Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Pep Gurdiola Awaomba Radhi Manchester United “Kinafiki”

$
0
0
Baada ya mchezo kati ya Manchester United na Man City mwishoni mwa wiki iliyopita, inadaiwa kuliibuka fujo kubwa katika eneo la kuelekea vyumba vya kubadilishia nguo la uwanja wa Old Traford.

Chanzo cha fujo hiyo kinatajwa kwamba ni kitendo cha Manchester City kushangilia sana na kupiga kelele nyingi, jambo hilo liliwakera baadhi ya watu wa United akiwemo Jose Mourinho na mvutano ulianzia hapo.

Pep Gurdiola ambaye ndiye aliwaongoza vijana wake kuichapa United bao 2 kwa 1 amesema hawakuwa na nia ya kuwakera Manchester United kwani wao walikuwa wakishangilia tu lakini kama wamekereka anawaomba msamaha.

“Lakini na wao kuna michezo ambayo walishinda na wakashangilia sana, sisi tumeshinda Derby na tulipaswa kufurahia hilo na kama limewaudhi tunaomba radhi kwa kila mtu wa United aliyekereka” alisema Pep.

Pep Gurdiola amesisitiza kwamba akama timu ikifanya vizuri uwanjani na ikaibuka na ushindi kinachofuatia ni kwenda katika vyumba vya kubadilishia nguo ambapo watu wanakwenda kufurahia walichofanya.

Tayari shirikisho la soka nchini Uingereza FA limeiandikia Manchester United barua kuhusiana na tukio hilo ambapo inadaiwa kwamba kulikuwa na vitendo vya urushwaji wa chupa za maji na maziwa kati ya pande hizo mbili.

Van Gaal Aibuka na Kuishambulia United kwa Mpira Mbovu Pamoja na Mkurugenzi wao

$
0
0
Jose Mourinho alitua Manchester United kuchukua mikoba ya kocha Mdachi Louis Van Gaal jambo ambalo hadi leo Mdachi huyo amekuwa akililalamikia sana kwa jinsi alivyoondolewa United.

Van Gaal amekuwa mkimya sana na hazungumzii sana maisha yake yalivyokuwa United lakini safari hii LvG ameibuka na kuishambulia Manchester United akidai kwamba wanacheza kpira mbovu.

Baada ya mchezo kati ya Manchester City zidi ya Manchester United Van Gaal amesema United hawavutii kuwatizama kwa sasa na kama utamuuliza anapenda kuingalia timu gani ni Man City.

Van Gaal amesema wakati yupo Manchester United alikuwa akicheza zaidi mchezo wa kushambulia lakini wapinzani walikuwa wakizuia tofauti na sasa ambapo United wanaonekana kuzuia zaidi.

Kuhusu kuwa na bifu kati yake na Mourinho ,LVG amesisitiza kwamba hana ugomvi na Mourinho ila ana tatizo na mkurugenzi wa klabu hiyo Ed Woodward kutokana na namna ambayo mkurugenzi huyo alimfukuza kazi Van Gaal.

Kinachomuuma zaidi Van Gaal ni namna ambavyo mke wake alifahamu kufukuzwa kwake ambapo LVG anadai mkewa aligundua kuwa Van Gaal anafukuzwa wakiwa kwenye lift na familia ya Woodward.

Kutana na Mtabibu wa Nyota Duniani Maalim Fadhil Rashid Kutoka Comoro Kwa sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436

Husna Maulid Afunguka Kuhusu Bifu Lake na Wolper "Aliyekuwa Anatugombanisha ni Mwanaume"

$
0
0
 Husna Maulid Afunguka Kuhusu Bifu Lake na Wolper "Aliyekuwa Anatugombanisha ni Mwanaume"
MASTAA wawili waliokuwa na bifu kwa sababu ya kuchangia bwana Mkongo ajulikanaye kama Mwami Radjabu, Jacqueline Wolper na Husna Maulid wamemaliza uhasama kati yao na sasa ni full vicheko.

Hali hiyo ilijidhihirisha juzikati kwenye sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya Wolper, walipoonekana wakiwa karibu na

Husna Maulid.
kufurahi huku vyanzo vikisema warembo hao walielewana baada ya Husna kumwagana na bwana huyo.
“Si unajua Husna alishamwagana na Mwami ambaye alimvisha mpaka pete ya uchumba lakini hawakufanikiwa kufunga ndoa, kwa hiyo walimaliza tofauti zao,” kilisema chanzo.

Baada ya kuona na kupata habari kutoka kwa chanzo, Za Motomoto News

ilimtafuta Husna ambaye awali alikuwa hapendi kabisa kumsikia Wolper ambaye alikiri kumaliza tofauti zao.
“Tulishamaliza tofauti zetu, sina bifu na Wolper maana aliyekuwa anatugombanisha ni mwanaume na sisi ni wanawake hivyo wanawake tujifunze kuwa wanaume ni watu wa kupita tu,” alisema Husna.

Barnaba: Naitaji Wasanii wa Kike Katika Labe Yangu

$
0
0
Barnaba: Naitaji Wasanii wa Kike Katika Labe Yangu
Msanii wa muziki Bongo, Barnaba amesema mwakani anahitaji kuanza kuchukua wasanii kwa ajili ya label yake ila wa kike pekee.

Muimbaji huyo ameiambia 5 Selekt, EATV kuwa anahitaji wasanii wa kike watatu kwani wa kiume tayari wapo wengi katika game.

“Mimi label yangu ni changa hata mwaka jana nilisema nitatambulisha wasanii, mwakani nitamtoa (Mula) na nitaanza kuchukua chapa nyingine na in fact nimesema nahitaji wasanii wa kike sana, nahitaji wa kike watatu tu” amesema Barnaba.

“Kwa hiyo wa kiume atabaki Mula pekee na ni sababu ya msingi sana wanaume tupo wengi sana, halafu nimeamua kufanya hivyo kwa sababu mimi ni mwandishi mara nyingi nyimbo zangu zinawiana kwa mabinti na nimeamua kuja hivyo, am sure mtu kama Diamond ameshasaidia sana” ameongeza.

Mfungwa Mwenye Umri Mkubwa Aliyepata Msamaa Wa Rais Akili Kuua "Niliua Kweli, Naomba Mungu Anisamehe"

$
0
0
Mfungwa Mwenye Umri Mkubwa Aliyepata Msamaa Wa Rais Akili Kuua "Niliua Kweli, Naomba Mungu Anisamehe"
Matonya ndiye mfungwa mwenye umri mkubwa kuliko wote walioachiwa kwa msamaha wa Rais siku ya Uhuru, Desemba 9.

 “Bado ninalo neno la kumwambia Rais (John) Magufuli kama nitakutana naye, lakini kama nitashindwa kumuona nitabaki na neno hilo moyoni mwangu, ila Watanzania wajue kuwa niliua kweli naomba Mungu anisamehe na wao wanisamehe pia.” Hayo ni maneno ya Mganga Matonya.

Matonya ndiye mfungwa mwenye umri mkubwa kuliko wote walioachiwa kwa msamaha wa Rais siku ya Uhuru, Desemba 9.

Matonya (85), ambaye ametoka Gereza la Mkono wa Simba mkoani Morogoro na kurudi kijijini kwao Wiliko, Wilaya ya Chamwino anasema hadi sasa anahisi kama anaota kwa kuwa hakuwahi hata siku moja kuwaza kuwa angetoka gerezani na kurudi uraiani.

Kijiji cha Wiliko kipo umbali wa kilomita 81 kutoka katikati ya Mji wa Dodoma katika barabara ya kuelekea Iringa, kijiji hicho kipo mwishoni mwa wilaya hiyo jirani na Jimbo la Isimani mkoani Iringa.

Matonya ni nani

Mganga Matonya ‘Chigoma’ ni baba wa watoto sita, wajukuu 34 na vitukuu tisa ambao wanaishi kijijini hapo.

Matonya ni miongoni mwa wafungwa 8,157 waliopata msamaha wa Rais Magufuli, lakini akiwa mfungwa mzee kuliko wote huku akidumu gerezani kwa miaka 44 ambayo aliishi katika magereza ya Isanga (Dodoma) na Mkono wa Simba (Morogoro).

Kwanini alikwenda gerezani?

Tofauti na wengi ambao huzunguka pale wanapohisi kuwa wamekosea, Matonya anasema moja kwa moja kuwa, “niliua baada ya kuona mwenye mali analeta ugumu na mimi pamoja na wenzangu watatu tukachukua ng’ombe 12.”

“Nilikuwa na tabia ya wizi wa mifugo enzi hizo nikiwa kijana, maeneo mengi tuliiba, lakini siku hiyo ilikuwa mimi na rafiki yangu Muyeya Nyagalu ndugu zetu wa kabila la Masai wawili, tulikuta ng’ombe wale wazuri sana, lakini mwenye mifugo alikuwa mkali na kama tungekuwa watepetepe mmoja wetu angekufa hapo.

“Tulipomuua tuliondoka na mifugo na utaratibu huwa ni kugawana kila mtu anakwenda na mzigo wake, hapo ndipo kosa langu lilipotokea maana nilikwenda mnadani na nilikamatwa nikiwa na ng’ombe sita.”

Hata hivyo, anasema alipokamatwa mnadani, alifanikiwa kuwakimbia wakamataji na akarudi hadi nyumbani kwake, lakini siku tatu baadaye alishangaa kuona kundi la watu likiwa limezingira nyumba yake na wakati huo alikuwa juu ya nyumba yake ya tembe akiendelea kuezeka udongo kwa kuwa msimu wa mvua ulikuwa umekaribia.

Apelekwa Isanga

Tangu Oktoba 1974, Matonya ambaye alijulikana kwa jina la utani la Chigoma alikuwa katika mahabusu ya Gereza la Isanga, lakini miaka sita baadaye alihukumiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa.

Kwa mujibu wa maelezo yake, ushahidi usio na shaka uliwatia hatiani yeye na Nyagalu huku watu wengine waliokuwa wamekamatwa kwa makosa hayo wakiachiwa huru na wale ndugu zao wa kabila la Masai hawakuonekana hata kwenye kesi.

Kabla ya kueleza mengi, anakiri kuwa wapo watu waliofungwa magerezani kwa makosa ambayo hawakuyatenda lakini yeye alikuwa gerezani kwa kosa ambalo alilitenda.

Mzee huyo ambaye anarudia rudia maneno ya kuomba msamaha mbele za Mungu na wanadamu, anasema hukumu aliyopewa ilistahili kwa kuwa hata walipomuua mfugaji bado hakuona shaka kama damu ya mtu ilikuwa imemwagika bali aliwaza kupata mali.

Anasema katika hukumu hiyo ya mwaka 1983, alijua angenyongwa muda si mrefu na hivyo alikuwa amekata tamaa ya maisha na hakuwaza chochote zaidi ya kuagiza mkewe aende wakaonane na kumuaga.

“Kikubwa nilichokuwa nafanya mle gerezani ilikuwa ni kufanya kazi, kwa kweli mimi nimefanya kazi nyingi sana gerezani nilizotumwa na ambazo sikuwa nimetumwa, maana nilijua hiyo ndiyo sehemu ya kujiliwaza kwani ukifanya kazi ngumu unachoka na hivyo ukilala unapata usingizi,” anasimulia.

Abadilishiwa kifungo

Mzee Mganga anaukumbuka mwaka 1983 alipopelekewa taarifa na mkuu wa gereza ambaye amemsahau kwa jina kwamba Rais wa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere alikuwa amemsamehe adhabu ya kunyongwa hadi kufa na kuwa kifungo cha maisha.

“Ndiyo maana nasema kama mtu akinipeleka kwenye kaburi la Nyerere ningeinama na kumshukuru sana mzee huyu, maana asingefuta adhabu ya kifo huenda huyu wa sasa (Magufuli) asingenikuta hai,” anasema Mganga.

Anasema katika fikra zake aliamini kuwa angeweza kuishi walau hata miaka mitano mbele, lakini tumaini la kurejea uraiani halikuwapo.

Baada ya kubadilishiwa adhabu hiyo, alikaa Gereza la Isanga kwa mwaka mmoja kisha akapelekwa Gereza la Mkono wa Simba mkoani Morogoro ambako alikaa kwa miaka 33.

Maisha ya gerezani

Mzee huyo mchangamfu anasema maisha ya gerezani ni ya tabu na kukatisha tamaa.

“Kule hakufai, hakuna uhuru, hakuna masikilizano yaani kuna utofauti mkubwa na huku uraiani. Hata hivyo askari magereza wanafanya kazi ngumu sana maana mchanganyiko wa watu una shida kwa ujumla,” anasema mzee Matonya.

Anasema gerezani hakuna upendo na busara zake ndani ya gereza ndizo zilimpa nafasi nyingi za kuongoza wenzake na kuwasimamia mpaka ukafika wakati akaona walau ugumu wa maisha unapungua.

Hata hivyo, anasema katika maisha yake gerezani alikuwa mfano mzuri wa kuchapa kazi.

Nini anakikumbuka gerezani?

“Siwezi kukumbuka kitu mle ndani zaidi ya kuwaombea ndugu na vijana wangu niliowaacha mle ambao wengi naamini itawachukua muda mrefu kurudi uraiani,” anasema.

Kingine anachokumbuka ni namna ambavyo mkewe na watoto walivyokuwa wakimtembelea mara kwa mara akiwa Isanga, lakini anataja ugumu wa maisha kuwa uliifanya familia yake ishindwe kwenda mara nyingi mkoani Morogoro.

Anakumbuka mke wake alikwenda mara moja mkoani humo katika kipindi cha miaka 33, huku mtoto wake mkubwa akifika mara mbili na mkewe lakini mwanawe wa tatu alikwenda mara nyingi zaidi na familia yake.

Kitu gani anatamani maishani?

Kwa sasa Mganga anatamani kupata nafasi ya kuwa mshauri wa vijana na watu wenye tabia za wizi na udokozi, akisema kuwa hazilipi hata kidogo zaidi ya kuwarudisha nyuma.

Kazi hiyo alikuwa akiifanya tangu alipokuwa gerezani na anasema baadhi ya watu aliokuwa akiwapa ushauri huko walikuwa wakirudi uraiani wanakuwa raia wema kiasi cha kumtembelea gerezani kwa ajili ya kumshukuru.

Ombi lake jingine ni kwa jamii pamoja na Serikali kumuonea huruma na kumwezesha walau kitu chochote cha kuanzia maisha na mkewe ambaye anasema kwamba alikuwa mvumilivu wakati wote, licha ya kuzaa watoto watatu nje ya ndoa yao lakini bado aliwaandika kuwa katika ukoo wake na alivumilia kuishi na familia yake hadi mwisho.

Anasema kwamba hawezi kurudia kosa la aina yoyote zaidi ya kuishi kwa kumtegemea Mungu na kujikita katika kilimo ili mvua zikinyesha apate chakula cha familia yake.

Alipataje taarifa ya kuachiwa?

Anasema siku ya sherehe za uhuru akiwa na wenzake na kwa sababu ya umri wake alikuwa amelala kivulini, huku wafungwa wengine wakisikiliza na kuangalia televisheni.

Anaeleza kuwa ghafla mfungwa mwenzake anayemtaja kwa jina moja la Mlyuka mwenyeji wa mkoa wa Njombe alimfuata na kumwambia kuwa majina yao yametajwa kwamba wamesamehewa.

“Nilimuuliza Mlyuka kama ni kweli akasema ni kweli tumetajwa,” anasema mzee Mganga na kuongeza kuwa baadaye wafungwa wenzake waliwapongeza kabla ya askari wa gereza kuwaita na kuwaambia wajiandae ili siku inayofuata waruhusiwe.

Mabadiliko anayoyaona

Kutokana na kuishi muda mrefu gerezani, anasema hata kijiji chake anaona si kile alichokiacha zaidi akikumbuka miti mikubwa michache aliyoiacha.

Kwa mujibu wa mzee huyo hata jua anaona linatokea upande ambao halikuwa likitokea na wakati mwingine anahisi kuwa hayuko katika dunia ya sasa.

Mzee Matonya anafurahi kuwa anaongea na watu kwa uhuru mpana tofauti na wakati ambao alikuwa anaongea na nduguze akiwa gerezani kwa kuhesabiwa dakika,.

Jambo jingine lisilomfurahisha ni namna ambavyo mazingira yameharibiwa zaidi kijijini kwao huku idadi ya watu wakiongezeka na majumba kuwa mengi.

Simulizi ya watoto

Kwa mujibu wa mtoto wa pili wa mzee huyo aitwaye Jeremiah Mganga, baba yake alikamatwa wakati yeye akiwa na miaka mitano na tangu wakati huo maisha yao yalikuwa magumu.

Jeremiah mwenye mke, watoto watatu na wajukuu watatu anasema wakati wote baba yao alikuwa akiwaagiza yeye na wadogo zake kwenda na mama yao katika Gereza la Isanga.

Anasema siku ya kukamatwa kwa baba yake alikuwa nyumbani kwao anacheza nje na mama yake, ndipo ghafla akaona watu wengi baadhi wakiwa wamevalia kofia, lakini kwa umri wake alijua ni ndugu waliokwenda kumchukua baba kwa ajili ya mambo yao.

Jeremiah anasema kuwa mama yake mzazi ndiye aliyepata wakati mgumu zaidi kwa kuwa alikuwa akitengwa sana na jamii kijijini na hata yeye (Jeremiah) aliona kila kitu hadi alipokuwa mtu mzima.

Anasema aliamua kuihamisha familia yao kutoka mahali alipowaacha baba yao na kwenda katika kitongoji kingine ndani ya kijiji hicho. “Lakini namshukuru sana mdogo wangu huyu Aron (anamuonyesha), mwenzetu alikuwa anakwenda mara kwa mara Morogoro na kutuletea taarifa za huko na alikwenda na familia yake mara kadhaa ndipo nasi tulikwenda mara mbili,” anasema.

Kwa sasa hana hofu juu ya maisha ya baba yake kwamba kurudi kwake hakuwezi kuhatarisha maisha kwa kuwa anaamini tukio lililomfanya afungwe ni la muda mrefu na hata familia ambayo ndugu yao aliuawa watakuwa wamewasamehe.

Kwa upande wake, Aron ambaye baba yake alimuacha akiwa bado tumboni mwa mama yake, anasema alikuwa akipata shida kuishi mbali na mzazi wake huyo na alianza kumfahamu akiwa gerezani.

“(Wakati yupo) Isanga nilikuwa bado mdogo, lakini nilipomaliza shule ya msingi nilitumia nguvu kubwa kumtafuta hadi nikamuona alipo, ndipo nikawa nakwenda mara kwa mara mimi na mke wangu pamoja na watoto wangu watatu,” anasema.

Aron anasema awali kaka yake aliwahi kuuza ng’ombe watatu ili amtafute baba yake gereza alilokuwa baada ya kuambiwa kuwa hayupo Isanga, lakini walishindwa hadi fedha ziliisha kabla ya yeye kumuibua mwaka 1997.

Anasema kabla ya kuachiwa kwa msamaha wa Rais, alitumia kila njia kuona baba yake anarudi uraiani lakini alishindwa na kwamba, alishangaa Desemba 9 akipigiwa simu kuambiwa kuwa jina la baba yao lilitajwa.

Aron anasema kama baba yake angekuwa nyumbani tangu 1974 na akajikita zaidi katika kilimo, maisha ya familia hiyo yangekuwa mazuri na yenye mafanikio kiuchumi.

Majirani wanamzungumziaje?

Victoria Ulaya (87) ambaye walikuwa majirani tangu wakati huo, anasema hakuwahi kujua kama Matonya ni mwizi wa mifugo kwa kuwa tabia hiyo hakuionyesha katika maeneo yao.

Anasema hata siku ya kukamatwa kwake wengi walionyesha mshangao kuona kumbe ndiyo kitu alichokuwa anakitegemea.

Victoria anasema kwamba siku alipokamatwa Matonya kundi la watu lilifika nyumbani kwake kutaka kujua kilichomsibu, lakini hata matajiri wa ng’ombe walimtetea.

“Tulishangaa zaidi tuliposikia kuwa ameiba tena ameua, ha! Ni huyu Mganga? Wakasema ndiyo, tukafumba midomo kweli, lakini kabla ya hapo alikuwa ni mstaarabu aliyempenda mke wake kweli,” anasema jirani huyo.

Balozi wa nyumba kumi

Balozi wa mtaa anaoishi Matonya, Ainea Sendu anasema maisha ya familia hiyo ni mazuri na hakuna mtoto hata mmoja aliyezaliwa na mzee huyo mwenye tabia ya udokozi.

Sendu (49) anasema alianza kusikia habari za Matonya tangu akiwa mtoto na kuwasikia watu wakiimba nyimbo kwenye vilabu vya pombe zilizomtaja, lakini hakuwa na tumaini kwamba ipo siku atakuja kukutana naye.

Balozi huyo anasema kwa sasa wanashirikiana na familia hiyo ili kutengeneza utaratibu wa kwenda kumshukuru Mungu kanisani.

Sendu anasema kwamba anakusudia kupeleka wazo kwa uongozi wa kijiji ili wamfanye mzee huyo kuwa mmoja wa wazee washauri.

Kiongozi huyo wa mtaa anasema sasa katika makazi ya Matonya ni kama kuna kituo cha utalii kwa kuwa idadi ya watu wanaofika eneo hilo ni kubwa zaidi kuliko maeneo mengine na wengi wanashinda hapo, huku wakimsikiliza mzee huyo ambaye wakati wote anaonyesha kujutia kosa alilofanya

Mo wa Simba Apata Pigo Afiwa na Mwanaye

$
0
0
Mo wa Simba Apata Pigo Afiwa na Mwanaye
Kiungo wa klabu ya Simba, Mohammed Ibrahim amepata pigo jana baada ya kumpoteza mtoto wake wa kiume aliyefariki dunia

Klabu ya Simba pamoja na mashabiki wa klabu hiyo wameungana na Watanzania wengine kumpa pole kiungo wao kwa pigo kubwa alilopata kumpoteza mtoto wake wa kiume ambaye bado alikuwa mdogo.

"Klabu ya Simba inatoa pole kwa kiungo wetu 'Mohammed Ibrahim' kwa kufiwa na mwanae mpendwa, tumeumia sote kwa msiba huu wa mtoto wetu mdogo kabisa. Klabu ya Simba inatoa pole kwa msiba huu mzito kwako na kwa famila nzima. Inna lillah wainna ilaihi Raajiun" alisema taarifa ya Simba 

Baada ya Taarifa ya Kuhojiwa Uraia Wake Askofu Niwemugizi JPM Ampigia Simu

$
0
0
Baada ya Taarifa ya Kuhojiwa Uraia Wake Askofu Niwemugizi JPM Ampigia Simu
Baada ya kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusu uhalali wa uraia wake Askofu wa Jimbo la Ngara - Rulenge, Severine Niwemugizi ameeleza kwamba amezungumza na Rais John Magufuli.

Askofu Niwemugizi akizungumza na Mwananchi kwa simu jana kujua kile walichozungumza na Rais Magufuli hasa baada ya kuandika ujumbe wa kumpongeza Rais kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Facebook, kiongozi huyo wa kiroho alisema, “Ni kweli leo (jana) nilizungumza na Rais Magufuli, alinipigia simu na tumekuwa tukiwasiliana kujuliana hali.”

Jana, askofu huyo alikaririwa akisema amehojiwa mara mbili na Uhamiaji katika kile kinachoelezwa ni utata wa uraia wake huku akieleza kuwa amezaliwa wilayani Biharamulo mkoani Kagera.

Alipoulizwa kama mazungumzo hayo ni baada ya taarifa za kuhojiwa na Uhamiaji, Askofu Niwemugizi alijibu huku akianza kwa kucheka, “Hahahahaha!! Ni kweli Rais kataka kujua hasa kuna nini, yeye amesema atalifuatilia na kukiwa na... nitamfahamisha.”

Askofu huyo ambaye Septemba mwaka huu aliibua mjadala wa Katiba Mpya na kusema kuwa yuko tayari kuitwa mchochezi endapo kundi la watetezi wa haki za binadamu watachukuliwa kama wachochezi alisema kuhojiwa huko hakutamrudisha nyuma katika misimamo yake, “Siwezi kurudi nyuma, nimetumwa na Kristo, Nabii anaweza kupendwa au kuchukiwa na mimi siwezi kunyamaza.”

Askofu Niwemugizi aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) alisema, “Mimi nazungumza lakini kuna Watanzania wengine wanazungumza sana. Lakini mimi kuhojiwa mara mbili hakutaninyamazisha.”

Ujumbe aliouweka Facebook, unasema, “Nasali Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, uniokoe na mtu wa hila asiye haki. Kwa kuwa wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?

Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea? ...Nafsi yangu, kwa nini kuinama, na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; kwa maana nitakuja kumsifu, aliye afya ya uso wangu na Mungu wangu” (Zab 43:1-2,5). Asante Rais wangu JPM kwa faraja uliyonipa.”

Wakichangia ujumbe huo, Deusdedit Mwombeki alisema “Amina Baba Askofu Severine Niwemugizi kwa ujumbe wako wa faraja nami umenigusa. Pole sana na hongera kwa faraja uliyopewa na Rais Magufuli.”

Prosper Mallya alisema, “Kweli humuweka mtu huru, kiongozi hukutana na misukosuko ila kwa kuwa wewe unawasemea wanyonge na Roho wa Bwana yu nawe, hutaogopa wala hutarudi nyuma. Mwenyezi akutie Roho wa hekima na akili uendelee kunena yale unayoona ni kwa manufaa na ustawi wa taifa letu.”

Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Askofu David Mwasota akizungumzia kitendo cha Uhamiaji kumhoji askofu huyo alisema kila nyakati na utendaji wake kikubwa ni kuliombea Taifa.

“Serikali ina macho na taarifa nyingi na labda inajua kwa nini inamhoji, lakini kwa heshima ilibidi hata taarifa zake zisijulikane...” alisema Askofu Mwasota na kuongeza:

“Tunawapa pole wenzetu wa Kanisa la Katoliki na tunawaomba kila mtu kwa nafasi yake tuliombee Taifa… lakini tuelewe kipindi hiki ni tofauti na kile cha Jakaya Kikwete.”

Mwananchi lilipomtafuta Rais wa TEC, Askofu Tarcisius Ngalalekumta kujua hatua ambazo baraza lake imechukua alisema “Kwanza ndiyo nasikia kutoka kwako, lakini kanisa linajiongoza, Serikali kama kuna kitu inakitafuta hatuwezi kuizuia.”

Ngalalekumtwa ambaye pia ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa alisema “Hilo sisi halina tatizo, Kanisa Katoliki halina mipaka, kuna maaskofu kutoka nchi mbalimbali.”
Chanzo: Mwananchi

Ratiba ya Simba, Yanga Raund ya Pili Kombe la Shirikisho Hii Hapa

$
0
0
Ratiba ya Simba, Yanga Raund ya Pili Kombe la Shirikisho Hii Hapa
Baada ya droo ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam (Azam Sports Federation Cup – ASFC), kukamilika Jumatano Desemba 06, 2017 kwenye Studio za Kituo cha Televisheni cha Azam,
kilichopo Tabata relini, Dar es Salaam, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa ratiba rasmi ya mechi hizo za raundi ya pili.

Kwa mujibu wa TFF, michuano hiyo imepangwa kucheza kwa siku tano ambazo ni Desemba 20, 21, 22, 23 na 24. Mchezo kati ya Simba na Green Warriors utaochezwa Desemba 22, utakuwa ni maalumu kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa michuano hiyo msimu. Sababu Simba ndiye bingwa mtetezi.

Ratiba hiyo iliyotolewa leo Desemba 12, 2017 inaonesha michezo ya Desemba 20, mwaka huu itakutanisha timu za JKT Mlale na KMC; Toto African ya Mwanza na Eleven Stars ya Kagera; Ambassador na JKT Oljoro; Boma FC na Ndanda; Mvuvumwa na JKT Ruvu; Abajalo itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons wakati Milambo ya Tabora itacheza Buseresere ya Geita.

Desemba 21, 2017 Mshikamano itacheza na Polisi Tanzania; Rhino ya Tabora na Alliance ya Mwanza; Majimaji Rangeres ya Lindi itapambana na Mbeya Kwanza ya Mbeya; Njombe Mji na Mji Mkuu ya Dodoma; Ashanti na Friends Rangers za Dar es Salaam; Kagera Sugar na Makambako wakati Stand United ya Shinyanga itacheza na AFC ya Arusha.

Desemba 22, mwaka huu kutakuwa na mechi za Green Warriors na Simba; Polisi Dar itapambana na Mgambo JKT ya Tanga; Kariakoo ya Lindi na Transit Camp ya Dar ila kwa sasa imeweka maskani Shinyanga; Biashara ya Mara itacheza na Mawenzi Market ya Morogoro; Ruvu Shooting ya Mlandizi mkoani Pwani itacheza na Madini FC ya jijini Arusha huku Mufindi United na Pamba ya Mwanza ilihali Singida United itacheza na Bodaboda FC.
Siku ya Desemba 23, mwaka huu Azam FC itacheza na Area C; African Lyon ya Dar es Salaam na Kiluvya United ya Pwani; Makanyagio itapambana na Mbao; Mwadui na Pepsi; Majimaji na New Generation wakati Mbeya City itacheza na Ihefu.
Desemba 24, 2017 Young Africans itacheza na Reha FC; Burkina ya Morogoro na Lipuli ya Iringa; Coastal Union ya Tanga na Dodoma FC ya Dodoma; Shupavu na Real Mojamoja wakati Villa Squad itacheza na Mtibwa Sugar ya Morogoro.

TBA Yaanza Ukarabati wa Kuziba Nyufa za Mabweni ya UDSM

$
0
0
TBA Yaanza Ukarabati wa Kuziba Nyufa za Mabweni ya UDSM
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeanza ukarabati wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yenye ufa.

Taarifa za kuwepo nyufa hizo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii usiku wa Desemba 3,2017 na baadaye ufafanuzi ulitolewa na TBA.

Uchunguzi uliofanywa na MCL Digital umebaini ukarabati umeanza, huku ikielezwa kuwa hauwaathiri wanafunzi wanaotumia mabweni hayo.

“Ukarabati umeanza, mafundi wanafanya kazi nje ya jengo kwa kuondoa plasta ili kuangalia tatizo liko wapi,” kimesema chanzo cha habari kilichozungumza na MCL Digital.

TBA iliyojenga majengo hayo ambayo bado yako katika usimamizi wake imeelezwa pia inaangalia dosari nyingine zilizopo.

Mtendaji Mkuu wa TBA, Mhandisi Elius Mwakalinga Desemba 4,2017 akizungumzia nyufa zilizoko kwenye jengo la Block A alisema hazina madhara na walizitarajia.

Alisema nyufa katika jengo hilo la hosteli ambalo ni kati ya sita yaliyopo Block A zimetokea eneo walilotarajia ambalo kitaalamu linajulikana (expansion joint) hivyo hazina madhara.

Mwakalinga alisema kwa kawaida udongo unaobeba jengo hutitia baada ya muda fulani, hivyo wakati wa ujenzi huacha nafasi kuliwezesha jengo kupumua bila kusababisha nyufa.

Mwakalinga alisema kuna makosa yalifanyika ya kuziba nafasi zilizoachwa (expansion joint) kwa kutumia saruji badala ya mbao au plastiki maalumu hivyo kuonyesha nyufa kwenye jengo hilo.

Kutokana na kusambaa kwa picha kuonyesha nyufa katika majengo hayo, mbunge wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), Kumbusho Dawson alishikiliwa na polisi kitengo cha makosa ya mtandao kwa kuhojiwa na baadaye aliachiwa.
Chanzo: Mwananchi

Penzi la Rayvany na Fahyma Mbioni Kuvunjika

$
0
0
Penzi la Rayvany na Fahyma Mbioni Kuvunjika
Msanii wa muziki wa kizaki kupya kutoka lebo ya WCB Wasafi Tanzania, Rayvanny na mrembo aliyepata naye mtoto wake Fahyma zimeanza kuibuka figisu figisu zenye dalili za wawili hawa kuachana.

Katika uwazi kila mmoja kuonekana kuwa tayari kuendelea na maisha yake, Rayvanny kupitia ukurasa wake wa Instagram alianza kwa kupost.
“Mpende ila Usimuamini , Mpe ila sio Vyote, mtunze ila Usimchunge, mpe mwili wako ila Usimpe Siri zako….. 😂😂 Ata mkojo ulikua Soda, Vitamu ndio Vichungu keep it your Mind.” Ujumbe ambao muda mfupi baadae ulijibiwa kwa post kutoka kwa Fahyma aliweka picha picha na kuandika “SINGLE Mama 😡
” kuonesha kuwa kwa sasa hayuko katika kahusiano.
Kilichofuata baada ya kuoneakana kuwa Rayvanny na Fayma hawako sawa, Diamond Platnumz alishuka kwenye uwanja wa maoni wa alichokipost Rayvanny na kutetea kuwa Fayma haliwi kwa naneno ambayo walielewana wao kisha akamtag Meneja Makame anayesimamia kazi za Rayvanny.

Rayvanny kugongelea nyundo zaidi aliweka post kwenye akaunti yake ya Instgram na kuliaga penzi la Fayma kwa kuandika “Safari njema But change that f****n name PERIOD.



Sehemu ya Helikopta ya Jeshi la Marekani Yaanguka Shuleni Japan

$
0
0
Sehemu ya Helikopta ya Jeshi la Marekani Yaanguka Shuleni Japan
Sehemu ya ndege ye jeshi la Marekani imeanguka kwenye shule katika kisiwa cha Okinawa nchini Japan na kuzua upya misukosuko na watu wa eneo hilo.
Sehemu hiyo ya dirisha ilianguka kwenye uwanja wa shule na kusabisha majeraha madogo kwa mwanafunnzi mmoja.

Sehemu ya helikopta ya jeshi la Marekani yaanguka shuleni Japan
Katika miaka ya hivi karibuni, ajali kadha na visa vya uhalifu vimesababisha kuwepo upinzani dhidi ya kambi hiyo ya Marekani.
Jeshi la Marekani lilithibitisha kuwa dorisha kutoka moja ya helikopta zake ilianguka kwenye uwanja wa michezo wa shule iliyo nje ya kambi ya yake ya jeshi la wanahewa.

Kwanini Wanawake Wengi Siku Hizi Hawaolewi? Jibu Mubashara Hili Hapa

$
0
0
KWA NINI WANAWAKE WENGI SIKU HIZI HAWAOLEWI? WENGI HUPISHANA NA WAUME ZAO*

Mwanamke anapigiwa simu kwa namba ngeni, anauliza namba yangu umeitoa wapi? Usiponiambia aliyekupa usinipigie. _HAPO UMEPISHANA NA MUME_

Mwanamke anaingia ndani ya daladala, amekaa na mwanaume, kwa maringo, anachukua earphone na kuweka masikioni na kuwasha mziki ili asiongeleshwe. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke anasalimiwa njiani, anaitikia, akiongeleshwa tena anachuna. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unatumiwa meseji inbox, hujibu. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unapigiwa simu na mwanaume, unaona kabisa anakupigia ila hutaki kupokea tu. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unakwenda gheto kwa mwanaume, una mkoba wako, ukifika muda wa kuondoka unaomba nauli. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unakwenda kwa mwanaume, badala ya kusonga ugali, cha kwanza unataka chipsi kuku. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unaanza uhusiano na mwanaume, siku ya pili tu unamwambia bebi sina hela ya vocha. _HAPO UMEPISHANA NA MWANAUME._

Mwanamke upo na mwanaume, anakwambia agiza chochote, bila kujishtukia unaagiza bia. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unachati na mwanaume, chatting zako ni K, P, Pw. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unaweka picha mapaja wazi, kifua umebust. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

Mwanamke unamwambia mwanaume akutumie video za ngono kwenye simu. _HAPO UMEPISHANA NA MUME._

_Usilalamike kwamba kwa nini mpaka sasa hivi hujaolewa. Niambie sasa ni mara ngapi umepishana na mume!_

Dr Lov
@2017

Huyu Hapa Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Vile Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha, Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa    dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SUPER POWER,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI
SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Soma Nafasi za Ajira Nyingi Zilizotangazwa Leo


Barua ya Dharula na ya Haraka Kwa Wanandoa Wote 'Nakala Kwa Mnaotarajia Kuingia Katika Ndoa'

$
0
0
Ndugu wanandoa,
Nawasalimu salamu za mwisho wa mwezi!

Mahusiano ya wanandoa wanaoishi sehemu tofauti kwa kigezo cha kazi au masomo ni hatari Sana kwa ustawi wa ndoa yako,ni sawa na mtu anayelima shamba Iringa yeye anaishi dar ,yeye anapiga simu tu na kutegemea kuvuna mavuno kedekede.

Mme unaishi Mwanza mke anaishi mtwara halafu mnasema mmeoana.

Kuna mambo mengine mkiwa mnaishi pamoja mke na mme shetani hawezi kuthubutu kuyaleta ila ile kutengana shetani anapata hapo mwanya wa kuja kuwajaribu.Nimeshuhudia ndoa nyingi ambazo zimepigwa kwa jinsi hii.Ninawaonya binti zangu  na wale mlio kwenye ndoa tayari kuepuka jambo hili kwa garama yoyote.Msije kusema sikuwambia.

ELOI! ELOI!

Mimi nina pointi zifuatazo kama nyongeza:-

1). Kinachosababisha kufika hali hii sio serikali kukataa kuhamisha watumishi, bali ni wafanyakazi wenyewe kukataa kuhamisha akili. Shida ya kwanza kwa wengi ni kuamini kwamba ajira ni kila kitu. Shida ya pili ni vipaumbele. Ukiona unaacha mke Dar unaenda kufanya kazi Mtwara, na mke nae akawa mwajiriwa na miongoni mwenu hakuna alietayari kuacha kazi kumfuata mwingine, mjue kwamba wote wawili hakuna ambae ameweka ndoa kama kipaumbele cha kwanza!

2). Nioneshe mtu aliewahi kuthamini ajira kuliko ndoa halafu ndoa ikabaki salama kwa muda mrefu. Mnaweza kusema ohooo, tunaaminiana, mara ohooo, mke wangu/mume wangu hawezi kunisaliti, sikatai! Enhee, akishakuwa hajakusaliti what is next? Nyie ni watu wazima bana, naomba niwaeleze kwamba kuna mambo ambayo maombi yanaweza kuhamisha, lakini kuna mambo yapo mwilini huwa hayahami kwa maombi ng'oooo. Ukiamua kubisha shauri yako mwenyewe! Wewe umekomaa na ajira yako huko Mwanza mume umemuacha Dar, halafu unategemea maombi ya , eti Mungu amlinde mumeo kule Dar? Subiri uvune mabua, ndio utaelewa!

3). Halafu aliewaambia kwamba mmoja akiacha ajira kumfuata mwingine, eti mtakufa na njaa nani? Shida yenu ni kwamba tukiwaelekeza ujasiriamali mnaona as if hauwahusu, ndio maana ajira mnazitetemekea kiasi cha ku-risk ndoa zenu. Aliekudanganya kwamba ukiwaachia liajira lao wanalokulipa "vilaki nane", ukamfuata mke/mme na kupiga ujasiriamali, utakosa kuzalisha zaidi ya laki nane, ni nani huyo? Unajua ninawamaindi kwa sababu, nilishawaelezaga kwamba kwenye ajira mnalipwa asilimia chini ya kumi ya mnachozalisha, sasa kinawashinda nini kuzitoa sadaka ajira ili mkaokoe ndoa? Nakuona tu unavyonibinulia midomo, na kunifyonya, lakini huu ndio ukweli.

4). Haya basi! Tuseme ninyi ni wa kisasa, so, ishu ya ndoa ya bluetooth haiwasumbui, je, hayo malezi ya watoto inakuwaje? Mke Kigoma, mume Arusha, watoto wako boarding Tabora!  Shida yenu mlio wengi mnadhani ni sifa kupeleka watoto wa chekechea boarding., baba kusubiri miezi sita ama mwaka ndio akawaone watoto kwa mkewe, maana watoto wanalelewa na mama Songea baba akiwa kazini Dodoma!

5). Hadi hapa najua nimeshawakorofisha watu, maana ndoa za masafa siku hizi imekuwa ndio fasheni, kwamba mke na mume wakikutana ni spesho kwa ajili ya ujauzito na from there huyu kule mwingine huko. Hivi aliewaeleza kwamba ndoa ni just ijulikane umeoa ama umeolewa ni nani? Kwani haijaandikwa kwamba mmeoana ili muishi pamoja?

Hata hizo hela mnazotafuta (if ni nyingi kihivo) mnawezaje kuzipangia matumizi na maendeleo ya familia? Au ndio mnategemea bando la halichachi na jazwa ujazwe na WhatsApp kujadiliana kuhusu familia? Hivi mnajua kwamba kuna nguvu kubwa kupanga mambo ya ndoa na familia mkiwa mnatazamana kwa macho na mwenzi wako? Mkoje, nyieeee? Kwani maparoko, mapasta na mashehe hawawaelezi haya?

Wakinga huwa wanasema vyungu viwili huwa vinamaliza kuni haraka. Mume uko Tanga una bajeti ya nyumba, mke yuko Geita nae ana bajeti ya nyumba, hee, kwa mishahara hii ya chini ya milioni mbili, lini mtafanya maendeleo ya maana?. Ni ujinga mkubwa wa kiwango cha utoroshaji wa makinikia, wanandoa kuishi mbalimbali na ku-risk ndoa eti kwa mishahara ambayo inaishia kwenye matumizi!

 Wengine wananiuliza, "Je, kwa waliopo masomoni inakuwaje?". Haaa! Haaa! Mie leo naongelea mnaofanya kazi, mengine msinipangie!

6). Mmeambiwa kwamba kisiwepo cha kuwatenganisha isipokuwa kifo. Hamuoni kwamba ajira zimeshakuwa vifo? Mnapata wapi ujasiri wa kuishi na kifo mkingali hai? Nyie mnaujasiri sana. Yaani kifo kinazunguka zunguka, mpo tu mwaka wa kwanza, mwaka wa pili, mwaka wa tatu mnakitazama tu???!!!?? Kweli? Mbona mna hatari namna hiyo!

7). Pointi hii yaweza kuwa ngumu zaidi. Unajua wanaume huwa wanasisimka kwa kuona(kutazama),, asipokua anakiona anachokipenda mara kwa mara (yaani mke wake) ataanza kuona mibadala,  " Mwanamke anasisimuliwa kwa kusikia, Ndio maana hata mke ukimuangalia usoni na kumwambia, "Nakupenda", anasisimka zaidi kuliko ukimpigia simu na kumwambia, "Nakupenda".

Mpo? Mwanamke anaihesabu "care" kwa kupima ukaribu, (yaani muda unaokua naye  Mwanamke yeyote unaweza kumpata kiurahisi ikiwa kuna factor mbili:- mosi, ikiwa mumewe amezembea kum-care. Pili, ikiwa muwindaji utatumia sayansi ya ku-care. (Mliooa shikeni pointi hapa mnafanya uzembe halafu nyani wanakula mahindi yenu).

So, mwanamke alieolewa anapokuwa mbali na mumewe, huwa anakuwa na gepu fulani, hata kama awe anajikaza. Kuna  gepu hilo likiwepo ndio anaweza kuendelea kujikaza lakini ikizidi sana atakuwa anaumia na itamuathiri. Akiwa anavumilia ashukuriwe Mola. Pili ni kwamba anaweza kutafuta mbadala.

Wanaume ukiona ametafuta mbadala automatically huwa ni kwa ajili ya ngono lakini wanawake huwa wanatamani just care, baasi.  wanaume wangapi wanaweza kuwa karibu na wake za watu kwa ku-care t halafu wawaache pasipo kuwakula? Ndio ile unakuta mke wa mtu ameshaliwa halafu anasema, "Wewe kaka Abdul nilikuwa nakuchukulia kama kaka yangu lakini umenifanya tumefanya hivi, basi iwe siri yetu".

Usidhanie ninakutisha, lakini ukatae ubishe, ni kwamba huko aliko mumeo ama mkeo ambako kuonana ni mpaka likizo hadi likizo, uwezakano wa wewe kula makombo ni mkubwa (hope mnanielewa). Jifariji uwezavyo, , mie ninakwambia fanya juu chini muishi pamoja, maana usalama ni mdogo.

8). Baadhi ya  wanawake mlioolewa katika ndoa hizi za bluetooth mnanichekeshaga sana. Unakuta unabana kabisa pua eti, "Siwezi kuacha ajira, coz wazazi hawatanielewa maana walinisomesha", heee! Unataka kueleweka kwa wazazi ama unataka kueleweka kwa mumeo? Shida yenu (baadhi yenu), vielimu vyenu vimeshawapotezea utii na unyenyekevu kiasi kwamba mnaamua ya kwenu ndani ya ndoa as if bado mko mabachela.   MAJADILIANO. Ukishabana pua yako na kuanza kuwasikiliza wazazi maana yake ni kwamba hamuwezi kufikia muafaka na mumeo kwa suala hili la ndoa ya bluetooth!


MAANA....

 Ukinimaindi mimi utakua umenionea,  kuna mtu  kanitumia  huu ujumbe kwang maana ndie alienituma nikueleze. Mjumbe hauwawiiiiiiiiii! #SmartMindBARUA YA DHARULA NA YA HARAKA KWA WANANDOA WOTE.......

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

Rais Magufuli Awapa Onyo la Mwisho Benki Kuu Tanzania

$
0
0
Rais Magufuli Awapa Onyo la Mwisho Benki Kuu Tanzania
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewapa onyo la mwisho Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kuwataka wawe wasimamizi wazuri wa fedha za nchi na kusema kama hawatajirekebisha basi wasijekumlaumu siku za usoni.

Magufuli amesema hayo leo alipokuwa akizindua tawi moja la Benki mjini Dodoma na kuzitaka benki zote pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuangalia suala la matumizi ya fedha za kigeni ndani ya nchi kwani jambo hilo linazidi kuuwa uchumi wa nchi.
"Haiwezekani nchi ikawa na 'curency' mbili,  tatu au zaidi zinazotumika zinaharibu uchumi, haiwezekani mtu ukiwa na dollar unakwenda kununua bidhaa dukani, ukiwa na pounds unakwenda kununua chochote nchini huu si utaratibu wa uchumi. Na hili nikuombe Waziri,  BoT na mabenki yote mlisimamie hili kikamilifu, na baya zaidi haya yamekuwa yakifanywa na BoT. Gavana upo hapa mnapotangaza tenda zenu hata za wafagiaji mnawalipa kwa Dollar " 
Rais Magufuli aliendelea kuelezea "Sasa haiwezekani nyinyi BoT ambao mnasimamia fedha nyinyi hao hao mnakuwa wabaya wa kudhibiti fedha za nchi hili lazima muende nalo na mbadilishe haraka. Msije kuwa chanzo cha kuharibu uchumi wa nchi yetu. Najua mnanielewa nililizungumza jambo hili mara ya kwanza nimelirudia leo mara ya mwisho litakalotokea msije kunilaumu" alisisitiza Rais Magufuli
Mbali na hilo Rais Magufuli amehitaji kuwe na uangalizi mzuri kwenye 'Bureau de Change' na kuwa na utaratibu ambao unaeleweka.

Uhamiaji Kutoa Ukweli Kuhusu Askofu Niwemugizi Baada ya Uchunguzi Kukamilika

$
0
0
Uhamiaji Kutoa Ukweli Kuhusu Askofu Niwemugizi Baada ya Uchunguzi Kukamilika
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala amesema uchunguzi utakapokamilika wataweka wazi sababu za kuhoji uraia wa Askofu wa Jimbo la Ngara - Rulenge, Severine Niwemugizi.

Dk Anna amesema hayo baada ya kuhojiwa na Mwananchi leo Jumatano kwa njia ya simu kuhusu sababu za kufanya mahojiano kuhusu uraia wa Askofu huyo.

“Hizo ni taarifa za kiuchunguzi, ambazo bado tunaendelea, huwezi ku-disclose kila kitu hata tunayemuhoji hatutakuwa tunamtendea haki, tunapokuwa na doubt ya uraia tunaruhusiwa kuchunguza,” amesema Dk Anna.

Alipoulizwa kuhusu madai ya msimamo wa Askofu Niwemugizi kuhusu Katiba mpya ndiyo pengine umesababisha kuhojiwa uraia wake, Dk Anna amesema hakuna haja ya kueleza chochote kuhusiana na madai hayo hivyo ni vyema kusubiri taarifa za uchunguzi wake.
Chanzo: Mwanamchi

“Hayo ni yake, sitaki kuongelea hilo, hayo tuyaache,” amesema.

Manara Amlilia Mtoto wa 'Mo' Amtumia Salamu za Pole "Tumeumia Sote kwa Msiba Pole sana Kiungo Wetu"

$
0
0
Manara Amlilia Mtoto wa 'Mo' Amtumia Salamu za Pole "Tumeumia Sote kwa Msiba Pole sana Kiungo Wetu"
Kiungo wa Simba, Mohamed Ibrahim ‘MO’ amefiwa na mtoto wake mchanga jana Jumanne katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara aliandika kwenye ukurasa wake wa Istagram akimtakia pole kwa niaba ya uongozi wa klabu hiyo.

Alisema msiba huo wa mtoto mchanga umewaumiza watu wengi, hivyo akimsihi kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Manara Aliandika hivi kwenye ukurasa wake wa instagram "pole sana kiungo wetu  mnyumbufu @mohammedibrahim04 'Mo' kwa kufiwa na mwanao mpendwa tumeumia sote kwa msiba huu wa mtoto wetu  mdogo kabisa ... kwa niaba ya @Simbasctanzania pokea salamu zetu za pole  kwa msiba huu mzito ww na mama wa mtoto  Inna lilah wainna ilahi Raajiun

Pia mchezaji mwenzake, Deus Kaseke alimtakia pole kwenye mtandao wa huo

TAARIFA: MSIBA WA MTOTO WA MOHAMMED IBRAHIM UPO MBAGALA KIWANGWA

Msiba wa Mtoto wa Mohammed Ibrahim upo nyumbani kwa familia ya Mohammed Ibrahim Mbagara Kiwangwa jijini Dar es Salaam.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images