Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live

Ambe Lulu Awatolea Povu Wanaomsema Prezzo "Usimfananishe Mume Wangu (Prezzo) na Young Dee"

$
0
0
Ambe Lulu  Awatolea Povu Wanaomsema Prezzo "Usimfananishe Mume Wangu (Prezzo) na Young Dee"
Msanii wa muziki Bongo, Amber Lulu amedai mpenzi wake Prezzo asifananishwe na Young Dee.

Amber Lulu amesema hao ni watu wawili tofauti hivyo kuwafaninisha ni kumkosea heshima Prezzo.

“Usimfananishe mume wangu na watu wengine kwa sababu unakuwa unamkosea adabu, kwa hiyo Young Dee ni Prezzo usiwakee kabisa pamoja kwa sababu ni watu wawili ambao hawezi kuendana hata kidogo,” Amber Lulu ameiambia Bongo5.

Pia Amber Lulu ameongeza kuwa mara baada ya kuachana na Young Dee hata tattoo yake aliyokuwa ameichora mkononi aliifuta kwani aliiweka kwa muda tu.

Kutana na Mtabibu wa Nyota Duniani Maalim Fadhil Rashid Kutoka Comoro Kwa sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436

Vigogo Watatu wa Halmashauri ya Hai Wafikishwa Mahakamani na Takukuru

$
0
0
Vigogo Watatu wa Halmashauri ya Hai  Wafikishwa Mahakamani na Takukuru
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imewafikisha kortini vigogo watatu wa zamani wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.

Waliofikishwa mahakamani leo Jumanne Desemba 19,2017 mbele ya Hakimu Mkazi, Arnold Kirekiano ni aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Melkzedeck Humbe ambaye sasa yuko Halmashauri ya Bariadi na wenzake wawili.

Wengine waliofikishwa mahakamani ni aliyekuwa mweka hazina wa Halmashauri ya Hai, Thadeus Meela na ofisa mwandamizi, Valentina Mollel.

Mwendesha mashtaka wa Takukuru, Susan Kimaro amedai Julai 8,2014 washtakiwa walighushi nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri na kufanya malipo ya Sh27 milioni.

Washtakiwa wamekana mashitaka na wameachiwa kwa dhamana.

Wamedhaminiwa kwa bondi ya Sh5 milioni kila mmoja na kesi imepangwa kutajwa Februari 15,2018.

Asante Kwasi Aibua Mapya Ashindwa Kushiriki Mazoezi na Simba

$
0
0
Asante Kwasi Aibua Mapya Ashindwa Kushiriki Mazoezi na Simba
KLABU ya Soka ya Lipuli inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) imesema mlinzi Asante Kwasi bado ni mchezaji halali wa kikosi hicho na alitakiwa kuripoti kambini tangu Desemba 16 mwaka huu lakini hajafanya hivyo hadi sasa.

 Lipuli kupitia kwa msemaji wake Clement Sanga imeeleza kusikitishwa kwake na taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa mchezaji huyo raia wa Ghana amejiunga na Klabu ya Simba, Sanga amesema taarifa hizo sio za kweli kwani bado anamkataba na timu hiyo licha ya kutoonekana klabuni hapo (kuingia mitini).



“Asante Kwasi tulimpa ruhusa ya kuhudhuria msiba wa baba yake nyumbani kwao Ghana, alitakiwa kurudi Desemba 16 mwaka huu na tulifuata taratibu zote ikiwemo kumtumia pesa ya tiketi ya ndege pamoja na mshahara wa mwezi uliopita, lakini hadi sasa hajafika hivyo tunashindwa kuelewa”, amesema Sanga.



Siku za hivi karibuni kumekuwepo na taarifa mbalimbali kuwa mlinzi huyo ambaye amefunga mabao matano hadi sasa kwenye Ligi Kuu, amesajiliwa na Simba japo vinara wa ligi hiyo hawajatoa taarifa juu ya usajili huo.



Tayari Lipuli imeshaweka hadharani majina ya wachezaji walioachwa na waliosajiliwa kwenye dirisha dogo ambapo walioachwa ni Waziri Ramadhani, Mussa Ngunda, Machaku Salum, Melvin Alistoto, Dotto Kayombo  na Ahmeid Manzi.



Waliosajiliwa ni Jamal Mnyate kwa mkopo kutoka Simba, Adam Salamba kutoka Stand United, Alex Ntiri kutoka Mbao FC ambaye ni raia wa Ghana, Miraji Mwilenga na Awadi Mauya kutoka Mufindi United pamoja na  Steven Mganga kutoka Pamba FC.

Irene Uwoya Amponza Shamsa Ford Amiminiwa Mvua ya Matusi Baada ya Kumsifia Uwoya

$
0
0
Irene Uwoya Amponza Shamsa Ford
Msanii wa filamu Shamsa Ford amefunguka na kusema kitendo cha kumsifia msanii mwezake wa filamu Irene Uwoya kuwa ndiye mwanamke mzuri kuliko wanawake wengine wote wa bongo movie na bongo fleva watu wametokwa na mapovu na kuanza kumtukana.


Shamsa Ford ameendelea kutia mkazo kuwa Irene Uwoya ndiye msanii mzuri kuliko wasanii wanawake wote na kusema labda kidogo ambaye anamkaribia Ray C na kudai Irene Uwoya amejaaliwa karibu kila kitu kuhusu muonekano na kusema yeye muda mwingine huwa anadhani lile ni jini.

"Yaani jana kusema huyu mwanamke ni mzuri kuliko wanawake wote wa Bongo movie imekuwa shida.Yaani mpaka mnanitumia message za matusi? Binadamu nyinyi ni watu wa ajabu sana aisee..Huu ndo ukweli mbishe na mkatae kwa upande wangu na nyinyi wote mnaokubali moyoni halafu machoni mnakataa huyu ndo mzuri..Hana kasolo hata moja kwa vitu vya muonekano..Amejaaliwa na Mwenyezi Mungu kuanzia juu mpaka chini. Mimi huwa nalionaga kama lijini" alisema Shamsa Ford

Aliendelea kusema kuwa "Mbaya zaidi ni mzuri na ana mvuto akipita lazima akusitue. Maana kuna wengine wazuri lakini hawana mvuto wakipita kama hajapita mtu..Wanawake kusifiana ni ngumu ila mimi niko tofauti huwa siwezi kuacha kumsifia mtu pale anapofanya jambo zuri au ana vitu ambavyo huwezi acha kumsifia. Narudia tena Iren ni mwanamke mzuri mwenye mvuto kuliko wanawake wote wa bongo movie hadi wanamziki amewafunika. Ingekuwa enzi zile angeshindana na dada yangu Ray c maana ndo mwanamziki wa kike ninaeonaga ana mvuto na mzuri" alisema Shamsa Ford

Rose Ndauka Afunguka Alichojifunza Katika Ujio wa Ramsey Bongo

$
0
0
Rose Ndauka Afunguka Alichojifunza Katika Ujio wa Ramsey Bongo
Msanii wa filamu Bongo Rose Ndauka amefunguka alichojifunza kutoka kwa Ramsey Nouah wa Nigeria katika ziara yake aliyoifanya Tanzania siku chache zilizopita.

“Nimepokea vitu vingi kwanza mabadiliko, yaani kama unahitaji mabadiliko yanaanza kwako wewe mwenyewe binafsi. Kwa hiyo nilichogundua kwamba wasanii watanzania vitu ambavyo tunalalamika hapa tatizo nini na wenzetu na wenzetu wanakutana na vitu kama hivyo wanakutana na vitu hivyo hivyo,” amesema Ndauka.

Muigizaji huyo ameongeza kwa kusema, “Lakini namna gani unataka kupiga hatua kwenda mbee hilo ndio linakuwa suala. Kwangu mimi ujio wa Ramsey Nouah kwa semina ametupatia leo nimejifunza vitu kutoka kwake na nimejifunza kuchukua Confidence yangu asilimia 100 na kuendelea kupambana na vitu vyangu nilivyokuwa navyo.”

Ramsey alikuwa na ziara nchini Tanzania wiki iliyopita na aliweza kutembelea kaburi la Marehemu Steven Kanumba pamoja na kukutana na waigizaji wa filamu nchini.

Sumatra Yawataka Wasafiri wa Mikoani Watakiwa Kupaza Sauti Wanapokuta Ongezeko la Nauli

$
0
0
Sumatra Yawataka Wasafiri wa Mikoani Watakiwa Kupaza Sauti  Wanapokuta Ongezeko la Nauli
Baraza la Ushauri la Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra CCC) limewataka watumiaji wa huduma za usafiri kutoa taarifa kwa mamlaka husika wanapokutana na ongezeko la nauli katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka.

Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dk, Oscar Kikoyo amesema tayari ameshaanza kusikia malalamiko ya upandishwaji wa nauli unaofanywa kinyemela na baadhi ya watoa huduma za usafiri na hatua zimeanza kuchukuliwa dhidi yao.

Amesema changamoto kubwa inayojitokeza ni watumiaji wa huduma hizo kuwa wazito kutoa taarifa wanapokutana na mambo yasiyofaa ikiwemo kupandishiwa nauli, mwendo kasi kwa kuhofia uhakika wa safari zao.

“Kuna kitu tunatakiwa tubadilike watanzania, yaani utakuta mtu anatozwa nauli kubwa na akiingia kwenye basi mwendo wa dereva unakuwa sio mzuri lakini hakuna anayesema. Wakati mwingine watu wa usalama barabarani wanaingia kwenye mabasi kuhoji lakini hakuna anayepaza sauti wanaishia kunung’unika,

“Tunaomba mtoe taarifa, nauli hazijapanda na usafiri upo wa kutosha ila kuna watu wachache wasio na nia njema wanataka kutumia mwanya wa kuwepo abiria wengi kutengeneza uhaba. Hakuna mmiliki wa chombo cha usafiri anayeruhusiwa kupandisha nauli kwa sababu abiria wapo wengi ,ukiona mtu anakutajia bei tofauti jitahidi hata umrekodi ili ashughulikiwe,” amesema

Kauli hiyo ya Dk Kikoyo imekuja ikiwa tayari hali ya sintofahamu imeanza kujitokeza katika kituo cha mabasi ya mikoani ya Ubungo ambapo baadhi ya watoa huduma ya usafiri wameanza kupandisha nauli.

Sanjari na ongezeko hilo haramu la nauli kumekuwepo pia msongamano wa abiria wanaotaka kwenda mikoani kwa ajili ya sikukuu za Krismasi na mwaka mpya.

Dk Kikoyo pia ametoa tahadhari kwa watoa huduma za usafiri kutoruhusu watu wanaopanda kwenye mabasi na kuhubiri dini na siasa.

Kando na hilo amesema abiria wasisite kutoa taarifa endapo nyimbo na video zitakazowekwa ndani ya basi zitakiuka maadili ya Kitanzania

Mtandao wa Facebook Waingia Kwenye Mtihani Mkubwa Watakiwa Kutoa Taarifa za Watumiaji Wake

$
0
0
Mtandao wa Facebook Waingia Kwenye Mtihani Mkubwa Watakiwa Kutoa Taarifa za Watumiaji Wake
Mtandao wa Facebook unapambana na changamoto ya kutakiwa kutoa taarifa za watumiaji wake kutoka katika mamlaka mbalimbali duniani.

Ingawa mtandao huo kuna baadhi ya taarifa hauzitoi, idadi ya maombi ya taarifa imeongezeka ikilinganishwa na miaka mitatu iliyopita.

Marekani, India, Uingereza, Ujerumani na Ufaransa zinaongoza kwa kuomba taarifa za watumiaji ikiwa ni asilimia 73 ya maombi yote yanayotumwa.

Hata hivyo, wakati mamlaka zikiongeza maombi, Facebook nao wameongeza orodha ya taarifa ambazo hawawezi kuzitoa.

Zipo taarifa ambazo Facebook kabla ya kuzitoa humtaarifu muhusika lakini zipo ambazo zinatolewa bila mhusika kujulishwa.

“Asilimia 57 ya taarifa zilizoombwa na mamlaka za Marekani hazikuturuhusu kuwataarifu wahusika, ikiwa ni ongezeko la asilimia 50 ukilinganisha na mwaka jana,” anasema Makamu Kansela wa Facebook, Chris Sonderby.

Mbali na maombi hayo ya mamlaka, Facebook pia imefungua milango ya maombi ya uwajibikaji katika taarifa zinazowekwa katika mtandao huo.

Katika kipindi cha mwaka mmoja jumla ya maombi zaidi ya  200,000 yalitumwa wakihusiana na taarifa za wizi wa hakimiliki na asilimia 68 ya kazi hizo ziliondolewa katika mtandao huo.

Baada ya Kuzushiwa Kifo Haji Manara Awatoa Hofu Wapenzi Wake

$
0
0
Baada ya Kuzushiwa Kifo Haji Manara Awatoa Hofu Wapenzi Wake
Afisa habari wa klabu ya Simba Haji Sunday Manara amesikitishwa na taarifa za kuzushiwa kifo zilizosambaa mitandaoni wakati yeye ni mzima kabisa.


Haji Manara amesema yeye yupo hai akiwa na afya imara na anamshukuru Mungu huku akitoa pole kwa ndugu na jamaa ambao wamepata usumbufu kwa namna moja ama nyingine kutokana na taarifa hizo za uongo.

“Taarifa zinazoenezwa mitandaoni juu ya uhai wangu si kweli, nipo hai na mzima wa afya kwa uwezo wa Mungu, poleni nyote mliokuwa msibani kwa kupewa taarifa isiyo sahihi, poleni pia familia yangu.hususani mama na dada zangu”, ameandika Manara kupitia Ukurasa wake wa Instagram.

Haji Manara amejizolea umaarufu nchini kutokana na uhodari wake wa kutekeleza majukumu ya kazi yake kama msemaji wa Simba ambapo mara nyingi hutumia maneno ya utani kufikisha taarifa zake hususani zile zinazohusu wapinzani wao wakuu klabu ya Yanga SC.

Kitendo hicho cha kuzushiwa Kifo kimeonekana kuwakera wafuasi wake wengi ambao wametoa pole zao kupitia sehemu ya maoni (Comment) katika picha aliyoiweka kwenye mtandao wake.
 

Chadema Wapingana na NEC "Kailima Hana Mamlaka ya Kutusemea"

$
0
0
Chadema Wapingana na  NEC "Kailima Hana Mamlaka ya Kutusemea"
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekanusha taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwa chama hicho kimechukua fomu za kugombea ubunge katika uchaguzi wa marudio jimbo la Singida Mashariki.


Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya CHADEMA, Tumaini Makene amemtaka Mkurugenzi wa NEC Ndugu Ramadhan Kailima kutojifanya msemaji wa chama hicho kwa hatua ya sasa na kudai kuwa wanafuatilia kupata taarifa za kina kuhusu kauli yake hiyo ambayo ameitoa leo Disemba 19, 2017 wakati akihojiwa na kituo kimoja cha Radio.

"Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakijateua mgombea kuwania nafasi ya ubunge katika uchaguzi huo wa marudio, Jimbo la Singida Kaskazini. Mkurugenzi wa NEC, Ndugu Ramadhan Kailima atambue kuwa suala la kugombea nafasi ya ubunge kwa mchakato wa ndani ya CHADEMA linasimamiwa na Kamati Kuu ya Chama na hivyo hivyo yeye hana mamlaka wala hawezi kuwa msemaji wa suala hilo katika hatua ya sasa" alisema Tumaini Makene

Makene aliendelea kusema kuwa "Tunafuatilia kupata taarifa za kina kuhusu msingi wa kauli ya Mkurugenzi hiyo, kisha tutatoa taarifa kamili katika hatua ya baadae"

CHADEMA walitoa msimamo wao kuwa hawatashiriki katika uchaguzi mdogo wa marudio wa nafasi za ubunge kama Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) haitaahirisha na kusogeza mbele uchaguzi huo katika majimbo matatu mpaka pale wadau wa siasa watakapokaa na kufanya tathmini juu ya kile walicholalamikia kuwa uchaguzi mdogo wa madiwani ambao umefanyika karibuni hakuwa huru na haki, na ulitawaliwa na uvunjwaji wa haki za binadamu.

Hamisa Mobetto Kufanya Part Siku Moja na Zari Uganda

$
0
0


Hamisa Mobetto Kufanya Part Siku Moja na Zari Uganda
Boss lady ambaye ni mpenzi na mama watoto wake Diamond Platnumz ametangaza kuwa siku ya December 21,2017 atafanya party yake ya “Zari All White Party” nchini Uganda ambapo ni desturi yake kufanya party hii kila mwaka.

Kupitia  instagram account ya Hamisa Mobetto ambaye pia ni mzazi mwenzake Diamond Platnumz ameahidi pia kufanya party nchini Uganda Decemeber 21,2017 siku moja na Zari the boss lady kasoro venue tu.

Baada ya Hamisa Mobetto kupost video katika ukurasa wake wa instagram na kuandika caption inayosomeka “Hakuna unachoweza badilisha
Kabiliana nalo..! 💪🏾 #InmyShemsvoice 🤣”



Baadhi ya mashabiki wakahusisha caption hiyo kuwa ni dongo kwa Zari kwani wote kwa pamoja wanafanya party siku moja na nchi moja na kudaiwa kuwa wawili hao hawako katika maelewano mazuri toka Zari agundue kuwa Hamisa amezaa na Diamond Platnumz.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Lipumba Apigwa Stop Kufanya Shughuri za CUF

$
0
0
Lipumba Apigwa Stop Kufanya Shughuri za CUF
Bodi ya (CUF) ambayo ipo chini ya Mwenyekiti wa (CUF), anayeungwa mkono na Msajili wa Vyama Vya Siasa nchini, Profesa Ibrahim Lipumba imepigwa marufuku kufanya shughuli zozote zinazoihusu Taasisi ya CUF mpaka pale shauri la msingi litakaposikilizwa.


Naibu Mkurugenzi Uwenezi wa CUF kwa upande wa Maalim Seif, Maharagande amesema kuwa maamuzi hayo yametolewa leo Disemba 19, 2017 mbele ya Jaji Wilfred Dyansobera katika Mahakamu Kuu Dar es Salaam ambapo Jaji Dyansobera ameitaka bodi hiyo inayodaiwa kuwa ni bodi feki kutojishughulisha na kazi zozote za taasisi ya CUF.

"Mbele ya Mheshimiwa Jaji Wilfred Dyansobera ameipiga marufuku bodi feki ya Lipumba kufanya shughuli zozote zinazoihusu CUF mpaka pale shauri la msingi litakapomalizika. Awali Jaji aliyatupilia mbali maombi ya Wakili msomi Ngole ya kumuomba Jaji asisome maamuzi hayo kwa madai kuwa wanakusudia kukata rufaa juu ya maamuzi ya Jaji kukataa kujitoa kusikiliza mashauri ya CUF. Jaji amesema hakuna hoja za kisheria zinazoizuia mahakama kuacha kuendelea na shughuli ilizozipanga" alisema Maharagande

Mbali na hilo Naibu Mkurugenzi Uwenezi wa CUF kwa upande wa Maalim Seif, Maharagande amesema kuwa CUF ni taasisi imara yenye viongozi makini na kudai kuwa kwa ushindi huo ni wazi kuwa CUF mpya inazaliwa muda si mrefu sana.

Soko la Filamu Lilikua Baya kwa Mwaka 2017- JB

$
0
0
Soko la Filamu Lilikua Baya kwa Mwaka 2017
Muigizaji na muongozaji wa filamu Tanzania Jacob Steven maarufu kama JB, amesema mwaka 2017 hakuwa mzuri kwa wasanii wa tasnia hiyo, kwani soko la filamu kwao lilikuwa la kusuasua.


Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, JB amesema tasnia ya filamu inakumbwa na tatizo kubwa la usambazaji wa kazi zao, kitendo ambacho wafanyabiashara wa filamu wanahofia kuwekeza pesa ya kutosha kwenye tasnia hiyo.

“Mwaka 2017 hakuwa mzuri kwa bongo movie, tumekuwa na tatizo kubwa sana la usambazaji, usambazaji ni tatizo kubwa sana, kwa sababu hawa watayarishaji ni wafanya bisahara pia, hawezi kuweka pesa zake kama haoni ni namna gani pesa zake zinaweza kurudi, hivyo tulikuwa tunasua sua lakini ujio wa barazani umesaidia sana, na nawaahidi mwaka 2018 tutafanya makubwa sana”, amesema JB.

Pamoja na hayo JB amekiri kuwa ubora wa filamu nao ni moja ya sababu ambazo zinafanya soko hilo kutofanya vizuri, jamboa ambalo pia amesema limefanyiwa kazi kwani kufikia mwakani hakuna filamu ambayo itashutiwa kwa camera za kawaida zaidi ya kutumika kwa red camera.

Patrick Kanumba Kurudi Tena Kwenye Soko la Filamu

$
0
0
Patrick Kanumba Kurudi Tena Kwenye Soko la Filamu
Msanii wa filamu, Othman Njaidi a.k.a Patrick Kanumba ambaye ni zao la marehemu Steven Kanumba amefunguka ujio wake katika tasnia hiyo.

Patrick amesema mwakani anatarajia kurejea katika filamu baada ya kujikita katika masomo kwa kipindi kirefu na kazi tayari zimeshafanyika.

“Mpaka sasa nipo kimya ila soon inshallah Mungu akifanya wepesi tunaanza mwakani rasmi upya, nilikuwa nasoma na bado mimi ni wanafunzi,” Patrick ameiambia Bongo5.

Katika hatua nyingine amesema kuna uwezekano wa kuja kufanya tena kazi na Jennifer ambaye waliigiza wote movie ya Uncle JJ na marehemu Kanumba.

“Zipo nyingi sana kama tulivyokuwa shule kazi nyingi zinakuwa zinajitokeza sema kwa sababu tuliamua tujikite kwanza kwenye masomo, kwa hiyo kazi nyingine tukawa tunaziacha na tunashuru Mungu waliokuwa wanataka kutupa kazi walikuwa wanatuelewa” amesisitiza Patrick.

Wananchi Wawatumbua Viongozi Wao

$
0
0
Wananchi Wawatumbua Viongozi Wao
Wananchi wa kijiji cha Msosa kilichopo Kata na Tarafa ya Ruaha Mbuyuni wilayani Kilolo mkoani Iringa wameiondoa kamati ya Mipango na Fedha kwa tuhuma za kufanya ubadhilifu wa mali za kijiji.


Uamzi huo umefikiwa na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini humo na baada ya kuwaondoa viongozi hao wanakijiji waliunda kamati mpya kwaajili ya kusimamia majukumu hayo.

Kwa upande wake mtendaji wa Kata hiyo Maiko Chabila ameafiki kuvuliwa madaraka kwa viongozi wa kamati ya mipango na fedha kutokana na tuhuma zinazowakabili.

East Africa Television imemtafuta Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Juma Abdallah, amesema suala hilo bado halijafika ofisini kwake lakinitayari ameshatuma wawakilishi wake kuhakikisha wanalifuatilia na kupata ufumbuzi wake.

Hata hivyo kamati hiyo ya Mipango na Fedha ya kijiji cha Msosa wamekubali kujiudhuru pamoja na kulipa pesa ambazo zimebainika kuwa walizitumia vibaya bila kuwashirikisha wananchi.

Mjadala wa Kikomo cha Umri wa Rais Wasitishwa Bungeni Uganda

$
0
0
Mjadala wa Kikomo cha Umri wa Rais Wasitishwa Bungeni Uganda
Spika wa bunge la Uganda, Rebecca Kadaga amelazimika kusimamisha mjadala wa muswada tata uliokusudia kufuta kipengele cha ukomo wa umri wa rais baada ya mbunge wa upinzani Lucy Akello kulalamika kuwa kulikuwa na wanajeshi kwenye moja ya kumbi za bunge inayotumika kufanya ibada.

Mwandishi wa BBC Patience Atuhaire, anaelezea kuwa baadhi ya wabunge waliorudi kutoka kuchunguza ukumbi huo walisema kuwa walipata chupa zenye mikojo, ambazo wanajeshi hao walikuwa wanatumia kujisaidia.

Walisema pia wamepata vyombo vilivyotumika na mabaki ya chakula.

Baadhi ya wabunge walijaribu kuvipeleka vyombo hivyo bungeni kabla ya kipindi kuanza lakini maafisa wa usalama walivinyakua.

Wabunge watwangana makonde Uganda
Museveni aamuru mateso kukomeshwa Uganda
Mwandishi wa BBC Patience Atuhaire anasema, hali ni ya taharuki ndani ya ukumbi wa bunge na mhemko ni mkubwa wakati wabunge wanaposema maeneo yao ya ibada yamedharauliwa

Kumbi zote za ibada za Wakatoliki na Waprotestanti zinaelezwa kutumika na wanajeshi.

Kisa hicho kiliwashutua raia wangi wa Uganda.

Maafisa wa polisi na wale wa kijeshi wamepelekwa nje ya bunge pamoja na maeneo mengine ya mji .

Mamlaka inasema kuwa wamejiandaa dhidi ya ghasia wakati wa mjadala.

Bunge linatarajiwa kuendelea siku ya Jumanne mchana.Wakati wa makabiliano kati ya wabunge wa upinzani mnamo mwezi Septemba , wanajeshi kutoka katika kikosi maalum waliokuwa wamevalia sare za raia waliingia katika bungeni na kuanza kuwapiga na kuwakamata wabunge.

Chadema Wageukana Singida Wasimamisha Mgombea

$
0
0
Chadema Wageukana Singida Wasimamisha Mgombea
Wakati zikiwa zimebaki siku 25 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo katika  Jimbo la Singida Kaskazini, kivuli cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Lazaro Nyalandu kimeigawa Chadema katika pande mbili.

Wakati Chadema taifa kikiwa kimeeleza kutoshiriki katika uchaguzi huo Januari 13 mwakani kwa madai ya kutokuridhishwa na uchaguzi wa udiwani wa Kata 43 uliofanyika Novemba 26, uongozi wa Chadema mkoa wa Singida jana umempitisha mgombea atakayepeperusha bendera ya chama hicho.

Uchaguzi wa jimbo hilo unafanyika baada ya Nyalandu kutangaza kujivua uanachama wa CCM Oktoba 30 na kujiunga na Chadema huku mrithi wake akikigawa Chama chake kipya cha Chadema.

Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Singida, Shaban Limu amesema leo Desemba 19  kuwa  wamemteua Djumbe David Joseph kupeperusha bendera ya Chadema na msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Singida naye amempitisha.

“Leo tunatarajia kufanya kikao cha kuweka mikakati ya kampeni. Kesho na kesho kutwa, tutaingia kazini kwa kufanya kampeni zitakazokileta chama matokeo tunayoyatarajia ambayo ni kushinda uchanguzi huo mdogo,” alisema Limu

Mbali na Djumbe, wagombea wengine na vyama vyao kwenye mabano ni Dalphina Patrice Mlewa (CUF), Omari Mohammed Sombi (Alliance for Tanzania Farmers Party), Monko Justein Joseph (CCM), Aloyce Mohammed Nduguta (Ada Tadea) na Mchungaji Samwel Libisu (CCK).

Wagombea hao walitangaza jana Desemba 18, 2017 na Msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Singida, Rashid Mandoa amesema wamepitisha wagombea hao baada ya kukidhi vigezo vyote vinavyo hitajika.

Mandoa amesema wagombea kutoka vyama vya NRC na UMD wao hawakupitishwa baada ya kushindwa kukidhi vigezo. Pia wagombea kutoka UDP na UDPP hawakurudisha fomu.

Akizungumzia uamuzi huo, Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema amesema; ‘’kwa mjibu wa Katiba ya Chadema, Kamati Kuu ndiyo inayopitisha jina la mgombea na Kamati Kuu haijakutana sasa hilo jina limepatikanaje.”

“Tutashangaa hata NEC (Tume ya Taifa ya Uchaguzi) kama wataendeleza mchakato wa jina hilo na tumeagiza tuletewe taarifa na hatua zitachukuliwa kwa wahusika kwani kilichofanyika ni kosa la jinai, kama barua ya Katibu Mkuu kuthibitisha kupitishwa na Chama haipo wao wameitoa wapi,” amehoji Mrema

Amesema kama kuna watu wametumiwa basi watambue kwamba msimamo wa chama haujabadilika na wanafuatilia suala hilo na hatua zitachukuliwa kwa viongozi waliohusika.

Baada ya Kuzushiwa Kifo Manara Apokelewa kwa Shangwe Msibani

$
0
0
Baada ya Kuzushiwa Kifo Manara Apokelewa Aibua Shangwe Msibani
Msemaji wa Simba, Haji Manara amekutana na wakati mgumu baada ya kuzushiwa kifo.

Baadhi ya watu wametupia mtandaoni wakielezea kuwa Manara amefariki dunia.

Hata hivyo, Manara amesema taarifa hizo ni uzushi mkubwa na alikwenda msibani na kupokelewa kwa shangwe kwa kuwa tayari watu walipata taarifa kwamba amefariki dunia.


"Jaman ndugu zangu toka Jana kuna habari zinazagaa kuwa nimekufa. Kaka yangu anaitwa Ramadhan kitenge alinipigia Jana kuwa kaona fb," anaelelezea Manara.

"Ndugu zangu na mama yangu mzazi nao walipigiwa simu, nikapuuza. Lakini leo wakati nikijiandaa kwenda msibani kwa mwanachama wetu maarufu dada Fii kambi.

"Nikapigiwa cm nyingi za kutaka kujua hali na uhai wangu na kweli nilipofika msibani nimekuta vilio vya kina mama kuwa nimefariki.

"Kiukweli mm ni mzima wa afya, siumwi chochote na Alhamdulillah naendelea na shughuli zangu kama kawaida. Kufa tutakufa tu kwa ahadi yake Mungu, puuzeni uvumi wa mitandaoni," anasisitiza Manara

Baadhi ya Sababu Kwanini Tunaingia Kwenye Ndoa na Watu Wasio Sahihi

$
0
0

Tendo la Ngono; Hili inapokua mapema ni kama kulisha kuku wa kisasa. Inafanya mahusiano yakue haraka bila kuwa na uimara au ubora wenye virutubisho vyenye ladha. :
.
Ngono ya mapema inatengeneza kitu kwa kitaalamu kinaitwa GMR - Genetically Modified, Relationship au Early maturing. Badala ya kifikiria jinsi ya kufanya mahusiano yawe bora, mtaanza kufikiri namna ya kufanya se..x vizuri zaidi mtakapokutana next time. :
.
Badala ya kutizama kama partner wako anafaa kuwa mume au mke, utaanza kutizama kama partner wako yuko vizuri au vibaya kitandani. Baada ya kupanga pamoja future yenu, mtakua mkipanga pamoja style za se....x basi, kama vile mnajiandaa kutengeneza video za ngono.

Money (Pesa): Ndio maana maandiko yanasema pesa ndio shina la kila mabaya (1 Timothy 6:10)...pesa zinaweza zikakufanya uoe au uolewe na mtu asie sahihi. :
.
Mathalani, mwanaume anapokua na pesa, wanawake wapenda pesa tu wataanza kujitokeza na kujigonga kwake, itaongeza chances za yeye kuoa wale wanaopenda pesa zake tu. Pesa zitampiga upofu na wala asione mtu sahihi. :
.

Vivyo hivyo, hata mwanamke anapokua na pesa, wanaume bora wasio jiamini watamuogopa, watajenga picha ya mwanamke alie na kiburi kutokana na pesa zake..hivyo basi huyo mwanamke atawavutia zaidi ma-handsome wenye pesa zaidi ambao hawana la ku-offer zaidi ya "Vitamin-D".
:
Kuwa na pesa nako ni kikwazo kikubwa katika kupata mtu sahihi. Busara na mtizamo ulio chanya vinahitajika sana.
:
Good looks (Muonekano mzuri): Ushawahi kuona reaction ya wale wanawake wanaojiona wazuri ukiwafuata. Kwa sababu wanajiona wako na demand kubwa, huwakataa wanaume walio bora na wanaongeza bar of standards. :
.
Kwa kufanya hivyo wanawakosa kabisa wale wanaume walio na nia ya dhati. Vilevile, katika kutafuta life partner, uzuri umekua ni giza linalofunika mengine mazuri ya mtu husika yasionekane. Bila ya kufahamu kuwa hata shetani (Lucifer) nae alikuwa ni mzuri mno na aliyeng'aa kabla ya kutaka kujiinua na Mungu akampiga chini.
:
Usikubali hips zikudanganye, usiruhusu six pack zikupige upofu...kwenye ndoa kuna zaidi ya muonekano wa nje wa mtu.

©kihuba
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live




Latest Images