Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Mbunge Chadema Amtaja Aliyetekeleza Shambulio la Kumuua Tundu Lissu

$
0
0
Mbunge Chadema Amtaja Aliyetekeleza Shambulio la Kumuua Tundu Lissu
Mbunge wa Serengeti, Marwa Ryoba Chaha (CHADEMA) amefunguka na kutaja sifa za mtu ambaye alitaka kumuua Tundu Lissu na kusema mtu huyo alishindwa kutekeleza hilo kwa kuwa Mungu hakupanga Lissu aondoke kwa kipindi hicho.

Marwa Ryoba amesema hayo kupitia mtandao wake wa Facebook baada ya kuweka picha ya Tundu Lissu akiwa hospitali ya Nairobi Kenya na kusema kuwa Mbunge huyo sasa anaendelea vizuri baada ya kutolewa risasi 16 mwilini.

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma, baadaye alisafirishwa na kupelekwa nchini Kenya jijini Nairobi ambapo mpaka sasa anapatiwa matibabu huko.



Mbunge wa Chadema Azua Gumzo Aitisha Mkutano na Waandishi wa Habari Ashindwa Kueleza Alichowaitia

$
0
0
Mbunge wa Chadema Azua Gumzo  Aitisha Mkutano na Waandishi wa Habari Ashindwa Kueleza Alichowaitia
Mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya CHADEMA kutoka Mkoa wa Geita, Upendo Peneza leo Desemba 15, 2017, ameitisha mkutano na Waandishi wa Habari, Mkutano ambao umeleta gumzo mitandaoni kutokana na wimbi la Wabunge wa Vyama vya Upinzani kukimbilia CCM.


Mhe. Peneza ameitisha mkutano huo bila kueleza nini hasa anachoenda kuzungumzia kitu ambacho kimeleta maswali mengi kwa wafuasi wa CHADEMA nchini Tanzania.

Mkutano huo unajiri ikiwa ni siku moja tu imepita tangu Mbunge wa jimbo la Siha, Mhe. Godwin Mollel kutangaza kukihama chama hicho na kuhamia CCM.

BOT Yaagizwa Kuzifutia Leseni Benki Zisizokidhi Vigezo Kufutwa

$
0
0
BOT Yaagizwa Kuzifutia Leseni Benki Zisizokidhi Vigezo Kufutwa
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ameiagiza Benki Kuu ya Tanzania BOT kuzifutia leseni benki zote za biashara pamoja na benki za wananchi zitakazoshindwa kukidhi vigezo vya kuendesha shughuli za kibenki nchini.

Ametoa agizo hilo mjini Dodoma katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, wakati akifungua Mkutano Maalum wa Wadau wa Jumuiya ya Benki za Wananchi Tanzania (COBAT).

“kwa taarifa niliyonayo hadi sasa baadhi ya benki hazijatimiza matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji wa kutosha, hali ambayo haiwezi kuachwa iendelea hata kidogo, kwani haiimarishi sekta ya fedha na haiwasaidii wananchi kuendelea kiuchumi” alisema Waziri Kassim Majaliwa katika hotuba hiyo.

Alisema Benki Kuu ilitoa muda hadi mwishoni mwa Desemba 2017, benki za wananchi ziweze kuongeza mtaji na kwamba muda huo hautaongezwa na wala Serikali haitatoa mtaji kwa benki hizo.

“Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania haitasita kuifungia benki yoyote na kufuta leseni yake ya biashara pindi itakapobaini inavunja sheria, ikiwa ni pamoja na kuwa na upungufu mkubwa wa mtaji na ukwasi ambao unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na amana za wateja kama tulivyofanya kwa Mbinga Community Bank PLC kuanzia tarehe 12/5/2017” alisema Dkt. Mpango kwa niaba ya Waziri Mkuu.

Maagizo hayo yamekuja siku moja baada ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kuiagiza Wizara ya Fedha na Mipango wakati akifungua tawi kuu la Benki ya CRDB mjini Dodoma, kuhakikisha kuwa Benki Kuu ya Tanzania-BOT, inazifuta benki zote zinazoshindwa kujiendesha kibiashara hata kama zinamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100.

Alisema Serikali inafanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha benki za wananchi zinaimarika zikiwemo kuruhusiwa kuanzisha mifumo ya ushirikiano katika Nyanja ya Mfumo wa Mawasiliano na Habari (ICT), Idara za Ukaguzi wa Ndani (Internal Audit Services), kupunguza wingi wa idara na kuwa na idara tatu (3) tu muhimu, kuruhusiwa kuungana (Federation), ambazo zitapunguza gharama za uendeshaji wa benki za wananchi na kuleta ufanisi katika kutoa huduma.

“Napenda kusisitiza kuwa sekta ya benki ni muhimu sana kwa uhai na ukuaji wa uchumi kama ilivyo damu kwa mwili wa binadamu na kutokana na umuhimu wake huo, sekta hii ni kati ya sekta chache zinazosimamiwa kwa karibu sana ili kulinda amana za wateja pamoja na kuhakikisha uhimilivu wa mfumo mzima wa sekta ya fedha na mwenendo wa uchumi wa Taifa” aliongeza Dkt. Mpango

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Benki za Wananchi Tanzania (COBAT) Bw. Rukwaro Senkoro, alisema hadi kufikia Juni, 2017, Benki za Wananchi nchini zilikuwa na wateja zaidi ya milioni 1.4, wateja wa vikundi zaidi ya 10,000, Matawi 12, Vituo 59, na wanahisa 66,492.

“Benki hizo zina amana zenye thamani ya shs bilioni 74.2, zimetoa mikopo ya sh. bilioni 56.8, na jumla ya mali zenye thamani ya shs. bilioni 92.3” Alisema Bw. Senkoro

Hata hivyo, kutokana na Utafiti wa Matumizi ya Huduma za Kifedha uliofanyika mwaka 2017 umebaini kuwa asilimia 28 ya wananchi bado hawapati huduma za kifedha hapa nchini hususan vijijini na kutaja changamoto ya ukosefu wa mitaji ya benki hizo kukwaza sekta hiyo.

Dhana kuu ya mkutano huo wa COBAT uliowashirikisha wadau mbalimbali kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ni “Mitaji na Mpango wa Kuziunganisha Benki za Wananchi Tanzania”, ambayo ni dhana mpya.

Zitto Kabwe Azidi Kumng'ang'ania Niki wa Pili Amtaka Kujiunga na Siasa "Njoo Tufanye Kazi Ngumu"

$
0
0
Zitto Kabwe Azidi Kumng'ang'ania Niki wa Pili  Amtaka Kujiunga na Siasa "Njoo tufanye kazi ngumu"
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameonyesha kutamani kufanya siasa na msanii wa bongo fleva, Niki wa Pili ambaye amekuwa na msimamo wake juu ya mambo mbalimbali ambayo yanaendelea nhini kwa sasa.

Zitto Kabwe amesema hayo kupitia mtandao wake wa Twitter wakati akijibu moja ya jumbe ya msanii huyo ambapo alikuwa akielezea juu ya ushindani wa uchaguzi uliopita ambao ulikuwa na mvuto wa aina yake kuanzia kwenye mikutano ya kampeni, ambapo mamia ya wananchi walikuwa wakifurika kwenye mikutano hiyo na kusema kero za wananchi ndizo zilipelekea watu wengi kujitokeza katika kampeni hata kupiga kura.
"Ushindani wa uchaguzi ulio pita na tsunami na mafuriko ulikuwa ni wingi wa wananchi na kero zao, tusiutafsiri kwa maana ya wanasiasa na kuwapa uhodhi wao, kama ulikuwa ni ushindani wao" aliandika Niki wa Pili
Kufuatia hoja hiyo ya Niki wa Pili ndipo hapo aliibuka Zitto Kabwe na kusema kuwa siasa za Tanzania zinahitaji watu wenye misimamo ya kiitikadi na bahati mbaya zaidi watu wenye misimamo hiyo wamekuwa hawataki kuingia kwenye siasa.
"Kaka siasa zetu zinakosa wanasiasa wenye 'convictions' ( sijui Kiswahili chake) kwa sababu watu kama wewe mwenye misimamo ya kiitikadi hamtaki kujiunga na vyama. Njoo tufanye kazi ngumu lakini muhimu ya kujenga siasa zinazoondoa uhodhi kwa wanasiasa" aliomba Zitto Kabwe

Tunda Man Awachana Wasanii Wanaotoa Nyimbo Kila Kukicha

$
0
0
Tunda Man Awachana Wasanii Wanaotoa Nyimbo Kila Kukicha
Kapteni wa Bongo Fleva Tundaman amewataka wasanii waache tabia ya kutoa toa nyimbo kila kukicha wakati nyimbo zenyewe mbovu na hazidumu kwa muda mrefu.

Akiongea na eNEWZ ya East Africa Television, Tunda Man amesema nyimbo zake anazoziandika zinaishi kwa mda mrefu na zinamaudhui yanayojitosheleza kuishi miaka mingi katika sanaa na ndio maana amekaa zaidi ya miaka miwili  tangu ameachia nyimbo yake ya mwisho Mama Kijacho.
Hata hivyo Tundaman anasema pamoja na wasanii wa sasa kuachia nyimbo nyingi kwa wakati mmoja, lakini wengine wanaachia nyimbo ambazo hazina ujumbe wala maana kwa jamii. “Wanatoa nyimbo mbaya ambazo zikipigwa kwenye vyombo vya habari wiki mbili tatu tu mwisho wa siku zinapotea kabisa”.

Tundaman pia ameongelea suala la wasanii kubebwa ambapo amesema katika mziki wa sasa wasanii wamekuwa wanabebwa mara nyingi kwenye vituo mbalimbali vya Radio na Television. Mklai huyo wa 'Hit' kibao ameachia ngoma yake mpya inayoitwa TOTO.
“Wakati mwingine unakuta mtu anatoa nyimbo ambayo hajaigharamia kwa chochote kwa kuwa tayari ana washikaji wengi watakao msaidia katika Video na hata Audio mwisho wa siku inatoka nyimbo mbaya au ambayo haina viwango” amesema Tundaman.

Odinga: Nipo Tayari Kukutana na Kukutana na Odinga kwa Mzungumzo Yenye Lengo la Kujenga Kenya si Siasa

$
0
0
Odinga: Nipo Tayari Kukutana na Kukutana na Odinga kwa Mzungumzo Yenye Lengo la Kujenga Kenya si Siasa
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema yuko tayari kukutana na wapinzani kutoka muungano wa Nasa lakini akasema atakuwa tayari kufanya hivyo iwapo mazungumzo yao yatakuwa na lengo la kuikwamua Kenya na wala siyo kujadili siasa.

"Niko tayari kwa mazungumzo na yeyote," alisema Rais Kenyatta wakati akizungumza katika kongamano la magavana ambapo aliahidi kushirikiana nao kuimarisha Kenya.

Kongamano hilo liliandaliwa ili kutoa mafunzo kwa magavana wapya, ikiwa ni pamoja na kuchagua mwenyekiti mpya wa baraza la magavana.

Gavana wa Turkana, Josphat Nanok ndiye mwenyekiti wa baraza hilo kwa sasa na atatetea kiti chake kinachomezewa mate pia na Gavana wa Kwale, Salim Mvurya. Gavana wa Kirinyaga, Anne Waiguru anamezea mate kuwa naibu mwenyekiti wa baraza hilo.

Katika hotuba yake Rais Kenyatta alisisitiza kuwa mazungumzo anayotaka na Nasa ni ya kuendeleza taifa na siyo kujadili kuhusu siasa. Awali, alisema siasa zitajadiliwa mwaka 2022 ambapo Naibu Rais William Ruto anatarajiwa kupeperusha bendera ya  Jubilee (JP) kuwania kiti cha urais.

Rais Kenyatta hata hivyo, alisema sheria zilizomo kwenye katiba sharti zifuatwe katika kila hatua kufanya mazungumzo na kuendesha taifa mbele.

"Kila tunachofanya kiegemee kwa msingi wa katiba. Watakaofanya nje ya katiba na sheria za nchi watakabiliwa vilivyo," alionya kiongozi huyo.

"Serikali yangu haitaruhusu yeyote atakayecheza na kuhatarisha maisha ya Mkenya ama kuharibu mali yake. Hiyo laini ukipita, sheria ni sheria itachukua mkondo wake," alisema.

Aliahidi kufanya kazi na kila gavana licha ya mrengo wa kisiasa anaoegemea. Jumapili iliyopita kinara mwenza wa Nasa, Musalia Mudavadi alisema muungano huo unaomba kufanya mazungumzo na Serikali ya Jubilee ili kujadili uwezekano wa kuandaliwa kwa uchaguzi mwingine.

Aliyekuwa waziri mkuu, Raila Odinga hivi karibuni aliahirisha mipango yake ya kuapishwa kama wa wananchi na kusema kazi hiyo itafanyika baadaye bila kutaja tarehe.

Kala Jeremiah Amwahidi Zawadi Mama Samia Suluhu

$
0
0
Kala Jeremiah Amwahidi Zawadi Mama Samia Suluhu
Baada ya msanii wa Hip Hop Kala Jelemiah kula shavu la nguvu la kusifiwa na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu kuwa ngoma yake mpya aliyoachia hivi karibuni “Kijana” amesema anajipanga kuilipa heshima hiyo aliyopewa na kiongozi wa nchini.

Akiongea kupitia eNEWZ ya     East Africa Television Kala amesema "nimefanya mziki kwa mda mrefu ila sijawahi kupata pongezi kutoka kwa kiongozi mkubwa wa nchi kama yule tena mbele za maelfu ya watu mara nyingi tumekuwa tukikutana na viongozi wa kawaida na kutupa pongezi za kawaida”.
Kala ameongeza kuwa alizipokea salamu za Makamu wa Rais kutoka kwa watu wengi  kitendo ambacho amekipokea  kwa mikono miwili na kuwa kauli hiyo ya Makamu wa Rais imempa deni la kuendelea kukaza buti na kuandaa nyimbo  nyingi  zitakazo kuwa mkombozi kwa Jamii.
Kala amemaliza kwa kusema  kauli ya Makamu wa Rais imempa faraja yeye na familia yake kwa ujumla na hata alipotumiwa kile kipande cha video ambayo Makam wa Rais alikuwa anamsifia aliiangalia mara nyingi kiasi kwamba hakuamini kitu ambacho alikuwa anakiona.
Msanii huyo wa Hip Hop kutoka Rock City anafunga mwaka kwa kauli yake ya kuwa hakuna mziki wa biashara bali kuna biashara ya muziki aliyoitoa hivi karibuni kupitia Enewz.

Abiria Waonywa Kula Hovyo Wakiwa Safarini Msimu Huu wa Sikukuu

$
0
0
Abiria Waonywa Kula Hovyo Wakiwa Safarini Msimu Huu wa Sikukuu
Abiria wanaosafiri katika msimu huu wa kuelekea sikukuu wametahadharishwa kutokula au kunywa vitu watakavyopatiwa ndani ya magari na watu wasiowafahamu.

Pia wametakiwa kutoa taarifa kwa wakati pindi watakapoona kuna ukiukwaji wa sheria na kanuni za usafirishaji ikiwa ni pamoja na kutozwa nauli tofauti na iliyopangwa pamoja na mwendo kasi au mtu yeyote atakapofanya vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wao.

Rai hiyo imetolewa leo Ijumaa Desemba 15 wakati Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Mtwara wakifanya operesheni katika mabasi ya abiria kituo kikuu cha Mtwara kabla ya kuanza safari ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa madereva, kondakta pamoja na abiria.

Akizungumza na abiria mkaguzi wa magari wa kikosi cha usalama barabarani, Said Masoud amewatahadharisha abiria kutokula hovyo vitu watakavyopatiwa kwenye magari na watu wasiowafahamu.

"Tunaelekea kipindi cha Krismasi na mwaka mpya ni kipindi cha hatari sana watu wako kazini, usimwamini uliyekaa naye kama humfahamu mmekutana kwenye kiti  anakupa pipi unakula, anakupa karanga unakula utaumia nawatahadharisha tena watu wapo kazini mmekutana kwenye gari salimianeni kama abiria ila usimuhisi kwamba hiyu ndio mwizi ili mkae kwa amani mfike salama," amesema Said.

Huyu Hapa Bingwa wa Magonjwa Sugu Kama Vile Pumu, Vidonda vya Tumbo, Busha, Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
BABU MADUHU NI BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU YANAYOSUMBUA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME, KISUKARI, MIVUTO YOTE, KUSAFISHA NYOTA, KURUDISHA MALI, NK.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa    dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SUPER POWER,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI
SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Wanaohama Chama Wachunguzwe Ili Kubaini Ukweli wa Sababu Zao- Peneza

$
0
0
Wanaohama Chama Wachunguzwe Ili Kubaini Ukweli wa Sababu Zao- Penez
Mbunge wa Viti Maalum wa Chadema, Upendo Peneza amesema hana sababu za kuhama chama hicho kikuu cha upinzani nchini huku akiwashangaa wanaochukua uamuzi huo.

Peneza amesema kuhama chama kunasababisha hasara kwa Taifa kwa kuingia katika uchaguzi wa marudio huku akipendekeza uchunguzi ufanyike kwa waliohama ili kubaini ukweli wa sababu wanazozitoa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Desemba 15, Peneza amesema hajafikiria kuhama chama lakini anasikitika watu walioaminiwa na wananchi wakajiuzulu kwa kutoa sababu zisizoeleweka.

“Nimehusishwa mimi kuhama chama changu, sina sababu za kuhama ila ninachotaka ni hawa wanaohama watueleze sababu za kutuingiza katika hasara ya kurudia uchaguzi,” amesema Peneza.

“Sioni sababu ya kwenda kuunga mkono halafu utuingize gharama, yaani furaha zako utuingize sisi gharama, hapana…watueleze sababu zao,” ameongeza

Amesema kuna haja ya kupitia Katiba au kuendeleza mchakato wa Katiba ili kuwazuia kugombea wale wanaojiondoa kwa sababu zisizoeleweka.



Peneza amesema “kama unasema unaunga mkono, useme umewafanyia nini wananchi wako au kuunga mkono kwani lazima uchukue kadi ya chama kingine, Watanzania tunachezewa na watu na huu ni mchezo wa kisiasa unafanyika.”

Akizungumza kwa msisitizo, Peneza amesema “ninapinga haya kwa sababu pesa za wananchi hazitumiki vizuri, tunabana matumizi, tunapinga mafisadi halafu fedha badala ya kwenda katika maendeleo lakini tunakwenda katika uchaguzi.”

“Tusiharibu hela kwa kile wanachosema tunamuunga mkono, kama Rais atajenga daraja la Mwanza kwenda Sengerema, nitampongeza, kama chama changu kitanifukuza haya,” amesema Peneza

“Kiuhalisia shida bado kubwa, mbunge wa Siha angesimama akasema amenijengea shule, ametatua matatizo ya wakulima, ardhi sawa ila hayo hayajatekelezwa unamuungaje mkono.”

Kuhusu kuhusishwa kwake na kuhama, Peneza amesema wakati akigombea alijua kuna CCM yeye aliamua kuwa Chadema ingawa akadokeza kwamba hawezi kusema atakuwa Chadema maisha yote.

“Sisemi maisha yangu kwamba nitakuwa hapa, niliapa Novemba 2015 kuwa mbunge naomna Mungu anisaidie nimalize muda wangu salama na nitimize wajibu wangu niliopewa,” amesema Peneza.

Askari Amuua Askari Mwenziye kwa Kumpiga Risasi Wakiwa Kazini

$
0
0
Askari Amuua Askari Mwenziye kwa Kumpiga Risasi Wakiwa Kazini
Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia kwa mahojiano askari Magereza wa Gereza la Kisongo jijini Arusha, Koplo Faustine Masanja kwa tuhuma za kumuua mwenzake wakiwa kazini.

Akizungumza na Vyombo vya Habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa limetokea Desemba 14,2017 majira ya saa 2:00 asubuhi.

Kamanda Mkumbo amesema baada ya Masanja kumjeruhi mwenzake kwa risasi, alipelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu ambako alifariki dunia.

Mkumbo ameahidi kutoa taarifa zaidi baada ya uchunguzi kukamilika ili kubaini chanzo na sababu za tukio hilo. Ingawaje taarifa za awali zinaonesha kuwa tukio hilo linaviashiria vya wivu wa mapenzi.

Pendeza na Kessy Products..Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Safi Kwa Products za Asilia Zisizo na Madhara

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA* 🍇🌾🌳
1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATAKS)KUNADAWA AINA TATU (@)JELI KUPAK_100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI NA MAPAJAN_80,000/
5)TOA KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE NA MANYAM YOTE
@) DAW YA MAJINI_100,000/NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME BILA KUVAA SIDIRIA_80,000/
8)KUONGEZA MAZIWA NA SAIZI NZURI_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA (kifaru)_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO YAKAWAIDA NA UZAZ_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_70,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA KWA DAW(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWLINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA JELI PAMOJA NA VIDONGE VYAAIN ZOT _100'000
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_ 120,000 /
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_80,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _80,000/
20)ONDOA MIKUNJO USON_70,000/(21) ENGEZA MGUU_80,000/🍍🍉🌾 *TUNAPATIKAN DAR E SALAAM* *NAKWA *MIKOANKOTE* UTAPATA *PIA* *NA NCHI ZOTE PIGA CM* (+255)0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product*
*Delivery POPOTE ULIPO,*

Waka’ ya Diamond Platnumz yaweka rekodi mpya Afrika Mashariki

$
0
0
Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.


Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.

Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k , Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika Mashariki.

Kwa sasa wimbo wa ‘Waka’ unaweka rekodi ya kuwa wimbo wa kwanza kutrend namba moja kwa nchi tatu za Afrika Mashariki kwenye mtandao wa YouTube.

Video hiyo mpaka jana usiku ilikuwa ndiyo video inayotazamwa zaidi mtandaoni (Trending) kwa kushika namba moja kwa nchi za Kenya, Uganda na Tanzania.


Wimbo wa ‘Waka’ awali ulipotoka ulikaa siku mbili kwenye mtandao wa YouTube hapa Tanzania bila kukaa kwenye namba 1 ya video zinazotrend hapa nchini. Lakini mpaka sasa video ya wimbo huo yenye siku saba mtandaoni ipo namba moja kwenye Trending.

Awali rekodi ya video iliyotrend namba 1 kwa nchi mbili tofauti tofauti ilikuwa ilikuwa inashikiliwa na video ya wimbo wa ‘Zilipendwa’ wa WCB , Salome ya Diamond Platnumz na Video ya wimbo wa ‘Seduce Me’ wa Alikiba ambapo video zote wakati zinatoka zilishika namba moja Tanzania na Kenya kwa muda tofauti tofauti.

Katika umri wa miaka 24, Ulimwengu anakwenda wapi baada ya kuondoka Sweden?

$
0
0
Na Baraka Mbolembole

JUNI 14, 1993 ndiyo alizaliwa Thomas Ulimwengu mahala mkoani Dodoma. Miaka 14 baadaye alikuwa sehemu ya wachezaji vijana U17 ambao walijumuhishwa katika kikosi cha timu ya soka ya mkoa huo kilichocheza michuano ya kwanza ya vijana Copa Coca Cola.

Akicheza eneo la mashambulizi Tom hakuishia katika michuano hiyo tu iliyofanyika Dar es Salaam bali uwezo wake ulimpatia nafasi ya kuchaguliwa na kuendelezwa katika kituo cha soka TSA kilichokuwa chini ya Shirikisho la Soka nchini-TFF.

WAKATI TIMU YA Taifa ya Tanzania Bara U17 ilipomaliza katika nafasi ya pili katika michuano ya vijana ya Cecafa mwaka 2009, Tom aliweza kutengeneza imani kubwa kwa wadau wa soka nchini baada ya kutwaa tuzo ya mfungaji bora wa michuano hiyo iliyofanyika nchini Burundi.

Klabu ya Moro United ilimsaini kwa makubaliano maalumu ya TSA kijana huyo kwa ajili ya kumtumia katika ligi kuu Tanzania bara msimu wa 2009/10. Kutokana na tamaa ya kutaka kufanikiwa haraka kimpira na majukumu mbalimbali ya timu za Taifa za vijana, Tom alishindwa kutulia Moro United.

Mwaka 2010 alifunga magoli kumi na kushinda tuzo nyingine ya ufungaji bora wakati alipokuwa akiiwakilisha timu ya Taifa U17 katika michuano ya Copa Coca Cola Afrika-michuano ambayo ilifanyika nchini Afrika Kusini.

Baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika michuano ya Copa Coca Cola Afrika, Julai, 2010, Tom aliweza kufanikiwa kujiunga na Athletic Football Club (AFC) ya Sweden wakati huo akiwa na miaka 17. Wakati yupo AFC alipata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Humberg ya Ujermani, lakini Julai 2011 alijunga na TP Mazembe ya DR Congo.

Misimu mitano TP Mazembe

Kujiunga Mazembe iliyokuwa bingwa wa Afrika mwaka mmoja nyuma huku pia kukiwepo na wachezaji wa kiwango cha juu kama Tresor Mputu na rafiki yake Mbwana Samatta ambaye pia alikuwa amejiunga na klabu hiyo bingwa mara tano ya Afrika akitokea Simba hakukumuogopesha Tom na badala yake kulimuongezea hamasa ya kufanya kazi yake kwa nguvu akiamini anaweza kutumia klabu hiyo kubwa Afrika kufika mbali kimpira.

Tom kama ilivyo kwa wachezaji wengi wa kiafrika wana ndoto za kucheza katika ligi kubwa za Ulaya. Alishinda mataji matatu ya ligi kuu DR Congo, taji moja la Afrika na hadi anaondoka klabuni hapo mwaka mmoja uliopita mchezaji huyo alikuwa sehemu ya mipango ya klabu na mmiliki wake Moise Katumbi.

Juni mwaka uliopita Tom alikuwa ni sehemu ya kikosi cha TP ambacho kiliichapa Yanga katika mchezo wa hatua ya makundi katika Caf Confederation Cup. Tom alicheza kwa kiwango cha juu mno katika mchezo huo ambao Yanga ilipoteza 1-0, lakini mwezi mmoja baadae mchezaji huyo akatangaza kutosaini mkataba mpya ambao TP walikuwa wamempa.

Sababu kubwa iliyotajwa wakati huo ni kuwepo kwa ofa nyingi huku meneja wa mchezaji huyo akinukuliwa mara kadhaa kuwa ‘zilifika ofa zaidi ya kumi’ kutoka Ulaya na klabu nyingine kubwa za Afrika. Wengi tulisubiri kuona kama ni kweli Besiktas ya Uturuki watamsaini mchezaji huyo, Rennes ya Ufaransa, Standard Liege, Oostende za Ubelgiji ama Esperance na klabu nyingine ambazo zilikuwa zikitajwa kumtaka.

Kuna baadhi ya wadau wa soka walikubaliana haraka na umamuzi wa Tom kuachana na Mazembe huku wakitoa sababu kuwa mmiliki wa klabu hiyo ni mgumu mno kuuza wachezaji wake hata barani Ulaya. Kutajwa mara kwa mara kwa klabu maarufu za Afrika na Ulaya kuwa zinamuhitaji Tom ndio kulipekea washauri wake kumzuia kusaini mkataba mwingine Mazembe jambo ambalo nililipinga sana wakati ule.

Ni ngumu sana mchezaji asiye na timu kupata klabu nzuri barani Ulaya na kitendo cha kukaa nje ya uwanja kati ya Septemba hadi Januari kulimpoteza zaidi mchezaji huyo na kushusha thamani yake haraka. Alikuwa na nafasi ya kushinda Caf Confederation Cup 2016 kwani baada ya kumalizika kwa mkataba wake na kugoma kusaini mwingine klabu hiyo ilikwenda kushinda taji la kwanza la michuano hiyo. Ambalo pia wamefanikiwa kulitetea msimu huu.

Alitoka klabu kubwa na kujiunga klabu ndogo

Achana na majeraha yanayomuandama mara kwa mara katika mwaka wake mmoja AFC Eskilstuna ya Sweden kwani hata wakati yupo TP Mazembe, Tom alikuwa mchezaji asiyeishiwa majeraha ya mara kwa mara. Kitendo cha kukubali kujiunga na AFC Eskilstuna upande wangu sikukipenda hasa kwa kiwango cha mchezaji huyo kilivyokuwa.

Tom tayari alikuwa mchezaji muhimu wa klabu kubwa Afrika ambako alidumu kwa misimu mitano. Ilishangaza sana wakati niliposikia amerejea AFC mahala ambako alianzia soka la kulipwa akiwa U17 mwaka 2010. Tom alirejea katika klabu hiyo kwa vile alikosa ofa mahala kwingine. Na hilo linatokana na uwepo wa ‘watu wengi’ wa kati na si mawakala ambao huzungumza na klabu zinazohitaji wachezaji.

Kujiunga AFC ilikuwa ni sawa na kurudi hatua nyingi nyuma katika jitihada ambazo alizifanya kwa miaka sita kucheza soka la kulipwa na lenye mafanikio. Katika umri wake wa miaka 24 hivi sasa, Tom anaweza kuibuka tena na kuwa mchezaji  mkali lakini lazima akubali kuwa alifanya kosa kuachana na klabu kubwa na kujiunga klabu ndogo, labda kwa vile Mazembe iko Afrika na AFC iko Ulaya.

Anaondoka AFC anakwenda wapi?

Tayari nimemsikia meneja wake Jamal Kisongo kuwa Tom anaondoka AFC, tena anaondoka kwa makubaliano ya kuvunja mkataba wake uliobakiza msimu mmoja katika klabu hiyo iliyoshuka daraja na kurejea katika ligi ya chini.

Katika maelezo aliyonukuliwa Kisongo anasema Tom anasubiri wakati wa usajili wa dirisha dogo ufike ili asajili katika klabu mpya. Najiuliza inawezekana vipi mchezaji huyo akapata usajili wakati kwa msimu mzima aliokuwa AFC hakucheza kutokana na majeraha? Nahitaji kumuona Tom akicheza katika klabu ya hadhi yake popote pale, ila ni wapi ataenda sasa? Hilo ni jibu ambalo tutalipata wakati utakapofika.

Lioneil Messi Anaamini Kombe la Dunia Mwakani litamlipa Kwa Alicholitendea Soka

$
0
0
Masuala mengine yanauma sana, lakini majonzi, furaha na huzuni ndivyo vinalifanya soka liwe tamu, pamoja na furaha yote waliyonayo CR7 na Lioneil Messi lakini nyota hao wawili hawajawahi kuchukua kombe la dunia.

Lakini Lioneil Messi anaamini muda sasa umefika ambapo mwakani nchini Urusi soka linaweza kumpatia kitu pekee ambacho amebakisha katika soka lake, nacho ni kombe la dunia jambo ambalo amekiri linamuumiza.

Messi anasema amemsikia kocha wake George Sampaoli aliyesema soka litatenda haki kama Messi akichukua kombe la dunia na Messi anaamini malipo hayo ya soma yanakwenda kutokea nchini Urusi 2018.

Lioneil Messi anasema anaumia sana akikumbuka fainali mbili za Copa America walizopoteza na fainali ya kombe la dunia 2014 waliyofungwa na Ujerumani kwani anaamini fainali hizo tatu walipaswa kuchukua angalau mbili.

Timu ya taifa ya Argentina imepangwa katika kundi moja na Nigeria, Iceland na Crotia katika michuano hiyo huku Messi akisisitiza kwamba yeye na wachezaji wenzake wamepanga kuwafuta machozi Wargentina kwa kubeba ndoo hiyo.

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Silinde: Siku Nikihama Chama Wananchi Wajitokeze Kuchoma Moto Nyumba Yangu

$
0
0
Silinde: Siku Nikihama Chama Wananchi Wajitokeze Kuchoma Moto Nyumba Yangu
Mbunge wa Momba (Chadema), David Silinde amesema siku akitangaza kukihama chama hicho wananchi wajitokeze kuchoma moto nyumba yake pamoja na mali zake zinazofahamika.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Desemba 15, muda mfupi baada ya kusambaa kwa taarifa za kutaka kukihama chama hicho kikuu cha upinzani nchini, Silinde amesema ubunge wa jimbo hilo aliutafuta kwa gharama kubwa.

“Kinachofanyika sasa ni kutaka kutuondoa katika hoja, kuna watu wanasema nitafanya mkutano na waandishi wa habari, mimi nikawajibu kuwa hilo haliwezekani. Siwezi kuhama,” amesema.

Akieleza sababu za kusambazwa kwa ujumbe huo amesema, “Wamesambaza uzushi huu baada ya mimi kuandika katika mitandao ya kijamii kuwa unapopigana vita unahitaji jeshi dogo lenye weledi, yaani unaweza kuwa na idadi kubwa ya wanachama lakini wakawa wasaliti.”

Kuhusu gharama za ubunge wake amesema wapo watu waliopigania ushindi awe mwakilishi wao bungeni huku baadhi kupoteza maisha, kufilisika, kufungwa jela na kwamba hawezi kuwasaliti kwa maslahi yake binafsi.

“Thamani ya ubunge haiwezi kushushwa kama vocha ya simu, kwamba ikiisha unaweza kukwangua nyingine,” amesisitiza.

Rekodi ya Arsenal Yavunjwa na Manchester City

$
0
0
Rekodi ya Arsenal Yavunjwa na Manchester City
USHINDI wa mabao 4-0, dhidi ya Swansea City umeifanya Manchester City kuvunja rekodi ya Arsenal ya kushinda mechi nyingi mfululizo katika Premier League.

Man City sasa imeshinda mechi 15 mfululizo na kuivuka Arsenal ambayo ilikuwa ikishikilia rekodi ya kushinda mechi 14 mfululizo lakini yenyewe ilifanya hivyo katika misimu miwili tofauti wakati City wao wamefanikisha ndani ya msimu mmoja.

Pamoja na rekodi hiyo bado City ina nafasi ya kuweka rekodi zaidi ya hapo kwa kuwa inaendelea kucheza.
Kwa takwimu hizo pia Man City imekuwa timu ya nne kwa Ulaya kushinda mechi nyingi mfululizo katika ligi kuu.

Makamu wa Rais Zanzibar Afunguka Kuhusu Suala la Kuongeza Muda wa Urais

$
0
0
Makamu wa Rais Zanzibar Afunguka Kuhusu Suala la Kuongeza Muda wa Urais
Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd amesema ushauri wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutaka kuongezwa muda wa urais madarakani badala ya miaka mitano iwe miaka saba ni suala ambalo zuri na linazungumzika bila ya matatizo.

Balozi Iddi aliyasema hayo leo Ijumaa Desemba 15 wakati akifunga mkutano wa nane wa Baraza la Tisa la Wawakilishi lilichukua muda wa wiki moja Zanzibar.

Awali baadhi ya wajumbe wa baraza hilo wakichangia Mswada wa Sheria ya Marekebisho ya Tume ya Uchaguzi ya mwaka 1984 na kuweka sheria ya mwaka 2017, walisema kuwa ili Zanzibar kuepukana na matumizi hasa kipindi cha uchaguzi hakuna budi kuongezwa kwa muda wa utumishi wa urais.

Mmoja wa  wawakilishi hao wa Jimbo la Shaurimoyo, Hamza Hassan Juma amesema kuwa ili kumpa Rais wakati mzuri wa kutumikia wananchi ipasavyo hakuna budi muda wake kuongezwa zaidi ili kuona kuwa ile mipango ya kufikisha maendeleo kwa wananchi iweze kufanikiwa.

Amesema kwa kuwa muda wa miaka mitano wa uongozi wa Rais madarakani ni mdogo na kuonekana kupoteza fedha nyingi za wananchi kwa kufanya uchaguzi kila miaka mitano, ni vyema uongozi kuliona hilo na kulifanyia kazi.

Amesema kuwa kwa mujibu wa tathmini yake ya uchaguzi Mkuu mara nyingi hutumia fedha nyingi za walipakodi kiwango ambacho kinaweza hata kujenga zaidi ya shule kubwa 20 ambazo zingesaidia jamii katika kuondokana na uhaba wa shule.

Amesema kuwa pamoja na katiba zote mbili ya Tanzania bara na Zanzibar kuweka muda huo wa miaka mitano lakini bado kuna nafasi kubwa kwa Zanzibar kufanya marekebisho ya katiba yao ili kuongeza muda, akidai kuwa ni jambo ambalo haliwezi kuathiri hata kidogo katiba ya Tanzania.

Juma amesema pindi ikiamuliwa kufanyika hivyo ni wazi kuwa faida kubwa inaweza kupatikana ikiwamo Rais kupata muda mwingi wa kutumikia jamii badala ya muda wa sasa miaka mitatu tu ya kutumia jamii huku miaka miwili iliyosalia akishughulikia masuala ya uchaguzi.

Balozi Iddi akitolea ufafanuzi suala hilo amesema kwa kuwa jambo hilo linahusiana na pande mbili za Muungano ni vema kwa wakati huu suala hilo likaachiwa kwa viongozi husika kwa kulifayia kazi ikionekana linafaa ni wazi linaweza kupunguza gharama kubwa hasa kwa upande wa chaguzi za viongozi wakuu.

“Hili itakuwa si suala jipya kwetu kwani hata ndugu zetu wa Rwanda nao wameongeza muda wa uongozi, hivyo nasi tukibadili miaka badala ya mitano tukaweka saba tunaweza kufanikiwa kimaendeleo kwa hatua kubwa,” amesema Balozi Iddi.

Mama Samia Ahamia Rasmi Dodoma Leo

$
0
0
Mama Samia Ahamia Rasmi Dodoma Leo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ahamia rasmi mjini Dodoma leo. Baada ya Rais Magufuli kuagiza serikali ya Awamu ya tano kuhamia mjini humo.

Akizungumza mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Kilimani mjini Dodoma, Samia ameomba wananchi wa mkoa huo kuonyesha ushirikiano katika kufanya kazi ili kulisukuma gurudumu la maendeleo

"Nilikuwa hapa kwa muda mrefu kidogo lakini nilipangiwa kuhamia rasmi leo Desemba 15 na nimefurahi kwamba nitafanya kazi mahala pangu pa kazi pa kudumu," amesema Samia.

Amesema kauli mbiu yake kwa wakazi wa Dodoma ni kuufanya mji huo kuwa wa kijani hivyo Desemba 21 ataendesha mpango wa kupanda miti katika wilaya zote.

"Kwa kuwa nasimamia pia masuala ya mazingira nitaendesha zoezi hilo ili kurudisha hali ya Dodoma," ameongeza.
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images