Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Rose Muhando Atangaza Kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM

0
0
Msanii wa nyimbo za Injili aliyetamba kwa vibao vyake murua na vyenye kuburudisha Rose Muhando, ametangaza kujunga rasmi na Chama cha Mapinduzi.

Msanii huyo ambaye aliomba kujiunga na chama hicho amekabidhiwa kadi ya Chama cha Mapinduzi leo yeye pamoja na kikundi chake, katika Mkutano Mkuu Maalum wa Tisa wa CCM Taifa, unaofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete, mjini Dodoma.

Rose Muhando kabla ya kukabidhiwa kadi ya chama cha CCM alitumbuiza kwa kibao maalumu alichokiandaa kwa ajili ya Rais John Pombe Magufuli ambacho amekipa jina la “Magufuli Tubebe”.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey polepole alitangaza kuwa Rose Muhando pamoja na Kundi lake wameomba kupewa nafasi ya kutumbuiza kwa wimbo huo maalumu pamoja na kukabidhiwa kadi za CCM.

“Kundi la Ndugu Rose Muhando na yeye mwenyewe niwakaribishe Jukwani kwa wimbo ambao wameutunga maalumu kwa Ndugu Magufuli. Kundi hili walipokuwa wanakuja walikuwa na maombi mawili, ombi la kwanza ni kupewa nafasi ya kuimba wimbo huu maalumu na pili kujiunga rasmi na CCM,” amesema katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole.

Hata hivyo Polepole amesema kuwa Rose Muhando na kundi lake watakabidhiwa kwa makatibu wa mikoa husika kwa ajili ya michakato ya kuwaandikisha kama wanachama wapya wa CCM.

Kinana Asema Yupo tayari kuitumikia CCM....Atoboa Siri ya Ushindi wa Kishindo

0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amesema yuko tayari kuendelea kukitumikia chama hicho.

“Neno la mwenyekiti kwangu ni amri kama umeona bado unahitaji niendelee kukusaidia niko tayari kufanya hivyo,” amesema Kinana leo Jumatatu Desemba 18,2017 katika mkutano mkuu wa CCM unaoendelea mjini Dodoma.

Kinana ametoa kauli hiyo wakati kukiwa na minong’ono kuwa ameandika barua akiomba kuachia nafasi yake ya ukatibu mkuu.

Awali, Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli aliweka wazi kuwa Kinana amekuwa msaada mkubwa katika kukiongoza chama hicho.

“Mzee Kinana amenisaidia sana. Amenisaidia mno kwenye kufanya mabadiliko ndani ya chama na ni mategemeo yangu ataendelea kunisaidia,” amesema.

Katika hatua nyingine, Kinana ametoa siri ya ushindi wa kishindo wa chama hicho katika uchaguzi kuwa ni kutokana na ilani bora, demokrasia  na kusikilia maoni ya wanachama.

Kinana amesema demokrasia imekuwa msingi wa chama hicho ndiyo sababu kinaimarika.

“CCM tunazingatia demokrasia, wanachama wapo huru kutoa maoni ndani ya chama. Hili linafanyika kwa kuwa usipowapa uhuru wa kusema ndani watasema nje,” amesema.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

0
0
HARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:
Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Makamba Awapa Ujumbe Huu CCM

0
0
Makamba Awapa Ujumbe Huu  CCM
Katibu Mkuu wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba amesema sifa za pekee ziwaendee waasisi wa Taifa, Julius Nyerere na Abeid Amani Karume kwa kulitetea taifa hadi kufika leo.


Makamba amepata nafasi ya kuongea hayo kwenye mkutano mkuu wa tisa wa Chama cha Mapinduzi mara baada ya Mwenyekiti wa muda Benjamin William Mkapa kumpa nafasi ya kuwasalimia wajumbe na wageni waliohudhuria mkutano huo.

''Tunajipongeza sisi tunasahau waliotengeneza nchi, waasisi Julius Nyerere na Abeid Karume,'' amesema. Akiongea kuhusu utendaji kazi wa Rais Magufuli amesema kwamba anampongeza kwa kufanya mambo kwa kutoogopa  kitu chochote na anafanya kazi kwa weledi.

"Siku moja nilitabiri kuwa Kikwete ana batiza kwa maji, lakini JPM anabatiza kwa moto na sasa yanatimia kupitia matokeo mazuri ya viti vya Udiwani katika uchaguzi mdogo ambayo ni matokeo ya utendaji kazi mzuri wa serikali ya awamu ya tano chini ya CCM”, ameongeza.

Katika hotuba yake ambayo imechukua dakika 13 amewatahadharisha wapinzani kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 haitokuwa rahisi kwao kwani Chama Cha Mapinduzi kimejipanga vizuri kuweza kushinda tena.

Wananchi Wasimamisha Msafara wa IGP Sirro

0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amesema Jeshi lake limeongeza nguvu ya ziada ya kupambana na uhalifu nchini hasa kwenye maeneo ya mipakani.


IGP Sirro ameyasema hayo leo mbele ya wananchi wa Wilaya ya Tunduma ambao walisimamisha msafara wake wakati akitokea mkoani Rukwa kurejea Jijini Dar es Salaam.

Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi amesema wamefanya hivyo kutokana na maeneo hayo kuonekana kuwa korofi kwa usalama wa raia hivyo wao kama Jeshi la polisi wana dhamana ya kuhakikishia wanaondoa hali hiyo kwa kuongeza nguvu zaidi.

Kwa upande wao wananchi wamepongeza jitihada mbalimbali za Jeshi hilo katika kulinda usalama wao. Pia wameeleza kufurahishwa na kitendo cha IGP Sirro, kusimamisha msafara wake na kwenda kuwasalimia.

IGP Sirro amemaliza ziara yake ya kikazi katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa ambapo mbali na shughuli zingine pia amekagua kambi mbalimbali za wakimbizi katika mikoa ya mipakani.

Wolper Awatolea Povu Wanaomuandama Kuhusu Jino Lake la Silver

0
0
Wolper Awatolea Povu Wanaomuandama Kuhusu Jino Lake la Silver
MWANADADA mwenye mvuto kwenye tasnia ya Filamu za Bongo, Jacquiline Wolper amewafungukia wanaochukua picha zake na kuzi-edit huku wakimchafua kuhusu jino lake analodai kuwa limetengenezwa kwa madini ya Silver.

Staa huyo ambaye ni maarufu pia kwa kutupia pamba za maana amedai kuwa alitumia gharama zake kupanda ndege kwenda Sauzi kuweka jino la silver huku akiwaita ‘Kunguni’ wanaomfanyia mchezo huo mchafu.

Ngoja niwaeleze kitu kimoja ambacho amkijui kuhusiana na hili pengo…hli pengo nimelipandia ndege kwenda south kulitoa nakuweka ma slver kwa meno yangu kwa mahaba yangu mwenyewe ya kuwa na mwanya wa pembeni 😂😂sasa we kunguni unayetokea pasipojulikana unakuja kuchukua pcha naku edt unavyojua wewe ukizani nitakasirika au nitaumia am soleeee 🙄…unapoteza muda wako me najipenda nilivyo naikitokea nimechoka nitanyanyua makalio yangu hapa nitajilipia nauli nakwenda kuweka jino niwe na jino so plz usitokwe na damu juu ya hlo pengo langu ndilo nalodangia kwa tarfa yako kma ulikua ujui😂😂😂🔫#Pengodanga💃🥂🍾

Ramsey Awapa Makavu Wema Sepetu na Ray

0
0
STAA wa sinema za Nigeria (Nollywood), Ramsey Nouah amewalipua waigizaji wa filamu za Kibongo kwa kushindwa kuendeleza sanaa hiyo kwa kiwango alichoishia marehemu Steven Kanumba huku akilizungumzia kaburi la staa huyo, Ijumaa Wikienda lina mkada kamili.

Unapozungumzia Bongo Movies unawagusa vinara wake, Vincet Kigosi ‘Ray’, Wema Isaac Sepetu, Kajala Masanja, Aunt Ezekiel, Jacob Steven ‘JB’, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na wengine wengi waliofanya kazi na Kanumba.

Katika Makaburi ya Kinondoni, Dar alikozikwa Kanumba miaka mitano iliyopita, Ramsey ambaye kwa mara ya kwanza alifika kaburini hapo wikiendi iliyopita alionekana mwenye huzuni kubwa na kushindwa kujizuia ambapo alimwaga machozi mfululizo kabla ya kutamka maneno mazito yaliyosisimua wengi waliofika kaburini hapo.


Mama Kanumba akilia kaburini kwa mwanaye.

MAMA KANUMBA

Muda mfupi baada ya kuwasili makaburini hapo, Ramsey alimshika mkono mama mzazi wa Kanumba, Flora Mtegoa na kumkumbatia na ndipo vilio vikashika nafasi hususan kwa mama huyo.
MAOMBI

Ramsey, alitumia dakika chache akiwa kimya huku uso wake ukionesha maumivu na ghafla alianza kushusha maombi akimuombea marehemu Kanumba huku watu wote wakimsikiliza.

“Baba, utukufu wako ni wa kipekee tazama tumesimama hapa leo tukiwa na huzuni mioyoni mwetu, machozi yakighubika mboni za macho yetu tukimkabidhi kwako mja wako, Steven (Kanumba) aliyelala hapa kwa mapenzi yako, mpokee mwanao baba na kumsamehe dhambi zake ili siku moja tuonane naye kwa mapenzi yako yakitimizwa, baba tazama moyo wangu ulivyokwazwa na kifo hiki, hakika sitaki kukufuru, lakini ulimchukua Steven wakati dunia ikimhitaji zaidi, lakini jina lako lihimidiwe kwa kila jambo,” aliomba Ramsey.
Baada ya kumaliza maombi hayo, Ramsey alianza kuzungumza maneno ambayo yaliashiria alikuwa akimwambia Kanumba, jambo lililoshangaza na kuvutia watu waliokuwepo.

“Steve, nimesimama mbele yako leo ukiwa hujitambui. Tuliachana ukiwa na pumzi yako, lakini leo (Jumamosi iliyopita) niko kando ya mahali ulipolala na huwezi kuamka japo kunipa mkono, lakini kibaya zaidi hukuniambia maneno ya kwaheri, kwa nini hukuniaga Steven? Kuna mahali nilikukosea?

Aaah nashindwa kuhimili maumivu haya, ninalo kaa la moto kifuani mwangu, lakini kinachoniumiza zaidi ni kwamba mahali ulipolala hapaendani na hadhi yako, hukupewa kabisa thamani yako kulingana na ulichokifanya kwenye tasnia ya filamu na bila kuficha ni kwamba filamu za Kitanzania zinakufa, najua huko uliko unaumia na kinachoendelea kwenye filamu zanu,” alisema Ramsey katika ‘mazungumzo’ yake na Kanumba.
Baada ya kumalizana na ibada ya kaburini kwa Kanumba, Ramsey alizungumza na waandishi wa habari na kulipuka maneno ambayo yalilenga kuwananga waigizaji wa filamu za Kibongo.

“Ni ukweli ulio wazi kwamba filamu za hapa (Bongo) zimekosa msisimko, lakini wanayo nafasi ya kurekebisha, nimesimama hapa na maumivu makali, lakini yote ninamshukuru Mungu na wito wangu kwa wasanii wamsaidie mama huyu (mama Kanumba) kwani mwanaye alitoa ajira kwa wasanii, lakini leo wanamuona mama huyo kama si chochote, wameshindwa kumuenzi Steven kulingana na thamani yake, waangalie mahali walipokosea ili laana ya Steven isizidishe makali yake, lakini kubwa wamsaidie mama huyu,” alisema Ramsey akipeleka ujumbe huo kwa wasanii wa Bongo Movies.
KUHUSU LULU

Katika mazungumzo hayo, Ramsey hakutaka kuingia kwa undani kuhusiana na msanii Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye kwa sasa yuko jela akitumikia kifungo cha miaka 2 baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia Kanumba, April 7, 2012 nyumbani kwa jamaa huyo, Sinza- Vatican, Dar.
Chanzo: Global Publishers

Huu Hapa Ujumbe wa Dogo Janja Kwa Irene Uwoya Katika Siku Yake ya Kuzaliwa

0
0
Huu Hapa Ujumbe wa Dogo Janja Kwa Irene Uwoya Katika Siku Yake ya Kuzaliwa
Msanii wa muziki Bongo, Dogo Janja ameandika ujumbe wa kumtakia kheri ya siku ya kuzaliwa mke wake, Irene Uwoya.
Ikiwa siku ya jana ndio ilikuwa birthday ya Irene, Dogo Janja ametumia ukurasa wake wa Instagram kuandika haya machache;

Umebadilisha maisha yangu kutoka nanii kua nanii!! Unanifanya nacheka mda wote hata nikiwa usingizini!! Ww ni mke wangu wakwanza na nimke wangu wamwisho!!tuipeleke dunia kwenye mwangaza waajabu tuwamulike wasioamini wakaamini kua sisi ni wazazi mwakani, wengi wameoana ila sisi tumefunga ndoa!! Happy birthday mke wangu🥂🍾 💍 #MrsAbdul

Taarifa za Dogo Janja na Irene Uwoya kufunga ndoa zilianza kuchipuka November 25 mwaka huu, hata hivyo ni vigumu kutaja tarehe kamili kutokana na namna walivyoliweka suala hilo.

Trump: China na Urusi Ndio Washindani Wakubwa wa Marekani

0
0
Trump: China na Urusi Ndio Washindani Wakubwa wa Marekani
Rais Donald Trump ametangaza mkakati wa kitaifa wa usalama katika utawala wake ambao unaangazia vipaumbele vya kwanza vya Marekani.

Mkakati huo umesisitiza ukuaji wa kiuchumi na usalama wa taifa hilo kwa kuweka sheria kali za kulinda mipaka na kuwa na jeshi imara.

Katika hotuba yake,rais Trump ametaja kuwa China na Urusi ni washindani wanaopinga ushawishi wa Marekani katika ngazi ya kimataifa.

Licha ya kuwa Marekani inaongoza kwa kuwa na jeshi lenye nguvu lakini bado wapinzani wake wa kisiasa na kiuchumi wanahangaika duniani kote ili kuitoa katika mstari.

Trump aapa kuujenga ukuta wa Mexico
Mexico yaponda sheria za uhamiaji za Marekani
Trump atia saini agizo la kudhoofisha Obamacare
Huku ikiwa inakabiliwa na makundi ya kigaidi ,mitandao ya wahalifu na watu wengine ambao wanachochea vurugu na uovu.

Aidha mkakati huo unajumuisha ujenzi wa ukuta katika mpaka wa Mexico, kuimarisha sheria za uhamiaji na kusitisha mpango wa kutoa viza za bahati nasibu.

Trump pia aliwakosoa pia Marais waliopita wa Marekani akisema wameshiriki katika ujenzi wa mataifa ya nje badala ya kuendeleza taifa lao .

Mrithi wa Zuma Apatikana Cyril Ramaphosa Kuwa Mwenyekiti Mpya wa ANC

0
0
Mrithi wa Zuma Apatikana Cyril Ramaphosa Kuwa Mwenyekiti Mpya wa ANC
Chama cha African National Congress (ANC), Afrika Kusini kimemchagua Cyril Ramaphosa, kuwa mwenyekiti mpya wa chama hicho akimrithi Jacob Zuma.

Ramaphosa amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama tawala nchini Afrika Kusini ANC leo baada ya kufanyika uchaguzi.

Makamu huyo wa  rais aliyeibuka mshindi alikuwa na upinzani mkali na waziri wa zamani Nkosazana Dlamini-Zuma, mke wa zamani wa  Zuma.

Kulikuwa na  mvutano, hisia zikipanda, wajumbe wakipiga kelele kupinga taratibu za upigaji wa kura.

Uwaniaji madaraka umeleta mvutano  wa kisiasa nchini humo  hali inayoleta hofu kuwa ANC inaweza kugawanyika kabla ya uchaguzi wa 2019.

Ramaphosa ameibuka mshindi kwa kupata kura  2,440 huku mpinzani wake  Dlamini-Zuma akipata kura 2,261



Faiza Afunguka Kuhusu Wanae Asema Anatamani Kuwa na Watoto Hata 10

0
0
Faiza Afunguka Kuhusu Wanae Asema Anatamani Kuwa na Watoto Hata 10
Msanii wa Filamu Bongo, Faiza Ally amesema katika maisha yake angetamani kuzaa hata watoto 10 lakini haiwekani.
Faiza ametaja sababu ya kutowezekana ni kutokana na gharama za maisha kuwa juu na kueleza watoto wake wawili alionao wanamtosha.

“Sina mpango wa kuwa na mtoto mwingine kwa sababu wawili wananitosha, I don’t need more because life is too expensive, so sitaki kuleta mtoto aje kupata shida lakini natamani ningezaa hata 10” Faiza ameiambia Bongo5.

Chadema Waijia Juu CCM "Hatutaki Yajirudie ya Idi Amin"

0
0
Chadema Yaijia Juu CCM "Hatutaki Yajirudie ya Idi Amin"
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekosoa kitendo cha CCM kuweka mgombea wake kwenye nafasi ya Spika wa Bunge la Afrika Mashariki wakati haikutakiwa kufanywa hivyo, na kusema kwamba kitendo hicho kitasababisha mgogoro wa kidiplomasia.


Kwenye taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kutoka kwa chama hiko, imesema CCM imekiuka utaratibu wa Bunge hilo la kumtafuta Spika la kuliongoza kwa kumuweka mtu wao kwenye kinyang'anyiro, wakati kiutaratibu ilitakiwa Spika wa awamu hii atoke nchi ya Rwanda kulingana na mzunguko ambao ulikuwa unafuatwa, na kwamba kitendo hicho kinaweza kuleta migogoro itakayoathiri Jumuiya hiyo kama kipindi cha Idi Amin.

"Awamu hii Spika alipaswa kutoka Rwanda, lakini Tanzania kwa kuwa CCM imezoea kutokuheshimu sheria na kanuni zilizopo imemteua mbunge wake Adam Kimbisa kugombea nafasi ya Spika kinyume kabisa na kanuni za Bunge hilo, na huu ukiwa ni mwendelezo wa utamaduni wao wa kutokuheshimu sheria na kanuni, kitendo ambacho kinatishia ustawi na uwepo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki", imeandika Taarifa hiyo.

Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa .."CHADEMA tunalaani kitendo hiki, CCM wajue kuwa watabeba lawama zote kama kutakuwa na mgogoro ndani ya Bunge la Afrika Mashariki ambayo unaweza kupelekea mgogoro wa kidiplomasia katika Jumuiya nzima kutokana na tabia yao ya kutoheshimu taratibu zilizowekwa. Ttunataka kanuni za EAC ziheshimiwe, kwani tunakumbuka matendo ya Idd Amin mwaka 1977 yalivyovunja

 Jumuiya hii, hatutaki yajirudie kamwe".

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

0
0

Ondoa Nyama Uzembe na Kupunguza Mwili Kwa Kutumia Virutubisho vya Edmark

0
0
NI VIRUTUBISHO AU CHAKULA MBADALA
ZIMEHAKIKIWA NA TFDA
Ni uhakika kwa afya yako,👉 kupunguza uzito na sumu mwilini,mafuta/lehemu mbaya, Kitambi na nyama uzembe na kutibu MAGONJWA Mbali mbali
@looseweight_trainer ni msaada wako text WhatsApp 0713 777 470 upate suluhisho la afya yako KARIBU
👉@looseweight_trainer

Baada ya Kupitia Changamoto Vanessa Mdee Ashuhudia Maajabu

0
0
Baada ya Kupitia Changamoto Vanessa Mdee  Ashuhudia Maajabu
Malkia wa Bongo Fleva anayefanya vizuri ndani na nje ya nchi, Vanessa Mdee amekiri kushuhudia maajabu ya Mungu baada ya kupitia changamoto miezi ya mwanzo wa mwaka na hatimaye kumaliza mwaka kwa kusaini mkataba mnene na Kampuni ya usambazaji wa


muziki 'Univesal Music Group'.

Kupitia ukurasa wake wa Istagram Vanessa ameweka furaha yake na kushangilia na mashabiki wake ambapo amewaambia kwamba huo ni mwanzo tu na kwamba mambo mengine makubwa yapo njiani.

"Nimeona niitumie siku na fursa hii kuwajulisha wapendwa mashabiki zangu mwanzoni mwa mwaka huu. Nilipitia changamoto nyingi Sana. Lakini kwa neema za Mungu. Nilitoka mahali pale na sio kuona baraka tu bali na maajabu mengi yaliyotokea kwenye maisha yangu i kiwemo kuwa mmoja wa familia ya Universal Music Group in a unique joint signing between Universal Music Germany, Airforce1 na Universal Music Group. Vanessa Mdee.



Ameongeza "hii ni mara ya kwanza kwa msanii wa kiafrika kupata deal ya aina hii yenye mkwanja mrefuu sana...Hii ni habari njema kwa mashabiki wangu na ndiyo kwanza tumeanza. Mambo makubwa zaidi yanakuja. Kumbuka kila mwisho wa Jumapili ndiyo mwanzo wa Jumatatu, usiogope kuanza upya"

Vanessa amewashukuru mashabiki zake, ndugu jamaa na marafiki ambao walikuwa pamoja na yeye kuanzia mwaka kuanza japo ulikuwa na changamoto mpaka sasa anbapo mwaka unaelekea kuisha.



Mbunge Sadifa Aachiwa kwa Dhamana Apewa Masharti Magumu

0
0
Mbunge Sadifa Aachiwa kwa Dhamana Apewa Masharti Magumu
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Dodoma iemwachia kwa dhamana aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis (Mbunge) anayekabiliwa na mashtaka ya kutoa rushwa wakati wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa UVCCM Taifa.

Sadifa ameachiwa leo Desemba 19, 2017 baada ya mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa mashtaka ambao waliliwasilisha mahakamani hapo kuweka zuio la kupewa dhamana.

Mtuhumiwa huyo ametakiwa kudhaminiwa na watu watatu pamoja na kusaini bondi ya Tsh. Milioni 1, huku akipewa masharti ya kutosafiri nje ya nchi.

Kikwete Afunguka Alivyompigania Magufuli Kuwa Mwenyekiti

0
0
Viongozi wastaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jana waliutumia Mkutano Mkuu wa chama hicho kueleza kilipo na kinapoelekea, huku Rais mstaafu Jakaya Kikwete akisema hakuna shule ya urais na uenyekiti.

Kikwete ambaye ni mwenyekiti mstaafu wa CCM akiwa wa kwanza kutoa salamu aliueleza mkutano huo mjini Dodoma kuwa nafasi hiyo hakuna anayesomea ila mhusika anasoma akiwa ndani.

Alisema alitambua fika kuwa Rais John Magufuli ndiye mtu anayestahili kwenye nafasi hiyo licha ya kupata maswali kutoka kwa watu walioonyesha wasiwasi. “Nilimtetea Magufuli watu walihoji hajawahi kuwa hata mjumbe wa shina iweje ghafla aje kuwa mwenyekiti wa chama. Nikawaambia ataweza kwani hahitaji shule,” alisema.

Alisema katika kipindi cha miaka miwili, Rais Magufuli amefanya mambo makubwa yanayoleta matumaini na ameonyesha ujasiri wa hali ya juu.

“Mpaka sasa ‘big up’ mtani wangu. Kazi hii ngumu sana, sababu mimi nimeifanya. Katika kazi ngumu duniani hii ndiyo kiboko. Uzuri na ubaya wa kazi hii ina upweke mkubwa,” alisema.

Kuhusu malalamiko ya hali ngumu ya maisha Kikwete alisema, “Kuweni na subira, viongozi wetu makini wanatambua matatizo yanayowakabili wananchi na ninaamini wanayatafutia ufumbuzi.”

Kikwete Afunguka Alivyompigania Magufuli Kuwa Mwenyekiti
Mwenyekiti huyo mstaafu wa CCM aligusia mwenendo wa chama hicho na kueleza kuwa wastaafu wanafarijika hali ya chama ikiwa shwari.

“Sisi tuliostaafu faraja yetu kubwa ni kuona chama chetu kinaendelea kuwa imara. Tukija kwenye mikutano na watu wanafurahi na sisi mioyo inakuwa baridi. Lakini tukisikia mivurugano kwenye chama tunaweza pata magonjwa ya moyo,” alisema.

Kauli ya Kikwete haikupishana na aliyoitoa waziri mkuu mstaafu, Mizengo Pinda aliyesisitiza usimamizi wa nidhamu ndani ya chama na Serikali.

Pinda alimtaka Magufuli kutosita kuchukua hatua ndani ya chama na Serikali endapo ataona wanajihusisha na vitendo vya rushwa.

“Nimefurahishwa na namna ulivyosimamia kupambana na rushwa. Nina imani umepata viongozi wasafi ambao hawatakuwa wakisemwasemwa. Ukimpata ambaye haeleweki si mbaya unamtoa na kumuweka mwingine,” alisema.

Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Yusuph Makamba aliamsha shamrashamra alipopanda jukwaani na kummwagia sifa Magufuli. “Tunakufahamu kuwa wewe una uwezo mkubwa kwa kazi ya urais na ndiyo maana Kamati Kuu ilipokutana ikakupendekeza. Wewe ndiye unastahili kuwa mwenyekiti wa CCM kwa kuwa moja ya matatizo tunayoyapata ndani ya CCM ni watu kutosema ukweli, wanageuza matatizo, fitina ndiyo ukweli,” alisema.

“Kuna siku nilikutumia meseji ukaniambia ushauri mbovu huutaki, hivyo ndivyo inavyotakiwa, mimi sikukasirika.”

Makamu mwenyekiti wa CCM Bara mstaafu, Samwel Malecela alisema, “Wenzetu wanaongoja kama fisi mkono udondoke watachukua muda mrefu sana maana chama chetu kipo vizuri.”

Alipotoa salamu, makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, Amani Abeid Karume alipongeza watu wapya waliochaguliwa kuingia kwenye uongozi wa chama hicho.

Abiria wamiminika Ubungo Daradara Zaruhusiwa Kwenda Moshi, Arusha

0
0
Abiria wamiminika Ubungo Daradara Zaruhusiwa Kwenda Moshi, Arusha
Magari ya abiria (daladala) yameanza kutumika kupakia abiria wanaosafiri kwenda mikoa ya Arusha na Kilimanjaro  ili kupunguza adha ya usafiri kwa abiria wanaosafiri msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

Akizungumza na Mwananchi, leo Jumanne Desemba 19, Mkuu wa Usalama Barabarani Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani Ubungo (UBT),Inspekta Swamix Ibrahimu amesema gari hizo zimeanza kubeba abiria na asubuhi ya leo daladala nne zimeondoka kuelekea Moshi na Arusha.

"Daladala unazoziona hapa, tunazikagua na zipo kwaajili  ya dharura  endapo itatokea abiria wakawa wengi basi tunaruhusu zinapakia "amesema.

Si kwamba zinapakia muda wowote, hapana tutakuwa na daladala tano kwa siku ambazo zinakuwepo ikitokea abiria wameongezeka na basi kubwa hakuna basi tunaruhusu" amesema

 Ibrahimu amesema abiria bado hawajawa wengi  kiasi cha kuruhusu daladala nyingi kupakia. Mmoja wa wasimamizi wa daladala ambazo zimekutwa zikikaguliwa, Ignas Swai amesema gari zake ni imara na tayari zimekaguliwa na Askari na kupewa kibali na Sumatra.

"Nauli tunatumia IleIle iliyowekwa na Sumatra na tunapakia abiria wanaoenda Moshi na Arusha "amesema.

Hussein Bashe Awatumia Ujumbe Mzito Makocha

0
0
Hussein Bashe Awatumia Ujumbe Mzito Makocha
Mbunge wa Nzega Mjini Mh. Hussein Bashe amemtaka kocha mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM na Makocha wasaidizi  kuwa na umoja na ushirikiano ili kufikia malengo ya Chama na Serikali.


Bashe ametumia ukurasa wake wa ‘Twitter’ kuwasilisha ombi lake hilo kwa uongozi wa juu ambao ulichaguliwa jana kwenye mkutano mkuu wa tisa wa Chama mjini Dodoma ambapo Mwenyekiti Rais Magufuli amechaguliwa kuongoza kwa miaka mitano.

“Kocha na Makocha wasaidizi Tunaamini Tumewaamini Tuliwaamini Kila la kheri ktk kukiongoza Chama Chetu 2017-22. (Alone we can do so LITTLE, together we can do so MUCH" Team work We rise by lifting others appreciating others and respecting others)”, ameandika Bashe.

Katika maneno yake ya Kiingereza Bashe amehimiza kufanya mambo kwa umoja ili kupiga hatua kubwa tofauti na mtu akifanya vitu peke yake atapiga hatua kidogo. Uongozi huo mpya utahudumu kwa miaka mitano 2017 hadi 2022.

Rais Magufuli alichaguliwa kwa kura zote 1821 za wajumbe wa mkutano mkuu. Rais Ali Mohamed Shein wa Zanzibar pia alichguliwa katika nafasi ya Mwenyekiti Zanzibar wakati nafasi ya Makamu Mwenyekiti alichaguliwa Ndugu Philip Mangula.

Zari na Hamissa Mobetto Wakutana Uso kwa Uso Uganda

0
0
Zari na Hamissa Mobetto  Wakutana Uso kwa Uso Uganda
Kama ulifikiri kuwa baby Mama wa Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady na Hamisa Mobetto bifu lao limetulia au kuisha kabisa utakuwa umekosea.

Zari na Hamisa wamekuwa wakiripotiwa kutoelewana na kurushiana vijembe katika mtandao tangu Hamisa alipozaa na Diamond wakati akijua fika Zari na muimbaji huyo wa WCB bado ni wapenzi.

Sasa Hamisa na Zari si kwamba wanaviambiana tu kwenye mitandao, bifu lao limeenda mbali zaidi lakini katika njia ambayo ni nzuri.

Wakati Zari akitarajia kufanya event yake ya Zari All White Party nchini Uganda nyumbani kwao December 21 mwaka huu, siku hiyo hiyo Hamisa naye ameenda event yake.

Hata hivyo utakumbuka si mara ya kwanza kwa Zari kufanya party kama hiyo nchini Uganda na hata Tanzania ameshafanya hivyo lakini kwa Hamisa ni tofauti kitu ambacho ninatafsiriwa kama bado wanazidizi kuonyeshana umwamba.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images