi Nimepata Bado Mume Tu- Tausi

$
0
0
Nimepata Gauni la Harusi Bado Mume Tu- Tausi
MUIGIZAJI wa filamu Bongo Tausi Mdegela amefunguka kwa kusema kuwa anatamani sana kuvaa gauni la harusi kwa muda mrefu na hatimaye ametimiza shauku yake baada ya kufanikiwa gauni hilo na kuliweka ndani kwake ni ishara njema siku yoyote akipata mume mwenye mapenzi atalivaa na kutimiza ndoto zake.

“Jambo jema unalitafutia njia mwenyewe maana kuna watu ambao huwa wanapata bahati ya kuolewa au kufunga pingu za maisha lakini hawana nguo za harusi kwa sababu ni aghari, lakini mimi ninalo Gauni la harusi tayari ndani,”alisema Tausi Msanii huyo alivyoulizwa na FC imekuwaje kununua gauni la harusi ambalo mwenyewe anadai kuwa ni gharama na hiyo fedha asifanyie kazi nyingine alisema kuwa amenunuliwa na msanii wa muziki wa kizazi kipya Ben Paul kwa ajili ya kushiriki katika show yake lakini moja ya masharti alimuomba gauni hilo liwe lake kwa ajili ya Harusi akibahatika. Ben Pol baada ya kukiki na mchekeshaji wa kike Ebitoke anabuni tukio lingine kwa akuandaa tukio la kiharusi Bibi harusi anakuwa Tausi Mdegela ambaye naye yupo katika kundi la wachekeshaji anatikisa kwa ubunifu wakenkulingana na show anayofanya akiwa na Ebitoke na sasa yupo na Tausi kikazi.

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0

JE, UNA UPUNGUVU WA NGUVU ZA KIUME, HAMU YA TENDO LA NDOA AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?
SOMA HAPA👇👇.
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea na matunda bila kemikali 🍇🍍🍓🌿🍉🍒🍎🍑 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Hii ndio droo ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya

$
0
0

Droo ya Hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya maarufu kwa jina la Champions League imepangwa na kuna michezo mitatu ambayo imeonekana kuwavutia watu wengi.

Juventus wanatarajia kukutana na Tottenham Hotspur wakati ambapo wababe wa Hispania Real Madrid wao watakula sahani moja na wababe wa Ufaransa, Paris Saint-Germain.

Ratiba hiyo inamaanisha kuwa staa wa PSG, Neyamr atakutana na Real Madrid kwa mara nyingine baada ya mchezaji huyo kukuna nao mara kadhaa lipokuwac akiitumikia Barcelona.

Gumzo zito ni juu ya  Chelsea wanaonolewa Kocha Antonio Conte ambapo wanatarajiwa kukutana na Barcelona.

Manchester City wao wataanzia ugenini ambapo huko watakipiga dhidi ya Basle wakati Porto wataikaribisha timu nyingine ya England, Liverpool katika hatua hiyo.

Sevilla wao wataanza nyumban I kuikaribisha Manchester United kabla ya timu hizo kurudiana wiki moja baadaye.

Michezo ya hatua hiyo itachezwa Februari, mwakani.

Ratiba kamili ya hatua hiyo ni hii hapa:
Juventus vs Tottenham Hotspur

Basle vs Manchester City

Porto vs Liverpool

Sevilla vs Manchester United

Real Madrid vs Paris Saint-Germain

Shakhtar Donetsk vs Roma

Chelsea vs Barcelona

Bayern Munich vs Besiktas

Shomari Kapombe ni ‘kipaji kilichopotea’ au ‘kujipoteza?’

$
0
0

Na Baraka Mbolembole

ILIONEKANA kama vile Shomari Kapombe angekuwa mwanasoka wa kwanza raia wa Tanzania kucheza soka katika ligi ya juu nchini Ufaransa wakati mlinzi huyo wa kulia aliposajiliwa na AS Cannes mwaka 2013 akiwa U23.

Sikuwahi kuwa na shaka kuhusu ubora wa kujituma, kiuchezaji na tamaa ya mafanikio alivyonavyo mlinzi huyo wa klabu ya Simba ambaye ni kati ya vijana waliopata bahati ya kuruka kutoka Moro Youth Soccer Academy hadi kusajiliwa na kucheza ligi kuu Tanzania Bara mwaka 2011 akiwa mchezaji wa timu ya Taifa ya vijana ya Tanzania U23.

Kapombe hakuchelewa kuingia katika beki ya kati pale Simba wakati huo kukiwepo pia wazoefu kama Victor Costa, Juma Nyosso, Kelvin Yondani. Alikuwa chaguo la kwanza chini ya kocha Moses Basena na baadae Milovan Cirkovic na akatokea kuwa beki bora wa pembeni nchini huku akihodhi namba mbili ya Taifa Stars.

Msimu wake wa kwanza Simba uliambatana na ubingwa Mei, 2012 huku akiwemo katika kikosi kilichowateketeza mahasimu wao Yanga 5-0 na kufika hatua ya ‘play off’ katika Caf Confederation Cup 2012. Uwezo wake wa kupandisha mashambulizi na kutengeneza magoli kwa wachezaji wenzake huku akifunga mara kadhaa ulimfanya atabiriwe na wengi kufika mbali kimpira.

Lakini miaka mitano sasa ni ‘aibu’ kwa mchezaji huyo kushinda taji moja tu la ligi, huku pia ndani ya uwanja akiwa mbali na tarajio la wengi kumuona akicheza nje ya Tanzania.

Kwanini alirudi Tanzania?

Novemba 2013 alipokuja kuichezea Tanzania, Kapombe hakutaka tena kurejea Ufaransa katika klabu yake ya Cannes na sababu kubwa aliyotoa ni klabu hiyo kushindwa kumlipa mshahara wake (inasemekana ni wa mwezi mmoja tu) Kapombe aliendelea kubaki nchini huku akijifua binafsi. Baadae akashinikiza kuuzwa na klabu hiyo iliona hakuna namna ikakubali kumuuza Azam FC katikati ya mwaka 2014.

Kuna mambo mengi yalimvutia Kapombe kuondoka Ufaransa na kurejea nchini. Inasemekana Azam FC ilikubali kuwaajiri ndugu wasiopungua watano wa Kapombe, Si hivyo tu mchezaji huyo na ndugu zake waliahidiwa kupelekwa na kugharimiwa matibabu mahala kokote pale kama ingetokea ulazima wa mgonjwa kufanyiwa hivyo, pia mchezaji mwenyewe aliahidiwa mshahara ambao hakuwahi kuupata Simba wala Cannes. Hadi anaumia katikati ya mwaka huu wakati akiichezea TaifaStars, Kapombe alikuwa mlinzi bora namba mbili nchini, ila si kwa kiwango kile ambacho kilimfanya Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’ kuwashinikiza Simba kumsaini kijana huyo akiwa na miaka 19 mwaka 2011.

Matatizo ya kiafya na majeraha yasiyokwisha kwa kiasi kikubwa yamemrudisha nyuma mlinzi huyo bora lakini kwa namna nyingine yeye mwenyewe pia anapaswa kujilaumu kwa hatua yake ya kuondoka Ufaransa wakati angali kinda kwa sababu za kimaslahi. Kapombe aliamini ni bora kucheza Tanzania kuliko daraja la nne Ufaransa lakini kwa miaka hii minne angekuwa wapi kama angeamua kukaza kama Mbwana Samatta ambaye alianza na mshahara mdogo TP Mazembe ambako alidumu kwa misimu mitano na sasa ni staa wa KRC Genk katika ligi kuu ya Ubelgiji huku akipata kipato cha juu zaidi ya kile alichokuwa akipewa TP?

Anaweza kutamba kwa mara nyingine na kufikia ndoto zake

Mlinzi huyo anatarajiwa kuanza kuonekana kwa mara ya kwanza akiichezea Simba tangu alipokubali kurejea klabuni hapo Agosti mwaka huu akitokea Azam FC. Licha ya kusumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara tangu alipokuwa Azam FC, Kapombe ni mchezaji ambaye hujituma na kuonyesha kiwango cha juu kila anapokuwa uwanjani.

Jambo la muhimu kwake hivi sasa ni kucheza kwa tahadhari, huku ikisemwa kuwa mchezaji huyo amekuwa muoga tangu alipopata matatizo ya tumbo miaka miwili iliyopita ni wazi itakuwa vigumu sana kwake kurejea katika ubora ambao watazamaji wamezoea kuuona anapokuwa uwanjani.

Bado ni kijana mdogo na kama Simba watamuhudumia kama walivyokuwa wakifanya Azam FC watamsaidia kurudisha ubora wake lakini wakimsema vibaya kama alivyofanya Zacharia Hans Poppe basi mwisho wa mchezaji huyo kuonekana katika jezi za klabu kubwa nchini itakuwa Mei, 2018 na huko kwingineko atakapokwenda ni wazi itakuwa ni kuhitimisha tarajio kubwa la watanzania ambao waliamini kijana huyo angecheza mahala kokote pale nje ya Tanzania.

Kwa kweli Kapombe yuko mbali sana na kiwango chake kilichomfanya wengi wamtabirie makubwa, ila bado anaweza kujaribu kupambana wakati nafasi yake ya mwisho itakaporejea Simba. Alishafanya makosa kurudi Tanzania mahala ambako mchezaji ‘majeruhi hathaminiwi’ hata kidogo.

Naamini hiki ni kipaji bora ambacho kimepotea kwa sababu kilitaka kupotea chenyewe. Kuondoka Simba hadi Cannes mwaka 2013 utabaki kuwa uamuzi bora kuwahi kufanywa na mchezaji huyo. Kulazimisha kuondoka Cannes na kujiunga Azam FC mwaka 2014 ilikuwa ni uamuzi mbaya japo kuna watu wake waliweza kunufaika. Kuondoka Azam FC na kurejea Simba kwa mara ya pili Agosti, 2017 ni uamuzi mbaya zaidi kuwahi kufanywa na Kapombe, wapi sasa atakwenda? Hakika hiki ni kipaji kinachokwenda kupotea tena kikiwa kimecheza VPL kwa misimu sita tu.

Hiki ndicho kilipelekea Mourinho na Arteta kupigwa chupa, Mourinho ndio chanzo

$
0
0

Ha ikuwa rahisi hata kidogo kwa Derby kubwa na ngumu kama ya Manchester kuisha hivi hivi bila kuwa na habari kubwa, na matokeo ya mechi ilikuwa habari iliyotarajiwa kwani mpira wowote lazima kuwe na matokeo.

Habari isiyotarajiwa ni tukio lililotokea baada ya mchezo huo ambapo inadaiwa kocha Jose Mourinho alikuwa chanzo cha fujo kubwa iliyotokea katila vyumba vya kubadilishia nguo baada ya mchezo huo.

Inadaiwa kwamba wachezaji wa Manchester City walikuwa wakishangilia sana katika vyumba vya kubadilishia nguo huku wakiwa wamefungulia sauti ya mziki kubwa sana kiasi cha kuwasumbua wengine.

Jose Mourinho hakufurahia jambo hilo na aliamua kwenda kuwaambia wapunguze sauti, lakini wakati Mou akiwaambia hivyo kulitokea hali ya majibizano kati ya wachezaji wa Citu wakiongozwa na golikipa Ederson na kocha huyo wa United.

Inadaiwa Ederson alikuwa akibishana na Mourinho na wakati wakiendelea kubishana ndipo kulirushwa kopo la maji ambalo halikumpata vizuri Mourinho na baadae watu wa usalama walituliza hali hiyo.

Lakini katika tukio lingine Mikel Arteta alionekana akitokwa na damu baada ya kupigwa na chupa, huku baadhi ya mashahidi waliokuwa katika tukio hilo wakidai kwamba Lukaku alikuwa karibu na eneo ambalo Arteta alipigwa chupa na inawezekana ndiye aliyeirusha.

Binamu Yangu Anapenda Kukaa Utupu Kila Akiniona Sijui Kwanini?

$
0
0
Mimi ni kijana ninaeishi na kufanya kazi Dodoma, mwezi desemba nilienda kumtembelea binamu yangu alieolewa Dar es salaam, anaishi maeneo ya ukonga.

Kuna matukio yanayotokea na kunishangaza,sasa chumba anacholala binamu yangu na mme wake vinapakana na choo na bafu kama mara tatu hivi wakat naenda bafuni kuoga nilimkuta binamu yangu kaacha mlango wazi huku yuko uchi nikageuka haraka nikarudi nilikotoka.

Mara ya pili binamu yangu alikua ametoka chooni, sasa mimi nilikua naenda kuoga nikamwona bwana akiwa uchi, mara ya tatu tena alikua uchi chumbani huku ameacha mlango wazi cha kushangaza alipogundua hakuhangaika kujisitiri aliendelea na mambo yake,nilipogeuka kumkwepa ndio nikasikia samahani huku yupo very relaxed.

Sijui nifanye nini wadau,msaada tafadhali

Wanaume: Hivi Kwanini Hatuwasifii Wake Zetu Huku Vijiweni Kama Tunavyosifia Michepuko?

$
0
0
Wanaume tumezoea kuwasifia wake zetu kwa namna mbalimbali, mfano; mchapa kazi, mpole, mrembo, ana huruma, roho nzuri, anajua kupika, ni dreva mzuri, n.k. Tukiwa vijiweni tunawasifia mademu wengine kuwa yule ni mtamu, ana manjonjo, analiaga vizuri, mashine mnato,mapaja yake n.k.

Lakini sijawahi kusikia mtu akimsifia mkewe kuwa ana mashine tamu, ana manjonjo katika mechi, anajua kweli mchezo, anajua kukata mauno, n.k. why hatuwasifii kwa haya mambo?Wazee wenzangu ebu tujadili kwanini hatuwasifii wake zetu kuwa ni watamu?

Vijiweni: sehemu za kazi, bar, club, mikutanoni (mida ya break), vibarazani, kunywa kahawa,n.k.

Akina Dada Msijidanganye la Sivyo Mtaishiwa Kufunuliwa tu Mpaka Akili ziwakae Sawa

$
0
0
Leo nimeona niwape vipande vyao hawa akina dada kuanzia umri wa miaka 30 na kuendelea ambao bado hawajaolewa, utakuta mdada mtu mzma kabisa ana umri wa miaka zaidi ya 30 anatafuta wanaume wa kumuoa kwa kuweka masharti lukuki tena magumu Kinoma

Mara nataka Mwanaume Handsome, Mcha Mungu, mwenye elimu ya degree, awe ameajiliwa au anabiashara.

Nabaki kuwashangaa sana nyiyi viumbe, unataka mwanaume mcha Mungu je wewe ni mcha mungu? Ungekuwa na tabia nzuri ungefikisha umri huo ukiwa nyumbani?

Tambua kuwa kitendo cha kufikisha miaka 30 nyumbani na huna mume wala mchumba inabidi ujiulize mara mbili ulikosea nini huko nyuma Kwasababu Kupata Mume umri huo kwa sasa ni Bahati , Wengine Kabisa wanakataa wachumba wakiwa kwenye early 20's Wakijua watastay young Forever...

Utakuta mwingne alizalia nyumban halafu anakuja naye na sifa zake eti nataka mwanaume mnyenyekevu na ambaye hajawai kuoa nyambaaafu wewe umezalia nyumban halafu leo unataka mwanaume ambaye hajawahi kuoa for what?

Mimi nawaambia msijidanganye hata kidogo, mkitaka masharti hayo mtaishia kufunuliwa tu mpaka akili ziwakae sawa.

KWAHERINI

Offer ya X Mass...Ongeza Hips, Makalio, Uume, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

🎁OFFER YA X-MASS.🎁
ONGEZA HIPS, MAKALIO, UUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA SASA.
KATIKA KUSHEREHEKEA MSIMU WA SIKUKUU @natural2162 TUNA PUNGUZO LA 20% KWA BIDHAA ZETU ZOTE, IKIWA NI SHUKRANI KWA KUTUUNGA MKONO.
BIDHAA ZETU ZOTE ZIMETENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA HAZINA KEMIKALI WALA MADHARA.
KWA WANAUME TUNATIBU👇👇
☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa nk.
@natural2162 tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @220,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @130,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @170,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @140,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @220,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @140,000/=
PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
1.Kuongeza hips, makalio na mapaja @180,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @130,000/=
3.Kuwa mweupe bila sugu kwa:-
(a)mafuta @130,000/=
(b) Vidonge @150,000
4.Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @130,000/=
5.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa vidonge (YODI PILLS ORIGINAL) @200,000/=
6Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @130,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @120,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za NATURAL BEAUTY CO

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0659618585 na
0759029968
UTAPATA HUDUMA.
👉🏻OUR WEBSITE:- www.naturalworldbeauty.og
👉🏻INSTAGRAM PAGE:-
@natural2162
@natural2162
@natural2162

Herry James Mwenyekiti Mpya Wa UVCCM , Makamu Wake Ni Tabia Maulid Mwita

$
0
0
Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) umemchagua Kheri James kuwa mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

James amepata kura 319 kati ya kura 583 zilizopigwa akimwacha kwa mbali mpinzani wake, Thobias Mwesiga aliyepata kura 127.

Uchaguzi huo uliofanyika Jumapili Desemba 10,2017 ukihusisha wagombea saba kwa nafasi ya mwenyekiti.

Katika uchaguzi wa makamu mwenyekiti wa UVCCM, Thabia Mwita ameshinda kwa kupata kura 286 dhidi ya mpinzani wake Rashid Mohamed Rashid aliyepata kura 282.

Msimamizi wa uchaguzi huo alikuwa William Lukuvi ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Wagombea wengine waliochaguliwa ni mwakilishi wa vijana katika jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT), Dotto Nyirenda; mwakilishi wa vijana kwenda Jumuiya ya Wazazi, Amir Mkalipa na wawakilishi watatu wa Tanzania Bara kwenda Baraza Kuu la UVCCM ambao ni Rose Manumba, John Katarahiya na Secky Kasuga.

Wengine ni wawakilishi wawili wa Zanzibar kwenda Baraza Kuu la UVCCM ambao ni Nasra Haji na Abdallah Rajabu.

Pia, wajumbe wawili kutoka Zanzibar wanaokwenda Halmashauri Kuu ya Taifa, Abdallaghari Idrisa Juma na Maryam Mohamed Khamis.

Wengine waliochaguliwa ni wajumbe watatu kutoka Tanzania Bara wanaokwenda Halmashauri Kuu ambao ni Sophia Kizigo, Mussa Mwakitinya na Keisha.

Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, mwenyekiti James amewataka vijana kufanya kazi kwa bidii na kutekeleza maagizo yaliyotolewa na mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli.

Ameagiza viongozi wa umoja huo hotuba ya Rais Magufuli aliyoitoa  akifungua mkutano wa tisa wa UVCCM ichapishwe na nakala zisambazwe kwa vijana mikoani na wilayani ili kutekeleza maagizo aliyoyatoa ikiwamo kupambana na rushwa na ubadhirifu wa mali za jumuiya hiyo.

Bei Mpya Ya Mafuta Kwa Mwezi Wa Disemba

$
0
0

MAMLAKA ya udhibiti wa huduma za nishati na maji( ZURA )  imetoa taarifa juu ya bei mpya za mafuta zitakazoanza kutumika rasmi kuanzia leo  Jumanne tarehe 12-12-2017.

Akizungumza na waandishi wa habari huko ofisini kwake Maisara Kaimu Mkurugenzi masuala ya wateja Mussa Ramadhani Haji  alisema kuwa bei hizo Zura imepanga kufuatia mambo yafuatayo;-

Wastani wa mwenendo wa mabadiliko ya bei za mafuta Duniani (Platts Quatations) katika mwezi wa Novemba 2017 , kwa lengo la kupata kianzio cha kufanyia mabadiliko ya bei za mafuta kwa mwezi wa Disemba 2017.

Pia thamani ya shillingi ya  Tanzania , gharama za usafiri , Bima na’ Premium ‘hadi Zanzibar  . Kodi za serikali  na kiwango cha faida kwa wauzaji wa jumla na rejareja.

Alisema bei za rejereja ya mafuta ya Petroli kwa mwezi wa Disemba, 2017 imepanda kwa shillingi (100) kwa lita kutoka shilling 2,130 Mwezi wa Novemba , 2017 hadi shilling 2,230 kwa lita katika mwezi wa Disemba , 2017 sawa na ongezeko la asilimia 4.5%.

Pia alisema bei ya rejereja ya mafuta ya Dizeli kwa Mwezi wa Disemba , 2017 imeshuka kwa shilling (90) kwa lita kutoka shilling 2,280 kwa lita katika mwezi Novemba hadi shilling 2,190 kwa lita katika mwezi wa Disemba, 2017 sawa na  asilimia 4%.

Aidha alisema bei ya reja reja ya mafuta ya Taa kwa mwezi wa Disemb 2017 imepanda kwa shilling (80)  kwa lita kutoka shillingi 1.539 kwa lita katika mwezi wa Novemba , 2017 hadi shilling 1,619 katika mwezi wa Disemba , 2017 sawa na ongezeko la asilimia 4.9%

Vilevile bei ya reja reja ya mafuta ya Banka kwa mwezi waDisemba,  2017 imeshuka kwa shilling (90) kwa lita kutoka shillingi 2,122 kwa lita katika mwezi wa Novemba, 2017 hadi shilling 2,032 katika mwezi wa Disemba , 2017 sawa na ongezeko la asilimia 4.4%.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.

M 2 The P adai hakuna beef la Diamond na Alikiba

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, M 2 The P amesema haamini iwapo Diamond na Alikiba wana beef kama inavyokuwa ikiripotiwa.

Amesema kilichopo kati ya Alikiba na Diamond ni ushindani wa kimuziki kitu ambacho ni kizuri katika ukuaji wa muziki wa Bongo Flava.

“Siwezi kusema wana beef labda wana ushindani wa muziki, kila mtu anajali kufanya kazi vizuri, Mungu awalijie waendelee kufanya vizuri, sitaki beef waendelee tu muziki wetu ufike mbali” M 2 The P ameiambia Bongo5.

M 2 The P amemtolea mfano Diamond kwa kusema ameweza kufanya kolabo na wasanii wengi wa kimataifa kitu ambacho kimeitangaza Afrika Mashariki kimuziki na ndivyo inavyotakiwa na siyo beef.

Ubunge: Steve Nyerere Kuziba Nafasi ya Mtulia Kinondoni (Video)

$
0
0
Msanii wa filamu, Steve Nyerere ameweka wazi mpango wake wa kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la Kinondani baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Mhe. Maulid Mtulia kupitia tiketi ya CUF na kukihama chama hicho na kuamua kuhamia CCM hivyo na kupoteza sifa ya kuwa mbunge.

VIDEO:

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Matokeo mabovu ya Kili Stars Julio kashindwa kuyavumilia

$
0
0
Kama unavyofahamu Kilimanjaro Stars imetupwa  nje ya kombe la Chalenji huku ikiwa haijashinda hata mchezo mmoja kati ya minne iliyocheza kwenye kundi lake lililokuwa na timu tano. Tanzania ilipoteza mechi zake tatu (Tanzania bara 1-2 Zanzibar, Rwanda 2-1 Tanzania bara, Kenya 1-0 Tanzania bara) na kutoka suluhu katika mechi moja (Libya 0-0 Tanzania bara).

Kocha mzoefu Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ambaye kwa sasa anafundisha Dodoma FC inayoshiriki ligi daraja la kwanza matokeo waliyopata Kili Stars kama wangepata vijana wa Serengeti Boys ‘sasa Ngorogoro Heroes’ waliocheza AFCON U17 hakuna mtu ambaye angeshangaa kwa sababu tungesema tunawapa uzoefu vijana.

Julio  pia amegusia suala la kocha Ammy Ninje kupewa timu, kwa upande wake amesema, hana tatizo na kocha huyo isipokuwa inawezekana hana uzoefu wa kutosha kufundisha timu ya taifa ukizingatia amekaa nje ya nchi kwa muda mrefu hivyo inawezekana anakosa uzoefu kwa wachezaji wa kibongo na tamauni zao.

“Mimi simpingi Ammy ni kijana wangu na alikuja kucheza kwenye timu ya taifa, lakini kwa jinsi alivyoishi huko hatujui kazi yake kubwa aliyokuwa anafanya ingawa inasemekana ni kocha wa vijana lakini tusiamini kila mtu kwa kipindi hiki tulichonacho. Wachezaji wetu wanahitaji kumzoea mtu kulingana na mazingira, anaweza kuja mtu akawa na style yake halafu wachezaji wakashindwa kwenda nayo kwa kipindi hicho kifupi cha mashindano.”

“Lakini kama suala la muungano si yupo Mecky Maxime ambaye ndio alikuwa kocha bora, unapokuwa kocha bora maana yake nini? Unapokuwa kocha bora inawezekanaje usiwe kocha wa timu ya taifa. Uongozi wa TFF uliopita ulikuwa na ukiritimba na chuki ya kukataa watu fulani kwa sababu ya faida zao sasa hivi naona TFF ina watu ambao tunategemea wanabusara na ueledi mkubwa watu kama Kidao amecheza mpira sasa hivi ni Kaimu Katibu wa TFF, Msafiri Mgoyi ni muumini wa timu za vijana.”

“Nilitarajia matokeo haya tungeyapata kwa timu yetu ya Serengeti Boys kwa sababu tungekuwa tunatengeneza exposure kwa vijana lakini tunapeleka timu hiyohiyo wachezaji ambao kila siku tunafungwa. Tungepeleka watoto tungesema tunawapa uzoefu lakini tumepeleka wakubwa ambao ndio tunawategemea kwenye mashindano yote lakini bado tumefungwa.”

“TFF waangalie kwa umakini mkubwa sio tunaaminia tu kwa sababu ambazo wanazijua wao mwisho wa siku Ammy anarudi Uingereza aibu inakuja kwetu. Tatizo halianguki kwa Ammy inaonekana TFF wakosefu hakuna makocha wa kufanya kazi.”

Kuna wakati Julio na Charles Boniface Mkwasa walikuwa makocha wa timu ya taifa, lakini jambo ambalo si la kutegemewa wachezaji wao waliwahi kuzomewa na mashabiki kutokana na matokeo mabovu, Julio ametoa ufafanuzi juu ya hilo.

“Mimi nimefundisha Simba, Mkwasa amefundisha Yanga kwa bhiyo tunapokuwa na wachezaji wa Yanga watatu, Simba saba kwa sababu yupo Julio, wachezaji wa Simba watazomewa lakini wakiwa wa Yanga tisa wa Simba watatu wa Yanga watazomewa. Hatuwezi kufika, na wapenzi wa soka ndio tunasababisha hali hii, turudi kwenye wakati ule aliokuwepo Marcio Maximo wakati timu inahamasishwa na na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete.”

“Rais Kikwete alikuwa analipa makocha na aliupenda mpira kwa kiasi kikubwa, kama tungempa support kubwa leo tungfekuwa mbali sana kwenye soka lakini mchango wote wa Kikwete umepotelea hewani bila kujijua matokeo yake leo tunahangaika.”

“Ninaimani TFF mpya iliyoingia kama wanataka kumpa timu kocha mzawa kama vile Mayanga basi apewe stahiki zote zinazostahili ambazo angepata kocha mzungu lakini ukimnyima inakuwa  tatizo na wapenzi nao wai-support timu yao ya taifabila kujali huyu Yanga wala Simba maana ndio siasa za mpira wan chi hii kinyume cha hapo hatuwezi kupata mafanikio ndio maana unaona timu yetu inaenda hovyo.”

“Wachezaji wetu lazima wajitoe bila kujitoa hatuwezi kupata mafanikio, angalia Zanzibar siku zote tukicheza nao, mimi nikiwa mchezaji wa timu ya taifa tumecheza na Zanzibar mara mbili, moja Uganda wakawa mabingwa marea ya pili Malawi zote walitufunga goli mojamoja kwa sababu wachezaji wa kizanzibar wana commitment wanapotaka kushindana matokeo yake leo wanaonekana wanatumia dawa za kusisimua misuli. Kwa hiyo tujifunze kutoka kwao.”

Hatua ya makundi ya Challenge Cup imehitimishwa jana jioni ambapo tayari timu nne zilizofuzu hatua ya nusu fainali zimeshajulikana na zilizoaga mashindano tayari zinafahamika. Zanzibar walipoteza mechi yao kwa kufungwa 1-0 na Libya lakini wamefanikiwa kupenya kucheza nusu fainali ambapo watacheza dhidi ya Uganda (mabingwa watetezi) siku ya Ijumaa.

“Timu ya Taifa si Sehemu ya Kujifunzia Ukocha”-Mwambusi Arusha Dongo

$
0
0
Kocha aliyetamba na kikosi cha Mbeya City Juma Mwambusi ametoa maoni yake kuhusiana na timu ya taifa ya Tanzania bara ‘Kilimanjaro Stars’ kufanya vibaya kwenye mashindano ya Chalenji 2017 ambapo amesema, timu ya taifa sio mahali pa kujifunzia ukocha.

Mwambusi ambaye amewahi kufanya kazi kama kocha msaidizi kwenye timu ya Yanga ameonesha kusikitishwa na matokeo mabovu ya Kili Stars kwenye mashindano ya mwaka huu na kuongeza huenda ugeni wa mwalimu ukawa moja ya tatizo kwa timu hiyo kushindwa kufanya vyema.

“Kinachosikitisha watanzania ni timu yetu kufanya vibaya sana katika mashindano ya Chalenji yanayoendelea kule Kenya. Kubwa kama mwalimu ni kuelezana ukweli, watanzania wanataka matokeo mazuri kitu ambacho kocha aliyeteuliwa na wachezaji lazima wajitume na kujitolea kwa ajili ya nchi yao.”

“Timu ya Taifa watu wanaitegemea ni kigezo gani TFF wanakitumia kuteua kocha ni swali ambalo nimekuwa nikiulizwa na wadau wengi wa soka kwa sababu wanaamini kutokana na taaluma yangu na uzoefu huenda nikawa najua, lakini hata mimi sifahamu TFF ndio wenye majibu na wanatakiwa kuwajibu watanzania wapenda michezo kwamba ni vigezo vipi wanavyovitumia.”

“Mwalimu huyu ni mgeni katika soka la Tanzania labda kama alicheza lakini hajafundisha kwa sababu lazima ufundishe vilabu vya ligi kuu ili uweze kuteuliwa mwalimu wa timu ya taifa, lakini sio kufundisha tu umefanya nini katika klabu au vilabu ulivyofundisha. Una wasifu mzuri unawajua watanzania unajua utamaduni wa wachezaji wetu, kwa sababu mwalimu anaweza kuwa mzuri lakini anafundisha katika mazingira yapi na yeye katoka mazingira gani?”

“Watanzania wataendelea kuumia hadi lini kutokana na matokeo ya timu yao ya taifa? Isiwe sehemu ya kujaribia makocha ni kutowapa thamani watanzania ambao mioyo yao inapenda sana matokeo mazuri kutoka kwa timu yetu.”

“Nakumbuka Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassani Mwinyi aliwahi kusema “timu yetu imekuwa kichwa cha mwendawazimu” kwa hiyo kuifuta hii kauli ni lazima tufanye vizuri. Inatakiwa timu iwe na mwelekeo, naishauri TFF kwamba walimu wapo waliofundisha ligi kuu wamefanya vizuri wanatakiwa wapewe nafasi wafundishe timu ya taifa tumechoka kuumia, timu ya taifa sio sehemu ya kwenda kujifunzia au kujaribia.”

“Wachezaji tutawalaumu lakini labda waliletewa utamaduni ambao hawajauzoea na wao wanatakiwa kujituma katika timu yao kwa sababu sisi watanzania tunaumia.”

Beny Kinyaiya Anatarajia Kuvuta Jiko

$
0
0
Beny Kinyaiya Anatarajia Kuvuta Jiko
MTANGAZAJI maarufu Bongo, Ben Kinyaiya amefunguka kuwa anatarajia rasmi kuvuta jiko.
Kinyaiya aliiambia Full Shangwe kuwa, Mungu akijalia hivi karibuni atauaga ukapera rasmi kwa kufunga ndoa na mwenza wake ambaye hakutaka kumuanika wazi.
“Unajua ndoa ni mapenzi ya Mungu, kama mwanadamu sina mamlaka kihivyo, ila Mungu akijalia ‘soon’ ninafunga ndoa na mwandani wangu,”alisema Kinyaiya.

Dully Sykse Atokwa Povu Kisa Bomberdier Atangaza Vita kwa Wasanii Wenzake

$
0
0
Dully Sykse Atokwa Povu Kisa Bomberdier Atangaza Vita kwa Wasanii Wenzake
ETI kisa Bombardier! Mkongwe wa Bongo Fleva nchini, Dully Sykse ametoa povu ikiwemo kutangaza vita na wasanii wa kizazi kipya kwa sababu ya kushindwa kumsapoti kwenye wimbo wake mpya.

Dully Sykes ambaye ameachia wimbo mpya wa Bombardier, alisema wasanii wa sasa ambao wengi ni wapya wana roho mbaya na yeye yuko tayari kupambana nao.

“Wasanii wa sasa wana roho mbaya, hawasapotiani kama wasanii wa zamani, ndiyo maana Bombadier yangu hawajanisaidia kuitangaz, hiyo inaonesha muziki ni vita na mimi niko tayari kupambana nao,” alisema Dully

M2 The P Afunguka Kuhusu Beef la Alikiba, Diamond

$
0
0
M2 The P Afunguka Kuhusu Beef la Alikiba, Diamond
Msanii wa muziki Bongo, M 2 The P amesema haamini iwapo Diamond na Alikiba wana beef kama inavyokuwa ikiripotiwa.

Amesema kilichopo kati ya Alikiba na Diamond ni ushindani wa kimuziki kitu ambacho ni kizuri katika ukuaji wa muziki wa Bongo Flava.

“Siwezi kusema wana beef labda wana ushindani wa muziki, kila mtu anajali kufanya kazi vizuri, Mungu awalijie waendelee kufanya vizuri, sitaki beef waendelee tu muziki wetu ufike mbali” M 2 The P ameiambia Bongo5.

M 2 The P amemtolea mfano Diamond kwa kusema ameweza kufanya kolabo na wasanii wengi wa kimataifa kitu ambacho kimeitangaza Afrika Mashariki kimuziki na ndivyo inavyotakiwa na siyo beef.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images