Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104755 articles
Browse latest View live

Wanaume Watakiwa Kuhudhuria Kliniki na Weza Wao

$
0
0
Wanaume Watakiwa  Kuhudhuria  Kliniki na  Weza Wao
Afisa Muuguzi msaidizi katika Hospitali ya Rufani ya mkoa wa Shinyanga, Dk. Rehema Kapita, ametoa wito kwa wanaume kujenga tabia ya kuhudhuria kliniki na wenzi wao pale wanapokuwa wajawazito, ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.


Amesema idadi kubwa ya wanaume mkoani Shinyanga hawana utamaduni wa kuhudhuria kliniki na wenzi wao, hivyo kukosa elimu ya afya ya uzazi tangu malezi ya mimba hadi kujifungua, na kupelekea mzazi kukosa huduma stahiki
za matunzo na kusababisha kujifungua kwa shida ama kupoteza maisha .

Ametoa wito huo jana wakati akizungumza na Nipashe katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga, kuzungumzia watoto waliozaliwa kwenye mkesha wa sikukuu ya Kristimas ambapo watoto 14 walizaliwa wakiume wa tano, tisa wa kike na wote wakiwa salama.

“Natoa wito kwa kinababa kujenga utamaduni wa kuhudhuria kliniki na wenzi wao ili wapate elimu ya afya ya uzazi, pamoja na malezi ya mimba hadi kujifungua kwa lengo la kupunguza vifo vitokananvyo na uzazi, sababu watashirikiana kwa pamoja namna ya kumtunza mtoto na hatimaye mama kujifungua salama,” amesema.


Hivi Ndivyo LLinah na etiti Mani Walivyonaswa Live

$
0
0
Hivi Ndivyo LLinah na etiti Mani Walivyonaswa Live
AMA kweli mastaa hawaishiwi vimbwanga! Hayo yalidhihirika usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita baada ya staa wa kike wa Bongo Fleva, Esterlina Sanga ‘Linah’ kudaiwa kutelekeza mwanaye mchanga na kunaswa akibanjuka na jamaa ambaye ni meneja wa wasanii wa Bongo Fleva, Petit Man.

Tukio hilo lililonaswa na Ijumaa Wikienda lilijiri ndani ya Ukumbi wa High Sprit ulipo Jengo la IT Plaza, Posta jijini Dar kulikokuwa na pati ya usiku wa staa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper.




Wakibanjuka muziki.

Katika tukio hilo, Linah alinaswa akibanjuka na Petit Man na kuibua minong’ono kwa jinsi viguo alivyovaa vilivyokuwa vya kimitego, baadhi wageni waalikwa waliokuwa ukumbini hapo walisikika wakiteta kuwa msanii huyo muda huo alitakiwa kuwa nyumbani ili kumpa mwanaye haki ya malezi bora ya mama.

Mmoja wa wadau aliyezungumza na gazeti hili alisema kuwa, kwa jinsi Linah alivyoanza kujirusha mapema na kuvaa viguo vya kimitego ilihali mtoto akiwa bado mchanga, anaweza kuhatarisha afya ya mtoto huyo na kutengeneza mazingira ya kupata kichanga kingine kama hatakuwa makini.


Wakikata viuno.

Ijumaa Wikienda lilimuwinda Linah ukumbini humo na kumuuliza kulikoni kujiachia hivyo na kwamba baadhi ya watu walikuwa wakidai alimtelekeza mwanaye mchanga ambapo alisema kuwa, hajamtelekeza mwanaye isipokuwa alimuacha sehemu salama ndiyo maana akawa na amani wakati akijiachia.

“Aaaa, usiseme nimemtelekeza bwana…unajua mwanangu ndiyo kila kitu. Unaponiona hapa ujue yuko sehemu salama ndiyo maana nina amani,” alisema Linah aliyejifungua mtoto huyo wa kike mwezi Julai, mwaka huu.

Trump Amualika Rais Kenyatta Marekani

$
0
0
Trump  Amualika Rais   Kenyatta Marekani
SERIKALI ya Kenya chini ya Rais Uhuru Kenyatta imepokea mwaliko kutoka nchini Marekani kuhudhuria katika hafla ya kuwashukuru kwa kuendeleza urafiki itakayofanyika Januari 13, 2018.

Mwaliko huo umekuja ikiwa ni baada ya Kenya kuwa miongoni mwa nchi ambazo hazikupiga Kura ya kupingana na uamuzi wa Rais wa Marekani, Donald Trump kuutambua Jerusalem kuwa Mji Mkuu wa Israeli

Siku moja kabla ya zoezi la upigaji kura, Rais Trump alionya kukata misaada kwa nchi zote ambazo zingepiga kura ya kumpinga

Tanzania ni miongoni mwa nchi 128 ambazo zilipiga kura ya kumpinga Rais Donald Trump huku Kenya ikiwa ni miongoni mwa nchi 9 pekee zilizomuunga mkono.

Kipi Kimemkumba Barnaba?....Sasa Aamua Kujiondoa Kwenye Mitanda ya Kijamii

$
0
0
Kipi Kimemkumba Barnaba?....Sasa Aamua Kujiondoa Kwenye   Mitanda ya Kijamii
Msanii wa muziki ambaye pia ni producer wa High Table Sound, Barnaba Classic,  ameweka wazi kuwa ukimya wake utaanzia kwenye mitandao ya kijamii ikiwa ni sehemu ya kujiandaa na kujipanga namna ya kuuanza kwa kishindo mwaka 2018.



“Nikiwa najitoa kwenye mitandao ya kijamii kidogo, ningependa kuwatakia mashabiki, marafiki na familia yangu Heri ya Christmas na Mwaka Mpya”, amefunguka Barnaba kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Pamoja na kujitoa kwake nyota huyo anayetemba na ngoma yake ya Mapenzi Jeneza ameongeza kuwa anajiweka vizuri kuanzia mwonekano mpaka sound ya hit zake zijazo.

“Ninapumzika kidogo ili kuweka mipango yangu vizuri kwaajili ya mwaka 2018. Nitawaletea Barnaba mpya mwenye kila jipya kimuziki na hata Sound” ameongeza.

Papa Francis Awatea Wahamiaji

$
0
0
Papa Francis   Awatea Wahamiaji
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amewataka Wakristo bilioni 1.3 duniani kutopuuza majanga yanayowakumba mara kwa mara wahamiaji “wanaofukuzwa kutoka nchi zao” na viongozi ambao wako tayari “kumwaga damu kwa watu wasio kuwa na hatia”.

Pia, kiongozi huyo amewataka waumini hao kuwa wakarimu na watu wenye huruma kwa wahamiaji. Amesema hayo katika hotuba yake aliyoitoa katika Sikukuu ya Krismasi.

Papa Francis, ambaye anajulikana kwa jina lake aliopewa na wazazi wake Jorge Bergoglio, mjukuu wa wahamiaji kutoka Italia, alizungumzia kuhusu hatima ya wakimbizi miaka mitano baada ya kuchukua uongozi wa Kanisa Katoliki duniani.

“Hakuna mtu anayepaswa kuhisi kuwa hana mahali hapa duniani,” alisema katika hotuba yake ya Krismasi.

Hayo yanajiri wakati ambapo kumeendelea kushuhudiwa makabiliano kati ya waandamanaji wa Kipalestina na wanajeshi wa Israel huku Wapalestina 12 wakipoteza maisha.

Uamuzi wa Marekani kuutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel umeelezwa na washirika wa Palestina kuwa umehatarisha uwezekano wa kupatikana kwa amani kati yake na Israel.

Kadhalika kiongozi huyo amewaombea watu wa kisiwa cha Mindanao nchini Ufilipino.

Kisiwa hicho kimeharibiwa na mafuriko na maporomoko ya ardhi baada ya kukumbwa na kimbunga tokea siku ya Ijumaa.

Papa Francis amesema dhoruba hiyo imewaathiri watu wengi na imesababisha uharibifu mkubwa. Papa Francis amesema anataka kuwahakikishia watu wa Mindanao sala zake ambapo alimuomba Mungu mwenye huruma apokee roho za waliokufa kwenye maafa hayo na wakati huo huo amewafariji wote wanaohusika waliofikwa na misiba. Zaidi ya watu 200 wamepoteza maisha kutokana na dhoruba hiyo huku wengine zaidi ya 140 wakiwa hawajulikani waliko.

Mjini Bethlehem nchini Israel, mji ambao Wakristo wanaamini kuwa Yesu alizaliwa, mwaka huu shamrashamra zinashuhudiwa lakini si kwa kiasi kikubwa.

Wasiwasi unashuhudiwa na watalii wengi, hawajakwenda katika mji huo kwa kuhofia usalama wao.

Hatua hii inakuja baada ya Marekani hivi karibuni, kutambua mji wa Jerusalem kama makao makuu ya Israel hatua ambayo imeikasirisha Palestina na mataifa ya Kiislamu na yale ya Kiarabu.

Wiki iliyopita kulikuwa na mkutano wa dharura wa Umoja wa Mataifa kulaani hatua hiyo ya Marekani. Katika hatua nyingine, waamini wa Kanisa Katoliki waliobahatika kupata nafasi katika maisha ya kisiasa wameaswa kuhakikisha wanasimama kidete kulinda, kutetea na kudumisha utu na heshima ya binadamu.

Wakati huohuo, ujumbe wa Vatican umewataka wanachama wa Umoja wa Mataifa daima kuzingatia historia na utambulisho maalum wa mji wa Yerusalemu ambao kimsingi ni kwa ajili ya mafao ya Jumuiya ya Kimataifa.

Jerusalemu ni mji mtakatifu unaoheshimiwa na waamini wa dini ya Kiyahudi, Kikristo na Kiislam. Ujumbe wa Vatican umesema kuwa suluhu ya amani katika eneo hilo itafikiwa kwa kuheshimu.

“Jumuiya ya kimataifa inaweza kusaidia kukuza na kudumisha misingi kuwepo kwa amani na hivyo kuuwezesha mji wa Jerusalemu kutunza umaarufu wake katika mchakato wa majadiliano na upatanisho,” umesema.

Ujumbe huo umewashuruku wanachama wa Umoja wa Mataifa, kwa kusimama kidete kulinda maamuzi ya UN ambayo imesaidia kudhibiti ghasia na machafuko ambayo yangeweza kujitokeza katika eneo hilo baada ya kupitisha azimio la kulaani hatua ya Marekani kuutambua mji wa Jerusalemu kama makao makuu ya Israel

Katibu mkuu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin amewataka waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi mema kuzingatia maana ya Sikukuu ya Krismasi kwa kuzingatia utu na matendo mema na kuacha kuendekeza mwelekeo wa sasa ambao umegeuza sikukuu hiyo kuwa ni tukio la kibiashara na ulaji wa kupindukia.

Kardinali Parolin, amewataka wanasiasa kutumia vyema dhamana na wajibu wao, kwa kusikiliza na kutafuta ufumbuzi wa kero na mahangaiko ya wanawanchi wa kawaida.

“Inasikitisha kuona siasa inageuzwa kuwa ni jukwaa la uchu wa mali, madaraka na mafao ya mtu binafsi, kiasi cha kusahau na kufumbia macho mahangaiko, matatizo na changamoto zinazowakabili wananchi wanao wawakilisha.

Siasa imekuwa ni uwanja wa malumbano, kejeli na vijembe mambo yasiyokuwa na tija wala mashiko kwa ustawi na maendeleo ya wengi,” alisema.

Alisema baadhi ya wanasiasa wamegeuka wajeuri na watu wenye kiburi kiasi cha kutupilia mbali fadhila ya unyenyekevu inayowasogeza zaidi kwa wananchi wa kawaida.

Alisema wanasiasa wanapaswa kutumia jukwaa la kisiasa kama uwanja wa umoja, upendo na mshikamano wa kitaifa.


Mambo Yawanyookea Yanga SC Waanza Matengenezo ya uUwanja Wao wa Kaunda

$
0
0
Mambo Yawanyookea  Yanga SC Waanza Matengenezo ya uUwanja Wao  wa Kaunda
Mabingwa watetezi  wa Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara, Yanga SC wameanza matengenezo ya uwanja wao  wa kaunda  uliopo eneo la Jangwani Jijini Dar es Salaam.


Mabigwa hao watetezi wa kupitia ukurasa wao wa  Instagram wameweka video ikionyesha ukarabati ukiendelea katika uwanja huo.

Video hiyo inaonyesha ikisawazisha vifusi vilivyokuwa vimemwagwa uwajani hapo kwa siku kadhaa zilizopita.

Picha: Tundu Lisu Asimama Mkwa Mara ya Kwanza

$
0
0
Picha: Tundu Lisu Asimama Mkwa Mara ya Kwanza
Picha kutoka Hospitali ya Nairobi ikimuonesha Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akifanya mazoezi ya kusimma kwa msaada wa madaktari wa hospitali hiyo

Hivi Ndivyo Safari za Mwisho wa Mwaka Zaliathiri Jiji la DSM

$
0
0
Hivi  Ndivyo  Safari za Mwisho wa Mwaka Zaliathiri Jiji la DSM
Madereva katika kituo cha mabasi cha Makumbusho Jijini Dar es Salaam wamelalamikia upatikanaji wa abiria kuwa mdogo katika kipindi hiki cha sikuu, kutokana na watu wengi kutokuwepo mjini.


Madereva hao sambamba na makondakta wametoa kilio chao hicho wakati huu baada ya abiria wengi kusafiri kwenda mikoani kuungana na familia zao kwa ajili ya sikukuu za Krismasi na mwaka mpya, na neema kuwaangukia wenzao wanaoendesha mabasi ya mikoani.

Wakizungumza na waandishi wa habari madereva hao wamesema ukosefu wa abiria kumewaathiri kipato chao cha kila siku, hali inayopelekea mabosi zao kutowaamini kwa kuwa wamezoea kufanya ruti kumi kwa siku na kipato kuwa cha juu, lakini kwa sasa wanafanya ruti tatu hadi tano kwa siku, hali inayochangia kushuka kwa makusanyo ya mapato yao ya kila siku.

Uchaguzi wa Rais Liberia Kati ya George Weah na Joseph Boakai Kufanyika Leo

$
0
0
Watu nchini Liberia wanapiga kura katika duru ya pili kati ya makamu wa rais Joseph Boakai na nyota wa zamani wa kandanda George Weah.

Bwana Weah, 51, alishinda duru ya kwanza lakini hakufanikiwa kupata asilimia 50 ya kura kumwezesha kuwa mshindi.

Duru ya pili ya uchaguzi wa urais kuchukua mahala pake Ellen Johnson Sirleaf, ilichelewa kufuatia kesi iliyokuwa mahakamani.

Vituo vya kupigia kura vinafunguliwa saa mbili asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili.

Zaidi ya watu milioni mbili wamejiandikisha kama wapiga kura.

Wagombea ni nani?
Bw. Boakai 73, amekuwa makamu wa rais nchini Liberia kwa miaka 12 lakini haonekani kunufaika na uungwaji mkono kutoka kwa rais.

Wenger apatwa na mtego wa habari za uzushi
Mahakama yasitisha uchaguzi wa rais Liberia
Naye Weah, ambaye ni nyota wa zamani wa kandanda ana matumaini ya kushinnda baada ya kuwania kwa mara ya tatu.

Alimshinda Bi Johnson Sirleaf wakati wa duru ya kwanza mwaka 2005, lakini akashindwa wakati wa duru ya pili.

Wakati wa uchaguzi ulioafuata akiwa mgombea mwenza, muungano wake ulisusia duru ya pili ukidai kuwepo udanganyifu.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

Lissu Aanza kusimama kwa Mara ya kwanza kwa Msaada wa Madaktari.

$
0
0
Lissu Aanza kusimama kwa Mara ya kwanza kwa Msaada wa Madaktari.
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu aliyelazwa katika Hospitali ya Nairobi Kenya baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana, ameanza kusimama kwa mara ya kwanza kwa msaada wa madaktari.


Taarifa kutoka Hospitali ya Nairobi imeeleza kuwa Lissu kwa mara ya kwanza ameweza kusimama kwa msaada wa Physiotherapist tangu  Septemba 7, mwaka huu alipopigwa risasi mjini Dodoma, hatua chache kabla ya kufika nyumbani kwake.

Akizungumza kutoka Hospitalini hapo, Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Rais wa Chama cha Wanansheria Tanganyika (TLS), amesema "Wapendwa wote wiki iliyopita niliwataarifu kwamba  madaktari wangu wamesema nitasimama, nitatembea na nitarudi Tanzania"

"Leo Boxing Day nimeweza kusimama kwa mguu mmoja kwa msaada wa mababa cheza kama inavyoonekana, hatua inayofuata nitawajulisheni," Lissu

Mwanjali Afunguka Baada ya kutemwa Simba

$
0
0
Mwanjali Afunguka Baada ya kutemwa Simba
PAMOJA na kuachwa katika kikosi cha Simba hivi karibuni, aliyekuwa beki wa timu hiyo, Mzimbabwe, Method Mwanjali, ameisifia klabu hiyo kwa kusema kuwa hajaona kama hiyo katika timu za Afrika alizocheza, kwani ni ya kipekee, huku akiitakia mafanikio mema kwenye michuano yake.
Beki huyu alikuwa nahodha wa kikosi hicho, ameachwa na Simba kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo huku nafasi yake ikichukuliwa na beki Mghana, Asante Kwasi.
Mwanjali alisema kuwa, licha ya kupitia timu kadhaa huko nyuma, Simba ni moja kati ya timu ambazo aliyafurahia maisha alipokuwa akicheza kwa takriban miaka miwili.
“Sina la kusema lakini najua Simba ni klabu kubwa na ya kipekee katika Ukanda wa Afrika Mashariki kutokana na jinsi ambavyo imekuwa ikipambana kuhakikisha inaweka historia katika ramani ya soka pamoja na inavyowatunza wachezaji wake.
“Kila la kheri na mafanikio mema katika michuano yote ambayo ipo mbele yao, wapambane na kuweza kufika mbali zaidi ya walipo sasa,” alisema Mwanjale.
Ikumbukwe kuwa, Mwanjale kwa muda ambao amecheza Simba, amefanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la FA pekee msimu uliopita.

Polisi Yawaonya Madereva wa safari Ndefu

$
0
0
Polisi Yawaonya Madereva wa safari Ndefu
 Polisi Mkoa wa Pwani imetoa agizo kwa wamiliki wa magari yanayofanya safari ndefu kuzingatia uwepo wa madereva wawili.

Jeshi hilo limesema kinyume cha hilo, magari hayo hayataruhusiwa kuendelea na safari.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shanna amesema hayo leo Jumanne Desemba 26,2017  akizungumzia namna walivyojipanga kidhibiti ajali.

Amewatahadharisha madereva wasio na uzoefu wa kwenda safari ndefu wasiendeshe magari ya abiria na badala yake watafute wazoefu ili kuepusha ajali zinazozuilika.

Amesema mwishoni mwa mwaka kumekuwa na ajali ambazo baadhi husababishwa na uzembe.

Taarifa ya Polisi Mkoa wa Pwani inaonyesha Januari hadi mwanzoni mwa Desemba mwaka huu matukio ya ajali yamepungua kutoka 396 za kipindi kama hicho mwaka jana hadi 98.

Kamanda Shanna pia ameonya wanaojihusisha na uhalifu na makosa mengine ya uvunjifu wa amani akisema wamejipanga kuwakabili.

Arsenal Kumuuza Sanchez Paundi Milioni 35

$
0
0
Arsenal  Kumuuza Sanchez Paundi Milioni 35
Klabu ya Arsenal inazidi kukosa uvumilivu juu ya Alexis Sanchez na inaelezwa kuwa wapo tayari kupokea ofa yoyote isiyopungua paundi milioni 35.



Mchezaji huyo wa kimataifa wa Chile alitolewa ofa ya paundi milioni 60 na Manchester City majira ya joto, lakini Gunners walikataa kwani hawakuweza kupata mbadala wake kwa wakati huo.



Hata hivyo wanaweza kuwa tayari kusikiliza ofa dirisha la uhamisho litakapofunguliwa – lakini kwa bei pungufu.

Wanaamini kwamba moyo wa mchezaji huyo unawaza zaidi kutimkia Man City ya Pep Guardiola.



Lakini kwa sababu atapatikana kama mchezaji huru mwisho wa msimu, mchezaji huyo wa Chile angependelea kubaki hadi aweze kuongeza thamani yake kwa maana ya kiwango.

Baadhi ya mashabiki wa Arsenal wanakerwa na ulegevu anaouonyesha mchezaji huyo kwa kutofanya juhudi – wakisema ni bora angeondoka majira ya joto.



Inaaminika kuwa Sanchez alikubali mkataba mpya Arsenal – Lakini akabadili mawazo yake.

Paris Saint-Germain wanavutiwa kumsajili mshambuliaji huyo – na pia wanaweza kumtumia Julian Draxler ambaye Arsenal wamekuwa wakimtamani siku nyingi kukamilisha uhamisho huo.



Lakini inaaminika Sanchez alikubali dili jipya miezi 12 iliyopita lakini alibadili akili yake Arsenal walipodhalilishwa na Bayern Munich kwa jumla ya kipigo cha mabao 10-2 Ligi ya Mabingwa kwa mujibu wa The Times.

Sasa kazi ipo kwa Arsenal Januari, wang’ang’anie kubaki na mchezaji asiye na furaha klabuni au wamuuze kwa mahasimu wao wa Ligi Kuu Januari.

Aliyekamatwa na Dawa za Maumivu Afungwa

$
0
0
Aliyekamatwa na Dawa za Maumivu Afungwa
Mwanamke wa Uingereza Laura Plummer aliyekamatwa na dawa za kutuliza maumivu katika uwanja wa ndege kwa ajili ya mumewe anayeishi nchini Misri afungwa miaka jela kwa miaka mitatu.


Lura ambaye alikamatwa Oktoba 9, 2017 katika uwanja wa ndege wa Misri baada ya kukutwa na vidonge vya dawa aina ya Tramadol, alivyokuwa akimpeleka mume wake anayekabiliwa na matatizo ya mgongo, kitendo ambacho kimeelezwa ni kosa kisheria nchini humo.

Familia ya Laura imesema inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo waliyoitaja kuwa ni ya uonevu, kwani vidonge hivyo havina madhara yoyote kwa kuwa nchini Uingereza vinaruhusiwa mtu kuwa navyo, lakini ni kinyume na Misri.

Laura ameolewa na raia wa Misri ambaye anaishi nchini humo, na mara kwa mara amekuwa akienda kumtembelea.

Mahusiano Kabla ya Ndoa Kati ya Msichana na Kijana wa Kiume.

$
0
0

Asanteni tena kwa kujumuika nasi hapa katika ukurasa huu unaolenga kuwafungua watu katika maswala mbali mbali ya kijamii, yanayokwamisha maendeleo ya watu pamoja na kusambalatisha mahusiano ya watu.

Leo tunaangalia mambo ya kuzingatia kabla ya kuingia katika ndoa, na hapa wengi huenda nikaenda tofauti nao, lakini ni jukumu langu kuelimisha jamii na sio kuifurahisha tuu. Kila mtu anafahamu neno mahusiano ya kirafiki kati ya jinsia mbili tofauti.

Kabla ya kuingia katika ndoa, lazima ufanye urafiki na mtu unayetaka kumuoa au kuolewa naye, ili uweze kubaini tabia na mwenendo wake kama unaendana na wakwako, au anamatatizo gani ya kiafya au kiukoo pia.

Tumekuwa tukikimbilia kufanya mapenzi ili kupima uwezo wa injini kama inahimili safari na kusahau usukani wa gari, kwani gari haliwezi kukufikisha pale unapotaka kwenda bila ya kuwa na uskani (staring).

Kwa wachumba na wasio wachumba yani Girlfriend na Boyfriend, kama kweli unampango wa kumuoa au kuolewa, ni vyema usiendekeze kufanya mapenzi na mwenzi wako, kwani kufanya mapenzi na rafiki yako unayetarajia kumuoa au kuolewa naye, hupunguza upendo au hisia na shauku ya kutaka kuishi kama mume na mke kwa baadae.

Kama kimwili utampa mpenzi wako kila kitu anachokitaka, then nini kitakuwa kimebakia katika mwili wako ambacho atakuwa na shauku ya kutaka kukipata? Hisia kubwa ya ndoa ni mapenzi na kupata watoto, na ndio maana wasichana wengi wanachelewa kuolewa au hata hawawezi kuolewa kwasababu hawana mipaka katika maamuzi ya mapenzi.

Kunanjia nyingi za kumridhisha mpenzi wako na akasahau kukuomba kufanya....., zipo nitaziweka katika makala ijayo, lakini cha msingi ni wewe kijana kujitunza na hata kama unafanya mambo haya fanya lakini mbakizie mkeo au mumeo ili akikuona kila siku anakuona ni kama kitu kipya.

Kwanini usijiulize ni kwanini nyumba ndogo zina dominate sana katika maswala ya unyumba? Ni kwasababu wanajipanga na kuonekana kila siku ni wapya kwa wapenzi wao, wanawasoma wapenzi wao na kujua wape madhaifu yalipo. Sasa basi wewe msichana weka mipaka katika mwili wako utaonekana wa thamani sana! Hata wewe kijana wa kiume muonyesha mpenzi wako kuwa unamalengo nae na mapenzi ni sehemu tu.

Tukutane katika makala nyingine za kusisimua kama, vitu vya kufanya na ukasahau mapenzi katika mahusiano kabla ya ndoa.

Sifa15 Zinazomfanya Mwanamke Kumpenda Mwanaume.

$
0
0

Pengine watu wengi wamekuwa wakitafuta ni jinsi  gani wanaweza kupendwa na wasichana au wanawake. Niwazi kabisa kila mwanamke anachaguo lake kwa mwanaume ampendae.Huenda ukawa unavigezo kibao lakini akapenda mweyevigezo vichache. Vifuatavyo ni vigezo 15 ambavyo wasichana wengi hupenda kutoka kwa mwanaume.

1. Kujiamini

2. Mcheshi

3. Mwenye utashi

4. Anayetoa msaada unapohitajika

5. Anaetunza siri

6. Mwenye kujithamini

7. Mwenye malengo / makini 

8. Mwenye mawazo mapana 

9. Muwazi na mkweli 

10. Anayeridhika     

11. Aliyeshupavu na jasiri

12. Mwenye huruma

13. Anaesamehe

14. Hadhi na heshima

15. Hisia ya uadilifu.

Mwanamke Anachotakiwa Kufanya ili Mume Wake Asitoke Nje ya Ndoa.

$
0
0

Mapenzi yana kanuni zake, kanuni ambazo usipozifuata huwezi kupata furaha uliyotarajia. Unapotokea kumpenda mtu, hiyo ni hatua ya kwanza lakini omba sana upate ile bahati ya kumpenda mtu ambaye naye anakupenda kwa dhati.

Kwa bahati mbaya ukitokea kumzimikia mtu ambaye wala hana hata chembe za penzi kwako, utaumia sana na kama utalazimisha kuwa naye, utakuwa unajitafutia vidonda vya tumbo.

Hata hivyo, wapo waliobahatika kuwapata wapenzi wa ukweli lakini kwa kushindwa kwao kujua yapi ya kufanya ili kudumisha penzi, leo hii wameachika na bado wanaranda mtaani.

Kwa kifupi ni kwamba, unapoingia kwenye uhusiano na mtu na ukabaini naye anakupenda, hutakiwi kubweteka bali unatakiwa kutumia utundu na ubunifu wako katika yale ambayo yatamfanya huyo mtu wako ahisi wewe ni wa pekee kwake.

Ninapozungumzia hayo, namaanisha ubunifu kwenye mambo mengi ambayo hakika nikianza kuyaelezea hapa, nafasi inaweza isitoshe ila kwa leo nigusie utundu katika uwanja wetu ulee wa kujidai.

Faragha ni eneo muhimu sana ambalo linaweza kubomoa au kuimarisha ndoa. Ninapozungumzia hilo, ni kwa wote yaani mke na mume.

Mwanaume anatakiwa kumridhisha mkewe kwa kiwango kinachostahili. Kusiwepo mazingira ya kupeana mambo kiduchu kwani ikiwa hivyo lazima mke atakosa furaha iliyokamilika.

Ila sasa leo nataka niwazungumzie kwa kirefu wanawake. Kuna wanawake ambao wamebahatika kupata wanaume wanaowapenda sana na kuwapatia kila wanachohitaji.

Hawa wanatakiwa kujiona ni wenye bahati kubwa kwani kwa hali ilivyo sasa, wanawake wengi wanatafuta wanaume wa kuwaoa hawawapati.

Kinachonishangaza ni kwamba, kuna baadhi ya wanawake ambao wako ndani ya ndoa lakini wamejisahau kwamba wana jukumu la kuwapa waume zao furaha ambazo hawawezi kuzipata kwingine.

Ukijaribu kuchunguza utabaini wanawake wengi walio ndani ya ndoa siku hizi wanasalitiwa sana. Hii ni kwa sababu wamekuwa waongeaji sana lakini wanapokuwa faragha unaweza ukadhani siyo wao. Hawajui kitu, wamekaa kama magogo tu halafu eti wanadhani hawatasalitiwa na ndoa zao zitadumu, zitadumu kwa misingi ipi?

Mwanamke akae akijua kwamba, mumewe ni kama mtoto ambaye anatakiwa kubembelezwa huku akipewa vitu vitamu ili kumpumbaza asishawishike kutoka nje. Ukiwa kwenye ndoa kisha ukachukulia kila kitu poa tu eti kwa kuwa tayari ulishapendwa ipo siku utajikuta ni mke wa pambo la nyumba tu.

Mtaani kuna utitiri wa nyumba ndogo, wanaume walioanzisha makoloni hayo nje ya ndoa zao walikosa wake sahihi ambao wanaweza kuwashikilia waume zao.

Matokeo yake sasa nyumba ndogo hizo ndizo zinazooonekana kuwashika waume za watu siku hizi na wanafanikiwa kwa kuwa ni watundu na wabunifu.

Sasa kwa nini wewe mwanamke uliye ndani ya ndoa usifanye kama yale wanayofanya nyumba ndogo? Kuna dada mmoja nilizungumza naye hivi karibuni akaniambia eti amenuniana na mumewe huu ni mwezi wa pili baada ya mwanaume wake huyo kutaka afanyiwe mambo ambayo yeye aliona kinyaa kuyafanya.

Kabla ya kumjibu kwanza niliguna, sababu ya kuguna ni kwamba niliyagundua hayo mambo ambayo aliona kinyaa kumfanyia mumewe. Niseme tu kwamba, mapenzi wakati mwingine ni uchafu, wanaojua mapenzi wanajua kwa nini nasema hivyo.

Nilichomjibu mwanamke huyo ni kwamba, kama mwanaume huyo anampenda amfanyie kila atakacho isipokuwa kukubali kufanya mapenzi  kinyume na maumbile na nikamwambia kuwa, mapenzi ni uchafu hivyo hayo ambayo anaona kinyaa kumfanyia mumewe ndiyo ambayo wengine wamekuwa wakiyafanya na wamefanikiwa kuzishika ndoa zao.

Naomba niseme tu kwamba, huenda unajiamini kuwa ni mzuri na umbo la kuvutia kiasi kwamba, ni rahisi kupata mwanaume wa kuoa lakini tambua bado utakuwa na kazi kwenye kuidumisha ndoa na kuhakikisha hukaribishi mazingira ya mumeo kutafuta nyumba ndogo.

Hakikisha unaonesha uanamke wako ili hata kama huyo mumeo atatoka nje, iwe ni kwa tamaa zake tu lakini mambo ya msingi uwe unampatilizia.

Mbinu 15 za Kumtongoza Mwanamke Akakupenda Daima

$
0
0

Kuna baadhi ya wanaume hawajui jinsi ya kuzungumza na mwanamke au msichana. Kwa njia hii wanaume wengi wanaishi maisha ya bila kumvutia mwanamke yeyote.

Hapa kunanjia 15 utakazozitumia wewe mwanaume ili kuhakikisha humkwazi mwanamke unayempenda mnapokuwa katika mazungumzo ;

1. Wakati ukizungumza nae, jaribu kuzungumzia "hisia" kama vile kumbu kumbu yako ya utotoni, matarajio ya baadae au matamanio yake. Mada hii ya mazungumzo yenu yatafungua milango ya hisia zake ghafla.

2. Wanawake huhitaji mwanaume asiyekuwa na uoga wa kuwamiriki na kuwaongoza. Wakati unazungumza na mwanamke tawala mazungumzo yenu na kamwe usimpe nafasi ya yeye kuanza kufikiri kuwa nini ulichokuwa ukizungumzia.

3. Kuwa makini wakati unapokuwa ukizungumza nae huku akikupatia majibu yasiyo na hisia zozote za mapenzi. Hapo utajua kunakitu, hivyo kama kwa bahati mbaya uko nae karibu kiasi cha kugusana, basi jisogeze pembeni wakati ukiwa unaendelea kuongea ili asishtukie au unaweza kumuona hayuko sawa katika utoaji majibu.. kwa kawaida atakuonyesha ishara, hivyo kuwa nazo makini.

4. Kumbuka hii kauli mbiu "Ucheshi/vituko si mapenzi". Wanawake huvutiwa sana na wanaume wanaoweza kuwafanya wawe na furaha muda wote. Usijikite zaidi katika kufanya utani unaopita kiasi na kusahau ulichokuwa unaongea. Bali jikite zaidi katika mambo yanayomfanya ajisikie kuwa na msisimko na starehe wakati ukonae.

5. Zama katika undani wa mazungumzo baina yako na yeye. Mwanamke huendana na mwanaume asiyekuwa muoga wa kuzungumzia mambo binafsi kwa ukaribu.

6. Wanawake wengi hupenda kujua maoni yako kuhusiana na jinsi unavyomuona. Mwambie vitu unavyoviona kutoka kwake, lakini jaribu kuwa makini ili usitamke vitu vingine vitakavyo msababishia apoteze furaha.

7. Epuka kumpa ofa nyingi mwanamke, mwanamke huwa na mashaka na mwanaume anayempatia vitu vingi kwa wakati mmoja ama kila mara. Kwasababu atafikiri vitu unavyompatia ni kutaka kumvutia tu ili umpate kiurahisi. Kitu ambacho baadae kitaleta madhara makubwa.

8. Kama unahitaji kujua njia nzuri ya kuweza kuongea na mwanamke au msichana bila kumfanya asikudharau au kuboreka, basi usitumie njia ya kumuuliza  maswali mengi katika mazungumzo yenu. Bali jaribu kueleza mawazo yako kuhusu vitu flani.

9. Kumbuka kauli juu ya kuuliza maswali: Badala ya kumuuliza "wewe umekulia wapi?", uliza "unaonekana kama hujakulia maeneo haya!" Hii itakusaidia wewe kufanya uchunguzi juu yake bila yeye kujua.

10. Usifiche utambulisho wako - zungumza vitu kutoka katika hisia zako, onyesha uhalisia wako katika kuzungumza na usitumie mikogo ya mtu yeyote.

Njia bora ya kufikiria jinsi ya kuzungumza na mwanamke, ni kutambua njia sahihi ya mazungumzo ya furaha na yakimahaba utakayopenda kuitumia, isipokuwa usimuige mtu. Kuzungumza na mwanamke sii vigumu bali nikujua ni vitu gani hasa mwanamke hapendi kuvizungumzia na vitu gani anapenda kuvisikia. Fuata maelekezo hapo juu utaona matunda yake...kisha rudi toa maoni yako hapa.

MUHIMU: Maelekezo haya yote yatafanikiwa kwa mwanamke mwenye kuhitaji mapenzi ya kweli - yani sio kwa wanawake wanaolenga kuchota pesa kwako na kutokomea. Hivyo kuwa makini sana.

Kufanya Mapenzi Ofisini Kunavyoadhiri Mtu Kisaikologia

$
0
0

Kula nanasi kunahitaji nafasi, wengi wamekuwa wakishawishika kufanya mapenzi katika eneo la kazi kutokana na kupendana ama vishawishi mbali mbali kutoka kwa kinadada hususani katika mavazi. Sina maana mbaya ninaposema kina dada kwasababu wengi wao ndio wanaoacha sehemu zao nyeti wazi, kwamfano kuvaa nguo fupi sana na kuvaa vitop vinavyoonyesha sehemu kubwa ya maziwa wazi.

Kwa asilimia miamoja watu wengi wanaofanya mapenzi kwa kuiba katika maeneo kama ya ofisini huwa hawakumbuki kuvaa kinga kutokana na mihemumko mikali na ya haraka kuliko kawaida wanayokuwa nayo kwa wakati huo. Ni vyema kujihadhali ma mihemuko hii kwani madhara yake ni makubwa.

Mihemuko hii huwakumba watu wote hata ambao wako katika ndoa, kutokana na vishawishi vya mwenzake basi anajikuta amezama katika saa za kazi. Tabia hii ikifanyika mara tatu huanza kuwa kama sehemu ya majukumu ya wezi hawa wa mapenzi. Kinadada wanaovaa nguo fupi katika makazi ya watu huenda wakawa wanafanya hivyo kwasababu ya fasheni, wengine kutafuta mvuto kwa wafanyakazi wenzie, lakini kwa wanaume huwa ni kishawishi kimoja kikubwa sana.

Kumbuka unapaswa kuishinda faragha yako na kujitambua kuwa hupaswi kufanya mapenzi na mke wa mtu au mume wa mtu. Unapoona vishawishi kama hivi jaribu kuwa bize na kazi, chukulia poa tu japokuwa wadada wengi huwa na njia mbali mbali za kukufanya ukanasa kirahisi kwa mfano kama mnakumbuka skendo ya Monica Lewinsky na aliyekuwa rais wa Marekani wakati huo walichokifanya ofisini na baadae kuja kuwa ni skendo kubwa sana.

Hasara ya mapenzi hayo ya kiwizi wizi katika masaa ya kazi ni kupata maambukizi ya Ukimwi bila kufahamu kwani utakuwa umemzoea mfanyakazi mwenzio kwa jinsi alivyo smati katika kazi, hivyo hutafikilia kama anawatu wengine nje ya kazi. Pia kuna maambukizi ya magonjwa ya zinaa, ambayo kwa wanawake hujificha kwa muda kabla ya kuonekana haraka kama wanaume.
Viewing all 104755 articles
Browse latest View live




Latest Images