Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Kimya Cha Wasomi Chamuogopesha Msigwa

$
0
0
Kimya Cha Wasomi Chamuogopesha Msigwa
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa ametoa lawama kwa wasomi nchini akidai wamekuwa wakikaa kimya hata pale wanapoona masuala ya Taifa hayaendi sawa.

Mchungaji Msigwa amesema hayo wakati wa mjadala uliofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha (RUCU) wakati wa kongamano kujadili kitabu kinachohusu miaka 70 ya kusaka demokrasia kwa nchi za ukanda wa Maziwa Makuu kilichoandikwa na Profesa Gaudence Mpangala wa chuo hicho.

 “Kwanza nimpongeze Profesa Mpangala kwa kuja na utafiti huu ambao unaonyesha hali ya kidemokrasia nchini bado iko chini, nchi hii inawategemea ninyi wasomi ili iweze kusonga mbele, lakini kwa bahati mbaya mmetuachia sisi vipofu ndio tunaowachaguliwa njia ya kupita,” amesema Mchungaji Msigwa.

Amesema, “Upo usemi nimekuwa nikiutumia hata bungeni ‘akili ndogo kuongoza akili kubwa’ na leo hapa niwaeleze kuwa licha ya kuwa Taifa linawategemea, ninyi ndio mnaofanya tafiti bado mmeacha sisi wenye akili ndogo kuwachagulia ngoma ya kucheza nanyi mnakubali kuicheza hata pale mnapoona Taifa linatumbukia shimoni,” amesema.

Mchungaji Msigwa amewataka wasomi kutimiza wajibu wao na kuwataka kutumia elimu waliyonayo kushauri na kukosoa pale wanapoona inafaa kufanya hivyo.

Amesema hatua hiyo itasaidia Taifa kujenga misingi bora ya demokrasia inayoheshimu haki za binadamu na utawala bora na kusaidia kuinua uchumi wa nchi.

Mwandishi wa kitabu hicho, Profesa Mpangala amesema ili hali ya usawa wa kidemokrasia nchini iweze kufikiwa ni lazima kuandika Katiba mpya kwa kurejea maoni yaliyomo katika rasimu ya iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.

Rais Magufuli Ataka Wapotoshwaji Takwimu Washughulikiwe

$
0
0
Rais Magufuli Ataka Wapotoshwaji Takwimu Washughulikiwe
RAIS Dkt. John Magufuli ametoa agizo kwa Mamlaka ya Takwimu ya Taifa (NBS) kuwachukuliwa hatua haraka mashirika, taasisi na watu wanaotoa takwimu potofu kuhusu ukuaji wa uchumi wa nchi na mambo mengine ya serikali ikiwemo kuwakamata na kuwafikisha mahakamani.

“Wanaosema vyuma vimebana vitaendelea kubama kweli kweli lakini wananchi wa Lindi na Mtwara wameamua kufanya kazi, kwao vyuma havitakaza kutokana na kupanda kwa bei ya Korosho. Nasikia wanawanywesha Mbuzi bia.

“Nyumba zimeanza kushuka bei Dar, walikuwa wanalipisha kwa Dola, nyumba hizo lwamezikimbia. Tusitake kutangaza kuwa vyuma vimekaza kwa nia mbaya, watu hao muwapuuze.

“Watu wanaolalamika eti vyuma vimebanwa vitabanwa kweli kweli. Tutabana vichwa, miguu, matumbo, tutabana kila kitu.

“Ninawaomba Watanzania mpuuze uzushi unaoendelea kwenye mitandao ya kijamii kwamba uchumi umeshuka. Tumieni takwimu zilizokusanywa na ofisi ya takwimu ya taifa. Achaneni na wanaosema vyuma vimekaza, tumelegeza kwa wananchi wa kawaida.

“Ili takwimu ziwe muhimu basi ziwe sahihi. Naendelea kusisitiza Taasisi ya Takwimu kuendelea kutoa takwimu sahihi. Natoa onyo kwa watu wanaotoa takwimu za uongo, naagiza mamlaka husika kuchukua hatua mara moja kwa watu wa namna hiyo.

“Ninaomba kutoa onyo hasa kwa wale ambao wanakuja na takwimu zao za mifukoni. Mamlaka husika mtumie sheria zilizopo kuwabana wale ambao wanataka kuwapotosha Watanzania kwa takwimu zao za uongo. Ukukosea kutoa takwimu…umeichafua nchi”

“Kifungu cha sheria kinasema atakayepotosha takwimu adhabu ni kifungo cha kuanzia miezi sita hadi miaka mitatu. Au faini ya Millioni moja hadi millioni kumi au vyote kwa pamoja. Tena mimi ningekuwa Jaji hii ya mwisho ndio ningetekeleza.

“Niwaombe vyombo vya habari na wataalam wa mitandao, muwaone wataaalm wanaohusika na takwimu, tusitafute takwimu za kupika.

“Natoa agizo, akitokea mtu anatoa taarifa za uongo na ikathibitika kweli amepotosha, chukueni hatua haraka. Awekwe mahabusu ili aendelee kujifunza namna ya kutoa takwimu sahihi,” alisema Magufuli.

Kocha wa Azam FC Aamua Kumpima Mshambuliaji Wake Mpya

$
0
0
Kocha wa Azam FC Aamua Kumpima Mshambuliaji Wake Mpya

Bosi wa benchi la Ufundi la Azam FC, Mromania, Aristica Cioaba, amefunguka kuwa licha ya mshambuliaji mpya wa timu hiyo, Mghana, Bernard Arthur kuanza kuonyesha uwezo mkubwa wa kufunga lakini ataitumia michuano ya Kombe la Mapinduzi kujua uwezo wake.

Arthur amejiunga na Azam katika usajili wa dirisha dogo kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Liberty Professional, amekuwa na mwenendo mzuri wa kufunga katika mechi mbili za kirafiki alizocheza.

Cioaba alisema kuwa atatumia michuano ya Mapinduzi katika kujua uwezo wa mchezaji huyo licha ya kuanza kuonyesha uwezo mkubwa katika safu ya ushambuliaji ambayo ilikuwa tatizo.

“Timu ipo vizuri, tunashukuru tumeweza kufanya vizuri katika huu mchezo na kila mchezaji ameonyesha utofauti katika kutafuta matokeo, haijalishi tumecheza na timu ya aina gani, kikubwa kilikuwa ni kuangalia timu yangu ipoje.


“Kuhusu Arthur, nadhani bado anahitaji muda zaidi, sawa leo (juzi) ameweza kufunga mabao kwa uhakika kitu ambacho mwanzoni kilikuwa tatizo katika timu yangu kutokana na wachezaji ambao walikuwepo, zaidi nitaitumia Kombe la Mapinduzi kujua uwezo wake halisi kwa sababu hatutaweza kuwa na Mbaraka Yusuf kwa kuwa ni majeruhi," alisema Cioaba.

Korea Kusini Yaitaka Marekani Kusitisha Mazoezi ya Kijeshi Nchini Humo

$
0
0
Korea Kusini Yaitaka Marekani Kusitisha Mazoezi ya Kijeshi Nchini Humo
Rais wa Korea Kusini Moon Jae-In ameitaka Marekani kuacha kwa muda mazoezi yake ya kijeshi nchini humo mpaka kumalizika kwa michuano ya Olimpiki itakayofanyika mapema mwakani.

Anasema hii itasaidia pia kuifanya Korea Kaskazini kutotilia shaka uwepo wa wanamichezo wake kwenye michuano hiyo.

Korea Kusini itakua mwenyeji wa michezo hiyo itakayofanyika katika mji wa Pyeongchang mwezi Februari ikiwa ni kilomita 80 kutoka mpaka wake na Korea Kaskazini.

Mapema Canada na Marekani ziliapa kuendeleza mazoezi hayo ili kuisukuma Korea Kaskazini kuachana na mpango wake wa nyuklia.

Image caption
Vikosi vya jeshi la Korea Kusini na Marekani vikifanya mazoezi ya kijeshi karibu na mpaka wa Korea Kaskazini
Marekani na Korea Kaskazini zimekuwa katika mgogoro wa muda mrefu kufuatia mpango wa matumizi ya mabomu ya nyuklia unaofanywa na Korea Kaskazini.

Michuano ya Olimpiki ya majira ya baridi inatarajiwa kuhusisha pia wanamichezo kutoka Korea Kaskazini jambo ambalo Rais wa Korea Kusini Moon Jae-In anaeleza kuwa ni la kuimarisha uhusiano zaidi.

Mgombea Ubunge wa Chadema Aliyepitishwa na NEC Ajitoa Katika Uchaguzi

$
0
0
Mgombea Ubunge wa Chadema Aliyepitishwa na NEC Ajitoa Katika Uchaguzi
Djumbe Joseph aliyepitishwa na (NEC) kugombea ubunge Jimbo la Singida Kaskazini kwa tiketi ya CHADEMA, ameandika barua ya kujitoa katika uchaguzi mdogo ambao unatarajiwa kufanyika Januari 13, 2018 kwa kile alichosema anafuata msimamo wa chama chake.

Akiongea na waandishi wa habari Djumbe Joseph amesema kuwa ameamua kuungana na viongozi wakuu wa chama chake kutoshiriki katika uchaguzi huo mdogo ambao unategemewa kufanyika mapema Januari 2018.


Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jana kilitangaza kuwa hakiweka muakilishi yoyote kugombea jimbo hilo la Singida Kaskazini kwa kile walichosema awali kuwa hawawezi kushiriki uchaguzi huo wa marudio bila tathimini kufanyika juu ya uchaguzi wa udiwani uliofanyika karibuni ambao ulitawaliwa na uvunjwaji wa haki na sheria pamoja na watu kupigwa hovyo.

JB Afunguka Kuhusu Gabo " Tulifanya Makosa Kumtengeneza

$
0
0
JB Afunguka Kuhusu Gabo " Tulifanya Makosa Kumtengeneza
Msanii mkongwe wa filamu bongo ambaye ni maarufu kwa kuibua vipaji vya wasanii wengine, Jacob Steven au JB, amesema wao kama wakongwe wa sanaa walifanya makosa kumtengeneza Gabo peke yake.

Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, JB amesema kitendo cha kumtengeneza Gabo peke yake kwa kipindi ambacho alianza kuwa kwenye 'pick', walitakiwa kuwatengeneza kina Gabo wengine kama watatu, ili kuweza kuleta changamoto zaidi kwenye tasnia ya filamu.

JB ameendelea kwa kusema kwamba hata ukiangalia historia ya sanaa ya bongo movie, walianza na 'intake' ya marehemu Kanumba na Ray, kisha wakaja kizazi cha kina Hemedi Suleiman na Yusuph Mlela, lakini kipindi cha Gabo hakukuwa na wengine ambao wangeweza kusimama kwenye soko na kuleta ushindani wa kazi, hivyo kumfanya Gabo asimame peke yake licha ya uwezo mkubwa alionao kwenye sanaa.

“Unajua tulifanya makosa kwa Gabo, tulifanya makosa makubwa sana, kipindi ambacho tulimtengeneza Gabo tulitakiwa kuwatengeneza kina Gabo wengine kama watatu hivi, nasema hivi kwa sababu ukiangalia kwenye bongo movie kuna intake ambazo zilikuwa zinaleta ushindani mkubwa sana kwenye soko, kulikuwa na kizazi cha Kanumba na Ray, kikaja kizazi cha kina Hemedi Suleiman na Yusuph Mlela, lakini kwa Gabo amekuwa peke yake, sisesemi kwamba hakuna wengine, ila ukiangalia ile trend tulipaswa kufanya hivyo ili kuleta changamoto na ushindani kwao, matokeo yake Gabo ndiye anaonekana bora kuliko wengine”, amesema Jacob Steven.

Licha ya hayo JB amekiri kuwa Gabo ndiye muigizaji bora kwa sasa, na ndiye ambaye yupo kwenye 'pick' kama ambavyo alikuwa marehemu Kanumba.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065

Wabunge wa Tanzania na Burundi wamkataa Spika

$
0
0
Wabunge wa Tanzania na Burundi wamkataa Spika
Baada ya Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika mashariki kuchaguliwa na wajumbe wa nchi nne za jumuiya badala ya sita wabunge kutoka Burundi na Tanzania na Burundi wamesema uchaguzi huo umekiuka misingi na kanuni za Jumuiya hiyo.


Wakizungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha, Mwakilishi wa wabunge hao wamesema hakukuwa na sababu ya kutumia nguvu jazba na uharaka wa kumchagua Spika kabla ya hoja zao ikiwemo ya kutaka kupata ufafanuzi wa mzunguko wa kumpata spika haujatolewa na kwamba hawakubaliani na na suala hilo na endapo  hali isipodhibitiwa malengo ya kuundwa kwa jumuiya hiyo hayatatimia.

Kwa upande wao Wabunge kutoka Tanzania wamesema hatua ya wabunge wa bunge hilo kuanza kukiuka viapo vyao muda mfupi baada ya kuapishwa ni dalili za kukosa moyo wa uvumilivu, umoja, na ushirikiano wa dhati ambao kwa muda wote ndio umekuwa msingi wa jumuiya hiyo na sio dalili nzuri hasa ikizingatiwa kuwa miongoni mwa malengo ya jumuya ni kudumisha mshikamano na kwamba kilichofanyika ni sio kumchagua Spika bali ni maoni yao kuwa Mh. Martin anafaa kuongoza.

Aidha Wabunge wa Tanzania wamesema kuwa wanaendelea kuziomba ngazi zinazohusika kuangalia upya suala hilo na kutoa nafasi ya majadiliano kwani ndio msingi wa kupata suluhu.

Kufuatia hali hiyo wabunge kutoka Burundi licha ya kudai kuwa hawamtambui Spika aliyechaguliwa wamesema hawawezi kushiriki kikao chochote kitakachoendeshwa na spika huyo.

Wabunge hao wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waliapishwa siku ya tarehe 18 /12 /2017 na wakati wa kumchagua spika uliibuka mjadala unaodaiwa kusababishwa na taarifa zilizotolewa na katibu wa Bunge kuwa wabunge wa nchi zote ispokuwa uganda wanaweza kuomba kugombea uspika wakati utaratibu wa awali ulikuwa ni wa kufuata mzunguko.

Wabunge hao wamefafanua kuwa hata kama mzunguko ungezingatiwa bado lingehitaji ufafanuzi ambao ungezihusisha Burundi, Rwanda na Sudani Kusini suala ambalo wanasema licha ya kuliwasilisha lilipuuzwa.

Rado Afunguka Atakavyowakutanisha Wasanii Zaidi ya 3,000 Katika Movie Moja

$
0
0
Rado Afunguka Atakavyowakutanisha Wasanii Zaidi ya 3,000 Katika Movie Moja
Msanii wa filamu Bongo, Rado amesema ana mpango wa kukutanisha wasanii/watu zaidi 3,000 katika movie moja.

Muigizaji huyo amesema hayo katika mahojiano na kipindi cha Uhondo cha E Fm ambapo ameeleza hiyo itakuwa pia ni kama kutoa fursa ya ajira kwa wale watakaoshiriki.

“kuna filamu nataka kuifanya mwezi wa tatu nafikiria kucheza na wasaniii zaidi ya  elfu tatu na hiyo itakuwa ni sehem ya ajira kwa watu hao” amesema Rado.

Hivi karibuni Rado alitoa filamu inayokenda kwa jina Bei kali.

Haya Ndio Maneno Aliyoandika Zahir Zorro “Nikifa Nitalala kwa Amani”

$
0
0
Haya Ndio Maneno Aliyoandika Zahir Zorro “Nikifa Nitalala kwa Amani”
Mwanamuziki mkongwe nchini  Zahir Zorro ambaye aliingia kwenye tasnia ya muziki 1968 na alifahamika zaidi alipokuwa kwenye band ya JKT Kimulimuli ambapo aliendelea kutamba kwenye fani hiyo sambamba na watoto wake Banana na Maunda Zorro.

Zahir Zorro amechukua headlines kupitia ukurasa wake wa twitter baada ya kuandika historia fupi ya maisha yake pamoja na watoto wake Maunda na Banana, alitamani sana kuishi Ulaya akiwa bado mwenye umri mdogo kwani alijua hela inapatikana nje ya Afrika.



Mama yake Zahir Zorro hakutaka mwanae atoke nje ya Afrika na kusema kuwa elfu 75 ni bei ya gari aina ya Peugeot 504 na kuwa sio hela kubwa ya kumudu maisha nje ya Afrika na ana uwezo wa kumnunulia gari hilo, hivyo ajiunge na jeshi kwanza.

Gari aina ya Peugeot 504



Ila kwa upande wa baba yake Zahir Zorro alitamani sana mwanae apitie maisha ya jeshi ili siku moja akifariki akapumzike kwa Amani akijua kuwa ameacha mtu imara mwenye uwezo wa kuisimamia familia yao, na hivyo alijiunga na kulitumikia jeshi kwa miaka 16.

Zahir Zorro hakuweza kufata mila na destruri za kijeshi na hakutaka watoto wake wapitie huko hivyo ilimgharimu kuwatafutia mwalimu wa Martial Arts(mafunzo ya karate) na mwisho wake Maunda alijiunga na Jeshi la Polisi lakini mwisho wa siku hakuweza kulitumikia jeshi hilo.



Baada ya yote hayo Banana Zorro alipata nafasi na bahati ya kuishi Uingereza lakini baada ya kuishi huko wiki mbili  alitamani apate uraia ili aishi huko milele ila kuna msemo unasema nyumbani ni nyumbani na hivyo Banana alirudi nyumbani kutokana na kumkumbuka sana baba yake “Nimekukumbuka sana siwezi kuishi mbali na wewe”



Zahir Zorro alitamba na ngoma zake tofauti tofauti zikiwemo Beatrice, Cleopatra, Danga Che na Chiku lala salama.


James Mbatia Avunjika Mkono Alazwa KCMC

$
0
0
James Mbatia Avunjika Mkono Alazwa KCMC
Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC mjini Moshi baada ya kuvunjika mkono.

Mbatia ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), amevunjika mkono wa kushoto baada ya kuteleza na kuanguka na amelazwa katika wodi za watu mashuhuri (VIP).

Msaidizi wa mbunge huyo, Hamis Hamis amesema leo Jumatano Desemba 20,2017 kuwa tukio hilo lilitokea jana saa 2:45 usiku wakati akiondoka hotelini kurejea nyumbani.

Hamis amesema Mbatia alikuwa akishuka ngazi katika hoteli ya Uhuru iliyopo eneo la Shanty Town ndipo alipoteleza na kuanguka.

“Bahati nzuri pale kulikuwa na daktari wa KCMC anaiwa Ansbert Sweetbert ndiye alitoa huduma ya kwanza hadi kumpeleka KCMC,” amesema.

Amesema, “Kwa kweli huyo daktari alikuwa msaada mkubwa. Ndiye aliyempeleka KCMC na alikaa naye hadi saa nane usiku. Wauguzi na madaktari KCMC walimpa msaada mkubwa.”

Mbatia ambaye pia ni mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi alipotafutwa leo mchana amesema bado maumivu aliyonayo ni makali kutokana na kuvunjika mkono.

“Bado nina maumivu makali. Nashukuru sana Mungu na jopo la madaktari limeshakutana na watafanya uamuzi,” amesema.

Mbatia amesema alishapatiwa matibabu ya mwanzo baada ya vipimo vya X-Ray kuthibitisha amevunjika mkono, lakini madaktari wanafanya tathmini ni huduma gani zaidi apewe.

Chanzo: Mwananchi

Ben Pol Awapa Makavu Wasanii Wenzake

$
0
0
Ben Pol Awapa Makavu Wasanii Wenzake
Msanii wa kiume wa bongo fleva Ben Pol, amewataka wasanii wenzake kuacha uvivu na kufanya kazi kwa bidii, kwani licha ya sanaa kuwahitaji, pia wana majukumu ya kutimiza.


Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Ben Pol amesema wao kama wasanii wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii, kwani kuna watu wanawategemea, ikiwemo familia zao na mashabiki wao.

“Niwaambie wasanii wenzangu tuache uvivu hii ni kazi yetu, familia zinatutegemea, tuna-teams ambazo zinaishi kupitia sisi, tuna mashabiki wanatuangalia, turudi studio turudi studio tutoe albam, kama kuna changamoto tutakabiliana nazo mbele kwa mbele”, amesema Ben Pol.

Ben Pol hakuishia hapo aliendelea kwa kuitaka serikali kuhakikisha wanasimamia ipasavyo kazi zao za sanaa, kwani na wao tayari wameshaanza kuchangia pato la serikali kwa kukatwa kodi.

“Tushaanza kulipwa kodi, kwenye shows tunakatwa, mtu anakuja pale mlangoni na mashine, kwa hiyo na wao serikali watusaidie kwenye biashara yetu”, amesema Ben Pol.

Ifahamike kwamba Ben Pol ni miongoni mwa wasanii wachache ambao mwaka huu wameachia albam, kitendo ambacho wasanii wengi wanakiogopa.

Nikki wa Pili Afunguka Kutoweka kwa Utamaduni wa Ngoma Hip Hap Kuwa na Verse Tatu

$
0
0
Nikki wa Pili Afunguka Kutoweka kwa Utamaduni wa Ngoma Hip Hap Kuwa na Verse Tatu
Msanii wa muziki Bongo, Nikki wa Pili amefunguka kutoweka kwa utamaduni wa ngoma nyingi za hip hop kuwa na verse tatu.

Rapper huyo kutoka kundi la Weusi amesema muziki unaendana na mapokeo yake na media nyingi sasa zinapiga muziki verse moja au mbili, pia wasanii wa Bongo Flava hawataki kukumbwa na kitu kilichokumba muziki wa band au taarab kutoka na nyimbo zao kuwa refu.

“Kwa hiyo watu wa media sasa hivi time zao ni ndogo, wanahitaji nyimbo fupi ili waweze kupiga muziki mwingi ili mtu anayesikiliza aone muziki unaenda ukibadilika, kwa hiyo sisi kama wasanii wa kizazi kipya tumeenda na time,” Nikki ameiambia Bongo5.

“Ukisema sasa unapiga verse tatu hamna mtu atasikiliza na kama unapiga inabidi iwe fupi, ndio maana ukisilikiza wimbo kama Dude au Madaraka ya Kulevya verse yangu ina mistari kama nane au 12 tu” ameongeza.

Nikki kupitia kundi la Weusi kwa sasa wanafanya vizuri na ngoma yao mpya ‘NiCome’.




TID Ananipa Vitisho Vingi Sana Kisa Demu – Calisah

$
0
0
TID Ananipa Vitisho Vingi Sana Kisa Demu – Calisah
Model Calisah amefunguka kwa kudai kwamba anapokea vitisho vingi kutoka kwa muimbaji, TID kwa madai anamchukulia demu wake.
Calisah amedai amekuwa akipokea vitisho kutoka kwa marafiki zake wa karibu wakidai wametumwa na muimbaji huyo aliyewahi kufanya vizuri na wimbo, Zeze.

“Ni kweli nimekuwa nikipokea vitisho kutoka kwa TID anadai namchukulia demu wake sio kweli,” Calisah aliimbia Bongo5. “Huyo demu nilikutana naye kwenye bwawa la kuogelea akajoin na mimi basi tukawa washkaji kabisa mpaka sasa tunaongea vizuri na ni watu wa kawaida,”

Muimbaji TID alimpost mrembo huyo kupitia instagram yake na kuandika “My melodies Sing back,Half human half Mnyama she is my Nusu kwa Nusu,”

Penzi kwa Simu Linanoga, ila Nikimuona Penzi Nywiii

$
0
0
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 24 naishi Dubai. Nimepata Mchumba ana umri wa miaka 37 na kakubalika nyumbani na tuko kwenye harakati za kufunga Ndoa.


Kwakweli huyu bwana ananipenda sana kupita kiasi . Ananijali na kunithamini na kuniongoza katika kila jambo na kunishauri mambo yake yote kuhusu maisha yake na kwa kila kitu kiasi ambacho kanisubiri muda wa Miaka mitano ili nimalize masomo ili anioe.

Kwakweli miaka yote hatuna tabia ya kutoka pamoja wala kuonana ila nimazungumzo kwenye simu tu kwa muda wa miaka miwili.

Anakuja kwetu kawaida na mie kwakweli namempenda huyu kwa jinsi anavyonipenda na kunijali na navutiwa naye sana nikiwa naongea kwa simu kiasi ambacho siwezi kukaa siku bila kuongea nae na siwezi kufanya jambo bila kumshauri yeye tu.

Lakini cha kunishangaza akija kwetu kuonana na mie Moyo wangu unabadilika nahisi kuwa kama sijampendaa huyu mtu!

Naomba usinielewe vibaya  kusema kweli  nikikaa nikifikiria kiakili nahisi  sijaimpenda sura yake kwakweli na kwajinsi nilivyo huwa inanijia kama tukitoka wote itakuwa vipi?

Ila moyoni nampenda sana na siwezi kumkosa kabisa. Kwakweli nahisi nachanganyikiwa sijui nijiamulie vipi niufate moyo wangu au akili yangu?

Naogopa sana ikaja ikawa tatizo kwenye ndoa yangu na kutompa furaha anayoitarajia au je hili halitokuwa tatizo nikioana nae kwa vile Moyoni nampenda ntakuja kumpenda na kutojali sura yake.

Naomba Ushauri


Mbinu Mpya za Wanawake wa Siku Hizi Wanao Saka Ndoa Kwa Nguvu

$
0
0
Siku ya kwanza atakuja na chupi 2, moja
anaifua
anaacha bafuni,nyingine anavaa asubuhi
anaondoka...
Siku ya 2 anakuja na khanga,anaivaa
usiku,asubuhi
anaianika nyuma ya mlango anaondoka...
Siku ya 3 anasahau pete na hereni juu ya meza
anakwambia 'Hny nitunzie nimesahau hereni
zangu
mezani'
Siku ya 4 anakuja na nguo 2 na vipedo vya
kubadilisha na viatu pea 2,anavua high heels
anaweka kwenye Shoe rack,asubuhi anaondoka
na
flat shoes kwenda chuo..
Baada ya mwezi chumba chako kinakuwa na
vitu
kadha wa kadha,na ole wako uvihamishe
alipoacha,kesi zinaanza...Hao ndo Wanawake
wa
kileo,akija na begi zima si utamuuliza Vipi
mwenzangu na utamkimbiza...Anahamia
taratibu..
Mwisho wa siku dressing table yako iliyokuwa
ina
perfume na mafuta ya Rays inakuwa imejaa
hereni
na 'Foundation'... My Brother,huna haja ya
kuuliza,NDO KASHAHAMIA HUYO....Kifuatacho
utaambiwa,''Honey I miss my days',Zamani
nilijua
ni Simu za mkononi tu ndo zina Missed
Calls,Siku
hizi kuna Missed days,ukiambiwa hivi tu jua
imekula kwako,inawindwa ndoa...

SHAMSA – “Mastaa Wamenitukana Wamekasirika Wanasema Kwani Wao Siyo Wazuri”

$
0
0
Kutoka Bongomovie Shamsa Ford amelezea kuhusu post yake aliyopost kwenye Instagram kwa kumsifia Irene Uwoya kuwa ni mzuri kuliko wanawake wote Bongo Movie ambapo amesema kwamba wapo mastaa waliomtumia Message wakimsema kuhusu kitu hicho.

“Ilikuwa ni birthday ya Irene Uwoya nikawa nimeandika happy birthday mwanamke mzuri kuliko wote bongo movie, watu wakaanza kunitukana hasa wanawake, wengine ni wasanii wakawa wananitukana kwa kutuma message,” – Shamsa

Bonyeza PLAY kumsikiliza Shamsa akielezea kila kitu

VIDEO:

Binadamu Mzee Zaidi Duniani, Mkoani Songwe Amefariki Dunia

$
0
0
Kutoka katika Mkoa mpya wa Songwe ambapo Mzee Ambilikile Panja mkazi wa Kijiji cha Majengo Kata ya Ihanda Wilaya ya Mbozi amefariki na kuzikwa akiwa na umri wa miaka 127.

Huyu Mzee amefariki katika Hospitali ya Vwawa wilayani Mbozi na inaelezwa kuwa ameacha mjane, watoto 24, wajukuu 113, vitukuu 282, vilembwe 157, vining’ina 25 na vilembwekezi wa 5.

Idadi ya watu katika familia yake ni 606 aliowaacha, sawa na idadi ya watu katika baadhi ya vijiji wilayani Mbozi.

Mzee huyu inasemekana kuwa ndiye binadamu mzee zaidi duniani na amevunja rekodi ya kumzidi mtu anayetambuliwa na Guinness Book of World Records Vailet Brown kwa miaka 10

Hii ndio timu inayoongoza kwa kupewa penati EPL, timu yako imepewa penati ngapi?

$
0
0
Ni Everton, hawa ndio vinara wa kupewa penati katika ligi kuu Uingereza EPL na juzi katika mchezo wao wa EPL vs Swansea ilishuhudiwa wakipewa tuta lao la 7 msimu huu lililowapeleka kilele cha penati.

Penati walizopata Everton zimewaweka juu ya vinara wa ligi kuu Uingereza Manchester Citu ambao hadi sasa wameshapewa zawadi ya mikwaju ya penati mara 5 ikiwa ni mbili nyuma ya Everton.

Leicester, Watford, Brighton and Hove, Crystal Palace na Southampton wanafuatia wakiwa wote wamepiga penati tatu tatu hadi kufikia sasa katika EPL.

Manchester United, Liverpool, West Ham na Arsena wanafuatia wakiwa wana penati mbili mbili huku Chelsea, Stoke City,Fc Bournamouth na Huddersfield town wenyewe hadi sasa wana penati moja moja.

Vilabi vya Tottenham Hotspur, Burnley, West Bromich Albion, Newcastle na Swansea hadi sasa hawajapata bahati ya kupewa zawadi ya pigo la penati hata mara moja.

“No uchaguzi, No mabadiliko Yanga”-Mzee Akilimali

$
0
0
Katibu wa baraza la Wazee wa Yanga, m zee Ibrahim Akilimali ameshikilia uzi ulele wa kutaka ufanyike uchaguzi wa kuchagua mwenyekiti wa klabu hiyo kabla ya kuanza mchakato wa mabadiliko ya uendeshaji ndani ya klabu hiyo ya Jangwani.

Mzee Akilimali anaunga hoja ya mabadiliko ya uendeshaji wa klabu hiyo lakini anachotaka ufanyike kwanza uchaguzi wa kumpata mwenyekiti kabla ya kuendelea na mchakato wa mabadiliko.

“Kutaka uchaguzi ndio naonekana napinga maendeleo? Nataka tufanye uchaguzi tuchague mwenyekiti wetu. Wafanye utafiti wanachama wangapi wa Yanga wanataka uchaguzi na wangapi hawataki uchaguzi halafu wapokee maoni na wawe wakweli.”

“Tunatakiwa tufanye uchaguzi tuchague tumpate kiongozi wetu baada ya kumpata kio9ngozi wetu, turudi kwenye katiba yetu maana hili jambo la kampuni lipo kwenye katiba. Ndani ya katiba yetu inaeleza klabu itakuwa na hisa asilimia 51 na wawekezaji watakuwa na asilimia 49, sasa tukishampata mwenyekiti viongozi wetu wanakaa kuandaa mpango wa mabadiliko.”

“Kwenda kwenye mabadiliko huku tukiwa na kaimu mwenyekiti hilo ndio sitaki, na ninajua mbinu hizo zinafanywa na watu wanatayarishwa kwa ajili ya kutuletea vitu vya namna hiyo.kinachofanya tusipate kwanza mwenyekiti ni nini?”

Jana December 18, 2017, viongozi wa umoja wa matawi ya Yanga walitangaza kuwa, wameandika barua kwa kamati ya utendaji ya klabu hiyo wakiomba mzee Akilimali afutwe uanachama wa Yanga kwa madai kwamba wamechoshwa na vitendo vya mzee Akilimali kwenda kinyume na taratibu za klabu hiyo.

Mwenyekiti wa umoja wa matawi ya Yanga Robert Kasela alisema, mzee Akilimali si mwanachama halali wa Yanga hivyo wameona hakuna sababu ya kuendelea kuwa naye kwakuwa siku zote amekuwa akipinga maendeleo ya klabu.

Mzee Akilimali amewajibu viongozi hao wa matawi kwa kusema, kwa sasa wanatakiwa kuangalia ni kwa namna gani wataifunga Mbao kwenye mchezo wao ujao ambapo watakuwa ugenini kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

“Tufikirie namna gani tutashindana na Mbao maana mpaka sasa hatujaifunga sisi ndio vitu vya kufikiria wana Yanga sio kufikiria kumuondoa mzee Akilimali, akiondoka Akilimali basi kuna akina Akilimali wengi watakuja na hao kwenye mkutano wataambiwa sio wanachama?”
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images